Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Safi sina Singanojr sie tunakufutilia kimya kimya huku, tunakusubiri jumatano utupe.mwendelezo!! Mambo ni fire kama inaisha mumbe watu wako 150...piga vioande virefu na huku mzee mzima!! Tuna alosto ya kufa mtu.
 
Safi sina Singanojr sie tunakufutilia kimya kimya huku, tunakusubiri jumatano utupe.mwendelezo!! Mambo ni fire kama inaisha mumbe watu wako 150...piga vioande virefu na huku mzee mzima!! Tuna alosto ya kufa mtu.
Usijali mkuu itashushwa hapa j5
 
Usijali mkuu itashushwa hapa j5
Tawile kaka j5 sio ndio kesho panapo majaaliwa ya Mola...anza kupika mzigo wa Roma uje wa mtomoto mkuu Singanojr...pawe.parefu basi maana wengine mzigo tunaumaliza ndani ya loasaa limoja tu...tunaacha kazi tunamfutilia mkuu Pluto. Ashapewa ukurugenzi wa kampuni mpya ya Enterment na Edina...yule dada aliueenda na Site mbagala nashangaa mpaka sasa..haja mpa mambo? Alafu Edna toka siku ya 1 tu mpaka leo hajaonjo mzigo...Roma anafail sasa na jiwe keshawapa wajapan...ashakuwa mlaini kwa Edna...
 
Saa tatu kamili siku ya jumatano. Mkuu, mtaalam, bingwa wa kalamu
 
Tawile kaka j5 sio ndio kesho panapo majaaliwa ya Mola...anza kupika mzigo wa Roma uje wa mtomoto mkuu Singanojr...pawe.parefu basi maana wengine mzigo tunaumaliza ndani ya loasaa limoja tu...tunaacha kazi tunamfutilia mkuu Pluto. Ashapewa ukurugenzi wa kampuni mpya ya Enterment na Edina...yule dada aliueenda na Site mbagala nashangaa mpaka sasa..haja mpa mambo? Alafu Edna toka siku ya 1 tu mpaka leo hajaonjo mzigo...Roma anafail sasa na jiwe keshawapa wajapan...ashakuwa mlaini kwa Edna...
inashuka leo ndeeefu Inshallah
 
SEHEMU YA 101

Roma alimwangalia Yezi kwa dakika kadhaa kama mtu aliekuwa akijiuliza maswali na kisha aliweka mfukoni ile cheni iliokuwa na kidani, Roma alitaka ampeleke Yezi sehemu anayoishi kwa kumpa Lift lakini mwanadada huyu alikataa na Roma hakutaka kufosi , alipanga gari na kuduti nyumbani.

“Oooshh…iii, Roma Please fanya taratibu”

“Okey! Wife ila kadri ninavyofanya taratibu ndio muda utaongezeka mpaka kumaliza”Aliongea Roma ambaye alikuwa akipiga kiuno taratibu huku akiwa ameweka kichwa chake kwenye shingo ya Edna.

“Argggh…Roma nimechoka naomba tuache”Aliongea Edna huku akiwa anahema kama mbwa aliekimbia maili nyingi , lakini Roma hakujali aliendelea kumuingia Edna na kutoka.

“Roma .. tuache … nataka nikajisaidie haja ndogo”.

“Hehe.. my Wife kojoa hapahapa”Aliongea Roma na kumfanya Edna akakamae huku akimn`gata Roma kwa nguvu , lakini Roma hakujali maumivu.

“Puuh!!!”Edna aliekuwa amelala kwenye ukingo wa kitanda akiwa amekumbatia mdori ambao ameupatia jina la pili la Roma yaani Ramoni , alijikuta akidondoka chini akiwa usingizini na alionekana alikuwa kwenye ndoto, na kitendo cha kudondoka chini kilimfanya ashituke kutoka usingizini , lakini sasa alijikuta akijishangaa kwa ndoto aliokuwa akiota.

Alichokifanya ni kukimbilia Bafuni na maji ya bomba yalisikika yakitiririka ndani ya chumba hiki na ni Dhahiri mwanadada huyu alikuwa akioga.

Edna aliwasha taa na kusogelea kioo akijiangalia huku akiwa amejifunga taulo, lakini kadri alivyokua akijiangalia na kukumbuka ndoto aliokuwa akiota dakika chache zilizopita , alijionea aibu , hakuelewa ni kwanini kwa mara ya kwanza katika maisha yake kuota ndoto kama hio, ndoto ambayo ilikuwa ikihusisha kufanya mapenzi na Roma.

Swala la kuota ndoto kama hio kwa Edna halikuwa swala dogo kwake na alilichukulia kwa uzito wake. kiasi kwmaba lilimkosesha usingizi , alijikuta akifungua mlango wa kiambaza(Balconi) kwa ajili ya kupigwa na upepo , licha ya kwamba usiku ulikuwa mkubwa na muda huo ilikuwa ni kama saa tano usiku.

Wakati Edna akiwa amesimama mara gari ya mtaalamu Roma ilionekana ikiingia hapo ndani na kuzunguka nyuma sehemu ya maegesho.

Mh! Yaani ndio anaanza kurudi..!?”Aliongea Edna huku akionesha hali ya kutofurahia Roma kurudi muda huo na katika akili yake aliwaza Roma alikuwa na mwanamke na ndio maana kachelewa , alijikuta ile ndoto aliokuwa akiota ikijirudia rudia kwenye akili yake na kujionea aibu Zaidi na kukimbilia ndani na kujirusha kitandani na kulala.

Ni muda wa asubuhi Roma akiwa ashamaliza kuoga na sasa alikuwa akijikausha kwa taulo , kwa ajili ya kujiandaa kuelekea kazini , simu yake ndogo ilianza kuita mfululizo na kumfanya aisogelee na kuangalia ni nani anampigia , ilikuwa ni namba ngeni ila ya kitanzania.

“Hello!!”

“Bro Roma ni mimi Mhando hapa”Ilisikika suati upande wa pili na kumfanya Roma akumbuke dili aliloingia na Mke wake.

“Yes mhando mambo vipi”

“Safi tu Bro nimekupigia kukupa shukrani zangu,Bro yaani siamini kama nimepata kazi , tena ya kudumu kaka asante sana Mungu akubariki mpaka ushangae”Roma alijikura akitabasamu kwani kwa jinsi ambavyo Mhando alikuwa akiongea kwa furaha ni kama sio yeye, kwnai alikuwa amemzoea Mhando kuwa mpole na mara nyingi alikuwa akiongea kidogo sana , lakini leo hii kutokana na furaha ya kupata kazi alisikika kuwa mchangamfu.

“Ni swala dogo sana hilo Mhando ,kwa vigezo vyako ulipaswa kupata kazi, hivyo nimesaidia kidogo tu”

“Ndio Kaka , lakini kutokana na namna ambavyo nilihangaika kupata kazi lazima nikupe shukrani zangu , I am so Touched bro with your help,nakuombea uzidi kufanikiwa ili utusaidie marafiki zako”Aliongea Mhando na Roma akaitikia kumridhisha.

Baada ya Roma kukata simu , alijikuta akitabasamu lakini pia na kufikiria kwa wakati mmoja , aliona Edna alikuwa ashakamilisha ahadi kwa upande wake na sasa yeye ndio amaetakiwa kutimiza ahadi yake.

Roma alishuka mpaka sebuleni na kumkuta Edna akiwa peke yake akijipatia stafutahi ya Asubuhi , akiwa ashajiandaa kuelekea kazini , Roma alimwangalia Mrembo huyu kwa jinsi alivyopendeza, alimuona Edna kama pambo ndani ya nyumba.

“Darling umeamkaje?”

“Safi”Aliitkia Edna huku akiendelea kuwa bize na alichokuwa akifanya , Roma alimwangalia na akatabasamu huku akiwaza ni lini mke wake ataacha ukauzu na kuchangamka mbele yake , kwani kuna muda aliona kama Edna alikuwa akimfanyia makusudi.

“Wife Asante kwa kumsaidia rafiki yangu”

“Hauna haja ya kunishukuru nilichofanya ni kutimiza ahadi na kazi iliobaki ni kwako kufanya kama ulivyoahdi”

“Wife usijali ,mimi ni mwanaume wa kutimiza ahadi na siwezi kwenda kinyume na maneno yangu”Aliongea Roma na Edna akamwangalia kwa dakika kadhaa Roma ni kama alikuwa akimkagua na kutafuta Dosari na Roma pia alishangaa kwanini Edna anamwangalia kwa namna hio.

“Baadae”

Aliongea Edna na kujifuta midomo kupitia kitambaa na akachukua mkoba wake na kuanza kupiga hatua kuelekea nje na kumuacha Roma kumwangalia Mke wake anavyotokomea kwa nje na kumuachia harufu yake nzuri ya Perfume.

Roma baada ya kumaliza kujipatia kifungua kinywa alimuaga Bi Wema na kisha aliingia kwenye gari yake na kuianza safari ya kwenda kazini , huku akiendesha taratibu , lakini pia yeye mwenyewe alikuwa akijishangaa kwani kwa jinsi maisha yake yalivyokuwa yakiendelea ndani ya kampuni , alijiona ni kama hakupaswa kwenda kazini kabisa , kwani hakuwa na mchango wowote.

Roma wakati akiwa kwenye gari simu yake ilianza kuita mfululizo na akaitoa na kupokea baada ya kuona jina la mpigaji.

“Ndio Afande Maeda kuna nini asubuhi yote hi?”

“Mr Roma naomba unisamehe kwa usumbufu ila nimekupigia kuthibitisha jambo”

“Jambo gani?”

“Sisi kama jeshi tulipewa jukumu la kulinda Jiwe la Kimungu na mpaka sasa tupo kwenye sintofahamu baada ya kushindwa kuwakamata Yamata , tupo na kikao hapa na wakuu wa usalama wa Nchi na tunataka kujua kama jiwe ulilotoa ni lenyewe au umewapa feki”

“Afande Maeda nadhani Ajenti Flamingo hakuwaeleza vizuri , mimi nimetoa jiwe lenyewe na sio feki kama mnavyodhania na kama mmeshindwa kuwapata hao Yamata hilo ni swala lenu kulifanyia kazi”Aliongea Roma.

“Okey !Mr Roma tulitaka kupata jibu kutoka kwako na kwakuaa umetuthibitishia kama ni kweli umetoa jiwe hilo kwa Yamata ,basi tunaamini hautoingilia maswala yote ambayo yanahusiana nalo”.

“Kaeni kwa Amani kabisa Afande na wenzio , sitakii kuhusika na jiwe hilo maana linaweza kuleta shida kwa watu wangu wa karibu”Aliongea Roma na kukata simu , lakini wakati huohuo uliingia ujumbe kwenye simu yake na kuangalia.

“Nadhani haujasahau ahadi ya kuonana kwetu , muda ni saa kumi na mbili za jioni Rozana Hoteli”

Ulikuwa ni ujumbe ambao Roma kwa kuangalia tu hio namba alijua inatoka kwa Mage na hakufikiria sana , alizidi kuendesha gari yake na ndani ya madakika kadhaa alikuwa akiingia Posta yalipo makao makuu ya kampuni ya Vexto.

Baada ya kupaki gari yake moja kwa moja alienda mpaka ofisini kwake na kuwakuta wafanyakazi wenzake wakiwa bize , lakini leo hii mazingira ya kampuni yalionesha kuwa sio ya kawaida.

“Recho kuna nini?”Aliuliza Roma mara baada ya kuketi.

“Hivi wewe inakuaje kila kinachoendelea kwenye kampuni haujui , ni mfanyakazi kweli”Aliongea Recho huku akionyesha hali ya kumzodoa Roma , lakini Roma aliishia kutabasamu.

“Niambie bwana acha maneno mengi Recho”

“Kuna mabadiliko katika uongozi,”

“Unamaanisha nini?”

“Leo ni siku ya kutambulishwa CEO msaidizi wa kampuni”Roma alishangaa kidogo , kwanza hakuwahi kujiuliza ni nani msaidizi wa Edna.

“Kumbe hakukuwa na msaidizi?”

“Ndio! Mara nyingi kama Edna akipatwa na dharula Nasra ndio alikuwa akimkaimu”Aliongea Recho na kumfanya Roma aelewe.

“Sasa kwa ajili ya kuja CEO msadizi ndio mmefanya haya mabadiliko ya mpangilio wa ofisi?”

“Huna unachofahamu Roma ,CEO anaekuja anasifika kwa ukali na kutopenda watu wavivu kazini , wafanyakazi wa tawi la Nairobi wanamfahamu kwa ukali wake”Aliongea Recho na kumfanya Roma ashangae kwanza hakuwahi kusikia kuwa Nairobi kuna kampuni iliokuwa ikisimamiwa na mke wake.

“Kwahio na Nairobi kuna kampuni iliochini ya Vexto pia?”Recho alishangaa kwani kwa namna ambavyo Roma alikuwa akiuliza maswali ni kama alikuwa mfanyakazi ambaye alikuwa akianza kufanya kazi ndani ya hio kampuni.

“Naona hauna unachofahamu , ngoja nikuelezee tu , kwa Afrika VExto ina matawi katika nchi nane ,Afrika ya Kusini , Botwana , Kenya Uganga , Rwanda ,Nigeria ,Namibia ,Ghana na Ethiopia”

“Vipi kuhusu nje ya Afrika”Recho alivuta pumzi kidogo.

“Ni Ufaransa peke yake”.

“Alright Mrembo ,ila leo umependeza na yenyewe ni kwa ajili ya CEO Msaidizi?”Aliongea Roma na kugeuza kiti chake kuendelea na kucheza gemu na Recho alimwangalia Roma kwa dakika kadhaa kama vile hajawahi kumuona na kisha aligeukia tarakishi yake na kuendelea na majukumu hakutaka kumjibu Roma na maswali yake ya kihuni.

Muda wa Saa sita hivi , Recho alimfinya Roma baada ya kumuona Edna alieambatana na baadhi ya wafanyakazi wakubwa wa kampuni kuingia hapo ndani ya kitengo cha PR, Edna alikuwa ameongozana na Dorisi , Nasra na wamama wawili ambao walikuwa ni watu wazima , ambao walikuwa ni wafanyakazi wakubwa wa kampuni hii ya Vexto , lakini pia alionekana kijana mmoja hivi anaelingana na Roma , alikuwa ni kijana mtanashati kweli ambaye alifanya warembo wa idara hii kuvutiwa nae.

Recho baada ya kuona anamfinya Roma aamke kutoka kwenye usingizi bila mafanikio alisimama yeye mwenyewe akimuacha Roma.

Benadetha aliekuwa ndio kiongozi wa Idara hii alikuwa akitoa maelezo kwa heshima kwa wakuu wake wa kazi huku akieleza kazi ambazo zinafanyika kwenye idara yao ya PR ,Mwanadada alielezea kwa umakini mkubwa akitumia lugha ya kingereza na bwana ambaye alijitambulisha kwa jina la Michal Ernest Komwe aliridhishwa na maelezo hayo.

Edna , Dorisi na Nasra muda wote macho yao yalikuwa kwenye meza ya Roma na Edna alikasirishwa na tabia ya Roma ila hakutaka kuongea , alijiambia mwisho wa Roma wa kulala kazini ni siku atakayompa kampuni.

“Mr pale ana nini mbona yuko tofauti na wenzake na nikama hayupo kazini”aliuliza bwana Michal.

“Hajisikii vizuri leo , ila ni mchapa kazi mahili ndani ya kampuni na ndie aliefanikisha dili kubwa la Yamakuza”aliongea Benadetha kwa kumtetea Roma na kumfanya Edna amwangalia namna ambavyo Benadetha alikuwa akimtetea , alijisikia vibaya na sio kwake tu hata Dorisi na Nasra hawakupendezwa na namna ambavyo Benadetha aanamkingia kifua Roma.

“Kama hajisikii vizuri kwanini yupo hapa , alipaswa kubaki nyumbani kuliko kushusha morali ya wenzake kufanyakazi kwa kulala ofisini”aliongea Michal.

“Na kama nilianza kujisikia vibaya nikiwa kazini je?”Aliongea Roma na kugeuza kiti chake na kufanya wadada hawa wamwangalie.

“Hilo linaeleweka , kampuni ya Vexto haipo kwa ajili ya kutesa wafanyakazi , ukijisikia vibaya unaaaga na unaondoka, sio ndio Miss Edna”aliuliza Michal huku akimgeukia Edna ambaye haikueleweeka alikuwa na hisia gani kwa wakati huo na alitingisha tu kichwa.

“Okey!Mr Asistant , ila hali yangu imerudi kwenye ukawaida yake baada ya kulala kidogo, sidhani kama itakuwa jambo zuri kama kila mfanyakazi anaejisikia vibaya kuondoka , muda mwingine tunahitaji muda wa dakika chache kupumzika na kurudi sawa”Aliongea Roma na kisha aligeuza kiti chake na kushitua tarakishi yake ambayo ilikuwa imejizima , lakini sasa Michal alijikuta akishangaa Zaidi baada ya kuona gemu la mpira kwenye skrini.

“Michael tushamaliza hapa , tunapaswa kwenda idara nyingine maana muda wa chakula cha mchana unakaribia”Aliongea Dorisi na Edna alikuwa wa kwanza kugeuka na kufanya wadada hawa wa PR washushe pumzi na kumgeukia Roma.





SEHEMU YA 102

Saa kumi na mbili za jioni Roma alitoka ndani ya Kigamboni kuitafuta Sinza eneo ambalo ndio Mage alitaka kwa wao kuonana a , aliendesha gari yake huku akijiuliza kwanini Mage achague maeneo ya mbali hivyo, ila hakutaka kuwaza sana , aliendesha gari yake kwa umakini na kwa spidi na ndani ya kama nusu saa hivi alikuwa akiingia ndani ya hoteli moja maarufu iliokuwa ikifahamika kwa jina la Rozana.

Baada ya kugesha gari yake kabla ya kushuka alitoa simu yake na kumpigia Mage kumuuliza yuko wapi kwani yeye alishafika.

“Ndio naingia na gari sasa hivi”Ilisikika sauti nyororo kwenye masikio ya Roma,.

Nusu dakika baada ya Roma kutoka kwenye gari yake hatimae aliweza kushuhudia gari ya kifahari ya Maserati Ghibli Trofeo ya mwaka 2022, iliokuwa ni ghali ambayo ilifanya watu wote ambao walikuwa kwenye haya maneo kuiangalia kwa macho ya wivu , Roma aliangalia gari hii mpaka pale ilipoisimama.

Roma alijikuta moyo wake ukimwenda spidi baada ya kushuhudia mwanamke mrembo aitoka kwenye gari hii , ni kama haamini kama mtu aliekuwa mbele yake alikuwa ni yule ambaye amemzoea kumuona kwenye mavazi yake ya kazi.

Ndio alikuwa ni mwanadada Mage ambaye leo hii hakuwa kwenye mavazi ya kipolisi , leo alikuwa ni mwanamke mrembo sana kawnye macho ya Roma kiasi kwamba ni kama haamini kama ni mage.

Mage aliikuta akitabasamu baada ya kumuona Roma kuwa katika aina hio ya mshangao.

“Roma..!!”Aliita Mage na kumfanya Roma kutikisha kichwa huku homoni zake za kiume pale aonapo mrembo zikiwa juu.

“Mpaka nimekusahau , Sikudhani yule polisi mbabe leo hii anaweza kuwa mrembo namna hii , Mage umeua leo”Aliongea Roma huku akiweka tabasamu na kumfanya Mage aone aibu na kujisikia utamu.

Mage alimkumbatia Roma , licha ya kwamba Roma hakutaka kabisa kumkumbatia lakini kutokana na watu walikuwa wakiangalia alijikuta akiacha Mage amkubatie kimahaba kabisa ni kama walikuwa wapenzi na hata kwa watu waliokuwa eneo hiilo walijua kabisa hao wawili ni wapenzi , na walimuona Roma kama mwanaume mwenye bahati kwa kung`oa mwanamke mrembo kama huyo na sio urembo tu lakini pia mwenyepesa , kwani kwa gari ambayo Mage amefika nayo ni watu wachache sana ambao wanaweza kuimiliki, lakini pia watu hao hawakumbeza Roma kwani licha ya Roma kuoneakna wa kawaida , lakini alikuwa amekuja na gari nzuri ya kifahari ambayo pia ni moja ya Gari chache sana ambazo zilikuwa zikipatikana ndani ya jiji hili la Dar ,BMW M7.

Mage alitangulia mbele huku Roma akiwa nyuma akimwangalia Mage kwa nyuma , Mage jioni hii alikuwa amevalia kikoti flani hivi aina ya Vest chenye vifungo ambavyo vinafungiwa kwenye ubavu cha rangi ya njano ambacho kwa juu kabisa kilikuwa kimenakishiwa kwa wavu flani hivi , lakini kwa mpangilio wa kupendeza , chini akiwa ametinga surali ya kitambaa yenye marinda mwishoni na kiatu kirefu aina ya Skuna, kwa muonekano wa nguo zake ni Dhahiri kwamba zilikuwa ni ‘Brand’ kutoka nje ya nchi.

Roma hakushangaa na aina haya mavazi ambayo kwake aliona ni ghali sana kwa mtu wa kawaida kuvaa , lakini pia mavazi ambayo yapo kifasheni kwani alikuwa akikumbuka vyema mama yake Mage alikuwa akimilikia bongeala duka la nguo eneo la Posta.

Watu waliokuwa ndani ya ukumbi wa chakula eneo la mgahawa ndani ya hoteli hii ya hadhi ya nyota tatu, walimuonea Roma wivu kwa kuongozana na mrembo kama huyo na hawakuacha kugeuka kuangalia umbo namba nane la Mage, lakini kwa Roma hakujali sana.

Upande mwingine ndani ya eneo la Masaki alionekana mama T ndani ya jumba hili la kifahari akiwa sebuleni akufungua friji na kutoka chupa ya ‘Red Wine’ na kisha akasogea mpaka kwenye masofa na kuweka glasi chini huku akimwangalia Kanali Agustine aliekuwa bize akiangalia Runinga.

“Unaokeana kuwa kwenye mudi nzuri leo mke wangu”aliongea Kanali Tobwe.

“Sana mume wangu”

“Sasa si uniambie hiko ambacho kinakufanya kuwa na furaha tufurahie wote , tumeanza kufichana habari nzuri tangu lini”

“Si naendelea na wewe , mbona unakimbilia mwisho”

“Hehe.. haya niambie mke wangu”

“Ni Mage”

“Kafanya nini Mage”

“Inaonekana Mage kuna mwanaume ambaye amempenda”Aliongea na kumfanya Kanali kushangaa.

“Unasema kweli , Mage kuna mwanaume amempenda?”

“Sina uhakika lakini naamini ni kweli , leo mchana nimepigiwa na Tusi Mage kaenda dukani kwetu kununua mavazi ya kutokea kwa usiku na kwa jinsi Tusi alivyoniambia ni dhahiri kabisa kuna mwanaume ambaye anaenda kuonana nae usiku wa leo, na kwa ninavyomjua mwanangu Mage kwa mavazi ambayo amechagua ni ghahiri mtu anaekwenda kuonana nae ni mwanaume”Aliongea Mama T na kumfanya Kanali atabasamu.

“Unaonaje ukipeleleza tukajua ni mwanume gani Mage katokea kumpenda , unaweza hata kumuuliza”

“Tusiwe na haraka , unajua hii ni mara ya kwanza kwa Mage, hivyo tunaweza kumkatisha tamaa , ngoja tusubiri subiri”Aliongea Mama T na kumfanyab Kanali kutabasamu.

“Utapendelea nini Roma?, unaweza ukaagiza chakula”Aliuliza Mage baada ya kumuona Roma ameshikilia kitabu cha orodha bila kuchagua.

“Hapana Mage , bado ni mapema sana , muda huu kama nitakula njaa itaniuma mapema” Na muda hui huo mhudumu aliwasogelea aktika kuchukua oda yao.

Mage aliagiza juisi kwani hata yeye aliona muda ni mapema sana kuagiza chakula na Roma hakuwa mpenzi wa juisi , yeye aliagiza Wine na kisha akamgeukia Mage ni kama alikuwa akimpa ishara aanze mazungumzo.

“Roma najua unashauku ya kujua ni kwanini leo nimeomba tukutane”

“Ndio na inabidi uniambie sasa”

“Roma ukweli ni kwamba tokea siku ile ya Kusanyiko la wafanya biasahra nimekuwa mtu wa kujiuliza maswali kuhusu wewe , wapi umetokea , ni vitu gani ulikuwa ukifanya huko nyuma na kwanini ulikuwa kama vile , licha ya kwamba ulipigwa Risasi lakini ulionesha hali ya kuwa kawaida, mpaka sasa nimekuwa wa kuwazia hayo maswali”Aliongea Mage kwa sauti ya chini na Roma alimwangalia Mage , lakini pia wakati huo huo mhudumu alileta oda yao na kuwapatia.

“Mage nakumbuka ulisema kwamba unatamani sana tuwe marafiki na mimi pia nikakubali , kama ni kweli unataka urafiki wetu uendelea nadhani itakuwa vyema sana usipo uliza hayo maswali , kwani nikuambie tu siwezi kukujibu na pia nadhani dada yako pia ameshindwa kukupa taarifa zote kuhusu mimi na ndio maana una shauku, hajakuambia kwasaabu huenda taarifa zangu ni nzito kidogo kwa kila mtu kujua”

Jibu hilo lilimfanya Mage kujisikia vibaya , aliona ni kama Roma alikuwa akijiweka mbali na yeye na alijawa na huzuni kwa wakati mmoja na Roma pia aliliona hilo na kushangaa kwanini Mage kabadilika ghafla.

“Mage ni nini tatizo , au hujaridhika na jibu langu?”Aliuliza Roma huku akiangalia saa kwenye simu.

“Roma hebu naomba uwe mkweli na mimi , naataka uniambie kama kukuomba sisi kukutana hapa unajihisi nimekupotezea muda wako?”Roma alishangazwa na aina hii ya swali.

“Kwanini unauliza hivyo Mage?”

“Unaonekana kama mtu ambaye muda wote utaaga na kuondoka , sioni hali ya utulivu kwenye macho yako , lakini pia na kuona kama mtu ambaye unajitahidi kujiweka mbali na mimi”

“Mage sijui ulitaka nikujibu nini , lakini hilo ndio jibu pekee ambalo ninaweza kukupa mpaka sasa , Wewe ni polisi na nadhani mpaka hapo umenielewa ninachojaribu kumaanisha”

“Lakini leo hii sijaja kama polisi Roma , nimekuja kama mwanamke ndio maana nikavaa nikaendeza hii yote ni kwa ajili yako” Roma siku zote alikuwa ni mtu mwenye kutawala maongezi , lakini leo hii mbele ya Mage alikosa jibu.

Wakati Roma kaifikiria jibu la kumpa Mage Mara simu yake ilianza kuita mfululizo na kumfanya aitoe mfukoni na kuangalia ni nani ambaye anampigia kwa wakati huo na alipoangalia jina aliona sio namba ya Tanzania, lakini ni kama alikuwa ashaitambua hio namba kwani ilionekana sio mara ya kwanza namba hio kumpigia.

“Hades habari za muda huu?”

“Balozi!!”

“Ndio Hades ni mimi”

“Ndio nakusikiliza Balozi”

“Hades nakutaarifu Sophie ashafika nchini na nadhani mpaka sasa hajakutaarifu”

“Hapana hajanitaarifu , lakini pia nadhani haina haja ya yeye kunipigia simu kwani hapa Tanzania ana ndugu”

“Hades ndio maana nimekupigia simu , kifupi ni kwamba Sophia bado yupo uwanja wa ndege tokea asubuhi anakusubiri ukampokee, na hata baadhi ya ndugu niliowaagiza kumfuata amewakatalia na anasema pasipo ya wewe kwenda kumpokea haondoki”Aliongea Balozi na Roma alidhania ni kama utani.

“Balozi uko siriasi juu ya hili?”

“Nisingekupigia simu Hades, ninachokuomba ukamtoe mwanangu Sophia uwanja wa ndege”Aliongea balozi na kukata simu.

Roma alijikuta akishangazwa na jambo hilo , ni kama hakuwa akiamini kama kweli Sophia ameshindwa kuondoka uwanja wa ndege kisa yeye hajaenda kumpokea , jambo hili lilimshangaza na kuona nikama majaribu kwake , kwani alikuwa ashaweka wazi msimamo wake kwa balozi kwamba hawezi kumfanya Sophia kuwa mke wake.

“Mage nadhani tutaongea siku nyingine kwa sasa nina dharula”Aliongea Roma huku akinyanyuka ni kama hakutaka kusubiria jibu kutoka kwa Mage.



SEHEMU YA 103

Upande mwingine , ndani ya eneo la Mbezi Beach mkabala na jengo la kanisa la KKKT, ndani ya jumba la kifahari anaonekana mwanadada mrembo Nadia au Goddes of Law akiwa amejiachia sebuleni kwake bila habari , na kwa jinsi ambavyo mwanamke huyu alikuwa amevaa kama ni mwanaume ungekuwa karibu yake ni hakika ungetegeka , kwani kigauni alichokuwa amevalia kilikuwa ni kifupi mno na chepesi na kumfanya mapaja yake yote kuwa wazi.

Muda huu mrembo huyu alikuwa ameshikilia Glassi ambayo ndani yake ilikuwa na kimiminika cha rangi ya Zamabaru iliokolea ikiwa imejaa nusu , na alikuwa akipeleka mdomoni kwa madaha kabisa huku akiangalia runinga iliokuwa ikionyesha ‘live Show’ ya mwanamuziki mkubwa wa kike duniani aliekuwa akifahamika kwa jina la Christine.

Wakati mrembo huyu akiwa ameweka umakini kwenye Runinga , mlango wa eneo la sebulenni ulifunguliwa na akaingia mwanaume mmoja wa Kiafrika mweusi alievalia tisheti ya Levi`s pamoja na jeans na miwani , alikuwa ni kijana alieonekana kuwa mtanashati sana.

“Evansi mpango wangu unaendaje mpaka sasa?”Aliuliza Nadia huku akikaa pozi lile lile pasipo kubadilika na kumtesa kijana huyu ambaye muda wote macho yake yalikuwa yakiufaidi mwili wa mrembo Nadia.

Evansi hakutaka kuongea Zaidi , alitoa simu yake mfukoni na kisha akmpatia Nadia alieipokea na kuangalia.

Kwenye simu hio zilionekana picha Za Mage na Roma wakiwa wamekumbatiana kimahaba , na kwa jinsi walivyokuwa wakionekana kwenye picha ni kama wawili hao walikuwa na mahusiano na haikueleweka ni kwa namna gani walipiga picha hizo kwani ni za muda mchache ambao Roma na Mage walikuwa Rozana ,Nadia aliendelea kuperuzi kwenda kulia kuangalia hizo picha nyingine ambazo zilimuonesha Roma na Mage wakiwa wameketi wakiangaliana uso kwa uso.

“Nataka uendelee kukusanya Zaidi taarifa ambazo , siku tukimtumia Edna lazima awehuke na zimfanye kuzidi kuweka umbali wa kimahusiano na Roma”Aliongea Nadia.

“Sawa bosi”

“Vipi kuhusu Najma?”

“Bado Roma hajakutana na Najma Bado na kwa ninavyoona hawawezi kuonana hivi karibuni”

“Hata wasipoonana tunazo zile picha zingine wakiwa wamekumbatiana najua Edna hafahamu kama Roma na Najma wanafahamiana na hii ni kete nyingine”Aliongea Nadia huku akionyesha hali ya kufurahia , mwanadada huyu alioneysha nia ya kuyavunja mahusiano yaliokuwepo kati ya Roma na Edna.

“Bosi mpaka sasa nashindwa kujua kwanini upo ‘obsessed’ na huyu mwanuame kwani kwangu ni wa kawaida sana”Aliongea Evansi.

“Hupaswi kufikiria sana Evans najua hisia zako juu yangu , lakini mimi nampenda Roma na nnikuwambie ni mtu ambaye hata mtokee Evansi ishirini niwaunganishe pamoja hamuwezi kumfikia Roma , unaweza kwenda”Aliongea Nadia na Evansi hakutaka kubakia hapo , licha ya kwamba maneno ya Nadia yalikuwa yakimuumiza lakini hakutaka kuonyesha hali hio mbele ya Nadia.

****

Roma hakuwa na jinsi kabisa , aliona kama kweli Sophia atakuwa uwanja wa ndege , basi anapaswa kwenda kumtoa, lakini licha ya hivyo alikuwa akiwaza akishamtoa atampeleka wapi.

“Nitajua mbele kwa mbele”Aliongea Roma huku akizidi kukanyaga pedeli kuelekea Gongo La mboto.

Dakika chache mbele alikuwa akiingiza gari sehemu maalumu kwa ajili ya maegesho na baada ya kuzima gari yake alitoka na kutembea kuelekea jengo la Terminal 3.

Roma baada ya kuingia ndani ya hili jengo alianza kuangalia kushoto na kulia kumtafuta Sophie , ni kama bwana huyu hakuwa akiamini maneno ya Balozi , alijongea kuingia ndani Zaidi sehemu ya mapumziko kwa abiria na hapa ndipo alipojikuta akisimama baada ya kumuona mwanadada mrembo aliekuwa ameketi kwenye viti akiwa hana habari kabisa , huku akiwa ameshikilia simu yake.

Katika macho ya Roma Sophia alikuwa ni mrembo sana , tena mrembo ambaye alikuwa akimkaribia Edna lwa asilimia themanini , lakini Roma katika akili yake alijiambia kabisa hawezi kuwa na mahusiano na Sophia kwani mke wake na huyu Sophia ni ndugu hata kama sio wa damu , hivyo aliona ugumu kwenye swala hilo na ndio maana alikataa katakata maneno ya balozi kuhusu kumuoa Sophie.

Roma alijongea taratibu kumsogelea Sophie huku akinwangalia msichana huyu , Sophie kwa muonekano tu alionekana kuwa mdogo , licha ya kwamba muonekano wake ulikuwa umepevuka , lakini sura ya utoto haikujificha kwa Sophia.

“Sophia?”Aliita Roma na kumfanya mwanadada huyu ainue macho na kumwangalia Roma, na walipokutanisha macho yao alijikuta akitoa tabasamu la aibu.

“Hades!!”Aliita Sophia huku akiwa na aibu za kike na kumfanya Roma atabasamu , alijiuliza huyu msichana kwa aibu hizi aliwezaje kukaa hapa ndani kwa Zaidi ya masaa kumi , au balozi kuna kamchezo anamfanyia , ila kwa wakati huo hakutaka kuwaza sana kwakua yupo hapo kwa ajili ya kumchuku Sophia.

Upande mwingine , wakati Roma anaingia hapa ndani ya uwanja wa ndege , mita kadhaa kutoka alipopaki gari yake kulikuwa na gari nyingine ya Forester , ndani ya gari hii alionekana Faridi mlinzi wa karibu wa mstaafu jenerali wa jeshi akibonyeza simu yake na ndani ya sekunde aliweka sikioni.

“Nipe ripoti Faridi?”

“Mr Roma nimemuona ndani ya haya maeneo , inaonekana ndio kafika kumchukua Sophie”

“Vizuri sana, endelea kufatilia ni wapi atampeleka haha.. nina hamu ya kujua Faridi”

“Lakini bosi jambo ambalo tunalifanya naona sio sawa kwani Edna na sophia ni ndugu”

“Faridi unanionaje, kungekuwa na tatizo nisingeruhusu Sophie kumsogelea Hades ,Balozi anajiona mjanja kwa kufanya mambo pasipo kunishirikisha , ila mimi najua kila kitu ,wewe nipe kila hatua wanayofikia”Aliongea Jenerali huku akionesha furaha kwenye simu na Faridi alipumua na kisha akamjibu sawa mkuu wake.

Baada ya kama dakika tano kupita , alimuona Roma na Sophie wakilisogelea gari ambalo Roma amekuja nalo.

“Sophia baba yako amekuambiaje kuhusu maamuzi yangu?”Aliuliza Roma mara baada ya kuweka mabegi kwenye buti ya gari.

“Ameniambie una mke tayari na huna mpango wa kuongeza mke wa pili”

“Sasa kama umelifahamu hilo kwanini upo hapa Tanzania ili hali unajua kuwa siwezi kuwa na mahusiano na wewe?”

“Lakini mimi nataka kuishi na wewe hata kama tusiwe wapenzi , I am full of curiosity abaout you Hades”Roma alijikuta akishangaa lakini pia kuona huyu mtoto anafikiria nini , kwani watawezaje kuishi pamoja bila ya kuwa na mahusiano.

“Utaishije na mimi ikiwa hatuna mahusiano?”

“Sister Edna ni dada yangu licha ya kwamba hanijui ila mimi namjua”

“Sijakuelewa bado”

“Hades unaonaje ukinitambulisha kama mdogo wako , mimi ninachotaka ni kuishi karibu na wewe”Roma alijikuta kichwa kikitaka kumpasuka alikuwa akiwaza hawa wanawake wananini juu yake.

“Sophia nikuambie tu msimamo wangu upo pale pale mimi na wewe hakiwezekani kitu , ila nitakufanya ndugu yangu kwa muda utakaa na Edna na hakikisha unakuwa upande mzuti na yeye akupende na baadaye tutamuambia wewe ni nani na kama atakukubali kama mdogo wako sawa akikataa utaondoka”Aliongea Roma na kumfanya Sophia atabasamu , hakudhania mambo yatakenda namna hiyo.

“Sawa Bro Hades”Alliongea Sophia na kumfanya Roma atamani kucheka , yaani alimuona Sophia kuwa mpole lakini akianza kuongea upole unaisha kabisa.

Roma kazi alioona imebaki kwa wakati huo ni kwenda kumdanganya Edna kwamba Sophia ni ndugu yake.

“Licha sipendi kuongea uongo ila kwa sasa sina jinsi , Ngoja Sophia akaishi na sisi atakapozeana na Edna nitamueleza ukweli wote”Aliwaza Roma na kukanyaga pedeli, na aliendesha kwa muda mfupi tu Sophia alikuwa ashalala muda mrefu na alionekana kuchoka mno na Roma alimuonea huruma Sophia.

“Sophia mimi ni kaka yako kuanzaia sasa sawa , na utamuheshimu Edna kama wifi yako na umetokea Marekani ,Michigani”Aliongea baada ya kumuamsha

“Bro kwanini nitokee Marekani sio hapa Tanzania?”

“Kwasababu Tanzania sina familia na Edna anafahamu hilo”

“Kwahio Bro Roma ndugu zako wapo Marekani?”

“Ndio ila ni familia niliolelewa , usiulize maswali mengi”

“Sasa kuhusu Kiswahili je?”Aliuliza na ni kama Roma alikuwa anakumbuka sasa kumbe Sophie alikuwa akizungumza Kiswahili na hii ingeleta maswali kwa Edna na muda wote wakati wakiongea walikuwa wamesimama nje ya geti Kigamboni na Geti lilikuwa limefunguliwa muda mrefu tu.

“Bro si umesema umelelewa Marekani?”Aliuliza Sophie mara baada ya kumuona Roma anafikiria sana na Roma aliitikia kwa kichwa.

“Na vipi ulimwambia Siter kuhusu familia iliokulelea?”Hapo Roma ni kama alikumbuka ni kweli hakumwambia Edna ni familia gani iliokuwa ikimlea huko Marekani.

“Sijamwambia , umepata wazo gani?”

“Okey Hades! Unaonekana hata huna akili za kutunga uongo ,Script yetu itakuwa rahisi, Mimi Sophia niliishi Tanzania kabla ya kwenda kuishi nchini Marekani “

“Ndio ushamaliza hivyo?”

“Ndio Bro hapo utamalizia au hujaelewa mpaka hapo?”Roma alijikuta akitoa tabasamu la uchungu kwani kwa namna ambavyo Sophie alikuwa akiongea ni kama walikuwa wamefahamiana miaka kadhaa nyuma.

“Elezea nikuelewe sasa mpango unakaa vipi , nikwambie tu mke wangu ana akili sana na hadanganyiki kizembe kwahio ni bora uongo wako ukanyooka na ukafanana na ukweli”Sophie alijikuta akijisikia Vibaya kwa namna ambavyo Roma anamsifia mke wake.

“Hapo ni rahisi tu unanitambulisha kama mtoto wa Baba mdogo kwa upande wa familia iliokulelea huko Marekani na niliishi na familia yangu Hapa Tanzania kabla ya kuhamia nchini Marekanni”Roma hapo alijikuta akimuelewa Sophia.

“Sikia huu uongo utadumu kwa muda mchache tu , misheni yako ni kuhakikisha Edna anakupenda kama mdogo wake na tutamuambia ukweli sawa , ukishindwa nitamuambia ukweli na akikufukuza au akitufukuza nitakuwa sina msaada tena,Misheni yako ni ya miezi miwili tu”

“Bro hilo hata usiwaze mimi ni rahisi kupendeka”Aliongea Sophie na kumfanya Roma asiongee kitu na kuingiza gari ndani.

Hades nitakufanya unanipenda kwa namna yoyote ile na utanianza mwenyewe”Aliwaza Sophie aliekuwa akitabasamu wakiingia ndani ya jumba hili.

“Nipe ripoti Faridi?”Ilisikika upande wa pili wa simu Faridi akiwa amesimamisha gari mita kadhaa kutoka iliponyuma ya Roma.

“Kamleta nyumbani kwake”

“Hahahaha…,Asante kwa kazi nzuri Faridi unaweza kurudi sasa , sisi tutakuwa ni wenye kuangalia nini kitaendelea Kama Edna akikubali kupokonywa mume ni shauri yake , akiweza kumfanya Sophie kama Mdogo wake hilo pia ni juu yake”Faridi aliitikia huku akishindwa kuelewa ni mpango gani Mzee Athumani anauandaa , maana alishindwa kung`amua kwa wakati mmoja.

Edna leo hii alikuwa ameketi sebuleni akiangalia Runinga huku Bi Wema akiwa bize kuandaa chakula na leo hii haikuwa kawaida , kwani walikuwa wamechelewa kidogo kupika ,kwani muda huo ilikuwa ya pata saa mbili na nusu za usiku na ratiba za kumaliza kula zilikuwa ni saa mbili.

Wakati Edna akiwa ameweka umakini kwenye taarifa ya habari mara mlango ulisukumwa na Roma na kumuona mume wake wa mkataba akiwa na mabegi, alishangaa kwanini Rmma karudi usiku na mabegi , lakini wakati akiwa amemkodolea macho Roma aliekuwa kwenye tabasamu , mara alitokea mwanamke mrembo sana aliekuwa nyuma ya Roma na kufanya moyo wake upige kwa nguvu , huku akishindwa kujielewa ni hali gani inaendelea kwenye moyo wake , kwani kwa jinsi msichana aelikuwa nyuma alivyokuwa mrembo alijihisi kuzidiwa uzuri.

“Roma nini kinaendelea?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi .
 
SEHEMU YA 104

Roma alimkaribisha kwanza Sophia mpaka kwenye masofa ya hapo sebleni , huku wakiwe mabegi pembeni, na wakati huu na Bi Wema alikuwa ashatoka jikoni na alikuwa ameketi sebuleni wakisubiri utambulisho kutoka kwa Roma.

Roma alimuelezea Edna kama alivyokuwa amepanga na Sophia , lakini kwa Edna alijikuta akishangaa , licha ya kwamba alionekana kuelewa lakini pia alibaki na maswali , kilichomfanya asiulize sana ni kutokana na kwamba hakuwa akimjua sana Roma kuhusu maisha yake ya nyuma na alichokuwa akijua tu ni kwamba Roma amelelewa huko Marekani na kuhusu taarifa za familia iliomlelea hakuwa nayo.

“Kwahio Sophia ni kama mdogo wako?”Aliuliza Bi Wema mara baada ya kuelewa utambulisho.

“Ndio Bi Wema ,Sophia ni mdogo wangu na ujio wake Tanzania ulikuwa wa ghafla sana, kwanza kanipigia akiwa tayari kashafika na sikutaka akaishi hotelini ukilinganisha na wema ambao familia yao imenitendea”Aliongea Roma kwa kudanganya na Sophia akamwangalia Roma na kujiambia kumbe Hades anajua kudanganya.

“Miss nadhani ni jambo zuri kama tutaishi na Sophia kwa muda , isitoshe Roma ni mumeo na ni sehemu ya familia”Aliongea Bi Wema Mzungu wa Roho.

Ukweli Bi Wema licha ya kwamba Edna na Roma walikuwa ni wanandoa wa mkataba lakini kwenye moyo wake alikuwa ashamkubali kabisa Roma kuwa mume wa Edna. Na alitaka na Edna pia amchukulie Roma kama mume wake , kitendo cha Roma kumleta Sophia hapo ndani ya familia alikipenda , aliona kama Edna ataendelea kukutana na baadhi ya familia ya Roma basi ukaribu wao utaongezeka.

Edna alimwangalia Roma ambaye alikuwa hana wasiwasi kabisa na kisha akageuza macho kwa Sophia na kumkagua juu hadi chini , Edna alimuona Sophia mrembo sana , na tofauti kati yake na yeye ilikuwa ndogo, na kwake ilikuwa afadhari baada ya kujua wawili hao ni kitu na mdogo wake,maana dakika kadhaa nyuma moyo wake uliogopa mpaka mwenyewe kushindwa kujielewa.

“Okey! Haina sababu ya Sophie kwenda kuishi sehemu nyingine wakati wewe ni sehemu ya familia yake”Aliongea Edna na kumfanya Roma atabasamu.

“My Wife licha ya kwamba umrembo kuliko wanawake wote ndani ya dunia hii , lakini pia umebarikiwa busara”Aliongea Roma na Edna alitabasamu , licha ya kwamba alijua Roma anampamba tu kutokana na kukubali kwa Sophia aishi hapo , ila ndani ya moyo wake aijisikia vizuri kusifiwa mbele ya Sophia.

“Sister Edna nitakuwa mtiifu na nitahakikisha sikukasirishi”Aliongea Sophie na kumfanya Edna ashangae , kilichomfanya kushangaa ni kwamba kwenye maisha yaaake hakuwahi kuitwa dada na leo ilikuwa mara yake ya kwanza.

Bi Wema alijikuta akitoa tabasamu baada ya kumuona Edna alivyobadilika baada ya kuitwa dada, na alishindwa kumuelewa Sophie kafikiria nini kumuita Edna dada na sio Wifi , ila hakutaka kujali sana kwanza kwa jinsi Sophie alivyokuwa mzuri aliona ni sawa tu kwa hao wawili kuitana dada.

“Roma unaonaje ukimwandalia Sophia chumba chake?”

“Bi Wema chumba kipi kitamfaa??”

“Nitamwandalia mimi”Aliongea Edna na kisha alimwangalia Sophie kwa kumpa ishara amfuate , huku Roma na yeye akinyanyuka kusaidia kubeba mabegi kwenda juu.

Chumba cha Sophia kilikuwa kikiangaliana na chumba cha Edna , Roma aliingiaza Mabegi na kuwaacha dada na mtu wasaidiane kuandaa chumba.

“Kesho tutaenda kununua baaadhi ya vitu ambavyo unataka viwekwe kwenye chumba chako”Aliongea Edna na Sophie alimwangalia Edna.

“Thank you Sister”Aliongea Sophie na kumfanya Edna atabasamu , hakujua kwanini Sophie kaamua kumwita Dada ila alipenda, kwani alimuona Sophia kuwa M’cute’.

Saa tatu kamili Bi Wema alikuwa ashamaliza kupika na Edna alimsaidia kuandaa chakula mezani , Sophie na yeye alikuwa ashamaliza kuoga na kubadilisha mavazi na alishashuka chini na kukaa kwenye masofa , baada ya dakika kadhaa za kuandaa , mtaalamu Roma alishuka chini kwa ajili ya kula chakula kwani njaa pia ilikuwa ikimnyanyasa.

Bi Wema alitabasamu baada ya kuona familia imeongezeka mtu mmoja ,Mama huyu hakuwa akipenda familia kuwa na watu wachache , alipenda familia ya watu wengi.

“Sophie elimu yako ni ya levo gani?”Aliuliza Edna na Roma alimwangalia Sophie ,maana licha ya kwamba amemleta hapo ndani lakini hakuwa na taarifa zozote kuhusu elimu ya Sophia.

“Nina Masters ya Uchumi”

“Kweli!!”

“Ndio Sister Edna,Mbona kama hauniamini”

“Hapana nimeshangaa , unaonekana mdogo kwa levo ya elimu yako”

“Nina ‘skills’ nyingi ambazo zitakushangaza Sister”

“Kama zipi?”

“Nina Mkanda wa Bluu (Blue Belt) kwenye mchezo wa Kung Fu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma atake kutema chakula alichokuwa akitafuna na Sophie alimwangalia Roma na kutabasamu.

“Blue Belt kwenye ‘Kung Fu’ ndio mkanda gani?”Aliuliza Edna kwani hakuelewa na Roma alitaka kumsikiliza Sophie atakavyojibu.

“Ni levyo ya kati ya mafunzo ya kimapigano ya kichina ni sawa tu kusema levo ya uvumilivu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma amwangalie na Sophie ni kama alifanya makusudi alimwangalia pia.

“Ilikuwaje sikufikria hili kabla , haikuwa kawaida kwa Sophie kuweza kuvumilia lile baridi kwenye ile Mashua”Roma aliwaza.

Ukweli ni kwamba kwa namna ambavyo Sophie na Shirani walivyokuwa wamepakiwa kwenye ile mashua ,lakini pia na kwa jinsi ambavyo ‘Pasific Ocean’ ocean ilivyokuwa na baridi ukijumlisha na barafu ambazo Roma alitengeneza isingekuwa rahisi kwa mtu wa kawaida kuvumilia ile baridi, na ni mtu mwenye mazoezi maalumu tu ya kimwili ndio ambaye alikuwa na uwezo huo.

Roma palepale alitengeneza miale ya rangi flani kwenye macho yake na kummulika Sophia pasipo mtu yoyote kugundua na hapo ndipo alipothibitisha ni kweli Sophia alikuwa na uwezo wa kimapigano kwa levo aliosema.

“Kwa hio Miss Sophie unajua kupigana?”AliongeaBi wema ambaye muda wote alikuwa akisikiliza lakini mazungumzo yalivyofikia hapo alijikuta akikosa uvumilivu na kuuliza.

“Ndio Bi Wema nina uwezo wa kupambana na watu kumi kwa wakati mmoja ambao hawana mafunzo ya kimapigano”

“Mimi siamini”Aliongea Edna na kumfanya Sophie atabasamu.

“Nitakuonyesha picha tukimaliza hapa”Aliongea Sophie na kweli hakutaka kuamini pasipo kuona , kwani kwa mwonekano wa Sophie , aliona ni mdada mrembo sana kuwa na uwezo wa kimapigano.

“Ujuzi wako mwingine ni upi?”Aliuliza Edna.

“Najua pia kuimba na sio kujua tu napenda kuimba na ndio maana nimerudi Tanzania nataka nijikite kwenye usanii”Aliongea na kumfanya Edna awe ni kama haamini hivi.

“Kwahio umerudi tu kwa ajili ya kuwa msanii, na kwanini usiimbe Marekani ukaja Tanzania?”

“Kwasababu napenda Bongo Fleva”Aliongea na kumfanya Edna aelewe , aliona pia sio jambo baya kwa mtu kupenda kufanya kile anachopenda.

Baada ya kumaliza kula chakula Sophie alienda na kuleta picha na kuanza kumuonesha Edna na Bi Wema , walionekana tayari washazoeana na Roma aliekuwa akishuka kutoka juu akiwa ameshikilia funguo za gari yake aliishia kutabasamu moyoni.

“Mafunzo ya Kung Fu yanaonekana kumfanya Sophie iwe rahisi kuwafanya watu waliokaribu yake kumzoea”Aliwaza Roma na kuwasogelea .

Roma alitoa taarifa kama anatoka na Edna hata hakujisumbua kugeuka Zaidi ya kunyoosha mkono tu kuitikia na Roma hakujali sana , alipanga siku hi ya leo akamtembelee mchepuko wake Rose kwani ni muda kidogo hakuwa amemtembelea tokea watoke Kisarawe , aloitaka kujua ni nini kilitokea baada ya pale.

Dakika chache tu Roma alikuwa ndani nya Mbagala , alinyoosha moja kwa moja mpaka ndani ya eneo la Club B na kuegesha gari yake , leo hii ndani ya hili eneo kulikuwa na watu wengi kidogo kutokana na kwamba magari hapo ndani yalikuwa mengi kiasi cha kumfanya Roma ashangae kidogo , kwani ilikuwa sio wikiend.

Roma aliingia ndani ya hili eneo ambalo lilikuwa limechangamka huku likiwa na harufu mchanganyiko za bia na Marashi.

“Hubby!!!”Aliita Rose baada tu ya Roma kuingia hapa ndani, Rose alikuwa amependeza sana usiku huu , akiwa amevalia suruali yake ya kitambaa rangi ya samawati pamoja na blazia nyekundu iliokiacha kifua chake wazi.

“Bebi Rose nimekumisi sana”Aliongea Roma mara baada ya kukumbatiana na Rose pasipo kujali macho ya watu wengi yaliokuwa yakiwaangalia.

“Nimekumisi pia mpenzi”Aliongea Rose kwa sauti yake nyororo ambayo ilimsimua Roma na kisha wakaachiana.

“Kama umenimisi mbona huajanitafuta?”

“Namuogopa mkeo”Aliongea Rose na kumfanya Roma atabasamu .

“Rose mbona leo kuna watu wengi hapa kuna nini?”Rose alitabasamu na kisha akamwangalia Roma.

“Tunasherehekea ushindi leo , unaowaona hapa wengi ni vijana wangu,”Aliongea Roma huku Rose akimshika mkobo Roma na kumuongoza upande mwingine.

Club B ilikuwa ikipendwa pia na matajiri kutokana na mgawanyo wake , kwani ilikuwa pia na upande wa VIP(Very important person), upande huu wa VIP ulikuwa pia ukihusisha makutano ya kibiashara hususani wafanyabiashara wa madawa ya kulevya ambao alikuwa wakitaka kuongea maswala ya kibiashara.

“Your Majest!!!”Roma alijikuta akigeuka mara baada ya kusikia sauti ambazo alikuwa akizifahamu na hii ni baada ya kuingia upande huu wa VIP akiwa ameambatana na Rose , lakini sasa Rose alijikuta akishangaa baada ya kuwaona mabwana hawa wa kizungu wakikakamaa kama vile wamemuona kiongozi mkubwa wa nchi.

The Eagles wote ni kama walikuwa wameambizana kwani kila mmoja alikuwa hapo ndani ,huku kwa wadada wakiwa na wanaume wa kibongo na kwa wanaume wakiwa na warembo wa kitanzania , Roma aliwaangalia mmoja mmoja na kugudua kuwa mtu pekee ambaye amekosekana ndani ya hilo eneo alikuwa ni Deigo na Btam.

“Bebi mbona wako hivyo”Aliuliza Roma huku akiwaangalia hawa vijana walivyobadilika ghafla.
























NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 105

Roma hakuona haja ya kumficha tena ili hali wanajeshi hawa wapo ndani ya hili eneo lakini pia Rose alikuwa ashaona namna ambavyo wanajeshi hawa wamebadilika , lakini pia aliona anasababu ya kumwambia Rose kutokana na kwamba yeye ndie aliemsadia makazi ya vijana wake hapa Tanzania pasipo kuuliza sana maswali.

“Mnaweza kuendelea na Starehe yenu vijana msinizigantie”Aliongea Roma na kuwafanya vijana hawa washushe pumzi kwani hawakuwa ni wenye kutegemea uwepo wa Roma maeneo hayo .

Ukweli ni kwamba The Eagles baada ya kufika Tanzania hawakupenda kujifungia ndani tu , walitamani pia kula bata kama binadamu wengine , na katika sheria za jeshi lao , hawakuwa pia wakizuiwa kula bata kisheria ,hivyo hawakuona tabu ya kutafuta warembo na wanaume pia, lakini sasa k katika kuchagua maeneo ya kula bata hawakutaka maeneo ambayo walidhania watagongana na Mfalme Pluto.

Na kwa kulijua hilo walianza kutafuta maeneo ya mbali na anapoishi Roma na katika tafuta yao walijikuta wakiangukia ndani ya Club B, huku wakidhania kuwa Roma hawezi kufika hayo maeneo , lakini pia walipendezwa na amsha asmha ndani ya Club hio.

“Darling ! Unamaanisha unamiliki wanajeshi?”

“Bebi Rose cha kushangaa nini sasa hapo , si kama wewe tu unavyomiliki kundi la Tembo”

“Hata kama mpenzi , lakini kumiliki wanajeshi sio jambo dogo , tena wakizungu lazima niwe na maswali”Aliongea Rose huku akiwa amemlalia Roma kwenye mapaja wakiwa wameketi kwenye masofa , huku Roma akicheza cheza na nywele za Rose.

“Unakumbuka mara yetu ya kwanza mimi na wewe kukutana?”

“Siwezi kusahau , nadhani ndio siku ya kipekee sana kwenye maisha yangu”

“Sasa ile ndio siku yangu ya kufika hapa Tanzania kupitia uwanja wa ndege wa Mwanza na mtu wa kwanza kuongea nae hapa Tanzania ni wewe”Rose alishangaa hakuwa akilijua hilo.

“Kwahio ulitokea wapi?”

“Nilitokea Uingereza”

“kwahio hawa wanaeshi [ia wametokea Uingereza”

“Sehemu waliotokea ni mbali na Uingereza , siku moja nitakupeleka”Aliongea Roma na kumfanya Rose ajinyanyue na kumkumbatia Roma.

Rose hakutaka kuuliza maswali mengi , kwani alijiambia kwa kila nafasi ambayo Roma atakuwa anamkumbuka atakuwa anaitumia vyema kufanya nae mapenzi , ili hata wasipoonana kwa muda mrefu asiwe na hamu tena.

Walifanyana kwa Zaidi ya Masaa matatu na hii ilimfanya Rose kuchoka mno na hawakutakia kubaki hapo ndani Bar, walihamia nyumbani kwa Rose na Roma hakupanga kabisa kurudi nyumbani usiku huo.

“Vipi ulimalizaje swala la Baba yako?”Aliuliza Roma uda wa asubuhi mara baada ya kupiga cha asubuhi , sasa Roma alikuwa akinywa chai kabisa kwani hakuwa na mpango wa kurudi nyumbani , alipanga aende moja kwa moja kazini.

“Kundi lake kwa sasa lipo chini yangu , nimemfilisi mali zak zote , ila kwenye kumuua nilishindwa kwani licha ya kwamba ni adui yangu , lakini pia ni baba yangu”Aliongea Rose.

“Kwahio umeamua kufanya nini?”

“Mpaka sasa ninavyoongea yupo Kisiwa cha Heligoland”

“Unamaanisha Ujerumani?”

“Ndio babe”Roma alijikuta akishangaa kwani alikuwa akikifahamu hiki kisiwa sana kwa kuwa mbali.

“Nimeamua kumpeleka huko akaanze maisha upya , sijamuachia hata shilingi licha ya kuagiza vijana wakamuweke huko”

“Ni wazo zuri pia , nadhani atazeekea huko na hatoweza kupata nafasi ya kurudi Tanzania”

“Ndio na nimehakikisha hana aina yoyote ya mawasiliano na watu wa Tanzania kwenye kundi lake”Aliongea Rose na kumfanya Roma afikirie kidogo.

“Rose najua mpaka sasa biashara yako imekuwa kubwa na ukubwa wa biashara yako ndio wingi wa maadui, unaonaje ukitumia wanajeshi wangu”

“Lakini bebi sijui hata kwasababu gani umewaleta Tanzania kwanini niwatumie?”

“Sababu ya kuwaleta Tanzania ni kutokana na kwamba kitendo cha mimi kuwa karibu na nyie kinawaweka kwenye uhatari kutokana na upande wangu wa pili ambao watu wengi hamuufahamu na nikwambie tu , mpaka sasa nina maadu kila nchi ndani ya hii dunia”Rose alishangaa.

“Yeah! Usishangae , nina maadui wengi na ndio maana nimewaingiza The Eagles ndani ya Tanzania na madhumuni makuu ni ili wanisaidie kugundua watu wabaya wanaongia(Detect) ndani ya Tanzania”

“Mpenzi sijui historia yako ya nyuma , lakini mimi nipo tayari kukabiliana na maadui zako muda wowote, ila kwa mkeo sidhani kama ataweza”

“Ndio maana nimewaleta hapa nchini, kitendo cha mimi kuona na Edna ni Dhahiri sasa maadui zangu watakuwa wanafahamu udhaifu wangu na watamtageti, hivyo napaswa kumlinda pia”

“Kwahio umewaleta kwa ajili ya Edna tu?”Aliuliza Rose kwa wivu na Roma alitabasamu na kumfinya.

“Sijawaleta kwa ajili ya Edna pekee na ndio maana nataka wakusiadie hata kuwafundisha mapigano vijana wako ili wawe na ujuzi”Aliongea Roma na Rose aliitikia.

“Nitatafuta nafasi ya kukupeleka kwenda kuonana na mkuu wa kikosi ,Diego ,ili nikutambulishe”

“Sawa Mpenzi,Kunywa chai unaachelewa la sivyo mkeo hatokupandisha cheo”

“Bebi Rose mke wangu ashanipandisha cheo tayari”

“Kweli!!”

“Yeah!Anapanga kunifungulia kampuni niiongoze”Aliongea Roma na kumfanya Rose aone Edna anampenda sana Roma maana mpaka kuwaza kumfungulia kampuni sio swala dogo.

“Kwa hio Mpenzi ukishakabidhiwa hio kampuni si utakuwa na maamuzi ya juu kabisa?”

“Ndio , ila sinampango wa kufanya kazi nitagawa majukumu kwa wasaidizi wangu , mimi kukaa ofisini , kufanya vikao na kuandaa nyaraka kutanichosha sana , ni bora unipe kazi ya kuilipua Marekani”Rose alijikuta akitabasamu.

“Bebi unaonaje nikiwa muewekezaji kwenye kampuni yako?”

“Unataka kuwekeza?”

“Ndio ukweli ni kwamba licha ya kwamba kikundi changu kinajihusisha na Madawa ya kulevya , lakini hii biashara siipendi na napanga niache kabisa , licha ya kwamba jina la kundi langu litabaki na kikosi kizima , lakini nataka niwe tofauti na makundi mengine, nataka niwekeze kwenye biashara halali niachane na uuzaji wa madawa ya kulevya , lakini licha ya kwamba nina pesa nyingi , lakini mpaka sasa nimekosa mahali sahihi pa kuziwekeza zijiongeze , ila kwasababu unakwenda kukabidhiwa kampuni nataka tuunde umoja, nitawekeza kwa siri pasipo ya mkeo kujua”Aliongea Rose.

“Kwahio unataka kuwekeza?”

“Ndio najua biashara ya burudani kwa Tanzania kwasasa haipo sana vizuri , ila kama utakuwa na mipango mizuri na kuitangaza kimataifa itaweza kukua haraka na faida kuwa kubwa , licha ya kwamba inaweza isiwe rahisi lakini naamini itatengeneza faida” Roma alitingisha kichwa na kuona ni jambo sawa tu kwa Rose kuwekeza kwenye kampuni, kwani pia hio itafanya kampuni kuimarika kwa upande wa kifedha.

“Umefikiria vizuri inaonekana mpenzi wangu baadae untakuja kuwa mfanyabiashara mkubwa”Aliongea Roma na kumfanya Rose atabasamu.

“Roma nataka siku tupigane?”

“Hahaha.. Rose najua una mafunzo ya kimapigano , lakini hata nisitumie uwezo wangu na uunganike na kikosi chako hamuuwezi kupambana na mimi”

“Hubby! Unajua ni kiumbe gani kina nguvu sana duniani?”Aliuliza Rose na Roma alitingisha mabega kwamba hajui.

“Kiumbe chenye nguvu sana duniani ni Mwanamke , Sisi kila mwezi tunableed’ lakini bado tunaonakena kuwa na nguvu , hivyo hata tukipigana siwezi kukubali unishinde kirahisi”Roma alitabasamu

“Hehe… Bebi Rose unatakiwa kujua mpenzi wako mimi sio wa kawaida , wanaume wengine wanaweza kulinda nyumba ili wezi wasiingie ndani kuiba ila mimi nahakikisha nalinda heshima yangu kitandani”

“Muone sasa ..mimi sijui hayo ila ninachojua wewe mwanaume ambaye huna aibu”Aliongea huku akimpokonya kikombe.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi asubuhi wanafamilia wanne yaani Bi Wema , Roma ,Sophie na Edna walikuwa mezani wakijipatia chai ya asubuhi nzito ambayo iliandaliwa na Sophia na Bi Wema.

Roma alionekana asubuhi hii kufurahia kweli chai hio , kwani alikuwa akila kwa spidi kubwa mno kiasi kwamba ni kama kuna mtu aliekuwa akishindana nae kula, Edna alijikuta akimwangalia Roma namna anavyokula na kujikuta akishindwa kuvumilia.

“Roma kula taratibu bwana , unakulaje kama mbuzi”

“Kama mimi ni mbuzi wewe utakuwa majani”Edna alijikuta akimpotezea kwani aliona ishakuwa tabia ya Roma , huku Sophia na Bi Wema waliokuwa pembeni wakiangalia wanandoa hawa walivyokuwa wakiongeleshana.

Sophia kwanza alishangazwa na maisha ya Roma na Edna , kwani hakutegemea wanandoa kuishi vyumba tofauti tokea afikie hapo , kuna muda alijiuliza labda ni kutokana na kwamba kuna migogoro kati yao , lakini alikaa Zaidi ya siku mbili kwenye hio familia na Roma na Edna hawakuonekana kulala pamoja na hili halikumhuzunisha ila lilimfurahisha, lakini sasa kwa macho yake jinsi alivyokuwa akimwangalia Roma na Edna aliona kuna kitu ambacho kinaendelea kwa hawa wanandoa , kwani licha ya kwamba walionyesha hali ya kuwa mbali kihisia ila aliona muunganiko ambao unaweza kuwa mgumu kwake kuuvunja na sio kwa Sophia tu ,hata Bi Wema alishaanza kuona tabia za mabadiliko za Edna tokea Roma afike hapo ndani kwenye familia , alimuona Edna akianza kubadilisha baadhi ya tabia zake ambazo alikuwa ashaanza kuzizoea na aliona kabisa Edna alikuwa akifanya makusudi tu lakini ana mapenzi na Roma.

Wakati Roma akiwa anaendelea kula pasipo kujali macho ya Edna , Simu yake iliingia meseji kwa kutetema ndani ya mfuko wake , aliitoa na kuangalia ni nani ambaye katuma ujumbe asubuhi hio siku ya jumamosi.

“Anko Roma leo usiku nafungua biashara kwa pesa ulionikopesha unaonaje ukiwa mteja wangu wa kwanza”Ilikuwani meseji kutoka kwa Yezi na Roma leo alimkumbuka, kwani zilikuwa zimepita takribani siku tatu tokea aonanae na Yezi, alitabasamu na kisha akaweka kijiko chini na kujibu.

“Okey saa ngapi utafungua, nije niweke Baraka”

“Saa mbili kamili”

“Okey nitafika”Alijibu Roma huku akitabasamu m hakuelewa kwanini anatabasamu , sasa wakati Roma anaendelea kuchati Edna alikuwa akimwangalia muda wote na kwa jinsi ambavyo alimuona Roma anachati, alijua tu ni mwanamke na hakujua ni mwanamke yupi kati ya wale aliokuwa akiwajua.

“Bi Wema naenda kazini , nitachelewa kurudi leo nina miadi na mtu usiku”Aliongea Edna huku akinyanyika na kuchukua mkoba wake.

“Miss lakini leo ni wikiend , tukuletee chakula mchana?”Aliuliza Bi Wema huku Roma akiendelea na kunywa chai yake bila habari hakuona utofauti wowote.

“Nitakula huko huko usiniletee na usiku msinihesabu”Aliongea na kutokomea nje na ni mvumo wa gari tu uliosikika kwenye masikio ya Bi wema na Roma pamoja na Sophie.

“Bro ila una mke ana wivu”Aliongea Sophie na kumfanya Roma amuangalie kwani hakuelewa alichokuwa anamaanisha.

“Unamaanisha nini Sophie?”

“Hahaha..yaani unashangaza kwakweli , unashindajwe kujua mabadiliko ya mkeo”

“Ndio Roma sidhani kama Edna ana miadi ya kuonana na mtu siku ya leo”Aliongea Bi Wema na kumfanya Roma asielewe vizuri.

“Mkeo alikuona unavyochatika na kisimu chako cha Bei Rahisi , huku ukiwa na tabasamu nje nje , yaani Roma unakichwa kigumu sijawahi pata ona”Aliongea Sophie na kumfanya Roma aelewe , hakujua kama kitendo cha kuchati kilimfanya Edna kuwa na wivu , lakini pia alijiuliza Wivu wa Edna umeanza lini.



SEHEMU YA 106

I990-CIA HQ USA ,VIRGINIA

Ilikuwa ni siku ya asubuhi ndani ya makao makuu ya CIA ambayo yanapatikana ndani ya jimbo la Virginia sehemu inayofahamika kwa jina la Lenley.

Sasa asubuhi hii ndani ya makao makuu haya alionekana bwana mmoja hivi wa kizungu aliekuwa akiingia ndani ya hili eneo akiwa na gari yake aina ya Benz , bwana huyu baada ya kushuka kutoka kwenye gari sehemu alipopaki , alifuatwa na bwana mwingine ambaye alikuwa akilingana nae kiumri , kwa makadirio ya miaka kama therathini hivi , utofauti wao kati ya mtu alieingia hapo ndani na aliemfata ndani ya eneo hilo la Maegesho ni unene , jamaa aliengia alikuwa ni ni mnene kidogo kutokana na mwili wake kuonesha ulikuwa ni ule wa mazoezi , lakini aliemfuata eneo la maegesho ya magari alikuwa ni mwembamba na hakua akionyesha kama mtu ambaye alikuwa ni wa kuchukua mazoezi.

“Mr Carlos ! Karibu sana kwa mara nyingine ndani ya makao makuu ya CIA , Naitwa ajenti Smith”

“Asante sana Mr Smith kwa kunipokea”

“Your Welcome , nifuate Director anakusubiria”Aliongea bana huyu huku akianza kutembea kuelekea ndani ya jengo hili kubwa ambalo kila mtu aliekuwwepo hapa ndani alikuwa bize na majukumu, ni eneo ambalo lina ulinzi mkubwa sana.

Carlos alionesha hali ya kukagua sana hili eneo , kwa muonekano wake ni kama alikuwa hajafika ndani ya hili eneo kwa muda mrefu sana , kwani alionesha hali ya kushangaa mabadiliko ya miundo mbinu.

“Kuna mabadiliko makubwa ndani ya hili eneo tokea nilivyoondoka kwenda Vietnam”

“You seems to be surprised?”

“Very Much”

“Since then we made a lot of Upgrade , All thanks to Mr President”Aliongea huku akifungua mlango mwingine upande wa kulia kwenye Korido hii ndefu iliokuwa na idara nyingi, jamaa huyu alievalia suti yake nyeusi alitabasamu na kumpa ishara ya kuingia na Carlosi akaingia.

“Carlos nice to meet you again after year`s”

“Nice To meet you too Powell”

“Karibu uketi”Aliongea Director mkuu wa kitengo cha intellijensia na kisha akaketi.

“Mr Smith nadhani kazi yako ishaisha na sasa nitaendelea na Carlos”

“Thank you Director”Aliongea Smith na kisha akatoka na kuwaacha Director na Carlos.

“Carlos kwanza ni kupe hongera sana kwa kazi kubwa uliokuwa unafanya Vietnam”

“Nashukuru sana Director”

“lakini pia nikupe pole , kwani baada ya kurudi ulipaswa kuwa likizo , lakini kutokana na kuwepo wa jambo la muhimu sana ,ambalo limetokea sikuwa na jinsi ya kukurudisha kazini, nadhani unafahamu kabisa kwamba kazi hii inahitaji kujitoa”

“Ndio naelewa Mr Powell na nadhani itakuwa vizuri sana kama utaenda moja kwa moja , kwani baada ya kupokea tu simu yako nilijua kuna jambo la muhimu na kama nisngetaka kulifanya usingeniona hapa, nadhani unanifahamu”

“Ndio nakuelewa kabisa Carlos”Aliongea bwana Poweli ambaye alikuwa mnene kidogo , mwenye nyywere nyeupe ambazo ziliashiria uzee , kwa haraka haraka alionekana kuwa na miaka sitini hivi kupanda, Poweli ni moja ya wafanyakazi wenye umri mkubwa sana kuhudumu ndani ya kitengo cha kijasusi cha CIA na hakuonesha dalili yoyote ya kustaafu.

“Okey Carlos nitakuomba usome hio karatasi kwa dakika chache kabla hatujaendelea na mazungumzo”Aliongea na kisha Carlos alichukua hio katatasi na kuanza kusoma.

“Pro Human Project !!”

“Ndio Carlos , hili ndio jambo ambalo unakwenda kulifanyia kazi nchini Bolivia”Aliongea na kisha akampatia karatsi nyingine.

“Ryan Fredrin ni moja ya watu ambao utakwenda kufanya nao kazi, kutokana na hio kambi kuwa msituni ndio maana tumekupendekeza”

“Misheni yangu ni ipi?”

“Unachotakiwa ni kuzamia ndani ya hii kambi pasipo kujulikana , ukishaingia kazi yako kubwa ni kuandaa mazingira kwa kazi ambayo ataifanya Ryani”

“And Then?”

“Kama Ryan akifanikisha wajibu wake hakikisha unamchukua mtoto , nina uhakika Ryani ataungana na mke wake kumlinda mtoto wao na pia wanaweza wakawa na mpango wa kukimbia na mtoto wao , hakikisha swala hilo halitokei, ukishampata mtoto hakikisha unamuua Ryani pamoja na Epholia”Carlosi alishangaa.

“Okey naomba kuuliza Poweli , kwa jinsi nilivyosoma hapa ni kwamba project hii inahusisha watoto kumi na mbili , kwanini mnataka mtoto mmoja tu huyu wa Ryan na Epholia?”

“Kwasababu hii project mheshimiwa 41 President alikuwa akiifatilia kwa muda mrefu sana tokea ikiwa kwenye Preliminary Stage(hatua za Mwnzo) na mafanikio yake mpaka sasa ni asilimia 8.3%, nadhani mpaka hapo unaelewa kwanini tunahitaji mtoto mmoja kati ya kumi na mbili?”Carlos alitikia kwa kichwa.

“Kwanini Ryani ahusishwe kwenye hii misheni , kwani ninaweza kwenda kumchukua mtoto pekee bila msaada wowote”Alitabasamu.

“Only parent can identify their Child without mistake. Hivyo hayahitajiki makosa, hatuna picha ya kumtambua mtoto wa Ryan, lakini tuna inntellijensia ya mtoto wa Epholia na Ryan kutengeneza asilimia 8.3 za mafanikio”Carlos alimuelewa vyema Director.

“Kwanzia muda huu misheni ishaanza na maandalizi yako ya safari yapo tayari , utaingia Bolivia kama Interpool Ajent , the Resr will depend with your efficiency , una wiki mbili tu tunahitaji taarifa kutoka kwako”

“Yes sir”Aliongea Carlos na kisha akatoka ndani ya ofisi hio.

Hii ni kabla ya kulipuliwa kwa kambi iliokuwa kule La Paz ,Bolivia kwenye ,msitu wa Amazoni.

Swali:Je Carlos alifanikiwa, tukio hilo linauhusiano gani na simulizi

Utaendelea ufahamu kadri simulizi inavyoendelea.





*****

Roma alijisikia aibu kwa namna ambavyo Sophie alikuwa amemshushua , ila hakutaka kufikiria sana , siku hii ya leo alipanga kubakia nyumbani tu.

Sophie na Bi wema walionekana kuzoeana kwa muda mfupi sana kwani walikuwa wakicheka na kumfanya Roma aliekuwa amejipumzisha chumbani kwake awasikie na aliishia kutabasamu tu kwa ujanja wa Sophia , kwani Sophia kwa kumuangalia alikuwa mpole ila akizoeana na mtu anakua muongeaji sana.

Chakula cha mchana Roma alishuka na kula kama kawaida na kurudi chumbani kuangalia runinga kupoteza poteza muda .

Licha ya Roma kutojali maneno ya Sophia juu ya wivu wa Edna lakini alikuwa akikumbuka kabisa , aliona kama maneno hayo yana ukweli basi huenda Edna ashaanza kumpenda , alikaa chumbani kwa kufikiria kwa masaa kadhaa na alijikuta akipotelea usingizini .

Roma alijikuta akija kushituka saa moja moja aliingia bafuni akaswaki na kuoga na akashuka mpaka chini sebuleni.

“Bi wema Edna asharudi?”Aliuliza Roma baada ya kumkuta Bi Wema aliekuwa bize kuangalia Runinga.

“Hajarudi bado”

“Bi Wema leo usiniwekee chakula”Aliongea Roma na kisha alipandisha juu na ndani ya dakika chache tu Bi Wema alimuona Roma akishuka akiwa amebadili mavazi , hakutaka kuuliza Roma anaenda wapi ila alikisia.

Roma alingia kwenye gari yake na kutafuta namba ya Edna na kupiga.

“Unasemaje?”Ilikuwa ni sauti ya Kibabe iliomfanya Roma atabasamu na ukauzu wa mke wake.

“Uko wapi?”

“Ofisini! Kuna nini?”

“Hakuna”Aliongea Roma na kisha akakata simu na kuwasha gari na kutoka.

Baada ya masaa kadhaa tu Roma alikuwa akiingiza gari sehemu ya maegesho kwenye kampuni ya Vexto , alimuona Chiara na John waliokuwa ndani ya eneo hili na kuwapa ishara waondoke na walitingisha vichwa vyao na wakawasha gari yao na kuondoka.

Edna alikuwa bize mno yaani haikueleweka alianza kufanyakazi saa ngapi kwani muda wote alikuwa amekodolea tarakishi yake macho huku akiwa amevaa miwani ya kumkinga na mwanga wa bluu.

Upande wa nje Monica pia alikuwepo na Roma ile anafika ndani ya hili eneo alimkuta mwanadada huyu akiwa amesinzia alionekana kuchoka kweli , na alimuonea huruma , hakutaka kumuamsha , alimpita na kuingia moja kwa moja ofisini kwa mke wake.

“Umekuja kufanya nini?”

“Edna Monica kalala , nenda kamwambie aende nyumbani , unamtesa mtoto wa watu hata kama unamlipa”Aliongea Roma huku akikaa kwenye masofa na Edna alijikuta akikumbuka kuwa Monica alikuwa amekuja nae siku hio na alikuwa amesahau kwani muda wote alikuwa amejichimbia kufanya kazi pasipo kupumzika.,aliangalia saa na kisha akatoka mpaka nje na kumuamsha Monica na kumwambia aende nyumbani.

“Malizia kuna sehemu nataka unisindikize”Aliongea Roma mara baada ya Edna kurudi na Edna alishangaa.

“Wapi nina majukumu mengi Roma”

“Wife kwanini wewe kila siku ni mwenye kuwa na majukumu unafikiri wengine hawana majukumu”Aliongea Roma na kumfanya Edna afikirie kidogo.

“Okey tunaweza kwenda nitamalizia nyumbani”Aliongea Edna na kumfanya Roma atoe tabasamu la uchungu.

Dakika chche mbele Roma alikuwa akiingiza gari ndani ya Kigamboni Pongoni Beach , mwanzo Edna aliwazia huenda Roma anamrudisha nyumbani , lakini walivyochukua barabara nyingine alishangaa kidogo lakini hakutaka kuuliza alisubiria kuona mwisho wake ni wapi Roma anampeleka.

“Wife leo ni siku yetu ya ‘Date’ aliongea Roma na kisha akamshika Edna mkono na kuanza kutembea kueleka upande wa Beach na hii ni baada ya kuegesha gari upande wa pili wa barabara.

Edna alitaka ajitoe kwa Roma ila alishindwa kwani Roma alimshika vizuri na alijiona hana ujanja Zaidi ya kufuata , watu walikuwa wakiawaangalia na kuishia kutabasamu , kwani licha ya giza , urembo wa Edna haukujificha.

Roma alijikuta akitabasamu mara baada ya kuona maboresho ambayo Yezi alikuwa ameyafanya kwenye kibanda chake cha chipsi na kutokana na leo ilikuwa ni wikiend watu walikuwa wengi wakipita pita eneo hili na Yezi aliekuwa bize, alikuwa akionekana kwenye macho ya Roma kwa umbali.

Yezi alikuwa bize mno na kumfanya roma atabasamu na kufurahishwa na juhudi za Yezi.

“Anko Roma !”Aliita Yezi baada ya kumuona na kuwasogelea.

“Sister Edna!!!”Aliita Yezi kwa mshituko

“Yezi!!!”Roma alishangaaa.

ITAENDELEA

NICHEKI WATSAPP 0687151346 NIKUPE UTARATIBU WA KUPATA MWENDELEZO , UNLESS OTHERWISE TUONANE JUMAPILI
 
Back
Top Bottom