Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 83.

Kwa maelezo ya Yang ,mkuu wa jeshi kutoka china alieleza kwamba Ares ni jina la kihistoria linalotoka katika historia ya Ugiriki ya kale , likimaanisha Mungu wa Vita.

Katika historia ya ugiriki ya Kale Ares ni sehemu ya miungu kumi na mbili katika hadithi za kigiriki, huku sifa kubwa ya Ares ikiwa ni Mungu wa vita , huku akiendelea na kusema kwamba sehemu hio ya miungu ni kama Hades pia , Poseidon na wengineo kumi .

“Afande jana kulitokea tukio la vijana watu kupoteza uwezo wao wa fahamu na kupelekea kufanya jambo la kumshambulia Hades, unalizungumziaje hili?”Aliuliza Afande Maeda.

“Hio ni sehemu ya uwezo wa Ares ,ni waambie tu Ares anauwezo wa kujibadilisha na kuwa kiumbe yoyote yule na ni mtu ambaye hana huruma kabisa”.Aliongea Afande Yang na kufanya kila mtu ashangazwe inakuwaje duniani kukawa na watu wa aina hio.

Wakati kikao hiki kikiendelea mara aliingia Ajenti Flamingo na kumsogolea Afande Maeda na kumwambia jambo na kisha afande Maeda akawageukia wenzake.

“Afande Yang kuna tukio la kulipuka kwa mlima wetu wa Volcano ambao haukuwahi kulipuka kwa muda mrefu sana, unaweza ukalihusisha jambo hili na Hades pamoja na Ares?”Aliulia Afande Maeda na kila mmoja alimwangalia Afande Yang , kwa kusubiria jibu.

“Sitaki kukoswa na jambo hilo na mlipaswa kuniambia hili mapema”Aliongea huku akinyanyuka.

“Unamaanisha nini Afande?”

“Hamtaki kushuhudia pambano la Hades na Ares? , Come on guys this is opportunity , tukishamaliza kushuhudia kinachoendelea tutaendeleza mazungumzo”Aliongea afande Yang na kuwafanya Mabosi hawa wajeshi kupata msisimko.

Kila mmoja alitaka kwenda kushuhudia kile ambacho kilikuwa kikiongelewa kuhusu Hades na Ares

Ndani ya dakika chache tu chopa za kijeshi zilitoweka ndani ya eneo la makao makuu ya jeshi.

*****

Ndani ya hoteli ya kitalii ilifahamikao kwa jina la Amesi , iliokuwa pembezoni mwa eneo la kitalii la Ziwa Natroni walionekana wazungu wawili , yaani mwanamke na msichana waliokuwa wamevaa mamiwani ya kisasa ambayo ukiyaangalia ni kama yale Virtual Reality(VR),Wazungu hawa wote walikuwa wameshikilia vifaa mikononi mwao kama Pad , lakini ukizisogelea karibu sio Pad bali ni vifaa vya kuendeshea Drone , vinavyotumia teknolojia ya GPS na LiDAR.

“Damn it Jessie , This fight won`t end soon as we Expected”

“It has Been more than twelve hours ,Since the Fight started Jasson , I am so hungry but I feel like this battle is more worth than my Hungry Stomach”Aliongea Jesie

“Hades seems to be Tired ,Come on Ares finish him, Damn it Hades you are Dumb Ass , this is over with your egoic manner”

“He is Healing , Hades come on My Love, I am here cheering up for you”.

Hawa walikuwa ni wazungu Jason na Jesie haikueleweka walikuja Tanzania saa ngapi , lakini muda huu walikuwa wakiangalia Pambano kati ya Hades na Ares ambao walikuwa wakipigana juu ya kilele cha Mlima Oldonyo Lengai.

Wananchi wa maeneo ya karibu na eneo hili walichokuwa wakijua ni kwamba mlima huu ulikuwa ukilipuka na Volcano , paisipo kuelewa sio Volcano kama walivyokuwa wakielewa bali kuna mtanange wa wanaojiita miungu, wakipigana ndani ya hilo eneo.

Walionekana wamasai , wakiswaga makundi yao ya Ng`ombe wakielekea mjini huku wakitukana kwa kimasai kwa tukio hilo.

Ndani ya hili eneo kulionekana hali ya mvua , ambayo sio kubwa sana.

Vyombo vya habari viliendelea kutoa habari ya mlipuko wa Mlima Oldonyo Lengai.

“Hades huniwezi tena , kubali kushindwa unipatie Godstone kama ulivyo ahidi kabla ya pmbano”

Aliongea Ares ambaye alikuwa akielea hewani , huku muonekano wake ukiwa ni kama wa shetani , alikuwa akitisha mmno, na ni kama alikua akiungua na moto , kwani alifuka moshi nadhani muonekano wake ndio uliofanya watu kuamini ni volcano.

Roma alikuwa amelala chini huku akiwa amebanwa na jiwe kubwa kwa chini kiasi kwamba alikuwa hana nguvu kabisa , alionekana alikuwa akikosa pumzi kwani alianza kukohoa damu

“Siwezo kukuachia ushinde hata siku moja Ares”Aliongea Hades huku macho yake yakiwa yanatoa mwanga wa njano , mfano wa jua huku akiwa hana mavazi ya aina yoyote ile.

Kwa namna ambayo hapo juu ya kilele palivyokuwa pakioonekana ni Dhahiri kwamba kulikuwa na shughuli pevu iliofanyika usiku kucha , kwani miti ilikuwa imeng`oelewa na mizizi yake , huku pambeni mawe makubwa yakiwa yamesambaa eneo zima na mchanga tifutifu.

Ares alikuwa akitabasamu huku akimwangalia Hades kifedhuli , bwana huyu hakuwa mtanashari , wala hakuonekana kama mtu , alionekana kama Roho ambayo imejitengenezea mwili, kwani mwili wake ulikuwa ukiperushwa na upepo wa eneo hili.

Roma aliekuwa chini ya mjabali , mwili wake uliendelea kupoteza nguvu kwa kiasi kikubwa mno , alionekana ni kama mtu ambaye alikuwa akishindana na mabadiliko ya mwili wake,

Hapana sitakiwi kutumia uwezo wangu wote , ugonjwa wangu unaweza kurudi na nikashindwa kurudi katika hali ya ubinadamu”aliwaza Roma huku mwili ukiendelea kutetema.

“Ares baada ya kuona Hades anazidi kukosa nguvu , aliona sasa ni wakati wa kummaliza kabisa Hades , kwani alianza kujikusanya kama mtu ambaye ana swali , kwanni alikuwa akikusanya mikono yake yote kwa wakati mmoja huku akielekezea kifuani kutoka juu angani na ndani ya dakika chache tu kwa kufanya kitendo hiko kwa Zaidi ya mara Tano , Sehemu ya ambayo alikuwa amelala Roma ilianza kutititia huku ikitengeneza shimo kwenda chini kwa mfumo wa duara .

“Hahahaha.. Hahahahaa…. Hades .. its over for you”aliongea Ares huku akizidi kukusanya mikono yake kwa wakati mmoja kutoka juu kwenda chini yaani ni kama kuna kitu ambacho alikuwa akituma chini.

Kadri alivyokuwa akifanya ndio shimo lilivyozidi kuwa refu huku akielea angani , ndani ya dakika kama kumi na tano , Roma alikuwa amefunikwa na majabali pamoa na mchanga na sasa hakuwa akionekana kabisa.

Baada ya Ares kuona zoezi lake limekamilika , aliridhika na kuacha alichokuwa anakifanya.

“Nitaenda kupindua nyumba yako , mpaka nipate Godstone , nina uhakika lazima litakuwepo ndani ya nyumba yako , haufichagi vitu mbali wewe .. hahahahaha”

Aliongea Ares kwa sauti ya kifedhuli ,m huku akianza kushuka chini taratibu taratibu na hali ikaanza kutulia , lakini sasa , wakati akiendelea kushuka , mara Arhi ilianza kutoa nyufa na mawe ya pembeni yakianza kusogea kwa kasi.

“Inawezekanaje hii?”Alishangaa Ares huku akirudi juu Zaidi akishangaa kile kinachotokea ,

“BOOM’

Kilikuwa ni kiumbe cha ajabu kweli , Roma alikuwa sio Ramoni hapa ni kama jitu la ajabu ambalo lilikuwa na mwili ambao ulikuwa ukimomonyoka kwa kujisafisha mchanga uliokuwa umemfunika , ile sura ambayo alikuwa amezoeleka nayo , haikuwa sura kilikuwa ni kiumbe cha kutisha , chenye mwili mkubwa, Macho ya Roma yalikuwa yakitoa milale miekundu , huku mdomo ukiwaumeongezeka na lips zake kuwa pana chepechepe.

“Ares !!,Ares!! , Ares!!”Ni mngurumo wa juu kabisa ambao kwa mtu wa kawaida ungesema ni ‘Thunder’Mgurumo unaombatana na Radi.

Ilikuwa ni jambo ambalo lilifanyika bila ya kuelewa , kwani wakati Ares akiwa juu akielea huku akionesha hali ya hofu , upande wa chini Hades alionekana kama mtu ambaye anachukua mazoezi ndani ya Gym kwani alianza kutunisha misuli huku mikono yake akiwa ameweka usawa unaolingana na kichwa chake halafu ameinama kidogo , lakini wakati huohuo alikuwa akizunguka kwa mfumo wa nusu duara , yaani alikuwa akitengeneza nyuzi 360.

Ares alishindwa kuelewa nini anakifanya Hades na hapa ndipo alipokosea , kwani ile Hades anamaliza kujizungusha kwa mara ya tano alijikakamua kama atataka kutoa ushuzi.

“Sh***T Anaita Radi”

“BOOM ,Traaa,, taaa!!!”.

Ares alikuwa amechelewa kwani ile anataka kuhama Radi ilimgonga palepale na kumfikisha chini , lakini radi hii haikuwa ile ya kupiga mara moja na kupotea hii ilikuwa mfululizo yaani, na Hades alikuwa akiiongoza , yaani Ares akienda kushoto inamfauta huko huko , akienda kulia inamfuata upande huo huo.

Lilikuwa ni tukio la kutisha na muda huo huo mvua ilianza kunyesha na haikuwa mvua ndogo , ilikuwa mvua ambayo iliambatana na mawe.

****

“Ameshinda, Hades ameshinda aliongea Jessie kwa furaha na kumfanya Jasoni amwangalie mrembo huyu.

“Kwa hio unataka kuniacha kisa ameshinda”Aliongea Jasoni huku akiwamgalia Jesie.

“Hades akiniomba Kitumbua siwezi kumkatalia, huo uwezo wa kumkatalia naota wapi Jasoni”Aliongea Jesie na kumfanya Jasoni akasirike.

Ndani ya dakika chache tu ,Jesie alikuwa amekunjwa kisawa sawa na Jasoni huku akishindiliwa mwichi na Jasoni kwa mtindo wa mbuzi kagoma , huku akilambishwa vibao.

“Niambie upo upande wa Hades tena?

“Arrgh..Aiissss”

“Paaa!!”

“Jason..iii”

Wakati Jasoni anaendelea kumnyanyasa Jesie mara simu yake ilianza kuita na alichukua ipod iliokuwa kwenye ‘Bedside’ na kuweka sikioni.

“Misheni imemelizika mnatakiwa kurudi kambini”Ilikuwa ni sauti ya kike iliokwenye Amri.

“Paah!”

“Aarrffh…Jasionii!!!”

“F***ck you Jason , I need you two, to return now”Sauti ilikoroma , ilionesha kukasirishwa na kitendo cha Jason na Jesie walichokuwa wakifanya na upande wa pili mwanamke huyo alionekana kwenye hali flani hivi kama ya wivu.

****

Ni ndani ya kambi ya jeshi la kujenga taifa ya Oljoro , walionekana wakuu wa jeshi la Tanzania wakiwa wameketi kwenye meza kubwa hapo ndani , huku sura zao zikionesha kama ni watu ambao walikuwa wamedhirai na sasa walikuwa wamepata fahamu.

Mtu pekee ambaye alikuwa kwenye hali ya ukawaida wake alikuwa ni Jeneral Yang.

“Okey! Maafande nadhani mpaka sasa tushaona uwezo wa Hades”Aliongea Afande Yang na kuwafanya mabwana hawa watingishe vichwa bila ya kuongea.

“Sasa jambo ambalo limenileta hapa Tanzania ni hili”Aliongea huku akimwangalia mkuu wa majeshi.

“Nataka mtengeneze kikundi cha wanajeshi wenye uzoefu wa hali ya juu ambacho kitakuwa macho, kitakuwa na taarifa zote za Hades anayoyafanya kila siku, masalani kwa upande wa mambo yote yanayohusiana na Godstone”Aliongea Afande Yang

“Kwa sasa litakuwa jukumu la Tanzania kuhakikisha Jiwe la Kimungu haliwafiki kwenye mikono ya watu wabaya , ni kizungumzia watu ambao hawana nia njema na dunia hii , endapo hili likifanikiwa inaweza kuwa mwisho wa dunia na tunaweza kumshindwa adui hata kama tutaungana”Aliongea Afande huyu kwa msisitizo na kumfanya General asimame na kisha akapiga saluti ya ishara ya kuliwakilisha kitaifa kwa ombi hilo.

“Mimi Afande Gambino Tozo ninalichukua ombi kwa niaba ya taifa , na nitahakikisha tunalifanyia kazi kwa maslahi ya taifa na dunia kwa ujumla”Aliongea Afande Tozo na Afande Yang na yeye akapiga saluti ya ishara ya makubaliano.
 
SEHEMU YA 84

TEXAS-DALLAS

11 YEARS AGO(MIAKA KUMI NA MOJA ILIOPITA)​

Ni tarehe ishirini na tatu kuamkia ishirini na nne mwezi wa kumi na mbili ndani ya jimbo la Texasi jijjini Dallas , ndani ya makazi ya watu, sehemu inayofahamika kwa jina la Greenville Avenue muda wa saa sita usiku.

Mwanamama wa umri wa miaka arobaini hivi aliekuwa akifahamika kwa jina la Mary , alionekana akishituka kutoka usingizini , baada ya kulala muda mrefu, mwanamama huyu baada ya kishituka alijikuta akipapasa mkono wake upande wa kushoto pasipo kugeuka kwa nia ya kutafuta mwili wa mime wake Phill, lakini mwanamama huyu baada ya kupapasa juu na chini mkono wake haukuambulia kitu na hii ilimfanya anyanyuke na kukaa kitako na kugeuza macho yake kulia, na hapo alijikuta akitoa shuka taratibu baada ya kumuona mume wake aliekuwa amepitiwa na usingizi katika meza yake ya kusomea huku pembeni ilionekana Printer ambayo na yenyewe ilionekana kuwa imewashwa pamoja na tarakishi.

Bi Mary alionekana kumuonea huruma mume wake kwa kitendo cha kupotelea usingizi akiwa mezani anasoma,mwanamama huuyu ambaye alikuwa amevalia nguo za kulalia alitembea kusogea upande ambao mume wake amelala kwenye meza ,na kabla hajamgusa ili aamke , mara Printer ilianza kutoa mlio wa sauti ya Kuprint karatasi.

Bi Mary alijikuta akighairisha zoezi lake na kisha kuchukua baadhi ya karatasi ambazo zilikuwa zikitemwa na Printer hio, karatasi ya kwanza ndio iliomshangaza mwanamama huyu:

Kwanza kabisa karatasi hio ilikuwa na ‘watermark’ ya neno ‘Confidential’ , ilionekana ilikuwa ni nyaraka ya siri ambayo Mume wake Phill alikuwa akiisubiria kiasi kwamba alijikuta akisinzia kwenye meza.

Bi Mary alijikuta akianza kutetemeka mikono kadiri alivyokuwa akisoma karatasi hio , huku mume wake akiwa bado amelala , mwana mama huyu alielewa kabisa taarifa hio ni nyeti , lakini kutokana na taarifa yenyewe kumshangaza alijikuta akiendelea kusoma, alimaliza katatasi ya kwanza akachukua nyingine akaimaliza , huku kila karatasi anayosoma ikimuacha mdomo wazi , alisoma nukta hadi nukta mwanamama huyu ambaye kazi yake kubwa ni kuuza maua.

Baada ya Bi Mary kumaliza kusoma , alijikuta mwili wake ukikosa nguvu , alichukua karatasi alizokuwa ameshikilia na akazirudisha kwenye mdomo wa Printer na baada ya kumaliza kusoma , alijikuta hata kile ambacho kimemsogeza kwenye meza aliolala mume wake Phill ,alisahau m alijongea na kurudi kwenye kitanda na kisha akajilaza na kujifunika shuka.

“Evidence regarding killing of Professor Banos and M-Airline Plane dissapearencce”

“Detailed Plan to Eliminate the World coming Enemy”

“Project LADO success Rate”

“Twelve Greek God`s to faight against the Wold Coming Enemy”

Hivyo ndio vichwa vya habari ambavyo Bi Mary alikuwa amevisoma na alikuwa akivifikiria akiwa ndani ya Blanketi huku machozi yakiwa yameujaza uso wake, hakuwamini kabisa kwa kile alichokiona.

Kulivyokucha Mary alijitahidi kuwa wa kawaida mbele ya mume wake amaye tayari alikuwa amevaa suti kwa ajili ya kuelekea kazini , ambayo Bi Mary siku zote alikuwa akijua mume wake alikuwa ni Mhandisi ndani ya kampuni ya kutengeneza magreda ya kuchimbia barabara.

Bi Mary aliwaangalia watoto wake watatu kwa namna ya kuwaonea huruma , na kisha akamgeukia mume wake Phill ambaye alionekana kutabasamu muda wote.

“Mary Yo seem to be off today , what the matter , Tomorrow is Christmas , why you are not happy like everyone else, Come on tell me”

“No Phill , I am fine ,Why?”

“Its nothing Mary if you are fine , then it`s okay , I will be off to work now”Aliongea bwana huyu na kisha alimsogelea mke wake na kumbusu shavuni na kisha akahamia kwa watoto wake wote ambao mmoja wa kike alikuwa na miaka kumi na mbili mwingine kumi na mmoja mine.

Baada ya dakika kadhaa za Phili kutoweka kwenye macho ya Mary , alikimbilia chumbani kwake na kuanza kutafuta zile karatasi sehemu ambazo alikuwa akiamini atazipata , lakini hakuweza kuzipata.

“Atakuwa ameenda nazo”Alijiongelesha huku akijilaumu kwanini hakupiga picha

“Pastor Edwardo , I have something very important to discuss with you”Aliongea akimaanisha kwamba anajambo la kuongea na mchungaji aliemtaja kwa jina la Edwardo na hii ni baada ya kusalimiana.

“Unaonaje mara baada ya mkesha wa leo , litakuwa jambo zuri , maana mchana wa leo ratiba zimebanana”Ilisikika sauti upande wa pili na Mary akakubaliana na Pastor.

“Sijui kama ninachofanya ni sahihi , lakini naamini ni vyema nikiongea na kiongozi wa dini , Phill sio wa kunidanganya mimi kwa Zaidi ya miaka ishirini tokea tuone, he is undercover agent with Zeros Organisation all this time?, Damn you Phill”Alijiongelesha mwanamama huyu huku akianza kutoa machozi ,alionekana taarifa ya jana usiku aliosoma ilikuwa ni kubwa kwake na yenye kumuumiza.

Usiku wa saa sita hivi kwenda saa saba za usiku ndipo tukio la kutisha lilipotokea na mkurdish Afshar alivyofanya yake ya kuwarushia risasi waumini wa kanisa la The Forgivven.

Upande wa Pastor na Mary walikufa wakiwa ndani ya chumba ambacho kilikuwa kinatumiaka kama ofisi ya mchungaji ndani ya kanisa hili la The Forgiveen.

Watoto watatu wote wa bwana Phill mzungu walikufa ndani ya tukio hilo wakiwa pamoja na mama yao.

Nini kilitokea , ni siri gani iliop juu ya mpango LADO , Nyaraka ya siri aliosoma Mary inamaanisha nini juu ya Adui wa ulimwengu anaekiuja, kwanini The God`s ndio inatakiw akupambana na Adui utaelewa kadiri tunavyosonga.

*****

Ni jumamosi muda wa saa moja kamili Mrembo Rose mmiliki wa kundi la Tembo alionekana kuwa ni mwenye wasiwasi sana , huku akiwa ndani ya gari iliokuwa ikielekea Kisarawe.

Mwanadada huyu , jambo ambalo lilimfanya kuwa na wasiwasi ni kutokupatikana kwa Roma hewani, kwani alijaribu kwa Zaidi ya mara kumi kwa muda tofauti , lakini bado hakuweza kumpata hewani.

Ile hali ya kujiamini aliokuwa nayo Rose , ilikuwa imepotea , alikuwa akijiamini kwa ajili ya mpango wake kutokana na kwamba alikuwa na uhakika wa Roma kuwepo , lakini sasa mtu ambaye alimuahidi kwa ajili ya kwenda nae Kisarawe kwenye sherehe iliokuwa ikihusisha maadui zake ndani ya biashara ya madawa ya kulevya hakuwa akipatikana.

“Hubby Come on!,Where are you?” Mwanamke huyu alikuwa akipiga piga simu yake mapajani huku akiwa ni mwenye kujiuliza Roma yuko wapi , alikuwa akipata hisia ambazo ni kama za mwanamke ambaye alikuwa ametelekezwa.

“Boss uko sawa?”Aliuliza Zonga ambaye muda huu alikuwa akiendesha gari.

“Niko sawa Zonga”

“Bosi usiwe na wasiwasi , mpango wetu lazima ufanikiwe , vijana tuliowapandikiza ndani ya kundi la Fupa Faru ni mzuri sana na Situ hawezi kuchomoka”Aliongea Zonga huku akiwa ni mwenye kujiamini , lakini licha ya hivyo kwa Rose bado hakuwa akijiamini.

Masaa kadhaa nyuma alikuwa akijiamini pale alipokuwa akikumbuka kuwa Roma ataongozana nae kwenye sherehe hio, lakini sasa kule kujiamini kulikuwa kumepungua kwa asilimia sitini.

Ndani ya dakika Arobaini na tano tu , walikuwa wakiingia ndani ya eneo la Ngekewa , ambapo ndipo linapatikana jumba lake la kifahari ambalo kwa sasa lilikuwa chini ya baba yake Situ mmiliki wa kundi la Fupa Faru.

Zonga alimfungulia mlango bosi wake mara baada ya kufika getini muda huu wa usiku wa saa mbili , na walinzi wa kundi la Fupa Faru , waliwapapasa kuhakikisha kama hawana siraha na baada ya hapo waliruhusiwa kuingia ndani.

Sherehe ilionekana kufanyikia eneo la nje ya nyumba kwenye bustani , ndani ya jumba hili ambalo kwa muonekano wake utadhani ni kasri , lilikuwa ni jumba kubwa ambalo ungeambiwa aliekuwa mmiliki ni Rose ungeshangaa.

Rose aliangalia watu waliokuwepo hapa ndani , alikagua mazingira yote na alijikuta akiridhika mara baada ya kuona baadhi ya vijana wake wakiwa ni walinzi nay eye mwenyewe alishangaa , kwani vijana wake pekee ndio walionekana kuwa walinzi licha ya mpango wao, alikuwa akiamini watakuwa walinzi mchanganyiko na wa kundi la Fupa Faru.

Unajua Situ alikuwa na vijana wengi sana , ambao walikuwa kwenye kundi lake la biashara na hakuwa akiwajua wote hivyo hii ilikuwa rahisi kwa rose kuingiza kikosi chake kwa siri kwa kuua baadhi ya vijana wa kundi la Fupa Faru.

Rose alikuwa amependeza sana usiku huu , alionekana kuwa kama malkia na hapa ndani licha ya kwamba walikuwa wapo wanawake warembo , lakini kwa Rose hakuna ambaye alikuwa akimfikia , ukiachana na uzuri wa Rose pia vazi alilokuwa amevaa usiku huu , lilikuwa sio la kawaida na baadhi ya wanawake walimwangalia na kujiuliza ni mwanamitindo gani ameweza kumtengenezea gauni hilo Rose , kwani lilikuwa na uzuri usio wa kawaida , lakini pia lilionekana kuwa na gharama kubwa.

Rose alijikuta akijisikia faraja baada ya kuona watu walivyhokuwa wakimwangalia kwa namna ya kumhusudu , wanaume kwa wanawake.

Zonga nae hakuwa nyuma, alikuwa amependeza na suti yake nyeusi , huku akijirembesha na kijiua kilichokuwa kwenye mfuko wa koti cha rangi nyekundu.

“Mungu nisaidie jaribio hili lifanikiwe , sijui ni nini kimemkuta Roma , najua ananipenda na chochote kinachoendelea naomba Mungu amlinde”Aliongea mwanadada huyu na haikueleweka alikuwa akiomba Mungu gani amlinde Roma kwani ni siku nyingi sana alikuwa ashaachana na mambo ya dini.

Wakati akiwa amesimama huku akisogea upande wa walipo wageni , mara alisogelewa na muhudumu wa kiume alievalia suruali nyeusi pamoja na shati jupe na kikofia.

“Mrembo umependeza sana leo , unaonaje ukitumia kinywaji ambacho nimekiandaa kwa ajili yako Usiku huu”Aliongea kwa sauti ya chini kidogo na kumfanya Rose atoe macho.

“Romaa…!”Rose hakuamini mtu aliekuwa mbele yake ni Mwanaume anaempenda m Roma, alitamani amrudikie.
 
SEHEMU YA 85

Siku ya jumamosi Mchana , wakati wananchi wengi wakiendelea kufuatilia taarifa iliokuwa ikihusisha kulipika kwa volcano ndani ya mlima Oldonyo Lengai Mkoani Arusha , upande mwingine ndani ya jiji la Dar ndani ya makao makuu ya Benki kubwa ya Kibiashara ,maarufu iliokuwa ikifahamika kwa jina la Chatex benki, ndani ya ofisi kubwa yenye samani za bei kubwa, anaonekana CEO Imani Maseko akiwa ameketi kwenye kiti chake cha mzunguko akiendelea na majukumu yake akiwa kwenye umakini mkubwa.

Imani Maseko ni moja ya vijana wenye mafanikio makubwa sana ndani ya Tanzania kutokana na uchapakazi wake uliotukuka , moja ya jambo ambalo linamfanya kijana huyu kuwa maarufu ni namna ambavyo aliweza kuifanya Benki ya Chetex kuwa benki kubwa ya kibiashara nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Wakati Imani Maseko anapandishwa cheo na kupewa majukumu kamili ya kuwa Mkurugenzi mtendaji wa benki ya Chatex , benki hii ilikuwa na mtaji wa Bilioni ishirini pekee na pia ilikuwa sio yenye msingi mzuri wa kibiashaara kwa wateja wengi , lakini jambo la kushangaza ni baada ya miaka minne tokea Imani Maseko akabidhiwe uongozi wa juu wa Benki hii mtaji wake kuongezeka kutokana na faida kufikia Bilioni mia moja , haya ndio mafanikio makubwa ambayo yameweka historia katika biashara ya miamala na uwekezaji kwa upande wa Kibenki ndani ya taifa la Tanzania na Afika Mashariki kwa ujumla.

Imani Maseko ni kijana mrefu wa saizi ya kati , mwenye rangi mchanganyiko ya Mzungu na Muafrika, alikuwa ni kijana Handsome sana ambaye wanawake wengi walikuwa wakimhusudu kuwa nae katika mahusiano ukilinganisha pia na mafanikio yake,Imani tokea aachane na mke wake Nairathi mwanamke mrembo wa kiarabu maarufu hakuwahi tena kuonekana na mwanamke yoyote na pia hakuwa na mtoto.

Sasa wakati Imani Maseko wakati akiendelea na majukumu yake ya kazi kama kawaida , mlango wake ulisukumwa na kumfanya kijana huyu ainue macho yake na kuangalia ni nani ambaye amefungua mlango wake , lakini mara baada ya kumuona mzee mmoja wa miaka kama sitini hivi wa Kizungu, alijikuta akionyesha hali ya kutofurahia uwepo wa mtu huyu ndani ya ofisi yake, lakini mwanaume huyu mtu mzima hakujali na mabadiliko hayo , aliingia na kwenda kuketi kwenye masofa.

“Kama umeshindwa kuniheshimu kama baba yako , unaonaje ukinipa heshima kama waziri wa Biashara na Viwanda?”Aliongea mzee huyu kwa kiaswahili chake ambacho hakijanyooka sana kutokana na rafudhi yake.

“Karibu sana Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara”Aliongea Imani huku awamu hii akiweka tabasamu bandia usoni.

“Hivi Imani mpaka lini utakuwa ni mwenye kunipotezea na kutoniheshimu kama baba yako na kuacha tabia yako chafu”

“Mzee nadhani unajua sababu ya haya yote yanayoendelea kati yangu na wewe , hivyo usilalamike sana kwani wewe ndio unanifanya niwe hivi”

“Niachie upumbavu wako mimi Imani , Hilo swala ambalo unataka Baraka kutoka kwangu nakuambia sahau, labda kama niwe nimekufa, licha ya mimi kuwa Waziri na Mbunge lakini pia mimi nafahamika kama Mchungaji Maseko Wright , siwezi kukubaliana na ujinga ambao unataka”Aliongea mzee huyu huku akiwa ni mwenye kuonesha hasira zake waziwazi lakini kwa Imani hakuonesha kuchukizwa na maneno ya baba yake , alionekana kuyazoea.

“Baba hivi unajua wewe ni mnafiki sana , ningetamani Watanzannia wangejua sura yako halisi, ila kwakuwa wewe ni baba yangu nitaendelea kukutunzia siri ,Anyway nadhani haujaja kwenye ofisi yangu kwa ajili ya kulalamika”Aliongea kijana Imani , na kwa namna ambavyo wawili hawa walivyokuwa wakiendeleza mazungumzo yao usingedhania walikuwa ni kitu na baba yake.

“Nimekuja kukuwekea msisitizo juu ya kuhudhuria sherehe ya kundi la Fupa Faru usiku wa leo, hutakiwi kukosa ,Nimekuja mwenywe badala ya kukupigia simu ili uone umuhimu wa hili jambo kwako na kwa hii biashara pia”Aliongea Waziri Maseko.

“Okey nitafika , kama ndio unavyotaka nifanye , nimekuwa ni mwenye kukutii licha ya kwamba nakuchukia”Aliongea kijana huyu lakini kwa Mzee Maseko hakujali.

“Muda ni saa mbili kamili”Aliongea na ki.sha akanyanyuka na kutoka ndani ya ofisi hii.

Dakika chache tokea atoke WaziriMaseko , kijana Imani alinyanyuka na kisha akasogelea dirisha na akasogeza pazia pembeni ndani ya ghorifa hili na kisha akaachia tabasamu.

“I am going to meet with that person for the first time , I have to make good impression,Dady I am Sorry I know what you are planning but too bad I am not man of type you want”Aliwaza Imani akimaanisha kwamba anakwenda kukutana na mtu asiefahamika , huku akipanga kwenda kumfanya mtu huyo apendezwe nae kwa mara ya kwanza lakini wakati huo huo akimuomba baba yake msamaha kwamba yeye sio aina ya mtoto anaemtaka.

*****

Kwa muonekano wa Roma ni kama hakukuwa na kitu ambacho kilitokea siku moja na masaa yaliopita , hakuonesha dalili yoyote ya mtu ambaye alikuwa akipigana na Ares , alikuwa Roma kama Roma aliezoelekea kwenye macho ya mwanadada Rose.

Mwanamke siku zote ni mwenye kuguswa na matendo ambayo hategemei kufanyiwa lakini yenye kufurahisha, na hii ndio hali aliokuwa nayo mrembo Rose , kitendo cha kumuona Roma akiwa ndani ya eneo hili pasipo kutegemea kilimgusa mno kiasi kwamba machozi yalianza kujitengeneza ndani ya mboni za macho yake.

Roma alimvuta Zonga mpaka upande wa bafuni na kisha akamuamuru kuvua nguo alizokuja nazo na Zonga alishindwa kukataa amri kutoka kwa Roma kutokana na mahusiano yake na bosi wake.

Dakika chache mbele Roma alikuwa amependeza akiwa na suti yake huku Zonga akiwa na mavazi ya wafanyakazi wa jumba hili, akiendelea na swala zima la kuhudumia wageni , jambo lililomfanya Rose amwangalie Roma machoni na kutabasamu.

Roma na Rose waliungana kama ‘Couple’ na kuanza kusalimia wageni waliokuwa hapo ndani,Situ aliekuwa akisalimiana na baadhi ya wageni alijjikuta akikasirishwa na uwepo wa Roma , na kwa upande wa Roma alilitambua hilo ila hakujali, na tena baada ya kumuona namna baba yake Rose alivyokasirishwa na uwepo wake , alimwambia Rose wamsogelee baba yake kwa ajili ya kumsalimia.

“Rose huyu kibwengo umekuja nae kufanya nini? , ushashau nilichokuambia kuhusu hii shughuli ni kwa ajili ya kumuona mumeo mtarajiwa niliekuchagulia mimi baba yako?”Aliongea Situ huku akionesha sura yenye kukasirika.

“Asante kwa kunijali Situ , ila swala la mimi kuchagua mume ni juu yangu na nimekuja hapa unioneshe huyo mwanaume ili nimkatae mbele yako,lakini pia kumtambulisha mwanaume ninaempenda”Aliongea Rose na kumfanya Situ atamani kumchapa vibao , lakini wakati huo huo walisogelewa na mtu ambae hata Rose mweyewe alishangazwa na uwepo wake hapa ndani, alikuwa ni waziri wa Viwanda na biashara bwana Maseko Wright, ambaye pia ni mchungaji wa kanisa moja maarufu na pia Mbunge.

Kilichomshangaza Rose sio uwepo wa Maseko hapa ndani kama Waziri , Mbunge au Mchungaji , ila kilichomshangaza ni kwamba Maseko alikuwa pia ni mfanyabiashara mwenye nguvu sana ndani ya biashara ya madawa ya kulevya nchini , kutokana na kuwa mmiliki wa Benki ya Chatex , Benki ambayo ilikuwa ikipitisha miamala yote ya fedha za wafanyabiashara wa madawa ya kulevya nchini kwa njia ambazo hazikuwa halali(Money Laundaring) yaani utakatishaji jambo ambalo linafanya wafanya biashara wengi kumheshimu na kuhitaji koneksheni na huyu Waziri.

“Rose kutana na baba mkwe wako mtarajiwa,Mchungaji Maseko”Aliongea Situ na kumfanya Rose kushangaa , maana alikuwa anajua kuwa Maseko alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume aliekuwa akifahamika kwa jina la Imani ambaye alikuwa ni CEO wa benkii ya Chatex.

Situ alijikuta akiwa ni mwenye kutabasamu mara baada ya kuona mshangao ambao Rose alikuwa nao , alikuwa akijua Rose alikuwa akifahamu nguvu ya Maseko katika biashara yao ya madawa ya kulevya.

“Nimefurahi kukutana na wewe Mheshimiwa kwa mara ya kwanza”

“Hahaha…!,Situ siawahi kufikiria kama una mtoto mrembo kiasi hiki, hakika nimemkubali , Rose na mimi pia nimefurahi kukutana na wewe kwa mara ya kwanza na huu ni mwanzo tu wa kufahamiana kwetu”Aliongea Mchungaji Maseko na kumfanya Rose atabasamu.

Muda huu Roma alikuwa pembeni akisikiliza kila neno na hakutaka kuingilia maongezi hayo , ukweli Roma alifika hapo kwa ajili ya ulinzi tu kwa Rose, jambo lolote baya lisije likamkuta kama yaliomtokea Mtwara siku chache zilizopita mpaka kupelekea kupigwa risasi.

“Waziri bado kijana wako sijamuona?”Aliuliza Situ na kumfanya mchungaji Maseko afikirie kidogo ,huku akimsema vibaya Imani kwenye moyo wake , kwa kitendo cha kutoonekana mpaka muda huo.

“Atafika muda si mrefu , kijana wangu ni mwenye majukumu mengi sana , ila amenitaarifu yupo njiani”Aliongea Maseko na kumfanya Situ mwili umsisimke.

Ukweli ni kwamba Situ alikuwa na mipango miwili katika kichwa chake , jambo la kwanza alitaka kuunganisha undugu kati ya familia ya Maseko na ya kwake ili iwe rahisi kwa biashara zake za madawa ya kulevya kufanikiwa ndani ya jiji hili la Dar na Pwani, ukizingatia ndio kwanza alikuwa akiweka makazi yake, hivyo alikuwa ni mwenye kuhitaji konekesheni nyingi ili kujiimarisha , lakini pia kwa wakati huohuo alikuwa na mpango wa kumfanya Rose awe chini yake na kama akikataa kuwa chini yake, amuue kabisa licha ya kwamba ni mtoto wake.

Sherehe ilifana kutokana na uwepo wa baadhi ya wanamuziki waliokuwa wakitumbuiza ndani ya eneo hili , lakini pia uwepo wa wafanyakazi wengi wa vitengo mbalimbali kutoka serikalini ilifanya sherehe hii ya kundi la Fupa Faru kufana sana , walikuwepo wanawake na wanaume wasichana kwa wavulana, na sio kama kila mmoja aliekuwa ndanin ya hili eneo alikuwa akifanya biashara ya madawa ya kulevya Situ alialika baadhi ya watu kwa ajili ya kuwafanya watu wake kutoka serikalini kwa kuwapitishia bahasaha ili biashara yake isikutane na migogoro mingi , na hii ni kawaida sana kwa wafanyabiashara hawa wa madawa ya kulevya , ukitaka biashara yako iwe imara kitu cha kwanza ni kujenga koneksheni na wanasiasa na pia vyombo vya usalama nchini kama vile polisi na maafisa usalama, na ndio maana kati ya wageni waliokuwepo , pia walikuwepo polisi wa vyeo tofauti tofuati na wote kabla ya kuja kwenye sherehe hii walipitishiwa bahasha.

Rose mwenyewe alikuwa akilielewa hilo na hata kwake pia alikuwa na watu wake katika ulingo wa siasa , lakini pia katika vyombo vya usalama na hii yote iliwezekana kutokana na kwamba alikuwa akilipa kamisheni ya faida yake yote kwa The Don.

The Don licha ya kwamba hakuwa akifahamika lakini yeye ni kama ndio mtawala wa biashara yote ya madawa ya kulevya nchini na Afika Mashariki kwa ujumla wake, na hii alifanya kwa urahisi sana , kwani mara nyingi kwa kila mfanyabiashara ndani ya taifa hili akitaka kuuza madawa ya kulevya nchini lazima asainishwe mkataba wa kuhakikisha anatoa asilimia arobaini ya fada kama kamisheni na kuingiza kwa The Don , huku The Don yeye akiwa ni mwenye kuhakikisha biashara yako haikutani na vikwazo vya aina yoyote kutokana na kwamba yeye mwenyewe alijiita ndio mmiliki wa wanasiasa wote nchini A.k.a The King Maker s lakini pia alikuwa na konekesheni na wakuu wa vyombo vya usalama,kwa hio ukiwa upo upande mbaya na The Don biashara yako ndani ya Tanzania au Afika mashariki kwa ujumla haiwezi kufanyika.

Mheshimiwa Waziri hakuwa na habari kabisa na Roma kwanza hakuwa akimjua kijana huyu , lakini pia alimuona kama mlinzi wa Rose hivyo hakutaka sana kumjua Zaidi , kwani pia alikuwa akisikiliza maneno ya Situ Zaidi.

Wawili hawa walionekana wapo tayari kuwafanya watoto wao kuungana na hatimae kuoana.

Naam ilikuwa imepita Zaidi ya nusu saa hivi wakati Situ na Mchungaji Maseko kusalimiana na Rose ,upande wa getini aliingia mgeni ambaye aliwafanya watu wote washangazwe na aina ya vazi ambalo mtu huyu alikuwa amevaa , lilikuwa ni vazi la kike ambalo kwa asilimia kubwa Rose alikuwa amepitwa pakubwa kwa muonekano mzuti wa kuvutia wa vazi hilo.

Lilikuwa ni gauni refu rangi nyekundu muundo wa kitenge , lenye maua mua flani hivi ya Rangi nyeupe , huku likiwa na mkanda uliiopita pegani kwa mfumo wa lubega na kuja kipitia kwapani , halafu mbele yake kukiwa na ua la kutengeneza muundo wa ‘Sunflower ‘, haikueleweka staili hio ya vazi ilikuwa ikiitwaje ,lakini pia ni kampuni gani ilikuwa imetengeneza vazi hilo.

Sasa Vazi hili lilipendeza Zaidi kutokana na mwanamke ambaye alikuwa akionekana mbele ya macho ya watu hawa ,Roma mwenyewe alijikuta akipagawa kwa muonekano wa mrembo alieingia hapo ndani na sio kwake tu ,Mzee Maseko pamoja na Situ wote macho yalikuwa kwa Mwanamke mrembo.

“What Alluring Queen of Night?”Aliongea bwana mmoja aliekuwa nyuma ya Rose na Roma na kumfanya Rose ahisi wvu kw anamna mwanaume huyo alivyomsifia mwanamke aliekuwa akiingia.

Mrembo yule baada ya kuingia moja kwa moja alienda upande wa jukwaa ambalo wapo wanamuziki waliokuwa wakitumbuiza hapa ndani ili kuifanya sherehe hii kuvutia.

Haikueleweka mwanamke huyu alikuwa akitaka kufanya nini , lakini kutokana na uzuri wake , kila mtu alitulia kuona ni kipi kinaenda kutokea, alitembea kama vile yupo kwenye shindano la mavazi, haikuonekana kasoro yoyote kwa mwanamke mrembo huyu ambaye amechukua macho ya kila mtu hapa ndani.

“Ladies And Gentlemen goodnight”

Ilikuwa ni sauti iliomvutia kila mmoja hapa ndani akiwemo mwamba Roma Ramoni na watu wote waliitkia.

“I know all of you are puzzled with my late suddenly Appearance, which is why I decided to come Strainght here on Stage to introduce myself so as to save time and also to share Story of my life”

“Najua wote hapa mmeshangazwa na kuonekana kwangu kwa ghalfa kwa namna ya kuchelewa ndio maana nikaona ni vyema kuja moja kwa moja mpaka kwenye steji kwa ajili ya kujitambulisha lakini pia kuwasimulia stori ya maisha yangu”

Aliongea na kisha akapozi kidogo na kuanza kuangalia mtu mmoa mmoja , Alianza kwa Roma ambaye alimwangalia kwa sekunde kama sitini hivi , jambo ambalo lilimfanya Rose mapigo ya moyo yapige kwa nguvu kwa kuogopa , kwani kitendo cha mrembo aliekuwa kweye steji kumkodolea macho Roma lilikuwa ni tishio kwake la kupokonywa mwanaume.

Mrembo yule mara baada ya kumwangalia Roma alihamia kwa mzee Maseko na kumwangalia kwa dakika chache , jambo ambalo kwa mzee huyu lilimfanya ashituke baada ya kukutanisha macho na mrembo aliekuwa kwenye steji , kwani ni kama macho yake aliyafahamu.

“Naomba isiwe yeye”Aliwaza Mzee Maseko akiwa ni mwenye kuwa na wasiwasi mkubwa.
 
SEHEMU YA 86

Mrembo yule baada ya kunyamaza kwa dakika mbili , huku akifanya hali ya hewa kuwa tulivu alianza kuongea.

“Chaneli ndio jina langu ambalo nalipenda sana , na kutokana na kuitwa Chaneli nimeamua kuchagua aina hili la Vazi kutoka kwa kampuni maarufu duniani ifahamikayo kwa jina la Chaneli”aliongea na kuwafanya wanawake hapa waliokuwa wakipenda kuvaa kuelewa sasa vazi zuri alilokuwa amevaa mrembo huyu ni kutoka kwa kampuni maarufu ya Chaneli.

“Kama nilivyosema, jina langu ni Chaneli Maseko , ni mtoto wa pekee wa kike wa mchungaji Maseko Wright “Watu kila mmoja alitoa macho na kumgeukia mchungaji Maseko ambaye alikuwa amekaa kama vile sanamu akiwa ametumbua macho.

“Najua wengi wenu hapa mmeshangaa na pia najua ni mara yenu ya kwanza kusikia jina langu, ila nitajitambulisha kwa jina langu ambalo watu wengi wanalifahamu ,ili nikianza stori ya maisha yangu kila mtu apate kunielewa”Kila mtu alipata mushikeli wa kutaka kujua ni nini mrembo ambaye yupo jukwaani anataka kuongea.

“Jina langu maarufu nafahamika kama Imani Maseko”

“Khaaa….!!!!”Watu wote walijikuta wakitoa sauti hio kwa kushangaa na muda huu watu walikuwa washatoa simu zao kurekodi kila kitu.

“Ndio mmeshangaa na pia mmekuwa sio wenye kuamini lakini mimi ni yule mfanyabiashara maarufu ambaye watanzania wengi wananifahamu kama mtu mwenye mafanikio … lakini licha ya kuwa na mafanikio hayo nimekuwa sio mwenye furaha katika maisha yangu yote ,na hii ndio imenifanya leo kuja mahali hapa na kutaka kuongea stori hii..”

Alijifuta machozi kwa namna ya kike kabisa na kufanya watu waliokuwa wakimjua Imanni Maseko wasiwe ni wenye kuamini kama aliekuwa kwenye Steji ni yeye mwenyewe, kila mmoja alikuwa na maswali , kuna waliokuwa wakijiuliza kama yeye ndie, ndevu ziko wapi , lakini pia kuna waliokuwa wakijiuliza kama yeye ndie, Sauti nzito ambayo wlaikuwa waiiskikia mara nyingi imeenda wapi , ki ujumla kila mtu alikuwa na lake kichwani ambalo halikuwa na majibu ambayo walitamani wakati huo.

Waziri na Mchungaji Maseko alikuwa kwenye hali mbaya kweli , alionekana lile jambo ambalo alikuwa akichukia kwa maisha yake yote leo limekuwa hadharani, lakini kwa wakati huu hakuna ambaye alimjali hata Situ ambaye dakika chache mbele alikuwa ni mwenye kujitamba kama amemtafutia mtoto wake Rose mchumba, saa hii alikuwa amesogea kiti cha mbele ili athibitishe kama ni kweli , mchumba aliemtafutia mwanae ndio huyo mwenye sauti nyorroro ya kupagawisha , waswahili wanaita ya kumtoa nyoka pangoni.

“Najua mpo kwenye maswali mengi ya kujiuliza kwa sasa ,lakini naomba niwajibu kwa neno moja tu ,Mimi nilizaliwa nikiwa na jinsia mbili”

“Khaaaa….!!!!”

“Ndio nimezaliwa na jinsia mbili na hili ni jambo ambalo mama yangu pekee ndio mwenye kulifahamu,Licha ya kuwa na jinsia Mbili, kwangu ni kama Mungu amenipa Adhabu ya kunipa muonekano ambao hauendani na mimi”aliongea kwa punguza sauti.

Upande wa Maseko alikuwa ashazimia muda mrefu tu kwenye meza yake , lakini hakukuwa na mtu ambaye amegundua kwani wote walikuwa wamesimama kwa mbele yake na macho yao yote yalikuwa kwenye Steji.

“Mungu kanipa sura ya kiume ilihali sehemu zangu za Siri zenye nguvu ni za kike , licha ya kwamba nina kiungo kikubwa tu cha kiume”

Watu walikuwa na mushikeli kiasi kwamba walitamani Imani Maseko avue nguo wathibitishe kwa macho yao , ni kama hawakuwa wakiamini amini hivi ,hata Roma mwenywe na umalaya wake hajawahi kukutana na mwanamke au mwanaume mwenye jinsia mbili.

“Nimeishi kwa mateso mengi na ndio maana leo nataka kuiambia dunia mimi sio mwanaume bali ni mwanamke ninaefahamika kwa jina la Chaneli Maseko , the Only child and Daughter of Pastor Maseko Wright na hii yote nimefanya kutokana na kwamba sitaki kumkosa mwanaume ambaye nimetokea kumpenda kwa miaka mingi”

“Khaaa…!!”

Hata Rose mwenyewe alikuwa ameshangazwa na jambo hilo , yaani mwili wake ulikuwa ukimsisimka ajabu,Roma licha ya kwamba alikuwa ni mwenye kushangaa , lakini yeye hakuwa mwenye kuonesha mshangao sana kama ilivyokuwa kwa wengine.

“Naomba leo nimtaje mwanaume ninaempenda ambaye nipo kwa ajili ya kufanya chochote , kwa ajili yake , yupo hapa najua hajui kama nampenda , ila leo nataka atambue kuwa kuna mrembo Chaneli hapa ambaye ametokea kumpenda kwa dhati kabisa”

“Mtajee…”

Watu walikuwa ni wenye kujiandaa kumjua mwanaume ambaye alikuwa akipendwa na Chaneli au Imani Maseko.

Chaneli alionekana kukosa uzalendo wa kuendelea kuvumilia , kwani baada ya watu kumwambia amtaje alitupa maiki chini na kisha akashuka kwenye jukwaa na kukimbia kwa madada kabisa, na kufanya watu wote wasogee kumpisha, yaani wanaume ndio waliokuwa wakisogea mbali kabisa , walionekana kumnyanyapaa Chaneli.

Wale wanaume waliosifika kwa kupenda pisi kali leo hii kwamara ya kwanza walikuwa wakimkimbia mrembo Chaneli, walionesha ile hali ya kuogopa.

Ilikuwa ni kitendo ambacho Roma mwenywe hakuwa amekitegemea , kwani alijikuta akikumbatiwa kwa nguvu na Chaneli , na watu wote walishangazwa mno na jambo hilo akiwemo Rose .

Lisaa lililopita nyuma Roma hakuonekana kama mtu ndani ya hili eneo , lakini sasa hivi watu wote w alionekana kushangazwa na uwepo wa Roma hapa ndani ambae alikumbatiwa na Chaneli huku watu wakichukua tukio hilo kwa simu zao.

“Paaa….. Paaaaa… Paaaa”

Ulikuwa ni mlio wa risasi ambao ulichafua hali ya hewa na kufanya watu waliokuwa kwenye mushikeli iliosababishwa na Chaneli sasa kuwa katika hali ya hofu baada ya kusikia mlio wa bunduki.

Haikueeleweka ni vipi Rose aliweza kupata siraha , lakini yeye ndie alifyatua risasi hewani na kufanya watu waanze kutawanyika kuokoa maisha yao.

Roma aliekumbatiwa na Chaneli aliinua macho yake na kumwangalia Rose ambaye alikuwa ameshikilia bastora, huku akijiuliza ni jambo gani Rose anataka kulifanya.

Muda uleule , vijana wa fupa Faru waliingia kwa kasi na kumzingira Situ , huku watu wakiwa wamepungua sana ndani ya hili eneo la Bustani wakikimbilia nje , lakini pia vijana wa kundi la Tembo ambao walikuwa wameingizwa hapo ndani kama kundi la Fupa Faru na wao walimzingira Rose.

Viana wa Tembo walimkinga Rose kwa mbele na Vijana wa Fupa Faru walimkinga Situ kwa mbele, ilikuwa ni kitendo kilichofanyika kwa dakika chache sana.

Chaneli aliekuwa akijiamin dakika chache zilizopita sasa alikuwa amejibana chini ya Meza , Roma yeye hakuwa na wasiwasi tena alikaa chini na akatulia na ni kama alikuwa akitaka kushuhudia nini kitajili baada ya Rose kuliamsha.

“Boss mpango wa kwanza umefeli,. Maseko anaonekana kashakufa muda mrefu na mwananae ndio hivyo ni Shoga , kilichobaki ni kumuua Rose”Aliongea Pengo aliekuwa nyuma na Situ.

Na Situ kabla hajajibu alitoa pakiti ya sigara yake na kisha akachomoa moja na kuanza kuichoma na moto wa kiberiti na kisha akampa Pengo kile kiberiti na kusogea mbele huku akipishwa na vijana wake na pia hivyohivyo kwa Rose , alisogea mbele.

“Paaa…paaaa,.. papapa”Yalikuwa ni makofi kutoka kwa Situ na haikueleweka kwanini bwana huyu alikuwa akipiga makofi.

“Mbinu nzuri sana Rose , Kitendo cha kuingiza Vijana wako ndani ya kambi yangu imenifurahisha , imedhihirisha kweli una damu yangu kwenye mwili wako”Aliongea Situ.

“Situ Achia jimbo langu na urudi Mwanza ukaendelee na maisha yako , sitaki uadui na wewe , licha ya kwamba umenianza”

“Hahaha… Unajiamini na nini Rose , licha ya kwamba vijana wangu na wako tupo sawa kiuwezo , isikupe kiburi kama utashinda , mimi ndio Situ , nimeanza kazi hii kabla hata sijafikiria kupata mtoto kama wewe, nikwambie tu sikio haliwezi kuzidi kichwa Rose , jisalimishe na uwe mtoto wangu mtiifu na nitahakikisha nakutafutia mume bora wa kuendana na wewe na uzae hatimae niweze kuitwa babu”Aliongea Situ.

Vijana wa situ na wa Rose walionekana kuwa tayari kwa mapambano, tena wote wakiwa na siraha mikononi za moto na kama wangeanza kurushiana riasisi ni Dhahiri kundi litakaloshinda hapa ndani ni lile ambalo litakuwa la kwanza kufyatua risasi ,kwani uwingi wao ulikuwa sawa baina ya makundi yote mawili.

“Situ Sina haja ya kuongea na wewe maana hakuna mafanikio , kwasababu umeingia kwenye koloni langu , basi sina budi kukutoa kwani mpaka sasa wewe ni adui”Aliongea Rose na palepale vijana wake wakakoki siraha zao tayari kwa mapambano , lakini sio kwao tu hata kwa watu wa Situ waliiweka tayari , kwa namna mambo yalivyokuwa yakiendelea hapa ndani ungesema hii sio Tanzannia bali ni nchi nyingine ambazo zilikuwa zikisifika kwa uhalifu duniani.

“Paaa…! Paaaa,Bang !!! Bang!!!!,Bang!!!!”Ilikuwa ni milio ya risasi ilioanza kusikika hapa ndani mfululizo kiasi kwamba , ile sehemu ambayo ilikuwa imepambwa kwa viti ilikuwa ni uwanja wa vita , vijana wa Rose na Situ wote walikuwa wakitumia viti na meza kujikinga na Risasi , huku waliokuwa wamejeruiwa wakiwa chini wakiugulia maumivu , huku wale ambao hawakua na bahati mbaya walikuwa washakufa.

Hali haikuwa shwali kwakweli kwa wakati huu , na kwa mtu ambaye hajawahi kusikia sauti ya Risasi huenda angezimia kabla ya risasi kumfikia , lakini kwa vijana hawa walionekana kuzoea.

Roma alikuwa upande wa kulia akiendelea kuangalia hali ilivyokuwa inaendelea , huku macho yake yakimwangalia Rose muda wote , alikuwa akiangalia kila upande kuhakiksha watu hawamdhuru.

Vijana wa Rose walionekana kuwa shupavu kweli kwenye kuwabananisha wenzao kwani ndani ya dakika chache tu watu wa Fupa Faru , walikuwa wapo chini wakiugulia maumivu , huku wengine wakiwa ni wenye kupambana na kifo.

Situ aliekuwa nyuma baada ya kuona hali haiendi kama alivyokuwa akitaka , alikimbilia ndani akiacha vijana wake waendelee na kazi na Rose alimuona ila hakutaka kumfuata , alitaka kwanza amalize vijana wake na ndio amfuate.

Mirindimo ya risasi ilikuwa ikiendelea , lakini wakati huu vijana walikuwa wakipigana kwa kuviziana kutokana na kwamba kulikuwa na viti pamoja na meza ndani ya hili eneo ambalo dakika chache nyuma lilikuwa na wageni , ila sasa kwa mvurugikano wa hili eneo usingedhania kama kuna sherehe iliokuwa ikiendelea.

Lakini sasa mambo yalionekana kuwabadilikia Rose mara baada ya gari tatu kuingia hapa ndani na wakashuka vijana ambao walianza kuwshambulia kwa nyuma , kitendo kilichomfanya Rose ajifiche chini akiwa na Zonga.

Kilikuwa ni kitendo cha dakika chache tu vijana wa Rose walikuwa chini wote wakiwa hawana uhai na sasa akabakia Rose , Zonga na Roma.

Chaneli kwa muda huu haikueleweka alikuwa wapi, kwani hakuonekana kabisa , Roma na yeye alikuwa upande wa kulia ambao alikuwepo Rose karibu.

“Shi**T inaonekna alituwekea mtego”Aliongea Rose akimwangalia Roma , na aliona kabisa hapa kashindwa kwani vijana waliongia hapa ndani aliwajua ni wakundi la Black Mamba na walikuwa ni wengi Zaidi ya ishirini hivi na wote wakiwa na siraha.

Rose aliona kabisa hakuna namna Zaidi ya kukimbia hapa ndani , alimjua Roma alikuwa na uwezo , ila aliona asingeweza kuwashinda vijana wengi kiasi hiko.

“Roma tutakimbia kuelekea mrango wa nyuma, ni rahisi kutoka kuliko wa mbele”Aliongea Rose.

“Boss mimi nitawakinga , hakikisheni mnatoka nikihesabu mpaka mbili”Aliongea Zonga.

“Hapa hakuna namna Rose huu ni mtego na ni lazima watakuwa wanajua tutakimbilia upande wa nyuma , na nia yao ni kuua hivyo ni bora kupambana kuliko kukimbia”

“Lakini ni wengi mpenzi , nisamehe kwa kuingiza kwenye haya mambo”Aliongea Rose huku akiona yeye ndio kamwingiza Roma kwenye hii hali, kwani huenda muda huo angekuwa nyumbani na mke wake.

Roma na yeye alitabasamu kwa uchungu kwa maneno ambayo Rose alikuwa akiongea.

“Rose unaonekana kusahau kama mimi ni mpenzi wako na nipo tayari kwa kufanya lolote kwa ajili yako , kwenye hali kama hii hutakiwi kuniomba msamaha,unatakiwa kusema asante bebi tunakwenda kufa pamoja”

Aliongea Roma huku akiwa ni mwenye tabasamu na kumfanya na Rose pia atabasamu.

“Rose jisalimishe mwenywe tumalize hili jambo m mpaka sasa ushashindwa”

Ilikuw ni sauti ya Situ ambayo ilisikika ndani ya masikio ya Zonga na Rose, lakini Rose hakujibu na alimwangalia Roma ni kama hakujua nini kinatakiwa kufanyika katika hali kama hio.

Na muda huu kulikuwa kumetulia tuli na Situ ambaye dakika chache nyuma alikuwa amekimbilia ndani sasa hivi alikuwa ni mwenye kujiamini huku akiwa amesimama na Hassani aliekuwa ni kiongozi wa kundi la Black Mamba huku wakiwa ni wenye kuongea kwa furaha kusherekea ushindi wao.

“Inabidi tujisalimishe”Aliongea Roma na kumfanya Rose amwangalie kwa wasiwasi ni kama hakuwa mwenye kukubaliana na maamuzi ya Roma.

“Fanyeni kama ninavyowaambia “Aliongea Roma huku akinyanyuka wa kwanza na kumfanya Situ acheke kwa furaha baada ya kuona kumbe hata kile Kibwengo kipo bado , ila kwa upande wa Hassanni alikuwa akimwangalia Roma kwa maswali.
 
SEHEMU YA 87

Roma na Rose walisogea mpaka katikati , huku wakiwa wamezungukwa na vijana wa kundi la Situ pamoja na wa Black mamba ambao kundi lake lilikuwa likiongozwa na Hassani.

Roma hakuonekana kuwa ni mwenye wasiwasi , ila kwa Rose alionyesha wasiwasi , kwani hakujua Roma ni jambo gani alilokuwa akitaka kulifanya.

Kiufupi licha ya Rose kujua Roma hakuwa ni wa kawaida na anajua kupigana, lakini mbele ya watu zaidi ya ishirini hakuamini kama Roma anaweza kuwamaliza wote kwa wakati mmoja , aliona ni jambo gumu kutekelezeka na ndio maana hakutaka Roma afanye jambo lolote hatarishi , kwani hakutaka kumuona akifa mbele yake.

“Dakika zilizopita ulikuwa ukijiamini sana Rose , kule kujiamini kumeenda wapi, angalia sasa unaonekana kama Sungura alienasa kwenye mtego”Aliongea Situ huku akimwangalia Rose kwa kejeli , lakini Rose aliishia kumwangalia baba yake kwa hasira , akishindwa ni kipi akifanye.

“Hassanni mbona unamwangalia sana huyu , kijana au na wewe unamfahamu?”Aliuliza Situ baada ya kuona Hasani muda wote alikuwa akimwangalia Roma.

“Situ huyu ndio mpuuzi aliemua Karimu Mtoto wa Meya”aliongea Hassani na kumfanya Situ ashangae , hakuwa ni mwenye kulijua hilo.

“Kama ni hivyo Hassani basi naamini leo kisasi chako kinakwenda kutimia na sio kwa Meya tu kwa kundi lote la Black Mamba kwa kupoteza kiongozi wenu, lakini Hassani ilikuweje Kibwengo kama huyu akamuua Karimu?”

“Hata mimi nashindwa kuelewa Situ , nipo kwenye mshangao kama wako , labda Karimu alikuwa amelewa”

“Bosi tunafanyaje?”Aliuliza Pengo ambaye alionekanaa kuchafuka kuliko alivyokuwa dakika chache zilizopita.

“Kuna kipi cha kufanya hapa, tunawaua kila mmoja na kwanzia leo kundi lote la Tembo litakuwa chini yangu … hahahaha”Aliongea huku akiwasha sigara yake kwa ajili ya kuvuta , lakini pia vijana wake wakicheka.

“Bosi unaonaje tukimuonja Rose kwanza , ninatamani kujua ni nini anakificha kwenye nguo kutokana na uzuri wake”.

“Licha ya Rose kuwa adui yangu lakini ni mwanangu , kumbaka ni kitendo cha kunidhalilisha , una bahati sana Pengo i mpala sasa ningekuwa nishakutandika Risasi”Aliongea Situ akiwa ni mwenye kuonesha hasira kweli , na Pengo akatulia tuli kwani alikuwa akimjua bosi wake hakuwa na utani kabisa ,akiamua kukuua haijalishi mmefahamiana kwa muda wa miaka mingapi anakupiga Risasi na hatonesha ishara yoyote ya kujutia.

Roma aliona mzee Situ licha ya kwamba alikuwa na roho mbaya lakini pia nati kuonekana kulegea , anagalau alimuona kama mtu anaelinda hadhi yake , kwani kwa maneno alioongea yalikuwa yakileta maana .

"Situ tunasubiria ruhusa yako maana wewe ndio mwenye shughuli , mimi nataka nianze na huyu mpuuzi hapa"Aliongea Hassani akimsogelea Roma alitaka kumshika .

"Usije ukanishika"

Aliongea Roma kwa tahadhari na sauti iliojaa lujiamini na kumfanya Hassani azuie mkono wake kwa sekunde na kisha akatabasamu na kuendelea kufanya kitendo chake na Roma alimkwepa.

Zonga mkojo ulikuwa ukitaka kumtoka , aliona anakwenda kufa usiku huo , hakuona namna yoyote ya wao kutoka Hai hapa ndani , na alimuona Roma kama kuku anaempigia kelele Mwewe .

"Jifanye jeuri tu , leo utakufa kifo cha maumivu , nitakuua taratibu kulipiza kisasi"Aliongea Hasaani , lakini Roma hakuwa na woga hata kidogo , alianza kuangalia mmoja mmoja hapa ndani , huku akianza kupiga hesabu zake

Na kwa haraka haraka aliona hawezi kuwamaliza vijana wote ishirini kwa wakati mmoja pasipo kujibadilisha lakini pia kwa vijana hao kumdhuru Rose , aliogopa pia kutumia uwezo wake kwani alijua anaweza asirudi kwenyehali ya kawaida ya ubinadamu.

Vijana walikuwa wamewazingira pande zote na ni malaika pekee ambaye Rose aliamini ndie ambaye angeweza kuwaokoa kwenye hali kama hio , hakuelewa ni jambo gani ambalo Roma anawaza , lakini licha ya hivyo aliona hakuna wazo ambalo linaweza likawaokoa pasipo yay eye kuchukua hatua.

“Situ nitakupa kila kitu ila naomba uwaachie Zonga na Mpenzi wangu waondoke”Aliongea Rose na kumshangaza Situ.

“Hahahaha…Rose unafikiriaje mapenzi kwenye hali kama hii, ni kwambie tu huna nafasi ya kufanya maongezi na mimi maana mpaka muda huu wewe ni mfu na kuhusu mali zako zipo mikononi mwangu dakika ambayo roho yako itaicha hii dunia”Aliongea Situ na kisha akampa ishara Hassani.

“Hassani naomba umalize kazi, muda unaenda , mpige Rose Rasisi ya moyo na kichwani ili kifo chake kisiwe cha maumivu”Aliongea Situ huku akitoa moshi mwingi wa sigara kupitia Puani huku macho yake yakiwa mekundu.

Hasaani Baada ya kuona kapata Ruhusa alimpa ishara kijana wake aliekuwa akimwamini ruhusa ya kufanya kama Situ alivyoelekeza , alitaka kumuua kwanza Rose halafu aondoke na Roma akampe mateso kwanza huku akimuua taratibu.

“Acha ujingaaa…!!!”

Ilikuwa ni sauti iliomshitua kijana ambaye alikuwa akitaka kumpiga Rose Risasi na hapa Sauti ya Roma haikuwa ya kawaida ilikuwa kama ya Roboti huku ikisikika mara mbili kwenye masikio ya watu hawa , ni kama ilikua ikitokea juu angani na kuja chini , kumbe aliekuwa ameongea yupo hapahapa ndani.

Situ ambaye alikuwa amegeuka nyuma na yeye aliisikia na kujikuta akiangalia upande wa alipo Hassani , ni kama hakuwa ni mwenye kuamini kama sauti hio imetokea hapa ndani.

Upande wa Rose na Zonga na wao waliogopeshwa na sauti hio,Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , kwani wakati wote alikuwa ameweka kichwa chake chini kusubiria Risasi.

Rose alijikuta akishangazwa na macho ya Roma yalikuwa ni ya Njano kama jua huku mwili wa Roma ukianza kutoa mvuke kiasi kwamba nguo zilianza kuloana kwa majimaji mazito yaliokuwa yakimtoka, huku harufu kama ya kuungua kwa nailoni ikianza kusambaa , vijana wa Situ wote waliweka sawa Bastora zao ,. Huku Hassani na Situ wakishangazwa na mabadiliko hayo, Hassani ile hali ya kujiamini ilipotea ghafla na alirudi nyuma haraka na pia hata Situ mwenyewe.

“Mpigeni Rasasi”Ilikuwa ni amri kutoka kwa situ na vijana wakainua risasi zao kwa ajili ya kufanya kazi lakini kilichotokea baada ya hapo kiliwaacha hoi na hali ya mshangao Situ na Hassani.

Ni kama kimbunga kilichoambatana na Mwanga ndio kilichoonekana katikati ya vijana wote wa kundi la Black Mamba.

“Tuuu.. Tuuu Crackk Tuu ….Shwa ..Swahaa !!!”ulikuwa ni mlio ambao haukua wa kawaida kabisa, yaani vijana hawa walikuwa wakirushwa juu kama makaratasi na kudondokea upande mwingine na hakukua na mwenye uhai hata kidogo kwa kila aliekuwa akidondoka na haikueleweka Roma alikuwa akiwafanya vipi maana ni kitendo cha kasi sana alichokuwa akifanya , ilikuwa ni picha ya kushangaza sana kwa Rose.

“Nani kasema unaweza kukimbia?”

Aliuliza Roma kwa sauti nzito mara baada ya ya kumaliza vijana wote ishirini kwa dakika moja tu,jambo ambalo lilimfanya Hassani kukimbilia getini kujiokoa , lakini Roma hakuwa tayari kumuacha Hassani aondoke.

Hassani mkojo ulikuwa karibu sana , baada ya kuona Roma yupo mbele yake huku akiwa ni mwenye kushangaa kafikiwa vipi ukijumlisha na namna ambavyo Roma alikuwa akionekana , matundu yake yote ya kutoa taka mwili yalifunguka.

“Crack”Bila huruma Roma alimvunja shingo Hassani na huo ukawa mwisho wake.

Rose aliekuwa amesimama mita kadhaa , alimwangalia Roma huku akishindwa kuelewa hata hisia zake zipoje kwa wakati huo, alifikiria vitu vingi kwa wakati mmoja.

Zonga na yeye mkojo haukumpa msamaha, licha ya kwamba Roma alionekana kuwalinda lakini jambo ambalo amelishuhudia alikuwa amezoea kuona kwenye muvi za kimarekani pekee , lakini leo hii alikuwa akiona kila kitu laivu.

Situ alishindwa kukimbia , alikuwa amekaa chini huku akishindwa kuelewa nini kinachoendelea , yaani mwili ulikuwa ukitaka kukimbia lakini alikuwa akishindwa kufanya hivyo , ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kukimbizwa lakini viungo vyake vya mwili vilikuwa vikimsaliti.

Roma alisimama katikati ya bustani huku akiwa ni mwenye kushindana na mwili wake , alikua akijaribu kujirudisha kuwa wa kawaida, lakini alishindwa kabisa na palepale macho yake yalianza kubadilika na kuwa ya Rangi nyekundu kutoka njano , huku nguo alizovaa zikichanika kwani alikuwa akiongezeka ukubwa , Zonga aliekuwa chini alianza kuburuzika kurudi nyuma kwa woga
ITAENDELEA JUMAMOSI
NICHEKI WATSAPP;0687151346
 
SEHEMU YA 87

Roma na Rose walisogea mpaka katikati , huku wakiwa wamezungukwa na vijana wa kundi la Situ pamoja na wa Black mamba ambao kundi lake lilikuwa likiongozwa na Hassani.

Roma hakuonekana kuwa ni mwenye wasiwasi , ila kwa Rose alionyesha wasiwasi , kwani hakujua Roma ni jambo gani alilokuwa akitaka kulifanya.

Kiufupi licha ya Rose kujua Roma hakuwa ni wa kawaida na anajua kupigana, lakini mbele ya watu zaidi ya ishirini hakuamini kama Roma anaweza kuwamaliza wote kwa wakati mmoja , aliona ni jambo gumu kutekelezeka na ndio maana hakutaka Roma afanye jambo lolote hatarishi , kwani hakutaka kumuona akifa mbele yake.

“Dakika zilizopita ulikuwa ukijiamini sana Rose , kule kujiamini kumeenda wapi, angalia sasa unaonekana kama Sungura alienasa kwenye mtego”Aliongea Situ huku akimwangalia Rose kwa kejeli , lakini Rose aliishia kumwangalia baba yake kwa hasira , akishindwa ni kipi akifanye.

“Hassanni mbona unamwangalia sana huyu , kijana au na wewe unamfahamu?”Aliuliza Situ baada ya kuona Hasani muda wote alikuwa akimwangalia Roma.

“Situ huyu ndio mpuuzi aliemua Karimu Mtoto wa Meya”aliongea Hassani na kumfanya Situ ashangae , hakuwa ni mwenye kulijua hilo.

“Kama ni hivyo Hassani basi naamini leo kisasi chako kinakwenda kutimia na sio kwa Meya tu kwa kundi lote la Black Mamba kwa kupoteza kiongozi wenu, lakini Hassani ilikuweje Kibwengo kama huyu akamuua Karimu?”

“Hata mimi nashindwa kuelewa Situ , nipo kwenye mshangao kama wako , labda Karimu alikuwa amelewa”

“Bosi tunafanyaje?”Aliuliza Pengo ambaye alionekanaa kuchafuka kuliko alivyokuwa dakika chache zilizopita.

“Kuna kipi cha kufanya hapa, tunawaua kila mmoja na kwanzia leo kundi lote la Tembo litakuwa chini yangu … hahahaha”Aliongea huku akiwasha sigara yake kwa ajili ya kuvuta , lakini pia vijana wake wakicheka.

“Bosi unaonaje tukimuonja Rose kwanza , ninatamani kujua ni nini anakificha kwenye nguo kutokana na uzuri wake”.

“Licha ya Rose kuwa adui yangu lakini ni mwanangu , kumbaka ni kitendo cha kunidhalilisha , una bahati sana Pengo i mpala sasa ningekuwa nishakutandika Risasi”Aliongea Situ akiwa ni mwenye kuonesha hasira kweli , na Pengo akatulia tuli kwani alikuwa akimjua bosi wake hakuwa na utani kabisa ,akiamua kukuua haijalishi mmefahamiana kwa muda wa miaka mingapi anakupiga Risasi na hatonesha ishara yoyote ya kujutia.

Roma aliona mzee Situ licha ya kwamba alikuwa na roho mbaya lakini pia nati kuonekana kulegea , anagalau alimuona kama mtu anaelinda hadhi yake , kwani kwa maneno alioongea yalikuwa yakileta maana .

"Situ tunasubiria ruhusa yako maana wewe ndio mwenye shughuli , mimi nataka nianze na huyu mpuuzi hapa"Aliongea Hassani akimsogelea Roma alitaka kumshika .

"Usije ukanishika"

Aliongea Roma kwa tahadhari na sauti iliojaa lujiamini na kumfanya Hassani azuie mkono wake kwa sekunde na kisha akatabasamu na kuendelea kufanya kitendo chake na Roma alimkwepa.

Zonga mkojo ulikuwa ukitaka kumtoka , aliona anakwenda kufa usiku huo , hakuona namna yoyote ya wao kutoka Hai hapa ndani , na alimuona Roma kama kuku anaempigia kelele Mwewe .

"Jifanye jeuri tu , leo utakufa kifo cha maumivu , nitakuua taratibu kulipiza kisasi"Aliongea Hasaani , lakini Roma hakuwa na woga hata kidogo , alianza kuangalia mmoja mmoja hapa ndani , huku akianza kupiga hesabu zake

Na kwa haraka haraka aliona hawezi kuwamaliza vijana wote ishirini kwa wakati mmoja pasipo kujibadilisha lakini pia kwa vijana hao kumdhuru Rose , aliogopa pia kutumia uwezo wake kwani alijua anaweza asirudi kwenyehali ya kawaida ya ubinadamu.

Vijana walikuwa wamewazingira pande zote na ni malaika pekee ambaye Rose aliamini ndie ambaye angeweza kuwaokoa kwenye hali kama hio , hakuelewa ni jambo gani ambalo Roma anawaza , lakini licha ya hivyo aliona hakuna wazo ambalo linaweza likawaokoa pasipo yay eye kuchukua hatua.

“Situ nitakupa kila kitu ila naomba uwaachie Zonga na Mpenzi wangu waondoke”Aliongea Rose na kumshangaza Situ.

“Hahahaha…Rose unafikiriaje mapenzi kwenye hali kama hii, ni kwambie tu huna nafasi ya kufanya maongezi na mimi maana mpaka muda huu wewe ni mfu na kuhusu mali zako zipo mikononi mwangu dakika ambayo roho yako itaicha hii dunia”Aliongea Situ na kisha akampa ishara Hassani.

“Hassani naomba umalize kazi, muda unaenda , mpige Rose Rasisi ya moyo na kichwani ili kifo chake kisiwe cha maumivu”Aliongea Situ huku akitoa moshi mwingi wa sigara kupitia Puani huku macho yake yakiwa mekundu.

Hasaani Baada ya kuona kapata Ruhusa alimpa ishara kijana wake aliekuwa akimwamini ruhusa ya kufanya kama Situ alivyoelekeza , alitaka kumuua kwanza Rose halafu aondoke na Roma akampe mateso kwanza huku akimuua taratibu.

“Acha ujingaaa…!!!”

Ilikuwa ni sauti iliomshitua kijana ambaye alikuwa akitaka kumpiga Rose Risasi na hapa Sauti ya Roma haikuwa ya kawaida ilikuwa kama ya Roboti huku ikisikika mara mbili kwenye masikio ya watu hawa , ni kama ilikua ikitokea juu angani na kuja chini , kumbe aliekuwa ameongea yupo hapahapa ndani.

Situ ambaye alikuwa amegeuka nyuma na yeye aliisikia na kujikuta akiangalia upande wa alipo Hassani , ni kama hakuwa ni mwenye kuamini kama sauti hio imetokea hapa ndani.

Upande wa Rose na Zonga na wao waliogopeshwa na sauti hio,Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , kwani wakati wote alikuwa ameweka kichwa chake chini kusubiria Risasi.

Rose alijikuta akishangazwa na macho ya Roma yalikuwa ni ya Njano kama jua huku mwili wa Roma ukianza kutoa mvuke kiasi kwamba nguo zilianza kuloana kwa majimaji mazito yaliokuwa yakimtoka, huku harufu kama ya kuungua kwa nailoni ikianza kusambaa , vijana wa Situ wote waliweka sawa Bastora zao ,. Huku Hassani na Situ wakishangazwa na mabadiliko hayo, Hassani ile hali ya kujiamini ilipotea ghafla na alirudi nyuma haraka na pia hata Situ mwenyewe.

“Mpigeni Rasasi”Ilikuwa ni amri kutoka kwa situ na vijana wakainua risasi zao kwa ajili ya kufanya kazi lakini kilichotokea baada ya hapo kiliwaacha hoi na hali ya mshangao Situ na Hassani.

Ni kama kimbunga kilichoambatana na Mwanga ndio kilichoonekana katikati ya vijana wote wa kundi la Black Mamba.

“Tuuu.. Tuuu Crackk Tuu ….Shwa ..Swahaa !!!”ulikuwa ni mlio ambao haukua wa kawaida kabisa, yaani vijana hawa walikuwa wakirushwa juu kama makaratasi na kudondokea upande mwingine na hakukua na mwenye uhai hata kidogo kwa kila aliekuwa akidondoka na haikueleweka Roma alikuwa akiwafanya vipi maana ni kitendo cha kasi sana alichokuwa akifanya , ilikuwa ni picha ya kushangaza sana kwa Rose.

“Nani kasema unaweza kukimbia?”

Aliuliza Roma kwa sauti nzito mara baada ya ya kumaliza vijana wote ishirini kwa dakika moja tu,jambo ambalo lilimfanya Hassani kukimbilia getini kujiokoa , lakini Roma hakuwa tayari kumuacha Hassani aondoke.

Hassani mkojo ulikuwa karibu sana , baada ya kuona Roma yupo mbele yake huku akiwa ni mwenye kushangaa kafikiwa vipi ukijumlisha na namna ambavyo Roma alikuwa akionekana , matundu yake yote ya kutoa taka mwili yalifunguka.

“Crack”Bila huruma Roma alimvunja shingo Hassani na huo ukawa mwisho wake.

Rose aliekuwa amesimama mita kadhaa , alimwangalia Roma huku akishindwa kuelewa hata hisia zake zipoje kwa wakati huo, alifikiria vitu vingi kwa wakati mmoja.

Zonga na yeye mkojo haukumpa msamaha, licha ya kwamba Roma alionekana kuwalinda lakini jambo ambalo amelishuhudia alikuwa amezoea kuona kwenye muvi za kimarekani pekee , lakini leo hii alikuwa akiona kila kitu laivu.

Situ alishindwa kukimbia , alikuwa amekaa chini huku akishindwa kuelewa nini kinachoendelea , yaani mwili ulikuwa ukitaka kukimbia lakini alikuwa akishindwa kufanya hivyo , ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kukimbizwa lakini viungo vyake vya mwili vilikuwa vikimsaliti.

Roma alisimama katikati ya bustani huku akiwa ni mwenye kushindana na mwili wake , alikua akijaribu kujirudisha kuwa wa kawaida, lakini alishindwa kabisa na palepale macho yake yalianza kubadilika na kuwa ya Rangi nyekundu kutoka njano , huku nguo alizovaa zikichanika kwani alikuwa akiongezeka ukubwa , Zonga aliekuwa chini alianza kuburuzika kurudi nyuma kwa woga
Nifanyeje ili niwe napata notification ya huu uzi?
 
SEHEMU YA 87

Roma na Rose walisogea mpaka katikati , huku wakiwa wamezungukwa na vijana wa kundi la Situ pamoja na wa Black mamba ambao kundi lake lilikuwa likiongozwa na Hassani.

Roma hakuonekana kuwa ni mwenye wasiwasi , ila kwa Rose alionyesha wasiwasi , kwani hakujua Roma ni jambo gani alilokuwa akitaka kulifanya.

Kiufupi licha ya Rose kujua Roma hakuwa ni wa kawaida na anajua kupigana, lakini mbele ya watu zaidi ya ishirini hakuamini kama Roma anaweza kuwamaliza wote kwa wakati mmoja , aliona ni jambo gumu kutekelezeka na ndio maana hakutaka Roma afanye jambo lolote hatarishi , kwani hakutaka kumuona akifa mbele yake.

“Dakika zilizopita ulikuwa ukijiamini sana Rose , kule kujiamini kumeenda wapi, angalia sasa unaonekana kama Sungura alienasa kwenye mtego”Aliongea Situ huku akimwangalia Rose kwa kejeli , lakini Rose aliishia kumwangalia baba yake kwa hasira , akishindwa ni kipi akifanye.

“Hassanni mbona unamwangalia sana huyu , kijana au na wewe unamfahamu?”Aliuliza Situ baada ya kuona Hasani muda wote alikuwa akimwangalia Roma.

“Situ huyu ndio mpuuzi aliemua Karimu Mtoto wa Meya”aliongea Hassani na kumfanya Situ ashangae , hakuwa ni mwenye kulijua hilo.

“Kama ni hivyo Hassani basi naamini leo kisasi chako kinakwenda kutimia na sio kwa Meya tu kwa kundi lote la Black Mamba kwa kupoteza kiongozi wenu, lakini Hassani ilikuweje Kibwengo kama huyu akamuua Karimu?”

“Hata mimi nashindwa kuelewa Situ , nipo kwenye mshangao kama wako , labda Karimu alikuwa amelewa”

“Bosi tunafanyaje?”Aliuliza Pengo ambaye alionekanaa kuchafuka kuliko alivyokuwa dakika chache zilizopita.

“Kuna kipi cha kufanya hapa, tunawaua kila mmoja na kwanzia leo kundi lote la Tembo litakuwa chini yangu … hahahaha”Aliongea huku akiwasha sigara yake kwa ajili ya kuvuta , lakini pia vijana wake wakicheka.

“Bosi unaonaje tukimuonja Rose kwanza , ninatamani kujua ni nini anakificha kwenye nguo kutokana na uzuri wake”.

“Licha ya Rose kuwa adui yangu lakini ni mwanangu , kumbaka ni kitendo cha kunidhalilisha , una bahati sana Pengo i mpala sasa ningekuwa nishakutandika Risasi”Aliongea Situ akiwa ni mwenye kuonesha hasira kweli , na Pengo akatulia tuli kwani alikuwa akimjua bosi wake hakuwa na utani kabisa ,akiamua kukuua haijalishi mmefahamiana kwa muda wa miaka mingapi anakupiga Risasi na hatonesha ishara yoyote ya kujutia.

Roma aliona mzee Situ licha ya kwamba alikuwa na roho mbaya lakini pia nati kuonekana kulegea , anagalau alimuona kama mtu anaelinda hadhi yake , kwani kwa maneno alioongea yalikuwa yakileta maana .

"Situ tunasubiria ruhusa yako maana wewe ndio mwenye shughuli , mimi nataka nianze na huyu mpuuzi hapa"Aliongea Hassani akimsogelea Roma alitaka kumshika .

"Usije ukanishika"

Aliongea Roma kwa tahadhari na sauti iliojaa lujiamini na kumfanya Hassani azuie mkono wake kwa sekunde na kisha akatabasamu na kuendelea kufanya kitendo chake na Roma alimkwepa.

Zonga mkojo ulikuwa ukitaka kumtoka , aliona anakwenda kufa usiku huo , hakuona namna yoyote ya wao kutoka Hai hapa ndani , na alimuona Roma kama kuku anaempigia kelele Mwewe .

"Jifanye jeuri tu , leo utakufa kifo cha maumivu , nitakuua taratibu kulipiza kisasi"Aliongea Hasaani , lakini Roma hakuwa na woga hata kidogo , alianza kuangalia mmoja mmoja hapa ndani , huku akianza kupiga hesabu zake

Na kwa haraka haraka aliona hawezi kuwamaliza vijana wote ishirini kwa wakati mmoja pasipo kujibadilisha lakini pia kwa vijana hao kumdhuru Rose , aliogopa pia kutumia uwezo wake kwani alijua anaweza asirudi kwenyehali ya kawaida ya ubinadamu.

Vijana walikuwa wamewazingira pande zote na ni malaika pekee ambaye Rose aliamini ndie ambaye angeweza kuwaokoa kwenye hali kama hio , hakuelewa ni jambo gani ambalo Roma anawaza , lakini licha ya hivyo aliona hakuna wazo ambalo linaweza likawaokoa pasipo yay eye kuchukua hatua.

“Situ nitakupa kila kitu ila naomba uwaachie Zonga na Mpenzi wangu waondoke”Aliongea Rose na kumshangaza Situ.

“Hahahaha…Rose unafikiriaje mapenzi kwenye hali kama hii, ni kwambie tu huna nafasi ya kufanya maongezi na mimi maana mpaka muda huu wewe ni mfu na kuhusu mali zako zipo mikononi mwangu dakika ambayo roho yako itaicha hii dunia”Aliongea Situ na kisha akampa ishara Hassani.

“Hassani naomba umalize kazi, muda unaenda , mpige Rose Rasisi ya moyo na kichwani ili kifo chake kisiwe cha maumivu”Aliongea Situ huku akitoa moshi mwingi wa sigara kupitia Puani huku macho yake yakiwa mekundu.

Hasaani Baada ya kuona kapata Ruhusa alimpa ishara kijana wake aliekuwa akimwamini ruhusa ya kufanya kama Situ alivyoelekeza , alitaka kumuua kwanza Rose halafu aondoke na Roma akampe mateso kwanza huku akimuua taratibu.

“Acha ujingaaa…!!!”

Ilikuwa ni sauti iliomshitua kijana ambaye alikuwa akitaka kumpiga Rose Risasi na hapa Sauti ya Roma haikuwa ya kawaida ilikuwa kama ya Roboti huku ikisikika mara mbili kwenye masikio ya watu hawa , ni kama ilikua ikitokea juu angani na kuja chini , kumbe aliekuwa ameongea yupo hapahapa ndani.

Situ ambaye alikuwa amegeuka nyuma na yeye aliisikia na kujikuta akiangalia upande wa alipo Hassani , ni kama hakuwa ni mwenye kuamini kama sauti hio imetokea hapa ndani.

Upande wa Rose na Zonga na wao waliogopeshwa na sauti hio,Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , kwani wakati wote alikuwa ameweka kichwa chake chini kusubiria Risasi.

Rose alijikuta akishangazwa na macho ya Roma yalikuwa ni ya Njano kama jua huku mwili wa Roma ukianza kutoa mvuke kiasi kwamba nguo zilianza kuloana kwa majimaji mazito yaliokuwa yakimtoka, huku harufu kama ya kuungua kwa nailoni ikianza kusambaa , vijana wa Situ wote waliweka sawa Bastora zao ,. Huku Hassani na Situ wakishangazwa na mabadiliko hayo, Hassani ile hali ya kujiamini ilipotea ghafla na alirudi nyuma haraka na pia hata Situ mwenyewe.

“Mpigeni Rasasi”Ilikuwa ni amri kutoka kwa situ na vijana wakainua risasi zao kwa ajili ya kufanya kazi lakini kilichotokea baada ya hapo kiliwaacha hoi na hali ya mshangao Situ na Hassani.

Ni kama kimbunga kilichoambatana na Mwanga ndio kilichoonekana katikati ya vijana wote wa kundi la Black Mamba.

“Tuuu.. Tuuu Crackk Tuu ….Shwa ..Swahaa !!!”ulikuwa ni mlio ambao haukua wa kawaida kabisa, yaani vijana hawa walikuwa wakirushwa juu kama makaratasi na kudondokea upande mwingine na hakukua na mwenye uhai hata kidogo kwa kila aliekuwa akidondoka na haikueleweka Roma alikuwa akiwafanya vipi maana ni kitendo cha kasi sana alichokuwa akifanya , ilikuwa ni picha ya kushangaza sana kwa Rose.

“Nani kasema unaweza kukimbia?”

Aliuliza Roma kwa sauti nzito mara baada ya ya kumaliza vijana wote ishirini kwa dakika moja tu,jambo ambalo lilimfanya Hassani kukimbilia getini kujiokoa , lakini Roma hakuwa tayari kumuacha Hassani aondoke.

Hassani mkojo ulikuwa karibu sana , baada ya kuona Roma yupo mbele yake huku akiwa ni mwenye kushangaa kafikiwa vipi ukijumlisha na namna ambavyo Roma alikuwa akionekana , matundu yake yote ya kutoa taka mwili yalifunguka.

“Crack”Bila huruma Roma alimvunja shingo Hassani na huo ukawa mwisho wake.

Rose aliekuwa amesimama mita kadhaa , alimwangalia Roma huku akishindwa kuelewa hata hisia zake zipoje kwa wakati huo, alifikiria vitu vingi kwa wakati mmoja.

Zonga na yeye mkojo haukumpa msamaha, licha ya kwamba Roma alionekana kuwalinda lakini jambo ambalo amelishuhudia alikuwa amezoea kuona kwenye muvi za kimarekani pekee , lakini leo hii alikuwa akiona kila kitu laivu.

Situ alishindwa kukimbia , alikuwa amekaa chini huku akishindwa kuelewa nini kinachoendelea , yaani mwili ulikuwa ukitaka kukimbia lakini alikuwa akishindwa kufanya hivyo , ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kukimbizwa lakini viungo vyake vya mwili vilikuwa vikimsaliti.

Roma alisimama katikati ya bustani huku akiwa ni mwenye kushindana na mwili wake , alikua akijaribu kujirudisha kuwa wa kawaida, lakini alishindwa kabisa na palepale macho yake yalianza kubadilika na kuwa ya Rangi nyekundu kutoka njano , huku nguo alizovaa zikichanika kwani alikuwa akiongezeka ukubwa , Zonga aliekuwa chini alianza kuburuzika kurudi nyuma kwa woga
Endelea boss au umepitiwa na usingizi wakati ukitype
 
Katuacha njiani haijulikani ali over sleep wakati akitype au ndio aliitwa ale ki maskhara
kwa akili zenu mnaona anatyipe halafu akimaliza anatuma hapa?


hakuna mwandishi anayefanya hivyo.

wao Huwa wanaandika siku mbili au tatu kabla.
 
kwa akili zenu mnaona anatyipe halafu akimaliza anatuma hapa?


hakuna mwandishi anayefanya hivyo.

wao Huwa wanaandika siku mbili au tatu kabla.
Simulizi iko season 5 kipande cha 127 ,nichek watsapp , jumamosi nitamalizia season 4
 
Back
Top Bottom