Singano jr
Member
- Oct 15, 2018
- 12
- 45
SEHEMU YA 595
Roma kwa haraka sana kumbukumbu zake ziliweza kurudi siku ambayo alikutana na Kizwe pamoja na Lekcha ndani ya Club B , Lekcha wa kipindi kile alikuwa wa kawaida sana na hakuwa tishio lakini Lekcha ambaye anamuona mbele yake alikuwa ni mwingine kabisa.
Kwa mtu mwingine angepingana na kauli ya Raisi Jeremy kusema Mtu anaefanana na Denisi ndio Joseph Bikindi , ila kwa upande wa Roma ambaye alikuwa na uzoefu wa mambo mengi ya kushangaza ilikuwa rahisi kwake kuweza kuelewa na kuamini.
“Ni wewe … sijategemea kukuona ukiendelea kuishi, nilijua tayari ulishauwawa kwa siri”Aliongea Roma kwa kejeli.
“Kwanini unadhania mwanaume ambaye sikuwa na thamani kama mimi kufa bila sababu ya msingi , siku uliomtuma yule malaya kuja kwangu haukuwahi kudhannia kila kitu unafanya kama nilivyokuwa nikipanga?, Unadhani ni kwa bahati mbaya mtu ambaye alikuwa akiishi kwa kuokota makopo na kuishi chini ya Daraja kuweza kuelea angani kama wewe hivi sasa? , unafikiri hii ni miujiza imeniokea?, wewe huna tofauti na wengine , unatumia wasifu wako kujaribu kudharau viumbe vya hali ya chini ila ukweli ni kwamba nyie watu hampo tofauti na sisi”Aliongea Lekcha.
“Nilidhani ulikuwa ukinichukia ndio maana uliweza kuwa na mipango mingi ya kunichafua , lakini kwa ninachoona hapa unatuchukia wote”
“Hahah… mimi niwachukie ,hamstahili uwekezaji wangu wa kihisia kwa ajili tu ya kuwachukia , kwangu mimi nawaona kama mawindo tu na nitawafanya ninachotaka”
“Unaonekana kujiamini , naona umeweza kumiliki nguvu ya Ant-matter , na kama sikosei naamini umefanikisha hayo yote kupitia Yan Buwen na hili linanifanya kuwa na shuaku ya kutaka kujua umefikia hatua gani, lakini hata hivyo naweza kuona wewe ni wa tofauti”Aliongea Roma huku akitoa kicheko.
“Bado tu unaongea na mimi kwa dharau … hicho ndio kinachonichukiza kuhusu nyie watu, nini kimekufanya kuja hapa na kutaka kuingilia mambo yangu ,au unahisi bado tu unaweza kunishinda?
Unatokea katika familia ambayo inasifika kuwa na nguvu ndani ya Tanzania lakini kwangu mimi naona ni ushenzi tu na utapeli wa famlia yenu ndio maana mnajiona mpo juu , kwangu mimi watu wa aina yenu mnastahili kushushwa kwa kipigo na kuliwa na mimi”Aliongea Joseph Bikindi kwa dharau huku akiwa na uso wa kujiamini.
Wakati Roma akifikiria nini cha kuongea ghafla tu aliweza kuhisi msisimko wa hali ya juu ukiwasogelea na kumfanya kukunja sura , ni msisimko uliokuwa ukitokea upande wa Magharibi.
Ni kufumba na kufumbua tu aliweza kuonekana mwanaume mweusi alievalia mavazi meupe marefu aina ya Robes.
Alikuwa na mwonekano wa kitajiri na kujiamini huku akiwa na sura ambayo imejaa ujeuri , macho yake kwanza aliyaelekezea kwa Raisi Jeremy ambaye alikuwa akizungukwa na mwanga mweupe na kisha akayageuza upande wa Roma aliekuwa juu yake kidogo.
“Master 4 asante kwa kufika mapema”Aliongea Raisi Jeremy huku akonyesha hali ya kupatwa na ahueni, haikueleweka kwanini anaitwa Masetr 4 lakini kwa haraka haraka Roma alitambua inawezekana akawa ndio Master mkuu namba nne katika jamii ya Panas.
Kuhusu uwezo wake Roma aliweza kugundua alikuwa levo ya kuipita dhiki akiwa na uwezo wa kutawala rangi tatu za moto , alionekana kuwa juu zaidi ya Nix na Gesha ila levo yake bado ilikuwa ya chini kuliko Rom ambaye alikuwa na uwezo wa kudhibiti mtoto wa kiroho wa rangi ya bluu pamoja na maji ya kiroho.
“Jeremy wewe mjinga sana , yaani umeshindwa kujilinda mpaka ukafikira hatua ya kutumia hio medali tena wanaokushughulikia ni wanafamilia wako mwenyewe?”Aliongea kwa lugha ya kifaransa.
“Master 4 mambo mengine hayazuiliki na sio kila tunalopanga linatokea , wana nguvu zaidi yangu na mipango yao ilikuwa ya siri tafadhari nisaidie kuwamaliza”Aliongea na Master 4 alimpotezea na kumgeukia Roma.
“Ninakujua wewe kijana kutoka Taifa la Tanzania , una umaarufu mkubwa sana katika ulimwengu wetu kwa kuweza kupita vizuizi vya tamaduni zetu kwa muda mfupi , nashindwa kuona uwezo wako ni katika levo ipi nadhani ni kama sifa zako zinavyojieleza hakika una stahili sifa unazopewa , kwa leo nipo hapa kwa ajili ya kumsaidia ndugu yetu upande wa mama sitaki kujiingiza sana na mambo ya dunia”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa kwani hakuelewa nini maana ya ndugu upande wa mama , akili yake ilifanya kazi kwa haraka sana na kujiuliza inamaana Raisi Jeremy na yeye amezaliwa nusu binadamu nusu jini, alijikuta sasa akielewa kwanini watu kutoka Panasi walitumwa kuja kumlinda , kumbe kuna sababu kubwa na sio maswala ya bahati mbaya.
“Wewe takataka umetokea wapi? , unajiona ni nani mpaka uje kuingilia hapa?”Aliongea Lekcha na bila ya kutaka kusubiri jibu palepale shoti za ant -matter zilimtoka kwenye mkono wake na kumshambulia Master 4 kwa spidi na kumshusha ardhini.
Masetr 4 alijikuta akishangazwa na namna shoti zile zilivyoweza kumtoka Lekcha kwani hakutarajia kama angekuwa na uwezo huo.
“Haha.. kwa udhaifu huo uliokuwa nao bado tu umekuja peke yako na bado unajitamba kutaka kumuokoa Jeremy? ,ila sio mbaya nitakuua nae”Aliongea huku hali ya kujiamini ikiongezeka mara mbili na alizidi kuongeza nguvu ya shoti ya Ant-matter kumshambulia Master 4 kumpeleka mpaka ardhini.
Roma alikuwa na nafasi ya kumzuia Lecka lakini hakutaka kujihusisha kabisa na watu wa jamii hizo zisizoonekana na wakati huo huo alitaka kumuona Lekcha uwezo wake kabla ya kupigana nae.
Upande wa Master 4 alionekana kushindwa kuelewa namna ambavyo aliikuwa akishambuliwa na kujilinda, alijikuta akianza kujutia maamuzi yake , huenda angekuja na watu wengi zaidi kwa ajili ya kupambana lakini alimdharau adui kwa kutarajia atakuwa wa kawaida ndio kilichomfanya kuja peke yake.
Dakika hio hio hakuwa na haja ya kumsaidia kwanza Raisi Jeremy kwani aliona anapoteza nguvu kwa boriti za shoti anazopokea.
Upande wa Raisi Jeremy ile kinga iliokuwa imemzingira ilitoweka palepale , ilionekana dakika therathini za kumlinda zilikuwa zimeisha na kumfanya aanze kuogopa kwani aliweza kushuhudia namna ambavyo Master 4 anavyopokea kichapo.
Muda uleule mwanga ule wa ngao baada ya kupotea Kizwe na Desmond walijikuta wakirejewa na hali zao upya za kujiamini na kutaka kulipiza kisasi.
“Baba umemua kunitelekeza mimi na ukamchagua yule Malaya wa Kitanzania kuwa mrithi wako , usinilaumu kwa kupindua meza muda huu”Aliongea Desmond huku akionyesha hasira kubwa sana zidi ya baba yake na mwili wake ulibadilika na kuwa kama kivuli huku akimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi huku aidhamiria kummaliza na pigo moja.
“Kuwa makini!!”
Sauti ilimtoka kizwe na kwa spidi sana aliweza kutokeza mbele ya Desmond akionyesha kumkinga.
“Poof!!”
Ni mlio wa sauti ya kuchoma iliosikika na boriti ya mwanga mweupe kama wa laser ulionekana kumchoma Kizwe katika kifua chake na kutoboa.
Katika umbali mfupi kutoka aliposomama alionekana Master 4 ambaye alikuwa ameinua mkono wake kuelekezea kwa Kizwe na boriti ya mwanga ule mweupe ulionekana kutoka katika kifaa ambacho hakikuwa kikielezeka kiumbo na ilikuwa ni kama dhana ambayo teknolojia yake ni ya hali ya juu sana, hazikuwa kama zile dhana ambazo Roma aliweza kuziona kwa baadhi ya watu wa Hongmeng.
Desmond alijikuta akishangazwa na jambo lile, hakuamini mwanamke ambaye hakuwa akimchukulia tena kama mama yake ameamua kujitoa kafara na kupokea shambulio badala yake.
Kwake ilikuwa ni kama muda ulikuwa ukienda mbele na kurudi kwa wakati mmoja.
Lekcha aliekuwa juu angani hakuonyesha kujali kile kilichokuwa kikiendelea ardhini , Kizwe na mtoto wake aliwaona kama watu ambao hawakuwa na thamani tena baada ya mpango wake kufeli, hivyo hakuwa na haja ya kujali kama wapo hai au ni wafu.
Raisi Jeremy alijikuta akitoa pumzi ya ahuenni , ilikuwa ni bahati kwake Masterr 4 hakuwa amesahau kumlinda , ilikuwa ni kidogo sana tu kuweza kujeruhiwa na Desmond , alijikuta akitoa tabasamu kumwangalia mwanamke huyo aliepiga magoti ardhini akipambana na maumivu.
Upande wa Roma alijikuta akishngazwa na tukio hilo ambalo limekaa kidrama zaidi , hakuweza kutarajia kama Kizwe ambaye hakuwa katika uhalisia wake kuweza kujitoa kafara kwa ajili ya Desmond ambaye pia alikuwa amepitia mabadiliko na kupoteza uhalisi wake.
Ijapokuwa mwili wa Kizwe ulikuwa na uwezo wa juu wa kujiponyesha lakini nishati ambayo imetoka katika Dhana ya Master 4 ilikuwa na kiwango kikubwa cha nishati ambayo haipo kwenye uwiano sawia na mwili wake ili kuweza kupona.
Wakati nguvu ile ya kijini ikitafuta balansi katika mwili wa Kizwe ili aanze kupona eneo ambalo limetoboelwa lilizidi kuongezeka ukubwa na kumfanya damu kuzidi kupotea chini na hakukua na namna ya kuzuia.
Desmond alijikuta akimshikilia Kizwe huku akiwa na macho yaliokuwa mekundu.
“Umefanya nini , kwanini umenikoa , umekua kichaa?”Aliongea kwa sati kubwa ya hasira kama vile ni mwenye hatia na kumfanya Kizwe kuinua mkono wake kwa taabu sana akitaka kumshika Desmond shavu lakini nguvu zake zilizidi kupotea na kuishia njiani .
“Mtoto mjinga … mimi ni mama yako ..”Aliongea Kizwe kwa sauri dhaifu.
Machozi yake alishindwa kuyazuia na yalidondokea katika kifua cha Kizwe na kupita moja kwa moja mpaka chini Ardhini kupitia tundu la jeraha.
“Na … najua ulikuwa ukichukizwa na mimi na unaniona kama malaya hivyo kuniona siwezi kuwa mama yako tena … lakini Des.. mond kwangu wewe siku zote utabakia ,, utabaia ,,,ku..kuwa mtoto waaang..” Kabla hata hajamalizia herufi ya mwisho ya sentensi yake palepale kichwa chake kikalegea na ndio ukawa mwisho kamili wa uhai wake.
“No!!”
Desmond alishindwa kujizuia na kujikuta akitoa ukulele ulichonganyika na maumivu makali , yalikuwa maumivu kama ambayo aliyapata siku alipoambiwa mama yake amefariki na muda huo huo maumivu yale yalijirudia..
Lekcha na shoti zake za Anti -matter alijaribu kila namna ya kuweza kummaliza Master 4 lakini ilikuwa ni kama vile mapigo yake ni dhaifu sana, lakini licha ya hivyo hakutaka kuleta kabisa ujinga kwani alipaswa kuimaliza kazi mapema , hakujali kufariki kwa Kizwe , kwanza katika maisha yake hakuwahi kumpenda na alikuwa amemtumia tu kukamilisha mipango yake ya kupata nguvu na mtu aliekuwa akimpenda kwenye maisha yake ni mwingine kabisa.
Roma palepale aliweza kuzingirwa na nguvu ya Ant – matter ambayo ilikuwa ikimzunguka kama kimbunga na alijitahidi kutengeneza baridi kali ili kujaribu kuipunguza kasi na hakutegemea mbin yake kufanya kazi baada ya kuona mafanikio na kutengeneza annihilation.
Hakutaka kuchelewa zaidi kwani palepale alichukulia hilo kama faida kwake kwani alitoka katika kimbunga kile cha Ant Matter na kwa spidi ya juu alimsogelea Lekcha akinuia kumshambulia.
BOOM!!!
Shambulizi lake lilileta mafanikio kwani baada ya kumsogelea Lekcha alimtandika kisawa sawa ngumi ya kichwa na kuuchangua kichwa chake.
Kichwa chake kilipasuka vipande vipande kama vile kimepigwa na bomu na damu pamoja na nyama nyama pamoja na ubongo vilianza kusambaaa hewani.
Lakini sasa sekunde hio hio tu mwili wa Lekcha ulibadilika na kutoa mn’gao wa aina yake huku zile nyama nyama na damu ziligeuka na kutoa shoti za umeme kama cheche kuelekea kila upande na kwa spidi kubwa sana na ilionekana kama vile ni shambilio , kwani cheche zile ambazo zilikuwa kama mishale midogo zilianza kumpiga Roma kwa spidi ya hali ya juu.
Ijapokuwa ni vjimishale vya Ant- matter vidogo sana lakini ilikuwa na nguvu yake na ikigusanana kitu chochote hutengeneza Annihilation(maangamizi) makubwa.
Roma alijua kama ataruhusu kuguswa na cheche hizo basi angepata pigo kubwa hivyo alijitahidi kukaa mbali na kujilinda kwa wakati mmoja.
Dakika ileile baada ya Lekcha kuona Roma anajikinga ghafla tu mng’ao ule wa ant-matter ulipotea na Lekcha alirudi upya katika umbo la bindamu akiwa na sura ya Denisi.
Roma kwa wakati huo alikosa mbinu ya kummaliza haraka haraka Lekcha kwani alionekana kushambulia kwa tahadhari na aliweza kukiri kimoyo moyo Lekcha alikuwa ni tofauti kabisa na Yan Buwen katika kupambana, alichokifanya ni kujaribu kumshambulia na moto wa rangi nyuepe na wa Bluu kwa wakati mmoja lakini mashambulizi yake yalionekana kukosa nguvu kabisa ya kumdhuru Lekcha.
Licha ya kwamba mapigo yake yalionyesha uwezo wa kumletea maangamizi lakini kwa wakati mmoja ilimfanya Lekcha kuweza kurudi katika hali yake ya kawaida.
Kilichomkasirisha zaidi Roma ni namna ambavyo Lekcha hakuonyesha mpango wa kuachana na mwili wa Denisi na mpaka hapo alijua huenda sio tu kwamba alikuwa amejibadilisha sura kuwa Denisi bali mwili wake ulikuwa umeungana pamoja na wa kwake.
Upande wa Desmond baada ya kutoa kilio cha uchungu mwingi hatimae aliinua sura yake na kumwangalia Raisi Jeremy kwa macho yaliojaa chuki .
Raisi Jeremy hakuwa na kinga tena kwani medali yake haikuwa na uwezo wa kumlinda mara mbili na sasa alikuwa ni mwepesi sana kuweza kushugulikiwa na Desmond.
“Haya yote ni kwasababu yako umemuua mama yangu na nitakuua , nitakucharua charua”Aliongea ka kufoka huku akimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi lakini Master 4 ambaye alikuwa mdhaifu aliweza kumkinga Desmond na nguvu ya kijini.
Kutumwa kwake kuja hapo alihitajika kumlinda Raisi Jeremy kwa hali na mali kwani ndio mwakilishi pekee wa mipango yao juu ya uso wa dunia hivyo hakutaka kushindwa kutimiza wajibu wake.
Siraha yake ambayo aliitumia kumuua nayo Kizwe alimshambulia nayo Desmond na ilikuwa ni kwa bahati aliweza kushitukia pigo hilo kwani alifanikiwa kukwepa lakini kwa wakati mmoja akikatwa mkono , jambo ambalo hakuonyesha kuathirika sana kwani mkono wake uliweza kurudi upya ndani ya sekunde tu.
“Desmond umekuwa kichaa? , huyo mwanamke sio mama yako , mama yako alikufa na huyo malaya ametengenezwa na yule mpuuzi mwenzake , alitutelekeza mimi na wewe unawezaje kumuita huyo ni mama yako ilihali hana thamani yoyote ya kuwa sehemu ya familia yangu?”
“Huna aibu baba , eti hana thamani , unafikiria ilikuwa hiari yake kuwa katika hali hio? , kama sio wewe ambaye uliamua kutoka nje ya ndoa na kupata mtoto unadhani haya yote yangetokea , hivi unafikiria kila kitu kilichomtokea ndio alichotoka , amegeuka kutoka kuwa mtu wa heshima na muungwana na kuwa malaya ambaye anachukuliwa na kila mmoja , je haya yote aliomba kumtokea? , ni kwasbabu ya wewe , umemuua mama yangu unapata wapi uthubutu wa kujiita baba yangu?”
Desmond kwa hasira kali alimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi kali huku awamu hii akinuia kumuua kwa namna yoyote ile.
Upande mwingine Lekcha alikuwa amemzingira Master 4 na kimbunga chakc cha shoti za Ant-matter na alishindwa kujua namna ya kumlinda tena raisi Jeremy.
“Roma mimi ni baba mkwe wako niokoe”Aliongea Raisi Jeremy kwa nguvu mara baada ya kuona hakuwa na msaada mwingine kwani Master 4 alionekana kuzidiwa.
Ijapokuwa Roma alikuwa akipambana na Lekcha lakini macho yake pia yalikuwa yakimwangalia Raiai Jeremy asidhurike , alijiambia huyo ni baba yake mzazi wa Edna na kwa na namna moja amna nyingine anapaswa kumlinda.
Roma hakutaka hata kuwaza ni kwa na namna gani Edna angemchukia mara baada ya kusikia ameshindwa kumlinda baba yake, hata kama Edna asingefahamu hilo asingepaa ujasiri wa kuweza kumsogelea tena.
Kabla ya Demsond kumfikia Raisi Jeremy palepale alijikuta akifunikwa mwili mzima na moto wa rangi nyeupe na kuanza kuyeyushwa mwili wake kwa spidi.
“Mama… Arggghhh!!”
Alijikuta akishindwa kuhimili maumivu na kwa wakati mmoja akishindwa kuuzima ule moto mwilini mwake, licha ya kuwa na uwezo wa kupona kwa haraka lakini spidi ya mwili wake kuungua ilikuwa ni kubwa mno.
Raisi Jeremy alijikuta akitokwa na jasho jingi mara baada ya kuona namna ambavyo Desmond alikuwa akitoa kilio , kama mzazi alijikuta akiona uchungu kwa swala kama hilo kutokea , lakini kwa upande mwingine aliona hicho ndio anachostahili.
“Mwanaharamu wewe , unastahili kuchomwa moto mpaka kufa , unathubutu vipi kunisaliti mimi baba yako ,nenda kuzimu na huyo mpuuzi unaemwita mama yako”Aliongea kwa hasira na muda uleule aliusogelea mwili wa Kizwe na kuupiga teke.
Desmond alikuwa akiungua na moto wa kijini ambao uliunguza nguo zote na sasa ulikuwa ukiunguzwa mwili na mifupa , alijaribu kutambaa kumsogelea mama yake aliefariki lakini alijikuta akikosa nguvu na kutawaliwa na maumivu na aliishia kulia kama mtoto mdogo.
Ilichukua dakika chache tu mwili wake wote uliyeyuka na vumbi lake likapotea kabisa kwenye hewa.
Roma ambaye aliweza kuona kila kitu alitamani kumyeyusha na baba mzazi pia lakini hakutaka kufanya hivyo kwa ajili ya Edna tu , alikuwa na chuki na Jeremy kwani alimuona mtu ambaye ana siasa nyingi na atakuja tu kumsumbua na mke wake.
“Naona umeweza kuharibu kabisa mipango yangu”Aliongea Lekcha kwa kejeli huku hasira zake zikiwa za viwango , kwa namna ambavyo Roma alikuwa akijiamini ilimfanya kuona anadharaulika.
“Kwa mbinu zako angalau naona kabisa huwezi kuhimili muda mrefu”
“Acha majigambo nitakupa nafasi ya mwisho ya sisi kufanya kazi pamoja?”
“Unataka tufanye kazi gani?”Aliuliza Roma.
“Nifuate mimi na tuubadilishe huu ulimwengu uliojaa ufisadi”
“Unataka mimi na wewe tuubadilishe ulimwengu?”Aliuliza Roma akicheka.
“Upo sahihi , wewe si ndio wanakuita Mfalme Pluto sehemu ya miungu , bila kujali kama kweli wewe ni sehemu ya miungu mimi na wewe tuna nafasi kubwa ya kubadlisha huu ulimwengu?”
“Hahaha.. hakika wewe ni tofauti kabisa na Yan Buwen , angalau yeye alionekana kachizika lakini wewe ni mwendawazimu”
“Wewe ndio mwendawazimu kwenye macho yangu , hustahili kabisa hata kupewa cheo cha U’pluto , huna thamani wala nguvu kwa sifa unazopewa”
“Wewe ni mtu wa aina gani unajiita mungu? , unapaswa kufaidika kutokana na cheo chako lakini nyie miungu mmeamua kuficha vichwa vyenu huku mikia yenu ikionekana , eti hatutapaswi kujihusisha na mambo ya dunia wanafiki wakubwa nyie, bahati mbaya unafiki haupo kwenu tu ni kwa kila mtu na katika kila taifa ,sijutii kwa wewe kumuua baba yangu maana alikuwa mnafiki na yeye lakini najutia kwa wale wote ambao wanajifanyisha ni wa thamani ya juu zaidi na kutuona sisi hatustahili hata kuwasogelea , hebu muangalie mtu ambaye umemlinda sasa hivi unadhani ni mtu wa aina gani , yule ni mnafiki tu ambaye anadanganya taifa huku akiwa na ajenda zake kichwani , ni kiongozi gani ambaye yupo tayari kuua familia kwa maslahi yake , inasitikisha sana .
Kizwe ni mwanamke ambaye alijitaji mapenzi na kusamehewa pale anapoonyesha udhaifu, hata kama imetokea akaguswa na wanaume wengine anatoa wapi hukumu ya kumuua , kama hamtaki si angemtafutia sehemu na kuishi na kuachana nae , kulikuwa na haja yoyote ya kumuua?., haya ni mambo ambayo mimi Joseph Bikindi a.k.a Lekcha nataka kurekebisha , nataka kuondoa uovu wote ndani ya dunia , nataka kubadilisha dunia hii na kufuta kitu kinachoitwa siasa maana ndio chanzo cha ufisadi na uovu , hivyo Pluto unaonaje tukiungana pamoja na kufagia ufisadi wote na kuanza kuwapa watu uhuru kamili , falsafa yetu itakuwa ni kurudisha nguvu kwa wanyonge ili washindane wenyewe na hawa mashetani wasio na huruma , hakuna haja ya dunia hii kuwa na watu wenye nguvu huku hawafanyi chochote na hata wakichukua hatua ni kwa faida zao wenyewe , Mr Roma Ramoni nitaweka yote ulionifanyia nyuma yangu na tuungane pamoja kubadili dunia hii, Hebu tuungane pamoja”
SEHEMU YA 596.
Sauti ya Lekcha ilikuwa kubwa kiasi kwamba ni kama vile anataka dunia yote imsikie.
Usiku huo kulikuwa na upepo mkali na anga halikuwa na dalili yoyote ya wingu kuashiria kama kuna mvua inayoweza kunyesha, ni vivuli tu vya watu ndio vilionekana angani na kwa mtu ambaye alikuwa kilomita moja kwa umbali asingeweza kuona kinachoendelea zaidi ya kusikia sauti na baadhi ya vimulimuli vya hapa na pale.
Lakini kwa sauti yake ilifanya watu wa jiji la Kigali kuwa katika tahadhari kubwa na kutetemeka , ilikuwa ni kama vile Mungu anaongea na binadamu.
Baada ya kimya cha muda mrefu, Roma ambaye alikuwa na mwonekanao usiolezeka alivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha akainamisha kichwa chake chini na kuanza kucheka.
“Perhaps it is inapropriate for me to say that you are madman, not only you’re a madman but also a coward”Aliongea Roma kwa kingereza akimaasha kwamba huwenda inaweza isiwe sawa kumuita mtu kichaa ila ukweli ni kwamba yeye sio tu kwamba ni kichaa lakini pia ni muoga.
Kauli yake ilimfanya Lekcha kufika kilele cha hasira zake baada ya kusikia jibu hilo na alitamani kumrarua Roma palepale.
“Unaniita mimi muoga? ,, hahaha… nadhani unaota maana muda wenyewe ndio huu umeenda”
Roma hakutaka kujibuzana nae na palepale aliita moto wa njano na kuunganisha na moto wa bluu na nyuepe.
“Tumalize kabisa hili , nimekupa nafasi ya kuishi lakini ukaipotezea , hivyo kila kitu ambacho nilikosea kukifanyia kazi nitakimaliza leo hii mimi mwenyewe”
“Unafikiri barafu na moto ni vitu ambavyo vinaweza kunidhuru? Unachekesha sana”Aliongea huku akiwa na mwonekano wa dharau.
“Hujui lolote kwasababu bado hujawahi kupambana na mimi”Aliongea na hakutaka kuchelewesha, aliuelekeza moto wa kijini kumshambulia Lekcha kwa kasi kubwa.
Halikuwa shambulia la kawaida kwani ilikuwa ni kama vile chembe chembe zote za anga zilikuwa hazitembei huku eneo lote likiwa halina aina yoyote ya upepo na kuufanya ule moto kutoa nguvu kubwa ya kiroho.
Master 4 kuona tukio lile alijikuta akishikwa na mshangao kwani ni kitu ambacho hakuwahi kushuhudia , hakuwahi kuona rangi zote za moto kutolewa kwa wakati mmoja zikiwa zimeunganika , lakini haikuwa hivyo tu kilichomchanganya zaidi ni namna moto ule ulibadilika na kuwa kama vinyoka nyoka , alijua kama yeye ndio anashambuliwa basi ni shambulizi moja tu atakwa tayari amekwisha kufariki.
Alijimbia kwa nguvu ya kiroho ambayo alikuwa akihisi , hana uhakika kama wakubwa zake wote katika miliki ya ulimwengu wao wanaweza kufanikiwa kushinda , alishangaa mara moja na kujiuliza imekuwaje kijana mdogo akawa na uwezo wa aina hio.
Upande wa Roma hakujuwa kwamba alikuwa akimshangaza mtu kwa wakati huo kwani alichokuwa akiwaza ni kumalizana na Lekcha moja kwa moja na kwenda kulala na familia yak.
Ukweli ni kwamba Lekcha alikuwa tofauti sana na Yan Buwen na alikuwa ni kama vile alipenda kuonja kila pigo ambalo alikuwa akipelekewa na Roma , kwani hakukwepa mashambulizo yake na hata ule moto aliacha umshambulie.
Ajabu ni kwamba licha ya Roma kuweza kutumia nguvu kubwa sana ya kutawala moto huo kushambulia lakini mbele ya nishati ya ant-matter ilionekana kutofanya kazi, nguvu ya Lekcha ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba moto ule ulikuwa ni kama vile unanyonywa na kuzimika kila unapogusana nae.
Roma kwa levo aliokuwa akitumia alijua ilikuwa juu zaidi kuliko aliotumia kupambana na Yan Buwen mpaka kumuua na ilimshangaza kwamba wakati huo Lekcha licha ya kumsbambulia alionekana kabisa hana hofu na chochote anachomuandalia na alikuwa na maendeleo ya juu mno.
“Hehe.. naomba unajitahidi sana hata hivyo nitakuchukulia kama jiwe la kujiimarisha zaidi ili niweze kutimiza malengo yangu , naona kabisa mbinu zako zote zimefikia ukomo, ni muda sasa kukuonyesha uwezo wangu halisi”Aliongea Lekcha.
Sekunde hio hio alibadilika kabisa na hakuwa biadamu tena bali nguvu yenyewe ya Ant-matter na alianza kwa kuwa kama mpira wa miguu na akaendelea kutanuka huku shoti zikisambaa kila kona na mpira ule ulizidi kujizungusha na kuanza kuonekana kuwa mkubwa zaidi .
Ni muda uleule wakati Roma akishangaa aliweza kuona shimo likijitengeneza juu yake na liliongezeka ukubwa huku anga likiwa ninazunguka kama vile kimbunga au singularity inayotokea juu kuja chini na ndani ya dakika chache tu sehemu aliosimama ni kama vile yupo kwenye chumba ambacho hakina hewa ndani yake na ilimfanya kushindwa kuita nguvu ya kimaandiko kumlinda kwani alishindwa kuwasiliana na elementi za dunia.
Kilichomshangaza Roma ni ufahamu wake kuanza kumpotea na kujihisi kama vile anaendeshwa kwa rimoti na hakuwa na uwezo wa kusogea kurudi nyuma wale mbele, alisimama kama vile ni sanamu.
“Chochote utakachofanya hakina maana , nishati yangu ya Ant – matter imeongezewa ubora kwa viwango vya juu na kuwa na tabia tofauti na zile ambazo wanasayansi wa kawaida wanajua , yote hayo yamefanikiwa kupitia kifaa maalumu cha kuibadilisha , unafikiri ningekuja kushindana na wewe nikiwa na nguvu kama zile za Yan Buwen … kinachotokea hapo ni matumizi ya magepu yaliopo kati ya anga mbalimbali zilizo sambamba, kwa uwezo wako huo licha ya kuwa na uungu ndani yako huwezi kuitoa roho yako na kutawala mwili mwingine maada itakuwa halali yangu”Sauti ya Lekcha iliweza kusikika lakini Lekcha mwenyewe hakuweza kuonekana na upande wa Roma aliweza kusikia kama vile ni mwangwi.
Roma uso wake ulianza kujikunja kunja kwa namna ya kulazimishwa huku akijaribu kuzuia mwoneknao wake usibadilike lakini mzunguko wa nguvu ya Ant-matter ulikuwa ukifyonza nguvu zake za mbingu na ardhi kila alipokuwa akijaribu kuziita ili kujiondoa kwenye mtego huo , mbaya zaidi ni kiwango kidogo sana ambacho alikuwa na uwezo wa kukiita kutokana na kuingizwa katika eneo ambalo kulikuwa na elemeti za anga hivyo kushindwa kufanya mawasiliano.
Roma alijikuta akipandwa na hasira na kujiambia alimchukulia wa kawaida ndio maana yupo katika hali kama hio , alikuwa bado hajapigana na majini katika ulimwengu usio onekana lakini alikuwa akijiamini kwamba alikuwa na uwezo wa kuwashinda lakini anachofanyiwa na Lekcha kilimpagawisha kwa wakati mmoja na kujiona huenda ni dhaifu.
Roma hakutaka kufanya ujinga ni kweli alikuwa na uungu ndani yake alioweza kurithi kutoka kwa Pluto wa Zamani hivyo kumpa uwezo wa kutawala mwili wowote lakini alihofia kwamba anaweza kuingia katika mwili ambao hauna vigezo na anaweza kuanza upya moja kwa moja kuvuna nishati za mbingu , isitoshe nguvu za kijini hawezi kuhama nazo.
Roma mara baada ya kuona yupo hatarini aliona hana chaguo lingine zaidi ya kuita Chaos Cauldron.
Lakini moyo wake ulikuwa mzito mno kwa kuhofia roho iliokuwa ndani ya Cauldron inaweza kutawala akili yake na asingejua ni kipi ambacho angeweza kufanya baada ya hapo , alihofia hilo kumkumba kwani ingekuwa mwisho wake.
“Roma umeweza kuwashinda watu wengi sana lakini sasa kiko wapi ,,, unakufa kwenye mikono yangu , kabla haujafa ngoja nikupe usharu kama zawadi , udhaifu wako mkubwa unaokufanya usiwe na nguvu ni kwasababu ya wasiwasi wako … huu ulimwengu ni kama msitu na mwenye nguvu ndio anaishi , siku zote binadamu mwenye nguvu atatumia utashi wa mnyama ili kuendelea kuishi , lakini wewe unadhani kutoa kafara matamanio yako ndio utaonekana mjinga , muoga , usie jiamini na dhaifu ,,, hayo yote ndio yanakuua leo hii hustahitili hata kuwa mshindani wangu , wewe ni dhiafu sana”Aliongea Lekcha kwa majigambo na kisulisuli cha nishati ya Ant-matter kikizidi kuongezeka maradufu.
Upande wa Master 4 aliweza kushuhudia mabadiliko hayo lakini hakutaka kujihususha zaidi kwani sio kilichomleta na palepale alibadilika na kuwa kama mwanga wa moto na kupotea eneo hilo akiwa pamoja na Raisi Jeremy.
Lekcha hakutaka kujihusisha zaidi na wao zaidi ya kuweka umakini katika kumuua Roma , alijiambia ni rahisi zaidi kuwatafuta mara baada ya kumalizana na Roma.
Dakika hio hio katika kisulisuli kile cha nishati isio maada ilitokeza miale yenye muundo wa macho rangi nyekundu huku sauti ikibadilika na kuwa kama ngurumo kubwa za radi na kumfanya Lekcha kushituka
“Hiki ni kitu gani?”
Nguvu yote ya Ant Matter ilianza kukosa nguvu , malengo ya Lekcha ilikuwa ni kujibadilisha na kuwa Roma lakini katika hali hio alishangaa mabadiliko makubwa kwani ni kama kuna kitu kilichokuwa kikifyonza nguvu yake kwa hali ya juu sana.
Upande wa Roma hakujali kabisa yupo kwenye hali ya hatari kama hio, kitu pekee ambacho alioona ni sahihi kukifanya ni kutumia cungu chake cha maafa lakini kwa tahadhari kubwa nafsi yake isije kumezwa na mwili wake kutawaliwa.
“Nani unasema hastahili kuwa mshindani wako”Sauti nzito iliweza kusikika.
Nguvu ilikuwa kubwa mno kiasi cha kufanya ule msukosuko wa hewa kupotea palepale na kumfanya Lekcha kurudi katika umbo la kibinadamu, lakini ni kama vile amefanya kosa kwani hapo ndipo aliposhuhudia kilichokuwa chini yake huku ndani yake kukionekana uwepo wa macho ya mnyama.
“Damn it what kind of monster is that….”Lekcha alijikuta akianza kuhofia maisha yake , kwa hali kama hio aliona kabisa ana uwezo mdogo wa kuishi.
Roma hakujali kutoa jibu na alikifanya chungu chake kuzidi kumsogelea Lekcha hatua kwa hatua na kadri kilivyokuwa kikisogea ndio hali ya hatari ilivyozidi kumkumba Lekcha kwani nguvu inavomvuta ilimvamia kwa hali ya juu sana
“Pengine upo sahihi , ulimwengu huu una machukizo mengi , unastahili kuhurumiwa , unastahili kuonyeshewa wema, lakini kwa mtanzao wangu wewe ndio chukizo kubwa zaidi la ulimwengu huu , umesema ni viongozi ambao ndio mafisadi na unataka kupambana zidi ya siasa , kama ni hivyo kwanini ulitaka kujibadilisha na kuwa Jeremy , umesema Kizwe ni mwanamke ambaye alikuwa na maisha magumu kama ni hivyo kwanini ukaaamua kumtumia na kisha ukampotezea , kama kweli ulikuwa ukimpenda kwanini hukumsaidia? , umesema miungu wameficha vichwa huku mikia yao ikionekana lakini kwanini ili tu kutimiza malengo yako unataka kuua watu utakavyo , ni haki gani ambayo unataka kutenda. Upo sahihi mimi Roma sina nguvu na siku zote ni muoga na mwenye wasiwasi mwingi na sina matamanio makubwa na ni mbinafsi na sistahili kabisa hata kuubadilisha huu ulimwengu..”
Wakati anamalizia kuongea alikuwa karibu kabisa na Lekcha na chungu chake kilikuwa kimemsogelea karibu zaidi na ilikuwa ni kama sunami , ni kama anga limekusanywa na kuwekwa sehemu moja na kuchezeshwa.
“Licha ya madhaifu yangu yote hayo sijawahi kujikataa , sijawahi kuficha udhaifu wangu , unafiki wangu na ubinafsi wangu ..mimi ndio mimi Roma ambaye uliweza kukutana nae kwa mara ya kwanza na sijabadilika, kwako wewe Joseph Bikindi mtu muoga sana , umeamua kutotumia sura yako halisi ili tu kutimiza malengo yako huku ukitumia mbinu zako za kusikitisha huku ukijifariji kwa uwezo wako mdogo , unachokionyesha ni inferiority Complex , wewe ni mtu ambaye huna lolote , wewe ni muoga ambaye unaogopa kuuangalia ulimwengu kwa jinsi ulivyo , kwa sifa zako hizo za kiuoga woga unathubutu vipi kupigana na mtu kama mimi”
“Mimi sipo hivyo , unangea upumbavu”Lekcha aliikuwa akijaribu kujitetea .
“Haijalishi kwasababu leo ndio mwisho wa maisha yako”
Roma palepale alizidi kubadilika na alikusanya nguvu zake zote na kukilisha kile chungu na ilimpelekea nguvu yake ya mvutano kuwa kubwa zaidi kama shimo jeusi .
Chungu hicho kilikuwa na uwezo wa kumeza kila kitu hata kama ni Ant Matter , nishati ambayo hufanya kazi kinyume na fizikia , hivyo kwa haraka haraka ni kwamba Lekcha hakuwa na pakukimbilia mbele ya Caulrdon.
Lekcha mpaka hapo alijua akileta mchezo ndio kifo chake , hivyo alitumia kila mbinu aliokuwa nayo kujaribu kukimbia lakini nishati yake ilikuwa ikimezwa kwa spidi kubwa na kumfanya kuzidi kuwa dhaifu.
Ilikuwa ni dakika chache tu wakati Roma akitaka kummaliza kabisa Lekcha kwa kumsukumia kwenye tanuru la kimaafa akili yake iliweza kuvamiwa palepale .
Roma alihisi ni kama ubongo wake umeingiwa na mdudu ambaye alikuwa akitifua tifua kuona sehemu ya kukaa.
Dakika ileile ni kama vile chungu hicho kiliachana na Lekcha na kiumgeukia Roma kuanza kushindana nae , ilikuwa ni mashindano ya nafsi na nafsi na Lekcha baada ya kuona amekuwa huru kutoka katika mvutano palepale aliona hi ndio nafasi pekee ya kukimbia , hakutaka kujiuliza kwanini imetokea hivi na vile lakini utashi wake ulimwambia aokoe maisha yake kwa vyovyote iwezekanavyo.
Alikusanya nguvu ya Ant Matter iliobakia katika mwili wake huku matamanio makubwa ya kujiokoa yakimpa nguvu ambayo ilimuwezesha kukimbia.
Lakini sasa dakika ileile anaweza kujiokoa upande wa Roma aliweza kuitawala akili yake kwa mara nyingine na kudhibiti nafsi ya mnyama iliokuwa kwenye chungu.
“Unaenda wapi?”
Aliongea Roma kwa nguvu akimwangalia Lekcha ambaye anajaribu kukimbia na alichokifanya Romna ni kumsogezea karibu zaidi chungu chake na kumfanya Lekcha kuzidi kuvutwa.
Ghafla tu ulipiga mwanga wa rangi ya Silver kama flash , ilikuwa ni kama mlipuko na uliweza kufanya mwili wa Denisi kujiachia na palepale ukamezwa na Cauldron.
Lekcha alijua kitu pekee ambacho kitamuokoa ni kuishi kama roho yenye umiliki wa nguvu ya Ant matter energy ili kujiuzia kutomezwa na chungu, ndio maana akaamua kuupoteza mwili wa Denisi.
Roma alishindwa kugundua hivyo mapema baada ya mwili wa Denisi kumezwa na chungu chake na baada ya kuelewa kilichotokea aliweza kugundua ni hila za Lekcha kujaribu kutoroka , kilichomezwa ni mwili usiokuwa na roho.
Mbinu aliotumia Lekcha iliweza kumuokoa kwani alitumia sekunde chache tu ambazo Roma alikuwa akizubaa na kupotea mbele yake akiwa ameipatanisha nafsi yake na nguvu ya Ant- matter energy hivyo kubakia katika umbo la mtu aliekuwa kama nishati.
Roma licha ya kugundua amechelewam hakutaka kumuacha aondoke kizembe , ijapokuwa Lekcha alipotea kwa haraka lakini alikuwa bado akipatwa na msisimko wa uelekeo wa nguvu ya Ant – matter na aliitumia hio kumfukuzia.
Roma palepale alirudisha chungu chake na kuanza kumfukuzia Lekcha ambaye alikuwa ni kama mwanga unasafiri angani.
Lekcha aliweza kuelewa hakuwa na spidi ya kutosha ya kumshinda Roma na kujua muda si mrefu anaweza kukamatwa na hapo ndipo wazo la mwisho la kujiokoa lilimjia akilini.
Ilikuwa ni njia pekee ambayo alikuwa ameipanga kwa ajili ya kujiokoa , akiwa katika hali ya hatari na muda kama huo ndio wazo hilo liliweza kumjia akilini na alitoa tabasamu la nia ovu, alijua kwa vovyote vile hakuna namna ambayo Roma anaweza kumdhuru kama atatekeleza wazo lake.
Upande wa Roma hakujua Lekcha anataka kufanya nini kwani ghafla tu alibadilisha uelekeo , lakini licha ya hivyo hakutaka kumuacha , alipanga kummaliza kabisa usiku huo huo.
Zilipita kama dakika herathini za Roma kumfukuzia Lekcha , shukrani kwa spidi ambayo walikuwa wakitumia hawakuweza kuonekana katika maeneo ambayo yalikuwa ni mchana.
Sasa baada ya kufika katika kilele cha mlima ambacho kwa ufahamu wa Roma katika matumizi ya Ramani aliweza kugundua eneo hilo ni ndani ya China , ilikuwa ni rahisi kusema ni mpaka unaoitengeanisha China na Mongolia.
Roma hakuelewa Lekcha anataka kufanya nini ila hisia zake zilimwambia kabisa amefikia mwisho wa kukimbia.
“Emei!!!”
Roma moyo wake ulipiga Kite kwa nguvu mara baada ya kugundua nini Denisi anataka kufanya.
SEHEMU YA 597.
Sio kwasababu tu ya Skendo ndio ilioweza kumfanya Sophia kuachana na maswala ya muziki.
Na sio pia kwasababu ya Skendo ndio akaamua kupotezea hisia zake na kuacha kabisa kumfikiria Roma au kuwa na mpango wa kutokuendelea kumtaka la hasha , mrembo Sophia alikuwa na lake kichwani ambalo alikuwa akipanga , alijiambia alikotoka ni mbali kuliko anakoelekea.
Kuachana na usanii na kurudi Japani ilikuwa ni kisingizio tu lakini katika kichwa chake alikuwa akipanga kujifunza kwa bidii zote namna ya kuvuna nishati za mbingu na Ardhi ili kuwa katika levo ya juu ya kuweza kubeba ujauzito wa Roma akiwa wa kwanza, hakujali Rose na Magdalena walikuwa wamemtangulia lakini alijiambia kutangulia sio kufika na isitoshe kupanda levo hakukutegemeana na muda wa mafunzo bali uwezo wa mtu kuelewa siri alizofichiwa binadamu juu ya ulimwengu.
Sophia aliamini kama ataweza kuwa katika levo za juu za mafunzo ya kijini hata hitaji kuwa na juhudi kubwa za Roma kumtaka.
Maelekezo ya namna ya kuvuna nishti za mbingu na Ardhi huwa mara nyingi yanahitajika maelezo ya mara moja tu ya namna inavyofanyika na baada ya kuelewa kinachofatia ni kazi ya mtu mwenyewe kuweza kufanya Tahajudi na kufikiria ili kupata ufunuo, isitoshe katika kujifunza mbinu za kijini hakuhitaji kuuliza maswali kwani hata kama uulize swali hakuna ambaye anaweza kujibu kutokana na msingi wa kwamba kila moja anapata ufunuo wa kwake mwenyewe juu ya kuweza kuvuna nishati hizo, mwisho wa safari unaweza kuwa mmoja lakini njia zikatofautina hio ndio maana ya uzoefu binafsi unaohitaji kutafuta jibu mwenyewe kwa kila swali.
Sophia alikuwa akielewa msingi huo na ndio maana hakuona haja ya kuwa na Roma karibu ili aweze kupanda levo bali ni juhudi zake pekee ambazo zingeweza kumpandisha Levo kwa haraka.
Hatua ya kwanza kwa Sophia ni kurudi Japani kwa wazazi wake na baada ya hapo angetafuta eneo tulivu ambalo lingemuwezesha kuvuna nishati ya mbingu na ardhi na sifa za eneo ambalo alikuwa akitaka Japani haikuwa jibu.
Temple ambalo alijifunzia Kung fu , maarufu kwa jina la Emei ndio mahali alipoona panamfaa sana , Emei ni Temple ambalo lilikuwa likipatikana katika mlima wa Emei katika dhehebu la Shushan chini China.
Roma licha ya kwamba hakumtafuta Sophia tokea siku ambayo ameondoka baada ya kutangaza kuachana na mambo ya usanii sio kwamba hakumfatilia.
Kitendo cha kumuona Lekcha ananyoosha moja kwa moja juu ya mlima wa Emei ilimkumbusha kwamba Sophia alikuwa akiishi katika eneo hilo na jambo hilo lilimfanya moyo wake kupiga kite kwani hakutegemea Lekcha angekuwa na uelewa juu ya Sophia kupatikana eneo hilo , kwa jinsi ambavyo walisafiri muda mrefu ilionekana hilo ndio wazo lake Lekcha la muda wote.
Akili yake ilifanya kazi kwa haraka sana na kitu pekee ambacho alihisia ni huenda Lekcha aliweza kufahamu eneo hilo kwa kuweza kutumia kumbukumbu za Denisi maana hata yeye alijifunzia mafunzo yake hapo.
Ndani ya eneo hili Shushan ndio mahali ambapo Sophia alikuwa akifanyia mazoezii yake ya kuvuna nishati ya mbingu na ardhi.
Ilikuwa muda wa asubuhi ndani ya Shushani , eneo hilo lilikuwa limejengwa kwa mtindo wa kizamani zaidi ni rahisi kusema Shushan ilikuwa na mfanano wa kiasi kikubwa na Dhehebu la Tang sehemu ambayo Magdalena alisomea mafunzo yake ya kichawi.
Katati ya eneo hilo kulikuwa na mnara(Tower) ,mrefu kwenda juu ambao ulikuwa umejengwa kwa utofauti mkubwa na minara iliokuwa katika madhehebu mengine, mnara huo ulikuwa na historia ndefu na inasemekana mnara huo ulikuwa ndio wa kwanza kujengwa kabla ya ujenzi wa nyumba na makazi ya kidhehebu na ni zaidi ya miaka mingi iliopita na hakuna historia yoyote ambayo ilieleza ni nani alihusika katika ujenzi, eneo hilo licha ya kuwa chini ya dhehebu la Shushani lakini kuhusu mnara ilikuwa siri ya taifa la China.
Sasa wakati huo ndani ya ukumbi mkubwa ndani ya eneo hilo walionekana wanawake wanne waliokuwa katika mavazi ya vitamba vya hariri vya rangi nyeupe , kati ya wanawake hao ni mmoja tu ndio ambaye alionekana kuwa na utofauti na wengine wote kutokana na rangi yake kuwa na mchanganyiko wa Kiafrika.
Sasa ilikuwa ni dakika chache tu wanawake hao wakati wakiongea kwa furaha ghafla tu kivuli cha mwanga wa Silver kiliweza kuonekana kikiingia hapo ndani na kusogelea wale wanawake kwa spidi kubwa.
Ilikuwa ni dakika ileile wale wanawake walijikuta wakipatwa na mshituko wa ghafla na kukwepa, yule mwingine aliekua na utofauti alijikuta akishikwa shingonni na kitu chenye ubaridi wa aina yake, akiwa kama yeye ndio aliekuwa mzembe wa kuwa kama wenzake lakiini ukweli ni kwamba wale hawakuwa walengwa ndio maana waliweza kuponyoka.
“Ring!!!”
Ulikuwa ni kama mlio wa kengele yule mwanamke alijikuta akifungwa kuanzia miguuni na shingoni kimajaabu na nyuzi za nishati ya Ant- matter.
“Sophia..!!”
Walijikuta wale wanawake wengine wakipiga makelele baada ya kuona kile kinachomtokea mwenzao.
“Wewe ni nani?”Walianza kupiga kelele kwa lugha ya Kimandari na kingereza kwa wakati mmoja.
Sophia akiwa katika hali ya aibu ya kutoweza kujiokoa na chuki alijikuta akishangaa kuona kiumbe kilichokuwa na muonekano wa kibinadamu , ilikuwa sahihi kusema kiumbe kutokana na mwonekano wake kutokuwa wa kawaida lakini palepale kiumbe kile kilibadilika na kuwa katika umbo halisia lakini sura yake bado hakuweza kuitambua.
Sophia alijaribu kuita nguvu ya kijini ili kuweza kujitoa katika vifungo alivyofungwa lakini hakufua dafu na kujikuta kuzidi kujawa na hofu , kilichomshangaza zaidi ni kwamba nguvu ambayo ilikuwa memfunga miguu yake haikuwa ya kawaida kabisa na ilikuwa katika hali ya ubarafu.
Dakika ileile wakati Sophia akifurukuta alijikuta akipigwa na mshituko zaidi mara baada ya Roma kuonekana mbele yake na mpaka hapo akili zake zilimwambia yupo katika hatari.
“Roma..!!”
Ijapokuwa wakati huo mtu aliemfunga kimaajabu alionyesha zaidi ukali wake lakini kwa Sophia alijikuta akipatwa na furaha isiokuwa na kifani , hakuamini angeweza kumuona Roma katika eneo hilo.
“Muachie tafadhari , matendo yako ndio yatarahisisha kifo chako”Aliongea Roma.
Roma mara baada ya kuona kuna nguvu ambayo imeifunga miguu ya Sophia alijua kabisa hapo anapaswa kuwa makini la sivyo ataleta matatizo zaidi.
Roma alijiambia huyo mwendawazimu amefanya chaguo sahihi kabisa kuja kujaribu kumteka Sophia maana alikuwa akimjali sana , ijapokuwa hakuweza kujua ni kwa namna gani mpaka aliamua kufanya chaguzi hio lakini ukweli ni kwamba kwa namna yoyote asingeweza kuona Sophia akipata matatizo.
“Umafikiri najali hilo , kwasababu najua naenda kufa nitamshikilia kama mateka ili nniweze kutoroka, najua una upendo wa juu sana kwa huyu mwanamke”
Roma kabla haa hajaongea Sophia alianza kuongea yeye kwa nguvu.
“Unaongea ujinga, wewe ni nani kwanza ?, mimi sio mwanamke ambaye Bro Roma ana mapenzi nae”
“Hahaha… Sophia kama nitakuwa sijakosea mashabiki zako wanatarajia ujio wako wa mara ya pili katika usanii tena kwa kishindo , wewe tayari ni Celebrity k wanini unajaribu kujishusha , nilishangaa sana kupata taarifa umekuja kujichimbia huku mbali maporini, halafu sijasema neno mapenzi bali nimesemea swala la upendo , inawezekana ni upendo kati ya dada na kaka hehe..”
Sophia mara baada ya kuumbuliwa aijikuta akigeuka kuwa nyanya kwa aibu.
Upande wa Roma hakuwa tayari kumuona Sophia akiwa hatarini na alijitahifi kuvuta pumzi ili kuweza kujituliza.
“Kwahio unadhani kumfanya mateka ndio kutanifanya nishindwe kumuokoa na wewe kukuua?”
“Haha,, kama unachosema ni kweli basi jaribu tuonea nani atakuwa na spidi ya kumuua mwenzake , mimi kumuua huyu mwanamke au wewe kuniua mimi”
Sophia baada ya kusikia maneno hayo aliweza sasa kuelewa nini kinachoendelea , alijua kwamba aliemteka ni adui wa Roma.
“Roma wewe huna haja ya kunijali mimi na kuanza kumsihi aniachie, anaonekana kuwa mhenzi kweli hivyo unapaswa kumuua ,sitojali kama nitadhuli…”Kabla hata hajaendelea kuongea alihisi maumivu makali kwenye shingo yake.
“Unamaanisha nini kwamba nisikujali wewe , kaa kimya maana sijakupa nafasi ya kuongea”Alifoka Roma huuku akimwangalia Sophia kwa macho makali.
Sophia palepale alijikuta akitoa machozi mengi huku akimwangalia Roma lakini upande wa Roma hakutaka kujali machozi yake bali usalama wake kwanza.
Roma palepale alisogea mbele huku akiachia mkandamizo mkali wa hewa wa levo za juu katika kuipita dhiki.
Kitendo cha Lekcha kuhisi mkandamizo ule aliona Roma alikuwa akipingana na onyo lake , Lekcha alikuwa akielewa kwamba kadri Roma anavyochelewa kufanya maamuzi ndio itamuonyesha ni kwa namna gani mateka wake ana thamani.
Lekcha palepale alitoa kamba nyingine kama shoti za Ant-Matter tatu kwa pamoja na kuwakaba shingo wale wanawake wengine waliokuwa wamebakia. Na hali hio ilimfanya Roma kusimama na kuacha kutoa mkandamizo.
“Unaonaje , mipango yangu imefeli kwasababu nilikudharau lakini hii hamaanishi kwamba wengine wanaweza kuhimili mashambulizi yangu , ijapokuwa mimi sio wewe lakini gepu la utofauti wetu kinguvu sio kubwa , hivyo kubali ninachokuambia la sivyo kabla hujanifikia mimi utaokota kwanza maiti ya huyu mrembo”
“Kwahio unanitishia?”
“Utanifanya nini kama unaona na kutishia , najua utahesabu kila kitu kilichotokea nyuma na utaniua kwa namna yoyote ile , hivyo kwanini nisihakikishe nawewe nakupisha kwenye machungu kabla ya kunifikia”Aliongea na kumfanya Roma kupandwa na jazba lakini mpaka hapo hakuwa akijua ni kipi anapaswa kufanya maana asingeweza kukubali kumuona Sophia akigeuka na kuwa maiti.
“Una taka nini?”Aliuliza Roma huku akikunja ngumi yake kwa hasira kiasi cha kufanya kucha zake zitoboe kiganja cha mkono.
‘Tutafanya hivi kwani ni rahisi sana , utaondoka hapa kwenda mbali baada ya kukuwekea nguvu kiasi ya Ant-Matter ambayo itanifanya kujua ni umbali gani umefikia na baada ya hapo nitamuachia Sophia na kukimbia”
‘Kwahio unanifanananisha na kitoto cha darasa la kwanza si ndio ?, kama nitakuacha hapa na kufanya unavyotaka sio tu kwamba utaendelea kumshikiria lakini pia utaenda kujificha na kunifanyia hila kwa mara nyingine, unajuaje huenda ukanigeuka pia na kumuua Sophia”
“Kwahio unataka nini , pointi ya msingi hapa ni wewe kufanya kama ninavyokuambia ,Sophia yupo mikononi mwangu na huna chaguo labda kama unataka kumchukua akiwa maiti “Aliongea na kumfanya Sophia amwangalie Roma na kuzidi kutokwa na machozi na ndani ya dakika kadhaa alijikuta akitoa tabasamu la uchungu , alikuwa ni kama vile kuna wazo limemjia.
“Roma siwezi kukurudisha nyuma na mipango yako”Aliongea
Wakati huo Roma alikuwa akiwaza achukue risk kumuokoa Sophia au afanye kama anavyotaka Lekcha
“Usiwe mjinga Sophia”Aliongea Roma kwa sauti lakini ni kama vile amechelewa kwani palepale Sophia alitema damu nyingi sana huku akiwa ni kama viungo vya ndani mwake vimepasuka.
Roma aliweza kujua Sophia ameweza kufanya jaribio la kujiua kwa kupasua mishipa yake ya damu na nguvu za kijini, hilo liliwezekana kutokana na Sophia alikuwa tayari amekwisha ingia katika levo ya mzunguko kamili.
Kitendo alichokiufanya kilimshangaza Lekcha , hakutegemea swala kama hilo kujitokeza , hakuamini kama Sophia angekuwa na uwezo wa kujiua kwa ajili ushindi wa mwanaume anaempenda
Kitendo chake cha kuchanganywa kidogo na Sophia palepale Roma alitumia nafasi hio vizuri kwani kwa spidi kubwa Roma alikuwa tayari ashamfikia Lekcha mbele yake na kumtwanga ngumi nziro ilioambatana na nguvu za mbingu na ardhi katika eneo la kichwa.
Kitendo cha kutawanyisha eneo la kichwa cha Lekcha hakutaka kusubiri tena kwani palepale alimnyakua Sophia na kupotea nae huku wakati huo huo akiita Caulrodn na kukiacha katika eneo hilohilo.
Roma alikuja kuibukia juu kabisa angani akiwa amemshikilia Sophia ambaye alikuwa amelegea kabisa shingo huku ikiwa haieleweki amepoteza maisha au vipi.
Hasira za Roma ndio ambazo zilimzidia mpaka kuita chungu cha maafa bila kujali matokeo na awamu hio kilikuwa na nguvu kubwa kuliko alivyokitumia mwanzo na kilikuwa na uwezo wa kuvuta kiumbe chochote chenye nguvu ya kiroho mpaka umbali wa kilomita moja.
SEHEMU YA 598A.
Chungu cha maafa kiliuelekezea mdomo wake sehemu ambayo amesimama Lekcha , lakini upande wa Lekcha alikuwa mwepesi sana kufanya maamuzi kwani aligeuka kutoka mwili wa kawaida na kurudi katika umbile la nishati lakini hata hivyo ilikuwa bure.
Lekcha kwa wakati huo alikuwa ametumia kiasi kikubwa sana cha nguvu ya nishati ya Ant- matter na yeye alikuwa tofauti na Roma ambaye nguvu zake hazikutegemea zile ambazo zipo nfdani yake , alikuwa na uwezo wa kuvuna nishati muda wowote na kuzitumia.
Ni muda huo huo mwili wake uliokuwa katika umbile la nguvu ya nishati ya Ant- matter ulianza kutawanyika vipande vipande.
“Hapana siwezi kufa …. Hapana!!”
Lekcha alijikuta akitoa ukulele wa aina yake kwani alishindwa kabisa kuzuia nguvu ya chungu kummeza.
Ilikuwa ni wakati ambao Lekcha aliona kabisa huo ndio mwisho wake, lakini katika hali ambayo hakuwa ameitarajia palepale kulitokea mabadiliko ambayo hayakugegemewa.
Roma mwenyewe hakuweza kutegemea kile ambacho kinakwenda kutokea , ule mnara uliokuwa umejengwa kwa usanifu wa kipekee ulikuwa ukionekana kama vile unacheza cheza , ilikuwa ni kama vile ni tetemeko kubwa la Ardhi ambalo lilikuwa likicheza cheza na ilichukua sekunde hio kulitokea boriti kama tano za mwanga uliokuwa kama Laser rangi ya dhahabuu na kugonga katika wingu ambalo lilikuwa likianza kuzunguka kama vile mvua inataka kunyesha.
Pale juu ya kichwa cha mnara ni kama kulikuwa na kimashine amaalumu kinachofanya kazi na kudhalisha boriti hizo za mwanga.
Cauldron yenyewe palepale iliweza kuzimika na nguvu yake ya mvutano iliisha na ikawa pona ya Lekcha kumezwa.
Roma mwenyewe hakuwa akieleewa ni kitu gani ambacho kinatokea katika hilo eneo na alianza kuzungusha kichwa chake kuangalia kulia na kushoto, hisia ambazo alikuwa akipata zilikuwa tofauti na zile za kupigwana radi baada ya kukiuka kanuni za anga.
Nafsi iliokuwa kwenye Cauldron na yenyewe ilianza kufurukuta kwa namna flani ya kuonyesha woga na jambo hilo lilimshangaza Roma na kujiuliza nini kinatokea
Lekcha ambaye alikuwa dhaifu sana hakuweza hata kukimbia licha ya kuachiwa na chungu na baada ya kuona Roma hakuwa akimwangalia palepale alijaribu kujitengenezea kamba kama vile ni Spider man ili kukimbia lakini ghafla tu ilitokea Flash ya mwanga mkali pamoja na shoti ya aina yake kwenye ule mnara.
Kitendo cha Lekcha kutaka kukimbia tu alijihisi nguvu ya ajabu ikimrudisha nyuma .
“Buzzz!!!!”
Ulisikika mlio wa aina yake wa Radi kutoka katika mawingu yaliokuwa yakizunguka juu na kupiga kwa nguvu ule mnara na kusababisha mpasuko mkubwa wa shoti za umeme.
“What the hell is happening!!!”
Roma alipiga yowe huku akirudi ardhini kwa tahadhari, alijawa na hofu isiokuwa ya kawaida , sekunde moja alidhania huenda n kutoka na kusafiri umbali mrefu sana hivyo akakiuka sheria za anga lakini kilichomshangaza ni kwamba mnara ndio uliokuwa wa kwanza kutoa mwanga wa kimaajabu na ilikuwa ni kama vile ndio uliochokoza radi.
Roma hakutaka kujiuliza mara mbilimbili wakati anahisi hatari alikuwa asharudisha tayari Sophia chini kwa kuhofia angedhurika lakini kwa namna ambavyo mnara huo ulikuwa ukishambuliwa na Radi kwa spidi hakutaka kubakia ttena katika eneo hilo..
Alimnyakua Sophia kwa haraka sana huku akiachana na wazo la kumuua Lekcha tena na kujiokoa yeye mwenyewe na Sophia.
Sophia hakuwa amekufa bado , ijapokuwa damu zimevilia kwa ndani lakini bado alikuwa akipumua kwa mbaali na Roma aliona aondoke ili akamsaidie mbele kwa mbele wakati huo akimwingizia nguvu ya kimaandiko ili kusaidia kupona.
Upande wa wanafunzi wote waliokuwa wakifanya mazooezi katika majumba tofaut tofauti waliweza kukurupuka walipokuwa na kutoka nje kushangaa nini kinaendelea, lakini baada ya kushuhudia mashambulizi kati ya anga na ule mnara walijikuta wakihofia uhai wao.
Dakika hio hio ilikuwa ni kama vile ule mnara unayeyuka katika kilele chake na kuonyesha chuma kikubwa kinachotoa mwanga wa rangi ya gray.ilikuwa rahisi kusema huenda huo mnara ulijengwa kwasababu ya kuzuia radi kutokana na namna ambavyo radi zilivyokuwa zikirindima huku ngurumo kubwa zikisikika pamoja na shoti lakini kwa wakati mmoja mnara ule haukuzima zile boriti zake za rangi ya gold zilizoelekea angani.
Kadri radi iliovyokuwa ikipiga ndio iliwezesha ule mnara kutoa mwanga kama vile ni projector na kuonyesha baadhi ya maumbo ya kimaandishi kama Runes hivi ambazo hazikuwa zikieleweka maana yake.
Roma hakutaka kendelea kushangaa palepale alipaa angani ili kukimbia na wakati huo huo na Lekcha na yeye alitumia nafasi hio kujaribu kutokea lakini ilikuwa ni kitendo cha kasi sana kilichotokea kwani zile boriti za miale ziliancha kumulika juu angani na ziligeuka na kuwa kama minyororo kwani wakati Roma anataka kukimbia alifungwa kiunoni akiwa na Sophia na kuvutwa kwa nguvu kubwa ilikuwa ni kama vile mnara ule ulikuwa ukiendeshwa na mtu na haikuwa kwake tu hata kwa Lekcha ilikuwa hivyo hivyo wote kwa pamoja waliweza kuvutwa kwa nvuvu na mnara ule kuelekea katika eneo ambalo kulikuwa kama vile kuna anga linachemka.
Roma baada ya kuona alikuwa ameshikilia Sophia kwenye mikono yake alikosa uamuzi wa haraka aa aidha amdondoshe chini lakini kiendo cha kutaka kumdondosha chini tu ni kama alishitukiwa na mnara ule kwani palepale na Sophia na yeye alifungwa fungwa na boriti za mwanga na wakaavutwa wote kwa pamoja kwa pamoja
Kilichokuwa kikimtokea Roma ndio kilichokuwa kikimtokea Lekcha , tena kwa Lecha ilikuwa rahisi sana kwani hakuwa na nguvu na alivutwa kwa spidi na kutupiwa katika eneo ambalo anga lake lilikuwa likichemka kama vile ni maji .
Upande wa Roma alijikuta roho ikimuuma kwani kadri alivyokuwa akipambana kwa kuita nguvu za kijini ndio alivyokuwa akizidi kuvutwa na kusogezwa karibu , huku akipatwa na hruuma na kuona anakufa akiwa na Sophia mkononi.
Alijaribbu kuita na chungu chake kiweze kumsaidia lakini hakukuwa na majibu na palepale bila ya kupenda alivutwa kwa kasi sana na kutupiwa katika mchemcho ule wa anga kama ilivyokuwa kwa Lekcha na wakapotea yeye na Sophia.
Ni dakika chache tu baaada ya Roma kupotelea kwenye kiwingu cha mnara ule , palepale ile radi ilipotea na mnara ukaacha kupiga shoti na kukawa kimya kwa mara nyingine
Wale wanafunzi wa pale wenyewe walijikuta wakianza kushangaa na kujaribu kwenda kusimama chini ya mnara kujua Roma na Sophia pamoja na Lekcha wamepotelea wapi lakini hakukuwa na chochote.
Kutokana na eneo hilo kuwa juu mlimani haikuweleweka kama watu wa mbali wameona nini lakini ilibakia kuwa stori ya siku hio kwa wanafunzi na walimu wa dhehebu la Shushani huku habari ikiwa ni kupotea kwa watu juu ya mnara huo ambao kwa mara ya kwanza tokea uwepo hapo hikuwahi kutokea kwa kitu kama hicho.
ITAENDELEA
WATSAPP 0687151346
Roma kwa haraka sana kumbukumbu zake ziliweza kurudi siku ambayo alikutana na Kizwe pamoja na Lekcha ndani ya Club B , Lekcha wa kipindi kile alikuwa wa kawaida sana na hakuwa tishio lakini Lekcha ambaye anamuona mbele yake alikuwa ni mwingine kabisa.
Kwa mtu mwingine angepingana na kauli ya Raisi Jeremy kusema Mtu anaefanana na Denisi ndio Joseph Bikindi , ila kwa upande wa Roma ambaye alikuwa na uzoefu wa mambo mengi ya kushangaza ilikuwa rahisi kwake kuweza kuelewa na kuamini.
“Ni wewe … sijategemea kukuona ukiendelea kuishi, nilijua tayari ulishauwawa kwa siri”Aliongea Roma kwa kejeli.
“Kwanini unadhania mwanaume ambaye sikuwa na thamani kama mimi kufa bila sababu ya msingi , siku uliomtuma yule malaya kuja kwangu haukuwahi kudhannia kila kitu unafanya kama nilivyokuwa nikipanga?, Unadhani ni kwa bahati mbaya mtu ambaye alikuwa akiishi kwa kuokota makopo na kuishi chini ya Daraja kuweza kuelea angani kama wewe hivi sasa? , unafikiri hii ni miujiza imeniokea?, wewe huna tofauti na wengine , unatumia wasifu wako kujaribu kudharau viumbe vya hali ya chini ila ukweli ni kwamba nyie watu hampo tofauti na sisi”Aliongea Lekcha.
“Nilidhani ulikuwa ukinichukia ndio maana uliweza kuwa na mipango mingi ya kunichafua , lakini kwa ninachoona hapa unatuchukia wote”
“Hahah… mimi niwachukie ,hamstahili uwekezaji wangu wa kihisia kwa ajili tu ya kuwachukia , kwangu mimi nawaona kama mawindo tu na nitawafanya ninachotaka”
“Unaonekana kujiamini , naona umeweza kumiliki nguvu ya Ant-matter , na kama sikosei naamini umefanikisha hayo yote kupitia Yan Buwen na hili linanifanya kuwa na shuaku ya kutaka kujua umefikia hatua gani, lakini hata hivyo naweza kuona wewe ni wa tofauti”Aliongea Roma huku akitoa kicheko.
“Bado tu unaongea na mimi kwa dharau … hicho ndio kinachonichukiza kuhusu nyie watu, nini kimekufanya kuja hapa na kutaka kuingilia mambo yangu ,au unahisi bado tu unaweza kunishinda?
Unatokea katika familia ambayo inasifika kuwa na nguvu ndani ya Tanzania lakini kwangu mimi naona ni ushenzi tu na utapeli wa famlia yenu ndio maana mnajiona mpo juu , kwangu mimi watu wa aina yenu mnastahili kushushwa kwa kipigo na kuliwa na mimi”Aliongea Joseph Bikindi kwa dharau huku akiwa na uso wa kujiamini.
Wakati Roma akifikiria nini cha kuongea ghafla tu aliweza kuhisi msisimko wa hali ya juu ukiwasogelea na kumfanya kukunja sura , ni msisimko uliokuwa ukitokea upande wa Magharibi.
Ni kufumba na kufumbua tu aliweza kuonekana mwanaume mweusi alievalia mavazi meupe marefu aina ya Robes.
Alikuwa na mwonekano wa kitajiri na kujiamini huku akiwa na sura ambayo imejaa ujeuri , macho yake kwanza aliyaelekezea kwa Raisi Jeremy ambaye alikuwa akizungukwa na mwanga mweupe na kisha akayageuza upande wa Roma aliekuwa juu yake kidogo.
“Master 4 asante kwa kufika mapema”Aliongea Raisi Jeremy huku akonyesha hali ya kupatwa na ahueni, haikueleweka kwanini anaitwa Masetr 4 lakini kwa haraka haraka Roma alitambua inawezekana akawa ndio Master mkuu namba nne katika jamii ya Panas.
Kuhusu uwezo wake Roma aliweza kugundua alikuwa levo ya kuipita dhiki akiwa na uwezo wa kutawala rangi tatu za moto , alionekana kuwa juu zaidi ya Nix na Gesha ila levo yake bado ilikuwa ya chini kuliko Rom ambaye alikuwa na uwezo wa kudhibiti mtoto wa kiroho wa rangi ya bluu pamoja na maji ya kiroho.
“Jeremy wewe mjinga sana , yaani umeshindwa kujilinda mpaka ukafikira hatua ya kutumia hio medali tena wanaokushughulikia ni wanafamilia wako mwenyewe?”Aliongea kwa lugha ya kifaransa.
“Master 4 mambo mengine hayazuiliki na sio kila tunalopanga linatokea , wana nguvu zaidi yangu na mipango yao ilikuwa ya siri tafadhari nisaidie kuwamaliza”Aliongea na Master 4 alimpotezea na kumgeukia Roma.
“Ninakujua wewe kijana kutoka Taifa la Tanzania , una umaarufu mkubwa sana katika ulimwengu wetu kwa kuweza kupita vizuizi vya tamaduni zetu kwa muda mfupi , nashindwa kuona uwezo wako ni katika levo ipi nadhani ni kama sifa zako zinavyojieleza hakika una stahili sifa unazopewa , kwa leo nipo hapa kwa ajili ya kumsaidia ndugu yetu upande wa mama sitaki kujiingiza sana na mambo ya dunia”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa kwani hakuelewa nini maana ya ndugu upande wa mama , akili yake ilifanya kazi kwa haraka sana na kujiuliza inamaana Raisi Jeremy na yeye amezaliwa nusu binadamu nusu jini, alijikuta sasa akielewa kwanini watu kutoka Panasi walitumwa kuja kumlinda , kumbe kuna sababu kubwa na sio maswala ya bahati mbaya.
“Wewe takataka umetokea wapi? , unajiona ni nani mpaka uje kuingilia hapa?”Aliongea Lekcha na bila ya kutaka kusubiri jibu palepale shoti za ant -matter zilimtoka kwenye mkono wake na kumshambulia Master 4 kwa spidi na kumshusha ardhini.
Masetr 4 alijikuta akishangazwa na namna shoti zile zilivyoweza kumtoka Lekcha kwani hakutarajia kama angekuwa na uwezo huo.
“Haha.. kwa udhaifu huo uliokuwa nao bado tu umekuja peke yako na bado unajitamba kutaka kumuokoa Jeremy? ,ila sio mbaya nitakuua nae”Aliongea huku hali ya kujiamini ikiongezeka mara mbili na alizidi kuongeza nguvu ya shoti ya Ant-matter kumshambulia Master 4 kumpeleka mpaka ardhini.
Roma alikuwa na nafasi ya kumzuia Lecka lakini hakutaka kujihusisha kabisa na watu wa jamii hizo zisizoonekana na wakati huo huo alitaka kumuona Lekcha uwezo wake kabla ya kupigana nae.
Upande wa Master 4 alionekana kushindwa kuelewa namna ambavyo aliikuwa akishambuliwa na kujilinda, alijikuta akianza kujutia maamuzi yake , huenda angekuja na watu wengi zaidi kwa ajili ya kupambana lakini alimdharau adui kwa kutarajia atakuwa wa kawaida ndio kilichomfanya kuja peke yake.
Dakika hio hio hakuwa na haja ya kumsaidia kwanza Raisi Jeremy kwani aliona anapoteza nguvu kwa boriti za shoti anazopokea.
Upande wa Raisi Jeremy ile kinga iliokuwa imemzingira ilitoweka palepale , ilionekana dakika therathini za kumlinda zilikuwa zimeisha na kumfanya aanze kuogopa kwani aliweza kushuhudia namna ambavyo Master 4 anavyopokea kichapo.
Muda uleule mwanga ule wa ngao baada ya kupotea Kizwe na Desmond walijikuta wakirejewa na hali zao upya za kujiamini na kutaka kulipiza kisasi.
“Baba umemua kunitelekeza mimi na ukamchagua yule Malaya wa Kitanzania kuwa mrithi wako , usinilaumu kwa kupindua meza muda huu”Aliongea Desmond huku akionyesha hasira kubwa sana zidi ya baba yake na mwili wake ulibadilika na kuwa kama kivuli huku akimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi huku aidhamiria kummaliza na pigo moja.
“Kuwa makini!!”
Sauti ilimtoka kizwe na kwa spidi sana aliweza kutokeza mbele ya Desmond akionyesha kumkinga.
“Poof!!”
Ni mlio wa sauti ya kuchoma iliosikika na boriti ya mwanga mweupe kama wa laser ulionekana kumchoma Kizwe katika kifua chake na kutoboa.
Katika umbali mfupi kutoka aliposomama alionekana Master 4 ambaye alikuwa ameinua mkono wake kuelekezea kwa Kizwe na boriti ya mwanga ule mweupe ulionekana kutoka katika kifaa ambacho hakikuwa kikielezeka kiumbo na ilikuwa ni kama dhana ambayo teknolojia yake ni ya hali ya juu sana, hazikuwa kama zile dhana ambazo Roma aliweza kuziona kwa baadhi ya watu wa Hongmeng.
Desmond alijikuta akishangazwa na jambo lile, hakuamini mwanamke ambaye hakuwa akimchukulia tena kama mama yake ameamua kujitoa kafara na kupokea shambulio badala yake.
Kwake ilikuwa ni kama muda ulikuwa ukienda mbele na kurudi kwa wakati mmoja.
Lekcha aliekuwa juu angani hakuonyesha kujali kile kilichokuwa kikiendelea ardhini , Kizwe na mtoto wake aliwaona kama watu ambao hawakuwa na thamani tena baada ya mpango wake kufeli, hivyo hakuwa na haja ya kujali kama wapo hai au ni wafu.
Raisi Jeremy alijikuta akitoa pumzi ya ahuenni , ilikuwa ni bahati kwake Masterr 4 hakuwa amesahau kumlinda , ilikuwa ni kidogo sana tu kuweza kujeruhiwa na Desmond , alijikuta akitoa tabasamu kumwangalia mwanamke huyo aliepiga magoti ardhini akipambana na maumivu.
Upande wa Roma alijikuta akishngazwa na tukio hilo ambalo limekaa kidrama zaidi , hakuweza kutarajia kama Kizwe ambaye hakuwa katika uhalisia wake kuweza kujitoa kafara kwa ajili ya Desmond ambaye pia alikuwa amepitia mabadiliko na kupoteza uhalisi wake.
Ijapokuwa mwili wa Kizwe ulikuwa na uwezo wa juu wa kujiponyesha lakini nishati ambayo imetoka katika Dhana ya Master 4 ilikuwa na kiwango kikubwa cha nishati ambayo haipo kwenye uwiano sawia na mwili wake ili kuweza kupona.
Wakati nguvu ile ya kijini ikitafuta balansi katika mwili wa Kizwe ili aanze kupona eneo ambalo limetoboelwa lilizidi kuongezeka ukubwa na kumfanya damu kuzidi kupotea chini na hakukua na namna ya kuzuia.
Desmond alijikuta akimshikilia Kizwe huku akiwa na macho yaliokuwa mekundu.
“Umefanya nini , kwanini umenikoa , umekua kichaa?”Aliongea kwa sati kubwa ya hasira kama vile ni mwenye hatia na kumfanya Kizwe kuinua mkono wake kwa taabu sana akitaka kumshika Desmond shavu lakini nguvu zake zilizidi kupotea na kuishia njiani .
“Mtoto mjinga … mimi ni mama yako ..”Aliongea Kizwe kwa sauri dhaifu.
Machozi yake alishindwa kuyazuia na yalidondokea katika kifua cha Kizwe na kupita moja kwa moja mpaka chini Ardhini kupitia tundu la jeraha.
“Na … najua ulikuwa ukichukizwa na mimi na unaniona kama malaya hivyo kuniona siwezi kuwa mama yako tena … lakini Des.. mond kwangu wewe siku zote utabakia ,, utabaia ,,,ku..kuwa mtoto waaang..” Kabla hata hajamalizia herufi ya mwisho ya sentensi yake palepale kichwa chake kikalegea na ndio ukawa mwisho kamili wa uhai wake.
“No!!”
Desmond alishindwa kujizuia na kujikuta akitoa ukulele ulichonganyika na maumivu makali , yalikuwa maumivu kama ambayo aliyapata siku alipoambiwa mama yake amefariki na muda huo huo maumivu yale yalijirudia..
Lekcha na shoti zake za Anti -matter alijaribu kila namna ya kuweza kummaliza Master 4 lakini ilikuwa ni kama vile mapigo yake ni dhaifu sana, lakini licha ya hivyo hakutaka kuleta kabisa ujinga kwani alipaswa kuimaliza kazi mapema , hakujali kufariki kwa Kizwe , kwanza katika maisha yake hakuwahi kumpenda na alikuwa amemtumia tu kukamilisha mipango yake ya kupata nguvu na mtu aliekuwa akimpenda kwenye maisha yake ni mwingine kabisa.
Roma palepale aliweza kuzingirwa na nguvu ya Ant – matter ambayo ilikuwa ikimzunguka kama kimbunga na alijitahidi kutengeneza baridi kali ili kujaribu kuipunguza kasi na hakutegemea mbin yake kufanya kazi baada ya kuona mafanikio na kutengeneza annihilation.
Hakutaka kuchelewa zaidi kwani palepale alichukulia hilo kama faida kwake kwani alitoka katika kimbunga kile cha Ant Matter na kwa spidi ya juu alimsogelea Lekcha akinuia kumshambulia.
BOOM!!!
Shambulizi lake lilileta mafanikio kwani baada ya kumsogelea Lekcha alimtandika kisawa sawa ngumi ya kichwa na kuuchangua kichwa chake.
Kichwa chake kilipasuka vipande vipande kama vile kimepigwa na bomu na damu pamoja na nyama nyama pamoja na ubongo vilianza kusambaaa hewani.
Lakini sasa sekunde hio hio tu mwili wa Lekcha ulibadilika na kutoa mn’gao wa aina yake huku zile nyama nyama na damu ziligeuka na kutoa shoti za umeme kama cheche kuelekea kila upande na kwa spidi kubwa sana na ilionekana kama vile ni shambilio , kwani cheche zile ambazo zilikuwa kama mishale midogo zilianza kumpiga Roma kwa spidi ya hali ya juu.
Ijapokuwa ni vjimishale vya Ant- matter vidogo sana lakini ilikuwa na nguvu yake na ikigusanana kitu chochote hutengeneza Annihilation(maangamizi) makubwa.
Roma alijua kama ataruhusu kuguswa na cheche hizo basi angepata pigo kubwa hivyo alijitahidi kukaa mbali na kujilinda kwa wakati mmoja.
Dakika ileile baada ya Lekcha kuona Roma anajikinga ghafla tu mng’ao ule wa ant-matter ulipotea na Lekcha alirudi upya katika umbo la bindamu akiwa na sura ya Denisi.
Roma kwa wakati huo alikosa mbinu ya kummaliza haraka haraka Lekcha kwani alionekana kushambulia kwa tahadhari na aliweza kukiri kimoyo moyo Lekcha alikuwa ni tofauti kabisa na Yan Buwen katika kupambana, alichokifanya ni kujaribu kumshambulia na moto wa rangi nyuepe na wa Bluu kwa wakati mmoja lakini mashambulizi yake yalionekana kukosa nguvu kabisa ya kumdhuru Lekcha.
Licha ya kwamba mapigo yake yalionyesha uwezo wa kumletea maangamizi lakini kwa wakati mmoja ilimfanya Lekcha kuweza kurudi katika hali yake ya kawaida.
Kilichomkasirisha zaidi Roma ni namna ambavyo Lekcha hakuonyesha mpango wa kuachana na mwili wa Denisi na mpaka hapo alijua huenda sio tu kwamba alikuwa amejibadilisha sura kuwa Denisi bali mwili wake ulikuwa umeungana pamoja na wa kwake.
Upande wa Desmond baada ya kutoa kilio cha uchungu mwingi hatimae aliinua sura yake na kumwangalia Raisi Jeremy kwa macho yaliojaa chuki .
Raisi Jeremy hakuwa na kinga tena kwani medali yake haikuwa na uwezo wa kumlinda mara mbili na sasa alikuwa ni mwepesi sana kuweza kushugulikiwa na Desmond.
“Haya yote ni kwasababu yako umemuua mama yangu na nitakuua , nitakucharua charua”Aliongea ka kufoka huku akimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi lakini Master 4 ambaye alikuwa mdhaifu aliweza kumkinga Desmond na nguvu ya kijini.
Kutumwa kwake kuja hapo alihitajika kumlinda Raisi Jeremy kwa hali na mali kwani ndio mwakilishi pekee wa mipango yao juu ya uso wa dunia hivyo hakutaka kushindwa kutimiza wajibu wake.
Siraha yake ambayo aliitumia kumuua nayo Kizwe alimshambulia nayo Desmond na ilikuwa ni kwa bahati aliweza kushitukia pigo hilo kwani alifanikiwa kukwepa lakini kwa wakati mmoja akikatwa mkono , jambo ambalo hakuonyesha kuathirika sana kwani mkono wake uliweza kurudi upya ndani ya sekunde tu.
“Desmond umekuwa kichaa? , huyo mwanamke sio mama yako , mama yako alikufa na huyo malaya ametengenezwa na yule mpuuzi mwenzake , alitutelekeza mimi na wewe unawezaje kumuita huyo ni mama yako ilihali hana thamani yoyote ya kuwa sehemu ya familia yangu?”
“Huna aibu baba , eti hana thamani , unafikiria ilikuwa hiari yake kuwa katika hali hio? , kama sio wewe ambaye uliamua kutoka nje ya ndoa na kupata mtoto unadhani haya yote yangetokea , hivi unafikiria kila kitu kilichomtokea ndio alichotoka , amegeuka kutoka kuwa mtu wa heshima na muungwana na kuwa malaya ambaye anachukuliwa na kila mmoja , je haya yote aliomba kumtokea? , ni kwasbabu ya wewe , umemuua mama yangu unapata wapi uthubutu wa kujiita baba yangu?”
Desmond kwa hasira kali alimsogelea Raisi Jeremy kwa spidi kali huku awamu hii akinuia kumuua kwa namna yoyote ile.
Upande mwingine Lekcha alikuwa amemzingira Master 4 na kimbunga chakc cha shoti za Ant-matter na alishindwa kujua namna ya kumlinda tena raisi Jeremy.
“Roma mimi ni baba mkwe wako niokoe”Aliongea Raisi Jeremy kwa nguvu mara baada ya kuona hakuwa na msaada mwingine kwani Master 4 alionekana kuzidiwa.
Ijapokuwa Roma alikuwa akipambana na Lekcha lakini macho yake pia yalikuwa yakimwangalia Raiai Jeremy asidhurike , alijiambia huyo ni baba yake mzazi wa Edna na kwa na namna moja amna nyingine anapaswa kumlinda.
Roma hakutaka hata kuwaza ni kwa na namna gani Edna angemchukia mara baada ya kusikia ameshindwa kumlinda baba yake, hata kama Edna asingefahamu hilo asingepaa ujasiri wa kuweza kumsogelea tena.
Kabla ya Demsond kumfikia Raisi Jeremy palepale alijikuta akifunikwa mwili mzima na moto wa rangi nyeupe na kuanza kuyeyushwa mwili wake kwa spidi.
“Mama… Arggghhh!!”
Alijikuta akishindwa kuhimili maumivu na kwa wakati mmoja akishindwa kuuzima ule moto mwilini mwake, licha ya kuwa na uwezo wa kupona kwa haraka lakini spidi ya mwili wake kuungua ilikuwa ni kubwa mno.
Raisi Jeremy alijikuta akitokwa na jasho jingi mara baada ya kuona namna ambavyo Desmond alikuwa akitoa kilio , kama mzazi alijikuta akiona uchungu kwa swala kama hilo kutokea , lakini kwa upande mwingine aliona hicho ndio anachostahili.
“Mwanaharamu wewe , unastahili kuchomwa moto mpaka kufa , unathubutu vipi kunisaliti mimi baba yako ,nenda kuzimu na huyo mpuuzi unaemwita mama yako”Aliongea kwa hasira na muda uleule aliusogelea mwili wa Kizwe na kuupiga teke.
Desmond alikuwa akiungua na moto wa kijini ambao uliunguza nguo zote na sasa ulikuwa ukiunguzwa mwili na mifupa , alijaribu kutambaa kumsogelea mama yake aliefariki lakini alijikuta akikosa nguvu na kutawaliwa na maumivu na aliishia kulia kama mtoto mdogo.
Ilichukua dakika chache tu mwili wake wote uliyeyuka na vumbi lake likapotea kabisa kwenye hewa.
Roma ambaye aliweza kuona kila kitu alitamani kumyeyusha na baba mzazi pia lakini hakutaka kufanya hivyo kwa ajili ya Edna tu , alikuwa na chuki na Jeremy kwani alimuona mtu ambaye ana siasa nyingi na atakuja tu kumsumbua na mke wake.
“Naona umeweza kuharibu kabisa mipango yangu”Aliongea Lekcha kwa kejeli huku hasira zake zikiwa za viwango , kwa namna ambavyo Roma alikuwa akijiamini ilimfanya kuona anadharaulika.
“Kwa mbinu zako angalau naona kabisa huwezi kuhimili muda mrefu”
“Acha majigambo nitakupa nafasi ya mwisho ya sisi kufanya kazi pamoja?”
“Unataka tufanye kazi gani?”Aliuliza Roma.
“Nifuate mimi na tuubadilishe huu ulimwengu uliojaa ufisadi”
“Unataka mimi na wewe tuubadilishe ulimwengu?”Aliuliza Roma akicheka.
“Upo sahihi , wewe si ndio wanakuita Mfalme Pluto sehemu ya miungu , bila kujali kama kweli wewe ni sehemu ya miungu mimi na wewe tuna nafasi kubwa ya kubadlisha huu ulimwengu?”
“Hahaha.. hakika wewe ni tofauti kabisa na Yan Buwen , angalau yeye alionekana kachizika lakini wewe ni mwendawazimu”
“Wewe ndio mwendawazimu kwenye macho yangu , hustahili kabisa hata kupewa cheo cha U’pluto , huna thamani wala nguvu kwa sifa unazopewa”
“Wewe ni mtu wa aina gani unajiita mungu? , unapaswa kufaidika kutokana na cheo chako lakini nyie miungu mmeamua kuficha vichwa vyenu huku mikia yenu ikionekana , eti hatutapaswi kujihusisha na mambo ya dunia wanafiki wakubwa nyie, bahati mbaya unafiki haupo kwenu tu ni kwa kila mtu na katika kila taifa ,sijutii kwa wewe kumuua baba yangu maana alikuwa mnafiki na yeye lakini najutia kwa wale wote ambao wanajifanyisha ni wa thamani ya juu zaidi na kutuona sisi hatustahili hata kuwasogelea , hebu muangalie mtu ambaye umemlinda sasa hivi unadhani ni mtu wa aina gani , yule ni mnafiki tu ambaye anadanganya taifa huku akiwa na ajenda zake kichwani , ni kiongozi gani ambaye yupo tayari kuua familia kwa maslahi yake , inasitikisha sana .
Kizwe ni mwanamke ambaye alijitaji mapenzi na kusamehewa pale anapoonyesha udhaifu, hata kama imetokea akaguswa na wanaume wengine anatoa wapi hukumu ya kumuua , kama hamtaki si angemtafutia sehemu na kuishi na kuachana nae , kulikuwa na haja yoyote ya kumuua?., haya ni mambo ambayo mimi Joseph Bikindi a.k.a Lekcha nataka kurekebisha , nataka kuondoa uovu wote ndani ya dunia , nataka kubadilisha dunia hii na kufuta kitu kinachoitwa siasa maana ndio chanzo cha ufisadi na uovu , hivyo Pluto unaonaje tukiungana pamoja na kufagia ufisadi wote na kuanza kuwapa watu uhuru kamili , falsafa yetu itakuwa ni kurudisha nguvu kwa wanyonge ili washindane wenyewe na hawa mashetani wasio na huruma , hakuna haja ya dunia hii kuwa na watu wenye nguvu huku hawafanyi chochote na hata wakichukua hatua ni kwa faida zao wenyewe , Mr Roma Ramoni nitaweka yote ulionifanyia nyuma yangu na tuungane pamoja kubadili dunia hii, Hebu tuungane pamoja”
SEHEMU YA 596.
Sauti ya Lekcha ilikuwa kubwa kiasi kwamba ni kama vile anataka dunia yote imsikie.
Usiku huo kulikuwa na upepo mkali na anga halikuwa na dalili yoyote ya wingu kuashiria kama kuna mvua inayoweza kunyesha, ni vivuli tu vya watu ndio vilionekana angani na kwa mtu ambaye alikuwa kilomita moja kwa umbali asingeweza kuona kinachoendelea zaidi ya kusikia sauti na baadhi ya vimulimuli vya hapa na pale.
Lakini kwa sauti yake ilifanya watu wa jiji la Kigali kuwa katika tahadhari kubwa na kutetemeka , ilikuwa ni kama vile Mungu anaongea na binadamu.
Baada ya kimya cha muda mrefu, Roma ambaye alikuwa na mwonekanao usiolezeka alivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha akainamisha kichwa chake chini na kuanza kucheka.
“Perhaps it is inapropriate for me to say that you are madman, not only you’re a madman but also a coward”Aliongea Roma kwa kingereza akimaasha kwamba huwenda inaweza isiwe sawa kumuita mtu kichaa ila ukweli ni kwamba yeye sio tu kwamba ni kichaa lakini pia ni muoga.
Kauli yake ilimfanya Lekcha kufika kilele cha hasira zake baada ya kusikia jibu hilo na alitamani kumrarua Roma palepale.
“Unaniita mimi muoga? ,, hahaha… nadhani unaota maana muda wenyewe ndio huu umeenda”
Roma hakutaka kujibuzana nae na palepale aliita moto wa njano na kuunganisha na moto wa bluu na nyuepe.
“Tumalize kabisa hili , nimekupa nafasi ya kuishi lakini ukaipotezea , hivyo kila kitu ambacho nilikosea kukifanyia kazi nitakimaliza leo hii mimi mwenyewe”
“Unafikiri barafu na moto ni vitu ambavyo vinaweza kunidhuru? Unachekesha sana”Aliongea huku akiwa na mwonekano wa dharau.
“Hujui lolote kwasababu bado hujawahi kupambana na mimi”Aliongea na hakutaka kuchelewesha, aliuelekeza moto wa kijini kumshambulia Lekcha kwa kasi kubwa.
Halikuwa shambulia la kawaida kwani ilikuwa ni kama vile chembe chembe zote za anga zilikuwa hazitembei huku eneo lote likiwa halina aina yoyote ya upepo na kuufanya ule moto kutoa nguvu kubwa ya kiroho.
Master 4 kuona tukio lile alijikuta akishikwa na mshangao kwani ni kitu ambacho hakuwahi kushuhudia , hakuwahi kuona rangi zote za moto kutolewa kwa wakati mmoja zikiwa zimeunganika , lakini haikuwa hivyo tu kilichomchanganya zaidi ni namna moto ule ulibadilika na kuwa kama vinyoka nyoka , alijua kama yeye ndio anashambuliwa basi ni shambulizi moja tu atakwa tayari amekwisha kufariki.
Alijimbia kwa nguvu ya kiroho ambayo alikuwa akihisi , hana uhakika kama wakubwa zake wote katika miliki ya ulimwengu wao wanaweza kufanikiwa kushinda , alishangaa mara moja na kujiuliza imekuwaje kijana mdogo akawa na uwezo wa aina hio.
Upande wa Roma hakujuwa kwamba alikuwa akimshangaza mtu kwa wakati huo kwani alichokuwa akiwaza ni kumalizana na Lekcha moja kwa moja na kwenda kulala na familia yak.
Ukweli ni kwamba Lekcha alikuwa tofauti sana na Yan Buwen na alikuwa ni kama vile alipenda kuonja kila pigo ambalo alikuwa akipelekewa na Roma , kwani hakukwepa mashambulizo yake na hata ule moto aliacha umshambulie.
Ajabu ni kwamba licha ya Roma kuweza kutumia nguvu kubwa sana ya kutawala moto huo kushambulia lakini mbele ya nishati ya ant-matter ilionekana kutofanya kazi, nguvu ya Lekcha ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba moto ule ulikuwa ni kama vile unanyonywa na kuzimika kila unapogusana nae.
Roma kwa levo aliokuwa akitumia alijua ilikuwa juu zaidi kuliko aliotumia kupambana na Yan Buwen mpaka kumuua na ilimshangaza kwamba wakati huo Lekcha licha ya kumsbambulia alionekana kabisa hana hofu na chochote anachomuandalia na alikuwa na maendeleo ya juu mno.
“Hehe.. naomba unajitahidi sana hata hivyo nitakuchukulia kama jiwe la kujiimarisha zaidi ili niweze kutimiza malengo yangu , naona kabisa mbinu zako zote zimefikia ukomo, ni muda sasa kukuonyesha uwezo wangu halisi”Aliongea Lekcha.
Sekunde hio hio alibadilika kabisa na hakuwa biadamu tena bali nguvu yenyewe ya Ant-matter na alianza kwa kuwa kama mpira wa miguu na akaendelea kutanuka huku shoti zikisambaa kila kona na mpira ule ulizidi kujizungusha na kuanza kuonekana kuwa mkubwa zaidi .
Ni muda uleule wakati Roma akishangaa aliweza kuona shimo likijitengeneza juu yake na liliongezeka ukubwa huku anga likiwa ninazunguka kama vile kimbunga au singularity inayotokea juu kuja chini na ndani ya dakika chache tu sehemu aliosimama ni kama vile yupo kwenye chumba ambacho hakina hewa ndani yake na ilimfanya kushindwa kuita nguvu ya kimaandiko kumlinda kwani alishindwa kuwasiliana na elementi za dunia.
Kilichomshangaza Roma ni ufahamu wake kuanza kumpotea na kujihisi kama vile anaendeshwa kwa rimoti na hakuwa na uwezo wa kusogea kurudi nyuma wale mbele, alisimama kama vile ni sanamu.
“Chochote utakachofanya hakina maana , nishati yangu ya Ant – matter imeongezewa ubora kwa viwango vya juu na kuwa na tabia tofauti na zile ambazo wanasayansi wa kawaida wanajua , yote hayo yamefanikiwa kupitia kifaa maalumu cha kuibadilisha , unafikiri ningekuja kushindana na wewe nikiwa na nguvu kama zile za Yan Buwen … kinachotokea hapo ni matumizi ya magepu yaliopo kati ya anga mbalimbali zilizo sambamba, kwa uwezo wako huo licha ya kuwa na uungu ndani yako huwezi kuitoa roho yako na kutawala mwili mwingine maada itakuwa halali yangu”Sauti ya Lekcha iliweza kusikika lakini Lekcha mwenyewe hakuweza kuonekana na upande wa Roma aliweza kusikia kama vile ni mwangwi.
Roma uso wake ulianza kujikunja kunja kwa namna ya kulazimishwa huku akijaribu kuzuia mwoneknao wake usibadilike lakini mzunguko wa nguvu ya Ant-matter ulikuwa ukifyonza nguvu zake za mbingu na ardhi kila alipokuwa akijaribu kuziita ili kujiondoa kwenye mtego huo , mbaya zaidi ni kiwango kidogo sana ambacho alikuwa na uwezo wa kukiita kutokana na kuingizwa katika eneo ambalo kulikuwa na elemeti za anga hivyo kushindwa kufanya mawasiliano.
Roma alijikuta akipandwa na hasira na kujiambia alimchukulia wa kawaida ndio maana yupo katika hali kama hio , alikuwa bado hajapigana na majini katika ulimwengu usio onekana lakini alikuwa akijiamini kwamba alikuwa na uwezo wa kuwashinda lakini anachofanyiwa na Lekcha kilimpagawisha kwa wakati mmoja na kujiona huenda ni dhaifu.
Roma hakutaka kufanya ujinga ni kweli alikuwa na uungu ndani yake alioweza kurithi kutoka kwa Pluto wa Zamani hivyo kumpa uwezo wa kutawala mwili wowote lakini alihofia kwamba anaweza kuingia katika mwili ambao hauna vigezo na anaweza kuanza upya moja kwa moja kuvuna nishati za mbingu , isitoshe nguvu za kijini hawezi kuhama nazo.
Roma mara baada ya kuona yupo hatarini aliona hana chaguo lingine zaidi ya kuita Chaos Cauldron.
Lakini moyo wake ulikuwa mzito mno kwa kuhofia roho iliokuwa ndani ya Cauldron inaweza kutawala akili yake na asingejua ni kipi ambacho angeweza kufanya baada ya hapo , alihofia hilo kumkumba kwani ingekuwa mwisho wake.
“Roma umeweza kuwashinda watu wengi sana lakini sasa kiko wapi ,,, unakufa kwenye mikono yangu , kabla haujafa ngoja nikupe usharu kama zawadi , udhaifu wako mkubwa unaokufanya usiwe na nguvu ni kwasababu ya wasiwasi wako … huu ulimwengu ni kama msitu na mwenye nguvu ndio anaishi , siku zote binadamu mwenye nguvu atatumia utashi wa mnyama ili kuendelea kuishi , lakini wewe unadhani kutoa kafara matamanio yako ndio utaonekana mjinga , muoga , usie jiamini na dhaifu ,,, hayo yote ndio yanakuua leo hii hustahitili hata kuwa mshindani wangu , wewe ni dhiafu sana”Aliongea Lekcha kwa majigambo na kisulisuli cha nishati ya Ant-matter kikizidi kuongezeka maradufu.
Upande wa Master 4 aliweza kushuhudia mabadiliko hayo lakini hakutaka kujihususha zaidi kwani sio kilichomleta na palepale alibadilika na kuwa kama mwanga wa moto na kupotea eneo hilo akiwa pamoja na Raisi Jeremy.
Lekcha hakutaka kujihusisha zaidi na wao zaidi ya kuweka umakini katika kumuua Roma , alijiambia ni rahisi zaidi kuwatafuta mara baada ya kumalizana na Roma.
Dakika hio hio katika kisulisuli kile cha nishati isio maada ilitokeza miale yenye muundo wa macho rangi nyekundu huku sauti ikibadilika na kuwa kama ngurumo kubwa za radi na kumfanya Lekcha kushituka
“Hiki ni kitu gani?”
Nguvu yote ya Ant Matter ilianza kukosa nguvu , malengo ya Lekcha ilikuwa ni kujibadilisha na kuwa Roma lakini katika hali hio alishangaa mabadiliko makubwa kwani ni kama kuna kitu kilichokuwa kikifyonza nguvu yake kwa hali ya juu sana.
Upande wa Roma hakujali kabisa yupo kwenye hali ya hatari kama hio, kitu pekee ambacho alioona ni sahihi kukifanya ni kutumia cungu chake cha maafa lakini kwa tahadhari kubwa nafsi yake isije kumezwa na mwili wake kutawaliwa.
“Nani unasema hastahili kuwa mshindani wako”Sauti nzito iliweza kusikika.
Nguvu ilikuwa kubwa mno kiasi cha kufanya ule msukosuko wa hewa kupotea palepale na kumfanya Lekcha kurudi katika umbo la kibinadamu, lakini ni kama vile amefanya kosa kwani hapo ndipo aliposhuhudia kilichokuwa chini yake huku ndani yake kukionekana uwepo wa macho ya mnyama.
“Damn it what kind of monster is that….”Lekcha alijikuta akianza kuhofia maisha yake , kwa hali kama hio aliona kabisa ana uwezo mdogo wa kuishi.
Roma hakujali kutoa jibu na alikifanya chungu chake kuzidi kumsogelea Lekcha hatua kwa hatua na kadri kilivyokuwa kikisogea ndio hali ya hatari ilivyozidi kumkumba Lekcha kwani nguvu inavomvuta ilimvamia kwa hali ya juu sana
“Pengine upo sahihi , ulimwengu huu una machukizo mengi , unastahili kuhurumiwa , unastahili kuonyeshewa wema, lakini kwa mtanzao wangu wewe ndio chukizo kubwa zaidi la ulimwengu huu , umesema ni viongozi ambao ndio mafisadi na unataka kupambana zidi ya siasa , kama ni hivyo kwanini ulitaka kujibadilisha na kuwa Jeremy , umesema Kizwe ni mwanamke ambaye alikuwa na maisha magumu kama ni hivyo kwanini ukaaamua kumtumia na kisha ukampotezea , kama kweli ulikuwa ukimpenda kwanini hukumsaidia? , umesema miungu wameficha vichwa huku mikia yao ikionekana lakini kwanini ili tu kutimiza malengo yako unataka kuua watu utakavyo , ni haki gani ambayo unataka kutenda. Upo sahihi mimi Roma sina nguvu na siku zote ni muoga na mwenye wasiwasi mwingi na sina matamanio makubwa na ni mbinafsi na sistahili kabisa hata kuubadilisha huu ulimwengu..”
Wakati anamalizia kuongea alikuwa karibu kabisa na Lekcha na chungu chake kilikuwa kimemsogelea karibu zaidi na ilikuwa ni kama sunami , ni kama anga limekusanywa na kuwekwa sehemu moja na kuchezeshwa.
“Licha ya madhaifu yangu yote hayo sijawahi kujikataa , sijawahi kuficha udhaifu wangu , unafiki wangu na ubinafsi wangu ..mimi ndio mimi Roma ambaye uliweza kukutana nae kwa mara ya kwanza na sijabadilika, kwako wewe Joseph Bikindi mtu muoga sana , umeamua kutotumia sura yako halisi ili tu kutimiza malengo yako huku ukitumia mbinu zako za kusikitisha huku ukijifariji kwa uwezo wako mdogo , unachokionyesha ni inferiority Complex , wewe ni mtu ambaye huna lolote , wewe ni muoga ambaye unaogopa kuuangalia ulimwengu kwa jinsi ulivyo , kwa sifa zako hizo za kiuoga woga unathubutu vipi kupigana na mtu kama mimi”
“Mimi sipo hivyo , unangea upumbavu”Lekcha aliikuwa akijaribu kujitetea .
“Haijalishi kwasababu leo ndio mwisho wa maisha yako”
Roma palepale alizidi kubadilika na alikusanya nguvu zake zote na kukilisha kile chungu na ilimpelekea nguvu yake ya mvutano kuwa kubwa zaidi kama shimo jeusi .
Chungu hicho kilikuwa na uwezo wa kumeza kila kitu hata kama ni Ant Matter , nishati ambayo hufanya kazi kinyume na fizikia , hivyo kwa haraka haraka ni kwamba Lekcha hakuwa na pakukimbilia mbele ya Caulrdon.
Lekcha mpaka hapo alijua akileta mchezo ndio kifo chake , hivyo alitumia kila mbinu aliokuwa nayo kujaribu kukimbia lakini nishati yake ilikuwa ikimezwa kwa spidi kubwa na kumfanya kuzidi kuwa dhaifu.
Ilikuwa ni dakika chache tu wakati Roma akitaka kummaliza kabisa Lekcha kwa kumsukumia kwenye tanuru la kimaafa akili yake iliweza kuvamiwa palepale .
Roma alihisi ni kama ubongo wake umeingiwa na mdudu ambaye alikuwa akitifua tifua kuona sehemu ya kukaa.
Dakika ileile ni kama vile chungu hicho kiliachana na Lekcha na kiumgeukia Roma kuanza kushindana nae , ilikuwa ni mashindano ya nafsi na nafsi na Lekcha baada ya kuona amekuwa huru kutoka katika mvutano palepale aliona hi ndio nafasi pekee ya kukimbia , hakutaka kujiuliza kwanini imetokea hivi na vile lakini utashi wake ulimwambia aokoe maisha yake kwa vyovyote iwezekanavyo.
Alikusanya nguvu ya Ant Matter iliobakia katika mwili wake huku matamanio makubwa ya kujiokoa yakimpa nguvu ambayo ilimuwezesha kukimbia.
Lakini sasa dakika ileile anaweza kujiokoa upande wa Roma aliweza kuitawala akili yake kwa mara nyingine na kudhibiti nafsi ya mnyama iliokuwa kwenye chungu.
“Unaenda wapi?”
Aliongea Roma kwa nguvu akimwangalia Lekcha ambaye anajaribu kukimbia na alichokifanya Romna ni kumsogezea karibu zaidi chungu chake na kumfanya Lekcha kuzidi kuvutwa.
Ghafla tu ulipiga mwanga wa rangi ya Silver kama flash , ilikuwa ni kama mlipuko na uliweza kufanya mwili wa Denisi kujiachia na palepale ukamezwa na Cauldron.
Lekcha alijua kitu pekee ambacho kitamuokoa ni kuishi kama roho yenye umiliki wa nguvu ya Ant matter energy ili kujiuzia kutomezwa na chungu, ndio maana akaamua kuupoteza mwili wa Denisi.
Roma alishindwa kugundua hivyo mapema baada ya mwili wa Denisi kumezwa na chungu chake na baada ya kuelewa kilichotokea aliweza kugundua ni hila za Lekcha kujaribu kutoroka , kilichomezwa ni mwili usiokuwa na roho.
Mbinu aliotumia Lekcha iliweza kumuokoa kwani alitumia sekunde chache tu ambazo Roma alikuwa akizubaa na kupotea mbele yake akiwa ameipatanisha nafsi yake na nguvu ya Ant- matter energy hivyo kubakia katika umbo la mtu aliekuwa kama nishati.
Roma licha ya kugundua amechelewam hakutaka kumuacha aondoke kizembe , ijapokuwa Lekcha alipotea kwa haraka lakini alikuwa bado akipatwa na msisimko wa uelekeo wa nguvu ya Ant – matter na aliitumia hio kumfukuzia.
Roma palepale alirudisha chungu chake na kuanza kumfukuzia Lekcha ambaye alikuwa ni kama mwanga unasafiri angani.
Lekcha aliweza kuelewa hakuwa na spidi ya kutosha ya kumshinda Roma na kujua muda si mrefu anaweza kukamatwa na hapo ndipo wazo la mwisho la kujiokoa lilimjia akilini.
Ilikuwa ni njia pekee ambayo alikuwa ameipanga kwa ajili ya kujiokoa , akiwa katika hali ya hatari na muda kama huo ndio wazo hilo liliweza kumjia akilini na alitoa tabasamu la nia ovu, alijua kwa vovyote vile hakuna namna ambayo Roma anaweza kumdhuru kama atatekeleza wazo lake.
Upande wa Roma hakujua Lekcha anataka kufanya nini kwani ghafla tu alibadilisha uelekeo , lakini licha ya hivyo hakutaka kumuacha , alipanga kummaliza kabisa usiku huo huo.
Zilipita kama dakika herathini za Roma kumfukuzia Lekcha , shukrani kwa spidi ambayo walikuwa wakitumia hawakuweza kuonekana katika maeneo ambayo yalikuwa ni mchana.
Sasa baada ya kufika katika kilele cha mlima ambacho kwa ufahamu wa Roma katika matumizi ya Ramani aliweza kugundua eneo hilo ni ndani ya China , ilikuwa ni rahisi kusema ni mpaka unaoitengeanisha China na Mongolia.
Roma hakuelewa Lekcha anataka kufanya nini ila hisia zake zilimwambia kabisa amefikia mwisho wa kukimbia.
“Emei!!!”
Roma moyo wake ulipiga Kite kwa nguvu mara baada ya kugundua nini Denisi anataka kufanya.
SEHEMU YA 597.
Sio kwasababu tu ya Skendo ndio ilioweza kumfanya Sophia kuachana na maswala ya muziki.
Na sio pia kwasababu ya Skendo ndio akaamua kupotezea hisia zake na kuacha kabisa kumfikiria Roma au kuwa na mpango wa kutokuendelea kumtaka la hasha , mrembo Sophia alikuwa na lake kichwani ambalo alikuwa akipanga , alijiambia alikotoka ni mbali kuliko anakoelekea.
Kuachana na usanii na kurudi Japani ilikuwa ni kisingizio tu lakini katika kichwa chake alikuwa akipanga kujifunza kwa bidii zote namna ya kuvuna nishati za mbingu na Ardhi ili kuwa katika levo ya juu ya kuweza kubeba ujauzito wa Roma akiwa wa kwanza, hakujali Rose na Magdalena walikuwa wamemtangulia lakini alijiambia kutangulia sio kufika na isitoshe kupanda levo hakukutegemeana na muda wa mafunzo bali uwezo wa mtu kuelewa siri alizofichiwa binadamu juu ya ulimwengu.
Sophia aliamini kama ataweza kuwa katika levo za juu za mafunzo ya kijini hata hitaji kuwa na juhudi kubwa za Roma kumtaka.
Maelekezo ya namna ya kuvuna nishti za mbingu na Ardhi huwa mara nyingi yanahitajika maelezo ya mara moja tu ya namna inavyofanyika na baada ya kuelewa kinachofatia ni kazi ya mtu mwenyewe kuweza kufanya Tahajudi na kufikiria ili kupata ufunuo, isitoshe katika kujifunza mbinu za kijini hakuhitaji kuuliza maswali kwani hata kama uulize swali hakuna ambaye anaweza kujibu kutokana na msingi wa kwamba kila moja anapata ufunuo wa kwake mwenyewe juu ya kuweza kuvuna nishati hizo, mwisho wa safari unaweza kuwa mmoja lakini njia zikatofautina hio ndio maana ya uzoefu binafsi unaohitaji kutafuta jibu mwenyewe kwa kila swali.
Sophia alikuwa akielewa msingi huo na ndio maana hakuona haja ya kuwa na Roma karibu ili aweze kupanda levo bali ni juhudi zake pekee ambazo zingeweza kumpandisha Levo kwa haraka.
Hatua ya kwanza kwa Sophia ni kurudi Japani kwa wazazi wake na baada ya hapo angetafuta eneo tulivu ambalo lingemuwezesha kuvuna nishati ya mbingu na ardhi na sifa za eneo ambalo alikuwa akitaka Japani haikuwa jibu.
Temple ambalo alijifunzia Kung fu , maarufu kwa jina la Emei ndio mahali alipoona panamfaa sana , Emei ni Temple ambalo lilikuwa likipatikana katika mlima wa Emei katika dhehebu la Shushan chini China.
Roma licha ya kwamba hakumtafuta Sophia tokea siku ambayo ameondoka baada ya kutangaza kuachana na mambo ya usanii sio kwamba hakumfatilia.
Kitendo cha kumuona Lekcha ananyoosha moja kwa moja juu ya mlima wa Emei ilimkumbusha kwamba Sophia alikuwa akiishi katika eneo hilo na jambo hilo lilimfanya moyo wake kupiga kite kwani hakutegemea Lekcha angekuwa na uelewa juu ya Sophia kupatikana eneo hilo , kwa jinsi ambavyo walisafiri muda mrefu ilionekana hilo ndio wazo lake Lekcha la muda wote.
Akili yake ilifanya kazi kwa haraka sana na kitu pekee ambacho alihisia ni huenda Lekcha aliweza kufahamu eneo hilo kwa kuweza kutumia kumbukumbu za Denisi maana hata yeye alijifunzia mafunzo yake hapo.
Ndani ya eneo hili Shushan ndio mahali ambapo Sophia alikuwa akifanyia mazoezii yake ya kuvuna nishati ya mbingu na ardhi.
Ilikuwa muda wa asubuhi ndani ya Shushani , eneo hilo lilikuwa limejengwa kwa mtindo wa kizamani zaidi ni rahisi kusema Shushan ilikuwa na mfanano wa kiasi kikubwa na Dhehebu la Tang sehemu ambayo Magdalena alisomea mafunzo yake ya kichawi.
Katati ya eneo hilo kulikuwa na mnara(Tower) ,mrefu kwenda juu ambao ulikuwa umejengwa kwa utofauti mkubwa na minara iliokuwa katika madhehebu mengine, mnara huo ulikuwa na historia ndefu na inasemekana mnara huo ulikuwa ndio wa kwanza kujengwa kabla ya ujenzi wa nyumba na makazi ya kidhehebu na ni zaidi ya miaka mingi iliopita na hakuna historia yoyote ambayo ilieleza ni nani alihusika katika ujenzi, eneo hilo licha ya kuwa chini ya dhehebu la Shushani lakini kuhusu mnara ilikuwa siri ya taifa la China.
Sasa wakati huo ndani ya ukumbi mkubwa ndani ya eneo hilo walionekana wanawake wanne waliokuwa katika mavazi ya vitamba vya hariri vya rangi nyeupe , kati ya wanawake hao ni mmoja tu ndio ambaye alionekana kuwa na utofauti na wengine wote kutokana na rangi yake kuwa na mchanganyiko wa Kiafrika.
Sasa ilikuwa ni dakika chache tu wanawake hao wakati wakiongea kwa furaha ghafla tu kivuli cha mwanga wa Silver kiliweza kuonekana kikiingia hapo ndani na kusogelea wale wanawake kwa spidi kubwa.
Ilikuwa ni dakika ileile wale wanawake walijikuta wakipatwa na mshituko wa ghafla na kukwepa, yule mwingine aliekua na utofauti alijikuta akishikwa shingonni na kitu chenye ubaridi wa aina yake, akiwa kama yeye ndio aliekuwa mzembe wa kuwa kama wenzake lakiini ukweli ni kwamba wale hawakuwa walengwa ndio maana waliweza kuponyoka.
“Ring!!!”
Ulikuwa ni kama mlio wa kengele yule mwanamke alijikuta akifungwa kuanzia miguuni na shingoni kimajaabu na nyuzi za nishati ya Ant- matter.
“Sophia..!!”
Walijikuta wale wanawake wengine wakipiga makelele baada ya kuona kile kinachomtokea mwenzao.
“Wewe ni nani?”Walianza kupiga kelele kwa lugha ya Kimandari na kingereza kwa wakati mmoja.
Sophia akiwa katika hali ya aibu ya kutoweza kujiokoa na chuki alijikuta akishangaa kuona kiumbe kilichokuwa na muonekano wa kibinadamu , ilikuwa sahihi kusema kiumbe kutokana na mwonekano wake kutokuwa wa kawaida lakini palepale kiumbe kile kilibadilika na kuwa katika umbo halisia lakini sura yake bado hakuweza kuitambua.
Sophia alijaribu kuita nguvu ya kijini ili kuweza kujitoa katika vifungo alivyofungwa lakini hakufua dafu na kujikuta kuzidi kujawa na hofu , kilichomshangaza zaidi ni kwamba nguvu ambayo ilikuwa memfunga miguu yake haikuwa ya kawaida kabisa na ilikuwa katika hali ya ubarafu.
Dakika ileile wakati Sophia akifurukuta alijikuta akipigwa na mshituko zaidi mara baada ya Roma kuonekana mbele yake na mpaka hapo akili zake zilimwambia yupo katika hatari.
“Roma..!!”
Ijapokuwa wakati huo mtu aliemfunga kimaajabu alionyesha zaidi ukali wake lakini kwa Sophia alijikuta akipatwa na furaha isiokuwa na kifani , hakuamini angeweza kumuona Roma katika eneo hilo.
“Muachie tafadhari , matendo yako ndio yatarahisisha kifo chako”Aliongea Roma.
Roma mara baada ya kuona kuna nguvu ambayo imeifunga miguu ya Sophia alijua kabisa hapo anapaswa kuwa makini la sivyo ataleta matatizo zaidi.
Roma alijiambia huyo mwendawazimu amefanya chaguo sahihi kabisa kuja kujaribu kumteka Sophia maana alikuwa akimjali sana , ijapokuwa hakuweza kujua ni kwa namna gani mpaka aliamua kufanya chaguzi hio lakini ukweli ni kwamba kwa namna yoyote asingeweza kuona Sophia akipata matatizo.
“Umafikiri najali hilo , kwasababu najua naenda kufa nitamshikilia kama mateka ili nniweze kutoroka, najua una upendo wa juu sana kwa huyu mwanamke”
Roma kabla haa hajaongea Sophia alianza kuongea yeye kwa nguvu.
“Unaongea ujinga, wewe ni nani kwanza ?, mimi sio mwanamke ambaye Bro Roma ana mapenzi nae”
“Hahaha… Sophia kama nitakuwa sijakosea mashabiki zako wanatarajia ujio wako wa mara ya pili katika usanii tena kwa kishindo , wewe tayari ni Celebrity k wanini unajaribu kujishusha , nilishangaa sana kupata taarifa umekuja kujichimbia huku mbali maporini, halafu sijasema neno mapenzi bali nimesemea swala la upendo , inawezekana ni upendo kati ya dada na kaka hehe..”
Sophia mara baada ya kuumbuliwa aijikuta akigeuka kuwa nyanya kwa aibu.
Upande wa Roma hakuwa tayari kumuona Sophia akiwa hatarini na alijitahifi kuvuta pumzi ili kuweza kujituliza.
“Kwahio unadhani kumfanya mateka ndio kutanifanya nishindwe kumuokoa na wewe kukuua?”
“Haha,, kama unachosema ni kweli basi jaribu tuonea nani atakuwa na spidi ya kumuua mwenzake , mimi kumuua huyu mwanamke au wewe kuniua mimi”
Sophia baada ya kusikia maneno hayo aliweza sasa kuelewa nini kinachoendelea , alijua kwamba aliemteka ni adui wa Roma.
“Roma wewe huna haja ya kunijali mimi na kuanza kumsihi aniachie, anaonekana kuwa mhenzi kweli hivyo unapaswa kumuua ,sitojali kama nitadhuli…”Kabla hata hajaendelea kuongea alihisi maumivu makali kwenye shingo yake.
“Unamaanisha nini kwamba nisikujali wewe , kaa kimya maana sijakupa nafasi ya kuongea”Alifoka Roma huuku akimwangalia Sophia kwa macho makali.
Sophia palepale alijikuta akitoa machozi mengi huku akimwangalia Roma lakini upande wa Roma hakutaka kujali machozi yake bali usalama wake kwanza.
Roma palepale alisogea mbele huku akiachia mkandamizo mkali wa hewa wa levo za juu katika kuipita dhiki.
Kitendo cha Lekcha kuhisi mkandamizo ule aliona Roma alikuwa akipingana na onyo lake , Lekcha alikuwa akielewa kwamba kadri Roma anavyochelewa kufanya maamuzi ndio itamuonyesha ni kwa namna gani mateka wake ana thamani.
Lekcha palepale alitoa kamba nyingine kama shoti za Ant-Matter tatu kwa pamoja na kuwakaba shingo wale wanawake wengine waliokuwa wamebakia. Na hali hio ilimfanya Roma kusimama na kuacha kutoa mkandamizo.
“Unaonaje , mipango yangu imefeli kwasababu nilikudharau lakini hii hamaanishi kwamba wengine wanaweza kuhimili mashambulizi yangu , ijapokuwa mimi sio wewe lakini gepu la utofauti wetu kinguvu sio kubwa , hivyo kubali ninachokuambia la sivyo kabla hujanifikia mimi utaokota kwanza maiti ya huyu mrembo”
“Kwahio unanitishia?”
“Utanifanya nini kama unaona na kutishia , najua utahesabu kila kitu kilichotokea nyuma na utaniua kwa namna yoyote ile , hivyo kwanini nisihakikishe nawewe nakupisha kwenye machungu kabla ya kunifikia”Aliongea na kumfanya Roma kupandwa na jazba lakini mpaka hapo hakuwa akijua ni kipi anapaswa kufanya maana asingeweza kukubali kumuona Sophia akigeuka na kuwa maiti.
“Una taka nini?”Aliuliza Roma huku akikunja ngumi yake kwa hasira kiasi cha kufanya kucha zake zitoboe kiganja cha mkono.
‘Tutafanya hivi kwani ni rahisi sana , utaondoka hapa kwenda mbali baada ya kukuwekea nguvu kiasi ya Ant-Matter ambayo itanifanya kujua ni umbali gani umefikia na baada ya hapo nitamuachia Sophia na kukimbia”
‘Kwahio unanifanananisha na kitoto cha darasa la kwanza si ndio ?, kama nitakuacha hapa na kufanya unavyotaka sio tu kwamba utaendelea kumshikiria lakini pia utaenda kujificha na kunifanyia hila kwa mara nyingine, unajuaje huenda ukanigeuka pia na kumuua Sophia”
“Kwahio unataka nini , pointi ya msingi hapa ni wewe kufanya kama ninavyokuambia ,Sophia yupo mikononi mwangu na huna chaguo labda kama unataka kumchukua akiwa maiti “Aliongea na kumfanya Sophia amwangalie Roma na kuzidi kutokwa na machozi na ndani ya dakika kadhaa alijikuta akitoa tabasamu la uchungu , alikuwa ni kama vile kuna wazo limemjia.
“Roma siwezi kukurudisha nyuma na mipango yako”Aliongea
Wakati huo Roma alikuwa akiwaza achukue risk kumuokoa Sophia au afanye kama anavyotaka Lekcha
“Usiwe mjinga Sophia”Aliongea Roma kwa sauti lakini ni kama vile amechelewa kwani palepale Sophia alitema damu nyingi sana huku akiwa ni kama viungo vya ndani mwake vimepasuka.
Roma aliweza kujua Sophia ameweza kufanya jaribio la kujiua kwa kupasua mishipa yake ya damu na nguvu za kijini, hilo liliwezekana kutokana na Sophia alikuwa tayari amekwisha ingia katika levo ya mzunguko kamili.
Kitendo alichokiufanya kilimshangaza Lekcha , hakutegemea swala kama hilo kujitokeza , hakuamini kama Sophia angekuwa na uwezo wa kujiua kwa ajili ushindi wa mwanaume anaempenda
Kitendo chake cha kuchanganywa kidogo na Sophia palepale Roma alitumia nafasi hio vizuri kwani kwa spidi kubwa Roma alikuwa tayari ashamfikia Lekcha mbele yake na kumtwanga ngumi nziro ilioambatana na nguvu za mbingu na ardhi katika eneo la kichwa.
Kitendo cha kutawanyisha eneo la kichwa cha Lekcha hakutaka kusubiri tena kwani palepale alimnyakua Sophia na kupotea nae huku wakati huo huo akiita Caulrodn na kukiacha katika eneo hilohilo.
Roma alikuja kuibukia juu kabisa angani akiwa amemshikilia Sophia ambaye alikuwa amelegea kabisa shingo huku ikiwa haieleweki amepoteza maisha au vipi.
Hasira za Roma ndio ambazo zilimzidia mpaka kuita chungu cha maafa bila kujali matokeo na awamu hio kilikuwa na nguvu kubwa kuliko alivyokitumia mwanzo na kilikuwa na uwezo wa kuvuta kiumbe chochote chenye nguvu ya kiroho mpaka umbali wa kilomita moja.
SEHEMU YA 598A.
Chungu cha maafa kiliuelekezea mdomo wake sehemu ambayo amesimama Lekcha , lakini upande wa Lekcha alikuwa mwepesi sana kufanya maamuzi kwani aligeuka kutoka mwili wa kawaida na kurudi katika umbile la nishati lakini hata hivyo ilikuwa bure.
Lekcha kwa wakati huo alikuwa ametumia kiasi kikubwa sana cha nguvu ya nishati ya Ant- matter na yeye alikuwa tofauti na Roma ambaye nguvu zake hazikutegemea zile ambazo zipo nfdani yake , alikuwa na uwezo wa kuvuna nishati muda wowote na kuzitumia.
Ni muda huo huo mwili wake uliokuwa katika umbile la nguvu ya nishati ya Ant- matter ulianza kutawanyika vipande vipande.
“Hapana siwezi kufa …. Hapana!!”
Lekcha alijikuta akitoa ukulele wa aina yake kwani alishindwa kabisa kuzuia nguvu ya chungu kummeza.
Ilikuwa ni wakati ambao Lekcha aliona kabisa huo ndio mwisho wake, lakini katika hali ambayo hakuwa ameitarajia palepale kulitokea mabadiliko ambayo hayakugegemewa.
Roma mwenyewe hakuweza kutegemea kile ambacho kinakwenda kutokea , ule mnara uliokuwa umejengwa kwa usanifu wa kipekee ulikuwa ukionekana kama vile unacheza cheza , ilikuwa ni kama vile ni tetemeko kubwa la Ardhi ambalo lilikuwa likicheza cheza na ilichukua sekunde hio kulitokea boriti kama tano za mwanga uliokuwa kama Laser rangi ya dhahabuu na kugonga katika wingu ambalo lilikuwa likianza kuzunguka kama vile mvua inataka kunyesha.
Pale juu ya kichwa cha mnara ni kama kulikuwa na kimashine amaalumu kinachofanya kazi na kudhalisha boriti hizo za mwanga.
Cauldron yenyewe palepale iliweza kuzimika na nguvu yake ya mvutano iliisha na ikawa pona ya Lekcha kumezwa.
Roma mwenyewe hakuwa akieleewa ni kitu gani ambacho kinatokea katika hilo eneo na alianza kuzungusha kichwa chake kuangalia kulia na kushoto, hisia ambazo alikuwa akipata zilikuwa tofauti na zile za kupigwana radi baada ya kukiuka kanuni za anga.
Nafsi iliokuwa kwenye Cauldron na yenyewe ilianza kufurukuta kwa namna flani ya kuonyesha woga na jambo hilo lilimshangaza Roma na kujiuliza nini kinatokea
Lekcha ambaye alikuwa dhaifu sana hakuweza hata kukimbia licha ya kuachiwa na chungu na baada ya kuona Roma hakuwa akimwangalia palepale alijaribu kujitengenezea kamba kama vile ni Spider man ili kukimbia lakini ghafla tu ilitokea Flash ya mwanga mkali pamoja na shoti ya aina yake kwenye ule mnara.
Kitendo cha Lekcha kutaka kukimbia tu alijihisi nguvu ya ajabu ikimrudisha nyuma .
“Buzzz!!!!”
Ulisikika mlio wa aina yake wa Radi kutoka katika mawingu yaliokuwa yakizunguka juu na kupiga kwa nguvu ule mnara na kusababisha mpasuko mkubwa wa shoti za umeme.
“What the hell is happening!!!”
Roma alipiga yowe huku akirudi ardhini kwa tahadhari, alijawa na hofu isiokuwa ya kawaida , sekunde moja alidhania huenda n kutoka na kusafiri umbali mrefu sana hivyo akakiuka sheria za anga lakini kilichomshangaza ni kwamba mnara ndio uliokuwa wa kwanza kutoa mwanga wa kimaajabu na ilikuwa ni kama vile ndio uliochokoza radi.
Roma hakutaka kujiuliza mara mbilimbili wakati anahisi hatari alikuwa asharudisha tayari Sophia chini kwa kuhofia angedhurika lakini kwa namna ambavyo mnara huo ulikuwa ukishambuliwa na Radi kwa spidi hakutaka kubakia ttena katika eneo hilo..
Alimnyakua Sophia kwa haraka sana huku akiachana na wazo la kumuua Lekcha tena na kujiokoa yeye mwenyewe na Sophia.
Sophia hakuwa amekufa bado , ijapokuwa damu zimevilia kwa ndani lakini bado alikuwa akipumua kwa mbaali na Roma aliona aondoke ili akamsaidie mbele kwa mbele wakati huo akimwingizia nguvu ya kimaandiko ili kusaidia kupona.
Upande wa wanafunzi wote waliokuwa wakifanya mazooezi katika majumba tofaut tofauti waliweza kukurupuka walipokuwa na kutoka nje kushangaa nini kinaendelea, lakini baada ya kushuhudia mashambulizi kati ya anga na ule mnara walijikuta wakihofia uhai wao.
Dakika hio hio ilikuwa ni kama vile ule mnara unayeyuka katika kilele chake na kuonyesha chuma kikubwa kinachotoa mwanga wa rangi ya gray.ilikuwa rahisi kusema huenda huo mnara ulijengwa kwasababu ya kuzuia radi kutokana na namna ambavyo radi zilivyokuwa zikirindima huku ngurumo kubwa zikisikika pamoja na shoti lakini kwa wakati mmoja mnara ule haukuzima zile boriti zake za rangi ya gold zilizoelekea angani.
Kadri radi iliovyokuwa ikipiga ndio iliwezesha ule mnara kutoa mwanga kama vile ni projector na kuonyesha baadhi ya maumbo ya kimaandishi kama Runes hivi ambazo hazikuwa zikieleweka maana yake.
Roma hakutaka kendelea kushangaa palepale alipaa angani ili kukimbia na wakati huo huo na Lekcha na yeye alitumia nafasi hio kujaribu kutokea lakini ilikuwa ni kitendo cha kasi sana kilichotokea kwani zile boriti za miale ziliancha kumulika juu angani na ziligeuka na kuwa kama minyororo kwani wakati Roma anataka kukimbia alifungwa kiunoni akiwa na Sophia na kuvutwa kwa nguvu kubwa ilikuwa ni kama vile mnara ule ulikuwa ukiendeshwa na mtu na haikuwa kwake tu hata kwa Lekcha ilikuwa hivyo hivyo wote kwa pamoja waliweza kuvutwa kwa nvuvu na mnara ule kuelekea katika eneo ambalo kulikuwa kama vile kuna anga linachemka.
Roma baada ya kuona alikuwa ameshikilia Sophia kwenye mikono yake alikosa uamuzi wa haraka aa aidha amdondoshe chini lakini kiendo cha kutaka kumdondosha chini tu ni kama alishitukiwa na mnara ule kwani palepale na Sophia na yeye alifungwa fungwa na boriti za mwanga na wakaavutwa wote kwa pamoja kwa pamoja
Kilichokuwa kikimtokea Roma ndio kilichokuwa kikimtokea Lekcha , tena kwa Lecha ilikuwa rahisi sana kwani hakuwa na nguvu na alivutwa kwa spidi na kutupiwa katika eneo ambalo anga lake lilikuwa likichemka kama vile ni maji .
Upande wa Roma alijikuta roho ikimuuma kwani kadri alivyokuwa akipambana kwa kuita nguvu za kijini ndio alivyokuwa akizidi kuvutwa na kusogezwa karibu , huku akipatwa na hruuma na kuona anakufa akiwa na Sophia mkononi.
Alijaribbu kuita na chungu chake kiweze kumsaidia lakini hakukuwa na majibu na palepale bila ya kupenda alivutwa kwa kasi sana na kutupiwa katika mchemcho ule wa anga kama ilivyokuwa kwa Lekcha na wakapotea yeye na Sophia.
Ni dakika chache tu baaada ya Roma kupotelea kwenye kiwingu cha mnara ule , palepale ile radi ilipotea na mnara ukaacha kupiga shoti na kukawa kimya kwa mara nyingine
Wale wanafunzi wa pale wenyewe walijikuta wakianza kushangaa na kujaribu kwenda kusimama chini ya mnara kujua Roma na Sophia pamoja na Lekcha wamepotelea wapi lakini hakukuwa na chochote.
Kutokana na eneo hilo kuwa juu mlimani haikuweleweka kama watu wa mbali wameona nini lakini ilibakia kuwa stori ya siku hio kwa wanafunzi na walimu wa dhehebu la Shushani huku habari ikiwa ni kupotea kwa watu juu ya mnara huo ambao kwa mara ya kwanza tokea uwepo hapo hikuwahi kutokea kwa kitu kama hicho.
ITAENDELEA
WATSAPP 0687151346