maubusu
Senior Member
- Oct 18, 2018
- 122
- 77
Tuwaunge mkono waandishi,mimi nilimtumia 2500 kanitupia mpaka 271,sio tunalalamika tu tuwafidie muda waojiwe yeye alikuwa anatunza tu na halina athari liwepo au lisiwepo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tuwaunge mkono waandishi,mimi nilimtumia 2500 kanitupia mpaka 271,sio tunalalamika tu tuwafidie muda waojiwe yeye alikuwa anatunza tu na halina athari liwepo au lisiwepo
Vipi kuhusu lile jiwe lingine ambalo Roma aliwapa wale jamaa waliomteka Edina na Bi Wemajiwe yeye alikuwa anatunza tu na halina athari liwepo au lisiwepo
SEHEMU YA 223.
Naam ndani ya kampuni ya Edna mambo yalikuwa yakienda kama kawaida na Sasa Edna kidogo alikuwa amepunguza majukumu yake kwa kuyapunguza rasmi kwa CEO msaidizi Marko Ernest Komwe.
Edna alifanya hivyo kwa ajili ya kujikita zadi katika kazi zake nyingine ambazo zilikuwa zinahusiana na kujipanua Zaidi kibiashara huku akiacha maswala ya ndani ya kampuni yakiendeshwa na Ernest , lakini pia alitaka kuendelea kufanyia kazi swala ambalo alilipata kulifahamu kutoka kwa mheshimiwa Senga na hili ni swala ambalo lipo kwenye Flash aliopewa siku za nyuma na raisi , swala ambalo lilikuwa likihusiana na kisasi ambacho alikuwa nacho mama yake , kisasi ambacho hakikuweza kukamilika kutokana na kwamba mama yake alifariki mapema kabla ya jambo hilo kutimia.
Kwahio majukumu ya Edna ni kuhakikisha kisasi hiko kinatimia kwa namna yoyote ile na ili kufanikisha hilo aliamini alikuwa akihitaji muda wa kutosha kwa ajili ya kusuka mipango yake , alikuwa akiamini kuwa ana maadui wengi ambao wanamuangalia kwa kila hatua anayopitia , lakini swala hilo hakuwa tayari kulifanya lipunguze ile ari aliokuwa nayo juu ya utimilifu wa mpango wake.
Asubuhi ya leo mrembo huyu alikuwa ameketi kwenye kiti chake akiwaza hili na lile , ukweli alijiona kwamba siku kadhaa za nyuma kulikuwa na mambo mengi ambayo yamemfanya kutofikiria Maisha yake kwa ujumla na uelekeo ambao anauchukua ,lakini pia sura mpya ya biashara zake ambazo anakwenda kuanzisha.
Katika kichwa cha Edna mawazo yalikuwa mengi kwanza kabisa alikuwa akiwaza juu ya baba yake mzazi wa damu , alikuwa akiliwazia hili swala tokea siku ambayo alipata kujua kuwa Mzee Adebayo sio baba yake wa damu na alikuwa akijitahidi kujisahaulisha , lakini kadri alivykuwa akijitahidi hakuweza kusahau , alikuwa akimfahamu mama yake mzazi nje ndani , licha ya kwamba hawakuishi sana wakiwa Pamoja kutokana na mama yake kuwa bize na maswala ya kampuni lakini vilevile kwa upande wake kuwa bize na masomo mpaka pale mama yake kifo kumkuta Ghafla , lakini kwa machache ambayo alikuwa akifahamu kutoka kwa mama yake , aliamini baba yake huwenda akawa ni mtu ambaye yupo karibu yake kuliko ambavyo anafikiria kwani alimjua mama yake sio mtu wa kuokoteza okoteza wanaume , ni mwanamke ambaye alikuwa na sheria zake.
Mtu aliekuwa akijiita The Protector ni swala ambalo pia alikuwa akilifikiria katika kichwa chake , kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kabisa mtu huyo ni baba yake , lakini alijitahidi kupotezea hisia hizo , lakini licha ya hivyo hakushindwa kufikiria juu ya mtu huyo lakini pia juu ya baba yake mzazi.
Edna na Roma sasa ni takribani miezi mitatu Kwenda minne tokea wafunge ndoa yao ya mkataba na ni mambo mengi ambayo yametokea katikati yao, na mengi yalikuwa ya kuogofya sana , lakini licha ya hivyo wazo la kuachana na Roma baada ya miezi sita kuisha aliona ni gumu kutekelezeka , aliamini kama ataendelea na mpango wa kutimiliza kisasi ambacho bado hakujua kinahusiana na nini aliamini katika mchakato huo kutakuwa na maadui wakubwa ambao watajiinua zidi yake , hivyo anahitaji ulinzi na mtu pekee ambaye anapaswa kumlinda kwa hali na mali ni Roma peke yake.
Katika kufikia sehemu ya mawazo hayo mrembo huyu alijikuta akianza kukumbuka Maisha yake na Roma kuanzia mwanzo mpaka walipofikia , alihesabu meizi walioishi Pamoja , alikumbuka matukio yote kwanzia ya Tanzania mpaka yaliotokea Paris na alijikuta mwili wake ukisisimka.
“Roma kwasasa ashakuwa sehemu ya Maisha yangu , na sijui kama tunaweza kuachana hata baada ya miezi sita ya mkataba wetu kuisha , Mama yake anaonekana pia kunipenda na anaamini mimi ni mume halali wa mtoto wake, nadhani inanipaswa kumkubali sasa Roma kama mume wangu kihalali licha nina wasiwasi na wanawake wake aliokuwa nao, Lakini safari ya mapambano ambayo nimeanzisha inanihitaji kuwa nae kwa kila hatua kwa ajili yakufanikiwa lakini…..”Alijikuta akiishia kuwaza.
“Lakini siwezi kukubali aendelee kuwa na wanawake wengine , ilihali mimi ndio mke wake kihalali , kama nitampokea kama mume kamili jambo la kwanza ni kuhakikisha anaachana na wake zake na kuniangalia mimi tu”Alifikiria Edna , lakini licha ya kuwaza hivyo alionekana kukosa namna ya kulikamilisha jambo hilo.
Upande wa ofisi ya PR , Roma alionekana leo kuhudhuria kazini kama kawaida na alikuwa akicheza gemu kama ilivyokuwa kawaida yake , madhumuni ambayo alikuwa nayo kwa kuja kazini ni kutokana kutaka kuwaaga wafanyakazi wenzake kwasababu muda si mrefu angetakiwa kufanya kazi katika kampuni ambayo imefunguliwa na mke wake.
Wafanyakazi wenzake akiwemo Recho walionekana kuwa bize na kazi kama ilivyokuwa kawaida.
“Kamani leo mnaonaje tukikutana usiku kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo na kuwa Director wa kampuni mpya?”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma asubirishe gemu lake na kugeuka.
“Naunga mkono hoja”Ilisikika sauti ya Nasra ikiingia ndani ya idara hii na wote wakamwangalia na haikueleweka Nasra alikuwa hapo kufanya nini , lakini alionekana kupendeza , alimwangalia Roma na kutabasamu baada ya kumuona.
“Nani anapinga juu ya hili?”Aliuliza Benadetha na wafanyakazi wote walionekana kukubaliana na jambo hilo na aliebakia Roma kukubaliana na wengine.
“Roma kusanyiko ni kwa ajili yako , kama hukubaliani na sisi tutaghairisha”
“Nakubali gharama zitakuwa juu yangu, chagueni hoteli.”Aliongea Roma na kufanya wote wapige makofi.
“Kilimanjaro hoteli napendekeza”Aliongea Recho haraka haraka na kufanya wote waangaliane kwa pendekezo alilotoa Recho.
“Tina unasemaje , ushawahi kufika Kilimanjaro Hotel?”Aliuliza Recho kwa namna ya kumkeheli Tina.
“Sijawahi kufika .. umefurahi?”Aliongea Tina huku akivuta mdomo lakini Recho alionekana kutojali.
“Roma unasemaje , wewe ndio unakwenda kulipia?”Aliongea Benadetha akimwangalia Roma.
“Limepita kama wote mnataka twende Kilimanjaro Hoteli mimi sina tatizo”Aliongea Roma na kufanya Recho kushangilia.
“Muone wote tunajua hapa unataka ukapige picha tu za kuoshea mtandaoni”Aliongea Tina kwa kumshushua.
“Kama ninaenda kupiga picha wewe inakuuma nini fyuu.. unaongea kama hutopiga hizo picha”Aliongea Recho na kufanya hata Roma acheke kwa utani uliokuwepo kati ya Tina na Recho
……………….
Ni muda wa saa moja kamili , Roma alionekana kujiandaa tayari kwa ajili ya kuelekea sehemu ambayo alikuwa amekubaliana na wenzake kwa ajili ya Kwenda kuhudhuria kusanyiko kwa ajili ya kupongezwa kwa kupandishwa cheo.
Roma alishuka mpaka chini sebuleni kwa ajili ya kutondoka , Blandina mama yake Roma usiku huo hakuwepo kwani alikuwa ameshinda nyumbani kwa baba yake na alitegemewa kulala huko huko mpaka siku inayofuata.
“Wife natoka”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna aliekuwa ameketi kwenye masofa na Yezi na Sophia wakipiga Stori.
“Kama unaenda kwenye kusanyiko na wafanyakazi wa Idara ya PR na mimi naenda”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.
“Wife unauhakika unataka Kwenda?”Aliuliza Roma kwa mshangao.
“Ninaenda nisubiri , labda kama hutaki nikihudhuria”Aliongea Edna huku akianza kupiga hatua kuelekea juu kujiandaa akimuacha Roma akiwa amesimama huku akimshangaa Edna, kusanyiko lilikuwa ni la wafanyakazi wa Idara ya Public Relation, hivyo asingetegemea Edna kuhudhuria kusanyiko kama hilo , lakini swala la pili ni kwamba kama ataenda na Edna inamaanisha uhusiano wao utakuwa wazi kwa wafanyakazi wenzake ndio maana Roma alishangaa.
“Yezi chuo unaanza lini?”aliuliza Roma na kukaa kwenye Sofa akimsubiria Edna.
“ Mwezi wa kumi na moja ndio tunaanza usaili Anko…”
Yezi tokea aje hapo ndani Roma hakuwa amepata nafasi ya kuongea na Yezi kabisa na kumuuliza maswala ya chuo, licha ya kujua mipango hio.
“Umefanya maamuzi mazuri kurudi chuo, inabidi ujitahidi ili baadae uje kufanya kazi , usiwe kama Sophia alieweka vyeti kwenye kabati”Aliongea Roma na kumfanya Sophia amkate Roma jicho na kuendelea kuangalia simu yake.
Ukweli Sophia siku mbili hizi tokea Roma kurudi kutoka Ufaransa alikuwa ametulia sana , hakuwa wa kuongea sana na Roma alishindwa kujua tatizo la Sophia ni nini , ila alishindwa kumuuliza.
Edna alichukua dakika kumi na tano tu kujiandaa na kumfanya Roma afurahi kwani haikuwa mategemeo yake kwa Edna kutumia muda mfupi kwa ajili ya kujiandaa.
“Wife umevaa kawaida sana , lakini ulivyopendeza kama vile umetumia lisaa kujiremba”Aliongea Roma na kumfanya Roma aone aibu na hii ni kutokana Roma alimsifia mbele ya Sophia na Yezi.
Sophia na Yezi waliishia kuangalia Roma na Edna ambao walikuwa wakitomomea nje ya mlango , walionekana ni wenye kutamani Kwenda na wao kwenye bata la usiku.
******
Ni baada ya nusu saa Edna na Roma walionekana wakiikaribia Hoteli ya Kilimanjaro , sehemu ambayo yeye na wafanyakazi wa idara yake ndio walipanga kwa ajili ya Mkusanyiko wa chakula cha usiku.
Hoteli ya Kilimanjaro ni moja ya Hoteli nzuri za nyota tano ambazo zilikuwa zikitoa huduma ya mikusanyiko midogo na mikubwa, Benadetha ndio alipewa kadi ya benki ya Roma kwa ajili ya kuandaa sehemu maalumu kwa ajili ya mkusanyiko wao huo mdogo ambao wameandaa.
Na muda ambao Roma na Edna wapo njiani Recho , Tina Benadetha na wafanyakazi wengine wawili wa kike walikuwa washafika tayari ndani ya hoteli hio na walikuwa washapata eneo maalumu binafsi ndani ya hoteli hii kwa ajili ya mkusanyiko wao.
Na walionekana wakipiga stori za hapa na pale na kufanya eneo lote kusikika sauti zao , Nasra alievalia gauni zuri la kupendeza aliingia ndani ya chumba hiko kikubwa na alionekana ndio kwanza na yeye alikuwa anafika.
“Jamani jamani siku zote nawaambiaga Nasra Mrembo , hebu muangalieni”Aliongea Recho na kufanya wenzake wote wageuze macho na kumwangalia Nasra ambaye aliona aibu kwa namna ambavyo alikuwa akisifiwa.
“Jamani najua na mimi sijaalikwa ila nimehudhuria…”Ilisikika sauti ya kiume kutoka mlangoni na kuwafanya warembo hawa waliopendeza usiku huu kugeuza macho yao na kumwangalia aneongea na kufanya kundi lote kukosa utulivu.
Alikuwa ni Ernest Komwe CEO msaidizi aliekuwa ametangulizana na Dorisi alikuwa amependeza Haswa na suti yake hata kwa Dorisi pia.
“Kuweni na amani hili ni kusanyiko kama tafrija ndogo , hivyo tusiangaliane kwa vyeo vya kazini tuweni huru , nimekuja kuungana na ninyi ili tupate kuzoeana , si eti Nasra?”Aliongea Ernest na kumfanya Nasra kutabasamu na kutingisha kichwa na Ernest alionekana kujiamini kwani alisogea na kwenda kuketi karibu na Benadetha.
Uzuri ni kwamba meza zilikuwa zimeunganishwa Pamoja na viti vilikuwa vingi kiasi kwamba hata watu ishirni wanaweza kutosha ndani ya hilo eneo.
“Hi Guys!”Ilisikika sauti nyingine kutoka mlangoni na kufanya wote wageuke na kuangalia sauti ya mwanamke mrembo aliekuwa akiingia hapo ndani , mrembo mwenyewe hakuwa mwingine bali alikuwa ni Nadia Alfonso na wote baada ya kumuona walitabasamu, Nasra alikuwa amependeza mno n ani kama amefanya makusudi kuchagua mavazi ambayo yatamfanya kupendeza kuliko wengine wote.
Kusanyiko liliandaliwa na idara ya Public Relation kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo , lakini wafanyakazi kutoka idara nyingine walihudhuria na haikueleweka taarifa wamezipata vipi.
“Msishangae hata mimi pia ni mmoja ya wafanyakazi wa Vexto hivyo naweza kusema kama ni mhusika kwenye hii tafrija ilioandaliwa kimya kimya”Aliongea Nadia , alionekena kuwa kwenye mudi nzuri mno na ni kama hakuna jambo ambalo limemtokea siku chache nyuma nchini Ufaransa.
“Jamani CEO Edna na yeye yupo njiani kuja kwenye kusanyiko hili”Aliongea Dorisi na kufanya kila mtu kushangaa.
“Dorisi unamaanisha CEO anakuja?”Aliuliza Recho kama mtu ambaye hajasikia vizuri.
“Ndio kanitumia ujumbe yupo njiani”Aliongea Dorisi pasipo kujali na kukaa
IJUMAA ASUBUHI MWENDELEZO
0687151346 nicheki watsapo tuendelee
Mapema sana..
.
Mapema kivipi si aliahidi ataweka asubuhiMapema sana..
.
waiting
Chukua gomba mana ya leo ni ya kibabe unatupiwa mzigo wa mpaka jumapiliMZEE NISHACHUKUA POPCORN HAPA
HahahahahaChukua gomba mana ya leo ni ya kibabe unatupiwa mzigo wa mpaka jumapili
mambo ya coment peleka facbook kwa washamba wenziokumbe wafuatiliaji ni wengi wanasomaga kimya kimya. Mzee usiweke mzigo mpaka comment zizidi 200 kama itakupendeza