SEHEMU YA 558.
Kama ni chakula cha usiku , kilikuwa chakula cha usiku kweli kutokana na eneo ambavyo lilipambwa na kupendeza na ilimgusa mno Edna.
Upande wa Roma alionekana kufanya hivyo kumuonyesha Edna namna gani anaheshimu ndoa yake na mrembo huyo licha ya kwamba ilianzia katika mkataba.
Kitendo cha Edna siku nzima kuhofia pengine Roma hamtaki tena kutokana na kilichotokea usiku , ilimfanya kuguswa mno mara baada ya kugundua kumbe yeye alichokiwaza ilikuwa tofauti kabisa.
Inasemekeana wanawake wanapenda sana surprise na kwa mwonekano wa Edna alionekana ameguswa mno , kwanza ameguswa na namna ambavyo eneo limepambwa , lakini pili aligusswa na namna ambavyo Roma aliamua kuonyesha namna ambavyo yupo siriasi na yeye.
Wanasema ‘Surprise’ humfanya mwanamke kujihisi kuwa wa kipekee na kumuonyeshea kwamba muda wote unamfikiria.
Roma mara baada ya kuona mke wake yuko katika hali ya kukumbwa na mshituko wa kisaikolojia palepale alimvutia kwake na kumkumbatia.
“Hey Babe hata kama umeguswa na ‘surprise’ yangu haina haja ya kutoa machozi , nimefanya haya yote ili uwe na furaha”Aliongea Roma.
“Wewe ni mtu mbaya sana”Alilalamika huku akianza kumpiga piga kwenye kifua chake mara nyingi , lakini vingumi vyake vilikuwa vile vilaini.
“Unajua ni kwa kiasi gani nilikuwa na wasiwasi wewe kuondoka bila ya kuaga na kutokuwepo kwako nyumbani asubuhi , nilifikiiri hukutaka kuongea na mimi tena , nili,, nilifikiri umeshanitelekeza tayari na hunipendi, unajua ni kwa namna gani nimeogopa?”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na kauli yake na palepale akamshika mikono.
“Sikufikiria hivyo , nilikuwa nikitafuta namna ya kukufanya uwe na furaha , najua ndoa yetu ilianza kwa mkataba na hakukuwa na hisia zozote zilizohusika , lakini unapaswa kuelewa siku ile sikufanya maamuzi kwa kukurupuka , Edna nataka utambue ni kwa kiasi gani nakuheshimu na kukupenda kama mke wangu, siku zote utakuwa kipaumbele kwenye maisha yangu..”
“Usiongee tena nitalia..”
“Lakini ushalia tayari “
“Wewe ndio umenifanya nilie”
“Lakini sijakulazimisha ulie si ndio , Tangu lini ukawa na adabu hivi?”
“Mkorofi sana wewe”
“Hehe.. kheri ya mwaka mmoja wa ndoa mke wangu”Aliongea Roma huku akimkumbatia.
“Usinikumbatie, bado nina hasira na wewe na nakuchukia kwa kunichanganya”
“Lakini nilitaka kukumbatia na kukufanya uwe na furaha kwasababu nakupenda”
“Roma nakuchukia”
“Edna nakupenda”.
Sauti ya kimapenzi kati ya mwaname na mwanamke ilisikika ndani ya eneo zima , lilikuwa ni eneo tulivu mno ambalo haikuweleweka kama kulikuwa na mtu mwingine.
Baada ya kubishana kwa muda na kukumbatiana hatimae Edna aliishia kucheka kwa furaha na sasa kuingia ndani katika jumba hilo kwa ajili ya chakula cha usiku maarufu kama Candlelight dinner.
***********
Siku iliofuata iliwakuta kwenye kitanda cha sita kwa sita katika jumba hilo la kifahari.
Mazingira ya jumba hilo yalizidi kuvutia mara baada ya jua la asubuhi kuangaza , ni kama vile miti iliozunguka jumba hilo ilipandwa kuakisi namna nzuri ya mwanga unavyomulika madirisha na kuingia ndani.
Alijihisi uchomvu mno licha ya kwamba alilala fofofo , hio yote ni kutokana na kile kilichotokea usiku mzima.
Kutokana na juhudi alizoonyesha mwanaume wake hakuwa na nguvu ya kumkatalia kufanya ule mchezo ndio maana wakajikuta wakifanya muda mrefu na hata muda ambao alipotelea usingizini hakuelewa.
Sasa muda ambao Edna alimaliza kupambana na mwanga wa jua akitaka kujiondoa katika mwili wa Roma uliomkubatia alijikuta akiguna, alikuwa kama alivyozaliwa na namna ambavyo manyonyo yake yalivyokandamiza kifua cha mwanaume huyo ilimfanya kuona aibu na kuchukia kidogo kwa wakati mmoja.
Lakini hata hivyo wakati alivyotaka kurudisha kiuno nyuma alijikuta akitoa mguno mkubwa zaidi kuliko wa mwanzo .
Ni kwasababu Gobole la uhai la mwanaume huyo bado lilikuwa limemwingia katika sehemu zake za uzazi, Edna hakuelewa ilikuwa ni Roma ambaye hakumaliza usiku hivyo kumsababishia Gobole hilo kutuna au alimfanyia hivyo asubuhi asubuhi.
Alitaka kujiondoa kwake lakini alishindwa kufanya hivyo kutokana na kushikiliwa lakini kwa wakati mmoja kuona aibu za kike.
Wakati akiendelelea kuwaza cha kufanya huku akimwangalia Roma , aliweza kuona Lips za mwanaume huyo zikicheza.
“Wewe,, kumbe upo macho..halafu unajifanyisha kulala”Aliongea huku akimsukuma Roma kifuani kwa nguvu.
“Hahaha..”Roma alijikuta akitoa cheko mara baada ya mchezo wake kugundulika.
“Wewe…acha kucheka mtoe huyo shetani wako nje”Aliongea akitaka kujichomoa lakini alikuwa ameshikiliwa vizuri sana.
“Kwanini nimtoe , My Dear Edna ni vizuri kama tutafanya mazoezi ya asubuhi asubuhi , ukiendelea kujipinda pinda utaimeza yote , sikujua kumbe una hamu ya kula kiasi hicho”
“Wewe ndio mwenye hamu kubwa ya kula , umeilazimisha hapo , siwezi kuendelea hivi”
“Kweli?’ mbona kama unaipenda iwe yote angalia namna ulivyo mwekundu sasa”
“Wewe.. Ah.. hapana”Edna alitaka kujitoa lakini aliwekwa vizuri na kabla hajashitukia ilikuwa tayari kimiani
“Babe , jana ulilala mapema kabla hata ya kuniruhusu nishushe japo risasi moja , nimevumilia kwa kutokukuamsha , tusifanye chochote asubuhi hii mpaka nikushushie mzigo wote , ukikataa sitokuwa na uwezo wa kuvumilia”Baada ya kuongea hivyo alimpelekea mdomo mke wake na kilichoendelea hapo ni miguno iliodumu muda mrefu.
******
Naam ilipita wiki moja tokea Roma na Edna kupata chakula cha usiku katika jiji la Dubai kusherehekea mwaka wao mmoja wa ndoa.
Katika wiki hio Magdalena aliweza kufika katika levo ya Nafsi akiwa sawa na Rose.
Kutokana na kwamba sheria zilikuwa zikimzuia Magdalena kubakia katika ulimwengu wa kawaida mara baada ya kufikia levo hio ilibidi Roma apendekeze Rose na Magdalena kwenda kuishi visiwa vya wafu kwa muda huku wakiendelea kujifunza zaidi kuvuna nishati za mbingu na ardhi kwani asingeweza kuhonga tena kama Magdalena atashitukiwa.
Mwanzoni Rose alikataa kwenda visiwa vya wafu kwa kuogopa kwamba angekuwa mpweke , lakini mara baada ya kuona hata Magdalena anapaswa kwenda huko hakuona tatizo tena ns isitoshe alikuwa na shauku ya kuona nchi ya Roma.
Upande wa Magdalena licha ya kwamba hakuwa na mahusiano na Roma lakini alijisikia vizuri kwamba ni yeye pia ni sehemu ya watu Roma anaowajali.
Magdalena licha ya kwamba alilazimishwa mara kibao kuoana na mwanaume aliefahamika kwa jina la Jumbe aliweka ngumu zaidi huku sababu yake kubwa ikiwa ni kisingizio cha mafunzo ya mbinu za kijini.
Wakati Magdalena alivyoenda nchini China akiwa na Roma aliambiwa na Master wake kwamba kama anataka kupanda levo kwa haraka katika mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na Ardhi basi ahakikishe hafanyi mapenzi na anabakia kuwa bikra kwani ingemsaidia sana.
Hivyo Mage alitumia mbinu hio kuepuka ndoa na hata swala la kwenda nje ya nchi kwa muda kuepuka kupelekwa katika miliki za kijini kulingana na sheria kwake alichukulia hio kama fursa ya kukimbia usumbufu wa Jumbe.
Afande Tobwe mara baada ya kuambiwa sheria iliopo juu ya binadamu anaejifunza mbinu za kijini aliefikia katika Levo ya Nafsi alishangaa na hakuwa tayari kuona Magdalena anaenda katika miliki za kijini kuishi , hivyo yeye na mke wake walikubali Roma amchukue na ampeleke katika miliki yake.
Mama T kitendo cha Magdalena kutaka kwenda nje ya nchi , tena katika miliki ya Roma alipatwa na wasiwasi kwa kuona mapenzi ya Magdalena kwa Roma yangeongezeka maradufu na kusababisha watoto wake wote mapacha kuwa michepuko wa mwanaume mmoja , lakini licha ya wasiwasi wake huo hakutaka pia kumuona Magdalena akienda miliki za kijini kulingana na sheria, hivyo kishingo upande alikubali huku akimsisitiza Mwanae huyo kuachana na mawazo juu ya mpenzi wa pacha mwenzake , lakini kwa Magdalena maneno ya mama yake yaliingia sikio la kulia na kutokea la kushoto , alijiambia ‘what if’ yeye na pacha wake wakitoka kimapenzi na mwanaume mmoja kwanza yeye na pacha wake walishakaa chini na kuyaongea na kukubaliana kufuata mioyo yao , ilikuwa ujinga lakini mapenzi yalikoleza ujinga wao na hawakujali huko mbeleni watu wangewachukuliaje.
Ni siku moja kabla ya Roma kumpeleka Rose na Magdalena katika visiwa vya wafu, usiku wa siku hio Sophia aliweza kurudi kutoka Japani , alikokuwa ameenda kwa ajili ya kusalimia familia yake.
Kurudi kwa Sophia usiku huo kumlimfanya Lanlan kufurahi kwani alimtaka Shangazi yake huyo amfundishe namna ya kuimba.
Lanlan siku iliokuwa ikifuatiwa walikuwa na maonyesho maalumu shuleni kwao ambayo yalihusisha na kuimba na hata Edna na Roma walipaswa kushiriki kama wazazi.
Hivyo wanafunzi wote walipewa kazi ya kuchukua mazoezi nyumbani namna ya kuimba ili siku inaofuata kufanya vizuri mbele ya wazazi.
Sasa Lanlan mara baada ya kugndua mama yake Edna hakuwa akijua kuimba ndio maana alimkimbilia Sophia amsaidie yeye katika kufanya mazoezi hayo.
Sophia kama shangazi alivyoombwa na Lanlan alikubali kumsaidia kwa furaha zote, kwanza kabisa alimpenda Lanlan kutokana na akili yake na siku hio Lanlan aliishia kulala chumbani kwa Sophia mpaka asubuhi.
Siku iliofuata kwasababu Sophia hakuwa na chakufanya nyumbani Edna alimuomba waende pamoja shuleni kwa Lanlan kwa ajili ya kuangalia maonyesho yao na Sophia hakubisha lakini ilimbidi kwanza kutafuta kofia na miwani kuvaa ili asitambulike kutokana kipindi hicho umaarufu wake ulizidi kuwa mkubwa kutokana na kuigiza muvi ambayo kwa mara ya kwanza ilikuwa ikitarajiwa kuonekana katika mtandao wa Netflix.
Baada ya kufika chuleni hapo,waliweza kupokelekewa na kuonyeshwa mahali maalumu pa kukaa.
Braeburn ilikuwa shule kubwa na watoto hawakufundishwa kusoma tu , lakini pia walipewa nafasi ya kushiriki katika michezo mbalimbali , lakini pia kuwajengea hali ya kujiamini na zaidi sana kuwasaidia kutambua vipaji vyao, ndio maana waliwapatia nafasi ya kufanya matukio ya aina nyingi , yawe ni ya kuimba ya kucheza mpira , kuchora , kuvutana kamba na kuruka.
Kwenye maonyesho ya kuimba Edna alimuacha Lanlan afanye atakavyo , lakini akamuonya kwenye maonyesho ya kutumia nguvu asitumie uwezo wake afanye kawaida tu na Lanlan alionekana kuelewa.
Edna alifurahi sana kuona kwamba mtoto wake alikuwa akichangamana na marafiki zake vizuri tokea mara ya mwisho kutokea kwa tukio la Lanlan kumnyofoa mtoto mwenzie nywele, watoto ni wepesi kusahau na hiko ndio kilichotokea na ilimfurahisha zaidi.
Asubuhi michezo ilioanza kwa watoto ilikuwa ni kuruka kamba , kuvuta kamba kitimu , pamoja na kushuti maputo angani kwa siraha maalumu za kitoto.
Katika maonyesho yote hayo Lanlan alifanikiwa kuibuka kidedea , alishusha karibia maputo yote kwenye kushuti na wakati wa kuvutana kamba alisaidia sana timu yake kushinda na lilipokuja tukio la kuruka Kamba alionyesha ubingw wa kuruka pasipo ya kuchoka haraka.
Roma aliona mambo aliofanya Lanlan ni kawaida lakini kwa Edna alikuwa akijivunia mno kuona mwanae ndio kawa kivutio kikubwa.
Baadhi ya wazazi walimuuliza Edna na Roma siri ya mafanikio yao ni nini mpaka mtoto wao kuwa na nguvu hizo na Roma alichukua nafasi hio kujigamba na kuawaambia siri kubwa ni msosi.
Wakati wa mchana mara baada ya mapumziko ulikuwa ni wakati wa wazazi kupata chakula kilichoandaliwa hapo shuleni.
Shule kubwa kama hio haikuona tatizo kufanya matukio ya namna hio na kuonekana kwenye vipindi vya watoto kwenye runinga ili kuzidi kujiongezea umaarufu, lilikuwa tukio ambalo lipo kimkakati zaidi wa kimatangazo.
Baada ya chakula cha mchana, uliwadia muda sasa wa watoto kuonyesha vipaji vya kucheza mziki pamoja na kuimba.
Zamu ya Lanlan na wenzake ilipowadia Edna alishindwa kujizuia na kusimama ili kuosgea mbele kumrekodi lakini Roma alimwambia ataenda yeye.
“Hapana nitaenda mimi , ili kuleta maana zaidi”Aliongea Edna akikataa na kumfanya Roma ashindwe kuongea chochote huku akishindwa kuelewa kuna maana gani tofati akimrekodi yeye.
“Sister Edna anaonekana amekolea kwenye malezi”Aliongea Sophia aliekuwa pembeni huku akiwa anacheka.
Edna ijapokuwa alikuwa bize katika kazi lakini pia alionekana likija swala la malezi alikuwa vizuri zaidi na Roma aliona Edna ni mama mzuri kuliko mke.
Sasa kuna muda ambao Sophia alijisahau na kutoa kofia yake aina ya Hat pamoja na miwani na kumfanya sura yake kuonekana muda huo, kitendo kile kilimfanya Paparazi aliekuwa mita kadhaa kutoka walipokuwa wamekaa yeye na Roma apige picha kwa kutumia Kamera yake ya Lens kubwa bila ya uelewa wa sophia wao.
Baada ya kundi la Lanlan kumaliza kuimba na Roma kumgeukia Sophia , aligundua ashajisahau na kuacha sura yake kuonekana na palepele alimsaidia kumvalisha kofia na akampa ishara na kumwambia avae miwani vizuri ili asionekane sura yake kwa watu kutokana na umaarufu wake.
Na Sophia mwenyewe alishangaa kujisahau kwake , huenda ni kutokana na kufarahishwa na kile ambacho watoto walikuwa wakifanya , kwani ukiachana na kuimba lakini walifanya vizri sana kwenye kucheza na kilichomfurahisha zaidi wimbo wake ndio waliokuwa wakitumia watoto hao kucheza.
Baada ya matukio yote kumalizika wote kwa pamoja waliingia kwenye gari na kuanza safari ya nyumbani.
Lanlan alikuwa amechoka mno na mara baada ya kuingia tu kwenye gari alipotelea usingizini kwenye mikono ya Edna , huku akichezesha midmo yake kana kwamba kuna kitu ambacho anakula.
Edna na Sophia walikuwa wamekaa siti ya nyuma , Sophia yeye alikuwa bize kungalia vidio zote zilichochukuliwa kwa simu na Edna kwa kuzirudia rudia , na alijikuta zikimfurahisha na aliendelea kuzingalia huku akiwa amepunguza sauti ili asimsumbue Lanlan aliekuwa usingizini.
Roma aliekuwa akiendesha baada ya kuangalia Kamera ya nyuma na kuona namna ambavyo Sophia na Edna walivyotabasamu pamoja na mtoto wake kuwa katika pozi la usingizi alijikuta moyo wake ukipatwa na joto ambalo halikuwa la kawaida kabisa, hakuamini maisha yake yamefikia steji hio na alijiambia kweli safari ya binadamu ni yenye mambo mengi ambayo sio yenye kufahamika zaidi ya muda pekee kuamua.
Aina ya maisha hayo miaka kadhaa yalikuwa kama ndoto tu na hata wakati aliporudi Tanzania ilikuwa ni kwa ajili ya kutafuta familia yake na angalau kutibu tatizo lake , lakini mambo yalitokea mfululizo kiasi kwamba yamemfikisha katika hatua hio , aliweza kujisikia hali ya kuridhika na furaha kwa wakati mmoja na alijiambia kama hakuna mtu ambaye angeweza kumsmbua kwa wakati huo basi maisha yatakuwa mazuri sana kwake .
Siku iliofuata alfajiri Roma aliwachukua Rose pamoja na Magdalena kuwapelekea katika makazi yake ya visiwa vya wafu.
Kabla ya kuanza safari alikuwa tayari ashamtaarifu Ron ili kuandaa mazingira na mahitaji kwa ajili ya wanawake wawili.
Na aliweza kurejeshwa taarifa kwamba tayari amekwisha kutafuta wafanyakazi wa ndani ambao wangewasaidia katika mahitaji yao ya kila siku.
Hawakubeba nguo nyingi kuelekea huko , ni mabegi tu ya mgongoni ndio ambayo walitumia na hio yote ilikuwa ni kupunguza uzito.
Ilikuwa mara ya kwanza Roma kupaa angani akiwa amefuatana na warembo wake , hakika alijisikia kama mtu ambae amefanikkisha jambo kubwa sana katika maisha yake.
Iliwachukua dakika ishirini tu kutoka Tanzania mpaka visiwa vya wafu , kwasababu Rose na Magdalena hawakuwa mwishoni mwa levo ya Nafsi Roma hakuhofa wao kukumbwa na adha ya kupigwa na radi kutokana na kukiuka kanuni za anga.
SEHEMJU YA 559.
Muda ambao waliweza kufika ilikuwa ni usiku kama saa tisa hivi, lakini licha ya hivyo kutokana na uwezo wao wa kichawi haikuwazuia kushangazwa na mazingira.
“Nyie watu mpo hapa ndani ya muda muafaka kipupwe ni cha wastani na mvua sio nyingi lakini sio kukavu wala ubaridi vilevile , mpo hapa kufurahi”Aliongea Roma kwa tabasamu mara tu baada ya kufika
Rose na Magdalena walikuwa na mshangao wa kuvutiwa na namna mazingira yalivyokuwa yakionekana , mwanzoni walikuwa wakisita sita kuja lakini mara baada ya kujionea wenyewe kwa macho yao waliona ni kama wamepiga ndege wawili na jiwe moja , wangeweza kuwa mbali na watu jamii ya majini na vilevile wangetumia muda huo kama wa mapumziko.
Kwa namna ambavyo waliweza kutua katika fukwe ya bahari , huenda mtu ambaye angeweza kuwashuhudia moja kwa moja angejisemea hao ni Majini halisi.
Roma aliwaongoza warembo hao kuelekea katika makazi yake maana haikuwa mbali na sehemu waliotua.
“Honey , umesema kila kitu hapa ni cha kwako ?”Aliuliza Rose ambaye alikuwa akichezea gamba la konokono wa baharini.
“Unaweza kusema hivyo , lakini watu wa hapa niliwakuta hivyo siwezi kusema nawamiliki lakini jeshi lote lipo chini yangu, hili eneo ni Grey Zone hivyo hakuna taifa ambalo linawea kusogea wala kulinasa katika ramani”
“Je miungu wote wana maeneo yao au ni kwa wewe tu?”Aliuliza Magdalena na kumfanya Roma kufikiria kidogo.
“Hata mimi mwenyewe sina uhakika , dunia sio kubwa kihivyo lakini sio ndogo vilevile , miungu yote iliopo hapa duniani wana miaka mingi sana hivyo wanajua kila kona ya dunia , kama wangetaka kuwa na eneo kama hili nadhani ni rahisi sana kwao labda tu kama hawakuwa tayair lakni niliwahi kusikia Christen ana eneo lake nchini Canada na Poseidon yeye ana eneo lake katika visiwa vya Hawaii Marekani , sijui kuhusu wengine , kila mmoja vipaumbele vyake ni tofauti hivyo kuna uwezekano wasipendelee kuwa na maeneo binafsi.”
“Kama ipo hivyo nadhani majini ndio yanatia huruma , maisha yao yote ni kujificha katika ulimwengu wa kufikirika”
“Huenda ni kwasababu ya uwepo wa Athena na isitoshe kuvuna nishati za mbingu na ardhi sio jambo jepesi , sio wote ambao wana uwezo wa kupanda levo zaidi kupita nafsi ili kuweza kushindana nao”
Roma alifikiria katika moyo wake kama miungu kipindi hiki walikuwa na asilimia therathini ya uwezo wao je kipindi wakati wanafika ilikuwaje.
Alijiambia huenda Majini yalikuwa yakiogopa kitu ambacho hawakijui ndio maanda waliishia kujifiacha katika ulimwngu wa kufikirika , huku kisingizio chao kikubwa ni kutotaka kuingilia maswala ya dunia ya kawaida.
Bila kuelewa wakati wakiendelea kuongea hatimae waliweza kufika chini ya ngome kubwa.
Rose na Magdalena wote walimwangalia Roma kwa mshangao kutokana na jengo hilo lilivyokuwa kubwa , ilikuwa ni kama ngome za wafalme wa Ulaya wa enzi hizo.
Roma aliwashika wanawake hao wte wawili mikono na kisha aliruka nao wote kwa pamoja walikwenda kutua juu ya mlima katika mlango wa kuingilia katika jengo hilo .
Nje kabisa alionekana Ron ambaye alikuwa akisubiria, alikuwa amevalia suti ya rangi nyeusi na tai nyekundu , hakuwa peke yake, aliambatana na baadhi ya watu waliokuwa wakiishi katika visiwa vya wafu ambao wote kwa pamoja walikuwa wamepanga mstari kumsubiria Roma.
“Your Majesty Pluto , two beutifull ladies welcome home”Aliongea Ron kwa lugha ya kingereza na huku akiinamisha kichwa chake kwa heshima na wale wanaume na wanawake alioambatana nao pia waliinamisha vichwa kwa heshima.
Roma alimsogelea Ron na kisha alimpiga piga beganni na kisha akamalizia kusalimiana na kila moja aliekuwepo hapo , wote walikuwa wakimjua Roma hivyo salamu zilikuwa ni zile za kuulizana maendeleo yao.
Wanaume hao na wanawake walikuwa ni maninja na wanajeshi wastaafu wa kikosi cha New Zero na Sea Eagles.
Uhusiano wao ulikuwa upo zaidi katika damu walizomwanga wakati walipokuwa wakipambana pembeni ya Roma, ni uhusiano ambao haukuwa na meneno mengi ya kuuelezea kwani ulijitambulisha.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Rose na Magdalena kuona upande wa pili wa kivuli cha Roma kwa ukaribu zaidi , wanaume waliokuwa mbele yao licha ya kwamba walionekana kuwa wakarimu kwao lakini bado walitoa aura ambayo ilionyesha wamemwaga damu nyingi na kuwafanya washindwe kujua nini cha kusema zaidi ya kutoa tu mikono na kutabasamu.
Baada ya kuingia ndani kila mmoja alitafuta siti yake ya kuketi katika meza kubwa ya chakula na muda huo huo Vijakazi wa kizungu waliovalia sare maalumu waliweza kuandaa chakula.
Ron na wengine hawakuwa na wasiwasi sana na wanawake hao wawili ambao hwakuwa wakiwafahamu na waliweza kuongea nao kawaida jambo ambalo lilimfanya Rose na Magdalena kupata utulivu.
“Enyi wanawake wawili , nimewaleta wapishi wawili wakubwa mmoja ametokea Ufaransa na mwingine kutokea Tanzania kwa ajili ya kuwaandalia chakula, mnaweza kuwaagiza chochote mnachotaka”
“Asante sana Mr Ron, umewaza vizuri”Aliongea Magdalena.
“Msijali hapa hatuna watu wengi , hivyo tunakaribisha wageni kuungana na sisi , isitoshe nyie wote ni Wapenzi wa mfalme Pluto hivyo moja kwa moja mtapewa heshima yenu”Aliongea na kumfanya Magdalena kuona aibu kwani hakuwa kwenye hatua ya kuitwa mpenzi wa Roma , upande wa Rose yeye hakuona tatizo , lakini ndio hivyo kutokana na waembo hao kuambatana na Roma kwenye macho ya watu wa visiwa hivyo wangewachukuliwa kama michepuko yake.
Baada ya Ron na wezake kunywa nusu chupa ya mvinyo sauti zao sasa zilianza kupoteza ustaarabu na kuwa za juu na hali ile ilifanya eneo kuchamganka
Mwanaume aliekuwa na nywele nyingi kuzunguka mdomo wake aliefahamika kwa jina la Collejon , ni bwana mmoja ambaye ashawahi kuwa kiongozi wa kikosi cha The Eagles katika Ukanda wa Kaskazini mwa Ulaya, ashawahi pia kuishi kwa miaka mitano nchini Kenya na muda huo alikuwa tayari kwenye umri miaka sabini hivi.
Muda huo alikuwa ameshilikia Goblet(kikombe) rangi ya madini ya fedha(Silver) na baada ya kunywa kidogo alimwangalia Roma na kisha akaongea.
“Mfalme Pluto wiki ijayo ni ‘Caesar Conference’ kwanini usikae kwa muda na kuchukua familia yako kwenda kuwaangalia vijana?”Aliongea bwana aliefahamika kwa jina la Callejon.
“Caesar Conference? Ni kweli imepita miaka miine tayari ni wapi linafanyika mwaka huu?”Aliuliza Roma.
“Sio mbalisana ni upande wa pili nyumbani kwao Ron”Alijibu mwanaume mwngine mwembamba.
“Linafanyikia Visiwa vya Cicilly , naona Ron utakuwa bize , usije kuruhusu watu kusogelea hadhina yako?”Aliongea Roma kwa kutania.
“Sijahusika na maswala ya kifamilia kwa muda , nadhani niwaache tu wafanye wakavyo”Alijibu Ron
Rose hakuwa akielewa lugha waliokuwa wakiongea na alimwangalia Magdalena.
“Wanaongea kuhusu nini?”
“Wanaongea kwa lugha ya kiitaliano na kirusi, mimi najua kingereza, kifaransa na kispanishi”Aliongea Magdalena na Ron aliona warembo hao hawakuwa wakielewa chochotehivyo aliamua kuwatafsiria.
“Tunazungumzia kuhusu Caesar Conferenece”
“Ndio nini?”Aliuliza Rose.
“Baraza la Kaisari ni baraza linahusisha makudi ya kimasenari dunia nzima ambayo yanajiamini kuwa na uwezo wa kushindana , sababu ambayo imefanya baraza hili kuitwa Baraza la Kaisari ni kwasababu mwanzoni kabisa lilianzishwa katika kusherehekea mashujaa wa kirumi waliopambana chini ya utawala wa Kaisari, katika miaka ya hivi karibuni pia baraza hili linafahamika kwa jina la Mkusanyiko wa Masenali, imani yetu ni kwamba kama tunahitaji kupata tenda zaidi kutupatia hela itatupasa kuwa katika sehemu ya juu katika mashindano haya ,Baraza la Kaisari lilikuwa ni endelevu tokea enzi za zama zile na lilikuja kusitishwa wakati wa vita ya pili ya dunia kwasababu masenari wa kupindi hicho walikuwa na utajiri mkubwa lakini mara baada ya vita ya pili ya dunia lilianza kufanyika kila baada ya miaka miinne , ni tukio kubwa sana la siri na ukiachana na wateja wetu wakubwa duniani wanaoishiriki lakini pia baadhi ya mataifa makubwa hutuma wawakilishi ili kuangalia ni Masenari wapi wenye uwezo ambao wanaweza kuwachukua , hivyo kila kundi kubwa la Masenari lazima wajiunge la sivyo wataonekena wadhaifu”
Baraza la kaisari ni kusanyiko la siri ambalo hufanyika kila mara baada ya miaka minne ambalo huhusisha wanajeshi wa kukodi wa makundi maalumu binafsi ambao kwa lugha ya kingereza ndio huitwa Marcenary , mfano wa kundi la Marcenari ni Wagner Group na Sea Eagles na mengineyo.
Rose ambaye alikuwa ni wa ulimwengu wa kiza na Magdalena ambaye ni mwanajeshi wa kitengo maalumu cha taifa, wote kwa pamoja walivutiwa na kusanyiko hilo.
Walijiambia mapigano ya Masenari duniani kote? , huenda ni kitu kizuti kushuhudia kikifanyika.
‘Mr Ron nani ambaye alishinda katika baraza hilo miaka minne iliopita?”Aliuliza Rose kwa kingereza.
“Should be Sea Eagles right , aren’t they the strongest mercenary corps along with Red Storm?”Alijibu Magdalena akisema lazima watakuwa ni The Eagles , kwani wao ndio kundi la Masenari ambalo lina nguvu duniani pamoja na kundi la Dhoruba nyekundu.
Ron mara baada ya Magdalena kuongea hivyo alitingisha kichwa kuashiria kwamba sio kweli kwamba Sea Eagles na Red Storm ndio ambao walishinda kwenye baraza hilo la Kaisari.
NB: Red Sand Storm inamaanisha kundi la masenari la Dhoruba nyekundu, hili lipo chini ya Zeros organisation na Zeros organisation kiongozi wao mkuu ambaye ni kivuli ni Athena , ambaye siku zote huwakilishwa sana sana na taifa la Marekani tutaona mbele.
SEHEMU YA 560.
Magdalena na Rose waliangaliana mara baada ya kuona Ron akipingana na kauli zao , kwani wao wote waliamini kundi la Masenari ambalo lingeshinda katika pambano hilo ni The Eagles kutokana na sifa zake zilizotukuka.
“Ukweli ni kwamba licha ya The Eagles kuwa kundi namba moija la kimasenari au la pili ambalo ni bora lakini halijawahi kushinda zidi ya Masenari wanaoshindana katika Baraza la Kaisari”Aliongea Ron na kuwafanya Rose na Magdalena kujawa na shauku ya kutaka kujua ni kundi gani la Masenati ambalo limeshinda katika mashindano hayo kama sio The Eagles wala Dhoruba nyekundu.
“Mr Ron kwanini usituambie , unatuacha hewani , tuambie kuhusu hilo kundi ni lipi?”Aliuliza Rose kwa shauku kubwa na Roma mara baada ya kuona namna Rose alivyo ilibidi aingilie yeye mwenyewe.
“Ni kundi ambalo linatoka katika ukoo unaoitwa PS , lilikuwa kundi namba moja duniani kabla sijaja kumiliki The Eagles”Aliongea Roma.
“PS! , Inamaanisha nini?”
“Inamaanisha Cyclops , wametengenezwa na Mungu kama ilivyo kwa Titans , wanasifika kwa ujuzi wa kutengneeza siraha”Alijibu Ron. Na kisha akaendelea kuelezea.
“Ijapokuwa ukoo huo ni wa kushangaza sana na hakuna ambaye anajua makao makuu yao yako wapi lakini ni binadamu wa kawaida na sio Cyclops halisi , lakini hata hivyo kila mwanajeshi wao ana nguvu kubwa pamoja na miili mikubwa , ni wakatili mno na kuna muda baadhi ya watu wanashuku chanzo cha damu yao halisi kinatokana na nini , lakini mwisho wa siku haikushangaza sana kwani kuna makundi mengine ya siri kama vile Panther na Shaman ambayo wanachama wake wote wamezaliwa na uwezo wa ajabu ukijumlisha pia na kundi la wachawi kutoka Scotland la SIS ambao uwezo wao ni wa kurithi, hawa Ps kuna tajiri mmoja alitaka kuwakodi lakini aliishia kuuliwa yeye mwenyewe na pesa yake ikachukuliwa , licha ya kuwa na sifa mbaya lakini bado kila mashindano yanapofanyika wanaruhusiwa kushindana katika Baraza la kaisari , lakini hata hivyo hawafahamiki sana kwani sio wenye kujiweka wazi hivyo ni watu wachache sana wanaowafahamu”
“Aisee , inaonekana wanaogofya sana”Aliongea Rose na kisha akamgeukia Roma aliekuwa kimya akiwa bize na chakula.
“Hubby vipi kuhusu wewe , mwaka jana hukujiunga kwenye mashindano hayo , je wana nguvu kuliko wewe?”
“Unafikiria sana , siruhusiwi kuingia katika mashindano hayo na isitoshe siwezi kukodi Masenari na pia mimi nina uungu ndani yangu hivyo sheria zinanizuia kuhusika katia maswala ya kimataifa , wanaoshiriki katika mashindano hayo kwa upande wangu ni wanajeshi wabobevu wa The Eagles lakini hata hivyo Ps wanauwezo wa ajabu hivyo ni halali kwamba hawakuhaki kushika namba moja”
“Bahati nzuri ni kwamba katika Baraza hili hairuhusiwi kuua kwa makusudi “Aliongea Callejon huku akicheka.
“Mfalme Pluto unaonaje tukienda pamoja kuangalia mechi angalau hata moja jumatatu ijayo ,, nimesikia washiriki kutoka kikosi cha The Ealges wa mwaka huu wana ujuzi wa hali ya juu . kuna uwezekano wakawaangusha Ps awamu hii”Aliongea Callejon.
Roma hakuwa na tamaa ya kwenda kuangalia , kitu ambacho ameweza kukishuhudia miaka minne iliopita ni kwamba hao wanachama wa kundi la ps kama angewafananisha na majini basi wangekuwa katika levo ya mzunguko kamili kutokana na namna ambavyo walikuwa na miiili iliojengeka na nguvu za ajabu.
Hivyo alijua kabisa hata kama wanajeshi wake kuwa na uwezo mkubwa lakini hawawezi kuwashinda Ps.
Rose na Magdalena alikuwa wakimwangalia kwa namna ya kumtaka akubali kushiriki ili na wao waende wakaone kitu hiko kinavyofanyika katika ulimwngu wa underworld,.
Ndio Baraza la Kaisari halikuwa likisimamiwa na sheria za ulimwngu wa halali bali shetia zake zilikuwa ni zile zilizokuwa zikitumika katika ulimwngu wa wahalifu maarufu kama Undeworld.
“Mbona mnanniangalia hivyo , mnataka kwenda kuona?”Aliuliza Roma na wote kwa pamoja walitingisha vichwa vyao.
“Tunaweza kwenda , lakini siwezi kukaa hapa kwa wiki nzima , nyie mnaweza kubakia hapa kwanza na nitarudi wiki ijayo kuwasindikiza”Aliongea Roma , hakutaka kubakia hapo kwani angemfanya Edna kuwa na wivu.
Roma mara baada ya kuongea hivyo Magdalena na Rose walijawa na shauku kubwa na kuisubiria siku ifike kwa hamu zote.
Kwa mtu yoyote ambaye akisikia wanajeshi wakipigana ndani ya ulingo lazima awe na shauku ya kutaka kuhudhuria kwani tamaduni hizo ni kama zimeshsahaulika kwani zilifanyika katika miaka mingi iliopita.
Lakini ajabu ni kwamba bado tamaduni hizo zilikuwa zikifanyika ila kwa siri sana na hata wale watu wakubwa wanaoenda kushiriki kuangalia mapambanno hayo ni wale ambao wanapokea mialiko maalumu na wenye uhusiano wa moja kwa moja na ulinwengu wa kihalifu.
Unaweza ukashangaa na kuona labda Baraza hilo halikuwa na faida , lakini ukweli ni kwamba faida yake ni kubwa sana , ukisikia biashara ni matanganzo basi baraza hilo ni kama sehemu ya matanganzo kwani wanajeshi hao wa kukodi wangeonyesha ustadi wao wote ili kuweza kupata tenda.
Baada ya chakula Roma aliwatembeza Rose na Magdaleana katika vyumba vyote vilivyokuwa ndani ya ngome hio , baada ya kuona vyumba ni vingi na vyote vikiwa ni vya kulala ukijumlisha na tabia yake waliweza kupata kujua nia yake kama ilivyokuwa kwa Edna mara ya kwanza kufika hapo.
Roma aliwaonyesha baadhi ya vitu vyake vya thamani alivyokusanya na baadhi ya vifaa vya mazoezi na kisha akampa Ron baadhi ya maelekezo na kisha akaaga na kuondoka.
Ilikuwa ni mchana kabisa wakati ambao anafika Dar, alikuwa ametumia zaidi ya masaa matatu kwenda na kurudi.
Baada ya kufika nymbani , nyumba ilikuwa nyeupe kwani Sophia alikuwa ashasafiri kuelekea Dodoma ambako ndio makazi rasmi ya babu yake Afande Athuman.
Roma alifanya maamuzi ya haraka kuelekea ofisni na alitumia muda mchache sana kuendesha gari mpaka kufika kutokana na muda huo hakukuwa na foleni kubwa.
Baada ya kufika katika Floor ya kampuni yake ya habari alijikuta akishangaa kidogo kwani hali ya hewa kidogo ilionekana haikuwa sawa kama alivyozoea , ni kama vile kuna kitu kinaendelea.
Roma mara baada ya kuingia ofisni kwake aliweza kumuona Daudi aliekuwa akitembea huku na huko akiwa kama mtu ambaye amechangayikiwa na baada ya kumuona Roma alionekana kupata ahueni.
“Mkurugenzi hatimae umefika “
“Nini kinaendelea , kwanini kila mtu anaonekana kama kuna jambo baya ambalo limetokea?”
“Nilijua tu hutakuwa na taarifa , nimempigia simu Boss Edna muda si mrefu na ameniambia nikupe taarifa uende makao makuu kwa ajili ya kikao, nilikuwa nikikusubiri hapa”Aliongea
“Edna ananiita kwenye kikao?”Aliuliza Roma huku akikunja sura kwani ilikuwa ni mara chache sana Edna kumwita ofisini kwake kwa ajili ya kikao kwasababu hakupenda namna watu wanavyowaangalia kutokana na uhusiano wao.
Daudi palepale alimvuta Roma mpaka kwenye meza yake na kumwonyesha Monitor ya tarakishi kabla ya kumuonyesha magazeti na baadhi ya habari zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
“Angalia Mkurugezi hili jambo mpaka sasa linaelekea kuwa nje ya uwezo wetu”
Roma alijikuta sura yake ikikunjamana mara baada ya kuona kitu kinachozungumziwa .
“Sophia Achafua hali ya hewa , Wahi kwenye App Fasta”
“Mrembo na Malkia wa Mziki Sophia ni mchepuko wa kiongozi mkubwa wa kampuni anayomdhamini”
“Sophia Star wa kimataifa aonekana katika shule ya watoto ya Braeburn , Inawezekana akawa na mtoto kwa muda mrefu”
“CEO wa kampuni ya Vexto kudhalilishiwa, Msanii aliepo chini ya kampuni yake anatoka kimapenzi na mume wake”
“Mrembo wa kupindukia hatimae kila kitu kipowazi juu ya mtu anaetoka nae kimapenzi , aonekana kwenye picha za kimahaba na mwanaume”.
“Siri ya mafanikio ya Mrembo Sophia yafichuka , inasemekana anatoka kimapenzi na bosi wa kampuni ilioendesha mashindano ya Kizazi nyota”
Vilikuwa ni vichwa vya habari katika magazeti na baadhi ya chaneli za mitandaoni za habari , zikimzungumzia Sophia huku mwanadada kutoka Marekani , Mtanzania mbea wa taifa akilivalia sana swala hilo njuga.
Katika baadhi ya picha zilizoambatanishwa katika habari hizo ni wakati ambao Roma alimvalisha Sophia kofia baada ya kujisahau na kuivua wakati wakimpigia makofi Lanlan mara baada ya kumaliza kucheza na kuimba na kundi la watoto wenzake.
Zilikuwa ni picha shawishi kuamini watu ambao wapo kwenye hizo picha kuwa katika mahusiano , kwani Roma alikuwa kwenye tabasamu na Sophia vilevile alikuwa kwenye tabasamu.
Huenda Paparazi aliechukua picha hizo alifanya makusudi kwani kabla ya tukio la Sophia kujisahau na kutoa miwani na kofia yake , Edna alikuwa ndio kwanza ameondoka kwenda mbele kwa ajili ya kumpiga Lanlan picha.
Roma mikono yake ilianza kumtetemeka mno kwa hasira na kidogo tu avunje meza.
“Uzushi , Uzushi, nani ambaye amevujisha huu uzushi mitandaoni , je wanakitafuta kifo?”Aliongea kwa hasira.
Ilikuwa bora kama wangemuhusisha yeye mwenyewe , lakini kitendo cha kumuingiza Edna katika jambo hilo kilimuuzi sana na kumfanya Sophia aonekane kama malaya.
Hakuwahi kudhania kama kuna mtu ambaye anaweza kuwachukua picha kwa muda mfupi sana ambao Edna aliwaacha na alijilaumu kwa kufanya kosa la namna hio kwa kutokuwa makini.
“Director hata mimi nakuamini”
“Daah , nitawaua hao wapuuzi ambao hawatuamini”
“Director punguza jazba , hatuwezi kutatua hili tatizo kwa namna hio ,nilituma mtu kuulizia ni Paparazi gani aliwezesha kuchukua hizio picha na kuzisambaza mtandani lakini hatukupata maelezo ya kutosha , lakini taarifa ya watu walioanza kuisambaza ni kwamba zilipigwa na watu kutumia simu kwa siri na kisha wakaziuza kwa mwanadada mmoja anaefahamika kwa jina la Kimambi na kuzisambaza, tuna uhusiano wa karibu na baadhi ya vituo vikubwa vya habari hivyo hawajaripoti mpaka sasa hivi na wanaosambaza ni baadhi ya chaneli za mitandaoni na baadhi ya Blog, kwasasa kinachopaswa kufanyika ni kuanglaia namna gani tunaweza kulisafisha jina la Sophia pamoja na Boss Edna”
“Okey nitaenda makao makuu kwasasa kwa ajili ya kikao , fanya chochote kinachowezekana ili tuweze kudhibiti hio hali , pia jaribu kuchimba ili kujua chanzo cha picha hizo ni kutoka kwa nani , ninataka niwafahamishe hao wajinga kwamba wamechokoza mtu ambaye hawakupaswa kuchokoza”Aliongea Roma kibabe.
Dakika chache tu Roma aliweza kufika katika ofisi ya Ednam, alimkuta akiongea na simu,
“Mh..Sawa , asante sana mama .. nipo sawa”Aliongea Edna na kisha akakata simu na kumwangalia Roma.
“Umemuomba mama msaada?”Aliuliza Roma mara baada ya kusikia Edna anataja jina la Mama.
“Ndio sina koneksheni kubwa na viongozi , mama ana njia zake ndio maana nikaona nijaribu kumuomba msaada”Aliongea Edna na Roma hakuona ni jambo baya , ilikuwa sahihi kumuomba msaada mama yake kwani alikuwa na koneksheni zake licha ya kwamba sio mke wa raisi wa Kenya tena, lakini kupitia familia yake nchini Tanzania ilikuwa rahisi kuomba msaada.
Asichokijua Roma ni kwamba mama yake alikuwa na mahusiano mazuri tu na baba yake mzazi ambaye ni raisi wa Tanzania na ashaanza ya kumfanya Raisi Senga kumtambua Roma kama mwanae na maendeleo yaliridhisha.
“Edna sijategemea hili kutokea , ni kosa langu sikuwa makini , sikuweza kuhisia kuna mtu ambaye anatupiga picha”Aliongea Roma
“Hatuna haja ya kulaumiana nani anakosa , kwasasa tunapaswa kutafuta namna ya kumsaidia Sophia kwani anasingiziwa kitu ambacho hajafanya, bado ni mdogo na hajui mambo mengi , sijui kama anaweza kuvumilia”Aliongea Edna huku akianza kutokwa na machozi
“Nilikuwa na wasiwasi ulimwengu wa kistaa utakuwa mgumu kwake na nilianzisha kampuni kwa ajili ya kumlinda lakini licha ya hivyo bado tu hili limeweza kutokea , haya yote ni kwasababu ya miimi kumuomba twende nae kule shuleni”
“Usiongee hivyo , ulikuwa na nia nzuri tu ya kutomfanya kujisikia vibaya akibaki mwenyewe nyumbani na isitoshe Sophia anafurahia kazi yake hivyo usijipe lawama , Je umewasiliana na walimu wa shulenni kwa Lanlan , maana waandishi wa habari lazima watawatafuta na kuwahoji”
“Nimempa kazi hio Benadetha kushughulika nayo , yupo vizuri sana kwenye maswala ya kijamii kama haya , tatizo kubwa ni kwmaba kuna vituo vingi vya habari mitandaoni ambavyo vinavumisha sana hili swala na inakuwa ngumu kudili nao mmoja mmoja , kama hili litaendelea tunafanyaje?”
Aliuliza lakini Roma alikosa jibu kwani hakuwahi kushughulika na maswala ya aina hio.
Muda huo huo wakati wakifikiria cha kufanya sauti ya Recho ilisikika ikijaribu kumzuia mtu kuingia ofisini kwa Edna na palepale mlango ulifunguliwa na kumfanya Roma kukunja sura.
Aliengia hapo ndani alikuwa ni Balozi Ramadhani baba yake Sophia na ilimshangaza Roma kumuona Mzee huyo kuwepo nchini.
Balozi alionekana kuwa katika kukasirika mno, huenda habari ya uvumi unaosambaa mtandaoni umemkasirisha sana kama mzazi.
“Edna nipo hapa kuhitaji majibu tu , nini kinachoendelea?”aliongea kibabe pasipo hata kujali kusalimia.
“Balozi najua mimi ndio niliemruhusu Sophia kufanya kazi za kisanii ambazo zimemfanya kuwa maarufu, kosa hili nusu limesababishwa na mimi hivyo nitafanya juu chini kusafisha jina lake”Aliongea Edna.
“Niambieni mnapanga vipi kusafisha jina lake , huu uzushi unasambaa kwa haraka sana lakini sioni hatua yoyote mnayofanya , kila mmoja anamuongelea vibaya , nyie ndio mmemfanya mwanangu kuwa maarufu hivyo mlipaswa kuchukua tahadhari mapema …..” Roma na Edna ilikuwa mara yao ya kwanza kumuona Balozi amekasirika hivyo , huenda ni kwasababu ya kumpenda sana binti yake maana alifoka na kuanza kumsingizia Edna kuwa yeye ndio kafanya mchezo huo kwa kuogopa Sophia kumpokonya mume , ilibidi Roma achukue hatua ya kumtuliza.
Muda huo huo wakati wakiendelea kuzozana kati ya Balozi , Edna na Roma aliongezeka mtu mwingine katika ofisi hio , alikuwa ni mlinzi wa Afande Athumanni afahamikae kwa jina la Faridi na ilimshangaza Roma kumuona hapo.
“Balozi nadhani hili swala sio la kumlaumu Mr Roma na Edna , tunapaswa kuelekea Dodoma , unapaswa kuwa karibu na binti yako”Aliongea Farid.
Balozi alionekana kuheshimu pendekezo ambalo limetolewa na mlinzi wa mzee Athumani na alituliza jazba yake na kuwahimiza Roma na Edna kutafuta ufumbuzi mapema.
Kwa jinsi alivyokuwa amebadilika utadhani sio yule ambaye alikuwa akimlazimisha Roma kumuoa binti yake kwa lazima, alionyesha hali ya kukasirika na hata ule woga wa kumuogopa Roma hakuwa nao tena.
“Farid ,Asante kwa msaada wako wa siku ile nilifanikiwa kumuokoa Edna kwasababu yako”Aliongea Roma akimshukuru mlinzi wa mzee Athumani.
“Msaada wangu!? , unamaanisha nini?”Aliuliza yule mlinzi kwa mshangao akionyesha hajui Roma anachomaanisha.
“Ni kuhusiana na mshipi wa kichawi , ulikuja nyumbani na kunipatia taarifa nikamsaidie Edna”Aliongea Roma na kumfanya yule bwana kushangaa na kukunja sura kwa wakati mmoja.
“Umenifananisha nilikuwa Japan kwa muda mrefu sana na tumerudi hivi majuzi , nadhani unapaswa kuelewa sasa hivi nimekuwa Bodigadi wa Balozi, nahusika vipi na mshipi wa kichawi?”Aliuliza na kumfanya Roma kushangaa na kujiuliza kama sio yeye yule aliekuja kumpa taarifa alikuwa nani.
Roma hapo hapo baada ya kumchunguza Farid aligundua alikutana na wat wawili tofauti , yule aliekutana nae alikuwa akitoa Aura inayofanana na maninja wa kundi la Yamaguchi lakini Faridi huyu alikuwa na mafunzo ya Kung Fu tu na hakuwa amebadilika kwani hata kipindi alipokutana nae mara ya kwanza alikuwa hivyo hivyo.
Roma alijikuta akijipiga kichwa kwa kutoweza kutilia mashaka jambo hilo , lakini swali liliibuka kama sio Faridi yule ni nani, alin’gata meno kwa hasira kwa kuona kuna mtu alimchezea hata kama alimsaidia.
ITAENDELEA