Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 293

Ni ndani ya masaa machache tu kwa kutumia gari ambayo ilikuwa ikiendeshwa na Tanya , waliweza kufika ndani ya jiji la Osaka , katika uwanja wa ndege wa Kansai.

Watu wengi walikuwa wakimwangalia Roma alietangulizana na mrembo Tanya kwa macho yasiokuwa ya kawaida , lakini Roma wala hakujali na hivyohivyo kwa Tanya hakuonyesha hali ya kujali macho ya wajapani wenzake , alichokifanya ni kumuongoza Roma mpaka upande wa VIP kwa ajili ya kupita bila ukaguzi , kwani alikuwa akitumia ndege binafsi.

Dakika chache mbele walikuwa kwenye gereji ndani ya uwanja huu wa ndege na Roma aliweza kushuhudia ndege ndogo aina ya Airbus , ilikuwa ni ndege ambayo licha ya kuonekana kuwa ndogo , lakini Roma aliamini Gharama yake itakuwa ni kubwa sana kuinunua kwani kama utaifananisha na ndege ya kawaida basi italingana na ndege za shirika la Precision air kwahapa Tanzania.

Sasa Roma kwa kuona ukubwa na ufahari wa ndege hii aliamini moja kwa moja maneno ya Tanya juu ya thamani halisi na ukubwa wa kundi la Yamata, aliamini kama kweli kila kiwanja ndani ya Japani kuna ndege ya ukubwa huo basi Yamata ni kundi kubwa sana kushinda hata la Takamagahara.

Roma aliingia ndani ya Cabin katika ndege hio na kujikuta akitabasamu baada ya kuona samani za bei ya juu , ndege hio kwa ndani ilionekana kupambwa kwa namna ya kipekee sana , masofa yaliotengenezwa kwa Ngozi ya kondoo wa sufu kutoka Japani , lakini pia thamani zilizotengenezwa na Mahogany lakini pia chupa za bia ambazo zilikuwa ndani ya jokofu zilimfanya Roma kujihisi ni kama yupo hotelini na sio kwenye ndege.

Roma baada ya kukaaa na kupumua kwa ahueni alijikuta akijishangaa kwanini Maisha yake nchini Tanzania ni ya kawaida sana , kwani alikuwa na pesa nyingi sana benki pesa ambazo kama ataamua kutumi pasipo kufanya kazi basi anaweza kuishi miaka mia pasipo ya hela yote kuisha , alijiambia kuna ulazima akirudi Tanzania kufikiria namna ya kuishi kutokana na thamani ya utajiri wake.

Tanya alikuwa ashabadili mavazi yake na sasa alikuwa amevalia mavazi ya kitamaduni ya kijapani mara baada ya kuingia kwenye ndege hio huku akiwa ameshikilia sahani , alionekana yeye ndio anakwenda kuwa mhudumu akimsindikiza Roma mpaka Hokkaido.

Roma alimwangalia Tanya kwa jinsi alivyovaa na kuamini mwanamke huyo alikuwa akitafuta namna ya kuziamsha hisia zake , kwani vazi lake licha ya kwamba lilionekana kuwa la kitamaduni , lakini eneo la kifua chake lilikuwa wazi na kufanya manyonyo yake kuonekana.

“Mfalme hii wine ni kwa ajili yako , imetengenezwa na mchele kutoka Hokkaido , lakini pia na maji maalumu kutoka Nishinomiya na mbinu yetu maalaumu ambayo sisi Yamata huitumia”Aliongea Tanya huku akiminina wine kwenye glass na kumfanya Roma kumeza mate kwani harufu tu ilimfanya kuamini Wine hio itakuwa tamu.

Tanya mara baada ya kuminima kwa mapozi ile wine , Roma aliichukua Glass na kisha akagida wine yote kwa mkupuo mmoja na ile anarudisha glass chini alijikuta macho yake yakiongezeka ukubwa , kwani Tanya alievalia Kimono , alikuwa amefungua mkanda kulifunga gauni lake na kumfanya kumuacha wazi , na Roma aligundua mrembo huyo ndani yake hakuvalia nguo yoyote Zaidi ya vazi hilo la kitamaduni, Roma alielewa mtego wa Tanya , lakinii hakuw akwenye mudi ya kufanya chochote.

“Unaweza Kwenda kufanya mambo yako , sitaki ujitoe sana kwangu”Aliongea Roma na kumfanya Tanya kuonyesha hali ya kutofurahishwa na jibu la Roma , ni kama alitegemea kufanywa na Roma na jibu lake lilimnyong`onyesha.

*********

Profesa Clark aliekuwa ndani ya jiji la Hongkong kwa ajili ya semina maalumu ndani ya chuo kikuu cha Hongkong , mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Hades na kujua hali yake, alionekana kuwa na wasiwasi mno.

Mrembo huyo hakuwa na muda wa kupoteza kabisa, kwani ndani ya madakika kadhaa tu alikuwa kwenye ndege ya kukodi akielekea Hokkaido Japani , yaani wakati Roma anapanda ndege Kwenda Sapporo , upande wa Clark alikuwa na masaa mawili angani tokea aanze safari.

Upande wa Roma hakuwa na wasiwasi sana juu ya ndoa ya Mrembo amina , kutokana na taarifa za Makedoni alivyomwambia ni kwamba ndoa yake ilikuwa ikitarajiwa kufungwa siku mbili mbele yaani tarehe 26 ndani ya jiji la Otaru Ishikari Bay , hivyo mpango wake wa kwanza ni Kwenda kwanza Sapporo kuonana na Profesa Clark na baada ya hapo ndio aende Otaru.

Masaa mawili ya kuwa angani hatimae Roma aliweza kufanikiwa kufika ndani ya ya jiji la Sapporo.

Profesa Clark aliekuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau alionekana akiwa ameegamia gari aina ya Nissani nyeupe yenye namba za usajli 370Z , ilionekana mrembo huyo alikuwa amefika hapo uwanja wa ndege muda mrefu kidogo.

Watu mbalimbali waliokuwa ndani ya eneo hilo walikuwa wakimwangalia kwa macho ya kumsanifu kutokana na urembo wake, lakini sio hivyo tu baadhi ya watu waliweza kumtambua kama mtoto wa malkia kutoka Wales na hio ilifanya kuzidi kushangaa na kujiuliza yupo hapo uwanja wa ndege kumsubiria nani.

Profesa Clark alijikuta akibetua mdomo mara baada ya kumshuhudia Roma akitoka kwenye mlango wa wanaowasili akiwa ametangulizana na mwanamke wa kijapani ambaye alionekana kuwa mrembo kwenye macho yake , katika akili yake aliamini huenda huyo mwanamke ni hawala wa Roma.

“Is she your new lover again?”Aliuliza Clark pasipo hata ya salamu , alionekana kuwa na wivu , lakini pia alikuwa akifahamu Roma alikuwa na wanawake wengi hivyo aliuliza namna hio kwa kudhania ni ongezeko lingine.

“Do I look like someone so casual?”Aliongea Roma akimaanisha kwamba je anaonekana kama mtu muhuni muhuni

“You don’t look like one , you are one”Aliongea Clark akimwambia kwamba sio kwamba anaonekana kama muhumi , bali ni kweli yeye ni muhui , Roma alitabasmau huku akishika pua yake.

“Unaonaje tukiingia kwenye gari kwanza ndio unifokee, Tanya wewe tafuta vijana wako, nitaondoka na huyu mwanamke”Aliongea Roma na Tanya aliinamisha kichwa kuonyesha heshima mpaka pale gari ilivyoondolewa.

“Huyo mrembo ni kiongozi mpya wa kundi la Yamata , anafahamika kwa jina la Tanya”Aliongea Roma na kumfanya Clark kushangaa kidogo.

“Ninachofahamu ni kwamba kiongozi wa kundi la Yamata Sect ni Noriko Okawa… Roma usiniambie umemuua?”Aliongea kwa mshangao

“Ndio amekufa , lakini siwezi kusema mimi ndio nimemuua , ni maelezo ambayo nitakuelezea baadae”Aliongea Roma na Clark alitingisha kichwa huku macho yake yakiwa barabarani.

“Ilikuwaje mpaka ukawekewa sumu? , sijawahi kudhania kama kuna mtu anaweza akafanikiwa kukuwekea sumu?”

“It can’t be explained in short time”AliongeaRoma huku akijiegamiza kwenye kiti , ukweli ni kwamba alikuwa akijisikia vibaya bado na alihisi kama mwili wake ulikuwa kidonda chenye usaha, ijapokuwa aliweza kutumia mbinu ya kijini kushindana na nguvu ya sumu , lakini hapo haikumaanisha kwamba amepona , kwake lilikuwa swala la muda tu sumu hio isipoondolewa kumletea shida.

“I asked one of my student to empty out bioengineering research institute before I came here , we can go over there to conduct a comprehensive inspections”Aliongea akimaanisha kwamba amemuomba moja ya wanafunzi wake kuondoa watu waliokuwa ndani ya taasisi ya kibiolojia ili aweze kumfanyia Roma majaribio kufahamu afya yake ilivyo kwa kina.

“Una wanafunzi kila kona ya dunia”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Ni kweli , ijapokuwa sikutaka kuchukua baadhi yao , lakini wamekuwa ving’ang’anizi na kujikuta sina jinsi ya kuwasapoti “Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu.

“Kila mara tunapo onana nakuona kama umebadilika , miaka kumi na moja nyuma wakati nakuokoa wewe na Cahethirne sikuamini mtoto kama wewe utakuja kuwa msaada mkubwa kwangu”Aliongea Roma

“Mimi sio mtoto , mtu yoyote akituona atasema tunalingana tu”Aliongea akionyesha hakupenda kuitwa mtoto.

Gari ilikuja kusimama upande wa magharibi wa jiji la Sapporo pembeni kidogo ya eneo lenye kijimsitu na mlima na kwa maelezo ya Clark sehemu hio ndio kwenye taasisi hio ya kufanyia majaribio.

Dakika chache mbele Clark na Roma waliingia ndani ya jengo hilo la gorofa kama tano Kwenda juu la kisasa kabisa, lilikuwa na jengo ambalo lina vifaa vyenye teknolojia ya hali ya juu , nadhani ndio maana Clark akachagua sehemu hio kwa ajili nya kumfanyia Roma majaribio mwili wake.

Profesa Clark baada ya kumuongoza Roma mpaka kwenye maabara , alichukua sindano na kisha alitoa damu yake kiasi na kisha akamwambia Roma asubiri nje mpaka atakapomaliza ndani ya lisaa limoja na Roma kwakua alikuewa akielewa moja ya tabia za wanasayansi kutotaka kusimamiwa wakati wa kufanya kazi zao , aliamua kutoka kupandisha mpaka juu kabisa ya jengo hilo kwa ajili ya kupigwa na upepo.

Lucha ya kwamba kulikuwa na baridi lakini kwake haikumsumbua kama watu wa kawaida na hio ni kutokana na namna ya mwili wake ulivyo.

Masaa machache mbele hatimae Profesa Clark alipandisha mpaka juu ya ghorafa hilo kwa ajili ya kumpatia Roma majibu yake.

“Judging from your look the situation is more serious than I imagined”Aliongea Roma na hio ni mara baada ya kuona wasiwasi uliokuwa kwenye macho ya Profesa Clark na alijiambia lazima kuna tatizo kubwa , lakini alijikuta akishangaa Zaidi baada ya Clark kuanza kulia kwa kwikwi kama mtu aliefiwa.

ITAENDELEA WEEKEND

IMEDHAMINIWA NA WAFUATILIAJI KUTOKA GRUPU LA WATSAPP :0687151346
[emoji120]
 
Mtunzi anajua kutupaisha na kutuacha angani tunaning’inia kama hatuna msaada daaaaah!!! Sawa mtunzi tubebeeee
 
SEHEMU YA 294

Roma ilibidi kwanza ambembeleze mrembo Clark kwanza ili kufahamu ni kitu gani kapata kwenye majaribio ya damu yake, lakini licha ya kumbembeleza ,mrembo huyo bado alionekana kuwa na wasiwasi sana.

“Roma niambie , imekuwaje ukalishwa kitu cha ajabu namna hii?”Aliuliza Clark huku akimwangalia kwa macho yenye wasiwasi.

Roma ilibidi aanze kumueleza kila kitu kwanzia sababu ya kuja Japani lakini pia namna ambavyo amekutana na Seventeen feki na kumlisha sumu , mpaka anamaliza stori yake Clark alishangaa na kusikitishwa na jambo hilo

“Roma huyu Seventeen ni muhimu kwako mpaka unashindwa kujua mtego wa wa namna hio, kwanini hutaki kukubaliana na ukweli kwamba alishakufa na huwezi kumuona tena , Roma kwanini hubadiliki?”Aliuliza Clark kwa hasira mno na kwa jinsi alivyo, alionekana kuwa mtu ambaye alikuwa akimjali sana Roma Ramoni na ndio maana alikuwa amekasiika mno , mrembo huyu alikuwa akikumbuka mengi ya nyuma , Roma alikuwa akifanya mambo mengi ya kijinga mara baada tu ya Seventeen kufariki na ndio maana alilalamika na kuona licha ya kwamba tukio la Seventeen kufa lilitokea miaka mingi iliopita , lakini kwa upande wa Roma alionekana kama mtu ambaye hakuwa tayari kukubali ukweli kama Seveteen ashakufa , kuna muda Profesa aliamini uwepo wa Edna utamfanya Roma kumsahau Seventeen , lakini kwa namna ambavyo Roma alikamatika kwenye mtego wa kijinga namna hio aliamini bado Roma alikuwa na kumbukumbu za Seventeen.

“Roma unafikiria nini kitatutokea mara baada ya wewe kufariki, ni maadui wangapi watatuandama siku wakisikia kifo chako , sisi tunaishi kwa amani na maadui zetu wanatuogopa kwa ajili ya uwepo wako , lakini siku wakisikia kifo chako ni Habari nyingine…”Mrembo Clark alionekana kulalamika sana.

Ni kweli kabisa anachoongea Clark ,kwa mfano siku ikatokea Roma akafariki maadui wengi wa familia ya kifalme ya Wales watapata nafasi sasa ya kuwashambulia , kwani siku zote hawakuweza kufanya hivyo kutokana na uwepo wa Hades na jeshhi lake la The Eagles, na ndio maana Clark alikuwa akiogopa sana Roma akipatwa na matatizo na alitaka sana kumlinda , lakini tabia za Roma za kibinafsi za kumfikiria Seventeen mpaka kujiingiza kwenye matatizo zilimuumiza sana moyo wake.

Roma mwenyewe aliona kuna ukweli juu ya maneno ya Clark , kwa mfano sumu ya Polonium ilioingia kwenye mwili wake , kama angetemegea uwezo wa mwili wake tu pasipo kuwa na mbinu za kijini kujiponyesha huenda ingekuwa ni habari nyingine kuhusu yeye.

“Roma Do you know its real possible for you to die?”Aliuliza Clark huku akimwagalia Roma

“Is it very serious?”Aliuliza Roma kwani alikuwa kwenye sintofahamu kwani mrembo huyu badala ya kumueleza hali yake analia.

“Right now ,every single drop of the blood in you body is mixed with countless amount of lethal toxins , including heavy metal and radioactives ones , if all the element in your body combined can be used to develop nuclear bomb”

“Kwasasa damu yako kila tone limechanganyika na kiasi kisichohesabika cha sumu kali ukijumlisha na madini mazito kama elementi ndani ya mwili wako zikaambatanishwa basi zinao uwezo wa kuzalisha bomb la nuklia”Aliongea Jane na kumfanya Roma kutoa macho ni kweli alikuwa akifahamu sumu ya Polonium ni kali sana , lakini hakuamini kama inaweza kuwa na hatari kubwa namna hio.

Radioactives element maana yake ni aina flani ya madini ambayo yanadharisha mionzi mikali sana , mionzi ambayo kama itagusana na mwili wa binadamu athari zake ni kuua seli za mwili , mfano wa madini hayo ni Polonium , Uranium , sasa madini hayo ndio yanayotumika kutegenezea mabomu ya nyuklia.

Sasa ilishangaza sana kwa mwili wa Roma kuweza kuhimili sumu aina ya Polonium.

“Unauhakika kwamba chembe za sumu ambazo zipo kwenye mwili wangu zinaweza kutegeneza bomu?”Aliuliza Roma akiwa katika mshangao wa kutokuamini maneno ya Profesa Clark.

“Unafikiri natania , unahisi nimelia vyote hivi kwasababu uko sawa, nipo hapa mwenyewe nikishangaa umewezaje kuishi Zaidi ya siku mbili ukiwa na sumu mwilini”Aliongea

Roma mpaka hapo aliamini kwamba mbinu ambayo Master Chi aliomfundisha inauwezo mkubwa sana.

“Okey , niambie kama nitaweza kupona?”Aliongea Roma

“Inawezekana kuua dutu zote ambazo zipo kwenye mwili wako , ijapokuwa teknolijia ya sumu ulioingiziwa inatoka ndani ya kundi la Dhoruba nyekundu,lakini siwezi kushindwa kuiyeyusha sumu yote , lakini shida moja ni kwamba ijapokuwa ninaweza kutengeneza ‘Antidote’ lakini mwili wako kwasasa wote unasumu , jambo ambalo linanifanya kuona itakuwa ngumu sana kumaliza sumu yote mwilini”Roma alifikiria kidogo baada ya kusikia maelezo hayo.

“Vipi kama nitatumia uwezo wangu kuikusanya sumu yote mwilini na kuiweka sehemu moja?”Aliongea Roma na kumfanya Clark kushangaa.

“Can you really do it , there is no scientific theories at all that make it possible”Aliongea akimaanisha kwamba hakuna nadharia yoyote ya kisayansi ambayo inawezekana kwa mtu kukusanya sumu mwilini na kuiweka sehemu moja , Profesa Clark alionekana kuwa katika mshangao.

“Ninachokifanya sio kama Sayansi”Aliongea Roma

“Unazungumzia mbinu ya mazingaombwe ambayo uliniambia ulijifunzia Mongolia?”Aliuliza na Roma alitingisha kichwa , kwani katika stori yake hakumueleza Clark kwamba ameshafika levo ya juu kabisa , levo ya kuzaliwa upya, sasa Roma kipindi alipokuwa anaishsi Uingereza ashawahi kumwambia kuwa alikuwa akijifunza mafunzo ya kijini , ambayo yalikuwa yakimsaidia katika uongojjwa wake wa kuwa kichaa , ugonjwa ambao ulikuwa ukisababishwa na Saratani iliokuwa kwenye ubongo wake.

“Kama unaweza kufanya hivyo basi itakuwa rahisi , nitategeneza dawa haraka haraka , wanasayansi wengi ambao wapo ndani ya Dhoruba nyekundu ni wanafunzi wangu”Aliongea Clark.

Unachotakiwa kuelewa ni kwamba Redstorm au Dhoruba nyekundu ipo chini ya Zeros Organisation, lakini sasa misheni nyingi sio kama zilikuwa zikiongozwa na Zeros Organisation moja kwa moja bali ni kupitia kundi hili la Dhoruba Nyekundu , ni kwa mfano uchukulie Marekani kama Zeros halafu C?IA kama Dhoruba nyekundu.

Sasa Zeros ni Secret international Organisation ambayo imeundwa na mataifa makubwa duniani , lakini hio haimaanishi kwamba mataifa mengine madogo hayapo ndani ya Zeros , ukweli ni kwamba mataifa yote yapo ndani ya Zeros lakini sio wahusikaji wa moja kwa moja.

“Naona wanafunzi wako ndio wanataka kuniua?”Aliongea Roma akimwangalia Profesa Clark.

“Unatakiwa ujione kama mtu mwenye bahati , kwani wanasayansi wengi duniani hawaamini katika maswala ya mbinu za kijini unazotumia, mim mwenyewe kuna muda nilijaribu kufanya utafiti juu ya sayansi za kijini lakini mwisho wa siku kichwa kiliniuma kwani mambo mengi yanakosa Nadharia ya kufanyia Practical Experiment.”Aliongea Clark.

Unachotakiwa kuelewa ni kwamba katika ulimwengu wa Sayansi vitu havitokei bahati mbaya , au wanasayansi hawafanyi gunduzi kwa bahati mbaya , kinachokamilisha gunduzi kwa mwanasayansi ni Nadharia(Theories) ambayo ina Thesis ndani yake , Sasa usichanganyikiwe sana katika sayansi kunaanza ‘hypothesis’ halafu ndio inafuatia Nadharia, unaweza kuwa na ‘Thesis’ halafu ukakosa nadharia(Failed Thesis) , lakini huwezi kuwa na nadharia halafu ukakosa ‘Thesis’.

Ijapokuwa Clark hakuwa na uelewa na mbinu za kijini ambazo Roma alikuwa akitumia lakini alizipenda kwani zilikuwa na manufaa makubwa kwa Roma kuliko hasara , kwa mfano Roma kama isingekuwa mbinu hizo angekuwa sio binadamu Zaidi ya kuwa mnyama ambaye mara zote matamanio yake yatakuwa ni kuua pekee yaani asingeweza kuiongoza akili yake.

Roma kabla ya kupitia project LADO saratani yake ilikuwa ikisambaa mwilini kwa kiasi kikubwa sana na kipindi hiko alikuwa na miezi michache sana ya kuishi , lakini mara baada ya kupitia project hio faida kubwa aliopata ni kwaba ile saratasi ilibadilika kutoka malignant(Kansa inayosambaa kwa kasi) Kwenda ‘Benign’(Kansa ambayo haisambai inakuwa kama uvimbe),sasa kutokana na uvimbe huo kuwa katika ubongo inanamfanya muda mwingine kutoweza kujiongoza , Sasa mafunzo ambayo alifundishwa na Master Chi , yalimuongezea uwezo mkubwa sana wa kuongoza akili yake , yaani ilikuwa ni mara chache sana kwa yeye kupitia mabadiliko halafu akashindwa kurudi katikahali ya kawaida.

Roma baada ya kusikia maelezi ya Clark lakini pia namna mrembo huyo alivyokuwa akilia mbele yake , alijikuta pia akianza kumkumbuka mke wake kauzu , alitoa simu yake na kujaribu kupiga Kwenda Tanzania kwa kutumia namba yake iliozoeleka , lakini simu haikuweza kuunganishwa , ikimaanisha kwamba mtandao wa kitanzania haukuwa na huduma ya kupiga simu kimataifa.

Roma baada ya kuachwa na Clark ambaye alienda kutegeneza Dawa ya kumaliza sumu katika mwili wake , aliona awasiliane na Tanya .

“Contact the telecomunication Company immediately , ensure my number will be able to make and receaive call from Tanzania”Aliongea Roma akimpa maelekezo Tanya kwama ahakikisha namba yake inauwezo wa kupokea simu na kupiga ndani ya Japani Kwenda Tanzania.

Tanya upande wa pili ni kama alikuwa amepewa kazi anayoipenda kwani alipokea maagizo hayo kwa furaha kubwa na zilipita nusu saa tu namba ya Roma ilisoma mtandao na palepale alitafuta namba ya mke wake Edna na kupiga Kwenda Tanzania.

Na simu iliita kwa madakika kadhaa na kupokelewa .



SEHEMU YA 295

“Babe Wifey , mnaendeleaje huko Tanzania, nimekumiss sana mke wangu kipenzi”Aliongea Roma , lakini hakukuwa na jibu upande wa pili na kumfanya kutoa simu sikioni na kuangalia kama imekatwa , lakini aligundua simu haijakatwa.

“Wife muda si mrefu nitarudi Tanzania , nipo Hokkaido huku , niambie unataka nikuletee zawadi gani wewe na Lanlan , Unataka pete ya Almasi yanye ukubwa kama jicho , vipi kuhusu mkufu wa dhahabu wa thamani kubwa , vyote hivyo nitanunua nimeingiza pesa ndefu mumeo”Alijiongelesha Roma mwenyewe , lakini hakukuwa na jibu kabisa.

Upande wa Tanzania ilikuwa ni usiku kama wa saa saba za usiku na mrembo Edna alionekana mpaka muda huo hakuwa amelala kabisa, alikuwa na wasiwasi pia kwani zilipita takribani siku mbili tokea Roma atoke Tanzania Kwenda Japani lakini hakupokea hata simu ya kujulishwa kama alifika salama , mwanzoni hakuwa na tatizo , kwani alikuwa akiamini uwezo wa Roma , lakini bado alikuwa na wasiwasi , lakini pia mrembo huyo alikuwa na mawazo , maswala ambayo ameongea na Amiri juu ya dokta Sheba , yalikuwa yakizunguka kwenye kichwa chake , kuna hisia ambazo zilikuwa zikimwambia kwamba kifo cha mama yake hakikuwa cha kuitwa na Mungu bali kilikuwa cha kusababishwa na binadamu.

Ijapokuwa uchugugzi wa Amiri haukuwa umekamilika lakini kifo cha Dokta huyo siku mbili baada ya kuthibitisha kifo cha mama yake kilimfanya kuwa na wasiwasi sana na kuamini kuna jambo ambalo lilikuwa likiendelea ambalo yeye mwenyewe hakuwa akilifahamu , aliamini huenda kisasi ambacho alikuwa akizungumzia mama yake kilikuwa kikihusiana na kifo chake.

Sasa Edna akiwa kwenye wakati mgumu kama huo, ndio alijikuta akiwa na mawazo mno na hata kuanza kumkumbuka Roma , ijapokuwa ni kweli licha ya kwamba hawakua wa kukaa Pamoja mara nyingi , lakini Edna kwenye moyo wake aliona miezi mitano ambayo aliishi na Roma ilikuwa ni kama miaka miwili na aliamini uwepo wake karibu yake ulikuwa ukifaa Zaidi na kumfanya kutokujihisi mpweke.

Sasa baada ya siku nzima kuangalia simu yake huku akimtukana Roma kimoyo moyo kwa kutokumtaarifu kama amefika salama huko Japani , lakini pia kutowajulia hali , alijikuta akiwa na wasiwasi na hasira juu yake , muda wa saa saba hata alipoona simu ya Roma hakutaka kusikiliza pumba zake kabisa , alikuwa na hasira mno na alichokifanya ni kupokea na kuweka simu sikioni pasipo kujibu chochote mpaka pale Roma alipokata simu.

Edna aliamini kutokuongea ilikuwa ni adhabu nzuri kwa Roma , ndio alifurahi kwamba Roma amemkumbuka , lakini wakati huo alikuwa na hasira nae hivyo alimkalia kimya.

Baada ya kusikia sauti ya Roma , alirudi kitandani na kisha aakamwangalia Lanlan aliekuwa amelala Fofo na kumbusu kwenye maji la uso na kisha akajifunika shuka na usingizi ulimchukua dakika kadhaa mbele.

Asubuhi kulivyokucha Edna alimfikishia Blandina juu ya Roma kupiga simu usiku.

“Edna kasema yuko salama , anaendeleaje na kasema anarudi lini?”Aliuliza Blandina mfululizo huku akiwa ameshikilia ‘Cleaner’na alikuwa akisafisha eneo la sebuleni.

“Yuko salama mama , hupaswi kuwa na wasiwasi tena”Aliongea Edna lakini alijikuta akigeuka nyuma mara baada ya kukumbatiwa kwa nyuma na aligundua aliemkubatia alikuwa ni Lanlan aliekuwa akifikicha macho akionesha ndio kwanza anaamka.

“Mama Lanlan ananjaa…”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kutabasamu kwa uchungu , yaani ndio kwanza anaamka na kitu pekee ambacho anaulizia ni chakula hata salamu hakutoa.

“Lanlan msalimie kwanza bibi na unisalimie na mimi ndio nitakuandalia chakula”Aliongea Edna akimfundisha Lanlan.

“Goodmorning Grandma , Goodmorning Mom “Aliongea Lanlan na Blandina alitabasamu na kuitikia salamu ukweli kila alipokuwa akimuona Lanlan alitamani awe mtoto wa damu wa Roma , aliamini angejisikia vizuri kwa Roma kuwa na mtoto wake wa kumzaa ambae asubuhi angemuita bibi.

Upande wa Qian Xi Maisha yake ndani ya familia ya Edna aliyafurahia , rafiki yake mkubwa alikuwani Yezi na moja ya sababu kubwa ya kujiweka karibu na Yezi ni kutokana na kwamba wote walikuwa na asili ya bara moja , yaani Yezi alikuwa ni Mkorea upande wa baba na Mtanzania upande wa Mama.

Yezi licha ya kwamba alikuwa akipata kila kitu ndani ya familia ya Edna , lakini hakubweteka , mrembo huyo alikuwa amepata kazi kwenye moja ya mgahawa wa Kikorea hapohapo Osterbay , hivyo mara nyingi kila akitoka chuo anaunga moja kwa moja kufanya kazi , licha ya kwamba Edna alikuwa na pesa , ila hakupenda kabisa kumuomba na alitamani kushika hela alioitolea jasho yeye mwenyewe, Blandina ambaye alimchukulia Yezi kama mtoto wake hakupenda kabisa kwa Yezi kufanya kazi , lakini pia hakupenda kumuingilia kwani Yezi alikuwa mtu mzima.

Blandina sasa akili yake ilitulia baada ya kupewa taarifa na Edna kama Roma yupo salama , ule wasiwasi aliokuwa nao uliisha na hali ya furaha ilirudi kwa mara nyingine na hilo Edna aliliona na kumfanya hata kumkumbuka mama yake mzazi Rahel.

*******

Ni siku ya tarehe 25 jioni , yaani siku moja kabla ya ndoa ya Amina na Fayezi ndani ya taasisi ya utafifi wa kibaiolojia , Profesa Clark alionyesha kuridhishwa na dawa yake ilivyofanya kazi ndani ya mwili wa Roma , licha ya kwamba ilikuwa jambo la kushangaza kwa Roma kukusanya sumu yote mwilini mwake na kuisukuma mpaka kwenye mikono yake , lakini alijikuta akifaurahi baada ya kuona Roma kapona.

Upande wa Roma baada ya sumu ile kuisha kwenye mwili wake , hatimae aliweza kujisikia hali ambayo hakuwahi kuisiikia hapo kabla , ni kama mwili wake ulikuwa ukipitia mabadiliko ya hali ya juu sana , kwanza kabisa alijihisi kuwa mwepesi mno na alikuwa ni kama mtu ambaye amepoteza kumbukumbu na sasa akili yake ilikuwa ikianza upya kuhifadhi mafaili , alijikuta mara baada ya kunyanyuka kwenye kitanda akitabasamu huku akimwangalia Profesa Clark.

“Kipi kinakufanya kutabasamu?”

“Mwili wangu ni mwepesi sana , sijawahi kujisikia hivi hapo kabla”Aliongea Roma kwa furaha na kujiona sasa ile levo namba tisa ya kuzaliwa upya ndio anaihisi kikwelikweli.

Profesa Clark baada ya kuona Roma ni mwenye furaha , alishindwa kujizuia na kumsogelea Roma na kumbusu kwenye paji la uso huku akiwa ni mwenye hisia kali , kitendo ambacho kilimshangaza Roma , lakini pia kumfanya kuwa na aibu kwa mara ya kwanza kwenye Maisha yake , kwani kitendo cha mwanamke kumbusu kwenye paji la uso haikuwa cha kawaida hata kidogo na yeye ndio alipaswa kumfanyia mwanamke hivyo.

“Mwili wako ushakuwaa sawa kwa sasa”Aliongea Profesa Clark huku akipotezea tukio alilolifanya kwa kuangalia data zilizokuwa zikionekana kwenye Skrini.

“Thank you , you are always the one who can solve my biggest Troubles”

“Asante sana , siku zote umekuwa mtu wa kutatusha matatizo yangu makubwa”Aliongea Roma kwa namna ya shukrani kwa moyo msafi kabisa , ni kweli mrembo Clark alikuwa ni moja ya msaada mkubwa sana kwake, kwa mfano tu tokea jana yake hakulala alikesha ndanni ya maabara akitengeneza dawa ya kumtibu Roma.

Ukweli ni kwamba moja ya sababu ya Profesa Clark kusoma mambo ya biolojia ni kutokana na matatizo ya ubongo aliokuwa nayo Roma , tokea siku ambayo alifahamu kwamba Roma alikuwa na shida , alitumia muda mwingi sana kuangalia namna ya kumsaidia na mrembo huyo alikuwa ameweka nadhiri zake kwa Roma kwamba ipo siku lazima agundue dawa ya kuponya kansa, hivyo kumhudumia Roma ilikuwa ni jambo ambalo alikuwa akilipenda sana , na juu ya yote ni kwamba membo huyo alikuwa akimpenda sana Roma kwa mapenzi ya dhati kabisa tokea alivyokuwa mtoto hakujali kabisa Roma alikuwa akijihusisha kimapenzi na mama yake mzazi , kwake alitii hisia zake na aliamini Roma siku moja atakuwa wake na mpaka umri aliokuwa nao huo wa kuitwa Profesa hakuwahi kuguswa na mwanaume , alikuwa ni kama anamtunzia Roma.

Ukumbuke Roma wakati anamuokoa Catherine kwenye mikono ya maadui zake , Clark alikuwa ni wa umti wa miaka kumi na moja , lakini kutokana na kujaaliwa kwake uwezo mkubwa wa akili Clark alipofikisha umri wa miaka kumi na tano alikuwa ashafanya vitu vikubwa sana katika ulimwengu wa Sayansi , vitu ambavyo wanasayansi wa kawaida wangechukua miaka Zaidi ya arobaini katika ‘Carear’ zao.

“Kama unapenda nipokee sukrani zako , usiwe unafanya mambo ya kijinga na kujiweka katika hali hatarishi, ukumbuke wewe ni Pluto”Aliongea Clark.

“Hilo ni jina tu , lakini mimi pia ni binadamu , tukio la juzi limetokea kwasababu kumbukumbu za Maisha yangu ya nyuma ni za kuumiza sana na siwezi kuzifuta mara moja , hayo ni makosa ya kibinadamu tu , lakini nina uhakika swala hili haliwezi kujitokeza tena”Aliongea Roma.

“Hujaniambia una mpango gani na Kundi la Dhoruba nyekundu Pamoja na Takamagahara na Innova?”

“Kwasasa sina mpango wa kudili nao , nimeaachia vijana wao kwakua nina mpango wangu kichwani , miaka iliopita niliharibu makao makuu yote ya Zeros , lakini mpaka sasa naamini wamejikusanya upya mahali na wanaendeleza ushetani wao , nimeachia vijana wangu waendelee kufatilia taarifa zote za Zeros , siku wakijichanganya sitosita kuua mmoja mmoja nihakikishe nimeondoa mzizi wote”Aliongea Roma kwa ukawaida kabisa

“Umebadilika sana Roma , nimependezwa sana na mabadiliko yako”Aliongea na kisha akaweka baadhi ya mambo yake vizuri na kisha wote kwa Pamoja walitoka kwenye hio maabara , kazi ya Clark ilikuwa ishaisha hata hivyo kwahio kubaki hapo ndani ya maabara ilikuwa ni kama kupoteza muda.

Roma jana usiku wake alikuwa amewapa kazi kundi la Yamata Sect kuangalia nini kinaendelea sehemu ambayo Amina alikuwa amezuiliwa na taarifa zilionyesha kwamba licha ya mrembo huyo kuzuiwa kutotoka , lakini alikuwa akipata huduma zote kama vile malkia na Roma aliona haina haja ya Kwenda haraka , kwanza kabisa mpango wake haukuwa kumuokoa Amina tu , alikuwa na mpango mwingine kichwani , alijiambia kama kilichomleta Japani ni kuzia ndoa ya Amina basi angeagiza vijana wake tu kufanya kazi hio.

Upande mwingine ndani ya hoteli ya hadhi ya nyota tano ndani ya jiji la Otaru Hoteli iliofahamika kwa jina la El-Fadh, anaonekana mheshimiwa kigombola akiwa ndani ya eneo la VIP akiongea na Dodi Fayez.

“Mheshimiwa nadhani kwasasa unaweza kuwa na amani kabisa , nilikuambia kwamba ninao uwezo kumzimisha yule mpumbavu”Aliongea Fayezi kwa lugha ya kingereza na kumfanya mheshimiwa Kigombola asijue nazungumzia nini.

Kigombola alikuwa ndani ya Japani kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya harusi ya Amina na Fayezi , yeye akiwa kama rafiki wa karibu wa Familia ya Tajiri Khalifa hakuwa na mpango wa kukosa kabisa sherehe hio kwani pia alikuwa na mwaliko maalumu.

“Mr Fayezi sijui unachomaanisha “Aliongea Mheshimiwa Kigombola alievalia suti yake huku akiwa ameshikilia Glass ya wine .

Fayezi alitabasamu na kisha alitoa simu yake kampuni ya Apple na kisha akaenda upande wa picha na kumpatia mheshimiwa Kigombola na mheshimiwa alijikuta ni kama mtu ambaye hakuwa akiamini kile alichokuwa akiangalia kwani kwenye simu hio kulikuwa kukionekana picha ya Roma Ramoni akiwa amelala kwenye kitanda cha kusukuma kwa mataili.

“Mheshimiwa nadhani sasa ushaelewa ninachomaanisha”

“Unataka kusema Roma…. no I mean Hades amekufa?”Aliuliza mheshimiwa kwa namna ya kubabaika.

“Ndio amekufa , kama unavyoona picha yake hapo , mtego ambao aliwekewa ilikuwa ni ngumu sana kuukwepa”Aliongea Fayezi kwa furahsa sana na aliminimna Mvinyo kwenye glass zote mbili na kisha akampa ishara mheshimiwa kugongesha ‘Cheers’ kusherehekea.

Mheshimiwa Kigombola licha ya kuangalia picha hizo hakuwa akiamini kabisa maneno ya Fayezi , aliamini huenda mtu aliekuwa kwenye picha sio Roma mwenyewe , maana tokea siku ambayo amepata kusikia mambo ya kisaynasi kutoka kwa Yan Buwen , alikuwa na wasiwasi sana na kila mtu mwenye uwezo wa ajabu , aliamini huenda huko duniani kuna watu wawili wawili , yaani Clone za watu wengi sana na hata yeye mwenyewe alikuwa akitamani kutengeneza kopi yake.

“Hongera sana Fayezi kwa kufanikisha jambo ambalo nilishindwa kulikamilisha , hakika baba yako amekuwa mwenye maamuzi sahihi sana kukurithisha mali za familia”Aliongea Mheshimiwa Kigombola , ukweli hakutaka hata kusikia ni kwa namna gani ambavyo aliweza kumdhibiti Roma.

Baada ya mheshimiwa raisi kuachana na Fayez na yeye kuingia kwenye chumba chake ndani ya hoteli hio ya El Fadhi , alitoa simu yake haraka haraka na kisha akatafuta namba ya mtu Tanzania na ndani ya dakika kadhaa tu simu ilipokelewa.

“Mr Yan Buwen ninayotaarifa ambayo bado haina uthibitisho”Aliongea Mheshimiwa huku akisikiliza kwa umakini kwenye simu yake.

“Ni uzushi gani huo mheshimiwa unataka kuniambia ukiwa Japani?”Ilisikika sauti tulivu upande wa pili.

“Ni juu ya Hades, nimepata taarifa kutoka kwa mtoto wa Khalifa kutoka Dubai kwamba amekufa”Aliongea.

“Hahaha.. Hahahaha” kilisikika kicheko upande wa pili.

“Mr Yan Buwen mbona unacheka”

“Kigombola mimi pekee ndio mwenye nafasi ya kumuua Hades , hakuna binadamu ambaye ataweza kumuua Hades na mtu yoyote mwenye mpango wa kumuua tofauti na mimi mwenyewe ni adui yangu”

“Mr Yan Buwen lakini nimeona picha yake kabisa kwa macho yangu, na ni yeye kabisa”

“Mheshimiwa unaonaje ukiweka akili yako kwenye mpango wetu, wa kupata damu ya Hades tofauti na kuongea mambo yasio na maana usiku wote huu?”Sauti ilisikika upande wa pili na kumfanya mheshimiwa Kigombola kutulia kwa dakika kadhaa na kisha akavuta pumzi na kuzishusha.

“Sawa Mr Yan , naamini maneno yako Zaidi kuliko ya Fayezi , Hades hajafa bado”

“Safi mheshimiwa … mtu pekee ambaye unaweza kumuamini akikuambia kama Hades amekufa ni mimi peke yangu mheshimiwa , wengine wote wanazungumza uzushi , lakini hata hivyo taarifa yako inanifanya nitake kufanya jambo kabla ya Hades hajafufuka ….”

“Unataka kufanya nini?”

“Utapata matokeo mheshimiwa”Aliongea Yan Buwen na kisha akakata simu.
 
SEHEMU YA 296

Upande wa Tanzania wakati mheshimiwa Kigombola anawasiliana na Yan Buwen ilikuwa ni usiku wa manane , yaani wa kuamkia siku ya tarehe ishirini na sita.

Yan Buwen mara baada ya kuongea na simu na mheshimiwa Kigombola alijikuta akicheka sana , akicheka kiasi kwamba hata mwanamke wa Kitanzania aliekuwa juu ya kitanda kushangazwa na namna mchina huyo alivyokuwa akicheka.

“Hades kesho lazima nifanye jambo ambalo litakuachia kovu kubwa sana ,lazima niue mwanafamilia wako mmoja ili kuinua ukichaa wako hahahaha,…”Aliongea Yan Buwen pasipo kueleweka anawaza nini , kwake licha ya kwamba taarifa ya mheshimiwa Kigombola kuiona ni ya kizushi , lakini alipata faida moja , alifahamu kwamba Roma hakuwa Tanzania bali yupo Japani sasa aliona hio ni nafasi pekee ya kumchallenge Roma na kuinua ukichaa wake , Yan Buwen alikuwa na taarifa zote za Roma kupoteza uwezo wa kurudi kwenye hali yake pale anapokuwa ni mwenye hasira kali , hivyo aliona atumie nafasi hio adhimu sana ya kumchokoza Roma kwa kumtengenezea maumivu makali sana kwenye moyo wake.

Asubuhi yake Yan Buwen mara baada ya kumfukuza kimada alielala nae usiku kucha alijiandaa haraka haraka kwa kuvaa tisheti na jeansi na kisha alishuka mpaka neneo la maegesho ya magari na kusogela gari aina ya V8 na aliingia ndani ya gari hio na kulitoa taratibu taratibu.

Dakika kama kumi hivi alikuwa akiingiza gari ndani ya jengo la Bima ya taifa lililokuwa limepakana kwa mita kadhaa na hospitali ya Ocean Road.

Yan Buwen mara baada ya kuingia ndani ya jengo ili hakujali sana watu waliokuwa wakimwangalia , alijali kile anachofikiria , kwanza alikuwa ni mbaguzi wa rangi wa kupindukia , alikuwa akiwadharau kwa kiasi kikubwa sana watu Weusi , hivo hata watu walikuwa wakimwangalia aliwaona kama manyani hivi.

Baada ya kuingia ndani ya Lift namba tatu ya jengo hilo , Lift ambayo mara nyingi hutumika kwa utaratibu maaliumu , Yan Buwen aliachana na batani za kawaida ndani ya lift hio na akagukia batani zingine ambazo zilikuwa kama Keypad na aliingiza namba ambazo zilionekana kama Nywila na pelapele lift ile badala ya Kwenda juu ilishuka chini ya jengo hili , ikimaanisha kwamba alikuwa akielekea ndani ya ‘Basement’ Lift ile ilikuja kufunguka kwenye Floor ambayo , licha ya kwamba ilikuwa na msururu wa vyumba , lakini milango yake yote ilikuwa ni ya chuma na kwa mbele kulikuwa na kioo kilichotegenezwa na namna ya shepu mraba , kidogo sana ambacho kinamuwezesha mtu kuona ndani.

Milango yote hii ambayo juu yake ilikuwa na namba Pamoja na Camera, ilikuwa imepakwa rangi aina ya samawati na hii pia ni rangi ambayo ilikuwa ikitofautisha na Floor za juu kabisa ya jengo hili la Bima.

Yan Buwen alitembea kwenye Floor hio huku akionekana kujisikia vizuri , alihesabu vyumba hivyo ambavyo kwa haraka haraka jumla yake vilikuwa kama ishirini yaani upande wa kulia na kushoto na alisimama kwenye mlango uliokuwa na namba saba na aliiweka jicho lake sehemu maaalumu ambayo imeunganishwa na mfumo wa ‘Retina Scan System’ na kwa dakika kadhaa tu mlango ulijitoa ‘Lock’ na alishika kitasa na kuingia ndani .

Ajabu ni kwamba chumba ambacho Yan Buwen ameingia kilikuwa ni kama wodi ya kisasa mno , mbele yake kulikuwa na kitanda kama cha hospitali , lakini hiki kikiwa na utofauti kidogo kwani kilikuwa kimefungwa mitambo ya kisasa ambayo ilikuwa ikitoa mwanga flani wa rangi nyekundu kwa kubip juu ya kitanda hiko kulikuwa na mtu ambaye amefungwa pia kwenye kuta za kitanda na kifaa flani hivi kama pingu , lakini sio pingu kwani vigaa hivyo vimeungana moja kwa moja na kitanda hiko cha kisasa cha chuma.

Mtu aliekuwa kwenye kitanda hakuonekana sura , lakini alikuwa uchi, mwenye Ngozi nyeupe ambaye kwa haraka harkaa kama utamwangalia vizuri basi utagundua kuwa ni mtu aliechanganya rangi kati ya mwafrika na Mhindi.

Bwana huyo alikuwa kwenye kitanda huku akiwa amebandikwa nyaya falani hivi za kupima mapigo yake ya moyo za rangi tofauti(Arduino Heart rate Sensors) , miguuni alikuwa pia amefungwa pia.

Juu ya kitanda usawa wa kichwa kuna Bulb kubwa(Halogen Lamp) ambayo ilikuwa ikimmulika mgonjwa huyo alielala kwenye kitanda , Taa hizo ni kama zile ambazo zinatumika kwenye vyumba vya upasuaji.

Pembeni ya chumba hiki kuna Skrini kubwa mafano wa Tv ambayo ilikuwa ikionyesha ubongo wa mgonjwa aliekuwa amelela chali(Supine position) halafu pembeni yake kuna kabati juu ya ukuta la chuma ambalo lilikuwa na lebo ya ‘Specimen’.

Yan buwen alimwangalia bwana alielala chali kwa dakika kadhaa na kisha akageukia Skrini na kukagua ubongo wa bwana huyo kwa dakia kama mbili hivi na alijikuta akitabasamu na alisogelea upande wa meza iliokuwa upande wa kulia na kubeba rimoti na alibonyeza na palepale kitanda ambacho mgonjwa amelalia kilinyanyuka taratibu na kukaa kwa namna ya kuegamia(Fowler’s position).

Yan Buwen baada ya kuridhika na mkao wa mgonjwa wake alivaa Gloves na kisha akasogelea kikabati ambacho ndani yake kuna sindano na vijichupa(Vials) vingi vingi ambavyo ndani yake vina vimiminika vya rangi tofauti, alitoa kijichupa kimoja mabacho kina kimiminika cha rangi nyeusi na kuchukua bomba na kufyonza kimiminika na kisha akarudisha kichupa kile kwenye kabati na akamsogelea mgonjwa wake , baada ya kukaribia alinyoosha mkono kwenye Drip ambalo limening’nia na kuchoma na sindano na kuruhusu kimiminika ambacho kipo ndani ya bomba kuingia kwenye maji yale na palepale yalibadilika rangi na kuwa ya kahawia.

Yan Buwen baada ya kuona zoezi lake limekamilika aligeukia Skrini na kuangalia namna ubongo wa mgonjwa wake unavyopokea taarifa kutoka kwenye mwili na alijikuta akitabasamu huku akishangazwa na namna ubongo wa mgonjwa wake ulivyokuwa unapitisha mawimbi ya mawasiliano na ukumbuke mwanzoni kwenye skrini hio licha ya kwmaba ubongo wake ulikuwa ikionekana ila hakukua na aina ya mawasiliano ambayo yalikuwa yakionekana , yaani ulikuwa ni kama ubongo wa mtu ambaye amekwisha kufa., lakini baada ya Yan Buwen kuchoma na kuingiza maji yale kwenye mwili wa mgonjwa huyo ubongo wake ulianza kufanya kazi kwa kupitisha mawimbi ya mawasiliano kwa haraka sana kiasi ambacho kilimridhisha na kumgeukia mgonjwa wake na ndani ya dakika kama kumi na tano tu , mgonjwa yule alishituka katika usingizi wake na kumfanya Yan Buwen kuanza kupiga makofi.

“Karibu tena Duniani kwa mara nyingine Mr Salah Hubert”Aliongea Yan Buwen kwa furaha sana.

Ndio mtu ambaye aliekuwa ni mgonjwa alikuwa ni Salah , mwanaume ambaye siku kadhaa nyuma alinyongwa na Roma kule baharini , sasa haikueleweka Yan Buwen kafanya nini , lakini Salah alionekana kuwa mzima wa Afya.

Salah ambaye alionekana kama mgonjwa alierudiwa na fahamu alimwangalia Yan Buwen kwa dakika kadhaa na kisha akageuza macho yake kwenye mikono yake na aliangalia kwa dakika kadhaa tu kama mtu anaeshangaa na katika hali ambayo haikuwa ya kawaida , Salah alinyanyua mikono yake kwa wakati mmoja na kisha akavunja zile pingu kama vile zilikuwa Kamba za kawaida sana , kwani hakutumia hata nguvu na kitendo kilimfanya Yan Buwen kumwangalia Salah kwa macho ya kebehi.

Salah aliangalia na miguu yake iliofungwa kama anaishangaa kama vile roboti na sekunde zilikuwa nyingi kwani Kamba zile zile zilikatika kama uzi wa kushonea.

Salah baada ya kuona zoezi lake limekamilika alishka kwenye kitanda chake na kisha alimsogelea Yan Buwen aliesimama pembeni akimwangalia na baada ya kumsogelea alimkagua pasipo ya kuongea neno kuanzia kwenye kichwa mpaka chini na kisha akarudisha macho yake kwa Yan Buwen na wakaangaliana kwa kukodoleana macho , huku Yan Buwen hakuonyesha hofu , ni kama alikuwa akijua Salah hamfanyi kitu na kwa upande wa Salah hivyo hivyo alimwangalia Yan Buwen.

Yaani alichokuwa akikifanya Salah ni kama mtu ambaye yupo mbele ya kioo akijiangalia ndivyo ilivyokuwa kwa Salah , yaani alikuwa akitumia mwili wa Yan Buwen kujiangalia yeye mwenyewe.

“Hahaha…”

“Hahaha…”

“Hehehe….”

“Hehehe..”

Yan Buwen alikuwa akicheka na Salah hivyo hivyo alikuwa akicheka kwa namna ya kuigiza , Yan Buwen alivyotabasamu na Salah hivyo hivyo alitabasamu , sasa haikueleweka ni nini kinaendelea , lakini jambo moja kwa uhakika ni kwamba alichokuwa akifikirtia Yan Buwen ndio ambacho Salah alikuwa akifikiria.

Zilipita kama dakika kama kumi hivi za Yan Buwen kuonyesha ishara mbalimbali na Salah kuziigiza.

“Nahitaji kichwa cha Mama yake Hades…”Aliongea Yan Buwen.

“Nahitaji kichwa cha mama yake Hades….”Aliigizia Salah na Yan Buwen palepale aliwaza kichwa chake kuvaa nguo zilizotungikwa kwenye kona ya chumba na Salah alisogelea nguo hizo na kisha akazivaa haraka haraka na ndani ya dakika chache Salah alikuwa kwenye suti nzuri sana ilimpendeza na haikueleweka Yan Buwen kawaza nini , lakini Salah alitoka ndani ya chumba hio cha wodi na kumuacha Yan Buwen kuanza kucheka kwa nguvu kama vile anakichaa.

Sasa mpaka hapo tunaona kwamba Salah ambaye siku kadha alikuwa amekufa kwa kuuliwa na Roma , alionekana kufufuka , sasa haikuelweka kwamba Yan Buween kamfufua au Roma hakumuua vizuri ,haikueleweka , lakini jambo moja ambalo ni la uhakika Salah alikuwa na uwezo wa ajabu sana ambao ameamka nao.

“Specimen alizoniachia mrembo The Doni sio za kawaida , I, now can revive the dead , I thik I am becoming God hahahaha… haha”.
 
SEHEMU YA 297

Dakika kama tano hivi zilipita tokea Salah kuondoka , Ytan buwen aliekuwa ndani ya chumba ambacho alikuwa amelazwa Salah akimfanyia matibabu , alisogelea na kushika kijichupa ambacho ndani yake kilikuwa na kimiminika cha rangi nyeusi na kukiangalia kwa namna ya kama mtu ambaye alikuwa akishangaa.

Jambo moja ambalo lilikuwa likipita katika kichwa cha Yan Buwen ni juu ya kimiminika hiko , ukweli ni kwamba hakuwa na elimu yoyote iliopo nyuma ya kimiminika hicho kutokana na kwamba yeye alikabidhiwa tu na Athena ,sasa tokea siku ambayo amekabidhiwa kimiminika hiko alikuwa akijaribu kutafuta sayansi iliopo ndani ya kimiminika hiko , lakini alishindwa kabisa kujua kanuni yake na ndio maana muda huo alikuwa akikishangaa na kujiuliza maswali mengi kwa wakati mmoja.

Salah kwake ilikuwa ni maiti ya kumi kuirudishia uhai wake tokea siku ambayo alipewa kimiminika hiko na Athena kwa ajili ya kukifanyia majaribio na kugundua kanuni yake.

Yan Buwen aliangalia kichupa hiko kwa dakika kama tano hivi akikigeuza kulia na kushoto na baada ya kuridhika kwa kiasi Fulani alikirudisha kwenye kikabatii kilichokuwa ndani ya wodi hio.

Yan Buwen mara baada ya kukiweka alitoa tena kishikwambi ambacho hakikujulikana ni cha kampuni gani na baada ya kushikilia kile kishikwambi na kukiwahsa alienda moja kwa moja mpaka sehemu iliokuwa na ‘icon’ ilioambatana na jina la NLC2P(Neural Link Chip Control Pad).

Baada ya kufungua ‘App’ hio moja kwa moja ilikonekti na satilaiti na palepale ilionekana ramani ya jiji la Dar es salaam lote juu kukiwa na kidoti cha rangi nyekundu , kidoti hiko kikionyesha kilikuwa kikisogea kwa kasi sana ndani ya barabara ya Bagamoyo Road kama ilivyokuwa ikionyesha kwenye Ramani.

Yan Buwen alijikuta akitabasamu kifedhuli mara baada ya kuona kidotii kile kilikuwa kwenye kasi sana na mpaka hapo aliamini Salah atakuwa kwenye gari.

Unachotakiwa kuelewa ni kwamba Yan Buwen licha ya kwamba alikuwa ameuamsha mwili wa Salah , lakini jambo moja tu ambalo kimiminika kile kilishindwa kufanya kazi ni kurudisha nafsi yote ya mtu aliekufa , Sasa Yan Buwen kabla hajamdunga mtu na kimiminika, kitu cha kwanza anachokifanya ni kuingiza ‘Neural Link Chip’ katika ubongo.

Chip ambayo anamuwekea mtu mara nyingi haina kumbukumbu za iana yoyote ile , yaani kwa maneno marahisi ni kwamba Salah hakuwa Salah kama alivyokuwa awali kabla ya kifo chake , bali Salah ni mtu mwenye kumbukumbu zingine kabisa ambazo alikuwa akizipata kupitia Chip iliowekwa kwenye ubongo, sasa mafaili ambayo yamewekwa kwenye ubongo ndio yanayomuongoza katika ufanyaji wa matendo yake pamoja na kufikiria.

“Ameamka na sasa yupo njiani kwenye gari na nadhani anakuja nyumbani”Aliongea Yan Buwen kwa kingereza mara baada ya kupiga namba ya simu ambayo mpaka muda huo haikuwa ikieleweka alikuwa akiongea na nani.

“Tunatakiwa kufanya nini mara baada ya kufika?”

“Mnatakiwa kumuacha na kumuona wa kawaida tu , nimejitahidi kuingiza baadhi ya taarifa zinazomuhusu lakini zoezi halikukamilika kwa asilimia mia moja , naweza kusema nimesevu asilimia hamsini ya taarifa zake alipokuwa hai , teknolojia hii bado ipo katika maboresho”Aliongea Yan buwen kwa namna ya upole.

“Okey nitawasiliana na mtu wa nyumbani na kuwapa tahadhari” Sauti ilisikika na palepale simu ilikatwa.

******

Upande mwingine ndani ya familia Mzee Maya ni kama hakuna kitu ambacho kimetokea kama baadhi ya watu walivyokuwa wakifahamu, ni kweli kwamba siku kadhaa nyuma watu walishuhudia kifo cha Salah , lakini jambo la kushangaza ni kwamba ndani ya familia hii yenye makazi yake ndani ya eneo la Mbweni , hakukuwa na aina yoyote ya kuashiria kuna msiba.

Hata Mage na Magdalana ambao walikuwa ni watu walioshihudia kifo cha Salah walionekana kuwa kwenye mshangao na kutoelewa ni kipi kinaendelea , ni kweli kwamba Mgadalena au Ajenti Flamingo alipokea maagizo kutoka kwa Afande Maeda kuhakikisha swala la kifo cha Salah hakimletei shida Roma , lakini jambo la kushangaza ni kwamba kesi ya Salah ilifutwa polisi na mwanasheria wa familia ya Mzee Maya Huberi na kuwafanya warembo hao kutoelewa kinachoendelea , lakini kwasababu jambo hilo lilikuwa heri kwao basi waliona watulie kimya , lakini licha ya hivyo kuna jambo ambalo lilikuwa likiwatekenya mno , yaani walitaka kujua nini kinachoendelea , mapacha hao wote ni wanausalama , hivyo walitaka angalau kujua ni sababu gani kwa familia ya Mzee Maya kufuta kesi ya kuuliwa kwa mtoto wao ndani ya polisi.

Upelelezi wa warembo hao wawili uliwafikisha ndani ya nyumba ambayo inaaminika ndio makazi ya mke wa Tajiri Maya Hubert kwa hapa Tanzania , ili kuangalia ni nini kinaendelea , lakini baada ya kuuliza baadhi ya majirani nje ya geti la jumba hilo ni kwamba, jambo la kushangaza hakuna ambaye alikuwa amesikia kama kuna msiba , yaani hakuna jirahi yoyote ambaye alikuwa akielewa kinachoendelea ndani ya familia hio , jambo ambalo liliwafanya maswali kuibuka katika vichwa vyao.

Wakati wakiwa ndani ya gari , Mage akiwa na Magdalena , mara simu ya Ajenti Flamingo ilitoa mwashirio kwamba inaita na kwa haraka sana Magdalena aliitoa kwenye surauali yake ya jeans na kuangalia ni mtu gani ambaye anampigia na alijikuta akijiweka sawa mara baada ya kugundua ni mkuu wake wa kazi , yaani afande Maeda.

“Jambo Afande”

“Jambo Afande! ,Ajenti Flamingo nadhani mpaka sasa unafahamu kesi ya Salah familia imeamua kuifuta , hivyo nakupigia simu hii kukupa maelekezo mengine uache kufatilia kabisa juu ya kesi hio na swala ambalo limetokea lisifahamike tena, nishawalisiana na makao ya polisi na jarada la Salah lishafungwa”

“Afande kwan…?””

“AJenti Flamingo taarifa ni hio , na kwanzia sasa endelea na kazi yako ya kuwa karibu na Hades na kuhakikisha jambo la namna hio halitokei tena , ili kupunguza maswala yasio na majibu”Na palepale simu ilikatwa na kumfanya Magdalena kumwangalia pacha wake Mage.

“Kuna nini Magdalena?”

“Nimepewa oda ya kuacha kufuatilia chochote kinachomuhusu Salah , na jambo hilo liwe kama halijatokea , hayo ndio maagizo yetu na hapa tunapaswa kuondoka”Aliongea Magdalena kwa wasiwasi na kumfanya Mage kushangaa.

“Mbona sielewi, kuna nini kinaendelea?”

“Mage tunapaswa kushukutu pia kwani tumeondolewa mzigo , najua jambo hili linamaswali mengi ila inabidi tutii tulichoambiwa”Aliongea na Magdalena hakusubilia jibu la pacha wake na palepale aliendesha gari kuelekea barabara kuu wakitoka eneo la Mbweni.

“Magdalena angalia kushoto”Aliongea Mage kabla ya Magdalena kukata kushoto karibu na kituo cha kuwekea mafuta cha Lake Oil wakati akitaka kuingia barabara kuu na Magdalena ile anaangalia kushoto alijikuta na yeye akitumbua macho ni kama wote wameona mzimu.

“Salah!!!!”Magdalena alijikuta akikanyaga breki mara baada ya kumuona mwanaume ambaye walikuwa wakimtambua , mwanaume ambaye walikuwa wakijua amekufa kwa kuuliwa na Roma , Mage alijikuta akipagawa na kufungua mlango haraka haraka na kukimbilia nyuma kumuwahi mtu ambaye aliamini ni Salah na kwa upande wa Magdalena hivyo hivyo alikimbilia nyuma kumuwahi dada yake.

“Salah!!!!”Aliita Mage kwa nguvu mara baada ya kumkaribia mwanaume ambaye anaamini ni Salah na pelapele mwanaume yule alievalia suti alisimama na kisha akageuka nyuma na kumwangalia Mage na wote kwa Pamoja wlaijikuta wakirudi hatua mbili nyuma kwa kujikokota huku wakiwa hawaamini macho yao.

Salah alimwangalia Mage na Magdalena kama mtu ambaye alikuwa akijaribu kuwakumbuka , lakini aliishia kutowatambua watu wa mbele yake , lakini pia hakuongea neno lolote Zaidi ya kugeuka na kuendelea na safari yake na kuwafanya Mage na Magdalena kuangaliana.

“Labda watakuwa mapacha”Aliongea Mage na Magdalena na yeye aliunga hoja , walikuwa wakiamini Salah amekwisha kufa hivyo hakuna uwezekano wa Salah kuwa hai na hivyo waliemuona alikuwa ni pacha wake Salah , walikubaliana kutokana na wao pia kuwa mapacha wanaofanana hivyo hoja ya kuona ina mashiko.
 
SEHEMU YA 298.

Roma aliona sasa ni muda sahihi w kufanya kile ambacho kimemleta Japani , ndoa ya Amina ilikuwa ikitarajiwa kuanza siku ya kesho yake asubuhi , hivyo aliona inambidi kuwahi kabla ya hatua za mwisho za maandalizi , ijapokuwa hakupokea meseji tena kutoka kwa mrembo Amina juu ya kuomba msaada lakini kwa taarifa alizokuwa nazo aliona ni jambo la lazima kumuokoa mrembo huyo katika kufunga ndoa ambayo hakuwa akiipenda.

Roma ilibidi amtumie Tanya ili kupata usafiri utakaomtoa hapo Sapporo Kwenda Otaru City sehemu ambayo kwa maelezo ya Makedoni ni kwamba Amina alikuwa amefungiwa ndani ya jengo la hoteli ya nyota tano ambayo inamilikiwa na kampuni ya Emaar kutoa Dubai.

Masaa mawili mbele Roma alikuwa ashafika ndani ya jiji hili la Otaru akiwa anatumia gari ndogo kampuni ya Honda, baada ya kufika ndani ya jiji hili kwanza hakutaka Kwenda moja kwa moja ndani ya hoteli hio kwani kwa maelezo ni kwamba kuna walinzi wengi waliokuwa wakilinda kwa eneo la nje , alichokuwa akitaka kufanya kwanza ni kuhakikisha tumbo lake limeshiba , kwani alikuwa hajala muda mrefu kidogo.

Alisimamaisha gari yake kwenye moja ya mtaa ambao ulikuw ana msururu wa maduka Pamoja na migahawa ya kitamaduni na alichagua mgahawa mmoja uliomvutia upande wa kushoto na kuagiza chakula ca kitamaduni ana ya Tambi(Ramen)na kwakua alikuwa na uzoefu na chakula hiko alikifagilia kwa dakika zisizopungua kumi mpaka kumaliza.

Roma baada ya kumaliza kupata chakula na kuridhika , alianza sasa kufikiria namna ya kuingia ndani ya hoteli hio kwa ajili ya kuonana na mrembo Amina.

Upande mwingine , wakati Roma akiendelea kuwaza, ndani ya hoteli iliokuwa kando ya bahari ndaji ya jiji hili la Otaru , alionekana membo Amina akiwa ndani ya chumba kiikubwa cha ‘Presidential Suite’ akiwa amezungukwa na wanawake warembo wa kiarabu wakiwa katika harakati za kumremba kwa kumchora mikononi kama ilivyokuwa tamaduni za kiarabu pale mwanamke anapotaka kuolewa.

Amina alionekana kama malaika kwa urembo wake kwa namna ambavyo alikuwa amevaa , usiku huo alikuwa ameletewa gauni la harusi kwa ajili ya kujaribisha kulivaa kabla ya siku ya kesho , yaani asubuhi mara baada ya taratibu za kidini za kufungisha ndoa kumaliziaka basi alipaswa kuvaa gauni hilo kwa ajili ya sherehe itakayofanyikia kwenye ukumbi ndani ya meli kubwa ya kifahari.

Licha ya mrembo huyu kuwa katika hali ya kuvutia sana kutokana na namna alivyorembwa akarembika , lakini jambo moja ambalo liliwashangaza warembaji ni hali ya huzuni aliokuwa nayo Amina, Warembaji walikuwa wakimshangaa Amina kwani mwanaume ambaye alikuwa akienda kuoelwa nae alikuwa ni wakuliliwa na wanawake wengi kwa ajili ya kuitwa mume wao , lakini bahati hio kaipata Amina lakini anaonekana kua na huzuni na kuwafanya kushangazwa na jambo hilo mno.

“Nadhani tayai nishajaribisha na limenikaa vizuri , mnaweza kuondoka nitalivua mwenyewe”Aliongea Amina akiamrisha wale wahudumu wa kiarabu kuondoka na hawakaugoma kutii , walimkabidhi Amina ua ambalo alitakiwa kulishikiria akiingia ukumbini na kisha wakamuacha na kuondoka.

Amina baada ya kuona wameondoka , jambo la kwanza ambalo alifanya ni kurusha lile kwa hasira na likaenda kutua kwenye kioo na kwa huzuni alisimama na kusogelea dirisha na kusukuma pazia na kuinua kichwa chake juu angani na kuangalia nyota,Alionekana kuwa kwenye mawazo.

“Natamani Roma angekuwa anajua kinachoendelea na atokee kama muujiza na kuniokoa , nitampenda mpaka kifo changu licha ya kuwa ana mke”Aliwaza Amina huku mchirizi ya machozi ikionekana kwenye uso wake.

Ukweli ni kwamba mrembo huyu licha ya kukamatwa na kuletwa ndani ya hoteli hii na baba yake mzazi Pamoja na Fayezi , kwenye akili yake yote alikuwa akimuwaza Roma Ramoni pekee , alikuwa akitamani sana kumuona angalau kwa mara ya mwisho kabla ya kuingia kwenye gereza la huzuni ambalo linafahamika kwa jina la Ndoa.

Kwake Fayezi alikuwa hampendi hivyo aliamini kinachokwenda kumtokea kitamfanya kutokuwa na furaha kwenye Maisha yake yote na ndio maana alikuwa akiamini ndoa hio inakwenda kuwa gereza la furaha yake.

Alijikuta akigeuka nyuma mara baada ya kuhisi mlango kufuguliwa na alijikuta sura ikimshuka mara baada ya kuona aliengia hapo ndani ni Fayezi mume wake mtarajiwa.

Fayezi aliona mabadiliko ya Amina , lakini hakujali sana , alimwangalia mrembo wake kwa dakika kadhaa kwa jinsi alivyopendezwa na kujikuta akitabasamu.

“Mpenzi wangu Amina , kesho ndio siku yetu , vipi kuna kitu ambacho haujaridhika nacho mpaka sasa kibadilishwe au kiongezwe”Aliongea huku akimsogelea Amina.

“Usinisogelee , ongea kwa mdomo wako tu ninaweza kukusikia”Aliongea Amina huku akimwangalia Fayezi kwa chuki na kwa Fayezi alitabasamu kifedhuli.

“Unajifanya mjanja sana , mwanaume ambaye ulimpa bikra yako nishamuua na huna jipya tena , baada ya ndoa nitakueleza kifo chake ndio zawadi yangu kwako”Aliuwaza Fayezi kwenye moyo wake.

“We’ll immediately be a legally married couple tomorrow. Can’t we get intimate a day before the wedding night?”

“Tutakuwa wanandoa kesho asubuhi , vipi tunaweza kufanya tendo la ndoa kabla ya sherehe za ukumbini usiku?”Aliuliza Fayezi huku akijaribu kumsogelea.

“Nimekwambia usinisogelee Fayezi”Aliongea Amina kwa namna ya kutahadharisha huku akimtishia na kibanio cha nywele na kumfanya Fayezi kusimama katikati ya chumba.

“Okey sitaki kukukwaza usiku huu , kwani kesho ni siku yetu kubwa ,nitakuacha upumzike”Aliongea Fayezi na kisha akageuka.

Pumbavu zako Amina unajifanyisha kama mwanamke Bikra , baada ya ndoa utanijua mimi ni nani haswa”Aliwaza na kisha akafunga mlango kwa hasira na kutokomea na kumfanya Amina kupumua , mrembo huyo hakuwa tayari kabisa kumvulia Fayezi nguo yake ya ndani na alitamani kabisa muujiza utokee ili kikombe hicho cha ndoa kimuepuke , lakini kila alipokuwa akifikiria aliona jambo hilo haliwezi kutokea.na alipaswa kukubaliana na hali.

Kwanza hakuwa na mpenzi ambaye angeamini labda angekuja kumuokoa , pili mwanaume ambaye alikuwa amempatia usichana wake walishamalizana kipindi kilekile kule polisi Tanzania hivyo hakuwa na tumaini nae tena , lakini pia alijiambia hata kama mwanaume yule angekuwa na taarifa za kulazimishwa kuoelewa asingekuwa na msaada wowote kwake , kwani alikuwa akiangalia walinzi waliokuwa wametapakaaa kuzunguka hoteli hio kumlinda , yaani kwa maneno marahisi ni kwmaba hoteli hio ya nyota tano haikuwa na mgeni wa aina yoyote Zaidi ya Amina peke yake na Fayezi ambao walikuwa wakisubiria ndoa yao siku ya kesho.

Akiwa ameupa mgongo mlango wa chumba chake , mara mtu aliufungua tena na alijikuta akiwa na hasira na pasipo kugeuka alianza kufoka.,

“Nimesema toka kwenye chumba changu , nahitaji kupumzika Fayezi m sikutaki sikutaki mimi”Aliongea Amina akidhania aliekuwa nyuma ya mlango alikuwa ni Fayezi alierudi kwenye chumba chake.

“Bibie tuliza munkari, nitatoka kama hutaki kuniona tena”Sauti ilisikika kwenye masikio ya Amina na kumfanya kufuta machozi haraka haraka . sauti alioisikia alikuwa akiikumbuka sana tu na alijihisi ni kama alikuwa kwenye ndoto , kwani mwenye sauti hio hakuwa akimtegemea kuwepo hapo nchini Japani kwa muda huo.

Amina baada ya kuangalia vizuri mwanaume aliekuwa mlangoni alijikuta akipagawa.

“Roma … una,,, una fanya nini hapa?”Aliuliza kwa namna ya kubabaika akishindwa kuelewa imekuwaje Roma mwanaume aliekutana nae kwa usiku mmoja na kumtoa usichana wake kuwa mbele yake , hakuelewa kabisa na ndio maana alikuwa kwenye mshangao.

Licha ya Mrembo aliekuwa mbele yake kushangaa uwepo wake , yeye hakjibu chochote Zaidi ya kuingia ndani na kuruidishia mlango huku akimwangalia kwa tabasamu huku akimpa ishara ya kutaka kumbatio.

Amina alijikuta akishindwa kujizuia kabisa , alitaka kujua ni kweli anaota au anachokiona ni uhalisia, kwani alichokifanya ni kumkimbilia Roma na kujirusha kwenye mwili wake kama mtoto na alijikuta akiamini hakuwa akiota baada ya kunusa harufu ya mwili ya mwanaume huyo , harufu ambayo hawezi kuisahau kwenye Maisha yake , harufu ya mwanaume ambaye alikuwa amemmissi sana na kumkumbuka kila wakati tokea walipoachana.

Amina alijikuta akianza kulia kwa kwikwi mara baada ya kujua kuwa mwanaume aliekuwa mbele yake ndie aliekuwa ametokea kumpenda , alilia kama mtoto ambaye alikuwa ametelekezwa na sasa mama yake ametokea tena.

Dakika kumi na tano zote alimaliza kulia kwenye kifua cha Roma mpaka kumloanisha shati lake.

“Babe Amina hupaswi kulia tena , ni mimi mwanaume mumeo”Aliongea Roma na kmfanya Amina kutabasamu kwa aibu.

“Unakuwaje mume wangu wakati una mke tayari au umemuacha ndio maana umekuja mpaka Japani kuniepusha na janga linalonikaribia?”

“Umeonyesha kunihitaji ndio maana nimetoka Tanzania mpaka hapa kuja kukuokoa , kwanini unakuwa kwenye mshangao , au ulidhania siwezi kuja Japani?”Aliongea Roma na kumfanya Amina kushangaa kidogo , hakuelewa Roma alikuwa akimaanisha nini , lakini hata hivyo alifurahi kumuona mwanaume huyo mbele yake na alimshika mkono na wakakaa kwenye masofa yaliokuwa ndani ya chumba hiko.

“Sijakuita uje Japani na sikutegemea kama unaweza kuja wakati kama huu ambao nilikuwa nikikuhitaji”Aliongea Amina na kumfanya Roma kushangaa kidogo , kwa jinsi ambavyo Amina anaongea aliamini huenda meseji alizokuwa akipokea hazikuwa zikitoka kwa Amina.

Roma alitoa simu yake na kisha akaenda upande wa meseji na kumpatia Amina aangalie jumbe ambazo zimetumwa kwake, Amina alijikuta akishangaa na kutoelewa kinachoendelea.

“Roma sio mimi niliotuma hizi jumbe”Aliongea Amina kwa kuonyesha hali ya kweli katika macho yake na Roma aliamini ni kweli Amina hakuwa ametuma hizo jumbe na mpaka hapo aliamini mpango wote wa kuja Japani ulikuwa ni kwa ajili ya kuingia kwenye mtego wa Kundi Takamagahaea Pamoja na Yamata Sectna mpaka hapo aliamini kwa asilimia miamoja na Fayezi anahusika.

Roma alitabasamu na kuchukua simu yake na kuirudiasha mfukoni na kisha kumwangalia Amina kwa jinsi alivyopendeza na kujikutaka hata pepo la ngono likimvaa.

“Nadhani ni majaliwa ya kimungu ndio yamenifanya kuja hapa , kwani licha ya kwamba haukunitumia wewe hizi jumbe , lakini ulikuwa ukinihitaji na kwa muonekano wako inaonyesha ulikuwa ukipitia wakati mgumu”Aliongea Roma na Amina alianza kutoa machozi kwa mara nyingine na kumsogleea Roma na kumkubatia tena

“Ni kweli nilikuwa nikikuwaza usiku na mchana kukuona tena, tokea siku tulioachana , sikudhania kama nitakuona wakati kama huu ninaokuhitaji kuliko kitu chochote , Asante sana Mpenzi wangu kwa kuja kuniokoa , hakika imepangwa mimi na wewe kuwa pamoja”Aliongea

“Usinishukuru mapema hivi , ijapokuwa nimekuja hapa ndani lakini sijajua namna ya kukuokoa”Aliongea Roma na kumfanya Amina amwangalie.

“I’m not stupid. You tracked me down so easily and managed to enter the presidential suite while being unnoticed, you must have a plan. I’m too lazy to ask you about it, I’ll just do whatever you say.”

“Mimi sio mjinga , umeweza kugundua kirahisi nipo hapa na kuingia mpaka ndani ya chumba hiki cha Presidential pasipokugundulika , lazima utakuwa na mpango , ninahisi uvivu kukuuliza ila nitafanya kila utakachoniambia”Aliongea Amina.

“Inaonekana unauwezo mkubwa sana wa kuelewa mambo , inaonekana tunaendana kwa kiasi kikubwa”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Kwasababu ulishafika sitokuacha tena kwemye Maisha yangu , nitafanya kila utakaloniambia ilimradi tuweze kuondoka Pamoja”Aliongea na kumfanya Roma mwili usisimke , mwanamke aliekuwa akimwambia maneno hayo alikuwa ni mrembo mno na kwa mwaaume rijali yoyote ni lazima angesisimka , Roma hakutaka kuchelewesha palepale alimvutia Amina kwake na kuanza kumkisi mdomoni.

“Mhmh..!!” Aliguna Amina na kujitoa kwa Roma na kumfanya Roma kushangaa, yaani yeye ashapata moto halafu anajitoa kwake tena.

“Geuka nyuma kwanza kuna kitu nifanye kabla hatujaanza kufanya”Aliongea Amina psipo aibu na kwa namna ya kuwa siriasi na Roma hakubisha , aligeuka nyuma akimwacha Amina.

“Unaweza kugeuka sasa”Aliongea Amina na kumfanya Roma kugeuna na alishangaa mno kwa kitendo alichofanya Amina , alikuwa amevaa shera kwa kujifunika kichwa na alikuwa akimsubiria Roma kumfunua mwali wake.

Laiti Fayezi angeona mambo ya kipuuzi ambayo yanataka kufanyika hapo ndani ni dhahiri kama ana siraha mtu wa kwaza kumiminia risasi atakuwa ni Amina.

“Roma naonekana mrembo?”Aliuliza huku akijichekesha na Roma alikuwa ametegeka kwa Amina kwani palepale alimsogeleana na kisha kumkubatia na ile anamwachia alimfunua ile shera na kisha kuanza kumkissi mdomoni na kwa upande ewa Amina na yeye hisia zishampanda na alichokifanya ni kuning’inia kwenye mwili wa Roma na wakaendelea kudendeka kwa kupiga Romansi.

Roma alimbeba juu juu mrembo Amina na Kwenda kumtupia kitandani , huku akiangalia gauni la harusi ambalo Amina amelivaa.

“Hili gauni ni refu sana tunalivuaje?”

“Usiogope kuliharibu , ukitaka lichane kabisa kwanza limetolewa na familia ya Fayezi”Aliongea Amina pasipo kujali gharama ya gauni hilo , alichotaka kwa muda huo ni Roma amvue nguo zote na kisha amwingie

Kwa Roma kauli hio ilikuwa ni kama vile njiti ya kiberiti ikitupiwa kwenye tanki la Petroli kwani mizuka ilimpanda maradufu na ukizingatia na mwanamke anaeyatamka maneno hayo alivyokuwa mrembo ilikuwa ni raha sana kwa upande wake na alijisifia kwa kujiona ni moja ya wanaume ambao wamependelewa sana kwenye dunia hii.

Roma alitoa tabasamu lake la kifedhuli huku akimwangalia Amina aliejichanua kwenye kitanda hicho cha sita kwa sita na Alichokifanya ni kushika ukingo wa gauni hilo kutoka miguunu na kilichosikika ni .. Traaa.. tratata, Gauni lilichanwa kuanzia miguuni mpaka kiunoni na kufanya nguo ya ndani rangi ya pink iliovalia mrembo huyo kuonekana wazi na kumfanya Roma aone kanzi nzuri amefanya kuchana gauni la harusi.

Dakika kadhaa mbele ndani ya chumba cha kifahari ambacho kimeandaliwa na familia ya Tajiri Khalifa kwa ajili ya mkwe wao , kilichosikika ni miguno ya kimahaba kwa takribani masaa mawili yote, huku gauni ambalo lilikuwa likitarajiwa kuvaliwa na mrembo huyo likiwa limachwana na kutupwa pembeni , na kilichoonekana ni mwili wa rangi nyeusi ukiwa umeungana na mwili wa rangi nyeupe ya kiarabu.

“Roma umekuja kuniokoa au kuniadhibu?”Alilalamika Amina mara baada ya Roma kutua mzigo wake wote wa dhambi ndani ya Amina.

“Hehe.. ulivyoniambia nichane gauni lako la harusi ulikuwa ukitaka nifanyeje?”

“Nilikuambia uliharibu ila sio kuniadhibu kwa Zaidi ya masaa mawili”Aliongea na Roma alimfinya mashavu akimwambia aache kulalama.

“Hujaniambia tunatokaje sasa hapa ndani?”Aliuliza Amina akitaka kujua mpango wa Roma ni upi.

“Hakuna kutoka hapa ndani , kesho utaendelea na harusi kama kawaida , kiufupi unatakiwa kufanya kila watakachokuambia na ufuate taratibu zote, panda meli ambayo imeandaliwa kwa ajili ya harusi na baada ya hapo nitawapatia zawadi niliowaandalia”Aliongea Roma na Amina kwakua alikuwa akiamini mipango ya Roma aliitikia kwa kichwa kwa furaha na dakika chache mbele alipotelea usingizini kwenye kifua cha Roma huku akionekana kuwa hoi taabani kwa bakora za kimkakati alizopaitiwa.

Roma baada ya kumuweka vizuri Amina kitandani na kmfunika na shuka , alisogelea simu yake na kisha akaitoa na aliona meseji ambayo imeingia , aliifungua na kusoma ujumbe uliokuwa umetumwa.

“Mission Accomplished”Meseji hio ilisomeka hivyo na Roma alitabasamu.
 
Back
Top Bottom