singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #2,961
SEHEMU YA 538.
Ijapokuwa mwanzoni alisema hatomtambua Edna hadharani kama mtoto wake , lakini likija swala linalomuhusu mara nyingi huwa siriasi sana , hivyo mara baada ya Linda kumwmabia kwamba kuna kitu kinachoendelea katika jumuia ya siri ya Ant- illuminat kinachohusiana na Edna mapigo yake ya moyo yaliongezeka kasi.
“Edna anaetarajiwa kuwa kiongozi wa kundi la Ant – illuminat”Aliongea Linda na kumfanya raisi Jeremy kuwa kama mtu ambaye hajasikia vizuri.
“Linda unataka kumaanisha nini ?”
“Ni kama nilivyosema mheshimiwa , Edna ndio kiongozi mtarajiwa wa kundi la Ant- illuminat na mpaka sasa umoja upo katika hatua ya pili kuthibitisha hilo”Aliongea Linda na kumfanya Raisi Jeremy kuegamia kiti chake kwa muda kama mtu ambaye anajaribu kusharabu maneno ambayo amaeambiwa.
“Mheshimiwa nadhani upo kwenye mshutuko na taarifa hii , lakini ninachojaribu kukuambia ni kitu kilichotokea , Edna amepitia hatua ya kwanza kuthibitika kama kiongozi”
“Kama kauli yako ni sahihi, Linda unamaanisha nini swala la kuthibitisha , Edna hana uhusiano wowote na kundi la Ant- illuminat na sio mwanachama kwanini itokee tu awe kiongozi?”
“Hata hilo ni swali ambalo wengi walijiuliza na mpaka sasa hakuna jibu kamili”
“Unamaanisha nini hakuna jibu kamili?”Aliuliza na kumfanya Linda kufikiria na kisha akaamua kumwelezea kwa ufupi kile kilichotokea Tanzania mwezi uliopita Edna kutoa pete ambayo inamtambulisha kama kiongozi , mpaka anakuja kumaliza Raisi Jeremy alikuwa kwenye mshangao mno na hakuamini maneno ya Linda.
“Linda hiki ulichosema ni kweli?”
“Ni kweli mheshimiwa , lakini licha ya hivyo mpaka sasa Edna bado hajatambulika kama kiongozi , kilichofanyika ni hatua ya kwanza tu ya kuona kama kweli ni yeye”.Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kuwaza, kama kweli kulikuwa na pete je pete hio Edna kaitoa wapi? Au Roma ndio kampatia , alijiuliza maswali ya aina hio.
“Okey tuseme maneno yako ni sahihi, vipi kuhusu hatua ya pili?”
“Mheshimiwa kuhusu hilo sijui chochote, lakini ninachofahamu upo mchoro wa unabii ambao ndio utathibitisha hilo”
“Mchoro wa unabii!!?”
Kila neno ambalo amesikia kutoka kwa Linda lilikuwa la kushangaza ambalo halikuaminika kabisa kwake.
“Mheshimiwa nilichojaribu kukuambia ni siri ya jumuia, nimejitoa muhanga kuvunja sheria kutokana na deni kubwa ambalo unanidai, hivo sina kingine cha kuelezea ila hiko ndio kinachoendelea na kinachomuhusu Edna”Aliongea na Raisi Jremy hakutoa jibu lolote zaidi ya kuonekana kuwaza kwa takribanni dakika mbili a kisha akamwangalia Linda.
“Jana nimepewa taarifa ya siri ambayo inahusiana na mpango TASAC na nilichosikia ni kwamba jamii hii ya Ant- illuminat ipo chini ya ushawishi wa ukamilishwaji wa mpango TASAC na mimi ndio kiongozi ambaye nilipatia jukumu la kuusimamia katika bara la Afrika”
“Najua hilo mheshimiwa wewe kuwa kiongozi wa mpango huo , lakini sina taarifa za mpango huu kuwa chini ya ushawishi wa umoja wetu”
“Ninachotaka kusema Linda kamnitaendelea kuendelea kuwa kiongozi basi nitahitaji majibu ninayoyataka”Aliongea Jeremy na kumfanya Linda kushangaa.
“Mheshimiwa unamaanisha?”
“Linda nadhani unakumbuka makubaliano yangu na raisi wa Urusi yalikuwaje?”
“Ndio nakumbuka mheshimiwa”
“Nilikubali kuongoza mpango huu kutokana na kwamba nilihitaji majibu , kwa upande wangu nimefanya kazi kubwa lakini kwa upande wao hawajatimiza ahadi yao mpaka sasa , ni kweli kwamba nilipata baadhi ya taarifa lakini hawakutimiza kitu nilichokuwa nikitaka , kitu kinachohusiana na mtoto wangu Lorraine, kama kweli mpango TASAC upo chini ya ushawishi wa umoja huu basi nahitaji majibu zaidi”
“Lakini mheshimiwa ulishasema serikali ya Urusi imeacha kabisa kufatilia swala linahosiana na mpango LADO, unafikiri wanaweza kuwa na majibu unayoyataka?”
“Upo sahihi Linda kwasasa wanaweza wasinipe majibu kwasababu Rwanda ni nchi ndogo , ila kwa kushirikiana na PANAS nitapata majibu ya maswali yangu yote na isitoshe ushasema kuna mchoro wa unabii”
“Ndio mheshimiwa nimesema hilo lakini ni swala ambalo halijathibitishwa”
“Na siwezi kusubiri lisibitishwe ndio nichukue hatua , kwasasa Desmond hayupo nchini na haonekani mahali alipo na inabidi nianze harakati za kumrudisha Edna nchini Rwanda kwa namna yoyote ile na hatua ya kwanza lazima nimwambie kila kitu kuhusu pacha wake nadhani ana maswali juu ya hilo”Aliongea.
“Mheshimiwa kila kitu?, huoni kama mume wake kamficha kwasababu maalumu”
“Unafikiri kuna sababu gani ya kumficha mpaka sasa , Roma alipaswa amuambie kabla hata hawajaenda kufanya sherehe lakini akamficha , kama ameshindwa kumwambia yeye nitamwambia mimi kama mzazi”
**********
“Mkurugenzi , timu ambayo inasimamia filamu imetuma ripoti kwamba wanamalizia kipengele cha mwisho hapa nchini Tanzania kukamilisha muvi yote , hivyo mpango wao ni kuandaa sherehe ya kuwapongeza waigizaji na watu wote waliohusika?”Aliongea Daudi.
“Unamaanisha Muvi anayoongoza director Fabby Lassay?”
“Ndio mkurugenzi”.
Roma alijikuta kidogo akiwaza tokea muvi ianze ni kama hajahusika hata kidogo kufatilia maendeleo ya Sophia na isitoshe ni mara yake ya kwanza kuigiza filamu.
“Sindhani kama ni tatizo kampuni yetu inaweza kusaidia kuandaa kila kitu nadhani ndio maana wakakupatia taarifa”Aliongea Roma na Daudi alikubali.
“Sijamuona Wendy tokea asubuhi?”
“Ndio mkurugenzi Wendy yupo likizo ya uzazi?”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa lakini aliishia kutingisha kichwa.
Roma alijiuliza kama asingekuwa wa tofauti huenda muda huo angekuwa na watoto wengi tu , lakini vilevile aliona huenda maisha yake yasingekuwa ya aina hio, baada ya kupata wazo la watoto hapo hapo alimkumbuka Rose ambaye hakuw akijua maendeleo yake , kwani katika wanawake wake wote aliekuwa akipanda levo kwa spidi alikuwa ni Rose.
Siku chache mbele , ikiwa ndio inaelekea mwishoni mwa mwezi wa sita Roma alitumia muda mwingi kufika kazini kama kawaida, ijapokuwa hakuwa na majukumu makubwa lakini aliweza kufanya baadhi ya vikao na kushiriki baadhi ya matukio ya kampuni na hakuboreka kwani aliona ratiba hizo ni kama kiungo tu kwenye maisha yake ya kiburudani, hakutaka kujichosha sana , kwani alichukulia kama vile yupo likizo ya maisha,
Aliona kazi kubwa alishafanya tokea alipokuwa mdogo na siku ambayo aliamua kujitoa katika maisha yake aliokuwa akifanya na kurejea Tanzania ilikuwa ni kama mapumziko au kustaafu , lakini licha ya hivyo historia ilikuwa ikimfuata kila mahali , hivyo hakutaka kushidana na kile kinachotokea mbele yake , kukiwa na tatizo aliona atashughulika nalo na akipata muda wa mapumziko anautumia vizuri.
Upande wa Tanya aliweza kukamilisha kazi ambayo aliagizwa na siku chache tu kifo cha Mzee Longoli kilitangazwa katika vyombo vya habari , huku chanzo cha kifo chake kikiwa ni mzee huyo kujipiga mwenyewe risasi , lakini ukweli ni kwamba Tanya aliweza kumchoma Mzee huyo na dawa maalumu ambayo ilimsababishia maumivu makali sana , maumivu ambayo alishindwa kuyavumilia na kuishia kukatisha uhai wake.
Staili hio ya kimauaji ilikuwa ikifanyika sana katika ulimwengu wa kihalifu lakini tatizo ni kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kutoa dawa hio na asigundulike.
Baada ya kifo cha Mzee Longoli moja kwa moja aliehusishwa kufanya jambo hilo ni ukoo wa Kweka , kwani kwa muda mrefu Raisi Senga na familia yake hawakuwa na mahusiano mazuri kutokana na mzee huyo kumsapoti sana marehemu raisi Kigombola, hivyo kifo chake kilitafsiriwa kama ukoo huo unajaribu kumaliza maadui zake na kuendeleza kujikita zaidi katika siasa ndani ya Tanzania.
Ilionekana kama babu yake Roma alikuwa akitarajia maamuzi ambayo angefanya kwani mara baada ya taarifa ya kifo cha Mzee Longoli kazi kubwa ilifanyika kutuliza familia nzima hususani mtoto wake mkubwa ambaye ni raisi.
Mheshimiwa Raisi Hassani Longoli kutoka Zanzibar alijua ni kipi kinaendelea lakini kwa wakati huo hakuwa na nguvu ya kisiaza zaidi kama ilivyo kuwa mwanzo wakati Raisi Kigombola akiwa hai, hivyo akafunika kombe mwanaharamu apite.
Jambo moja ambalo lilimshangaza Roma ni namna ambavyo Raisi Senga alihusika kwa kiasi kikubwa kuzima swala hilo na haikumshangaza yeye tu hata babu yake Afande Kweka aliliona hilo na moja kwa moja alichukulia kama ishara nzuri ya familia kurudi na kuwa kitu kimoja.
Tanya mara baada ya kazi hio , Roma hakuta aendeleee kubaki Tanzania , kwani alimleta kutokana na hofu ya Yan Buwen , hivyo alimpa likizo ya kurudi Japani ili kuendelea kusimamia maendeleo ya kundi la Yamata.
Roma alitumia muda mwingi kusimamia warembo wake kujifunza mbinu za kijini na wakati huo huo akiendelea kutengeneza vidonge na alijikuta akifarijika mara baada ya kuona karibia wote walikuwa na maendeleo makubwa zaidi.
Mtu ambaye alikuwa ndio anaanza ni Najma lakini alibahatika yeye kuanza na vidonge hivyo hakutumia nguvu nyingi kama ilivyokuwa kwa wenzake ambao walianza bila viodonge , lakini licha ya hivyo Roma aliamini atapanda levo taratibu.
Ilikuwa bado ni giza licha ya kwamba saa kumi na mbili asubuhi ilikuwa imetimia , pengine ni kutokana na dalili ya mvua ya siku hio.
Katika kitanda kikubwa cha tano kwa sita alionekana Amina ambaye alikuwa amelalia kifua cha Roma kama kifaranga cha kuku , mabega yake ya rangi nyeupe yalionekana wazi lakini muda huo alikuwa kwenye usingizi mzito na hio yote ni kutokana na kazi nzito ambayo imefanyika usiku kucha.
Roma tokea arudi Korea utaratibu wake ulikuwa ni uleule , kwasababu Lanlan alikazania kulala na mama yake, basi asingeendelea kulala peke yake na kukumbatia mto , hiyo ilimpa nafasi ya kwenda kutembelea wanawake zake usiku.
Mara nyingi Roma kila muda wa chai ukikaribia basi atakuwa chumbani kwake ndani ya muda akiwa ashajiandaa tayari ili kuonyesha kwamba alikuwa amelala ndani ya nyumba , lakini ukweli alikuwa akijua kabisa wanafamilia hao walikuwa wakijua kile kinachoendelea , lakini licha ya hivyo hakuna ambaye alikuwa na ujasiri wa kuongea neno lolote kuuliza.
Wakati Roma akiwa amefumba macho ghafla tu alishtuka kutoka usingizini na kufumbua macho na kitendo cha kutingishika kilimwamsha Amina.
Honey , unafanya nini , bado nina usingizi”Alilalamika mrembo Amina.
“Nimeweza hata kupata msisimko kwa hapa , Rose kafanikiwa kupata ufunuo na kukamilisha kuingia katika levo ya Nafsi”Aliongea Roma huku akionyesha furaha.
SEHEMU YA 539.
Kwa kipindi chote ambacho Roma alikuwa nje ya nchi Rose ndio ambaye pekee alionyesha jitihada kubwa za kujifunza mbinu hizo za kichawi , alikuwa ni mara chache sana kuonekana mtaani , kila alipoamka alikuwa akijifungia chumbani kwake na muda mwingine angetafuta mlima wowote na kutulia huko akiendelea kujifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Roma tokea arudi alishindwa kumpata , kwani hakuwepo hata nyumbani na alijua atakuwa sehemu akiendelea kujifunza , hivyo hakutaka kumsumbua kumtafuta na kuacha yeye mwenyewe kuweza kufanikisha bila ya kumuingilia.
Sasa alikuwa na uwezo wa kuweza kupata hisia za uwepo wa mtu anaetumia nguvu za kijini hata kwa mbali kwasababu Tanzania ni nchi tulivu na ina nguvu kidogo sana za kiroho tofauti na nchi nyingine.
“Kweli , lakini umejuaje?”
“Tanzania inatembelewa na majini ndio , lakini hakuna jini lolote ambalo linajifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi na sio hivyo tu kwa binadamu pia , ukiachana na mtu ambaye najua yupo kwenye levo ya Nafsi , sidhani kama kuna mwingine ambaye anaweza kuwa katika levo hio akawa hapa Tanzania ,sasa kumeongezeka mtu mwingine ambaye yupo tayari kwenye levo ya Nafsi ambaye ashapata ufunuo wa siraha , unadhani atakuwa nani kama si Rose?”Aliongea Roma na palepale alitoka kitandani na kuvaa mavazi yake na kuondoka akimuaga kwamba anaenda kumtafuta Rose
Dakika chache mbele Roma aliweza kufuata upande ambao anapata msisimko na alikuja kutokezea kwenye kilele cha mlima wa msitu wa Pugu.
Kwa mazingira namna yalivyotulia , hakika ilionyesha Rose alikuwa ameamua haswa kutaka kujifunza mbinu hizo , maana ni ngumu sana kumkuta mtu ndani ya msitu huo bila ya kuwa na wasiwasi na baridi yote hio ya asubuhi , lakini licha ya hivyo Rose mwili wake haukua ukipata baridi kwani tayari alikuwa na nguvu za kijini zinazozunguka kwenye mwili wake , hivyo kuwa rahisi kuvumilia baridi kali.
Roma alimkuta Rose akiwa amesimama kwenye kilele hicho akionekana kushangaa mazingira , alikuwa amevalia sweta la rangi ya bluu na suruali ya jeans.
Katika macho ya Roma alimuona kama mrembo huyo amezaliwa upya , urembo wake uliongezeka maradufu mno na kwa mwanaume yoyote ambaye angemuona huenda angetokea kumpenda sana kwani alikuwa akisambaza Aura ya mvuto usiokuwa wa kawaida, hakika nguvu za kijini zilikuwa zinafaida.
Rose mara baada ya kuhisi mtu nyuma yake aligeuka na alijikuta akishangaa huku akimwangalia Roma , alijikuta akijawa na tabasamu kwani ni zaidi ya mwezi hawakuwa wameonana.
“Vipi unaonaje , kama vile umeingia kwenye ulimwengu mpya kabisa si ndio?”Aliuliza Roma
“Hapana”
“Kama sio hivyo unajisikiaje?”
“Ni ulimwengu huu huu, lakini kila kitu kinaonekana kuwa tofauti na zamani”Aliongea na kumfanya Roma kutingisha kichwa.
“Kila mtu ni tofauti hususani kwenye swala la utashi na hisia za kimazingira , hata kama kuwe kuna mfanano lakini ufunuo wa kiuelewa utakuwa tofauti , hivyo siwezi kuelewa ni kipi umefunuliwa mpaka kukamilisha levo ya nafsi na hivyo hivyo siwezi kujua wengine watapata ufunuo gani wa kimazingira”
Baada ya kuingia levo ya Nafsi moja kwa moja Rose ni kama amezaliwa upya kimwonekano , ijapokuwa alikuwa akionekana kwa nje ni yuleyule na ngozi yake ileile , lakini alikuwa akizingirwa na nguvu isiokuwa ya kawaida ambayo ilikuwa ikimlinda
Muda huo huo alihisi mkono waRoma ukipita ukipita juu ya uso wake na palepale wimbi la nguvu ya mbingu na ardhi liliweza kutikisa miti na kuinua upepo mkali.
“Ijapokuwa ni mwaka na nusu sasa tokea mara ya kwanza tulivyokutana lakini ni mara yangu ya kwanza kuhisi kuwa na ukaribu zaidi na wewe , ijapokuwa uwezo wangu bado ni wa chini lakini nimeanza kuelewa mawazo yako pamoja na hisia zako , kila kitu sasa ni uhalisia wenye kueleweka katika akili yangu , ninajihisi kuwa mwenye furaha sana”Aliongea Rose.
“Nadhani ni vizuri ukiachana na maswala ya furaha kwa sasa , ushaingia katika levo ya Nafsi lakini bado unapaswa kuendelea zaidi na zaidi , nimekuja na vidonge vya daraja la kati , unaweza sasa kutumia kwasababu ushapata ufunuo wako “Aliongea na kisha palepale alicheza na kauni za anga na palepale lilionekaa vijichupa vya platiki ambavyo huhifadhia vidonge kwenye mikono yake.
“Kuna vidonge vitano hapa vya mawingu na kimoja cha anga la bluu , unaweza kumeza kidongea cha mawingu ili kukusaidia kuweza kukusanya mvuke na kuugeuza mai na baada ya hapo kufanya maji kuwa siraha ya kiroho ya msisimko na baada ya hapo utatumia sasa kidonge cha anga la bluu na kitakusaidia sasa kuelewa zaidi mpangilio wa mbingu , kwa maelezo ya Rufi kidonge cha anga la bluu ni adimu sana katika miliki za kijini , kama sio bahati na uwezo wangu basi ingekuwa ni ngumu kwa binadamu wa kawaida kama wewe kuweza kupata kidonge cha aina hii”
Aliongea Roma na kisha akampatia Rose kijichupa ambacho kilikuwa na vidonge vya mawiangu na kimoja cha anga la bluu.alikwa anapenda sana kuendelea kuvuna nishati ya mbingu na ardhi hivyo hakutaka kukosa nafasi ya kupata kidonge.
Roma mara baada ya kumwangalia Rose aliekuwa na mwoneonako wa furaha na moyo wake ulipata joto la furaha pia.
“Nimekupa vidonge vya thamani kubwa , ni muda wako na wewe angalau kunipa hata zawadi”Aliongea Roma na Rose palepale alimkumbatia Roma na kuzungusha mikono shingoni na kumbusu
“Hubby kwahio mpaka sasa siwezi kuzeeka haraka ?”Aliuliza Rose na Roma alitingisha kichwa kukubali.
“Kwasasa huwezi kuzeeka haraka , lakini licha ya hivyo hupaswi kupumzika jitahidi angalau ufikie mwisho kabisa mwa levo ya Nafsi huenda ukafanikiwa kuingia katika levo ya Dhiki na kuipita kabisa lakini yote hayo yatatokea baaada ya kukusanya nguvu nyingi”
“Kwahio kama nitafika katika levo ya kupita dhiki nitakuwa na uwezo wa kuingia katika steji ya kudhibiti moto wa aina tatu , kubadilisha mvuke kuwa barafu na kudhibiti Radi si ndio?”Aliuliza Rose.
“Sijajua lakini naamini ni zaidi ya hivyo, mbinu yangu niliowapatia ni ya kipekee sana, sidhani kama ni kweli imeweza kutokea katika miliki ya kijini ya PANAS kama wengi walivyosema lakini kwa staili nilivyoirahisisha ni zaidi ya mbinu zote zinazotumiwa na majini”
PANAS ni jamii ya kijini pia kama ilivyo kwa Hongmeng , lakini inasemekana utofauti wa PANAS na Hongmeng ni kwamba miliki hio ipo nje ya bara la Asia na hata Hongmeng ambao walijaribu kusafiri kwenda PANAS ilibidi kwanza wasafiri kuja Afrika, ni jamii ambayo haina muunganiko wowote kabisa na jamii kibinadamu kwa miaka na miaka , lakini hivi karibuni jamii hio inaanza kuonyesha matamanio yao na binadamu wa kawaida.,
Rose sasa alikua sio wa kawaida, alikuwa binadamu ambaye amefanikiwa kupata ufunuo wa nguvu za kijini na hisia alizokuwa akipata akiangalia mazingira ni tofauti kabisa na binadamu wa kawaida na alijikuta hata kundi lake la Tembo kuona ni kitu ambacho hakina maisha marefu kabla ya serikali kuingilia.
Rose sasa alikuwa akipaa tu angani kama Roma na zoezi lake la kwanza kufanikiwa kupaa ni kurudi nyumbani kwa kumfuata Roma nyuma na alijikuta kufumba na kufumbua wapo maeneo ya Ununio na alijikuta mapigo ya moyo yakidunda kasi mno akiwa kama haamini , kwani kila kitu kinaonekana kuwa kipya kwake.
Baada ya kutembea wakipita nje ya nyumba ya Nasra waliweza kukukutana na mama yake Nasra ambaye alikuwa akitoka kwenda kukimbia kuchukua mazoezi.
Tokea mama yake Nasra kufika jijini alikuwa amebadilika mno , kwanza alinenepa na pia mwonekano wake ni wa kitajiri zaidi , hakuwa tofauti sana na Blandina au Bi Wema.
Licha ya kumuona Roma na Rose wakiwa pamoja asubuhi hio hakushangaa sana kwani alikuwa akijua bwana huyo alikuwa na zaidi ya wanawake wengine nje na hata ile hatia aliokuwanayo juu ya Nasra kutoka na mume wa rafiki yake kupungua.
Roma mara baada ya kufika katika nyumba ya Rose waliweza kumkuta Dorisi akitokea jikoni , ilionekana ndio alikuwa akiandaa kifungua kinywa.
Dorisi uwezo wake wa kuvuna nishati za mbingu na Ardhi ulimtegemea zaidi Roma katika kufanya nae mapenzi, baada ya kusikia mwenzake kapasua , alijikuta akiona wivu na kuamini mtu ambaye ataweza kupata mtto wa Roma mapema basi ni Rose na sio yeye.
Roma hakujali sana mawazo ya Dorisi zaidi ya kumwambia ahimize kufungua kinywa kwani leo atapatia hapo hapo kabla ya kurudi nyumbani.
Roma mara baada ya kusema hivyo alimpigia simu mama yake na kumweleza kwamba asihesabiwe kwenye kifugua kinywa , lakini pia alimweleza juu ya mafanikio ya Rose na mara baada ya Blandina kusikia taarifa hio alijikuta akifurahi mno.
Alikuwa na wasiwasi kutokana na Roma kutokuwa wa kawaida hivyo kumpelekea kutokupata mtoto , lakini mara baada ya kusikia kuhusu Rose kupanda levo alijikuta akifurahi mno hakujali ni mwanamke gani wa kwanza kumzalia Roma mtoto , yeye shida yake ni mjukuu tu , alikuwa na mjukuu Lanlan lakini bado hakuridhika kwani bado alijua Lanlan ni wa kulelewa.
“Roma nadhani tusherehekee mafanikio ya Rose”
“Mama unataka tusherehekee vipi??”
“Leo si wikiend na hakuna mambo mengi ya kufanya , kwanini tusiwaalike wengine wakifika nyumbani na kupika chakula na kufurahi?”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kuona sio jambo zuri kidogo kutokana na Edna lakini aliependekeza ni mama yake na ni kweli Rose kapata mafanikio makubwa na anapaswa kupongezwa.
“Kama ni hivyo basi tumshirikishe Edna kwanza na baada ya hapo nitawaambia”Aliongea Roma na kisha walikubaliana na kukata simu.
“Mbona unacheka Dorisi?”Aliuliza Roma mara baada ya kuwaambia pendekezo la mama yake.
“Najua mama anamtumia Rose kama kisingizio tu , ukweli ni kwamba ulivyokuwa Korea mara nyingi tulishinda nyumbai kwako tukicheza karata, nadhani anataka tukusanyike tuendelee na mchezo”
“Kucheza karata?”Roma alishangaa kwani ilikuwa ni habari mpya lakini wakati huo huo moyo wake ukiwa na wasiwasi , kwanni kama kitu kama hiko kikiendelea basi Edna lazima hatopendezwa na jambo hilo na kupelekea migogoro.
Roma mara baada ya kumaliza kifungua kinywa alipokea simu kutoka kwa Daudi akimkumbushia swala la tafrija ndogo inayohusiana na waigizaji wote walioshiriki katika filamu hivyo kumweleza eneo ambalo tafrija hio ingefanyika, baada ya kukata simu aliona itakuwa vizuri kumpigia simu Sophia kwa kufanikisha swala hilo.
Baada ya kukaa muda mfupi aliondoka na kurudi nyumbani na aliweza kumkuta Edna akicheza na Lanlan eneo la sebuleni na alimweleza juu ya Sophia na watu wa kampuni ya Penguin kuandaa tafrija lakini Edna alionyesha kujua kila kitu.
“Unaweza kwenda , mimi nitashiriki siku ya uzinduzi wa filamu “
“Lakini Sophia anaweza kuwa na huzuni kama hutoenda”
“Nishampigia tayari Sophia na kumpongeza na nimemwambia sitohudhuria , sidhani kama atahuzunika kwa jinsi tulivyokubaliana”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuelewa , hata hivyo Edna alikuwa karibu sana na maendeleo ya Sophia kuliko ilivyokuwa yeye.
“Hubby! Je utamfundisha na Lanlan kuvuna nishati hapo baadae?”Aliuliza Edna wakati Roma akicheza gemu la kuzungusha boksi la kufananisha rangi.
“Hilo lipo wazi, Lanlan ni binti yetu hatuwezi kumuacha asijifunze na isitoshe Lanlan ana vigezo vikubwa zaidi kuliko hata mimi wakati nikijifunza , mpango wangu ni kumrithisha nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo , ni mtoto wetu wa kwanza hivyo lazima apate vipaumbele”
“Kama ni hivyo kwanini hujamwelekza chochote?”
“Kwanza kabisa Lanlan bado ni mdogo , hawezi kuelewa baadhi ya mambo kwa umri wake, kitu cha pili siwezi kumpatia vidonge na kisha nikamrithisha andiko anaaweza kugeuka na kuwa mkatili , tatu sina uhakika maadui zangu ambao watajitokeza , kama ujuavyo andiko hili huwindwa na watu wengi hivyo nikimrithisha akiwa na umri mdogo moja kwa moja namfanya kuwa mlengwa , hivyo watu watataka kupata mbinu yangu kupitia kwake na nitamuweka kweye hatari, kwasasa tumuache afurahie utoto wake”
“Malengo yangu ni kumuona akiendelea kuwa na siha njema na kuweza kujilinda yeye mwenyewe , lakini nina wasiwasi anaweza kuja kuwa kama wewe kuanza kupigana nakuwa na utukutu mwingi akishaanza kujifunza , hata kama ataweza kushida kila wakati lakini bado itanifanya kuwa na wasiwasi”Aliongea Roma lakini hakutaka kuongezea neno kwani alijua huo ni waswasi wa kawaida kwa mama kwenda kwa mtoto.
Ilionekana Blandina alikubaliana na Edna, hivyo muda wa mchana warembo wote waliweza kukusanyika katika nyumba ya Roma kusherehekea mafanikio ya Rose, aliekosekana alikuwa ni Neema Luwazo ambaye alikuwa nje ya nchi kikazi pamoja na Mage ambaye alikuwa kazini.
Roma mara baada ya kuona kundi lote hilo la wanawake alijikuta akijisikia vibaya na vizuri kwa wakati mmoja.
Baada ya chakula kama kawaida Blandina alitoa karata na kuwataka wote wakusanyike eneo la sebuleni kwa ajili ya kucheza.
Najma pia alikuwepo na ndio ambaye alitoa sababu kwamba hakuwa akijua kucheza karata na Edna hivyo hivyo alipoambiwa ajiunge kucheza alisema hajui , lakini Nasra alimlazimisha na kumwambia atajifunza.
Roma kwa hali hio hakutaka kuendelea kubakia hapo tena, kwasababu siku hio alikuwa na ratiba ya kuhudhuria tafrija ya Sophia na waigizaji wenzake , basi aliona akatembee na kisha aunge moja kwa moja.
***********
Tafrija ilikuja kumalizika saa nne za usiku na Roma aliagana na Sophia kurudi nyumbani.Sophia alionekana kuzidi kupendeza mno na kila mwanaume ambaye alikuwa akimwangalia alimtamani.
Roma mara baada ya kuingiza gari lake ndani ya geti alishangaa mara baada ya kuona gari la Amina bado lipo , lakini pia taa za sebuleni zikiwaka muda huo.
Baada ya kuingia ndani ndipo alipokuja kushangaa mara baada ya kukuta hali ni kama alivyoiacha , lakini utofauti tu ni kwamba wengine walikuwa washaanza kusinzia kwenye masofa , huku mezani alikuwepo Edna na Amina waliokuwa wakicheza karata wakiwa siriasi.
Blandina mara baada ya Roma kuigia eneo hlo alijikuta akipata ahueni na kumwambia Roma amshawahisi Edna waghairishe wataendelea kesho.
Roma mara baada ya kuambiwa hivyo alitaka kujua kwanza kinachoendelea na hapo ndipo aliposikia kwamba baada ya Edna kufundishwa na kuelewa namna ya kucheza hakutaka kupumzika kabisa na kuchukulia siriasi mchezo huo na mtu ambaye alikuwa akiongoza kushinda ni Amina, hivyo Edna alitaka kulipa pointi zote za Amina,lakini mwishowe kila akicheza anaishia kufungwa na bado hakutaka kukata tamaa.
Roma mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akijawa na mshangao na kumwangalia Edna namna ambavyo alikuwa siriasi.
“Edna huo mchezo ni wa kubahatisha, hakuna ufundi ,unaweza kucheza mpaka kesho na usipate ushindi”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia na kisha akaangalia watu waliozunguka na kisha akageuza macho kwa Amina.
“Amina nitakupigia simu , lazima nikulipe pointi zako ulizonifunga leo”Aliongea Edna na kisha akasimama.
“Edna huu ni mchezo wa karata tu kwanini unauchukulia kama vile ni ushindani wa kibiashara?”
“Sijauchukulia kama biashara , bali ni kwamba unafurahisha , siku nyingine mkicheza lazima na mimi niwepo”Aliongea na kisha alipandisha juu kumwangalia Lanlan.
Roma alijikuta akipata ahueni na kuwasindikiza, Najma alikuwa akikaa mbezi kwenye apartment hivyo alipanda gari ya Amina na wakaondoka kwani muda ulikuwa umeenda.
Ilipita wiki moja moja , ikiwa ni siku ya jumamosi jioni wakati Roma akitoka nyumbani kwa Najma mbagala, aliweza kupokea simu kutoka nyumbani na aliekuwa akipiga ni mama yake.
“Mama kuna nini?”
“Mheshimiwa raisi Jeremy amefika na yupo na Edna wanaongea”Aliogea Blandina na kumfanya Roma kushagazwa na kauli hio.
“Lakini mbona unaongea kwa wasiwasi sana?”
“Ni kuhusu Rose”
“Rose kafanyaje?”
“Kuna watu wamejitambulisha wanatokea PANAS, wanasema Rose ashafikia levo ya Nafsi na sheria haimruhusu kuendelea kuishi katika ulimwengu wa kawaida , hivyo wanataka kuondoka nae”
“PANAS!!”Roma alijikuta akimaka , kwa mara ya kwanza anasikia watu kutoka PANAS.
“Mama nakuja sasa hivi”
“Wahi maana Rose kakataa na kasema watampata kama wataweza kumshinda baada ya pambano , hivyo wametoka kwenda kupigana”Aliongea na kumfanya Roma kuzidi kuwa na wasiwasi na aliona hawezi kuendesha gari na alimgeukia Najma na kisha akalipaki pembeni na kumpatia ufunguo wa gari na kumwambia anapaswa kuondoka kuwahi nyumbani , lakini nasra alipotaka kumwambia Roma hajui kuendesha gari , Roma ashapotea kwenye macho yake na kumuacha akiwa amekodoa macho.
Ijapokuwa mwanzoni alisema hatomtambua Edna hadharani kama mtoto wake , lakini likija swala linalomuhusu mara nyingi huwa siriasi sana , hivyo mara baada ya Linda kumwmabia kwamba kuna kitu kinachoendelea katika jumuia ya siri ya Ant- illuminat kinachohusiana na Edna mapigo yake ya moyo yaliongezeka kasi.
“Edna anaetarajiwa kuwa kiongozi wa kundi la Ant – illuminat”Aliongea Linda na kumfanya raisi Jeremy kuwa kama mtu ambaye hajasikia vizuri.
“Linda unataka kumaanisha nini ?”
“Ni kama nilivyosema mheshimiwa , Edna ndio kiongozi mtarajiwa wa kundi la Ant- illuminat na mpaka sasa umoja upo katika hatua ya pili kuthibitisha hilo”Aliongea Linda na kumfanya Raisi Jeremy kuegamia kiti chake kwa muda kama mtu ambaye anajaribu kusharabu maneno ambayo amaeambiwa.
“Mheshimiwa nadhani upo kwenye mshutuko na taarifa hii , lakini ninachojaribu kukuambia ni kitu kilichotokea , Edna amepitia hatua ya kwanza kuthibitika kama kiongozi”
“Kama kauli yako ni sahihi, Linda unamaanisha nini swala la kuthibitisha , Edna hana uhusiano wowote na kundi la Ant- illuminat na sio mwanachama kwanini itokee tu awe kiongozi?”
“Hata hilo ni swali ambalo wengi walijiuliza na mpaka sasa hakuna jibu kamili”
“Unamaanisha nini hakuna jibu kamili?”Aliuliza na kumfanya Linda kufikiria na kisha akaamua kumwelezea kwa ufupi kile kilichotokea Tanzania mwezi uliopita Edna kutoa pete ambayo inamtambulisha kama kiongozi , mpaka anakuja kumaliza Raisi Jeremy alikuwa kwenye mshangao mno na hakuamini maneno ya Linda.
“Linda hiki ulichosema ni kweli?”
“Ni kweli mheshimiwa , lakini licha ya hivyo mpaka sasa Edna bado hajatambulika kama kiongozi , kilichofanyika ni hatua ya kwanza tu ya kuona kama kweli ni yeye”.Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kuwaza, kama kweli kulikuwa na pete je pete hio Edna kaitoa wapi? Au Roma ndio kampatia , alijiuliza maswali ya aina hio.
“Okey tuseme maneno yako ni sahihi, vipi kuhusu hatua ya pili?”
“Mheshimiwa kuhusu hilo sijui chochote, lakini ninachofahamu upo mchoro wa unabii ambao ndio utathibitisha hilo”
“Mchoro wa unabii!!?”
Kila neno ambalo amesikia kutoka kwa Linda lilikuwa la kushangaza ambalo halikuaminika kabisa kwake.
“Mheshimiwa nilichojaribu kukuambia ni siri ya jumuia, nimejitoa muhanga kuvunja sheria kutokana na deni kubwa ambalo unanidai, hivo sina kingine cha kuelezea ila hiko ndio kinachoendelea na kinachomuhusu Edna”Aliongea na Raisi Jremy hakutoa jibu lolote zaidi ya kuonekana kuwaza kwa takribanni dakika mbili a kisha akamwangalia Linda.
“Jana nimepewa taarifa ya siri ambayo inahusiana na mpango TASAC na nilichosikia ni kwamba jamii hii ya Ant- illuminat ipo chini ya ushawishi wa ukamilishwaji wa mpango TASAC na mimi ndio kiongozi ambaye nilipatia jukumu la kuusimamia katika bara la Afrika”
“Najua hilo mheshimiwa wewe kuwa kiongozi wa mpango huo , lakini sina taarifa za mpango huu kuwa chini ya ushawishi wa umoja wetu”
“Ninachotaka kusema Linda kamnitaendelea kuendelea kuwa kiongozi basi nitahitaji majibu ninayoyataka”Aliongea Jeremy na kumfanya Linda kushangaa.
“Mheshimiwa unamaanisha?”
“Linda nadhani unakumbuka makubaliano yangu na raisi wa Urusi yalikuwaje?”
“Ndio nakumbuka mheshimiwa”
“Nilikubali kuongoza mpango huu kutokana na kwamba nilihitaji majibu , kwa upande wangu nimefanya kazi kubwa lakini kwa upande wao hawajatimiza ahadi yao mpaka sasa , ni kweli kwamba nilipata baadhi ya taarifa lakini hawakutimiza kitu nilichokuwa nikitaka , kitu kinachohusiana na mtoto wangu Lorraine, kama kweli mpango TASAC upo chini ya ushawishi wa umoja huu basi nahitaji majibu zaidi”
“Lakini mheshimiwa ulishasema serikali ya Urusi imeacha kabisa kufatilia swala linahosiana na mpango LADO, unafikiri wanaweza kuwa na majibu unayoyataka?”
“Upo sahihi Linda kwasasa wanaweza wasinipe majibu kwasababu Rwanda ni nchi ndogo , ila kwa kushirikiana na PANAS nitapata majibu ya maswali yangu yote na isitoshe ushasema kuna mchoro wa unabii”
“Ndio mheshimiwa nimesema hilo lakini ni swala ambalo halijathibitishwa”
“Na siwezi kusubiri lisibitishwe ndio nichukue hatua , kwasasa Desmond hayupo nchini na haonekani mahali alipo na inabidi nianze harakati za kumrudisha Edna nchini Rwanda kwa namna yoyote ile na hatua ya kwanza lazima nimwambie kila kitu kuhusu pacha wake nadhani ana maswali juu ya hilo”Aliongea.
“Mheshimiwa kila kitu?, huoni kama mume wake kamficha kwasababu maalumu”
“Unafikiri kuna sababu gani ya kumficha mpaka sasa , Roma alipaswa amuambie kabla hata hawajaenda kufanya sherehe lakini akamficha , kama ameshindwa kumwambia yeye nitamwambia mimi kama mzazi”
**********
“Mkurugenzi , timu ambayo inasimamia filamu imetuma ripoti kwamba wanamalizia kipengele cha mwisho hapa nchini Tanzania kukamilisha muvi yote , hivyo mpango wao ni kuandaa sherehe ya kuwapongeza waigizaji na watu wote waliohusika?”Aliongea Daudi.
“Unamaanisha Muvi anayoongoza director Fabby Lassay?”
“Ndio mkurugenzi”.
Roma alijikuta kidogo akiwaza tokea muvi ianze ni kama hajahusika hata kidogo kufatilia maendeleo ya Sophia na isitoshe ni mara yake ya kwanza kuigiza filamu.
“Sindhani kama ni tatizo kampuni yetu inaweza kusaidia kuandaa kila kitu nadhani ndio maana wakakupatia taarifa”Aliongea Roma na Daudi alikubali.
“Sijamuona Wendy tokea asubuhi?”
“Ndio mkurugenzi Wendy yupo likizo ya uzazi?”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa lakini aliishia kutingisha kichwa.
Roma alijiuliza kama asingekuwa wa tofauti huenda muda huo angekuwa na watoto wengi tu , lakini vilevile aliona huenda maisha yake yasingekuwa ya aina hio, baada ya kupata wazo la watoto hapo hapo alimkumbuka Rose ambaye hakuw akijua maendeleo yake , kwani katika wanawake wake wote aliekuwa akipanda levo kwa spidi alikuwa ni Rose.
Siku chache mbele , ikiwa ndio inaelekea mwishoni mwa mwezi wa sita Roma alitumia muda mwingi kufika kazini kama kawaida, ijapokuwa hakuwa na majukumu makubwa lakini aliweza kufanya baadhi ya vikao na kushiriki baadhi ya matukio ya kampuni na hakuboreka kwani aliona ratiba hizo ni kama kiungo tu kwenye maisha yake ya kiburudani, hakutaka kujichosha sana , kwani alichukulia kama vile yupo likizo ya maisha,
Aliona kazi kubwa alishafanya tokea alipokuwa mdogo na siku ambayo aliamua kujitoa katika maisha yake aliokuwa akifanya na kurejea Tanzania ilikuwa ni kama mapumziko au kustaafu , lakini licha ya hivyo historia ilikuwa ikimfuata kila mahali , hivyo hakutaka kushidana na kile kinachotokea mbele yake , kukiwa na tatizo aliona atashughulika nalo na akipata muda wa mapumziko anautumia vizuri.
Upande wa Tanya aliweza kukamilisha kazi ambayo aliagizwa na siku chache tu kifo cha Mzee Longoli kilitangazwa katika vyombo vya habari , huku chanzo cha kifo chake kikiwa ni mzee huyo kujipiga mwenyewe risasi , lakini ukweli ni kwamba Tanya aliweza kumchoma Mzee huyo na dawa maalumu ambayo ilimsababishia maumivu makali sana , maumivu ambayo alishindwa kuyavumilia na kuishia kukatisha uhai wake.
Staili hio ya kimauaji ilikuwa ikifanyika sana katika ulimwengu wa kihalifu lakini tatizo ni kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kutoa dawa hio na asigundulike.
Baada ya kifo cha Mzee Longoli moja kwa moja aliehusishwa kufanya jambo hilo ni ukoo wa Kweka , kwani kwa muda mrefu Raisi Senga na familia yake hawakuwa na mahusiano mazuri kutokana na mzee huyo kumsapoti sana marehemu raisi Kigombola, hivyo kifo chake kilitafsiriwa kama ukoo huo unajaribu kumaliza maadui zake na kuendeleza kujikita zaidi katika siasa ndani ya Tanzania.
Ilionekana kama babu yake Roma alikuwa akitarajia maamuzi ambayo angefanya kwani mara baada ya taarifa ya kifo cha Mzee Longoli kazi kubwa ilifanyika kutuliza familia nzima hususani mtoto wake mkubwa ambaye ni raisi.
Mheshimiwa Raisi Hassani Longoli kutoka Zanzibar alijua ni kipi kinaendelea lakini kwa wakati huo hakuwa na nguvu ya kisiaza zaidi kama ilivyo kuwa mwanzo wakati Raisi Kigombola akiwa hai, hivyo akafunika kombe mwanaharamu apite.
Jambo moja ambalo lilimshangaza Roma ni namna ambavyo Raisi Senga alihusika kwa kiasi kikubwa kuzima swala hilo na haikumshangaza yeye tu hata babu yake Afande Kweka aliliona hilo na moja kwa moja alichukulia kama ishara nzuri ya familia kurudi na kuwa kitu kimoja.
Tanya mara baada ya kazi hio , Roma hakuta aendeleee kubaki Tanzania , kwani alimleta kutokana na hofu ya Yan Buwen , hivyo alimpa likizo ya kurudi Japani ili kuendelea kusimamia maendeleo ya kundi la Yamata.
Roma alitumia muda mwingi kusimamia warembo wake kujifunza mbinu za kijini na wakati huo huo akiendelea kutengeneza vidonge na alijikuta akifarijika mara baada ya kuona karibia wote walikuwa na maendeleo makubwa zaidi.
Mtu ambaye alikuwa ndio anaanza ni Najma lakini alibahatika yeye kuanza na vidonge hivyo hakutumia nguvu nyingi kama ilivyokuwa kwa wenzake ambao walianza bila viodonge , lakini licha ya hivyo Roma aliamini atapanda levo taratibu.
Ilikuwa bado ni giza licha ya kwamba saa kumi na mbili asubuhi ilikuwa imetimia , pengine ni kutokana na dalili ya mvua ya siku hio.
Katika kitanda kikubwa cha tano kwa sita alionekana Amina ambaye alikuwa amelalia kifua cha Roma kama kifaranga cha kuku , mabega yake ya rangi nyeupe yalionekana wazi lakini muda huo alikuwa kwenye usingizi mzito na hio yote ni kutokana na kazi nzito ambayo imefanyika usiku kucha.
Roma tokea arudi Korea utaratibu wake ulikuwa ni uleule , kwasababu Lanlan alikazania kulala na mama yake, basi asingeendelea kulala peke yake na kukumbatia mto , hiyo ilimpa nafasi ya kwenda kutembelea wanawake zake usiku.
Mara nyingi Roma kila muda wa chai ukikaribia basi atakuwa chumbani kwake ndani ya muda akiwa ashajiandaa tayari ili kuonyesha kwamba alikuwa amelala ndani ya nyumba , lakini ukweli alikuwa akijua kabisa wanafamilia hao walikuwa wakijua kile kinachoendelea , lakini licha ya hivyo hakuna ambaye alikuwa na ujasiri wa kuongea neno lolote kuuliza.
Wakati Roma akiwa amefumba macho ghafla tu alishtuka kutoka usingizini na kufumbua macho na kitendo cha kutingishika kilimwamsha Amina.
Honey , unafanya nini , bado nina usingizi”Alilalamika mrembo Amina.
“Nimeweza hata kupata msisimko kwa hapa , Rose kafanikiwa kupata ufunuo na kukamilisha kuingia katika levo ya Nafsi”Aliongea Roma huku akionyesha furaha.
SEHEMU YA 539.
Kwa kipindi chote ambacho Roma alikuwa nje ya nchi Rose ndio ambaye pekee alionyesha jitihada kubwa za kujifunza mbinu hizo za kichawi , alikuwa ni mara chache sana kuonekana mtaani , kila alipoamka alikuwa akijifungia chumbani kwake na muda mwingine angetafuta mlima wowote na kutulia huko akiendelea kujifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Roma tokea arudi alishindwa kumpata , kwani hakuwepo hata nyumbani na alijua atakuwa sehemu akiendelea kujifunza , hivyo hakutaka kumsumbua kumtafuta na kuacha yeye mwenyewe kuweza kufanikisha bila ya kumuingilia.
Sasa alikuwa na uwezo wa kuweza kupata hisia za uwepo wa mtu anaetumia nguvu za kijini hata kwa mbali kwasababu Tanzania ni nchi tulivu na ina nguvu kidogo sana za kiroho tofauti na nchi nyingine.
“Kweli , lakini umejuaje?”
“Tanzania inatembelewa na majini ndio , lakini hakuna jini lolote ambalo linajifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi na sio hivyo tu kwa binadamu pia , ukiachana na mtu ambaye najua yupo kwenye levo ya Nafsi , sidhani kama kuna mwingine ambaye anaweza kuwa katika levo hio akawa hapa Tanzania ,sasa kumeongezeka mtu mwingine ambaye yupo tayari kwenye levo ya Nafsi ambaye ashapata ufunuo wa siraha , unadhani atakuwa nani kama si Rose?”Aliongea Roma na palepale alitoka kitandani na kuvaa mavazi yake na kuondoka akimuaga kwamba anaenda kumtafuta Rose
Dakika chache mbele Roma aliweza kufuata upande ambao anapata msisimko na alikuja kutokezea kwenye kilele cha mlima wa msitu wa Pugu.
Kwa mazingira namna yalivyotulia , hakika ilionyesha Rose alikuwa ameamua haswa kutaka kujifunza mbinu hizo , maana ni ngumu sana kumkuta mtu ndani ya msitu huo bila ya kuwa na wasiwasi na baridi yote hio ya asubuhi , lakini licha ya hivyo Rose mwili wake haukua ukipata baridi kwani tayari alikuwa na nguvu za kijini zinazozunguka kwenye mwili wake , hivyo kuwa rahisi kuvumilia baridi kali.
Roma alimkuta Rose akiwa amesimama kwenye kilele hicho akionekana kushangaa mazingira , alikuwa amevalia sweta la rangi ya bluu na suruali ya jeans.
Katika macho ya Roma alimuona kama mrembo huyo amezaliwa upya , urembo wake uliongezeka maradufu mno na kwa mwanaume yoyote ambaye angemuona huenda angetokea kumpenda sana kwani alikuwa akisambaza Aura ya mvuto usiokuwa wa kawaida, hakika nguvu za kijini zilikuwa zinafaida.
Rose mara baada ya kuhisi mtu nyuma yake aligeuka na alijikuta akishangaa huku akimwangalia Roma , alijikuta akijawa na tabasamu kwani ni zaidi ya mwezi hawakuwa wameonana.
“Vipi unaonaje , kama vile umeingia kwenye ulimwengu mpya kabisa si ndio?”Aliuliza Roma
“Hapana”
“Kama sio hivyo unajisikiaje?”
“Ni ulimwengu huu huu, lakini kila kitu kinaonekana kuwa tofauti na zamani”Aliongea na kumfanya Roma kutingisha kichwa.
“Kila mtu ni tofauti hususani kwenye swala la utashi na hisia za kimazingira , hata kama kuwe kuna mfanano lakini ufunuo wa kiuelewa utakuwa tofauti , hivyo siwezi kuelewa ni kipi umefunuliwa mpaka kukamilisha levo ya nafsi na hivyo hivyo siwezi kujua wengine watapata ufunuo gani wa kimazingira”
Baada ya kuingia levo ya Nafsi moja kwa moja Rose ni kama amezaliwa upya kimwonekano , ijapokuwa alikuwa akionekana kwa nje ni yuleyule na ngozi yake ileile , lakini alikuwa akizingirwa na nguvu isiokuwa ya kawaida ambayo ilikuwa ikimlinda
Muda huo huo alihisi mkono waRoma ukipita ukipita juu ya uso wake na palepale wimbi la nguvu ya mbingu na ardhi liliweza kutikisa miti na kuinua upepo mkali.
“Ijapokuwa ni mwaka na nusu sasa tokea mara ya kwanza tulivyokutana lakini ni mara yangu ya kwanza kuhisi kuwa na ukaribu zaidi na wewe , ijapokuwa uwezo wangu bado ni wa chini lakini nimeanza kuelewa mawazo yako pamoja na hisia zako , kila kitu sasa ni uhalisia wenye kueleweka katika akili yangu , ninajihisi kuwa mwenye furaha sana”Aliongea Rose.
“Nadhani ni vizuri ukiachana na maswala ya furaha kwa sasa , ushaingia katika levo ya Nafsi lakini bado unapaswa kuendelea zaidi na zaidi , nimekuja na vidonge vya daraja la kati , unaweza sasa kutumia kwasababu ushapata ufunuo wako “Aliongea na kisha palepale alicheza na kauni za anga na palepale lilionekaa vijichupa vya platiki ambavyo huhifadhia vidonge kwenye mikono yake.
“Kuna vidonge vitano hapa vya mawingu na kimoja cha anga la bluu , unaweza kumeza kidongea cha mawingu ili kukusaidia kuweza kukusanya mvuke na kuugeuza mai na baada ya hapo kufanya maji kuwa siraha ya kiroho ya msisimko na baada ya hapo utatumia sasa kidonge cha anga la bluu na kitakusaidia sasa kuelewa zaidi mpangilio wa mbingu , kwa maelezo ya Rufi kidonge cha anga la bluu ni adimu sana katika miliki za kijini , kama sio bahati na uwezo wangu basi ingekuwa ni ngumu kwa binadamu wa kawaida kama wewe kuweza kupata kidonge cha aina hii”
Aliongea Roma na kisha akampatia Rose kijichupa ambacho kilikuwa na vidonge vya mawiangu na kimoja cha anga la bluu.alikwa anapenda sana kuendelea kuvuna nishati ya mbingu na ardhi hivyo hakutaka kukosa nafasi ya kupata kidonge.
Roma mara baada ya kumwangalia Rose aliekuwa na mwoneonako wa furaha na moyo wake ulipata joto la furaha pia.
“Nimekupa vidonge vya thamani kubwa , ni muda wako na wewe angalau kunipa hata zawadi”Aliongea Roma na Rose palepale alimkumbatia Roma na kuzungusha mikono shingoni na kumbusu
“Hubby kwahio mpaka sasa siwezi kuzeeka haraka ?”Aliuliza Rose na Roma alitingisha kichwa kukubali.
“Kwasasa huwezi kuzeeka haraka , lakini licha ya hivyo hupaswi kupumzika jitahidi angalau ufikie mwisho kabisa mwa levo ya Nafsi huenda ukafanikiwa kuingia katika levo ya Dhiki na kuipita kabisa lakini yote hayo yatatokea baaada ya kukusanya nguvu nyingi”
“Kwahio kama nitafika katika levo ya kupita dhiki nitakuwa na uwezo wa kuingia katika steji ya kudhibiti moto wa aina tatu , kubadilisha mvuke kuwa barafu na kudhibiti Radi si ndio?”Aliuliza Rose.
“Sijajua lakini naamini ni zaidi ya hivyo, mbinu yangu niliowapatia ni ya kipekee sana, sidhani kama ni kweli imeweza kutokea katika miliki ya kijini ya PANAS kama wengi walivyosema lakini kwa staili nilivyoirahisisha ni zaidi ya mbinu zote zinazotumiwa na majini”
PANAS ni jamii ya kijini pia kama ilivyo kwa Hongmeng , lakini inasemekana utofauti wa PANAS na Hongmeng ni kwamba miliki hio ipo nje ya bara la Asia na hata Hongmeng ambao walijaribu kusafiri kwenda PANAS ilibidi kwanza wasafiri kuja Afrika, ni jamii ambayo haina muunganiko wowote kabisa na jamii kibinadamu kwa miaka na miaka , lakini hivi karibuni jamii hio inaanza kuonyesha matamanio yao na binadamu wa kawaida.,
Rose sasa alikua sio wa kawaida, alikuwa binadamu ambaye amefanikiwa kupata ufunuo wa nguvu za kijini na hisia alizokuwa akipata akiangalia mazingira ni tofauti kabisa na binadamu wa kawaida na alijikuta hata kundi lake la Tembo kuona ni kitu ambacho hakina maisha marefu kabla ya serikali kuingilia.
Rose sasa alikuwa akipaa tu angani kama Roma na zoezi lake la kwanza kufanikiwa kupaa ni kurudi nyumbani kwa kumfuata Roma nyuma na alijikuta kufumba na kufumbua wapo maeneo ya Ununio na alijikuta mapigo ya moyo yakidunda kasi mno akiwa kama haamini , kwani kila kitu kinaonekana kuwa kipya kwake.
Baada ya kutembea wakipita nje ya nyumba ya Nasra waliweza kukukutana na mama yake Nasra ambaye alikuwa akitoka kwenda kukimbia kuchukua mazoezi.
Tokea mama yake Nasra kufika jijini alikuwa amebadilika mno , kwanza alinenepa na pia mwonekano wake ni wa kitajiri zaidi , hakuwa tofauti sana na Blandina au Bi Wema.
Licha ya kumuona Roma na Rose wakiwa pamoja asubuhi hio hakushangaa sana kwani alikuwa akijua bwana huyo alikuwa na zaidi ya wanawake wengine nje na hata ile hatia aliokuwanayo juu ya Nasra kutoka na mume wa rafiki yake kupungua.
Roma mara baada ya kufika katika nyumba ya Rose waliweza kumkuta Dorisi akitokea jikoni , ilionekana ndio alikuwa akiandaa kifungua kinywa.
Dorisi uwezo wake wa kuvuna nishati za mbingu na Ardhi ulimtegemea zaidi Roma katika kufanya nae mapenzi, baada ya kusikia mwenzake kapasua , alijikuta akiona wivu na kuamini mtu ambaye ataweza kupata mtto wa Roma mapema basi ni Rose na sio yeye.
Roma hakujali sana mawazo ya Dorisi zaidi ya kumwambia ahimize kufungua kinywa kwani leo atapatia hapo hapo kabla ya kurudi nyumbani.
Roma mara baada ya kusema hivyo alimpigia simu mama yake na kumweleza kwamba asihesabiwe kwenye kifugua kinywa , lakini pia alimweleza juu ya mafanikio ya Rose na mara baada ya Blandina kusikia taarifa hio alijikuta akifurahi mno.
Alikuwa na wasiwasi kutokana na Roma kutokuwa wa kawaida hivyo kumpelekea kutokupata mtoto , lakini mara baada ya kusikia kuhusu Rose kupanda levo alijikuta akifurahi mno hakujali ni mwanamke gani wa kwanza kumzalia Roma mtoto , yeye shida yake ni mjukuu tu , alikuwa na mjukuu Lanlan lakini bado hakuridhika kwani bado alijua Lanlan ni wa kulelewa.
“Roma nadhani tusherehekee mafanikio ya Rose”
“Mama unataka tusherehekee vipi??”
“Leo si wikiend na hakuna mambo mengi ya kufanya , kwanini tusiwaalike wengine wakifika nyumbani na kupika chakula na kufurahi?”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kuona sio jambo zuri kidogo kutokana na Edna lakini aliependekeza ni mama yake na ni kweli Rose kapata mafanikio makubwa na anapaswa kupongezwa.
“Kama ni hivyo basi tumshirikishe Edna kwanza na baada ya hapo nitawaambia”Aliongea Roma na kisha walikubaliana na kukata simu.
“Mbona unacheka Dorisi?”Aliuliza Roma mara baada ya kuwaambia pendekezo la mama yake.
“Najua mama anamtumia Rose kama kisingizio tu , ukweli ni kwamba ulivyokuwa Korea mara nyingi tulishinda nyumbai kwako tukicheza karata, nadhani anataka tukusanyike tuendelee na mchezo”
“Kucheza karata?”Roma alishangaa kwani ilikuwa ni habari mpya lakini wakati huo huo moyo wake ukiwa na wasiwasi , kwanni kama kitu kama hiko kikiendelea basi Edna lazima hatopendezwa na jambo hilo na kupelekea migogoro.
Roma mara baada ya kumaliza kifungua kinywa alipokea simu kutoka kwa Daudi akimkumbushia swala la tafrija ndogo inayohusiana na waigizaji wote walioshiriki katika filamu hivyo kumweleza eneo ambalo tafrija hio ingefanyika, baada ya kukata simu aliona itakuwa vizuri kumpigia simu Sophia kwa kufanikisha swala hilo.
Baada ya kukaa muda mfupi aliondoka na kurudi nyumbani na aliweza kumkuta Edna akicheza na Lanlan eneo la sebuleni na alimweleza juu ya Sophia na watu wa kampuni ya Penguin kuandaa tafrija lakini Edna alionyesha kujua kila kitu.
“Unaweza kwenda , mimi nitashiriki siku ya uzinduzi wa filamu “
“Lakini Sophia anaweza kuwa na huzuni kama hutoenda”
“Nishampigia tayari Sophia na kumpongeza na nimemwambia sitohudhuria , sidhani kama atahuzunika kwa jinsi tulivyokubaliana”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuelewa , hata hivyo Edna alikuwa karibu sana na maendeleo ya Sophia kuliko ilivyokuwa yeye.
“Hubby! Je utamfundisha na Lanlan kuvuna nishati hapo baadae?”Aliuliza Edna wakati Roma akicheza gemu la kuzungusha boksi la kufananisha rangi.
“Hilo lipo wazi, Lanlan ni binti yetu hatuwezi kumuacha asijifunze na isitoshe Lanlan ana vigezo vikubwa zaidi kuliko hata mimi wakati nikijifunza , mpango wangu ni kumrithisha nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo , ni mtoto wetu wa kwanza hivyo lazima apate vipaumbele”
“Kama ni hivyo kwanini hujamwelekza chochote?”
“Kwanza kabisa Lanlan bado ni mdogo , hawezi kuelewa baadhi ya mambo kwa umri wake, kitu cha pili siwezi kumpatia vidonge na kisha nikamrithisha andiko anaaweza kugeuka na kuwa mkatili , tatu sina uhakika maadui zangu ambao watajitokeza , kama ujuavyo andiko hili huwindwa na watu wengi hivyo nikimrithisha akiwa na umri mdogo moja kwa moja namfanya kuwa mlengwa , hivyo watu watataka kupata mbinu yangu kupitia kwake na nitamuweka kweye hatari, kwasasa tumuache afurahie utoto wake”
“Malengo yangu ni kumuona akiendelea kuwa na siha njema na kuweza kujilinda yeye mwenyewe , lakini nina wasiwasi anaweza kuja kuwa kama wewe kuanza kupigana nakuwa na utukutu mwingi akishaanza kujifunza , hata kama ataweza kushida kila wakati lakini bado itanifanya kuwa na wasiwasi”Aliongea Roma lakini hakutaka kuongezea neno kwani alijua huo ni waswasi wa kawaida kwa mama kwenda kwa mtoto.
Ilionekana Blandina alikubaliana na Edna, hivyo muda wa mchana warembo wote waliweza kukusanyika katika nyumba ya Roma kusherehekea mafanikio ya Rose, aliekosekana alikuwa ni Neema Luwazo ambaye alikuwa nje ya nchi kikazi pamoja na Mage ambaye alikuwa kazini.
Roma mara baada ya kuona kundi lote hilo la wanawake alijikuta akijisikia vibaya na vizuri kwa wakati mmoja.
Baada ya chakula kama kawaida Blandina alitoa karata na kuwataka wote wakusanyike eneo la sebuleni kwa ajili ya kucheza.
Najma pia alikuwepo na ndio ambaye alitoa sababu kwamba hakuwa akijua kucheza karata na Edna hivyo hivyo alipoambiwa ajiunge kucheza alisema hajui , lakini Nasra alimlazimisha na kumwambia atajifunza.
Roma kwa hali hio hakutaka kuendelea kubakia hapo tena, kwasababu siku hio alikuwa na ratiba ya kuhudhuria tafrija ya Sophia na waigizaji wenzake , basi aliona akatembee na kisha aunge moja kwa moja.
***********
Tafrija ilikuja kumalizika saa nne za usiku na Roma aliagana na Sophia kurudi nyumbani.Sophia alionekana kuzidi kupendeza mno na kila mwanaume ambaye alikuwa akimwangalia alimtamani.
Roma mara baada ya kuingiza gari lake ndani ya geti alishangaa mara baada ya kuona gari la Amina bado lipo , lakini pia taa za sebuleni zikiwaka muda huo.
Baada ya kuingia ndani ndipo alipokuja kushangaa mara baada ya kukuta hali ni kama alivyoiacha , lakini utofauti tu ni kwamba wengine walikuwa washaanza kusinzia kwenye masofa , huku mezani alikuwepo Edna na Amina waliokuwa wakicheza karata wakiwa siriasi.
Blandina mara baada ya Roma kuigia eneo hlo alijikuta akipata ahueni na kumwambia Roma amshawahisi Edna waghairishe wataendelea kesho.
Roma mara baada ya kuambiwa hivyo alitaka kujua kwanza kinachoendelea na hapo ndipo aliposikia kwamba baada ya Edna kufundishwa na kuelewa namna ya kucheza hakutaka kupumzika kabisa na kuchukulia siriasi mchezo huo na mtu ambaye alikuwa akiongoza kushinda ni Amina, hivyo Edna alitaka kulipa pointi zote za Amina,lakini mwishowe kila akicheza anaishia kufungwa na bado hakutaka kukata tamaa.
Roma mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akijawa na mshangao na kumwangalia Edna namna ambavyo alikuwa siriasi.
“Edna huo mchezo ni wa kubahatisha, hakuna ufundi ,unaweza kucheza mpaka kesho na usipate ushindi”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia na kisha akaangalia watu waliozunguka na kisha akageuza macho kwa Amina.
“Amina nitakupigia simu , lazima nikulipe pointi zako ulizonifunga leo”Aliongea Edna na kisha akasimama.
“Edna huu ni mchezo wa karata tu kwanini unauchukulia kama vile ni ushindani wa kibiashara?”
“Sijauchukulia kama biashara , bali ni kwamba unafurahisha , siku nyingine mkicheza lazima na mimi niwepo”Aliongea na kisha alipandisha juu kumwangalia Lanlan.
Roma alijikuta akipata ahueni na kuwasindikiza, Najma alikuwa akikaa mbezi kwenye apartment hivyo alipanda gari ya Amina na wakaondoka kwani muda ulikuwa umeenda.
Ilipita wiki moja moja , ikiwa ni siku ya jumamosi jioni wakati Roma akitoka nyumbani kwa Najma mbagala, aliweza kupokea simu kutoka nyumbani na aliekuwa akipiga ni mama yake.
“Mama kuna nini?”
“Mheshimiwa raisi Jeremy amefika na yupo na Edna wanaongea”Aliogea Blandina na kumfanya Roma kushagazwa na kauli hio.
“Lakini mbona unaongea kwa wasiwasi sana?”
“Ni kuhusu Rose”
“Rose kafanyaje?”
“Kuna watu wamejitambulisha wanatokea PANAS, wanasema Rose ashafikia levo ya Nafsi na sheria haimruhusu kuendelea kuishi katika ulimwengu wa kawaida , hivyo wanataka kuondoka nae”
“PANAS!!”Roma alijikuta akimaka , kwa mara ya kwanza anasikia watu kutoka PANAS.
“Mama nakuja sasa hivi”
“Wahi maana Rose kakataa na kasema watampata kama wataweza kumshinda baada ya pambano , hivyo wametoka kwenda kupigana”Aliongea na kumfanya Roma kuzidi kuwa na wasiwasi na aliona hawezi kuendesha gari na alimgeukia Najma na kisha akalipaki pembeni na kumpatia ufunguo wa gari na kumwambia anapaswa kuondoka kuwahi nyumbani , lakini nasra alipotaka kumwambia Roma hajui kuendesha gari , Roma ashapotea kwenye macho yake na kumuacha akiwa amekodoa macho.