singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #221
SEHEMU YA 36
RWANDA -KIGALI 2014
Ni ndani ya hoteli kubwa iliokuwa ndani ya jiji hili la Kigali , hoteli iliokuwa ikifahamika kwa jina la The Aquad alionekana mwanamke na mwanaume wakiwa ndani ya chumba kikubwa cha hoteli hii , katika floor ambayo ilikuwa ikihudumia VIP , huku nje ya Floor hii wakiwa walinzi wengi waliokuwa wamevalia suti.
Ndani ya chumba hiki mwanaume alionekana akiwa amepiga magoti chini , huku mwanamke mmmoja mrembo wa mweupe wa kabila la wanawake wa Babati yaani Wairaq akiwa amesimama huku akiwa na machozi mengi usoni , alionekana kulia mfululizo huku akiwa ameshikilia moyo wake.
“Nisamehe sana Raheli, naomba unisamehe mpenzi ,,, sikudhania haya yote yatatokea”
“Jeremy acha kuomba msamaha wako wa kipuuzi mbele yangu , unazidi kuniumiza , kwanini ulinificha muda wote kama Lorraine alikufa , kwanini Jeremy haukuniambia hii.. hiii…kwanini Jeremiiii…..”Mwanamke alionekana kulia kilio ambacho hakikiwa cha kawaida huku akimshutmu Jeremiii.
“Sikuwa na jinsi Rahel , sikutaka upitie maumivu niliopitia mimi”.
“Hata kama Jeremy , Lorraine ni mwanangu nilipaswa kujua haya yote ,hivi unajua ni siku ngapi nilitumia kuchukua maamuzi ya kukukabidhi Lorraine na kubaki na Edna eeh , unajua ni uchungu gani niliopitia kuwa mbali na mwanangu , hayo yote nilifanya kwasababu nakupenda Jeremy .. lakini kwanini ulishindwa kumlinda…..”Kilio kilikuwa ni cha aina yake kwa mwanamama huyu alionekana kumlaumu Jeremy kwa yale ambayo yamemtokea Lorraine , lakini pia anamlalamikia Jremy kwa kutompa taarifa ya kifo cha mwanae ,
“Rahel naomba unisamehe , najua ni maumivu gani unapitia baada ya taarifa hii , najua ulitarajia kumuona Lorraine akiwa na furaha ndani ya mikono yangu , lakini mimi pia kama baba yeke nilikuwa nikimpenda sana Lorraine na nilipanga kumpa Maisha mazuri , lakini haya makafir.. ya Dunia yamenichukulia mwanangu”.
“Unamaanisha nini Jeremy?”Aliuliza mwanamama huyu huku akisimama , hakumuelewa Jeremy baada ya kusema makafir alitaka kujua anamaanisha nini, Na kwa Jeremy alijikuta akijilaumu kwa kuropoka.
“Unamaanisha nini Jeremy ukisema Makafir ndio waliomchukua Lorraine?”
“Sijamaanisna hivyo Lorraine.. ni …”Kabla hajamaliza kuongea alikuwa ashashikwa tai na Raheli , mwanamama huyu alionekana kuzingatia kila neno mtu analoongea na ndio maana aliweza kumsikia vyema Jeremy alipo sema Makafir .
“Rahel namaanisha ,,”
“Usipo nipa maelezo ya kutosha leo Jeremy nakwambia hapa hutoki …”Jeremy alikuwa akimjua sana Rahel akiamua lake jambo lazima litimie , lakini hakutaka kumwambia Rahel juu ya kile anachokijua na anachoendela kukitafutia ukweli wake.
Jeremy aliamini kwa asilimia mia moja Ndege ile haikuanguka , bali kuna mpango wa siri ambao ulikuwa ukiratibiwa na mataifa yenye nguvu duniani , mpango ambao ulihusisha ndege hio kupotea, aliogopa kumwambia Rahel ukweli.
“Jeremy umenificha kwa miaka kumi na sita juu ya kifo cha mtoto wangu .. ukinificha jambo lolote na nikagundua jua sitokuja kukusamehe mpaka naingia kaburini”Aliongea mwanamama huyu huku akionesha hasira zake waziwazi.
Jeremy hakuwa na jinsi aliona Rahel anapaswa kuujua ukweli ule ambaye yeye alikuwa akiufahamu , aliona haina maana ya kumficha.
“Rahel tokea siku ambayo ndege ile ilipotea moyo wangu haukuwa na Amani kabisa , niliona kabisa kuna jambo ambalo halikuwa sawa , sikuwa na amani nilikuwa nikiota kila siku Lorraine yupo hai lakini sehemu aliokuwepo anateseka..”Alitulia kwanza na kufuta machozi na kisha akasimama huku akiwa anaangalia dirisha kama mtu aliekuwa akitafuta kitu.
“Kupotea kwa ndege ya shirika la M ilikuwa ni mpango wa wazungu”Rahel ni kama hakuwa amemsikia vizuri , kwani alinyanyuka na kwenda mpaka mbele ya Mheshimiwa Jeremy na kumwangalia vizuri usoni.
“Nieleze vizuri nielewe Jeremy .. mpango wa Wazungu ,, unanichanganya hebu eleza nielewe”
“Siwezi kukueleza mengi Rahel lakini naamini Lorraine yupo hai .. hakuna ushahidi wowote wa ile ndege kuanguka Rahel , yote ni mipango na mahesanu ya wazungu juu ya mpango ambao mpaka sasa hatuujui , mpango ambao umeratibiwa na mataifa makubwa yenye nguvu.. hii ni siri kubwa Rahel na sitaki kukuambia Zaidi ila naomba uelewe nitahakikisha naujua ukweli wote , nitatumia nguvu zangu zote kuhakikisha naupata ukweli wote na kama Lorraine yupo hai nitamrudisha “.
Taarifa hio ilionekana kuwa nzito sana kwa mwanamama Rahel , alikuwa akimjua Jeremy kwa muda mrefu tokea walivyokutana miaka kadhaa nyuma na kuanzisha mahusiano yao , alikuwa akimjua kuwa hawezi kuongea jambo ambalo hana uhakika nalo , alijikuta nguvu zikimuishia na kurudi kukaa kwenye sofa huku machozi yakiendelea kumbubujika.
Ukweli ni kwamba mwanamama huyu sababu ambayo ilimfanya asigundue kuwa Lorraine amekufa ni kutokana na kwamba Jeremy alitumia Mchezo wa kumuigizia kuwa anamchukia , kipindi chote ambacho Rahel alijaribu kuwasiliana na Jeremy , mheshimiwa huyo alionyesha kumchukia sana Rahel na hakutaka mazungumzo, na hata pale ambapo aliomba kuonana na Lorraine mheshimiwa alimtishia Rahel kukaa mbali na Lorraine la sivyo ataongea ukweli wote na dunia ijue kuwa Edna ni mwanae.
Kwa upande wa Rahel hakuwa tayari kwa watu kujua kuwa Edna sio mtoto wa Adebayo kwani kulikuwa kuna mkataba wa siri ambao alisaini na familia ya Adebayo , mkataba ambao Raheli alisainishwa na mama yake Adebayo.
“Jeremy una uhakika ndege ile haikudondoka na yote uliosema juu ya mpango ya wazungu ni kweli?”Aliuliza kwa sauti ndogo iliokuwa dhaifu na Jeremy alimuonea huruma sana Rahel , alijua ni afadhali kwake maumivu ya kumpoteza Lorraine yamezoeleka kwani tukio lilikuwa ni la muda mrefu tarkribani Zaidi ya miaka kumi na sita , alimsogelea Rahel na kisha akamkumbatia na walianza kuambizana kulia.
Kwa namna ambavyo Jeremy alikuwa akillia usingedhania ni kiongozi mkubwa wa taifa , kiongozi ambaye wananchi wa Rwanda wanamtegemea sana kuwafikisha katika nchi ya Ahadi.
“Ni kweli Rahel nina amini kwa asilimia kubwa Lorraine yupo hai na ninaompango wa kuhakikisha namrudisha”.
Rahel alifuta machozi na kisha alijitoa kwenye mikono ya Jeremy na akaweka sura ya usiriasi .
“Jeremy kama haya unayoyasema ni ya kweli hakikisha unaujua ukweli la sivyo sitokusamehe kwa kumpoteza mwanangu Lorraine”Aliongea mwanamama huyu na akafuta machozi na kuchukua mkoba wake na kutoka ndani ya chumba hiko.
****
Ilikuwa ni muda wa saa sita kamili za mchana alionekana Roma akiingiaa maeneo ya Club B , alikuwa na muda mrefu hajaingia ndani ya hii club , kwani tokea apate mke mara nyingi alikuwa akienda moja kwa moja nyumbani kwa Rose , lakini leo alikuwa amewahi sana kuja haya maeneo na alijua kabisa Rose hakuwa kwake na atakuwa ofisini na mawazo yake yalikuwa sahihi kwani alimkuta mwanada huyo akiwa kazini kama ilivyokuwa kawaida yake na kwa Rose alishangaa ujio wa Roma muda huo wa mchana.
“Hubby karibu” Aliiongea Rose huku akitoka kwenye meza na kuja kukaa kwenye masofa , huku akimwangalia Roma kwa kumsanifu , aliwaza Roma kaja muda huo kwasababu gani.
“Bebi Rose nimekuja leo nina shida”Aliongea Roma mara baada ya kuketi.
“Shida gani mpenzi , ongea tu nipo tayari kukusaidia”
“Unamiliki nyumba ngapi?”
“Bebi kwanini unauliza hivyo nina nyumba nne mbili hapa Dar na nyingine zipo nje kidogo ya Dar , kuna ambayo ipo Kisarawe na Bagamoyo “
“Kwa hapa Dar ukiachana na unayoishi hio nyingine ipo maeneo gani?”
“Ipo Kigamboni Mbutu huko”
“Hio ndio shida yangu , nahitaji nyumba nina marafiki zaku kutoka nje ya nchi ambao wanaingia leo nchini nataka niwahifadhi kwa muda , ila sina nyumba kwa sasa”Aliongea Roma na Rose alitabasamu.
“Hubby chukua ya Kigamboni itakufaa , pia ni sehemu nzuri kwani ipo ufukweni na isitose ni mpya na nilikuwa nikipanga kuipangisha lakini sikupata mtu”Aliongea Rose na Roma alitabasamu na kumkiss Rose.
“Nataka nikaione leo maana marafiki zangu wakifika nchini moja kwa moja nataka niwapeleke na wanaingia leo usiku”Aliongea Roma na Rose hakukataa , kwanza alijisikia fahari kwa Roma kumuomba msaada yeye, msaada ambao Roma ameomba kwake ulikuwa na maana kubwa.
Ni ndani ya dakika chache tu walikuwa washafika Mbutu , hii sehemu ilikuwa nzuri licha ya kwamba haikuwa na nyumba nyingi , lakini mazingira yake yalikuwa safi sana kiasi cha Roma kupapenda na kuona wanajeshi wake kukaa hapo ni chaguzi sahihi.
Waliona jumba hili ambalo lilikuwa kubwa sana kiasi kwamba hata Roma mwenyewe alishangaa , licha ya kwamba alikuwa akijua Rose ni Tajiri kwa kufanya biashara yake ya kuuza madawa ya kulevya , lakini hakujua kama anapesa kiasi hiko cha kumiliki mjengo kama huo. Walikabidhiana nyumba hio na Roma akamrudisha Rose nyumbani.
Saa mbili kamili Roma alikuwa nyumbani kwa ajili ya chakula , sebuleni alimkuta Bi Wema pamoja na Edna kama kawaida na walikuwa washaanza kula, alimsalimia Bi Wema na kisha akamgeukia mke wake na kumwangalia anavyokula kimapozi , Edna alikuwa bize na chakula chake , lakini ile anapeleka kijiko mdomoni alimwangalia Roma na kukuta Roma anamwangalia.
“Mbona unaniangalia hivyo?”
“Bebi unajua hata staili yako ya kula inakufanya uwe mrembo kuliko wanawake wote duniani”Edna alijikuta akimwangalia Bi Wema na kuona aibu kiasi kwamba mwili wake ulipata uwekundu.
“Kaa pakua chakula kula”Aliongea Edna na kumfanya Bi wema aliekuwa pembeni atabasamu kwa kushuhudia aibu za Edna.
Roma alipakua chakula chote kilichokuwa kwenye mabakuli na kujaza kwenye sahani kama mlima Kilimanjaro na kuanza kula , bila habari .
“Roma..!”Aliita Edna huku akimwangalia Roma na sahani yake na Roma alimwangalia Edna bila kuongea.
“Kesho kutwa ndio siku ya kwenda Japan , ujiandae basi nitakupatia baadhi ya karatasi za mkataba uzisome”.
“Mke wangu mimi naenda kama mkalimani kuna haja gani ya kuzisoma?”
“Ndio najua lakini huu mkataba ni muhimu sana kwa kampuni na kukitokea tatizo lolote ninaweza kufirisika moja kwa moja , ni vizuri ukijua nini kinaendelea ili kama ikitokea tatizo iwe rahisi ya wewe kuligundua kuliko kumwachia kila kitu Doris”.
“Sawa nitazipitia mke wangu”.
Baada ya Roma kushiba , aliangalia saa yake na kuona ni muda muafaka wa kuelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya kupokea wageni wake , kwani mchana alikuwa ashawasiliana na Sauroni na kumpa taarifa kuwa wataingia Tanzania saa nne usiku.
“Wife ninatoka kidogo”
“Leo naomba usiende”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashangae na sio Edna tu hata Bi Wema alishangaa , lakini alitabasamu moyoni .
Ukweli ni kwamba Edna mchana yote alikuwa akifikiria swala la kujaribu kumpa Roma kitumbua na alishinda kwa kutafuta mitandaoni jinsi ya kumuanza mume wake maana alikuwa na aibu sana , alitamani kumuuliza Bi Wema ampe mbinu lakini aliona aibu na msaada pekee aliona ni kuingia mtandaoni na kutafuta namna ya kumuanza Roma.
“kama nitakuwa nampa maramoja moja anaweza kutulia nyumbani”Aliwaza wakati akiendelea kusoma mbinu mtandaoni.
Na alijikuta akipata mpango kabambe wa kumpagawisha Roma huku akiamini kama atafanikiwa katika mpango huo basi anaweza kumtuliza Roma nyumbani.
Na alipanga mpango wenyewe ili ukamilike lazima Roma alale nyumbani na ndio maana baada ya Roma kumwambia anataka kutoka aliona mpango wake hautofanikiwa na alitaka kuukamilisha kabla ya Roma na Dorisi kwenda Japani.
KIONJO .. MWENDELEZO NAUWEKA KABLA YA JOGOO LA ASUBUHI…
Roma hakujua sababu ya Edna kumwambia abaki nyumbani ,lakini kwake yeye alikuwa na jambo muhimu sana la kufanya usiku huo na kwa vyovyote vile asingeweza kukubaliana na mke wake.
“Mke wangu ninatoka ila nitarudi”Aliongea Roma na akanawa mikono na kuchukua ufunguo wa Gari yake na kuondoka.
Edna aliishia kusikilizia tu mngurumo wa gari ukifubaa kwenye masikio yake , Bi wema hata yeye alijisikia vibaya , alitamani Roma abaki nyumbani kama Edna alivyopendekeza lakini hakubaki , aliwaza ni jambo gani la muhimu ambalo Roma anaenda kulifanya nje kuliko kubaki na mke wake , hakujua lakini hakutaka kuwaza Zaidi , kwani Roma alikuwa ni mwanaume na pia hakutaka kuangilia katika mahusiano yake yeye na Edna.
Edna alirudi chumbani kwake , huku akijisikia mnyonge sana lakini pia akiwa na hasira nyingi , katika akili yake alijua kabisa Roma alikuwa akienda kuonana na wanawake wake.
“Mimi sio muhimu kwake , wanawake wake ndio muhimu ..Damn you Roma .. nimejipanga vyote hivyo leo kwa ajili yako halafu unaniona sina thamani… shenz kabisa , nakuambia hivi Roma utanisikia kwenye bomba ,Kwanza nini kilinipata mpaka nikawa na mawazo ya kijinga ya kumpa mwili wangu …Aaah Edna wewe mjinga kweli, Roma sio wa kumpa mwili wako ni Malaya yule mwanaume”Ungemuona Edna anavyoongea na mto usingemdhania ni yule CEO mwenye heshima zake , alikuwa akiongea mweyewe huku akiangalia mto uliokuwa kitandani kwake.
“Ila mimi mjinga sana hadi aibu ..Aaa nisingemwambia abaki nimejidharirisha leo …Edna usie ukarudia tena”Aliendelea kuongea mwenywe na kisha akachukua shuka na kujifunika gubigubi.
Upande wa Roma alifika Uwanja wa ndege kama kawaida muda ulikuwa ni saa tatu hivi kama na nusu , baada ya kusimama nje ya jingo la Terminal 3 akisubiria wageni wake , alikuja mwanaume mmoja wa kizungu alievalia suti bila tai huku akiacha vifungo viwili vya shati lake kuwa wazi na kumfanya nywele za kifuani kuonekana, aligonga gari la Roma mara mbili kwenye kioo cha mbele.
“You are Mister Roma ??”Aliuliza yule mzungu na Roma alitingisha kichwa kukubali kuwa ni yeye , yule mzungu alitoa ufunguo mfukoni na kumpatia na Roma alitabasamu na kisha akauchukua ule ufunguo huku bwana yule wa kizungu akiondoka mbele ya gari la Roma , alionekana kazi ambayo ilikuwa imemleta mahali hapo alikuwa ashaimaliza.
Baada ya dakika kama mbili hivi kupita ,Roma alitoka kwenye gari yake akiwa ameshikilia ile funguo ya gari na kisha alianza kubonyeza bonyeza kitufe cha rimoti iliokuwa imeambatana na ufunguo na gari lilitweak na kuwahsa taa za mbele na Roma alitabasamu na kuisogelea.
Ilikuwa ni gari kubwa kutoka kampuni ya Toyota , iliokuwa na uwezo wa kubeba Zaidi ya watu kumi na tano na ilikuwa imeletwa hapo na Ubalozi kwa ajili ya kuwasafirisha wageni kutoka uwanja wa ndege kwenda kwenye makazi yao.
Roma baada ya kuikagua na kuridhika , alitoka nje na ndani ya dakika chache tu , alishuhudia ndege kubwa kampuni ya KLM ikiiambaambaa kwa kushuka ndani ya uwanja huu wa Dar es salaam, aliendelea kusubiri kwa takribani dakika kumi na tano na hatimae alianza kuona wageni wake wakitoka nje kabisa ya mlango wa ‘Arrivals’.
Wa kwanza kabisa alikuwa ni mwanamke mzungu aina ya Cauccasian aliekuwa amevalia surali ya jeans rangi ya bluu n araba nyeupe huku akiwa amefunga kiunoni shati moja ya draft akiwa amevalia miwani , alionekana mrembo.
Wasichana wengine watatu walitoka huku nyuma yao wakifuatiwa na wanaume sita wote walionekana kuwa katika lika moja la ujana kati ya miaka 25 kwenda 30 , Roma aliwaona wazungu hao na kutabasamu , kwa namna ambavyo walikuwa wamebaba mabegi yao walionekana kama watalii , karibia wote walikuwa wakitafuna bublish.
“Your Majest Pluto”Aliongea yule mwanamke kwa mshangao , huku akionesha heshima ya hali ya juu kwa Roma lakini Roma alimpa ishara na mzungu yule alielewa na wenzake walielewa na kutulia .
“Welcome in Tanzania guys”
“Thank you” waliitikia wote kwa pamoja na Roma alitabasamu na kumrushia kijana mmoja funguo ambaye alikuwa mwembaba.
“You will drive along with me”Aliongea Roma na kuwaonyesha gari iliokuwa upande wao wa kushoto na wote wakatabasamu na kuisogelea na wote wakaingia ndani , lakini wakati Roma ashaanza kulisogeza gari lake kuingia barabara kuu , mara zilikuja gari tatu diffenda na kusimama barabarani na palepale walionekana wanajeshi wakiruka kwa ustadi mkubwa kwenye gari wakiwa na siraha na kisha kulizunguka gari lile walilopanda wazungu , walionekana walikuwa wamejipanga kweli.
Roma alishuhudia kitendo kile akiwa ndani ya gari yake na kujikuta misuli ya uso ikisimama , kwa namna wanajeshi hao walivyokuwa wanaonekana mahali hapo ilionesha kabisa walikuwa na taarifa za kutosha na ndio maana walionekana kujipanga.
Baada ya kuona gari lile limezingirwa Roma alishuka kwenye gari yake na kusogea upande wa wale wanajeshi walipo , lakini kabla hajawafikia gari iliokuwa mbele yake mita kadhaa , gari ambayo ilikuwepo hapo muda mrefu kidogo kwani aliiona , ilifunguliwa na akatoka mzee mmoja hivi mwenye mwili mkubwa wenye afya alievalia miwani pamoja na suti ,Roma hakumjua mzee huyu.
Yule mzee alimsogelea Roma huku wanajeshi watatu wakimzingira upande wa kulia na kushoto na nyuma wakionesha kumlinda ,Roma aliendelea kujiuliza mtu huyu ni nani na kwanini amewazingira wageni wake , kwani swala la wageni wake kuja ndani ya taifa la Tanzania lilikuwa ni siri sana na waliokuwa wakijua ni watu wachache sana ndani ya ubalozi wa Sweden.
“Tunaomba mshuke kwenye gari”Aliongea kwa kingereza moja ya wanajeshi ambae alikuwa na nyota tatu begani na wale wazungu waliangaliana na jamaa mmoja mwenye mwili mkubwa aliwapa ishara wenzake washuke na wakashuka huku wakiwa wamenyoosha mikono juu kuonesha kwamba hawapo kishari.
“Tupo hapa baada ya kupata taarifa ya nyie kuwa wanajeshi mnaokusudia kuingia ndani ya nchi yetu bila ruhusa”Aliongea yule Mwanajeshi alieonekana kuwa kiongozi na wakati huu Roma alikuwa ashafika upande aliosimama mzee ambaye alikuwa amevalia suti na yule mzee alimwangalia Roma na kisha wakasogeleana.
“Habari yako mzee , unaonakana wewe ndio kiongozi mkuu hapa , nini kinaendelea mbona wageni wangu wanazuiwa”.
“Nadhani mpaka sasa ushajua kwanini wanazuiwa Mr Roma Ramoni , Sisi ndio walinzi wa mipaka ya taifa hili na tunajua kinachoendelea nje na ndani ya mipaka yetu na hatupo tayari kuona wanajeshi wanaingia ndani ya taifa hili bila kuwa na kibali maalumu”
“Una Ushahidi gani kama wakujitosheleza kama hawa ni wanajeshi?”Mzee huyu alitabasamu.
“Hawa ni wanajeshi kutoka kundi la The Eagles na taarifa za ujio wao tulizipata kutoka kwa watu wetu ndani ya ubalozi”.Aliongea mzee huyu na Roma alimwangalia na kuwageukia wanajeshi wake waliokuwa katika hali ya wasiwasi.
“Mr Roma tunajua wanajeshi hawa wanauwezo mkubwa wa kimapigano , lakini leo lazima sheria za nchi zifuatwe hatuwezi kuwaachia wakaingia uraiani pasipo kujua ni sababu zipi zimewafanya kuingia hapa nchini , hivyo tutaenda nao pamoja na wewe kambini kwa ajili ya mahojiano”
“Hapana,naondoka na wageni wangu”Aliongea Roma na kumfanya mzee huyu amshangae na kisha akatabasamu
“Hauna uamuzi katika hili”: aliongea na kisha aliwapa ishara wanajeshi wafanye kazi , lakini ile wanataka kuwasogelea wale wanajeshi wa kizungu walishusha mikono chini na wanajeshi wa kitanzania walikuwa fasta sana kwani walikuwa ashakoki siraha zao tayari kwa mashambulizi.
Wanajesh wale wa kuzngu walimwangalia Roma huku wakionesha wanataka Ruhusa kutoka kwake , ila Roma aliwaangalia na kisha akamgeukia huyu mzee huku akiwaza jambo la kufanya , lakini kabla hajaongea ziliingia ndani ya eneo hili gari nyingine mbili moja Range Vx na moja difenda na baada ya gari hizi kusimama alishuka mzee mwingine alievalia gwanda huku mabega yake yakiwa yamechafuka kwa vyeo vingi, wale wanajeshi baada ya kuona mtu huyo ametoka kweye gari na na kumtambua walijikuta wakitoa heshima na kushangaa kwa wakati mmoja kwanini mkuu wao yupo hapo.
Upande wa huyu mzee aliekuwa akiongea na Roma pia alishangazwa na ujio wa mkuu wake , ghafla tu alikakamaa mwili.
“Jambo Afande” lakini Mzee huyu hakuongea chochote Zaidi ya kuinua mkono ya kumwambia alegeze na kumsogelea Roma.
“Mr Roma unaweza kuondoka na wageni wako , mengine tuongee siku ya kesho baada ya kuwasiliana ”Aliongea huyu mzee mwenye manyota mengi na Roma alitingisha kichwa pasipo kusema lolote na kisha akawapa ishara wanajeshi wa kizungu na wote wakaingia kwenye gari na kuondoka eneo hili Roma akiwa ametangulia.
RWANDA -KIGALI 2014
Ni ndani ya hoteli kubwa iliokuwa ndani ya jiji hili la Kigali , hoteli iliokuwa ikifahamika kwa jina la The Aquad alionekana mwanamke na mwanaume wakiwa ndani ya chumba kikubwa cha hoteli hii , katika floor ambayo ilikuwa ikihudumia VIP , huku nje ya Floor hii wakiwa walinzi wengi waliokuwa wamevalia suti.
Ndani ya chumba hiki mwanaume alionekana akiwa amepiga magoti chini , huku mwanamke mmmoja mrembo wa mweupe wa kabila la wanawake wa Babati yaani Wairaq akiwa amesimama huku akiwa na machozi mengi usoni , alionekana kulia mfululizo huku akiwa ameshikilia moyo wake.
“Nisamehe sana Raheli, naomba unisamehe mpenzi ,,, sikudhania haya yote yatatokea”
“Jeremy acha kuomba msamaha wako wa kipuuzi mbele yangu , unazidi kuniumiza , kwanini ulinificha muda wote kama Lorraine alikufa , kwanini Jeremy haukuniambia hii.. hiii…kwanini Jeremiiii…..”Mwanamke alionekana kulia kilio ambacho hakikiwa cha kawaida huku akimshutmu Jeremiii.
“Sikuwa na jinsi Rahel , sikutaka upitie maumivu niliopitia mimi”.
“Hata kama Jeremy , Lorraine ni mwanangu nilipaswa kujua haya yote ,hivi unajua ni siku ngapi nilitumia kuchukua maamuzi ya kukukabidhi Lorraine na kubaki na Edna eeh , unajua ni uchungu gani niliopitia kuwa mbali na mwanangu , hayo yote nilifanya kwasababu nakupenda Jeremy .. lakini kwanini ulishindwa kumlinda…..”Kilio kilikuwa ni cha aina yake kwa mwanamama huyu alionekana kumlaumu Jeremy kwa yale ambayo yamemtokea Lorraine , lakini pia anamlalamikia Jremy kwa kutompa taarifa ya kifo cha mwanae ,
“Rahel naomba unisamehe , najua ni maumivu gani unapitia baada ya taarifa hii , najua ulitarajia kumuona Lorraine akiwa na furaha ndani ya mikono yangu , lakini mimi pia kama baba yeke nilikuwa nikimpenda sana Lorraine na nilipanga kumpa Maisha mazuri , lakini haya makafir.. ya Dunia yamenichukulia mwanangu”.
“Unamaanisha nini Jeremy?”Aliuliza mwanamama huyu huku akisimama , hakumuelewa Jeremy baada ya kusema makafir alitaka kujua anamaanisha nini, Na kwa Jeremy alijikuta akijilaumu kwa kuropoka.
“Unamaanisha nini Jeremy ukisema Makafir ndio waliomchukua Lorraine?”
“Sijamaanisna hivyo Lorraine.. ni …”Kabla hajamaliza kuongea alikuwa ashashikwa tai na Raheli , mwanamama huyu alionekana kuzingatia kila neno mtu analoongea na ndio maana aliweza kumsikia vyema Jeremy alipo sema Makafir .
“Rahel namaanisha ,,”
“Usipo nipa maelezo ya kutosha leo Jeremy nakwambia hapa hutoki …”Jeremy alikuwa akimjua sana Rahel akiamua lake jambo lazima litimie , lakini hakutaka kumwambia Rahel juu ya kile anachokijua na anachoendela kukitafutia ukweli wake.
Jeremy aliamini kwa asilimia mia moja Ndege ile haikuanguka , bali kuna mpango wa siri ambao ulikuwa ukiratibiwa na mataifa yenye nguvu duniani , mpango ambao ulihusisha ndege hio kupotea, aliogopa kumwambia Rahel ukweli.
“Jeremy umenificha kwa miaka kumi na sita juu ya kifo cha mtoto wangu .. ukinificha jambo lolote na nikagundua jua sitokuja kukusamehe mpaka naingia kaburini”Aliongea mwanamama huyu huku akionesha hasira zake waziwazi.
Jeremy hakuwa na jinsi aliona Rahel anapaswa kuujua ukweli ule ambaye yeye alikuwa akiufahamu , aliona haina maana ya kumficha.
“Rahel tokea siku ambayo ndege ile ilipotea moyo wangu haukuwa na Amani kabisa , niliona kabisa kuna jambo ambalo halikuwa sawa , sikuwa na amani nilikuwa nikiota kila siku Lorraine yupo hai lakini sehemu aliokuwepo anateseka..”Alitulia kwanza na kufuta machozi na kisha akasimama huku akiwa anaangalia dirisha kama mtu aliekuwa akitafuta kitu.
“Kupotea kwa ndege ya shirika la M ilikuwa ni mpango wa wazungu”Rahel ni kama hakuwa amemsikia vizuri , kwani alinyanyuka na kwenda mpaka mbele ya Mheshimiwa Jeremy na kumwangalia vizuri usoni.
“Nieleze vizuri nielewe Jeremy .. mpango wa Wazungu ,, unanichanganya hebu eleza nielewe”
“Siwezi kukueleza mengi Rahel lakini naamini Lorraine yupo hai .. hakuna ushahidi wowote wa ile ndege kuanguka Rahel , yote ni mipango na mahesanu ya wazungu juu ya mpango ambao mpaka sasa hatuujui , mpango ambao umeratibiwa na mataifa makubwa yenye nguvu.. hii ni siri kubwa Rahel na sitaki kukuambia Zaidi ila naomba uelewe nitahakikisha naujua ukweli wote , nitatumia nguvu zangu zote kuhakikisha naupata ukweli wote na kama Lorraine yupo hai nitamrudisha “.
Taarifa hio ilionekana kuwa nzito sana kwa mwanamama Rahel , alikuwa akimjua Jeremy kwa muda mrefu tokea walivyokutana miaka kadhaa nyuma na kuanzisha mahusiano yao , alikuwa akimjua kuwa hawezi kuongea jambo ambalo hana uhakika nalo , alijikuta nguvu zikimuishia na kurudi kukaa kwenye sofa huku machozi yakiendelea kumbubujika.
Ukweli ni kwamba mwanamama huyu sababu ambayo ilimfanya asigundue kuwa Lorraine amekufa ni kutokana na kwamba Jeremy alitumia Mchezo wa kumuigizia kuwa anamchukia , kipindi chote ambacho Rahel alijaribu kuwasiliana na Jeremy , mheshimiwa huyo alionyesha kumchukia sana Rahel na hakutaka mazungumzo, na hata pale ambapo aliomba kuonana na Lorraine mheshimiwa alimtishia Rahel kukaa mbali na Lorraine la sivyo ataongea ukweli wote na dunia ijue kuwa Edna ni mwanae.
Kwa upande wa Rahel hakuwa tayari kwa watu kujua kuwa Edna sio mtoto wa Adebayo kwani kulikuwa kuna mkataba wa siri ambao alisaini na familia ya Adebayo , mkataba ambao Raheli alisainishwa na mama yake Adebayo.
“Jeremy una uhakika ndege ile haikudondoka na yote uliosema juu ya mpango ya wazungu ni kweli?”Aliuliza kwa sauti ndogo iliokuwa dhaifu na Jeremy alimuonea huruma sana Rahel , alijua ni afadhali kwake maumivu ya kumpoteza Lorraine yamezoeleka kwani tukio lilikuwa ni la muda mrefu tarkribani Zaidi ya miaka kumi na sita , alimsogelea Rahel na kisha akamkumbatia na walianza kuambizana kulia.
Kwa namna ambavyo Jeremy alikuwa akillia usingedhania ni kiongozi mkubwa wa taifa , kiongozi ambaye wananchi wa Rwanda wanamtegemea sana kuwafikisha katika nchi ya Ahadi.
“Ni kweli Rahel nina amini kwa asilimia kubwa Lorraine yupo hai na ninaompango wa kuhakikisha namrudisha”.
Rahel alifuta machozi na kisha alijitoa kwenye mikono ya Jeremy na akaweka sura ya usiriasi .
“Jeremy kama haya unayoyasema ni ya kweli hakikisha unaujua ukweli la sivyo sitokusamehe kwa kumpoteza mwanangu Lorraine”Aliongea mwanamama huyu na akafuta machozi na kuchukua mkoba wake na kutoka ndani ya chumba hiko.
****
Ilikuwa ni muda wa saa sita kamili za mchana alionekana Roma akiingiaa maeneo ya Club B , alikuwa na muda mrefu hajaingia ndani ya hii club , kwani tokea apate mke mara nyingi alikuwa akienda moja kwa moja nyumbani kwa Rose , lakini leo alikuwa amewahi sana kuja haya maeneo na alijua kabisa Rose hakuwa kwake na atakuwa ofisini na mawazo yake yalikuwa sahihi kwani alimkuta mwanada huyo akiwa kazini kama ilivyokuwa kawaida yake na kwa Rose alishangaa ujio wa Roma muda huo wa mchana.
“Hubby karibu” Aliiongea Rose huku akitoka kwenye meza na kuja kukaa kwenye masofa , huku akimwangalia Roma kwa kumsanifu , aliwaza Roma kaja muda huo kwasababu gani.
“Bebi Rose nimekuja leo nina shida”Aliongea Roma mara baada ya kuketi.
“Shida gani mpenzi , ongea tu nipo tayari kukusaidia”
“Unamiliki nyumba ngapi?”
“Bebi kwanini unauliza hivyo nina nyumba nne mbili hapa Dar na nyingine zipo nje kidogo ya Dar , kuna ambayo ipo Kisarawe na Bagamoyo “
“Kwa hapa Dar ukiachana na unayoishi hio nyingine ipo maeneo gani?”
“Ipo Kigamboni Mbutu huko”
“Hio ndio shida yangu , nahitaji nyumba nina marafiki zaku kutoka nje ya nchi ambao wanaingia leo nchini nataka niwahifadhi kwa muda , ila sina nyumba kwa sasa”Aliongea Roma na Rose alitabasamu.
“Hubby chukua ya Kigamboni itakufaa , pia ni sehemu nzuri kwani ipo ufukweni na isitose ni mpya na nilikuwa nikipanga kuipangisha lakini sikupata mtu”Aliongea Rose na Roma alitabasamu na kumkiss Rose.
“Nataka nikaione leo maana marafiki zangu wakifika nchini moja kwa moja nataka niwapeleke na wanaingia leo usiku”Aliongea Roma na Rose hakukataa , kwanza alijisikia fahari kwa Roma kumuomba msaada yeye, msaada ambao Roma ameomba kwake ulikuwa na maana kubwa.
Ni ndani ya dakika chache tu walikuwa washafika Mbutu , hii sehemu ilikuwa nzuri licha ya kwamba haikuwa na nyumba nyingi , lakini mazingira yake yalikuwa safi sana kiasi cha Roma kupapenda na kuona wanajeshi wake kukaa hapo ni chaguzi sahihi.
Waliona jumba hili ambalo lilikuwa kubwa sana kiasi kwamba hata Roma mwenyewe alishangaa , licha ya kwamba alikuwa akijua Rose ni Tajiri kwa kufanya biashara yake ya kuuza madawa ya kulevya , lakini hakujua kama anapesa kiasi hiko cha kumiliki mjengo kama huo. Walikabidhiana nyumba hio na Roma akamrudisha Rose nyumbani.
Saa mbili kamili Roma alikuwa nyumbani kwa ajili ya chakula , sebuleni alimkuta Bi Wema pamoja na Edna kama kawaida na walikuwa washaanza kula, alimsalimia Bi Wema na kisha akamgeukia mke wake na kumwangalia anavyokula kimapozi , Edna alikuwa bize na chakula chake , lakini ile anapeleka kijiko mdomoni alimwangalia Roma na kukuta Roma anamwangalia.
“Mbona unaniangalia hivyo?”
“Bebi unajua hata staili yako ya kula inakufanya uwe mrembo kuliko wanawake wote duniani”Edna alijikuta akimwangalia Bi Wema na kuona aibu kiasi kwamba mwili wake ulipata uwekundu.
“Kaa pakua chakula kula”Aliongea Edna na kumfanya Bi wema aliekuwa pembeni atabasamu kwa kushuhudia aibu za Edna.
Roma alipakua chakula chote kilichokuwa kwenye mabakuli na kujaza kwenye sahani kama mlima Kilimanjaro na kuanza kula , bila habari .
“Roma..!”Aliita Edna huku akimwangalia Roma na sahani yake na Roma alimwangalia Edna bila kuongea.
“Kesho kutwa ndio siku ya kwenda Japan , ujiandae basi nitakupatia baadhi ya karatasi za mkataba uzisome”.
“Mke wangu mimi naenda kama mkalimani kuna haja gani ya kuzisoma?”
“Ndio najua lakini huu mkataba ni muhimu sana kwa kampuni na kukitokea tatizo lolote ninaweza kufirisika moja kwa moja , ni vizuri ukijua nini kinaendelea ili kama ikitokea tatizo iwe rahisi ya wewe kuligundua kuliko kumwachia kila kitu Doris”.
“Sawa nitazipitia mke wangu”.
Baada ya Roma kushiba , aliangalia saa yake na kuona ni muda muafaka wa kuelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya kupokea wageni wake , kwani mchana alikuwa ashawasiliana na Sauroni na kumpa taarifa kuwa wataingia Tanzania saa nne usiku.
“Wife ninatoka kidogo”
“Leo naomba usiende”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashangae na sio Edna tu hata Bi Wema alishangaa , lakini alitabasamu moyoni .
Ukweli ni kwamba Edna mchana yote alikuwa akifikiria swala la kujaribu kumpa Roma kitumbua na alishinda kwa kutafuta mitandaoni jinsi ya kumuanza mume wake maana alikuwa na aibu sana , alitamani kumuuliza Bi Wema ampe mbinu lakini aliona aibu na msaada pekee aliona ni kuingia mtandaoni na kutafuta namna ya kumuanza Roma.
“kama nitakuwa nampa maramoja moja anaweza kutulia nyumbani”Aliwaza wakati akiendelea kusoma mbinu mtandaoni.
Na alijikuta akipata mpango kabambe wa kumpagawisha Roma huku akiamini kama atafanikiwa katika mpango huo basi anaweza kumtuliza Roma nyumbani.
Na alipanga mpango wenyewe ili ukamilike lazima Roma alale nyumbani na ndio maana baada ya Roma kumwambia anataka kutoka aliona mpango wake hautofanikiwa na alitaka kuukamilisha kabla ya Roma na Dorisi kwenda Japani.
KIONJO .. MWENDELEZO NAUWEKA KABLA YA JOGOO LA ASUBUHI…
Roma hakujua sababu ya Edna kumwambia abaki nyumbani ,lakini kwake yeye alikuwa na jambo muhimu sana la kufanya usiku huo na kwa vyovyote vile asingeweza kukubaliana na mke wake.
“Mke wangu ninatoka ila nitarudi”Aliongea Roma na akanawa mikono na kuchukua ufunguo wa Gari yake na kuondoka.
Edna aliishia kusikilizia tu mngurumo wa gari ukifubaa kwenye masikio yake , Bi wema hata yeye alijisikia vibaya , alitamani Roma abaki nyumbani kama Edna alivyopendekeza lakini hakubaki , aliwaza ni jambo gani la muhimu ambalo Roma anaenda kulifanya nje kuliko kubaki na mke wake , hakujua lakini hakutaka kuwaza Zaidi , kwani Roma alikuwa ni mwanaume na pia hakutaka kuangilia katika mahusiano yake yeye na Edna.
Edna alirudi chumbani kwake , huku akijisikia mnyonge sana lakini pia akiwa na hasira nyingi , katika akili yake alijua kabisa Roma alikuwa akienda kuonana na wanawake wake.
“Mimi sio muhimu kwake , wanawake wake ndio muhimu ..Damn you Roma .. nimejipanga vyote hivyo leo kwa ajili yako halafu unaniona sina thamani… shenz kabisa , nakuambia hivi Roma utanisikia kwenye bomba ,Kwanza nini kilinipata mpaka nikawa na mawazo ya kijinga ya kumpa mwili wangu …Aaah Edna wewe mjinga kweli, Roma sio wa kumpa mwili wako ni Malaya yule mwanaume”Ungemuona Edna anavyoongea na mto usingemdhania ni yule CEO mwenye heshima zake , alikuwa akiongea mweyewe huku akiangalia mto uliokuwa kitandani kwake.
“Ila mimi mjinga sana hadi aibu ..Aaa nisingemwambia abaki nimejidharirisha leo …Edna usie ukarudia tena”Aliendelea kuongea mwenywe na kisha akachukua shuka na kujifunika gubigubi.
Upande wa Roma alifika Uwanja wa ndege kama kawaida muda ulikuwa ni saa tatu hivi kama na nusu , baada ya kusimama nje ya jingo la Terminal 3 akisubiria wageni wake , alikuja mwanaume mmoja wa kizungu alievalia suti bila tai huku akiacha vifungo viwili vya shati lake kuwa wazi na kumfanya nywele za kifuani kuonekana, aligonga gari la Roma mara mbili kwenye kioo cha mbele.
“You are Mister Roma ??”Aliuliza yule mzungu na Roma alitingisha kichwa kukubali kuwa ni yeye , yule mzungu alitoa ufunguo mfukoni na kumpatia na Roma alitabasamu na kisha akauchukua ule ufunguo huku bwana yule wa kizungu akiondoka mbele ya gari la Roma , alionekana kazi ambayo ilikuwa imemleta mahali hapo alikuwa ashaimaliza.
Baada ya dakika kama mbili hivi kupita ,Roma alitoka kwenye gari yake akiwa ameshikilia ile funguo ya gari na kisha alianza kubonyeza bonyeza kitufe cha rimoti iliokuwa imeambatana na ufunguo na gari lilitweak na kuwahsa taa za mbele na Roma alitabasamu na kuisogelea.
Ilikuwa ni gari kubwa kutoka kampuni ya Toyota , iliokuwa na uwezo wa kubeba Zaidi ya watu kumi na tano na ilikuwa imeletwa hapo na Ubalozi kwa ajili ya kuwasafirisha wageni kutoka uwanja wa ndege kwenda kwenye makazi yao.
Roma baada ya kuikagua na kuridhika , alitoka nje na ndani ya dakika chache tu , alishuhudia ndege kubwa kampuni ya KLM ikiiambaambaa kwa kushuka ndani ya uwanja huu wa Dar es salaam, aliendelea kusubiri kwa takribani dakika kumi na tano na hatimae alianza kuona wageni wake wakitoka nje kabisa ya mlango wa ‘Arrivals’.
Wa kwanza kabisa alikuwa ni mwanamke mzungu aina ya Cauccasian aliekuwa amevalia surali ya jeans rangi ya bluu n araba nyeupe huku akiwa amefunga kiunoni shati moja ya draft akiwa amevalia miwani , alionekana mrembo.
Wasichana wengine watatu walitoka huku nyuma yao wakifuatiwa na wanaume sita wote walionekana kuwa katika lika moja la ujana kati ya miaka 25 kwenda 30 , Roma aliwaona wazungu hao na kutabasamu , kwa namna ambavyo walikuwa wamebaba mabegi yao walionekana kama watalii , karibia wote walikuwa wakitafuna bublish.
“Your Majest Pluto”Aliongea yule mwanamke kwa mshangao , huku akionesha heshima ya hali ya juu kwa Roma lakini Roma alimpa ishara na mzungu yule alielewa na wenzake walielewa na kutulia .
“Welcome in Tanzania guys”
“Thank you” waliitikia wote kwa pamoja na Roma alitabasamu na kumrushia kijana mmoja funguo ambaye alikuwa mwembaba.
“You will drive along with me”Aliongea Roma na kuwaonyesha gari iliokuwa upande wao wa kushoto na wote wakatabasamu na kuisogelea na wote wakaingia ndani , lakini wakati Roma ashaanza kulisogeza gari lake kuingia barabara kuu , mara zilikuja gari tatu diffenda na kusimama barabarani na palepale walionekana wanajeshi wakiruka kwa ustadi mkubwa kwenye gari wakiwa na siraha na kisha kulizunguka gari lile walilopanda wazungu , walionekana walikuwa wamejipanga kweli.
Roma alishuhudia kitendo kile akiwa ndani ya gari yake na kujikuta misuli ya uso ikisimama , kwa namna wanajeshi hao walivyokuwa wanaonekana mahali hapo ilionesha kabisa walikuwa na taarifa za kutosha na ndio maana walionekana kujipanga.
Baada ya kuona gari lile limezingirwa Roma alishuka kwenye gari yake na kusogea upande wa wale wanajeshi walipo , lakini kabla hajawafikia gari iliokuwa mbele yake mita kadhaa , gari ambayo ilikuwepo hapo muda mrefu kidogo kwani aliiona , ilifunguliwa na akatoka mzee mmoja hivi mwenye mwili mkubwa wenye afya alievalia miwani pamoja na suti ,Roma hakumjua mzee huyu.
Yule mzee alimsogelea Roma huku wanajeshi watatu wakimzingira upande wa kulia na kushoto na nyuma wakionesha kumlinda ,Roma aliendelea kujiuliza mtu huyu ni nani na kwanini amewazingira wageni wake , kwani swala la wageni wake kuja ndani ya taifa la Tanzania lilikuwa ni siri sana na waliokuwa wakijua ni watu wachache sana ndani ya ubalozi wa Sweden.
“Tunaomba mshuke kwenye gari”Aliongea kwa kingereza moja ya wanajeshi ambae alikuwa na nyota tatu begani na wale wazungu waliangaliana na jamaa mmoja mwenye mwili mkubwa aliwapa ishara wenzake washuke na wakashuka huku wakiwa wamenyoosha mikono juu kuonesha kwamba hawapo kishari.
“Tupo hapa baada ya kupata taarifa ya nyie kuwa wanajeshi mnaokusudia kuingia ndani ya nchi yetu bila ruhusa”Aliongea yule Mwanajeshi alieonekana kuwa kiongozi na wakati huu Roma alikuwa ashafika upande aliosimama mzee ambaye alikuwa amevalia suti na yule mzee alimwangalia Roma na kisha wakasogeleana.
“Habari yako mzee , unaonakana wewe ndio kiongozi mkuu hapa , nini kinaendelea mbona wageni wangu wanazuiwa”.
“Nadhani mpaka sasa ushajua kwanini wanazuiwa Mr Roma Ramoni , Sisi ndio walinzi wa mipaka ya taifa hili na tunajua kinachoendelea nje na ndani ya mipaka yetu na hatupo tayari kuona wanajeshi wanaingia ndani ya taifa hili bila kuwa na kibali maalumu”
“Una Ushahidi gani kama wakujitosheleza kama hawa ni wanajeshi?”Mzee huyu alitabasamu.
“Hawa ni wanajeshi kutoka kundi la The Eagles na taarifa za ujio wao tulizipata kutoka kwa watu wetu ndani ya ubalozi”.Aliongea mzee huyu na Roma alimwangalia na kuwageukia wanajeshi wake waliokuwa katika hali ya wasiwasi.
“Mr Roma tunajua wanajeshi hawa wanauwezo mkubwa wa kimapigano , lakini leo lazima sheria za nchi zifuatwe hatuwezi kuwaachia wakaingia uraiani pasipo kujua ni sababu zipi zimewafanya kuingia hapa nchini , hivyo tutaenda nao pamoja na wewe kambini kwa ajili ya mahojiano”
“Hapana,naondoka na wageni wangu”Aliongea Roma na kumfanya mzee huyu amshangae na kisha akatabasamu
“Hauna uamuzi katika hili”: aliongea na kisha aliwapa ishara wanajeshi wafanye kazi , lakini ile wanataka kuwasogelea wale wanajeshi wa kizungu walishusha mikono chini na wanajeshi wa kitanzania walikuwa fasta sana kwani walikuwa ashakoki siraha zao tayari kwa mashambulizi.
Wanajesh wale wa kuzngu walimwangalia Roma huku wakionesha wanataka Ruhusa kutoka kwake , ila Roma aliwaangalia na kisha akamgeukia huyu mzee huku akiwaza jambo la kufanya , lakini kabla hajaongea ziliingia ndani ya eneo hili gari nyingine mbili moja Range Vx na moja difenda na baada ya gari hizi kusimama alishuka mzee mwingine alievalia gwanda huku mabega yake yakiwa yamechafuka kwa vyeo vingi, wale wanajeshi baada ya kuona mtu huyo ametoka kweye gari na na kumtambua walijikuta wakitoa heshima na kushangaa kwa wakati mmoja kwanini mkuu wao yupo hapo.
Upande wa huyu mzee aliekuwa akiongea na Roma pia alishangazwa na ujio wa mkuu wake , ghafla tu alikakamaa mwili.
“Jambo Afande” lakini Mzee huyu hakuongea chochote Zaidi ya kuinua mkono ya kumwambia alegeze na kumsogelea Roma.
“Mr Roma unaweza kuondoka na wageni wako , mengine tuongee siku ya kesho baada ya kuwasiliana ”Aliongea huyu mzee mwenye manyota mengi na Roma alitingisha kichwa pasipo kusema lolote na kisha akawapa ishara wanajeshi wa kizungu na wote wakaingia kwenye gari na kuondoka eneo hili Roma akiwa ametangulia.