Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Mkuu singanojr tumekuwa pamoja kwenye simulizi hii tangu tarehe 10 agust 2022! Ni miez minne sasa tupo pamoja! Fikiria mara 2 uone jins gan umepata follower wengi na pia wateja! Umejenga jina lako na utunzi wako huu umekufanya kujulikana zaidi kama nguli wa riwaya tamu! Miezi yote hyo naamin kilichobaki ni kidogo! Tafadhal mkuu tunaomba utupostie tupone. Nakuahidi mimi MTENGETI nikifanikiwa kuuza choroko zangu nitanunua smat na ntainunua hii riwaya yote hata kama utakuwa umemalza kupost humu! Tupostie mheshimiwa

Yan kama utamu ndo unaanza mkuu huko kwenye grup tunaenda sehemu ya 350[emoji28][emoji28]
 
mzee baba singanojr tupe muendelezo tumuone roma anavyokuja juu kwa speed ya mwendo kas
 
Lipieni tu maana kwa sasa mwandishi anafanya biashara na si burudani ya bure.
 
SEHEMU YA 290.

Ni siku mbili sasa upande wa Tanzania , licha ya kwamba Edna hakupata taarifa yoyote kutoka kwa Roma , lakini alionekana kutokuwa na wasiwasi kabisa , alikuwa akiamini kwamba hakuna baya lolote ambalo litamkuta Roma , kwani kwa jinsi alivyokuwa akimfahamu aliamini ndani ya dunia hii Roma ni kiumbe cha pekee sana ambaye hakuna binadamu wa kawaida anaweza kumdhuru.

Edna alikuwa ni moja ya watu ambao wameshuhudia mambo makubwa na ya kutisha ambayo Roma ameweza kufanya na hii imemfanya mrembo huyu kuona haina haja ya kuwa na wasiwasi kwani Roma ni lazima atarudi akiwa salama na kimya cha Roma kwake akikumsumbua .

Upande wa Blandina mama yake Roma hali ilikuwa tofauti kabisa , mwanamama huyu alikuwa akijaribu kupiga namba ya Roma kila baada ya masaa mawili , alikuwa na wasiwasi mno , ukijumlisha ndoto mbaya ambayo ameweza kuota lakini pia namna ambavyo Roma amekuwa kimya huko Japani kwake ilikuwa ni kama ugonjwa ambao tiba yake ni kusikia sauti ya Roma pekee.

Ni saa nne asubuhi Edna alionekana kuwa kazini akiendelea na majukumu yake kama kawaida na ndani ya ofisi yake alionekana Monica ambaye alikuwa akimpa baadhi ya maelekezo kwa takribani dakika kumi mpaka kutoka, dakika nne nyingine mlango tena ulifunguliwa na Monica.

“Boss Mr Amiri amefika”Aliongea Monica na Edna alimpa ishara ya kumruhusu na alionekana mwanaume alievalia suti akiingia hapo ndani akiwa na mkoba mweusi, alikuwa ni Amiri kiongozi mkuu wa kitengo cha Athena.

“Karibu Amiri”Aliongea Edna huku akinyanyuka kutoka kwenye kiti chake na kusogea mpaka kwenye masofa na kumpa ishara Amiri kuketi kwa ajili ya mazungumzo.

“Mmepata nini mpaka sasa na kutaka kuongea na mimi moja kwa moja?”Aliuliza Edna na Amiri alitabasamu kidogo na kisha alichukua mkoba wake na kuufungua ndani na kutoa karatasi yenye nembo ya taifa la Tanzania na kumkabidhi Edna.

“Kama ulivyoniambia nifuatilie kuhusu kampuni ya Maya na Innova nimegundua baadhi ya taarifa muhimu ambazo naweza kwa namna moja ama nyingine zinaiunganisha kampuni ya Vexto na Maya, hio karatasi ulioshika ni mkataba wa kazi kati ya Dr Seba Tinde na hospitali ya Maya tawi la Dar es salaam”Aliongea Amiri na kumfanya Edna asielewe.

“Mkataba huu kwanini unanionyesha?”Aliuliza Edna na Amiri hakuongea neno , alichokifanya ni kuvuta karatasi nyingine kwenye mkoba wake na kumpatia Edna.

“Nadhani Boss hujawahi kumfahamu Dr Seba Tinde , kwa taarifa tuliokuwa nayo ni kwamba Dokta Seba Tinde alikuwa ni daktari wa baba yako mzazi”Aliongea na kumfanya Edna kushangaa kidogo.

“Inawezekana nikawa namjua kwa sura ila simfahamu kwa jina , sikuwa na ukaribu sana na Maisha ya baba , ila bado hujaniweka wazi swala la Dokta Seba linahusiana vipi na kazi niliokupatia”

“Dokta Seba ndio aliekuwa akimhudumia Boss Raheli Adebayo mpaka saa ya mwisho ya pumzi ya uhai wake , kwa maneno marahisi kifo chake kilithibitishwa na Dokta Seba ndani ya hospitali ya Maya lakini jambo la kushangaza boss kwa uchunguzi ambao tumefanya tumegundua pia Dokta Seba alifariki siku mbili baada ya kifo cha Boss Rahel”Aliongea Amiri na kumfanya Edna kushikwa na mshangao mno ni kama kuna jambo alikuwa akianza kulihisi kwa mbaali na aliomba lisiwe la kweli.

**************

Hakuna ambaye aliweza kuelewa kwanini Jessie alikuwa akitaka kuona Jeraha ambalo lipo kwenye mwili wa Hades, lakini kwasababu mwili wa Roma ulikuwa umelipiwa maamuzi yalitakiwa yafanywe na wale wawakilishi wa kampuni ya Innova wenyewe.

“Jasie unaweza kuangalia , japo hatujui dhumuni lako ni nini?’Aliongea Bruno na Jassie kupata ahueni mara baada ya kuruhusiwa.

Tanya ndio mtu ambaye alikuwa amesimama karibu na mwili wa Roma na tokea wamwingize kwenye chumba cha baridi lakini pia kutoa kisu walichomchoma nacho , hawakuwa wameangalia jeraha lake na hio yote ni kutokana na kuamini haikuwa na maana tena , kwani mtu mwenyewe alikuwa amekwisha kufa.

Jessie baada ya kufungua sehemu ambayo Roma amechomwa na kisu alijikuta akipagawa ghafla kiasi cha kumfanya Tanya na Jasoni waliokuwa karibu yake kutaka kujua ni kwanini alikuwa akishangaa.

Lakini na wao baada ya kushudia kile ambacho Jessie amekiona walijikuta wakitoa mshituko.

“Tanya kuna nini , mbona mnaonekana kushangaa”Aliongea Okawa akitaka majibu, lakini Tanya hakujibu Zaidi ya kukimbilia kuweka mkono upande wa moyo wa mwili wa Roma na alijikuta akipagawa baada ya kuhisi mwili wa Roma kuwa na joto kama la mtu aliehai lakini pia moyo wake kudunda.

“Master He is alive”Aliongea Tanya akimaanisha kwamba Roma bado anaishi , kauli yake iliwafanya watu wote kushangaa na ni kama hawakuwa wakiamini, na Okawa aliekuwa kwenye kiti chake cha Enzi alishuka haraka haraka chini kutaka kuthibitisha , lakini kabla hajafika akiwa na panga lake Roma aliekuwa amefumba macho aliyafumbua na kumwangalia Jessie aliekuwa akimshangaa na wote kwa Pamoja walijikuta wakirudi nyuma kwa mshituko.

Noriko Okawa baada ya kugundua Roma yupo hai bado alijikuta akipagawa mno na hakuelewa jambo hilo linawezekana vipi , kwani yeye mwenyewe ndio aliemkita Roma na panga lake kwenye moyo.

Wale waliokuja kununua mwili wa Roma pia walionekana kuwa kwenye mshangao na macho yao yote waliyapeleka kwa Okawa , lakini walimkuta bwana huyo na yeye akiwa kama wengine tu kwa mshangao.

Kwanza kabisa walichokiona Jessie na wengine ni kwamba sehemu ambayo Roma alikuwa amechomwa na Kisu pamoja na panga la Masamura pamekuwa pameshaziba kabisa na hapakuwa na alama yoyote ya kuonyesha kama kulikuwa na jeraha, sasa haikueleweka imekuwaje lakini Roma alionekana kuwa hai.

Sasa wale walinzi ambao sasa walakuwa wamemshikilia Kawanako walijikuta wakisahau kazi yao na kumfanya mwanadada yule kuchoropoka na kuukimbilia mlango lakini kabla hajatoka , alijikuta mkojo ukitaka kumtoka kwani mtu aliekuwa mbele yake alikuwa ni Hades, hakuelewa imekuwaje akawa mbele yake kwani alikuwa amemuacha nyuma yake akiwa kwenye kitoroli akiwa amelala licha ya kufumbua macho , mrembo huyu alikuwa akijihadhari baada ya kugundua Roma hajakufa..

“Nani kasema unaweza kunikimbia…”Aliongea Roma huku macho yake yakianza kubadili rangi na kuwa ya kijani tupu , huku sauti yake ikisikika kwa besi sana kiasi cha kutetemesha kila mmoja aliekuwa hapo ndani.

Kawanako baada ya kuona Roma yuko mbele yake alikimbia kurudi na Kwenda kusimama nyuma ya Noriko Okawa.

“Inawezekana vipi hili..?”Aliuliza Okawa kwa mshangao , hakuelewa bado kwanini Hades alikuwa hai licha ya dakika kadhaa kuwa mfu.

“Usishange, licha ya kwamba ulikuwa ndani ya Zeros organisation haimaanishi kwamba ulikuwa unanijua wewe pamoja na wanasayansi wenzako, baada ya kuharibu makao yenu kule Madagascar sikuondoka na Seventeen na Kwenda kukaa tu kizembe, Okawa nadhani hata huelewi kwanini Master Chi aliuliwa na Dhoruba nyekundu?”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la kifedhuli akimwangalia Okawa aliekuwa bado kwenye mshangao.

“Unataka kusema nini kuhusu Tang Chi?”Aliuliza na Roma alitabasamu.

“Master Tang Chi ndio alikuwa mkufunzi wangu baada ya kufika nchini Mongolia kutafuta namna ya kuendeleza Maisha nikiwa na Seventeen”Aliongea na hapo sasa Okawa ni kama akili yake inaanza kufanya kazi , ni kweli alishawahi kusikia juu ya Dhoruba Nyekundu kumuwinda Tang Chi lakini licha ya kusikia Habari hizo hakuwahi kujua sababu kumbe yote hayo yalikuwa ni baada ya kujihusiha na kumfundisha Hades.

“Siku ya kifo cha Seventeen niliweza kufikia levo namba nane ya uwezo wa kijini , levo ya uhai na kifo na kwanzia siku ile nilijitahidi sana kufikia levo namba tisa ya Kuzaliwa upya(Rebirth) lakini ilishindikikana , shukrani zikuendee wewe kwani leo hii nimeweza kufanikiwa kufikia levo namba tisa ya kuzaliwa upya , Sikuweza kufahamu kwamba ili kufikia levo namba tisa ni mpaka nitakapoweza kukiona kifo kwanza”

“Hades tuambie unawezaje ukapitia kifo na wakati huo ukaweza kurudi hai?”Aliuliza Jessie kwa shauku kubwa.

“Kwasababu ya kanuni nyepesi ambayo binadamu wa kawaida mpaka sasa hamjaweza kuifahamu , Kanuni ambayo inahusiana na Nishati inayotokana na maada na ile ambayo haitokani na Maada(Ant-Matter and Matter Energy) ,Nilichokifanya ni kuizuia roho yangu huku nikiruhusu mwili wangu kufa, Sumu mlioniwekea ilisababisha mwili wangu kushindwa kujiponyesha lakini haimaanishi kwamba nina mbiniu moja tu ya kuufanya mwili wangu kujiponyesha, nilichokifanya ni kuutelekeza mwili kwa kutumia Nguvu isiotokana na maada huku nikiruhusu nguvu ya maada kuuponyesha mwili wangu.”Aliongea Roma , lakini bado ilionekana anachoongea hakieleweki. Na ambaye alionekana kutokuelewa kati ya wote ni Noriko Okawa.

“Unaongea ujinga gani?”Aliongea Noriko kwa hasira huku akijiandaa kwa ajili ya mapambano.

“Okawa niseme tu kwamba nimependa ulivyonichoma na hilo panga lako lakini pia na kuchukia kwa wakati mmoja , umenichoma nikanufaika na kuingia levo namba tisa ya kuzaliwa upya lakini pia kitendo chako cha kunishambulia kinanifanya nitake kukuua , unafikiri ni upande gani napaswa kuchagua?”

Noriko Okawa kwa kutumia uwezo wake wa kichawi aliweza kuona Roma ni kama mtu mpya kuliko na alivyokuwa mwanzo , hakuamini kama mpango wao wa kumuua Roma umempelekea Kwenda levo nyingine Zaidi
 
SEHEMU YA 291

Moja ya sababu ambayo ilimpelekea Master Chi kumfundisha Roma mbinu ya kujiponyesha kutoka ujinini ni kutokana na ugonjwa Roma aliokuwa nao , ugonjwa wa saratani ya ubongo , ugonjwa ambao licha ya kwamba mwili wake ulifanyiwa sayansi , lakini ilishindikana kupona kabisa kwa asilimia mia moja , hivyo mara nyingi kumpelekea kushindwa kujizuia pale mwili wake unapopitia mabadiliko.

Ijapokuwa Master Chi aliweza kumfundisha mbinu hio Pamoja na levo zake , lakini hakumwambia jina la mbinu hio linaitwaje , Sasa Roma alijifunza kwa miaka mingi pasipo kujua jina lake , baada ya kifo cha Seventeen ndio aliweza kuvuka kutoka levo namba saba ya Lango na kuingia levo namba nane ya Kifo na Uhai na baada ya hapo ndipo alipoaamua kuipatia mbinu yake jina la kingereza ‘Endles Resolve restoration Scripture’ na kwa lugha ya Kiswahili ni Nguvu ya kimaandiko ya urejesho isiokuwa na kikomo.

Moja ya sababu ya kuipatia jina hilo ni kutokana na kwamba kila akitaka kuitumia mbinu hii lazima atamke baadhi ya meneno maalumu ili kuweza kupata kuitumia , unaweza kuifanananisha na ‘Spirity energy’ au kama vile ‘Albadir’ katika dini ya uislamu lakini utofauti wake ni kwamba mbinu yake Roma haikuwa ikitegemea ‘Freewill’ au Imani kuweza kuitumia , bali alikuwa akitumia kanuni za namna ambavyo ulimwengu umeumbwa.

Dunia imeumbwa kwa namna ya uwili(Duality) kwa falsasa za kichina wanaita Yin and Yang, yaani ukinyume unaoungana , kwa mfano kinyume cha mwanamke ni mwanaume , knyume cha dunia ni mbingu , kinyume cha uhai ni kifo na kinyume cha Nishati Maada(Matter Energy ) ni Nishati isio Maada(Ant-Matter Energy).

Sasa Roma ili mbinu yake kufanya kazi lazima atumie siri iliopo kati ya ‘Matter Energy’ na ‘Anti-Matter energy’ ili kupata nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo , mbinu hii ndio moja ya njia ambazo majini wengi hutumia kufanya mambo mengi yanayofanana na miujiza au Mazingaombwe(Magic).

Sasa Noriko Okawa na wenzake ambao waliandaa mpango wa kumuua Roma hawakuamini kama mpango wao ndio umemuwezesha Roma kupanda levo nyingine, licha ya kwamba hakuna ambaye alikuwa akifahamu ni mbinu gani hio Roma aliokuwa akiizungumzia ya kumfanya kuingia levo nyingine , lakini Noriko Okawa kwa kutumia uwezo wake aliona kabisa Roma alikuwa ni wa tofauti na alivyokuwa mwanzo.

Roma licha ya kwamba alikuwa ameamka , lakini alionekana kuwa katika mawazo , ni kama mtu ambaye alikuwa akitafakari kilichotokea siku mbili zote akiwa ndani ya jokofu.

Muda huo huo mvua na yenyewe ilianza kunyesha nje kiasi chakumfanya Roma kuzidi kuingia katika tafakuri nzito, mwili wake haukuwa kama ulivyokuwa kabla ya kuja hapa Japani na msisimko anaousikia ulikuwa wa kipekee sana na ndio uliomfanya kuanza kufikiria.

Sasa wale wawakilishi kutoka Innova baada ya kuona Hades hajafa , waliona sehemu hio sio mahali pake kubakia , walimwangalia Roma na kuona alikuwa kama mtu ambaye yuko kwenye mawazo na waliona huo ni wakati sahihi kwa wao kuondoka ndani ya hilo eneo .

Jasie na Jasoni pia waliona hapo sio mahala pake , kwani muda wowote ambao Roma atarudi kutoka kwenye hali yake ya kutafakari basi ni hakika kwamba hawawezi kupona hata kidogo.

Kwa kutumia kelele zilizokuwa zikisababishwa na mvua waliamini Roma mpaka akigeuza macho upande wao basi watakuwa wametoweka lakini jambo ambalo hawakuwa wakijua ni kwamba , licha ya Roma kuwa kwenye tafakari , lakini bado alikuwa akielewa kila kinachoendelea, ni kama alikuwa akiwasubiria wafike mlangoni kama ilivyokuwa kwa Kawanako.

“Hakuna mtu kuondoka hapa ndani bila ruhusa yangu”Aliongea Roma alieibukia mbele ya Jessie na Jassoni na mabwana hao walianza kutetemeka na kurudi nyuma kwa woga na ile wanafika kati walishangaa kitendo cha ajabu kikitokea , milango yote pamoja na madirisha yalijifunga yenyewe kwa wakati mmoja na kumfanya hata Noriko Okawa na Tanya kushangazwa na uwezo wa aina hio.

Roma aliwaangalia maadui zake kwa tabasamu la kifedhuli na akili yake ilichokuwa ikimwambia kwa wakati huo ni kuwaua wote.

“Kama nakumbuka vizuri miaka kadhaa nyuma nilitaka kuharibu makao makuu ya Innova kwa uchokozi wao usiofika mwisho , lakini kwasababu ya heshima ya Aphrodite niliwasamehe , ila kwa siku ya leo sidhani kama awamu hii nitaweza kutoa msamaha , nisipopata maelezo ya kutosha kutoka kwenu , basi viongozi wenu wakubwa watanipa maelezo baada ya vifo vyenu”Aliongea Roma huku akitembea taratibu akiwasogelea wawakilishi wale wa Innova , ambao sasa kila Roma akipiga hatua moja na wao walikuwa wakipiga hatua mbili kurudi nyuma , walionekana kuwa katika hofu isiokuwa na kifani.

“Hades tupo hapa kwa maelekezo kutoka makao makuu , hatuhusiki juu ya hili”Aliongea Bruno na Roma wala hakumzingatia bali macho yake yalimwangalia Jasoni pamoja na Jessie ambao na wao walikuwa wakimwangalia kwa wasiwasi.

“Nina maswali pia kwanin Dhoruba nyekundu wananifuatilia sana na nina mashaka hata muda huu kuna kamera za siri walizotega na wanaona kila kitu kinachoendelea hapa”Aliongea Roma.

“Hades mimi ni shabiki wako wa siku zote na sijawahi kukusudia kifo chako , mimi pamoja na Jasoni na kundi lote la Dhoruba nyekundu”Aliongea Jessie na kumfanya hata Jasoni kumshangaa mwenzake.

“Kama kweli wewe ni shabiki yangu , kwanini mpo mahali hapa mkiambatana na wahalifu na kwanini Innova wametaka muwekwe huru kwa dili alilolifanya Noriko Okawa kwa kutumia mwili wangu?”Aliuliza Roma na Jasoni alimshika mkono Jessie akionyesha ishara ya kwamba haruhusiwi kuongea na Roma aliwaangalia kwa dakika kadhaa na kisha akaachana nao na akamwangalia Kawanako , mwanadada ambaye ndio aliemwingiza mtegoni kwa kumuigizia kuwa ni Seventeen.

Roma alimwangalia mwanamke huyu aliejificha nyuma ya Noriko Okawa kwa sekunde kadhaa na akili yake ilimkumbusha miaka kadhaa nyuma , siku ambayo Seventeen alijirusha kutoka kwenye mwamba na kutua kwenye bahari na ikafuatia mlipuko ambao kwanzia siku hio alikuwa akitafuta wahusika.

Roma alijiambia kwenye moyo wake siku ya leo ndio ya kulipiza kisasi, kwanza kabisa Kawanako alikiri mwenyewe kwamba Seventeen hakujirusha kwa hiali yake , bali yeye ndio alimsukuma , hivyo moja kwa moja ikimaanisha kwamba yeye ndio aliemuua , Roma alimwagalia kwa dakika kadhaa na alijikuta tukio la Seventeen kujirudia rudia kama mkanda wa video unaopelekwa mbele na kurudishwa nyuma, na kadri alivyokuwa akishuhuduida tukio lile kwenye akili yake ndio hasira zilianza kumjaa na kufanya macho yake ambayo yalikuwa na kiini cha rangi ya kijani kubadilika na Kwenda kwenye tangi ya njano na kumfanya Jasoni na Jessie waliokuwa wakishuhudia tukio hilo kujawa na wasiwasi , kwani walikuwa wakijua maana ya rangi za macho ya Roma zinamaanisha nini.

“Jessie this time there is no way out for us to be alive”

“Jasoni ningejua hii misheni ilikuwa ya aina hii nisingeleta mguu wangu hapa , hata kama makao makuu ndio wangenipa oda ya moja kwa moja , wametuweka kwenye misheni ya kifo”Aliongea Jessie kwa wasiwasi mno.

“Jessie tumefunzwa kutii oda kutoka kwa wakubwa wetu , haijalishi misheni ni ya aina gani lakini lazima tutii kile tunachoagizwa”

“Na nini kitatokea baada ya hapa , tunakufa hapa huku makao makuu wakishuhudia vifo vyetu?”Aliuliza Jessie kwa namna ya hasira lakini kabla Jasoni hajampa jibu walijikuta wakiziba mdomo mara baada ya kushuhudia Kawanako akiwa kwenye mikono ya Roma akining’inia hewani akiwa amekabwa shingo.

Noriko Okawa ambaye alikuwa tayari kupambana na Roma hakuelewa hata Roma alipotea vipi na kuibuka nyume yake , kwani kitendo hiko kilikuwa hca haraka sana.

‘Puuh’

“Nadhani kabla ya kutekeleza kifo chako nikupe nafasi ya kuonyesha uwezo wako , naamini haujapewa jina la Mbweha wa miguu tisa bila sababu”Aliongea Roma baada ya kumtupa chini Kawanako.

“Hades ijapokuwa naweza nisikushinde lakini asante kwa kunipa nafasi ya kupambana kabla ya kuniua , sijutii kufa kwa mikono yako katika harakati za kujaribu kulipiza kisasi cha dada yangu”Aliongea Kawanako na palepale alinyanyuka haraka sana na kusimama , huku mwili wake ukainza kupitia mabadiliko na kufanya kila mmoja aliekuwa hapo ndani kuhisi msisimko usiokuwa kawaida.

Kawanako dakika ileile alipotea alipokuwa amesimama kama jini na kumfanya Roima kutabasamu kifedhuli na kufumba macho na kilikuwa ni kitendo cha nusu dakika tu Roma alisogea pembeni kwa namna ya kukwepa hewa na hapo hapo Kawanako alionekana akiwa mbele yake huku mwili wake ukiwa umebadilika na kuwa na nywele nyingi nyeupe kama vile paka , huku vidole vyake vikiwa na kucha zilizochomoza.

“Wow I like it”Aliongea Roma kwa tabasamu baada ya kuona Kawanako kabadilika na kuwa na mwonekano kama wa paka Shume.

Kawanako baada ya kuona Roma kamkwepa kwa mara ya kwanza aligeuka kwa spidi kubwa na kumsogelea Roma tena huku awamu hii akidhamiria kumpiga ngumi .lakini Roma alikuwa amemtegemea kwani ile anamfikia alimuwahi ngumi ya kifua na kumfanya kurudishwa nyuma na kudondoka chini.

“Inukaaaa…!!!”Aliongea Kawanako kwa lugha ya kijapani huku akionyesha hali kama mtu ambaye alikuwa akiita mapepo , kwani mikono yake yote miwili alipeleka mble kama vile mtu anasali.

“Inukaaa… Frujooof.. Frujoof!!!!”

“Boom! Boom!”

Hakuna mtu ambaye alitegemea lile tukio , kwani baada ya Kawanako kupandisha mashetani palepale sakafu ilipasuka na kusababisha mawe kuruka juu na kugonga ukuta , kitendo ambacho kilimfanya Roma kusogea sehemu aliosimama , kwani kidogo tu apigwe na jiwe.

“Damn it you are Demonic Cat!!?”Aliongea Roma kwa mchango baada ya kuona sehemu ambayo alikuwa amesimama kuchimbika na hapo ndipo alipogundua hakuwa akipambana na mtu mwenye nguvu mithili ya Mbweha wa vichwa tisa , bali alikuwa akipambana na Demon- Cat yaani pepo la kichawi sura ya paka.

Kawanako licha ya Roma kuongea kwa upande wake alionekana kama vile hakuwa akijielewa alichokifanya , na macho yake yalikuwa yamevilia damu mpaka alikuwa akitisha , ukijumlisha na Ngozi yake ambayo ilikuwa na vimelea vingi ilimfanya hata wale ambao hawakuwahi kukutana na hali kama hio kuwa katika mshangao mkubwa sana , akiwemo Jasoni na Jessie.

Kawanako baada ya kuona jaribio la kwanza limeshindikikana aliona atumie mwili wake kama siraha, alianza kuzungusha mikono yake juu kama vile anatafuta balansi ya kuruka sarakasi na Kumfanya Roma kutaka kujua anataka kufanya nini , lakini ghalfa palepale Kawanako aligeuka kama mpira ambao umezingiwa na miale kama radi ya rangi ya pimk na kumsogelea Roma kwa spidi kali , lakini mtaalamu Roma alikuwa amesimama palepale na ile mwili wa Kawanako unamfikia aliinua mkono wake juu na kisha akapiga ngumi mpira ule na Kawanako alirushwa na Kwenda kutua kwenye ukutana mpaka akatoka damu , lakini bado alionekana nguvu za kupigana anazo.

“Noriko unaonaje tukiunganisha nguvu kupigana kwa Pamoja , najua tulikuwa kwenye sintofahamu kati yetu lakini muda huu ni wa kifo na uhai”

“Sitaki kuichafua ‘Legacy’ ya mababu zangu kwa kuchangiana na mwanamke katika mapambanoo , wewe ukishindwa mimi nitapigana nae kwa wakati wangu”Aliongea kwa Kebehi , licha ya kwamba alijua Roma ana uwezo mkubwa , lakini aliamini kupigana kwa kusaidiana na mwanamke kwake ni matusi.

Kawanako baada ya kuona hana msaada palepale alijibadilisha mwili wake na kuwa Seventeen na kumfanya Roma kushangaa kutokana na mabadiliko hayo ya Ghalfa.

“Thirteen .. please don’t kill me anymore..”Aliongea Kawanako Seventeen feki huku akijifanyisha myonge mbele ya Roma,. Aliamini hiio ndio mbinu pekee ya kumchanganya Hades.

Roma baada ya kuona mwanamke ambaye alikuwa akifanana na Seventeen kwa kila kitu alijikuta macho yake yakitoka kwenye unjano na kurudi kuwa kawaida na jambo hilo lilimfanya hadi Noriko Okawa kutabasamu na kwa upande wa Kawanako aliona hio ndio nafasi pekee ,kwani palepale alitoka alipokuwa amesimama na ile anaibukia alikuwa juu ya shingo ya Roma , lakini pia haikuwa kwa Kawanako tu baada ya Noriko Okawa kuona Roma alikuwa amechanganyikiwa kwa dakika kadhaa na yeye alitoa upanga wake wa Masamura na kumsogelea Roma kwa nyuma na ile anamfikia tu alitumai nguvu zote kumchoma Roma mgongoni kwa panga lake , lakini alijikuta akitoa macho kwani panga lake lilipita hewani na Kwenda kumchoma Kawanako mwenye muonekano kama wa Seventeen.

“Why..!!!”Alishangaa Noriko O?kawa baada ya kugundua kuwa kilichokuwa mbele yake sio mwili wa Roma bali ni kama picha iliokuwa kwenye mfumo wa Hologam na kitendo chake cha kutumia nguvu kuchoma picha hio panga lake limeenda kumchoma kawanako.

Kawanako ambaye alikuwa akitokwa na damu mfuliulizo alimwangalia Roma aliekuwa nyuma yake kwa macho ya huzuni , alionekana alikuwa akimlaani hata akiwa kwenye kifo chake , Noriko Okawa baada ya kuvuta panga lake nje palepale Kawanako alidondoka chini na kufa hapohapo akiwa kwenye sura ya Seventeen ileile na kitendo kile kilimfanya Roma kuwa katika hali ambayo haikuwa ikielezeka kama alikuwa na fuaraha ama huzuni , ila alimwagalia Kawanako kwa namna isiokuwa ya kwaiada.

Noriko Okawa baada ya kugundua kuwa yupo kwenye hatari kubwa ilibidi awaangalie Tanya na Tanuki waliokuwa pembeni muda wote , Jesie na Jasoni pia walikuwa wamejibanza kwenye kona wakishuhudia kile ambacho kinaendelea na pia kwa upande wa Bruno na mwenzake pia walikuwa wakishuhudia kila kitu , lakini walionekana kuwa katika hali ya hofu mno .

“Kama mnataka kuishi inabidi mpambane na mimi”Aliongea Noriko Okawa kwa kuwaamrisha Tengu na Tanya kuungana kumshambulia Roma. ,lakini kwa Tengu aliona Master wake hana nafasi ya kumshinda Roma , hivyo aliamini mbinu pekee ya kuweza kuishi ni kutafuta namna ya kukimbia , aliangalia upande wa darini ambao umeharibika baada ya Kawanako kutumia nguvu zake za kichawi na alijiambia hio ndio sehemu pekee kwa yeye kukimbilia ili kuweza kutoka , lakini ni kama Roma alikuwa amemsoma mawazo yake kwani ile anapiga hatua tu Roma yuko mbele yake.

“Mara ya mwisho ulivyokuja Tanzania na kumteka mke wangu , nilitamani sana kukuua lakini nilikuacha kwasababu sikuwa kwenye nafasi nzuti , lakini leo hii ni swala tofauti”Aliongea Roma na palepale kwa kutumia mikono yake miwili alimpiga Tengu kichwani na kwasababu nguvu aliokuwa akitumia ilikuwa sio ya kwaida basi palepale Tengu alipasuka pasuka kama vile ni tikiti maji.

“Tanya anza kushambulia na mimi nitakufuatia kwa nyuma yako”Aliongea Noriko Okawa ambaye bado aikuwa ameshikilia mystical Masamura huku akionekana ni mwenye wasiwasi kweli.

“Sawa baba mlezi”Aliongea Tanya.

Ukweli ni kwamba Noriko Okwa alikuwa pia akitafuta upenyo wa kuchoropoka hapo ndani na mbinu pekee ambayo aliamini ingefanyakazi ni kumfanya Tanya kupigana na Hades na yeye kutoweka.

Sasa Noriko alikuwa amempa mgongo Tanya ambaye alikuwa ameshikilia kisu kwa namna ya kijihami , wakati Roma akishangaa uhusiano wa Tanya na Noriko , jambo la kushangaza lilitokea , kwani Tanya kwa spidi kubwa sana alimsogelea baba yake mlezi kwa nyuma , bwana Noriko Okawa na kumkita na kisu mgongoni na kikatokea mbele kifuani.

Jessie , Jassoni na Bruno na mwenzek walishangazwa na tukio hilo na hawakuelewa kwanini Tanya aliamua kufanya maamuzi ya kumshambulia Noriko Okawa ilihali ni kiongozi wake.











SEHEMU YA 292

Noriko Okawa alikuwa ni kama hakuwa akiamini kama mtu aliemdhuru alikuwa ni mtoto wake wa kike aliemlea kwa miaka mingi na kumpa cheo kikubwa ndani ya kundi la Yamata Sect.

“Usishange Noriko Okawa , hii nafasi nilikuwa nikiitafuta kwa miaka mingi”Aliongea Tanya na kisha alichomoa kisu chake na kumkita kwa mara ya pili Noriko Okawa na kumfanya panga lake la Masamura kudondoka chini.

“Tanya kama umeamua kumuua baba yako mlezi ukiamini kwamba nitakuacha hai naomba ulisahau , hilo mimi sina huruma kiasi hiko”Aliongea Roma aliekuwa amesimama mita kadhaa kutoka waliposimama.

Tanya alimwangalia Noriko Okawa uku akibubujkwa na machozi na alitumia tena nguvu zake zote kunyanya kisu alichokishikiria na kumchoma nacho Okawa eneo la moyo na pale ndio ilikuwa safari ya mwisho ya Noriko kwani alimwachia na akadondoka chini.

“Mfalme Pluto nilichotaka kwenye Maisha yangu ni kulipiza kisasi kwa huyu mwanaume kwa kuniulia familia yangu , lakini pia kunibaka tokea nikiwa mtoto mpaka sasa hivi , huku akiendeleza unafiki kwa kuniita mtoto wake”Aliongea kwa hasira huku akimwangalia Noriko Okawa mfu pasipo ya kuonyesha hali ya kiujutia hata kidogo.

Roma alisogea mpaka akalifikia panga alilokuwa akitumia Norio okawa , panga la Mystical Masamura na kisha alianza kulichunguza , lilikuwa ni panga zutri sana kwake na kwa kuliangalia tu lilimkumbusha mambo mengi ya nyuma , kipindi ambacho alikuwa akitumia panga katika kufanya mauaji, kipindi hiko akifahamika kwa jina la Thirteen , kabla ya kupata cheo cha Hades.

Roma baada ya kuangalia panga hilo kwa sekunde kadhaa alimrushia Tanya aliekuwa amepiga magoti chini akitoa kilio na Tanya baada ya kuona panga lile limerushwa kwake , ni kama alielewa nini anapaswa kufanya kwani alilichukua na kisha akaliweka kwenye shingo yake akiwa tayari kujiua kwa kujichinja.

“Sijakupa maagizo ya kujiua”Aliongea Roma kwa sauti ya kawaida.

“Kama sio hivyo hili..”

“Utakufa mpaka nitakapokupa ruhusa ya kufa , kwasasa unapaswa kuwa hai kwani utakuwa wa manufaa kwangu”Aliongea Roma

Ukumbuke pia hapo ndani walikuwepo Jasie na Jasoni Pamoja na wale wawakilishi wa Innova.

Tanya baada ya kusikia Roma anasema atakuwa wa manufaa kwake , palepale alianza kuona aibu za kike , kwake alikuwa akielewa kabisa kwamba mwanaume akimwambia mwanamke ana manufaa basi anamaanisha kumpa mwili wake kutumia.

Tanya alisimama na kisha akafungua gauni lake la kininja alilovaa kutoka kwenye mabega na likadondoka chini na kumuacha uchi na kuufanya mwili wake wa kijapani kuonekana wazi, Roma akifaidi kwa mbele uku wale wengine wakifaidi kwa nyuma kwani Tanya alikuwa amewapa mgongo.

Roma alimchunguza Tanya kwanzia juu mpaka chini na macho yake yakanasa sehemu ya katikati ya mwili wa mwanamke huyo kwa madakika kadhaa , aliangalia Tatoo iliochorwa kuzunguka sehemu ya uzazi na kumfanya kushangaa kwa sekunde kadhaa.

“Unafanya nini?”Aliuliza Roma.

“Mfalme Pluto nipo tayari kwa chochote unachotaka kwenye mwili wangu”Aliongea Tanya kwa kingereza.

Roma alimwangalia Tanya kwa macho kidogo ya huruma , aliamini Tanya yuko kama hivyo kutokana na Maisha yake aliokulia , mwanamke siku zote kuwa chombo cha starehe kwa mwanaume ndio Tanya alichokuwa amezoea na ndio maana alikuwa tayari kumhudumia Roma kwa kutumia mwili wake.

“Unafikiri nitautamani mwili wako? , nimekuacha hai kwasababu moja tu , Yamta Sect ni kubwa na siwezi kuijua yote na namna inavyojiendesha , hivyo nataka unisaidie katika hilo , panga la Masamura nadhani ndio ishara ya mamlaka kwa Ninja wote wa kundi la Yamata Sect na mimi nakupa mamlaka hayo”

“Ah .. Mfalme Pluto sikujua kama ulikuwa ukimaanisha kitu kingine , nilijua unataka …”Alisita kuongea huku akiona aibu na kuvaa gauni lake la kininja

“Mfalme Pluto kama unataka Yamta Sect kuwa chini yako , wala jambo hilo sio gumu ninaweza kulikamlisha hata kwa kutokutumia hili panga, kwasababu sasa hivi Okawa amekufa na Tengu, mimi ndio mwenye nguvu katika Ninja wote ivyo lazima waheshimu kile ninachowaambia”

Roma alijikuta akishangaa , hakujua kwamba kupata kundi lote la Yamta Sect ni rahisi namna hio, ukweli ni kwamba hakutaka kumuua Tanya kwasababu moja , aliamini kama Yamata Sect ikaachwa bila ya kuwa kiongozi basi kuna uwezekano wa watu wengine kuwa kiongozi na kuanza kumsumbua tena , jambo ambalo hakuwa akitaka litokee , hivyo aliamini akiacha kiongozi ambaye atakuwa anatii maagizo yake basi atakuwa na amani na baadhi ya mambo yake mengi yatarahisishika hata akiwa kwa Tanzania tu.

“Okey basi kwasasa Yamata Sect itakuwa chini yako , na wewe utakuwa chini yangu , sitaki ufanye kila kitu kwa maagizo yangu bali mtafanya mambo yenu kama ilivyokuwa mwanzo , lakini pale ambapo nikitaka kutumia hili kundi basi sitaki mambo ya kipumbavu yajitokeze , kuhusu mtu ambaye anaweza kuwa hatarishi na kutaka kukuondoka kwenye uongizi mimi nitadili nae mwenyewe”Aliongea Roma na kisha akawageukia watu wanne walijibanza ndani ya jengo hili wakiwa hawana tumaini tena la kuishi.

Roma mwenyewe alijishangaa kwani alikuwa hana hamu ya kuua kabisa kama ilivyokuwa mwanzo , alijiuliza huenda ni kwasababu ya kuingia levo nyingine ya Kuzaliwa Upya na ndio maana ashaanza kuwa na huruma , kwani alivyowaangalia watu hao wanne , alikuwa akishikia Roho ya huruma ikimwambia awaache hai na ilionekana kuwa na nguvu mno , kitu ambacho hakijawahi kumtokea hapo kabla.

Kwa mfano Tanya alimsamehe kirahisi sana licha ya kwamba ashawahi kumchokoza yeye na wenzake kwa kumteka mke wake , lakini akaamua kumpa msahama bila hata yakufikiria makosa yake, lakini pia muda huo alikuwa akiona kwa Jessie , Jasoni na wale wawakilishi wa Innova kutaka kuwasamehe.

“Sina mudi kabisa ya kuua leo , lakini haimaanishi kwamba nimewasamehe , kila mmoja wenu ili kupata msahamaha wangu lazima aniembie maisha yake hapa duniani ni ya thamani kiasi gani, Ofcourse kama kuna mmoja wenu anahisi maisha yake hayana thamani basi sitosita kumuua”Aliongea Roma akiwaamrisha Jasoni , Jessie na Bruno na wenzake kuongea.

Walijikuta wakiangaliana kwa kutokujua namna ya kujibu , kwani mpaka wakati huo licha ya kwamba wameishi , hawakujua Maisha yao yanathamani kiasi gani na swali la Roma kwao lilionekana kama mtego.

“Uthamani wa Maisha yangu unategemeana na wale watu wanaonipenda na kunithamini , hivyo siwezi kusema kwa hakika Maisha yangu yanathamani kiasi gani”Aliongea Bruno kwa wasiwasi na kumfanye Roma tabasamu kifedhuli.

“Okey tukiachana na wale wanaokutegemea , wewe mwenyewe unajihisi unathamani kiasi gani katika kipimio cha hela?”Aliongea Roma na sasa kuwafanya wote kuelewa swali.

“Maisha yangu yana thamanii ya Dollar milioni mia moja”Aliongea Jessie na kumfanya Roma amwangalie na kuona huenda mwanamke huyo ameji ‘overate’ sana, Jasoni na yeye alijiambia kuwa ana thamani ya Dollar milioni mia tatu , wakaja wale mabwana wawili wakasema wao wanathamani ya Dollar milioni hamsinni hamsini kila mmoja na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli.

“Kwahio jumla ya thamani ya Maisha yenu wote ni dollara milioni mia tano?”Aliongea Roma na wote walitingisha vichwa na Roma alimgeukia Tanya.

“Hela zilizolipwa kwa ajili ya mwili wangu ni kiasi gari?”

“Mfalme Pluto ni Dollar milioni mia tano na kumi”Aliongea Tanya na Roma alitngisha kichwa.

“Okey nitawaacha muendelee kuishi na kwakua malipo mshayatanguliza basi nitakata Dollar milioni mia tano kama malipo ya thamani ya uhai wenu na Dollar milioni kumi iliobaki nitajilipa kama sehemu ya usumbufu”Aliongea Roma na sasa kuwafanya Jassie na wenzake kuelewa alichokuwa akimaanisha Roma , kumbe alikuwa akitafuta uhalali wa kumiliki pesa ambazo zilikuwa zimeskwisha kulipwa kwa ajili ya mwili wake, lakini hakuna hata mmoja alietaka kuleta kipingamizi , wote kwa Pamoja walishukuru kutoka hai.

Roma alimpa malekezo Tanya ya kutuma hela zote ambazo zimelipwa kwa ajili ya mwili wake Kwenda kwenye akaunti yake ya Swiss na Tanya kwa haraka haraka alituma hela hizo kutoka katika Wallet ya Bitcoin Kwenda Swiss Bank.

“Mfalme Pluto kuna hizi pesa taslimu zilizobaki”Aliongea Tanya huku akimuonyesha Roma maburungutu ya pesa yaliokuwa kwenye Briefcase na alifikiria kidogo na kuona sio mbaya kama hela hizo ataziingiza kwenye akaunti yake ya kawaida.

Roma alimpa Tanya namba ya akaunti ya kawaida anayotumia akiwa Tanzania na kumpa maagizo ya kuziingiza pesa hizo kwake.

“Nadhani unajua cha kufanya juu ya kundi la Yamata Sect na taratibu zingine za kuongoza?”

“Ndio Mfalme Pluto ninalijua kundi hili nje ndani hivyo sio ngumu kiliongoza”Aliongea na Roma alitingisha kichwa na kuamini Tanya ni mtu sahihi kumuachia aongoze kundi hili la Yamata Sect ambalo mpaka muda huo ni kama la kwake.

Roma alibadili nguo zote alizokuwa amevaa kwani zilikuwa zimechafuka na Damu na sasa akili yake ilianza kurudi kwenye jambo ambalo limemleta Japani , swala la kumuokoa mrembo Amina.

Lakini bado mwili wake ni kama haukuwa sawa , sumu ambayo ilikuwa imeingizwa kwenye mwili wake bado haikuwa imeisha kabisa na kumsababishia kuhisi kizunguzungu, aliamini kama sumu hio itaendeea kuwa ndani ya mwili wake inaweza kumletea shida , hivyo aliamini kuna ulazima wa kuitafutia dawa yake , wakati akiendelea kuwaza aliamini mtu pekee ambaye anaweza kumsaidia kutoa sumu hio kwenye mwili wake ni Profesa Clark, Roma alijaribu kutoa simu yake kumpigia Profesa Clark na bahati nzuri iliita kwa dakika kama moja hivi mpaka kupokelewa.

Mwanzoni sauti ya mrembo Profesa Clark ilionekana kuwa katika furaha mara baaada ya kujua Hades ndio kampigia , lakini sekunde chache mbele sauti ya mwanamke huyo ilijawa na wasiwasi mara baada ya Roma kumwambia kwamba amewekewa sumu kwenye mwili wake na bado hajisikii vizuri na anataka ajaribu kumwangalia,

“Hades nipo Hongkong nilikuwa na semina ya siku tatu na tumemaliza leo , nitafanya safari ya dharula, niambie ni wapi tunapaswa kuonana niweze kuangalia hali ya afya yako”Aliongea Profesa Clark kwa wasiwasi mkubwa

“Tukutane Hokkaido Sapporo City”Aliongea Roma na Profesa Clark alionekana kuelewa na hapo hapo Roma alikata simu na kumwangalia Tanya aliekuwa pembeni yake akisikiliza mazungumzo yao.

“Your Majest Pluto ,do you need me to employ our private jet?”Aliulia Tanya na hio ni mara baada ya kusikia mazungumzo ya Roma Kwenda Sapporo City hivyo alijiongeza haraka haraka na kutoa pendekezo ambalo kidogo lilimshangaza Roma.

“What private jet?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“We have exclusive jets in every airport in Japan , its not publicly known since its secret, all of them are at your service anytime”

“Tunazo ndege binafsi kwa kila uwanja wa ndege hapa Japani ambazo hazifahamiki kwani ni za sirisa na ndege zote hizo zipo kwa ajili ya kukuhudumia”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa , hakuwa na taarifa kwamba Yamata Sect ilikuwa na pesa kiasi gani.

“Hili kundi la Yamata Sect lina thamani ya kiasi gani in total Asset?”aliuliza Roma , alitaka kujua ni thamani kiasi gani kwa kundi lote.

Kwa maelezo ya Tanya thamani yote ya kundi la Yamata Sect ni dollar za kimarekani bilioni sita kuanzia pesa iliokuwa ndani ya benki , lakini pia baadhi ya vitu biashara ambazo zipo chini ya Yamata Sect.

Roma alitabasamu baada ya kugundua kumbe kundi hilo lina thamani kubwa kiasi hiko , alijiambia safari yake ya kuja Japani haikuwa ya kupoteza muda kwani mpaka hapo alikuwa ametengeneza kiasi kikubwa sana cha pesa ndani ya siku mbili takribani Dollar bilioni saba.
 
SEHEMU YA 293

Ni ndani ya masaa machache tu kwa kutumia gari ambayo ilikuwa ikiendeshwa na Tanya , waliweza kufika ndani ya jiji la Osaka , katika uwanja wa ndege wa Kansai.

Watu wengi walikuwa wakimwangalia Roma alietangulizana na mrembo Tanya kwa macho yasiokuwa ya kawaida , lakini Roma wala hakujali na hivyohivyo kwa Tanya hakuonyesha hali ya kujali macho ya wajapani wenzake , alichokifanya ni kumuongoza Roma mpaka upande wa VIP kwa ajili ya kupita bila ukaguzi , kwani alikuwa akitumia ndege binafsi.

Dakika chache mbele walikuwa kwenye gereji ndani ya uwanja huu wa ndege na Roma aliweza kushuhudia ndege ndogo aina ya Airbus , ilikuwa ni ndege ambayo licha ya kuonekana kuwa ndogo , lakini Roma aliamini Gharama yake itakuwa ni kubwa sana kuinunua kwani kama utaifananisha na ndege ya kawaida basi italingana na ndege za shirika la Precision air kwahapa Tanzania.

Sasa Roma kwa kuona ukubwa na ufahari wa ndege hii aliamini moja kwa moja maneno ya Tanya juu ya thamani halisi na ukubwa wa kundi la Yamata, aliamini kama kweli kila kiwanja ndani ya Japani kuna ndege ya ukubwa huo basi Yamata ni kundi kubwa sana kushinda hata la Takamagahara.

Roma aliingia ndani ya Cabin katika ndege hio na kujikuta akitabasamu baada ya kuona samani za bei ya juu , ndege hio kwa ndani ilionekana kupambwa kwa namna ya kipekee sana , masofa yaliotengenezwa kwa Ngozi ya kondoo wa sufu kutoka Japani , lakini pia thamani zilizotengenezwa na Mahogany lakini pia chupa za bia ambazo zilikuwa ndani ya jokofu zilimfanya Roma kujihisi ni kama yupo hotelini na sio kwenye ndege.

Roma baada ya kukaaa na kupumua kwa ahueni alijikuta akijishangaa kwanini Maisha yake nchini Tanzania ni ya kawaida sana , kwani alikuwa na pesa nyingi sana benki pesa ambazo kama ataamua kutumi pasipo kufanya kazi basi anaweza kuishi miaka mia pasipo ya hela yote kuisha , alijiambia kuna ulazima akirudi Tanzania kufikiria namna ya kuishi kutokana na thamani ya utajiri wake.

Tanya alikuwa ashabadili mavazi yake na sasa alikuwa amevalia mavazi ya kitamaduni ya kijapani mara baada ya kuingia kwenye ndege hio huku akiwa ameshikilia sahani , alionekana yeye ndio anakwenda kuwa mhudumu akimsindikiza Roma mpaka Hokkaido.

Roma alimwangalia Tanya kwa jinsi alivyovaa na kuamini mwanamke huyo alikuwa akitafuta namna ya kuziamsha hisia zake , kwani vazi lake licha ya kwamba lilionekana kuwa la kitamaduni , lakini eneo la kifua chake lilikuwa wazi na kufanya manyonyo yake kuonekana.

“Mfalme hii wine ni kwa ajili yako , imetengenezwa na mchele kutoka Hokkaido , lakini pia na maji maalumu kutoka Nishinomiya na mbinu yetu maalaumu ambayo sisi Yamata huitumia”Aliongea Tanya huku akiminina wine kwenye glass na kumfanya Roma kumeza mate kwani harufu tu ilimfanya kuamini Wine hio itakuwa tamu.

Tanya mara baada ya kuminima kwa mapozi ile wine , Roma aliichukua Glass na kisha akagida wine yote kwa mkupuo mmoja na ile anarudisha glass chini alijikuta macho yake yakiongezeka ukubwa , kwani Tanya alievalia Kimono , alikuwa amefungua mkanda kulifunga gauni lake na kumfanya kumuacha wazi , na Roma aligundua mrembo huyo ndani yake hakuvalia nguo yoyote Zaidi ya vazi hilo la kitamaduni, Roma alielewa mtego wa Tanya , lakinii hakuw akwenye mudi ya kufanya chochote.

“Unaweza Kwenda kufanya mambo yako , sitaki ujitoe sana kwangu”Aliongea Roma na kumfanya Tanya kuonyesha hali ya kutofurahishwa na jibu la Roma , ni kama alitegemea kufanywa na Roma na jibu lake lilimnyong`onyesha.

*********

Profesa Clark aliekuwa ndani ya jiji la Hongkong kwa ajili ya semina maalumu ndani ya chuo kikuu cha Hongkong , mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Hades na kujua hali yake, alionekana kuwa na wasiwasi mno.

Mrembo huyo hakuwa na muda wa kupoteza kabisa, kwani ndani ya madakika kadhaa tu alikuwa kwenye ndege ya kukodi akielekea Hokkaido Japani , yaani wakati Roma anapanda ndege Kwenda Sapporo , upande wa Clark alikuwa na masaa mawili angani tokea aanze safari.

Upande wa Roma hakuwa na wasiwasi sana juu ya ndoa ya Mrembo amina , kutokana na taarifa za Makedoni alivyomwambia ni kwamba ndoa yake ilikuwa ikitarajiwa kufungwa siku mbili mbele yaani tarehe 26 ndani ya jiji la Otaru Ishikari Bay , hivyo mpango wake wa kwanza ni Kwenda kwanza Sapporo kuonana na Profesa Clark na baada ya hapo ndio aende Otaru.

Masaa mawili ya kuwa angani hatimae Roma aliweza kufanikiwa kufika ndani ya ya jiji la Sapporo.

Profesa Clark aliekuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau alionekana akiwa ameegamia gari aina ya Nissani nyeupe yenye namba za usajli 370Z , ilionekana mrembo huyo alikuwa amefika hapo uwanja wa ndege muda mrefu kidogo.

Watu mbalimbali waliokuwa ndani ya eneo hilo walikuwa wakimwangalia kwa macho ya kumsanifu kutokana na urembo wake, lakini sio hivyo tu baadhi ya watu waliweza kumtambua kama mtoto wa malkia kutoka Wales na hio ilifanya kuzidi kushangaa na kujiuliza yupo hapo uwanja wa ndege kumsubiria nani.

Profesa Clark alijikuta akibetua mdomo mara baada ya kumshuhudia Roma akitoka kwenye mlango wa wanaowasili akiwa ametangulizana na mwanamke wa kijapani ambaye alionekana kuwa mrembo kwenye macho yake , katika akili yake aliamini huenda huyo mwanamke ni hawala wa Roma.

“Is she your new lover again?”Aliuliza Clark pasipo hata ya salamu , alionekana kuwa na wivu , lakini pia alikuwa akifahamu Roma alikuwa na wanawake wengi hivyo aliuliza namna hio kwa kudhania ni ongezeko lingine.

“Do I look like someone so casual?”Aliongea Roma akimaanisha kwamba je anaonekana kama mtu muhuni muhuni

“You don’t look like one , you are one”Aliongea Clark akimwambia kwamba sio kwamba anaonekana kama muhumi , bali ni kweli yeye ni muhui , Roma alitabasmau huku akishika pua yake.

“Unaonaje tukiingia kwenye gari kwanza ndio unifokee, Tanya wewe tafuta vijana wako, nitaondoka na huyu mwanamke”Aliongea Roma na Tanya aliinamisha kichwa kuonyesha heshima mpaka pale gari ilivyoondolewa.

“Huyo mrembo ni kiongozi mpya wa kundi la Yamata , anafahamika kwa jina la Tanya”Aliongea Roma na kumfanya Clark kushangaa kidogo.

“Ninachofahamu ni kwamba kiongozi wa kundi la Yamata Sect ni Noriko Okawa… Roma usiniambie umemuua?”Aliongea kwa mshangao

“Ndio amekufa , lakini siwezi kusema mimi ndio nimemuua , ni maelezo ambayo nitakuelezea baadae”Aliongea Roma na Clark alitingisha kichwa huku macho yake yakiwa barabarani.

“Ilikuwaje mpaka ukawekewa sumu? , sijawahi kudhania kama kuna mtu anaweza akafanikiwa kukuwekea sumu?”

“It can’t be explained in short time”AliongeaRoma huku akijiegamiza kwenye kiti , ukweli ni kwamba alikuwa akijisikia vibaya bado na alihisi kama mwili wake ulikuwa kidonda chenye usaha, ijapokuwa aliweza kutumia mbinu ya kijini kushindana na nguvu ya sumu , lakini hapo haikumaanisha kwamba amepona , kwake lilikuwa swala la muda tu sumu hio isipoondolewa kumletea shida.

“I asked one of my student to empty out bioengineering research institute before I came here , we can go over there to conduct a comprehensive inspections”Aliongea akimaanisha kwamba amemuomba moja ya wanafunzi wake kuondoa watu waliokuwa ndani ya taasisi ya kibiolojia ili aweze kumfanyia Roma majaribio kufahamu afya yake ilivyo kwa kina.

“Una wanafunzi kila kona ya dunia”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Ni kweli , ijapokuwa sikutaka kuchukua baadhi yao , lakini wamekuwa ving’ang’anizi na kujikuta sina jinsi ya kuwasapoti “Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu.

“Kila mara tunapo onana nakuona kama umebadilika , miaka kumi na moja nyuma wakati nakuokoa wewe na Cahethirne sikuamini mtoto kama wewe utakuja kuwa msaada mkubwa kwangu”Aliongea Roma

“Mimi sio mtoto , mtu yoyote akituona atasema tunalingana tu”Aliongea akionyesha hakupenda kuitwa mtoto.

Gari ilikuja kusimama upande wa magharibi wa jiji la Sapporo pembeni kidogo ya eneo lenye kijimsitu na mlima na kwa maelezo ya Clark sehemu hio ndio kwenye taasisi hio ya kufanyia majaribio.

Dakika chache mbele Clark na Roma waliingia ndani ya jengo hilo la gorofa kama tano Kwenda juu la kisasa kabisa, lilikuwa na jengo ambalo lina vifaa vyenye teknolojia ya hali ya juu , nadhani ndio maana Clark akachagua sehemu hio kwa ajili nya kumfanyia Roma majaribio mwili wake.

Profesa Clark baada ya kumuongoza Roma mpaka kwenye maabara , alichukua sindano na kisha alitoa damu yake kiasi na kisha akamwambia Roma asubiri nje mpaka atakapomaliza ndani ya lisaa limoja na Roma kwakua alikuewa akielewa moja ya tabia za wanasayansi kutotaka kusimamiwa wakati wa kufanya kazi zao , aliamua kutoka kupandisha mpaka juu kabisa ya jengo hilo kwa ajili ya kupigwa na upepo.

Lucha ya kwamba kulikuwa na baridi lakini kwake haikumsumbua kama watu wa kawaida na hio ni kutokana na namna ya mwili wake ulivyo.

Masaa machache mbele hatimae Profesa Clark alipandisha mpaka juu ya ghorafa hilo kwa ajili ya kumpatia Roma majibu yake.

“Judging from your look the situation is more serious than I imagined”Aliongea Roma na hio ni mara baada ya kuona wasiwasi uliokuwa kwenye macho ya Profesa Clark na alijiambia lazima kuna tatizo kubwa , lakini alijikuta akishangaa Zaidi baada ya Clark kuanza kulia kwa kwikwi kama mtu aliefiwa.

ITAENDELEA WEEKEND

IMEDHAMINIWA NA WAFUATILIAJI KUTOKA GRUPU LA WATSAPP :0687151346
 
SEHEMU YA 293

Ni ndani ya masaa machache tu kwa kutumia gari ambayo ilikuwa ikiendeshwa na Tanya , waliweza kufika ndani ya jiji la Osaka , katika uwanja wa ndege wa Kansai...
Ah bro SinganoJR yan apa nimejikuta nikiisoma hii riway since Ijumaa wiki iliopita nilipokuja kuiona. Sikutegemea kabisa nitanogewa maana imekaa kiunyama sana.

Mimi nikiwa kama mpenz wa kusoma riwaya za kiingereza na kiswahili nimejifunza vitu vingi umu. Apa nasubiri tu iyo mda iinge next chapter
 
Ahsante mkubwa! Na mteja wa choroko amepatikana! Baada ya wikiend tu nakuja wasapu
 
SEHEMU YA 293

Ni ndani ya masaa machache tu kwa kutumia gari ambayo ilikuwa ikiendeshwa na Tanya , waliweza kufika ndani ya jiji la Osaka , katika uwanja wa ndege wa Kansai.

Watu wengi walikuwa wakimwangalia Roma alietangulizana na mrembo Tanya kwa macho yasiokuwa ya kawaida , lakini Roma wala hakujali na hivyohivyo kwa Tanya hakuonyesha hali ya kujali macho ya wajapani wenzake , alichokifanya ni kumuongoza Roma mpaka upande wa VIP kwa ajili ya kupita bila ukaguzi , kwani alikuwa akitumia ndege binafsi.

Dakika chache mbele walikuwa kwenye gereji ndani ya uwanja huu wa ndege na Roma aliweza kushuhudia ndege ndogo aina ya Airbus , ilikuwa ni ndege ambayo licha ya kuonekana kuwa ndogo , lakini Roma aliamini Gharama yake itakuwa ni kubwa sana kuinunua kwani kama utaifananisha na ndege ya kawaida basi italingana na ndege za shirika la Precision air kwahapa Tanzania.

Sasa Roma kwa kuona ukubwa na ufahari wa ndege hii aliamini moja kwa moja maneno ya Tanya juu ya thamani halisi na ukubwa wa kundi la Yamata, aliamini kama kweli kila kiwanja ndani ya Japani kuna ndege ya ukubwa huo basi Yamata ni kundi kubwa sana kushinda hata la Takamagahara.

Roma aliingia ndani ya Cabin katika ndege hio na kujikuta akitabasamu baada ya kuona samani za bei ya juu , ndege hio kwa ndani ilionekana kupambwa kwa namna ya kipekee sana , masofa yaliotengenezwa kwa Ngozi ya kondoo wa sufu kutoka Japani , lakini pia thamani zilizotengenezwa na Mahogany lakini pia chupa za bia ambazo zilikuwa ndani ya jokofu zilimfanya Roma kujihisi ni kama yupo hotelini na sio kwenye ndege.

Roma baada ya kukaaa na kupumua kwa ahueni alijikuta akijishangaa kwanini Maisha yake nchini Tanzania ni ya kawaida sana , kwani alikuwa na pesa nyingi sana benki pesa ambazo kama ataamua kutumi pasipo kufanya kazi basi anaweza kuishi miaka mia pasipo ya hela yote kuisha , alijiambia kuna ulazima akirudi Tanzania kufikiria namna ya kuishi kutokana na thamani ya utajiri wake.

Tanya alikuwa ashabadili mavazi yake na sasa alikuwa amevalia mavazi ya kitamaduni ya kijapani mara baada ya kuingia kwenye ndege hio huku akiwa ameshikilia sahani , alionekana yeye ndio anakwenda kuwa mhudumu akimsindikiza Roma mpaka Hokkaido.

Roma alimwangalia Tanya kwa jinsi alivyovaa na kuamini mwanamke huyo alikuwa akitafuta namna ya kuziamsha hisia zake , kwani vazi lake licha ya kwamba lilionekana kuwa la kitamaduni , lakini eneo la kifua chake lilikuwa wazi na kufanya manyonyo yake kuonekana.

“Mfalme hii wine ni kwa ajili yako , imetengenezwa na mchele kutoka Hokkaido , lakini pia na maji maalumu kutoka Nishinomiya na mbinu yetu maalaumu ambayo sisi Yamata huitumia”Aliongea Tanya huku akiminina wine kwenye glass na kumfanya Roma kumeza mate kwani harufu tu ilimfanya kuamini Wine hio itakuwa tamu.

Tanya mara baada ya kuminima kwa mapozi ile wine , Roma aliichukua Glass na kisha akagida wine yote kwa mkupuo mmoja na ile anarudisha glass chini alijikuta macho yake yakiongezeka ukubwa , kwani Tanya alievalia Kimono , alikuwa amefungua mkanda kulifunga gauni lake na kumfanya kumuacha wazi , na Roma aligundua mrembo huyo ndani yake hakuvalia nguo yoyote Zaidi ya vazi hilo la kitamaduni, Roma alielewa mtego wa Tanya , lakinii hakuw akwenye mudi ya kufanya chochote.

“Unaweza Kwenda kufanya mambo yako , sitaki ujitoe sana kwangu”Aliongea Roma na kumfanya Tanya kuonyesha hali ya kutofurahishwa na jibu la Roma , ni kama alitegemea kufanywa na Roma na jibu lake lilimnyong`onyesha.

*********

Profesa Clark aliekuwa ndani ya jiji la Hongkong kwa ajili ya semina maalumu ndani ya chuo kikuu cha Hongkong , mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Hades na kujua hali yake, alionekana kuwa na wasiwasi mno.

Mrembo huyo hakuwa na muda wa kupoteza kabisa, kwani ndani ya madakika kadhaa tu alikuwa kwenye ndege ya kukodi akielekea Hokkaido Japani , yaani wakati Roma anapanda ndege Kwenda Sapporo , upande wa Clark alikuwa na masaa mawili angani tokea aanze safari.

Upande wa Roma hakuwa na wasiwasi sana juu ya ndoa ya Mrembo amina , kutokana na taarifa za Makedoni alivyomwambia ni kwamba ndoa yake ilikuwa ikitarajiwa kufungwa siku mbili mbele yaani tarehe 26 ndani ya jiji la Otaru Ishikari Bay , hivyo mpango wake wa kwanza ni Kwenda kwanza Sapporo kuonana na Profesa Clark na baada ya hapo ndio aende Otaru.

Masaa mawili ya kuwa angani hatimae Roma aliweza kufanikiwa kufika ndani ya ya jiji la Sapporo.

Profesa Clark aliekuwa amevalia suti ya rangi ya zambarau alionekana akiwa ameegamia gari aina ya Nissani nyeupe yenye namba za usajli 370Z , ilionekana mrembo huyo alikuwa amefika hapo uwanja wa ndege muda mrefu kidogo.

Watu mbalimbali waliokuwa ndani ya eneo hilo walikuwa wakimwangalia kwa macho ya kumsanifu kutokana na urembo wake, lakini sio hivyo tu baadhi ya watu waliweza kumtambua kama mtoto wa malkia kutoka Wales na hio ilifanya kuzidi kushangaa na kujiuliza yupo hapo uwanja wa ndege kumsubiria nani.

Profesa Clark alijikuta akibetua mdomo mara baada ya kumshuhudia Roma akitoka kwenye mlango wa wanaowasili akiwa ametangulizana na mwanamke wa kijapani ambaye alionekana kuwa mrembo kwenye macho yake , katika akili yake aliamini huenda huyo mwanamke ni hawala wa Roma.

“Is she your new lover again?”Aliuliza Clark pasipo hata ya salamu , alionekana kuwa na wivu , lakini pia alikuwa akifahamu Roma alikuwa na wanawake wengi hivyo aliuliza namna hio kwa kudhania ni ongezeko lingine.

“Do I look like someone so casual?”Aliongea Roma akimaanisha kwamba je anaonekana kama mtu muhuni muhuni

“You don’t look like one , you are one”Aliongea Clark akimwambia kwamba sio kwamba anaonekana kama muhumi , bali ni kweli yeye ni muhui , Roma alitabasmau huku akishika pua yake.

“Unaonaje tukiingia kwenye gari kwanza ndio unifokee, Tanya wewe tafuta vijana wako, nitaondoka na huyu mwanamke”Aliongea Roma na Tanya aliinamisha kichwa kuonyesha heshima mpaka pale gari ilivyoondolewa.

“Huyo mrembo ni kiongozi mpya wa kundi la Yamata , anafahamika kwa jina la Tanya”Aliongea Roma na kumfanya Clark kushangaa kidogo.

“Ninachofahamu ni kwamba kiongozi wa kundi la Yamata Sect ni Noriko Okawa… Roma usiniambie umemuua?”Aliongea kwa mshangao

“Ndio amekufa , lakini siwezi kusema mimi ndio nimemuua , ni maelezo ambayo nitakuelezea baadae”Aliongea Roma na Clark alitingisha kichwa huku macho yake yakiwa barabarani.

“Ilikuwaje mpaka ukawekewa sumu? , sijawahi kudhania kama kuna mtu anaweza akafanikiwa kukuwekea sumu?”

“It can’t be explained in short time”AliongeaRoma huku akijiegamiza kwenye kiti , ukweli ni kwamba alikuwa akijisikia vibaya bado na alihisi kama mwili wake ulikuwa kidonda chenye usaha, ijapokuwa aliweza kutumia mbinu ya kijini kushindana na nguvu ya sumu , lakini hapo haikumaanisha kwamba amepona , kwake lilikuwa swala la muda tu sumu hio isipoondolewa kumletea shida.

“I asked one of my student to empty out bioengineering research institute before I came here , we can go over there to conduct a comprehensive inspections”Aliongea akimaanisha kwamba amemuomba moja ya wanafunzi wake kuondoa watu waliokuwa ndani ya taasisi ya kibiolojia ili aweze kumfanyia Roma majaribio kufahamu afya yake ilivyo kwa kina.

“Una wanafunzi kila kona ya dunia”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Ni kweli , ijapokuwa sikutaka kuchukua baadhi yao , lakini wamekuwa ving’ang’anizi na kujikuta sina jinsi ya kuwasapoti “Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu.

“Kila mara tunapo onana nakuona kama umebadilika , miaka kumi na moja nyuma wakati nakuokoa wewe na Cahethirne sikuamini mtoto kama wewe utakuja kuwa msaada mkubwa kwangu”Aliongea Roma

“Mimi sio mtoto , mtu yoyote akituona atasema tunalingana tu”Aliongea akionyesha hakupenda kuitwa mtoto.

Gari ilikuja kusimama upande wa magharibi wa jiji la Sapporo pembeni kidogo ya eneo lenye kijimsitu na mlima na kwa maelezo ya Clark sehemu hio ndio kwenye taasisi hio ya kufanyia majaribio.

Dakika chache mbele Clark na Roma waliingia ndani ya jengo hilo la gorofa kama tano Kwenda juu la kisasa kabisa, lilikuwa na jengo ambalo lina vifaa vyenye teknolojia ya hali ya juu , nadhani ndio maana Clark akachagua sehemu hio kwa ajili nya kumfanyia Roma majaribio mwili wake.

Profesa Clark baada ya kumuongoza Roma mpaka kwenye maabara , alichukua sindano na kisha alitoa damu yake kiasi na kisha akamwambia Roma asubiri nje mpaka atakapomaliza ndani ya lisaa limoja na Roma kwakua alikuewa akielewa moja ya tabia za wanasayansi kutotaka kusimamiwa wakati wa kufanya kazi zao , aliamua kutoka kupandisha mpaka juu kabisa ya jengo hilo kwa ajili ya kupigwa na upepo.

Lucha ya kwamba kulikuwa na baridi lakini kwake haikumsumbua kama watu wa kawaida na hio ni kutokana na namna ya mwili wake ulivyo.

Masaa machache mbele hatimae Profesa Clark alipandisha mpaka juu ya ghorafa hilo kwa ajili ya kumpatia Roma majibu yake.

“Judging from your look the situation is more serious than I imagined”Aliongea Roma na hio ni mara baada ya kuona wasiwasi uliokuwa kwenye macho ya Profesa Clark na alijiambia lazima kuna tatizo kubwa , lakini alijikuta akishangaa Zaidi baada ya Clark kuanza kulia kwa kwikwi kama mtu aliefiwa.

ITAENDELEA WEEKEND

IMEDHAMINIWA NA WAFUATILIAJI KUTOKA GRUPU LA WATSAPP :0687151346
Asante sana
 
Back
Top Bottom