Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 549.

Edna alijikuta akimeza maneno yake aliotaka kuongea kutokana na namna Roma alivyomwangalia.

Maneno yale aliongea Roma ni kama yaligeuka na kuwa jiwe ambalo limetua moja kwa moja kugonga katika moyo wake uliokuwa kama barafu.

Alimwangalia machoni kwa muda mrefu kabla ya kuvuta pumzi na kuzitoa na kisha akalamba lipsi za midmo yake na kuongea.

“Wewe ni mbinafsi sana”

“Nakubali mimi ni mninafsi , ndio maana sitokubali sisi kutalakiana . siwezi kukuruhusu ukaondoka kwenye maisha yangu ,siwezi kupiga magoti pia na kukuomba tena wala sitoomba msamaha , unayo kila haki yakubakia hapa lakini wewe ni wangu na hilo haliwezi kubadilika”

“Unaongea mambo ambayo hayana sababu ya msingi”Aliongea huku akishikilia kwa nguvu nguo yake ya kulalia.

“Nataka uone uhalisia ulivyo , wewe unadhani mama amekukera sana kwa kualika wale wanawake nyumbani , unafikiria sisi wote tulikuwa tukikuchokoza kwa kukushuku , mbona unakuwa mwenye kutukandamiza , unaweza kuwa na kisirani chako kwangu utakavyo na naweza kuvumilia lakini hasira zako za haraka zilifanya kila mtu kukosa furaha , je unadhani wewe ndio unaepaswa kufanya tu hivyo , kwanini unataka kushindana na mimi? , mimi ni mume wako na uyle ni mama mkwe wako na sisi ni wanafamilia , kwanini unataka kutuletea tabu”

“Wewe… nilijua tu hujawahi kunionea huruma”

“Naongea ukweli”

“Inaniuma kwasababu kila kitu ulichoongea ni ukweli”Baada ya kumaliza kauli hio aliingia ndani na kufunga mlango wa balkoni na Roma aliishia kumwangalia lakini hakuwa na sababu ya kumsogelea tena kuingia ndani , aliamua zake kupotea na kurudi nje.

Alijikuta akisimama nje kwa muda akivuta upepo mkali unaotoka baharini na baada ya dakika tano aliingia kwenye gari , lakini ile anataka tkuliwasha simu yake ilianza kuita na aliekuwa akimpigia ni Neema Luwazo.

“Kipenzi changu , uko wapi?”Sauti ya kichokozi ya kumnyanyua nyoka pangoni ilisikika kwenye ngoma zake za masikio.

“Sauti yako inaonyesha kama unajua kinachoendelea”

“Wewe hujui wafanyabiashara mtaji wetu ni taarifa na isitoshe ni swala linalokuhusu , nasikia umekosana na mkeo na amehama kabisa nyumbani?”

“Umesikia wapi , Nasra ndio kakuambia?”

“Ah..,! Nasra sio mtu wa kuongea ongea umbea nadhani hata wengine hajawaambia , nilienda nyumbani kwenu nikakuta hakuna mtu ndio nilipofanya maamzui ya kumpigia Bi Wema na akaniambia kinachondelea , kwanini unajaribu kutuficha , haujui mtu kama mimi ambaye siku zote nina ajenda za siri nilikuwa nikisubiria hii siku itimie kwa hamu zote , namchukulia Edna kama mshindani wangu hata hivyo”Aliongea huku akicheka na kumfanya na Roma pia kucheka kutokana na utani wake.

“Inakupasa usubiri muda mrefu, kwani kisheria haturuhusiwi kupeana talaka angalau tuwe tumeishi pamoja miaka miwili”

“Haha.. Naamini atarudi tu ndani ya siku chache zijazo , nadhani sina haja ya kuendela na mpango wangu , unaonaje ukinisindikiza twende Shopping, hutujaonana muda mrefu”

“Si kwasababu muda wote unasema upo bize wewe , uko wapi nije sasa hivi kukuchukua”

“Nipo nyumbani kwangu , Donyi kaondoka leo asubuhi kulekea Los Angels na mchumba wake Kasimu nipo mpweke mno”

Baada ya kuambiwa hivyo moja kwa moja aliendesha gari kurudi uelekeo wa nyumbani kwa ajili ya kumfuata Neema.

Ndani ya madakika kadhaa Roma aliweza kufika na kusimamisha gari nje ya geti na Neema Luwazo alikuwa ashatoka nje na kumpokea kwa kumbatio , alionekana ashajiandaa tyaari kwa ajili ya kuondoka, aikuwa amevalia blauzi na suruali ya jeans ambayo ilimpendeza na kuchora umbo lake namba nane.

“Unaangalia nini , ingia kwenye gari tuondoke”Aliongea kwani Roma alikua akiangalia mtetemno kwa nyuma huku akiwa ameweka tabasamu a kifedhuli , aliishia kucheka na kungia ndani ya gari.

“Mh! Jamani mbona hili gari linanuka sigara”Aliuliza lakini Roma hakujibu zaidi ya kuguna na kumfanya Neema kumwangalia.

“Kwahio mawazo yamekuwa mengi , sijawahi kukuona ukivuta sigara , nilidhani mwanaume wangu ni wa kipekee lakini inaonekana kumbe hauko imara kudhibiti mawazo yako”Aliongea huku akivuta mdomo na kumfanya Roma kucheka.

“Okey kwanzia leo nitaacha, Wapi unataka kwenda?”

“Mimani City , tunaweza pia kula huko huko chakula cha mchana , unaonaje?”Aliuliza na Roma hakubisha kwanza hata hivyo asingerudi nyumbani na kukaa peke yake wikiend yote hio , hivyo aliona huenda ingekuwa afadhali.

Baada ya kufika Mlimani walianza kupita kwenye kila duka kwasababu Neema hakuwa na kitu kichwani anachotaka kununua hivyo alijaribisha kila kitu kilichomfurahisha , lakini mwisho wake hakuridhika na wakaishia kwenda kwenye Brand maarufu za Balenciarga , Dr Martens, Luis Vuiton na lancome.

Roma aliishia kumsindikiza maana wafanyakazi walikuwa wakimsaidia kushika kila ambacho anachagua , lakini Roma kwenye upande wa nguo hakuona kwanini Neema anachagua aina hizo za nguo kwani hazikuwa zikimvutia.

“Hey , kama unataka kununua nguo nadhani ulizopita kule nyuma ndio zinakufaa zaidi , hizi nguo nadhani ni kwa ajili ya maonyesho ya fasheni, hakuna maana kuziangalia”Aliongea Roma.

“Wewe mwanaume huelewi kama nisipovaa nguo ambazo ni za brand kubwa nikienda kwenye vikao wataniona kituko , sisi wanawake siku hizi tunajali sana kile ambacho tunavaa kuendana na wakati”

“Kuna haja gani ya kujali watu wanasemanini , kwani hakuna anaeweza kuipima thamani yako kupitia mavazi”.

“Hehe ndio dunia inavyoenda , kama sio hivyo unadhani makampuni kama haya yangekuwa maarufu , kampuni ya mkeo ukiachana na upande wa kampuni zake ndogo ndogo za ujenzi na mambo ya mafuta lakini pia upande wa fasheni umemuinua sana kiuchumi”

“Inaonekaa hufatilii sana kile ambacho kinaendelea kwenye kampuni , hivi majuzi tu aliweza kuingia ubia wa kibiashara na kampuni zenye majina makubwa makubwa kuomba haki ya kusambaza bidhaa zinazotokana na malighafi mpya , kampuni alizoingia nazo mkataba ni kama Prada , Hermes na Burberry , faida alizopata kwenye ubia na kampini hizo ni mara mbili yake anayopata kwenye kampuni zake za ujenzi ukiachana na mafuta pamoja na viwanda vya utengenezaji wa bidhaa za ndani”

“Ana kipaji cha kufanya biashara , lakini nadhani anapaswa kujifunza namna ya kuwa mke bora”Aliongea lakini Neema alicheka.

“Mbona unacheka?”

“Ni hivyo uliposema ana kipaji cha biashara lakini kwa mtazamo wangu naamini ni kinyume chake , ameweza kufanikisha yote hayo kutokana na ukweli kwamba baba yake ni mtu mzito na ana ushawishi mkubwa kwa Raisi Senga na nchi zote za Afrika ya mashariki na kati

“Unamaanisha nini?”

“Wafanyabiashara kama sisi siku zote tunapaswa kufanya vitu kwa wakati sahihi , sehemu sahihi na watu sahihi , kuwa na watu sahihi sio kitu kigumu kwasababu unachotakiwa ni kuwa na ushawishi tu na maipo mazuri , kuhusu sehemu sahihi inategemeana na bahati yako katika biashara , kama sio kampuni ya Vexto kuchagua maeneo sahihi katika kufanya biashara basi siamini ingeweza kuwa na mafanikio makubwa kwa nchi kama hii ya kwetu ambayo ndio kwanza inaendelea , kitu kigumu katika biashara ni kufanya vitu kwa wakati sahihi kwasababu kikawaida inategemnea sana na sera za nchi , kadri utakavyofanya vitu ndani ya sera za serikali basi huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu fursa za kibiashara , kama sera haiendani na biashara yako hata uwe na mtaji mkubwa kiasi gani huwezi kufanikiwa na ndio maana wawekezaji wanapoenda kuwekeza kufanya biashara katika mataifa ya nje wanachoangalia ni Sera”

“Kwahio unachomaanisha ni kwamba Raisi Jeremy alikuwa akimsaidia Edna katika maswala ya sera ndio maana kampuni yake inafanya vizuri?”

“Ndio maana nakushauri kuwa makini na Raisi Jeremy , ijapokuwa hakuwahi kumtambua Edna waziwazi kama mtoto wake, lakini amesaidia sana kampuni ya Vexto kufikia pale ilipo, huenda kama atakuja kumwambia Edna mambo ambayo amefanya Edna moja kwa moja ataguswa”Aliongea Neema na kumfanya Roma kukumbuka kuna siku Edna ashawahi kumwambia kuhusu mtu anaefahamika kwa jina la the Protector ni kama maneno ya Neema yamemkumbusha kuhusu hilo jina kwani alikuwa amesahau kwa muda mrefu.

“Kwanini unaniambia haya ghafla tu, unadhani kwanini Jeremy anaushawishi mkubwa ndani ya Afrika mashariki na kati?”

“Kuna kitu sikukuambia kwasababu nilikuwa bize na kazi , lakini katika moja ya vitu ambavyo niliweza kugundua katika baadhi ya nyaraka alizoacha mstaafu Kigombola ni juu ya raisi Jeremy na siri zake”

“Siri zake!”

“Ukweli kama ningeona taarifa hizo miaka ya nyuma kabla ya kukutana na wewe nisingezielewa wala kuamini , lakini kwa kipindi ambacho tumekutana na nikajua mengi ambayo hayaonekani katika huu ulimwengu ndio maana nimefanikiwa kuelewa kile alichoandika”

“Umegundua nini?”

“Kwa maelezo ya Kigombola ni kwmaba Raisi Jeremy ana nguvu kubwa nyuma yake ambayo inamlinda na inahusiana na viumbe wasioonekana(majini) , katika nyaraka nilizoweza kupata kusoma jamii hio inafahamjka kwa jina la Panas kama sikosei”Roma alishangaa maneno ya Neema.

“Amejuaje kuhusu hii jamii kuwa nyuma ya Jeremy , mwenyewe nilianza kufikiria hili swala mara baada ya kuona watu wawili kutoka Panas ambao tayari wapo katika levo ya Nafsi wakimsindikiza kama mabodigadi”

“Nini!!, kwahio nilichosoma ni kweli jamii hio ipo, kama ndio hivyo inamaanisha kwamba wametoka katika maficho yao sasa wanataka kuingilia amswala ya kawaida ya dunia?”Aliongea Neema Luwazo kwa mshangao.

“Siwezi kujua, lakini uwepo wao hapa nchini ulinipa maswali mengi ambayo sijayapatia majibu bado na kama uliosema ni kweli basi naanza kupata picha lakini pia shauku yangu kuzidi kuongezeka , je hakuna kitu kingine ambacho uliweza kupata katika maelezo uliosoma?”

“Maelezo niliosoma ni hayo pekee na ndio nguvu kubwa ya Raisi Jeremy nchini Rwanda , ilionekana Kigombola bado hakuwa na majibu ya kutosha na hata alichokiandika hakikuwa na ushahidi , lakini baada ya wewe kusema wameonekana hapa Tanzania sasa naamini maneno yake”Roma alifikiria kidogo na kuona huenda kuna sababu ambayo watu wa Panas wakaamua kuja upande wa duniani , lakini kama ni hivyo kwanini Aphrodite na wenzake hawakumweleza kuhusu hii jamii maana kama na wao walikuwa wakitumia nguvu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi basi wangewalaetea mtafaruku wakati walipokuja duniani.

“Kama ni hivyo je unadhani swala hili linaweza kumuhusu Edna?”

“Lazima liwe linamuhusu , nadhani mpaka sasa huna taarifa, ukweli ni kwamba mpaka sasa mtoto wa pekee wa Raisi Jeremy hafahamiki alipo , ijapokuwa taarifa hio ni ya siri lakini hawezi kuificha kwa watu kama sisi ambao tunahusiano wa moja kwa moja na serikali, kama hisia zangu zitakuwa sahihi basi naamini anataka kumfanya Edna kuwa mrithi wake”Aliongea na kumfanya sasa Roma kuelewa kitu.

“Nadhani ndio maana alionekana kuwa na haraka ya kumtaka Edna kumtambua kama baba”

“Unamaanisha alishaanza kuongea na Edna?”

“Siku ambayo niliwaona hao watu kutoka Panas ndio wakati ambao alifika nyumbani kwetu kwa ajili ya kuongea nae , lakini inaonyesha Edna hakuwa tayari kukubali”

“Wasiwasi wangu ni kwamba ataishia kukubali na kama hilo litatokea mkeo anaweza akakuingiza kwenye mtego , mpaka sasa naamini Hongmeng ni maadui zako na hata jamii hio ya Panas sidhani kama wanakuchukulia kama rafiki au adui, Jeremy ndio mtu pekee ambaye atafanya kila kitu kwa faida yake na mawazo yake yote ni kuona Rwanda inakuwa kimaendeleo kwa kunyonya rasimali za nchi zinazomzunguka kupitia njia za kijasusi”Roma alijikuta akianza kuwa na wasiwasi, alijua msimamo wa Edna ulivyo likija swala la familia.

“Lakini sidhani Edna anaweza kuwa mwepesi namna hio”Aliongea Roma.

“Hata mimi natumaini asiwe mwepesi wa kukubali kila kitu”

“Okey, nimekuja kurelex sio kuongea mazungumzo haya , hebu tuendelee na kilichotuleta”Aliongea Roma na kisha waliendelea kufanya shoping.

Ni muda wa saa saba wakati wakiwa kwenye mgahawa wakipata chakula cha mchana Roma aliweza kupata msisimko wa kuongezeka kwa mtu mwenye nguvu za kijini na kujikuta kugeuza shingo yake kuangalia upande wa kulia na palepale aliweza kumuona Omari Tozo akiingia eneo hilo.

Omari alikuwa amevalia mavazi ya suti na kwa mwonekano wake ni kama vile amekuja hapo ndani kwa ajili ya kuonana na mtu , baana ya kukagua baadhi ya watu palepale aligeukia upande wa aliposimama Roma na kisha akatabasamu na kupiga hatua kumsogelea.

Tokea siku ambayo waliweza kuhudhuria harusi yake hawakuwahi kuonana tena.

“Madam Neema nadhani hutonilaumu kwa kuingilia muda huu mzuri kwenu wa chakula cha mchana nikimchukua kwa dakika huyu kiumbe , si ndio?”Aliongea Omari huku akiweka tabasamu.

Kwa muonekano wa Omari alivyo alijua tu kuna kitu anahitaji kuongea nae.

“Nadhani ndoa tamu , naona una mabadiliko makubwa ya kiafya”Aliongea Neema kwa utani na kumfanya Omari kutoa cheko kama kawaida yake.

“Nadekezwa mwenzenu , nashindwaje kunenepa sasa”Aliongea na kisha wakasogea meza ya pembeni kwa ajili ya kuongea,.

“Kwa muonekano wako nadhani hatujakutana hapa kwa bahati mbaya si ndio?”

“Upo sahihi , nipo hapa kwa niaba ya serikali chini ya TSS kukuuliza maswali kadhaa ya kiusalama”

“Maswala ya kiusalama , tangu lini serikali ikaniuliza maswala ya kiusalama wakati mimi ni rais mwema?”Aliuliza Roma kwa mshangao.











SEHEMU YA 550.

Roma alijua sio rahisi kwa Omari kumtafuta na kutaka kuongea nae maswala ya kiusalama , lazima kutakuwa na kitu ambacho kinaendelea ambacho yeye hakifahamu , imepita wiki kama tatu tokea The Eagles kuondoka Tanzania na kurudi visiwa vya Mediterranian hivyo hakuwa na chanzo sahihi cha taarifa.

Aliwaondoa kwasababu ya kwamba tishio la kiusalama lilishaisha kutokana na kumuua Yan Buwen na washirika wake akiwemo Mzee Longoli.

“Kwa muonekano wako naamini huna taarifa ya makundi ya watu waliongia Tanzania hivi majuzi?”

“Ndio sina taarifa nadhani mnafahamu The Eagles project yao hapa Tanzania imesitishwa na kurudi, kwasasa nipo mwenyewe tu hapa Dar es salaam”

“Ndio maana hujaweza kupata taarifa”

“Kuna nini kinachoendelea?”

“Intellijensia ya usalama wa taifa imeweza kubaini kikosi cha giza cha Siraha Kwenye Jiwe(SIS) kutoka Scotland ,Bunge la Kiza likijumuisha wanachama wao wa kundi la Camarilla na Sabbat wapo hapa nchini , kuna pia baadhi ya makundi madogo ya watu wanaotumia nguvu za giza pia wamefika”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa.

“Wamekuja hapa Tanzania , kwasabau gani , kama ni jiwe la Kimungu nadhani wanajua halipo chini ya umiliki wangu?”

“Nadhani hawajaja kwa ajili yako na isitoshe sidhani kama wana uwezo wakupigana na wewe”

“Kama sio hivyo kwanini wamefika?”

“Intellijensia tulioweza kuvujishiwa kutoka nje ya nchi ni kwamba wapo hapa kwa ajili ya siraha ya kichawi ifahamikayo kwa jina la Magical Girdle”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa kwani neno la Magical Girdle ashawahi kusikia.

“Unamaanisha siraha iliopo kwenye hadithi za miungu ya kigiriki ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Aphrodite?”

Katika hadithi za miungu ya kigiriki na kiroma , mungu wa urembo aliefahamika kwa jina la Venus kwa kirumi au Aphrodite kwa kigiriki alikuwa na siraha ya mvuto ya mshipi wa kichawi wa dhahabu ambao uliwafanya miungu mingine kuvutiwa nae sana kimapenzi.

Inasemekana alitumia siraha hio kuwapumbaza miungu na kutawala akili zao kihisia , alifikia hatua ya kushindana na Athena pamoja na Hera katika kujiongezea mvuto kwa kutumia siraha hio na alifanya miungu yote kumchagua yeye kama mrembo zaidi.

Lakini hata hivyo ni hadithi tu , kitu ambacho kilitungwa na binadamu wakiwa wamedhibiitwa kiakili ili kufanya binadamu wengine kuwaabudu viumbe hao waliovamia dunia na kuona Binadamu ni kiumbe dhaifu.

Sasa Roma hakuwahi kusikia kutoka kwa Christen kama kweli alishawahi kuwa na siraha hio ya kichawi ifahamikayo kwa jina a magical Girdle lakini kama ilivyokuwa kwa Hades wa zamani kutokumuambia kuhusu siraha yake ya Helmeti of Invisibility(Helmet la kutokuonekana) wakati alivyomuachia urithi basi aliona huenda ni sawa kwa Christen pia.

Siraha za aina hio hata hivyo hazikuwa na maana sana kwa viumbe hawa wa sayari nyingine ambao wameishi hapa duniani kwa muda mrefu , kutokana na kwamba wanakosa miili yao halisi.

Na Roma aliona kama Christen kweli alikuwa na huo mshipi kwa alivyokuwa akimtamani huenda angeshaidhibiti akili yake na kumfanya alale nae au kufanya zaidi ya hivyo na hana uhakika kama angeweza pia kutawala akili ya Zeus na wengine.

“Kama ni hivyo unamaanisha wanatafuta huo mshipi hapa Dar es salaam ,unamaanisha mshipi huo umeonaka hapa Tanzania?”

“Hata sisi hatuna uhakika pia , na tumeshindwa kuweza kujua taarifa kamili”

“Kama ni hivyo wamejuaje kama Mshipi huu wa kichawi upo hapa Tanzania?”

“Kuna mtu ambaye ametumia Mshipi huo wa kichawi kuwadhibiti wanajeshi wa kitengo maalumu na aliweza kuonekana kwenye Rekodi ya Vidio , hio Vidio ndio ambayo imesambazwa kwa Kundi la SIS , Bunge la Kiza na baadhi ya makundi madogo madogo, Eneo ambalo limeonekana kwenye Vidio hio ni katika kambi yetu ya kijeshi ya Ruvu”

“Kama unayo hio vidio unaweza kunionyesha?”Aliuliza Roma huku akianza kuwa siriasi na Omari alionekana alishajiandaa kabla ya kufika hapo na alitoa simu yake na kuchezesha kicha akamkabidhi Roma.

“Kwenye Vidio hio ilionyesha kivuli cha mtu mwenye ngozi nyeusi yaani muafrika akijaribu kutawala akili za wanajeshi waliokuwa katika Demo ya mazoezi ya siraha na kwa kutumia Mshipi wa Dhahabu palepale wale wanajeshi waligeukana wao wenyewe na kupigana risasi.

“Ni Vidio fupi sana , tukio hili mpaka sasa ni siri ya serikali na limetokea wiki iliopita , baada ya uchunguzi wa kina kufanyika na kivuli cha mtu kinachoonekana kwenye hio Vidio kutotambulika Serikali ilipanga kikao kuzima swala hili ili kubakia siri , lakini ajabu ni kwamba hio Vidio ilisambaa nje ya nchi kwa makundi hayo ya watumiaji wa nguvu za giza”

“Inasemekena pia mtu ambaye anatumia hio Dhana ametangaza kwamba ameipata kwabahati mbaya na anashindwa kufahamu namna ya kuitumia hivyo anapanga kuiachia kwa watu wengine wenye uwezo na ameificha ndani ya jiji la Dar es salaam na mtu ambaye atabahatika kuipata ndio atakuwa mmiliki”Roma alijikuta akiwaza kidogo kusharabu maneno hayo.

“Nadhani sio sawa ,kama kweli hio dhana ni yenyewe sidhani Aphrodite angeshindwa kuinasa kihisia, lakini mpaka sasa hakuna hatua aliochukua na isitoshe siraha hio haiwezi kutumiwa na mtu yoyote kwani inahitajika kuwa na nguvu ya kiuungu ndani yake, Kwahio hamjatambua kabisa hiko kivuli cha mtu ni nani na nia yake ya kufanya hivyo?”

“Bado hatujaweza kufahamu , ni swala ambalo ucunguzi wake unaendelea kwani mpaka sasa linaumiza vichwa vya wakuu wa majeshi , maana tukio la kupigana risasi wanajeshi kwa wanajeshi ni la kuogofya sana kwa usalama wa nchi”Aliongea na kumfanya Roma aanze kufikiri.

Kuna kipindi wakati alipokuwa Ufaransa watu walikusanyika kwa ajili tu ya kutaka kuipata siraha ya Thanatos , lakini sio hivyo tu hapa Dar es salaam ni kama tukio hilo linajirudia , kwani mara ya kwanza Dhana ya Holly Grail ilionekana Tanzania na makunndi ya nguvu za giza na za Nuru walifika na kuanza kupigana kuipata.

Roma mara baada ya kuwaza aliishia kucheka , alijua hata kama inaweza kuwa halisi , hakuna uwezekano kwamba wanaweza kuitumia kupumbaza watu kwani ni siraha inayomjua mmiliki.

“Lakini kwanini hili swala naona kama ni mtego , nadhani nyie watu msijisumbue , ngoja wafanye wanachoweza kufanya na sisi tuone”Aishauri Roma,

“Bro unapaswa kutusaidia katika hili , hawa watu kama itatokea wakahatarisha usalama wa nchi vikosi vyetu vya idara ya uchawi sidhani kama wanaweza kufanikisha kuwadhibiti na isitoshe wewe pi ni mtoto wa raisi na familia yenu imeweka mizizi katika usaama wa taifa”

“Ohoo!, siwezi hata kumdhibiti mke wangu mwenyewe, halafu nijihusishe katika haya mambo . kwanini niingilie?”Aliongea Roma akijaribu kukataa.

“Kama huwezi kuingilia tunalo ombi moja kwa sasa , wewe unafahamiana na miungu wenzako mathalani Aphrodite mungu wa urembo, kama kutakuwa na uwezekano wa kujitokeza na kutusaidia , maana kama watu hao wataanzisha vurugu mambo yanaweza kuwa nje ya uwezo wetu”Roma alifikiria kidogo.

“Okey nitampigia simu baadae”

“Mpigie sasa hivi Bro wakuu wanasubiri majibu muda huu”Aliongea kwa msisitizo na kumfanya Roma kukosa neno la kuongea na palepale aliamua kutoa simu yake na kutafuta namba ya Christen na kupiga na iliita kwa muda mrefu kidogo lakini Roma hakukata tamaa kwani alijua muda huo Los Angeles itakuwa ni usiku kukikaribia kupambazuka.

“Hades , are you calling to ask me about Magical Girdle too?”Aliuliza akimaanisha kwamba je anampigia kwa ajili ya kuulizia mshipi wa kichawi pia.

“Ndio”Alijibu Roma.

“Mshipi wangu wa thamani kubwa haujaibiwa , ninao siku zote hivyo naomba usiulizie tafadhari , Mshipi ambao umeonekana kwenye vidio unafanana sana na wa kwangu lakini ni feki , kuna wachawi wengi wa kiroho dunia hii, kwa mfano kundi la kichawi la Siraha kwenye Jiwe wanaweza kutengeneza udanganyifu , hivyo kwanini iwe dhana yangu ya Mshipi wa dhahabu”Aliongea kwa namna ya kujitetea na kukereka kwa wakati mmoja na kumfanyaRoma kukunja sura.

“Kwanini sasa unaonekana kuwa na hasira , miimi nimepiga simu kwa niaba ya jeshi la Tanzania kitengo cha wachawi kwani hawana uwezo wa kukuuliza moja kwa moja na isitoshe nilijua usingeshindwa kunasa kihisia pale mtu anapotumia dhana yako”

“Tatizo mnanisumbua , muda si mrefu Poseidon ,Hermes na Artemis wamenipigia na kuniamsha kwenye usingizi , naomba usijihusishe , waache watafute kama wanavyoamani lakini kama utagundua muhusika wa kuzusha uongo huo ni nani niambie nitahakikisha namchuna ngozi akiwa hai”

“Sawa lakini kwa nilivyosikia kundi la Sabbat pia lipo hapa nchini , nadhani chuki zako uzielekezee kwa Raphael kwani ndio kiongozi wa kundi hilo ambae ameagiza watu wake kuja hapa nchini na wakafatia kundi la Camarilla”

Raphaeli ndio kiongozi wa kunti la Tzimisce ambaye anatumia mwili wa Vampire , ni kiumbe kutoka sayari nyingine ambaye alifanya watu duniani wamuabudu kwa kumuita Hermes mchunga kondoo.

“Hermes ni mtu wa ajabu na sipendi kuongea nae, nadhani amefanya hivyo kutokana na kuficha uhusika wake, mpaka sasa hakuna Vampire anaemfahamu kwa jina la Hermes, Hades nitakuw amkweli kwako kila dhana ambayo tulikuja nayo imeunganishwa na roho zetu kuna zile zilizopotea na tulizobakiwa nazo , ndio maana hata Artemis aliweza kuhisia uwepo wa Selene nchini Korea kusini licha ya kwamba alikuwa umbali wa takribani nusu ya dunia, mpaka sasa dhana pekee ambayo imepotea na na imeshindikana kufahamika imepotelea wapi ni Helmeti la kutokuonekana ambalo ni siraha yako , kama hujui, Helmet hilo ni kama taji na nitofauti sana na dhana tulizokuja nazo kwani teknolojia yake ilikuwa ni ya hali ya juu sana na Hades wa dhamani kwasababu alikuwa ni mwanasayansi ndio anajua siri yake”

“Ndio maana Hades wa zamanni sikuwahi kumuona nalo , kumbe ni dhana ambayo haionekani”

“Nadhani umeelewa sasa narudi zangu kulala , kama utakuwa na muda naomba uniangalizie nani kaanzisha huo uvumi , niambie na nitakuja kumuua mwenyewe , anadhani kujificha Tanzania siwezi kumpata na kumuua”

“Kuhusu hilo usijali nitakusaidia ,lakini na mimi utanisaidia kujibu maswali yangu yote ya kile kilichotokea Korea kusini bila kunificha kitu”Aliongea Roma na kauli yake ilimfanya Christen kuwa kimya.

“Nilishakujibu tokea muda mrefu hukuzingatia ndio maana , mimi nalala”Aliongea na kisha akakata simu na kumfanya Roma kukuna kichwa chake na kujiambia atajua tu ukweli wote kuliko mambo nusu nusu wanayomwambia.

Roma ilibidi amwelezee Omari juu ya alichoweza kupata na wote walijikuta wakiwa na ahueni na aliwathibitisha hakuna mgogoro unaoweza kutokea baina ya wageni hao kama tu Mshipi huo hautakuwa halisi.

“Asante sana Bro , nadhani napaswa kuondoka sasa nikuache na shemeji, tutakutaarifu tukimpata muhusika”

“Haina haja ya kunifahamisha , hilo ni swala ambalo halinihusu”Aliongea na Omari aliaga na kuondoka.

Neema hakumuuuliza sana maswali Roma juu ya kile ambacho alikuwa akiongea na Denisi , kwani mara baada ya kurudi kwenye meza walikula chakula kama wapenzi huku wakishushia na mvinyo.

Wikiend nzima Roma alimalizia kwa Neema Luwazo na walipika na kupakua na alimsaidia pia kwenye kuvuna nishati za mbingu na ardhi.

Siku ya jumatatu mara baada ya kuamka mawazo ya Edna yalianza kukisumbua kichwa chake na wakati alipokuwa akipata kifungua kinywa kilichoandaliwa na Neema alimkumbuka na alijiambia kutokana na anavyo mjua Edna muda huo atakuwa hajapata chochote , hivyo alimwambia Neema amwandalie vitu vya kuondoka navyo kwani anampelekea mke wake, aliongea bila ya kupindisha kauli.

Neema baada ya kuambiwa hivyo alimuonea wivu Edna lakini aliishia kuandaa kwani alijua yeye ni mchepuko tu na ili aendeee kufurahia penzi na kijana huyo mdogo basi ni kuhakikisha anamfurahisha na kumsapoti kwa kila kitu na isitoshe anapata faida kubwa ya kuvuna nishati kitu kitakachompeekea kuwa mrembo muda mrefu.

Roma asubuhi hio mara baada ya kufika nje ya ofisi ya Edna aliweza kukutana na Recho ambaye alikuwa akitoka katika ofisi ya Edna na kwa haraka haraka alijua huenda alikuwa akisafisha na kuweka mazingira sawa lakini aligundua sio hivyo mara baada ya kuona amebeba mabakuli na juisi kwenye mfuko wa plastiki.

Hakuwa amemuona Recho kwa muda mrefu kidogo ni kama zaidi ya miezi mwili , lakini alionekan hakuwa amebadilika sana zaidi ya kwamba kipindi hiko alionekana ni mwanamke mwenye kujiamini sana kuliko alivyokuwa mwanzo na ni kama urembo wake umeongezeka zaidi.

“Ni wewe .,… nikajua Boss ndio amefika”Aliongea huku kidogo akionyesha hofu.

Tokea kitendo kilichotokea miezi kadhaa iliopita ilifanya wao kujihisi vibaya kila pale wanapokutana .

“Edna yuko wapi , bado hajafika kazini?”Aliuliza Roma na kumfanya Recho kushangaa kidogo.

“Kuna chochote kilichotokea kati yako na Boss? Kwanini amehamia Msasani?”

“Nadhani haina haja ya kuongelea hilo kwasasa”Aliongea Roma maana hakutaka kutanganza matatizo ya ndoa yake hadharani.

“Ulichobeba ni kifungua kinywa kwa ajili ya Edna?”Aliulizia Roma kupotezea mada.

“Ndio , amenipigia simu nimwandalie ..”Aliongea Sekretari Recho huku macho yake yote akiwa ameyaelekeza chini , alikuwa na aibu za kike kwani alishindwa kumwangalia Roma usoni.

Ukweli ni kwamba Recho licha ya kwamba alikuwa na maisha mazuri na kule kukataliwa na wanaume kuisha , lakini akili yake haikufuta tukio la kufanya mapenzi na Roma , ni tukio ambalo muda mwingine hujirudia hata wakati anapofanya mapenzi na mpenzi wake mpya na kadri siku zinavyozidi kuendelea ndio ambavyo tukio lilizidi kutawala akili yake lakini hakupata ujasiri wa kumsogelea Roma tena kwani ni mke wa bosi wake na aliogopa ikija kugundulika , kwani maisha yake wakati huo na familia yake yalikuwa mazurri kutokana na mshahara mnono pamoja na posho anazopata kutoka kwa Edna.

Muda huo ambao hawakuwa wakijua ni topiki gani waendelee nayo kuongea wakimsubiria Bosi hatimae Edna alitokea kwenye lift na kuingia eneo hilo na alijikuta akipatwa na ubaridi mara baada ya kumuona Roma mbele yake.

Jicho moja tu kwa Recho ni kama aliona lazima kuna kitu kilichotokea kati ya Roma na sekretari wake na hapo hapo alizidi kuongeza ukauzu wake.

“Boss karibu kazini , nimekuandalia ulichoniagiza”Aliongea Recho kwa mtindo wa heshima kwa bosi huku akiwa na afadhali.

Edna alimpita Roma kama hamjui na kisha alimsogelea Recho na kuchukua mfuko alioshikilia mkononi na kisha akatingisha kichwa kama ishara ya kushukuru na kupiga hatua kuingia ofisini kuingia kwake , lakini kabla hajafikia mlango Roma alianzisha maongezi.

“Edna na mimi nimekuletea kifungua kinywa mke wangu, niliju tu muda huu utakuwa hujapata chochote”Aliongea huku akimwonyeshea mfuko alioshikilia na Edna alijikuta akitoa kicheko hafifu cha kukera.

“Una uhakika umeleta kwa ajili yangu?”











SEHEMU YS 551.

Upande mwingine nyumbani kwa Afande Kweka mara baada ya Lanlan kufika nyumbani hapo akiwa ametangulizana na Qiang , aliweza kupokelewa kwa furaha na wazee wawili ngozi tofauti ,mmoja akiwa ni Mzee Kweka mwenyewe na mwingine alikuwa ni Pastor Cohen.

Pastor Cohen mara baada ya kumuona Lanan alimwangalia Afande Kweka kwa tabasamu kubwa na kutingisha kichwa kuonyesha ishara ya kukubali jambo.

Ukiachana na maswala mengi ambayo Afande Kweka na Pastor Cohen waliweza kuzungumza lakini kubwa zaidi ni swala la Lanlan kuwa mtoto wa Seventeen pacha wa Edna ambaye aichanganywa na Roma kwenye mpango LADO.

Pastor Cohen na Afande Kweka ndio watu ambao walioratibu mchakato wa kumuingiza Roma na Seventeen katika mpango LADO na moja wapo ya matokeo hayo ni uwepo wa Lanlan duniani.

“Komredi nikiri hapa hakuna ubishi , lakini nashindwa kuelewa inakuaje Roma kushindwa kumfahamu binti yake mwenyewe”

“Komredi hilo ni swali gumu kwangu , najua nilihusika kuwaingiza kwenye mpango LADO lakini uendelevu wake sikuhusika”

“Sio wewe tu ambaye hukuhusika , wote hatukuhusika, mpango LADO kumbuka ulikuwa chini ya Zeros organisation na sisi tulichokifanya ni kufuata maagizo ya kuchomeka watu ambao hawakuwa katika mpango ili kutengeneza mafanikio”Aliongea na Afande Kweka alionekan kutopinga.

“Nadhani imekuwa ngumu kutokumfahamu mtoto wake kutokana na kilichomtokea Seventeen”

“Nakuunga mkono , lakini bado kuna kitu nashindwa bado kuelewa , kama wewe umeweza kumfahamu mjukuu wako kwanini yeye baba ameshindwa hilo”

“Ukiniuliza hilo nitasema ni uzoefu lakini nikikujibu kwa niaba yake nitasema licha ya mengi ambayo yametokea lakini bado mtoto wake ameweza kurudi nyumbani kumfuata , damu ni nzito kuliko maji”

“Ningetamani kujua kila kilichotokea , nadhani mzee mwenzangu una shauku ya kujua pia nini kilitokea baada ya kupotea kwa ile ndege , kwani mpaka sasa ni mpango wa siri ambao ni watu wachache sana duniani wanaoufahamu”

“Ninatamani sana , lakini kwa uzee huu nadhani naweza kuangulie mbele za haki bila kujua kile kilichotokea”Aliongea na kumfanya Pastor Cohen kutingisha kichwa.

“Wewe ni mimi Komredi hatuna haja ya kuwa na huzuni ilimradi tulichokifanya kinakwenda kuisaidia dunia , kwasasa nadhani shauku yangu imetimia sasa , nimemwona kitukuu chako, nadhani ni muda wa mimi kuondoka , lakini kabla ya yote nataka kukueezea kile kinachoendelea ndani ya umoja”

“Nakusikiliza Komredi”

“Kwasasa ndani ya kundi , kuna ‘interval’ kubwa ya tarehe katika kalenda kwa kile ambacho wanachana wanapaswa kufanya”

“Unamaanisha nini Komredi?”

“Ukiachana na taratibu za kawaida ambazo zinaendelezwa kufanywa na wanachama kwa sasa kinachosubiriwa ni siku ya kwanza ya mvua ya theluji kwa bara la Afrika”Aliongea na kumfanya Afande Kweka kushangaa.

“Mvua ya kwanza ya Theluji katika bara la Afrika , unamaanisha Tanzania Mvua ya Theluji itawezekana kunyesha?”

“Hakika , ndio ishara kubwa inayosubiriwa “

“Ishara hii inamaanisha nini?”

“Katika umoja wetu ishara hii inamaanisha ule wakati uliosubiriwa umetimia ni kama unabii umetimia , kwa upande wa Illuminat na Allien kwao ni ishara ya utawala wao duniani kuanza”

“Nini kitatokea baada ya hapo?”

“Kwasasa hakuna majibu sahihi ,mpaka itakapojulikana ni kipi kingine kinapaswa kufanyika kulingana na Kalenda , lakini mpaka sasa tunaweza kufanya makisio, nadhani unajua nini kinasababisha Theluji?”

“Najua ni Baridi?”

“Sahihi kabisa, makisio ni kwamba kuna uwezekano joto la dunia kushuka katika viwango vya chini sana kiasi cha kupelekea bara la Afrika kuweza kupitia vipindi vya majira ya mvua ya Theluji”Aliongea na kumfanya Afande Kweka kushika kidevu , ijapokuwa hakuonyesha mshangao wake waziwazi lakini ilikuwa dhahiri taarifa hio ilikuwa ya kumshangaza.

*****

Roma alijikuta akishangazwa na swali la mke wake kwani hakuwa amemulewa kabisa , alimbebea yeye kifungua kinywa lakini tena anatilia mashana nia yake ya kumletea.

“Edna unamaanisha nini?”

“Nadhani Recho hajapata kifungua kinywa bado , usipoteze hela zako kwa mtu kama mimi , nitajifanya sijaona chochote”Aliongea na Roma palepale aliweza kuelewa anachomaanisha na kushindwa kuzuia hasira zake .

“Edna hata kama unataka kuonyesha hasira zako hupaswi kwenda mbali hivyo , ndio nimefika sasa hivi na kukutana na Recho hapa , hata kama unadhani sina jema lakini huwezi kuongea hivyo kwa kumsingizia msaidizi wako”

“Nimeonyesha wapi hasira? , au umeelewa vipi kauli yangu , kwanini unajishtukia kama huna hatia?”Aliongea na kumfanya Roma kuwa katika mtego wa maneno.

Alikuwa na hasira na kauli ya Edna lakini alishindwa kukataa wala kukubali , kwani ni kweli kuna dhambi ambayo alishawahi kufanya na Recho.Aliona kama angekataa asingeweza kuituliza roho yake yenye dhamira ya kuhukumu.

“Madam , tafadhari naomba usituelewe vibava Mr Roma amenikuta hapa na amekuletea kifungua kinywa , hakuna chochote kinachoendelea baina yetu naomba usifikirie hivyo tafadhari”Aliongea kwa uwoga huku akiangalia chini.

Roma baada ya kumuona namna ambavyo Recho anajitetea ilimfanya amuonee huruma , kwani alikuwa kwenye hali ya taharuki mno , alikuwa kama mtu ambaye amekamatika katika jambo na sasa anahofia kibarua chake kuota nyasi.

“Recho wewe unaweza kutumia hiki kifungua , kama mtu hataki haina haja ya kumlazimisha ilihali wahitaji wapo”Aliongea Roma na kuweka kwenye miguu ya Recho ule mfuko na kisha aliondoka hilo eneo na kuzisogelea lift.

Recho mara baada ya kuona ameachiwa msala alitamani kupiga magoti , lakini palepale aliushika ule mfuko kwenye sakafu na kisha akamnyoshea Edna aupokee.

“Madam naomba usimfikirie vibaya , Mr Roma kakuletea hiki kifungua kinywa kwa ajili yangu naomba ukichukue..”

Edna aliangalia ule mfuko aliopewa na Recho ulivyotuna na kisha alimsogelea Recho na kuuweka chini.

“Unaweza kuchukua na hiki pia , sina hamu ya kula chochote leo”Baada ya kusema hivyo aliingia ofisini kwake.

Recho aliona siku hio imeanza vibaya sana kwake , alijikuta akiangalia ile mifuko yote miwili , alioleta Roma na alioleta yeye mwenyewe na kujikuta akikosa cha kufanya kwani aliishia kusimama katika sehemu moja bila ya kusogea.

**********

Upande mwingine katika ofisi ya Raisi Senga asubuhi hio , Raisi wa nchi ya Tanzania akiwa ofisini kwake akiendelea na majuku yake , aliweza kufika Kabwe nje ya ofisini huku ameshikilia faili mkononi na baada ya kuruhusiwa kuingia ndani moja kwa moja alimsalimia Mheshimiwa.

“Vipi kuna jipya , kuna chochote ambacho mmefanikiwa kupata?”Aliuliza Raisi Senga kwa shauku.

“Mheshimiwa mpaka sasa hatujapata mwanga wowote wa kumpata Denisi , lakini vijana wamejjitahidi kutafuta taarifa ambazo kwa kiasi flani zinatupa tafsiri ya kile kinachoendelea”Aliongea Kabwe.

“Nipe taarifa”

“Kuna baadhi ya watu hapa nchini tuliweza kuwahoji , mmoja wapo ni Abubakari Hamadi mtoto wa Mzee Alex mmiliki wa kampuni ya JR na mwingine ni Elvis Temba mtoto wa Mkuu wa mkoa wa Dodoma”

“Na mlichogundua ni kitu gani?”

“Nadhani Denisi alikuwa na mpango anaoendeleza yeye na Yan Buween kwa siri hapa nchini kwani kwa maelezo tuliokusanya ni kwamba aliwaambia marafiki zake wote kwamba kuna kitu ambacho wanapanga kumfanyia Roma”

“Lakini Yan Buwen si ameshakufa?”

“Hili ni tukio ambalo limetokea miezi takribani mitano nyuma Mheshimiwa kabla hata ya mheshimiwa Kigombola na Yan Buwen kufariki”

“Kama usemayo ni sahihi basi hayapingani na taarifa tulioweza kupata ya Denisi kuwa na uwezo wa ajabu si ndio?”

“Ndio Mheshimiwa”

“Kama ni hivyo kapotelea wapi?, mwezi wa pii na nusu huu haonekani nyumbani na mbaya zaidi kakomba hela zangu zote zilizokuwa chini ya jina lake katika visiwa vya Shelishei , kapeleka wapi pesa zote hizo?”

“Mheshimiwa nadhani swala hili linahusiana na kinachoendelea nchini Rwanda kwani kati ya marafiki wa karibu wa Denisi ni Desmond mtoto wa Raisi Jeremy”

“Nimejaribbu kumuhoji Jeremy lakini anakuwa mgumu wa kufunguka , lakini chanzo kinaanzia katika kifo cha mke wake, sijui nini ananificha kwasasa inanipa wasiwasi kuhusu Denisi mahali alipo kama yupo salama”

“Mheshimiwa kwanini usifanye kama ambavyo Madam anapendekeza , nadhani Mr Roma atakuwa na majibu sahihi zaidi”Alipendekeza Kabwe na kumfanya Raisi Senga kusimama akitoka kwenye kiti chake.

Ukweli ni kwamba Raisi Jeremy familia yake haikuwa na amanni hata kidogo na yote hayo ni juu ya swala la kupotea kwa Denisi , lakini vile vile kuwa na uwezo wa ajabu ambao alikuwa na uhakika ni uwezo ambao amepewa na Yan Buwen.

Mama yake Denisi yaani Damasi alikuwa na mawazo sana na muda wote ni mwenye kumbebesha Lawama mume wake kwa kutokuwa makini na mtoto mpaka kufikia katika hatua ya kupotea.

Ilikuwa ni miezi miwlii imepita sasa , tokea Denisi alivyopotea ghafla mara baada ya kuweza kukwapua kiasi kikubwa cha pesa cha baba yake alichokificha katika visiwa vya Shelisheli.

Hofu ya Damasi ni kwamba alijua fika kuna uwezekano kuna jambo baya ambalo Denisi analiandaa na hilo linaweza kumuweka katika hatari ya kuuliwa na Roma kwani kwa muda mrefu alishaweza kufahamu kinyongo cha Denisi kwenda kwa kaka yake , hivyo hofu yake ilikuwa ni kubwa mno huku akimlazimisha mume wake kuchukua hatua za haraka kuweza kunusuru hali hio kabla kubwa zaidi halijatokea.

Kilichomshangaza zaidi Senga ni kwamba tukio ambalo linamtokea yeye mwenyewe ni kama linalomtokea rafiki yake Jeremy raisi wa Rwanda, kwani wote watoto wao wa kiume ambao wanaamini kuwa warithi wao hawaonekani walipo na kila dalili inaonyesha hawawezi kuwa sawa tena.

Ilikuwa ni afadhali kwa Raisi Senga kwani alikuwa na Ashley ambaye ni mkubwa na angemrithisha kila kitu chake , lakini bado sheria za ukoo wako zinampa nafasi kubwa mtoto wa kiume.

“Kabwe nadhani kwasasa sina jinsi , ni muda sahihi wa kumkubali Den.. namaanisha Roma kama mtoto wangu”Aliongea Raisi Senga na kumfanya Kabwe kidogo kutoa macho ya mshangao.

“Mheshimiwa unataka nifanye nini?”

“Blandina aliniomba nimsaidie yule msichana Najma nafasi serikalini kama hatua ya kwanza ya kujenga uhusiano wangu na Roma nadhani kwanza nitekeleze hilo”

“Ndio mheshimiwa nitakuletea faili lake”

“Haina haja, fanya utaratibu wa kuangalia nafasi gani itaweza kumfaa katika Wizara ya elimu”

“Sawa mheshimiwa”

“Kingine nitaenda nyumbani kuonana na mzee jioni ya leo na nitapata chakula cha usiku huko huko”

“Sawa mheshimiwa nitaandaa itifaki?”Aliongea na kisha akampa ruhusa ya kuondoka na kumfanya Raisi Senga kuonekana kuwa katika mawazo.

“Huenda uamuzi wangu ukawa sahihi , nikirudisha ukaribu na Roma na kuzuia hatari yoyote kumtokea Denisi nitaweza kupata faida nyingine , naweza kuushinda udhaifu walionitengenezea Freemason na naweza kurudi kwenye mstali kama kiongozi wa taifa hili”Aliwaza mheshimiwa Senga lakini muda ule ule katibu Muhtasi aligonga mlango na kumshtua katika mawazo na aimruhusu kuingia.







SEHEMU YA 552.

Ilikuwa ni saa moja za jioni , haikueleweka Roma alishinda wapi lakini muda huo alionekana ndio kwanza anarudi kuelekea Ununio nyumbani, alikuwa na haraka kwani alikuwa na miadi na Rufi siku hio kwenda kula chakula cha usiku nyumbani kwa Bi Wema , kwani tokea Bi Wema anunue nyumba ambayo anaishi na Rufi mtoto wake wa kike hakuwahi kufika.

Sasa wakati akiwa Tegeta aliweza kupokea ujumbe wa meseji ambao ulimfanya atabasamu kifedhuli ulikuwa ni ujumbe unaotoka kwa namba ambayo hajaisajili kwenye simu yake lakini kutokana na kilichotokea dakika chache zilizopita alijua nani katuma ujumbe huo na alishangaa kwa kuona kwamba mtu huyo hakuwa amekata tamaa , kwani ilikuwa ni kama mwezi mmoja umepita huenda na zaidi tokea akutane nae.

Dakika chache nyuma wakati akiwa anatokea Mbagala akiwa anapita uwanja wa taifa aliweza kugundua kuna gari inamfuatilia nyuma na licha ya kugundua hilo hakutaka kwanza kumchezea mchezo mtu aliekuwa akimfuatilia , kwani aliendesha gari kusonga mbele bila wasiwasi lakini alipokuja kupita katika daraja la Kijazi interchange Ubungo ndio alipanga namna ya kumpotezea mtu ambaye alikuwa akimfatilia nyuma nyuma.

Mtu aliekuwa anemfuatilia alikuwa ashamtambua na ilionekana pia hata mtu huyo ashajua kama ashajulikana kutokana na kwamba alikuwa akisambaza nguvu za kijini na kwa kufahamu uwezo wa Roma alijuwa atakuwa amehisi uwepo wake, lakini haikumkatisha tamaa kutimiza dhamira yake.

Roma mara baada ya kuingia katika barabara ya Sam Nujoma sehemu pekee ambaye aliamini anaweza kumpoteza mtu anaemfatilia ni eneo la Mwenge Mataa na kweli aliweza kufanikisha hilo kwani alihakikisha alikuwa mbele kabisa anagalau mbele ya magari mawili kutoka kwa mtu anaemfatilia na hio alilifanikisha na wakati tu ambao anakaribia Mwenge taa za kijani zilimruhusu kupita lakini kitendo cha kupita tu taa za rangi nyekundu ziliwaka na kuzuia magari yaliokuwa nyuma yake kupita.

Ilikuwa ni tukio la kushangaza kwani ilionekana kwa wale wanaoendesha magari kama taa hizo zilikosea kimahesabu katika kupitisha magari kwani taa iliwaka kwa sekunde sita tu na kuzima na kisha ikawaka nyekundu.

Mtu aliekuwa akimfatilia Roma katika gari aina ya Toyota Camry alitoa tusi kwa lugha ya kichina huku akigonga usukani kwa hasira na kujiapiza.

Sasa Roma alipokuwa katika eneo la Mbuyuni akikaribia Tegeta aliweza kupokea ujumbe kutoka kwa namba ambayo hakuwahi kuisevu lakini alikuwa akiikumbuka ilikuwa ikimtumia meseji za ajabu ajabu.

Roma licha ya kwamba aliweza kumpoteza mtu huyo lakini wasiwasi wake ni kwa Rufi kwani aliamini kama mtu huyo ataendeea kumfuatiia na kujua anapoishi na kuja mara kwa mara basi nafasi ya kumuona Rufi ingekuwa kubwa.

Ndio alikuwa ni msichana wa kichina afahamikae kwa jina la Xiao Xiao ambaye kwa maelezo ya Rufi alikuwa anatokea katika familia ya wakwe zake katika ulimwengu wa jamii za watu wasionekana za kichina.

Roma alipotezea kwanza swala hilo na kuwa na umakini katika kuendesha gari kwani muda umeenda, ndani ya dakika chache tu aliwea kufika nyumbani kwake na laishangaa kumkuta mtu akiwa amesimama nje ya geti na alipoangalia kwa umakini alikuwa ni Rufi na ilionyesha alishindwa kuingia ndani kwani alikuwa amefunga geti kabisa wakati wa kutoka.

“Rufi kwanini umenisubiri hapa, ungekaa nyumbani kwenu tu ningekukuta”Aliongea Roma mara baada ya kusimamisha gari.

“Ni sawa tu , nilikuwa nikipata hewa safi ya bahari”

“Msichana mjinga , huwezi kuvuna nishati za mbingu na ardhi na mishipa yako ya damu ni myembaba kwasasbu ya kiwango kikubwa cha nishati ya Yin, unatakiwa ujali afya yako upepo kama huu unakuumiza”

“Kweli?”

“Ndio”

“Nilipatwa na wasiwasi maana sikukuona siku zaidi ya tatu zote , nilikuwa na shauku kubwa ulivyosema utakuja kuungana na sisi kwa ajili ya chakula cha usiku, niishindwa kuvumilia ndani ndio maana nikaja kukusubiri hapa”Aliongea na kumfanya Roma kuguswa na matedo yake na kumwambia aingie kwenye gari waelekee nyumbani kwao , kwani ilikuwa ni upande wa pili.

Baada ya kufika na kuingiza gari ndani Roma alishuka na kumfugulia Rufi mlango na kisha alimshika mkono na kumfanya mrembo huyo kutoa tabasamu na kuona aibu kwa wakati mmoja.

Bi Wema alikuwa amenunua nyumba nzuri , ijapokuwa haikuwa kubwa kama ya kwao , lakini ilitosha familia ya watu saba na mazingira yake yalikuwa mazuri pia kufanya watu wanaoishi hapo kuonekana wa kipato cha juu , lakini ajabu kwake ni kwamba hakuwahi kuingia ndani , licha ya kwamba alipafahamu.

Baada ya kuingia ndani aliweza kuona ubunifu wa mapambo ya ndani haukuwa na utofauti na nyumbani kwake , kitu kidogo kiichotofatiana ni kwamba nyumba hio haikuwa na mapambo mengi eneo la sebuleni , ubunifu wake ulikuwa ni ule wanaoitwa Simple enterior design.

Bi Wema alitoka akiwa ameshikilia mabakuli akionekana alikuwa jikoni akiandaa chakula.

“Sir ushafika , karibu sana ndio naandaa chakula na kuna vitu vichache naendelea navyo muda si mrefu chakula kitakuwa tayari , karibu uketi”Aliongea Bi Wema kwa ukarimu.

Ukwei Bi Wema hapo alikuwa akimchukulia Roma kama Mkwe wake sio kwa Edna bali kwa mtoto wake wa kike Rufi.

“Halafu nimesahau kwenye gari nimenunu samaki , ngoja nikawalete”Aliongea Roma akitaka kutoka lakini Bi Wema alimzuia na kumpa kazi hio Rufi aifanye na Roma alitingisha kichwa kukubali na kumwachia Rufi ufunguo.

Muda wa saa mbili wakati Roma aipojikaribisha Mezani kwa ajili ya kushambulia chakula mlango wa kuingiia ulifunguliwa na kumfanya Roma ageuke na kumwangalia mgeni aliefika.

“Aisee, kunanukia vizuri jamani , naona nimechelewa , Bi Wema , Rufi nimekuja tena”Ilikuwa ni sauti ya Amina na kiswahili chake kisichonyooka na alijikuta akishangaa baada ya kumuona Roma pia yupo kwenye meza.

“Mpenzi kwanini uko hapa , na wewe umekuja kwa ajili ya chakula cha usiku?”Aliuliza kwa kingereza.

“Kwannini inaonekana kama vile unakuja mara kwa mara?”Aliuliza Roma huku akiwa ameupamba uso wake na tabasamu kwa furaha ya kumuona huyo mrembo na alishangazwa siku hio kumuona Amina akiwa amevalia Shungi kichwanni na kumfanya kupendeza zaidi.

“Anasema hajisikii kula peke yake , lakini pia anapenda mapishi ya Mama , amekuwa bize kwenye siku hizi chache hatujaonana kwa muda”Aliongea Rufi.

Amina kutokana na baba yake kusafiri kwenda nje ya nchi kimatibabu kwa mara nyingine alijikuta akiishi peke yake , kutokana na kwamba hakuwa na uzoefu na maswala ya biashara za baba yake ilimchukua muda mrefu kukaa kazini na kukamilisha majukumu yake.

“Mr unaweza ukawa hujui , ukweli ni kwamba Amina na Rufi ni marafikii wakubwa na kipidi ulipokuwa nnje ya nchi walikuwa wakitoka mara nyingi pamoja kufanya shopping na aimfundisha pia namna ya kujiremba”Aliongea Bi Wema.

“Yeah mimi sio kama nakula bure nafanya juhudi pia”Aliongea Amina na kisha aliweka chini mifuko aliokuja nayo na kusogea mezani.

Roma aligundua hakuwa makini na hawa wanawake, hakuwa na uelewa kwamba Rufi na Amina wamekuwa marafiki kama iivyokuwa kwa Dorisi na Rose kuwa marafiki, lakini ilileta maana , ukiachana na kwamba wote hawakuwa wakielewa vizuri kiswahili lakini pia walikuwa na tabia zinazoendana.

Muda wote wa chakula Amina alikuwa akipiga stori na Rufi ambazo hazikuwa na miguu wala kichwa na Roma hakutaka kuingilia zaidi ya kuweka umakini wake kwenye kula.

“Halafu sikukuona wiki nzima , ulikuwa umeenda wapi?”Aliuiza Rufi na kumfanya Amina kushika shingo yake kuizungusha kuonyesha ishara ya kuchoka.

“Nimekuja kugundua kuongoza kampuni sio mchezo , tokea nirithi nafasi ya baba yaani mambo ndani ya kampuni ni mengi , wakurugenzi wa bodi kazi yao ni kunilalamikia hili halipo sawa lile halipo sawa khaa”

“Nini kimetokea kwani?”

“Washindani wetu wa kibiashara wanahati hati ya kupata tenda ya kufunga mitambo ya gesi kwenye baadhi ya hoteli na majumbani hio ni mara baada ya kupata uwekezaji mkubwa kutoka nje ya nchi , nadhani unajua tunajihusisha zaidi katika uwekezaji wa nishati , sasa kama zabuni hio tukikosa hisa za kampuni zitaporomoka maana washindani wetu wanasapoti kubwa serikalini”Aliongea huku akitia huruma.

“Lakini kampuni yenu si ilifanya Merge na baadhi ya biashara zilizokuwa chini ya Tajiri Khalifa Tanzania , bado kuna kampuni inayoweza kuwaletea ushindani?”

“Hakika ipo , mambo kwasasa yanabadilika sana tena kwa haraka sana , ni rahisi kujenga kampuni yenye msingi mzuri wa kibiashara kadri utakavyokuwa na rasilimali watu wenye talanta kubwa ya ubunifu lakini pia wenye ushawishi wa juu , Washindani wetu inapokea sapoti kubwa kutoka serikaini hivyo kazi lazima ifanyike kwa umakini katika kudili nao , najihisi muda mwingine kuzimia nikiwa ofisini”

“Hubby tafadhari msaidie Amina anatia huruma , wewe si una hela nyingi kwanini usinunue hio kampuni?”Aliongea Rufi.

“Ujinga , kwanini nifanye hivyo wakati hawajafanya hila yoyote , wameonyesha ushindani wa haki na kama nitaingilia kwasababu tu mimi tajiri itanifanya nionekane muhun na sina maadilii, hata kama nikifanikiwa kununua vipi kuhusu makampuni mengine lazima na yenyewe niyanunue ili kumuondolea ushindani, haina haja ya kuwa na wasiwasi , Amina hata kama kampuni yako ikifilisika nitakuwa na pesa za kuwatunza wote”

“Okey nimeelewa , lakini sipendi kuona akipoteza kampuni ambayo ndio kwanza amepewa kuongoza”

“Nilishawahi kujiambia kuongoza kampuni sio jambo gumu sana lakini tokea nilivyopewa majukumu yote na baba , niligundua ni kazi ngumu mno , kuna baadhi ya vitu najikuta kwenye Dilemma hata kuvitolea maamuzi , nimejikuta nikimkubali Dada Edna , Ameweza kuwa CEO wa kampuni katika umri mdogo lakini anazidi kung’ara tu”Aliongea kwa kulalamika , lakini mara baada ya kmtaja Edna moyo wa Roma ulishituka tena na hata hamu ya chakula ikapungua palepale.

“Sir sijawahi kukuuliza , Je ulienda kumtafuta Edna nakuongea nae kwenye siku hizi mbli , amekubali kurudi nyumbani?”Aliuliza Bi Wema mara baada ya kusikia jina la Edna, kwa wakati huo Bi Wema alikuwa akijua kingeereza licha ya kwamba alikuwa na ugumu kwenye kuongea lakini aliweza kusikia baadhi ya maneno na alijifunza kwa ajili ya Rufi.

Amina na Rufi walimwangalia Roma wakitaka kusikia jibu kutoka kwake kuhusu Edna, lakini swali hilo lilimfanya Roma kuvuta pumzi na kuzishusha.

“Bi Wema nafikiri Edna hatorudi nyumbani hivi karibuni?”

“Kwanini unaongea hivyo , nini kimetokea?”Aliliza Bi Wema kwa wasiwasi na Roma hakuona haja ya kuwaficha na aliwaeleza mambo alioyafanya katika siku zote alizoenda kuongea na Edna na kuchomolewa.

“Bi Wema nashindwa kujua ni namna gani naweza kumaliza tatizo , nilimpelekea kifungua kinywa kwasababu nilikuwa nikimuwazia lakini badala ya kunipoktea alinishuku na Recho ambaye nilimkuta ofisini akiwa yeye hajafika kazini, kwanini akaanza kupandisha jazba na kutaka ugomvi?”Aliongea kwa kulalamika na kumfanya Rufi na Amina kiumwangalia kwa huzuni na walishindwa kuongea chochote.

“Mr Najua umekasirika namna ambavyo Edna anakufanyia lakini naamini anajua unafanya hayo yote kumbembeleza , lakini muda mwingine wanawake wanapofikiria kitu hawazingatii kipi ni sahihi na kipi sio sahihi wala kujali nani anatakiwa kuwajibika “

“Kwahio anataka nini sasa?”

“Mtazamo wako”

“Mtazamo wangu?”

“Ndio wanawake wanajali sana mtazamo wa mwanaume kwao , inaweza ikaonekena labda napindisha lakini hata kama amefanya makosa kukufanyia hivyo , mtazamo wako ndio tatizo , kwa mfano ulienda anapoishi kuomba msamaha lakini hukumtaarifu kwamba unaenda na ulienda kama vile atakusikiliza na kukusamehe hapohapo, nadhani hicho kimemfanya ajisikie vibaya zaidi , Edna anatabia ngumu sana kuzoeleka lakini ni mtu mkarimu na mwenye moyo mzuri, angekusamehe kama ungeongea nae vizuri , kuhusu kifungua kinywa cha leo nadhani usingemjibu wala kuonyesha kukasirika , alikuwa anajaribu kutafuta sababu tu ya kukukasirikia , sidhani kama alifikiria kweli kuna kitu kinaendelea kati yako na Recho”Aliongea Bi Wema na Roma aliona ni sahihi , alikuwa akijiamini sana mambo yangekuwa marahisi kwake kusamehewa , ijapokuwa aliomba msamaha kwa dhati lakini hakuonyesha uhatari wa kuona kwamba hatosamehewa alionyesha mwonekano ambao ni kama vile ni haki yake Edna kumsamehe na hapo ndio alipoona amekosea..

“Bi Wema upo sahihi , lakini bado naweza kusema mpaka sasa hatua ambayo tumefikia sidhani mambo yatakuwa marahisi na sioni sababu yake ni hasira zake juu yangu kumshuku au kuna mengine , sina mpango wa kumtafuta kwa sasa”Aliongea Roma.

“Unaonaje mimi nikienda na kuongea nae?”Amina aliongea na kumfanya Roma kucheka.

“Amina humuogopi Edna ?”

“Namuogopa ndio lakini sidhani kama atakataa kuonana na mimi , kwasababu siku zote ananichukulia mimi ni mwepesi kwake .. ninaweza kwenda na kumuuliza baadhi ya mbinu za kibiashara pia”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria.

Ijapokuwa aliona sio wazo zuri kwani lingemkasirisha zaidi Edna , ila aliona ni kheri Amina na yeye kwenda kujaribu maana yeye amekwama.
ITAENDELEA - MAWASILIANO 0687151346
Watsapp tunaelekea mwishoni mwishoni mwa hii simulizi... tunaelekea sehemu ya 700 wiki hii nicheki kama unahitaji mwendelezo
Ohooooooo!Iioii
 
SEHEMU YA 479.
Uhai na kifo ni kitu kimoja kama ilivyo mto na bahari kuwa kitu kimoja , Yan Buwen licha ya kuwa na nguvu kwa kiasi kikubwa lakini hakuwahi kuwaza kifo chake ni baada ya kuhamisha kumbukumbu zake kwenye mwili mpya.
Upande mwingine nae Roma akijua kwamba amemuua Yan Buwen hakujua kwamba mwenzake alikuwa hai na aliweza kuuliwa na watu dhaifu kama Kizwe na Lekcha.
Lekcha alitemea mate maiti ya Yan buwena kana kwamba anautangazia ulimwengu mwanasayansi nguli kutoka taifa la China ameweza kufa kikatili.
“Una uhakika unaweza kutumia teknolojia zake?”Aliuliza Denisi.
“Ushasahau alichoongea , amesema kuna kitu ametumia ku syncronize memori zake kwenye mwili wake mpya”
“Lekcha unamaanisha Biochip?”Aliuliza Kizwe.
“Upo sahihi , tunachotakiwa kufanya ni kupasua ubongo wake na kuitoa na tunaweza kupata kila taarifa na baada ya hapo tutakuwa na uwezo wa kupata nguvu , nina uhakika kama hatutamshambulia Roma ana kwa ana kama huyu mjinga tunaweza kumshinda huku sisi tukiwa nyuma ya pazia”Aliongea Lekcha akimaanisha kwamba kwasababu Yan Buwen ameshindwa kumdhibiti Roma basi uwezekano wao wa kumshinda kwa kupigana nae ana kwa ana unaweza usifanikiwe , hivyo njia pekee ya kumzidi ni kumshambulia kwa njia isiokuwa ya moja kwa moja.
“Kama ni hivyo basi nipo tayari , nitahakikisha mahitaji yote unapata ya kiuendeshaji”Aiongea Denisi.
“Licha ya kwamba baba yako ni raisi lakini kupata kiasi kikubwa cha pesa kusapoti uendeshaji wa hili eneo sidhani kama utakuwa nao”Aliongea Kizwe.
“Hilo lisikupe shida , mimi ni mtoto pendwa kutoka kwa baba yangu hawezi kushindwa kunifanyia uchochoro wa kukwapua bilioni kadhaa za watanzania”Aliongea na Kizwe na Lekcha waliangaliana na kutabasamu.
*******
Upande wa Tanzania ilikuwa ni kizaa zaa mara baada ya raisi Kigombola kujipiga mwenyewe risasi ya kichwa , Roma kama angeamua kumuokoa angefanikisha lakini hakutaka kufanya hivyo.
Watu wote walishangazwa na maamuzi yake , lakini hakuna ambaye alimlaumu kwa maamuzi alioyachukua kutokana na makosa ambayo amefanya na kama sheria ingechukua mkondo wake huenda angehukumiwa jera miaka isiopungua therathini kisheria hivyo ingekuwa moja kwa moja maisha yake yote angeyamalizia gerezani na huenda ndio sababu alioona inafaa kujimaliza mwenyewe .
Neema licha ya kwamba alimchukia alijikuta akilia mno na sio yeye Donyi pia alimlilia baba yake , kila mmoja alieweza kushuhudia kile kilichotokea aliweza kulia na kushikwa na huzuni.
Licha ya kigombola kujiua , lakini huku nyuma alikuwa ameacha kiasi kikubwa cha utajiri na kutokana na mali zake alivyokuwa akizimiliki basi hata kama serikali itachukua hatua ya kuzifuatilia ingekuwa ngumu kuzitaifisha , kwani nyingi zilikuwa kwa majina bandia.
Athari kubwa ambayo inatarajiwa kutokea kwasababu ya kifo chake ni ile nguvu aliokuwa nayo serikalini kupotea , watoto wake ndio walikuwa wanasiasa lakini walikuwa na nguvu kutokana na kwamba baba yao ndio aliekuwa akiendesha usukani, sasa dereva amekufa gari halina budu kuyumba na hatimae kupoteza mwelekeo.
Kifo cha Kigombola watu ambao wanakwenda kunufaika kwa kiasi kikubwa ni familia ya Afande Kweka, mathalani kwa raisi mwenyewe Senga, kwani tokea ayachukue madaraka kuna maamuzi ambayo alikuwa akishindwa kuyachukua kutokana na namna ambavyo Kigombola alikuwa akiingilia uongozi wake , hivyo kifo chake ni kama angeenda sasa kuwa raisi kamili na mwenye ushawishi kwenye maeneo karibia yote ndani ya taifa.
Huenda baada ya habari kuzisikia kutoka Marekani alipokuwepo kikazi atakuwa anashangilia kwa shangwe.licha ya kwamba yeye sio aliefanikisha kifo chake bali msababishaji mkuu ni mtoto wake Roma ambaye siku zote hakutaka kumtambua.
Baada ya taratibu zote hapo ndani kumalizika za kuondoa mwili wa marehemu kwa ajili ya kupeleka hospitalini kuhifadhia , Roma alikadiria muda ambao Edna angefika Tanzania na kwa haraka haraka aliamini kama ni kufika Dar es salaam ingekuwa ni usiku sana , hivyo hakuwa na haja ya kurudi nyumbani kwani angeenda kuwa mwenyewe.
Alichokifanya ni kuondoka na Neema Luwazo pamoja na Donyi ambao wote walikuwa kwenye majonzi ya kifo cha Kigombola , aliona akae nao karibu kwa ajili ya kuwafariji.
Neema mara baada ya kurudi kwenye jumba lake wageni waliokuwa wakimpa salamu za pole walikuwa wengi mno , maana habari za kifo cha mheshimiwa zilikuwa zishawafikia watu wengi.
Roma aliwasiliana na Ron kuulizia kama Edna amekwisha kuondoka Visiwa vya wafu na Rona alimwambia Edna anatarajia kuondoka asubuhi ya saa tano mchana kwani na Blandina na Bi Wema wote hawakuona haja ya kuendelea kubakia kwenye hivyo visiwa ilihali hakuna ambae walikuwa wakiwafahamu.
Roma baada ya kusikia hivyo aliamini mpaka muda ambao watakuja kutua nchini Tanzania ni siku inayofuata sasa, muda wa asubuhi siku hivyo alimpigia simu Diego na kumtaarufu amerudi na Edna angerudi siku inayoafuata hivyo wanapaswa kuwa makini na usalama wake atakapofika.
*******
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa , Roma aliamkia ndani ya nyumba ya Neema Luwazo kama vile yeye ndio mwenye nyumba, baada ya kupata kifungua kinywa aliamua kuwasindikiza mpaka msibani ambako alikaa kwa masaa kama matano hivi.
Baadhi ya watu walikuwa wakimwangalia kwa chuki lakini hakujali , kwanza sio yeye ambaye alimuua Kigombola bali alijiua mwenyewe, hakuhisi hatia ya kile kilichotokea.
Wakati Roma anatoka msibani kurejea mjini ilikuwa ni saa nane kwenda saa tisa , wakati alipokuwa kwenye gari alikuwa akijaribu kufanya mawasiliano kwa kumpigia Edna simu lakini ajabu ni kwamba simu yake haikuwa ikipatikana, alishangaa kwani kwa muda huo atakuwa tayari ashafika Tanzania kama kweli walitoka saa tano , sasa alijiuliza imekuwaje simu yake isiwe hewani, alijua Edna anaweza kuwa na hasira na yeye lakini hawezi kuzima simu ili asipatikane hewani kwa makusudi , alichokifanya ni kumpigia simu mama yake mzazi.
Na ndipo alipoambiwa Edna aliondoka nyumbani mara baada ya kurudi tu na kuaga anaelekea kazini.
“Roma nenda huko huko ofisini kwake ,mkayamalize maana alikuwa amenuna njia nzima mpaka tunafika Tanzania , msipo yamaliza mapema hali inaweza kuwa mbaya zaidi mbeleni , umekosea mwenyewe kumuacha mwenzio wakati ulikuwa usiku wake wa kwanza baada ya ndoa,Mnunulie na chakula umpelekee”Aliongea Blandina kwenye simu na Roma alimwambia anaelekea huko na asiwe na wasiwasi atayamaliza.
Ilionekana Blandina mara baada ya kutoka Visiwa vya wafu alikwenda kuishi tena nyumbani kwa mwanae .
Roma baada ya kufika Posta aliingia kwenye mgahawa wa vyakula vya haraka (Fastfood) na kununua chakula ambacho aliamini Edna atakipenda , aliotea kwamba muda huo Edna atakuwa hajala chochote kutokana na kuwa na hasira pamoja na mawazo ndio maana alichukua maamuzi ya kufanya hivyo
Dakika kumi na tano mbele aliweza kufika ndani ya jengo la kampuni ya Vexto na alishuka na kisha aliingia kwenye lift na kupandisha moja kwa moja mpaka kwenye floor ambayo ofisi ya Edna inapatikana.
Roma baada ya kufika kwenye meza ya sekretari aliweza kumuona Recho akutokea ndani ya ofisi ya Edna.
Alikuwa amevaa suti ya rangi nyeusi na viatu vya visigino virefu huku mkononi akiwa ameshikilia mafaili , Roma alijiambia Recho anazidi kupendeza siku hadi siku na hivi karibuni alionekana kuonesha mabadiliko makubwa zaidi , kwanza alionekana kuwa na furaha.
“Roma umerudi? Umechelewa kuja maana naona bosi hayupo kwenye mudi nzuri”Aliongea Recho kwa heshima huku akitabasamu.
“Ndio maana nimekuja kumuona , huenda naweza kumfanya kuwa na furaha”Aliongea Roma na kumfanya Recho kutabasamu.
“Yupo kwenye ofisi yake lakini ana mgeni”.
“Mgeni?”Roma alishangaa kwani kwa alivyokua akielewa taarifa za Edna kuwa likizo zilikuwa ni rasmi , hivyo ilikuwa ngumu kwa mgeni kuja ofisini kwake kwa siku kama hio ambayo ndio kwanza tu amerudi kutokea Mediterranian.
“Ni nani?, au ni mtu ambaye namfahamu?”
“Sina uhakika kama unamfahamu, kwa majina yake ni Hanson , ni mzungu na inaonekana wanafahamiana sana na bosi”Aliongea Recho na kumfanya Roma sura yake kujikunja .
“Asante , unaweza kuendelea na kazi zako”
Recho alitaka kuongea neno lakini alishindwa kuongea lolote , kwa namna ambavyo Edna alionekana tokea asubuhi , kama mwanamke alijua tu kulikuwa na tatizo kati yake na Roma , hata hivyo alikuwa na taarifa zote kwamba Edna alikuwa amesafairi kwa ajili ya kwenda kufanya sherehe ya harusi na hata yeye mwenyewe alishangazwa na kurudi kwake kwa ghafla.
Roma alivuta pumzi na kisha aligonga mlango.
“Come in”Sauti nyororo ya Edna kutokea ndani ilijibu na Roma alisukuma mlango na kisha akaingia ndani huku mkononi akiwa na mfuko wake wa vyakula.
Edna hakuwa amekaa kwenye kiti chake cha kufanyia kazi , bali alikuwa amekaa kwenye sofa , alionekana kupauka kidogo lakini kauzu zaidi , hisia mbalimbali zilipita kwenye moyo wake mara baada ya kumuona Roma.
Roma macho yake yote yalikuwa kwa mwanaume wa kizungu ambaye alikuwa amekaa upande wa kushoto kwenye sofa.
Alikuwa ni Hanson , yule yule wa miezi kadhaa iliopita baada ya kukutana nae mara ya kwanza kwenye kusanyiko la wahitimu wa chuo cha oxford ,wanadarasa wa Edna.
Hanson baada ya kumuona Roma ndio ameingia alisimama kwa haraka na kisha alimwinamia kwa ishara ya kumsalimia.
“Mr Roma nice to meet you again”Aliongea Hanson lakini Roma hakujibu salamu yake zaidi ya kwenda kuweka ule mfuko juu ya meza.
“Mama kanipigia simu na kuniambia nikuchukulie chakula kwa waswasi hujala chochote mchana”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu hafifu akimpotezea Hanson mzungu.
Edna aliangalia ule mfuko kwa dakika kadhaa na kisha akarudisha macho yake chini.
“Haina haja, nishakula tayari”Aliongea Edna kwa sauti kavu
“Ndio usijali Mr Roma nilimshawishi muda wa mchana tukapate chakula mara baada ya kugundua hajakula chochote tokea asubuhi”Aliongea Hanson
“Kwahio unasema mlipata chakula cha mchana pamoja?”Aliuliza Roma huku akianza kupandwa na hasira pamoja na wivu.
Edna ambaye alikuwa akiangalia sakafu alihisi Roma kuwa katika hasira hivyo aliinua shingo yake na kumwangalia.
“Ndio tumekula pamoja, nimefahamiana nae kwa muda mrefu sikuona kuna tatizo kama nitakula nae chakula cha mchana”Aliongea na kumfanya Roma amwangalie Hanson kwa macho makali na alimfanya mwenzake kuhisi ubaridi wa woga kusambaa mgongoni.
“Kwanza kwanini upo hapa?”Aliuliza swali Roma kwenda kwa Hanson
“Mr Roma tafadhari usifikirie vibaya , nadhani unajua nimechaguliwa kuwa mwakilishi wa kampuni ya magari ya BMW ndani ya Afrika ili kupanua soko hivyo kampuni imeamua kufungua tawi ndani ya Afrika mashariki na nimeichagua Tanzania, nimeona nifanye ushirikiano wa kibiashara na Edna”Aliongea.
“Nenda kwenye idara husika sio hapa, halafu siku nyingine ukikutana na mke wangu sitaki umwite kwa jina lake unaweza kumuita kama Mrs Roma au CEO Edna”Aliongea kibabe na kumfanya mzungu wa watu kupauka uso kwa woga.
“Romaa!” Edna alikunja sura kwa hasira na kisha akasimama.
“Nani kakupa ruhusa ya kumkaripia mgenni wangu na kumpa maagizo utavyo?,Kwanini unaingilia kazi yangu?”Aliongea kwa kufoka.
“Mpaka sasa unatakiwa kuelewa nimejitahidi kuwa mpole la sivyo angekuwa marehemu tayari”Aliongea Roma huku akimwangalia Hanson kwa macho makali mno na kumfanya kutetemeka.
“Ndio kwanza umerudi nchini, tena kabla hata likizo yako haijaisha lakini ameweza kufahamu umerudi na kuja moja kwa moja ofisini kwako na kuanza kuzungumzia maswala ya kazi , nani mwenye akili timamu anaweza kuamini hakuna ajenda nyingine anapanga kwenye kichwa chake?,Unataka uniambie amekuja ofisini na kubahatika kukutana na wewe?”
“Unamaanisha nini wewe?”
“Unaniuliza namaanisha nini tena?”Aliongea Roma huku akicheka kwa kicheko cha hasira huku akimwangalia.
“Kama amekuja hapa akifahamu upo ofisini basi ninaweza kusema sio bahati mbaya bali kuna uwezekano nyie wawili mna mahusiano au mnawasiliana kwa siri, au nadanganya?”Aliuliza Roma.
“Mr Roma nadhani unanifikiria vibaya , niliweza kupata taarifa Edna asharudi hapa nchini na imetokea na mimi sijaondoka hivyo nikaona sio mbaya kuja kuonana nae ili kujadili kuhusu mipango yangu ya kibiashara”.
“Unafikiria ninaweza kukuamini?” Aliongea na kumfanya Hanson kukaa kimya huku akitetemeka.
Upande wa Edna alijikuta machozi yakianza kujitengeza kwenye macho yake , ilionyesha muda wowote angetoa kilio.
“Roma unanishuku...?”
“Nimeona kwa macho yangu na kusikia pia kwa masikio yangu, kwaninni useme nakushuku wakati ushahidi upo?”
“Tulikula chakula pamoja huku tukizungumzia maswala ya biashara , kwanini unakuwa na uwezo mdogo wa kufikiria?”
“Unaniambia nina uwezo mdogo wa kufikiria ?”Aliongea Roma huku akitingicha kichwa chake kwa hasira.
“Unajiona upo sahihi kumwambia ana uwezo mdogo wa kufikiria mbele ya huyu mwanaume , ujasiri huo unautoa wapi?”
“Bora hata yeye hawezi kuingia kwenye ofisi ya watu na kuanza kutoa vitisho bila kuelewa ukweli wote”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma kwa macho makali.
Roma alijikuta kichwa chake kutaka kumpasuka kutokana na hasira alizokuwa nazo kwa Edna kumjibisha ujinga na kumlinganisha na Hanson.
Haikueleweka Hanson kawezaje kupata taarifa ya kurudi kwa Edna nchini , lakini ujio wake ndani ya ofisi ni kutaka kujenga ukaribu wa kibiashara na Edna, hakuwa na mawazo ya kumfanya mwanamke wake wala mchepuko bali alichokuwa akilenga ni kutaka kuwa na ukaribu na Roma pia kupitia kwake ili aweze kufanikisha maswala yake ya uwekezaji na wazo hilo alipewa na Tajiri Azizi kwamba ili arahisishe maswala yake ya uwekezaji nchini basi anapaswa kuwa na urafiki na Roma.
Lakini tatizo kwa mtu yoyote lazima angefikiria kama Roma kwa hali ilivyokuwa , Edna alikuwa amesafiri na likizo yake ilikuwa ikifahamika kiofisi na mara baada ya kukatisha likizo yake tu na kurudi ofisini Roma anamkuta yupo na Hanson , ukizingatia urembo wa Edna lakini pia umaarufu wake kama mwanamke tajiri ni sahihi kwa mwanaume huyo kuona anammendea au wana mawasiliano.
Hanson hakuelewa kama kuna ugomvi kati yao na mbaya zaidi ni kama alijiingiza na kuwa katikati ya ugomvi.
“Mr Roma and CEO Edna , I shall take my leave , Please calm down”Aliongea Hanson lakini kutokana na macho makali ya Roma alishindwa kujua aondoke au abaki.
“Mr Hanson unaweza kuondoka hatokufanya chochote”Aliongea Edna na kumfanya Hanson kujisikia ahueni na kisha aliondoka huku akiwa mwekundu na jasho kumtoka, alikuwa akizisikia habari za Roma ndio maana alikuwa akimhofia na mbaya zaidi alikuwa kwenye nchi ambayo sio yake.
Edna alimwangalia Roma usoni kwa dakika kadhaa na kisha akarudi kwenye meza yake ya kufanyia kazi.
“Ameondoka sasa, umeridhika?”
“Kwahio ulidhania nilishindwa kutomfanyia chochote?” Aliongea Roma huku bado akionekana kuwa na hasira na kumwangalia.
“Unataka kufanya nini tena, si yashaisha?”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu.
“Tokea siku ambayo tumeweza kukutana nilifanya kila kitu ambacho ulitaka nifanye , nilikuacha pia ufanye vile utakavyo na nilijitahidi sana kukufarahisha, nakubali nimefanya mambo mengi ya kukukasirisha na kwa hilo naelewa sana na ndio maana sikutaka kukulazimisha kunifanyia chochote”Alivuta pumzi na kuendelea.
“Sikuweza kuwa makini kwenye usiku wa ndoa na kukukasirisha na hilo nakubali na najua nimefanya makosa kuondoka lakini nikuambie kwamba sijutii kabisa maamuzi yangu , sijutii kwani maamuzi nilioyafanya yalisaidia kuokoa maisha ya watu , Haijalishi una hasira kiasi gani lakini angalau jaribu kuelewa wapi natokea na mimi ni nani , najua wewe ni mgumu sana kujishusha mpaka kufanya maamuzi ya kurudi mapema nje ya makubaliano hilo pia kwangu ni sawa kwani nakufahamu ulivyo , lakini nimekuja hapa kwa ajili ya kuyamaliza..”Aliongea Roma na hasira zilianza kujitengeneza kwenye macho ya Edna.
“Kwahio hicho ndio kimekuleata hapa , kwamba nikushukuru kwa kipindi chote mabacho umenivumilia na kuniaacha nikifanye nikavyo?”
“Hapana, ninachokuelezea ni kwamba kuna baadhi ya mambo napaswa kufanya bila hata ya kukutaarifu, Unajua unanifanya muda mwingine niwe na shauku ya kujua nini kipo ndani ya moyo wako , Kwanini unakosa huruma?’Aliongea Roma huku akijitahidi kujiruliza.
“Unamaanisha nini mimi kukosa huruma?”Aliongea huku akionyesha kutoridhishwa na kauli yake.
“Edna hivi unafikiri ninaweza kuvumilia tabia yako, au niache kila kitu kinachonihusu kwa ajili yako , ninaweza kuvumilia kisirani chako, ninaweza kukuvumilia kwa kunikataa kwenye usiku wetu wa ndoa , ninaweza kukuvumilia kwa kurudi bila hata ya kutaka ruhusa yangu au kutotaka kunisikiliza ….Lakini swezi kukuvumilia kukutana na mwanaume yoyote yule bila mimi kufahamu, hususani mwanaume kama yule au unafikiri nina moyo mkubwa wa kukuruhusu unisaliti , unadhani ninaweza kukunyenyekea na kukuruhusu kukutana na mtu yoyote unavyojisikia kwasababu na mimi nina wanawake nje?”
“Naomba usiendelee kuongea” Aliongea Edna huku akitetemeka na machozi kumtoka.
“Huwezi kuniongelesha hivyo mimi”
“Hahaha,,, kwanini nisiweze , Edna hivi unajiona wewe ni keki au mungu mtu na kukuacha ufanye utakavyo , ngoja nikuambie kwangu wewe ni muhimu na nakiri nakupenda lakini ukithubutu kunikasirisha na kutaka kua juu yangu sishindwi kukutembeza uchi kwenye hio mitaa ya jiji huko nje , usitumie mapenzi yangu kama siraha ya kutaka kunipanda kichwani , huna thamani yoyote bila mimi wewe…”
“Wewe..”
Edna alishindwa kuongea lakini hakuwa tayari kusikia maneno yake tena , alijihisi kukosewa sana , alikuwa na hasira kiasi kwamba alinyanyua mkono wake kutaka kumpiga Roma kibao , lakini Roma hakutaka kumpa nafasi aliushika mkono wake kwa kuudaka.
“Unataka kunipiga, unafikiri kama nitaamua kupigana na wewe unaweza hata kunigusa.?”
“Wewe…wewe mwanaharamu nakuchukia..”Aliongea na kuanza kulia kwa kwikwi lakini machozi yake hayakumyumbisha Roma.
“Sasa hivi nimekuja kugundua kukujali kwangu sana imenifanya kuwa kipofu na unaanza kunichukulia poa..”Aliongea Roma na kisha alimsukumia kwenye meza.
Alibananishwa kwenye meza kiasi kwamba aliweza kuhisi pumzi za Roma kumpuliza usoni..
Walijikuta wakiangaliana usoni kama makondoo huku wakiachana nafasi kwa umbali wa sentimita moja, Edna alianza kupaniki lakini upande wa Roma aliachia tabasamu flani hivi kama vile aliekuwa mbele yake ni adui, lilikuwa tabasamu la kifedhuli.
“Edna siwezi kuwaacha wanawake wote ambao nawapenda , wanastahidili ulinzi wangu haijalishi ni Rose ,Amina au Nasra , kwanini niwaache wakati wapo tayari kufanya chochote kwa ajili yangu au unafikiri kwamba wao ni tofauti na sio warembo na wasingeweza kupata mwanaume bora zaidi yangu? , ngoja nikuambie Neema alikuwa tayari kufa na mimi licha ya kwamba alikuwa na nafasi ya kuachana na mimi na kuyaokoa maisha yake , kwanini unajiona kama wewe ndio pekee ambaye unaweza kuwa mke wangu na wao hawawezi?”
“Kama unawaona bora zaidi acha kupoteza muda wako na mimi na chukua mmoja wapo umuoe”Aliongea Edna kwa kiburi.
“Unaongea nini wewe, nikuache wakati hatujamalizana”Aliongea Roma na kisha alianza kuyalamba masikio ya Edna kwa spidi..
Edna damu zilianza kumchemka huku akishindwa kujua Roma anataka kufanya nini , lakini kwa jinsi Roma alivyomkaribia hakuwa mjinga kufahamu ni nini kinafuatia.
NB: kipande kinachofuatia kina mambo ya ki utu uzima kama wewe ni mtoto ishia hapa tukutane next season.




SEHEMU YA 480.
Roma macho yake yalichanua huku akijihisi msisimko usioelezeka, upande wa Edna alishindwa kufanya chochote.
“Nilijitahidi sana kuvumilia kwa zaidi ya miezi tisa, lakini sasa hivi tushafunga ndoa rasmi nadhani ni muda sahihi wa kukamilisha ndoa yetu”
“Roma …Romaa..”
“Nini .. au wewe sio mke wangu?”
“Roma najua haupo hivyo … subiri tusifanyie hapa ofisni”Edna alibembeleza lakini maneno yake hayakuwa na athari kwa mbogo ambayo ishaamua lake kichwani na alijihisi mwichi kugusana na mapaja yake.
Ijapokuwa lilikuwa ndani ya suruali lakini aliweza kuhisi joto lake na namna ambavyo limetuna alizidi kuona aibu za kike , Roma hakujali , alianza kumbusu kwenye paji la uso akaenda kwenye mashavu , mdomoni na kisha akanyanyua kidevu chake juu na kuanza kulamba shingo.Mtekenyo wa ulimi ulimfanya kuanza kuhema kwa shida
“Roma…”
“Unanukia vizuri sana mke wangu”
Harufu nzuri Roma aliokuwa akiinusa kwenye mwili wa mrembo Edna ilimfanya mashetani yake kucharuka maradufu na hakukuwa na uwezo wa kuyashusha kwa muda huo.
Alimwangalia usoni huku akitabasamu na kisha akapitisha mkono wake kwenye kiuno chake na kumminyia kwake na hakuishia hapo tu mkono mwingine aliupandisha mpaka kwenye nyonyo zake zilizosimama , mkono wa kushoto haukuishia kwenye kiuno tu bali uliendelea kusafiri mpaka kwenye makalio na kuyaminya minya kama embe.
Koti lake la suti alilovaa liliachia lenyewe na kumfanya iwe rahisi kuanza kufungua vifungo vya shati lake na kuchomoa nyonyo na kulipima na kiganja chake cha mkono na aliona linaenelea vyema na kuanza kuminya minya.Yalikuwa malaini kiasi cha kushindwa kufanannisha na kitu chochote.
Edna aliweza kuhisi mwili ukimtetemeka kila muda ambapo alikuwa akisungua chuchu zake, ilionyesha ndio eneo ambalo lilikuwa likiamsha muwasha washa na kumfanya kuanza kushindwa kuvumilia na kugugumia kwa kutoa kilio ambacho kilizidi kumfanya Roma kuchanganyikiwa , Macho ya Roma yalivyolegea ilionyesha kama mtu ambaye alikuwa na kiu na mbele yake ni mto na hakuna namna anaweza kuvuka upande wa pili pasipo kukata kiu yake.
Edna alijikuta akihisi kusisimkwa na mwili sana kila saa anayoguswa na alijikuta akiacha kukamaa mwili na kulegea mwenyewe ili kuruhusu utamu usambae kila kona ya mwili wake.
Alifumba macho kwa utamu huku machozi yakianza kumtirika, sio kwa kuchukia kile anachofanyiwa bali alishindwa kuyazuia kutokana na kiwango kikubwa cha hisia, ni msisimko ambao ndio mara yake ya kwanza kuhisi.
Alijikuta hata akiona aibu baada ya kuhisi mchuzi ukianza kutoka sehemu zake za siri na ilikuwa ni kama eneo limekuwa wazi na upepo kuingia hivyo kuhitaji kitu chochote cha kuongezea ili kuziba upepo usiingie.
Alijiambia huyu mwanaume alianza kumkasirisha na kumfokea lakini bado tu amefanikiwa kumnyegesha na sasa amejilegeza na kuacha afanye kile anachotaka.
Edna alikuwa na wasiwasi kwasababu wapo ndani ya ofisi lakini alishindwa hata kuinua mdomo na kusema Roma usiendelee, ni zaidi ya miezi nane tokea waishi pamoja na huenda alitakiwa kumruhusu kumfanyia hivyo mapema , lakini kwa muda huo ni kipi angeweza kufanya , hata hivyo ni mume wake.
Alijiambia labda maisha yake yote ataishi kwa kukasirishwa na kuchokozwa na huyu mwanaume lakini mwisho wa siku angejilegeza kwake.
Edna akili ilimtoka mara baada ya Roma kushusha suruali yake ya suti chini kwa kuikusanya na nguo ya ndani na kisha kupeleka mkono kwenye mbususu yake, alijikuta akikosa uvumilivu na kutoa mguno wa mahaba lakini Roma hakutaka apige kelele alimshika kidevu chake na kuanza kumpa kiss na aliweza kupokea kwa hiari yake kwa pupa huku miguu yake ikikosa balansi maana alianza kutetema kama Mayele lakini Roma alikuwa imara kumshikili.
Alijikuta akihisi kitu kama mkojo ukimtoka na alishindwa kujizuia na kuruhusu utoke , lakini aliishia kuona aibu na kuanza kulia, huku akishindwa kuelewa kwanini mwili wake unamwaibisha na kuanza kujikojolea.
“Sijategemea mke wangu kuwa hisia kali kiasi hichi , sio kwa maporomoko haya ya maji”Aliongea Roma kwa kutania lakini Edna alishindwa kuongea zaidi ya kuguna na Roma alimbusu shavuni kwa upole.
“Wakati tunafanya kwa mara yetu ya kwanza ulikuwa umelewa , lakini sasa hivi upo na akili yako timamu nataka ujue kwamba itakuwa inauma lakini tamu na ole wako siku nyingine unichokoze mwendo ni huu huu…”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kuelewa anamaanisha nini kwani alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa.
Roma na yeye hakujali sana , alichokifanya ni kumalizia kutoa nguo zake zote zilizobakia mwilini na kumuacha akiwa mtupu kabisa na kisha akapeleka mdomo kwenye manyonyo na kuanza kunyonya na kumfanya Edna kuweka mkono yake mdomoni akijiuzia asitoe sauti kubwa kwa kuhofia huenda Recho yupo nje.
Roma hakujali aliendelea na kazi pasipo ya kujali mtetemo wa Edna na baada ya kuridhika alivua suruali yake na kuishusha chini na mtambo ukafyatujka kwa nje huku ukiwa na hasira.
Roma alimshika kiuno na kisha alimnyanyua na kumpandisha kwenye meza huku akiendelea kumpiga Denda kwa dakika kadhaa na huku chombo yake ikiisuguanisha karibu na mlango wa kuingilia ndani , Edna alizidi kutoa unyevu nyevu mtelezo kwa wingi.
“Hubby …naogopa” Aliongea Edna kwa sauti ndogo ya kubembeleza lakini ya kuvutia.
Roma muda huo alikuwa kama amechangayikiwa na hakuwa na mpango wa kuacha kile alichokipanga .
“Nishakuambia itakuwa inauma lakini muda huo huo itakuwa tamu”Aliongea Roma kwa sauti nzito lakini yenye kubembeleza na Edna kabla hajaitikia alishitukia tu mwichi ukizama ndani na kumsababishia ubaridi wa aina yake uliosafiri kuanzia kichwani kupitia mgongoni na kwenda kutua kwenye mbususu.
“Oh…”
“Ah.!”
Wakati Roma akihisi utamu , upande wa Edna alihisi maumivu na machozi yalianza kumtoka, ijapokuwa alikuwa ashawahi kufanya lakini kutokana na kukaa muda mrefu sehemu yake ni kama imerudi kuwa ya msichana tena.
Roma alifurahia mno mchezo maana alikuwa akibanwa vizuri mno na aliweza kuhisi hisia za aina yake , ni hisia ambazo zilikuwa za tofauti mno na zile alizokuwa akipata wakati akifanya mapenzi na wanawake wake wengine.
Mpaka hapo sasa tunaweza kusema ndoa yao imekamilika maana ndoa hukamilishwa na tendo la ndoa na hicho ndio ambacho kilikuwa kikifanyika , ijapokuwa ilikuwa ni ofisini lakini maana ni ileile tu kwamba hilo nalo ni tendo la ndoa linalofanyikia ofisini.
Zilipita kama dakika kumi na tano wakati Roma akiendelea kupeleka mbele na nyuma kama anacheza amapiano alijihisi naniliu yake uvutwa kwa ndani kwa staili ya kukabwa , alishindwa kuamini anachofanyiwa na Edna na aliishia kumwangalia usoni na kutabasamu.
“Edna mke wangu , sikujua kama una mbinu zako za siri, umefanya kwa kudhamiria nini , unaonekana kama mzoefu umewezaje kuifinyia kwa ndani”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kujibu chochote zaidi ya uangalia pembeni kwa kuona aibu kumwangalia usoni hata hivyo alishindwa kumuelewa anamaanisha nini kusema kufinyia kwa ndani.
Roma alijiua Edna hakuwa akifanya makusudi kuifinyia kwa ndani ila ni namna ya asili ya mwili wake ulivyo, hata hivyo licha ya kwamba Edna hakuwa na udhoefu lakini alitokea kumpagawisha na kumfanya ajihisi kama yupo juu kileleni mawinguni.
Alikuwa amekutana na wanawake wengi na kuwa mdhoefu lakini hisia alizokuwa akipata zilikuwa za aina yake, Edna na yeye ni kama alikuwa akianza kuishiwa na pumzi maana ni zaidi ya magori ambayo amefunga.
“Arrgh…Romaa …taratibu ..inauma ..oooh!”Alijikuta akilalamika lakini Roma alikuwa kama kiziwi na kuendelea kuongeza spidi na ilifikia muda akaona staili ya kimeza meza haimtoshi hivyo alimgeuza na kumshikisha mikono kwenye meza huku akiwa ameinama na kufanya msambwanda wote kurudi nyuma na Roma aliingiza tena na kuendelea kusukuma songombile yake.
Alihisi maumivu kidogo lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea alizidi kupata raha na sehemu zake ni kama sasa zishaanza kuzoea ukubwa wa mwichi wa mume wake na shoti za utamu alizokuwa akisikia zilimfanya kujihisi yupo mbingu ya saba.
Edna baada ya kuona dudu ya Roma ilikuwa ikiyasugua makalio yakekwakupita na kumwingia kwenye kitumbua chake alihisi aibu , lakini hata hivyo alishindwa kuacha kumuangalia Roma usoni.
Alijihisi utamu kwa jinsi Roma alivyokuwa akimwangalia kwa upole na kuridhika , hata hivyo ilikuwa ni kama mara yao ya kwanza kufanya mapenzi.
Edna alishindwa kuongea chochote na kuona aibu karibia muda wote tendo linafanyika na aliishia kutii maagizo kila staili ambayo alikuwa akiambiwa akae.
Mchezo uliendelea kwa zaidi ya lisaa limoja na walianzia kwenye meza na kisha wakahamia kwenye sofa, lakini Roma akaona haitoshi na kwenda kumshikisha mikono kwenye vioo vya madirisha na kumfanya Edna aliangalie jiji huku akiendelea kuhisi utamu usio na kipimo ambao ulianzia kwenye vidole vya miguu na kusambaa mwili mzima na kumwingia ubongoni.
Huenda kama kuna mtu angekuwa na darubini jengo la pili yake angeona kile ambacho kilikuwa kikifanyika , lakini Roma hakufanya mambo bila ya kuwa makini aliweza kutumia uwezo wake kuchunguza maeneo ya mbali ili isije ikatokea mtu anawaangalia.
Roma aliendelea na shughuli yake kwa muda mrefu na kufanya sauti kama za watu wanaopiga makofi kusikika ndani ya ofisi nzima.
Paah! ..Paah!!
Ilifikia kipindi Edna hakutaka kuendelea na kutaka kupumzika kwani alipiga magori mengi na kujikojolea kiasi kwamba alikosa idadi na sasa mwili wake ulikuwa umechoka mno.
“Huby inatosha .. tupumzike .. niche nipumzike kidog…”Aliongea Edna huku akihema kama mbwa ambaye amekimbia maili nyingi.
“Ni saa limoja tu lakini unaonyesha kuchoka , tufanye angalau yawe mawili , babe sikujua kumbe unatembea na Dhana ya kimaajabu kwenye mwili wako”Aliongea Roma lakini Edna alikuwa akielekea kwenye kuzimia kwani hakusikia tena utamu lakini ilionyesha kuzidi kumfurahisha Roma , huenda ni kwasababu alishaanza kuvimba sehemu zake kwa ndani hivyo eneo kuzidi kuwa dogo.
“Tafadhari Hubby … siwezi kuendelea ..naomba unionee huruma..”Aliongea na kuanza kulia kama mtoto na kumfanya Roma amwangalie namna ambavyo amelegea , hakuamini ndio yule mke wake aliekuwa akijifanyisha kauzu , muda huo alikuwa kama mtoto mchanga.
“Huwataki wanawake wangu wengine… lakini huwezi kudumu kwa zaidi hata ya lisaa kwa staili hii unakwenda kushindana nao vipi”?”
“Wewe…! kwanini uzungumzie wanawake wengine kwenye muda kama huu?” Aliongea na kumfanya Roma amlambe kibao cha kalio la kulia.
“Sihitaji ruhusa yako ninapotaka kuwazungumzia , nilichoongea ni kweli, sijatoa bao hata moja lakini bado unaonekana umechoka ,utawezaje kunizalia mtoto kwa namna hii?”Aliongea Roma na kumfanya Edna ashindwe kujibu , hakujua kama kosa lilikuwa lake kuchoka haraka au ni la mtu mwingine.
Roma ilibidi amuonee huruma na alimbeba na kumkalisha kwenye sofa ili apumzike.
“Hata hivyo mke wangu umefanya kazi nzuri angalau umenifanya nijisikie vizuri kuliko mwanamke yoyote yule”Aliongea Roma huku akimfinya mashavu lakini Edna alishia kutojibu kwani alikuwa akihema kwa tabu , alishukuru tu ameachiwa maana hakujua nini kingeendelea kama Roma angeng’ang’nia mpaka atakapotoa bao.
“Nisikilize kwa umakini siku nyingine usije ukanichokoza na kunikasirisha , wewe ni mwanamke wangu na siwezi kukuruhusu kukutana na wanaume waliokaa kihuni huni , ninaweza kuonekana sina sababu za msingi lakini unapaswa kunisikiliza mimi tu kwasababu wewe ni wa kwangu milele , unaweza usikubali lakini hakuna mtu yoyote anaweza akaja kukusaidia kama nitaamua kukuadhibu , hata hivyo kama utataka tena lazima uniombe…., Hahaa..Kaone sasa kanavyotia huruma, haina haja ya kuniangalia kwa macho lawama umeyataka mwenyewe…”Aliongea na kumfanya Edna atamani kulia.
“Mwanaume mdhalimu wewe”
“Hehe ..niiite vyovyote unavyotaka , nilifikira mambo mengi usiku wote wa jana na nimegundua hata kama nijizuie kutokufanyia chochote bado wewe ni mke wangu , hata nikiamua kukufosi pia wewe ni mke wangu ya nini kujiumiza wakati upo”Aliongea Roma na kisha alimshika kidevu na kupitisha kidole chake kwenye lipsi zake kwa kusugua sugua.
Edna alionekana kuwa na adabu sasa, hakuleta ubishi na alikuwa kama piritoni,ule ubosi kwisha habari yake.
“Pumzika bibi harusi wangu , tutaendelea tena angalau kwa lisaa lingine, unifanye agalau nimwage bao moja”Aliongea Roma.
“Lakini sitosikia chochote tukifanya tena, nahisi kumevimba..”Aliongea huku akionekana kutia huruma lakini Roma hakuwa kwenye nafasi ya kumuonea huruma maana bado hata dudu yake haijalala.
“Nitakuponyesha, kaa vizuri niingize na nitakuonyesha kwanini naitwa mfalme Pluto” Aliongea Roma na kabla Edna hajajibu alishangaa ashawekwa sawa na yote ikazama.
“Ah..!”Alijikuta akihisi damu kumcheka huku Roma akiwa amemuweka kifo pendwa cha yule mdudu msumbufu usiku anaeogpwa na wadada , wakati akidhania angehisi maumivu Roma alikusanya nguvu ya kimaandiko na kuipeleka kwenye dudu yake na Edna alihisi mtekenyo wa aina yake na aliishia kutoa mdomo kama kabanwa na mlango.
Lisaa lingine mbele alijihisi uji uji mzito ukimwagika ndani ya sehemu zake za uzazi , ulikuwa wa moto kiasi kwamba alihisi raha ya ajabu na alijikuta akikakamaaa mwili na yeye kufunga goli ambalo haikueleweka lilikuwa la ngapi na aliishia kuhema huku akimwangalia Roma usoni na alijikuta akiachia tabasamu huku akiwa amelembua na kuangalia pembeni kwa aibu.
Naam hivyo ndivyo ilivyokuwa……..
MWISHO WA SEASON 16.
WWTSAPP 0687151346 NICHEKI KUOATA MWENDELEZO , SIMULIZI NDIO INAANZA
Naendelea na hii
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI:SINGANOJR



SEHEMU YA 482.



Baada ya kupata taarifa wanasubiriwa nyumbani hawakutaka kuendelea kukaa , kwani hatahivyo walimaliza rayari kupata chakula , Roma alilipa na alimbeba Lanlan na kuingia kwenye gari.

“Mhh! nahisi wale wenza waliongia sio watu wazuri”Aliongea Edna mara baada ya kuingia kwenye gari.

“Kwanini unasema hivyo?”

“Roma unanitega sio?,nilikuona ukiwaangalia hata wewe kwa macho ya wasiwasi”Aliongea Edna na kumfanya Roma atabasamu kwa uchungu hakujua Edna angefahamu nia yake.

“Wanaonekana sio wazuri lakini huna haja ya kuwa na wasiwasi”Aliongea Roma na kumfanya Edna kukaa kimya na safari ya kurudi nyumbani ilianza.

Ulikuwa umbali mrefu lakini kwasababu hakukuwa na foleni muda huo haikuwachukua muda mrefu kufika.

Baada ya kutoka kwenye gari waliweza kupokelewa na Blandina aliekuwa akiwasubiria na alishangaa kumuona Lanlan.

“Grandmaa…”Lanlan alimkimbilia bibi yake na kwenda kumkumbaria miguuni.

“Oh! Lanlan Bibi alikumisi sana, Edna mmemtoa wapi nilijua bado yupo Songea”

“Lanlan alituona njiani , alikuwa na Anna na ndio wamefika leo mjini”Aliongea na kumfanya Blandina kuelewa.

“Sophia anawasubiria , mnapaswa kawenda kuonana na mgeni”Aliongea na Roma na Edna walitangulia na kuingia ndani huku Mama yao akimchukua Lanlan na kwenda kumkabidhi kwa Qiang Xi abadilishwe mavazi pamoja na kuogeshwa.

Baada ya kuingia eneo la sebuleni waliweza kukutana na mwanaume mtu mzima ambaye alikuwa amekaa akiangalia runinga akiwa pamoja na Sophia, alikuwa ni mzungu miaka kama arobaini hivi na Roma na Edna walisalimiana nae na kisha wakaketi.

“Sister huyu ni Director Fabby Lassay kutoka kampuni ya uzalishai wa filamu ya Penguin Production kutoka Afrika ya kusini”Alitambulisha Sophia kwa lugha ya kingereza.

“Mniwie radhi kwa kuwavamia hapa nyumbani , kama alivyosema Miss Sophia nafahamika kwa jina la Fabby Lassay ni Executive Director wa Penguin Production na nipo hapa kwa ajili ya maongezi juu ya ushirikiano wa uandaaji wa filamu:”

“Mr Fabby wewe ni mtu maarufu?”Aliuliza Roma na kumfanya Fabby kutabasamu.

“Mr Roma kama utakuwa mpenzi wa filamu basi jina langu halitokuwa geni , kabla ya kufanya kazi kama Directori katika kampuni ya Penguin nilifanya kazi na Paramaount kama Producer msaidizi na Screen Writer nina kazi nyingi ambazo naweza kusema zinanifanya kuwa mtu maarufu na nishawahi kufanya kazi na Christen atanifahamu pindi utakapomtajia jina langu”

“Okey Mr Fabby kwahio ujio wako hapa ni kutaka kumuhiisha Sophia kwenye filamu au unataka kampuni yetu kuwekeza?”

“Nipo hapa kwa ajili ya kuomba ruhusa kwenu ya kumuhusisha Sophia kwenye filamu kama mhusika mkuu wa kike , nilijaribu kuwasilisha ombi langu kupitia wakala wake lakini majibu nilioyapata ni Miss Sophia kuwa na ratiba ngumu, nilijaribu kuwasiliana na Sophia moja kwa moja na aliniambia kama nyie wawili mtampa ruhusa basi haina haja ya kupitia kwa menejimenti yake wala kampuni”

“Sophia unapenda kuigiza filamu?”Aliuliza Roma huku akmwangalia.

“Hata kama niseme napenda , nina wasiwasi naweza nisifanye vizuri kwanni sina mafunzo maalumu hivyo kuharibu kazi”

“Miss Sophia hilo lisikupe shida , nimeweza kuangalia matamasha yako na nimegundua unafaa kabisa na kwasababu tuna mwezi mzima wa matayarisho tunaweza kukuelekeza na ndani ya muda utakuwa umeelewa namna ya kuwa muhusika mkuu na kuzoea Script na isitoshe stori inaendana sana na mwonekano wako”

“Director kama unadhani Sophia anaweza kufiti kwenye nafasi ya uhusika wa stori basi hatuna haja ya kumzuia , lakini kama mambo yakienda vibaya kutokana na Sophia kukosa uzoefu nadhani hatuwezi kuhusika”

“Hilo lisiwape shida , hatujafanya makosa kumchagua Sophia katika nafasi ya uhusika mkuu na hakuna lawama yoyote kama atashindwa kuendelea”

“Kama ni hivyo nadhani hakuna haja ya kumzuia kwani itakuwa na faida kwake , Lakini Director kuhusu malipo nadhani yanapaswa kuwa ya kuridhisha”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie , yaani hata hawajafikia kwenye hitimisho lakini alishatanguliza maslahi.

“Mr Roma hilo halina shaka kabisa, bajeti ni kubwa hivyo malipo yatakuwa makubwa , lakini pia kwa kulinda heshima yangu katika ‘industry’ siwezi kutoa malipo kidogo”Aliongea na Roma aliridhika , hata hivyo alimuona Director Fabby kuwa mtu siriasi maana kuwasubiri kwa muda mrefu pasipo ya kuondoka sio jambo la kudharau, lakini pia aliwaamini sana Wazungu kwa kujali heshima yao , kama kweli Director amefanya kazi na Christen basi alijua malipo hayatakuwa haba na itamuongezea Sophia umaarufu.

Hakukuwa na maongezi ya ziada hivyo Director aliaga na kuondoka huku taratibu za mikataba zingefuata siku kadhaa zinazofuata kupitia kampuni ya Vexto Media pamoja na menejimenti, Sophia yeye hakuondoka kwasababu ishakuwa tayari usiku.

Baada ya kuongea kwa muda mfupi kama wanafamilia Bi Wema ndio aliekuwa wa kwanza kuaga kwenda kulala.

“Lanlan atalala na mama?”Aliongea Lanlan na kumfanya Roma kung’ata meno kwa kuona Lanlan anamchawia na mbaya zaidi alijitia huruma mbele ya Edna.

“Kibonge utalala na mlezi wako Qiang Xi , huwezi kunipokonya mke wangu”

“Lakini Lanlan hawezi kulala bila mama” Aliongea huku akimwangalia Edna kwa kutia huruma .

“Lanlan usiwe hivyo, utalala na Mama, Sawa mtoto mzuri”Aliongea Edna na kumfanya Lanlan kutabasamu huku akitingisha kichwa na kumwangalia baba yake kana kwamba anamwambia ameshinda.

“Wewe kibonge nyanya nisikilize mimi baba yako kama unataka zawadi”

“Mr Roma nadhani tumuache Lanlan afanye kama anavyotaka, usiku anatabia ya kushituka na kukaa macho nikilala nae na anapaswa kuamka mapema kwenda shule”

“Qiang Xi mbona hujawahi kusema” Aliongea Blandina kwa mshangao.

“Lanlan ndio alivyo tokea nilipoanza kumlea tena imekuwa afadhali tokea aishi na mama yake amekuwa akipata usingizi mapema”

“Ah…!!”Roma alijikuta akikosa neno la kusema na kumfanya Edna amwangalie na kufurahia mwonekano wake.

“Roma lakini kwanini unalazimisha Lanlan akalale na mlezi wake, si nyie mnalala vyumba tofauti au…”

“Mama ni kwamba mimi na Edna tume…”

“Wewe usije ukaongea” Edna alimkatisha huku akitamani amtie Roma ngumi , alishindwa kumuelewa Roma ni mtu wa aina gani anataka kuropoka bila aibu mbele ya mama yake, hakutaka siri ya wao kufanyia ofisini ifahamike.

Roma mara baada ya kuona amekatishwa na Edna alitabasamu na kuonyesha ishara ya kuziba mdomo.

Blandina alishaelewa kilichokuwa kikiendelea hivyo hakutaka kutia neno hata kwa Sophia hivyo hivyo waliishia kutabasamu.

“Sister Edna Hongera sana na kwako Shemeji nadhani unapaswa kutafuta namna ya kushindana na Lanlan”Aliongea Sophia huku akisimama na kumfanya Edna atamani kuwe na shimo atumbukie kwa aibu alizojisikia.

“Hahaha… nyie watoto mnanifurahisha, Roma nadhani uvumilie , Mjukuu wangi Lanlan anapaswa kupata usingizi mapema ili asijekwenda kusinzia shule”

“Grandma is so nice”.

“Lanlan umeelewa nilichoongea?”Aliuliza Blandina kwa mshangao na Lanlan alitingisha kichwa, alionekana ashaanza kukamata baadhi ya maneno ya kiswahili na kuanza kuyaelewa.

“Mjukuu wangu una akili nyingi , utakuja kuwa mtu mkubwa baadae”Aliongea huku akimshika shavu na Lanlan aliishia kutabasamu kwa kutoa meno yake machache nje.

Baada ya Roma kuona amepokonywa mke na mtoto wake , ilibidi kwanza akae sebuleni , hata hivyo kuna kitu alichokuwa akisubiria kwa hamu zote.

Baada ya watu wote kuondoka kwenda kulala, hatimae mwili wake ulianza kusisimka huku vinyweleo kusimama.

“Naona hatimae mmekuja?” Aliwaza kwenye akili yake na kuzima runinga na palepale alipotea na kutokezea nje ya geti , lakini ile anaibukia aliona vivuli vya watu wawili vikipotea kwenye upeo wa macho yake.

Walikuwa ni walewale aliokutana nao kule PalmVillage Restaurant, Roma alijua walikuwa wakitoka hapo ili wasionekane na aliwafuata kwa harufu yao na ndani ya sekunde alikuja kuibukia kwenye fukwe mita kadhaa kutoka nyumbani kwake na hatimae aliweza kukutana na watu wawili waliosimama wakiwa wamempa mgongo.

Roma alitabasamu mara baada ya kugundua wote wawili wamebadilika kimuonekano, walikuwa wamevaa mavazi ya kitamaduni maarufu kama Robes , walionekana kama vile ni wale waigizaji wa filami za kale za mataifa ya Asia, mfano Jumong.

Wote walikuwa wamefunga nywele zao kwa nyuma huku mkononi wakiwa wamshikilia upanga(sword) ambao upo ndani ya Ala kwa kila mmoja.

“Nyie ni wakina nani kwanini mnanifuatilia” Aliongea Roma na wale watu waligeuka na kumwangalia na hapo Roma ndipo alipowaona sasa , walikuwa sio wenye asili ya wasomali tena bali mmoja wa kiume alionekana kama Mchina na wa kike alionekana kama mkorea.

Kwa haraka haraka alijua mwanamke alikuwa mtu mzima kuliko wa kiume na huenda hio ndio ilifanya yeye kuwa na uwezo mkubwa kuliko mwenzake , kwani alikuwa kwenye levo ya Nafsi na mwanaume alikuwa mwishoni mwa levo ya Mzunguko kamili.

Kuna muda Roma alijiuliza Hongmeng ni majini kama majini au ni watu wanaoishi miliki za kijini maana miili yao haikuwa na utofauti na ya binadamu wa kawaida , jambo moja tu la kimaajabu ambalo lilimvutia ni namna ambavyo waliweza kutumia sura za watu ili wasitambulike, ijapokuwa uwezo huo hata Yamata walikuwa nao , lakini kwa jinsi walivyoonekana pale mgahawani walionekana kuwa na uzoefu mkubwa.

“Wewe ni Roma Ramoni?”Aliuliza yule mwanaume.

“Nadhani mpaka kuja nyumbani kwangu mshajua mimi ni nani , kuna haja gani ya kuthitisha?”

“Acha jeuri na jibu maswali yetu kama hutaki kuingia kwenye matatizo na sisi , tunataka kujua kuhusu Monk Tianyi alieuliwa na Yan Buwen”

“Monk Tianyi ndio nani?, sijawapata bado”

“Acha kujifanyisha humjui , tumepata taarifa wewe ndio umemuua Yan Buwen hivyo hutokosa kumfahamu Monk Tianyi”

“Kama ni hivyo kwanini msigemuuliza Omari na kja kwangu”Aliongea Roma, alishajua watu hao ni kutoka Hongmeng kutokana na medali zao za dhahabu walizoning’iniza kiunonni, zilikuwa zikifanana kwa kiasi kikubwa na ile aliochukua kwa monk mweusi aliemteka mke wake.

“Omari tushaongea nae na ndio alietuambia umemuua Yan Buwen kwa kumshushia Radi , je ni kweli unao uwezo wa kudhibiti Radi?”Aliuliza yule mwanaume huku wote wakionyesha shauku kwenye macho yao.

“Kwahio mmeshindwa kumuamini Omari ndio maana mkaja kunitafuta?”

“Tunataka kujua , sio jambo jepesi kwa binadamu wa kawaida kuweza kudhibiti radi kwa kutumia nishati ya mbingu na Ardhi na kama kweli ulikuwa na huo uwezo , kwanini ukamuacha Monk Tianyi akafariki kwa mikono ya Yan Buwen bila kumsadia”

“Kwahio hio mpo hapa kwa ajili ya kulalamika kwasababu Yan Buwen kamuua Monk ambaye alifanya maaamuzi ya kijinga kwa kujiona anao uwezo mkubwa kuliko wa Yan Buwen , mnachoongea ni upumbavu kwanza kwanini niwasaidie”Aliongea Roma.

“Kwahio unatuona sisi ni wapumbavu sio, nadhani kufanikisha kwako kuzijua tamaduni zetu kuna kufanya ujione uko juu sana”

“Kwahio mnasemaje sasa?”Aliongea Roma huku akianza kukosa uvumilivu na yule mwanaume alimzuia yule mwanamke asiendelee kuongea.

“Mr Roma nadhani Monk ndio mwenye makosa kwa kushindwa kukadiria uwezo wake na wa Yan Buwen , Monk Tianyi alikuwa mjumbe ambaye alitumwa kwenye ulimwengu wa kawaida kwa ajili ya kumuwinda Yan Buwen kwa kipindi cha mwezi mzima na juzi ndio tuliweza kugundua taa ya nafsi yake imezima kama ishara ya kifo chake , hivyo tumeagizwa kuja kufuatilia Dhana zake na tunaamini wewe umezichukua hivyo tunazihitaji”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu kwa uchungu , Rufi alimweleza katika miliki za kijini ukoo wa Hongmeng licha ya kuwa na nguvu ndani ya taifa la China lakini walikuwa ndio wanaongoza kwa umasikini wa Dhana na baadhi ya dawa za kuwasaidia katika kuvuna nishati za mbingu na Ardhi na hili linajidhihirisha, wamekuja mpaka Tanzania kwa ajili tu ya kutafuta dhana zao basi walionyesha kuwa na uhaba.

“Nadhani hata hilo swali mlipaswa kumuuliza Omari pia, kwanini mnataka kunisumbua?”

“Acha kujiona kijogoo , tunahitaji Dhana zetu, wewe ni mrithi wa Pluto na unao uwezo wa kutumia kanuni za anga hivyo kuna uwezekano ukawa umezificha kwenye parallel space na Omari ameshindwa kugundua”

“Kwahio mnanihisi mimi mwizi si ndio?”

“Tuna kila sababu ya kukuona wewe ni mwizi labda kama utarudisha Dhana zote na tukuache na amani,usije ukajifanya mjanja na kuona hatuwezi kukushughulikia”

“Okey! Yan Buwen aliharibu Dhana zote za Monk kwa kutumia Ant -matter hivyo sijachukua Dhana zenu, nadhani hilo jibu linawatosha”

“Sababu unayotueleza haina mashiko yoyote , zile ni dhana ambazo zimejaa uungu ndani yake na sio ngumu kuyeyuka”

“Kama hamuwezi kuniamini siwezi kuwaamisnisha , jibu langu ndio hilo”

“Inaonekana unaona hatuwezi kukuadabisha sio, nikutahadharishe tu tunatokea Hongmeng na ukishindana na sisi unashindana na jamii yetu yote.”Aliongea yule mwanamke , alionekana kuwa kiburi na aliamini Roma hawezi kuchukua hatua kwasababu wanatokea Hongmeng.

“Kwahio mnanitishia?”Aliongea Roma na kumfanya yule mwanamke kuchomoa upanga wake ambao haukuwa wa kawaida kutokana na Aura yake lakini yule mwenzake alimzuia.

“Senior Dong hatuwezi kupambana nae , anao uwezo mkubwa kuliko wa kwetu ndio maana hatuwezi kuona yupo hatua ipi kwenye mwili wake , tunapaswa kwenda kutoa taarifa kwa Master wafanye maamuzi”Alimtuliza.

“Mr Roma unapaswa kuelewa , bado hatujamalizana na wewe , tunaondoka na kwenda kutoa taarifa na Master mwenyewe atatoa maamuzi , usijione una nguvu huwezi kushindana na wazee wetu wakiamua kukuadabisha”Waliongea na kisha wakajiandaa kuondoka , lakini Roma aliwazuia.

“Sio kwa haraka hizo, mimi bado sitaki muondoke maana hata nyumbani sijawakaribisha kuweka hata baraka kwa kikombe cha chai?”

“Huna sifa ya kuweza kutukaribisha sisi , labda raisi wa taifa hili anaweza angalau kutushawishi”

“Oh! ,, Lakini nikiwaachia mkiondoka na sintofahamu huoni kwamba mnaweza kwenda na kuja na mtu hatari zaidi na ikawa shida kwangu?”

“Hilo lisikupe shida kama haujaiba Dhana zetu Wazee wetu hawawezi kuchukua maamuzi yasio ya busara , unatakiwa kuelewa zile Dhana hazikuwa za Monk bali aliazimishwa na ukoo”

“Okey , basi naomba niwaulize swali, Je kila mmoja ndani ya Hongmeng ana Taa ya uhai wa nafsi yake(Lantern of Soul)”

“Kwanini unatuuliza hivyo?”.

“Kwasababu kuna rafiki yangu mmoja ambaye nilikutana nae , alionekana kubeba medali kama hizo mlizoning’iniza na amesema ametokea Hongmeng , Oh.! tena anamiliki Kisu cha damu ya Joka”Aliongea Roma akimaanisha Blood Dragon Dagger , alikuwa akimzungumzia yule Monk mweusi aliemteka Edna na kumuua.

“Unamaanisha Msaliti Abeo unamfahamu?”Aliongea yule mwanamke huku akionyesha mshangao.

“Kumbe anaitwa Abeo , ndio namfahamu alikuja kwangu akihitaji niwe rafiki yake kwanini mnamuita msaliti”Aliongea Roma na kuwafanya wote kuangaliana.

“Haiwezekani , Abeo hawezi kufanya urafiki na mtu yoyote , ni msaliti kwa Hongmeng kwani aliasi kwa kuhamia kwenye miliki nyingine kutokana na tamaa zake , binadamu wote hamna shukrani , tulimkaribisha na kumuacha ajifunze tamaduni zetu lakini mwisho wa siku akatugeuka kwasababu ya tamaa ya utajiri na nguvu”

“Alikuja kwangu kwasababu nina Vidonge nilivyopatiwa na Master wangu , vinavyonisaidia kwenye kuvuna nishati za mingu na ardhi , hivyo alitaka nibadilishane nae kwa kunipa kisu cha damu ya Dragoni”

“Unamaanisha unavyo Vidonge ambavyo Abeo alikuwa tayari kukupatia dhana yake?”

“Unafikiri nadanganya, vidonge nilibyokuwa navyo vina uwezo wa hali ya juu sana , nadhani hata nyie wenyewe mnaona nipo na miaka ishirini na kitu lakini nimefikia levo za juu”Aliongea Roma , alikuwa akidanganya ili kuwaingiza kwenye mtego anao waandalia.

Dong anaongea ukweli , unaona sisi tuna miaka sabini mpaka saa lakini tupo kwenye levo ya nafsi , nadhani tunapaswa kuhakikisha kupata hivyo vidonge kutoka kwake hata kama ni kumuua”Waliongeleshana kwa kutumia hisia.

Roma hakuwaelewa walichokuwa wakiongea lakini alijua wanawasiliana kwani alihisi msisimko wa hali ya juu.

Naunga mkono hoja, hatuwezi kumruhusu binadamu mweusi kumiliki kitu cha thamani , tukivipata naamini ndani ya muda mfupi tutakuwa levo za juu na hakuna yoyote anaeweza kutuchukulia wa kawaida

Kwahio tunafanyaje?”

Wewe niachie mimi , huyu ni binadamu anawezaje kutushinda viumbe kama sisi ambao tunaweza kufanya chochote”

“Mr Roma vidonge unavyozungumzia ni vya aina gani unaweza kuvielezea?”

“Rangi yake ni njano kama vimeunguzwa na moto mkali ukubwa wake ni kama gororoli”

“Huateng nadhani anazungumzia Poya, vidonge namba moja wanavyomiliki wale wazee wa Kekexil hakika tukivipata lazima tuvunje levo za juu”Waliongeleshana tena kwa njia ya hisia.

“Mr Roma nadhani unazungumzia vidonge maarufu daraja la kwanza vya Poya?”

“Oh! …. Ndio jina lake hilo , Master alinipatia vya kutosha lakini hakuwahi kunielezea jina lake na niliweza kupanda levo bila hata ya usimamizi wake”Aliongea na kuwafanya waangaliane kwa kupeana ishara ya kuridhika.

Huateng kwahio tunafanyaje?”

“Senior Dong nadhani atuonyeshe vilipo, itakuwa rahisi kuvichukua”


Upo sahihi” Waliendelea kuwasiliana na kumfanya Roma azidi kuona mtego wake unafanya kazi.

“Mr Roma unaweza kutuonyesha japo hata kidonge kimoja ili tuweze kuvihakiki”

“Nipo tayari, ninaweza kuwapatia kila mmoja vitatu vitatu , kila kidonge kimoja kitakuwezesha kupanda levo moja”

Roma aliona tayari ndoano yake ishakamata samaki , kuhusu vinavyofanana hakuotea ni kweli alikuwa akijua kuhusu Vidonge na aliweza kujifunza uwepo wake mara baada ya kwenda China katika ngome za Tang kusoma nyaraka za mafunzo ya kijini na utamaduni wa kichina kwa ujumla.

“Tutashukuru sana Mr Roma kama utatupatia , hakika hatuwezi kusahau ukarimu wako?”Aliongea yule mwanamke ambaye mara ya mwisho alionyesha jeuri , lakini kwasababu ya kuwa na tamaa ya kutaka kupanda levo ya juu zaidi , alionyesha kuhiraji kwa hali na mali vidonge vinavyozungumziwa.

Roma katika mazungumzo hayo alikuwa ashaweza kupata mambo mawili , jambo la kwanza alijua kabisa kuhusu Taa ya uhai wa Nafsi na kama wameweza kujua mahali ambapo Monk amekufa ni hapa Tanzania basi ni hakika walitumia hizo Lantern kufatilia.

Alijiambia kama atawauwa wakiwa ndani ya mipaka ya Tanzania basi Hongmeng watafahamu , hivyo mpango wake wa kwanza ni kuwatoa Tanzania na kuwapeleka hata Kenya na kisha angewaua na kuchukua Dhana zao pamoja na vidonge ambavyo ameviona wameficha kifuani na kisha angempelekea Rufi na kuvithaminisha kama vingekuwa na uwezo na usalama na angewapa wanawake wake wameze ili iwarahisishie kupanda levo kwa haraka.

Hayo ndio aliojifunza katika nyaraka alizosoma China, aliamini kama angepata vidonge basi ingekuwa rahisi kwake kurahisisha mafunzo kwa warembo wake na mwisho wa siku wangeweza kufikia levo ya nafsi kwa haraka na angepata amani ya kupata mtoto.

Shida moja ni kwamba hakujua ni kwa namna gani angeweza kupata vidonge , hivyo mpango ulikuwa ni mmoja tu kila atakapokatama kiumbe chochote kutoka Hongmeng angeua na kisha kuiba Dhana pamoja na vidonge.

“Kama mnahitaji kuviona na niwapatie basi mnapaswa kunifuata, kutokana na ubora wake nilivificha mbali na hapa ili watu wenye tamaa wasije kuviiba”

“Tupo tayari kukusindikiza ili mradi utimize ahadi yako ya kutupatia vitatu vitatu”

“Kama mpo tayari nifuateni”Aliongea Roma na kuwafanya waangaliane

“Huateng , tunachukua vyote halafu tunamuua , tukirudi kwenye miliki lazima watunyenyekee”

“Senior , upo sahihi , safari yetu ya dunianni imeleta baraka
”Waliongeleshana tena na kisha walimfuata Roma.

Roma hakujua hata uelekeo , yeye alitambaa kwa spidi kubwa huku akitafua eneo zuri ambalo lingefaa kuwamaliza.

Nani kasema majini hayana tamaa licha ya kuwa na uwezo wa juu wa kufunuliwa mambo mengi, Tamaa ndio udhaifu mkubwa ambao sio binadamu aliewekewa bali kwa kila kiumbe chenye utashi wa akili , asilimia kubwa ya Dhambi zote zinazofanyika chanzo chake ni tamaa na watu hutofautiana viwango vya tamaa kutokana na mazingira , udhaifu wa tamaa unaweza ukalala ndani ya mtu lakini siku atakayopatwa na shida na njia ya haraka ya kutatua shida ikajitokeza basi tamaa huamka na kuzivaa akili , wachache walioweza kuzishinda tamaa ndio wameweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Roma alikuwa akiwaza hivyo kwenye akili yake huku akitafuta mahali , pazuri na baada ya kusafiri umbali mrefu kwa muda mfupi aliweza kuhisi wapo nje ya Tanzania na kwa haraka haraka akili yake ilimwambia yupo Kenya.

Hili eneo ndio sahihi , kuna mifupa mingi hili eneo yenye roho za chuki zilizolala , nadhani waliokufa hapa wengi sio kwa hiari yao”Aliwaza Roma mara baada ya kutua kwenye moja wapo ya shamba kubwa ndani ya Kenya.

Mchawi hahitaji macho kujua uwepo wa kaburi ,anahitaji uwezo wake wa kichawi kutambua roho za binadamu zilizolala.

Kwa mfano kundi la Takamagahara nido kundi la kichawi kutoka Japani ambalo hutumia roho za wafu waliokufa wakiwa na chuki na hukusanya ile mifupa na kuigeuza kuwa pepo na ndio hutengeneza siraha zao za kichawi.

Katika ulimwengu wa Roho binadamu akifa akiwa na chuki au akifa kifo cha kulazimishwa ni ‘Asset’ kwa wachawi kwasababu roho yake hupatikana kwa urahisi kupitia mifupa yake , ndio maana siku zote waganga wa kienyeji na wachawi hutumia makaburi ya wafu waliokufa kwa chuki katika kazi zao za ulozi au tiba.

“Mr Roma kweli umechagua eneo sahihi , hii sehemu inaonyesha kuwa na roho za binadamu waliokufa kwa kulazimishwa na naona nyingi zimeshikiliwa na mifupa naaminni hili eneo limetengenezwa kwa kazi maalumu”.

Ilikuwa kama Roma alivyofikiria , hili eneo lilionekana kutegenezwa kwani hakuna makaburi kwa juu bali kuna vifusi pekee vyya makaburi na Roma aliweza kuona ndani ya kaburi moja kuna zaidi ya miili ya watu wawili.

“Mr Roma nadhani unapaswa kutonyesha sasa na kutupatia ili kutimiza ahadi yako”.

“Sikuwa na mpango wa kuwaonyesha vidonge, kama mlivyosema hili shamba limetengenezwa kwa ajili ya ibada za kishetani basi sina budi kuongezea na roho zenu hapa?”Aliongea Roma.

“Kwahio ulikuwa ukitudanganya?”

“Pigia mstari , unafikiri mimi ni mjinga niweze kuweka ahadi na watu kama nyie ambao mnaongozwa na tamaa , leo ndio mwisho wenu, kosa kubwa ambalo mmefanya ni kujaribu kunitishia lakini pili kudharau juhudi zangu , mheshindwa kudhibiti raia wenu wanakumbwa na ukichaa halafu bado mnajiita ndio mnaolinda misingi ya Taifa la China , niliwasaidia kuwaondolea adui yenu lakini hamuonyeshi Shukrani , labda vifo vyenu vinaweza kuwa zawadi kwangu”Aliongea Roma na kabla hawajajua cha kufanya Roma alimsogelea Huateng kwa kasi na kuinua mkono wake huku akiita nguvu ya kimaandiko kuielekezea mkononi na kuisha akapiga kibao hewani akiwa amemlenga , Huateng alionekana mzoefu kwani aliweza kukwepa haraka na laiti kingempata kutokaa na levo yake ingekuwa kifo chake.

Na palepale bila ya kuchelewa alitoa upanga wake kwenye Ala na Aura ya upanga wake ilisababisha baadhi ya Roho zilizolala kwenye mifupa kuanza kuamka na Roma aliona hio ni hatari kwani Roho hizo zikitoka kwenye mifupa yake zinageuka kuwa mapepo na kwenda kuvamia watu wenye nguvu chache za ki ulinzi kiroho.

Alichokifanya ni kuachia nguvu ya kijini kulifunika eneo lote ili isitokee Roho hata moja kutoka kwenye mifupa yake.

Upanga wa Huateng uling’aa na kutoa mwanga uliombatana na ukungu kama moshi na mng’ao mithiri ya mwezi.

“Go Xuanshui” Aliongea maneno ya kichina ambayo Roma hakuyaelewa lakini alijua yanavyotamkwa na palepale upanga ulitoa mng’ao zaidi na kumuumiza macho kiasi cha kuyafumba na ile anafumbua aliweza kuona ukuta kama wa barafu mbele yake umejitengeneza kichawi.

Roma alishangaa uwezo huo wa kimajabu uliofanikishwa na siraha ya upanga tu , lakini hata hivyo kwake ukuta huo ulikuwa mwepesi sana kuubomoa. Haukuwa ukuta kama ukuta halisi wa barfu bali ni wa kichawi.

Huateng baada ya kutengeneza ukuta ule , alipata muda na palepale aliongea maneno mengine ya kichina yasioeleweka na palepale kwenye mikono yake iliweza kuonekana Gukini(Guqin), ni aina flanii hivi za gitaa au Zeze ambazo zilitumika sana kipindi cha enzi za kale katika tamaduni za China na mara nyingi huwa na nyuzi saba ambazo hutoa sauti zinazotofautiana, Huateng hakuishia hapo alitoa pia unyonya wa ndege maarufu wa kichawi Phoenix.

Roma alishangaa lakini aliweza kugundua kitu kimoja cha kufurahisha , alishawahi kusikia kuhusu lugha maalumu ambayo majini na watu wanaoabudu vitu vyenye asili ya ushetani hutumia lugha kuingia kwenye mzingo wa Sumeru , kilichomfurahisha Roma ni kwamba hakujua kama unaweza kuiiita Sumeru ukiwa ndani ya bara la Afrika , alijua iliwezekana tu kwa bara la Asia.

“Unapata wapi uthubutu wa kujifanya mjanja mbele yetu”Aliongea Huateng na kisha akajikalisha kwenye hewa kwa kukunja miguu kama vile amekaa chini kwenye mkeka au zulia na kisha akaweka lile gitaa huku akianza kurekebisha zile nyuzi akionyesha anataka kuanza kupiga mziki.

Roma alishindwa kuelewa ni nini anataka kufanya , kwani hakuwahi kufikiria uwepo wa Dhana ya aina hio lakini aliishia kujawa na msisimko wa kutaka kufahamu.

“Tii , Taaa, Tuu….!!” Huateng alidokoa nyuzi moja moja kwa namna ya kupiga akitumia ule unyoya na Roma ndipo alipoweza kujua nini kinatokea.
Ni furahaaaa
 
SEHEMU YA 585.

Roma mara baada ya taarifa hio kugonga masikio yake alianza kujiuliza maswali , alijiuliza imekuwaje alama zake zikawepo na ni nani ambaye amefanya mauaji hayo kwa staili inayofanana kama ya kwake, alijua kabisa tukio hilo limetengenezwa kumchafua lakini alishindwa kujua muhusika mkuu ni nani.

Alijiambia kama ni kupindi cha nyuma basi moja kwa moja angejua aliefanya hivyo ni Yan Buwen lakini tayari amekwisha kumuua hivyo hakuweza kukisia ni nani kwa wakati mmoja zaidi ya kuwa na hisia tu za kushuku baadhi ya watu.

Damasi na Edna waliweza kusikia taarifa hio pia na alijikuta akiwa na wasiwasi mkubwa huku akiwa na wasiwasi juu ya Roma, ijapokuwa alijua Roma alikuwa ni mwepesi kuua mtu lakini moyo wake ulimwambia kabisa sio yeye , lakini kwa maelezo aliopatiwa alikosa ushihidi wa kumkingia kifua..
xhukhran mkuu mzigo tumeuona
 
SEHEMU YA 483.

Gukini ilionekana kuwa na muunganiko wa moja kwa moja na nguvu za kijini za Huateng , alikuwa kila akidokoa uzi na ule unyoya mara tatu kulitokea mshale wa kichawi na ulinyooka mahali sawa na Roma aliposimama na mbaya zaidi uliweza kupita kwenye ule ukuta wa barafu bila ya kizuizi.

Roma alifurahishwa mno na hio Dhana alijiambia mwenyewe kwa mfano angempa Edna aimiliki hiyo haitampa shida hata ya kupambana kazi yake ni kucharaza gitaa tu na maadui wanadondoka.

Roma alijiambia Yes, Dhana zote hizo mpaka muda huo ni za kwake na anachotakiwa kufanya ni kuwaua na kuchukua, lakini kabla ya yote lazima aangalie kwanza zinavyotumika.

Roma hakujisumbua hata kukwepa ile mishale , kwani uwezo wake ulikuwa mdogo sana kumdhuru ,hivyo aliita nguvu ya Kimaandiko na kutengeneza ngao na mishale ilipogusana ngao tu ulipotea bila ya kumfikia , ukweli hata kama angeruhusu umchome isingemletea pia shida maana anao uwezo wa kujiponyesha.

Huateng alicharaza gitaa kama mwehu , alianza taratibu taratibu na kuanza kukoleza na alionekana mzoefu mno kwani alitengeneza mziki wa solo wa aina yake , lakini sauti yake ilikuwa ikiamsha siraha za kichawi na kumshambulia Roma , kila alipojitahidi hakuna kilichoonekana kuleta madhara kwa Roma kwani mishale yake ilipotea.

“Inawezekanaje Gukini na unyoya wa Phoenix ushindwe kukudhuru?”Aliongea Dong kwa mshangao kwani hakuamini Roma angekuwa na uwezo mkubwa wa kujikinga.

Dong yule mwanamke palepale alianza kuchezesha elemeti za anga na mkono wake ukatengeneza mpira wa barafu na kuurusha kwa nguvu zote kumlenga Roma.

Roma nae alikusanya nguvu zote kwenye kiganja na lile barafu kabla halijamfikia aliachia wimbi na vikakutana katikati kwenye ule ukuta na ukaporomoka wote.

Wakati Roma anapambana na Dong , Huateng aliendelea kucharaza Zeze lake kama kichaa lakini hata hivyo kila siraha iliomfikia Roma ilikuwa kwake kama upepo kwani haikumdhuru.

Sio kwasababu Dhana zao zilikuwa na uwezo mdogo , lakini ukweli ni kwmaba wao ndio ambao walikuwa na uwezo mdogo wa kuziendesha kwa kiwango chake cha mwisho, ni sawa na kusema kama Roma akaamua kuicharaza Gukini ya Huateng basi angeweza kuleta madhara makubwa kwasababu levo yake ilikuwa kubwa.

“Kimbia”Aliongea Dong akimwamrisha Huategn kukimbia , mpaka hapo alishaona wakiendelea kushindana na Roma wangeishia kupoteza maisha.

Huateng aliona atii kauli ya mwenzake na palepale alijikusanya na kuanza kukimbia kuelekea katikati ya nchi ya Kenya huku Dong akijaribu kupambana na Roma.

Roma aliona huo ni ujinga palepale alianza kufanya kitu cha ajabu ambacho ghafla tu kilitengeneza moto wa njano kama dhahabu kwenye mikono yake na ukawa kama vinyoka nyoka na aliviachia na kumfuata Huateng kwa kasi na vilionyesha kuwa na spidi kuliko ya kwake.

Dong alionyesha mshangao mara baada ya kushuhudia uwezo ule , ulikuwa ni uwezo wa juu kabisa ambao alijua mtu mwenye uwezo huo lazima afikie levo ya kuipita Dhiki na mpaka hapo alijua alikuwa akipambana na mtu wa levo ya juu kuliko yeye , ilikuwa ni kama anapambana na wazee wa miliki ya jamii yake.

Vile vinyoka vyoka vya moto vilianza kumzingira Huateng kwa spidi kali na kutengeneza kama dura huku yeye akiwa katikati , bado hakuwa ameachia zeze lake na alijitahidi kuzuia joto kwa kuendelea kulicharaza kisawa sawa na ule unyoya lakini moto wake ulikuwa mkali kama wa kuyeyushia chuma.

“Sikia nadhani muacha kukimbia kwani mtanifanya niharibu hizo Dhana wakati nazihiraji”Aliongea Roma huku akicheka.

“Mr Roma naomba utusamehe”Aliongea huku akianza kutetemeka ule ujasiri wa kupambana na mtu mwenye uwezo wa kudhibiti moto wa rangi ya njano aliogopa.

Ukweli Roma muda huo alitamani kutumia moto wa rangi nyeupe , lakini alishindwa kuelewa kilichofanyika kwani wakati anapambana na Yan Buwen mwili wake ulikuwa ukitumika tu na mtu anaeishi ndani yake ambaye ana mpango wa kutawala mwili wake.

Hivyo kama ni kujifunza ni machache aliopatia kama kudhibiti moto wa joto la hali ya juu.

Roma mara bada ya kuona ashawadhibiti na hakuna namna ya kukimbia alitengeneza upanga wa moto kwa kuchezesha viganja vya mikono yake huku akiongea maneno yasioeleweka na palepale mapanga mawili yalifyatuka na kuwasogelea kwa kasi na Huateng ndio aliekuwa wa kwanza kunaswa eneo la tumboni na akafuatia Dong.

Roma alijiambia ndio kazi nzuri , aliwasogela huku akiwangaalia kwa tabasasamu la dhihaka.

“Unaweza kutuambia kwanini unataka kutuua , hata kama tulikuonyeshea kiburi lakini hatukua na nia mbaya na wewe”Aliongea yule mwanamke Dong huku akitia huruma.

“Jibu ni rahisi kwanza kabisa mmedharau ukarimu wangu , pili mlianza kunitishia huku mkiamini siwezi kuwafanya chochote kwasababu mnatokea Hongmeng , ngoja niwaambie ukishanikasirisha mimi sina huruma na kuua mimi ni jambo jepesi kuliko kusamehe”

“Huoni kwamba unajiingiza kwenye matatizo , kama wazee watafahamu umehusika na vitu vyote lazima watalipiza kisasi na hutowaweza kwani wapo kwenye levo ya anga kati ya mbingu na Ardhi, nadhani shida yako ni Dhana zetu pamoja na vidonge lakini nakuhakikisha kinachokusubiria ni kikubwa zaidi ya vifo vyetu”’

“Hata kama ningewaacha watu kama nyie mkaondoka , lazima kuna wengine wangekuja kunichokoza tu na kutaka ugomvi na mimi , nitakuwa mjinga kama sitochukua hatua mapema”

“Nakuambia utajutia kitendo chako cha leo”Aliongea Dong.

“Asante kwa kujali , lakini usiwe na wasiwasi nitawatuma wenzako wengine ambao watajaribu kunichokoza ili usiwe mpweke sana”Aliongea Roma na palepale ule upanga uliomchoma eneo la tumboni ulianza kuongezeka ukubwa na alianza kuyeyuka palepale taratibu taratibu na kikawa kifo chake , hivyo hivyo kwa Huateng akapoteza maisha.

Roma alianza kuchukua Dhana zao , alichukua Gitaa na unyoya wake , Upanga ambao uliitwa Xuanshui na kisha aliweza pia kupata pete pamoja na chupa ya vidonge vinavyofanana kabisa na P2 na Roma alipoisoma ile pete aliweza kugundua sasa hio ndio aliotumia Huateng kufungua Sumeru, ilikuwa ni Sumeru Ring .

Roma mara baada ya kuona kazi yake imemalizika hakutaka kubakia hapo tena , hata hivyo halikuwa eneo zuri kutokana na roho za wafu , aliondoka na kurudi Tanzania , alijua fika kwamba muda si mrefu Hongmeng watafatilia vifo vyao , aliwaua Kenya ili wasije wakafahamu kwa haraka kama amehusika , lakini alijua muda si mrefu wataagiza mwingine kuja kwake kwa ajili ya mahojiano na alijisemea akija mwingine anaua tu na kuwaibia.

Mpango wake haukuwa kuwaibia tu , alipanga pia akipata Dhana sahihi basi angezamia ujinini kwenda kuiba vizuri.

Siku iliofuata asubuhi wote waliamkia Chapati za maji ambazo zilipikwa na Mama yake Roma.

“Lanlan hio chapati ya mwisho ni ya kwangu”Aliongea Roma akimwangalia Lanlan ambaye alikuwa kwenye mavazi ya shule na alishangaa siku hio kachelewa.

“Baba hashindani na mtoto kula”Aliongea Lanlan huku Roma akitaka kupeleka mkono kuchukua chapati , lakini Edna alimpiga kwenye kiganja cha mkono.

“Usishindane na mtoto kula , anahitaji kula ashibe ili akue , wewe hata usishibe sio kwamba utakufa”Aliongea Edna

“Haha… Shemeji inabidi ufanye juhudi kwa staili hii Lanlan anaweza kukufunika kabisa”Aliongea Sophia na kumfanya Roma amwangalie kwanza hajazoea Sophia kumuita Shemeji.

“Acha kunitania la sivyo siwezi kukusindikiza kwenda studio kama ulivyoomba”.Aliongea na kumfanya Edna awaangalie na akaanza kumnawisha mikono Lanlan .

“Halafu mbona kachelewa leo kwenda shule?”

“Nitaenda nae leo nataka nikaongee na mwalimu wake nijue maendeleo yake kwa ujumla anavyochangamana na wengine”.

“Sister unahofia kwasababu sio mtoto wa kawaida anaweza kushindwa kuchangamana vizuri?”

“Hilo sihofii kwani Lanlan ni msikivu , ila kuna tahadhari napasawa kuchukuwa”

“Wife usiwe na wasiwasi , haina haja ya kuchukua tahadhari , Lanlan uwezo wake inaonyesha ni kwa ajili ya kujilinda sidhani ni tatizo”.

“Kwahio unanishauri nisiwaambie kuhusu uwezo wake?”

“Haina haja, unapaswa kumuamini kama unavyoniamini, Lanlan ni mtoto wangu na hawezi kuwa wa kawaida”Aliongea Roma na kumfanya Edna kupata ahueni, ukweli kila muda ambao Lanlan anakuwa shuleni anakuwa na wasiwasi mno.

Baada ya Edna kuondoka na Lanlan na Roma na yeye aliondoka akiwa ameambatana na Sophia , mpango wake amfikishe Studio na baada ya hapo amtafute Rufi ampe maelezo kuhusu Dhana na Vidonge alivyoweza kupata.

Roma alikuwa na siku nyingi hajaenda ofisini lakini hata hakujali, siku hio alikuwa na ratiba nyingi alipanga kumtembelea Rose kujua maendeleo yake na baada ya hapo amtafute Amina.

Baada ya kumfikisha Sophia Studio moja kwa moja alianza safari ya kurudi Mikocheni na ilimchukua dakika chache tu aliweza kufika.

Wakati Roma anataka kuingia upande wa lift , aliweza kumuona Rufi akiingia upande wa Supermakert , alimfuata nyuma nyuma lakini mara baada ya kufika katikati akiwa hjamuona Roma , ghafla alisimama huku akionyesha wasiwasi.

Roma aliangalia mbele kwa mshangao na kuona nini tatizo na aliweza kumshuhudia msichana wa kichina alievalia begi akiwa ameshika trey , alikuwa rika la Rufi ki umri.

Kabla yule mwanadada hajageuka nyuma Rufi aligeuza alikotoka na kuanza kukimbia, alimuona Roma mbele yake lakini hakuongea nae na kumpita, kitendo kile kilimshangaza Roma na kumfanya amchunguze yule msichana na alugundua alikuwa binadamu wa kawaida lakini mwenye mafunzo ya kijini tena akiwa levo ya nusu mzunguko.

Alikuwa mrembo haswa na rangi yake nyeupe pamoja na nywele ndefu , ambacho Roma hajapenda ni shepu tu basi lakini sura ilivutia, alikuwa amevalia Haedphone masikioni.

Roma hakuona haja ya kuendelea kumwangalia na aligeuza kumfuata Rufi.Baada ya kupandisha juu kwa lift, mlango wa nje ulionyesha kufunguliwa hivyo aliingia bila ya hodi na kumkuta Rufi amekaa kwenye Sofa.

“Inaonyesha umenifuata , kuna unachotaka nikusaidie”Aliongea Rufi huku akionyesha kuwa siriasi na Roma hakumzoea hivyo ila hakutaka kuleta mbwembwe maana yupo hapo kwa ajili ya kuongea nae vitu vya msingi.

Alimtolea vile vitu vyote alivyowachukulia wale watu wa Hongmeng na kuweka mbele ya Rufi.

“Umevitoa wapi hivi?”Aliuliza Rufi huku akionyesha mshangao. Na Roma alimwelezea kila kitu.

“Umefanya vizuri kuwaua , wanajikuta wana dharau sana binadamu wa kawaida , ningekuwa na uwezo ningewaangamiza wote , Hongmeng sijuo Kekexil wote ni mashetani na hawajawahi kuwa na wema wowote kwa binadamu wanachowaza ni faida tu”Aliongea Rufi huku akionyesha chuki ya wazi wazi.

“Unapaswa kuiona dunia kwa uzuri wake wa nje na sio chuki ndani yake , ukiishi hivyo utaishia kuwa mwenye maumivu”

“Kwa upande wako sawa , kwasababu nao uwezo wa kuamua matokeo ya maisha yako lakini kwangu mimi ni tofauti kabisa , sijawahi kuwa na tumaini maisha yangu yote zaidi ya chuki na maumivu yalioujaza mwili wangu ,siku nitakayopata nafasi nitawarudishia mara mia moja”Aliongea kwa hasira mno na kwa jinsi mudi yake ilivyo Roma alijua mwananemke ambaye Rufi alikuwa akimkimbia huenda anamfahamu, ila hakutaka kuuliza kwa muda huo kwanza , alichokuwa akipanga baada ya hapo ni kumfatilia yule mwanamke na kumjua vizuri , Rufi ashakuwa jukumu lake la kumlinda hivyo alipaswa kuhakikisha anakuwa salama na hivyo kwa kipindi hicho Hongmeng walionyesha kutokuwa na wasiwasi kuvuka bara la Asia , basi aliona kama sio leo au kesho basi keshokutwa wanaweza kunyaka uwepo wa Rufi Tanzania na kutaka kumrudisha.

“Naomba unisamehe kwa kuonyesha hasira zangu mbele yako”Aliongea huku akiwa anaangalia vile vitu kwa namna ya kuvikagua.

“Nafikiri sasa unapendeza zaidi , kuliko kipindi ulivyokuwa ukinitega”Aliongea Roma na kumfanya Rufi atingiche mabega huku akikosa ujasiri wa kumwangalia machoni .

“Hizi zote ni dhana ambazo zipo daraja la pili , nafikiri wamepewa kuja navyo kwa namna ya kuazimwa huo upanga licha ya kutengenezwa kwa chuma kutoka ncha ya Kaskazini lakini pia umezindikwa na nguvu ya barafu ya kichawi , huu unyoya siwezi kuelezea sana ni wa ndege wa Phoenix ukiunganisha na Gukini ni dhana yenye uwezo mkubwa sana kukaribia za daraja la juu kabisa , inaonyesha aliekuwa akitumia uwezo wake wa kuudhibiti ulikuwa mdogo, kuhusu hii pete inatumika kufungulia anga la Sumeru lakini sidhani kama inaweza kufanya kazi kubwa zaidi kutokana na malighafi yake”

“Unamaanisha kuna yenye uwezo zaidi ya hii?”

“Ndio na haitumiki kufungulia anga tu lakini pia inafungua milango mingi ya kiroho”

“Vipi kuhusu hivyo vidonge?”

“Hivi naweza kusema una bahati kubwa kuvipata ,ijapokuwa ni vidongea daraja la mwisho lakini vinauwezo wa kubusti mtu anaeanza mafunzo na kuingia mzunguko kamili kwa urahisi hata pia kuweza kufikia levo ya nafsi , kwa mtu mwenye levo ya juu havina msaada mkubwa , kwa makadirio uwezo wake ni asilimia hamsini tu”

“Hamsini mbona ndogo sana”Aliongea Roma huku akionyesha hajapenda

“Unachukulia kawaida asilimia hamsini, Vidonge katika miliki za kijini ni muhimu zaidi kuliko hata Dhana , kwasababu mimea ambayo hutumika kutengenezea imeshapotea kwenye mazingira yao na mara nyingi huja huku duniani kuitafuta”

Roma aliona ni kweli , kama vidonge hivyo vilikuwa vikisaidia watu kuingia kwenye levo ya Nafsi , basi huko kwenye miliki watakuwa wengi ambao wapo kwenye levo hio na sio vya kudharauliwa hata kidogo.

“Vina athari yoyote?”

“Havina athari kwa ambaye amefikia levo ya nusu mzunguko na kutaka kuingia mzunguko kamili au levo ya Nafsi”Aliongea na kumfanya Roma kuona basi mtu sahihi anaepaswa kumeza ni Magdalena , maana mara ya mwisho wakati anapambana na Yan Buwen alikuwa ashaingia mzunguko kamili.

Wakati Roma anataka kuuliza swali lingine , simu yake ilianza kuita na alipoitoa kuangalia jina la anaepiga alishangaa kuona namba ni mpya , lakini pia haikuwa ya kitanzania kwa uzoefu wake wa kuishi mataifa mengi aliweza kujua ni kutoka Korea Kusini alipokea.

“Hello!”

“Hello”Sauti ilijibu ya kike lakini ilikuwa dhaifu mno.

“Yezi!”Aliita Roma mara baada ya kuifahamu lakini baada ya kuongea hivyo upande wa pili kulianza kusikika vilio na kumfanya Roma kuwa na wasiwasi , ni kweli hajawasiliana na Yezi tokea aondoke , lakini alishangaa amempigia na kuanza kulia.
Oooky
 
Edna alishangaa , ijapokuwa hakuwahi kuwa na ukaribu na Kizwe lakini ashawahi kumuona ana kwa ana , kubadilika kwake na kuwa kama kijana kulimshangaza mno na kuogopesha kwa wakati mmoja.

“The old Kizwe is dead . I have been reborn”Aliongea akimaanisha kwamba Kizwe wa zamani amekwisha kufa na yeye amezaliwa upya.

Edna alikuwa akitetemeka mno na kilichomjia akilini muda huo ni kukimbilia nje na Kizwe alimuacha apite huku akicheka , lakini ile anafikia mlangoni alizuiwa na Desmond.

“Ni wewe..?”Edna alijikuta akianza kuhofia na akili yake ilimwambia huenda kila kitu kimepangwa , kwanzia sherehe kufanyikia huku mbali lakini pia swala la Roma kushindana mbio za magari na yeye kumwagiwa Mvinyo.

“Vipi ,mbona unashangaa kuniona?”Aliongea Desmond huku akiwa ameweka tabasamu la kejeli na kumfanya Edna kurudi nyuma kwa wasiwasi.

“Desmond usije ukathubutu kunifanya chochote , Roma atarudi muda si mrefu na mtakuwa kwenye matatizo”Alitahadharisha Edna.

“Relax , tutamalizana na wewe kabla hata hajamaliza pambano”Aliongea huku akimsogelea karibu na Edna alianza kurudi nyuma nyuma.

“Mume mume wangu atawaua msithubutu kunigusa”Aliongea Edna

“Haha…So what , Tutakufa kwa mikono yake tu hata kama hatutokugusa , hivyo badala ya kufa bila sababu tutajitengenezea sababu”Aliongea Kizwe.

“Edna ,,, nimeisubiria hii siku kwa muda mrefu sana , usijali sana , Roma anahitaji angalau dakika kumi mpaka kuja kukupata , lakini kabla ya muda huo ngoja nikupatie kitu cha kipekee usiku wa leo”Aliongea

“Desmond huwezi kunifanyia hivi , huwezi kufanya hivi”Aliongea Edna na hakuwa na pakukimbilia kwani Desmond ashamshika tayari mkono huku akimsogezea sura yake karibu.

“Desmond hakikisha unafanya haraka nitaondoka baada ya kuifurahia show”Aliongea Kizwe bila aibu , ni kana kwamba Desmond hakuwa mtoto wake kabisa.

“Mama mpango wangu nataka nijipigie taratibu taratibu na muda ambao Roma anafika nashusha wazungu huku anaona”Aliongea huku akiweka tabasamu la kebehi.

“Hehe. kama huo ndio mpango wako basi sina budi kusubiri”Aliongea Kizwe lakini muda ule ule yule muhudumu ambaye alimchafua Edba aliingia.

“Madam , What are your orders?”Aliuliza kwa Kingeereza.

“Jeremy yupo wapi , bado hajafika tu?”Aliuliza kizwe.

“Mheshimiwa atafika hivi punde , tayari wanausalama washawasili”Alijibu na kumfanya Kizwe kuonyesha tabasamu la furaha , alijiambia anakwenda kumkomoa Jeremy kwa Desmond kumla dada yake.

Raisi Jeremy alikuwa nchini Tanzania kuhhudhuria mazishi ya kifo cha Raisi mstaafu wa Tanzania Kigombola , ilionekana walitumia nafasi ya uwepo wake nchini kukamilisha mpango wao.

Desmond alizidi kumkandamiza Edna kwenye ukuta na lile koti ambalo alipewa kuvaa na Roma lishadondoka chini na hivyo mabega yake kuwa wazi

“Desmond tafadhari nakuomba usifanye hivi , mimi ni ..”Edna alianza kushikwa na kigugumizi.

“Wewe ni nani , Sema..?”Aliongea kwa kingereza.

“My…”Edna alishindwa kuongea huku machozi yakimtoka mfululizo huku akimwangalia mwanaume ambaye alionekana kama kichaa mbele yake.

Kizwe mara baada ya kuona Edna anataka kuongea kitu kumwambia Desmond alimsogelea kwa spidi pale waliposimama huku akimwangalia kwa macho yaliojaa sumu.

“Desmond usijali chochote atachokuambia , anajaribu kuvuta muda , usimuamini kabisa”

“Hata mimi nimeona hilo , Edna usijifanye mjanja mimi ni mjuzi likija swala la mitego , uliweza kuwashinda wengine lakini sio mimi na hata kama nikikubaka Roma hawezi kufanya chochote mbele ya baba yangu”Baada ya kusema hivyo alimwinamia Edna akinuia kumpiga kiss kwenye lips , lakini Edna alitumia nguvu kumsukuma na kumkwepa huku akikimbilia kwenye vyoo.

“Mama anajaribu kukimbia” Aliongea Desmond lakini palepale Kizwe alipotea na kwenda kuibukia mbele yake na kumzuia asiingie chooni na kujifungia na kitendo kile cha Kizwe kutokea mbele yake ghafla kilimuogopesha mno Edna.

Desmond hata yeye mwenyewe alishangazwa na uwezo wa mama yake , kwani hakuwahi kumuona akiwa hivyo

“Edna mpenzi, nadhani utii shuruti la sivyo mama yangu hatokuvumilia”

“Hapana Desmond , huwezi kufanya hivyo kwasababu mimi ni dada yako”Aliongea Edna kwa sauti huku akianza kulia kwa kwikwi na Desmond alijikua akisimama akionyesha mshituko lakini Kizwe alishika mikono Edna kwa nguvu na kusimama nyuma yake na kisha akamwangalia Desmond.

“Unafanya nini Desmond , fanya haraka acha kusita sita nakushikilia iwe rahisi”Aliongea Kizwe, alionekana hakubadilika mwili tu lakini hata nafsi yake pia imebadilika.

“Unajifanyisha kunitega , hahaha…, lini ukawa dada yangu , Mama yangu tangu lini akawa na mtoto wa kike”Aliongea Desmond huku akianza kupandwa na jaziba na palepale alimsogelea Edna bila ya huruma na Edna alikosa matumaini na tegemeoo lake muda huo ni Roma , asingetokea basi ndio anakwenda kubakwa na kaka yake lakini ile Desmond anataka kushika mkanda wa gauni..

BOOM!

Lilikuwa wimbi la upepo lililoambatana na rangi ya kijani ambalo lilimkumba Desmond kwa nguvu na kurudishwa kwa kasi na kama sio Kizwe kuwahi kumuachia Edna na kwenda kumzyia basi angegonga kichwa moja kwa moja kwenye Sink.

Rangi ya choo ilibadilika kabisa na kuwa ya kijani na kuambatana na ukungu, Kizwe alijikuta akipagawa na kujiuliza nini kilichotokea.

Edna na yeye alishangaa lakini mkono wake wa kushoto ulikuwa ukitetemeka mno na alipoangalia aliona mwanga ulikuwa ukitoka kwenye ile bangiri ya ajabu, alikumbuka Roma alimwambia ni ya ulinzi lakini hakuamini mpaka muda huo alipofanya maajabu yake na kumuokoa.

Alikumbuka Roma akimwambia aivae na asiivue wakati wakija ndani ya hilo eneo na alimwambia kabisa kwa muda huo ilikuwa kama urembo tu.

Asichokifahamu Edna na Roma pia ni kwamba bangiri ile haikuwa Dhana za kawaida na hata mtu ambaye yupo kwenye levo ya Nafsi hajui namna inavyotumika na sio kwa Roma tu hata kwa Zenzhei mwenyewe hakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu hio bangiri.

“Desmond upo sawa?” Aliuliza Kizwe huku akimshikilia Desmond vizui akimwangalia kwa wasiwasii.

“Desmond alijitahidi kusimama mwenyewe na kusaficha damu iliokuwa ikitoka kwenye midomo yake , ilionekana aliumia kwa ndani.

“Niko sawa mama, There is something wrong with that bitch” Aliongea

“Huenda Roma alijua siku moja jambo kama hili lingemtokea?”Aliongea Kizwe huku wakimwangalia Edna ambaye anaishangaa bangiri yake iliomuokoa.

“Kwahio nawezaje kumfikia sasa?”Aliongea huku akionyesha woga wa kupiga hata hatua maana nguvu iliompiga haikuwa ya kawaida kabisa.

Kizwe aling’ata meno yake kwa hasira na kisha akapotea aliposimama Desmond lakini ile anataka kutokea aliposimama Edna bangiri ilitoa tena mwanga wa mng’ao wa kuumiza macho wa kijani kwa nguvu kubwa kiasi cha Edna kufumba macho.

Lakini ujinga aliofanya Kizwe ni kupotezea ule mwanga na kutaka kumsogelea Edna na kumshika na alipigwa na wimbi ambalo sio tu kumrudisha nyuma lakini pia lilimuunguza kwenye mikono kiasi hata nguo aliovaa iliungua na mwanga ulirudi tena kwenye ile bangiri na Edna alionekana kutopata madhara yoyote.Ilionekana ile Dhana ni kama ngao kwa Edna na ilitambua wakati gani alikuwa kwenye hatari.

“Damn it her bangle’s the one causing trouble , I can’t get close either”Aliongea Kizwe kwa hasira huku akimaanisha kwamba nni Bangiri yake ndio inamzuia kutokumsogelea pia.Desmond alijawa na wasiwasi huku akimwangalia Edna na kumuona kama kiumbe cha ajabu.

“Mama hatuna muda wa kutosha na Roma muda wowote atarudi , si ulisema hata kama nikimbaka baba atanilinda , yupo wapi muda huu?”

“Nina uhakika tayari ashakwisha kufika na kama ukitoka nje unaweza kumuona”Aliongea .

“Na vipi kuhusu Edna?”

“Kwanini unajali sana kuhusu yeye , mpango wetu umefeli hivyo ukiulizwa kaelekea wapi wewe jibu hujamuona na hukumfanya chochote na Roma atakosa ushahidi wa kukushambulia mbele ya baba yako”Aliongea kizwe.

“Nadhani kwa hilo nitajua namna ya kufanya mwenyewe”Aliongea Desmond na Kizwe alimwangalia mtoto wake kwa dakika kadhaa na kisha akamwangalia Edna kwa chuki nyingi na kisha palepale alipotea, ilionekana alikimbia hilo eneo.

Desmond mara baada ya mama yake kupotea hakutaka kuruhushu mshangao wake uchukue nafasi kwani angekutwa ndani ya vyoo hivyo vya kike ingekuwa tatizo na asingeweza kujitetea hivyo aliondoka haraka kutoka nje.

Edna alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akijiegamiza kwenye ukuta , hakuamini alikuwa amepona kwenye adha iliokuwa ikikaribia kumkumba , shukrani kwa Bangiri lake mkononi limeweza kumuokoa.

Desmond mara baada ya kufika nje alijikuta akihema kwa nguvu na kushika magoti yake, ijapokuwa alijitahidi kuwa sawa mbele ya mama yake , lakini alimuona ni wa tofauti kabisa na kila kitu kilikuwa zaidi ya maajabu, alijitahidi kujituliza na kutembea kuelewa alipowaacha watu wengine.

Roma ndio aliekuwa wa kwanza kugusa mstari wa mwisho , hivyo kufanikiwa kushinda na watu walimshangilia , akiwemo Fredi ambaye alimsahau hata Edna , watu wengine pia walimshangilia.

“Mr Roma ninashauku na jambo moja , kwannini unao uwezo mkubwa wa kuendesha magari?”Aliuliza Tusiman.

“Ni sababu gani imekupelekea kuendesha magari?” Aliuliza Roma.

“Kwasababu napenda magari lakini pili ndio fani niiochagua kufanya kwenye maisha yangu”

“Sababu zetu ni tofauti, mimi nikishikilia usukani naendesha kuyaokoa maisha yangu na sio kushinda kama wewe”Aliongea Roma na kumfanya Tusimani kuchangayikiwa kwani hakumuelewa maana Roma kaongea kimafumbo.

Roma alianza kuitafuta sura ya Edna , lakini hakuiona , aliangalia pia kumtafuta Desmond lakini pia hakumuona lakini muda ule ule aliweza kumuona Desmond akitokea upande wa nyuma akirudi kwa kukimbia.

“Nadhani kila mmoja ameweza kufurahia zawadi ya macho niliowaandalia na huu ni muda wa kuanza kile kilichotukusanya leo hii , wote tukusanyike ndani ya ukumbi “Aliongea Fredi huku akiwa na furaha kwani siku yake ilionekana kama ya kipekee mno.

Roma kitendo cha kutokumona Edna kilimfanya kuwa na wasiwasi na alitumia uwezo wake wa kijini kutafuta ndani ya eneo hilo na aliweza kumuona akiwa eneo la maliwatoni , upande ambao Desmond alitokea , alishangazwa na jambo hilo na kuanza kutembea kuelekea upande huo.

Lakini ile anakata tu kona aliweza kukutana na Edna njiani , alimwangalia na kugundua gauni lake limechafuka kwa kuwa na rangi, licha ya kuumizwa na muonekano wa Edna lakini alijitahidi kujituliza , hata hivyo alishatarajia mara tu baada ya kumuona Desmond ndani ya hilo eneo.

“Vipi umefanikiwa kumwambia?”Aliuliza Roma mara baada ya kumfikia na kumfanya Edna ainue macho yake na kumwangalia maana alielewa Roma anachouliza , alikuwa akiuliza amefanikisha kumwambia kama wao ni ndugu.

“Ulikuwa ukijua hili litatokea, inaonekana ilikuwa mpango wao kukushindanisha kwenye mbio za magari ili kukuweka mbali na mimi na kwa mwonekano wako ni kama ulifahamu kinachoendelea , Ulifanya hivyo kwasababu ulifahamu nina hii bangiri na ingenipa ulinzi?”Aliuliza Edna

“Baada ya kumuona hapa nilijua kuna kitu anapanga”

“Ungeniambia sasa na wewe mapema , vipi kama angekuwa na mpango mwingine?”Aliongea Edna huku aking’ata meno kwa hasira maana mpaka muda huo bado hakuwa akiamini kama amepona.

“Ningekuambia anachokipanga ,usingepata ujasiri wa kumuweka wazi na kuendelea kukuangalia na macho yake ya kimatamanio, nilichotaka ni kwanza aondoe mawazo yake ya kipumbavu kwa kuujua ukweli maana hili lisipoisha leo lazima lingejirudia, hata hivyo nilijua ungekuwa salama”.

“Wewe mwanaume ni umenikatili sana unajua nilikuwa kwenye hali ganni?”

“Nimefanya yote kwa faida yako na angalau kwa sasa utaachana na mawazo yako ya kimatarajio”Aliongea akimaanisha kwamba ataachana na mawazo yake ya kusubiria jambo ambalo haliwezi kutokea bila yeye kuchukua hatua.

Na alichoongea Roma ni nusu ukweli , Edna hakuchukua hatua ya kumpigia simu Raisi Jeremy na kusubiria yeye ndio amtafute na amtambue kama mtoto wake na alijua Edna angeendelea kusumbuliwa na Desmond na asingechukua hatua ya kumueleza ukweli.

“Sikuwa hivyo..”

“Unaweza kujidanganya mwenyewe na mtu yoyote ndani ya dunia hii lakini huwezi kunidanganya mimi , siku zote unaigiza kutokujali lakini nina uhakika unamjali Desmond na baba yako na leo nataka nikuambie kwamba Desmond hawezi kubadilika na huenda muda sio mefu nikayakatisha maisha yake”.

“Umekuwa chizi , umuue ? Utaishije Tanzania ukishafanya hivyo?”

“Kitu muhimu kwangu mimi ni wewe kuwa na furaha na mpaka sasa huenda yupo hai kwasababu yako , naogopa kufanya hivyo kwasababu unaweza kunikasirikia”

“Sijui chochote mimi , sitaki hata kufikiria akili yangu sasa hivi imejaa ukungu na nashindwa kabisa kufanya maamuzi sahihi ya kila kitu kilichoppo mbele yangu”Aliongea huku akishindwa kuzielewa hisia zake , tokea arudi kutoka visiwa vya wafu alikuwa akiangalia ujumbe wake umejibiwa lakini wapi , alikuwa akitamani hata ampigie Desmond amuulize kuhusu baba yake lakini angeanzaje, alitaka kujua angalau kidogo kwanini kadi la kliniki wakati mama yake akiwa mjamzito ilionyesha alikuwa na mapacha, lakini alikosa ujasiri wa kufanya hivyo , alitegema kupata majibu kupitia kwa Raisi Jremy lakini vipi kama raisi Jeremy angekataa kumtambua na kusema hana uhusiano nae wowote.

Lakini angefanyaje sasa huo ndio udhaifu wake , alikuwa akijali familia yake kuliko kitu chochote na ndio maana hata mpaka muda huo alikuwa na mawasiliano na Ernest Komwe licha ya yale aliotaka kumfanyia na tena sio kuwa na mawasiliano tu alikuwa bado akiwasaidia na pesa ya matumizi kwa siri, huyo ndio Edna uhusiano wa damu ndio udhaifu wake mkubwa.

“Unajihisi kuchanganyikiwa kwasababu , mbele yako ni kiza na hauna tochi ya kukupa mwanga wa kuona mbele na kama ni hivyo mimi nitakuazimisha tochi yangu ili uweze kuendelea na safari”Aliongea Roma na kumfanya atabasamu huku akishindwa kutoa jibu.

“Unadhani kama nikimuua Desmond itakuchukua siku ngapi kuomboleza ?”

“Hapana , usije ukafanya jambo lolotea la kijinga, Kizwe ineonekana amemualika raisi Jeremy kuja hapa na huenda anaweza kufika muda wowote”

“Unamaanisha nini kuhusu Kizwe!!! ?”Aliuliza kwa mshangao mara baada ya Edna kutaja jina la Kizwe.

“Ndio” huku akikunja sura.

“Ndio alieandaa kila kitu kumsaidia Desmond , anaonekana kuwa kijana zaidi kuliko mara ya mwisho nilivyomuona lakini pia anaonekana kuwa na nguvu na spidi kubwa tofauti na binadamu wa kawaida na alipotea mbele ya macho yangu”

“Hahaha… Yan Buwe realy was extraordinary…”Alicheka Roma , alijua lazima ni matumizi ya Ressutection Fluid , lakini kilichomshangaza kama Kizwe kafufuliwa na kikimiminiika hiko na bado anaonekana kujiendesha mwenyewe kwanini wale wengine walionekana kama misukule.

Jibu ni moja tu kwake lililomjia , huenda aliendelea zaidi na zaidi upande wa teknolojia ya kibailojia , lakini hata hivyo hakuwa na wasiwasi kwani muda huo alikwisha mmaliza, ila kuna hisia zililimjia na alijifariji mwenyewe kwa kujiambia hakuna uwezekano wa Kizwe kuwa kama Yan Buwen na kitu pekee ambacho anapaswa kuhofia labda ni ukakamavu wake tu na kuwa na spidi ya kupigana , lakini sio kutumia kaunini za anga kama ilivyokuwa kwa Clone.

“Vipi utafanya nini , naamini karudi kwa ajili ya kisasi?”aliuliza Edna.

“Simuogopi , unachopaswa ni wewe kujichunga tu ,.. njoo tuondoke hapa turudi kabisa nyumbani huwezi kuendelea ukiwa umechafuka namna hio”Aliongea Roma huku akimshika mkono , lakini bado alionekana kusita sita na Roma aliweza kusoma mawazo yake , huenda alichokuwa akitaka muda huo ni kusubiri Jeremy kufika.

“Kama unataka kumuona mzazi wako basi tufanye hivyo na kama humhitaji katika maisha yako nipo tayari kumuua?”

“Unataka kumuua Raisi , Unatania wewe?”

“Vipi unadhania siwezi, kama sio kwa ajili yako huenda ningeshamuua”Aliongea Roma akikumbuka ile siku kule kigamboni alivyokutana na Raisi Jeremy na kumkwida mbele ya wana usalama wake baada ya kumwambia hana mpango wa kumtambua Edna kama mtoto wake.,

“Twende tu nyumbani , baada ya leo sitaki kuwaona tena”

“Ni ngumu sana , nina uhakika Desmond atakutafuta tena ndio maana natamanni kumaliza tatizo moja kwa moja , lakini unasita sita”

“Roma nisikilize tuondoke”Alibembeleza , ashaona Roma ni mtu mwepesi kuchukua maamuzi bila ya kufikira nini kitatokea baadae ndio maana alitaka kumtoa hapo haraka.

Ile wanakuja kufikia upande wa mbele wa jengo hilo la Maple Resort , msururu wa magari uliingia na wanausalama waliovalia suti walitoka kwenye magari ya mbele na nyuma kwa kasi na kuzagaa eneo lote kila mtu akiangalia upande wake ,

Baada ya dakika kama tano kupita gari iliokuwa katikati ilifunguliwa na alitoka mwanaume mweusi alievalia miwani na kusogela mlango wa gari ya abiria na kisha akafungua mlango na Raisi Jreremy aliweza kutoka na kukanyaga ardhi na kugeuza macho yake mbele na hapo ndipo alipomuona Edna akiwa amesimama na Roma wanamwangalia.
Ooooky
 
Edna alishangaa , ijapokuwa hakuwahi kuwa na ukaribu na Kizwe lakini ashawahi kumuona ana kwa ana , kubadilika kwake na kuwa kama kijana kulimshangaza mno na kuogopesha kwa wakati mmoja.

“The old Kizwe is dead . I have been reborn”Aliongea akimaanisha kwamba Kizwe wa zamani amekwisha kufa na yeye amezaliwa upya.

Edna alikuwa akitetemeka mno na kilichomjia akilini muda huo ni kukimbilia nje na Kizwe alimuacha apite huku akicheka , lakini ile anafikia mlangoni alizuiwa na Desmond.

“Ni wewe..?”Edna alijikuta akianza kuhofia na akili yake ilimwambia huenda kila kitu kimepangwa , kwanzia sherehe kufanyikia huku mbali lakini pia swala la Roma kushindana mbio za magari na yeye kumwagiwa Mvinyo.

“Vipi ,mbona unashangaa kuniona?”Aliongea Desmond huku akiwa ameweka tabasamu la kejeli na kumfanya Edna kurudi nyuma kwa wasiwasi.

“Desmond usije ukathubutu kunifanya chochote , Roma atarudi muda si mrefu na mtakuwa kwenye matatizo”Alitahadharisha Edna.

“Relax , tutamalizana na wewe kabla hata hajamaliza pambano”Aliongea huku akimsogelea karibu na Edna alianza kurudi nyuma nyuma.

“Mume mume wangu atawaua msithubutu kunigusa”Aliongea Edna

“Haha…So what , Tutakufa kwa mikono yake tu hata kama hatutokugusa , hivyo badala ya kufa bila sababu tutajitengenezea sababu”Aliongea Kizwe.

“Edna ,,, nimeisubiria hii siku kwa muda mrefu sana , usijali sana , Roma anahitaji angalau dakika kumi mpaka kuja kukupata , lakini kabla ya muda huo ngoja nikupatie kitu cha kipekee usiku wa leo”Aliongea

“Desmond huwezi kunifanyia hivi , huwezi kufanya hivi”Aliongea Edna na hakuwa na pakukimbilia kwani Desmond ashamshika tayari mkono huku akimsogezea sura yake karibu.

“Desmond hakikisha unafanya haraka nitaondoka baada ya kuifurahia show”Aliongea Kizwe bila aibu , ni kana kwamba Desmond hakuwa mtoto wake kabisa.

“Mama mpango wangu nataka nijipigie taratibu taratibu na muda ambao Roma anafika nashusha wazungu huku anaona”Aliongea huku akiweka tabasamu la kebehi.

“Hehe. kama huo ndio mpango wako basi sina budi kusubiri”Aliongea Kizwe lakini muda ule ule yule muhudumu ambaye alimchafua Edba aliingia.

“Madam , What are your orders?”Aliuliza kwa Kingeereza.

“Jeremy yupo wapi , bado hajafika tu?”Aliuliza kizwe.

“Mheshimiwa atafika hivi punde , tayari wanausalama washawasili”Alijibu na kumfanya Kizwe kuonyesha tabasamu la furaha , alijiambia anakwenda kumkomoa Jeremy kwa Desmond kumla dada yake.

Raisi Jeremy alikuwa nchini Tanzania kuhhudhuria mazishi ya kifo cha Raisi mstaafu wa Tanzania Kigombola , ilionekana walitumia nafasi ya uwepo wake nchini kukamilisha mpango wao.

Desmond alizidi kumkandamiza Edna kwenye ukuta na lile koti ambalo alipewa kuvaa na Roma lishadondoka chini na hivyo mabega yake kuwa wazi

“Desmond tafadhari nakuomba usifanye hivi , mimi ni ..”Edna alianza kushikwa na kigugumizi.

“Wewe ni nani , Sema..?”Aliongea kwa kingereza.

“My…”Edna alishindwa kuongea huku machozi yakimtoka mfululizo huku akimwangalia mwanaume ambaye alionekana kama kichaa mbele yake.

Kizwe mara baada ya kuona Edna anataka kuongea kitu kumwambia Desmond alimsogelea kwa spidi pale waliposimama huku akimwangalia kwa macho yaliojaa sumu.

“Desmond usijali chochote atachokuambia , anajaribu kuvuta muda , usimuamini kabisa”

“Hata mimi nimeona hilo , Edna usijifanye mjanja mimi ni mjuzi likija swala la mitego , uliweza kuwashinda wengine lakini sio mimi na hata kama nikikubaka Roma hawezi kufanya chochote mbele ya baba yangu”Baada ya kusema hivyo alimwinamia Edna akinuia kumpiga kiss kwenye lips , lakini Edna alitumia nguvu kumsukuma na kumkwepa huku akikimbilia kwenye vyoo.

“Mama anajaribu kukimbia” Aliongea Desmond lakini palepale Kizwe alipotea na kwenda kuibukia mbele yake na kumzuia asiingie chooni na kujifungia na kitendo kile cha Kizwe kutokea mbele yake ghafla kilimuogopesha mno Edna.

Desmond hata yeye mwenyewe alishangazwa na uwezo wa mama yake , kwani hakuwahi kumuona akiwa hivyo

“Edna mpenzi, nadhani utii shuruti la sivyo mama yangu hatokuvumilia”

“Hapana Desmond , huwezi kufanya hivyo kwasababu mimi ni dada yako”Aliongea Edna kwa sauti huku akianza kulia kwa kwikwi na Desmond alijikua akisimama akionyesha mshituko lakini Kizwe alishika mikono Edna kwa nguvu na kusimama nyuma yake na kisha akamwangalia Desmond.

“Unafanya nini Desmond , fanya haraka acha kusita sita nakushikilia iwe rahisi”Aliongea Kizwe, alionekana hakubadilika mwili tu lakini hata nafsi yake pia imebadilika.

“Unajifanyisha kunitega , hahaha…, lini ukawa dada yangu , Mama yangu tangu lini akawa na mtoto wa kike”Aliongea Desmond huku akianza kupandwa na jaziba na palepale alimsogelea Edna bila ya huruma na Edna alikosa matumaini na tegemeoo lake muda huo ni Roma , asingetokea basi ndio anakwenda kubakwa na kaka yake lakini ile Desmond anataka kushika mkanda wa gauni..

BOOM!

Lilikuwa wimbi la upepo lililoambatana na rangi ya kijani ambalo lilimkumba Desmond kwa nguvu na kurudishwa kwa kasi na kama sio Kizwe kuwahi kumuachia Edna na kwenda kumzyia basi angegonga kichwa moja kwa moja kwenye Sink.

Rangi ya choo ilibadilika kabisa na kuwa ya kijani na kuambatana na ukungu, Kizwe alijikuta akipagawa na kujiuliza nini kilichotokea.

Edna na yeye alishangaa lakini mkono wake wa kushoto ulikuwa ukitetemeka mno na alipoangalia aliona mwanga ulikuwa ukitoka kwenye ile bangiri ya ajabu, alikumbuka Roma alimwambia ni ya ulinzi lakini hakuamini mpaka muda huo alipofanya maajabu yake na kumuokoa.

Alikumbuka Roma akimwambia aivae na asiivue wakati wakija ndani ya hilo eneo na alimwambia kabisa kwa muda huo ilikuwa kama urembo tu.

Asichokifahamu Edna na Roma pia ni kwamba bangiri ile haikuwa Dhana za kawaida na hata mtu ambaye yupo kwenye levo ya Nafsi hajui namna inavyotumika na sio kwa Roma tu hata kwa Zenzhei mwenyewe hakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu hio bangiri.

“Desmond upo sawa?” Aliuliza Kizwe huku akimshikilia Desmond vizui akimwangalia kwa wasiwasii.

“Desmond alijitahidi kusimama mwenyewe na kusaficha damu iliokuwa ikitoka kwenye midomo yake , ilionekana aliumia kwa ndani.

“Niko sawa mama, There is something wrong with that bitch” Aliongea

“Huenda Roma alijua siku moja jambo kama hili lingemtokea?”Aliongea Kizwe huku wakimwangalia Edna ambaye anaishangaa bangiri yake iliomuokoa.

“Kwahio nawezaje kumfikia sasa?”Aliongea huku akionyesha woga wa kupiga hata hatua maana nguvu iliompiga haikuwa ya kawaida kabisa.

Kizwe aling’ata meno yake kwa hasira na kisha akapotea aliposimama Desmond lakini ile anataka kutokea aliposimama Edna bangiri ilitoa tena mwanga wa mng’ao wa kuumiza macho wa kijani kwa nguvu kubwa kiasi cha Edna kufumba macho.

Lakini ujinga aliofanya Kizwe ni kupotezea ule mwanga na kutaka kumsogelea Edna na kumshika na alipigwa na wimbi ambalo sio tu kumrudisha nyuma lakini pia lilimuunguza kwenye mikono kiasi hata nguo aliovaa iliungua na mwanga ulirudi tena kwenye ile bangiri na Edna alionekana kutopata madhara yoyote.Ilionekana ile Dhana ni kama ngao kwa Edna na ilitambua wakati gani alikuwa kwenye hatari.

“Damn it her bangle’s the one causing trouble , I can’t get close either”Aliongea Kizwe kwa hasira huku akimaanisha kwamba nni Bangiri yake ndio inamzuia kutokumsogelea pia.Desmond alijawa na wasiwasi huku akimwangalia Edna na kumuona kama kiumbe cha ajabu.

“Mama hatuna muda wa kutosha na Roma muda wowote atarudi , si ulisema hata kama nikimbaka baba atanilinda , yupo wapi muda huu?”

“Nina uhakika tayari ashakwisha kufika na kama ukitoka nje unaweza kumuona”Aliongea .

“Na vipi kuhusu Edna?”

“Kwanini unajali sana kuhusu yeye , mpango wetu umefeli hivyo ukiulizwa kaelekea wapi wewe jibu hujamuona na hukumfanya chochote na Roma atakosa ushahidi wa kukushambulia mbele ya baba yako”Aliongea kizwe.

“Nadhani kwa hilo nitajua namna ya kufanya mwenyewe”Aliongea Desmond na Kizwe alimwangalia mtoto wake kwa dakika kadhaa na kisha akamwangalia Edna kwa chuki nyingi na kisha palepale alipotea, ilionekana alikimbia hilo eneo.

Desmond mara baada ya mama yake kupotea hakutaka kuruhushu mshangao wake uchukue nafasi kwani angekutwa ndani ya vyoo hivyo vya kike ingekuwa tatizo na asingeweza kujitetea hivyo aliondoka haraka kutoka nje.

Edna alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akijiegamiza kwenye ukuta , hakuamini alikuwa amepona kwenye adha iliokuwa ikikaribia kumkumba , shukrani kwa Bangiri lake mkononi limeweza kumuokoa.

Desmond mara baada ya kufika nje alijikuta akihema kwa nguvu na kushika magoti yake, ijapokuwa alijitahidi kuwa sawa mbele ya mama yake , lakini alimuona ni wa tofauti kabisa na kila kitu kilikuwa zaidi ya maajabu, alijitahidi kujituliza na kutembea kuelewa alipowaacha watu wengine.

Roma ndio aliekuwa wa kwanza kugusa mstari wa mwisho , hivyo kufanikiwa kushinda na watu walimshangilia , akiwemo Fredi ambaye alimsahau hata Edna , watu wengine pia walimshangilia.

“Mr Roma ninashauku na jambo moja , kwannini unao uwezo mkubwa wa kuendesha magari?”Aliuliza Tusiman.

“Ni sababu gani imekupelekea kuendesha magari?” Aliuliza Roma.

“Kwasababu napenda magari lakini pili ndio fani niiochagua kufanya kwenye maisha yangu”

“Sababu zetu ni tofauti, mimi nikishikilia usukani naendesha kuyaokoa maisha yangu na sio kushinda kama wewe”Aliongea Roma na kumfanya Tusimani kuchangayikiwa kwani hakumuelewa maana Roma kaongea kimafumbo.

Roma alianza kuitafuta sura ya Edna , lakini hakuiona , aliangalia pia kumtafuta Desmond lakini pia hakumuona lakini muda ule ule aliweza kumuona Desmond akitokea upande wa nyuma akirudi kwa kukimbia.

“Nadhani kila mmoja ameweza kufurahia zawadi ya macho niliowaandalia na huu ni muda wa kuanza kile kilichotukusanya leo hii , wote tukusanyike ndani ya ukumbi “Aliongea Fredi huku akiwa na furaha kwani siku yake ilionekana kama ya kipekee mno.

Roma kitendo cha kutokumona Edna kilimfanya kuwa na wasiwasi na alitumia uwezo wake wa kijini kutafuta ndani ya eneo hilo na aliweza kumuona akiwa eneo la maliwatoni , upande ambao Desmond alitokea , alishangazwa na jambo hilo na kuanza kutembea kuelekea upande huo.

Lakini ile anakata tu kona aliweza kukutana na Edna njiani , alimwangalia na kugundua gauni lake limechafuka kwa kuwa na rangi, licha ya kuumizwa na muonekano wa Edna lakini alijitahidi kujituliza , hata hivyo alishatarajia mara tu baada ya kumuona Desmond ndani ya hilo eneo.

“Vipi umefanikiwa kumwambia?”Aliuliza Roma mara baada ya kumfikia na kumfanya Edna ainue macho yake na kumwangalia maana alielewa Roma anachouliza , alikuwa akiuliza amefanikisha kumwambia kama wao ni ndugu.

“Ulikuwa ukijua hili litatokea, inaonekana ilikuwa mpango wao kukushindanisha kwenye mbio za magari ili kukuweka mbali na mimi na kwa mwonekano wako ni kama ulifahamu kinachoendelea , Ulifanya hivyo kwasababu ulifahamu nina hii bangiri na ingenipa ulinzi?”Aliuliza Edna

“Baada ya kumuona hapa nilijua kuna kitu anapanga”

“Ungeniambia sasa na wewe mapema , vipi kama angekuwa na mpango mwingine?”Aliongea Edna huku aking’ata meno kwa hasira maana mpaka muda huo bado hakuwa akiamini kama amepona.

“Ningekuambia anachokipanga ,usingepata ujasiri wa kumuweka wazi na kuendelea kukuangalia na macho yake ya kimatamanio, nilichotaka ni kwanza aondoe mawazo yake ya kipumbavu kwa kuujua ukweli maana hili lisipoisha leo lazima lingejirudia, hata hivyo nilijua ungekuwa salama”.

“Wewe mwanaume ni umenikatili sana unajua nilikuwa kwenye hali ganni?”

“Nimefanya yote kwa faida yako na angalau kwa sasa utaachana na mawazo yako ya kimatarajio”Aliongea akimaanisha kwamba ataachana na mawazo yake ya kusubiria jambo ambalo haliwezi kutokea bila yeye kuchukua hatua.

Na alichoongea Roma ni nusu ukweli , Edna hakuchukua hatua ya kumpigia simu Raisi Jeremy na kusubiria yeye ndio amtafute na amtambue kama mtoto wake na alijua Edna angeendelea kusumbuliwa na Desmond na asingechukua hatua ya kumueleza ukweli.

“Sikuwa hivyo..”

“Unaweza kujidanganya mwenyewe na mtu yoyote ndani ya dunia hii lakini huwezi kunidanganya mimi , siku zote unaigiza kutokujali lakini nina uhakika unamjali Desmond na baba yako na leo nataka nikuambie kwamba Desmond hawezi kubadilika na huenda muda sio mefu nikayakatisha maisha yake”.

“Umekuwa chizi , umuue ? Utaishije Tanzania ukishafanya hivyo?”

“Kitu muhimu kwangu mimi ni wewe kuwa na furaha na mpaka sasa huenda yupo hai kwasababu yako , naogopa kufanya hivyo kwasababu unaweza kunikasirikia”

“Sijui chochote mimi , sitaki hata kufikiria akili yangu sasa hivi imejaa ukungu na nashindwa kabisa kufanya maamuzi sahihi ya kila kitu kilichoppo mbele yangu”Aliongea huku akishindwa kuzielewa hisia zake , tokea arudi kutoka visiwa vya wafu alikuwa akiangalia ujumbe wake umejibiwa lakini wapi , alikuwa akitamani hata ampigie Desmond amuulize kuhusu baba yake lakini angeanzaje, alitaka kujua angalau kidogo kwanini kadi la kliniki wakati mama yake akiwa mjamzito ilionyesha alikuwa na mapacha, lakini alikosa ujasiri wa kufanya hivyo , alitegema kupata majibu kupitia kwa Raisi Jremy lakini vipi kama raisi Jeremy angekataa kumtambua na kusema hana uhusiano nae wowote.

Lakini angefanyaje sasa huo ndio udhaifu wake , alikuwa akijali familia yake kuliko kitu chochote na ndio maana hata mpaka muda huo alikuwa na mawasiliano na Ernest Komwe licha ya yale aliotaka kumfanyia na tena sio kuwa na mawasiliano tu alikuwa bado akiwasaidia na pesa ya matumizi kwa siri, huyo ndio Edna uhusiano wa damu ndio udhaifu wake mkubwa.

“Unajihisi kuchanganyikiwa kwasababu , mbele yako ni kiza na hauna tochi ya kukupa mwanga wa kuona mbele na kama ni hivyo mimi nitakuazimisha tochi yangu ili uweze kuendelea na safari”Aliongea Roma na kumfanya atabasamu huku akishindwa kutoa jibu.

“Unadhani kama nikimuua Desmond itakuchukua siku ngapi kuomboleza ?”

“Hapana , usije ukafanya jambo lolotea la kijinga, Kizwe ineonekana amemualika raisi Jeremy kuja hapa na huenda anaweza kufika muda wowote”

“Unamaanisha nini kuhusu Kizwe!!! ?”Aliuliza kwa mshangao mara baada ya Edna kutaja jina la Kizwe.

“Ndio” huku akikunja sura.

“Ndio alieandaa kila kitu kumsaidia Desmond , anaonekana kuwa kijana zaidi kuliko mara ya mwisho nilivyomuona lakini pia anaonekana kuwa na nguvu na spidi kubwa tofauti na binadamu wa kawaida na alipotea mbele ya macho yangu”

“Hahaha… Yan Buwe realy was extraordinary…”Alicheka Roma , alijua lazima ni matumizi ya Ressutection Fluid , lakini kilichomshangaza kama Kizwe kafufuliwa na kikimiminiika hiko na bado anaonekana kujiendesha mwenyewe kwanini wale wengine walionekana kama misukule.

Jibu ni moja tu kwake lililomjia , huenda aliendelea zaidi na zaidi upande wa teknolojia ya kibailojia , lakini hata hivyo hakuwa na wasiwasi kwani muda huo alikwisha mmaliza, ila kuna hisia zililimjia na alijifariji mwenyewe kwa kujiambia hakuna uwezekano wa Kizwe kuwa kama Yan Buwen na kitu pekee ambacho anapaswa kuhofia labda ni ukakamavu wake tu na kuwa na spidi ya kupigana , lakini sio kutumia kaunini za anga kama ilivyokuwa kwa Clone.

“Vipi utafanya nini , naamini karudi kwa ajili ya kisasi?”aliuliza Edna.

“Simuogopi , unachopaswa ni wewe kujichunga tu ,.. njoo tuondoke hapa turudi kabisa nyumbani huwezi kuendelea ukiwa umechafuka namna hio”Aliongea Roma huku akimshika mkono , lakini bado alionekana kusita sita na Roma aliweza kusoma mawazo yake , huenda alichokuwa akitaka muda huo ni kusubiri Jeremy kufika.

“Kama unataka kumuona mzazi wako basi tufanye hivyo na kama humhitaji katika maisha yako nipo tayari kumuua?”

“Unataka kumuua Raisi , Unatania wewe?”

“Vipi unadhania siwezi, kama sio kwa ajili yako huenda ningeshamuua”Aliongea Roma akikumbuka ile siku kule kigamboni alivyokutana na Raisi Jeremy na kumkwida mbele ya wana usalama wake baada ya kumwambia hana mpango wa kumtambua Edna kama mtoto wake.,

“Twende tu nyumbani , baada ya leo sitaki kuwaona tena”

“Ni ngumu sana , nina uhakika Desmond atakutafuta tena ndio maana natamanni kumaliza tatizo moja kwa moja , lakini unasita sita”

“Roma nisikilize tuondoke”Alibembeleza , ashaona Roma ni mtu mwepesi kuchukua maamuzi bila ya kufikira nini kitatokea baadae ndio maana alitaka kumtoa hapo haraka.

Ile wanakuja kufikia upande wa mbele wa jengo hilo la Maple Resort , msururu wa magari uliingia na wanausalama waliovalia suti walitoka kwenye magari ya mbele na nyuma kwa kasi na kuzagaa eneo lote kila mtu akiangalia upande wake ,

Baada ya dakika kama tano kupita gari iliokuwa katikati ilifunguliwa na alitoka mwanaume mweusi alievalia miwani na kusogela mlango wa gari ya abiria na kisha akafungua mlango na Raisi Jreremy aliweza kutoka na kukanyaga ardhi na kugeuza macho yake mbele na hapo ndipo alipomuona Edna akiwa amesimama na Roma wanamwangalia.
Comradeee
 
SEHEMU YA 487.

Baada ya dakika kama tano kupita gari iliokuwa katikati ilifunguliwa na alitoka mwanaume mweusi alievalia miwani na kusogela mlango wa siti ya abiria na kisha akafungua mlango na Raisi Jreremy aliweza kutoka na kukanyaga ardhi na kugeuza macho yake mbele na hapo ndipo alipomuona Edna akiwa amesimama na Roma wanamwangalia.

Raisi Jeremy kabla hajapiga hatua kusogea mbele alimpa ishara msaidizi wake kumsogelea na kisha aliteta nae jambo na akaitikia kwa ishara na kisha alipiga hatua kusogelea mbele.

Alikuwa ashaanza kuzeeka kwani nywele zake zilikuwa na mvi , lakini licha ya hayo bado alionekana kuwa na afya nzuri.

Haikueleweka kwanini akafanya safari ya dharula mpaka kuja ndani ya hilo eneo kwani ni hakika sherehe ya Fredi haikuwa ikimuhusu.

Macho yake yalififia mara baada ya kugundua Edna alikuwa akiangalia upande mwingine kama vile hakuwa akimtambua na baada ya kuwafikia alisimama.

“Edn…CEO Edna”Aligwaya kwa kutaka kutaja jina la Edna lakini akabadilisha na kutaja jina la CEO.

Wageni ambao walikuwa wamealikwa kwenye sherehe hio walikuwa na shauku ya kujua nini kinaendelea , baadhi yao walikuwa wakimfahamu Raisi Jeremy hivyo mara baada ya kumuona walishangaa kwani ujio wake haukutegemewa , lakini ni kwamba wasichokijua kabla ya ujio wa raisi huyo hapo Maple speed Resort kuna baaadhi ya wanausalama walikwisha kufika mapema kuimaliza protakali za ki ulinzi..

Wengi walishangazwa kuona Raisi Jeremy amesimama mbele ya Roma na Edna, walijua Edna alikuwa mfanyabiashara lakini haiwezekani kama mheshimiwa kaja mahali hapo kwa ajili yake na moja kwa moja waliamini itakuwa ni Desmond mtoto wake.

“Mr President can I help you ?”Aliongea Roma akimaanisha kuna kitu anataka amsaidie huku akionyesha kutopenda kabisa kuongea nae.

“Hongera kwa kuweza kurudi katika familia yako baada ya kupotea kwa muda mrefu , naamini kutokana na baba yako kuwa kiongozi mkubwa wa nchi tutapata nafasi ya kuonana mara kwa mara”.

“Acha kujikweza , mtu kama wewe huwezi kukutana na mimi”Aliongea Roma na kauli yake iliwafanya wanausalama kumwangalia kwa macho ya tahadhari, maana hawajawahi kuona mtu wa kawaida kuongea na raisi vile anavyotaka hata kama sio raisi wa Tanzania walijiambia anapaswa kuheshimiwa.

“Ineonyesha ukoo umepata mrithi mwenye uwezo mkubwa na kujiamini, nimefahamiana na baba yako kwa kipindi kirefu sana na urafiki wangu na yeye ulianza kwasababu yako , lakini mara baada ya kurudi kwako , kila ninapomuuliza kuhusu bahari zako hataki kabisa kunipa majibu ya moja kwa moja”.

“Sijui unaemzungumzia, Mr President nipo hapa na mke wangu kwa ajili ya kushiriki party lakini imeharibika hivyo tunaondoka kama huna lingine la kuongea”Aliongea Roma na kisha akamshika mkono kumuashiria waondoke..

“Subirini kwanza msiondoke”Sauti ya Desmond kutoka nyuma ilisikika na kumfanya Roma ageuke na kumwangalia , awamu hii alionyesha ile hofu aliokuwa kwenye macho yake imekwisha kumpotea na sasa alikuwa akijiamini ,alikuwa ameshikilia glasi ya mvinyo huku akiwa ameachia tabasamu.

“Nyie wote ni wageni wa heshima ambao mmealikwa kwenye hii sherehe , kwanini ya kuondoka mapema, isitoshe mtu muhimu mheshimiwa yupo hapa nadhani ni fursa pia kwenu”Aliongea Desmond kana kwamba sherehe hio ilikuwa ya kwake.

Raisi Jeremy macho yake yote yalikuwa kwa Desmond , ni kama alikuwa akichunguza kitu flani lakini alishindwa kukiona.

Roma alishindwa kufanya maamuzi na kumwangalia Edna , hata hivyo aliekuwa mbele ni baba yake hivyo alitaka ampe nafasi ya kuamua kubaki au kuondoka , upande wa Edna hakuwa akijiamini kukaa mbele ya mwanaume anaefahamika kama baba yake ambaye hataki hata kumtambua na ni zaidi ya miezi minne alikuwa akijaribu kutuma nyumbe za barua pepe.

“Edna my young sister nadhanni baba kafika hapa kwa haraka kwasababu yako , sidhani unapaswa kuondoka bila ya kuongea nae kwani mnakutana mara moja kwa mwaka”Al;iongea Desmond na kuufanya moyo wa Edna kupiga kite kwani hakutegemea Desmond kuropoka.Roma ilibidi amshikilie mkono mara baada ya kuona Edna anatetemeka.

“Desmond unaongea ujinga gani?”Alifoka Raisi Jeremy huku akianza kubadilika sura lakini na Desmond na yeye alianza kubadilika vilevile.

“Unashangaa nini baba kutotoboa siri yako ulioficha kwa muda mrefu?”Aliongea na kumfanya Raisi Jeremy kwanza kuangalia mazingira japo watu walikuwa mbeli na waliposimama , lakini alijua kama angegombana na mtoto wake mbele ya watu ingempunguzia heshima yake kama kiongozi na wasaidizi wake waliona hilo na haraka sana walianza kutawanyisha watu.

“Unapata wapi ujasiri wa kuongea ki mitego mitego mbele yangu?”.

“Usingefika hapa kama hukutaka ukweli ujulikane,baba nilichoongea ni kweli Edna ni mtoto wako na kama naongopa kanusha akiwa mbele yake”

“Kimya …!”Aliongea kwa hasira na muda huo huo alimwita bodygurad wake na kumpa maelekezo ya kughairisha shughuli zote zinazoendelea hapo na kila mmoja atawanyike na swala lile lilifanyika kwa haraka sana , kwani ndani ya dakika chache watu wote washapanda magari na kuondoka na wakabakia wanafamilia.

“Desmond kilichonileta hapa nikutaka kujua kama yule mwanamke ushakutana nae tayari?”Aliongea .

“Mwanamke gani?”

“Mama yako?”

“Haha.. mama ashakufa tayari , Baba huwezi ukaongea hivyo wakati uliongoza raia kuomboleza kifo chake”Aliongea Desmond na hapa ilionyesha kabisa Raisi Jeremy alishakutana na Kizwe.

“Acha kunipotezea muda wewe mtoto , kama hamjaonana usingeongea ujinga wako , ndio sababu moja tu ilionileta hapa la sivyo nisingepoteza muda wangu”Aliongea huku akionyesha kuwa na hasira mno.

“Baba kwanini unaongea kwa hasira namna hio , nadhani uwepo wa mama kwenye maisha yetu ni jambo la kufurahia”

“Unajua nini wewe,nijibu swali langu Kizwe yupo wapi?”

“Baba sijui unachoniuliza ni nini , na laiti ningejua kuhusu kilichomtokea mama yangu nisingepoteza machozi yangu namna ile na nisingeumia moyo wangu kwasababu ya Edna , ndio maana ulikuwa mkali sana kutotaka ni mguse kumbe alikuwa ni mtoto wako wa nje ya ndoa na ulivyoona mama anataka kumfilisi ukaamua kupanga njama za kumuua”

“Wewe mtoto nimekuambia kaa kimya?”Alifoka.

“Kwani nakosea? , haishangazi ndio maana ulinipiga vibao bila ya kunijali , siku zote tumeishi pamoja , mama alikujali sana na kuwa msaidizi wako lakini kwasababu ya mtoto wa nje ya ndoa ukafanya maamuzi ya kumuua”Aliongea huku akitoa tabasamu la hasira.

“Kama kweli ulikuwa ukimjali kwanini hukuwahi kumtambua? Au ulikuwa ukiogopa watu kukunyooshea vidole ,haijalishi wewe ni raisi lakini ni binadamu vilevile haikuwa na haja ya kukaa kimya, unajua najisikiaje baada ya kugundua mwanamke niliekuwa nikimtamani ni mdogo wangu ?”

SLAP!

“Unanipiga tena?, kwanini usiniue tu na ukamalizana na mimi pia moja kwa moja , hata hivyo tayari ushapata mrithi wako”Aliongea huku akionekana kama mtoto mdogo mwenye wivu , kwa umri wake huenda hakupaswa kuwa kama hivyo.

Roma hakutaka kumvumilia Desmond na palepale alimpiga teke na kumfanya adondoke kama furushi, kitendo kile kiliwafanya walinzi kutoa siraha zao haraka na kumnyooshea Roma ,sio kwamba hawakumfahamu Roma alivyo ilikuwa mara ya pili kukutana nae na akafanya vitendo vya hatari kwa mheshimiwa hivyo muda huo walikuwa makini sana na yeye

“Roma usimpige tena”Aliamrisha Raisi Jeremy mara baada ya Roma kutaka kumuongezea lingine.

“Unajua maana ya kupiga , sijampiga bali nimemsukuma tu”Aliongea Roma na kumfanya Jeremy amwangalie kwa macho makali.

“Roma tuondoke”Aliongea Edna kwa kubembeleza alikuwa ashaanza kutokwa na machozi na kumshika mkono Roma na hakutaka kumkatalia aliona ndio anaeumia zaidi.

Desmond alijilazimisha kusimama huku akiugulia maumivu akiwaangalia Roma na Edna wanavyoondoka bila waswasi.

“Raisi Jeremy , unamwachaje mtu kama yule aondoke ilihali kampiga mtoto wako wa kipekee , mrithi wako, unapaswa kuwa kweli raisi wewe kama unamuogopa kinyamkela kama yule”

“Desmond nitakupiga nikuue , kaa kimya , huoni kwamba ukimchokoza zaidi atayakatisha maisha yako”

“Aniue.. Hahaha… kabla hajaniua nitahakikisha namuonja yule malaya hata kama ni ndugu yangu wa damu”Aliongea ilionekana hata hivyo kilevi kilishamkolea ndio maana alikuwa akiongea bila ya kufikiria.

Roma aliweza kusikia lile tusi na alijikuta akisimama kabla hajafungua mlango wa gari na kuingia..

“Nadhani hupendi kuendelea kuishi , unadhani siwezi kukufanya chochote kwasababu upo mbele ya baba yako kwa kumtukana mke wangu?”Aliongea Roma huku hasira zilianza kujitengeneza kiasi kwamba hata macho yake yalitisha.

Lakini kabla hawajaelewa kinachotkea Roma alipotea aliposimama na ile anaibuka alikuwa mbele ya Desmond na kuinyakua shingo yake na kuing’ingiza juu Desmond alijitahidi kujinasua kwenye mkono wa Roma lakini jitihada zake zilikuwa bure , wale walinzi pia walitaka kumuokoa lakini waliogopa kushambulia kwani wangemdhuru na Desmond hivyo walimwangalia Raisi Jeremy kupata amri yake.

Ndio wakati ambao Desmond alijua sasa kifo chake kinaweza kutekelezwa muda wowote na alifanya kosa kumchokoza bila ya kufikiria mara mbili.

“Roma hapana…”

Edna alikimbia na kwenda kumshika Roma tisheti akimzuia asimuue Desmond na ilikuwa bahati kwa Desmond maana alitaka akaze mkono na kumkatisha uhai palepale.

“Usimuue , Roma nakuomba tafadhari usimuue”Aliongea Edna lakini Roma aliendelea kuminya na kumfanya kuanza kurusha miguu kulia na kushoto akionyesha dalili ya kupoteza hewa.

“Edna mwambie aache tafadhari , Desmond hayupo kwenye akili zake timamu kwasasa ndio maana kaongea ujinga na ndio mtoto wangu wa pekee na mrithi niliebakiwa nae sitaki kumpoteza pia”Aliongea na kumfanya Edna amgeukie Jeremy na kumuangalia ‘neno mtoto wangu wa pekee niliebakiwa nae’ lilijirudia mara mbili mbili.

Edna aling’ata meno yake kwa hasira na kisha akamshika mkono wa kushoto Roma.

“Mwachie aondoke”Aliongea.

“Unamaanisha nini nimuachie wakati kakutukana”Aliongea Roma huku akionyesha ishara ya kutotii ombi la Edna.

“Honey …Edna alianza kupasha viganja vya mikono huku akijaribu mbinu za kike kumlegeza.

“Hii ni mara ya mwisho nakuomba , tafadhari….sitokuomba tena naomba usimuue , akirudia tena sitokuomba tena umsamehe”Roma alijikuta akikasirika.

“Una uhakika gani hatorudia , haujamsikia alivyokutukana”Edna alijikuta akishindwa kujua cha kufanya , alimwangalia Raisi Jeremy na kuona yupo kwenye wasiwsi na ameshindwa kuchukua hatua zozote kutokana na kumhofia Roma.

“Roma kama utamuua leo hii siwezi kukusamehe maisha yangu yote”Aliongea Edna na kumfanya Edna kumwangalia kwa mshangao na hakujua hata ni muda gani ameachia mkono wake na kumruhusu Desmond kudondoka chini kama furushi.

“Edna unanitishia kisa hii taka taka , unanitishia mimi mume wako?”

“Hapana …najua nimekosea na sio fair lakini hii ni mara ya mwisho haitorjirudia”Aliongea huku akimuogopa Roma yeye mwenyewe.

“Okey sitomuua”Aliongea Roma na kumfanya Raisi Jeremy kuvuta pumzi za ahueni na kuwapa ishara walinzi kushusha siraha chini na Roma baada ya kuona hivyo alimwangalia tena Desmond aliekuwa amejichanua chali mbele yake akivuta hewa na palepale alimpiga teke lingine sehemu zake za uzazi .

“Ow..!!”Hata sauti haikumtoka kutokana na maumivu alioyasikia na palepale alipoteza fahamu.

“Desmond!!”

Raisi Jeremy alikimbilia alipolala Desmond bila ya kujali tena , Alimshika mabega na kuanza kumtingisha lakini hakukuwa na majibu ya aina yoyote kutoka kwake.

Edna alijikuta akimwangalia Roma kwa mshituko bila ya kuelewa hisia zake , alijua Roma ashakubaliana na ombi lake lakini yamegeuka kuwa mengine.

“Umeomba nisimuue lakini sio kutokumuadhibu kutokana na makosa yake”Aliongea Roma na kisha akamsogelea karibu.

“Una baki au tunaondoka wote?”Aliuliza Roma kibabe na kumfanya ameze mate ya huzuni.

“Kwanini umemfanyia hivyo?”

“Unabaki au unaondoka?”Aliuliza mara nyingine. Na kumfanya Edna amwangalie Mheshimiwa Raisi Jeremy aliechuchumaa huku akiwa ameshikilia Desmond kwa huzuni , alijikuta akiumia ndani kwa ndani kwa kuona hakuna dalili ya kutambulika kama mtoto tena.

Walinzi walipisha njia wenyewe , hakuna ambaye alikuwa na ujasiri wa kumfanya Roma chochote kutokana na kutahadharishwa na mheshimiwa mwenyewe , hivyo waliishia kumwangalia Roma na Edna wanaingia kwenye gari.

“Roma kama mwanangu akapatwa na ukilema nitakufanya jambo ambalo hutokaa usahau”Aliongea Raisi Jeremy kwa hasira lakini Roma hakumjali zaidi ya kuingia kwenye gari.

Muda huo huo na wale walinzi walimsogela Mheshimiwa na kisha wakamchukua Desmond na kumuingiza kwenye gari kwa ajili ya kumuwahisha hospitalini.

Roma aliendesha gari kimya kimya , hakuwa na mudi yoyote ya kuongea na Edna alikosa amani kutokana na ukimya wake , alijua amekosea lakini asingeweza kuona Roma akimuua ndugu yake wa damu mbele yake.

“Bado una hasira na mimi?”Aliuliza.

“No”

“Unazo , Roma naomba tusahau yaliotokea leo , kwanzia leo nawasahau kwenye maisha yangu”

“Usiwazie sana , No means no”

“Unanidanganya acha kujizuia na kama ni kunifokea nifokee yaishe”Aliongea na kumfanya Roma kung’ata meno kwa hasira na kukanyaga padeli na kufanya gari lianze kunguruma kama simba huku likitembea kwa kasi kama mshale.

“Sina haja ya kukufokea , haujafanya chochote kibaya”Alijibu Roma na kumfanya Edna ashindwe kujua nini kingine cha kuongea na aliishia kukaa kimya.

Saa tatu usiku ndio muda ambao waliweza kufika na Blandina alishangaa kuona wamerudi mapema , alitarajia kurudi kwenye saa tano na namna pia Edna alivyonekana kuchafuka , lakini pia nyuso zao zilivyokosa nuru ya furaha ilimshangaza na Edna mara baada ya kusalimia nae alipandisha ngazi.

“Nini kimetokea Roma , mbona mmeondoka mkiwa vizuri na mmerudi mkiwa mmenuniana”

“Hakujatokea kitu Party haikuwa nzuri sana tumeamua kurudi”

“Mh! Naona kabisa mmegombana”Aliongea.

“Mama usiwe na wasiwasi”Aliongea Roma na kisha akapandisha juu kwenye chumba chake na alipoingia alijibwaga kwenye sofa na kuvuta pumzi nyingi huku akiwa amefumba macho.

Zilipita kama nusu saa tu mlango ulifunguliwa na Edna aliingia huku akiwa ashabadili mavazi na kuvaa ya kulalia kitambaa cha hariri , baada ya kumuona Roma amelala kwenye sofa akiwa gizani alijihisi kuumia na kuona huenda alichokifanya kimemkwaza sana .Alitembea taratibu na kwenda kusimama pembeni yake na Roma alifumbua macho na kumwangalia na kisha akayafumba tena.

“Hubby nimekuandalia chakula tayari nikuletee hapa hapa au unashuka tukale wote?”Aliongea Edna huku akijaribu kulegeza sauti awezavyo lakini Roma hakujibu kitu.

“Au unataka kuoga kwanza nitapasha maji yako moto yawe ya uvuguvugu na yatakuweka sawa”

“Huna haja ya kunifurahisha ki makusudi”

“Sio hivy… Sifanyi kimakusudi ni kwasababu napaswa kufanya hivi kama mkeo”Aliongea na kumfanya Roma asimame.

“Ulitakiwa kuniacha nimmalize Desmond moja kwa moja kwanini ukanitishia kutokunisamhehe kwasababu ya yule mpuuzi?”

“Bado una hasira na mimi?”

“Kwannii niwe na hasira na wewe , hasira ni juu yangu mwenyewe najilaumu kwanini nimemuachia kwa kukusikiliza wewe , nishawahi kumsamehe mara ya kwanzo na akarudia na nina uhakika atarudia tena , ulichofanya leo kitakuingiza kwenye matatizo baadae, Sijui kwanini nnimekuwa mjinga na kukusikiliza”Aliongea Roma na kisha akavua tisheti na suruali bila ya kumjali Edna aliesimama na aliingia bafuni na kubamiza mlango kwa nguvu.

Edna alisimama palepale akiwa hajui cha kufanya maana alimuona Roma kuwa mwenye hasira na alijikuta machozi yakianza kujitengeneza.

Roma mara baada ya kuingia bafuni alivua bukta yake na kisha akafungulia bomba la mvua(Shower) na kuacha maji ya mloanishe huku akiwa amefumba macho na kufanya kifua chake kilichojengeka kimazoezi kupanda na kushuka akijitahidi kutuliza hasira zake.

Lakini mlango wa bafuni ulisukumwa na Edna na kumfanya ageuke na kumwangalia.

“Unafanya nini?”Aliuliza Roma kwani alijua Edna hajawahi kufanya kitu kama hicho kwenye maisha yake.

“Kwanini unanifanyia hivyo Roma?”

“Unamaanisha nini?”

“Nimekuomba na kukuomba na nimejitahidi kukujali ili unisamehe , kwanini unashindwa kuacha hili lipite”

“Tutaongea nikimaliza kuoga”

“Hapana..!!, umenisaliti mara kibao lakini mwisho wa siku niliishia kukusamehe , kwanini mimi unanikatili wakati nishakuomba msamaha?”

“Edna nilichotaka kufanya ni kwa ajili yako , kwanini huelewei , Desmond hawezi kubadilika na Jeremy umeshuhudia mwenyewe hana mpango hata wa kukutambua”

“Ndio maana nimesema ni mara ya mwisho , kwanini hunielewi?“Aliongea Edna bila kujali maji ya bomba yanamloanisha.

“Una baba na kaka ambao wewe huwatambui na wao hawakutambui lakini huwezi kupotezea uwepo wao kwenye maisha yako , kwa mfano Denisi ni mara ngapi uliweza kumsamehe na kumuachia , je kama ni mtu mwingine aliekuchokoza ungemwachia na kuondoka?”

“Kwanini nipotezee kila kitu najua hakuna anaenihitaji na Desmond kanikosea lakini kwanini unaona ni kosa kwangu kuwaachia waondoke kwa mara ya mwisho?, ila sawa tu fanya utakavyo mimi ndio ambaye napaswa kukusamehe kila mara unaponisaliti , sawa usinisamehe na mimi nitakusamehe kila unaponikosea”Aliongea na kisha kihasira aligeuka lakini alijikuta akikanyaga sabuni na kuteleza lakini kabla hajatua chini Roma aliwahi kumdaka na maji ndio yalimloanisha kisawa sawa na kufanya nguo kugandia mwili wake.

Roma alimwangalia usoni huku akiwa amebadilika na kurudi kwenye hali yake ya kawaida.

“Unanicheka ?”Aliongea huku akijitahidi kuangalia pembeni akionyesha hajaathirika maana Roma hana nguo.

“Nafikiri ishaongezeka na kuwa kubwa,,”Aliongea na kumfanya Edna kuona aibu za kike,lakini Roma hakuwa na namna ya kumuachia kwa muda kama huo.

Na kilichoendelea kilianzia bafuni huko huko na kuhamia chumbani na ni vilio tu vilivyosambaa kila kona.

Upande mwingine wakati Roma akifurahia uanaume wake kwa kumlaza mke wake mrembo Edna kunako sita kwa sita ndani ya hospitali ya Aghakhan ilikuwa taarifa mbaya kwa raisi Jeremy.

“Mr President we tried our best but we cannot recover his reproductive organs , it has been damaged both internally and externally beyond repair”

“Mheshimiwa tumejitahidi kadri ya uwezo wetu lakini hatuwezi kurudisha tena mfumo wa ogani zake za uzazi , zimeharibika nje ndani kiasi cha kutotibika tena”Aliongea dokta kihindi

Ilikuwa taarifa mbaya kupokea huenda katika maisha yake yote , Desmond ndio mtoto wake wa pekee wa kiume ambaye alitarajia kuendeleza kizazi chake , anapokeaje taarifa ya kwamba hawezi tena kuwa mwanaume aliekamilika.

Baada ya kusharabu kauli ya daktari alijiambie hapana , lazima kuwe na namna ya kumuokoa mtoto wake kwa namna yoyote ile.

“Have our medical staff come over to take care him and you prepare plane we are going back”Aliongea akimaanisha kwamba watu wao wa afya waje kumuangalia mgonjwa na mwingine aandae ndege kwani wanarudi Rwanda.













SEHEMU YA 488.

MWEZI MMOJA NYUMA KIGALI.

Ilikuwa ni mtanange wa kibabe kati ya Kizwe na Lekcha , ijapokuwa aliwahi kufunga goli la kwanza kutokana na ukame wa muda mrefu aliokuwa nao , lakini mzunguko wa pili ulidumu kwa muda mrefu.

Huenda mwanafunzi yoyote wa chuo ambaye angesogelea ofisni ya mkufunzi wa fiizikia angesikia kwa nje kile kichokuwa kikiendelea ndani kwani Kizwe alionyesha kutoweza kuhimili hisia na kupiga makelele huku akitaja jina la Kilema.

Baada kama ya nusu saa Lekcha miguu ilimtetema na ilikuwa ni muda ambayo alikuwa akikamilisha mzunguko na alijitupa pembeni huku akihema kama mbwa baada ya kuwashusha wote.

“Kilema wangu , umeimarika sana kwa siku zote ambazo hatukuonana”aliongea.

“Niite Lekcha sio kilema”Aliongea

“Hapana ‘kilema’ ni jina ambalo limekaa kimahaba mpenzi , naomba usinizuie kukuita hivyo kuanzia leo”Aliongea na kumfanya Lekcha kutabasamu kifedhuli, tokea aanze kupata ufadhili kutoka kwa raisi wa taifa la Rwanda maisha yake yalikuwa mazuri na hata ule ukilema ulipotea mbele za macho ya watu kutokana na kupata matibabu mazuri ya viwango.

Hakupenda jina la Kilema kwani lilimkumbusha maisha yake ya nyuma , lakini Kizwe tokea wanaanza mchezo ameng’ang’ania kutaja jina la Kilema mwanzo mwisho, lakini kwa muda huo hakuona shida , alijiambia labda ni kwasababu ndio namna inavyomfanya kupandwa na hisia zaidi.

“Such a bitch”Aliwaza Lekcha kwenye akili yake , ijapokuwa ndio mara yake ya kwanza kukutana na Kizwe mara baada ya kushuhudia kifo chake , lakini ujio wake haukumfurahisha na sio kwamba alikuwa akimpenda.

“Umekuwa mrembo sana Kizwe”Aliongea Lekcha na kumfanya Kizwe kumsogelea na kumkumbatia.

“Nimerudi kwako kwasababu najua ni wewe pekee unaenipenda kwa mapenzi ya dhati”

“Mtu kama mimi mwenye ukilema , unaamini vipi nakupenda?”

“Haijalishi ilimradi nauona upendo wako juu yangu ni wa dhati hilo ndio la muhimu”Aliongea na kumfanya Lekcha kutabasamu.

“Niambie nini kimetokea mpaka ukawa hai na kuwa na mwonekano wa kitoto kama huu huenda na mimi ninaweza kuponyesha huu mguu”.

“Unamaanisha unataka kua kama mimi?”

“Sio kuwa kama wewe nataka kujua nini kimetokea , hivi unajua ni maumivu kiasi gani nimeishi nayo kwa kushuhudia kifo chako , niliishi kwa chuki sana zidi ya aliekuua”Aliongea na kumfanya Kizwe kutabasamu.

“Niliweza kuishi tena baada ya kufufuliwa na Yan Buwen , ndio aliehusika na mimi kuwa kama hivi”Aliongea.

“Yan Buwen!!!”Aliongea kwa kuhamaki.

“Ndio ambaye amekusaidia?”

“Mbona umeshangaa kama unafahamu jina lake?”Aliuliza.

“Nafahamu jina lake ndio , hakuna mwanasayansi siriasi ambaye hamfahamu , Yan Buwen ni mwanasayansi ambaye alikataa tuzo ya Noble Prize na umaarufu wake ulianzia hapo”Aliongea na kumfanya Kizwe kushangaa kidogo.

“Lekcha unashangaza , unaonyesha kujua mambo mengi na hata nilipopata taarifa umeweza kuwa Profesa wa chuo kikubwa kama hiki nilishangaa na kujiuliza maswali mengi kwanini ulikuwa Tanzania kwenye majalala tena ukiwa raia wa Rwanda?”Aliongea na kumfanya Lekcha kutulia kidogo.

“Nadhani mpaka sasa ushafahamu taarifa zangu si ndio?”

“Nataka uniambie wewe mwenyewe Lekcha haijalishi najua nini kuhusu wewe , ila nataka kusikia kila kitu kutoka kwako ,mara ya mwisho uliniambia siwezi kukutimizia unachotaka kupitia pesa na shauku yangu ndio hio , nataka kukujua kwa udani maana najua wewe sio mtu wa kawaida ambay hukupaswa kuokota makopo”

“Nitakueleza muda muafaka ukiwadia ila ninachoweza kusema adui wako ni adui wangu wa muda mrefu”

“Unataka kumaanisha nini?”Aliongea Kizwe kwa mshangao na Lekcha alisimama na kisha akasogelea droo ya meza na kuivuta na kisha akatoa picha chakavu na kumpatia.

“Huyu ni…”Aliuliza Kizwe kwa mshangao akiangalia picha ya kijana mmoja alievalia mavazi ya kininja.

“Anafahamika kwa jina la Ajent code 13 huyu ndio adui yangu ambaye ni adui yako”

“Sijakuelewa”

“Huyu ajent 13 ni siraha iliotengenezwa na taasisi ya siri ya Zeros organisation na ndio Roma Ramoni adui yako wa sasa”Aliongea na kumfanya Kizwe kushangazwa na maneno ya Lekcha.

“Ndio mtu ambaye alinipatia huu ukilema na ndio adui yangu namba moja na wewe kunikuta Tanzania ni mwendelezo wa kutafuta namna ya kulipiza kisasi changu”Aliendelea kuongea huku awamu hii akionyesha kukasirika na Kizwe alimwangalia kwa mshangao na kuanza kujiuliza Roma ni nani haswa ,kwanini hata kwa Yan Buwen alikuwa na kisasi nae.

Clelia mpenzi wangu nipo njiani naja.. nitamtumia huyu mwanamke kumsogelea Yan Buwen na kupitia yeye nitamuua Hades na kama ulivyosema utanipokea baada ya kukuonyesha uwezo na nguvu zangu”Aliwaza Lecha akitaja jina la Clelia na aligeuza macho yake na kuangalia picha iliokuwa imetundikwa ukutani.

“Lekcha kwanini unaangalia sana hio picha?”Aliuliza Kizwe akiangalia picha iliokuwa ukutani yenye maandishi ya United Nation general Secretary, Clelia Allisanto.

“Kwasababu niliikuta imetundikwa hapo ukutani na inashangaza”

“Inashangaza nini?”

“Wewe huoni umri wa Clelia Allisanto na nafasi yake?”Aliongea na kumfanya Kizwe kuwaza kimantiki sasa , mwanzoni aliangalia uzuri wa mwanamke huyo lakini hakuangalia cheo chake na kweli haiwezekani kwa umri wake kuweza kufanikisha hilo tena akiwa ni mwanamke.

**********

Katika wanawake wake wote ambaye alikuwa amepiga hatua kimafunzo ni Rose pekee na Roma ilimshangaza kwani aliweza kuingia kwenye levo ya nusu mzunguko kwa muda mfupi sana , ijapokuwa ilikuwa levo ya chini katika mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , lakini ilikuwa ni hatua kubwa ambayo amefikia na Roma ilibidi ampatie vidonge ambavyo alivichukua mara baada ya kuwaua watu wa hongmeng ili kumuwezesha kupanda levo kwa haraka.

Huwenda sababu ambayo ilimfanya Rose kupanda levo kwa haraka ni kutokana na kutokuwa na kazi ambazo zinamchukulia muda mwingi kama ilivyo kwa wenzake

Kwa mfano Amina alikuwa nyuma sana na yote hayo ni kutokana na majukumu kwani baba yake mzazi alikuwa nje ya nchi na yeye alipaswa kusimamia biashara zake kwa muda kutokana alikuwa akisumbuliwa na magonjwa.

Upande wa Nasra yeye alikuwa bize na ujenzi wa mradi wa Adani hivyo kazi ndani ya kampuni zilikuwa zimeongezeka maradufu.

Jambo moja ambalo lilimshangaza Roma ni juu ya Dorisi pekee, Roma aliona kitu cha ajabu ambacho alihisi huenda Dorisi alivyokutana na mwanamke anaefahamika kwa jina la Clelia Allisanto kuna kitu kilitokea.

Kila alipokuwa akifanya mapenzi na Dorisi alikuwa akijihisi kuchoka mno na ni kama nguvu zake zinanyonywa na kitu kingine Doris alionekana alikuwa akiimarika zaidi kila wanapokutana na hilo ndio ambalo lilimshangaza na kuona Dorisi ndio ambaye hakuwa wa kawaida , lakini hata hivyo hakutiliia sana maanani hisia zake.

Alijiambia kama Dorisi anaimarika kwa kufanya nae mapenzi basi atajitahidi kuhakikisha anamsaidia katika hilo.

Edna ndio pekee ambaye alikuwa kawaida tu , licha ya kwamba alikuwa akichukua mazoezi kila asubuhi lakini Roma hakumruhusu kuanza kwa kuhofia kwamba mwili wake ni mdhaifu mno.

Ijapokuwa Edna hakupenda kuwa nyuma nyuma , lakini hakuwa na jinsi kwasababu Roma ndio mwalimu wake na ilipaswa amsikilize hata kama hakuwa akiridhika na alichofanya ni kuendelea kujitahidi kuchukua mazoezi.

Ni saa tisa mchana siku ya ijumaa Edna na Suzzane walionekana ndani ya hoteli ya Peacock kwa ajili ya miadi na mgeni siku hio.

Edna alishangazwa sana jana yake Suzzane kumpigia simu akielezea kwamba Tajiri Khalifa mwenyekiti wa taasisi ya Emaar Foundation ndio ambaye amefika nchini kwa ajili ya kuonana nae.

Khalifa alikuwa tajiri mkubwa na ilishangazwa na ujio wake , ijapokuwa hata yeye ni tajiri mkubwa lakini kujilinganisha na Khalifa alieanza biashara zaidi ya miaka hamsini iliopita ilikuwa ni kumvunjia heshima.

Ndio maana muda huo wakati wanashuka kwenye gari alikuwa na mchecheto , kwanza kabisa alikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Khalifa kachangia mchango mkubwa kwenye taasisi yake , lakini muda huo uho akataka kuonana nae , hayo ndio maswali ambayo Edna alikuwa nayo na aliamini majibu yake yangeweza kujibika mara baada ya kukutana na mgeni huyo kutoka Taifa la urabuni Abu dhabi.

Kwasababu walikuwa na miadi waliweza kupokelewa na mhudumu na kuwaongoza mpaka kwenye lift na kutokea kwenye Floor za juu kuelekea kwenye chumba ambacho alikuwepo Tajiri khalifa , Edna alikuwa akijiamini kwasababu hakuwa peke yake.

Ila asichokijua ni kwamba Fayezi mtoto wa Tajiiri Khalifa aliuliwa na Roma mara baada ya kutaka kumlazimisha Amina afunge nae ndoa.

Baada ya kufunguliwa mlango na mhudumu mwenye asili ya kiarabu alievalia suti , Edna alishangazwa kukuta sio mtu anaekutana nae bali ni jopo la watu kama ishirini waliojipanga kwenye meza na ajabu ni kwamba mara baada tu ya kuingia wote walisimama kiheshima na kati ya sura alizozifahamu ni moja tu ambaye ni Nadia Alfonso mwanasheria wake.

Upande mwingine Roma akiwa kazini aliweza kupigiwa simu na Afande Kweka , alishangaa kupigiwa simu na huyo mzee babu yake kwani haikuwa kawaida yake.

“Uko wapi wewe mtukutu?”Aliuliza Afande Kweka kama kawaida yake.

“Nipo kazini tena kwenye kikao”

“Kuna mambo nahitaji tuongee lakini pia Zenzhei anaondoka”Aliongea.

“Unamaanisha nini Zenzhei kuondoka”Aliongea Roma na kumpa ishara Tanya ya kuendelea na alichokuwa akijadiliana nae na Tanya alitikisa kichwa na kutoka kwenye ofisi ya Roma.

“Muda wake wa kukaa kwenye ulimwengu wa kawaida ushafika kikomo na anapaswa kurudi kwenye miliki ya Hongmeng , anataka muonane kabla ya kuondoka”Aliongea Afande Kweka na kumshangaza.

“Kwani alikuwa na ukomo wa kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida?”

“Kama unataka majibu ya swali lako hakikisha kabla ya saa kumi na mbili za jioni upo hapa , alipaswa kuondoka jana lakini aliomba kuongezewa masaa mpaka leo jioni”Aliongea Afande na kumfanya Roma kushangaa lakini kwasababu alijua mzee huyo asingejibu maswali yake basi alimuambia anakuja.

Wakati Roma akipokea simu na Edna akikutana na jopo la watu asiowatambua upande mwingine katika mkoa wa Pwani Bagamoyo , Blandina na yeye alikuwa na miadi na mtu ambaye hakuwaza kama atakuja kumtafuta na kuongea nae tokea arudi nchini.

Ukweli mwanamama huyu alijishauri sana kwenda kuonana na mtu huyo tokea alipopata ujumbe wake na yote hayo ni kutokana na kukosa ile hali ya kujiamini.

Alijihisi kuwa mkosaji mbele ya Senga na chochote kilichotokea miaka kadhaa iliopita yeye ndio mkosaji , kwani yeye ndie aliefanya maamuzi ambayo yalikuwa ya ki usaliti , ijapokuwa hakufanya maamuzi hayo ya kiusaliti kwa makusudi lakini haikuwa ikimfanya kutokuwa mkosaji.

Raisi Senga alitaka kuonana na Blandina na muda huo wa mchana wakati Raisi huyo alipokuwa kwenye ziara ya mradi wa bandari Bagamoyi, alipanga miadi hio ya siri ili mke wake asije kufahamu.

Naam ni ndani ya hoteli ya Bagamoyo Resort ndio sehemu ambayo Blandina alikuwa akipaswa kukutana na mheshimiwa na muda huo alishuka eneo la maegesho, alifika mwenyewe akiendesha hivyo mara baada ya kushuka kutoka kwenye gari alifuatwa na Kabwe msaidizi namba moja wa Raisi Senga na kumuongoza njia.

Kule Jopo linamkaribisha Edna , kule Blandina na Senga , Upande mwingine ni Roma na Zenzhei.
Hatari na nusu
 
SEHEMU YA 489.
Baada ya kufunguliwa mlango na mhudumu mwenye asili ya kiarabu alievalia suti , Edna alishangazwa kukuta sio mtu anaekutana nae bali ni jopo la watu kama ishirini waliojipanga kwenye meza na ajabu ni kwamba mara baada tu ya kuingia wote walisimama kiheshima , kati ya sura alizozifahamu ni moja tu ambaye ni Nadia Alfonso mwanasheria wake.
Edna na Suzzane walihisi wamekosea chumba walichopaswa kuingia na Edna alitoa ishara ya kuomba msamaha kwa kuingilia kikao.
“Karibu sana Madam Persephone” Waliongea wote kwa pamoja kwa lugha ya kingereza na kisha waliinamisha vichwa kuonyesha ishara ya heshima jambo ambalo lilimpagawisha Edna na moyo wake kupiga kwa nguvu , alijihisi ni kama anaota na akishituka ingekuwa ndoto.
Kwa mara ya kwanza alihisi jina la Madam Persephone ambalo alilikuwa akiitwa mara kwa mara bila ya kujua sababu yake alihisi sio la kwake , ule ujasiri aliokuwa nao kwa muda huo ulimpotea na aliishia kuduwaa.
Suzzane pia alikuwa kwenye mshangao asijue nini kinatokea mbele ya macho yake , walikuja hapo kwa minajili ya kukutana na Tajiri Khalifa kutoka Dubai , mtu ambaye alichangia kiasi kikubwa cha pesa katika taasisi ya Edna Foundation na uwepo wao hapo ni kutii wito wa kuonana na tajiri huyo , lakini mambo yanaonyesha kuwa tofauti.
Licha ya kwamba alihisi yupo ndotoni lakini ulikuwa uhalisia na jinsi watu waliokuwa mbele yake walivyokuwa wakimwangalia alijua kabisa walimlenga yeye na ndio ambaye alikuwa akisubiriwa, lakini bado alijiuliza kwanini yeye na ni maigizo gani yanafanyika.
Kwanza chumba kilionekana kilikuwa cha mikutano ndani ya hoteli hii ya Peacock, pili mpangilio wa hapo ndani ulikuwa ni wa kikao muhimu kutokana na watu waliokuwepo , ilikuwa ni meza ndefu ambayo inajumla ya watu kumi kila upande kukamilisha watu ishirini na ni kiti kimoja tu ambacho kilikuwa wazi , kiti cha katikati ambacho huruhusu mkaliaji kuona nyuso za kila mtu aliekuwa mbele yake , ni rahisi kusema ndio kiti cha mwenyekiti kama ni kikao ambacho kinatarajiwa kufanyika.
Watu waliofahamika ambao wapo ni Shekhe Assad , Tajiri Khalifa , Mellisa Luiz , Pastor Cohen , Nadia Alfonso , Zoe Kovacic , Phill Knight na wengine wengi ambao ilionyesha ni wanachama wa Ant- illuminat.
Mwanadada mmoja aliekuwa wa kifilipino , alievalia suti alimsogelea Edna na kuinamisha kichwa mbele yake kwa namna ya heshima na kisha akavuta kiti kilichokuwa wazi na kumuonyesha ishara ya kukaa.
Edna bado aikuwa kwenye mshangao na alishindwa kujua achukue maamuzi , ya kuondoka au abaki na hata aliponyeshwa kiti cha kukaa bado hakupiga hatua kukisogelea maana alijua kukaa kwenye kile kiti ni kama yeye ndio anakwenda kuongoza kile ambacho kingekwenda kuendelea hapo ndani , kitu ambacho hata hakijui ni nini.
“Madam!!!” Suzzane alimshitua Edna ambaye bado alishindwa kufanya chochote licha ya kuonyeshwa kiti cha kukaa.
Edna aliinua uso wake na kuanza kuangalia kila mmoja ambaye yupo ndani ya hiko chumba, kuna wengine alikuwa akiwafahamu na kuna wengine hakuwahi kuwaona popote.
Lakini ghafla tu Edna alitoa tabasamu hafifu kama vile anavyofanyaga akiwa kwenye kampuni yake akiwa na kikao na wafanyakazi wake na alisogelea kile kiti na kuketi na kuwaangalia watu wote waliokuwa hapo ndani kama vile alikuwa akiwajua.
Ni kintendo ambacho hakikumshangaza Suzzane tu lakini kila mmoja kilimuacha na maswali lakini sio hivyo tu pia kiliwafanya kuwa na tumaini.
**********
Roma baada ya kuambiwa na Afande Kweka kwenda kuonana na Zenzhei , hakutaka kuchelewa sana , alikuwa na shauku ya kujua kwanini Zenzhei anataka kurudi Hongmeng baada ya kuishi Tanzania kwa muda mrefu.
Alitaka pia kujua ni jambo gani ambalo Zenzhei alitaka kumwambia , alikuwa na shauku kubwa kutokana na kwamba alikuwa na mpango wa kuivamia Hongmeng siku moja hususani muda huo ambayo alijua kabisa yeye ni adui na jamii hiyo , hivyo alitaka kukusanya kila taarifa iliokuwa ikihusiana na jamii hizo ili kumsaidia huko mbeleni.
Roma alimuaga sekretari wake kwamba anatoka na anagerudi siku iliokuwa inafuata , Tanya alishangaa kutokana na kwamba kuna baadhi ya maamjuzi yalikuwa yakimpasa kuyashughulikia siku hio hio lakini alikosa ujasiri wa kumzuia Master wake.
Ni zaidi ya miezi sasa tokea Tanya achukue majukumu ya Amina kama Secretari na alionekana ashanza kuipenda kazi yake na kuizoea na alikuwa ni msaada mkubwa kwa Roma kwani mambo mengi aliyafanyia kazi.
Muonekano wake ulikuwa umebadilika kwa asilimia mia moja na ilikuwa ngumu kujua ndio anaehusika kuongoza kundi la Yamata kutoka Japani ambalo linamilikiwa na Roma.
Roma alitumia muda machache sana kufika nyumbani kwa babu yake na baada ya kusalimiana na Afande Mstaafu Camilius Kweka ilisalimiana na Zenzhei pia wote walikuwa wamekaa nje kwenye bwawa la kuogelea na ilionekana walikuwa wakiongea.
“Nitawaacha muongee”.
“Camilius haina haja ya kuondoka , ninachoongea na Mr Roma sio kipya kwako”
“Hapana umesubiria muda mrefu na huu ni muda wako, Wewe mtukutu ukimaliza unione kwanza kabla ya kuondoka”Aliongea Afande Kweka na kisha aliondoka eneo hilo.
“Mr Roma samahani kama nimekuchukulia muda wako , muda huu ulipaswa kua kazini”
“Usijali kuhusu hilo , nilipaswa kuja hata jioni lakini kwasababu sikuwa na kitu cha kufanya kazini nimeona nije mapema”Aliongea Romana kumfanya Zenzhei kutingisha kichwa kumuelewa.
Na muda huo mfanyakazi aliwaletea Juisi ya matunda na kuweka mbele yao na kisha akaondoka.
“Mr Roma muda wangu wa kukaa kwenye ulimwengu wa kawaida umeisha”
“Nilipoambiwa unaondoka nimeshangaa , kwani ulikuwa na ukomo wa kuishi Duiani?”
“Nadhani ushawahi kisikia sheria za miliki za kijini juu ya binadamu au viumbe wanaojifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi?”
“Najua watu wa jamii kutoka miliki za kijini na binadamu ambao wamefikia katika levo ya Nafsi hawapaswi kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida”
“Upo sahihi Mr Roma na mimi muda wangu wa kuishi hapa duniani ushafikia ukomo?”
“Lakini uliishi kwa miaka mingi hapa Tanzania na naamini bado ulikuwa kwenye levo ya Nafsi , kwanini unaondoka sasa?”
“Ni stori ndefu Mr Roma ambayo nataka unipe muda wako nikuelezee ili upate kujua nia ya mimi kutaka haya maongezi na wewe”
“Nipo tayari kukusikiliza”Alijibu Roma kwa msisimko na Zenzhei alianza kumuhadhithia Roma kila kitu kuanzia namna ambavyo Zenzhei na familia yake walivyokimbia katika miliki za kijini na kuja katika ulimwengu wa kawaida , alielezea namna ambavyo baba yake mzazi na mama yake mzazi walivyopambana na wajumbe kutoka Hongmeng mpaka kuwaua , aliendelea kuelezea namna ambavyo baba yake alipambana na mtu asieonekana ambaye ndio aliyakatisha maisha ya wazazi wake mbele yake , namna ambavyo alipona , namna ambavyo alijiunga na kundi la kininja la Yamaguchi kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa The Doni.(Rejea episode ya 317).
Roma alishangazwa na stori nzima ya Zenzhei na sasa alielewa uwepo wa Zenzhei kwenye maisha ya Afande Kweka ni kutokana na misheni aliopewa na kundi la Yamaguchi kukaa nae karibu.
Roma alikuwa akielewa kuhusu Yamaguchi lakini kwenye maisha yake hakuwahi kulipa umuhimu kundi hilo na yote hayo ni kwasababu aliyachukulia kama makundi mengine tu ya kininja ambayo yalikuwa yakiua kwa ajili ya pesa ,lakini hakufahamu kuna zaidi ya hayo.
“Kwahio kundi la Yamaguchi hawakuweza kukufahamu kama unatokea Hongmeng?”
“Hawakuweza kunifahamu mpaka baadae sana nilipowakatalia misheni ya kumuua Cammilius”
“Ushawahi pewa mishenni ya kumuua Afande Kweka?”
“Ndio lakini sikutekeleza agizo, Camillius nilifahamiana nae kwa muda mrefu tokea mke wake akiwa hai na amenisaidia kwenye mambo mengi ambayo yalinigusa moja kwa moja na kwangu nilimchukulia kama ndugu,nilipomuelezea ukweli juu ya kwanini nipo kwenye maisha yake hakukasirika na aliniacha nifanye chaguzi mimi mwenyewe kumchagua yeye au kundi na mamuzi nilioyafanya ni kumchangua yeye na ndio nilipokuja kuwa mlinzi wake mpaka leo hii”
“Nikupe pole kwa yaliokukuta , lakini bado sijapata jibu la moja kwa moja umeishi miaka mingi ndani ya Tanzania na Hongmeng hawajakusumbua , kwanini sasa hivi?”Aliuliza Roma , alishangaa kwani ni kweli Zenzhei alikuwa kwenye levo ya Nafsi na kwa sheria za Hongmeng hakutakiwa kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida , lakini ajabu ameshaishi miaka mingi sana bila ya kurudishwa.
“Wazee wa Hongmeng hawakufahamu uwepo wangu duniani , walifahamu nimekwisha kufariki miaka mingi iliopita”.
“Lakini mara ya mwisho ulisema ulikuwa na mawasiliano na Hongmeng”
“Ambao wanafahamu uwepo wangu hawakuuweka wazi kwa Wazee wa Hongmeng , ndio maana nikasema Wazee hawakufahamu uwepo wangu duniani”
“Kama ni hivyo naweza kutafsiri ulikuwa na mawasiliano na wajumbe wa Hongmeng pekee na walificha uwepo wako lakini ukawa unaendelea na mawasiliano nao kama ni hivyo naamini kuna sababu wakaamua kuficha uwepo wako”Aliongea Roma.
“Upo sahihi kuna sababu kubwa ya kuficha siri ya uwepo wangu duniani na ni kutokana na ahadi ya faida”
“Ahadi ya faida?”
“Ndio Mr Roma unaweza kusema niliwaahidi kitu chenye faida ili waendelee kunifichia siri ya uwepo wangu hapa Tanzania”
“Kama ni hivyo kwanini sasa hivi wanataka urudi?”
“Kwasababu ahadi sijaitimiza na siwezi kutimiza kutokana na nia yangu ya kulipiza kisasi kwa kile kilichowatokea wazazi wangu, kutokana na kutotimiza ahadi walinitishia mara nyingi kwenda kutoa taarifa kwa Wazee , lakini nilijitahidi kuwa mjanja kwa kuwasubirisha kwa maneno nikisubiria ujio wako”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa ujio wake tena.
“Unamaanisha nini kusubiria ujio wangu?”Aliongea Roma na Zenzhei alitabasamu.
“Kwasababu kuna mtu nilikutana nae miaka iliopita na akaniomba msaada na kisha akaniambia ikiwa ni muda sahihi rudia haya maneno ‘ Damu na Giza ni laana’”Aliongea Zenzei nakumfanya Roma kutoa macho.
“Ulishawahi kukutana na mtangulizi wangu?”Aliuliza Roma akiwa haamini Zenzhei anafahamu hayo maneno kwasababu yalikuwa ni maneno ambayo ni fumbo.
Mara ya mwisho Roma kuongea na Hades wa zamani alimwambia maneno hayo ya fumbo na kumpa maelekezo mtu yoyote ambaye angeyatamka mbele yake anapaswa kumsaidia.
“Mr Roma kukujibu swali , nitasema ndio nilikutana nae mara moja tu na aliniomba msaada wa kumtambua mwalimu”Aliongea na kumfanya Roma kuzidi kujawa na shauku na mshangao kwa wakati mmoja na Zenzhei alijua Roma hakumuelewa hivyo akamwelezea kwa kirefu.
Kwa maelezo ya Zenzhei ni kwamba Hades wa zamani alimuomba msaada wa kumtajia mwalimu ambaye anaweza kufundisha binadamu mbinu za uvunaji wa nishati ya mbingu na ardhi kwa njia ndefu yaani ile ya Maandiko ya urejesho isio na kikomo ambayo ndio hio aliojifunza Roma na mtu ambaye alimtajia ni Tang Chi yaani master wake Roma.
Kwa lugha nyepesi Zenzhei alimpendekeza Tang Chi kwa Hades wa zamanni na Tang Chi akaja kuwa Master wa Roma.
Roma alishangazwa na ufunuo huo wa mambo lakini bado ilimchanganya kwani kwa namna ambavyo alikutana na Tang Chi ilikuwa ni kabla alipokutana na Hades wa zamani , kuna kitu kilimwambia huenda Master Tang Chi aliagizwa na Hades wa zamani kumfundisha yeye mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Roma alijikuta akikumbuka namna ambavyo alikutana na Master Tang Chi ilikuwa ngumu sana kuamini alikuwa ameagizwa na mtu.
“Mr Roma najua mtangulizi wako hajakuambia mambo mengi na mimi pia sio jukumu langu kukuambia yale ambayo hajakuambia kwani hata hivyo siyajui , nilimpendekeza Tang Chi kwasababu ndio binadamu pekee ambaye nilimfahamu kwa mara ya kwanza kujifunza tamaduni za jamii zisizoonekana na tokea nilipomsaidia hatukuwahi kuonana tena , lakini aliniambia msaada niliompatia ukizaa matunda basi nitayashuhudia kwa macho yangu na ndio ninapaswa kutamka maneno ya Damu na Giza ni laana”Aliongea Zenzhei na kumfanya Roma kukuna kichwa , ni kweli hakuwa akijua mambo mengi kuhusu Hades wa zamani na ilikuwa sawa kutokumuelewa, kwanza mtu mwenyewe aliishi miaka mingi hivyo huenda alikuwa na mipango mingi, Roma alifikiria na alijikuta akivuta pumzi.
“Kama ni hivyo nadhani unapaswa kuniambia shida yako na mimi nitakusaidia”Aliongea Roma na kumfanya Zenzhei kuvuta pumzi.
“Ninarudi Hongmeng kwasababu nahitajika kurudi , lakini naenda kukusubiria, mpaka sasa Mr Roma umekuwa adui namba moja wa Hongmeng na muda na saa yoyote watatoka huko walipo na kuja kukushambulia kabla ya muda huo kufika unapaswa kuwa wa kwanza kuchukua hatua”
“Unamaanisha niende Hongmeng na kupigana nao?”
“Ndio njia pekeee ya wewe kuwa salama na watu wako unaowapenda , mbinu uliojifunza ni hatari zaidi na hakuna mtu wa hongmeng yoyote ambaye amefanikisha kufikia leo ya Kuzaliwa upya”
“Lakini kama nitakuja kupambana Hongmeng watanizidi kwa uwezo wangu niliokuwa nao huu na isitoshe taarifa zinaonyesha ni wengi ambao wameshavuka levo ya Dhiki”
“Kuhusu uwezo wako sina wasiwasi umeweza kufikia levo ya kuipita Dhiki ndani ya umri mdogo sana hivyo natarajia utaenda juu zaidi ndani ya muda mfupi sana , nimekuambia nimevunja ahadi ndio maana Wazee wakagundua uwepo wangu duniani basi kile nilichoahidi nitakupatia wewe”Aliongea.
“Unamaanisha?”
“Mr Roma haikuwa bahati mbaya familia yangu kushambuliwa ni kwasababu ukoo wetu ulimiliki kitu cha thamani sana ambacho Baba na Mama hawakuwa tayari kukiweka wazi”Aliongea na kisha akampatia Roma karatasi.
“Hio karatasi imejaa taarifa ambayo ndio inanifanya nirudi Hongmeng, ndio urithi wa pekee kutoka kwa familia yangu nilioutunza kwa muda mrefu, nakupatia wewe kwasababu ni mtu sahihi wa kuwa nao”Aliongea na kumfanya Roma aifungue ile karatasi na alijikuta akishangaa baada ya kuona ni kanuni ya utengenezaji wa vidonge vya kusaidia mafunzo ya kuvuna nishati ya mbingu na Ardhi.
“Hii ni kanuni ya kutengenezea vidonge vya Poya?”
“Inaonekana ushalifahamu tayari jina lake , jibu ni ndio kama utaweza kufanikisha kutengeneza hivyo vidonge itakuwa rahisi kwako kupanda levo ya juu zaidi na hakuna kiumbe chochote kutoka Hongmeng kitakuwa tishio kwako”Aliongea na kumfanya Roma macho yake kuchanua kwa furaha na kupitia kwa haraka ile katatasi.
“Kwanini hukutengeneza hivi Vidonge wewe na kukuwezesha kupanda levo za juu zaidi na kulipiza kisasi?”
“Mr Roma nimekupatia kanuni tu , uwezekano wa kukamilisha utengenezwaji wa hivyo vidonge haitokuja kuwa rahisi na haikuwa rahisi wangu pia kutengeneza nikiwa hapa duniani na sitoweza kutengeneza nikiwa Hongmeng wewe pekee ndio naamini unaweza kukamilisha”Katika siku ambayo Roma alipata kitu cha thamani basi ni siku hio, hakuamini Zenzhei alikuwa na material muhimu na hamwambii mpaka wakati anaondoka , huenda angemsaidia hata kutafsiri kanuni hio.











SEHEMU YA 490.
Abu Dhabi- UAE.
Ni baada ya mwezi mmoja tokea waanze uchunguzi wa kile ambacho alifanya Chriss , kitendo cha kutaka kumuua Edna, waliamini kabisa majaribio ya kuuwawa kwa Edna ni nje ya malengo ya jumuia yao hio ya siri na ndio maana walitaka kuufahamu ukweli , kwanini Chriss kafanya maamuzi alioyafanya.
Uchunguzi ulikamilika mara baada ya Nadia Alfonso kumuhoji Roma na kupata majibu ya kile kilichotokea na pia kumuhoji Suzzane kwa kile ambacho kilitokea na baada ya kupata maelezo yao na kuona yanafanana waliendelea na uchunguzi wa kutaka kujua zaidi kuhusu Chriss aliishi wapi mara baada ya kuokolewa na Hades wa zamani gerezani katika mikono ya CIA.
Naam sasa ilikuwa ni siku ya ijumaa mara baada ya swala ya mchana muda wa saa tisa katika moja ya makazi ya Tajiri Khalifa ndani ya Abu Dhabi kulikuwa na kikao cha siri sana ambacho kilikuwa kikiendelea.
Ni kikao ambacho hakikuhusisha watu wengi sana ,waliohudhuria ndio mhimili wa umoja huo wa siri ufahamikao kwa jina la Ant Illuminat.
“Mmefikia katika hitimisho?”Aliuliza mwanaume mmoja alievalia kilemba kichwani na kanzu.
“Ndio Shekhe”Alijibu kijana alievalia suti huku akiwa ameshikilia kishikwambi mkonnoni na jibu lake liliwafanya watu sita walioketi kwenye meza ya pembe nne wamwangalie kwa shauku ya kutaka kumsikiliza.
“Unaweza kuendelea”Aliongea mwanaume mwingine alievalia suti na miwani , alikuwa ni mzee ambaye umri wake ulionyesha kuwa mkubwa kutokana na nywele zake kuwa nyeupe.
“Nadia Alfonso alifanikisha kufanya mahojiano na Roma Ramoni juu ya kile kilichotokea na ameweza kutupatia majibu yaliorahisisha uchunguzi”Aliongea na kisha akafanya ‘casting’ ya kishikwambi chake na Screen ya TV ya nch 85 ya kampuni ya Sumsung na palepale ilionekana picha ya ua.
“Mnachokiona kwenye Screen ni ua adimu linalofahamika kwa jina la Blue Ghost Orchid, kwa maelezo ya Mr Roma Ramoni kutoka Tanzania anasema kabla ya Chirss hajamshambulia CEO Edna na Miss Suzzane alitokea mwanamke na akawaokoa na baada ya Chriss kufariki mwanamke huyo aliacha zawasi ya hilo ua , Maelezo haya yanafanana na ya Bi Suzzane ambaye pia tulichukua maelezo yake”Aliongea na kisha akapozi kidogo na kuangalia kishikwambi chake na kwenda ukurasa wa pili.
“Blue Ghost Orchid ni utambuisho wa taasisi ya siri yenye makao makuu nchini Singapore lakini pia ni utambulisho rasmi wa mwanachama baada ya kupokea ua hilo kama zawadi kutoka kwa The Doni”aliongea na kuwafanya wale wazee kuangaliana.
“Kwa maelezo yako tunapaswa kuamini The Doni ndio aliemuokoa CEO Edna si ndio?”Aliuliza na kumfanya kijana yule kutingisha kichwa na kisha akaendelea.
“ Kwa maelezo ya Bi Suzzane na Mr Roma mwanamke aliemuua Chriss ni Clellia Allisanto ambaye ni katibu mkuu wa umoja wa mataifa”Aliongea na kuwafanya wote kuangaliana.
“Mr Alban unatuambia kwamba aliemuokoa Edna ni Katibu mkuu wa umoja wa mataifa?”Aliuliza mzee mwingine wa kiafrika alievalia suti.
“Tumeshindwa kufikia kwenye hitimisho kutokana na kwamba hakuna namna yoyote ya kuthibitisha kama Clellia Allisanto ni The Doni”Aliongea na kuwafanya waanze kuongeleshana wao kwa wao kwa dakika kadhaa na kisha wakamgeukia.
“Vipi kuhusu Chriss, aliishi wapi mara baada ya kutolewa gerezani na kwanini alitaka kumuua Bi Edna kuna dhamira yoyote mmepata kuifahamu?”.
“Kamati yetu ya uchunguzi iliweza kupokea nyaraka iliotumwa kwetu kwa njia ya barua pepe na mtu ambaye hakujitambulisha jina na imetoa majibu ambayo tumeshindwa kuyahakiki na nitayaweka wazi”Aliongea na kisha alienda kwenye Gmail na kufungua nyaraka iliotumwa na palepale ilionekana kwenye Skrini na kuwafanya wale wazee wenye miwani kuziweka vizuri ili kusoma na wale ambao macho yao yalikuwa imara walikodoa macho.
“Nyaraka hii inaonyesha Chriss aliishi ndani ya Vatican mara baada ya kutolewa gerezani nchini Marekani na alikuwa ni mkutubi wa maktaba Chemba namba 4”Alielezea ile nyaraka na kuwafanya wale wazee kuendelea kushangaa.
“Kuna taarifa yoyote inaonyesha alikuwa na dhamira ya kutaka kumuua Bi Edna?”Aliuliza na Alban alitingisha kichwa kuashiria jibu ni ndio na kisha akapangusha kishikwambi chake na akatoa nyaraka nyingine iliotumwa kwao kama barua mfumo wa portable file(PDF).
“Hii ni barua ambayo tunaamini imeandikwa na Chriss mwenyewe kabla ya kutekeleza misheni ya kutaka kumuua Bi Edna nchini Tanzania na inaonyesha sababu kwanini alifanya maamuzi tofauti na misheni aliopatiwa.”Aliongea na palepale alianza kuisoma.
Kwa maelezo ya barua inaonyesha ni kweli Chriss alikuwa akiishi ndani ya Vatican kwa kipindi chote tokea atoroshwe kwenye gereza chini ya serikali ya kimarekani , anasema kwamba aliishi kwa Dilema ni upande upi anapaswa kuegamia kutokana na mfanano wa malengo ya dunia ijayo kati ya taasisi mbili tofauti yaani hio ya Ant-Illuminat na nyingine ambayo hakuitaja.
Anaendelea kusema maamuzi alioyafanya ni chaguzi alioifanya yeye mwenyewe na barua hio kama wataisoma basi atakuwa tayari amekwisha kufariki na misheni yake imefeli.
Mwisho kabisa anawafunulia kwamba misheni aliopewa kwa ajili ya Ant -illuminat ni kuwajuza kwamba kiongozi wanaemgojea sio yule ambaye wanamfikiria bali ni yule ambaye anapewa ulinzi na yule wanaemfikiria na ushahidi wa maneno yake upo kwenye mchoro wa unabii.
Mwisho kabisa wa barua anasema kama watakuwa wamefanikisha kupata barua yake basi misheni aliopewa na aliemuokoa imekamilika na atapumzika kwa amani akimlenga Hades wa zamani aliempatia misheni.
“Mchoro wa unabii!!??”Walijikuta wakiongea wote kwa wakati mmoja kwani hawajaelewa.
“Barua hii ni ya kweli inetokea kwake kutokana na sahihi na nadhani kabla ya kufikiria mchoto wa unabii tunapaswa kujua kauli yake: ‘yule tunaemfikiria sio mwenyewe bali yule anaelindwa na tunaemfikiria’ tuanzeni na kufumbua kauli yake”Aliongea mwanaume alievalia suti na Collar ya kiuchungaji.
“Albani kuna taarifa nyingine ambayo bado haujatupatia?”
“Hakuna Shekhe”
“Kwasasa uchunguzi wenu uhamie upande wa Clellia Allisanto ili kufahamu kama ndio The Doni, kuhusu kuthibitisha uwepo wa Chriss ndani ya Vatican tutatumia koneksheni tulizokuwa nazo”Aliongea Shekh na Albani alitingisha kichwa kukubali.
“Unaweza kwenda kwasasa , tunapaswa akujadili”Aliongea na kisha Albani aliondoka , haikueleweka alikuwa akitokea kitengo gani ndani ya taasisi hio ya Ant-illuminat lakini ni dhahiri ni sehemu ya kamati ya uchunguzi ilioutwa kutafiti kifo cha Chriss.
“Pastor Cohen nini maoni yako?”Aliuliza Shekhe na kumfanya mzee alievalia suti na kuwa na kipara cha nywele nyeupe kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Mpaka kufikia leo hii ni mengi ambayo yamefanyika na tumejipanua sana ndani ya mabara karibia yote na tuna washirika wengi wa kutuunga mkono kupambana na uovu , lakini licha ya mapambano yetu hatukuwa na kiongozi na wote tunajua tarehe 24 ya mwezi wa nne kwa mujibu wa Kalenda ndio siku ya kumtambua kiongozi wetu , nadhani alichoongea Chriss tunapaswa kukifiria mara mbili ili kupata majawabu lakini pia kuihakikisha kauli yake”Aliongea Paster Cohen kwa lugha ya kingereza.
“Naungana na Pastor Cohen ,nadhani ni wakati sahihi kwanza kuchambua kile alichoandika kwenye barua yake ili tufanye reasoning”Aliongea mwingine.
“Tunaefikiria siku zote kama kiongozi wetu ajae ni mrithi wa Hades ambaye ni Mr Roma Ramoni lakini kama sio yeye kwa kauli ya Chriss je anaemlinda ni nani?”
“Nadhani kujibu swali hilo kwa wepesi ni sisi kujiuliza ni nani wa muhimu kwenye maisha ya Hades mpya?”
“Mke wake ndio muhimu zaidi”
“Upo sahihi Shekhe Assad, nadhani hili pia linatoa majawabu ya kauli ya Chriss kuwa katika Dilema”Aliongea mwingine .
“Kwa haraka haraka inaonyesha Chriss hakuwa akifanya kazi tu kama mkutubi ndani ya Vatican , huenda kuna watu aliokutana nao na kujenga nao mahusiano ambayo yamempelekea kwenye dilema na huenda dilema aliokuwa nayo ni katika kuchagua upande aidha wa kwetu au wa kwao na ni sahihi pia kuamini huenda ndio wamemuonyesha kitu alichokiita mchoro wa unabii”
“Unafikiri huo mchoro wa unabii unahusiana na Edna?”
“Kama Bi Edna anapaswa kuwa kiongozi wa umoja wetu ambaye amechaguliwa na Hades wa zamani nadhani kuna uwezekano mchoro huo wa unabii unamzungumzia na ndio maana Chriss akachagua kutaka kumuua kwa kuagizwa na upande mwingine”
“Lakini kama mchoto unamzungumzia Edna kuwa kiongozi wetu kwanini na The Doni akamuokoa?”.
“Hili ni fumbo gumu , lakini naamini majibu yake tunayo wenyewe”
“Unamaanisha nini Paster Cohen?”
“Wote tunajua namna ambavyo Hades wa zamani alivyomuhusisha Seventeen kwenye mpango LADO, mnafikiri ilikuwa bahati mbaya , Seventeen na Edna ni mapacha tena wa kufanana kabisa na mpaka sasa hatujui Seventeen yuko wapi na tukumbuke yeye ni mwanachama wa ant-illuminat na ndio ambaye alimwingiza Zoe Kovac kwenye uanachama na haikuwa hivyo tu, Seventeen alikuwa na madaraka ya kuchagua mwanachama mpya wa ‘first echelon’ cheo ambacho ni kikubwa katika jumuia yetu na ni madaraka makubwa”
“Lakini wote tunaamini kiongozi wetu amekabidhiwa muhuli na Hades wa zamani , si ndio ulivyosema Shekh Assad namna ya kumtambua?”
“Uko sahihi kwa maelezo ya Hades wa zamani tutamtambua kiongozi kwa kutuonyesha pete ya muhuri(signet ring)?”
“Basi nadhaini hilo ni jibu la hiki tunachojadiliana hapa, kama maneno ya Chriss yapo sahihi na Hades mpya sio mwenye umiliki wa pete yenye muhuri basi mke wake Edna atakuwa nao”
“Upo sahihi ndugu Khalifa , lakini kalenda yetu inatupa muda mchache sana wa kutambua nani mmiliki wa pete hio ya muhuri wa uongozi , kalenda yetu inaonyesha tarehe 24 mwezi wa nne ndio siku ambayo tunapaswa kumtambua kiongozi”Aliongea na kuwafanya watu wote kuingia kwenye mawazo na waliona ana point.
“Nadhani kuna namna moja tu ya kuthibitisha maneno ya Chriss ni ya kweli au ya uongo?”Aliongea Shekhe Assad.
“Unataka kusema nini?”
“Tarehe ishirini na nne ndio siku katika kalenda yetu ya kumtambua kiongozi wetu na Chriss katuachia tayari fumbo na wote tunafahamu mtu muhimu katika maisha ya Hades mpya ni Edna mke wake , nadhani hili ni jibu tosha kwetu, Kama Edna kweli ni kiongozi wetu basi lazima atakuwa na pete ya muhuri wa uongozi na siku hio anapaswa kutuonyesha”Aliongea na kufanya chumba kukaa kimya.
“Wajumbe mnasemaje juu ya wazo la Shekhe Assad?”
“Kama kweli fumbo la Chriss linamuonyesha Edna ndio kiongozi wetu basi lazima atakuwa na muhuri wa uongozi”Alirudia mwingine kauli ileile ya Shekhe Assad.
“Na kama hatokuwa na pete ya muhuri basi tutatambua moja kwa moja yeye sio mlengwa na sio kiongozi wetu na fumbo la Chriss sio sahihi”Aliongea na wote walikubaliana na wazo lake.
“Kama ni hivyo tunafanikishaje kumfanya atuonyeshe pete hio?”Aliuliza Tajiri Khalifa.
“Tunatakiwa kumfanya atuonyeshe na ili hilo lifanikiwe lazima tuwe na mpango, Miss Edna anaweza kuwa na muhuri lakini hana ufahamu wowote kuhusu jumuiya yetu”
“Naunga mkono hoja na matukio mengi yanaonyesha ndio kiongozi wetu na wote hatujui hapa huenda Hades mpya amemkabidhi Edna pete hio kwa maelekezo ya Hades wa zamani”
“Ni kweli kabisa hakuna ambaye anajua nini Hades wa Zamani na Hades mpya waliongea wakati wakukabidhiana urithi , huenda alimwagiza Edna apatiwe muhuli na yeye ndio anaepaswa kumlinda”
“Mimi nina mawazo tofauti , kwa maelezo ya Hades wa Zamani hajamwambia Hades mpya kitu chochote kuhusu Ant illuminat na ameseme yeye mwenyewe angefahamu kitu kimoja kimoja kadri ya muda unavyosonga,tutaomba CEO Edna atuonyeshe muhuri wa uongozi kama kweli anao lakini tusiende na wazo la kuamini kwamba Hades mpya kampatia pete hio ya muhuri wa uongozi, nadhani mpaka sasa tunaelewa kwamba Hades hajamwambia mkewe chochote kuhusu Seventeen kuwa ni pacha wake , unafikiri ingekuwa rahisi kwake kumpatia Muhuri”Aliongea Shekhe na maneno yake yalionekana kuwa na mantiki.
Makubaliano ni tarehe ishirini na nne mwezi wa nne kuonana na Edna ili aonyeshe pete ya muhuri wa uongozi wa jumuia hio ya ant-illuminat.
Naam Edna kukutana na jopo la watu hao kwa kisingizio cha kuonana na Tajiri Khalifa ilikuwa ni mbinu tu, lakini vipi kuhusu hio pete.





SEHEMU YA 491.
ROME – ITALY- Miezi miwili iliopita.
Ni miezi miwili iliopita mashariki mwa jiji la Rome katika moja ya jengo la makumbusho ya kitaifa usiku wa saa mbili na nusu kwenda tatu kulikuwa na kikao cha watu wazito.
Ni watu wazito haswa kutokana na itifaki za ki usalama ambazo zilikuwa zimekwisha kuchukuliwa , jengo hilo lilikuwa kikitumika kama la makumbusho na mara nyingi muda wote linakuwa wazi mpaka saa nne za usiku kuruhusu watu , lakini siku hio jengo hilo lenye muundo wa kikale lilifungwa kwanzia muda wa saa kumi za jioni.
Ilikuwa ni sehemu sahihi sana kwa kufanyia mikutano ya siri kutokana na muundo wa jengo lenyewe lakini kitu kingine barabara ya kuingia ndani ya hili jengo haikuwa na pilikapilika nyingi kama barabara za katikati ya jiji.
Sasa usiku ndani ya vyumba vya Ardhi ndani ya jengo hili kulikuwa na kikao ambacho hakikujumuisha watu wengi sana , jumla ya watu waliokuwa wakifanya kikao walikuwa ni wanne tu, watatu wote walikuwa wamevalia suruali nyeusi na mashati ya rangi ya bluu iliokolea na kuvaa na Collar ambazo kwa harakaraka ziliwatambulisha kama wachungaji.
Mtu mmoja pekee ndio ambaye alivalia suti pamoja na tai , mwanga wa hapo ndani haukuwa mkali sana kutokana na taa zake za rangi ya njano zilizokuwa zikiendana na muundoo wa chumba.
“Barrack nadhani unaelewa sipendezwi na vikao vya dharula”Aliongea mzungu mmoja ambaye umri wake kwa haraka haraka ni kama miaka sabini hivi.
“Andre siwezi kusahau jambo muhimu kama hilo , lakini leo tulipaswa kuonana kwa dharula na nimefarijika mmeweza kutii wito kwa haraka”Aliongea yule mwanaume ambaye amevalia suti na tai akiwaangalia wale wenzake ambao walionyesha kuwa ni wachungaji au mapadri..
“Nini kimetokea?”
“Ni kuhusu Chriss mkutubi wetu ambae alienda Tanzania kwa maagizo yetu”Aliongea na kuwafanya wale wachungaji kuangaliana lakini mwanaume alieitwa kwa jina la Andre alionyesha utofauti.
“Nini kimetokea kuhusu Chriss , makubaliano yetu ajiingize ndani ya jumuia ya Ant Illuminat ili kupata kujua kila kitu kinachoendelea”
“Pastor Michal hiko ndio ambacho kimenifanya kuitisha hiki kikao cha dharula , taarifa zilizonifikia mpaka sasa Chriss amefaiki”Aiongea mwanaume aliefahamika kwa jina la Barrack na kimya kilitawala.
“Nini kimetokea? Je amegundulika ni shushu wetu?”
“Hilo haliwezekani ndio maana nahitaji kusikia kutoka kwenu wote,sisi wanne ndio tunajua kuhusu Chriss na Pastor Andre ulihusika kumbadilisha Chriss na kuwa double agent kazi ambayo ilichukuwa muda mrefu na hata aliporudi kuwa chini yangu ulinihakikishia ni Asset ya faida kwetu na ndio maana nilimsamehe na kumpa nafasi nyingine”
“Mr Barrack tunataka kusikia nini kimepelekea kifo cha Chriss?”Aliongea mchungaji michael.
“Taarifa nilizopata inaonyesha alienda kinyume na misheni aliopewa na Hades wa zamanni ndani ya Ant illuminat na akamshambulia Edna Adebayo mke wa Hades”Aliongea na kufanya wote kumaka lakini Andre muonekano wake haukutafsirika na Barrack aligundua hilo.
“Andre mbona unaonekana kutoshangaa?”
“Chriss alipaswa kunitafuta mara baada ya misheni”Aliongea Andr.
“Unamaanisha nini Andre”
“Ni mimi niliewasiliana nae dakika za mwisho kabisa na kumwambia misheni imebadilika”
“Kwanini?”
“Wameniambia kama hatuwezi kubadili unabii tunaweza kubadili matokeo”Aliongea na kuwafanya wenzake wote kushindwa kumuelewa.
“Nilipokea ujumbe kutoka kwa baraza la 33rd degree ya kumbadilishia Chriss misheni yake na wakati nawasiliana nae aliniambia ashafika eneo la tukio na muda si mrefu angekutana na Edna Adebayo”
“Mbona mimi ndio niliwasiliana nae na kumbadilishia misheni siku moja kabla nini kinaendelea?”Aliwaza ndugu Barrack.
“Andre ni watu gani hao?”
“Prior of sion, wanajua kila kitu ambacho tunakifanya na mipango yetu na hata kifo cha Chriss waliniambia wao wenyewe muhusika mkuu ni Minerva”
“Athena ndio aliemuua Chriss?”Aliuliza Barrack huku akionyesha wasiwasi.
“Hivyo ndio walivyoniambia”
“Papa Andre , ulishawahi kunihadithia umekutana na Athena ana kwa ana nadhani huu ndio muda wa kutuambia anafanana vipi? Je ni kweli Clelia Allisanto ndio yeye?”Aliuliza kwa kutanguliza jina la Pope Mwanzoni.
“Clellia Alisanto katibu wa umoja wa mataifa sio Minerva bali Athena anatumia Clone nina uhakika na hilo”
“I knew it”Aliongea akimaanisha kwamba alijua tu.
Naam mwanaume anaefahamika kwa jina la Barrack ni raisi mstaafu waMarekani na Andre ni Pope , wawili ni Michale ambaye cheo chake haikuwa wazi na pia John cheo chake haikuwa waz.

*********
MASAA KADHAA NYUMA
Ni muda wa saa sita usiku mara baada ya Roma kuondoka nyumbanni na kwenda kuzamia nyumbani kwa Nasra kwa kupitia balkoni, muda huo huo katika chumba chake alionekana mtu mwingine akiibukia na kuanza kuangalia mazingira ya hapo ndani na mara baada ya kuridhika aliingia kwenye chumba anacholala Roma na kuwasha taa na baada ya kuona kitanda hakina mtu alitabasamu kwa kebehi.
“Kulikuwa na haja gani ya kufanya sherehe kubwa na kutuharibia maua kama unakuja kulala mwenyewe”Aliongea kwa lugha ya chini huku akigeuka nyuma.
Alikuwa ni Hermes au Prince Raphaeli ambaye mwezi mmoja nyuma alimuokoa Denisi kwa kumdhibiti Roma kupitia ndoto.
Baada ya kukagua chumba cha Roma kwa dakika kadhaa alitoka kwenye chumba hiko na kuingia kwenye korido na ndani ya dakika chache tu aliibukia kwenye chumba cha Edna.
Baada ya kuingia ndani ya chumba hicho hakuacha kuangalia mandhari ya chumba kizima na kisha akahamia kwenye kitanda na kumwangalia Edna na Lanlan ambao wamelala fofo,
“Hades unaishi na mtoto wako lakini mpaka muda huu umeshindwa kumfahamu, aliesema huna akili kweli kapatia”Alijiwazia huku akimwangalia Lanlan aliemuwekea Edna mguu kwenye shingo.
“Athena sijui ananitakia nini , Hades akiniona namwangalia mke wake namna hii lazima ataniua, inabidi nifanye haraka kilichonileta na kuondoka”Alijiwazia mwenyewe na kisha akanyanyuma mkono wake na kumnyooshea Edna kama vile anamwombea na muda uleule Edna alianza kutingisha kichwa kama vile mtu ambaye yupo ndotoni na Hermes alidumu vilevile kwa dakika kama tano na kisha akaonyesha kuridhika na akageuza macho kwa Lanlan na kumnyooshea mkono kama alivyofanya kwa Edna na Lanlan alianza kutafuna tafuna kwa kasi kama vile kuna kitu analishwa na Hermes alitabasamu na kisha akaondoa mkonno wake.
“Persephone , kwanzia kesho utafanya mambo yako yote bila kujielewa chini ya udhibiti wangu ukiwa ndotoni”Aliongea huku akimwangalia Edna kwa dakika na kisha akafungua mlango wa kutokezea kwenye balkoni na palepale alipotea kufumba na kufumbua.
*********
“Madam Persephone tusamehe kwa kukufanyia hii surprise , yote yamefanyika kwa kuzingatia itifaki za kiusalama wa kuficha kile ambacho kinakwenda kuzungumziwa hapa ndani, nadhani upo kwenye mshituko lakini kabla ya kuendelea na hatua ya pili tutaomba utoe wasiwasi kabisa na kama kila kitu kikienda sawa huenda sisi wote tukawa chini yako”Aliongea Shekh Assad na Edna alishindwa kujibu chochote na alishangaa pia uwepo wa Nadia Alfonso.
“Kwa majina yangu naitwa Ally Assad na ndio msemaji mkuu wa hili jopo lote la watu waliopo mbele yako na Kabla ya kujitambulisha kwako mmoja mmoja na kukuelezea dhumuni la uwepo wetu hapa ndani tunataka ututhibitishie kwa kutuonyesha pete ya muhuri unaokutambulisha kama kiongozi wetu”Aliongea.
“Shekhe Ally Assad unaweza kuketi”Aliongea Edna bila wasiwasi na Shekh Assad alikaa chini na watu wote walimwangalia Edna kwa shauku ya kile ambacho anakwenda kufanya.
Edna hakuonekana kuongea chochote zaidi ya kuchukua mkoba wake na kutoa kijiboksi kidogo cha rangi nyeusi , ni viboksi flani kama vile vya kuwekea pete au mkufu.
Kitendo kile cha kushikiria kile kiboksi kabla hata ya kukifungua kiliwafanya watu wote hapo ndani kuwa na mchecheto wa aina yake.
“Kwasababu wote mmekuja kukutana na mimi leo hii , basi sina budi kuwadhirihirishia kwenu muhuri ambao unanitambulisha kama kiongozi wenu”Aiongea Edna akiwa kama sio yeye vile na kisha akafungua kile kiboksi na ndani yake ilionekana pete ambayo kwa kuiangalia tu haikuwa ya kawaida, ilikuwa na mchoro juu yake ulionakshiwa kwa madini ya shaba , mchoro ulikuwa kama vile ni tunda ambalo limekatwa kwa mshazari katikati sasa ule muonnekano wake wa ndani ndio ulifanana na hio pete.
Edna aliitoa na kuishikilia mkononi na kisha kwa mbwembwe zote aliingiza kidoleni katika mkono wake wa kulia na akaunyoosha juu ule mkono kuelekezea ule upande wa pete kuonekana kwa watu waliokaribu.
“Shekh Ally Assad hii ni Signet ring inatumika kama muhuri na ni kwa muda mrefu haijatumika , unaweza kuiangalia kwa ukaribu kuona kama mchoro wake unafanana na muhuri unaonitambulisha kama kiongozi wenu”Aliongea Edna na Shekhe Ally Assad aliangalia kwa umakini ile pete na alijikuta akipatwa na mshangao usiokuwa wa kawaida na palepale aliwageukia wenzake wote na kuwapa ishara ya kuashiria ndio muhuri wenyewe na wote kwa pamoja walisimamaa na kuinamisha vichwa chini kwa mara nyingine.
“Karibu sana Malkia wetu Persephone”Waliongea kwa mara nyingine baada ya kusimama na Edna alinyoosha mkono juu kuwazuia na akawaambia waketi chini na walitiii.
Suzzane na Nadia walikuwa na mshangao kwani hawakutegemea kutokutana na upinzani kutoka kwa Edna , lakini alionyesha kana kwamba watu waliopo mbele yake anawafahamu mbaya zaidi aliongea kimadaraka.
“Leo nimejitambulisha kwenu kikalenda , lakini muda wangu wa kuwaongoza bado , mpaka muda utakapokuwa sahihi nitawatafuta, kwasasa Shekh Assad ataendelea kuongoza jumuia yetu kwa niaba yangu na malengo yote yanapaswa kutimia kabla ya siku ya kurudi kwangu”Aliongea na kuwafanya kuonyesha sura za kutoelewa maana ya maneno.
*********
Blandna alijikuta akishangaa mara baada ya kuambiwa na raisi Senga kuhusu Roma kile alichomfanyia Desmond mtoto wa raisi Jeremy, hakujua jambo hilo kama limetokea kwani Roma na Edna hawakumwambia.
Usiku wa juzi walivyorudi alijua kabisa kuna jambo ambalo limetokea lakini hakuhoji sana kwani Roma alimwambia hakukuwa na tatizo na ni sherehe tu ambayo haikuwa nzuri.
Na yeye alipotezea baada ya kuwaona Edna na Roma asubuhi walikuwa wamepatana na ile hali ya kununiana ilikuwa imeisha na ndio maana hakuhoji sana.
“Kwahio hiki ndio ambacho ulitaka kuongea na mimi?”Aliuliza Blandina
“Kuna lingine ambalo ulitarajia kusikia kutoka kwangu , nimekuita hapa kukuambia kile alichokifanya mtoto wako ili umuonye kwani akiendelea kuchafua amani ya nchi yangu nitamchukulia hatua”Aliongea na kumfanya Blandina kumwangalia Senga kwa huzuni.
“Kwanini unamwita mtoto wangu peke yangu Senga , Wewe sio mtoto wako? Au ni kwasababu amebadilisha jina na kuitwa Roma ndio kinachokupa shida ya kumtambua, Senga najua huwezi kunisamehe lakini Roma bado ataendelea kuwa mtoto wako”
“Kimya!!!, wewe na Roma kwangu mlishakufa na ndege na sitaki kuhusika na maisha yenu , ninachotaka kutoka kwako ni kumuonya Roma aache kuharibu diplomasia ya nchi”
“Senga tangu lini ukawa mnafiki wa hisia zako mwenyewe?”
“Unamaanisha nini?”Aliongea Raisi Senga huku awamu hii akionyesha kakarisika maradufu.
“Maneno yako yapo tofauti na hisia zako Senga, unafikiria sijui kinachoendelea kwenye moyo wako , ulifikiri nitashindwa kujua kile unachojisikia , sijakusahau Senga”
“Kimyya , Blandina naomba usinikasirishe zaidi kukaa na mimi chumba kimoja usijipe ujasiri wa kuongea unavyojisikia , wakati ule ulishapita na sasa nimekuwa raisi kwa juhudu zangu wakati wewe ukijificha”
“Kinachokusumbua Senga ni kwasababu Roma ana nguvu zaidi kuliko wewe , uwezo wake na nguvu zake zinakufanya ujihisi huwezi kuwa baba mbele yake, Senga acha kuishi kwa mateso unapaswa kuachilia baadhi ya mambo megine yasahaulike kwenye moyo wako”
“Kuna vitu naweza kusahau , lakini siwezi kumsahau mwanamke alienisaliti”Aliongea na kumfanhya Blandina kuanza kutokwa na machozi.
Muda huo maongezi yao walikuwa wakiyafanyia ndani ya chumba cha hoteli hivyo ilikuwa ngumu kwa mtu wa nje kujua kile ambacho kinaongelewa na ilikuwa mara ya kwanza kwa Senga na Blandina kukutana wakiwa peke yao tokea arudi Tanzania na huenda ni mwanzo mzuri wa mapatano.
“Najua Senga huwezi kusahau na huwezi kunisamehe lakini upendo wangu kwako hakuwahi kupotea kwa miaka yote ambayo hukuweza kufahamu nipo hai”
“Blandina acha kuwa mnafiki mbele yangu utanikasirisha , nimekuja hapa kukuonya kuhusu Roma kuingilia amani ya taifa”
“Una uhakika ndio kitu pekee ambacho ulitaka kuniambia mpaka kutaka kuongea na mimi kwa kujificha ficha?”Aliuliza na kumfanya Senga amwangalie Blandina huku akikosa neno la kuongea.
Alichoongea Blandina ni ukweli mtupu, kama kweli alitaka kumuonya tu kuhusu Roma haikuwa na haja ya kumuita hotelini kwenye chumba cha Presidontial Suite tena kwa siri.
Blandina alimwangalia kwa muda namna ambavyo amekosa neno la kuongea na kisha akaangalia mkoba wake na akauchukua.
“Kwa mra ya kwanza nimefurahi kukuona kwa ukaribu Senga, nitamwonya Roma kutokuingilia uongozi wako”Aliongea na kisha alisogelea mlango akitaka kutoka.
“Subiri..!!!”Aliongea na kumfanya Blandina kusimama na kugeuka na Senga aliingiza mkono kwenye mfuko wa koti na ilionekana kuna kitu anatoa.




SEHEMU YA 492
Roma hakujua kinachoendelea kabisa na baada ya kutoka kwa Afande Kweka hakupitia nyumbani kabisa , akili yake ilimwambia aende kuonana na Rufi kwanza kuongea nae kuhusu kanuni aliopewa na Zenzhei ya kutengeneza vidonge vya nguvu za kijini , alikuwa na muwashawasha wa kufahamu kama Rufi angeweza kuelewa kanuni zote.
Dakika chache mbele mara baada ya kuendesha gari aliweza kufunga breki chini ya jengo la apartment anapoishi Rufi na alitoka kwenye gari na kuzisogelea lift.
Baadaya kuingia kwenye lift na kubonyeza kitufe cha floor husika simu yake ilitoa mtetemo wa ujumbe wa meseji ulioingia ,alifungua na kuona ni ujumbe ulitoka kwa Xiao Xiao na aliupotezea palepal.
Ilikuwa ni siku zaidi ya mbili msichana huyo wa kichina hakukata tamaa kutuma jumbe za kumsalimia Roma na nyingine za kuchombeza lakini Roma hakujibu hata moja , hakutaka matatizo na mke wake lakini pia alijua akiwa na ukaribu na msichana huyo itakuwa rahisi kwa Rufi uwepo wake hapa Tanzania kufahamika kwa wepesi , hivyo alijiambia anapaswa kumuepuka kwa nguvu zote.
Baada ya kutoka kwenye lift alibonyeza kengere na mlango kwa ndani ulifunguliwa na Rufi ambaye amevalia tisheti ya jezi ya Man U huku mkononi akiwa ameshikilia juisi ya matunda.Alitabasamu na kumpa ishara ya kuingia na Roma alifanya hivyo.
“Inaonekana unapenda sana mambo ya kompyuta , kwa mwonekano wako ulipaswa kujifunza vitu vilaini vilaini visivyotumia akili nyingi”Aliongea Roma mara baada ya kuona tarakishi ikionyesha namba namba ambazo hata hakuelewa.
“Kompyuta naipenda kwasababu nahisi kama dunia yote naiona , nimejifunza mambo mengi sana na kwasasa najaribu kutafuta Proffesional Hacjer anielekeze baadhi ya mambo madogo madogo”
“Kwahio unataka kuwa mdukuzi , haupendezi kabisa kwa fani hio?””
“Kipi kinanipendeza? Au kutapeli watu ndio kazi nzuri inayonifaaa?”Aliongea na Roma hakumjibu na aliishia kumwangalia tu kuona kama ana shida yoyote kwani tokea amuache mara ya mwisho hakuwasiliana nae kabisa na kumpa habari za Xiao Xiao msichana wa kichina aliemkimbia.
“Unaendelejeaje, ulitoka kweli humu na kwenda kutembea?”
“Naogopa hata kwenda Supermarket na hofia naweza kukutana nae tena” Aliongea huku akijibwaga kwenye sofa kivivu na kumfanya Roma amuonee huruma.
“Unapaswa kutoka bila ya kuhofia chochote hakuna mtu yoyote wa kuja Tanzania na kukufosi urudi ilihali mimi nipo”.
“Ah .. najua unaweza kunilinda lakini hawatoacha kuja mara kwa mara lazima watalazimisha nirudi sitaki kukuongezea zaidi matatizo”
“Nishakuambia usiwe na wasiwasi juu ya hilo nimefuatilia taarifa za msichana uliekuwa unamkimbia yupo Tanzania kikazi”
“Kweli?”
“Unafikiri nakudanganya? , umeacha lini kutokuniamini?”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutabasamu na kushindwa kuongea chochote na Roma aliona apotezee mada hio na kwenda moja kwa moja kwa kile kilichomleta.
“Nimekuja kukuuliza namna ya kutengeneza vidonge”
“Unataka kutengeneza vidonge!?”
“Kwanini unaonyesha kushangaa ,ushasema mwenyewe vidonge ni muhimu katika kusaidia kupanda levo naweza nisihitaji mimi lakini warembo wangu nataka niwapatie ili viwasaidie”
“Ndio vidonge ni muhimu sana kwa wanaoanza mafunzo , lakini kuna mahitaji yake na kanuni za kutengeneza”
“Ndio maana nimekuja kwako nataka kujua hayo mahitaji”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kufikiria kidogo.
“Kama kweli una nia ya kutengeneza vidonge. kuna changamoto tatu ambazo unapaswa kuzivuka , Changamoto ya kwanza lazima upate mimea ambayo hutumika kutengenezea, hii sio rahisi kwasababu mimea hio ni adimu sana kupatikana na hata ile ambayo inatengeneza vidonge vya thamani kubwa imepotea kabisa, katika miliki za kijini kwenyewe huwezi kuipata hio mimea na ndio maana licha ya uwepo wa wenye ujuzi mkubwa wa kutengeneza wameishia kutengeneza vidonge vya kawaida tu”
“Lakini umesema kuna wanaokuja huku duniani kutafuta hio mimea ?”
“Ndio kuna wanaosafiri mpaka duniani kwa ajili ya kutafuta mimea ya kutengenezea vidonge lakini mara nyingi huishia maeneo ya karibu na bara la Asia , kwani wengi wao wanasema wanaogopa kuvunja sheria za the gods treaty”
“Kama ni hivyo basi uwezekano wa kupata hio mimea upo ,ninachotakiwa kufanya ni kutuma watu wangu wajaribu kufatilia, je ni wapi ambapo unaamini mimea hio inawezekana kupatikana?”
“Sina uhakika ila marra nyingi ni sehemu ambazo ustaarabu wa kale ulianzia kama vile Misri na maeneo mengine kama hayo”Aliongea na kumfanya Roma kutingisha kichwa kumuelewa.
“Vipi kuhusu changamoto inayofuatia?”
“That is even harder , You would need a high Quality Cauldron”Aliongea akimaanisha kwamba changamoto ya pili ni ngumu zaidi kwasababu atahitajika kuwa na Cauldron.
“Cauldron?”Roma aliuliza.
“Ndio Cauldron ni Dhana ambayo ipo mfano wa chungu kikubwa ambacho kimetengenezwa kwa madini maalumu ambayo yalipatikana enzi za kale,ni madini ambayo yana uwezo wa kuhimili kiwango kikubwa cha joto , kwa uelewa wangu katika miliki za kijini vipo vitano tu hivyo vyungu , Kekexil wanavyo vitatu ,ukoo wa wakwe zangu wanacho kimoja na Hongmeng wenyewe wanacho kimoja , kama kuna jamii nyingine ambazo wana aina hio ya chungu kinaweza kuwa nje ya matumizi hivyo haitokuwa rahisi”
“Changamoto ya tatu ni kuweza kudhibiti moto wa njano na mweupe ambao ndio hutumika kutengenezea hivyo vidonge kwa joto kubwa sana zaidi ya joto la kuyeyushia chuma na kubalansi na Chungu hiko”Chungu kinachozungumziwa hapo ni cha kijini ambacho ni kama Cauldron
“Changamoto ya tatu ya kudhibiti moto wa rangi ya njano na mweupe sio tatizo”
“Unamaanisha unao uwezo huo?”aliuliza huku akionyesha mshangao na Roma alitingisha kichwa.
“Kwanini hujazungumzia kuhusu andiko la kanuni za kutengenezea hizo dwa?”Aliuliza Roma akimaanisha andiko la kanuni alilopatiwa na Zenzhei.
“Kila koo ina kanuni zake , lakini ilisemekana mwanzoni Hongmeng walikuwa na andiko la kanuni ambayo hutengeneza vidonge vyenye uwezo mkubwa sana ,lakini bahati mbaya andiko hilo lilipotea, ndio ninachojua japo sina uhakika,lakini hilo lisikupe shida haina haja ya kuwa na hizo kanuni kikubwa ni namna ya kudhibiti joto la moto wa kichawi mweupe na wa njano ukishafanikisha kupata hiko Chungu”Aliongea
“Nitakuwa naendelea kuvuna nishati huku nikisubiria watu wangu waweze kutafuta hayo maeneo uliozungumzia , unaonaje kama wakifanikisha unisindikize”
“Mimi? , unamaanisha twende pamoja?”
“Ndio ,najua itakuwa usumbufu lakini siwezi kujua mimea inayohitajika nikienda mwenyewe”
“Lakini inawezekana ikawa ni mbali na Tanzani misituni huko”
“Usiwe na wasiwasi nishaishi sana msituni hivyo nina uzoefu wa kutosha”Aliongea Roma.
“Mimi sina tatizo lakini vipi mkeo anaweza akakasirika?”Aliongea kwa sauti ndogo huku akiona aibu.
Na kabla Roma hajajibu simu yake ilianza kuita na aliitoa na kuangalia mtu anaempigia na alishangaa ni Bi Wema , alipokea harakaharaka na kuweka sikioni.
“Mr Roma nadhani Miss Edna kapatwa na tatizo”
“Unamaanisha nini kapatwa na tatizo Bi Wema , nini kimetokea?”
“Amerudi kutoka kazini saa kumi kamili za jioni na akasema ana usingizi , amelala mpaka muda huu na nimejaribu kumuamsha haamki , Lanlan na yeye amejaribu kumuamsha kwa nguvu lakini hajashituka”Aliongea Bi Wema huku sauti yake ikionyesha wasiwasi na kumfanya Roma kuguna.
“Ana pumua?”
“Ndio kifua kinapanda na kushuka ndio hivyo haamki , nadhani ni vyema ukarudi umuangalie nina wasiwasi kwani sio kawaida mtu kulala na kushindwa kuamka”Aliongea Bi Wema na kumfanya Roma apumue kidogo kwa ahueni.
“Nakuja sasa hivi Bi Wema”Aliongea Roma na kisha akata simu.
“Nadhani mke wangu kapatwa na tatizo , ngoja niwahi”Aliongea Roma na Rufi alitingisha kichwa .
******
Afande CammiliusKweka alionekana kuathirika sana na taarifa ya Zenzhei kutaka kurudi Hongmeng , alijitahidi kuonyesha kuwa sawa lakini ukweli alikuwa akiumia kiume lakini hakuwa na uwezo wowote wa kumzuia kutoondoka kwani asingeweza kumlinda zidi ya Hongmeng.
“Zenzhei niseme asante sana’Aliongea Afande Kweka kwa sauti hafifu na muda huo ni kama masaa mawili mara baada ya Roma kuondoka.
“Camillius kwanini unanishukuru?”
“Asante sana kwa kwa kujjifanya kuwa mzee mbele ya macho ya watu ili mradi unilinde bila watu kukushitukia , asante kwa kufanya kazi za hapa kama vile ni mfanyakazi wa ndani , asante sana kwa kumfanya mke wangu kipindi kile kufa kifo cha amani”Aliongea Afande Kweka huku macho yakiwa makundu na hata Zenzhei mwenyewe alishindwa kujizuia na kudondosha chozi.
“Hupaswi kusema hivyo Cammilius ulikuwa ni wajibu wangu”
“Hapana, nimekukatili sana kwa kipindi chote ulichokuwa na mimi lakini bado nikakosa aibu na kuwa mbinafsi na kukufanya uendelee kuwa karibu yangu”
“Camillius usiongee hivyo nilikuwa na furaha kuishi na wewe”
“Zenzhei matumaini yangu ni kwamba hutonichukia , najua kwanini ulikaa na mimi kwa miaka mingi sana lakini nilishindwa kufanya chochote juu ya hisia zako kutokana na kukosa ujasiri , nilishindwa kuzipokea na mpaka sasa nashindwa kuzipokea licha ya uzee huu”Aliongea afande Kweka na kumfanya Zenzhei kufumba macho yake huku machozi yakimtoka.
Ni kweli alikuwa akimpenda Afande Camillius Kweka tokea mara ya kwanza walipokutana , lakini licha ya kuonyesha hisia zake kwa mzee huyo hakuchukua hatua yoyote na yeye kukosa ujasiri wa kuchukua hatua zaidi.
“Camilius kabla sijaondoka nitarudi kwenye mwonekano wangu wa mwanzo wakati tunakutana nadhani itakufanya usijione mwenye hatia” Aliongea Zenzhei na palepale mwili wake ulibadilika taratibu ,ilikuwa ikishangaza mno kwani ndani ya nusu dakika alibadilila na kuwa msichana kama wa miaka ishirini na nne mwanamwali , ilikuwa ni sahihi kusema alikuwa akifanana kabisa na Xiao Xiao japo yeye kidogo alikuwa na umbo la kuvutia na huenda angekutana na Roma angefanya jambo la kueleweka.
Ilionekana ili kuishi na Afande Kweka ilibidi ajizeeshe ili kuficha ujini wake , kwani kama asingefanya hivyo angebakia kuwa msichana mdogo ilihali Afande Kweka alikuwa anazeeka.
“Nakumbuka mara ya kwanza tulipokutana Sudani ulikuwa na miaka hamsini Camilius”Aliongea Zenzhei na sio sura tu iliobadilika hata sauti yake pia ilikuwa imebadilika.
“Haha.. bado urembo wako uko vilevile hakujabadilika chochote”Aliongea huku akitoa kicheko chenye machungu na kumfanya Zenzhei kutabasamu akikosa neno.
“Nadhani hii ni kwaheri ya moja kwa moja, naamini siku ukirudi nitakuwa tayari nimeshakufa”aliendelea kuongea na kumfanya Zenzhei kuingiwa na huzuni.
“Kwaheri ya kuonana Camilius” Aliongea Zenzhei.
“Kwaheri ya kuonana Zenzhei hakikisha unakuwa na maisha ya furaha na kutafuta mtu anaekupenda”
“Asante sana Camilius”Aliongea na kisha wakaangaliana usoni kwa madaki kakadhaa na Zenzhei alikosa ujasiri wa kuendelea kusimama mbele ya Camilius na palepale alipotea kwenye macho yake.Na hio ndio safari ya Zenzhei kurudi ujinini ikaanza rasmi.
Hatariiii
 
SEHEMU YA 493.
Roma kwanza baada ya kufika nyumbani alijaribu kumuasha Edna kwa njia ya kawaida kwa kumshitua , lakini ilionekana kweli Edna hakuwa akiamka na jambo hilo hata yeye kwake lilimshangaza.
Alianza kuukagua mwili wake kwa kuupiga X-Ray na nguvu zake za kijini na alionyesha kuwa sawa kiafya na hakuwa na shida yoyote lakini jambo moja kubwa tu la kushangaza ni mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi mno.
Roma aliamua kumuingizia nguvu ya kimaandiko ya urejesho kiasi kidogo akidhamiria kumuondolea uchomvu na baada ya kumaliza tu Edna alishituka kutoka usingizini na kufumbua macho yake taratibu..
Baada ya kushituka alionekana kushangaa Roma akiwa mbele yake na alianza kuangaza mazingira ya chumba, Roma alimwangalia kwanza pasipo ya kumuongelesha neno.
Edna mara baada ya kuangalia saa ya mshale iliokuwa kwenye meza alijikuta akishangaa na palepale alitoka kitandani na kusogelea dirisha na kisha akasukuma pazia na kuangalia nje.
“Roma nini kinaendelea mbona ni saa moja na nusu usiku sio asubuhi?”Aliuliza Edna huku akionyesha hali ya kuchanganyikiwa na kumfanya Roma hata yeye mwenyewe amshangae na kujiuliza mke wake kapatwa na nini au kuna kitu kilimpata.
“Mbona hunijibu sasa hivi ni saa ngapi?”Aliuliza kwa mara nyingine na Roma alimsogelea na kisha akamshika mkono na kumkalisha kwenye sofa alijua moja kwa moja huenda amemka na mawenge.
“Nini kimekuchosha kazini mpaka ukapatwa na usingizi mzito mpaka unatia watu wasiwasi?”Aliuliza Roma lakini Edna alishindwa kujibu na haikueleweka alikuwa akifikiria nini kwenye kichwa chake na hata Roma alishindwa kumuelewa.
Edna katika uhalisia tukio la mwisho ambalo alikumbuka ni usiku wa jana yake muda ambao alikuwa akimwangalia Lanlan uso wake wakati wote wakiwa kitandani na hata muda ambao alipotelea usingizini hakukumbuka na matukio yaliotokea siku nzima mara baada ya kuamka asubuhi kwake ilikuwa ni kama ndoto na ndio kwanza ameshituka kutoka usingizini akitarajia muda huo iwe ni asubuhi.
Roma kuna kitu alihisi sio cha kawaida na palepale alimsogelea Edna na kumshika mabega.
“Edna niangalie usoni”Aliongea Roma na Edna alimwangalia Roma kwa namna ya kuchanganyikiwa na upande wa Roma alichokuwa akidhamiria ni kutaka kuangalia kiini cha macho ya Edna , kuna jambo alihisi ndio maana alitaka kufanya hivyo.
“Edna niambie umeota nini?”Aliongea Roma mara baada ya kuona kitu ambacho alikuwa akikitafuta kwenye macho yake.
“Edna unakumbuka ulichokiota?”Aliuliza Roma kwa mara nyingine mara baada ya kuona Edna hatoi majibu na Edna alitingisha kichwa kama anakumbuka alichokiota na Roma alijikuta akipata ahueni na kukaa kwenye sofa pembeni yake.
“Anza kukumbuka taratibu taratibu na unifahamishe ulichoota katika mtiririko wa matukio?”Aliongea.
********
Ndoto yake ilianzia asubuhi ,alianza na taratibu zake za kawaida za kila siku kama ilivyozoeleka na hata muda ambao alikutana na wanafamilia na kuwasalimia hakuna ambaye alijua mwenzao anaota.
Edna siku hio ndio aliemsindikiza Lanlan mpaka barabarani na kuchukuliwa na bus lao la shule na baada ya hapo alirudi ndani na akajiandaa na akaelekea kazini kama kawaida na baada ya kuingia ndani ya jengo la makao makuu ya kampuni alisalimiana na wafanyakazi baadhi aliokutana nao njiani , akiwemo Dorisi , Nasra na Benadetha.
Na kila kitu kilikuwa sawa kabisa , bado hakuna aliejua kabisa Edna akili yake muda huo ilikuwa chini ya utawala wa mtu mwingine na alichokuwa akikiona kwake ni kama ndoto.
Baada ya kuingia kwenye ofisi yake Recho msaidizi wake aliingia na kisha akamsomea ratiba zake za siku hio kwanzia asubuhi mpaka muda wa kutoka kazini na baada ya kuridhika akampa maagizo ya kazi ambazo anapawa kufanya kwa siku hio na kisha akatoka.
Baada ya kufanya kazi kama nusu saa tu mlango uligongwa na akaruhusu mgongaji kuingia na alikuwa ni Recho ambaye mkononi alionekana kushikilia Parcel iliofungwa kwa karatasi za Khaki.
“Boss kuna mzigo wako umefikia kutoka mapokezi”Aliongea Recho kwa heshima na Edna alimpa ishara amfikishie mezani kwake.
Baada ya kupokea kwanza alianza kusoma anuani ya mzigo huo na hakika yeye ndio aliekuwa mlengwa kwani jina lake liliandikwa kwa usahihi na mahali ambapo mzigo ulipaswa kufika, lakini kati ya mizigo mingi ambayo anapokea huu ndio mzigo ambao haukuwa na jina la mtu alietuma.
“Unaweza kwenda” Aliongea na kumfanya Recho kuinamisha kichwa na kisha akatoka ndani ya ofisi hio na Edna alichana ile bahasha ili kuangalia nini kipo ndani yake na hapo ndipo alipokutana na kiboksi cha rangi nyeusi , vilikuwa ni viboksi ambavyo alikuwa akivifahamu vinahifadhia vito vya thamanni kwa mfano pete , mikufu na Saa.
Alishangaa kupokea mzigo wa aina hio ambao ulitoka kwa mtu ambaye hajaweka jina lake wazi , lakini kwakuwa alikuwa na shauku ya kutaka kujua nini kipo ndani yake , hakutaka kupoteza muda bali alifungua ndani na kuangalia na hapo ndipo alipojikuta akitoa macho mara baada ya kuona pete.
“Hii petee…!!”Alijikuta akikosa neno la kuongea na kuitoa taratibu na kuishika na mkono wake wa kulia na kuanza kuiangalia kwa namna ya kuichunguza.
Ni pete ambayo ilikuwa mpya kwenye macho yake lakini kwa wakati mmoja haikumshangaza, kwake ilikuwa ni kama pete ambayo ashawahi kuimiliki katika nyakati ambazo ni kama amezisahau kwenye maisha yake na baada ya kuiona ni kama kumbukumbu zilikuwa zikija na kupotea.
Aliiangalia kwa muda kama wa nusu saa kwa kuichunguza mpaka muda ambao Recho aliingia tena kwenye ofisi yake na kumjulisha dakika kumi tano zijazo atakuwa na kikao na idara ya uhasibu na mipango na taarifa hio ilimfanya airudishe ile pete kwenye kijiboksi chake na kisha kaweka kiboksi kile ndani ya mkoba wake na akageukia tarakishi yake na kuanza kusoma baadhi ya taarifa ambazo alipaswa kuzi ‘adress’ siku hio kwenye kikao cha asubuhi.
Kwa kawaida Edna hufanya vikao viwili mpaka vitatu kwa siku hivyo mpaka inafika muda wa mchana alikuwa alishakamilisha taratibu zote za kawaida na kutoa maagizo na ratiba iliokuwa imebaki ni moja tu ya saa tisa kamili,ambayo alipaswa kwenda kuonana na Tajiri Khalifa akiwa yeye na Suzzane.
*******
Edna alikuwa akimuelezea Roma kuhusu ndoto yake , lakini kwa wakati mmoja alihisi kile alichokielezea ni kama kumbukumbu , ilikuwa ni kama mgonjwa ambaye amepoteza kumbukumbu na sasa ndio zinaanza kurejea ndio kilichokuwa kikiendelea katika kichwa chake kadri alivyokuwa akisimulia.
Upande wa Roma kuna jambo ambalo sio la kawaida amegundua kupitia macho ya Edna na hata kumwambia amuelezee upya kile alichokiota alikuwa na maana yake.
Mpaka Edna anakuja kumaliza aliweza sasa kuona hakuwa ndotoni na kila kitu alikifanya katika uhalisia , hata ile hali ya kuchanganyikiwa ilianza kupotea ,alianza kushangaa nini kimetokea kwani dakika zilizopita nyuma alijihisi kama alikuwa ndotoni na baada ya kurudia kumuelezea Roma kile alichokiota kila kitu kiligeuka kuwa uhalisia kwa kumbukumbu zake kukaa sawa.
“Ikiwa mtu umeshikiliwa ufahamu na uhalisia kugeuka ndoto, ili kutoka kwenye mtego unachotakiwa kufanya ni kukumbuka mwanzo na mwisho”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutokumuelewa..

“Unamaanisha nini kushikiliwa ufahamu?”
“Sasa hivi unajionaje , unahisi ulichonielezea ni ndoto?”Aliuliza Roma akipotezea swali lake.
“Sijui hata nini kinanitokea?”Aliongea huku akionekana kuchanganyikiwa kuna baadhi ya vitu hakuweza kuelewa , hata kama kile alichohadithia hakikuwa ndoto kwanini alifanya baadhi ya vitu bila ya uelewa wake.
Roma alijua Edna atakuwa mwenye kuchanganyikiwa na hakutaka kumuona akizidi kuumiza kichwa. alichokifanya ni kumshika mkono na kumpitishia nguvu ya kijini ambayo ilimfanya Edna kuegamia kwenye sofa na kupotelea usingizini kwa mara nyingine.
Baada ya kulala alimbeba na kumlaza kitandani na kisha akasogelea mkoba wake alioenda nao kazini.
Katika maelezo ya Edna alisikia neno pete na ndio ambacho alitaka kutafuta na aliweza kuona boksi la rangi nyeusi ndani ya mkoba wake na akahisi huenda ndio ambao alikuwa amezungumzia.
Mpaka hapo Roma alishajua mke wake siku hio kuna mtu alimchezea kwa kushikilia ufahamu wake na alijiambia hatua yakwanza kuthibitisha kile kilichotokea ni kuanza na ushahidi wa pete ambayo alizungumzia.
Katika maisha Roma alishapitia vitu vingi vya ajabu ambavyo vingi kwa binadamu wa kawaida vilikuwa ni vya kustaajabisha , hivyo hata swala la Edna halikumshangaza bali lilimuacha na maswali mengi.
Roma mara baada ya kufungua kijiboksi alichokuta katika mkoba wa Edna aliona sio kile ambacho anatafuta , kiboksi alichotoa kilikuwa kina saa ya pocket watch ambayo alimpatia Edna na ilionekana Edna alitengnenezea boksi lake ili kuitunza.
Roma aliangalia uwepo wa kitu kingine ambacho kingeendana na maelezo ya Edna lakini hakuona kitu na alijiuliza pete aliokuwa akizungumzia iko wapi.
Mpaka hapo aliona njia pekee ya kupata kufahamu ukweli ni kwa kumtumia Nadia Alfonso na Suzzane kwani katika maelezo ya Edna mtu ambaye alimtambua ni Nadia Alfonso na Suzzane
Roma alitoa simu yake na kisha akapiga na ndani ya muda mchache tu iliweza kuita na kisha ikapokelewa na Roma alimuuliza Nadia yupo wapi muda huo na alijibiwa yupo Mbezi Beach nyumbani kwake.
Roma alifikiria kwa dakika na kuona haina haja ya kuonana na Nadia usiku huo aliona aonane nae kesho, alihofia jambo baya kumpata tena Edna na ndio maana alitaka kuchukua tahadhari kwa kubakia nyumbani.
Baada ya Nadia kumkubalia waweze kuonana kesho alikata simu mara moja na kisha akatoka ndani ya chumba hicho na kushuka chini sebuleni , alipaswa pia kumtoa Bi Wema hofu ya kile kilichotokea.
Alijua Edna alipatwa na shida lakini hakuwa na mpango wa kuwaelezea kila kitu kilichotokea kwa kuhofia kuwachanganya na wangeshindwa pia kumuelewa.
“Roma ameamka?”
“Ndio Bi Wema usiwe na wasiwasi , inaonekana alikuwa na uchomvu sana”Aliongea Roma na sababu yake haikumwingia akilini Bi Wema lakini alishindwa kuhoji , kwenye maisha yake hajawahi kumuona Edna akalala muda mrefu tena fofo na kushindwa hata kushituka.
“Lanlan unachora nini?”Aliuliza Roma mara baada kumuona Lanlan akiwa bize kuchota na kalamu zake za rangi, namna ambavyo alikuwa bize ilimfurahisha Roma.
“Lanlan anachora wanafamilia”Aliongea na kumfanya Roma amsogelee na kutaka kuangalia hao wanafamilia lakini Lanlan alificha akimzuia Roma asione.
“Hutaki baba wa familia kuona eh , unachora wanafamilia gani hao”
“Mama ndio wa kwanza kuona , Lanlan amemchora mama kwanza”Aliongea na kumfanya Roma atabasamu kwa uchungu maana katika maisha ya Lanlan mama yake ndio kitu cha kwanza na wengine wote walikuwa wa ziada.
Asichokijua Roma Lanlan maisha yake yote alilelewa na mama ndio maana kwake ndio kipaumbele na baba na wengine ni wa ziada tu.
Lakini hata hivyo Roma alifurahia uwepo wake hapo nyumbani na hata kushikwa na tamaa zaidi ya kupata watoto na wazo hilo lilimfanya akumbuke hajawasiliana na Sauroni juu ya kuwapa maelekezo baadhi ya vijana wake kutafuta maeneo ya kale ambayo wameishi watu na kwa muda huo yametelekezwa.
Kwa maelezo ya Rufi hizo ndio sifa ambazo aliamini mimea ambayo ingeweza kutengeneza vidonge vya kijini ingepatikana.
Baada ya kuongea kwa madakika kadhaa na Sauroni kwa lugha ya kilatini ulikuwa ni muda ambao na chakula kishaiva na Lanlan ndio aliekuwa wa kwanza kukusanya kila alichokuwa akikifanya na kukimbilia mezani na kukalia kiti chake cha siku zote , alikuwa na kiti chake ambacho hakutaka kikaliwe na mtu na kama atakuta mtu amekaa anasimama pembeni halafu anajinunisha, tabia yake iliwafanya wanafamilia kuwa na tahadhari na kiti chake.
Wakati Roma anapanga kupandisha juu kumuamsha Edna alishangaa kumuona akishuka yeye mwenyewe na ilionyesha amaamka muda, Roma alimwangalia kwa macho ya kumkagua na Edna alimwangalia Roma kwa dakika na kisha bila ya kuongea neno alitembea mpaka jikoni.
Roma alijiambia ili kuhakikisha usalama wa mke wake lazima achimbe ajue ukweli nini kilichomtokea siku hio nzima kuna hisia zilimwambia huenda ni Hermes aliefanya kitendo hiko , lakini alikosa sababu za msingi za kumshuku.
Roma alikuwa akielewa jicho ni dirisha la nafsi na alielewa iwapo binadamu atavamiwa na nguvu ya ziada na nguvu hio ikataka kuukimbia mwili basi sehemu pekee ambayo huacha alama ni kwenye macho na ndio maana aliyachunguza macho ya Edna na kuweza kugundua mara moja akili yake ilikuwa imetawaliwa kichawi na kitendo cha kulala muda mrefu bila kushituka ilimpa uthibitisho wa kipi kilimtokea na ndio maana alitaka Edna kusimulia kila kitu ambacho alihisi alikuwa akiota , ilikuwa mbinu ya kumuweka Edna sawa kiakili ili asisahau kilichotokea.
“Bi Wema simuoni Mama”
“Karudi mchana na kuaga anaenda nyumbani kumuangalia baba mzazi , kasema atarudi kesho”
“Ah.!”Aliongea na kisha akamgeukia Roma.
“Roma unaonaje tukimtembelea Babu Atanasi , najua tokea mara ya mwisho kumuona hujawahi kwenda tena”Alipendekeza Edna.
“Hata mimi naunga mkono hoja ni wazo zuri na Lanlan pia ataweza kumuona babu yake”Aliongea Bi Wema na Roma aliona Edna alipendekeza jambo zuri na alijishangaa siku zote hakuwahi kuwa na mawazo ya kwenda kumsalimia.
………….
Siku iliofuata Roma alimpigia simu Nadia Alfonso ili kujua wanaonana saa ngapi kwani jioni ya siku hio alipaswa kwenda kumsalimia Mzee Atanasi.
Edna yeye siku hio ya jumamosi hakutoka kwenda kazini na Roma aliona amefanya maamuzi mazuri.
Ukweli sio kwamba Edna hakutaka kwenda kazini lakini ni alikuwa amechanganyikiwa na kila kitu kilichotokea jana yake na aliamini hata kama angeenda kazini angekuwa kwenye mawazo.
********
Upande mwingine katika hoteli ya Maple iliopo Kunduchi a alionekana Prince Rapahaeli akiwa amekaa kwa kujiachia kwenye sofa huku akiwa ameshikilia Kishikwambi cha kampuni ya Appple,alionekana kuna mtu aliekuwa akiongea nae kwa njia ya Vidio call huku akicheka.
Sura iliokuwa ikionekana kwenye skrini ni ya mwanaume alievalia kikofia cha rangi nyeupe na Apron pia ya rangi nyeupe na shati la rangi nyeusi ndani yake.
“Unaniuliza maswala ya vyakula kama vile unapendelea , nipe mrejesho wa kilichokupeleka Tanzania”
“Kwanini siku hizi una shauku ya kila ninachokifanya”
“Sina shauku ya kufahamu unachokifanya ila nataka kujua kwani ni maswala yanayonihusu”
“Kama yanakuhusu unapaswa kuhusika kuliko kuwa mnafiki”
“Hahaha….Uniambie usiniambie najua mwisho wa siku lazima utahitaji msaada wangu na sio kwangu tu wote tuliobakia”
“Unamaanisha nini kuhusu kuomba msaada?”
“Najua mipango ya Athena ya kufufua roho ya Gaia ili kuweza kuamsha roho za ndugu zetu zilizomezwa na binadamu lakini unafikiri kwa teknolojia iliopo kwa sasa atafanikisha, lazima atahitaji msaada wetu”Aliongea kwa kijerumani na kumfanya Prince Raphaeli kukaa vizuri kwenye sofa.
“Lakini hatufahamu wapi Zeusi alificha jiwe lenye Roho yake mpaka sasa na imetuchukua miaka mingi kutafuta sana kati ya binadamu”
“Nikajua unaamini unabii Hermes”.
“Unabii ule niliacha kuamini muda mrefu lakini Athena bado anaamini Hades ndio njia ya kufanikisha kuupata moyo wake”
“Haha.. wewe ni mnafiki sana Hermes kama upoTanzania kwa maagizo ya dada yako basi ni dhahiri bado unaamini unabii”..
“Haijalishi najali kuhusu unabii au lah , kwangu mimi matokeo ni muhimu”
“Nieleze kwanza matokeo uliyoyafanikisha kwa Persephone , ninashauku ya kufahamu”
“Kuna kitu hakipo sawa kwa Persephone, ni binadamu wa kwanza nilietumia nguvu nyingi sana kuidhibiti akili yake”.
“Niambie zaidi , ni kipi kimetokea?”
“Poseidon kwanini unashauku sana na Persephone”
“Nielezee bwana unaelewa kwanini nina shauku ya kujua”Aliongea na kumfanya Hermes kufikiria kidogo kama mtu anaetafuta maneno ya kuongea na kumfanya Poseidon kumwangalia kwa shauku.
“Unajua mbinu pekee ya kutawala ufahamu wa mtu ni kupitia mawazo yake mwenyewe?”
“Hilo naelewa”
“Kazi niliopaswa kufanya ilikuwa ni kuhakikisha anatambulika kama kiongozi wa ant-illuminat kama mbadala wa Seventeen na kazi yangu kubwa ilikuwa ni kutumia akili yake kumthibitisha lakini jambo la kushangaza nilifanikisha kuyatawala mawazo yake kwa muda mrefu lakini nilifeli kutawala namna anavyopaswa kuongea na wanachama mara baada ya kuonyesha Pete ya Muhuri wa uongozi”
“What …!!”Alishangaa.
“Ilikuwa ni kama kuna nafsi nyingine iliojificha ndani yake, wakati nikiwa nimeshikilia nafsi yake nikashindwa kuzuia nyingine kuchukua nafasi yake”
“Kwahio unamaanisha kuna nafsi inautawala mwili wake bila yeye kufahamu”
“Ndio na kitendo cha kutumia nguvu nyingi kutawala mwili wake naamini ndio chanzo kilichoamsha nafsi yake nyinginew, lakini bahari nzuri tulichotaka kilifanikiwa na sasa ataweza kurithi nafasi ya pacha wake”Aliongea na kumfanya Poseidon kufikiria kidogo.
“?Kwanini usingejaribu kusoma mawazo yake huenda ungejua nafsi yake nyingine iliolala”
“Nilijaribu kwa kumfanya alale usingizi mzito ili kutafuta kumbukumbu zinazohusiana na nafsi hio lakini sikuambulia chochote , yuko imara kuliko isivyokuwa kwa binadamu wa kawaida”
“Na Athana anasema nini juu ya hilo ?”
“Unafikiri angejibu nini?”
“Haha,,, naona lazima amesema kila kitu kipo chini ya udhibiti wake”
“Hakika ndio jibu ambalo amenipatia” Aliongea na wakaanza kucheka tena.









SEHEMU YA 494.
Saa tano kamili Roma aliweza kufika nyumbani kwa Nadia,ilikuwa mara yake kufika hapo na kulikuwa na umbali mfupi sana kutoka nyumba ya Amina ilipo, hivyo ilikuwa ni kamaa majirani tu.
Nadia ilionekana alikuwa na furaha sana na ujio wa Roma, mwanadada huyu mrembo mwenye rangi ya kibantu mapenzi yake kwa Roma huwa hayapimiki na siku zote alijiambia kadri atakavyokuwa chini ya kundi la Ant-Illuminat ndio Roma atazidi kumuhitaji na itatokea tu siku akaja kuwa sehemu ya wapenzi wake.
“Hili jumba ni zuri hongera sana”
“Mafanikio yangu kama mwanasheria yamefikia hapa kwasababu yako”Aliongea huku akiwa anatabasamu na Roma alitoa tabasamu hafifu na kuketi.
“Vipi mgeni nikuletee maji , juisi au bia”
“Niko vizuri unaonaje ukaketi ili tuongee”Aliongea Roma na kumfanya Nadia kumwangalia kwa muda na kisha akatoa tabasamu hafifu na kwenda kukaa mbele ya Roma na kukunja nne na kufanya kigauni chake kuyaacha mapaja yake wazi na Roma hakutaka kuyakodolea macho maana alikuwa akijua nini kingetokea kama angejihusisha na Nadia.
“Nataka kujua kwanini jana mlimwita mke wangu kwenye kikao chenu bila kumjuza mapema”Aliongea Roma huku akiweka usiriasi.
“Hata mimi nilishangaa kumuona mkeo Edna kujitambulisha kama kiongozi wetu”
“Unamaanisha nini?”
“Nimepewa ruhusa ya kujibu maswali yako yote utakayo uliza , nikianza na swali lako ujio wa Edna kwenye kikao chetu haukuwa wa bahati mbaya na hilo nilijua mara baada ya kikao kuisha …..”Alianza kuongea kwa kumuelezea juu ya hitimisho lililofanyika juu ya uchunguzi wa sababu ya Chriss kutaka kumuua Edna.
Na kwa maelezo yake anamwambia Roma Chriss aliacha ujumbe ambao unamuonyesha Edna ndio kiongozi wa jamii yao ya siri na uwepo wa mchoro wa unabii ambao bado hawajapata kuuona.
Maelezo yalimshangaza Roma kwasababu moja Chriss alifikishwa Vatican na Hades wa zamani na kwa haraka haraka aliamini kuna misheni ambayo alipewa kufanya ndani ya nchi hio ndogo ya kikanisa.
Kwa maelezo ya Nadia Roma aliona anapapaswa kuanza kuchukulia siriasi ya kile kinachoendelea kama anataka kumlinda mke wake.
Ukweli Roma hakutaka kujihusisha na maswala ya ulimwengu tena kwasababu alitaka amani, katika maisha yake aliamini kadri atakavyoingilia mambo yaliokaa kisasa ataishia kutengeneza maadui wengi kwani asingevumilia propaganda na uongo.
Roma imani yake kubwa ilikuwa ni kuilinda familia yake isipatwe na shida yoyote na sio kujiingiza kwenye mambo ya kibinadamu ambayo yalikaa kisiasa zaidi.
“Roma kuna mambo mengine unaweza kusema hayakuhusu , lakini kadri yanavyojikusanya na kuwa makubwa yatakuletea athari”
“Nadia unahisi kuna mambo gani ambayo unaona yananihusu na nayapotezea?”
“Kwa mfano Edna alitaka kushambuliwa na Chriss ni juhudi ganii ambazo umefanya kujua ukweli wa kile kilichotokea au ni dhamira gani ambayo imempelekea kuamua kufanya vile? Ungeujua ukweli itakuwa rahisi zaidi kumlinda”
“Kuna mambo mengine sio ya kutumia nguvu kuyafuatilia nikitaka kufuatlia kila kinachoendelea dunia hii unafikiri nitaweza kuishi kwa amani”
“Lakini kuna vitu vingine sio vya kupotezea kabisa”Aliongea na kumfanya Roma kukuna kichwa na kujiambia Nadia anamjua nini yeye , mpaka muda huo alikuwa akijitahidi sana kuiheshimu mipaka yake kisheria na ndio maana hakupenda kuungana na upande wowote.
“Kwahio mnamdhania mke wangu ni kiongozi wenu?”
“Jana ilikuwa ni hatua ya kwanza ya kumtambua kiongozi na nilichoweza kusikia kuna zaidi ya hatua tano na kama Edna ni kiongozi wetu kweli atatimiza hatua zote tano, Roma umoja wetu ni mkubwa sana na watu ambao Edna amekutana nao jana ni wawakilishi tu”
“Sitaki kuwaingilia sana na kile mnachokifanya na ndio maana sijataka hata kuyafahamu malengo yenu , Edna ni mke wangu mimi na sio kiongozi na kama mnatarajia kuona akifanikisha hatua zote tao mtapoteza muda”Aliongea Roma.
Kuna kitu hata hivyo kilikuwa kimfikirisha na aliamini Nadia asingekuwa na majibu anaoyataka.
Mchoro wa unabii alihitaji kuuona lakini kitu kingine alihitaji kujua nani ambaye jana alimteka kiakili mke wake na kumfanya akajitambulisha mbele ya watu ambao hata hawafahamu.
"Kwasasa siwezi kusema neno lolote kwani uchunguzi wangu haujakamilika ila nawatahadhalisha muwe makini na mnachokifanya , inaonekana kuna watu wanaona kila kitu"Aliongea Roma na kuzidi kumchanganya Nadia.
“Unamaanisha nini kusema kuna watu wanaona kila tunachofanya?”Aliuliza lakini Roma alitingisha mabega kama hajui na kumfanya Nadia kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha
"Nadia kwa leo nishasikia nilichotaka kusikia na kabla sijaondoka nataka nikuombe uniambie kitakachojili mkipata huo mchoro wa unabii"
"Unataka niwe shushu wako??
"Mbona unafikiria mbali ninachotaka ni taarifa moja tu ambayo ni hio ya mchoro , ili niweze kujua kama unamuhusu mke wangu".
"Nipo tayari kuwa spy kwa ajili yako" Aliongea huku akitabasamu kimadaha , alijiambia ndio, hivyo ndio alikuwa akitaka , aliamini lazima Roma kuna siku atataka kujua kile kinachoendelea katika jumuia yao ya siri na mtu wa karibu ambaye anaweza kumuomba taarifa ni yeye, umoja wa kundi hilo hata hivyo malengo yake yalikuwa ni kunsaidia yeye mwenyewe huko mbeleni kushindana na uovu , alijiambia kama kwa kutumia sheria imeshindikana kumuweka Roma karibu basi atatumia njia nyingine.
"Nadia unajua maana ya kuwa Spy ??"
"Spy ni neno lenye maana kubwa katika ujasusi na kazi ambayo unataka nikusaidie kufanya haiko mbali na U spy"Aliongea na kumfanya Roma ashindwe kujua hata namna ya kumjibu alitaka kujua kuhusu mchoro huo wa unabii unahusiana vipi na Edna.
Roma alianza kujifikiria na kuona kama mchoro huo kweli upo, na Chriss aliweza kuuona moja kwa moja alijiambia kuna jamii nyingine ya siri ambayo imeuona pia na huenda ndio maana wakataka kumuua Edna.
Siku ile wakati anapata taarifa juu ya kile kilichomkuta Chriss kwa Athena kumlinda mke wake alijua huenda ni swala ambalo linahusiana na mpango LADO na ndio maana alikuwa makini katika kulishughulikia swala hilo , hata hivyo mpango LADO ulikuwa ukimuhusu yeye na Seventeen.
Roma alijiambia kuna kitu alikuwa akipotezea kukifanyia kazi na huo ndio muda muafaka.
“Nadia sitaki uwe shushu kwa ajili yangu , mpaka sasa nakuona upo kwenye hatari na kadri unavyojihusha na jamii hio unakuwa adui mlengwa na jamii nyingine ambayo mnaenda nazo kinyume na mimi sitoweza kukupaatia ulinzi kwani sitaki kuongeza maadui”Aliongea Roma na kumfanya Nadia ile sura yake iliopambwa na tabasamu kupotea.
“Nitakuambia nikipata taarifa yoyote inayohhusiana na mkeo usijali sana kuhusu usalama wangu kwani hata hivyo sio kama wewe ni boyfriend wangu?”Aliongea na kumfanya Roma atingishe kichwa kukubaliana nae tokea afahamiane na Nadia miaka mingi iliopita hakuwahi kumuomba msaada na huenda hio ndio siku ya kwanza kwake na aliona huenda ndio maana Nadia alitaka kumsaidia kazi yake ingali ya uhatari wenyewe lakini alishangazwa na maneno yake yaliokaa kimitego.
“Utafanya nini kuhusu mchoro maana sio rahisi kuupata”
“Chriss amewaambia ili kujua uhalali wa kiongozi wenu ni kutumia mchoro huo wa unabii si ndio?”Aliuliza Roma.
“Ndio barua yake ilivyoweka wazi”
“Mnafahamu Chriss ni jamii gani ya siri aliokuwa akijihusisha nayo?”Aliuliza Roma.
“Hilo hatufahamu na tunalifanyia kazi”.Aliongea na kumfanya Roma afikiria kitu na kisha akasimama.
“Unaondoka?”
“Ndio kilichonileta nishakipata”
“Ah.. nikajua unakaa kaa”Aliongea kwa sauti ya chini na kumfanya Roma amwangalie Nadia kwa kumchunguza na kisha akaona ni muda muafaka wa kuaga na kisha akaondoka akisindikizwa na Nadia mpaka nje.
Mara baada ya kutoa gari Nadia alitoa tabasamu hafifu na kisha akarudi ndani na kuchukua simu yake na akaingiza namba kwa kuziandika na kisha akapiga.
“Umefanikiwa kuongea nae”
“Ndio nimemaliza maongezi na nimemwambia kila kitu kilichotokea inaonekana ni kweli kama mlivyodhania”
“Amesemaje kuhusu mchoro wa unabii?”
“Hajaongea chochote kuhusu mchoro ila ameonyesha kuvutiwa na taarifa hio”
“Kama ameonyesha kuvutiwa hiko ndio tulichokuwa tukitaka ,kwasasa utabakia Tanzania hakikisha unajenga ukaribu na Edna”
“Sawa Madam”Aliitikia na kisha simu ilikatwa.
Roma baada ya kutoka nyumbani kwa Nadia akili yake ilimwambia aende kwanza Kigamboni kuonana na Diego kabisa ana kwa ana , alihitaji kujua uchunguzi kuhusu Chriss ulifikia wapi.
Roma mambo mengine hakuwa na haja ya kuyatolea maagizo na wanajeshi wake wenyewe walipaswa kujiongeza hivyo hata swala la Chriss sio kama halikuwa likifanyiwa uchunguzi ila ni kwamba uchunguzi ulikuwa ukiendelea na ulichukua muda mrefu kutokana na Chriss kutojulikana mahali alipoishi kwamuda mrefu hivyo taarifa zake kuwa ngumu kupatikans
Roma hakutana kuamini moja kwa moja kama Raisi mstaafu waMarekani ndio alitaka kumuua Edna kwa kumtumia Chriss alitaka kwanza ushahidi wa kueleweka ndio aweze kuchukua hatua, hata hivyo Raisi Barrack Mabo katika ile sauti ambayo ilirekodiwa hakuwa akiongea kuhusu Edna kuuwawa tu lakini pia alionyesha alihusika katika mpango LADO na ndio maana Roma alijiambia anapaswa kuwa makini.
Baada ya dakika kama arobaini na tano aliweza kufika Kigamboni Mbutu na kuingiza gari ndani ya geti na alipokelewa na Diego.
“Mfalme Pluto sikutegemea ungetutembelea leo”Aliongea na kumfanya Roma kuona kweli alikuwa na siku nyingi hajafika hapo.Alianza kukagua mazingira na kuona hakuna kilichobadilika.
“Hii sehemu imetulia sana Diego”
“Ndio mfalme Pluto kila mmoja ametawanyika kwenda kutimiza wajibu wake na kwasasa yupo Bram na mimi hapa ndani”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa wanajeshi wa The Eagles waliongezeka na kuwa wengi ,inakuwaje wote wakawa wametawanyika kwenda kwenye majukumu.
“Kuna kazi ya ziada ambayo Sauron amewapatia kuifanyia kazi?”
“Ndio mfalme Pluto nilipaswa kutoa ripoti baada ya kukamilika”
“Inahusiana na nini?”
“Zeros organisation!!!”Aliongea Diego na kumfanya Roma asimame mbele ya mlango na kumwangalia Diego.
“Ndio mfalme Pluto mwezi uliopita tulipata ‘intel’ ya kufuatilia taarifa zinazomuhusu Joseph Bikindi”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuvutiwa na maongezi na aliingia ndani kwanza ili aweze kupata kumsikiliza vizuri.
“Joseph Bikindi ni nani na anahusiana vipi na Zeros organisation?”Aliuliza Roma maana alishindwa kukumbuka jina lake na muda uleule na Bram alievalia Headphone alitokeza na kumsalimia Roma.
Na kisha wote waliingia kwenye chumba cha kuendeshea mitambo yao ya kuchakata taarifa.
“Mfalme Pluto hii ni picha ya Joseph Bikindi”Aliongea Diego na Roma aliweza kuona picha ya mwanaume mweusi alievalia Jacketi la baridi na boshori ni picha ambayo ilikuwa ikimuonyesha akiwa kwenye mandhari yake ya miti iliofunikwa na barafu na aliweza kugundua eneo hilo kwa harak.
Roma baada ya kuangalia picha hio kwa umakini aliona kama sura inakuja na kupotea ni kama alishawahi kukutana na mtu huyo lakini alimsahau .
“Mfalme hii ni picha nyingine iliopigwa hivi karibuni’Aliongea Diego na kisha Bram akaonyesha picha nyingine ambayo ya wakati huu ilikuwa na sura za watu wawili ambao alikuwa akiwatambua.
Ilikuwa ni picha ya Kizwe na Lekcha wakiwa na mwonekano ambao aliweza kuutambua , haraka haraka kumbukumbu zake zilimrudisha siku ambayo alikutana na Lekcha Club B akiwa na kizwe , siku kadhaa mara baada ya kumfanya Kizwe abakwe na mafukara.
“Mfalme Pluto umegundua nini kwenye hii picha?”Aliuliza Deigo na Bram alirudisha picha ya mwanaume wa kwanza ambayo alimuonyesha na palepale sasa aliweza kuelewa Joseph Bikindi aliekuwa kwenye picha yenye mandhari ya eneo lenye barafu alikuwa ni mwanaume aliemuona ameambatana na Kizwe.
Kwa maelezo ya Diego ni kwamba walipokea taarifa ya kufatilia taarifa za Joseph Bikindi na hata picha ambayo alimuonyesha Roma ilitumwa kwao na mtu ambaye hakufahamika.
Na baada ya kufanya uchunguzi ndipo walipoweza kugundua Joseph Bikindi alikuwa nchini Tanzania muda mrefu akijifanyisha ni fukara ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kuokota makopo huku akifahamika kwajina maarufu la Lekcha.
Kilichomshangaza Roma zaidi ni pale alipoambiwa Lekcha aliishi kwenye chumba chake yeye ambacho alitumia kabla ya kukutana na Edna , haraka haraka kwa maelezo hayo alihisi haikuwa bahati mbaya.
“Imekuwaje mkamuunganisha Jospeh Bikindi na Zeros organisation?”Aliuliza Roma.
“Mfalme kupitia hii picha ndio tuligundua Joseph sio mtu wa kawaida”Aliongea Diego na kumfanya Roma aiangalie , ni picha ambayo ilikuwa ikimuonyesha mwanaume wa kizungu aliekuwa kwenye gari katika msururu foleni ya magari akiwa ameshusha kioo akimwangalia omba omba mmoja akiwa amenyoosha mkono kama vile anasaidiwa kitu na yule mzungu.
“Huyo anaetoa msaada mfalme Pluto anafahamika kwa jina la Efani Trudman ni ajent wa siri wa kundi la Dhoruba nyekundu lakini pia ni mwanasayansi kitengo cha utafiti katika kampuni ya J&J kampuni ambayo Joseph Bikindi katika CV yake inaonyesha alifanya kazi hapo kabla ya kufukuzwa”Aliongea na kisha akatoa taarifa zote ambazo zilikuwa zikihusu taaluma ya Joseph Bikindi na Roma alishangaa zaidi baada ya kuona Lekcha alikuwa msomi wa kiwango cha juu.
“Kwanini alifukuzwa kazi?”
“Mfalme Pluto kama nilivyosema bado tunaendelea kufanya uchunguzi lakini wiki iliopita tuliweza kupata ufunuo ambao umetuaminisha moja kwa moja huenda ndio sababu ambayo imemfukuzisha kazi”Aliongea na kisha akapozi na kumpa ishara Bram na palepale alifukunyua picha na kuzionyesha kwenye skrini.
“Inaonyesha Joseph alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na huyu mrembo , anafahamika kwa jina la Clelia Allisanto ambaye ni katibu wa umoja wa mataifa wa sasa”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na taarifa hio.
Kwa haraka haraka Roma alijua kila kitu kuhusu Lekcha yalikuwa na maigizo na hata kuwa na Kizwe huenda ilikuwa ni mipango lakini kuwa na mahusiano na Clelia ilimshangaza mno na isitoshe mrembo huyo alikuwa akimshuku kuwa ni Athena ila tu hakuthibitisha.
Alishindwa kupata majibu zaidi ya maswali yake kwani Diego hajakamilisha uchunguzi.
“Ukiachana na huyu Bikindi kuwa na ukaribu na Efani kuna sababu nyingine ambayo inamuunganisha na Zeros?”
“Ndio mfalme Pluto baba yake Joseph alikuwa ni mwanasayansi chini ya kampuni ya kisayansi ya utafiti ya Innova kutoka Italia kabla ya kuacha kazi na kujiunga na taasisi ya utafiti ya siri iliokuwa chini ya Zeros organisation ambayo ilikuwa na Research Base katika visiwa vya madagascar mwaka 2004”
“Unaweza kunionyesha picha ya Bikindi?”Aliongea Roma mara baada ya kusikia neno Madagascer na Diego muda uleule alitoa picha na kisha akamuonyesha Roma na kumfanya ashangae na simu yake ilianza kuita na kuitoa mfukoni na kugundua anaempigia ni mama yake , alipokea palepale na kuweka sikioni.
“Roma babu yako kafariki”Ilikuwa sauti upande wa pili ya mama yake ambayo ilisikika kinyonge.
Sawaaa
 
Mkuu singanojr tuwekee sehemu ya 584 ili tupate muunganiko mzuri
SEHEMU YA 583.
Baada ya chakula cha usiku Aloni ndio aliemfuata Roma na kuondoka nae kuelekea Club ya Pink Lady.
“Bro mmiliki wa Pink Lady ni mwanamke ambae ametokea kuwa rafiki yangu sana, lazima atatuletea warembo wa kutosha leo hii ili kusindikizia bia zetu”Aliongea Aloni huku akiendesha gari.
“Umenialika mimi tu na Omari?”
“Hapana , Bro Denisi hajakuambia nimemualika pia?”Aliongea na Roma alitingisha kichwa na kukaa kimya.
Dakika chache mbele waliweza kufika nje ya hoteli hio na eneo lilionekana kuchangamka kutokana na uwingi wa magari na watu waliokuwa wakiingia , zilikuwa ni taa tu za rangi maalumu zilizokuwa zikimuliika na kufanya eneo lote kupendeza na ilimfanya Roma kushangaa kwani hakutegemea uwepo wa eneo kama hili kwa mkoa huo wa Iringa.
Omari alikuwa tayari amekwisha kufika na alikuwa akimsubiria Roma huku kidogo akionyesha hali ya wasiwasi kwenye macho yake.
“Bro ni mara chache sana nakujaga kwenye maeneo kama haya , kidogo sijiamini”
“Kama ni hivyo kwanini upo hapa?”
“Mimi ni mwanaume pia , siwezi kukaa nyumbani muda wote na kwasababu upo hapa kidogo hali yangu ya wasiwasi imeondoka”Aliongea Omari na kumfanya amwangalie na kutabasamu na kuona licha ya kujiamini kwa Omari lakini bado alikuwa akiogopa vitu vidogo kama hivyo.
Ilionekana Denisi bado hakuwa amefika kwani mara baada ya wote watatu kuingia kwenye Club hio iliochangamshwa na mziki pamoja na warembo hawakumuona.
Aloni alionekana kujizolea umaarufu kwani alisalimiwa na wateja wengi ndani ya hilo eneo.
“Bro tutaenda moja kwa moja upande wa VIP na nitaita warembo kadhaa kuja kutufanyia masaji”Aliongea Aloni kwa kujigamba.
Dakika hio hio wakati Aloni akiwa anajaribu kupamba eneo hilo kwa maneno mazuri kuhusu huduma zinazopatikana , ghafla tu mhudumu aliekuwa ameshikilia tray la glass za bia alikumbana nae na kumwagikiwa na baadhi ya bia na glasi kupasuka na kumfanya kuloana.
“Ah!…Samahani , samahani sana kaka sio maku ..”Yule muhudumu alijikuta akiwa katika mshituko huku akimwangalia Aloni na uso uliojaa woga.
“What the f**…. Una shida gani wewe?”Alijikuta akipandwa na jaziba huku akiangalia nguo zake zilizochafuka kwa kumwagikiwa na mapombe.
“Unafikiri kuomba msamaha kunatosha eh? Unajua hii suti bei yake ni shilingi ngapi wewe?, au unafikiri kwa kujiuza kwako unaweza kuinunnua”Aliongea huku akimshika yule mwanamke ukola wa tisheti yake ya kihudumu.
Alikuwa ni msichana mdogo mno aliekuwa amepaka kwa mbali vipodozi , hakuwa mrembo sana wala mjanja lakini alikuwa na muonekano flani hivi tofauti na makahaba waliokuwa hapo ndani.
Makelele ya Aloni yaliweza kumfikia mwanamke ambae alikuwa meneja wa Club hio na kusogea haraka kujua nini kinaendelea na baada ya kuona suti ya Aloni na glassi zilizodoka chini na kupasuka hakuwa na haja ya kuuliza maswali.
“Mr Aloni tafadhari punguza jazba , huyu msichana ndio ameanza kazi, ni mwanachuo tu ambaye anafanya kazi ya muda na huenda akawa amechoka mchana yote kwa kufanya kazi”Aliongea kumtetea lakini Aloni ni kama hakuwa akisikia alichokuwa akiongea na kuendelea kumwangalia yule msichana kwa macho makali .
“Samahani kaka yangu ninaweza kukufidia ,, naomba nikaisafishe..”Aliongea yule mshichana kwa kutetemeka.
Roma muda wote yeye alikuwa kimya tu lakini upande wa Omari alianza kungiwa na huruma mara baada ya kusikia mwanamke huyo ni mwanachuo , alikuwa akijua maisha ya chuo kwa hapa Tanzania muda mwingine yanavyokuwa magumu na huenda ndio ilisababisha mrembo huyo kuja kufanya kazi katika mazingira kama hayo.
“Ni koti tu lilichofauka sana , unaonaje ukaachana nae isitoshe ushaambiwa ni mgeni hapa hebu punguza hasira zako”
“Sawa Bro Omari..”Alitikia kinyonge.
Yule meneja mara baada ya kusikia jina la Omari aliweza sasa kujua watu hao ndio watu muhimu ambao alikuwa wakitarajiwa kufika na kwa haraka sana alitoa tabasamu lake la ukarmu na kushukuru na yule msichana ambae waliweza kumjua kwa jina la Fetty aliwashukuru kwa kutoyafanya mambo kuwa makubwa.
Baada ya kuonyeshwa eneo maalumu lililojitenga kwa ajili yao kama VIP muda huo huo warembo walifika huku wahudumu na wenyewe hawakucheza mbali kwani waliweza kuwahudumia vinwaji walivyotaka.
Roma alijikuta akicheka mara baada ya kahaba mmoja kumshika mabega yake na kuanza kumfanyia masaji kwa namna ya kumtekenya na kumfanya Omari kuruka kama kijana ambaye hajaifikia balehe.
Muda huo huo na Denisi na yeye aliweza kufika na kumkuta kila mtu akiwa amezungukwa na warembo , alikuwa ameshikilia sigara mkononi na alitoa tabasamu mara baada ya kumuona Omari anavyofumba fumba macho kutokana na kushikwa shikwa na mikono ya mwanamke mrembo.,
“Bro Omari naona mwenyewe huduma imekukolea , warembo wa hapa ni wa viwango”
“Unaonekana haya ni maeneo yako “Aliuliza Roma.
“Ni kwasababu Aloni anafahamiana na mmiliki ndio maana nakuja mara kwa mara”
“Bro Denisi kaa kwa kutulia muda si mrefu Sister Tasi analeta ndafu tushushie na bia zetu”Aliongea akimaanisha mbuzi wa kuchoma
Ni muda huo huo mwanamke ambaye alikuwa amevalia suruali na blauzi ya rangi ya pink mikono mirefu aliweza kuingia huku akiwa amevalia miwani kwenye macho yake , hakuwa peke yake bali alikuwa ameongozana na watoto wa kike na kwa haraka haraka walionekana kuwa ni wanachuo ambao wamezoea kuja hapo kujipatia ‘madanga’, wote walikuwa wamevalia nusu utupu na kumfanya Omari mwili wake kumsisimka.
“Aloni nimechelewa kidogo kutokana na kuwa bize kuwaandalia warembo wa kuusindikiza usiku wenu vizuri , wote hawa ni warembo wa chuo na wako ‘fresh’ na watamu balaa lakini kidogo wana aibu , unaonaje?”
Roma aliangalia wanawake hao walioletwa na kwa upande wake hawakuwa warembo sana lakini maumbo yao yalikuwa yakivutia mno na kupagawisha.
“Bro hii ndio mara ya kwanza nakuja katika haya maeneo , hapa vipi napaswa kuchagua au inafanyika vipi?”Aliuliza Omari.
“Ndio maana yake na unaweza hata kumchagua mmiliki kama hao wengine hawakuridhishi”Alijibu Roma huku akimnyosshea mwanamke mwenye nywele zilizopakwa rangi ya pinki.
Upande wa Roma aliweza kuona sura ya mwanamke huyo anaefahamika kama mmiliki kama ameiona mahali lakini hakuweza kujua ni wapi lakini kwasababu kila kitu kilionekana kuwa kawaida ilimfanya kujawa zaidi na shauku.
“Au sijaumbiwa kuja haya maeneo , nahisi kama vile nawaonea hao wanawake kwa kuchagua”Aliongea Omari.
“Hao wasichana hawajali huruma zako bro na wapo hapa kwa ajili ya hela zako tu kama utaamua kucheza nao wala sio kulala nao basi watakuwa tayari pia”
“Hamna leo hii nipo hapa kwa ajili ya kuonyesha watu , ili kupunguza maneno ya watu wanaosema nimewekewa Limbwata na mke wangu”
“Sister Tasi kwa muonekeno wa Mabraza hapa inaonyesha hawa warembo sio wazuri kwao , tunaomba awamu nyingine tafadhari”Aliongea Aloni alionekana mzoefu sana kwenye hayo maeneo lakini hata hivyo shughuli ililiuwa ya kwake ndio maana alikuwa akijitahidi kumfanya kila aliemualika kuwa katika hali ya kufurahi.
Tasi mara baada ya kuambiwa hivyo hakuchelewa kwani dakika chache tu mara baada ya wale kuondoka waliweza kuingia wanawake wengine ambao awamu hio walikuwa wameziba maeneo machache tu kwenye miili yao huku wakiacha sehemu zingine zote kuwa wazi kwa ajili ya matangazo.
“Gentlemen!!, hawa ni warembo ambao wamemaliza chuo kabisa na ni wastaarabu, unaweza kuwaita ‘high classic chicks’ sidanganyi na kama mnataka kuwaonja hawatowaangusha lakini bei yao imechangamka kidogo lakini naamini kwauzito majina yenu hamna wasiwasi na bei”
Omari macho yake yalichangamka , ijapokuwa hakuwa muhuni lakini alipenda kuona wanawake warembo .
Upande wa Denisi hakutaka kupoteza muda , palepale alinyoosha mkono wake na kuwapa ishara wanawake wawiri warembo wamsogelee na wale warembo walichangamka kwa kutabasamu na kumkimbilia kwa mbwembwe zote za kimadaha.
“Bro Omari kama hawakupendezi bado Sister Tasi anao wengine ni wewe tu kutaja aina ya mwanamke unaemtaka”Aliongea Aloni na kumfanya Omari kukohoa kidogo , moyo wake ulikuwa ukisukuma damu kwa haraka sana na ili asionekane mshamba alinyooshea wanawake wawili ambao walikuwa na shepu kubwa na wakamsoogelea.
Upande wa Roma alishangaa kidogo kwani wanawake Omari aliochagua walikuwa na maumbo sawa kama la Queen
“Mr Roma wewe utahitaji yupi hapa?”Aliuliza Tasi na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli.
“Hakuna alienivutia hapo tofauti na wewe mwenyewe”Alongea Roma na kumfanya Tasi tabasamu lake kidogo kubadilika kwani hakutegemea kauli yake lakini palepale alipotezea na kutoa kicheko.
“Hehe Mr Roma unatania bwana, mimi nishazeeka tayari na isitoshe nipo bize na biashara”
“Mimi sijali chochote kama una biashara au mambo gani , kama hutonihudumia basi nitaharibu hili eneo usiku huu”Aliongea Roma kibabe na palepale yule mwanamke alijikuta akikosa kujiamini na kumwangalia Denisi aliekuwa pembeni na kisha akamgeukia Roma kinyonge.
“Kama ni hivyo basi sina usemi, lakini kwanini unataka kuadhibu mwanamke mzee kama mimi jamanii..”Aliongea kimadaha na kisha aligeukia wale wanawake waliobaki na kisha akawapa ishara ya kuondoka na akamsogelea Roma huku akijiegamiza kwake na kufanya manyonyo yake kugusana na kifua cha Roma,
Mwili wa mwanamke huyo ulikuwa mlaini mno na harufu ya manukato yake yalikuwa ni yale ambayo hayasahualiki kwa haraka.
“Binamu hakika una macho makali , Sister Tasi ndio habari ya mjini hapa”Aliongea Aloni akimsifia Roma
“Mr Aloni usiongee kuhusu mimi kwanza lakini kwanini hukuchagua mtu wa kuusindikiza usiku wako leo”Aliuliza Kizwe na ni kweli Aloni hakuwa na mtu ambaye ameambatana nae kama ilivyokuwa kwa kile mtu hapo ndani.
“Kuna yule mrembo uliesema ni mgeni , anaitwa Fetty ndio namuhitaji , nataka umlete chumba cha pili nimalizane nae usiku huu”Aliongea na kumfanya Tasi sura yake kubadilika kidogo.
“Aloni unajua kwamba sitaki kukuangusha lakini hao wasichana wapo hapa kwa ajili ya kazi tu na sio kujiuza”
“Huo ni ujinga , kwahio unaniambia kwamba kuna wanawake hapa waliokuja kuafanya kazi na hawapo tayari kujiuza hata kama nikitoa hela za kutosha?”
“Bro hebu achana nae , ushaambiwa kaja hapa kwa ajili ya kazi tu , si halali kufanya hivyo”Aliongea Omari na mwonekano wa Aloni ulikuwa ni ule wa kukosa uvumilivu.
“Bro inaonekana huna uzoefu sana wa kuja maeneo ya starehe , nimeingia kwenye Casino na Bar nyingi na wanawake wa namna hii nimekutana nao sana tu na mara nyingi wanajifanyisha kufanya kazi kwa kutotaka kujiuza lakini ukweli wapo tayari kufanya chochote ukiwapa hela , wanachokifanya ni sitaki nataka ili kupandisha hadhi yao tu wapate hela nyingi na isitoshe sisi wanaume hatutoshelezwi na mwanamke mmoja na mwanaume dhaifu pekee ndio atabakia kuwa na mwanamke mmoja, halafu muda mwingine kama utachagua mwanamke ambaye muda wowote yupo tayari kukubali inapunguza radha bro , ukipata kanakojifanyisha fanyisha kanakuwa katamu balaa”
Upande wa Oamri sura yake ilijikunja mara baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwaAloni kwani ni kama anadhihakiwa na alijikuta akimwangalia Roma kwa dakika lakini upande wa Roma hakutia neno.
“Sister Tasi namhitaji yule Fetty kwa ajili ya usiku wangu wa leo , ukweli najua taarifa zake zote na nimeambiwa anatokea katika vijiji vya huko Bukoba na familia yake ni ya kimasikini sana na mkopo anaopata haumtoshelezi kulipia ada na mahitaji yake , kama atakubali kuwa na mimi usiku huu nitahakikisha namtafutia kazi nyingine na akimaliza chuo nitamtafutia kazi Dar, nasikia hao warembo wanatembea na Dawasa zao nataka nijionee mwenyewe haha..”
Baada ya kuona Omari kaomba sana alimpa ishara meneja na upande wa Aloni alitabasamu na kisha akasimama na kutoka kuingia chumba cha pembeni huku akimkonyesha Denisi
Upande wa Roma alikuwa kimya muda wote na mara baada ya Aloni kutoka hapo alimgeukia mrembo wake aliekuwa pembeni yake.
“Hey mrembo umekuwa hapa kwa muda gani”Aliuliza Roma na Tasi alitabasamu.
“Kaka kwanini unauliza maswali hayo , maswala ya biashara yanaondoa mudi kwanini usiendelee kunywa kinwaji chako na tuhamie kwenye mchezo?”
“Je kama bado nataka kujua ?”
“Nimeanza kufanya biashara katika hili eneo kwa zaidi ya miaka mitano licha ya mwanzo nilikuwa nimejikita upande wa hoteli tu”Aliongea
“Kweli?, ndio umejenga hii hoteli?”
“Ndio nilijenga mimi”Alijibu na kumfanya Roma kutabasamu.
“Kwa taarifa nilizokuwa nazo hii hoteli imejengwa miaka kumi iliopita na imeweza kuwa na wamiliki wawili tofauti kabla yako na ilianza kama ukumbi wa uliotambulika kwa jina la Golden Hall na baadae ikaja kuwa hoteli ikitambulika kwa jina la Golden Hotel”Aliongea Roma.
“Sina uhakika kama taarifa uliokuwa nayo ni sahihi , lakini wewe si mgeni hapa Iringa? umejuaje yote hayo au kuna kitu unataka kujua kutoka kwangu?”
“Nilikutana na rafiki yangu nje ya nchi miaka kadhaa iliopita na wakati narudi Tanzania aliniambia alishawahi kukutana na mwanamke nchini Tanzania na ni mmiliki wa hoteli ya The Golden kwa zaidi ya miaka kumi na kuniomba kama nitafika nijaribu kumtafuta nimfikishie salamu”Aliongea Roma.
“Samahani kama ni hivyo kwani siwezi kukusaidia”Aliongea Tasi huku akijaribu kutingisha mabega na aliishia kumwangalia Denisi ambaye alikuwa kimya muda wote lakini alikuwa kama vile hakuwa akisikia chochote na aliendelea kutaniana na warembo aliokuwa nao akiwashika shika katika maeneo nyeti..
“Mr Roma kama utakuwa unakuja mara kwa mara huenda ninaweza kukutafuuta huyo mtu , isitoshe hili eneo kuna watu wazee sana ambao wameanza kufanya kazi muda lakini pia kuna wageni wengi wanafika”
“Kama ni hivyo nitashukuru sana”Aliongea Roma.
Ukweli ni kwamba alitunga kuhusu mwanamke na rafki yake lakini kuhusu hoteli hio kuitwa The Golden hakuwa amekosea kwani kabla ya ujenzi wake kulianza kujengwa ukumbi ambao ulikuwa ukifanyia matamasha mengi ndani ya eneo hilo la Iringa ,ukumbi uliofahamika kwa jina la Golden Hall, Roma maelezo hayo alikuwa nayo kutokana na kwamba kabla ya kuja alishafanya utafiti wake tayari.
Muda huo huo mlango wa kuingilia ulifunguliwa kwa nguvu na msichana alidondoka chini akionekana kama vile alikuwa akikimbia.
“Sister Tasi tafadhari nisaidie”
Alikuwa ni yule msichana aliefahamika kwa jina la Fetty na baada ya kusimama alienda moja kwa moja kupiga magoti mbele ya Tasi.
“Sister Tasi walinzi wanataka kunikamata tafadhari waambie mimi ni mhudmu tu sio kahaba”Aliongea akijitetea mbele ya Tasi na kufanya wale makahaba wengine kumwangalia na kisha wakamsonya.
Ilionekana mara baada ya ya mwnamke aliefahamika kwa jina la Tasi kutoa maelekezo kwa meneja alimuelekeza kwenda kwenye chumba cha Aloni lakini akakataa na kupelekea kukamatwa na wale walinzi ili kulazimishwa.
Alikuwa akilia wakati ambao alikuwa akiomba na kwa muonekano wake alikuwa akitia huruma sana na muda uleule wale walinzi waliingia katika Cabin yao wakiwa wameongozana na Aloni.
“Wewe Malaya unathubutu vipi kuonyesha ujeuri wako?”Aliongea Aloni huku akijaribu kumshika yule msichana ili kumvutia kuelekea kwenye chumba lakini Fetty alitaka kukimbia tena lakini wale mabodigadi walimzidi nguvu na kumbeba juu juu.
Upande wa Tasi hakuonyesha uso wa huruma hata kidogo lakini upande wa Omari ambaye alikuwua akimiminiwa mvinyo na mrembo alikosa uvumilivu wa kushuhudia kitendo kile.
“Hey Aloni hebu muache huyo msichana kama hataki”Aliongea kwa sauti.
“Bro tusiharibiane starehe zetu kwasababu kila mmoja hapa yupo kwa ajili ya kuburudika”
“Kwahio kubaka ndio unakuita Sterehe , kama msichana hafanyi kazi hio haina haja ya kumlazimisha kwani unakuwa ni kama ubakaji”Aliongea na kumfanya Aloni kumgeukia yule mrembo alieshikiliwa na mabodigadi na kisha akamshika mkono na kuongea nae kwa sauti ya chini.
“Fetty wewe mwambie braza yangu pale , je upo tayari kuwa na mimi kwa hiari yako au lah?”Aliuliza lakini Fetty alikuwa akitoa machozi , alionekana ni wale wasichana aina flani hivi wachanga wenye ujinga wa kutoelewa mambo mengi ya kimjini.
Lakini kitu cha kushangaza mara baada ya kuulizwa lile swali alitingisha kichwa kwamba anakubali.
“Acha kuwa muoga kama haupo tayari wewe niambie au kuna kitu kakutishia nacho?”Aliendelea kuuliza Omari lakini Fetty aliishia kung’ata meno yake kwa hasira na kisha akatingisha kichwa kwa namna ya kukataa kwamba hakuna kitu ambacho ametishiwa nacho.
“Nishakuambia braza hawa wanawake wa siku hizi ni waelewa sana maadamu utakuwa na faida kwao , wewe furahia maisha na warembo na mimi ngoja nikainjoi nae niyatiririshe haha..”Aliongea kwa furaha na huku akaondoka lakini Omari bado alikuwa kwenye hali ya kutoridhika.
“Bro Ommy kuwa mpole , yeye ndio kaamua na atapata malipo, haina haja ya kuwa na wasiwasi”Aliongea Denisi.
“Hapana siwezi kutulia , Roma, Aloni ni binamu yako na lazima atakusikiliza hebu chukua hatua, nina uhakika kuna kitu amemtishia yule mwanamke ndio maana amekubali kishingo upande”Aliongea na kumfanya kwanza Roma kucheka.
“Umenialika kuja hapa nikusindikize kwa ajili ya burudani lakini ninavyokuona unanitafutia tu matatizo”Aliongea Roma lakini kwa namna ambavyo Omari alikuwa na uso wa usiriasi Roma aliamua tu kusimama na kuelekea upande wa pili wa chumba alichoingia Aloni na yule msichana.
Baada ya Roma kufundua tu mlango kidogo aliweza kusikia sauti za kilio kutoka kwa Fetty huku akitoa makelele ya kumwambia Aloni aache na mabodigani waliokuwa mbele walitaka kumzuia Roma kuingia lakini yule mwanamke Tasi aliwapa ishara ya kuondoka.
“Bro Roma kwanini upo hapa tena”Aliuliza Aloni kwa mshangao mara baada ya kumuona Roma kaingia..
Aloni muda huo alikuwa kwenye kitanda tayari akiwa amemkalia yule msichana kwa juu na ilionekana alikuwa akimlazimisha kuvua nguo ya ndani na Roma hakujali sana zaidi ya kusogea mpaka kwenye kile kitanda na kisha akamtoa kwa nguvu..
“Ondoka hapa na katafute wanawake wanaopenda hayo mambo ndio ucheze nao”
“Kwasababu Bro wewe ndio umeongea basi nitaondoka, sisi ni binamu hata hivyo”Aliongea na kisha akatoka na kufuatiwa nyuma nyuma na Tasi.
Fetty ambaye tayari alikuwa nusu uchi aliishia kukumbatia vigoti vya miguu yake huku akitoa machozi na kutetemeka.
“Asante sana kaka”Aliongea kushukuru.
“Nilijua unaigiza mwanzoni lakini baada ya kuona hisia zako sio feki nikaona nije nikusaidie”
“Naigiza…! Kivipi kaka?”alitaka kuongea huku akifuta machozi yake kumwangalia Roma kwa mshangao lakini Roma alimzuia.
“Hakuna kitu”Aliongea Roma huku akimwangalia yule msichana kwa dakika kadhaa na kisha akatabasamu mara baada hana kitu cha pekee kwenye mwili wake zaidi ya nguvu ya kawaida ya kiulinzi ya kichawi aliowekewa kimila.
Alijiambia huenda anafikiria mbali , kwanini msichana mpole kama huyo kumuigizia na kumuingiza kwenye mtego hivyo aliamua kupotezea.
“Bro je unaweza kuniambia namba yako ya simu, ninataka kukushukuru siku moja , baba yangu ameniambia kama hutoweza kulipa fadhila basi nitapigwa na radi”Aliongea huku sauti yake ikitoka katika hali ya huzuni na kuwa ile ya kike ya kushawishi mwanaume.



SEHEMU YA 584.
Roma bakutaka kuvutana nae hivyo aliamua tu kumpa namba yake ya simu na kisha kumuacha.
Baada ya kurudi kwenye Cabin yao aliwakuta Denisi na Omari akiwa tayari washachangamka na walikuwa wakila ‘goodtime’, ijapokuwa Aloni alionekna hakuwa amependezwa na kumkosa yule msichana lakini tayari alikuwa ashajitafutia mwanamke mwingine.
Sister Tasi aliita wanawake(Chicks) wawili kwa ajili ya kukaa na Roma mpaka muda wa usiku, upande wa Roma na Omari kutokana na mafunzo yao ya kijini ilikuwa ngumu sana kuelewa na mara baada ya kuona muda umeenda alimpa ishara kwamba waondoke.
Omari alichukua njia yake kwa kuendesha Range yake na Roma aliendesha gari ya Aloni mpaka nyumbani.
Roma kabla hata hajaingia ndani simu ya Omari iliingia na akaipokea palepale na kumwambia ashafika nyumbani.
“Bro nadhani nimezima maneno ya watu kwa leo hii , nilikuwa nikijisikia vibaya sana pale kuwa mbali na mke wangu”
“Nilijua ulikuwa ukiburudika na wale warembo kumbe ulikuwa ukimuwazia mkeo?”
“Unanichukuliaje wewe , ninaweza kuwa na hela kama wewe lakini mimi nina sheria zangu na isitoshe sasa hivi ni baba wa mtoto hivyo lazima niishi kama baba , tukiachana na hayo vipi kuna kitu chochote ambacho sio cha kawaida uliona pale?”
“Nimeona lakini sio sana , angalau nimeweza kujua yule Tasi sio mmiliki halali wa ile hoteli licha ya kwamba anaonekana kabisa kama mmiliki wa mwanzo, lakini bado sio yeye”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Unakumbuka nilisema hoteli ile ilikuwa ikiitwa Golden na ilianzia kama ukumbi?, kabla ya kuja pale nilikuwa nishafanya tafiti zangu tayari na ni kweli wakati ilipobadilishwa jina ilinunuliwa na mwanamke ambaye kwenye picha nilionyeshwa kabisa ni yule yule wa leo , lakini ajabu ni kwamba nilivyomuuliza kuhusu jina la hoteli hio miaka kumi iliopita hakuwa akifahamu , kwa maelezo niliopewa yule Tasi mmiliki wa ile hoteli ni Mkinga ambaye alirithi mali kutoka kwa mume wake ndio akainunua na ni mkazi wa hapa hapa wa muda mrefu, kitu kingine muda wote yule mwanamke alikuwa akimwangalia Denisi , ijapokuwa alikuwa na uwezo mkubwa wakuigiza lakini bado hakuwa mkamilifu, lakini siwezi kusema wana uhusiano wowote mpaka sasa kwani hakuna ushahidi wa moja kwa moja”
“Kwanini tusimkamate yule Tasi , kuna uwezekano kabisa akatuamnbia kila kitu na kugundua uhusiano uliopo kati yake na Denisi pamoja na yule Haruni”
“Iwe ni familia ya Mzee Longoli au yule mwanamke hata kama pia ni Denisi , sidhani kama ndio watu pekee ambao wapo nyuma ya kila kitu , mchezo wao haujafikia patamu bado nikiwa na haraka unafikiri ninawezaje kumkamata muhusika mkuu?”Aliongea Roma.
“Nilikuwa na shauku huenda ukakosa uvumilivu lakini naona , hebu tutaongea kesho nasikia sauti za jembe langu likilia huko ndani , ngoja nikambembeleze.”Aliongea na kisha akakata simu bila ya kuaga na kumfanya Roma kutabasmau kwa uchungu aliona licha ya bwana huyo kutoka katika mafunzo ya kijinni lakini amegeuka kuwa ‘Super daddy’.
Roma alikuwa akiongea huku akitembea na muda huohuo alikuwa tayari nje ya mlango wa chumba chao na alishangaa kukuta bado taa zinawaka , lakini hakufikiria sana zaidi ya kufungua mlango na kuingia.
*****
Kule kwenye ile Club ya Pink Lady katika chumba kikubwa cha kifahari , Denisi alionekana akiwa amelela uchi chali huku mdomoni akiwa na sigara inayotoa moshi , chini ya kiuno chake alikuwepo Kizwe aliekuwa kama ‘Ndama’ yenye njaa ya maziwa kwa namna alivyokuwa akinyonya.
Denisi mara baada ya kuvuta sigara kwa dakika kadhaa na kuitupia pembeni aliinua uso wake na kumwangalia mwanamke anaejaribu kumfurahisha na alikumbuka jambo na palepale aliinua mguu na kumpiga teke.
“Uwii…!!”
Alitoa ukulele yule mwanamke wa maumivu huku akimwangalia Denisi kwa macho ya kupaniki na mshangao.
“Kilema wangu , ni kosa gani ambalo nimefanya mpaka kunipiga?”
“Tofauti na kuwa Malaya nadhani ubongo wako ni kama wa ng’ombe , ni mara ngapi nilikuambia ujiandae? , hivi unajua jina la Golden hoteli na Golden Hall aliotaja Roma yana uhusiano gani na hii hoteli?, kwanini hujafanya kazi yako kikamilifu , si nilikuambia kuchukua uhusika wote wa Tasi bila kusahau chochote?”
“Nini.. ! nilimfatilia kwa kila kitu mpaka ndugu zake lakini sikuweza kufikiria mbali kufanya uchunguzi wa hoteli hii miaka kumi iliopita , isitishe ni kipindi kirefu nadhani ameweza kugundua?”
“Unafikiria Roma ni mjinga kama wewe mpaka kuuuliza vile , ni kwasababu tu hajajua ni nani ambaye yupo nyuma ya kila kitu ndio maana akakaa kimya , lakini bado naona anakiburi cha kudhania anaweza kuifanya dunia yote ikawa chini yake”
“You seem to know him well”(Unaonekana kumjua vizuri?”)
“Because I am not the second Yan Buwen”(Kwasaabu mimi sio Yan Buwen mwingine”.
Aliongea huku akicheka akimaanisha kwamba yeye ni tofauti na sio kama Yan Buwen .
“Kwahio tunafanya nini ?”
“Tutafanya kinachopaswa kufanyika , ni kama ilivyopangwa , kete yangu ni kumfanya aamini kabisa huu ni mpango uliotengenezwa lakini mwisho wa siku ashindwe kufanya chochote na kuishia kukubali tu”
Baada ya kuona tabasamu la Denisi ilimuaminisha kwamba kila kitu kinaenda sawa na hakuacha na yeye kutoa tabasamu lililojaa kisasi ndani yake.
*******
Siku nyingine asubuhi wakati Roma na Edna wanafika eneo la Dining kwa ajili ya kupata kifungua kinywa , Lanlan tayari alikuwa amekaa na alikuwa ashaandaliwa uji wa maziwa na bibi yake Damasi kwenye bakuli kubwa na alikuwa akihangaika nalo.
Aliongekana kutopenda aina ya kifungua kinywa kilichopo kutokana na kukosekana kwa nyama , lakini alijitahidi kula kwa namna zote kukamilisha kile alichoandaliwa .
Kilichomshangaza Roma ni kwamba kwenye meza alikuwepo Damasi tu mama yake wa kambo na Babu yake hakuwepo na Ashley pia hakuwepo pamoja na Denisi.
“Mama Ashley huyu mzee kaelekea wapi?”
“Asubuhi aliweza kuondoka kwenda kwenye kikao pamoja na baba yako ,Raia wa Zanzibar wameanzisha maandamano kutaka mabadiliko ya kisheria kati ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kama tu hutofikishwa mbele ya sheria kwa kile ulichokifanya , hivyo wanajeshi wa vyeo vya juu wamekutana kwa ajili ya kikao cha dharula”
“Kwanini sijaambiwa chochote wakati mimi ndio chanzo?”
“Watu wa jeshi wanajua tabia yako ndio maana , hao watu wanakuona kama vile ni muuaji na unaweza kusababisha matatizo zaidi kama utahusishwa , kinachofanyika huko ni kujaribu kumpoza raisi wa Zanzibar kwani inaonekana ndio anaehusika kwa kila kitu”Aliongea Damasi na kumfanya Roma kushangaa kidogo , lakini aliamini huenda mtu ambaye amehusika na kila kitu ni Raisi Senga ili yeye asipatiwe taarifa.
Hata hivyo uzuri wa kikao hicho kilikuwa kikifayikia ndani ya eneo hilo hilo la Afande Kweka kwani lilikuwa limeandaliwa kwa baadhi ya vikavo vya siri sana vya Deep state ndani ya Tanzania.
Sasa upande wa eneo hilo maalumu la mikutano Raisi Senga ndio ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti cha mwanzo kama kiongozi , huku aifuatiwa na Afande Kweka na kisha mkuu wa majeshi Afande Tozo , huku wengine wote wakiwa ni wana usalama waandamizi pamoja na wanasiasa.
Upande wa Afande Kweka alionekana kusoma karatasi ambayo alikuwa amekabidhiwa na mpaka anamaliza kuisoma uso wake ulizidi kuwa mweusi na alipiga meza chini kwa nguvu.
“Jemadari vikosi vyote ambavyo vipo upande wa visiwani chini ya kamanda Razaq vinatii maagizo kutoka kwa raisi wa Zanzibar na kwenda kinyume na katiba ya muungano, tusipochukua hatua za mapema kesho wataanza kuungana na wananchi kufanya maandamano”
“Yeye ni raisi wa Zanzibar tu anapata wapi uthubutu wa kujjipatia madaraka ya kugeuza vikosi vya nchi kuwa upande wake , anachokifanya ni kujaribu tu kutupa presha”
“Ni zaidi ya presha , anajaribu kuchukua hii hali kama fursa ya kutaka kuonyesha ukubwa wa Visiwani, kama ataungwa mkono na baadhi ya nchi za kiarabu , kwa upande wetu hii itakuwa mbaya sana na itatengeneza mgawanyiko mkubwa sana ndani ya Tanzania maana tuna wanajeshi wa asili ya Zanzibar pia”
“Haya yote yanatokea kwasababu ya mtoto wangu ambaye amekosa maadili mazuri ya kimalezi na kiburi kilichozidi , naombeni radhi kwa niaba yake”Aliongea Raisi Senga na kufanya baadhi ya watu waliokuwa hapo ndani kujaribu kumfariji.
“Nadhani sijaomba mtu yoyote kuomba msamaha kwa ajili yangu na isitoshe sina mpango wowote wa kuyatambua makosa yangu”Sauti ya Roma iliweza kusikika akiingia hapo ndani huku walinzi wakimfuatia nyuma kwa tahadhari.
Watu wote hapo ndani walimwangalia kwa macho makali lakini yenye wasiwasi ndani yake , wale waliokuwa na gwanda za kijeshi na pia wale ambao walikuwa na mavazi ya kawaida ikimaanisha wanasiasa wote walikuwa wakimwangalia Roma kwa wasiwasi na yote hayo ni kwamba walikuwa wakimhofia.
“Nimepata taarifa kuna maandamano huko yanatokea kutokana na kifo cha Haruni , nimepewa taarifa pia Kamanda Razaq ni ndugu na mume wa Shangazi yangu Theresia, lakini taarifa nyingine nasikia ni mtu jasiri sana ndani ya jeshi ndio maana akapewa ukamanda upande wa Visiwani sijui taarifa hizi chache nilizopewa ni sahihi?”
“Upo sahihi ukiacha na sifa ulizotaja lakini pia Afande Razaq ni mtu ambaye anaheshimika sana kwa weledi wake sio upande wa bara tu mpaka visiwani kote wanajeshi wanamheshimu na ndio maana ana nguvu kubwa , tumemuweka upande wa Visiwani kwasababu tuliamini ni mtu ambaye yupo ‘neutral’ na hapendi siasa kuingiliana na jeshi”Aliongea Afande Tozo.
“Kama ni hivyo kwanini akachagua upande na kuungana na raia kwenye kuandamana?”
“Hio ndio sababu ambayo mpaka sasa hivi haijatufikia na ndio maana tupo hapa kujadili namna ya kumaliza hili tatizo , niseme chanzo cha migongano hii kilianzia kwa kufariki kwa Mzee Longoli na ilikuwa ikitafutwa tu sababu”Aliongea Afande mwingine mwenye kitambi na kumfanya Roma kumgeukia babu yake.
“Mzee ni kipi kinapaswa kufanyika?”
“Unamuuliza ni kipi cha kufanyika? , wanachotaka ni kitu kimoja aidha kuwepo na marekebisho ya vipengele vya muungano au ufikishwe mbele ya sheria, lakini hilo bado hatujaliafiki,. tulichoona kinafaa ni wewe mwenyewe kwenda kuonana na Raisi wa Zanzibar na kumtuliza kwa muda huku tukiendelea na uchunguzi , Afande kashasema kuna sababu iliokufanya kuchukua maamuzi ya kumuua Haruni hadharani na tuna taarifa ya uchunguzi uliofanyika hospitalini mara baada ya mwili wa marehemu kufikishwa mochwari , hivyo tukiendelea na ufumbuzi zaidi wewe ndio unaepaswa kwenda nyumbani kwa mheshimiwa na kumuomba msamaha na hata wakikuzuia itakuwa ni kwa muda tu, ilimradi maandamano yakome na vipengele vya muungano kundelea kubakia kama vilivyoasisiwa”Aliongea Brigedia mmoja ambaye Roma hakumfahamu.
“Kwahio unashauri kwamba mimi nijitoe kafara niende mpaka Zanzibar bila ya kujali uhatari wote na nikaombe msamaha? , yaanni unaniambia nikaombe msamaha kwa mtu ambaye ananichukulia kama muuaji? , unadhani atakubali kuutoa huo msamaha?”Aliongea Roma akipandisha sauti na kufanya watu wote kuangaliana.
“Nadhani kipaumbele kwasasa ni kujua kwanini Afande Razaq kaamua kuchagua upande wa Zanzibar na kukiuka sheria za muungano na isitoshe anao udungu wa mbali na mzee wetu Afande Kweka”Aliongea Afande Tozo lakini muda huo huo zilisikika purukushani kutoka nje na mlinzi wa Raisi Senga alimsogelea na kumwambia jambo na kumpa ishara ya ndio na kisha akatoka na muda uleule aliingia Afande Maeda .
“Afande Kuna nini?”Aliuliza Afande Tozo na Afande Maeda ambaye hakuwa kwenye Kombati za jeshi alitoa salamu kwa maafande kwa kukakamaa mwili bila sauluti na baada ya salamu yake kuitikiwa aligeuza macho yake yenye wasiwasi upande wa Roma.
“Jana usiku tumepokea taarifa ya kifo cha Aloni Sauli Shabibu kutoka kwa jeshi la polisi mkoa wa Iringa”Aliongea na kufanya watu wote akiwemo Roma kuwa katika hali ya mshangao, lakini aliendelea kuelezea namna ya kifo hicho kilivyotokea na matokeo ya uchunguzi wa Awali na kwa maelezo yake ni kwamba kifo hicho kimetokea nje ya hoteli ya Pink Lady katika maegesho ya magari na mtu alieonekana kufanya hivyo ni Mr Roma Ramoni kwa staili ileile ambayo alimuua Haruni , yaani kupasuliwa kichwa kama tikiti.
Akaendelea kusema uchunguzi wa awali umethibitisha alama za vidole ni za Roma Ramoni bila ubishi na akaenda mbali kusema habari hio imeweza kumfikia baba yake Aloni yaani Shabibu ambaye ni kaka wa Afande Razaq na huenda ndio sababu ambayo imemfanya kukubali kuungana na Raisi wa Zanzibar kuwapa ushirikiano Raia.
Roma alijikuta akishangaa sana na haikuwa kwake tu kila mmoja hapo ndani alimgeukia yeye mwenyewe na kumwangalia kwa macho makali mno , upande wa Afande Kweka na yeye alimwangalia Roma kwa wasiwasi mkubwa , waliamini ndio wanaongea kumaliza tatizo lakini ndio mwanzo wa tatizo lingine.
ITAENDELEA.
 
Weka mwendelezo kk Leo wikiend iend vzl bada ya dabi yetu hii kaz njm kwako na wikiend njm bro...
 
Back
Top Bottom