SEHEMU YA 232
“Malengo yao hapa duniani ni kwa ajili ya kuitawala dunia”Aliongea Zoe na kumfanya Nadia kushangaa mno.
“Lakini umesema kwamba wana uwezo mkubwa , kwanini mpaka sasa hawajaweza kufanya hivyo?”
“Niliuliza hivyo hivyo Nadia, na alinijibu kwamba miungu hio mpaka sasa haijaweza kuwa na uwezo wao wa kawaida kwani walipoteza mawe waliokuja nayo duniani ambayo yanawapa nguvu , kwa maneno marahisi ni kwamba miungu hio mpaka sasa ni dhaifu na siku ambapo itaweza kupata ‘Godstone’ zote basi nguvu zao zitarudi upya na watakuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote hata kuponya magonjwa, na hapo ndipo ‘New World Order’ itakapoanza , kwasababu watajifanya kuwa wao ndio Mungu, kwani watakuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote ambalo Mungu anaweza kulifanya , wataweza kushusha mvua , wataweza kuponya magongwa na kuyasababisha , wtafanya miujiza mingi na kwasababu binadamu tunapenda ushahidi wa kimiujiza basi tutawafuata”Nadia alijikuta akiogopa sana juu ya meneno hayona kwake aliona ni kama jambo ambalo haliwezekani.
“Unaweza ukashangaa ndio maana Kwa kukurahisishia tu ni kwamba hawa viumbe wanabadilisha miili yao kila baada ya miaka kadhaa na wanafanya ‘Transmigration’ tena na hii yote ni kutokana na kwamba miili yetu sisi binadamu ni ‘mortal’ yaani miili yetu inazeeka baada ya muda na kufa”
“Nadia nadhani uliona Cromwell family, Stern na Alice kuwa ndugu wa damu na ukashangaa kwanini hawa ndugu wa damu wa kawa wapenzi , jibu ni kwamba licha ya wao kuwa na damu zinazofanana za kindugu lakini nafsi zao za kibinadamu zishatekwa na wanatawaliwa na nafsi ya Artemis na Apollo”Alimalizia.
“Lakini mbona Stern na Alice wananguvu za ajabu kwa nilivyoona?”
“Ndio sijasema hawana nguvu, ila ukweli ni kwamba nguvu wanazo ila ni kidogo sana , robo tatu za nguvu zao zilikuwa zikitawaliwa na miili yao , lakini miili yao ilishindwa kuhimili mazingira ya dunia, hivyo hatua ya kwanza ambayo wataweza kurudisha nguvu zao ni kuhakikisha wanapata Godstone na kwakutumia hizo Godstone wataweza kuifanya miili kuwa Immortal na nguvu zao zitarudi upya na hapo utawala rasmi wa hao viumbe wa kishetani utaanza”
“Wako wangapi waliofika duniani?”
“Paa..Paah …!!”Mrembo Zoe alipiga makofi kwa kufurahishwa na swali la Naidia.
“Mellisa tunae mtu sahihi , swali zuri sana Nadia umeuliza”
“Kwa maelezo ambayo hayajathibitika ni kwamba wapo Zaidi ya maelfu”
“Nini… a!!!”
“Ndio hivyo, lakini licha ya hivyo kati ya hao wote waliokuwa na nguvu Zaidi kuliko wengine ni kumi na mbili pekee na hao wote kumi na mbili ni wa ukoo mmoja yaani familia moja na hadithi zinaonyesha kwamba huenda hao kumi na mbili walitokea katika familia za kifalme huko kwenye dunia yao “
“Kuhusu wengine vipi?”
“Wengine haijafahamika , lakini kuna wanaoamini kwamba wengi wao nafsi zao zimebebwa na raia wengi wa Marekani , Uchina, Korea, Urusi ….. hakuna Ushahidi wowote unao onyesha viumbe hawa kuvaa jamii ya Kiafrika na baadhi ya Sehemu nyingi ndani ya mataifa ya bara la Asia japo wapo”Aliongea na kumfanya Nadia kuvuta pumzi , ukweli siku hio ya leo alijikuta kujua mambo mengi ambayo hakuwahi kuyafahamu hapo kabla.
Sasa mpaka hapo maelezo ya Zoe Pamoja na Mellisa ni kwamba kuna Zaidi ya majiwe ya Kimungu ambayo yapo hapa duniani na yanamilikiwa na binadamu wa kawaida na hawa miungu watu ili kupata nguvu zao upya ni lazima wapate Godstone`s zao.
“Naomba niulize swali la mwisho”
“Nadia kuna mambo mengi sana ambayo sijayaelezea ila kwa sasa hupasiwi kuuliza maswali mengi kwani tutakesha pasipo kuzungumza mpango mwingine , lakini nitakuruhusu kuuliza swali lingine”
“Umesema Hades wa zamani alikuwa na tabia kama za wengine wote , lakini pia ukasema kwamba Roma hajatawaliwa na nafsi ya Hades , sasa kama ni kweli nafsi ya Hades wa zamani iko wapi?”
“Hilo swali halina majibu halisi na hata Seventeen hakuweza kutuelezea , ila inasemekeana Nafsi yake ilikufa kabisa na alijiua yeye mwenyewe , lakini kutoka tetesi kutoka kwa jamii nyingi za siri wanaamini Nafsi ya Hades imerudi ilikotoka”Aliongea Mellisa .
“Kwahio Nadia we are here to fight the Darknes”Aliongea Zoe.
“And what abaout our Allies?”
“You will learn them as far as you prove to be usefull for the plan , as for now the plan is to replicate”
“Unamaanisha nini ku replicate ?”
“Nadia mambo haya mpaka sasa hayajatokea kwasababu tu, watu wa nuru ni wengi kuliko watu wa kiza , ikitokea watu wa kiza wakaongezeka kuliko wa nuru basi ndio utakuwa mwisho , hivyo ili kuhakikisha kiza hakichukui nafasi yake lazima tunaofanana tuwe wengi , huo ndio mpango”Aliongea Mellisa.
“Ni kweli Mungu yupo , yeye mwenye ukuu wa kila kitu?”Aliuliza Nadia lakini Mellisa alitabasamu.
“Nadia nafasi ya kuuliza kwa leo ishaisha , lakini kukupa motisha ni kwamba , yes Mungu yupo na huenda binadamu hatujafaamu namna halisi ya kuuelezea uwepo wake that is why things for now is complicated but all prophecies seems to be true”
Unafikiri wataweza kushindana na unabii , ngoja tuone yajayo.
*********
(UNKOWN PLACE)
SEHEMU ISIOFAHAMIKA NDANI YA DUNIA
Ni sehemu abayo haifahamiki ndani ya dunia kama ipo juu ya Ardhi au chini ya maji , ila ni sehemu ambayo ipo duniani.
Sasa basi ndani ya hii sehemu anaonekana Athena , mwanamke mrembo akiingia ndani ya eneo moja zuri mno lililotegenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu , naweza kusema kwamba eneo hili kama utalitafuta hapa Duniani basi huwezi kupata , juu na chini ndani ya eneo hili kulikuwa kunafanana , yaani nikimaanisha kwamba rangi na muundo uliokuwa upo juu na chini yake vinafanana kwa kila kitu , lakini utofauti wa eneo hili na maeneo mengine ni kwamba tu humu ndani ni kama jengo ambalo linaelea angani , lakini wakati huo huo eneo hili lilionekana kama sehemu ambayo imejengwa juu ya jangwa ni sehemu ambayo uwezi kuelezea kwa maneno yakinifu na yakaeleweka.
Sasa ilishindikikana kuelewa ni wapi ndani ya hili eneo kwasababu namna ambavyo Athena ameweza kuingia ndani ya hili eneo ni kwa namna ya kipekee sana , yaani namna ya kuibukia kama jini.
Sehemu hii ilikuwa na mwanga , lakini chanzo cha mwanga hakikuonekana yaani ni kama uingie ndani ya chumba kuwe na mwanga alafu huoni taa zilipo sasa ndio ndani ya hili eneo.
Mrembo Athena kwenye mikono yake hakuwa peke yake bali alikuwa amembeba mwanamke alievalia mavazi meusi kabisa na kutokana na mwanga ukimwangalia huyu mwanamke anafanana kwa asilimia mia moja na Edna.
Athena alitembea huku akiwa amembeba Mwanamke kwenye mikono yake kama mtoto huku akipita kwenye Korido ambavyo imejengwa kama Tunnel , na alikuja kusimamma mwisho kabisa wa korido hio na mwanga uliokuwa nyuma yake ulipotea na kukawa giza tii, lakini muda uleule mbele yake kukafungunga mlango kwa namna ya ‘pentagon, na eneo la mbele liling`aa kwa mwanga hafifu wa kuvutia rangi ya LED na baada ya kuingia ndani mlango ulijifunga vilevile .
“Naira I am Back”Aliongea Athena huku akiingia ndani ya eneo lililokuwa limejengwa kwa utaalamu mkubwa na vioo vingi na chuma kiasi , huku vifaa vingi vya kilektronic vikibip sauti , lilikuwa ni eneo zuri kwa kweli ambalo halielezeki.
“Who is this?”Aliuliza Naira alievalia Miwani kubwa na nguo za bluu tupu kwanzia juu hadi chini , alikuwa ni mwanamke mrembo sana na kwa kumwangalia umbo lake ni kama Nasra, tofauti pekee ni kwamba yeye alikuwa mzungu.
“Huyu ni Seventeen , Mpenzi wa Hades”Aliongea Athena huku akimpita Naira aliesimama na alikunja kushoto na kufikia mlango wa kioo na ulijufungua wenyewe na akaingia ndani , sehemu ambayo ipo na makabati mengi majeneza lakiini ya kioo tupu jumla yake manne , yaliopangwa kwa ustadi mkubwa kwakuachana kwa mita moja moja , huku eneo hilo linatoa mwanga flani hivi ambao umeambatana na mvuke kama vile maji yanachemka na haikueleweka mvuke huo unatoka wapi.
“Nishaua nafsi yake na kuiharibu kabisa , hivyo kwasasa huyu sio binadamu bali ni Shell”Aliongea.
“Unataka kutumia mwili wake?”Aliuliza Naira na Athena mrembo alitabasamu.
“Yes , ana mwili mzuri sana na ni mrembo kupindukia na napenda mwili wa mwanamke mrembo kama nitataka kuitawala dunia, nitamtumia lakini sio sasa , huu mwili niliokuwa nao unanitosha , she will be in Cryosleep mpaka nitakapo muhitaji”Aliongea huku akiingiza mwili wa Seventeen kwenye jeneza la kisasa.
“Boss lakini kwanini nahisi kama kuna jambo halipo sawa na sauti yako , there is no Confidence the way you sound”Aliongea Naira na Athena alifikiria kidogo huku akinuna.
“It`s nothing Naira , twende ukanipe ripoti”Aliongea na kisha wakatoka na kwa jinsi eneo hili lilivyokuwa tulivu ilionyesha kabisa wapo watu wawili pekee.
Walirudi katikati ya lile na kisha wakachukua upande wa kulia na walisimama mbele ya mlango ambao ulijifungua kwa namna flani hivi ya kushangaza kama vile uliyeyuka hewani , yaani unachotakiwa kuelewa ndani ya hili eneo vifaa vyote havijatengenezwa kwa mundo wa pembe nne , ni duara na Pentagon peke yake..
Baada ya kuingia ndani ya chumba kingine, hatimae ilionekana maabara kubwa ya kisasa , lakini jambo la kushangaza ni kwamba hakukuwa na ina yoyote ya kemikali bali kulikuwa na meza kubwa upande wa kulia , juu ya meza hii kulikuwa na vifaa flani hivi kama vile jiko la mkaa lakini la bati ambalo ni duara kamili , juu yake kulikuwa na sinia flani linalong`aa kama kijiko ila juu ya sinia limefunikwa na bakuli muundo wa chupa kubwa ,ila yenye rangi ya kioo , ukiangalia kwa mbali utadhania ni balbu za taa , kwani machupa yale yalikuwa yakitoa mng`ao flani hivi na ilionyesha nani yake kuna kitu ambacho kilikuwa kikisababisha mwanga kutoka , jumla yake machupa yapo kumi pekee.
“Naweza kuona maendeleo ni mazuri Naira , you worked hard for this, When we find the last one , we will finalize the Mission and Stage four will follow”Aliongea na kisha akafunua bakuli moja na palepale mwanga ukapotea kwenye lile bakuli na ndani yake kulionekna jiwe la Kimungu, ‘Godstone”
“Boss kwahio likipatikana jiwe la mwisho misheni itakuwa tayari?”
“Ndio Naira kila kitu kitakuwa tayari “
“Lakini kwa maelezo ulisema mawe haya yanatakiwa kuwa kumi mbili na hapa yapo kumi na moja pekee”
“Uko sahihi hapa kuna mawili hayapo, moja lipo kwenye misheni nyingine na la mwisho sijalipata bado, Naira wewe ni rafiki yangu na nimekupenda kwakua umeamua kunitii ,hata nilivyoamua kuwaua wazazi wako Pamoja na wa rafiki yako Dorisi hukuweka kinyongo na mimi , ndio maana nakujibu kila unapouliza swali”Aliongea na kurudisha lile bakuli juu yake na likaungana na mengine kuwaka rangi kwa namna ya kupumua.
“Nilikubali kuwa mshirika wako, licha ya kuwaua Ryan na Epholia wazazi wangu kwasababu una ndoto za kuubadilisha ulimwengu na kuwa sehemu salama Zaidi , wamekufa kwa ajili ya sababu kubwa hivyo naamini vifo vyao havitopotea bure”Aliongea Naira na Athena alitabasamu na kisha wote wakatoka.
“Una akili kubwa sana you are far different”Aliongea
“Thank you The Doni”Aliongea Naira huku akicheka cheka.
“I hate those Stupid human being when they address me with that horrible name, it`s no swag at all”
“Ni kwasababu hukuwapatia jina zuri kwa ajili ya kukuita”aliongea Naira na Athena akatabasamu.
“Naira naona kila kitu unachofikiria kwenye moyo wako, nitakutumia kwa sasa na baada ya thamani yako kwangu kuisha nitakuua , umepata bahati ya kufanya kazi na mimi kwasababu ulikuwa wa tofauti”Aliwaza Athena kwenye moyo wake.
Sasa hapa haikueleweka Athena alikuwa na mpango gani , lakini pia haikueleweka , Mchina yaani babu yake Lanlan waliishia wapi kwani jana yake walikuwa wakifukuziana na sasa tunamuona
Seventeen akiwa ashakufa tayari na mwili wake upo kwenye Cryosleep.
Transmigration ni kitendo cha nafsi(Saoul) kuhama kutoka katika mwili mmoja Kwenda kwa mwingine.
Cryosleep ni pale binadamu anapohifadhiwa kwenye mashine kama friji ili asiweze kuoza ama kuzeeka hata kama alale miaka mingapi.
Hapa inaonekana Seventeen alikuwa akikiona kifo chake ndio maana akavunja uhusiano na mtoto wake , je atakuwa anafahamu uwepo wa Edna ndio maana akafanya vile, noja tuone.
Usichanganyikiwe kila kitu nimekipangilia vizuri yaani…..