Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Daaaah nkajua tutashushia na dinner ndgukumbe leo no j5 basi notaweka jioni
Nitasuburi nishaagiza popcornkumbe leo no j5 basi notaweka jioni
Naipataje mpaka ulipoishia.Haijafika mwisho ipo sehemu ya 123
Nifanyeje ili niwe napata notification ya huu uzi?SEHEMU YA 87
Roma na Rose walisogea mpaka katikati , huku wakiwa wamezungukwa na vijana wa kundi la Situ pamoja na wa Black mamba ambao kundi lake lilikuwa likiongozwa na Hassani.
Roma hakuonekana kuwa ni mwenye wasiwasi , ila kwa Rose alionyesha wasiwasi , kwani hakujua Roma ni jambo gani alilokuwa akitaka kulifanya.
Kiufupi licha ya Rose kujua Roma hakuwa ni wa kawaida na anajua kupigana, lakini mbele ya watu zaidi ya ishirini hakuamini kama Roma anaweza kuwamaliza wote kwa wakati mmoja , aliona ni jambo gumu kutekelezeka na ndio maana hakutaka Roma afanye jambo lolote hatarishi , kwani hakutaka kumuona akifa mbele yake.
“Dakika zilizopita ulikuwa ukijiamini sana Rose , kule kujiamini kumeenda wapi, angalia sasa unaonekana kama Sungura alienasa kwenye mtego”Aliongea Situ huku akimwangalia Rose kwa kejeli , lakini Rose aliishia kumwangalia baba yake kwa hasira , akishindwa ni kipi akifanye.
“Hassanni mbona unamwangalia sana huyu , kijana au na wewe unamfahamu?”Aliuliza Situ baada ya kuona Hasani muda wote alikuwa akimwangalia Roma.
“Situ huyu ndio mpuuzi aliemua Karimu Mtoto wa Meya”aliongea Hassani na kumfanya Situ ashangae , hakuwa ni mwenye kulijua hilo.
“Kama ni hivyo Hassani basi naamini leo kisasi chako kinakwenda kutimia na sio kwa Meya tu kwa kundi lote la Black Mamba kwa kupoteza kiongozi wenu, lakini Hassani ilikuweje Kibwengo kama huyu akamuua Karimu?”
“Hata mimi nashindwa kuelewa Situ , nipo kwenye mshangao kama wako , labda Karimu alikuwa amelewa”
“Bosi tunafanyaje?”Aliuliza Pengo ambaye alionekanaa kuchafuka kuliko alivyokuwa dakika chache zilizopita.
“Kuna kipi cha kufanya hapa, tunawaua kila mmoja na kwanzia leo kundi lote la Tembo litakuwa chini yangu … hahahaha”Aliongea huku akiwasha sigara yake kwa ajili ya kuvuta , lakini pia vijana wake wakicheka.
“Bosi unaonaje tukimuonja Rose kwanza , ninatamani kujua ni nini anakificha kwenye nguo kutokana na uzuri wake”.
“Licha ya Rose kuwa adui yangu lakini ni mwanangu , kumbaka ni kitendo cha kunidhalilisha , una bahati sana Pengo i mpala sasa ningekuwa nishakutandika Risasi”Aliongea Situ akiwa ni mwenye kuonesha hasira kweli , na Pengo akatulia tuli kwani alikuwa akimjua bosi wake hakuwa na utani kabisa ,akiamua kukuua haijalishi mmefahamiana kwa muda wa miaka mingapi anakupiga Risasi na hatonesha ishara yoyote ya kujutia.
Roma aliona mzee Situ licha ya kwamba alikuwa na roho mbaya lakini pia nati kuonekana kulegea , anagalau alimuona kama mtu anaelinda hadhi yake , kwani kwa maneno alioongea yalikuwa yakileta maana .
"Situ tunasubiria ruhusa yako maana wewe ndio mwenye shughuli , mimi nataka nianze na huyu mpuuzi hapa"Aliongea Hassani akimsogelea Roma alitaka kumshika .
"Usije ukanishika"
Aliongea Roma kwa tahadhari na sauti iliojaa lujiamini na kumfanya Hassani azuie mkono wake kwa sekunde na kisha akatabasamu na kuendelea kufanya kitendo chake na Roma alimkwepa.
Zonga mkojo ulikuwa ukitaka kumtoka , aliona anakwenda kufa usiku huo , hakuona namna yoyote ya wao kutoka Hai hapa ndani , na alimuona Roma kama kuku anaempigia kelele Mwewe .
"Jifanye jeuri tu , leo utakufa kifo cha maumivu , nitakuua taratibu kulipiza kisasi"Aliongea Hasaani , lakini Roma hakuwa na woga hata kidogo , alianza kuangalia mmoja mmoja hapa ndani , huku akianza kupiga hesabu zake
Na kwa haraka haraka aliona hawezi kuwamaliza vijana wote ishirini kwa wakati mmoja pasipo kujibadilisha lakini pia kwa vijana hao kumdhuru Rose , aliogopa pia kutumia uwezo wake kwani alijua anaweza asirudi kwenyehali ya kawaida ya ubinadamu.
Vijana walikuwa wamewazingira pande zote na ni malaika pekee ambaye Rose aliamini ndie ambaye angeweza kuwaokoa kwenye hali kama hio , hakuelewa ni jambo gani ambalo Roma anawaza , lakini licha ya hivyo aliona hakuna wazo ambalo linaweza likawaokoa pasipo yay eye kuchukua hatua.
“Situ nitakupa kila kitu ila naomba uwaachie Zonga na Mpenzi wangu waondoke”Aliongea Rose na kumshangaza Situ.
“Hahahaha…Rose unafikiriaje mapenzi kwenye hali kama hii, ni kwambie tu huna nafasi ya kufanya maongezi na mimi maana mpaka muda huu wewe ni mfu na kuhusu mali zako zipo mikononi mwangu dakika ambayo roho yako itaicha hii dunia”Aliongea Situ na kisha akampa ishara Hassani.
“Hassani naomba umalize kazi, muda unaenda , mpige Rose Rasisi ya moyo na kichwani ili kifo chake kisiwe cha maumivu”Aliongea Situ huku akitoa moshi mwingi wa sigara kupitia Puani huku macho yake yakiwa mekundu.
Hasaani Baada ya kuona kapata Ruhusa alimpa ishara kijana wake aliekuwa akimwamini ruhusa ya kufanya kama Situ alivyoelekeza , alitaka kumuua kwanza Rose halafu aondoke na Roma akampe mateso kwanza huku akimuua taratibu.
“Acha ujingaaa…!!!”
Ilikuwa ni sauti iliomshitua kijana ambaye alikuwa akitaka kumpiga Rose Risasi na hapa Sauti ya Roma haikuwa ya kawaida ilikuwa kama ya Roboti huku ikisikika mara mbili kwenye masikio ya watu hawa , ni kama ilikua ikitokea juu angani na kuja chini , kumbe aliekuwa ameongea yupo hapahapa ndani.
Situ ambaye alikuwa amegeuka nyuma na yeye aliisikia na kujikuta akiangalia upande wa alipo Hassani , ni kama hakuwa ni mwenye kuamini kama sauti hio imetokea hapa ndani.
Upande wa Rose na Zonga na wao waliogopeshwa na sauti hio,Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , kwani wakati wote alikuwa ameweka kichwa chake chini kusubiria Risasi.
Rose alijikuta akishangazwa na macho ya Roma yalikuwa ni ya Njano kama jua huku mwili wa Roma ukianza kutoa mvuke kiasi kwamba nguo zilianza kuloana kwa majimaji mazito yaliokuwa yakimtoka, huku harufu kama ya kuungua kwa nailoni ikianza kusambaa , vijana wa Situ wote waliweka sawa Bastora zao ,. Huku Hassani na Situ wakishangazwa na mabadiliko hayo, Hassani ile hali ya kujiamini ilipotea ghafla na alirudi nyuma haraka na pia hata Situ mwenyewe.
“Mpigeni Rasasi”Ilikuwa ni amri kutoka kwa situ na vijana wakainua risasi zao kwa ajili ya kufanya kazi lakini kilichotokea baada ya hapo kiliwaacha hoi na hali ya mshangao Situ na Hassani.
Ni kama kimbunga kilichoambatana na Mwanga ndio kilichoonekana katikati ya vijana wote wa kundi la Black Mamba.
“Tuuu.. Tuuu Crackk Tuu ….Shwa ..Swahaa !!!”ulikuwa ni mlio ambao haukua wa kawaida kabisa, yaani vijana hawa walikuwa wakirushwa juu kama makaratasi na kudondokea upande mwingine na hakukua na mwenye uhai hata kidogo kwa kila aliekuwa akidondoka na haikueleweka Roma alikuwa akiwafanya vipi maana ni kitendo cha kasi sana alichokuwa akifanya , ilikuwa ni picha ya kushangaza sana kwa Rose.
“Nani kasema unaweza kukimbia?”
Aliuliza Roma kwa sauti nzito mara baada ya ya kumaliza vijana wote ishirini kwa dakika moja tu,jambo ambalo lilimfanya Hassani kukimbilia getini kujiokoa , lakini Roma hakuwa tayari kumuacha Hassani aondoke.
Hassani mkojo ulikuwa karibu sana , baada ya kuona Roma yupo mbele yake huku akiwa ni mwenye kushangaa kafikiwa vipi ukijumlisha na namna ambavyo Roma alikuwa akionekana , matundu yake yote ya kutoa taka mwili yalifunguka.
“Crack”Bila huruma Roma alimvunja shingo Hassani na huo ukawa mwisho wake.
Rose aliekuwa amesimama mita kadhaa , alimwangalia Roma huku akishindwa kuelewa hata hisia zake zipoje kwa wakati huo, alifikiria vitu vingi kwa wakati mmoja.
Zonga na yeye mkojo haukumpa msamaha, licha ya kwamba Roma alionekana kuwalinda lakini jambo ambalo amelishuhudia alikuwa amezoea kuona kwenye muvi za kimarekani pekee , lakini leo hii alikuwa akiona kila kitu laivu.
Situ alishindwa kukimbia , alikuwa amekaa chini huku akishindwa kuelewa nini kinachoendelea , yaani mwili ulikuwa ukitaka kukimbia lakini alikuwa akishindwa kufanya hivyo , ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kukimbizwa lakini viungo vyake vya mwili vilikuwa vikimsaliti.
Roma alisimama katikati ya bustani huku akiwa ni mwenye kushindana na mwili wake , alikua akijaribu kujirudisha kuwa wa kawaida, lakini alishindwa kabisa na palepale macho yake yalianza kubadilika na kuwa ya Rangi nyekundu kutoka njano , huku nguo alizovaa zikichanika kwani alikuwa akiongezeka ukubwa , Zonga aliekuwa chini alianza kuburuzika kurudi nyuma kwa woga
Endelea boss au umepitiwa na usingizi wakati ukitypeSEHEMU YA 87
Roma na Rose walisogea mpaka katikati , huku wakiwa wamezungukwa na vijana wa kundi la Situ pamoja na wa Black mamba ambao kundi lake lilikuwa likiongozwa na Hassani.
Roma hakuonekana kuwa ni mwenye wasiwasi , ila kwa Rose alionyesha wasiwasi , kwani hakujua Roma ni jambo gani alilokuwa akitaka kulifanya.
Kiufupi licha ya Rose kujua Roma hakuwa ni wa kawaida na anajua kupigana, lakini mbele ya watu zaidi ya ishirini hakuamini kama Roma anaweza kuwamaliza wote kwa wakati mmoja , aliona ni jambo gumu kutekelezeka na ndio maana hakutaka Roma afanye jambo lolote hatarishi , kwani hakutaka kumuona akifa mbele yake.
“Dakika zilizopita ulikuwa ukijiamini sana Rose , kule kujiamini kumeenda wapi, angalia sasa unaonekana kama Sungura alienasa kwenye mtego”Aliongea Situ huku akimwangalia Rose kwa kejeli , lakini Rose aliishia kumwangalia baba yake kwa hasira , akishindwa ni kipi akifanye.
“Hassanni mbona unamwangalia sana huyu , kijana au na wewe unamfahamu?”Aliuliza Situ baada ya kuona Hasani muda wote alikuwa akimwangalia Roma.
“Situ huyu ndio mpuuzi aliemua Karimu Mtoto wa Meya”aliongea Hassani na kumfanya Situ ashangae , hakuwa ni mwenye kulijua hilo.
“Kama ni hivyo Hassani basi naamini leo kisasi chako kinakwenda kutimia na sio kwa Meya tu kwa kundi lote la Black Mamba kwa kupoteza kiongozi wenu, lakini Hassani ilikuweje Kibwengo kama huyu akamuua Karimu?”
“Hata mimi nashindwa kuelewa Situ , nipo kwenye mshangao kama wako , labda Karimu alikuwa amelewa”
“Bosi tunafanyaje?”Aliuliza Pengo ambaye alionekanaa kuchafuka kuliko alivyokuwa dakika chache zilizopita.
“Kuna kipi cha kufanya hapa, tunawaua kila mmoja na kwanzia leo kundi lote la Tembo litakuwa chini yangu … hahahaha”Aliongea huku akiwasha sigara yake kwa ajili ya kuvuta , lakini pia vijana wake wakicheka.
“Bosi unaonaje tukimuonja Rose kwanza , ninatamani kujua ni nini anakificha kwenye nguo kutokana na uzuri wake”.
“Licha ya Rose kuwa adui yangu lakini ni mwanangu , kumbaka ni kitendo cha kunidhalilisha , una bahati sana Pengo i mpala sasa ningekuwa nishakutandika Risasi”Aliongea Situ akiwa ni mwenye kuonesha hasira kweli , na Pengo akatulia tuli kwani alikuwa akimjua bosi wake hakuwa na utani kabisa ,akiamua kukuua haijalishi mmefahamiana kwa muda wa miaka mingapi anakupiga Risasi na hatonesha ishara yoyote ya kujutia.
Roma aliona mzee Situ licha ya kwamba alikuwa na roho mbaya lakini pia nati kuonekana kulegea , anagalau alimuona kama mtu anaelinda hadhi yake , kwani kwa maneno alioongea yalikuwa yakileta maana .
"Situ tunasubiria ruhusa yako maana wewe ndio mwenye shughuli , mimi nataka nianze na huyu mpuuzi hapa"Aliongea Hassani akimsogelea Roma alitaka kumshika .
"Usije ukanishika"
Aliongea Roma kwa tahadhari na sauti iliojaa lujiamini na kumfanya Hassani azuie mkono wake kwa sekunde na kisha akatabasamu na kuendelea kufanya kitendo chake na Roma alimkwepa.
Zonga mkojo ulikuwa ukitaka kumtoka , aliona anakwenda kufa usiku huo , hakuona namna yoyote ya wao kutoka Hai hapa ndani , na alimuona Roma kama kuku anaempigia kelele Mwewe .
"Jifanye jeuri tu , leo utakufa kifo cha maumivu , nitakuua taratibu kulipiza kisasi"Aliongea Hasaani , lakini Roma hakuwa na woga hata kidogo , alianza kuangalia mmoja mmoja hapa ndani , huku akianza kupiga hesabu zake
Na kwa haraka haraka aliona hawezi kuwamaliza vijana wote ishirini kwa wakati mmoja pasipo kujibadilisha lakini pia kwa vijana hao kumdhuru Rose , aliogopa pia kutumia uwezo wake kwani alijua anaweza asirudi kwenyehali ya kawaida ya ubinadamu.
Vijana walikuwa wamewazingira pande zote na ni malaika pekee ambaye Rose aliamini ndie ambaye angeweza kuwaokoa kwenye hali kama hio , hakuelewa ni jambo gani ambalo Roma anawaza , lakini licha ya hivyo aliona hakuna wazo ambalo linaweza likawaokoa pasipo yay eye kuchukua hatua.
“Situ nitakupa kila kitu ila naomba uwaachie Zonga na Mpenzi wangu waondoke”Aliongea Rose na kumshangaza Situ.
“Hahahaha…Rose unafikiriaje mapenzi kwenye hali kama hii, ni kwambie tu huna nafasi ya kufanya maongezi na mimi maana mpaka muda huu wewe ni mfu na kuhusu mali zako zipo mikononi mwangu dakika ambayo roho yako itaicha hii dunia”Aliongea Situ na kisha akampa ishara Hassani.
“Hassani naomba umalize kazi, muda unaenda , mpige Rose Rasisi ya moyo na kichwani ili kifo chake kisiwe cha maumivu”Aliongea Situ huku akitoa moshi mwingi wa sigara kupitia Puani huku macho yake yakiwa mekundu.
Hasaani Baada ya kuona kapata Ruhusa alimpa ishara kijana wake aliekuwa akimwamini ruhusa ya kufanya kama Situ alivyoelekeza , alitaka kumuua kwanza Rose halafu aondoke na Roma akampe mateso kwanza huku akimuua taratibu.
“Acha ujingaaa…!!!”
Ilikuwa ni sauti iliomshitua kijana ambaye alikuwa akitaka kumpiga Rose Risasi na hapa Sauti ya Roma haikuwa ya kawaida ilikuwa kama ya Roboti huku ikisikika mara mbili kwenye masikio ya watu hawa , ni kama ilikua ikitokea juu angani na kuja chini , kumbe aliekuwa ameongea yupo hapahapa ndani.
Situ ambaye alikuwa amegeuka nyuma na yeye aliisikia na kujikuta akiangalia upande wa alipo Hassani , ni kama hakuwa ni mwenye kuamini kama sauti hio imetokea hapa ndani.
Upande wa Rose na Zonga na wao waliogopeshwa na sauti hio,Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , kwani wakati wote alikuwa ameweka kichwa chake chini kusubiria Risasi.
Rose alijikuta akishangazwa na macho ya Roma yalikuwa ni ya Njano kama jua huku mwili wa Roma ukianza kutoa mvuke kiasi kwamba nguo zilianza kuloana kwa majimaji mazito yaliokuwa yakimtoka, huku harufu kama ya kuungua kwa nailoni ikianza kusambaa , vijana wa Situ wote waliweka sawa Bastora zao ,. Huku Hassani na Situ wakishangazwa na mabadiliko hayo, Hassani ile hali ya kujiamini ilipotea ghafla na alirudi nyuma haraka na pia hata Situ mwenyewe.
“Mpigeni Rasasi”Ilikuwa ni amri kutoka kwa situ na vijana wakainua risasi zao kwa ajili ya kufanya kazi lakini kilichotokea baada ya hapo kiliwaacha hoi na hali ya mshangao Situ na Hassani.
Ni kama kimbunga kilichoambatana na Mwanga ndio kilichoonekana katikati ya vijana wote wa kundi la Black Mamba.
“Tuuu.. Tuuu Crackk Tuu ….Shwa ..Swahaa !!!”ulikuwa ni mlio ambao haukua wa kawaida kabisa, yaani vijana hawa walikuwa wakirushwa juu kama makaratasi na kudondokea upande mwingine na hakukua na mwenye uhai hata kidogo kwa kila aliekuwa akidondoka na haikueleweka Roma alikuwa akiwafanya vipi maana ni kitendo cha kasi sana alichokuwa akifanya , ilikuwa ni picha ya kushangaza sana kwa Rose.
“Nani kasema unaweza kukimbia?”
Aliuliza Roma kwa sauti nzito mara baada ya ya kumaliza vijana wote ishirini kwa dakika moja tu,jambo ambalo lilimfanya Hassani kukimbilia getini kujiokoa , lakini Roma hakuwa tayari kumuacha Hassani aondoke.
Hassani mkojo ulikuwa karibu sana , baada ya kuona Roma yupo mbele yake huku akiwa ni mwenye kushangaa kafikiwa vipi ukijumlisha na namna ambavyo Roma alikuwa akionekana , matundu yake yote ya kutoa taka mwili yalifunguka.
“Crack”Bila huruma Roma alimvunja shingo Hassani na huo ukawa mwisho wake.
Rose aliekuwa amesimama mita kadhaa , alimwangalia Roma huku akishindwa kuelewa hata hisia zake zipoje kwa wakati huo, alifikiria vitu vingi kwa wakati mmoja.
Zonga na yeye mkojo haukumpa msamaha, licha ya kwamba Roma alionekana kuwalinda lakini jambo ambalo amelishuhudia alikuwa amezoea kuona kwenye muvi za kimarekani pekee , lakini leo hii alikuwa akiona kila kitu laivu.
Situ alishindwa kukimbia , alikuwa amekaa chini huku akishindwa kuelewa nini kinachoendelea , yaani mwili ulikuwa ukitaka kukimbia lakini alikuwa akishindwa kufanya hivyo , ni kama alikuwa kwenye ndoto ya kukimbizwa lakini viungo vyake vya mwili vilikuwa vikimsaliti.
Roma alisimama katikati ya bustani huku akiwa ni mwenye kushindana na mwili wake , alikua akijaribu kujirudisha kuwa wa kawaida, lakini alishindwa kabisa na palepale macho yake yalianza kubadilika na kuwa ya Rangi nyekundu kutoka njano , huku nguo alizovaa zikichanika kwani alikuwa akiongezeka ukubwa , Zonga aliekuwa chini alianza kuburuzika kurudi nyuma kwa woga
Katuacha njiani haijulikani ali over sleep wakati akitype au ndio aliitwa ale ki maskharaMkuu leo vipande viongezeke basi
kwa akili zenu mnaona anatyipe halafu akimaliza anatuma hapa?Katuacha njiani haijulikani ali over sleep wakati akitype au ndio aliitwa ale ki maskhara
Simulizi iko season 5 kipande cha 127 ,nichek watsapp , jumamosi nitamalizia season 4kwa akili zenu mnaona anatyipe halafu akimaliza anatuma hapa?
hakuna mwandishi anayefanya hivyo.
wao Huwa wanaandika siku mbili au tatu kabla.
hakuna taabu chief we tupia Kwa muda wako nilikuwa nakutetea kutokana na hao wanaofikiri unaandika Kisha unatupia hapa muda huo huo.Simulizi iko season 5 kipande cha 127 ,nichek watsapp , jumamosi nitamalizia season 4