singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #2,161
SEHEMU YA 403
Licha ya kuanza kuhisi huenda Hades hajapoteza uwezo wake kama taarifa zilivyowafikia lakini bado hawakutaka kuamini kama wameshindwa , kitendo cha Gashadokuro kupotea kwa namna ya kuyeyuka kilifanya wote kuwa ni wenye kiwewe.
Nurarihyon alikuwa ni moja ya watu waliokuwa kwenye mshangao mkubwa alijiuliza inakuwaje mtu akawa na uwezo wa namna hio halafu asione nguvu alizokuwa nazo kwa namna yoyote ile,jambo hilo lilimshangaza mno.
“Inaonekana uwezo wako haukupotea kama tulivyopata taarifa , lakini haimainishi kama tutakimbia na kukubali kushindwa, tutapigana mpaka pumzi yetu ya mwisho”Aliongea Generali Nurarihyon na palepale aliwapa ishara vijana wake wote kushambulia , akiwemo Namera ambaye alikuwa na mpango wa kulipiza kisasi cha mrembo wake SnowGirl.
Ni kama Roma alikuwa akisubiria mashambulio ya pamoja , Namera na yeye hakuwa vibaya kwenye kutumia uwezo wake , kwani palepale alifanya tukio la ajabu, haikueleweka majani ya miti yalitokea wapi , lakini yalianza kudondoka kuelekea sehemu ambayo Roma amesimama na yalipomfikia karibu na kichwa yaligeuka kutoka kuwa majani na kuwa mawe ghafla yakimshukia Roma kwa namna ya kumjeruhi.
Roma alikuwa ashausoma mchezo kwani baada ya majani yale kugeuka na kuwa mawe aliyageuza tena na kuwa majani na kumfanya Namera kutoa macho baada ya kugeuka majani , tena yalishika moto halafu akayakusanya kwa macho na kuyatengeneza kama mpira na kwa kasi ya ajabu yaliwafuata na kuwalipukia.
Ni kitendo cha ajabu mno kwani Roma hajasogea hata hatua moja, lakini vilevile hakuwa akitumia mikono kutengeneza maajabu anayoyataka.
Baada ya kuona hali imekuwa mbaya Nurarihyon na jeshi lake walimchangia kwa pamoja kwa kasi kubwa kwa namna ya kupaa lakini walijikuta kila wakitaka kumsogelea Roma aliposimama hawamfikii , ni kama kuna nguvu isio kuwa ya kawaida iliokuwa ikiwasukuma nyuma na kushindwa kusogea.
“Pluto naomba kabla haujaniua uniambie umewezaje kutuzuia tusikufikie , umewazeaje kumyeyusha Gashakoduro?”
“Hahaha….hata mimi siwezi kuelewa ukishajua ushajua na kama hujui hujui tu , hisia zangu ndio zinaniambia fanya hivi na akili yangu ikikubali kila kitu kinatokea”Aliongea Roma kwa furaha na palepale Nurarihyon na maninja wake walipotea na kumfanya Seidel pamoja na Stark kushangaa.
“Puu!!!!”
Maninja wote walionekana kudondoka kutoka juu na kupoteza Maisha palepale akiwemo mkuu wao Nurarihyon.
Seidel baada ya kuona aliowategemea kufa kifo kibaya kama vile wamesukumwa kutoka kwenye jengo refu , aliwaamsrisha wanajeshi waliobaki kushambulia kwa risasi.
“Ratatatata….”
Milindimo ya risasi ilifunika eneo lote kwa muda wa dakika mbili huku wanajeshi wakishambulia sehemu moja ambayo Roma amesimama na kufanya eneo hilo kufuka moshi na kumfanya asionekane.
Ile wanakuja kuacha walijikuta wakipagawa na kutetemeka kwani risasi zote zilikuwa hewani ni kama zimegoma kumfikia Roma kwa kushikiliwa na kitu hewani.
Roma alitabasamu kifedhuli na risasi zile ziligeuka kama nyuki na kujigeuza kwa kasi kama vile zimetoka kwenye bunduki na kuwarudia wale wanajeshi na ndani ya dakika wanajeshi wote wako chini.
Seidel na Stark baada ya kuona wamebaki walikunja ngumi na kumsogelea Roma kwa kasi , lakini kabla hata hawajamfikia walijikuta wakielea hawani huku damu zikianza kuwatoka , walikuwa ni kama bendera juu ya mlingoti na Roma baada ya kuona ameridhika aliwaachia na ile wanakuja kudondoka hawakuwa hai tena.
Kazi ikawa imeisha lakini Roma alijiambia haijaisha kama anavyotaka alikumbuka katika watu ambao walikuwa wakijua juu ya yeye kupoteza uwezo wake ni Prandell ambaye ni Poseidon , pamoja na Christen lakini pia alikutana na Robert Mueller Kamishina wa FBI lakini pia mkuu wa kikosi cha Dhoruba nyekundu ndani ya taifa la Marekani.
Roma alishakuwa na kisasi cha muda mrefu na Robert Mueller tokea tukio lililotokea kule Japani na alijiambia haondoki Marekani mpaka aone mwisho wake.
Baada ya kazi yake kukamilika alipotea na alipokuja kutokea ni kwenye balcony ya jumba la Christen.
Sally alishangazwa na Roma kutokezea kwa juu kwani hakumuona akiingia wakati alikuwepo ndani ya eneo hilo la sebuleni muda wote.
“Mr Roma kuna kitu chochote unataka nikuhudumie?”Aliuliza baada ya kusimama na kumpa heshima yake.
“Nina njaa andaa chakula kitamu kuliko vyote”Aliongea na kumfanya Sally atabasamu , mwanzoni alijua Roma atarudi akiwa amekula , lakini imekuwa tofauti.
Baada ya Sally Kwenda kuandaa chakula Roma alisogelea simu ya ukutani iliokuwa hapo eneo la sebuleni na kuingiza namba anazozifahamu yeye.
“Mfalme Pluto tokea usiku ule nimeshindwa kukupata hewani, ulipotelea wapi?, kwanini namba yako inasoma upo Marekanni?”Ilisikika sauti inayotumia lugha ya Kiebrania upande wa pili, alikuwa ni Makedon jasusi wa Mossad.
“Huna haja ya kujua maelezo yote Makedon muda mchache , nimekupigia simu kwasababu kuna taarifa ninazozihitaji , itakuwa vyema sana kama utafanikisha kabla sijamaliza kula chakula cha usiku, mtu ninaetaka taarifa yake sio mgeni kwa Mossad hivyo naamini taarifa zake mtakuwa nazo”
“Who is it ?”
“Robert Mueller”
“The Commisioner , Mfalme Pluto unataka kuanzisha vita na Marekani , Kujiingiza kwenye maswala ya kisiasa si nje ya kanuni zako?”
“Sina haja na taifa la Marekani, ninachotaka ni huyu mpuuzi Robert Mueller anajaribu kunichokonoa na unajua sipendezwi na watu wa namna hio , Kazi yako ni kuelewa tu ninachotaka kwako na kunipa majibu, je tupo sawa?”
“Ni furaha kwangu kukusiidia Mfalme Pluto ,endelea na chakula chako nitakupatia taarifa muda si mrefu”Aliongea Makedon na simu ilikatwa.
Christen alikuwa bado hayupo nyumbani ikiashiria bado yupo kazini na Roma hakujali sana kuhusu hilo kwanza ilimpa uafadhali wa kuwa mwenyewe .
Dakika chache mbele Roma aliwekewa mezani chakula kitamu na Sally , chakula ambacho aliona ni kweli mrembo huyo alikuwa amefuzu sio tu kwenye maswala ya ukijakazi lakini pia katika maswala ya upishi na Roma aliona ndio maana Christen akamchangua.
Roma alikula mapande mawili ya nyama ya kuoka , akamalizia na kuku nusu na baada ya hapo akashushia na Champaigne kisha akaongezea juu na Soseji zinazotoka Urusi.
Sallly muda wote alikuwa pembeni akishangazwa na uwezo wa kula wa Roma , lakini Roma hakumjali muda huo alijali kwanza tumbo lake na baada ya kumaliza ndio akamwangalia.
“Sally unaniangalia kama mtu unaetegemea chochote kutoka kwangu?”
“Mr Roma nipo tayari kukuhudumia kwa kila utakachotaka?”
“Una uhakika!! je kama hatakupa hela tena?”
“Atanipa nina uhakika”Aliongea huku akitabasamu , ilionekana hela aliopoewa asubuhi ilishamnogea na sasa alikuwa tayari Kiiendelea Zaidi na Zaidi na Zaidi.
“Leo huna bahati naweza kusema , kwani kuna sehemu natakiwa Kwenda, labda siku nyingine “Aliongea huku akinyanyuka na kisha akapandisha Kwenda juu ghorofani.
Ukweli Roma hakutaka tena kumtumia Sally kutokana na kwamba alihisi utofauti mkubwa kati yake na mrembo Rufi , kila akikumbuka Ngozi laini ya Rufi hamu na Sally ilipotea .
Roma alikuwa akijihisi mwepesi sana kuliko isivyokuwa kawaida , ijapokuwa mwanzoni alikuwa akiogopa kusafiri kwa kuteleport , lakini muda huo hakuwa na woga , kila ambacho alikuwa akihofia kilishapita huku akijiambia kama kuna hatua ya Dhiki labda ni kwenye Maisha yake ya kawaida lakini sio kugongwa na Radi tena, baada ya kuwaza kidogo tu alipotea tena bila kueleweka anaelekea wapi.
********
Upande mwingine ndani ya Marekani katika jimbo la Washington D.C inaonekana jengo ambalo limesimama kama vile ni ngome , hilo ndio jengo ambalo linatumiwa kama makao makuu ya FBI linalofahamika kwa jina maarufu la Hoover Building.
Ni jengo ambalo lilisimamishwa tokea miaka ya 70 na ni moja ya sehemu ambayo ilikuwa ikiangaliwa na wananchi wengi kwa matamanio kutokana na ndoto za kupenda kufanya kazi katika jengo hilo.
Lakini licha hivyo wafanyakazi wanaofanya kazi ndani yake hawana utofauti sana na wafanyakazi wanaofanya kazi katika maeneo mengine , wote walikuwa wakifanya kazi muda wote na kulipwa mshahara wao na serikali kama ilivyo tu kwa wafanyakazi wengine wa serikali na hakuna mfanyakazi ambaye unaaweza ukasema ni Tajiri kuliko mwenzake kutokana na wote kuendesha magari ya kawaida ya bei rahisi kilichowatofautisha ni ile heshima kwenye jamii ni pale wanapojitambulisha kama FBI a. k.a ‘Law enforcers’.
Kamishina wa FBI ni Robert Mueller , ijapokuwa hakikuwa cheo kikubwa sana lakini vile vile hakikuwa cheo kidogo kama kiongozi wa FBI kwa maana kwamba kulikuwa na wakubwa wake Zaidi kicheo.
Ni saa nne sasa za usiku ndani ya jengo lakini jengo lilionekana kutoa mwanga ikionyesha wafanyakazi walikuwa wakiendelea na majukumu yao ya kuhakikisha Marekani inakuwa salama kwa raia na sheria inafuatwa kikamilifu.
Upande wa chini katika vyumba vya ardhi sauti ya Robert Mueller ilisikika kwenye korido yote ikiwa katika jazba kubwa sana.
“Nakuuliza wewe mpuuzi , unaniambiaje wanajeshi wote wamekufa halafu kusiwe na damu sehemu ya tukio?”Aliongea Robert Mueller huku akipiga kofi kwenye meza na kufanya makaratasi yalio juu yake kupeperushwa na upepo.
Mbele yake walionekana wanajeshi waliokuwa katika sare wakiwa wamesimama kwa wasiwasi mita moja kutoka kwenye meza yake.
Hasira ya Robert Mueller ilitokana na taarifa alioipokea juu ya wanajeshi aliowaagiza Kwenda kumkamata Hades mara baada ya kupata taarifa kwamba amepoteza uwezo wake.
Roberts Muellerr licha ya kwamba alikuwa kiongozi wa Dhoruba nyekundu tawi la Marekani lakini haikumaanisha alikuwa na nguvu Zaidi ya kujiamulia baadhi ya mambo kwasababu kulikuwa na wakuu wake ambao wanampa maagizo na kuyafuata.
Baada ya taarifa za Hades kupoteza uwezo wake ziliweza kufika katika makao makuu ya Dhoruba nyekundu na Robert alielekezwa kutofanya kitu chochote mpaka kutakapokuwa na taarifa za kutosha kutoka makao makuu ya Zeros organisation juu ya uwezo wa Ajent 13 kupotea.
Sasa Robert akadharau maagizo ya mabosi wake na kutoa kikosi Kwenda kumkamata Hades, ukweli ni kwamba Robert hakuwahi kabisa kumpenda Hades kutokana na Ngozi yake na hata wakubwa zake aliwashangaa kwa kumruhusu mwafrika kuwa na nguvu kubwa ambayo imekuwa tishio.
Hivyo baada ya kusikia kutoka kwa Prandell kama Hades amepoteza uwezo wake , aliona hio ndio nafasi yake , aliamini anchokifanya wakuu wake watakuja kumuelewa na kumshukuru baadae tu.
Mpango wake ulikuwa ni kumkamata Hades na kumuweka nyuma ya nondo na wakati ho huo akitafuta namna ya kumpunguza nguvu kwa kumshawishi kuachia baaadhi ya mali na nguvu ya kijeshi anayoimiliki ndani ya The Eagles.
Alifanya hivyo kwakuwa alikuwa akimwamini Zaidi Poseidon kuliko hata Zeros ambao wenyewe ndio waliohusika katika kumtegeneza , alijiambia miungu inatambuana , kama imesema Hades kapoteza uwezo wake basi hilo ndio jibu na sio la Zeros.
Yaani kwa lugha nyepesi hakutaka kutilia maanani wasiwasi wa Zeros , kwani kwa upande wao waliamini huenda Roma hajapoteza uwezo wake wote kutokana na kwamba hawakuwa na uelewa wa kisayansi juu ya mbinu za kijini anazojifunza.
Sasa baada ya kuletewa taarifa kwamba wanajeshi wake wamekufa na Hades pasipo kuonekana ndani ya eneo alipagawa mno na kupandwa na Jaza kali.
“Boss nadhani upunguze jazba , licha ya kwamba wanajeshi tuliotuma wamekufa haimaanishi misheni yetu imefeli , bado tunaamini yule mpuuzi kapoteza uwezo wake, kukimbia kwake hakuwezi pia kutuletea shida”Aliongea.
“Ubongo wako umekufa ?, unafikiri unachoongea sijakifikiria , ninachokifanya muda huu ni kuhakikisha namkamata wa kwanza , unafikiri kama atakamatwa na maadui zetu nini kitatokea? , jibu ni kwamba watamshawishi atoe hatimiliki za vile vyote vilivyopo chini yake na hilo litakuwa tatizo wewe mpuuzi uliejaza makamasi kichwani”Aliongea kwa hasira.
Lakini muda huo akiendelea kuwazodoa wanajeshi wake mtaalamu wa mitambo alitokezea kwenye mlango wa ofisi akiwa kwenye haraka huku akihema kama mbwa.
“Sir pardon my interruption but our systems seemed to be attacked by unkown hacker, The entire server now is out of our control”
“Sir naomba unisamehe kwa kuwaingilia lakini mifumo yetu imeshambuliwa na mdukuaji asiefahamika na Seva zote zipo nje ya uwezo wetu wa udhibiti”
Aliongea Mzungu huyo wa makamo ambaye ni mtaalamu wa mitambo ya teknolojia ya jengo hilo aliekuwa akiaminika na mara nyingi akiongea kauli ya namna hio inamaanisha kwamba ni kweli kuna shida.
********
Upande mwingine muda huo huo kukiwa na tofauti ya lisaa tu yaani ikiwa ni saa tatu za usiku ndani ya jimbo la Illnois-Chicago , ni katika makazi ya raisi mstaafu wa Marekani bwana Barack Mabo , katika kizuizi cha kuingia katika eneo hilo la kifahari lililokuwa kando ya bahari , ilionekana gari aina ya Ford rangi nyeusi ikiruhusiwa kupita mara baada ya kufanyiwa ukaguzi na walinzi.
Dakika chache tu mara baada ya gari hio Kwenda kusimama katika maegeisho ya muda mfupi , alionekana mwanamama Dyana alievalia vazi la suti nyeusi akitoka kwenye gari mara baada ya mlango wa gari yake kufunguliwa.
“Miss Dyana! Welcome my friend”Ilisikika sauti upande wa kulia kwake kutokea kwenye bustani na alionekana Raisi Barack Mabo akiwa na mtoto mdogo wa kiafrika ambaye ni mjukuu akiwa ameshikilia mpira wa kuchezea basketi ball na ilionekana yeye na babu yake walikuwa wakicheza licha ya usiku kuwa mkubwa.
“Thanks Barrack”Alijibu Diana na kumsogelea mheshimiwa na kukumbatiana kishikaji na kisha kuachiana.
“Joe tangulia ndani , tunakuja kujumuika kwenye chukula cha usiku”Aliongea mheshimiwa mstaafu na Joe alitingisha kichwa na kukimbilia ndani.
“Mara ya mwisho namuona Joe alikuwa na mwaka mmoja, nadhani ilikuwa mara yetu ya mwisho ya sisi kuonana”Aliongea Diana.
“Upo sahihi kabisa , ni muda mrefu hatujaonana Zaidi ya kuwasiliana kwa njia ya simu”Aliongea huku akimpa ishara ya kutembea kuelekea upande wa kushoto kwenye bustani , sehemu ambayo imejengwa kama sehemu ya mapumziko na kukaa chini huku wakiongea kwa kucheka walionekana kuzoeana , hata hivyo ni jambo la kuzoeleka kwani raisi huyo alisifika kwa ucheshi wakati wa uongozi wake.
“Nipe ripoti Diana , naamini jambo ambalo limekuleta ni muhimu Zaidi , kwani ni mara chache unatoka makao makuu Kisiwani”Aliongea mheshimiwa na kumfanya Diana kuvuta pumzi kidogo.
“Tuna wasiwasi na ajenti 13 mheshimiwa, amepitia mabadiliko makubwa kuliko sisi wenyewe tulivyotegemea”
“Unamaanisha nini?”Aliuliza na kumfanya Diana kutoa simu na kupangusa kwa dakika kadhaa na kumpatia na kuanza kuangalia, ilikuwa ni Vidio ikionyesha Roma akipambana na watu waliotumwa na Robert.
“ Nadhani taarifa ya mwisho ilielezea amepoteza uwezo wake na yupo nyumbani kwa Christen , kwanini anaonekana kuwa kama mwanzo?”
“Hayupo kama mwanzo Mheshimiwa na hili ndio limenileta kwa dharula nyumbani kwako”
“Unamaanisha nini?”
“Amekuwa vile ambavyo hatukutaka, kama unavyoona hapo alikuwa akipambana lakini hakuna ishara yoyote kama anatumia uwezo tuliomtengenezea sisi , anatumia mbinu ambayo alifundishwa na yule mpuuzi Tang Chi”Aliongea na kumfanya Barack Mabo macho yake kuongezeka ukubwa kidogo , ni kama mtu ambaye hajaelewa vizuri na alituliza mawazo na baada ya dakika kadhaa alitabasamu na kumfanya Diana aliekuwa na wasiwasi kushangaa.
“Kwa maneno yako napaswa kuamini kwamba amekuwa Hades na sio Ajent 13 tena?”
“Naaweza kujibu ndio kwasababu mpaka sasa hatuna uwezo wa kumfuatilia kwa ukaribu kama ajenti 13 , amekuwa Hades ndio kwasababu hategemei tena kile tulichokiweka kwenye mwili wake”Aliongea.
“Diana this is good news?”Aliongea akimaanisha kwmaba hio ni Habari njema.
“Unamaanisha nini mheshimiwa?”
“Nilikuwa kwenye mazungumzo ya muda mrefu na The First Black miaka mitatu iliopita mara baada ya kupewa uongozi wa juu wa Zeros , Diana unajua kwanini nilifungua maabara ya teknolojia ya juu nchini Tanzania na yapi yalikuwa malengo yangu kwa taifa la Marekani na dunia kwa ujumla?”Aliuliza kwa sauti ya chini.
“Hatujawahi kupata nafasi ya kuzungumzia maswala yako ya kisiasa , licha najua wewe ni moja ya raisi uliepigania maslahi ya taifa na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa”Aliongea Diana na kumfanya Barak kutabasamu.
“Sijapigania tu maslahi ya taifa la Marekani , bali naendelea kupigania maslahai ya Marekani licha ya kwamba nimetoka madarakani , moja ya ndoto yangu kubwa ni kupunguza nguvu ya The Doni katika hii dunia”Aliongea na kumfanya Diana kutoa macho.
“Mheshimiwa unamaanisha..?”
“Exactlly..”
“Taifa letu kwa ujumla linamhitaji Zaidi Hades kuliko Agent 13, kama ulivyosema amekuwa Hades kwa maana anaendelea kuwa huru, Zeros licha ya kwamba ni ya kimuunganiko katika mataifa makubwa lakini nguvu yake imeshikiliwa na The Doni”
“Lakini mheshimiwa sera za kimsingi za serikali yetu zimeasisiwa na The Doni na wanasiasa tunaendelea kuzipigania kuhakikisha kufanikiwa”
“Unachoongea ni sahihi lakini Marekani ni taifa na haliweze kuendelea kutokana na maagizo ya mtu mmoja , kwa nje tunaonekana kama wanademokrasia wa kweli , lakini kwa ndani tunatawaliwa kwa mawazo ya mtu mmoja , tunahitaji mtu ambaye atampunguza nguvu na kuwa mshindani wake, hii ni dunia yetu kwanini tuendelee kutawaliwa na mawazo ya mtu kutoka sayari nyingine”Aliongea na kisha akatabasamu na kuendelea.
“Diana nataka muendelee kutimiza wajibu wenu ndani ya Zeros HQ, kazi pale ni kubwa na sio ya kumfuatilia Agent 13 peke yake ,Dunia haipo salama Zaidi kama inavyoonekana kwa sasa na Marekani siku zote italinda maslahi ya taifa letu pamoja na dunia kwa ujumla”
“Mheshimiwa kabla sijaondoka naomba kuuliza swali?”Aliongea na kisha Mheshimiwa akatingisha kichwa kumruhusu.
“Matokeo ya mashambulizi ya meli yetu ya kivita , je ni kile kinachoendelea ndani ya Even Lab?”Aliuliza na mheshimiwa alitingisha kichwa akikubali.
“Matokeo hayo, je ni sehemu ya faida uliotegemea?”
“Diana katika moja ya vitu ambavyo najilaumu mpaka leo hii ni ujenzi wa ile maabara , mwanzoni nilifahamu naijenga kwasababu ya kushindana na The Doni , nakiri nilikuwa na mawazo hayo mara baada ya kushawishiwa na The First Black kuijenga kwa ajili ya Profesa Shelukindo lakini mwisho wa siku nilikuja kugundua nilikuwa nikitumika”
“Unamaanisha ujenzi wa Even Lab yalikuwa maagizo ya The Doni pasipo ya wewe kufahamu?”
“Exactly na zipo maabara kama zile Zaidi ya tano ambazo zipo chini yake , tunajaribu kupambana lakini yule mwanamke mipango yake ni kama imeandikwa kwenye karatasi kwani hakosei , ana akili nyingi sana kutuzidi nategemea mabadiliko makubwa ya dunia ndani ya miaka ijayo kama dunia haitoshituka mapema , kinachotupa changamoto ni kutokana na kwamba wote hatuna taarifa zilizokamili , kwani mipango yake tumeikuta na tunakufa na kuiacha na anakuja kutafuta wengine wa kuendeleza huo ndio udhaifu mkubwa tuliokuwa nao, Wewe ni rafiki yangu ndio maana nahitaji uendelee na majukumu yako, tunatakiwa kushukuru mabadiliko ya Agent13”
“Lakini mheshimiwa hujawahi kuhisi kuna kitu hakipo sawa , wote tunafahamu The Doni ndio aliependekeza utekelezwaji wa Mpango LADO ambao ulikuja kufanikiwa , lakini baada ya kutimiza hatua ya pili ya mpango Ajent 13 akaenda tofauti na kile kilichokuwa kwenye ramani ya mpango na sasa matokeo yamekuwa haya , huoni kuna kitu ambacho hakija kaa sawa”.
“Diana hakika unaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria , ni kweli kabisa kwa nafasi yako kuna mambo ambayo hauyajui licha ya kuwa katika mstari wa kutekeleza majukumu yako , Zeros kwa maneno ya The First Black hawakupenda Ajent 13 kujifunza mbinu za kijini ambazo hazina maelezo kisayansi , lakini mwisho wa siku The Doni mwenyewe ndio alieruhusu kwa Ajent 13 kufanya anachotaka, bado kuna kitu kikubwa Zaidi nyuma ya pazia ambacho serikali yetu haikifahamu ndio maana nasema ndani ya miaka michache ijayo tutarajie mabadiliko makubwa ya dunia”
Waliendelea kuongea mpaka walipokuja kufuatwa kwa ajili ya chakula cha usiku , lakini Diana aligoma na kuondoka na Mheshimiwa Barrack hakumzuia.
Licha ya kuanza kuhisi huenda Hades hajapoteza uwezo wake kama taarifa zilivyowafikia lakini bado hawakutaka kuamini kama wameshindwa , kitendo cha Gashadokuro kupotea kwa namna ya kuyeyuka kilifanya wote kuwa ni wenye kiwewe.
Nurarihyon alikuwa ni moja ya watu waliokuwa kwenye mshangao mkubwa alijiuliza inakuwaje mtu akawa na uwezo wa namna hio halafu asione nguvu alizokuwa nazo kwa namna yoyote ile,jambo hilo lilimshangaza mno.
“Inaonekana uwezo wako haukupotea kama tulivyopata taarifa , lakini haimainishi kama tutakimbia na kukubali kushindwa, tutapigana mpaka pumzi yetu ya mwisho”Aliongea Generali Nurarihyon na palepale aliwapa ishara vijana wake wote kushambulia , akiwemo Namera ambaye alikuwa na mpango wa kulipiza kisasi cha mrembo wake SnowGirl.
Ni kama Roma alikuwa akisubiria mashambulio ya pamoja , Namera na yeye hakuwa vibaya kwenye kutumia uwezo wake , kwani palepale alifanya tukio la ajabu, haikueleweka majani ya miti yalitokea wapi , lakini yalianza kudondoka kuelekea sehemu ambayo Roma amesimama na yalipomfikia karibu na kichwa yaligeuka kutoka kuwa majani na kuwa mawe ghafla yakimshukia Roma kwa namna ya kumjeruhi.
Roma alikuwa ashausoma mchezo kwani baada ya majani yale kugeuka na kuwa mawe aliyageuza tena na kuwa majani na kumfanya Namera kutoa macho baada ya kugeuka majani , tena yalishika moto halafu akayakusanya kwa macho na kuyatengeneza kama mpira na kwa kasi ya ajabu yaliwafuata na kuwalipukia.
Ni kitendo cha ajabu mno kwani Roma hajasogea hata hatua moja, lakini vilevile hakuwa akitumia mikono kutengeneza maajabu anayoyataka.
Baada ya kuona hali imekuwa mbaya Nurarihyon na jeshi lake walimchangia kwa pamoja kwa kasi kubwa kwa namna ya kupaa lakini walijikuta kila wakitaka kumsogelea Roma aliposimama hawamfikii , ni kama kuna nguvu isio kuwa ya kawaida iliokuwa ikiwasukuma nyuma na kushindwa kusogea.
“Pluto naomba kabla haujaniua uniambie umewezaje kutuzuia tusikufikie , umewazeaje kumyeyusha Gashakoduro?”
“Hahaha….hata mimi siwezi kuelewa ukishajua ushajua na kama hujui hujui tu , hisia zangu ndio zinaniambia fanya hivi na akili yangu ikikubali kila kitu kinatokea”Aliongea Roma kwa furaha na palepale Nurarihyon na maninja wake walipotea na kumfanya Seidel pamoja na Stark kushangaa.
“Puu!!!!”
Maninja wote walionekana kudondoka kutoka juu na kupoteza Maisha palepale akiwemo mkuu wao Nurarihyon.
Seidel baada ya kuona aliowategemea kufa kifo kibaya kama vile wamesukumwa kutoka kwenye jengo refu , aliwaamsrisha wanajeshi waliobaki kushambulia kwa risasi.
“Ratatatata….”
Milindimo ya risasi ilifunika eneo lote kwa muda wa dakika mbili huku wanajeshi wakishambulia sehemu moja ambayo Roma amesimama na kufanya eneo hilo kufuka moshi na kumfanya asionekane.
Ile wanakuja kuacha walijikuta wakipagawa na kutetemeka kwani risasi zote zilikuwa hewani ni kama zimegoma kumfikia Roma kwa kushikiliwa na kitu hewani.
Roma alitabasamu kifedhuli na risasi zile ziligeuka kama nyuki na kujigeuza kwa kasi kama vile zimetoka kwenye bunduki na kuwarudia wale wanajeshi na ndani ya dakika wanajeshi wote wako chini.
Seidel na Stark baada ya kuona wamebaki walikunja ngumi na kumsogelea Roma kwa kasi , lakini kabla hata hawajamfikia walijikuta wakielea hawani huku damu zikianza kuwatoka , walikuwa ni kama bendera juu ya mlingoti na Roma baada ya kuona ameridhika aliwaachia na ile wanakuja kudondoka hawakuwa hai tena.
Kazi ikawa imeisha lakini Roma alijiambia haijaisha kama anavyotaka alikumbuka katika watu ambao walikuwa wakijua juu ya yeye kupoteza uwezo wake ni Prandell ambaye ni Poseidon , pamoja na Christen lakini pia alikutana na Robert Mueller Kamishina wa FBI lakini pia mkuu wa kikosi cha Dhoruba nyekundu ndani ya taifa la Marekani.
Roma alishakuwa na kisasi cha muda mrefu na Robert Mueller tokea tukio lililotokea kule Japani na alijiambia haondoki Marekani mpaka aone mwisho wake.
Baada ya kazi yake kukamilika alipotea na alipokuja kutokea ni kwenye balcony ya jumba la Christen.
Sally alishangazwa na Roma kutokezea kwa juu kwani hakumuona akiingia wakati alikuwepo ndani ya eneo hilo la sebuleni muda wote.
“Mr Roma kuna kitu chochote unataka nikuhudumie?”Aliuliza baada ya kusimama na kumpa heshima yake.
“Nina njaa andaa chakula kitamu kuliko vyote”Aliongea na kumfanya Sally atabasamu , mwanzoni alijua Roma atarudi akiwa amekula , lakini imekuwa tofauti.
Baada ya Sally Kwenda kuandaa chakula Roma alisogelea simu ya ukutani iliokuwa hapo eneo la sebuleni na kuingiza namba anazozifahamu yeye.
“Mfalme Pluto tokea usiku ule nimeshindwa kukupata hewani, ulipotelea wapi?, kwanini namba yako inasoma upo Marekanni?”Ilisikika sauti inayotumia lugha ya Kiebrania upande wa pili, alikuwa ni Makedon jasusi wa Mossad.
“Huna haja ya kujua maelezo yote Makedon muda mchache , nimekupigia simu kwasababu kuna taarifa ninazozihitaji , itakuwa vyema sana kama utafanikisha kabla sijamaliza kula chakula cha usiku, mtu ninaetaka taarifa yake sio mgeni kwa Mossad hivyo naamini taarifa zake mtakuwa nazo”
“Who is it ?”
“Robert Mueller”
“The Commisioner , Mfalme Pluto unataka kuanzisha vita na Marekani , Kujiingiza kwenye maswala ya kisiasa si nje ya kanuni zako?”
“Sina haja na taifa la Marekani, ninachotaka ni huyu mpuuzi Robert Mueller anajaribu kunichokonoa na unajua sipendezwi na watu wa namna hio , Kazi yako ni kuelewa tu ninachotaka kwako na kunipa majibu, je tupo sawa?”
“Ni furaha kwangu kukusiidia Mfalme Pluto ,endelea na chakula chako nitakupatia taarifa muda si mrefu”Aliongea Makedon na simu ilikatwa.
Christen alikuwa bado hayupo nyumbani ikiashiria bado yupo kazini na Roma hakujali sana kuhusu hilo kwanza ilimpa uafadhali wa kuwa mwenyewe .
Dakika chache mbele Roma aliwekewa mezani chakula kitamu na Sally , chakula ambacho aliona ni kweli mrembo huyo alikuwa amefuzu sio tu kwenye maswala ya ukijakazi lakini pia katika maswala ya upishi na Roma aliona ndio maana Christen akamchangua.
Roma alikula mapande mawili ya nyama ya kuoka , akamalizia na kuku nusu na baada ya hapo akashushia na Champaigne kisha akaongezea juu na Soseji zinazotoka Urusi.
Sallly muda wote alikuwa pembeni akishangazwa na uwezo wa kula wa Roma , lakini Roma hakumjali muda huo alijali kwanza tumbo lake na baada ya kumaliza ndio akamwangalia.
“Sally unaniangalia kama mtu unaetegemea chochote kutoka kwangu?”
“Mr Roma nipo tayari kukuhudumia kwa kila utakachotaka?”
“Una uhakika!! je kama hatakupa hela tena?”
“Atanipa nina uhakika”Aliongea huku akitabasamu , ilionekana hela aliopoewa asubuhi ilishamnogea na sasa alikuwa tayari Kiiendelea Zaidi na Zaidi na Zaidi.
“Leo huna bahati naweza kusema , kwani kuna sehemu natakiwa Kwenda, labda siku nyingine “Aliongea huku akinyanyuka na kisha akapandisha Kwenda juu ghorofani.
Ukweli Roma hakutaka tena kumtumia Sally kutokana na kwamba alihisi utofauti mkubwa kati yake na mrembo Rufi , kila akikumbuka Ngozi laini ya Rufi hamu na Sally ilipotea .
Roma alikuwa akijihisi mwepesi sana kuliko isivyokuwa kawaida , ijapokuwa mwanzoni alikuwa akiogopa kusafiri kwa kuteleport , lakini muda huo hakuwa na woga , kila ambacho alikuwa akihofia kilishapita huku akijiambia kama kuna hatua ya Dhiki labda ni kwenye Maisha yake ya kawaida lakini sio kugongwa na Radi tena, baada ya kuwaza kidogo tu alipotea tena bila kueleweka anaelekea wapi.
********
Upande mwingine ndani ya Marekani katika jimbo la Washington D.C inaonekana jengo ambalo limesimama kama vile ni ngome , hilo ndio jengo ambalo linatumiwa kama makao makuu ya FBI linalofahamika kwa jina maarufu la Hoover Building.
Ni jengo ambalo lilisimamishwa tokea miaka ya 70 na ni moja ya sehemu ambayo ilikuwa ikiangaliwa na wananchi wengi kwa matamanio kutokana na ndoto za kupenda kufanya kazi katika jengo hilo.
Lakini licha hivyo wafanyakazi wanaofanya kazi ndani yake hawana utofauti sana na wafanyakazi wanaofanya kazi katika maeneo mengine , wote walikuwa wakifanya kazi muda wote na kulipwa mshahara wao na serikali kama ilivyo tu kwa wafanyakazi wengine wa serikali na hakuna mfanyakazi ambaye unaaweza ukasema ni Tajiri kuliko mwenzake kutokana na wote kuendesha magari ya kawaida ya bei rahisi kilichowatofautisha ni ile heshima kwenye jamii ni pale wanapojitambulisha kama FBI a. k.a ‘Law enforcers’.
Kamishina wa FBI ni Robert Mueller , ijapokuwa hakikuwa cheo kikubwa sana lakini vile vile hakikuwa cheo kidogo kama kiongozi wa FBI kwa maana kwamba kulikuwa na wakubwa wake Zaidi kicheo.
Ni saa nne sasa za usiku ndani ya jengo lakini jengo lilionekana kutoa mwanga ikionyesha wafanyakazi walikuwa wakiendelea na majukumu yao ya kuhakikisha Marekani inakuwa salama kwa raia na sheria inafuatwa kikamilifu.
Upande wa chini katika vyumba vya ardhi sauti ya Robert Mueller ilisikika kwenye korido yote ikiwa katika jazba kubwa sana.
“Nakuuliza wewe mpuuzi , unaniambiaje wanajeshi wote wamekufa halafu kusiwe na damu sehemu ya tukio?”Aliongea Robert Mueller huku akipiga kofi kwenye meza na kufanya makaratasi yalio juu yake kupeperushwa na upepo.
Mbele yake walionekana wanajeshi waliokuwa katika sare wakiwa wamesimama kwa wasiwasi mita moja kutoka kwenye meza yake.
Hasira ya Robert Mueller ilitokana na taarifa alioipokea juu ya wanajeshi aliowaagiza Kwenda kumkamata Hades mara baada ya kupata taarifa kwamba amepoteza uwezo wake.
Roberts Muellerr licha ya kwamba alikuwa kiongozi wa Dhoruba nyekundu tawi la Marekani lakini haikumaanisha alikuwa na nguvu Zaidi ya kujiamulia baadhi ya mambo kwasababu kulikuwa na wakuu wake ambao wanampa maagizo na kuyafuata.
Baada ya taarifa za Hades kupoteza uwezo wake ziliweza kufika katika makao makuu ya Dhoruba nyekundu na Robert alielekezwa kutofanya kitu chochote mpaka kutakapokuwa na taarifa za kutosha kutoka makao makuu ya Zeros organisation juu ya uwezo wa Ajent 13 kupotea.
Sasa Robert akadharau maagizo ya mabosi wake na kutoa kikosi Kwenda kumkamata Hades, ukweli ni kwamba Robert hakuwahi kabisa kumpenda Hades kutokana na Ngozi yake na hata wakubwa zake aliwashangaa kwa kumruhusu mwafrika kuwa na nguvu kubwa ambayo imekuwa tishio.
Hivyo baada ya kusikia kutoka kwa Prandell kama Hades amepoteza uwezo wake , aliona hio ndio nafasi yake , aliamini anchokifanya wakuu wake watakuja kumuelewa na kumshukuru baadae tu.
Mpango wake ulikuwa ni kumkamata Hades na kumuweka nyuma ya nondo na wakati ho huo akitafuta namna ya kumpunguza nguvu kwa kumshawishi kuachia baaadhi ya mali na nguvu ya kijeshi anayoimiliki ndani ya The Eagles.
Alifanya hivyo kwakuwa alikuwa akimwamini Zaidi Poseidon kuliko hata Zeros ambao wenyewe ndio waliohusika katika kumtegeneza , alijiambia miungu inatambuana , kama imesema Hades kapoteza uwezo wake basi hilo ndio jibu na sio la Zeros.
Yaani kwa lugha nyepesi hakutaka kutilia maanani wasiwasi wa Zeros , kwani kwa upande wao waliamini huenda Roma hajapoteza uwezo wake wote kutokana na kwamba hawakuwa na uelewa wa kisayansi juu ya mbinu za kijini anazojifunza.
Sasa baada ya kuletewa taarifa kwamba wanajeshi wake wamekufa na Hades pasipo kuonekana ndani ya eneo alipagawa mno na kupandwa na Jaza kali.
“Boss nadhani upunguze jazba , licha ya kwamba wanajeshi tuliotuma wamekufa haimaanishi misheni yetu imefeli , bado tunaamini yule mpuuzi kapoteza uwezo wake, kukimbia kwake hakuwezi pia kutuletea shida”Aliongea.
“Ubongo wako umekufa ?, unafikiri unachoongea sijakifikiria , ninachokifanya muda huu ni kuhakikisha namkamata wa kwanza , unafikiri kama atakamatwa na maadui zetu nini kitatokea? , jibu ni kwamba watamshawishi atoe hatimiliki za vile vyote vilivyopo chini yake na hilo litakuwa tatizo wewe mpuuzi uliejaza makamasi kichwani”Aliongea kwa hasira.
Lakini muda huo akiendelea kuwazodoa wanajeshi wake mtaalamu wa mitambo alitokezea kwenye mlango wa ofisi akiwa kwenye haraka huku akihema kama mbwa.
“Sir pardon my interruption but our systems seemed to be attacked by unkown hacker, The entire server now is out of our control”
“Sir naomba unisamehe kwa kuwaingilia lakini mifumo yetu imeshambuliwa na mdukuaji asiefahamika na Seva zote zipo nje ya uwezo wetu wa udhibiti”
Aliongea Mzungu huyo wa makamo ambaye ni mtaalamu wa mitambo ya teknolojia ya jengo hilo aliekuwa akiaminika na mara nyingi akiongea kauli ya namna hio inamaanisha kwamba ni kweli kuna shida.
********
Upande mwingine muda huo huo kukiwa na tofauti ya lisaa tu yaani ikiwa ni saa tatu za usiku ndani ya jimbo la Illnois-Chicago , ni katika makazi ya raisi mstaafu wa Marekani bwana Barack Mabo , katika kizuizi cha kuingia katika eneo hilo la kifahari lililokuwa kando ya bahari , ilionekana gari aina ya Ford rangi nyeusi ikiruhusiwa kupita mara baada ya kufanyiwa ukaguzi na walinzi.
Dakika chache tu mara baada ya gari hio Kwenda kusimama katika maegeisho ya muda mfupi , alionekana mwanamama Dyana alievalia vazi la suti nyeusi akitoka kwenye gari mara baada ya mlango wa gari yake kufunguliwa.
“Miss Dyana! Welcome my friend”Ilisikika sauti upande wa kulia kwake kutokea kwenye bustani na alionekana Raisi Barack Mabo akiwa na mtoto mdogo wa kiafrika ambaye ni mjukuu akiwa ameshikilia mpira wa kuchezea basketi ball na ilionekana yeye na babu yake walikuwa wakicheza licha ya usiku kuwa mkubwa.
“Thanks Barrack”Alijibu Diana na kumsogelea mheshimiwa na kukumbatiana kishikaji na kisha kuachiana.
“Joe tangulia ndani , tunakuja kujumuika kwenye chukula cha usiku”Aliongea mheshimiwa mstaafu na Joe alitingisha kichwa na kukimbilia ndani.
“Mara ya mwisho namuona Joe alikuwa na mwaka mmoja, nadhani ilikuwa mara yetu ya mwisho ya sisi kuonana”Aliongea Diana.
“Upo sahihi kabisa , ni muda mrefu hatujaonana Zaidi ya kuwasiliana kwa njia ya simu”Aliongea huku akimpa ishara ya kutembea kuelekea upande wa kushoto kwenye bustani , sehemu ambayo imejengwa kama sehemu ya mapumziko na kukaa chini huku wakiongea kwa kucheka walionekana kuzoeana , hata hivyo ni jambo la kuzoeleka kwani raisi huyo alisifika kwa ucheshi wakati wa uongozi wake.
“Nipe ripoti Diana , naamini jambo ambalo limekuleta ni muhimu Zaidi , kwani ni mara chache unatoka makao makuu Kisiwani”Aliongea mheshimiwa na kumfanya Diana kuvuta pumzi kidogo.
“Tuna wasiwasi na ajenti 13 mheshimiwa, amepitia mabadiliko makubwa kuliko sisi wenyewe tulivyotegemea”
“Unamaanisha nini?”Aliuliza na kumfanya Diana kutoa simu na kupangusa kwa dakika kadhaa na kumpatia na kuanza kuangalia, ilikuwa ni Vidio ikionyesha Roma akipambana na watu waliotumwa na Robert.
“ Nadhani taarifa ya mwisho ilielezea amepoteza uwezo wake na yupo nyumbani kwa Christen , kwanini anaonekana kuwa kama mwanzo?”
“Hayupo kama mwanzo Mheshimiwa na hili ndio limenileta kwa dharula nyumbani kwako”
“Unamaanisha nini?”
“Amekuwa vile ambavyo hatukutaka, kama unavyoona hapo alikuwa akipambana lakini hakuna ishara yoyote kama anatumia uwezo tuliomtengenezea sisi , anatumia mbinu ambayo alifundishwa na yule mpuuzi Tang Chi”Aliongea na kumfanya Barack Mabo macho yake kuongezeka ukubwa kidogo , ni kama mtu ambaye hajaelewa vizuri na alituliza mawazo na baada ya dakika kadhaa alitabasamu na kumfanya Diana aliekuwa na wasiwasi kushangaa.
“Kwa maneno yako napaswa kuamini kwamba amekuwa Hades na sio Ajent 13 tena?”
“Naaweza kujibu ndio kwasababu mpaka sasa hatuna uwezo wa kumfuatilia kwa ukaribu kama ajenti 13 , amekuwa Hades ndio kwasababu hategemei tena kile tulichokiweka kwenye mwili wake”Aliongea.
“Diana this is good news?”Aliongea akimaanisha kwmaba hio ni Habari njema.
“Unamaanisha nini mheshimiwa?”
“Nilikuwa kwenye mazungumzo ya muda mrefu na The First Black miaka mitatu iliopita mara baada ya kupewa uongozi wa juu wa Zeros , Diana unajua kwanini nilifungua maabara ya teknolojia ya juu nchini Tanzania na yapi yalikuwa malengo yangu kwa taifa la Marekani na dunia kwa ujumla?”Aliuliza kwa sauti ya chini.
“Hatujawahi kupata nafasi ya kuzungumzia maswala yako ya kisiasa , licha najua wewe ni moja ya raisi uliepigania maslahi ya taifa na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa”Aliongea Diana na kumfanya Barak kutabasamu.
“Sijapigania tu maslahi ya taifa la Marekani , bali naendelea kupigania maslahai ya Marekani licha ya kwamba nimetoka madarakani , moja ya ndoto yangu kubwa ni kupunguza nguvu ya The Doni katika hii dunia”Aliongea na kumfanya Diana kutoa macho.
“Mheshimiwa unamaanisha..?”
“Exactlly..”
“Taifa letu kwa ujumla linamhitaji Zaidi Hades kuliko Agent 13, kama ulivyosema amekuwa Hades kwa maana anaendelea kuwa huru, Zeros licha ya kwamba ni ya kimuunganiko katika mataifa makubwa lakini nguvu yake imeshikiliwa na The Doni”
“Lakini mheshimiwa sera za kimsingi za serikali yetu zimeasisiwa na The Doni na wanasiasa tunaendelea kuzipigania kuhakikisha kufanikiwa”
“Unachoongea ni sahihi lakini Marekani ni taifa na haliweze kuendelea kutokana na maagizo ya mtu mmoja , kwa nje tunaonekana kama wanademokrasia wa kweli , lakini kwa ndani tunatawaliwa kwa mawazo ya mtu mmoja , tunahitaji mtu ambaye atampunguza nguvu na kuwa mshindani wake, hii ni dunia yetu kwanini tuendelee kutawaliwa na mawazo ya mtu kutoka sayari nyingine”Aliongea na kisha akatabasamu na kuendelea.
“Diana nataka muendelee kutimiza wajibu wenu ndani ya Zeros HQ, kazi pale ni kubwa na sio ya kumfuatilia Agent 13 peke yake ,Dunia haipo salama Zaidi kama inavyoonekana kwa sasa na Marekani siku zote italinda maslahi ya taifa letu pamoja na dunia kwa ujumla”
“Mheshimiwa kabla sijaondoka naomba kuuliza swali?”Aliongea na kisha Mheshimiwa akatingisha kichwa kumruhusu.
“Matokeo ya mashambulizi ya meli yetu ya kivita , je ni kile kinachoendelea ndani ya Even Lab?”Aliuliza na mheshimiwa alitingisha kichwa akikubali.
“Matokeo hayo, je ni sehemu ya faida uliotegemea?”
“Diana katika moja ya vitu ambavyo najilaumu mpaka leo hii ni ujenzi wa ile maabara , mwanzoni nilifahamu naijenga kwasababu ya kushindana na The Doni , nakiri nilikuwa na mawazo hayo mara baada ya kushawishiwa na The First Black kuijenga kwa ajili ya Profesa Shelukindo lakini mwisho wa siku nilikuja kugundua nilikuwa nikitumika”
“Unamaanisha ujenzi wa Even Lab yalikuwa maagizo ya The Doni pasipo ya wewe kufahamu?”
“Exactly na zipo maabara kama zile Zaidi ya tano ambazo zipo chini yake , tunajaribu kupambana lakini yule mwanamke mipango yake ni kama imeandikwa kwenye karatasi kwani hakosei , ana akili nyingi sana kutuzidi nategemea mabadiliko makubwa ya dunia ndani ya miaka ijayo kama dunia haitoshituka mapema , kinachotupa changamoto ni kutokana na kwamba wote hatuna taarifa zilizokamili , kwani mipango yake tumeikuta na tunakufa na kuiacha na anakuja kutafuta wengine wa kuendeleza huo ndio udhaifu mkubwa tuliokuwa nao, Wewe ni rafiki yangu ndio maana nahitaji uendelee na majukumu yako, tunatakiwa kushukuru mabadiliko ya Agent13”
“Lakini mheshimiwa hujawahi kuhisi kuna kitu hakipo sawa , wote tunafahamu The Doni ndio aliependekeza utekelezwaji wa Mpango LADO ambao ulikuja kufanikiwa , lakini baada ya kutimiza hatua ya pili ya mpango Ajent 13 akaenda tofauti na kile kilichokuwa kwenye ramani ya mpango na sasa matokeo yamekuwa haya , huoni kuna kitu ambacho hakija kaa sawa”.
“Diana hakika unaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria , ni kweli kabisa kwa nafasi yako kuna mambo ambayo hauyajui licha ya kuwa katika mstari wa kutekeleza majukumu yako , Zeros kwa maneno ya The First Black hawakupenda Ajent 13 kujifunza mbinu za kijini ambazo hazina maelezo kisayansi , lakini mwisho wa siku The Doni mwenyewe ndio alieruhusu kwa Ajent 13 kufanya anachotaka, bado kuna kitu kikubwa Zaidi nyuma ya pazia ambacho serikali yetu haikifahamu ndio maana nasema ndani ya miaka michache ijayo tutarajie mabadiliko makubwa ya dunia”
Waliendelea kuongea mpaka walipokuja kufuatwa kwa ajili ya chakula cha usiku , lakini Diana aligoma na kuondoka na Mheshimiwa Barrack hakumzuia.