Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.


MTUNZI: SINGANOJR.


Mono no aware

SEHEMU YA 728.
Tabasamu la uovu ambalo alikuwa akionyesha ‘Roma’ liliwafanya wale majini kujihisi ubaridi usiokuwa wa kawaida.
“Uwezo wake sio wa kawaida”Aliongea Jini Anjiu kwa hamaki mara baada ya kuona Roma amebadilika.
Senjii na Sena wote walionyesha nyuso za wasiwasi na kweli waliweza kuona uwezo wa Roma ulikuwa umeongezeka kwa kiasi kikubwa tofauti na dakika kadhaa zilizopita.
Ijapokuwa hawakuweza kukadiria uwezo wake ulikuwa mkubwa kiasi gani lakini mkandamizo wa nguvu za kijini aliokuwa akitoa ulikuwa ni wa levo nyingine kabisa kuliko mwanzo.
Chaos hakutaka kujisumbua kabisa na namna majini hao walivuokuwa wakimwangalia badala yake alionyesha furaha kwa namna ya kupumua kwa nguvu.
“Tamuuu…. Pumzi yenu inatamanisha sana”Chaos aliekuwa katika sura ya Roma aliongea na kumfanya Senji kuzidi kuwa na wasiwasi.
“Anajaribu kututania huyu… msiwe na wasiwasi , lazima atakuwa ametumia mbinu ya hadaa kujaribu kutuaminisha uwezo wake umeongezeka , hakuna jini au binadamu mwenye uwezo wa kupandisha uwezo wake ndani ya dakika kadhaa tu”
“Upo sahihi hakuna kumuachia aondoke hapa”Aliunga mkono Senji na palepale alitoa Dhana yake ya alama ya kiganja cha mkono na kurushia hewani na palepale maandishi ya njano yaliweza kuonekana.
“Mkondo nyota , kupasuka kwa anga!!”.
Ndani sekunde tu kulikuwa na wingu kubwa la nguvu za mbingu na ardhi ambazo zilikuwa zimejikusanya juu ya Chaos na ziliongezeka na kutengeneza nguzo kubwa ya kinishati ni shambulizi ambalo lilitolewa na Senji.
“Boom!!!”
Nguzo ile kubwa ya kinishati ilidondoka kutoka juu kwenda chini na kusambaza mionzi ambayo ilisambaa karibia eneo lote la chini yake , ilikuwa ni kama vile anga linaharibika.
Lakini hata hivyo Chaos hakuonyesha kujali kabisa na shambulizi hilo na aliruhusu kushambuliwa na palepale aligeuza nguvu zote hizo na kuzisharabu kwa kuzigeuza nishati za mbingu na ardhi.
Katika spidi ya kupepesa macho mashambulizi hayo yalionekana kuwa ya kawaida mbele ya Chaos.
Takribaki miaka elfu nne iliopita majini wa enzi hizo waliweza kumiliki nguvu ya Radi , ni sanaa ambayo waliweza kuistadi kwa kuweza kuvuna nishati za mbingu na ardhi lakini licha ya hivyo iliwachukua miaka kumi katika kumfungia Chaos katika gereza la Cauldron.
Kitendo cha Chaos kuweza kumiliki mwili wa Roma alihamisha nguvu zote ambazo zilikuwa kwenye Cauldron na kuziingiza katika mwili wa Roma ndio maana alionekana kuwa na uwezo wa juu sana tofauti na mwanzo.

Kwasababu Chaos alikuwa tayari ashamiliki mwili huo hakutaka kuficha uhusika wake kamili na iliamua kufanya mashambulizi kwa kasi kubwa.
Siku zote Chaos alitaka kupata mwili wenye nguvu ambao utamuwezesha kurudisha utukufu wake kuliko kuendelea kukaa katika gereza la chungu.
Yaani njia pekee ya Chaos kuweza kutoka katika gereza ni kuweza kuvamia mwili wa Roma
“Hayo ndio mashambulizi yenu , nyie majini hamna kitu kizuri zaidi cha kunipiga nacho tofauti na hii mitekenyo yenu?”Chaos alitoa tabasamu la kejeli na baada ya kauli yake hio ilimrushia Rufi ndani ya kile chungu ili kuendelea kumpatia ulinzi.
Rufi alishajua mtu ambaye yupo mbele yake sio Roma bali ni Chaos na Roho ya Roma ilikuwa imefungiwa , alikuwa kwenye hali ya wasiwasi lakini alishindwa kutoa hata sauti kutokana na hali ya woga aliokuwa nao.
Anjiu alionekana kufikria jambo na kugundua kitu na palepale akapaza sauti kubwa.
“Wewe sio Roma Ramoni , wewe ni mnyama wa kishetani wa machafuko , The Chaos!”
“Nini?”Kauli ya Anjiu ilishitua wale wengine lakini Chaos alitoa cheko kubwa la kishetani.
“Haijalishi mimi ni nani , muhimu ni kwamba nyie wote mnakwenda kuwa chakula changu”
“Unajiona ni nani wakati ndio mwisho wako leo ,Ewe Joka sanaa ya wino tokaa… Hasira ya Joka kuu!!”Aliongea Sena kwa nguvu na hakuonyesha kuogopa kabisa.
Dakika ileile wino ulifyatuka kutoka kwenye mwili wake na kutengeneza kizingia ambacho ndani ya dakika tu kilibadilika na kuwa Joka kubwa mno ambalo lina meno marefu na kuanza kushambuliana na Chaos.
Chaos hakuweza kukwepa shambulizi lake na alikutana nalo ana kwa ana lakini kabla hajaguswa palepale ule wino uliyeyuka na kugeuzwa nishati ya mbingu na ardhi na ukamezwa palepale , shambulizi hilo linaweza kuonekana la kimaajabu lakini mbele ya Chaos lilikuwa ni la kitoto sana.
“Bi Sena kuwa makini”Anjiu aliongea kwa nguvu lakini alionekana kuchelewa kumtahadharisha.
Chaos tayari alikuwa akimsogelea Bi Sena kwa spidi na Sena alionekana hakutegemea Chaos angeweza kumsogelea kwa kasi na muda huo kitu pekee alichokumbuka kutoa kama siraha yake ni Dhana ya Kilio cha pepo.
“Cling , Clng , Cling!!!”
Dhana ya kawaida kama hio mbele ya macho ya Chaos ilikuwa ni kama kijiti na ilivunjwa vunjwa palepale.
“Arghhhh…!!!”
Sena aliishia kutoa kilio kikali mno ambacho kilisambaa na kutengeneza mwangwi mara baada ya kukamatwa na Chaos na kupigwa kibao cha kichwani.
Kichwa cha Bi Sena kilipasuliwa palepale kama vile ni tikiti lililopigwa na nyundo na damu zilifyatuka kama vile ni Fountain.
Tabasamu la Chaos lilikuwa la ukichaa kabisa mara baada ya shambulizi hilo lakini kwa majini wengine walaikuwa katika hali ya mshituko kwa kile ambacho kimetokea.
Roma ambaye sasa ndio Chaos mwenyewe mara baada ya kumpasua Sena kichwa chake ilichomoa mishipa mikubwa ya damu iliokuwa shingoni na kuanza kuinyonya damu yake kwa starehe zote kama vile alikuwa na kiu ya damu ya muda mrefu sana.
Baada ya damu kukauka ilirarua mwili wake palepale na kisha kuanza kutafuna nyama yake , ijapokuwa kwa nje alikuwa akionekana kama Roma lakini matendo aliokuwa akiyafanya ni ya kimnyama kabisa hasa wakati alivyokuwa akitafuna nyama ya jini Sena.
“Arghhhh…!!!”
Rufi alishindwa kuvumilia na kuishia kutoa kilio mara baada ya kuona mpenzi wake akitafuna nyama mbichi , ijapokuwa alikuwa akijua anaemwangalia sio Roma ni Chaos lakini bado hakuamini macho yake.
Majini wengine wa miliki hio ambao walikuwa kwa mbali waliishia kushikwa na bumbuazi huku miguu yao ikilainika na nyuso zao kupauka, hawakuelewa ni kwa namna gani meza imegeuzwa.
Jini ambaye alikuwa amefikia mwishoni mwa levo ya maji ya kiroho alikuwa ameuliwa kwa kuraruliwa namna hio na mtu kama mnyama ambaye yupo katika sura ya Roma.
Machafuko aliangalia juu mara baada ya kumaliza kutafuna na sura yake yote ilikuwa imefunikwa na damu na vipande pande vya nyama , ilikuwa ni kama vile imeibukia kutoka kwenye dimbwi la damu , ijapokuwa alikuwa amefunikwa na damu mwili mzima lakini alikuwa akitoa tabasamu kama vile alikuwa akiufurahia muonekano wake.
“Utamu ambao nilikuwa nikiuota mara kwa mara hatamae nimeweza kuuonja katika uhalisia .. Daah …!!”Aliongea huku akilamba midomo.
Kama kuna yoyote ambaye angeweza kusikia kauli yake , na kuona tukio hilo na pia kama usingeweza kuamini maneno ya Anjiu alioongea basi hakika mtu huyo angesema Roma ni kichaa tena zaidi ya neno lenyewe la ukichaa.
Machafuko au Maafa ndio jina lake halisi , alikuwa ni mnyama aliepewa jina hilo kutokana na matendo yake, alikuwa ni mnyama wa Ghasia, mnyama wa kigaidi ambaye wakati huo alikuwa akimiliki mwili wa Roma na kuonyesha uhalisia wake.
Dakika chache zilizopita walikuwa wana uhakika wa kumshinda Roma lakini sasa hivi mashambulizi yao yalikuwa ni kama vile wanarusha mayai kwenye jiwe na hatimae wanakuja kuelewa sababu ni nini.
“Kimbieni , Kimbieini wote katika uelekeo tofauti tofauti!!”
Anjiu mara baada ya kuona hali sio hali palepale aliona sulushisho ni kukimbia kwa majini hao katika kila pande , maana aliona hakuna namna wanaweza kushinda pambano hilo mbele ya Machafuko kwa tukio lile la kuweza kumuua Sena kwa shambulizi moja tu.
Anjiu hata yeye hakutaka kubakia tena katika eno hilo na alitimua nduki kuelekea upande wa kusini magharibi, wakati huo akipaza sauti kuwaamrisha majini wengine kukimbia bila kufuatana.
Uelekeo ambao alichukua nni kuelekea upande wa miliki ya Panas , Anjiu alijiua kama Chaos ataamua kumfukuzia basi ni vizuri kuelekea upande ambao kuna wajuzi wa mbinu za kijini za juu ili kuweza kusaidiana katika kumdhibiti.
Lakini sasa wakati Anjiu yeye akifanikiwa kushituka kwa dakika na kuanza kutimua jini ambaye alifika hapo pamoja na Senji yeye alichelewa kidogo licha ya kwamba alijua kabisa hana uwezo wa kushinda na alipaswa kukimbia hata kabla ya kauli ya Anjiu.
Kitendo cha Anjiu kutoa agizo la majini kukimbia, Machafuko alionekana kukasirika sana na kujiambia hawa kunguni wanathubutu vipi kukimbia , haileti tofauti yoyote kwani tayari yupo katika mwili wa Roma hivyo ingekuwa ni swala la muda tu kuwararua wote na kuwatafuna.
Lakini sasa kitendo cha majini hao kukimbia katika uelekeo tofauti ilimuia vigumu kuwakamata wote kwa wakati mmoja na alibakiwa na chaguo moja tu la kuchagua upande wa kufukuzia na hapo ndio iliona jini mzee ambaye yupo katikati mwa levo ya maji ya kiroho ambaye alizubaa.
“Arghh…!!!, tafadhari usinitafunee”
Jini yule mzee mara baada ya kuona Machafuko amemuungia spidi alipiga makelele huku akiwa na wasiwasi namna ambavyo anakwenda kuraruriwa , hakuamini miaka yake mia moja aliotumia kuvuna nishati za mbingu na ardhi itaishia katika mdomo wa Chaos.
Licha ya kujitahidi kukimbia huku akipiga yowe Chaos alikuwa na spidi kuliko yeye na ndani ya dakika tu alishikiliwa mkono na kuvutwa kwa nguvu na kukamatwa shingo ambayo ilivunjwa palepale na kuanza kunyonya damu na nishari yake yote ya mbingu na ardhi na kisha kugeuzwa majivu.
Majini wote wa miliki ya Xia walikuwa wametoweka katika makao hayo kwa kukimbia pande tofauti tofauti na Chaos hakutaka kujisumbua kuwafukuzia.
Chaos aliona hana haja ya kujisumbua ili hali ana uelewa juu ya Roma alichoona mara baada ya kufika katika miliki ya Kekexil , kama ni kutaka kwenda kuendelea kujipatia vitoweo basi tofauti na kufukuzia majini waliosambaa itakuwa vizuri kuelekea Kekexil kula nyama ya majini na baada ya hapo angeenda na Hongmeng na kisha Panas kumalizia na hatimae utukufu wake ungeonekana.
Kutokana na Chaos kuwa mnyama ambaye hana mwisho , mnyama ambaye hafi na wa kishetani uwezo wake wa kiakili ulikuwa mkubwa mno lakini licha ya hivyo kitu kimoja ambacho hakuwa na uwezo wa kujizuia ni tamaa ya kunyonya kila aina ya nguvu ambayo ipo katika ulimwengu huo na kisha kuhamia katika ulimwengu wa kawaida na kula kila kiumbe kinachovuta pumzi.
Ilikuwa ni kwasababu hio hio ya tamaa ya mnyama huyo ndio maana aliishia kwenye mtego wa chungu na kufungiwa kwani kama sio hivyo angeweza kufuta jamii ya kibinadamu na majini mara moja.
Hayakuwa maamuzi ya mnyama huyo bali ilikuwa ni hatima yake , ni swala ambalo ili kuendelea kuishi asingeweza kuepuka kufanya hivyo.
“Mh wapo vizuri kwenye mikimbio…”Aliongea huku akimalizia utamu wa mwisho mwisho wa nyama mbichi na mara baada ya kukamilisha iligeuza macho yake kwa Rufi ambaye alikuwa amemhifadhi kwenye chungu.
Rufi mara baada ya kukutanisha macho na Chaos alihisi kutetemeka kusikokuwa kwa kawaida.
“Umemfanyia nini mume wangu?”Aliongea Rufi kwa kujikaza.
“Bado tu unapata ujasiri wa kuniongelesha wewe msichana… mwanaume wako tayari hayupo hapa na kuanzia leo na kuendelea huu mwili ni mali yangu na si vinginevyo”
“Wewe ni muongo , mpenzi wangu hawezi kukupatia mwili wake kirahisi hivyo”Aliongea Rufi huku machozi mengi yakimtoka akiwa na tumaini hafifu kwenye moyo wake na kujiambia Roma ataweza kuishinda nafsi hio.
“Hahahaha…. Hahahaha.. sina muda wa kupoteza na binadamu usie na thamani kama wewe.. Roma alileta ujuaji na kuniambia oh eti nilindie mpenzi wangu mpuuzi yule , nilimkubalia ndio lakini haikuwa nia yangu ya dhati kukulinda, nilitaka akubaliane na matakwa yangu tu, ili kurudisha uwezo wangu katika viwango ninatakiwa kuendelea kunywa damu ya
majini na sina muda wa kujibishana na binadamu mimi”
Chaos muda huo alikuwa akiendeshwa na roho ya kisasi kwa kile majini walichomfanyia mpaka kumfukia katika chungu na alitaka kulipa kisasi kwa kuwatafuna.
“Roma anadharau sana ameshiindwaje kuniheshimu wakati nilipokuwa dhaifu na kunifanya mbwa wake, sasa ili kulipiza machungu ya kunidharau nitaanza na wewe mwanamke wake na baada ya hapo nikimalizana na kunywa damu ya majini nitaenda kisiwani kwake na kula wengine ili kutuliza chuki yangu, lakini kwasasa ninachotamani ni kuona wewe mrembo ukiomba huruma yangu hahahaha… nitakusamehe kama utanifurahisha pengine unaweza kuwa mpenzi wangu”
“Wewe ni mnyama tu unaesikitisha na kutia huruma na utabakia kuwa hivyo , niue kama unataka unafikiri nitaomba uniache hai , mwanamke dhaifu kama mimi bado tu pia ninao uwezo wa kukudharau”Aliongea Rufi kwa hasira na kumfanya
Chaos kutoa tabasamu la kifedhuli na hasira kuongezeka maradufu huku macho yake yakizidi kuwaka taa nyekundu.
“Kwasababu unaleta ujeuri mbele yangu nitararua mwili wako vipande vipande na kukutafuna , sipati picha Roma atakavyojiskia mara baada ya kujua amemtafuna mpenzi wake”
Baada ya kumaliza kauli hio Chaos alimsogelea Rufi kwa spidi kwa kulenga kifua chake akidhamiria kunyofoa moyo wake nje.
Lakini kadri alivyokuwa akijitahidi kunyoosha mkono wake kumfikia Rufi alishindwa kabisa kumfikia na aliishia kufurukuta na kutetemeka kaa vile anaishiwa na nguvu.
“Nini… imewezakenaje… pumbavu.. noo!!”
Chaos alijikuta akizidi kupagawa huku mwili wake ukitetemeka , kiini cha macho yake ambacho kilikuwa ni cha rangi nyekundu kilianza kufifia na nguvu yake ya giza ilianza kupungua pia.
Rufi ambaye alikuwa amefumba macho yake na
masikio yake akiwa tayari kufa ghafla tu alihisi jambo ambalo halikuwa la kawaida na kujikuta akiingiwa na tumaini na wasiwasi kwa wakati mmoja.
Wakati huo kulikuwa na vita kali vya kifahamu kati ya Chaos na Roma, ufahamu wa Roma ulikuwa ni kama unaibukia ulikolala na kumfaya Chaos kuzidi kupambana lakini alionekana kushindwa vita.
“Wewe mwanaharamu nilijua tu huwezi kutii ahadi yako ulidanganya kwa kuniahidi kulinda wanawake wangu , lakini je unaona mimi ni mtoto mdogo mpaka kukuamini sio?”
Fahamu mbili zilikuwa zikishindana Roma alikuwa akiongea akionekana alikuwa na ngauvu zaidi ya fahamu ya Chaos.
“Huu uwezo wako umetokana na kuimarika kwa uungu wako!!?”Chaos hatimae alielewa nini kinacheondela , alichokuwa akipambana nacho sio
Roma bali ni uungu wa Hades ambao Roma aliurithi.
Lakini sasa kwa namna isioelezeka uungu huo ulionekana kuimarika sana kuliko ilivyokuwa mwanzo na hakutarajia hilo wala kugundua.
Roma alitoa tabasamu huku macho yake yakionyesha hali ya msisimko kuendelza vita hivyo ya kifahamu.
“Unaonaje, nadhani hukutegemea nilikuwa na mpango wangu kichwani , ijapokuwa umeweza kurejesha sehemu ya uwezo wako lakini Caulrdon imefungia kiini cha nafsi yako ndio maana unao uwezo wa kutumia mwili wangu lakini Roho yako halisi ya ndani kama sikosei haina nguvu ya kutosha kumeza nafsi yangu vinginevyo ungekuwa ushannimeza muda mrefu na usingeanza kunibembeleza bembeleza kukuruhusu kutumia mwili wangu”
Kauli hio ilifanya nafsi ya Roho ya Chaos kuchanganyikiwa na kuwa na hasira kwa wakati mmoja , ilikuwa ni kweli roho yake ilikuwa imefungiwa katika Cauldron na hakuna njia rahisi ya kutoka huko kutokana na vizuizi.
Kutokana na athari ya Chungu ilikuwa pia ni ngumu kupata uwezo wake wote na kukimbia au kujitoa na kitu pekee kupata nguvu zake ni kujiambatanisha katika nafsi ya Roma.
Kama nafsi yake halisi ilikuwa na nguvu zake za kutosha roho hio ingekuwa ishammeza Roma muda tu tena bila hata ya kumbembeleza mbeleza.
Sasa muda huo mara baada ya kuona Roma yupo kwenye majanga iliona hio ndio nafasi adhimu ya kumfanya Roma kumwachia mwili wake kihalali na kujikusanyia nguvu kwa haraka na kuizima Roho ya Roma moja kwa moja kumbe alikuwa akitegwa.
Nafsi hio iliamini haijalishi uwezo wa Roma upoje ili mradi Roma atatoa mwili wake kwa hiari yake hatokuwa na uwezo wa kulera ukinzani katika kurudisha nafsi yake , sasa yote hayo yalikuwa ni makisio tu na ilionekana mpango wake haukwenda kama alivyokuwa amepanga kutokana na kutokutegemea uwezo wa akili wa Roma ugekuwa na nguvu kubwa namna hio.
“Imekuwaje , imekuwaje utimamu wako wa akili ukaongezeka kiasi hicho?”Roho Chaos aliongea.
“Kitu pekee ambacho unaweza kuona katika akili yangu ni tabia yangu lakini huwezi kujua mawazo yangu ya ndani , siku chache zilizopita tokea kuanza kwa kufufuka kwa moyo wa Gaia uwezo wangu wa kiuungu wa akili umeongezeka kwa kiasi kikubwa mno , haikuwa kwangu tu hata kwa miungu uwezo wao wa akili pia ulikuwa ukiimarika , usingeweza kujua hili kwasababu mimi situmii kanuni za anga mara kwa mara hivyo ulishindwa kujua kama uwezo wangu wa akili umeongezeka au lah , kitendo cha kuanza kufufuliwa kwa moyo wa Gaia nafsi yangu iliimarika licha ya kwamba uwezo wangu wa
nishati za mbingu na ardhi ulibakia vilevile , hivi unadhani utimamu wangu wa akili unaweza kulingana na huo wa kwako dhaifu , ki ufupi ni kwamba nishakupita muda mrefu na hakuna namna unaweza kunifikia na ukatawala akili yangu labda nikuruhusu”
Maneno ya Roma yalishusha hali ya majigambo ya roho ya Chaos , haijalishi roho hio ilijitahidi vipi lakini haikuweza kufanikiwa hata kutingisha ufahamu wa Roma.
Ki ufupi ni kwamba Chaos aliingia kwenye mtego wa Roma kwa kuamini Roma wa kule Korea aliemeza moyo wa Kibudha ni huyo huyo mara baada ya moyo wa Gaia kuanza kufufuka.
“Hapana , siwezi kupoteza kwako kizembe hivi , hii sio sawa,, arghhh..”
Chaos alijikuta akipambana lakini ilikuwa haina maana tena kwasababu ufufuo wa Moyo wa Gaia ulikuwa ukiimarisha nafsi za miungu hii ni kwasabau nafsi zao zimeungana na Gaia.
Mpango wa Athena ulikuwa ni kufufua ndugu zake ambao nafsi zao zilimezwa na binadamu hivyo njia pekee ya kufanikisha hilo ni kufanya moyo wa Gaia kuwa na nguvu zaidi ambayo itawezesha zile Roho ambazo zilimezwa kuamka, sasa kwasababu na Roma alikuwa na uungu ndani yake moja kwa moja ni kwamba anakuwa na Koneksheni na moyo wa Gaia hivyo kadri moyo huo unavyofufuka ndio ambavyo uwezo wake wa akili pia huimarika.
“Nilishakuambia kwangu wewe huna tofauti na mbwa tu , unatoa wapi ujasiri wa kutaka kummiliki anaekufuga , nina madaraka kamili zidi yako na kitendo chako cha kuonyesha uwezo ambao ulikuwa umeficha muda si mrefu nitaweza kutawala Radi kama siraha , kama unataka kuendelea kula keki yangu basi hakikisha unaendelea kuwa mbwa mtiifu” “Binadamu fisadi sana wewe… hapana.. kafiri wewe”
Nguvu ya Chaos katika fahamu za Roma iliendelea kufifia na mwishowe ikapotea kabisa katika ufahamu wake na kurudi katika Cauldron.









SEHEMU YA 729.
Sasa mara baada ya Roma kuweza kumiliki mwili wake kikamilifu kwa kumfukuza Chaos katika ufahamu wake na kwenda kwenye Chungu macho yake yalirudi katika muonekano wa kawaida , ukiachana na damu ambazo zilikuwa zimemchafua lakini kila kitu kilikuwa sawa.
Kitendo cha Chaos kutumia mwili wa Roma ilimfanya kutoa uwezo wake wa kijini ambao alikuwa ameficha na hilo lilikuwa kosa kwake kwani Roma aliweza kumiliki uwezo huo , ukijumlisha na mapigo matatu ya awamu za radi alijihisi kujiamini maradufu zaidi na kuamini anao uwezo wa kuwashinda Anjiu na wengine.
Baada ya kumtoa Rufi kwenye Chungu na kumkumbaita palepale Roma alikificha, ki ufupi ni kwamba Roho ya mnyama huyo milele itakuwa chini ya Roma na kuwa kama mbwa tu wa kumsaidia kushambulia maadui.
Roma mara sasa baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha hatimae aligeuza macho yake na kumwangalia Rufi na kutoa tabasamu.
“Rufi wewe kilaza unalia nini sasa hebu kaone ? Si nipo sawa?”Aliongea Roma mara baada ya Rufi kuanza kulia kilio cha Kwikwi kama kafiwa vile.
“Hubby…nili ,,,nilijua umesha..”Mwili ulimsisimka kila akikumbuka tukio ambalo limetokea dakika kadha zilizopita.
“Nilikuambia pale kwamba ninabetia uwezo wa Cauldron na sio kwamba nilisema ninakipa mwili wangu , inamaana hukuniamini na ulijua nitamezwa?”
“Mimi ningejua vipi unachomaanisha … hukuniambia nikaelewa”
“Kaone sasa kalivyo kajinga … kama ningekuambia kila ninachowaza Chaos angenishtukia na mpango ungefeli”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutoa kicheko kilichoambatana na aibu.
“Roho ya Chaos imeingia cha kike , Babe wewe ni mjanja sana unajua”
“Hehe sikuwa na jinsi muda ule , hawa majini walikuwa wamenipania si mchezo na kabla ya kuanza pambano nilijua ninaweza kuingia katika hatari hivyo niliiandaa ‘ escape plan’ mapema … nimefaidika sana hata hivyo kwasasa uwezo wangu umeongezeka maradufu na ninaweza kuwaua muda wowote nitakaotaka”Aliongea Roma huku akikumbuka Lahani na baba yake walivyotoroka lakini hata hivyo alikuwa ashaua majini zaidi ya wa nne wa levo za maji ya kiroho katika miliki hio.
Kama utafananisha na hasara waliopata kati ya Kekexil na Xia basi miliki ya Xia imepoteza zaidi majini wenye nguvu kuliko ilivyokuwa kwa Kekexil ambao walipoteza kwa kiasi kikubwa madawa hivyo hasara ni ya kawadai kwani ni rahisi kutafuta madawa na vidonge kuliko kupandisha uwezo wa kijini.
Rufi sasa alipatwa na msisimko na furaha mara baada ya kutoka katika hali ya hatari.
“Hubby kwahio muda si mrefu utakuwa na uwezo wa kudhibiti Radi , nadhani kwa msaada wa Cauldron haitokuwa ngumu kupita dhiki ya radi ya mapigo mengi , ukijumlisha na utimamu wako wa mwili kila kitu kinafaida kwako”
“Upo sahihi kwasasa nguvu zangu ni za kutosha na busara pia zimeimarika lakini bado nitahitajika kuwa na muda sahihi kabla ya kupita , nataka kupata fursa ya kuelewa kanuni za mbingu zinavyofanya kazi , ni kama Anjiu tu ambaye alisubiri muda mrefu ili kuja kuelewa fumbo la kaunni za mbingu
zilivyo”Aliongea Roma na Rufi alitingisha kichwa na furaha ilikuwa imemtawala na alishindwa kuyazuia mahaba yake na kumkumbaita Roma na kumbusu shavuni licha ya kwamba alikuwa amechafuka na damu.
“Hey embu acha kunibusu huoni namna ambavyo Chaos amechafua mwili wangu , Babe Rufi ninafuraha hatujapata majeraha na pia tumeweza kupata faida kubwa , nitakupeleka sasa visiwani , nikishakamilisha maswala yangu huko duniani nitarudi tena na kuwaua wote”
Rufi alitingisha kichwa kwa mchecheto huku akiwa na hamu kubwa ya kukutana na mlezi wake Sui.
Roma bila ya kuchelewa alimshikilia vizuri na kumuwekewa kinga ili aweze kupumua na kisha alianza safari ya kuelekea kusini magharibi, ilikuwa ndio ulelekeo ambao Anjiu alikimbilia lakini Roma hakuwa na mpango wa kumfukuzia tena, mpango wake ilikuwa ni kurudi Visiwa vya wafu mapema kadri iwezekanavyo kwani misheni ya kumuokoa Rufi ilikuwa imekamilika.
Wakiwa njiani Roma alimuuliza Rufi namna ambavyo alilelewa kwani aliletwa katika ulimwengu huo akiwa mdogo sana na ilionekana Rufi aliweza kuwa mkubwa kutokana na kunyonyshwa maziwa ya kopo ambayo yalitokea katika ulimwengu wa kawaida.
Ukweli ni kwmaba majini kwao hawakuwa wakipika chakula kama binadamu kwao wale wasile haina madhara kwao vyakula vyao vimekaa kama madawa madawa , wanatafuna mizizi na majani si mchezo.
Hatimae bila ya kukutana na jini mwingine njiani waliweza kufanikiwa na kutokea katika ulimwengu wa kawaida kupitia baharini.
Baada ya safari ndefu ya nusu dunia hatimae waliweza kufika Mediterranian muda wa jioni kabla ya machweo na kukaribishwa na upepo wa bahari.
Uwezo wa utambuzi wa Roma ulikuwa mkubwa mno hivyo aliweza kuchunguza eneo ambalo Sui alipo na ndani ya muda tu aliweza kugundua Sui yupo na Bi Wema na wengine wamekaa nje ya kijumba kilchotengenezwa kwa miti pembezoni mwa fukwe mita kadhaa kutoka ngome ilip.
Roma kabla ya kufika katika visiwa hivyo alikuwa ashabadili mavazi na kujisafisha kabisa ili asije kutisha watu hivyo moja kwa moja alienda mpaka walipo.
Ilikuwa ni nyumba ya miti ambayo ilikuwa ikitumiwa na Ron kwa mapumziko na ndani yake alikuwa sio Bi Wema tu walikuwepo Neema Luwazo , Nasra na Doris.
Wakati huo huo Edna na Lanlan walikuwa wakicheza kwenye bembea katika bustani ambayo imezungukwa na maua ya kuvutia katika eneo hilohilo.
Ijapokuwa Lanlan alikuwa na uwezo wakuharibbu bembea hio ya chuma kwa uwezo wake lakini alijitahidi kujifanyisha mtoto wa kawaida.
Mara baada ya Roma kutua kutoka angani akiwa na Rufi kila mmoja aligeuza shingo yake na kuwaangalia kwa mshituko na furaha pamoja na shukrani ya kuona wote walikuwa wazima wa afya.
“Hubby !, Rufiii..!!!””Nasra ndio aliekuwa wa kwanza kutoka kwenye mshituko na kupiga kelele za shangwe.
“Omg,,, naona mnatufanyia surprise si mtoe hata taarifa jamani kabla ya kuja”Aliongea Neema kwa utani.
Lanlan ambaye hakuwa mbali na eneo hilo alitoka kwenye bembea na kutimua mbio kwenda kumlaki baba yake, huku Edna ambaye bado alikuwa amekalia bembea aliishia kutoa tabasamu hafifu huku akitingisha kichwa chake kwa namna ya kusikitika kutokana na spidi ya Lanlan.
Bi Wema upande wake palepale aliangua kilio mara baada ya kuwaona na mara baada ya kujihakikisha hakuwa akiota alikimbia na kwenda kumkumbatia Rufi.
“Mwanangnu …. jamani binti yangu mimi…. umejua kunitia wasiwasi”Rufi alianza kuchunguzwa kwanzia nywele mpaka vidole ili kuona kama kuna sehemu iliokuwa na jeraha.
Laiti angemuona Rufi na yale makovu pengine angepoteza fahamu hapo hapo na ilikuwa afahdali Roma alikuwa amechukua hatua ya kumponyesha kabla ya kumrudisha.
Rufi aliishia kumkumbatia mama yake huku machozi yakimtoka na aliishia kuangaliana na Sui na wote kwa pamoja waliishia kutokwa na machozi na aliishia kuita jina la mlezi wake’ nanny’ ijapokuwa alitaja kwa sauti ya chini lakini Sui alisihindwa kujizuia na yeye kwenda kuungana nao katika kukumbatiana.
Onesho la wanawake watatu wakiwa wamekumbatiana huku wakilia ilimfanya Roma kuguswa , ilikua hivyo lakini kwa namna moja alihisi kutojisikia vizuri na aliishia kukumbaitia na Lanlan na kisha alimwangalia Edna wa kwanza na kumpa tabasamu la ushindi na kisha akageuza macho yake kwa wengine na kuwapa ishara zinazofanana.
“Hehe… mnaonaje ushujaa wa mume wenu katika misheni za ki uokozi”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la kihuni huku akiangaliwa na warembo wake.
Hakuna ambaye alikwepesha macho na wote walikuwa na sura za kutaka kujua kile kilichojiri katika ulimwengu huo wa majini.
“Punguzeni munkari …. nitawaambia stori yote baadae, ukiachana na hivyo huyu mzee Ron yuko wapi?”Aliongea Roma na dakika ileile aliweza kuhisi uwepo wa Ron kwenye msitu uliokuwa nyuma ya kibanda hicho.
“Wewe Ron hebu leta uzee wako hapa”
Kiongozi wa kundi la kimafia Ron alikuwa bize kupunua bustani yake ya miti na mua kwenye msitu huo na mara baada ya kusikia sauti ya Roma aliacha kila alichokuwa akifanya na kukimbia.
“You have returned , your Majesty Pluto”Aliongea Ron huku akitoa tabasamu la kiaina hivi , alikuwa amevalia mavazi ya kishamba na kofia aina ya hat huku akiwa ameshikilia koleo.
“Una maagizo yoyote mfalme?”
“Mzee hayo mavazi naona yamekupendeza sana… ninataka kusherehekea kuungana kwa Rufi , Bi Wema na Sui , nataka uandae mvinyo mzuri kutoka kwenye Cellar”
“Does the 1982 Margarita sound good, Your majesty Pluto?”Aliuliza Ron.
“Ndio itafaa , kwanza sijui ni mvinyo upi umebakia kule chini lakini nikipata chupa kadhaa za aina hio itakuwa bomba”Aliongea Roma na Ron alitingisha kichwa lakini Edna alimkodolea macho Roma .
“Ron ni mbunifu wa kimataifa lakini pia mzee wa kuheshimika kwanini unamfanya kama vile ni kijakazi wako , huo ni ukorofi huoni Lanlan anakuangalia?”
“Ohoo.. Wife hapo sasa ndio unakosea , kama nitakuwa mpole mbele ya hawa watu wataona labda napanga kuwaua lakini nikiwa mkorofi mbele yao kwao ndio wananiona mkarimu”Aliongea Roma huku akicheka na kumfinya Lanlan shavu lake , alijisikia amani sana mara baada ya kurudi nyumbani.
Bi Wema, Rufi na Sui hatimae walipoa na kisha kurudi na kukaa kwenye banda hilo la mapumziko
Sui na Bi Wema walitaka hata kumpigia Roma magoti kuonyesha shukrani zao lakini Roma aliwazuia na palepale alimshusha Lanlan chini.
“Kwanini ndio nyie tu , Yezi , Rose na wengine wapo wapi?”
“Hao wadada wameenda mbali kule kisiwani kwa ajili ya kuendelea kujifunza kwani hawakutaka kusumbua watu wakati wakipambana wao kwa wao”Alijibu Dorisi.
“Mage na Yezi pia wameenda? , unamaanisha washaingia..”
“Ndio wamefanikiwa .. Mage aliingia levo ya nafsi masaa kadhaa baada ya wewe kuondoka , sijajua nini lilikuwa tatizo lake lakini kitendo cha Amina kufanikiwa ilimfanya kuwa na wasiwasi lakini wasiwasi huo ndiio uliomsaidia kuingia levo ya nasi , kwa Yezi inaonekana ana kipaji na alifuatia mara baada ya Mage na sasa wanalingana”Aliongea Neema.
Roma alishangaa na hakutegemea kama Yezi ambaye alianza kwa kuchelewa kuweza kufikia levo ya nafsi ndani ya muda mfupi hivyo.
Ijapokuwa walikuwa wakitumia vidonge lakini kupata uelewa na ufumbuzi ilikuwa ni kitu kingine kabisa.
Inaonekana maisha ambayo Yezi amekulia ndio ambayo yamempa uzoefu ambao umemsaidia kupata ufunuo kwa haraka..
Ni Edna , Dorisi , Neema , Nasra na Najma ndio ambao hawakuwa wamefikia levo ya nafsi ,Rufi yeye hakuwa akihesabika kwani hakuwa na uwezo wa kujifunza.
“Wenzenu wamefanikiwa kupita nyie hamna wasiwasi?”
“Ndio tulichokuwa tukijadiliana hapa , na kujiuliza au ni kwasababu ya umri , wenye umri mdogo wanaonekana kupanda levo kwa haraka kuliko sisi ambao umri umeenda kidogo”Aliongea Dorisi na kumfanya Roma kutoa tabasamu na kumwagalia Edna.
“Honey , huoni kuna kitu hakipo sawa katika maneno ya Dorisi , ninachojua unalingana na Mage na Magdalena au nimekosea?”
Upande mwingine Edna hakuonyesha wasiwasi na alikuwa na muonekano wa maringo na alichukua juisi yake ya matunda nakunywa kidogo na kisha akamwnagalia Roma.
“Sina haraka”
Jibu hilo la kawaida lilimfanya Roma kukosa usemi lakini hata hivyo aliishia kutoa tabsamu bila ya kuongea chochote.
“Ukiachana na hayo , Hubby, Mage akirudi hebu angalia ufunuo ambao amepata ni wa ajabu mno”
“Kwanini ni wa ajabu?”
Muda huo wakati wakiongea ndio Ron aliweza kufika akiwa na chupa za mvinyo mwekundu wa Margarita , mvinyo huo gharama yake haina kiwango maalumu sokoni , Margarita ya kawaida ambayo haijazeeshwa kwa muda mrefu inagharimu zaidi ya dola elfu moja sasa hizo ambazo zina umri mkubwa thamani yake ilikuwa ngumu kueleweka.
Lakini Roma kutokana na kuwa na koneksheni dunia nzima marafiki zake walimletea kama zawadi na aliishia kuzihifadhi katika chumba cha ardhi katika Cellar.
Roma mara baada ya kufungua chupa baadhi alimwambia Ron kubakia hapo na kuungana nao kwani alikuwa na maswali anataka kumuuliza lakini pia ilikuwa siku nzuri kwa Roma.
Roma alikuwa na hamu kubwa ya kuwasubiria Rose kurudi pia.
Harufu nzuri ya mvinyo huo iligusa pua za warembo huo na Edna ndio aliekuwa wa kwanza kuomba na yeye apatiwe lakini sasa mara baada ya kuonja aliitema chini akisema mvinyo huo mwekundu ulikuwa hata ukizidiwa utamu na maziwa na juisi ya matnda.
Muda huo huo Roma pia alianza kuelezea kile ambacho kilitokea katika ulimwengu wa majini watu na namna ambavyo Rufi alitoa ushirikiano kwa kutokuwa na hofu kubwa katika kupitia hali hio ya kuogofya.
Mara baada ya kuona Roma alikuwa amepanda zaidi kilevo walishangaa na kuwa na furaha kwa ajili yake.
Kwa upande wa Roma alijua kabisa bado hakuwa juu zaidi ya sehemu ambayo anataka , bado hakuwa na uwezo wa kupambana na jini yule ambaye alikutana nae Dodoma yaani Master namba moja.
Ron hakuelewa chocho te ambacho walikuwa wakiongea kwani kiswahili ndio kilichokuwa kikitumika zaidi na kingereza mara chache.
“Mfalme Pluto , kwasababu ndio umerudi nina taarifa ya kukupatia”Aliongea Ron mara baada ya maongezi kukauka.
“Oh , ni taarifa gani hio?”
“Ni kuhusu Princess Clark , amepanga kugeuza makazi yake hapa kisiwani kuwa maabara , tayari ashasafirisha vifaa vya kimaabara kuja na baadhi ya nyaraka na malighafi kutoka London, muda ambao vitu hivyo vinakaridiwa kufika ni usiku na atafika wakati huo”
“Yale ni makazi yake hivyo muache afanye anachotaka , pia inamuokolea muda kwenda na kurudi kwa ajili ya majaribio ana ukichaa na maswala ya kitafiti ni kama vile hawezi ishi bila ya kuwa na maabara”Aliongea Roma akiwa hana mshangao.
Tokea siku ambayo Roma aliweza kupatiwa hatimiliki ya visiwa hivyo Catherine na Clark walikuwa wakipenda sana kuja kutembelea na walikuwa na ardhi yao kabisa na ilikuwa kubwa mno saizi ya kisiwa na walijenga majengo kama hoteli kwa ajili ya mapumziko.
Zamani Clark alikuwa akija kisiwani hapo mara chache sana lakini furaha ya kuja kisiwani hapo kuungana na wavuna nishati wenzake ilikuwa kubwa ndio maana alitaka kufanya makazi yake kuwa katika eneo hilo ili kuwa rahisi kuendeleza kazi yake na kupata uzoefu katika mafunzo kwa kupambana na wenzake.
Lisaa limoja mbele hatimae wanawake waliokuwa na muonekano wa kimaringo waliweza kufika kutokea kusini , alikuwa ni Rose na wengine na mara baada ya kumuona Roma na Rufi iliwafanya kuwa na furaha isiokuwa na kifani , awamu nyingine ya vicheko na maelezo ilihitajika.
Roma kwa kuwachunguza Rose , Magdalena na Amina walikuwa washaanza kuingia katika mwisho mwa levo ya nafsi , uwezo wa Amina ulikuwa umeongezeka kwa spidi kubwa nje ya matarajio na kuwakaribia Rose na Magdalena na kitu kingine kilichomfanya Roma kushangazwa na Amina kiini cha macho yake ni kama kimebalika na kuwa na ukijani ndani yake na alikuwa akikumbuka aina ya macho hayo kuna mahali aliyaona ila hakuwa akikumbuka vizuri.
Upande wa Yezi na Magdalena walikuwa wamepiga hatua na Roma alijua kutokana na uwepo wa vidonge basi muda si mrefu watafikia mwishoni mwa levo hio.
“Babe otea nilichoweza kufanikisha?”Mage hakutaka hata kuulizwa na alikuwa na hamu ya kumuonyesha Roma.
“Nitajuaje sasa wakati kila mmoja anasema ni kitu cha kushangaza?”


















SEHEMU YA 730.
Mage alikuwa na hamu ya kumuonyesha Roma ufunuo ambao amepata kwa kugeuza nguvu za mbingu na ardhi na kuwa siraha na ndani ya sekunde tu aliweza kubadilisha nguvu zile na kutengeneza moto mweupe kama wingu kwenye mkono wake.
Roma alishangazwa na kitu kile na hakujua moto ule ni wa aina gani kwani hakuwahi kuuona.
“Huo utakuwa ni moto wa maajabu!!”Aliongea Roma aliekuwa katika hali ya mshangao.
“Hubby kumbe unaujua ?, Aunt Sui amesema inawezekana ikawa ni Heart flame sehemu ya moto wa kimaajabu”
“Heart flame!!!?”
Roma alishangazwa na kauli ile na kugeuza macho yake kwa Sui na palepale alielezea.
Heart flame maana yake moto wa moyo , ilikuwa ni kweli ni sehemu ya moto wa kimaajabu , ambao mara nyingi huweza kutengenezwa kwa kugeuza nguvu za mbingu na ardhi na majini ambao wana hasira za haraka, sasa kutokana na tabia zao zilivyo majini wa namna hio hawanaga muda wa kukaa chini na kuvuna nishati hivyo moto wa namna hio kuona unatumika kama siraha ni mara chache sana.
Isitoshe hata hivyo kuwa na hasira za haraka haitoshi kugeuza nishati za mbingu na ardhi kwenda kuwa moto huo bali lazima kwanza mtu kuwa na moyo wa barafu ikimaanisha kwamba tofauti na kuwa na hasira za haraka lazima uwe na kiasi walau kidogo katika kutuliza hasria zako.
Sasa Afande Mage tabia yake ilikuwa ikijulikana kabisa , alikuwa ni mwanamke ambaye ana hasira za karibu na ni hasira hizo hizo ambazo zilimkutanisha na Roma. Hivyo kutokana na tabia yake hio alijikuta akibatatika kupata moto wa namna hio.
Roma alimwambia Mage kujaribu kumshambulia na huo moto na alikuja kugundua sio moto ambao ulikuwa ukiunguza bali ni moto ambao ulikuwa ukifanya akili yako kupatwa na ukichaa ni kama vile shambulizi la kichawi hivi.
Ilikuwa ni kwasababu uwezo wa Roma ulikuwa juu sana ndio maana athari zake zilikuwa kidogo lakini kama Mage atakutana na mshindani ambaye ni wa levo yake akigusana na huo moto kuna uwezekano wa kumfanya kuwa kichaa.
Upande wa yezi licha ya kuingai levo ya nafsi lakini bado ufunuo wa kisiraha hajapata bado, lakini hata hivyo haikuwa na maana kwamba kila ukiingia katika levo ya nafsi ndio moja kwa moja unapata ufunuo wa kisiraha.
“Hii ni kwa ajili yako , upanga wa daraja la kati huu,
ninaona unakufaa sana hivyo usiwe na huzuni”aliongea Roma akimkabidhi Yezi upanga kwasababu bado hakuwa na uwezo wa kisiraha.
Wote walijikuta wakishangazwa na uzuri wa upanga huo ambao katikati ulikuwa umeandikwa jina la Manjushage.
“Manjushage? Hii ni Dhana ya daraja la kati ambayo ni maarufu ndani ya ulimwengu wa kijini , hubby umeipata mara baada ya kuua jini wa miliki ya Xia?”Aliuliza Rufi.
“Ndio nimeaua majini wengi na kuangalia siraha zao lakini ni huu upanga tu ambao mashambulizi yake yamenifurahisha na nimeona unafaa kabisa kutumiwa na Yezi , kwanini unasema ni maarufu sana?”
“Hii ni Dhana ambayo ni mbili kwa moja kadri uwezo wako unavyoongezeka neno manjushage linagawanyika mara mbili na kuwa Manju na Shage, ukishajigawanya mmoja unaweza kutumia kama siraha ya mashambulizi na nyingine unaweza kutumia kama kinga, faida nyingine ni kwamba ukitumia unakuongezea spidi wenywe katika mshambulizi , kama una msingi mzuri wa mashambulizi ya upanga basi inageuka kuwa Dhana ya hatari sana ambayo inaweza kuua hata jini wa nafasi ya maji ya barafu, lakini kama uwezo wako ni wa chini basi inaweza kutokuwa na maana kubwa na inaweza kuwa hatari kwani wenyewe unanyonya nguvu za kijin”
Licha ya Yezi kutokuwa na msingi mzuri wa kutumia panga lakini hakutaka kupokonywa na alificha upanga wake..
“Haijalishi ili mradi nimepewa basi ni zawadi yangu , nitajifunza namna ya kutumia na naahidi kutoitumia kabla sijaelewa namna ya kuitumia”
Uzuri wa upanga huo wa kioo ulimfanya Amina kuwa na wivu na kumwangalia Roma kwa macho ya kurembua na kutia huruma.
“Hubby kwanini unakuwa na upendeleo kwa kumpa
Yezi zawadi peke yake?”
“Sister Amina aisee huna aibu na umri wako huo bado tu unafanya hivyo?”Aliongea Yezi na kumfanya Amina kuona aibu na kujiweka sawa
Roma mara baada ya kuona kila mmoja alitegemea zawadi aliamua kutoa kila Dhana aliopata , Magdalena alipatiwa ule mkanda wa ngurumo radi , upande wa Rose alipewa siraha ya Sanyua na Mage akapewa kisu cha mfupa wa Dragon.
Kila mmoja alipata Dhana kasoro Edna tu ambaye yeye alikuwa na bangiri kwenye mkono wake.
Ukweli ni kwamba licha ya Roma kuwa na uwezo mkubwa sana wa nguvu za kijini lakini mpaka wakati huo alishindwa kujua nguvu halisi ya bangiri hio ambayo amevaa Edna ikoje.
Kwa namna moja ama nyingine ni kama bangiri hio ilikuwa na muunganiko wa moja kwa moja na mvaaji.
Roma hakumsahau kipenzi chake Lanlan pia kwani na yeye alimpa siuraha za daraja la chini kwa ajili ya kuchezea.
Ikiwa giza limeingia kabisa hatimae Roma alihisi ongezeko la mtu mwenye uwezo wa nafsi na alipotumia uwezo wake wa utambuzi alikuja kugundua ni Clark
Kwasababu hawakuwa na chakufanya Roma na warembo wake walianza kutemba kandokando ya fukwe hio na ndio wakati ambao waliweza kuona meli kubwa ya mizigo ya Uingereza iliokuwa na chata la ‘British Royal Cargo’ ikielea taratibu kuelekea kwenye gati.
Ilikuwa na bendera ya jumba la kifalme la Wales kama utambulisho ambayo ilikuwa ikipeperushwa na upepo.
Ni kama nusu saa mbele wanajeshi wa jeshi la majini wa Uingereza ambao wamevalia kombati za kijeshi walionekana kuwa bize kushusha maboksi kadhaa na baadae makontena na kupandishwa kwenye gari na kunza kusafirisha kuelekea makazi ya Clark , sehemu ambayo ndio anapanga kufungua rasmi maabara ya ki utafiti.
Dakika chache mbele helicopter ilionekana kushuka tataribu upande wa mbali kidogo na kushusha baadhi ya watu.
Alionekana mwanamke alievalia shati la kola lenye vifungo kutoka chini mpaka juu ambalo limemkaa vizuri rangi nyeupe , huku akiwa na suruali yenye michirizi miwili ya rangi nyeupe pande zote , nywele zake za kahawia ziliuwa zimechanguka kutokana na upepo uliokuwa ukizipeprusha, ni umaridadi na hadhi ya utukufu ndio vilionekana kutoka kwake..
Clark alitembea kwa kuwasogelea Roma akiwa na tabasamu huku nyuma yake akifatiwa na wanawake wawili wote wakiwa ni wazungu , mmoja alikuwa na muonekano wa kitajiri na mwingine alikuwa ni mwenye wasiwasi na kutokuwa na hali ya kujiamini kidogo.
Mwanamke mrembo mwenye muonekano wa ki utu uzima alikuwa akifanana na Clark kwa vitu vingi , alikuwa ni Catherine mama yake , alikuwa ni ‘hot’ na ‘sexy’ hususani na mavazi yake aliokuwa amevalia.
“Oh my , Clark walk slower , wait fo mama..”
Catherine alikuwa akimpigia makelele Clark akimwambia atembee taratibu lakini Clark ni kama vile hajamsikia na alitembea kuelekea kwenye kundi la watu waliokuwa mbele yake.
Edna na Roma pamoja na wengine wote walisalimiana na Clark huku Roma akimkumbatia kawaida.
“Mama yako anafanya nini hapa?”Aliuliza Roma huku akiwa na wasiwasi kidogo na muonekano wa Catherine.
“Alikuwa akijua mara baada ya kuanza harakati za kuhamisha vitu vyangu na alilazimisha kuja na mimi huku kwa kuogopa namkimbia na kumuacha mwenyewe”
Roma aliishia kutingisha kichwa kwa maneno hayo, yalienda sawa na haiba ya Catherine.
Muda huo huo mara baada ya Catherine kumfikia Roma alishindwa kuzuia furaha yake na kumsogelea akiwa amchanua mikono yake na kumkumbatia.
“Oh my Dear Roma Ramoni , it has been a while don’t you mis me? Mwaaaahh.”
Catherine alimpiga busu shavuni kiasi cha kuacha alama na muda huo Roma alijihisi ubaridi mgongoni na kuishia kugeuka na kuangalia warembo wake ambao walikuwa wakimwangalia kwa macho ya kutisha.
Roma alijihisi kuogopa ,ijapokuwa mabusu hayo kwa wazungu ni kitu cha kawaida na yeye na Catherine ni marafiki lakini ukweli ni kwamba urafiki wao ni wa faida kwani walikuwa wakinyanduana.
Isitoshe kwa wakati huo Clark alikuwa tayari ni mpenzi wake hivyo ni kama Roma anakula kuku na mayai yake.
“Hello , your majesty Pluto”
Sauti ya wasiwasi ilitoka kwa mwanadada ambaye alikuwa ameongozana nao.
Roma alikuwa bize wakati huo na hakuwa amesalimiana nae na palepale alimkumbuka na kutoa tabasamu.
“You must be Grace , the student Clark
Accepted?”Aliuliza Roma akimaanisha kwamba huyo atakuwa ni Grace mwanafunzi ambaye alikubaliwa na Clark.
“Ndio Mfalme Pluto bado unanikumbuka?”
“Bila shaka , ndio ulieokoa maisha ya Rufi lazima nikukumbuke”Aliongea Roma na kisha alisalimiana nae kwa kumpatia mkono,
“Ni Profesa ndio ambaye alimponya Rufi mimi nilifanya wajibu wangu tu”
Wanawake hao hawakuelewa kwanini maongezi yako hivyo lakini Clark aliwaelezea kile kilichomkuta Rufi kule kwenye msitu wa Australia mpaka kumpeleka hospitali ya London kwa ajili ya matibabu na Grace akaonyesha ujasiri wa kutaka kumsaidia Rufi licha ya kuwa nesi asiwe na cheo chochote.
“Kwanini umekuja nae?”Aliuliza Roma mara baada ya kuona Grace alikuwa akijua jina kamili la Roma.
“Ni mwepesi kujifunza na ana kipaji , na zaidi ya yote ana mtazamo chanya na mkarimu , nadhani kipaji chake kilikuwa kimejificha tu kutokana na mazingira pamoja na kutopata elimu sahihi , nipo katika hatua za kumfunza ili kuwa msaidizi wangu namba moja ili baadae aje kutidhi tafiti zangu , hivyo nimekuja nae kwa ajili ya kuona mahali ambapo masomo yake yataanzia”
Grace aliishia kuona aibu huku akifurahia kwa wakati mmoja namna bosi wake anavyomsifia.
Roma aliishia kumchokoza Clark kwa kumgonga kwenye paji la uso, ilikuwa ni Roma na Catherine tu ambao walikuwa wakiruhusiwa kumfanyia hivyo Clark kutokana na cheo chake cha uprincess.
“Hivi tayari ndio ushazeeka mpaka kutaka mrithi , jifanyishe mbele ya wanafunzi wengine lakini sio mble yangu ,… haya waachieni wanajeshi hio mizigo na tutarudi ngomeni kwa ajili ya chakula cha usiku .. oh ?yeah Grace na wewe ungana na sisi”Aliongea Roma akiona amkaribishe na Clark aliishia kutabasamu akimwangalia namna Grace ambavyo alikuwa na wasiwasi.
Kwa kutembea wote walirudi ngomeni huku stori zikiendelea kimakundi makundi na ziliendelea hata wakati wa chakula cha usiku na ilikuwa ni lugha ya kisawahi na kingereza ndio iliokuwa ikisikika hapo ndani ,
Roma alimuuliza Clark kama alikuwa na uhitaji wa Dhana lakini alikataa na sababu ni kwamba Dhana hizo aliona ni dhaifu sana.
Upande wa Catherine alitaka na yeye vidonge vya kuendeleza urembo wake na Roma alimpatia mpaka mbinu za kufanya ili kuendelea kudumisha ujana wake asizeeke haraka na kuhusu kufanikiwa Roma hakutaka kujisumbua sana.
Ki ufupi kila mmoja alionekana kuwa na furaha ndani ya eneo hilo , upande wa Lanlan Roma Ramoni alikuwa amekaa kwenye kiti chake maalumu cha kitoto akiendelea kufurahia nyama yake.
“Hubby unapanga kukaa hapa kwa muda gani , nimesikia kutoka kwa Rufi unapanga kurudi kwenda kuua wanafamilia wa miliki ya Xia?”Aliuliza Afande Mage huku akioneysha hali ya msisimko sana na kumfanya Roma atabasamu kwani ni kama vile anajua anachofikiria.
“Mage najua unachofikiria lakini lazima nikuambie ijapokuwa unamiliki moto huo wa kimaajabu lakini uwezo wako upo chini , Anjiu yule mshenzi anao uwezo wakuua watu wa levo yako elfu moja kwa shambulizi moja tu la moto wake wa ndege wa Dhahabu, hivyo usifikirie kabisa mimi kukupeleka”
“Acha hizo basi , wewe si utakuwepo na utatulinda ?”Mage alibembeleza , kwa haiba ya Mage kwake ilikuwa ni mateso kuvuna nishati bila ya kupambana katika mapigao ya uhalisia , alikuwa ni polisi
mpenda haki na alikuwa na hamu ya kuua jini hata moja ambaye amemsababishia Rufi mateso.
“Mage inatosha bwana ukienda nae utamuongezea tu mzigo , atakuwa mwepesi akiwa peke yake lakini na sisi itakuwa ni udhaifu kwake”Aliongea Magdalena.
“Dada unaongea kama vile hutaki kwenda , mimi shauku yangu ni kuona ulimwengu wa majini ulivyo tu”
“Hakuna kikubwa cha kushangaza , ulimwengu wa majini ni ardhi ya kimisitu na barafu tu kama Antarctica pamoja na nyumba za kimaajabu ajabu”Aliongea Roma huku akicheka.
“Kwahio ukirudi huko kumuua baba na mtoto si itakuwa kazi rahisi?”Aliuliza Rose,
“Nataka kwanza kuacha kufikiria kuhusu hili na kufanya mazingatio mengi lakini kwasababu nina uhakika ninao uwezo wa kuwaua sina haraka , ninachotaka ni kupata uwezo wa juu zaidi kupitia uzoefu wa kule hasa katika kudhibiti radi , pia natamani wao ndio waje huku niwapigie huku huku na kujaribisha na kanuni za anga lakini sidhani kama watakuja kutokana na hofu ya kukutana na miungu , ila kwa siku hizi chache kwanza nataka kukaa na nyie huku nikiangalia ukuaji wa Lanlan, sio kwamba napenda sana kuua majini ila nafanya yote kwa ajili ya maisha yetu kuwa salama yasiokuwa na misuko suko”
Kila mmoja alikuwa kimya wakati Roma akiongea na walimwangalia Roma kwa macho ya shukrani.
“Kama sio wewe vile wa kuongea maneno ya namna hio ukiwa na muonekano wa usiriasi hivyo?”
Edna ambaye alikuwa pembeni ya Roma aliongea huku akimwangalia Roma kwa macho ya kuibia ibia.
“Haha … mwanaume ambaye amekwisha oa mara nyingi hupevuka haraka , tumeona kwa miaka inaenda mitatu sasa na yote hayo ni kutokana na juhudi zako boss wangu”
“Acha kuwa chawa basi”Aliongea huku akimzodoa kichwa chake kwenda pembeni na kumfanya Roma kucheka.
“Nataka kusubiri subiri pia kwani Kule Bagamoyo nimemuacha Tannya ambaye anejifanyisha kuwa Maimuna , nataka nipate taarifa ya nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif kuchukua hatua, hilo ni jambo ambalo napaswa kushughulika nalo pia , ukiachana na hayo nasubiria uwezo wenu kuwa mkubwa ili niwe na amani hata kama hao washenzi wakitoka huko na kuvamia muweze kudili nao”
“Unaongea kama vile upo vizuri sanaa na hatuwezi kupambana pia lakini jua kama kitu kibaya kitakupata na sisi tutapotea hivyo uelewe kwamba katika hili haupo peke yako”Aliongea Nasra.
Maneno yake yalipeleka wimbi la usiriasi katia sura za wanawake hao na kuanzia muda huo walijua wanapaswa kujiandaa kwa lolote lile baya ambalo linaweza kutokea.
Malkia Catherine kutokana na usriasi wa maongezi hayo alishindwa kuvumilia na akaweza uma na vijiko vyake chini.
“I say since Roma has returned and everyone is here , staying on the island may be too monotonous ,what about going to London to see a football game? Its all on me”
(“Nasema kwasababu Roma amesharudi na kila mmoja yupo hapa , kuendelea kubakia hapa kisiwani kunakuwa kunachosha sana vipi kama tukienda London kuangalia mechi ya mpira miguu , gharama zitakuwa juu yangu”
Alishauri Catherine na mtu wa kwanza kukunja sura alikuwa Clark kama vile hajaridhika na pendekezo hilo.
“Mama kwanini mpira ghafla hivyo na tangu lini tukapenda maswala ya mipira sisi?”
“Hicho sio nilichomaanisha , Clark unachojua ni utafiti tu na hujali nini kinatokea katika mazingira ya kukuzunguka tarehe nane ya mwezi ujao fainali ya UEFA Champion leagued inaenda kuchezwa katika uwanja wa Wembley”.
“Kama ni UEFA inahusiana nini na sisi?”
“Bila shaka lina wahusu , nadhani hamjapata taarifa Sophia msanii kutoka Tanzania amealikwa kutumbuiza, hivi unajua ni wasanii wangapi wameweza kupata nafasi ya kutumbuiza laivu katika mashindano makubwa kama hayo , hii ni mara ya kwanza kwa msani chipukizi kupewa nafasi hio “Kila mmoja alishangazwa na habari hizo kwani hakuna aliekuwa akijua.
“Pumbavu kabisa yaani Sophia ameshindwa kuniambia kuhusu hili , ni hatua kubwa mno amepiga halafu kutoka hapa kwenda Uingereza sio mbali”
“Wewe kama mwenyekiti wa Multinational Campany
unafikiri unao muda wa kujisumbua na kinachoendelea ndani ya kijikampuni kidogo cha habari na utamaduni? Nina uhakika Sophia yupo bize kujiandaa na kakosa muda wa kukupa taarifa”Aliongea Roma kwa kutania.
Kutokana na ukaribu uliopo kati ya hapo na Uingereza kila mmoja aliona hakuna haja ya kukataa kutokwenda kuona mechi hio isitoshe hata kama hawapendi mpira wachukulie kama kitendo cha kumsapoti Sophia.
Kutokana na kurudi kwa Roma hawakuona haja ya kuwa na wasiwasi na waliona kwasababu pesa wanayo sio mbaya kama watembelee taifa hilo kwenda kujifanyia manunuzi na kushangaa shangaa staarabu zingine.
*****
Upande mwingine katika ulimwengu wa majini katika miliki ya Panas kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea , Gefu hakuonyesha kuwa katika hali nzuri katika kusikia ripoti iliowafikia kutoka kwa shushu ambaye yupo ndani ya miliki ya Xia,
“Okey inatosha”Aliongea kwa kuonyesha ishara ya mkono na yule shushu alitoka katika chumba hicho cha mikutano.
Baada ya kutoka Gefu aligeuza macho yake na kuangalia ndugu zake na wazee wa ukoo huku akiweka tabasamu la uchungu usoni mwake.
“Huyu Roma Ramoni hakika ni binadamu mwenye bahati sana , ameweza kupona”
“Cha kuogopesha ni kwamba kama alichosema
Shushu ni sahihi basi hata Anjiu na Senji pamoja na wazee wengine waliopo levo ya maji ya kiroho ni kwamba wamemshindwa na kusambaratika kwa kukimbia , hili linamaanisha vitu viwili mosi Roma anaweza akawa tayari ashapitia mapigo zaidi ya mia moja…..”Aliongea Gefu.
“God damn it… huyu nwanaharamu imewezekanaje akawa na uwezo mkubwa hivi kuliko hata sisi majini wenyewe hakuwa ni wa kutsha sana mara ya mwisho nilivyomuona… uwezo huo ni wa majini wa karne zilizopita ambao ni wachache sana na ni levo ambayo ni ngumu kufikiwa katika kipindi hichi”Master namba nne aliongea.
“Kuweza kumiliki Dhana ya kihistoria kama Chaos Cauldron inamaanisha kwamba Roma sio binadamu wa kawaida , Mkuu hata kama miliki yetu haina uhusiano wa karibu na Roma hatupaswi kuwa na uadui nae vinginevyo hata kama wazee wetu wa miliki kuja kupambana bado tunaweza kumshindwa”Mwanaume mweupe ambaye alikuwa amevalia nguo za rangi ya majivu aliongea.
“Namba nne nadhani uende ulimwengu wa kawaida na kumpatia taarifa Jeremy kuwasiliana na binti yake , kupitia yeye nina imani Roma atakubali kukutana na sisi kwa siri”
“Nini , Kaka mkubwa ,,, hio ni hatari sana , huyu binadamu ni muuaji”Maneno yalimtoka Master namba nne akiwa na wasiwasi.
“Bila hatari bila faida”Aliongea




















SEHEMU YA 731.
Siku mbili mbele wanajeshi wa majini wa Uingereza waliondoka kisiwani mara baada ya kukamilisha utengenezaji wa maabara katika ukamilifu uliohitajika.
Roma alikuwa akiinjoi maisha bila mawazo kabisa katika siku mbili zote usiku na mchana , alikuwa akicheza na warembo wake kila wakati aliojisikia.
Hakujali mazingira ni kwenye mchanga wa fukwe au kwenye meli au chumbani kwao yeye aliendeleza kazi.
Viashiria vya kufanya mapenzi na wanawake hao viikuwa vikonekana kila mahali , Stamina yake isiokuwa kawaida ilidhihirika kwa mara nyingine.
Hajawahi kuwa mtakatufu hata hivyo hivyo hakuweza kuona aibu kuzungukwa na wanawake wengi namna hio , zaidi sana ni kwamba kila mwanamke wake alitaka kupata mimba yake hivyo hakuna ambaye alikataa kutoa utamu kwa Roma labda pale ambapo wanajishi kuwa wachomvu sana.
Roma hata pale anapofumwa na mwanamke mwingine asingeona aibu na kumwambia na yeye na ajiunge , ki fupi alijihisi ni kama yupo mbingu ya saba , maisha kwake yalikuwa ya burudani kiasi kwamba hakujua hata muda unavyoenda.
Upande mwingine wanawake ambao hakuwa nao karibu zaidi ni Clark na Yezi , sio kwamba hakuwahitaji lakini ni kama hakujisikia huru mbele ya Yezi na kuhusu Clark ni kwamba muda wote yupo bize na maswala yake ya kisayansi , alikuwa akifanya kazi bila ya kupumzika na msaidizi wake Grace.
Roma alilewa na marafiki zake wanajeshi ambao walifika kisiwani hapo kwa ajili ya kumtembelea , siku ya tatu wakati akirudi ngomeni moja kwa moja alienda hadi chumba cha Master ambacho analala Edna na alimkuta Edna akiwa bize kusoma nyaraka ambazo zimetumwa na Recho.
Alikuwa amevalia Lace blouse kama gauni hivi fupi la kulalia , na alikuwa ameupa mlango mgongo.
Roma aliekuwa amesismama nyuma yake aliweza kumwangalia mrembo huyo kuanzia chini mpaka juu na namna ambavo shepu ilivyojiachia kwenye kiti.
Roma aliishia kumeza mate mengi huku akimsogelea na kisha akamkumbatia kwa nyuma huku mkono wake ukitambaa kwenye mlima wa manyonyo yake.
Edna aliishia kutoa nywele zake ndefu ambazo zimemfunika uso na kumwangalia usoni.
“Nenda kalale kwenye chumba kingine , Lanlan anataka kulala na mimi”
“Aa.. Honey acha hizo basi , Lanlan anaweza kuja muda wowote tu kwani sio kwamba kuna utundu nitakufanyia , si itakuwa vizuri kama sisi wote watatu tukilala kitanda kimoja”Aliongea Roma huku akiminya minya na kufurahia manukato ya mke wake.
Edna alionekana kushindana na msisimko aliokuwa akisikia na aliishia kufumba macho na kulamba lipsi na hatimae alijitahidi na kuondoa mkono wa Roma kwenye nyonyo lake.
“Inatosha bwana , nina jambo muhimu nataka kuongea na wewe”
Roma alishangaa kidogo na aliishia kuweka tabasamu la kihuni kwenye uso wake.
“Jambo gani la usiriasi , ni kweli Mama alikupigia simu tena ? ,kuna kitu ameongea ambacho hakijakufurahisha , usiwe na wasiwasi siku zote lazima kuwe na migogoro na mama mkwe na mke ,
nadhani ni sahihi kwake kuwa na wasiwasi kwasababu tumeamua kukaa nje ya nchi , kesho nitaenda kumtembelea na Lanlan”
“Sio kuhusu mama …”Aliongea huku akionyesha ishara ya wasiwasi kwenye macho yake na aliishia kung’ata lipsi zake huku akionekana kama mwanamke ambaye anatafuta ujasiri.
“Ni kuhusu mheshimiwa Jeremy?”
Roma mara baada ya kusikia kauli hio tabasamu na hali ya utani ilimpotea palepale.
“Nini kuhusu Jeremy amekuambia nini awamu hii?”
Edna mara baada ya kuona muonekano wa Roma alijua kabisa hakuwa katika hali ya matani tena.
“Alitaka nikuambie kwamba mkuu wa miliki ya
Panas… anataka mkutane kwa siri . sasa nawaza kama unaweza kufanya hivyo kwa ajili yangu , wewe mwenyewe ndio utachagua mahali na muda”
Roma alishangazwa na jambo hilo mkuu wa miliki ya Panas anataka kukutana na yeye , ilikuwa sio kawaida kwa wakuu wa majini kutaka kuonana nae katika ulimwengu wa kawaida.
“Edna umesema nifanye hivyo kwa ajili yako , hilo limekuja katika moyo wako mwenyewe au amekulazimisha uongee hivyo mbele yangu?”
“Kauli yangu italeta utofauti wowote hata nikibaadilisha?”
“Ndio , kama wewe ndio umeamua hivyo kwa utashi wako nitaenda kukutana nae kwasababu siwezi kukataa ombi la mke wangu lakini kama ni Jeremy ambaye anajaribu kuchukulia kwa faida uhusiano wetu ili nikutane na nao sitoenda sitaki kuonana na mtu ambaye hawezi kuwa rafiki yangu , ni aidha nisiwe kabisa na uhusiano nae au nimuue kabisa , maana majini sio wa kuaminika kabisa siku zote wana ajenda zao za siri”
Edna aliishia kumwangalia mwanaume wake huku akiwa amezuia pumzi , sekunde kadhaa mbele alitoa tabasamu kana kwamba kuna mzigo ametua.
“Kama ni hivyo basi usiende , nitampatia jibu ake na usisumbuke kwa ajili yangu”
“Kwani kuna haja ya kuendelea kuwasiliana nae .. kwanini usiache kabisa kudili nae tena?”
“Kwasasa naona ni sawa tu .. siwezi fanya kitu cha kijinga ninao uwezo wa kufanya maamuzi”
“Yule mwanaume Jeremy sio mtu wa kuaminika kabisa , ni mtu ambaye haoni tatizo kuitelekeza damu yake… wasiwasi wangu ni baadae kukuumiza”Aliongea Roma hakuacha kufikiria namna mwisho wa Kizwe na Desmond ulivyowafika.
Edna aliishia kuinamisha kichwa chini bila ya kuongea chochote na Roma kwa wakati huo alijua hata kumshauri hakuna maana na ambacho anapaswa kufanya ni kumlinda pekee.
Kwasababu ya jambo hilo Roma alikosa mudi kabisa na baada ya Lanlan kufika na nguo zake za vidoti doti kwa ajili ya kulala alimlaza kitandani na kisha aliondoka.
Roma mara baada ya kutoka nje alienda kusimama juu kabisa ya ngome hio akiangalia mwezi angani , alikuwa na wasiwasi pengine kuna mtego Jeremy na familia yake ya majini wana kitu wanamwandalia.
Wakati akiangalia mandhari ya kisiwa hicho macho yake yalitua upande wa kilomita moja kutoka alipo na kuona mwanga na kumfanya kutoa tabasamu , ilikuwa ni maabara ya Clark ilioanzisha hapo rasmi ilikuwa ikitoa mwanga ikionyesha Clark hakuwa amelala bado.
Palepale alikumbuka alikuwa na maswali kwa Jiniasi huyo hivyo alielekea moja kwa moja upande huo , mara baada ya kuona hakuna mtu nje ya jengo hilo anaeangalia palepale alikwenda kutua katika floor ya kwanza na kuanza kutembea kupandisha juu
Jengo hilo lilikuwa ni la Ghorofa saba kwenda juu na mbili kwenda chini ya ardhi na ni floor moja tu ambao ndio hutumika kama makazi na floor zote ni maabara na maktaba.
Yaani kila floor ilikuwa ikihusiannisha tafiti zake , kulikuwa na vifaa vingi vya ajabu ndani ya eneo hilo ambavyo Roma aliamini hata wanasayansi wanaweza wasijue namna ya kuviendesha kutokana na ukisasa wake.
Hio ilikuwa ni Hazina ya Clark , wasichana wa umri wake wanapenda kuwa na mapochi ya brand kubwa au kumiliki vito lakini mapenzi ya princess huyo ni tofauti kabisa.
Kwa namna ambavyo jengo hilo lilivyo ilionyesha Clark alikuwa na mpango wa muda mrefu wa kuhamishia maabara hapo lilikuwa ni jengo ambalo hata madirisha yake hayakuw aya kawaida na ambayo yamefunwa kwa nje lilionekana kama boksi la kioo.
“Teacher the accelerator has reached the critical point of the force field..”
“What is the conversion efficency?”
“99.99% and above “
“Cordinates checked , start the countdown ..”
“Yes 5,4,3,1!”
Roma ambaye alikuwa ndio anafika floor ya juu kabisa ya jengo hilo ndio maneno ambayo alikuwa akisikia na alijiuliza ni nini hicho wanafanya au wanataka kurusha roketi kwenda angani.
Kidogo tu adondoke mara baada ya kuona hicho ambacho walikuwa wakifanya .
Katikati ya maabara hio kulikuwa na Silinda ya rangi
nyeupe kama darubini kubwa hivi ambayo inaangaliana na anga.
Boriti ya mwanga hafifu kama wa Laser ulitoka katika silinda ile na kuelekea angani.
Roma alishangazwa na jambo lile ijapokuwa hakujua ni nini lakini uwezo wake ulihisi mwanga huo haukuwa wa kawaida kabisa kutokana na nguvu yake ya kutisha.
Baada ya mwanga ule kufifia maabara hio ulirudi katika mwanga wake wa kawaida na ndio sasa Roma aliweza kumuona Clark na Grace wote wakiwa wamevalia mamiwani makubwa ya kujikinga na mwanga.
“Mwalimu kulingana na taarifa , ni kiasi cha 0.1 Attometer nje ya Accuracy ya tageti ,tumefikia malengo”Aliongea Grace huku akionyesha furaha.
Clark ambaye alikuwa upande mwingine kwenye mavazi ya kimaabara alivua miwani yake ile kubwa na kionyesha tabasamu usoni na ndio muda ambao aligeuzia macho yake na kumwangalia Roma.
“Grace umefanya kazi nzuri leo , unaweza kwenda kupumzika sasa nitamalizia palipobakia”
Grace pia alikuwa ashamuona Roma na kwa hali ya aibu kidogo alipita na kuanza kushuka kuelekea chini mara baada ya kuwatakia usiku mwema.
“Inaonyesha ulichagua mwanafunzi sahihi , anaonyesha kuridhika kabisa na utafiti mnaofanya”Aliongea Roma sasa akitembea kuelekea katikati ya maabara hio.
“Grace alikuwa akipenda maswala ya kitabibu mwanzoni lakini nilikuja kugundua ana kipaji cha kuwa mtafiti ..”Aliongea huku akivua gloves na kuzitupia kwenye dustbin na kisha akamsogelea Roma.
“Honey kujitokeza kwako usiku usiku kwenye muda kama huu sio kama wewe vile”
“Hebu tusiende huko kwanza , niambie kwanza mlichokua mkifanya hapa ni nini , mbona
inaonekana kama siraha yenye nguvu hivi?”Aliongea
Roma na Clark alianza kushika ile silinda kana kwamba anaparaza kwa kuoneysha ni kitu cha thamani.
“Huu ni utafiti ambao nilikuwa nikifanya kwa nusu mwaka mpaka sasa ni teknolojia ambayo nimeipatia jina la Cumberbatch Particle lightbeam Cannon’ unaiuonaje si inapendeza kwa kuangalia tu”
“Kupendeza tena?”
Mara baada ya kuelewa anachotaka kuongea Roma aliishia kutingisha kichwa huku akitabasamu.
“Inaonekana kupendeza sana”
Mara baada ya kupewa sifa na Roma macho yake yalionyesha furaha na kuanza kumuelezea Roma kuanzia Wazo la kimuundo , fizikia , mekanikia na nadharia za kimahesabu.
Roma alishangazwa na maneno ya Clark na mara baada ya kuona Clark anaenda mbele katika kuelezea vitu ambavyo vinamuumiza kichwa alimzuia asiendelee.
“Clark kuhusu hiki kifaa…. Kwanini usiende moja kwa moja na kuniambia inahusiana na nini na kazi yake ni nini au ni siraha ya kuua watu?”
“Kuu watu tena?”
“Unaweza kuwa sahihi kwani inaweza kuua lakini nimeitengeneza kwa ajili ya kuzuia vimondo na
Magimba kwa ajili ya spaceships hapo baadae”.
“Hebu rudia”
Roma alikuwa katika mshangao na kujiuliza kwanini maswala ya Spaceship tena.
“Alichosema Hawking ni sahihi , kuna mamilioni ya sayari angani , katika mtazamo wa kitakwimu uwepo wa viumbe tofauti na sisi binadamu ambavyo vipo vinaishi katika Cosmos havihesabiki bila hata ya kwamba hakuna viumbe kutoka sayari nyingine ambao wamegundulika mpaka sasa ukiachana na the gods , hiyo kama Alien wakitupata sisi kabla ya sisi kuwapata inamaanisha sisi bindamu ambao hatuna hata uwezo wa kupeleka kiumbe kwenye sayari ya Mars tutakuwa hatarini , kama mwanasayansi mchango mkubwa ambao anaweza kutoa ni kuwezesha binadamu kutoka duniani na kwenda kuishi katika sayari nyingine ili kulinda jamii yetu , imethibitishwa kwamba binadamu atafikia katika nyakati za Galactic kipindi ambacho tutakuwa na uwezo wa kusafiri kutoka sayari moja kwenda nyingine kwa urahisi tofaut na kusafiri bara moja kwenda bara lingine, sasa kama ni hivyo tunaweza kukutana na vitu kama Magimba , vimondo na mambo mengi hatarishi , sasa ndio wakati ambao kifaa hichi kitaingia katika matumizi , pili binadamu hawezi kusafiri kwenda sayari nyingine akiwa na mizigo mingi , hivyo niliona itakuwa sawa kama nitetengeneza siraha ambayo msingi wake ni
particle light beams, ni sawa na siraha ambazo
unaona kwenye muvi za sayansi fikirishi. Ofcoz hapa nimefanya mjaribio tu haimaanishi kwamba nimeshakamilisha , kama tutataka kutumia katika spaceship tutahitajika kujenga particle accelarotor kubwaa na ongezeko la sayansi itakayofiti muda huo , kukuelezea kwa kifupi ni kwamba sio ngumu kutengeneza siraha kwa kutumia hii Prototype, ninachojaribu kugundua ni kwamba ni namna ipi naweza kupata nishati yenye usanifu wa hali ya ambayo itatumika katika anga za mbali , lakini hilo sio tatizo kwasasa kwani naamini nikiendeleza juhudi nitapata majibu hata miaka mitatu ijayo?”
Roma mara baada ya kusikia maelezo hayo macho yake yalionyesha kutokuamini na kujiuliza hiko kitu kina uwezo wa kuharibu kimondo au magimba , kwahio inamaana kama nguvu yake itaongezeka ni kwamba risasi yake moja itaweza kusabaratisha mji,
“Bora tu mimi ndio mwanaume wako vinginevyo dunia itakuwa katika hatari kama dunia itakuibia tafiti zako hizi za hatari”
“Usiwe na wasiwasi mpenzi , najua mwisho wangu, katika kila vifaa hatarishi nilivyotengeneza nimeweka itifaki za ki usalama ngumu sana kuzijua , ukilazmisha tu inamaanisha unaharbu kabis kifaa hicho , hivyo hata kama mtu akiiba tafiti zangu itakuwa ni bure kabisa , hakuna mtu ambaye anaweza kuiba tafiti yangu na ikawa na maana kwake au kudukua mifumo yangu , ukweli ni kwamba hajawahi kutokea mtu wa aina hio ambaye anaweza kushindana na mimi ni Profesa Shelukindo na Yan Buwen pekee ndio waliokuwa wakinifikia, nimemkumbuka Yan Buwen sana alikuwa ni mwanasansi mwenye akili sana kuwahi kuwepo” “Sitaki hata ujaribu kumkumbuka , mwanaume pekee ambaye anatakiwa kutokea katika mawazo yako ni mimi tu”
Aliongea Roma huku akikaa katika kiti kilichokuwa wazi na kisha akamruhusu Clark kumkalia kwenye mapaja.
“Clark nina kitu ambacho siku zote nilitaka kukuuliza”Aliongea kwa namna ya kumnong’oneza sikioni na msisimko alioupata Clark ulimfanya kujihisi aibu na kuwa mwekundu kama yai.
“Niulize”
“Miezi kadhaa iliopita nilipokuwa Korea mara baada ya kukutana na Athena alisema sielewi msingi halisi wa nadharia ya kanuni za anga ni nini ,na pia alisema katika Anga hakuna ‘force’ kauli yake hii imenifanya kutokumuelewa kabisa , sasa kwasababu wewe ni mtaalamu wa maswala ya fizikia na unajimu kwanini usinielezee ni nini amemanisha kusema Angani hakuna ‘force’”
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: DR SINGANO JR

Mono no aware

SEHEMU YA 732.
Macho ya bluu ya Clark yalichanua baada ya Roma kuuliza swali lake , yalikuwa yakivutia kama vile ni madini na kutamani kuyaangalia muda wote.
“Vizuri , ukweli ni kwamba ni rahisi kuelewa ni kwamba tu wewe mwenyewe hukujaribu kuelewa..”
Akiwa ameng’ata lips zake alitoa tabasamu na kisha palepale akashika mkono wa Roma na kuuweka katika nyonyo lake.
Roma alikuwa akihisi kabisa mlima huo wenye ardhi tifutifu , licha ya kwamba bado alikuwa bikra lakini kifua chake kilikuwa kimetuna mno.
“Nisaidie kufungua basi”Aliongeea kwa sauti ya chini na Roma alimeza mate mengi bila kuelewa anachotaka kufanya mwanamke huyo lakini aliishia katika kumfungua na kufanya maembe dodo kuchomoka kutoka katika kizuizi chake na kuanza kupata hewa safi .
Clark alikuwa mtundu na hakuwa na aibu na aliishia kufurahi kwa namna ambavyo Roma alikuwa akimwangalia kwa uchu.
“Honey , basi chukulia haya manyonyo yangu kama ndio Anga na hii chuchu kama sayari , wewe chukulia ni sayari yoyote iwe dunia au jua , halafu tuseme labda uzito wa sayari umeongezeka..”
Wakati akiendelea kuongea Clark kwa utaratibu sana alimfanya Roma kushika ile chuchu na kuiminya na kufanya nyoyo kutuna upande wa chini .
“Sasa uzito wa sayari ukiongezeka anga linabadilika umbo na kuwa kama hivi na kila maada inakuwa katika udhibiti … labda tu iwepo sayari nyingine ambayo ina uzito mkubwa zaidi na kutengeneza huu mbonyeo na kuzifanya sayari nyingine kuwa katika duara kwa kusukumwa mbali..”
Roma alikuwa makini katika kusikiliza mlelezo hayo na alikuwa amependa namna ambavyo Clark alikuwa akimwelezea kwa njia ya ki ubunifu zaidi , hakuwahi kujua kumbe sayansi ilikuwa tamu namna hio.
Muda huo Clark alikuwa akihisi mkuki wa mwanaume wake ukinyooka kuelekea mbele kama vile unataka kumtoboa suruali yake na pumzi yake ilizidi kuongezeka.
“In Other word … in space , there is exists no force because the presence of mass will alter the shape of the space which eventually produces the ‘force’ we are talking about , but ofcourse this is just the most surfaced knowledge I shares ….”
Ghafla tu Roma alishika kiuno cha Clark na kukivutia kwake na kuanza kumbusu kwenye lips zake.
Busu hilo la papatupapatu lilimpelekea Clark kulala kwenye meza huku Roma akiendelea kubonyeza sayari na anga kwa spidi kubwa.
“Inatosha… nishakuelewa sasa kama nitaendelea kukusikiliza ninaweza kupatwa na ukichaa kwa kuvumilia muda mrefu”
Roma na tamaa zake alimbusu mrembo huyo kwenye shingo na kushuka kuelekea chini , alikuwa akifurahia kila eneo katika mwili wa Clark huku akifurahia manukato mazuri yaliochanganyika na harufu ya mwili wa kizungu pamoja na sanitaiza.
Ijapokuwa harufu hio ilikuwa na maajabu yake lakini bado Roma alionekakan kufurahi.
Ilikuwa hivyo hivyo kwa Clark , alionekana kutoa ushirikiano wa kutosha na kufurahia kile ambacho anafanyiwa na alitaka kuvua koti lake la kimaabara na kulitupia kule lakini Roma alimzuia.
“Usilivue hilo koti unaweza kuvua vya ndani vyote lakini sio hilo koti … ninapenda unavyoonekana ukiwa umevaa hio sare”Aliongea Roma akiwa na tabasamu la kifedhuli kama kawaida yake.
Clark alikuwa kwenye mshangao wa sekunde lakini aligeuza macho yake pembeni lakini kwa wakati mmoja alitii maagizo.
Dakika chache mbele alikuwa uchi kasoro koti tu ambalo lipo mwilini mwake na kuegamizwa kwenye meza na kufanya shepu yake yote kumwagika , alimwangalia Roma na macho yake kama vile ni ya paka na kufanya moyo wa Roma kumiminika.
Kilichofuatia hakikuwa tegemeo lake , utimamu wa mwili wa Clark ulikuwa haumpi nafasi ya kuhisi maumivu kabisa kwani alishitukia tu kifimbo cheza kikimwingia na alichoweza kuhisi ni hamu ya kutaka kuongezewa ujazo.
Roma aliishia kuinama mara baada ya kuhisi mkuki wake kubanwa kila kona na aliishia kutoa tabasamu huku akimwangalia mrembo wake usonni na tabasamu.
“Vipi hupati maumivu?”Aliuliza na kumfanya Clark kuona aibu.
“Honey , jana mama aliniambia kitu yako ni kubwa mnoo na unapenda kumgeuza , nimeamini sasa lakini usinifanyie hivyo maana vitauma”
Kutajwa kwa jina la Catherine katika wakati muhimu kama huo ilimfanya Roma kushangaa na kidogo tu shetani lake kulegea lakini Roma kwa bahati nzuri aliweza kuzizuia hsia zake na kumbusu mdomoni Clark ili asiendelea kuongea.
“Wewe mtoto unafikiri nitaacha ninachokifanya kwa kutaja jina la mama yako , kadri unavyozidi kuleta ukinzani ndio tamaa zinavyozidi kunivaa”
Clark aliishia kucheka bila ya kuongea chochote huku akijisikia vizuri kwa wakati mmoja namna ambavyo Roma anampa vitisho vya uongo.
Bila ya kuonyesha udhaifu wowote kama mwanamke ambaye ni bikra Roma alianza kazi ya kupeleka moto ndani ya maabara hio .
Uwazi wa maabara huo uliojaa baridi ulifunikwa na sauti ya vilio vya kimahaba ambavyo vilidumu mpaka saa saba za usiku.
Baada ya kumaliza Roma alimbeba na kwenda kutua nae katika floor ya juu kabisa ya jengo hilo na kuanza kupulizwa na upepo wa baharini huku wakiangalia nyota.
“Babe kwa uwezo wako huo si utaweza kusafiri kwenda anga za mbali?”
“Siwezi , ijapokuwa naweza kuingia katika anga za juu lakini kadri ninavyozidi kwenda anga za mbali nitakosa mawasiliano ya mbingu na ardhi na nishati itapungua sana ,, itafikia sehemu hakutakuwa na nishati ya mbingu na ardhi kabisa , kingine pia angani hakuna oxygen bila ya uwepo wa elementi hizo muhimu siwezi kumudu hata kwa sekunde na mionzi intaniua”
“Kama nilivyotarajia hakuna nishati ya kutosha , ni kama ‘spaceship’ tu, tatizo hapa ni namna ya kupata rasilimali kutoka huko”
“Babe usiniambie unawaza mambo ya majaribio hata muda kama huu?”
“Oops , I’ m not on purpose it’s just an occupational hazard..”
“Ni sawa tu hata kama umefanya makusudi bado napenda”
“Ndio maneno yenu hayo ya uongo ya kutulegeza sisi wanawake”
“Hapana , naongea kutoka katika uvungu wa moyo wangu”
“Hahaha..najua”
******
Nii katika ulimwengu wa majini katika miliki ya Xia , viashiria vya pambano lililotokea hapo siku kadhaa vilikuwa vikionekana wazi , jengo kubwa la Jade ambalo lilikuwa limesimama siku kadhaa nyuma lilikuwa limeharibika na kutokuwa katika ufahari wake.
Lakini haikuwa imekwisha kwani majini karibia wote bado walikuwa hai.
Katika nyumba ya makazi ya mkuu wa miliki kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea na Anjiu kama mkuu wa miliki ndie ambaye alikuwa akiongoza kikao hicho.
Chini yake kulikuwa na majini watu waliosimama katika mistari mwili na kila mmoja alikuwa aidha na cheo cha kifamilia au alikuwa na kazi ndani ya makao makuu hayo katika nafasi ya juu ya kumuwezesha kuhudhuria kikao.
Kwa namna ambavyo walisimama ni kama vile bado wanaishi katika enzi zile za kale.
Kila mmoja alikuwa amekakamaa mwili huku vichwa vyao walikuwa wameviinamisha chini wakisubiria Anjiu kuongea.
Wakati Jinii Anjiu akiwa katika levo ya maji ya kiroho majini hao walikuwa wakimuogopa mno na hakuna ambaye ashawahi kukataa maagizo yake lakini muda huo alikuwa ni jini ambaye amevuka steji ya radi , hofu yao zidi ya Anjiu ilikuwa kubwa mno.
“Kama nilivyokwisha kusema Roma ni Mhalifu muovu , ameshirikiana na yule msichana mwenye mwili wa Yin nyingi ili kuingia katika miliki yetu na kumuua Laofi , Mtumishi Lao na wazee wetu wawili kwa msaada wa roho ya mnyama inayoishi kwenye Cauldron… hii dharau haikubaliki hivyo nimewaita nyie wote hapa kwa ajili ya kufanya kazi pamoja na kuhakikisha Roma analipia mara mia kwa kile alichofanya”
Sauti ya Anjiu iligonga ngoma za masikio ya kila mhudhuriaji na kufanya kila kiongozi kuonyesha wasiwasi wake na hofu.
“Mkuu , kwasababu Roma ana nguvu nyingi je tutaweza vipi kujilinda kama atakuja kwenye miliki yetu kwa mara nyingine?”Aliuliza mzee mmoja aliekuwa mbele kabisa.
“Kiongozi Ngapu haina haja ya kuwa na wasiwasi ili kuweza kushindana na Roma babu yangu Senji amekuja na wazee wengine wa levo ya maji ya kiroho , pia baba yangu Chaopi amerudi na wazee ambao walikuwa wakilinda miliki , kwasababu nishapita levo ya Radi ninalingana ki uwezo na Roma na nitaendelea kuongeza uwezo wangu kadri siku zinavyosogea kama Roma akija tena ninatumaini tutafanya kazi pamoja na kumuonyesha uhalisia wa nguvu zetu, tuna mamia ya majini ndani ya makao makuu yetu hakuna haja ya sisi kumuogopa binadamu mmoja ambaye amejifunza tamaduni zetu” “Oh kumbe mkuu aliepita amerudi?”
Majini hao walionyesha kufurahia mara baada ya kusikia Chaopi mkuu wa miliki aliepita amekwisha kurudi , ijapokuwa babu yake Anjiu bwana Senji alikuwa na nguvu, jini ambaye aliweza kuiba kiti cha umiliki kwa kutumia uwezo wake tu wa kimapigano alikuwa ni jini Chaopi.
Baada ya Chaopi kuachia ngazi alipotea katika ulimwengu huo wa kijini na alikuwa akifahamika kwa uwezo wake wa kutumia siraha , Master Shagoni anaweza kuwa na uwezo lakini alikuwa cha mtoto sana mbele ya Chaopi.
Sasa jiniasi kama huyo akiamua kurudi kama Anjiu mtoto wake ameivuka radi basi pengine na Chaopi pia alikuwa juu zaidi.
Lakini Anjiu kwa wakati huo hakuongea chochote kuhusu levo ambayo baba yake amefikia katika kuvuna nishati za mbingu na Arrdhi.
Maili kadhaa kutoka makao makuu hayo kulikuwa na ardhi ambayo ilikuwa tambararae ambayo imejazwa na mimea ya aina yake ambayo ilikuwa ikitoa harufu mchanganyiko.
Katikati ya eneo hilo ambalo ni kama bustani kulikuwa na nyumba ndogo tatu au nne hivi ambazo ziliendana na eneo hilo , ilikuwa ni kama Utopia mbali na madhira ya dunia.
Katika wakati huo katika meza ya jiwe la mzunguko Senji alionyesha kucheza mchezo ambao haukufahamika na mzee mwingine ambaye alikuwa na ndevu.
Mara baada ya Anjiu kutua ndani ya eneo hilo kwa nje alisogelea eneo ambalo wazee wake walipo na kuangalia mchezo ambao walikuwa wakicheza lakini kwa namna gemu hilo linavyochezwa ilionyesha mwanaume ambaye hakuwa mzee sana ndio anaelekea kushinda lakini hakutaka kuongea neno lolote.
“Salamu kwenu babu na baba”
Haijalishi alikuwa akiogopesha vipi ndani ya ulimwengu huo wa majini watu lakini bado alikuwa akionyesha heshima mbele ya babu yake na baba yake, hao majini wawili ambao walikuwa mbele yake ndio ambao walikuwa na nguvu kubwa ambao wanastahili heshima yake.
“Vipi wakuu wa familia na koo washaondoka na kurudi makwao?”Aliuliza Senji ambaye alikuwa ameshikilia kete yake ya jiwe kwa namna ya kusita sita kuicheza.
“Ndio na nimeshawapaitia herufi za mawasiliano , kama Roma ataamua kurudi na kuua mmoja wapo
taarifa zitatufikia mara moja ., nishawapatia taarifa pia kurudi kwako baba”Alitingisha kichwa.
“Vipi huyo Binadmau Roma Ramoni bado hajachukua hatua yoyote?”
“Mashushu wetu ambao wameenda ulimwengu wa kawaida wamerudi na taarifa na kusema Roma alirejewa na ufahamu wake kwani aliwasiliana na familia yake , sina uelewa ni kwa namna gani ameweza kruudi katika hali yake ya kawaida lakini inasemekeana yupo nchi ya mbali na mashushu wetu bado wanatafuta kujua nchi hio , pengine pia anapanga kupumzika nadhani na hii inatupatia muda wa sisi kujijega upya”
“Inawezekana pia anataka kuingia katika levo zingine kabla ya kurudi huku , pengine anataka kujua mbinu ya kukitawala chungu vizuri au kuelewa matumizi ya radi ili kuja kutuzima kwa shambulizi moja tu”Aliongea Senji huku akikunja sura kwani mtoto wake alionekana kucheza vizuri.
“Lakini mimi naona tunawaza mbali , kudhibiti radi ya mapigo mengii sio jambo ambalo linawezekana kirahisi , ile siku alikuwa na bahati sana yule mnyama amemsadia , baba na mimi wote tushaipita radi na ni sawa na kusema analingana nae ki uwezo , kama Roma atarudi sidhani kama Chungu chake kitaweza kumsaidia tena”
“Nadhani pia nilishakuambia usijifikitie wa juu sana ki uwezo , adui ambaye ameweza kumuua Bi Sena na Tigola sio wa kawaida , kuingia tu katika levo ya kuipita Radi unajikuta kujiamini hivyo inaweza kukukost.”Aliongea Chaopi na kumfanya Anjiu kunywea.
“Ndio baba nimetambua makosa yangu”
“Wakati ambao unachukua nafasi kama mkuu wa miliki nilikuambia wewe na mimi tageti yetu ni nini , yule mtu hawezi hata kutuangalia kwa nafasi tuliopo na kuhusu kilichotokea juu ya Roma Ramoni ni swala dogo isitoshe hajakuua wakati nikiwa sipo , lakini kwasasa nimerudi na hakuna kingine ambacho naweza kufanya achana na huo mtazamo wako finyu na usijiweke katika kundi la majini wa kawaida ndani ya ulimwengu huu vinginevyo utakuwa mwenyewe siku zote”
“Nitakumbuka maneno yako baba”
“Vizuri , Chaopi inatosha sasa, Anjiu amekuwa akifanya kazi nzuri kuliko hata wewe wakati alipochukua nafasi yako , hakuna kosa katika kupanua miliki yetu isitoshe katika umri wake huo hamkua kwenye levo sawa hivyo ni kama amekuzidi”
“Najua unapaswa kudili na Zianji na wengineo hivyo sitaki kuongea sana , yeye pia ni mtoto wangu na ni mdogo wako maamuzi yapo juu yako , wewe ndio mkuu nina uhakika utakuwa na busara katika kudili na hilo swala”
Anjiu alikaa kimya kwa muda na kisha aliinamisha kichwa chake kama ishara ya heshima na kisha akaaga na kuondoka.
“Mtoto wangu na mjukuu wangu naona mshanizidi sasa”
“Wakati nikiwa mdogo ulikuwa ukiniambia kama mtoto akiwa dhaifu kuliko baba yake basi hapaswi kuzaliwa kabisa”Aliongea Chaopi.
Upande mwingine katika ngome ya makao makuu ya miliki, Anjiu alikuwa amesharudi na kumuiata mdogo wake Zianji na mke wake Leiana.
Zianji mtazamo wake mbele ya kaka yake ulikuwa umebadilika , ile hali ya maringo aliokuwa nayo ilikuwa imepotea na sasa alionekana kukata tamaa kutokana na nafasi ambayo kaka yake yupo.
Dakika ambayo aliingia katika chumba aliishia kuinamisha kichwa chake chini akiogopa hata kumwangalia Anjiu usonni.
Upande wa Leaiana yeye muda wote alikuwa amepamba uso wake kwa tabasamu kama vile hakuna kilichotokea.
Licha ya kwamba Anjiu ndio aliewaita lakini hakuongea neno na alikuwa amekaa tu kwenye kiti chake cha ukuu bila ya kuongea akiwa anawaangalia.
Baada ya kimya cha muda mfupi , Leiana alivunja ukimya.
“Anjiu umetuitia nini?”Aliuliza na kumfanya Anjiu kumwangalia.
“Lahani amejificha nyumbani kwako si ndio?”
“Ndio , amesema atakaa nyumbani kwangu kwa muda , nadhani anamuogopa yule mwizi”
“Haha,,, muoga kama nini , sidhani kama atakuja kufanikisha jambo lolote”Kwa mtazamo wake alijua Lahani alikuwa amejificha kwasababu anaogopa kukosolewa.
Wakati akipambana na Roma alishaona ni mtoto gani ambaye anapaswa kumuandaa kutokana na namna walivyochukulia tatizo lile,.
Ijapokuwa alimwambia Lahani kukimbia lakini mtoto wake wa kike ambaye ni Dhaifu hakukimbia na sio tu kuangalia lakini alijaribu kumuokoa baba yake , kupitia jambo hilo alijua ujasiri ambao upo ndani yake upo kwa uchache katika majini wengi wa kiume.
“Ukiwa na uwezo huwezi kukimbia matatizo”Ndio ambacho aliwaza Anjiu na kuamini.
Baada ya kusimama taratibu kwenye kiti chake ghafla tu Anjiu palepale aligeuza nguvu zake za kijini na kutengeneza kitenesi cha moto kama cha umeme vile katika kiganja chake ambacho kilikuwa kikitoa msisimko wa nguvu za giza.
Ni siraha ambayo ilikuwa imejazwa na nguvu ya kali mno na kubwa ambayo iliwafanya Zianji na Leaiana kurudi nyuma.
“Vipi mnahisi nguvu yake?”
“Taowu!!?”Aliongea Zianji kwa kumaka.
“Ndio , shukrani sikuendee wewe , Laofi na Mohi nimeweza kujipatia nguvu ya ajabu kutoka katika nafsi ya mnyama Taowu , inaweza kuonekana nguvu ya giza lakini imeweza kunipaisha ki uwezo sana na kufanya mbinu yangu ya kimashambulizi ya mshale wa radi uvukao anga kuwa mkubwa sana”
Kauli yake iliwaondolea hali ya tabasamu kabisa katika nyuso za Leaiana na Zianji na kukumbwa na huzuni.
“Kaka inamaana ulijua kila kitu kilichokuwa kikiendelea??”
“Nilijua wewe na Laofi mlikuwa na mahusiano na huyu mwanamke na kisha mkamuingiza na Lao mtumishi , hivi mnadhani lile banda lenu kule bwawani ni sehemu ambayo sifiki … lakini hata hivyo sikuwahi kuwaza mnaweza kupata damu ya mnyama Taowu na kuitumia kwangu , nilionekana mahesabu yangu hayakukaa sawa lakini hata hivyo haijalishi mlikuwa makini vipi mpango wenu umefeli , ninapaswa kuwashukuru kwa kutumia damu hio katika mwili wangu kwani imesaidia sana kupandisha uwezo wangu”
“Kaka .. kaka tafadhari yarehemu maisha yangu”Aliongea Zianji huku akipiga magoti na kutetemeka.
“Relax … sina mpango wa kukufanyia chochote bado una thamani kwa miliki kutokana na uwezo wako isitoshe umelala tu na huyo mwanamke na kufeli kuniwekewa sumu , baba ameniachia haya maamuzi na nimeamua kukuacha hai , lakini utambue hii ni nafasi yako ya mwisho”
“Baba .. amerudi kama ni hivyo kwanini haja…?”
“Kwanini hajakutana na wewe ,kwanini afanye hivyo?”
Maneno yake hayo yalimfanya Zianji kurudi nyuma nyuma kwa kujikongoja.
Ilikuwa ni kweli kutokana na uwezo wake mdogo baba yake hakuwa na haja hata ya kuonana nae kwani hakuwa kitu.
“Asante sana kaka ,,”Aliongea Zianji kwa kujikaza na kisha alisimama na kuondoka kwenye chumba hicho na kumuacha Leiana mke wa Anjiu.
“Kwanini ?... kama ulijua nilikuwa na mahusiano nao kwanini ukaamua kujizuia?”
“Haha.. kujizuia!?.Leiana usifikirie sana , kwanini nifanye hivyo , uhusiano wako na wanaume wengine haunihhusu”
“Mimi sio mkeo ,? Mimi ni mama mtoto wako kumbuka”
“Haha.. kwahio ndio nini sasa , wewe ni mke wangu tu kijina na mtoto wa mtoto wangu bado tu huelewi , nilichotaka kutoka kwako ni kuwa mwanamke wa nyumba yangu lakini haina maana unapaswa kulinda uanamke wako kwa ajili yangu , isitoshe umekuwa ukifanya mahusiano yako ni siri, si ndio?”
Maneno yale yalimuuma sana Leiana , ni zaidi ya Adhabu ambayo angepatiwa kwa usaliti na aliishia kutingisha kichwa akiwa kama haamini.
“Unanidanganya ,, kwanini unanifanyia hivi?”
“Leiana nimekuita hapa ili kukuonya uache mara moja kufanya hila zako zidi yangu , hakuna haja ya miliki yetu kuwa na mke wa mkuu au kuendelea kuwa mama kwa Lahani , isitoshe huna faida yoyote kwangu”
“Haha.. kwahio unasema kwamba unachojali ni madaraka yako na uwezo wako na vitu vingine havina maana kwako?”Anjiu alibakia kimya akionekana kukubaliana na kauli yake.
“Anjiu wewe hakika ni muoga kama Kunguru , hivi unajua ni kwanini nilitaka kukusaliti , kwasababu hujawahi kunijali tokea nilipo kuzalia mtoto , tokea nikiwa mtoto familia yangu iliniambia jina langu litabadilika kwasababu ninakwenda kuolewa na mtu mwenenguvu na kwa moyo mkunjufu nikakubali na
nikajitahidi kwa uwezo wangu kuwa mke mwema lakini nini ulikuwa ukinifanyia , ulijifanyisha tu unanipenda na kunipotezea , hukujaribu hata kuniangalia usoni, wewe ni mwanaume muoga ambaye uliogopa kukataa hisia zangu waziwazi na kuendelea kuwa mnafiki”Aliongea na kumfanya Anjiu kumwangalia kwa macho makali.
“Umemaliza? , kama umemaliza ondoka mbele yangu”
“Sijamaliza , niue hicho ndio ninachojali , tokea siku ambayo nilianza kushirikiana na Laofi na wengine sijawahi kuwaza kuishi , Anjiu mimi nakujua kuliko unavyojijua wewe wenyewe , wewe ni mwanaume ambaye unatia huruma na ambaye hujui ni kipi unapenda na kipi hupendi , ijapokuwa unapambana katika mafunzo ya nishati lakini umeshindwa kupotezea yaliokutokea ulimwengu wa kawaida , tokea siku ambayo umemleta Xiao katika huu ulimwengu nilishajua tayari ulikuwa na mtu umempenda , huyo mwanamke kutoka ulimwengu wa kawaida umempenda na umeshindwa kumpotezea , kwa ninavyokujua usingeruhusu akuzalie mtoto”
“Lakini hebu jiangalie unajitahidi kupotezea hizo hisia ili kuendelea kuwa na nguvu na kujifanyisha hujali lakini ukweli ni kwamba unashindwa kujizuia kumlinda , umemfanya Xiao uwezo wake kuwa wa chini ili asionekane kuwa tishio , hivi huchoki tu , mimi hata kwa kukuangalia hivi ninajichokea , huongei chochote na siku zote ni mtu wa kujifanyisha tu lakini nilishakuona tokea muda mrefu hujali uwepo wangu , Anjiu nakudharau, nakudharu sio kwasababau hunipendi au kuwa bize na kuvuna nishati lakini ni kwasababu upo tayari kupenda binadamu dhaifu kuliko mimi mwanamke ambaye nipo pembeni yako siku zote”
“Kimyaa..!!!”
Anjiu alipandisha hasira na nguvu nyingi za kijini huku akiwa amemkaba Leiana koo na kumfanya asipate hewa na kuishia kukohoa kwa kutema damu.
Mara baada ya kuona huo sio muda wake wa kufariki , aliamua kumauchia na kumsuumia mbali.
“Ondoka , usinifanye nipoteze uvumilivu wangu kwako”
Leaina alijikongoja na kusimama huku akishika shingo yake na kuonyesha tabasamu lililojaa kejeli.
“Naona una hasira , vizuri sana hatimae umeonyesha hisia zako”Aliongea na kumwangalia Anjiu kwa sekunde kadhaa na kisha akageuza na kuondoka lakini kabla hajatoka kabisa aligeuka.
“Hata kama hujawahi kunipenda lakini huwezi kukataa mimi ndio nakujua vizuri , kwasababu dakika ambayo unamfikiria huyo malaya wako mimi nipo nakuangalia usoni”Aliongea na kisha akaondoka na kufanya ukimya kutanda.
Anjiu aliishia kupumua kwa nguvu na dakika ileile alitoa pete ya madini ya Jade kutoka kwenye hifadhi yake na kuanza kuisugua sugua kama vile ina uchafu.









SEHEMU YA 733.
Ilikuwa tayari ni siku kadhaa kufikia siku ya fainali ya mashindano ya UEFA champion League , watu wengi wenye ushawishi na matajiri kutoka pande za dunia walikuwa wakielekea London na wengi ya matajiri waliamua kuegesha boti zao za kifahari ndani ya eneo la Canary Wharf.
Kwasababu ilikuwa ni eneo maarufu ndani ya jiji hilo la London kwa kuwa na biashara nyingi pamoja na mall za kufanyia Shopping wiki hio Mooring fees ilikuwa juu mno na iligharimu zaidi ya paundi elfu kumi kwa kuegesha boti kwa masaa ishirini na nne tu.
Lakini licha ya gharama hio kuwa kubwa haikuwa kikwazo kwa matajiri kwani kwao pesa waliichukulia kama namba tu, ukweli ni kwamba hata kam walikuwa na pesa nyingi eneo hilo halikuwa likitosha.
Mooring fees ni ada ambayo hulipwa kwa kuegesha chombo mfano wa boti katika eneo maalumu ambalo limetengwa karibu na biashara.
Sasa kuweza kuegesha boti yako katika eneo la Canary Wharf ni ishara ya kamili ya utajiri na hadhi.
Dakika hio hio boti moja kuubwa ya kifahari ambayo ilizidi kimo cha boti zote zilizokuwepo mahali hapo ilijongea taratibu na kwenda kusimama eneo la katikati ya Canary Wharf , wanaita sehemu ya Dhahabu ambayo inakupa nafasi ya kupata chochote.
Kitu cha kushangaza zaidi katika mbavu za boti hio kulikuwa kumeegeshwa makombora makubwa ambayo yalikuwa yakiwaka waka kutokana na kupigwa jua.
Kilichowauzi mabilionea wengi ni kwamba mtu huyo mmiliki wa hio boti alikuwa amenunua nafasi mbili zaidi za wazi kana kwamba hataki usimbufu wa kusogelewa na viboti vyao jambo ambalo walichukulia ni kama dharau.
Boti hio kubwa ya kifahari kuliko zote ndani ya eneo hilo ilikuwa ni Erebos , boti ambayo inamilikiwa na mfalme Pluto.
Baada ya kukubali mualiko wa Malkia Catherine
Roma alichukua wanawake wake wote na binti yake Lanlan na kuwapelekea London kwa ajili ya kuangalia onyesho la utumbuizaji wa Sophia kabla ya kuanza kwa fainali , ilikuwa hivyo kwasababu Roma alitumia muda huo kama likizo ya muda mfupi kutokana na kuvuna nishati kwa muda mrefu.
Kama vile iliikuwa ni trip ya kifamilia Roma hakusahau kusafiri na Bi Wema , Sui , Mlezi wa Lanlan Qiang , mama yake na ndugu zake na wengine wengi ambao aliwatumia mualiko na kukubali.
Mama yake Magdalena na Mage, Mama T alikuwa amefika pia , Mama yake Nasra kutoka kijijini Mponde aliweza kufika pia kwa mara ya kwanza katika jiji la raha , Shangazi yake Dorisi na mjomba wake pia walifika , bila kumsahau mke wa Juma pamoja na shangazi yake wote waliweza kusafiri.
Shangazi yake Dorisi na Mama T walikasirika mara baada ya kuona kundi hilo la wanawake wa Roma bila ya kufahamishwa lakini kwasababu watoto hao walikuwa washawaelezea kuwa Roma hakuwa wa kawaida basi hakuna ambaye alimkasirikia na kuishia kumuona sio mtu wa kawaida, hata mara baada ya kusikia kwamba wanao uwezo wa kuishi muda mrefu bila ya kuzeeka walifurahi.
Na Roma ili kuwapamba pamba aliwaahidi kuwapatia vidonge vya kuendelea kuwa vizuri kiafya na kuongeza umri wao wa kuishi.
Hata kama wewe ndio mzazi na watoto wako wote wanampenda mwanaume mmoja na huyo mwanaume mmoja anakuambia anao uwezo wa kukupatia kidonge cha kukuongezea miaka angalau hata kumi
ya kuendelea kuishi unadhani ungekataa , ki ufupi unaweza kwenda mbali na kumwambia’ Mkwe nitazaa mwingine nikupatie’ kwasababu hakuna biandamu ambaye anapenda kufa mapema licha ya kwamba kuna siku ya kifo.
Haikuwa hivyo tu Roma alikuwa tajiri wa kutisha , boti hio ya kifahari ilikuwa ni sababu tosha ya kukufunga mdomo na Roma hakuishia hapo tu hata huko Tanzania kwenyewe walifuatwa na ndege binafsi na kuwasomba wote kuja Uingereza na kuingia katika boti ya kifahari na baada ya hapo kila mmoja akapatiwa kijakazi wa kumsaidia shida zake zote.
Ki ufupi ni kwamba maisha yao ndani ya jiji hilo la London ni kama vile wapo ndotoni katika miliki ya Mfalme Pluto.
Mama T licha ya kuwa na pesa na kumiliki biashara kubwa ndani ya jiji la Dar es salaam hajawahi kuonja ufahari wa namna hio , waliopagawa zaidi ni mama yake Nasra na ndugu wa Najma yaani wifi yake na Shangazi yake..
Hakuna ambaye alikuwa jinga , walijua kwa uwezo wa Roma wa nguvu za kimaajabu wao ni kama sisimizi tu hivyo walijikuta automatiki wakiwa na adabu.
Ndani ya muda mchache tu boti hio ya Erebos ilijaa neema ya watu wengi.
Ijapokuwa London haikuwa na maeneo maarufu ya kufanyia Shopping kama Ginza, Avenue des champes elysee na Fifth Avenue lakini
Knightsbridge and Harrods ilikuwa ni sehemu nzuri kwao kufanya kufuru ya manunuzi.
Hata kwa mwanamke mpole kama Edna , Magdalena na Neema hawawezi kujizuia kuingia katika maduka makubwa ya kifahari ya eneo hilo.
Kuhusu Yezi na Rufi ambao hawakuwa na uelewa mkubwa kuhusu brand maarufu walikuwa na shauku ya kutaka kujua vitu vingi kwa kuuliza maswali.
Wazazi wao walikuwa ni umri tofauti tofuati lakini mwishowe walizoeana kupitia kufanya vitu pamoja.
Mwanzoni Roma alitaka kuwasindikiza kwenda kufanya shopping lakini haraka sana aligundua hawezi kuingilia hivyo aliacha wafanye wenyewe na yeye alikaa eneo la Lounge kusubiria akiwa na Lanlan.
Kwasababu Lanlan alikuwa bado mdogo hakuwa na haja ya kufanya shopping na alichokuwa akipenda sana ni midoli , kuhusu mavazi mashangazi zake na mama yake wangemnunulia tu.
Baba yake pia sio mtu wa mambo mengi isitoshe Roma alikuwa na furaha kuwa na Lanlan pembeni yake ambaye alikuwa mtiifu kuliko hata ya Edna mke wake.
Wanawake uwezo wao wa kununua mavazi na vitu vingine ulikuwa mkubwa mno na siku ya tatu kila mtu alikuwa amejaza hifadhi yake ya pete na wale wasiokuwa na pete walikuwa wamejeza kwenye vyumba vyao.
Siku ya nne kila mmoja hakuwa na hamu ya kununua kitu kingine tena hivyo walihamia kwenye kula vyakula vitamu juu ya boti hio ya kifahari.
Meza zilikuwa zimepangiliwa juu hapo na vijakazi ili kufanya eneo liwe la kutosha kwa kila mmoja.
Sasa jambo la ajabu ni kwamba licha ya kwamba ni mchana tena wa jua kali lakini wazee wote ambao hawakuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi kila mmoja alikuwa amevalia majaketi mazito mno na haikuwa kwao tu hata kwa raia wengi wa jiji la Uingereza.
Roma kwa kuona jambo hilo kuna kitu aliona kabisa hakipo sawa na aligeuza uso wake na kumuangalia Clark.
“Clark hali ya hewa ya kipindi hichi si inakuwaga ni ya kati kwanini inaonekana kama ni kipindi cha baridi hapa Uingereza?”
Kwasababu Clark alikulia London basi alikuwa akijua majira ya nchi hio kwa mwaka mzima.
“Ndio umegundua sasa hivi , joto limeshuka sana dunia nzima katika miezi hii , kawaida joto la London katika mwezi huu linapaswa kuwa kati ya nyuzi kumi na nane mpaka kumi na tisa lakini leo ni kumi na inaonekana linaendelea kushuka”Alijibu.
“Inaonekana hamuangalii taarifa ya habari , tokea wiki iliopita taarifa zinasema kwamba joto la dunia limeporomoka kwa kiwango kikubwa mno kama vile hakuna kabisa’ Global warming’ , hata katika ncha ya Kusini na Kaskazini inaripotiwa ukubwa barafu umeongezeka , wanasayansi duniani wapo katika utafiti ili kujua sababu ni nini”Aliongea Mjomba wake Dorisi ambaye alikuwa akikata kipande cha nyama , alionekana kuwa msomi na tajiri hivyo licha ya Roma na Clark kuongea kingereza alisikia.
Lakini pale pale ndio alipokuja kujua alikuwa akielewa kuongea kingereza na kirusi kwani elimu yake amepatia nchini Urusi na Marekani.
“Kama hata wanasyansi wameshindwa kujua nini tatizo kwanini wewe Clark hufanyii kazi swala hili?”Aliuliza Roma.
“Nishajua kuhusu tukio hili la ajabu hivyo nilishampa kazi Grace kukusanya taarifa kutoka pande zote za dunia , naamini nitaanza utafiti wiki inayokuja”
“Sister Clark you are amaizing , its like you excel in every field”Aliongea Yezi huku akimtolea Clark ulimi kumkejeli lakini kwa wakati mmoja akiwa na hali ya kumkubali.
“Every group has someone who is the best and one who is mediocre , I’m just luck to have a great mind”Aliongea Clark.
Wakati wakiwa wanaongea palepale simu ya Roma ilianza kuita na mara baada ya kuitoa mfukoni aligundua ni namba ngeni kutoka nje ya nchi yaani Tanzania kutokana na mwanzo wa code zake
Roma alikuwa akiijua hio namba na aliishia kumwangalia Mage na Magdalena na mama yao na aliona hawakuwa na uelewa kama ni Afande Tobwe ambaye alikuwa akipiga simu.







SEHEMU YA 734.
Roma alipokea simu na kuweka tabasamu usoni na kisha akaongea kwa sauti bila ya kujiuma uma.
“Hello , nnikusaidie tafadhari”Roma alienda moja kwa moja kama vile hamjui mzee huyo.
“Roma Balozi wa Hongmeng anataka kuonana na wewe”Aliongea Afande Tobwe kijeshi.
“Balozi wa Hongmeng? Nani huyo?”
“Amejitambuliza kwa jina la Xuan Jizi , amesema ni mjumbe wa majini wa Hongmeng katika upande wa dunia”
“Xuan Jizi?”Aliuliza Roma huku akijiambia pengine ni yule ambaye alimhonga vidonge au mwinginekwani hakujua jina lake halisi.
“Amesema sababu ya kutaka kukutana na mimi ni ipi?”
“Hajaongea chochote , hivyo nataka jibu kutoka kwako kama upo tayari kuonana nae au lah”
“Kama ni hivyo mwambie nipo vacation na siwezi kuongea nae chochote na kama anashida sana na mimi mwambie aje London atanikuta lakini sina uhakika kama anaweza kurudi hai maana hili ni eneo ambalo lipo chini ya Apollo na Artemis”
“Nilijua tu utajibu hivyo lakini usijali sana, kwasasa umekuwa na nguvu kubwa mno na unatisha hivyo siwezi kukushauri chochote , nitakupigia kama kuna tatizo”
“Asante sana baba mkwe”Aliongea Roma mara baada ya kucheka kidogo na kisha akakata simu.
“Hubby huyo ni baba yangu uliekuwa ukiongea nae? , kuna tatizo nyumbani au kuna mtu anataka ugomvi na wewe?”
“Ameniuliza ni lini atapata mjukuu ,, mzee ana tabu huyu”Aliongea Roma akiwa siriasi.
“Wewe…!”Mage aliishia kuangalia pembeni baada ya kupewa jibu hilo , tokea aanze kuwa mpnezi wa Roma ule ujeuri wake wote ulikuwa umeisha.
Mama T aliishia kushika nywele za Mage na kutabasamu bila ya kuongea chochote , ukwei ni kwamba licha ya kwamba ameridhia kishingo upande watoto wake wote kujihusisha kimapnzi na mwanaume mmoja lakini bado hakujisikia vizuri na alikuwa mkimya mno.
“Sir nnimesikia hilo jina , ni binadamu ambaye ana mafunzo ya kijini ambaye alijipatia umaarufu kwa miaka kadhaa kutoka Hongmeng , kama ndio ameagizwa kuja kama balozi basi naamini swala hilo sio jepesi”Aliongea Sui.
“Ngoja wafanye wanachotaka , haijalishi ni nini wanataka , kwasasa jambo hilo ni kiporo mpaka Sophia atakapo maliza show yake”
“Halitokuwa tatizo? , kumbuka babu na ndugu zeu wengine bado wapo Tanzania”Aliongea Edna.
“Ndio Roma usivuke mpaka wewe kwasasa ni mtanzania si ajabu wamemtumia Afande Tobwe kuwasiliana na wewe”Aliongea Blandina mama yake.
“Haina haja ya kuwa na wasiwasi kwasababu amekuja kama balozi hawezi kufanya kitu chochote kwani maamuzi hayo hana , wametumia serikali kutaka kuwasiliana na mimi ili waonekane ni kama wazito na muhimu lakini siwezi kuwapa nafasi hio , wakiona siwachukulii siriasi watagundua nguvu yao ni ndogo zidi yangu na hawawezi kuniamrisha amrisha , kama watagusa mtu yoyote ndani ya Tanzania itakuwa ni kukiuka sheria na isitoshe wao ndio wamepewa jukumu la kusimamia sheria hizo”
Wote walikubaliana nae na ukweli waliamini labda Hongmeng wamesikia kile ambacho Roma amekifanya katika ulimwengu huo wa majini maana miliki ya Xia ipo karibu sana na Hongmeng.
Baada ya chakula cha mchana kila mmoja alitawanyika wengine walienda kupumzika wengine walienda kuendelea na mafunzo na wengine kujaribisha kile walichonunua , Mage na Lanlan wao walichukuana na kwenda kuendesha speedboat.
Upande wa Roma alienda kuzamia katika chumba cha Neema Luwazo ambako alikaa muda mfupi sana na kisha akarudi juu kabisa na alimkuta Edna peke yake akiwa ameshikilia kikombe cha chai .
Edna ni kama vile alimtarajia na mara baada ya kumfikia aligeuka na kumwangalia.
“?Hebu kaa kwanza, vipi Neema yupo sawa naona amekuwa mnyonge?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Kwanini ghafla tu ukaanza kumjali Neema wewe ninachokumbuka ni kwamba humpendi”
“Hicho ndio unachowaza , mimi kama mwanamke namuona Neema ni mtu mzuri”Aliongea Edna na kisha akageuzia macho yake na kuangalia jiji, sauti yake ilikuwa nyororo na ya chini kana kwamba alikuwa akijiongelesha yeye mwenyewe.
“Edna umebadilika sana hivi karibuni na nashindwa kukuzoea unajua?”
“Unamaanisha nini?”
“Sijawahi kuwaza utakuja kupatana nao vizuri , ijapokuwa nilitamani ije kutokea lakini mabadiliko yako yamekuwa ya haraka sana na nashindwa kujizuia na kuona kuna kitu ambacho hakipo sawa ,unaweza kuniona labda ni mtu mgumu kufurahisha lakini hisia zangu zinaniambia kivingine kabisa”
“Unaogopa?”Aliuliza Edna akiwa na nusu tabasamu kwenye uso wake na swali lile lilimshangaza sana Roma lakini kwa namna moja swali hilo ni kama amejua kile ambacho Roma anajisikia.
“Unaona mambo kwa upeo wa tofauti nje ya matarajio yako na wasiwasi wako ni kesho yetu ambayo haijulikani , unajifanyisha kutokunielewa lakini ninachoona mimi hapa ni wewe ambae hutaki mimi nikuone kama unanishuku na mabadiliko yangu ndio maana unaniongelesha kwa namna hio”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu kwani ni kama amekamatika.
“Ukiachana na hayo nadhani ni jambo zuri , kwangu ni sawa tu hata usiniambie sababu ya mabadiliko yako , nilikuwa na wasiwasi kwamba huwezi kuishi nao lakini sasa hivi naona kabisa upo hiari kufanya nao shopping na kucheka wanapokutannia na kula nao , kwangu nashukuru sana kwa hili”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia kwa muda.
“Ukweli ni kwamba sijui siku nzuri kama hizi zitadumu kwa muda gani na ninachotaka ni kuwa na maisha ya utulivu na yasiokuwa na mawazo , vipi kama kila kitu kikibadilika siku moja , si itakuwa ni zaidi ya huzuni kwa kuwa na kumbukumbu pekee za sisi kugombana muda wote?”
“Kwanini unaongea hivyo ghafla tu?”Aliuliza Roma kwa kufosi tabasamu huku kope za macho yake zikitetema lakini Edna hakutoa jibu na aliweka kikombe chini na kusimama.
“Naenda kukaa na mama kwanza , kama utakuwa free nenda kamwangalie Lanlan na Mage , sitaki wasababishe matatizo kama jana baada ya kuvamia boti ya mtu mwingine na wenyewe kuwaona kama wezi”
“Sawa nimekuelewa nitaenda mpenzi”Aliongea Roma mara baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha huku akijitahidi kujituliza na kujiambia Edna yupo sawa na hakuna anamchomficha.
Unafikiri nini kinafanya joto la dunia
kushuka??Roma atarudi ujinini je akirudi atafanikiwa Aluta Continuara.
Tukutane jumanne kwa wale ambao siwadai.

Hatimae siku ya kesho yake iliwadia, siku ambayo ndio maalumu kwa fainali ya UEFA na Roma aliweza kuichukua familia yake katika eneo la watu mashuhuri(VIP) ndani ya uwanja wa Wembley.
Ijapokuwa walkuwa hapo kumwangalia Sophia atakavyo perfom tofauti na mecho lakini mazingira hayo ya shamra shamra yalikuwa mazuri kwao pia.
Malkia Catherine ambaye alikuwa mwenyeji wao aliwakariibisha , ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na Blandina mama yake Roma na walianza kuongea kwa pamoja kama vile wlaikuwa wakilingana umri.
Blandina na yeye alichukua fursa hio kumwelezea
Catheirne kile anachokifanya na ilimfurahisha
Catherine na kumwambia aatoa mchango wake katika taasisi yake ya vituo jumuishi vya kuelela Yatim.
Kitendo cha kukutana na mtu mzito kama huyo ilimfanya kujisikiavizuri kwa kuwa na mtoto kama Roma.
Kabla ya mecho kuanza Show ya Sophia na wasanii wengine ilipaswa kuanza na Sophia alikuwa ni msanii wa pili kutumbuiza na aliweza kuonekana akiwa amevalia viatu vya kimichezo.
Kutokana na muonekano wake wa umaridadi na urembo ilimfanya kuonekana vizuri mno katika runinga.
Sophia hakuwa tena yule msichana wa kawaida, wakati huo alikuwa ni Superstar ambaye ameshafanya kolabo na msanii mkubwa duniani kama Christen na wengine wengi na kazi zake zikafanya vizuri kimataifa.
Aliimba wimbo ambao ulikuwa na mchanganyiko wa lugha mbili kati ya kiswahili na kingereza na kutokana na kuwa na Vocal nzuri sauti yake iliteka hisia za watu wengi,
Baada ya Sophia kuondoka aliingia msannii mwingine mkubwa tu kutoka Marekani na alitumbuiza na kisha akaondoka na baada ya taratibu zingine kuisha hatimae mpira ulianza.
Baada ya kumaliza Show yake Sophia alikimbilia kwenda chumba cha VIP kwa ajili ya kukutana na ndugu zake , hata mama yake mzazi pia alikuwepo.
“Superstar wetu anazidi kuwa maarufu kadri siku zinavyosonga , naamini atakuwa ana mwingizia mapesa ya kutosha bosi wake Edna ?”Aliongea Mage kwa kutania.
“Ninachoingiza kwenye kampuni yake ni kidogo kulinganisha na anachokipata kwenye biashara zake zingine”Aliongea Sophia.
“Impressive perfomance “Aliongea Edna akimsifia na Sophia alijisikia vizuri kwa kauli hio , alijua kutokana na kilichotokea kati yake na Edna basi asingeongea nae hata kidogo lakini alifurahi kwamba hana kinyongo.
Baada ya kila mtu kuketi hatimae kila mtu alikaa kimya na kuendelea kuangalia mechi,
Mechi ilikuwa ni timu moja maarufu kutoka Hispania na ilikuwa ikishindana na timu kutoka moja Ufaransa hivyo shangwe ziliuwa juu sana kwa upande wa timu zote mbili.
Asilimi ya wote walikuwa hawana timu na hawakuwa bize sana na mpira kasoro ya Lanlan ambaye alikuwa amekodoa macho.
“Kwanini hawashindi ,mbona ni dhaifu vile na mpira
hauendi mbal, Mommy kwanini wanakimbia taratibu taratibu vile?”
Lanlan alikuwa kaiuliza maswali kama mashine huku Edna akijitahidi kujibu yote , ilionekana hakuelewa sheria za mpira zilivyo.
Baada ya kipindi cha kwanza kuisha wote wakiwa katika eneo la VIP kundi la watu ambao wamevalia mavazi ya suti walifika katika eneo hilo huku wengi wakiwa nnii weusi.
Walinzi waliofoka hapo hawakuoneysha kuzuia mwanaume mmoja ambaye ni mzungu alieongozana na wanaume wawili ambao wote walikuwa weusi.
Mshangao uliwashika warembo hao mara baada ya kugundua mtu ambae amefika katika eneo hilo , alikuwa ni Raisi Jeremy.
Edna alimwangalia Roma akimpa ishara kwamba hajui kama mtu huyo atafika Uingereza.
“Callum Boris I’ m sure you could have gotten a private room of your own to watch the match”Aliongea Catherine
“My apologies your Majesty”Aliongea m mwanaume huyo ambaye alikuwa ametanguliwa alikuwa ni waziri mkuu waUingereza afahamike kwa jina la Boris.
“Ni kwasababu rafiki yetu kutoka Rwanda mheshimiwa Jeremy amefika hapa akiwa na nia ya kuonana na kila moja lakini mathalani zaidi anataka kuonana na Mr Roma Ramoni”Aliongea , alikuwa akijua ubini halisi wa upluto wa Roma.
ITAENDELEA.
WATSAPP ONLY 0687151346
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 735
Callum waziri mkuu wa Uingereza alikuwa akimjua Roma na uhusiano wake na Edna pamoja na Raisi Jeremy , idara ya usalama ya Uingereza haikuwa kwa ajili ya maonyesho tu walikuwa wakijua mambo mengi.
Lakini hata hivyo hakuwa akijua nia halisi ya Raisi Jeremy kuja mpaka hapo lakini kwasababu ni swala ambalo lilikuwa linahusiana na Roma hakutaka kuvuka mipaka yake hiyo alijitahidi kuwa makini.
“Hakika una ushawishi mkubwa Raisi Jeremy , kuja London tu umeweza kutupata mara moja?”Aliongea Catherine akionekana kumtania raisi Jeremy, licha ya kwamba hawajawahi kukutana lakini bado alionyesha hali ya kumdharau pengine ni kutokana na kutokea taifa dogo.
“Nimesikia habari za kutosha kuhusu malkia wa Wales lakini sikutegemea kukuona hapa ,nipo hapa kwa ajili ya kikao cha umoja wa mataifa kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa dunia nzima na mara baada ya kusikia habari za binti yangu na mume wake wapo hapa nikaona sio mbaya kuwatembelea”Aliongea huku akiwa na uso uliopambwa na tabasamu.
Maelezo yake yalikuwa kamilifu na ilimfanya kuonekana kama vile alikuwa na ukaribu sana na Roma pamoja na Edna.
Baada ya salamu wengine wote walitoka nje na kumuacha Roma na familia yake ndani ya chumba hicho cha VIP.
“Kama upo hapa kwa ajili ya kunifanya nikutane na mkuu wako wa miliki basi sahau maana sina mpango wa kuonana nae kabisa , kama anataka sana kuonana na mimi basi mwambie aje huku yeye mwenyewe”Aliongea Roma na kufanya tabasamu la raisi Jeremy kupotea mara moja.
“Roma kuna haja ya kuwa hivyo mbele yangu , ninaweza nikawa nilifanya makosa lakini yaliopita si ndwele na isitoshe hatuna vinyongo kati yetu , nilifanya mambo yale kwasababu ya kutaka wewe na Edna kuishi kwa furaha”
Wakati wa kuongea alikuwa akimwangalia Edna kwa sura ya kumwambia amsadie kumuomba mume wake lakini Edna alionekana kumpotezea.
“Usingekuwa hai mpaka sasa kama sio kwa uhusiano uliopo kati yako na Edna , hiyyo acha kuzunguka zunguka na sema kilichokuleta”
“Sawa nitaenda moja kwa moja , mkuu wa miliki ya Panas anataka kuongea na wewe , kama utakataa kwenda katika miliki au kwenda Rwanda yupo tayari kuongea na wewe kwa njjia ya vidio Call , ukikataa kusikiliza utakuja kujutia baadae”
Ijapokuwa ulimwengu wa kijini ulikuwa ukijitegemea lakini majini waliokuwa wakiishi huko walikuwa na uwezo wa kufanya mawasiliano na ulimwengu wa nje bila shida yoyote kutokana na teknolojia ya ajabu ambayo iliasisiwa na mababu wa miliki hizo.
Kuhusu Roma hakushangazwa na maneno yake kwani alikuwa ashajua kiasi kuhusu miliki hizo za kijini hiyo aliamini ilikuwa ikiwezekana.
“Kama ni hiyo niunganishe nitaongea nae"
Raisi Jeremy alijisikia furaha na kujivunia huku akijiambia pengine Roma alikuwa akiogopa miliki ya Panas.
“Nifuate nje tutafute sehemu nzuri kama ni hiyo , kuna watu wengi hapa”
“Hakuna haja , hawa wote ni marafiki zangu na familia yangu hiyyo sio lazima kuficha kitu kwao, labda kama mheshimiwa Jeremy anaogopa kugundulika ana uhusiano na majini?”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la uchokozi.
Baada ya kusikia maneno hayo hakutaka kusita tena na alitoa kishikwambi cha aina yake na alianza kukipangusa na ilionekana Panas walikuwa washajiandaa muda mrefu kupokea simu hio.
Sura ya jini Gefu iliweza kuonekana katika kioo cha kishikwambi hicho na alikuwa ndani ya ofisi yake.
“Sir, Mr Roma Ramoni yupo hapa tayari kwa kuongea na wewe”Aliongea Jeremy kwa sauti ya unyenyekevu huku akiwa amepamba uso wake na tabasamu.
“Sikutegemea kukutana kwetu kwa mara ya kwanza kutakuwa kwa namna hii , Roma hakika ni ngumu sana kukupata”Aliongea Gefu akiwa na tabasamu.
“Oh! Kumbe mkuu wa miliki ya Panas ndio upo hiyyo ..”Aliongea Roma lakini upande wa pili Gefu hakuelewa Roma anachomaanisha.
“Nilikuwa na haja ya kuonana na wewe kwa haraka kwasababu nina jambo muhimu napaswa kukuambia linahusiana na usalama wako na wanaokuzunguka”
“Unajaribu kumaanisha kuna kundi la majini ambao wanataka kuniua muda si mrefu?”
“Ndio , kwasasa ni kama unatembea juu ya barafu nyembamba, lakini sio tu kwmaba najua maadui zako wote lakini pia nipo tayari kukusaidia”
“Haina haja , sijakubaliana kuongea na wewe ili kusikia unaongea upumbavu”
“Nini!!. Roma unamaanisha nini kuongea hivyo au huamini maneno yangu?”
“Sio maswala ya kuaminiana, mimi nilitaka tu kujua mkuu wa miliki ya Panas anaonekana ipi ili nikiivamia miliki yenu nisipate shida ya kukutafuta na kukuua”
Ishara ya hasira iliweza kuonekana katika uso wa Gefu mkuu wa miliki ya Panas lakini fasta sana alirudi katika hali yake.
“Kijana mdogo chunga kauli zako naamini haipaswi kuwa na ugomvi kati yetu”
“Nyie ndio mliovujisha taarifa ya Rufi kuishi Tanzania kwenda kwa miliki ya Xia , hio ni sababu tosha ya mimi kutaka kuivamia miliki yenu na kulipa kisasi kwa umbea wenu”Aliongea Roma bila ya ishara ya utani.
Maneno yake ya kibabe yalimshitua Master Namba nne huku akijiuliza Roma alijuaje yeye ndio alivujisha taarifa.
“Kwa muonekano wenu inaonyesha nilikuwa sahihi , kama ifahamikavyo ukuu wa miliki ya Panas katika kujua kinachoendelea kwenye ulimwengu wa kawaida”
Upande wa Gefu alijua Roma hakuwa na ushihidi hivyo hakutaka kukamatika kizembe na alijua pengine Roma anamjaribu.
“Unathubutu ipi kunijaribu wewe bindamu?”
“Kwahio unatakaje?”
“Unafikiri tunakuogopa , tunakupatia nafasi ya mwisho ya kuungana na Panas, kwasasa umekuwa adui wa miliki ya Xia ,Kekexil na Braki , unadhani kujificha huko nje ya nchi kunaweza kukufanya ukawa salama na miungu wenzako dhaifu kukusaidia?”Aliongea kwa kufoka.
“Braki!!!”
Roma sura ilijikunja mara baada ya kusikia anahusishwa na Braki na kujiuliza Braki ndio kitu gani lakini Gefu alionekana kujua kinachoendelea kupitia sura ya Roma.
“Unajisikiaje kutokujua baadhi ya maadui zako?”
Roma hakujibu swali na badala yake palepale alipiga chini kile kishikwambi na kupasuka pasuka vipande vipande.
“Siogopi kiumbe chochote mimi , kama kuna adui anajiona mbabe anitafute tumalizane”Aliongea Roma na palepale macho yake yalisinyaa wakati wa kmwangalia Jeremy.
“I am not in a good mood , so get lost now when I still give a damn about your relationship with my wife”Aliongea akimaanisha aondoke wakati anajali uhusiano uliopo kati yake na mke wake.
“You .. you are Vexing … kwa ajili ya Edna!?, Roma nataka nikupatie ushauri … sisi binadamu tunao wajibu wa kufuata sheria za hii dunia , kila mtu yupo chini ya sheria na kila mtu atakushambulia kama utazivunja kutokana na ukiburi wako na wakati hayo yanatokea hakuna ambaye atakusaidia”
Baada ya kuongea kauli hio palepale licha ya kuwa na hasira zake aliondoka ndani ya eneo hilo , kwani alijihisi kutamani kumuua Roma ni hivyo tu uwezo huo hakuwa nao.
Mara baada ya kuondoka Roma alisimama na kusogelea dirisha na kuangalia upande wa uwanjani ambako mechi ilikuwa mapumziko , huku hali ya hewa ikiwa sio ya kawaida ndani ya eneo hilo kwani watu wake wa karibu wote walionekana kuwa na wasiwasi.
Bila kujua Roma alikuwa amejiongezea adui mwingine ambaye hamfahamu anaefahamika kwa jina la Braki.
Ukweli ni kwamba alikuwa na maadui wengi ambao hakuwa akiwajua na baadhi yao walitokana na wanawake wake na wengine walikuwa wakimchukulia kama adui kutokana na kuwa na uwezo mkubwa.
“Rufi unajua chochote kuhusu miliki ya Braki?”Aliuliza Roma mara baada ya kujituliza.
“Sijawahi kuisikia , Nanny ushawahi kuisikia?” Rufi alionekana kutokukujua na alimtupia swali Sui lakini hata yeye alionyesha kutokujua chochote.
Ijapokuwa ilikuwa ikihusiana na ulimwengu wa majini lakini kutokana na ukawaida wao hawakuwa wakiijua.
“Mimi nadhani Braki inahusiana na familia ya Mzee Sharif , si ulisema walishawahi kuleta majini wengi kupambana na wewe , nadhani tufikirie hivyo kwa sasa?”Aliongea Rose na Roma alitingisha kichwa baada ya kuona alikuwa na pointi .
“Hubby unataka kweli kwenda kuivamia miliki ya Panas?”Aliuliza Edna ambaye alikuwa amekunja sura.
“Hautaki niende?”
“Nili…”
“Edna siwezi kukusikiliza awamu hii , kila kitu kingekuwa sawa lakini katika vitu ambavyo vinahusisha uhai wa wengine sitokuruhusu ubadilishe mawazo yangu”
Edna mara baada ya kuona usiriasi uliopo katika macho yake alishia kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Sijasema nataka kukuzuia , nikwamba naona itakuwa hatari sana”
“Tatizo hata kama niseme nisiende kuwavamia na kuwasambaratisha najua hawawezi kutulia na watatafuta tu namna ya kutaka kuniua … Hili ni daraja ambalo napaswa kuvuka na nikishapita kila kitu kitakuwa kimekwisha”Aliongea.
“Roma sidhani kama itakuwa ni rahisi, tayari tuna uadui na miliki tatu za kijini kubwa na tuna maadui maelfu na maelfu , unadhani ni sawa kuua na kuendelea kutengeneza maadui? , mimi naona labda hakuna haja ya kuua na tunaweza kutatua haya matatizo kwa njia nyingine , wao wanasheria zao pia na pale wanapojihakikishia kwamba huwezi zivunja hawawezi kukufanyia chochote”Aliongea Sophia.
“Sophia unaongea ujinga , hivi unajua tafsiri ya sheria mbele ya watu wenye nguvu ni tofauti na inavyotafsirika mbele ya watu dhaifu?”
Aliongea Roma na kisha alinyoosha kidole kuelekea uwanjani wakati wachezaji wakitoka katika vyumba ya mapumziko kwa ajili ya kuanza kwa kipindi cha pili.
“Hivi unajua ni kwasababu gani mpira wa miguu ni maarufu sana duniani na kwanini watu wengi kama hivi wanaupenda?”
Wanawake hao wote waliishia kushangaa tu wasiweze kuelewa swali lake,walijiambia wanaongea topiki ya hatari hiyo kuna haja gani ya kuhusisha mpira wa miguu lakini Roma alionekana kutojali mawazo yao.
“Ni kwasababu katika mechi ya mpira haijalishi timu ni bora kiasi gani au ni dhaifu kiasi gani lakini siku zote matokeo yanaanza sifuri kwa sifuri na mpira unachezwa kwa sheria, hii inamaanisha kwamba haijalishi timu ni dhiafu lakini kama watakuwa tayari kupambana katika kukaba kukimbia na kufunga hata wao pia wanaweza kuwa mabingwa , kwa maneno mengine hapo ndio wakati watu ambao sio wachezaji ndio wanajipatia riziki , sehemu ambayo uvumiliu wao huonekana , katika uwanja mshindi ndio bingwa hata kama ni dhaifu au alipendelewa kwa namna yoyote ile ili mradi tu ameifunga timu bora na yenye nguvu hata kama ni mara moja katika historia yake , hii inamaanisha kwamba wao pia wanayo nafasi ya kuwa nyota na hii ndio maana mpira wa miguu ni wa kuvutia sana”Aliongea na kisha akavuta pumzi na kuendelea.
“Lakini unadhani hio ni sawa kati ya wachezaji na wamiliki wa timu au wasimamizi wa mashindano? , ingawa mechi inaanzia sifuri kwa sifuri lakini kwa matajiri na wasimamizi wa UEFA mambo ni tofauti , kwao haijalishi nani anashinda bado watapiga pesa na kupata faida na ipo hivyo siku zote , kwa mfano mchezaji katika timu kama akishindwa kutoa ushirikiano wa maelekezo viongozi wanaweza kuto kumjumuisha katika mechi na kutoa sababu kama vile ni majeruhi au haendani na mfumo na mengineyo .. ,kwa lugha nyepesi ni kwamba wanaoendesha michezo na timu ndio wenye maamuzi ni taarifa gani iwafikie mashabiki na kuamua mchezo uwe vipi , unaweza kuona mechi kabisa hii mshindi ni wa kupangwa lakini wewe kama shabiki utafanya nini tofauti na kuongea ongea na kugoma, hakuna cha ziada ambacho unaweza kufanya kwasababu kwa nje wewe unaburudika na wachezaji wakicheza mpira lakini kwa ndani kuna mfumo ambao umetengenezwa kwa ajili ya kurahisisha maswala mengi aidha yawe ni ya kifedha au Ajenda zao za kijamii labda tu kama watu waache kuangalia mpira .. na huu ni mfumo endelevu na utaendelea hivi labda siku tu watu dunia nzima waseme hawaangalii mpira tena , sasa hili halipo kwenye mpira tu kila michezo maarufu yote wewe kama shabiki utaona ni burudani lakini nyuma ya pazia kuna mfumo..”
“Ndio inaweza kuonekana yanayofanyika ni uchafu lakini maisha ya kibinadamu tokea mwanzo yalianzia katika uchafu , sasa tuseme mimi ni kama mchezaji , Kocha au tuseme timu nyenye nguvu ambayo imepata umaarufu hivi karibuni, viongozi waandamizi na matajiri wote macho yao yatakuwa kwangu kwasababu mbili tu; mosi nifanye kazi kwao na niwasaidie kupata pesa au kutimiza ajenda zao , pili hawataki niwasaidie wengine kupata pesa, kwa maneno mengine ili nipate faida lazima na wao wapate faida na sasa hapa hizi ndio sheria ambazo wameweka ambazo hawataki mchezaji kuzivunja kwasababu zinaathiri utajiri wao pamoja na ushawishi wao”
“Kama nitafanya kazi nzuri kama mchezaji wataniacha niendelee kuishi kama mchezaji na kunifanya niendelee kuwa maarufu na watanipatia Ballon d‘or au Kiatu cha Dhahabu au watafanya hata timu yangu ya taifa kuwa bingwa wa dunia au club yangu kuwa bingwa wa UEFA na kama sitofanya vizuri au nikikataa matakwa yao watahakikisha wananizimisha aidha kwa kuniundia mchezaji uwanjanni ambaye atanijeruhi au kuanza kunitengenezea Zengwe nyingi tu ili kunitoa mchezoni hizi ndio sheria ambazo wameweka .. wakati nikiwa chini hawakuwa na habari na mimi na hawakuwahi kunichukulia siriasi lakini sasa nimekuwa tishio kwao hawataki kuzembea, hii haipo kwenye mpira tu kwa kila nyanja kuna huu mfumo na ambao wanasuka mipango hii ya kimfumo hawatojionyesha kamwe mpaka sekunde ya mwisho , isitoshe lazima wahakikishe mchezo ulikuwa ni wa haki”
Kila mmoja alijikuta akiwa kimya na kuangalia uwanjwani ambako mechi ilikuwa ikiendelea.
Maneno ya Roma yanaweza kuonekana kama yamebase upande mmoja lakini yalikuwa yamejaa ukweli mgumu(Harsh truth).
“Ijapokuwa hatuwezi kushiriki katika vita yako lakini kama mtu ambaye unapambania maisha ninaelewa hisia zako”Aliongea mmoja wapo na kumfanya Roma kuonyesha shukrani na palepale alimbeba Lanlan na kumpakata.
“Sina chaguo nyingine , kwasababu mpaka sasa hawaniangalii kama mtu Dhaifu , kama ninataka kuendelea kuishi ni aidha nishirikiane nao au kama sitaki kushirikiana nao niwaweke chini yangu kwa kuwapiga na kisha kuweka sheria zangu mimi”Aliongea na kisha aligeuza macho yake na kuangalia warembo wake waliokuwa wakimwangalia kwa macho ya matamanio na kisha akageuzia macho kwa Lanlan.
“Sio mimi tu lakini ni kwenu pia na kwa mtoto wangu”Aliongea Roma kwa sauti hafifu akionekana kama vile ni mtu ambaye anakumbukia maisha yake yaliopita na kitendo kile kilimfanya Blandina kukosa ujasiri wa kuendeea kusikiliza na machozi yalimtoka na kwenda kumkumbatia Roma na Lanlan na kuanza kulia.
Kila mmoja alijua hisia za Blandina zinatokea wapi , ilionekana alikuwa na hatia kama mzazi na kumfanya mwanae kupitia magumu mengi lakini kwa wakati huo machozi yake hayakuwakilisha huzuni tu lakini bali kujivunia kwa mafanikio ya mtoto wake.
Ukumbuke hapa ni ndani ya Chumba cha VIP ndani ya uwanja wa Wembley hivyo ni kama wamejitenga na mashabiki wengine.
Unadhani Roma yupo sahihi , ni kweli kuna mifumo ambayo imewekwa kwa ajili ya kushikiria mafanikio ya watu??






SEHEMU YA 736.
Ni upande wa Tanzania jijini Iringa muda wa mchana katika makazi ya Afande Kweka kulikuwa na kikao cha siri kilichokuwa kikiendelea.
Kikao hichi kilikuwa kikijumuisha watu kama saba hivi ambao ni Paster Cohen, Mellisa , Phill Knight , Nadia Alphonso , Suzzane , Linda na mwanamama mrembo kutoka Hungury afahamikae kwa jina la Zoe Kovacic.
Nadia ndio ambaye alikuwa akionekana kusoma ripoti licha ya kwamba kila mmoja ambaye alikuwa hapo ndani alikuwa ameshikilia kishikwambi, ilionekana ni kama vile walikuwa wakirudia kile ambacho Nadia alikuwa akisoma.
“Mzee kama mwanachama mkongwe wa jamii yetu, viongozi wameniagiza nikuelezee kuhusu ubini wa kiongozi wetu”Aliongea Mellisa kwa lugha ya kingereza.
“Kiongozi amekwisha kupatikana?”
“Ndio Komredi katika kikao cha mwisho kilichofanyika Saudi Arabia tumeweza kupata mawasiliano na Kiongozi kwa mara ya pili”Aliongea Pastor Cohen na kumfanya Nadia kuangaliana na Suzzane.
“Kulingana na Kalenda ya jamii yetu kiongozi alipaswa kufanya mawasiliano na viongozi wa juu ndani ya tarehe husika , ijapokuwa ilikuwa ni hatua ya pili ya kumthibitisha kama kiongozi, umoja umefurahi kwamba mpango A wa kalenda ulitimia na kwanzia tarehe hio Edna Adebayo anatambulika kama kiongozi wa Umoja wa Ant-Illuminat”Aliongea Mellisa na kumfanya Linda kuonyesha mshangao huku Afande Kweka yeye macho yake ya kizee yakichanua.
“Komredi ni kama tulivyotarajia”Aliongea Pastor Cohen.
“Kuna maswali mengi juu ya hili Komredi nilijua kiongozi ni Seenteen kulingana na maelezo yako Komred”
“Wote tulidhania kiongozi anakwenda kuwa Seenteen, kuna maswali mengi juu ya hili lakini kulingana na maelekezo ya mwasisi wa umoja wetu anasema Kalenda inakwenda kujibu maswali yote lakini ni Aidha kama Binadamu tutafanikiwa kuishinda vita na Miungu”.
“Viongozi wengi pia hawakuamini kama siku ya kikalenda Edna angefanya mawasiliano na sisi lakini ajabu alifanya hiyo na kila mmoja alishangaa lakini imeondolea umoja harakati za kuona mchoro wa Unabii?”
“Huu mchoro wa Unabii unaonyesha kitu gani , kwanini imekuwa kitu muhimu kwa pande zote mbili Mellisa?”
“Hatuwezi kujua kwa uhakika mchoro huu unamaanisha nini na nani anaonekana katika picha lakini makisio yetu ni kwamba mchoro huu unahusiana na kiongozi wa umoja wetu”
“Kwa taarifa za Shekh Assad ni kwamba mchoro huu pia una umuhimu kwa Illuminat na ndio kiongozi ambaye wanamsubiria, kama usemayo ni sahihi Edna ana uhusiano na huu mchoro wa unabii lakini si inamaanisha kwamba pia ndio kiongozi wao ambaye wanamtarajia kulingana na unabii?”
“Upo sahihi Zoe lakini kwasasa hata Illuminat wenyewe bado hawajaweza kuona mchoro huu wa Unabii kwani upo chini ya Vatican”Alijibu Mellisa.
“Madam kuna uwezekano wa Edna kuwa Seventeen?”Aliuliza Nadia.
“Kulingana na mpango ulivyokuwa , Seventeen ni zao la mpango LADO kama alivyo Roma Ramoni lakini majukumu yao tokea mwanzo yalikuwa ni tofauti , ijapokuwa mpaka sasa hivi hatujui Seventeen yupo hai chini ya Zeros lakini tokea mwanzo Seventeen ndio alikuwa ni msingi wa kufanikiwa kwa Ant-Illuminat”
“Kama ni hivyo kwanini Edna ndio awe kiongozi , sijawahi kuona ishara yoyote ya Edna kujua chochote kuhusu Ant- Illuminat?”Aliongea Suzzane.
“Ukweli ni kwamba tunaamini Seventeen amekwisha kufariki mpaka sasa chini ya maagizo ya Athena na kwa maelezo ya Chriss ili mchoro wa unabii kukidhi vigezo vya ki’unabii hakupaswi kuwa na uwepo wa watu wawili wenye sura zinazofanana”Aliongea Mellisa.
“Melllisa hili linajibu kilichopo kwenye mchoro huo wa Unabii , kama kweli maneno ya Chriss ni sahihi basi kuna uwezekano Mchoro wa Unabii unaonyesha sura ya Edna au Seventeen lakini kwasababu ni unabii wa mtu mmoja basi moja kwa moja mmoja wapo lazima atoweke”
“Naunga hoja ya Komredi lakini kwangu bado swali linaibuka Athena ni nani na kwanini mchoro wa Unabii kuwa na sura ya Edna , wote kati yetu tunajua mpango wa Athena ni nini zidi ya binadamu na hatari ya mipango yake kufanikiwa?”
“Afande mpaka sasa hatuwezi kujibu maswali lakini pia hatuwezi kufanya makisio kwani ipo kalenda ambayo inatuongoza ambayo haijawahi kufeli na hata pale ilipofeli kulikuwa na mpango B, nadhani wote tuamini katika Kalenda”
“Naunga hoja ya Mellisa akini je wakuu wanasemaje kuhusu hali inayoendelea kwa sasa?”Aliuliza Phill.
“Unazungumzia kushuka kwa joto la dunia?”Aliuliza Zoe na kufanya kila mmoja kumwangalia mwenzake kwa shauku kubwa ya kusikia jibu.
“Kulingana na Kalenda tukio muhimu ambalo ndio ishara kubwa ya hatua muhimu ya Athena kuchukua lakini vilevile hatua ambayo Umoja wetu unapaswa kuchukua ni kuona majira ya theluji katika bara la Afrika, nadhani hali hii ya hewa tunaelekea kuona ishara hii hivi karibuni hivyo tunaweza kusema mpaka sasa tunaingia katika hatua muhimu sana katika umoja wetu na kwa dunia kwa ujumla , hiki ndio ambacho viongozi waeniusia nikiseme katika kikao hichi na sio hapa tu dunia nzima vikao vya ajenda hii kwa wenzetu vinaendelea”Aliongea Mellisa.
“Mellisa yupo sahihi kushuka kwa joto la Dunia sio nchi moja bali ni dunia nzima lakini ni Afrika pekee ambayo inaonyesha joto kupungua taratibu sana , hii inamaanisha mpaka nyakati za theluji zikitufikia kuna uwezekano baadhi ya maeneo ya Dunia joto kushuka sana kiasi cha kuathiri maisha ya binadamu”
“Nadhani ndio maana Wanachama wengi wa Freemason na Illuminat wamenunua maneo mengi ndani ya Afrika kwa kipindi cha hivi karibuni huku wakifosi sheria nyingi za kimataifa kupitishwa , hii inaonyesha walikuwa wakiandaa mazingira rafiki kwa ajili ya kuishi wakiwa huru”Aliongea Zoe.
“Hii ni kweli na ni swala ambalo tulikuwa tukipambana nalo kama umoja,kuna baadhi ya mataifa ambayo tumeyachagua kama nguzo muhimu ya Umoja kwa ajili ya kulinda tamaduni zake ikiwemo Tanzania lakini kuna maeneo ambayo pia ndani ya Afrika yapo chini ya Illuminat na ushawishi wao ni wa juu na hili hatuwezi kulifanyia kazi kwani litaibua migororo”
“Nadhani naona unachojaribu kumaanisha Miss Mellisa , ni miezi kadhaa iliopita mataifa zaidi ya kumi ya Kiafrika yamepitisha sheria ya Ushoga kuwa huru hili ni swala ambalo linahusiana na ulichosema”
“Upo sahihi Linda , Tanzania ilikuwa ni nchi ambayo ingekuwa ya kumi na moja kutangaza hii sheria kama sio sisi kuingilia , shukrani kwa Suzzane na Nadia wameweza kutiisha misheni yao vizuri na sasa Tanzania imekuwa Neutral kwa sisi pamoja na wao”
“Urusi wanazungumziaje hili?”Aliuliza Afande Kweka.
“Wapo ndani ya mfumo , wanaweza kupinga wazi lakini ni taifa ambalo limegawanyika katika pande mbili”.
*******
Pumbavu zako Roma Ramoni , nitakuua tu siku moja”Aliongea Gefu kwa sauti kubwa na kwa hasira zake alipelekea kuharibu kila kitu kilichokuwa ndani ya ofisi yake lakini bado haikuwa ikitosha kutuliza hasira zake.
Mbele yake alikuwa ni Master Namba nne na mwingine mmoja ambao wote walikuwa katika hali ya wasiwasi kutokana na hasira za kiongozi wao mara baada ya kumaliza maongezi yake na Roma Ramoni.
Ilikuwa ni mara chache sana kwa Gefu kuwa katika hasira kama hizo , kitendo cha Roma kumdharau waziwazi mara nyingi mfululizo kilimfanya chuki yake kuongezeka maradufu.
“Kaka punguza jazba, ni sawa tu kama amekataa kuungana na sisi na kwasababu maadui zake ni pamoja na Braki lazima atakufa na sisi ndio tutachukua fursa hio ya kummalizia akiwa chini kabisa”
“Hawa majini kutoka Braki hawajawahi kuwepo katika uso wa dunia kwa zaidi ya milenia moja , nimesikia kutoka kwa wazee wanasema hawajui kabisa uwepo wa binadamu mwenye uwezo mkubwa kama Roma , Roma huyu mjinga amejitengenezea uadui na hawa mashetani ambao walikuwa wameshasahaulika”
“Namba nne fanya mawasiliano na Jeremy kusitisha mipango yetu yote ya kimsaada na Tanzania hususani familia ya Raisi Senga na kisha atasubiria maelekezo yangu ya mpango wa pili unaofuatia , pia tuma barua kwenda katika miliki zote zenye uadui na Roma hususani katika miliki ya Xia na Kekexil na waambie kupitia mashushusu wetu waliopo katika kila pande ya dunia ya kawaida watasaidia kujua nchi ambayo Roma anaishi na familia yake na kama wanahitaji msaada watuambie”
“Sawa kaka”Aliongea Master namba nne.
“Gegu chukua baadhi ya wazee kuelekea mlima Yoshe na mrudishe yule mtu kurudi Panas”
“Kaka namba moja sio kwamba ni mapema sana kumrudisha?”
“Fanya kama nilivyosema , vipi kama Roma akitushambulia unadhani nitaweza kuilinda miliki mwenyewe?”
“Umeeleweka bro”
Lakini sasa muda huo huo sura zao zilibadiika mara baada ya kuhisi kitu ambacho sio cha kawaida na Gefu ndio aliekuwa wa kwanza kupotea ndani ya ofisi hio na kuja kuibukia nje na kufuatiwa na wengine.
Wingu jeusi lilikuwa limejikusanya katika upande wa Kusini mwa eneo la miliki ya Panas , ngurumo na mwanga wa Radi vilikuwa vikisikika na kuonekana.
Sauti za ngurumo za radi zilikuwa kubwa kama vile anga linataka kuondoka chini.
Majini wengi wa miliki hio walikuwa nje wakiangalia hali hio ya kustaajabisha ambayo ni adimu sana kuonekana katika miliki za majini.
“Hii nii…”Jini mmoja ambaye alikuwa katike levo ya maji ya barafu aliongea.
“Hahaha…. tayari amekwisha kuipita levo ya maji ya kiroho , hii ni radi ya mapigo tisa ya adhabu ya anga”Aliongea mkuu wa miliki ya Panas kwa furaha.
“Hakika inashangaza ni juzi tu hapa Anjiu wa Xia ameweza kupita levo hii na leo ni zamu ya Rozu”
“Huu ni wakati wa kuwa na majini wa levo za juu katika ulimwengu wetu,ni heshima kwetu kuangalia kitu kama hichi kikubwa”Aliongea na kufanya wazee pamoja na majini wa miliki hio kuonyesha furaha zao.
“Kimya!!, huu ni mwanzo tu lakini hatuna uhakika kama ataweza kuvumilia mapigo hata matatu ya radi ya rangi ya Zambarau”
Baada ya kusikia kauli hio kila mmoja alipiga kimya kwani ni kweli radi hio haikuwa imeshuka bado na walikuwa na wasiwasi kwamba wanaweza kumpoteza mtu wao.
Majini wanaweza kupitia radi lakini sio wote ambao wanaweza kuihimili kwani ilikuwa na nguvu kubwa kwani dhumuni la kushuka kwake sio kwa ajili ya kunufaisha jini bali ni kwa ajili ya kutoa Adhabu kwa kukiuka sheria za anga.
Dakika chache mbele radi hio ilianza kuonyesha ghadhabu yake na boriti ya radi iliokuwa katika rangi ya Zambarau na bluu ilionekana ikishuka kama vile ni nyoka na kwenda kupiga katika sehemu ambayo yupo jini aliefahamika kwa jina la Rozu.
Ilikuwa ni sauti ya kuumiza masikio ya mwangwi ndio iliweza kusikika na kuwafanya majini kuogopa na kuwafanya wengine kukimbia
“Hii inatisha , sidhani kama Rozu ana Dhana ambayo inaweza kumkinga,atakuwa na uwezo wa kupita hii Adhabu bila kifo kweli?”
“Ni ngumu kusema na hatuwezi hata kusogelea eneo alipo kwasasa bila ya kupoteza nafsi zetu , hata mimi sijui kama ataweza kweli kuhimili?”.
Kila mmoja alikuwa akijiuliza swali linalofanana na kuna ambao walikuwa wakijutia kwa Rozu kukasirisha anga mpaka kupatwa na radi hio.
Dakika chache mbele radi ya pili ilipiga na ilikuwa kubwa kuliko ya mwanzo kiasi cha kutengeneza shimo na ndani ya dakika chache mara baada ya kufifia kitu kinachofanana na Dhahabu kilionekana katka lile eneo.
Kuna ambao waliweza kuona kitu hicho lakini hawakuweza kujua ni kitu gani lakini wakuu wa miliki hio walikuwa na uwezo wa kuhisia Rozu alikuwa hai bado kutokana na msisimko aliokuwa akidhalisha.
Hali hio iliwafanya wazee kujiuliza amewezaje kutoathirika katika mapigo hayo ya radi.
Radi ya tatu iliweza kupiga kwa awau nyingine na ilikuwa na nguvu kubwa zaidi lakini hata hivyo kile kitu ambacho kilikuwa katika muonekano wa Dhahabu bado kilikuwa kikionekana katika eneo lile.
Radi ile ilionekana haikuwa na mpango wa kuendeleza mapigo kwani mara baada ya mapigo matatu wingu lilianza kutawanyika na palepale shimo kubwa lilionekana kwa macho.
“Rozuu..!!!”
Mkuu wa miliki ndio aliekuwa wa kwanza kuita jina hilo lakini kufumba na kufumbua palepale alionekana mwanamke jini ambaye ameshikilia upinde wa Dhahabu akisogelea mbele ya kila mmoja akitokea eneo lile
Nywele zake ndefu zilikuwa hazijafungwa na zilisambaa kulingana na upepo ulivyokuwa ukivuma lakini licha ya hivyo hazikuweza kuficha uzuri wake wa ajabu na macho yake angavu , alikuwa mrembo haswa kwanzia ngozi , umbo la uso na kila kitu.
Alikuwa na muonekano wa ajabu kidogo mzungu sio mzungu , alikuwa ni kama vile ni mfilipino.
Ijapokuwa hakuwa na mavazi ya kirembo kama wanawake wa kidunia lakini upole wake pamoja na uwezo wake ulimfanya kuzidi kupendeza na kuwa ni mwenye kutamanika.
Huyu mwanamke alikuwa akifanana kwa kila kitu na mrembo ambae Hermes mjumbe wa miungu alikuwa akiongea nae katika kilele cha mlima kilimanjaro muda kadhaa mara baada ya Roma kumuokoa Edna katika mikono ya Vampire waliokuwa wakitafuta mshipi feki.
Ki ufupi ni kwamba ni huyu mwanamke bila shaka na haikueleweka ilikuwaje akawa katika jamii ya majini wa miliki ya Panas lakini ndio hivyo alionekana kupitia levo ya mapigo matatu ya radi ya mbingu na jina lake alikuwa akifahamika kwa jina la Rozu.
Ijapokwa Rozu hakuwa ameonyesha uwezo wake wote lakini kwa majini hao walijua alikuwa ni wa levo za juu sana , pengine alikuwa akilingaina ki uwezo na Jini Anjiu wa miliki ya Panas au kumpita.
“Hongera sana , kwasasa upo na uwezo mkubwa wa nguvu za kijini na hakuna ambaye anaweza kukushinda katika ulimwengu wa majini watu”Aliongea Master namba nne huku ile hofu yake ya kumhofia Roma na Anjiu ikiwa imetoweka kabisa , alijua kwa uwezo aliokuwa nao Rozu anapaswa kuwa na amani.
“Hongera sana , nilikuwa na wasiwasi muda si mrefu lakini kwa bahati nzuri umeweza kufanikiwa kupitia mapigo ya radi”Aliongea Mkuu wa miliki hio huku akijiuliza kimoyo moyo.
“Imekuwaje akapitia mapigo hayo ya dhiki ya radi kirahisi hivyo , anaonekana hajapatwa na majeraha ya aina yoyote yale”Aliwaza.
Ukweli ni kwamba kuna namna majini hao walikuwa wakimjua Rozu kama Rozu jini mwenzao lakini hawakumjua Rozu kama sehemu ya miungu , kitendo cha Rozu kuongea na Hermes juu ya mlima kilimanjaro ilimaanisha kwamba ni sehemu ya miungu lakini jina lake halifahamiki ni lipi katika miungu yote iliobaki ambayo hatujawaona wahusika wake.
“Kama hizi ni pongezi za dhati basi sina budi ya kuzipokea”Aliongea mwanadada mrembo Rozu huku akimwangalia Gefu kwa macho makali kidogo kiasi cha kumfanya Mkuu wa miliki hio kuwa na wasiwasi lakini alijitahidi kuonyesha tabasamu.
“Unapenda sana utani , sina haja ya kumuonea wivu mdogo wangu wa kike mafanikio yake , leo ni siku ya kusherehekea, uwepo wako unatufanya tusimhofie tena jini Anjiu”Aliongea.
Ukweli ni kwamba Rozu na Anjiu kidogo walikuwa na tofauti , wakati wa Anjiu anapokea mapigo ya radi chungu cha Roma ndio ambacho kilimkinga lakini kwa jini Rozu yeye ilikuwa tofauti kwa maana kwamba mapigo yote ya radi yalimfikia.
Majini wote walikuwa kwenye shangwe wakimzunguka Rozu na kumpa pongezi za dhati kabisa kwa kupigi hatua hio Adhimu.
Kuipita Dhiki ya radi ni hatua kubwa sana katika ulimwengu wa majini ndio maana.
Rozu mara baada ya kuweka upinde wake wa Dhahabu katika hifadhi ya pete alivuta pumzi nyingi na kisha kutoa tabasamu.
“Anjiu huna uwezo tena wa kunizidi, Hades namsapoti Athena na mipango yake na nataka nione ikifanikiwa”Aliwaza.
Haya sasa kuna kiumbe kingine katika miliki ya Panas , unadhani huyu jina lake halisi ni lipi kati ya miungu kumi na mbili ya mlima Olympus kutoka sayari ya Mars.
Hades A.k. a Roma Ramoni atamuweza kweli?.




SEHEMU YA 737.
Upande wa Roma mara baada ya mechi kumalizika hakuna ambaye alitamani kuangalia ugawaji wa makombe na medali hivyo walirudi moja kwa moja kwenye boti yao ya kifahari.
Upande wa Raisi Jeremy hakuwasumbua tena kwani alikuwa ndani ya Uingereza kwa ajili ya kikao cha Umoja wa mataifa kinachohusu mabadiliko ya hali ya hewa na hata Raisi Senga alikuwa ni moja ya viongozi ambao walihudhuria kikao hicho muhimu.
Kilikuwa ni kikao muhimu kutokana na mabadiliko ya ghafla ya hali ya hewa ya joto la dunia kuporomoka na kusababisha baridi kali licha ya kwamba katika maeneo mbalimbali ya dunia ilipaswa kuwa majira ya joto.
Ukiachana na wakuu wa mataifa lakini pia wanasayansi wengi na watu wa maswala ya kimazingira walikuwa wakihudhuria kikao hicho ili kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo mara baada ya kujua chanzo.
Clark ni moja ya wanasayansi muhimu kabisa ambao walialikwa katika kikao hicho muhimu lakini licha ya hivyo hakukuwa na maelezo ya moja kwa moja ambayo angeongea kwani ni swala ambalo bado hakuwa amelifanyia utafiti.
Roma mara baada ya kuingia katika boti ndio maandalizi ya kurudi katika visiwa vya wafu yalianza rasmi lakini ndio muda ambao aliweza kupokea simu kutoka kwa Afande Kweka.
“Wewe mtukutu hivi utaacha lini kuwa na huo ukiburi?”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kuishia kushangaa.
“Ongea vizuri mzee basi”
“Kwanini umekataa kuongea na wajumbe wa Hongmeng ?, angalau hebu ongea nao maana kwasababu yako kila saa wapo ndani ya makazi yetu, unafikiri nadili nao vipi viumbe wa ajabu kama hawa?”
“Unamaanisha huyo Xuan Jizi yupo ndani ya makazi yako?”Aliuliza Roma huku hasira zikianza kumvaa maana aliona ni kama usumbufu.
“Anaonekana kuwa na hasira sana na amesema kama hutorudi mapema anaenda kutoa taarifa Hongmeng , hebu rudi udili na hii hali nishazeeka sitaki kuingizwa kwenye matatizo ya namna hii mimi”Aliongea na palepale alikata simu ikionyesha dhahiri alikuwa amekasirika.
Roma aliweka simu yake mfukoni na kisha aliwasogelea wanawake wake na kuwaambia juu ya hali inayoendelea nchini Tanzania hivyo anapanga kuondoka.
Kwasababu walikuwa ni waelewa hawakumzuia Roma na dakika hio hio alianza safari kurejea nchini Tanzania.
Ulaya na Tanzania masaa yalipishana kidogo sana hivyo Roma alifika wakati wa usiku pia ndani ya jiji la Iringa na wakati wa kutua tu aliweza kuona kuna wageni wamekaa katika sebule ya wageni ndani ya nyumba hio , walikuwa wawili na wote ni Wachina.
Moja kati yao alikuwa akimjua na mwingine hakuwa akimjua lakini alionekana kuwa handsome mno , ilikuwa ni kama vile sio mchina na alikuwa katike levo ya maji ya kawaida.
“Naona Mjumbe umeimarika kuliko mara ya mwisho tulivyoonana”Aliongea Roma akimlenga mjumbe wa Hongmeng mpenda rushwa.
“Haha… sipo hapa kwa ajili ya kukumbushia namna tulivyoonana mara ya mwisho nimemleta balozi”Aliongea na kisha alimpa ishara balozi Xuan Jizi.
“Wewe ndio Roma Ramoni ulietibua hali ya hewa katika miliki ya Kekexil na Xia?”Aliuliza yule bwana bila hata ya salamu , alionekana kuwa na hali ya ujeuri hivi.
“Ndio umekuja kote huku kwa ajili ya kuuliza ujinga?”
“Acha maneno yako makali , hivi unajua upo kwenye matatizo?”
“Nielimishe”
“Nikuelimishe nini? , unadhani kuna hata haja ya kufanya hivyo , unajua mwenyewe namna ambavyo umekasirisha majini kutoka miliki ya Xia na Kekexil , ukaenda mbali na kuchokoza miliki ya Braki , nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif , unaonekana kabisa unaogopa ndio maana ukaikimbiza familia yako nje ya nchi”
“Umongea sana lakini sijui kilichokuleta ni nini?”
“Nipo hapa kwa ajili ya kupitisha maagizo niliopewa na wakuu wa miliki ya Hongmeng, wasimamizi wakuu wa sheria ya the gods treaty , ili kuongezea nguvu utulivu wa dunia na kukuzuia kupigana na miliki za kijini na kusumbua raia , Hongmeng kwasasa itakuwa ndio kimbilio lako licha ya kwamba kutakuwa na mashariti, ukikukubali hakuna miliki yoyote ambayo itakugusa”
“Roma usishangilie bado kuna masharti”Aliongea yule mjumbe na Xuan jizi aliendeea.
“Umekiuka sheria nyingi sana na kutumia uwezo wako vibaya na kuua wajumbe ambao waliagizwa kuja duniani kutimiza majukumu yao , lakini licha ya hivyo Hongmeng hawataki kulipiza kisasi na wameaua kukusamehe ili mradi tu kwa hiari yako utoe mbinu yako ya mafunzo , vidonge na Dhana ya Chaos cauldron na baada ya hapo sisi tutakupatia ulinzi”Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Roma kuangua kicheko.
“Unacheka nini?”
“Wewe Mzee Jizi, lazima kwenye kwenye kichwa chako kuna nati zimechomoka au hao Hongmeng hawajui nini kinaendeea , nadhani napaswa kuwafafanulia kwa sentensi rahisi”
“Acha kunitukana … tunazo taarifa umeiba hazina yote ya Kekexil na Xia na unazo Dhana na vidonge kedekede , hivi unadhani vitu vya thamani kama hivyo utaweza kuvilinda peke yako, hivyo acha ukiburi na sikiliza tunachokuambia”
“Vipi kama nikikataa mtanifanya nin?”
“Roma acha kujifanyisha kijogoo , sekunde ambayo nitakuripoti katika miliki ya Hongmeng basi ndio utakuwa mwisho wako kwani utakuwa ni adui namba moja wa Hongmeng”
Roma aliwaza na kujiambia tokea siku anajua uwepo wa Hongmeng ndio uadui wao ulipoanzia hivyo hana mpango wa kuwasikiliza kwa chochote , kwanza kabisa alikuwa na deni kwa Zenzhei kumsaidia kulipa kisasi na tokea siku waagane ni kama Zenzhei katika ulimwengu huo wa kijini alikuwa akimsubiria.
Roma bila ya kujiuliza mara mbili mbili aliita nguvu ya Cauldon bila ya kukitoa nje na kuingiza katika mwili wa Xuan Jizi na kuanza kunyonya nguvu zake za kijini na nguvu ya Cauldron ilikuwa kubwa mno na ndani ya dakika chache tu alikuwa ashapoteza uwezo wake wote na kubakia binadamu wa kawaida.
Xuan Jizi hakuwa jini kama jini wa Hongmeng , alikuwa ni binadamu tu ambaye alikuwa na mafunzo ya kijini hivyo ilikuwa rahisi kwa Roma kudili nae kwani alikuwa ndio kwanza yupo katika levo ya maji ya kawaida.
Hakuna ambaye alitegemea Roma kuchukua maamuzi kama yale , lakini kwa Roma alitaka kuonekana kuwa siriasi na kutangaza vita vyake rasmi na Hongmeng kabisa na ili kuonekana yupo siriasi alitaka kwanza kumuadabisha balozi wao.
Mjumbe wa Hongmeng aliebakia ndio alipewa jukumu la kurudi Hongmeng na kutoa taarifa ya kile kilichotokea,
“Rudi ujinini na toa taarifa hizi , kama hao majini wanataka Dhana zangu , vidonge vyangu na mbinu yangu ya mafunzo basi waje huku nilipo wavichukue kwa nguvu kama nilivyofanya katika miliki ya Kekexil,likija swala la watu wenye nguvu kama haina haja ya kutii sheria za ulimwengu bali sheria ya msituni ndio itumike , atakae weza kuishi mpaka mwisho huyo ndio mtawala”
Baada ya kusema hivyo Roma alimbeba mzobemzobe yule Xuan Jizi na kisha kumtupia mbele ya walinzi akiwaagiza kwenda kumtupia mtaani huko kwani ashakua ni wa kawaida.
Alijua asingeweza tena kurudi Hongmeng kwani miliki hio haichukui majini wadhaifu kama yeye.
“Vipi kila kitu kimemalizika?”Aliuliza Afande Kweka mara baada ya Roma kuingia katika sebule ya kawaida na Roma aliishia kutingisha kichwa tu akiitikia amemaliza.
“Unajisababisha matatizo zaidi na zaidi juka uchao kulikuwa na haja gani ya kumuondolea nguvu zake za kijini?”Aliongea Afande Kweka bila ya kubadilisha muonekano wake , yaani hakuwa na furaha wala hakuwa na huzuni na hata usingizi hakuwa nao licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda.
“Babu hicho ndio kitu pekee ambacho unaweza kuongea”
“Unadhani ni kipi ambacho naweza kuongea , mwenyewe nipo najiuliza mambo ambayo yanaendelea katika hii dunia, nina hasira nyanya zangu zote zimekauka kutokana na baridi kali , hii baridi sijawahi kuiona na uzee wangu huu”Aliongea na kumfanya Roma amuone huyu mzee anaonekana kuficha mambo mengi na kila anachoongea ni kama anamwigizia lakini hakutaka kumhoji sana.
Huo ndio ulikuwa ukweli ugomvi wa Roma na majini ulikuwa ni wa kutisha lakini ulikuwa haukwepeki lakini kubwa zaidi ni kwamba Mzee huyo alitamani sana Roma kwenda kuwashambulia Hongmeng ili kulipa fadhila za Zenzhei kwa kumlinda kwa miaka mingi, ukiachana na hilo lakini pia Afande Kweka ni mwanachama wa umoja wa Ant- illuminat na ni juzi tu hapo alikuwa na kikao cha siri na baadhi ya wanachama na alikuwa akijua Edna ndio mkuu wake.
Yani kwa lugha nyepesi ni kwamba Edna ni mkuu mbele ya Afande Kweka lakinin mzee huyo licha ya kujua hayo yote hakuwa tayari kumwambia Roma kwani alijua itafikia siku yeye mwenyewe atakuja kujua ukweli na hata hivyo sheria za umoja huo hazikumpa ruhusa ya kuongea chochote kwani ingeharibu kabisa mipango inayoendelea.
“Babu nadhanni baada ya Hongmeng kupokea ujumbe wangu sitoweza kuendelea kuishi hapa Tanzania kwa muda , unaonaje na wewe ukielekea visiwani kwa muda , unaweza kuondoka na baadhi ya watu wako wa karibu pia”
“Unataka nitoke hapa Tanzania kwenda wapi na kwanini?”
“Si kila kitu kipo wazi mzee , sitaki waje wakukamate na kutaka kunitishia uhai wako kama chambo cha kunikamata”
“Mimi nipo nje ya maswala yote ambayo yanahusiana na maadui zako na sio kwangu tu hata kwa baba yako , kinachoendelea ni vita kati yako na majini na hayahusiani na ukoo wetu hivyo pambana kivyako”
“Unaongea tu lakini wanaweza wakapania sana na kutumia njia yoyote ile”
“Hata iweje nasema hapa siondoki “Aliongea kibishi.
“Kwannini sasa , huu sio muda wa kuonekana shujaa mzee”
“Mimi ni mzee wa taifa hili lakini pia mkuu wa familia ya Kweka , siwezi kuondoka na kwenda mahali pengine nje ya Tanzania, unaweza kutafuta chumba ulale , muda umeenda naenda kupumzika”Aliongea na kisha aligeuza na kuingia chumbani kwake.
Roma alikuwa na usingizi na wakati akiwaza kwenda katika chumba cha wageni kwa ajili ya kulala simu yake ilianza kuita mlio wa kuingia meseji na alipoangalia ilikuwa imetokea kwa Tannya.
“Master kuna kundi la majini wamefika na wanakuulizia hapa Bagamoyo”Ujumbe wa meseji ulisomeka hivyo.
“Naona hatimae wamejitokeza licha ya kwamba ni kwa kuchelewa kama nilivyotegemea lakini ni bora wamekuja kabla sijarejea katika ulimwengu wa majini watu”Aliwaza Roma
Sasa mara baada ya Roma kuona kwamba nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya mzee Sharif imejitokeza hakutaka kupoteza muda kabisa na shauku ya kutaka kujua Braki ni majini wa namna gani ilimvaa.
Roma mara baada ya kuondoka ndani ya eneo la Iringa dakika chache tu aliweza kufika mkoa wa Pwani katika makazi ya Sharif na aliweza kumuona Tannya akiwa amesima katikati ya ukumbi wa mikutano , ilikuwa ni eneo ambao hutumika kupokelea wageni mara nyingi.
Mbele yake kulikuwa na wanachama wa familia ya Sharif na mara baada ya kuwachunguza kwa umakini Roma aligundua hawakuwa wa kawaida wote walionekana kama waarabu hivi na hajawahi kuwaoana na walikuwa na nguvu za kijini.
Tannya tokea muda tu alikuwa amebadilisha wafanyakazi wote wa Sharif na kuweka wa kwake , ijapokuwa alikuwa mjapani lakini alikuwa mjuzi sana katika kuigiza na tokea siku ambayo amefika na kujifanyisha ni Maimuna hakuwahi kuonyesha dosari yoyote na hata ibada alikuwa akiongoza.
Roma kwa kutumia jani lake la upofu aliishia kujificha juu ya jengo hilo huku akihakikisha anasikia kinachoendelea kwa kutumia uwezo wake na majini hao hakuna hata mmoja ambaye aliweza kugundua uwepo wake.
Kulikuwa na majini jumla saba, wote walikuwa wamevalia kanzu kwa upande wa wanaume na wanawake wenyewe walikuwa wamevalia Abaya nyeusi , karibia wote walikuwa na muonekano wa ki utu uzima.
Kati yao mmoja tu ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa mafunzo ya kijini kwani alikuwa mwanzoni mwa maji ya kiroho. Na wengine wote walikuwa katika levo za maji ya barafu kushuka mpaka moto wa njano.
“Wewe ndio kiongozi wa familia ya Sharif katika ulimwengu huu unaefahamika kwa jina la Maimuna si ndio?”Mwanaume ambaye alikuwa na muonekano wa kizee alimuuliza Tannya , alikuwa na nywele nyeupe na ndevu nyeupe kama vile ni Nandra Modi waziri mkuu wa India na ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa kijini.
“Ndio , kwasasa mimi ndio nililazimika kuwa kiongozi , hivyo sina uhakika namna ya kuwaita kwani siwafahamu”Aliongea Tannya aliekuwa katika sura ya Maimuna.
“Hakuna shida kwani hata babu yako Sharif hana uwezo wa kututambua,kwa majina nafahamika kama Zando , nikiwa mwanachama kutoka makao makuu ya miliki , hapa kuna mzee Nuli na Yejini pamoja na majini wanne unao waona , tumekuja hapa kujua ni kipi kinachoendelea kwasababu hatukuweza kusikia habari zozote kuhusu mwizi alieiba hazina yetu , taarifa za kubadilika kwa kiongozi wa familia na imani ni zaidi ya matarajio yetu”












SEHEMU YA 739.
Katika moyo wake Tannya ukweli hakuwa akijua namna ya kujibu, ijapokuwa alikuwa akijua muda kama huo ungewadia lakini ndio mara yake ya kwanza kukutana na majini wa namna hio na angalau ni kwamba alikuwa tayari ashamtumia Roma ujumbe wa meseji.
Tannya simu yake ilitoa mnguruo mara baada ya kutaka kujibu na mara baada ya kuangalia aliona Roma alikuwa ametuma ujumbe kwa lugha ya kijapani.
“Tafuta njia yoyote upate taarifa zinazohusiana na wanakotokea na historia yao kwa ujumla”Aliongea Roma katika ujumbe huo.
Roma alitumia kijapani kwa kuamini ingekuwa ngumu kwao kuelewa kile alichokuwa ameandika.
Tannya mara baada ya kujua Roma ashafika hali ya kujiamini iliongezeka kidogo na palepale aliomba radhi
“Naombeni mniwie radhi wakubwa zangu, nilitamani pia kutoa taarifa kuja makao makuu lakini kwa bahati mbaya babu , walinzi na wengine walikufa vifo vya haraka sana na sikujua namna ya kuwasiliana na nyie hivyo…”
“Haina haja ya kujilaumu , hata sisi pia tunaelewa namna ilivyo ngumu kuwasiliana na sisi , umefanikisha kuongoza familia ndani ya muda mfupi na kuendeleza ibada taarifa hizi zikimfikia mkuu wetu atafurahi”Aliongea.
“Tafadhari naomba mniwie radhi kama nitavuka mpaka , lakini je mnaweza kunielezea historia yote ya familia pamoja na imani yake , ili mimi Maimuna niweze kuwa na uelewa mzuri na kufanya vizuri kwa ajili ya manufaa ya miliki kwa ujumla”
“Kwasababu umekuwa kiongozi pekee uliebakia basi ki asili umekidhi vigezo vya kujua historia yote ya Kibraki , Babu yako Sharif ana uelewa mdogo sana kuhusu jamii ya majini wa Braki pengine amewahi kusikia hili jina mara moja au mara mbili tu , lakini kutokana na mabadiliko ya hali na matukio ya kutotarajia hapa duniani makao makuu wameona ni sahihi familia za binadamu zinazotuwakilisha hapa duniani kujua uhalisia wa historia yetu na imani yote kwa ujumla, hivyo nitakuelezea kila kitu”
Roma ambaye alikuwa akipiga chabo alijikuta akifurahi mara baada ya kusikia kauli hio kwani hakutegemea jini aliefahamika kwa jina la Zando angeweka wazi kuhusu nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif.
*****
Miaka elfu hamsini iliopita dunia iliingia katika hatua nyingine kubwa katika ustaarabu.
Wakati huu pia upande wa majini walikuwepo pia na wengi wao walikuwa katika levo za juu sana pengine levo ambayo haijawahi kufikiwa katika nyakati za sasa.
Kipindi hiki ni kabla ya miungu kufika katika sayari ya Dunia na ndio kipindi ambacho majini wengi walianza kupotea katika uso wa dunia na kuwaacha binadamu na baadhi ya majini watu.
Majini ni vumbe ambavyo vipo vya aina nyingi sana na tabia tofauti , ni kama ilivyo kwa makabila ya kibinadamu basi ndio ilivyo kwa majini hivyo hivyo.
Sasa kati ya majini wa enzi hizo ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uso wa dunia ni majini pepo na hawa majini pepo wenyewe walikuwa wamegawanyika katika aina nyingi sana.
Inasemekana katika kipindi hichi majini walikuwa wengi kuliko hata idadi ya binadamu kutokana na spidi yao ya kuzaliana.
Kati ya majini pepo ambao waliweza kufahamika enzi hizo ni kama vile Mbweha na Majoka ambao ndio walikuwa na uwezo mkubwa sana .
Majinii jamii ya Mbweha walikuwa ndio wenye busara kubwa na mbinu nyingi za kimaajabu tofauti hata na majini Joka ambao walikuwa wamezaliwa na nguvu za kimwili sana sana.
Ukiachana na majini hao lakini pia majini watu hawakuwa nyuma pia kwani wengi wao walikuwa katika levo za juu kwa kuweza hata kudhibiti radi na ilikuwa ni kawaida kwa majini watu kuweza kumiliki Dhana za hali ya juu kabisa na shida ilikuwa tu kwamba licha ya uwezo wao hawakuweza kupata mbinu ambayo inaweza kuwainua zaidi na zaidi.
Hawa majini watu ndio ambao walipenda kuwa wa wazi kabisa na waliweza kuishi katikati ya binadamu wa kawaida tofauti na majini pepo ambao walikuwa ni hatari kabisa kwa binadamu.
Majini pepo waliishi katika maumbo yao ya kawaida pasipo ya kubadilika na ukweli ni kwamba walikuwa wakitisha sana na hali hio ki ufupi ni kwamba hawakuipenda na hii iliongeza chuki yao zidi ya binadamu na majini watu.
Lakini mwishowe walijitahidi kutafuta namna ya kuboresha muonekano wao ndipo walipokuja kugundua mbinu mbadala ambayo ilikuwa ni kuamsha pepo wao wa ndani tofauti na kuwazimisha au kuwakata kama ilivyokuwa kwa majiini watu ,hapo sasa ndio ikazaliwa majini halisi ambao walikuwa na nguvu za kijini, majini ambao walikuwa na uwezo wa kupaa.
Sasa kutokana na kuwa na maumbo yenye nguvu kubwa pamoja na kumiliki nguvu za kijini pamoja na kuwa wengi walikuja kuwa tishio kubwa kwa jamii nyingine za kijini na binadamu wa kawaida kiasi cha kupelekea kuibuka kwa vita ambayo majini watu waliungana na binadau kuwashambulia Majoka.
Sasa kati ya majini pepo wakaja kuibuka jamii nyingine kati ambao walijiita mashetani pepo wa anga , hawa ndio walikuwa wabaya zaidi kwani walikuwa na uwezo wa kumuingia binadamu na kumfanya afanye kila anachotaka huku wale majini pepo wengine wakichinja binadamu na kunywa damu yao.
Binadamu alionekana kuingia katika hatari na kuanza vita na viumbe hawa majini ,vita ambayo ilidumu kwa muda mrefu sana takribani miaka mia moja na siku moja tu ilitokea majini pepo wengi katika ulimwengu wa kawaida kuanza kupotea ikiwemo Mbweha na Majoka.
Kupotea kwao baadae ilikuja kujulikana walikuwa wakivutwa katika ulimwengu mwingine kwa kutumia aina ya mitego ambayo ilikuwa imewekwa mfano wa mnara ambao Roma aliingia.
Ni asilimia chache tu ya majini pepo ambao walibakia na kati yao hawakuwa hata na uwezo mkubwa na hapo ndipo majini watu wa enzi hizo walipoona hakuna haja ya kuwaua bali kwenda kuwafungia katika ulimwengu Tenganifu wa jangwa.
Kitendo cha mashetani pepo wa anga, Majoka na Mbweha kufungiwa katika ulimwengu wa Jangwa Tenganifu kwa muda mrefu iliwafanya kuchukulia hapo kama makazi yao rasmi.
Mara baada ya kuwasili kwa miungu katika uso wa dunia ndipo ilipoibuka vita kati ya majini watu yaani Hongmeng na jamii nyingine za kijini , vita ambayo ilidumu muda mrefu sana mpaka Zeus na Athena kushindwa vita na kuzaliwa kwa the Gods treaty.
Mpaka vita hio inakuja kufikia mwisho majini pepo ambao walikuwa katika ulimwengu wa jangwa tenganifu walikuja kugundua miliki za majini watu walikuwa wamepungukiwa nguvu sana kutokana na kupigana vita na miungu na wengi wao kuuliwa na hapo ndipo walipoona ni fursa adhimu ya kujiendeleza wao wenyewe kutokana na kipindi hicho majini watu kutokuwa nao makinu.
Mbinu pekee ambayo iliwafanikisha kujiendeleza ni kufanya ushirikiano wa kiimani na binadamu wa ulimwengu wa kawaida taratibu taratibu kwa namna ambayo waliweza wao na mwisho wa siku wakajikuta wanakuwa na nguvu kubwa kwani walijipatia mali asili nyingi kutoka Duniani na kuziingiza katika ulimwengu wao huku wakibadilishana na binadamu madini mengi ya thamani.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba majini pepo wengi ikiwemo majoka na Mbweha ambao walikuwa na uwezo mkubwa walimezwa katika ulimwengu wa majini pepo kwa njia ambazo mpaka siku hio hawakuelewa imetokeaje , huku upande wa majini watu , yaani majini wa kawaida ambao mbinu zao sio kuamsha mapepo wao walijitenga na binadamu wa kawaida mara baada ya kugundua Dimension nyingine na kuanzia hapo kila majini wakajitegemea na kukawa na ulimwengu wa majini watu , ulimwengu wa majini pepo na ulimwengu wa Jangwa Tenganifu sehemu ambayo hupatikana miliki moja tu ya kijini ambayo hufahamika kwa jina la Braki.
Kwa historia hio ilimaanisha kwamba hapo zama za kale majini na binadamu waliishi katika ulimwengu mmoja kabla ya vita kutokea, vita ambayo mpaka wakati huo majini wote wanajiuliza ilimalizwa na nani kwani sio wao ambao waliwafanya majini pepo wenye nguvu kuvutwa kwenye ulimwengu mwingine.
Sasa kati ya majini pepo hao ambao walivutwa ni kama vile Aoiline Mbweha wa mikia tisa , Majoka na mashetani pepo wa anga.
Roma mara baada ya kusikia habari hio aliishia kushangaa , katika ulimwengu wa majini pepo Zimo alisema ulimwengu wao ulikuwa ni wa miaka mingi kuliko hata Hongmeng na hio ilimaanisha kwamba kabla ya kumezwa ulimwengu huo ulikuwepo.
Sasa Roma mara baada ya historia hio anajua nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif ni majini pepo na ni sawa na kusema ni ndugu wa Aoiline.
Kulinganana msaada ambao Aoiline alimfanyia na wengine Roma aliona ni dhambi kama ataingamiza miliki hio ya Braki ambayo inapatikana katika Ulimwengu wa Jangwa na anachopaswa ni kujaribu kufanya urafiki nao lakini kabla ya yote lazima ajue hazina yao ilikuwa ikimaanisha nini.
“Asante sana kwa kunielezea haya”
“Hivyo licha ya familia ya Sharf kuumiza watu wengi katika ulimwengu huu wa kawaida lakini kwa upande wetu sio jambo kubwa sana na sio maagizo yetu , Sisi sio kama majini kutoka Hongmeng na miliki nyingine ambao wanachotaka ni umaarufu tu , sisi leo tumetoka kuja katika ulimwengu wa kawaida kwasababu ya muovu Roma Ramoni ambae ameiba hazina yetu”
“Je naweza kuuliza, Hazina hio ina matumizi gani , je kutakuwa na athari zozote kama isipokuwa kwenye mikono yetu?”Aliuliza Maiuna feki na hapo ndipo Roma alipokuwa akitaka kujua ile kokoto ina maana gani.
ITAENDELEA ,WATSAPP 0687151346
 
Wakuu jamani natangaza nimemuona chaos mnyama wa maafa kwenye movie ya shazam fury of the gods ya mwaka 2023.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 735
Callum waziri mkuu wa Uingereza alikuwa akimjua Roma na uhusiano wake na Edna pamoja na Raisi Jeremy , idara ya usalama ya Uingereza haikuwa kwa ajili ya maonyesho tu walikuwa wakijua mambo mengi.
Lakini hata hivyo hakuwa akijua nia halisi ya Raisi Jeremy kuja mpaka hapo lakini kwasababu ni swala ambalo lilikuwa linahusiana na Roma hakutaka kuvuka mipaka yake hiyo alijitahidi kuwa makini.
“Hakika una ushawishi mkubwa Raisi Jeremy , kuja London tu umeweza kutupata mara moja?”Aliongea Catherine akionekana kumtania raisi Jeremy, licha ya kwamba hawajawahi kukutana lakini bado alionyesha hali ya kumdharau pengine ni kutokana na kutokea taifa dogo.
“Nimesikia habari za kutosha kuhusu malkia wa Wales lakini sikutegemea kukuona hapa ,nipo hapa kwa ajili ya kikao cha umoja wa mataifa kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa dunia nzima na mara baada ya kusikia habari za binti yangu na mume wake wapo hapa nikaona sio mbaya kuwatembelea”Aliongea huku akiwa na uso uliopambwa na tabasamu.
Maelezo yake yalikuwa kamilifu na ilimfanya kuonekana kama vile alikuwa na ukaribu sana na Roma pamoja na Edna.
Baada ya salamu wengine wote walitoka nje na kumuacha Roma na familia yake ndani ya chumba hicho cha VIP.
“Kama upo hapa kwa ajili ya kunifanya nikutane na mkuu wako wa miliki basi sahau maana sina mpango wa kuonana nae kabisa , kama anataka sana kuonana na mimi basi mwambie aje huku yeye mwenyewe”Aliongea Roma na kufanya tabasamu la raisi Jeremy kupotea mara moja.
“Roma kuna haja ya kuwa hivyo mbele yangu , ninaweza nikawa nilifanya makosa lakini yaliopita si ndwele na isitoshe hatuna vinyongo kati yetu , nilifanya mambo yale kwasababu ya kutaka wewe na Edna kuishi kwa furaha”
Wakati wa kuongea alikuwa akimwangalia Edna kwa sura ya kumwambia amsadie kumuomba mume wake lakini Edna alionekana kumpotezea.
“Usingekuwa hai mpaka sasa kama sio kwa uhusiano uliopo kati yako na Edna , hiyyo acha kuzunguka zunguka na sema kilichokuleta”
“Sawa nitaenda moja kwa moja , mkuu wa miliki ya Panas anataka kuongea na wewe , kama utakataa kwenda katika miliki au kwenda Rwanda yupo tayari kuongea na wewe kwa njjia ya vidio Call , ukikataa kusikiliza utakuja kujutia baadae”
Ijapokuwa ulimwengu wa kijini ulikuwa ukijitegemea lakini majini waliokuwa wakiishi huko walikuwa na uwezo wa kufanya mawasiliano na ulimwengu wa nje bila shida yoyote kutokana na teknolojia ya ajabu ambayo iliasisiwa na mababu wa miliki hizo.
Kuhusu Roma hakushangazwa na maneno yake kwani alikuwa ashajua kiasi kuhusu miliki hizo za kijini hiyo aliamini ilikuwa ikiwezekana.
“Kama ni hiyo niunganishe nitaongea nae"
Raisi Jeremy alijisikia furaha na kujivunia huku akijiambia pengine Roma alikuwa akiogopa miliki ya Panas.
“Nifuate nje tutafute sehemu nzuri kama ni hiyo , kuna watu wengi hapa”
“Hakuna haja , hawa wote ni marafiki zangu na familia yangu hiyyo sio lazima kuficha kitu kwao, labda kama mheshimiwa Jeremy anaogopa kugundulika ana uhusiano na majini?”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la uchokozi.
Baada ya kusikia maneno hayo hakutaka kusita tena na alitoa kishikwambi cha aina yake na alianza kukipangusa na ilionekana Panas walikuwa washajiandaa muda mrefu kupokea simu hio.
Sura ya jini Gefu iliweza kuonekana katika kioo cha kishikwambi hicho na alikuwa ndani ya ofisi yake.
“Sir, Mr Roma Ramoni yupo hapa tayari kwa kuongea na wewe”Aliongea Jeremy kwa sauti ya unyenyekevu huku akiwa amepamba uso wake na tabasamu.
“Sikutegemea kukutana kwetu kwa mara ya kwanza kutakuwa kwa namna hii , Roma hakika ni ngumu sana kukupata”Aliongea Gefu akiwa na tabasamu.
“Oh! Kumbe mkuu wa miliki ya Panas ndio upo hiyyo ..”Aliongea Roma lakini upande wa pili Gefu hakuelewa Roma anachomaanisha.
“Nilikuwa na haja ya kuonana na wewe kwa haraka kwasababu nina jambo muhimu napaswa kukuambia linahusiana na usalama wako na wanaokuzunguka”
“Unajaribu kumaanisha kuna kundi la majini ambao wanataka kuniua muda si mrefu?”
“Ndio , kwasasa ni kama unatembea juu ya barafu nyembamba, lakini sio tu kwmaba najua maadui zako wote lakini pia nipo tayari kukusaidia”
“Haina haja , sijakubaliana kuongea na wewe ili kusikia unaongea upumbavu”
“Nini!!. Roma unamaanisha nini kuongea hivyo au huamini maneno yangu?”
“Sio maswala ya kuaminiana, mimi nilitaka tu kujua mkuu wa miliki ya Panas anaonekana ipi ili nikiivamia miliki yenu nisipate shida ya kukutafuta na kukuua”
Ishara ya hasira iliweza kuonekana katika uso wa Gefu mkuu wa miliki ya Panas lakini fasta sana alirudi katika hali yake.
“Kijana mdogo chunga kauli zako naamini haipaswi kuwa na ugomvi kati yetu”
“Nyie ndio mliovujisha taarifa ya Rufi kuishi Tanzania kwenda kwa miliki ya Xia , hio ni sababu tosha ya mimi kutaka kuivamia miliki yenu na kulipa kisasi kwa umbea wenu”Aliongea Roma bila ya ishara ya utani.
Maneno yake ya kibabe yalimshitua Master Namba nne huku akijiuliza Roma alijuaje yeye ndio alivujisha taarifa.
“Kwa muonekano wenu inaonyesha nilikuwa sahihi , kama ifahamikavyo ukuu wa miliki ya Panas katika kujua kinachoendelea kwenye ulimwengu wa kawaida”
Upande wa Gefu alijua Roma hakuwa na ushihidi hivyo hakutaka kukamatika kizembe na alijua pengine Roma anamjaribu.
“Unathubutu ipi kunijaribu wewe bindamu?”
“Kwahio unatakaje?”
“Unafikiri tunakuogopa , tunakupatia nafasi ya mwisho ya kuungana na Panas, kwasasa umekuwa adui wa miliki ya Xia ,Kekexil na Braki , unadhani kujificha huko nje ya nchi kunaweza kukufanya ukawa salama na miungu wenzako dhaifu kukusaidia?”Aliongea kwa kufoka.
“Braki!!!”
Roma sura ilijikunja mara baada ya kusikia anahusishwa na Braki na kujiuliza Braki ndio kitu gani lakini Gefu alionekana kujua kinachoendelea kupitia sura ya Roma.
“Unajisikiaje kutokujua baadhi ya maadui zako?”
Roma hakujibu swali na badala yake palepale alipiga chini kile kishikwambi na kupasuka pasuka vipande vipande.
“Siogopi kiumbe chochote mimi , kama kuna adui anajiona mbabe anitafute tumalizane”Aliongea Roma na palepale macho yake yalisinyaa wakati wa kmwangalia Jeremy.
“I am not in a good mood , so get lost now when I still give a damn about your relationship with my wife”Aliongea akimaanisha aondoke wakati anajali uhusiano uliopo kati yake na mke wake.
“You .. you are Vexing … kwa ajili ya Edna!?, Roma nataka nikupatie ushauri … sisi binadamu tunao wajibu wa kufuata sheria za hii dunia , kila mtu yupo chini ya sheria na kila mtu atakushambulia kama utazivunja kutokana na ukiburi wako na wakati hayo yanatokea hakuna ambaye atakusaidia”
Baada ya kuongea kauli hio palepale licha ya kuwa na hasira zake aliondoka ndani ya eneo hilo , kwani alijihisi kutamani kumuua Roma ni hivyo tu uwezo huo hakuwa nao.
Mara baada ya kuondoka Roma alisimama na kusogelea dirisha na kuangalia upande wa uwanjani ambako mechi ilikuwa mapumziko , huku hali ya hewa ikiwa sio ya kawaida ndani ya eneo hilo kwani watu wake wa karibu wote walionekana kuwa na wasiwasi.
Bila kujua Roma alikuwa amejiongezea adui mwingine ambaye hamfahamu anaefahamika kwa jina la Braki.
Ukweli ni kwamba alikuwa na maadui wengi ambao hakuwa akiwajua na baadhi yao walitokana na wanawake wake na wengine walikuwa wakimchukulia kama adui kutokana na kuwa na uwezo mkubwa.
“Rufi unajua chochote kuhusu miliki ya Braki?”Aliuliza Roma mara baada ya kujituliza.
“Sijawahi kuisikia , Nanny ushawahi kuisikia?” Rufi alionekana kutokukujua na alimtupia swali Sui lakini hata yeye alionyesha kutokujua chochote.
Ijapokuwa ilikuwa ikihusiana na ulimwengu wa majini lakini kutokana na ukawaida wao hawakuwa wakiijua.
“Mimi nadhani Braki inahusiana na familia ya Mzee Sharif , si ulisema walishawahi kuleta majini wengi kupambana na wewe , nadhani tufikirie hivyo kwa sasa?”Aliongea Rose na Roma alitingisha kichwa baada ya kuona alikuwa na pointi .
“Hubby unataka kweli kwenda kuivamia miliki ya Panas?”Aliuliza Edna ambaye alikuwa amekunja sura.
“Hautaki niende?”
“Nili…”
“Edna siwezi kukusikiliza awamu hii , kila kitu kingekuwa sawa lakini katika vitu ambavyo vinahusisha uhai wa wengine sitokuruhusu ubadilishe mawazo yangu”
Edna mara baada ya kuona usiriasi uliopo katika macho yake alishia kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Sijasema nataka kukuzuia , nikwamba naona itakuwa hatari sana”
“Tatizo hata kama niseme nisiende kuwavamia na kuwasambaratisha najua hawawezi kutulia na watatafuta tu namna ya kutaka kuniua … Hili ni daraja ambalo napaswa kuvuka na nikishapita kila kitu kitakuwa kimekwisha”Aliongea.
“Roma sidhani kama itakuwa ni rahisi, tayari tuna uadui na miliki tatu za kijini kubwa na tuna maadui maelfu na maelfu , unadhani ni sawa kuua na kuendelea kutengeneza maadui? , mimi naona labda hakuna haja ya kuua na tunaweza kutatua haya matatizo kwa njia nyingine , wao wanasheria zao pia na pale wanapojihakikishia kwamba huwezi zivunja hawawezi kukufanyia chochote”Aliongea Sophia.
“Sophia unaongea ujinga , hivi unajua tafsiri ya sheria mbele ya watu wenye nguvu ni tofauti na inavyotafsirika mbele ya watu dhaifu?”
Aliongea Roma na kisha alinyoosha kidole kuelekea uwanjani wakati wachezaji wakitoka katika vyumba ya mapumziko kwa ajili ya kuanza kwa kipindi cha pili.
“Hivi unajua ni kwasababu gani mpira wa miguu ni maarufu sana duniani na kwanini watu wengi kama hivi wanaupenda?”
Wanawake hao wote waliishia kushangaa tu wasiweze kuelewa swali lake,walijiambia wanaongea topiki ya hatari hiyo kuna haja gani ya kuhusisha mpira wa miguu lakini Roma alionekana kutojali mawazo yao.
“Ni kwasababu katika mechi ya mpira haijalishi timu ni bora kiasi gani au ni dhaifu kiasi gani lakini siku zote matokeo yanaanza sifuri kwa sifuri na mpira unachezwa kwa sheria, hii inamaanisha kwamba haijalishi timu ni dhiafu lakini kama watakuwa tayari kupambana katika kukaba kukimbia na kufunga hata wao pia wanaweza kuwa mabingwa , kwa maneno mengine hapo ndio wakati watu ambao sio wachezaji ndio wanajipatia riziki , sehemu ambayo uvumiliu wao huonekana , katika uwanja mshindi ndio bingwa hata kama ni dhaifu au alipendelewa kwa namna yoyote ile ili mradi tu ameifunga timu bora na yenye nguvu hata kama ni mara moja katika historia yake , hii inamaanisha kwamba wao pia wanayo nafasi ya kuwa nyota na hii ndio maana mpira wa miguu ni wa kuvutia sana”Aliongea na kisha akavuta pumzi na kuendelea.
“Lakini unadhani hio ni sawa kati ya wachezaji na wamiliki wa timu au wasimamizi wa mashindano? , ingawa mechi inaanzia sifuri kwa sifuri lakini kwa matajiri na wasimamizi wa UEFA mambo ni tofauti , kwao haijalishi nani anashinda bado watapiga pesa na kupata faida na ipo hivyo siku zote , kwa mfano mchezaji katika timu kama akishindwa kutoa ushirikiano wa maelekezo viongozi wanaweza kuto kumjumuisha katika mechi na kutoa sababu kama vile ni majeruhi au haendani na mfumo na mengineyo .. ,kwa lugha nyepesi ni kwamba wanaoendesha michezo na timu ndio wenye maamuzi ni taarifa gani iwafikie mashabiki na kuamua mchezo uwe vipi , unaweza kuona mechi kabisa hii mshindi ni wa kupangwa lakini wewe kama shabiki utafanya nini tofauti na kuongea ongea na kugoma, hakuna cha ziada ambacho unaweza kufanya kwasababu kwa nje wewe unaburudika na wachezaji wakicheza mpira lakini kwa ndani kuna mfumo ambao umetengenezwa kwa ajili ya kurahisisha maswala mengi aidha yawe ni ya kifedha au Ajenda zao za kijamii labda tu kama watu waache kuangalia mpira .. na huu ni mfumo endelevu na utaendelea hivi labda siku tu watu dunia nzima waseme hawaangalii mpira tena , sasa hili halipo kwenye mpira tu kila michezo maarufu yote wewe kama shabiki utaona ni burudani lakini nyuma ya pazia kuna mfumo..”
“Ndio inaweza kuonekana yanayofanyika ni uchafu lakini maisha ya kibinadamu tokea mwanzo yalianzia katika uchafu , sasa tuseme mimi ni kama mchezaji , Kocha au tuseme timu nyenye nguvu ambayo imepata umaarufu hivi karibuni, viongozi waandamizi na matajiri wote macho yao yatakuwa kwangu kwasababu mbili tu; mosi nifanye kazi kwao na niwasaidie kupata pesa au kutimiza ajenda zao , pili hawataki niwasaidie wengine kupata pesa, kwa maneno mengine ili nipate faida lazima na wao wapate faida na sasa hapa hizi ndio sheria ambazo wameweka ambazo hawataki mchezaji kuzivunja kwasababu zinaathiri utajiri wao pamoja na ushawishi wao”
“Kama nitafanya kazi nzuri kama mchezaji wataniacha niendelee kuishi kama mchezaji na kunifanya niendelee kuwa maarufu na watanipatia Ballon d‘or au Kiatu cha Dhahabu au watafanya hata timu yangu ya taifa kuwa bingwa wa dunia au club yangu kuwa bingwa wa UEFA na kama sitofanya vizuri au nikikataa matakwa yao watahakikisha wananizimisha aidha kwa kuniundia mchezaji uwanjanni ambaye atanijeruhi au kuanza kunitengenezea Zengwe nyingi tu ili kunitoa mchezoni hizi ndio sheria ambazo wameweka .. wakati nikiwa chini hawakuwa na habari na mimi na hawakuwahi kunichukulia siriasi lakini sasa nimekuwa tishio kwao hawataki kuzembea, hii haipo kwenye mpira tu kwa kila nyanja kuna huu mfumo na ambao wanasuka mipango hii ya kimfumo hawatojionyesha kamwe mpaka sekunde ya mwisho , isitoshe lazima wahakikishe mchezo ulikuwa ni wa haki”
Kila mmoja alijikuta akiwa kimya na kuangalia uwanjwani ambako mechi ilikuwa ikiendelea.
Maneno ya Roma yanaweza kuonekana kama yamebase upande mmoja lakini yalikuwa yamejaa ukweli mgumu(Harsh truth).
“Ijapokuwa hatuwezi kushiriki katika vita yako lakini kama mtu ambaye unapambania maisha ninaelewa hisia zako”Aliongea mmoja wapo na kumfanya Roma kuonyesha shukrani na palepale alimbeba Lanlan na kumpakata.
“Sina chaguo nyingine , kwasababu mpaka sasa hawaniangalii kama mtu Dhaifu , kama ninataka kuendelea kuishi ni aidha nishirikiane nao au kama sitaki kushirikiana nao niwaweke chini yangu kwa kuwapiga na kisha kuweka sheria zangu mimi”Aliongea na kisha aligeuza macho yake na kuangalia warembo wake waliokuwa wakimwangalia kwa macho ya matamanio na kisha akageuzia macho kwa Lanlan.
“Sio mimi tu lakini ni kwenu pia na kwa mtoto wangu”Aliongea Roma kwa sauti hafifu akionekana kama vile ni mtu ambaye anakumbukia maisha yake yaliopita na kitendo kile kilimfanya Blandina kukosa ujasiri wa kuendeea kusikiliza na machozi yalimtoka na kwenda kumkumbatia Roma na Lanlan na kuanza kulia.
Kila mmoja alijua hisia za Blandina zinatokea wapi , ilionekana alikuwa na hatia kama mzazi na kumfanya mwanae kupitia magumu mengi lakini kwa wakati huo machozi yake hayakuwakilisha huzuni tu lakini bali kujivunia kwa mafanikio ya mtoto wake.
Ukumbuke hapa ni ndani ya Chumba cha VIP ndani ya uwanja wa Wembley hivyo ni kama wamejitenga na mashabiki wengine.
Unadhani Roma yupo sahihi , ni kweli kuna mifumo ambayo imewekwa kwa ajili ya kushikiria mafanikio ya watu??






SEHEMU YA 736.
Ni upande wa Tanzania jijini Iringa muda wa mchana katika makazi ya Afande Kweka kulikuwa na kikao cha siri kilichokuwa kikiendelea.
Kikao hichi kilikuwa kikijumuisha watu kama saba hivi ambao ni Paster Cohen, Mellisa , Phill Knight , Nadia Alphonso , Suzzane , Linda na mwanamama mrembo kutoka Hungury afahamikae kwa jina la Zoe Kovacic.
Nadia ndio ambaye alikuwa akionekana kusoma ripoti licha ya kwamba kila mmoja ambaye alikuwa hapo ndani alikuwa ameshikilia kishikwambi, ilionekana ni kama vile walikuwa wakirudia kile ambacho Nadia alikuwa akisoma.
“Mzee kama mwanachama mkongwe wa jamii yetu, viongozi wameniagiza nikuelezee kuhusu ubini wa kiongozi wetu”Aliongea Mellisa kwa lugha ya kingereza.
“Kiongozi amekwisha kupatikana?”
“Ndio Komredi katika kikao cha mwisho kilichofanyika Saudi Arabia tumeweza kupata mawasiliano na Kiongozi kwa mara ya pili”Aliongea Pastor Cohen na kumfanya Nadia kuangaliana na Suzzane.
“Kulingana na Kalenda ya jamii yetu kiongozi alipaswa kufanya mawasiliano na viongozi wa juu ndani ya tarehe husika , ijapokuwa ilikuwa ni hatua ya pili ya kumthibitisha kama kiongozi, umoja umefurahi kwamba mpango A wa kalenda ulitimia na kwanzia tarehe hio Edna Adebayo anatambulika kama kiongozi wa Umoja wa Ant-Illuminat”Aliongea Mellisa na kumfanya Linda kuonyesha mshangao huku Afande Kweka yeye macho yake ya kizee yakichanua.
“Komredi ni kama tulivyotarajia”Aliongea Pastor Cohen.
“Kuna maswali mengi juu ya hili Komredi nilijua kiongozi ni Seenteen kulingana na maelezo yako Komred”
“Wote tulidhania kiongozi anakwenda kuwa Seenteen, kuna maswali mengi juu ya hili lakini kulingana na maelekezo ya mwasisi wa umoja wetu anasema Kalenda inakwenda kujibu maswali yote lakini ni Aidha kama Binadamu tutafanikiwa kuishinda vita na Miungu”.
“Viongozi wengi pia hawakuamini kama siku ya kikalenda Edna angefanya mawasiliano na sisi lakini ajabu alifanya hiyo na kila mmoja alishangaa lakini imeondolea umoja harakati za kuona mchoro wa Unabii?”
“Huu mchoro wa Unabii unaonyesha kitu gani , kwanini imekuwa kitu muhimu kwa pande zote mbili Mellisa?”
“Hatuwezi kujua kwa uhakika mchoro huu unamaanisha nini na nani anaonekana katika picha lakini makisio yetu ni kwamba mchoro huu unahusiana na kiongozi wa umoja wetu”
“Kwa taarifa za Shekh Assad ni kwamba mchoro huu pia una umuhimu kwa Illuminat na ndio kiongozi ambaye wanamsubiria, kama usemayo ni sahihi Edna ana uhusiano na huu mchoro wa unabii lakini si inamaanisha kwamba pia ndio kiongozi wao ambaye wanamtarajia kulingana na unabii?”
“Upo sahihi Zoe lakini kwasasa hata Illuminat wenyewe bado hawajaweza kuona mchoro huu wa Unabii kwani upo chini ya Vatican”Alijibu Mellisa.
“Madam kuna uwezekano wa Edna kuwa Seventeen?”Aliuliza Nadia.
“Kulingana na mpango ulivyokuwa , Seventeen ni zao la mpango LADO kama alivyo Roma Ramoni lakini majukumu yao tokea mwanzo yalikuwa ni tofauti , ijapokuwa mpaka sasa hivi hatujui Seventeen yupo hai chini ya Zeros lakini tokea mwanzo Seventeen ndio alikuwa ni msingi wa kufanikiwa kwa Ant-Illuminat”
“Kama ni hivyo kwanini Edna ndio awe kiongozi , sijawahi kuona ishara yoyote ya Edna kujua chochote kuhusu Ant- Illuminat?”Aliongea Suzzane.
“Ukweli ni kwamba tunaamini Seventeen amekwisha kufariki mpaka sasa chini ya maagizo ya Athena na kwa maelezo ya Chriss ili mchoro wa unabii kukidhi vigezo vya ki’unabii hakupaswi kuwa na uwepo wa watu wawili wenye sura zinazofanana”Aliongea Mellisa.
“Melllisa hili linajibu kilichopo kwenye mchoro huo wa Unabii , kama kweli maneno ya Chriss ni sahihi basi kuna uwezekano Mchoro wa Unabii unaonyesha sura ya Edna au Seventeen lakini kwasababu ni unabii wa mtu mmoja basi moja kwa moja mmoja wapo lazima atoweke”
“Naunga hoja ya Komredi lakini kwangu bado swali linaibuka Athena ni nani na kwanini mchoro wa Unabii kuwa na sura ya Edna , wote kati yetu tunajua mpango wa Athena ni nini zidi ya binadamu na hatari ya mipango yake kufanikiwa?”
“Afande mpaka sasa hatuwezi kujibu maswali lakini pia hatuwezi kufanya makisio kwani ipo kalenda ambayo inatuongoza ambayo haijawahi kufeli na hata pale ilipofeli kulikuwa na mpango B, nadhani wote tuamini katika Kalenda”
“Naunga hoja ya Mellisa akini je wakuu wanasemaje kuhusu hali inayoendelea kwa sasa?”Aliuliza Phill.
“Unazungumzia kushuka kwa joto la dunia?”Aliuliza Zoe na kufanya kila mmoja kumwangalia mwenzake kwa shauku kubwa ya kusikia jibu.
“Kulingana na Kalenda tukio muhimu ambalo ndio ishara kubwa ya hatua muhimu ya Athena kuchukua lakini vilevile hatua ambayo Umoja wetu unapaswa kuchukua ni kuona majira ya theluji katika bara la Afrika, nadhani hali hii ya hewa tunaelekea kuona ishara hii hivi karibuni hivyo tunaweza kusema mpaka sasa tunaingia katika hatua muhimu sana katika umoja wetu na kwa dunia kwa ujumla , hiki ndio ambacho viongozi waeniusia nikiseme katika kikao hichi na sio hapa tu dunia nzima vikao vya ajenda hii kwa wenzetu vinaendelea”Aliongea Mellisa.
“Mellisa yupo sahihi kushuka kwa joto la Dunia sio nchi moja bali ni dunia nzima lakini ni Afrika pekee ambayo inaonyesha joto kupungua taratibu sana , hii inamaanisha mpaka nyakati za theluji zikitufikia kuna uwezekano baadhi ya maeneo ya Dunia joto kushuka sana kiasi cha kuathiri maisha ya binadamu”
“Nadhani ndio maana Wanachama wengi wa Freemason na Illuminat wamenunua maneo mengi ndani ya Afrika kwa kipindi cha hivi karibuni huku wakifosi sheria nyingi za kimataifa kupitishwa , hii inaonyesha walikuwa wakiandaa mazingira rafiki kwa ajili ya kuishi wakiwa huru”Aliongea Zoe.
“Hii ni kweli na ni swala ambalo tulikuwa tukipambana nalo kama umoja,kuna baadhi ya mataifa ambayo tumeyachagua kama nguzo muhimu ya Umoja kwa ajili ya kulinda tamaduni zake ikiwemo Tanzania lakini kuna maeneo ambayo pia ndani ya Afrika yapo chini ya Illuminat na ushawishi wao ni wa juu na hili hatuwezi kulifanyia kazi kwani litaibua migororo”
“Nadhani naona unachojaribu kumaanisha Miss Mellisa , ni miezi kadhaa iliopita mataifa zaidi ya kumi ya Kiafrika yamepitisha sheria ya Ushoga kuwa huru hili ni swala ambalo linahusiana na ulichosema”
“Upo sahihi Linda , Tanzania ilikuwa ni nchi ambayo ingekuwa ya kumi na moja kutangaza hii sheria kama sio sisi kuingilia , shukrani kwa Suzzane na Nadia wameweza kutiisha misheni yao vizuri na sasa Tanzania imekuwa Neutral kwa sisi pamoja na wao”
“Urusi wanazungumziaje hili?”Aliuliza Afande Kweka.
“Wapo ndani ya mfumo , wanaweza kupinga wazi lakini ni taifa ambalo limegawanyika katika pande mbili”.
*******
Pumbavu zako Roma Ramoni , nitakuua tu siku moja”Aliongea Gefu kwa sauti kubwa na kwa hasira zake alipelekea kuharibu kila kitu kilichokuwa ndani ya ofisi yake lakini bado haikuwa ikitosha kutuliza hasira zake.
Mbele yake alikuwa ni Master Namba nne na mwingine mmoja ambao wote walikuwa katika hali ya wasiwasi kutokana na hasira za kiongozi wao mara baada ya kumaliza maongezi yake na Roma Ramoni.
Ilikuwa ni mara chache sana kwa Gefu kuwa katika hasira kama hizo , kitendo cha Roma kumdharau waziwazi mara nyingi mfululizo kilimfanya chuki yake kuongezeka maradufu.
“Kaka punguza jazba, ni sawa tu kama amekataa kuungana na sisi na kwasababu maadui zake ni pamoja na Braki lazima atakufa na sisi ndio tutachukua fursa hio ya kummalizia akiwa chini kabisa”
“Hawa majini kutoka Braki hawajawahi kuwepo katika uso wa dunia kwa zaidi ya milenia moja , nimesikia kutoka kwa wazee wanasema hawajui kabisa uwepo wa binadamu mwenye uwezo mkubwa kama Roma , Roma huyu mjinga amejitengenezea uadui na hawa mashetani ambao walikuwa wameshasahaulika”
“Namba nne fanya mawasiliano na Jeremy kusitisha mipango yetu yote ya kimsaada na Tanzania hususani familia ya Raisi Senga na kisha atasubiria maelekezo yangu ya mpango wa pili unaofuatia , pia tuma barua kwenda katika miliki zote zenye uadui na Roma hususani katika miliki ya Xia na Kekexil na waambie kupitia mashushusu wetu waliopo katika kila pande ya dunia ya kawaida watasaidia kujua nchi ambayo Roma anaishi na familia yake na kama wanahitaji msaada watuambie”
“Sawa kaka”Aliongea Master namba nne.
“Gegu chukua baadhi ya wazee kuelekea mlima Yoshe na mrudishe yule mtu kurudi Panas”
“Kaka namba moja sio kwamba ni mapema sana kumrudisha?”
“Fanya kama nilivyosema , vipi kama Roma akitushambulia unadhani nitaweza kuilinda miliki mwenyewe?”
“Umeeleweka bro”
Lakini sasa muda huo huo sura zao zilibadiika mara baada ya kuhisi kitu ambacho sio cha kawaida na Gefu ndio aliekuwa wa kwanza kupotea ndani ya ofisi hio na kuja kuibukia nje na kufuatiwa na wengine.
Wingu jeusi lilikuwa limejikusanya katika upande wa Kusini mwa eneo la miliki ya Panas , ngurumo na mwanga wa Radi vilikuwa vikisikika na kuonekana.
Sauti za ngurumo za radi zilikuwa kubwa kama vile anga linataka kuondoka chini.
Majini wengi wa miliki hio walikuwa nje wakiangalia hali hio ya kustaajabisha ambayo ni adimu sana kuonekana katika miliki za majini.
“Hii nii…”Jini mmoja ambaye alikuwa katike levo ya maji ya barafu aliongea.
“Hahaha…. tayari amekwisha kuipita levo ya maji ya kiroho , hii ni radi ya mapigo tisa ya adhabu ya anga”Aliongea mkuu wa miliki ya Panas kwa furaha.
“Hakika inashangaza ni juzi tu hapa Anjiu wa Xia ameweza kupita levo hii na leo ni zamu ya Rozu”
“Huu ni wakati wa kuwa na majini wa levo za juu katika ulimwengu wetu,ni heshima kwetu kuangalia kitu kama hichi kikubwa”Aliongea na kufanya wazee pamoja na majini wa miliki hio kuonyesha furaha zao.
“Kimya!!, huu ni mwanzo tu lakini hatuna uhakika kama ataweza kuvumilia mapigo hata matatu ya radi ya rangi ya Zambarau”
Baada ya kusikia kauli hio kila mmoja alipiga kimya kwani ni kweli radi hio haikuwa imeshuka bado na walikuwa na wasiwasi kwamba wanaweza kumpoteza mtu wao.
Majini wanaweza kupitia radi lakini sio wote ambao wanaweza kuihimili kwani ilikuwa na nguvu kubwa kwani dhumuni la kushuka kwake sio kwa ajili ya kunufaisha jini bali ni kwa ajili ya kutoa Adhabu kwa kukiuka sheria za anga.
Dakika chache mbele radi hio ilianza kuonyesha ghadhabu yake na boriti ya radi iliokuwa katika rangi ya Zambarau na bluu ilionekana ikishuka kama vile ni nyoka na kwenda kupiga katika sehemu ambayo yupo jini aliefahamika kwa jina la Rozu.
Ilikuwa ni sauti ya kuumiza masikio ya mwangwi ndio iliweza kusikika na kuwafanya majini kuogopa na kuwafanya wengine kukimbia
“Hii inatisha , sidhani kama Rozu ana Dhana ambayo inaweza kumkinga,atakuwa na uwezo wa kupita hii Adhabu bila kifo kweli?”
“Ni ngumu kusema na hatuwezi hata kusogelea eneo alipo kwasasa bila ya kupoteza nafsi zetu , hata mimi sijui kama ataweza kweli kuhimili?”.
Kila mmoja alikuwa akijiuliza swali linalofanana na kuna ambao walikuwa wakijutia kwa Rozu kukasirisha anga mpaka kupatwa na radi hio.
Dakika chache mbele radi ya pili ilipiga na ilikuwa kubwa kuliko ya mwanzo kiasi cha kutengeneza shimo na ndani ya dakika chache mara baada ya kufifia kitu kinachofanana na Dhahabu kilionekana katka lile eneo.
Kuna ambao waliweza kuona kitu hicho lakini hawakuweza kujua ni kitu gani lakini wakuu wa miliki hio walikuwa na uwezo wa kuhisia Rozu alikuwa hai bado kutokana na msisimko aliokuwa akidhalisha.
Hali hio iliwafanya wazee kujiuliza amewezaje kutoathirika katika mapigo hayo ya radi.
Radi ya tatu iliweza kupiga kwa awau nyingine na ilikuwa na nguvu kubwa zaidi lakini hata hivyo kile kitu ambacho kilikuwa katika muonekano wa Dhahabu bado kilikuwa kikionekana katika eneo lile.
Radi ile ilionekana haikuwa na mpango wa kuendeleza mapigo kwani mara baada ya mapigo matatu wingu lilianza kutawanyika na palepale shimo kubwa lilionekana kwa macho.
“Rozuu..!!!”
Mkuu wa miliki ndio aliekuwa wa kwanza kuita jina hilo lakini kufumba na kufumbua palepale alionekana mwanamke jini ambaye ameshikilia upinde wa Dhahabu akisogelea mbele ya kila mmoja akitokea eneo lile
Nywele zake ndefu zilikuwa hazijafungwa na zilisambaa kulingana na upepo ulivyokuwa ukivuma lakini licha ya hivyo hazikuweza kuficha uzuri wake wa ajabu na macho yake angavu , alikuwa mrembo haswa kwanzia ngozi , umbo la uso na kila kitu.
Alikuwa na muonekano wa ajabu kidogo mzungu sio mzungu , alikuwa ni kama vile ni mfilipino.
Ijapokuwa hakuwa na mavazi ya kirembo kama wanawake wa kidunia lakini upole wake pamoja na uwezo wake ulimfanya kuzidi kupendeza na kuwa ni mwenye kutamanika.
Huyu mwanamke alikuwa akifanana kwa kila kitu na mrembo ambae Hermes mjumbe wa miungu alikuwa akiongea nae katika kilele cha mlima kilimanjaro muda kadhaa mara baada ya Roma kumuokoa Edna katika mikono ya Vampire waliokuwa wakitafuta mshipi feki.
Ki ufupi ni kwamba ni huyu mwanamke bila shaka na haikueleweka ilikuwaje akawa katika jamii ya majini wa miliki ya Panas lakini ndio hivyo alionekana kupitia levo ya mapigo matatu ya radi ya mbingu na jina lake alikuwa akifahamika kwa jina la Rozu.
Ijapokwa Rozu hakuwa ameonyesha uwezo wake wote lakini kwa majini hao walijua alikuwa ni wa levo za juu sana , pengine alikuwa akilingaina ki uwezo na Jini Anjiu wa miliki ya Panas au kumpita.
“Hongera sana , kwasasa upo na uwezo mkubwa wa nguvu za kijini na hakuna ambaye anaweza kukushinda katika ulimwengu wa majini watu”Aliongea Master namba nne huku ile hofu yake ya kumhofia Roma na Anjiu ikiwa imetoweka kabisa , alijua kwa uwezo aliokuwa nao Rozu anapaswa kuwa na amani.
“Hongera sana , nilikuwa na wasiwasi muda si mrefu lakini kwa bahati nzuri umeweza kufanikiwa kupitia mapigo ya radi”Aliongea Mkuu wa miliki hio huku akijiuliza kimoyo moyo.
“Imekuwaje akapitia mapigo hayo ya dhiki ya radi kirahisi hivyo , anaonekana hajapatwa na majeraha ya aina yoyote yale”Aliwaza.
Ukweli ni kwamba kuna namna majini hao walikuwa wakimjua Rozu kama Rozu jini mwenzao lakini hawakumjua Rozu kama sehemu ya miungu , kitendo cha Rozu kuongea na Hermes juu ya mlima kilimanjaro ilimaanisha kwamba ni sehemu ya miungu lakini jina lake halifahamiki ni lipi katika miungu yote iliobaki ambayo hatujawaona wahusika wake.
“Kama hizi ni pongezi za dhati basi sina budi ya kuzipokea”Aliongea mwanadada mrembo Rozu huku akimwangalia Gefu kwa macho makali kidogo kiasi cha kumfanya Mkuu wa miliki hio kuwa na wasiwasi lakini alijitahidi kuonyesha tabasamu.
“Unapenda sana utani , sina haja ya kumuonea wivu mdogo wangu wa kike mafanikio yake , leo ni siku ya kusherehekea, uwepo wako unatufanya tusimhofie tena jini Anjiu”Aliongea.
Ukweli ni kwamba Rozu na Anjiu kidogo walikuwa na tofauti , wakati wa Anjiu anapokea mapigo ya radi chungu cha Roma ndio ambacho kilimkinga lakini kwa jini Rozu yeye ilikuwa tofauti kwa maana kwamba mapigo yote ya radi yalimfikia.
Majini wote walikuwa kwenye shangwe wakimzunguka Rozu na kumpa pongezi za dhati kabisa kwa kupigi hatua hio Adhimu.
Kuipita Dhiki ya radi ni hatua kubwa sana katika ulimwengu wa majini ndio maana.
Rozu mara baada ya kuweka upinde wake wa Dhahabu katika hifadhi ya pete alivuta pumzi nyingi na kisha kutoa tabasamu.
“Anjiu huna uwezo tena wa kunizidi, Hades namsapoti Athena na mipango yake na nataka nione ikifanikiwa”Aliwaza.
Haya sasa kuna kiumbe kingine katika miliki ya Panas , unadhani huyu jina lake halisi ni lipi kati ya miungu kumi na mbili ya mlima Olympus kutoka sayari ya Mars.
Hades A.k. a Roma Ramoni atamuweza kweli?.




SEHEMU YA 737.
Upande wa Roma mara baada ya mechi kumalizika hakuna ambaye alitamani kuangalia ugawaji wa makombe na medali hivyo walirudi moja kwa moja kwenye boti yao ya kifahari.
Upande wa Raisi Jeremy hakuwasumbua tena kwani alikuwa ndani ya Uingereza kwa ajili ya kikao cha Umoja wa mataifa kinachohusu mabadiliko ya hali ya hewa na hata Raisi Senga alikuwa ni moja ya viongozi ambao walihudhuria kikao hicho muhimu.
Kilikuwa ni kikao muhimu kutokana na mabadiliko ya ghafla ya hali ya hewa ya joto la dunia kuporomoka na kusababisha baridi kali licha ya kwamba katika maeneo mbalimbali ya dunia ilipaswa kuwa majira ya joto.
Ukiachana na wakuu wa mataifa lakini pia wanasayansi wengi na watu wa maswala ya kimazingira walikuwa wakihudhuria kikao hicho ili kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo mara baada ya kujua chanzo.
Clark ni moja ya wanasayansi muhimu kabisa ambao walialikwa katika kikao hicho muhimu lakini licha ya hivyo hakukuwa na maelezo ya moja kwa moja ambayo angeongea kwani ni swala ambalo bado hakuwa amelifanyia utafiti.
Roma mara baada ya kuingia katika boti ndio maandalizi ya kurudi katika visiwa vya wafu yalianza rasmi lakini ndio muda ambao aliweza kupokea simu kutoka kwa Afande Kweka.
“Wewe mtukutu hivi utaacha lini kuwa na huo ukiburi?”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kuishia kushangaa.
“Ongea vizuri mzee basi”
“Kwanini umekataa kuongea na wajumbe wa Hongmeng ?, angalau hebu ongea nao maana kwasababu yako kila saa wapo ndani ya makazi yetu, unafikiri nadili nao vipi viumbe wa ajabu kama hawa?”
“Unamaanisha huyo Xuan Jizi yupo ndani ya makazi yako?”Aliuliza Roma huku hasira zikianza kumvaa maana aliona ni kama usumbufu.
“Anaonekana kuwa na hasira sana na amesema kama hutorudi mapema anaenda kutoa taarifa Hongmeng , hebu rudi udili na hii hali nishazeeka sitaki kuingizwa kwenye matatizo ya namna hii mimi”Aliongea na palepale alikata simu ikionyesha dhahiri alikuwa amekasirika.
Roma aliweka simu yake mfukoni na kisha aliwasogelea wanawake wake na kuwaambia juu ya hali inayoendelea nchini Tanzania hivyo anapanga kuondoka.
Kwasababu walikuwa ni waelewa hawakumzuia Roma na dakika hio hio alianza safari kurejea nchini Tanzania.
Ulaya na Tanzania masaa yalipishana kidogo sana hivyo Roma alifika wakati wa usiku pia ndani ya jiji la Iringa na wakati wa kutua tu aliweza kuona kuna wageni wamekaa katika sebule ya wageni ndani ya nyumba hio , walikuwa wawili na wote ni Wachina.
Moja kati yao alikuwa akimjua na mwingine hakuwa akimjua lakini alionekana kuwa handsome mno , ilikuwa ni kama vile sio mchina na alikuwa katike levo ya maji ya kawaida.
“Naona Mjumbe umeimarika kuliko mara ya mwisho tulivyoonana”Aliongea Roma akimlenga mjumbe wa Hongmeng mpenda rushwa.
“Haha… sipo hapa kwa ajili ya kukumbushia namna tulivyoonana mara ya mwisho nimemleta balozi”Aliongea na kisha alimpa ishara balozi Xuan Jizi.
“Wewe ndio Roma Ramoni ulietibua hali ya hewa katika miliki ya Kekexil na Xia?”Aliuliza yule bwana bila hata ya salamu , alionekana kuwa na hali ya ujeuri hivi.
“Ndio umekuja kote huku kwa ajili ya kuuliza ujinga?”
“Acha maneno yako makali , hivi unajua upo kwenye matatizo?”
“Nielimishe”
“Nikuelimishe nini? , unadhani kuna hata haja ya kufanya hivyo , unajua mwenyewe namna ambavyo umekasirisha majini kutoka miliki ya Xia na Kekexil , ukaenda mbali na kuchokoza miliki ya Braki , nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif , unaonekana kabisa unaogopa ndio maana ukaikimbiza familia yako nje ya nchi”
“Umongea sana lakini sijui kilichokuleta ni nini?”
“Nipo hapa kwa ajili ya kupitisha maagizo niliopewa na wakuu wa miliki ya Hongmeng, wasimamizi wakuu wa sheria ya the gods treaty , ili kuongezea nguvu utulivu wa dunia na kukuzuia kupigana na miliki za kijini na kusumbua raia , Hongmeng kwasasa itakuwa ndio kimbilio lako licha ya kwamba kutakuwa na mashariti, ukikukubali hakuna miliki yoyote ambayo itakugusa”
“Roma usishangilie bado kuna masharti”Aliongea yule mjumbe na Xuan jizi aliendeea.
“Umekiuka sheria nyingi sana na kutumia uwezo wako vibaya na kuua wajumbe ambao waliagizwa kuja duniani kutimiza majukumu yao , lakini licha ya hivyo Hongmeng hawataki kulipiza kisasi na wameaua kukusamehe ili mradi tu kwa hiari yako utoe mbinu yako ya mafunzo , vidonge na Dhana ya Chaos cauldron na baada ya hapo sisi tutakupatia ulinzi”Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Roma kuangua kicheko.
“Unacheka nini?”
“Wewe Mzee Jizi, lazima kwenye kwenye kichwa chako kuna nati zimechomoka au hao Hongmeng hawajui nini kinaendeea , nadhani napaswa kuwafafanulia kwa sentensi rahisi”
“Acha kunitukana … tunazo taarifa umeiba hazina yote ya Kekexil na Xia na unazo Dhana na vidonge kedekede , hivi unadhani vitu vya thamani kama hivyo utaweza kuvilinda peke yako, hivyo acha ukiburi na sikiliza tunachokuambia”
“Vipi kama nikikataa mtanifanya nin?”
“Roma acha kujifanyisha kijogoo , sekunde ambayo nitakuripoti katika miliki ya Hongmeng basi ndio utakuwa mwisho wako kwani utakuwa ni adui namba moja wa Hongmeng”
Roma aliwaza na kujiambia tokea siku anajua uwepo wa Hongmeng ndio uadui wao ulipoanzia hivyo hana mpango wa kuwasikiliza kwa chochote , kwanza kabisa alikuwa na deni kwa Zenzhei kumsaidia kulipa kisasi na tokea siku waagane ni kama Zenzhei katika ulimwengu huo wa kijini alikuwa akimsubiria.
Roma bila ya kujiuliza mara mbili mbili aliita nguvu ya Cauldon bila ya kukitoa nje na kuingiza katika mwili wa Xuan Jizi na kuanza kunyonya nguvu zake za kijini na nguvu ya Cauldron ilikuwa kubwa mno na ndani ya dakika chache tu alikuwa ashapoteza uwezo wake wote na kubakia binadamu wa kawaida.
Xuan Jizi hakuwa jini kama jini wa Hongmeng , alikuwa ni binadamu tu ambaye alikuwa na mafunzo ya kijini hivyo ilikuwa rahisi kwa Roma kudili nae kwani alikuwa ndio kwanza yupo katika levo ya maji ya kawaida.
Hakuna ambaye alitegemea Roma kuchukua maamuzi kama yale , lakini kwa Roma alitaka kuonekana kuwa siriasi na kutangaza vita vyake rasmi na Hongmeng kabisa na ili kuonekana yupo siriasi alitaka kwanza kumuadabisha balozi wao.
Mjumbe wa Hongmeng aliebakia ndio alipewa jukumu la kurudi Hongmeng na kutoa taarifa ya kile kilichotokea,
“Rudi ujinini na toa taarifa hizi , kama hao majini wanataka Dhana zangu , vidonge vyangu na mbinu yangu ya mafunzo basi waje huku nilipo wavichukue kwa nguvu kama nilivyofanya katika miliki ya Kekexil,likija swala la watu wenye nguvu kama haina haja ya kutii sheria za ulimwengu bali sheria ya msituni ndio itumike , atakae weza kuishi mpaka mwisho huyo ndio mtawala”
Baada ya kusema hivyo Roma alimbeba mzobemzobe yule Xuan Jizi na kisha kumtupia mbele ya walinzi akiwaagiza kwenda kumtupia mtaani huko kwani ashakua ni wa kawaida.
Alijua asingeweza tena kurudi Hongmeng kwani miliki hio haichukui majini wadhaifu kama yeye.
“Vipi kila kitu kimemalizika?”Aliuliza Afande Kweka mara baada ya Roma kuingia katika sebule ya kawaida na Roma aliishia kutingisha kichwa tu akiitikia amemaliza.
“Unajisababisha matatizo zaidi na zaidi juka uchao kulikuwa na haja gani ya kumuondolea nguvu zake za kijini?”Aliongea Afande Kweka bila ya kubadilisha muonekano wake , yaani hakuwa na furaha wala hakuwa na huzuni na hata usingizi hakuwa nao licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda.
“Babu hicho ndio kitu pekee ambacho unaweza kuongea”
“Unadhani ni kipi ambacho naweza kuongea , mwenyewe nipo najiuliza mambo ambayo yanaendelea katika hii dunia, nina hasira nyanya zangu zote zimekauka kutokana na baridi kali , hii baridi sijawahi kuiona na uzee wangu huu”Aliongea na kumfanya Roma amuone huyu mzee anaonekana kuficha mambo mengi na kila anachoongea ni kama anamwigizia lakini hakutaka kumhoji sana.
Huo ndio ulikuwa ukweli ugomvi wa Roma na majini ulikuwa ni wa kutisha lakini ulikuwa haukwepeki lakini kubwa zaidi ni kwamba Mzee huyo alitamani sana Roma kwenda kuwashambulia Hongmeng ili kulipa fadhila za Zenzhei kwa kumlinda kwa miaka mingi, ukiachana na hilo lakini pia Afande Kweka ni mwanachama wa umoja wa Ant- illuminat na ni juzi tu hapo alikuwa na kikao cha siri na baadhi ya wanachama na alikuwa akijua Edna ndio mkuu wake.
Yani kwa lugha nyepesi ni kwamba Edna ni mkuu mbele ya Afande Kweka lakinin mzee huyo licha ya kujua hayo yote hakuwa tayari kumwambia Roma kwani alijua itafikia siku yeye mwenyewe atakuja kujua ukweli na hata hivyo sheria za umoja huo hazikumpa ruhusa ya kuongea chochote kwani ingeharibu kabisa mipango inayoendelea.
“Babu nadhanni baada ya Hongmeng kupokea ujumbe wangu sitoweza kuendelea kuishi hapa Tanzania kwa muda , unaonaje na wewe ukielekea visiwani kwa muda , unaweza kuondoka na baadhi ya watu wako wa karibu pia”
“Unataka nitoke hapa Tanzania kwenda wapi na kwanini?”
“Si kila kitu kipo wazi mzee , sitaki waje wakukamate na kutaka kunitishia uhai wako kama chambo cha kunikamata”
“Mimi nipo nje ya maswala yote ambayo yanahusiana na maadui zako na sio kwangu tu hata kwa baba yako , kinachoendelea ni vita kati yako na majini na hayahusiani na ukoo wetu hivyo pambana kivyako”
“Unaongea tu lakini wanaweza wakapania sana na kutumia njia yoyote ile”
“Hata iweje nasema hapa siondoki “Aliongea kibishi.
“Kwannini sasa , huu sio muda wa kuonekana shujaa mzee”
“Mimi ni mzee wa taifa hili lakini pia mkuu wa familia ya Kweka , siwezi kuondoka na kwenda mahali pengine nje ya Tanzania, unaweza kutafuta chumba ulale , muda umeenda naenda kupumzika”Aliongea na kisha aligeuza na kuingia chumbani kwake.
Roma alikuwa na usingizi na wakati akiwaza kwenda katika chumba cha wageni kwa ajili ya kulala simu yake ilianza kuita mlio wa kuingia meseji na alipoangalia ilikuwa imetokea kwa Tannya.
“Master kuna kundi la majini wamefika na wanakuulizia hapa Bagamoyo”Ujumbe wa meseji ulisomeka hivyo.
“Naona hatimae wamejitokeza licha ya kwamba ni kwa kuchelewa kama nilivyotegemea lakini ni bora wamekuja kabla sijarejea katika ulimwengu wa majini watu”Aliwaza Roma
Sasa mara baada ya Roma kuona kwamba nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya mzee Sharif imejitokeza hakutaka kupoteza muda kabisa na shauku ya kutaka kujua Braki ni majini wa namna gani ilimvaa.
Roma mara baada ya kuondoka ndani ya eneo la Iringa dakika chache tu aliweza kufika mkoa wa Pwani katika makazi ya Sharif na aliweza kumuona Tannya akiwa amesima katikati ya ukumbi wa mikutano , ilikuwa ni eneo ambao hutumika kupokelea wageni mara nyingi.
Mbele yake kulikuwa na wanachama wa familia ya Sharif na mara baada ya kuwachunguza kwa umakini Roma aligundua hawakuwa wa kawaida wote walionekana kama waarabu hivi na hajawahi kuwaoana na walikuwa na nguvu za kijini.
Tannya tokea muda tu alikuwa amebadilisha wafanyakazi wote wa Sharif na kuweka wa kwake , ijapokuwa alikuwa mjapani lakini alikuwa mjuzi sana katika kuigiza na tokea siku ambayo amefika na kujifanyisha ni Maimuna hakuwahi kuonyesha dosari yoyote na hata ibada alikuwa akiongoza.
Roma kwa kutumia jani lake la upofu aliishia kujificha juu ya jengo hilo huku akihakikisha anasikia kinachoendelea kwa kutumia uwezo wake na majini hao hakuna hata mmoja ambaye aliweza kugundua uwepo wake.
Kulikuwa na majini jumla saba, wote walikuwa wamevalia kanzu kwa upande wa wanaume na wanawake wenyewe walikuwa wamevalia Abaya nyeusi , karibia wote walikuwa na muonekano wa ki utu uzima.
Kati yao mmoja tu ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa mafunzo ya kijini kwani alikuwa mwanzoni mwa maji ya kiroho. Na wengine wote walikuwa katika levo za maji ya barafu kushuka mpaka moto wa njano.
“Wewe ndio kiongozi wa familia ya Sharif katika ulimwengu huu unaefahamika kwa jina la Maimuna si ndio?”Mwanaume ambaye alikuwa na muonekano wa kizee alimuuliza Tannya , alikuwa na nywele nyeupe na ndevu nyeupe kama vile ni Nandra Modi waziri mkuu wa India na ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa kijini.
“Ndio , kwasasa mimi ndio nililazimika kuwa kiongozi , hivyo sina uhakika namna ya kuwaita kwani siwafahamu”Aliongea Tannya aliekuwa katika sura ya Maimuna.
“Hakuna shida kwani hata babu yako Sharif hana uwezo wa kututambua,kwa majina nafahamika kama Zando , nikiwa mwanachama kutoka makao makuu ya miliki , hapa kuna mzee Nuli na Yejini pamoja na majini wanne unao waona , tumekuja hapa kujua ni kipi kinachoendelea kwasababu hatukuweza kusikia habari zozote kuhusu mwizi alieiba hazina yetu , taarifa za kubadilika kwa kiongozi wa familia na imani ni zaidi ya matarajio yetu”












SEHEMU YA 739.
Katika moyo wake Tannya ukweli hakuwa akijua namna ya kujibu, ijapokuwa alikuwa akijua muda kama huo ungewadia lakini ndio mara yake ya kwanza kukutana na majini wa namna hio na angalau ni kwamba alikuwa tayari ashamtumia Roma ujumbe wa meseji.
Tannya simu yake ilitoa mnguruo mara baada ya kutaka kujibu na mara baada ya kuangalia aliona Roma alikuwa ametuma ujumbe kwa lugha ya kijapani.
“Tafuta njia yoyote upate taarifa zinazohusiana na wanakotokea na historia yao kwa ujumla”Aliongea Roma katika ujumbe huo.
Roma alitumia kijapani kwa kuamini ingekuwa ngumu kwao kuelewa kile alichokuwa ameandika.
Tannya mara baada ya kujua Roma ashafika hali ya kujiamini iliongezeka kidogo na palepale aliomba radhi
“Naombeni mniwie radhi wakubwa zangu, nilitamani pia kutoa taarifa kuja makao makuu lakini kwa bahati mbaya babu , walinzi na wengine walikufa vifo vya haraka sana na sikujua namna ya kuwasiliana na nyie hivyo…”
“Haina haja ya kujilaumu , hata sisi pia tunaelewa namna ilivyo ngumu kuwasiliana na sisi , umefanikisha kuongoza familia ndani ya muda mfupi na kuendeleza ibada taarifa hizi zikimfikia mkuu wetu atafurahi”Aliongea.
“Tafadhari naomba mniwie radhi kama nitavuka mpaka , lakini je mnaweza kunielezea historia yote ya familia pamoja na imani yake , ili mimi Maimuna niweze kuwa na uelewa mzuri na kufanya vizuri kwa ajili ya manufaa ya miliki kwa ujumla”
“Kwasababu umekuwa kiongozi pekee uliebakia basi ki asili umekidhi vigezo vya kujua historia yote ya Kibraki , Babu yako Sharif ana uelewa mdogo sana kuhusu jamii ya majini wa Braki pengine amewahi kusikia hili jina mara moja au mara mbili tu , lakini kutokana na mabadiliko ya hali na matukio ya kutotarajia hapa duniani makao makuu wameona ni sahihi familia za binadamu zinazotuwakilisha hapa duniani kujua uhalisia wa historia yetu na imani yote kwa ujumla, hivyo nitakuelezea kila kitu”
Roma ambaye alikuwa akipiga chabo alijikuta akifurahi mara baada ya kusikia kauli hio kwani hakutegemea jini aliefahamika kwa jina la Zando angeweka wazi kuhusu nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif.
*****
Miaka elfu hamsini iliopita dunia iliingia katika hatua nyingine kubwa katika ustaarabu.
Wakati huu pia upande wa majini walikuwepo pia na wengi wao walikuwa katika levo za juu sana pengine levo ambayo haijawahi kufikiwa katika nyakati za sasa.
Kipindi hiki ni kabla ya miungu kufika katika sayari ya Dunia na ndio kipindi ambacho majini wengi walianza kupotea katika uso wa dunia na kuwaacha binadamu na baadhi ya majini watu.
Majini ni vumbe ambavyo vipo vya aina nyingi sana na tabia tofauti , ni kama ilivyo kwa makabila ya kibinadamu basi ndio ilivyo kwa majini hivyo hivyo.
Sasa kati ya majini wa enzi hizo ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uso wa dunia ni majini pepo na hawa majini pepo wenyewe walikuwa wamegawanyika katika aina nyingi sana.
Inasemekana katika kipindi hichi majini walikuwa wengi kuliko hata idadi ya binadamu kutokana na spidi yao ya kuzaliana.
Kati ya majini pepo ambao waliweza kufahamika enzi hizo ni kama vile Mbweha na Majoka ambao ndio walikuwa na uwezo mkubwa sana .
Majinii jamii ya Mbweha walikuwa ndio wenye busara kubwa na mbinu nyingi za kimaajabu tofauti hata na majini Joka ambao walikuwa wamezaliwa na nguvu za kimwili sana sana.
Ukiachana na majini hao lakini pia majini watu hawakuwa nyuma pia kwani wengi wao walikuwa katika levo za juu kwa kuweza hata kudhibiti radi na ilikuwa ni kawaida kwa majini watu kuweza kumiliki Dhana za hali ya juu kabisa na shida ilikuwa tu kwamba licha ya uwezo wao hawakuweza kupata mbinu ambayo inaweza kuwainua zaidi na zaidi.
Hawa majini watu ndio ambao walipenda kuwa wa wazi kabisa na waliweza kuishi katikati ya binadamu wa kawaida tofauti na majini pepo ambao walikuwa ni hatari kabisa kwa binadamu.
Majini pepo waliishi katika maumbo yao ya kawaida pasipo ya kubadilika na ukweli ni kwamba walikuwa wakitisha sana na hali hio ki ufupi ni kwamba hawakuipenda na hii iliongeza chuki yao zidi ya binadamu na majini watu.
Lakini mwishowe walijitahidi kutafuta namna ya kuboresha muonekano wao ndipo walipokuja kugundua mbinu mbadala ambayo ilikuwa ni kuamsha pepo wao wa ndani tofauti na kuwazimisha au kuwakata kama ilivyokuwa kwa majiini watu ,hapo sasa ndio ikazaliwa majini halisi ambao walikuwa na nguvu za kijini, majini ambao walikuwa na uwezo wa kupaa.
Sasa kutokana na kuwa na maumbo yenye nguvu kubwa pamoja na kumiliki nguvu za kijini pamoja na kuwa wengi walikuja kuwa tishio kubwa kwa jamii nyingine za kijini na binadamu wa kawaida kiasi cha kupelekea kuibuka kwa vita ambayo majini watu waliungana na binadau kuwashambulia Majoka.
Sasa kati ya majini pepo wakaja kuibuka jamii nyingine kati ambao walijiita mashetani pepo wa anga , hawa ndio walikuwa wabaya zaidi kwani walikuwa na uwezo wa kumuingia binadamu na kumfanya afanye kila anachotaka huku wale majini pepo wengine wakichinja binadamu na kunywa damu yao.
Binadamu alionekana kuingia katika hatari na kuanza vita na viumbe hawa majini ,vita ambayo ilidumu kwa muda mrefu sana takribani miaka mia moja na siku moja tu ilitokea majini pepo wengi katika ulimwengu wa kawaida kuanza kupotea ikiwemo Mbweha na Majoka.
Kupotea kwao baadae ilikuja kujulikana walikuwa wakivutwa katika ulimwengu mwingine kwa kutumia aina ya mitego ambayo ilikuwa imewekwa mfano wa mnara ambao Roma aliingia.
Ni asilimia chache tu ya majini pepo ambao walibakia na kati yao hawakuwa hata na uwezo mkubwa na hapo ndipo majini watu wa enzi hizo walipoona hakuna haja ya kuwaua bali kwenda kuwafungia katika ulimwengu Tenganifu wa jangwa.
Kitendo cha mashetani pepo wa anga, Majoka na Mbweha kufungiwa katika ulimwengu wa Jangwa Tenganifu kwa muda mrefu iliwafanya kuchukulia hapo kama makazi yao rasmi.
Mara baada ya kuwasili kwa miungu katika uso wa dunia ndipo ilipoibuka vita kati ya majini watu yaani Hongmeng na jamii nyingine za kijini , vita ambayo ilidumu muda mrefu sana mpaka Zeus na Athena kushindwa vita na kuzaliwa kwa the Gods treaty.
Mpaka vita hio inakuja kufikia mwisho majini pepo ambao walikuwa katika ulimwengu wa jangwa tenganifu walikuja kugundua miliki za majini watu walikuwa wamepungukiwa nguvu sana kutokana na kupigana vita na miungu na wengi wao kuuliwa na hapo ndipo walipoona ni fursa adhimu ya kujiendeleza wao wenyewe kutokana na kipindi hicho majini watu kutokuwa nao makinu.
Mbinu pekee ambayo iliwafanikisha kujiendeleza ni kufanya ushirikiano wa kiimani na binadamu wa ulimwengu wa kawaida taratibu taratibu kwa namna ambayo waliweza wao na mwisho wa siku wakajikuta wanakuwa na nguvu kubwa kwani walijipatia mali asili nyingi kutoka Duniani na kuziingiza katika ulimwengu wao huku wakibadilishana na binadamu madini mengi ya thamani.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba majini pepo wengi ikiwemo majoka na Mbweha ambao walikuwa na uwezo mkubwa walimezwa katika ulimwengu wa majini pepo kwa njia ambazo mpaka siku hio hawakuelewa imetokeaje , huku upande wa majini watu , yaani majini wa kawaida ambao mbinu zao sio kuamsha mapepo wao walijitenga na binadamu wa kawaida mara baada ya kugundua Dimension nyingine na kuanzia hapo kila majini wakajitegemea na kukawa na ulimwengu wa majini watu , ulimwengu wa majini pepo na ulimwengu wa Jangwa Tenganifu sehemu ambayo hupatikana miliki moja tu ya kijini ambayo hufahamika kwa jina la Braki.
Kwa historia hio ilimaanisha kwamba hapo zama za kale majini na binadamu waliishi katika ulimwengu mmoja kabla ya vita kutokea, vita ambayo mpaka wakati huo majini wote wanajiuliza ilimalizwa na nani kwani sio wao ambao waliwafanya majini pepo wenye nguvu kuvutwa kwenye ulimwengu mwingine.
Sasa kati ya majini pepo hao ambao walivutwa ni kama vile Aoiline Mbweha wa mikia tisa , Majoka na mashetani pepo wa anga.
Roma mara baada ya kusikia habari hio aliishia kushangaa , katika ulimwengu wa majini pepo Zimo alisema ulimwengu wao ulikuwa ni wa miaka mingi kuliko hata Hongmeng na hio ilimaanisha kwamba kabla ya kumezwa ulimwengu huo ulikuwepo.
Sasa Roma mara baada ya historia hio anajua nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif ni majini pepo na ni sawa na kusema ni ndugu wa Aoiline.
Kulinganana msaada ambao Aoiline alimfanyia na wengine Roma aliona ni dhambi kama ataingamiza miliki hio ya Braki ambayo inapatikana katika Ulimwengu wa Jangwa na anachopaswa ni kujaribu kufanya urafiki nao lakini kabla ya yote lazima ajue hazina yao ilikuwa ikimaanisha nini.
“Asante sana kwa kunielezea haya”
“Hivyo licha ya familia ya Sharf kuumiza watu wengi katika ulimwengu huu wa kawaida lakini kwa upande wetu sio jambo kubwa sana na sio maagizo yetu , Sisi sio kama majini kutoka Hongmeng na miliki nyingine ambao wanachotaka ni umaarufu tu , sisi leo tumetoka kuja katika ulimwengu wa kawaida kwasababu ya muovu Roma Ramoni ambae ameiba hazina yetu”
“Je naweza kuuliza, Hazina hio ina matumizi gani , je kutakuwa na athari zozote kama isipokuwa kwenye mikono yetu?”Aliuliza Maiuna feki na hapo ndipo Roma alipokuwa akitaka kujua ile kokoto ina maana gani.
ITAENDELEA ,WATSAPP 0687151346
Aaaiseeeee...ila mimi nikifika sehemu ambayo kina Nadia nakuwa makini sana kupita maelezo.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 735
Callum waziri mkuu wa Uingereza alikuwa akimjua Roma na uhusiano wake na Edna pamoja na Raisi Jeremy , idara ya usalama ya Uingereza haikuwa kwa ajili ya maonyesho tu walikuwa wakijua mambo mengi.
Lakini hata hivyo hakuwa akijua nia halisi ya Raisi Jeremy kuja mpaka hapo lakini kwasababu ni swala ambalo lilikuwa linahusiana na Roma hakutaka kuvuka mipaka yake hiyo alijitahidi kuwa makini.
“Hakika una ushawishi mkubwa Raisi Jeremy , kuja London tu umeweza kutupata mara moja?”Aliongea Catherine akionekana kumtania raisi Jeremy, licha ya kwamba hawajawahi kukutana lakini bado alionyesha hali ya kumdharau pengine ni kutokana na kutokea taifa dogo.
“Nimesikia habari za kutosha kuhusu malkia wa Wales lakini sikutegemea kukuona hapa ,nipo hapa kwa ajili ya kikao cha umoja wa mataifa kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa dunia nzima na mara baada ya kusikia habari za binti yangu na mume wake wapo hapa nikaona sio mbaya kuwatembelea”Aliongea huku akiwa na uso uliopambwa na tabasamu.
Maelezo yake yalikuwa kamilifu na ilimfanya kuonekana kama vile alikuwa na ukaribu sana na Roma pamoja na Edna.
Baada ya salamu wengine wote walitoka nje na kumuacha Roma na familia yake ndani ya chumba hicho cha VIP.
“Kama upo hapa kwa ajili ya kunifanya nikutane na mkuu wako wa miliki basi sahau maana sina mpango wa kuonana nae kabisa , kama anataka sana kuonana na mimi basi mwambie aje huku yeye mwenyewe”Aliongea Roma na kufanya tabasamu la raisi Jeremy kupotea mara moja.
“Roma kuna haja ya kuwa hivyo mbele yangu , ninaweza nikawa nilifanya makosa lakini yaliopita si ndwele na isitoshe hatuna vinyongo kati yetu , nilifanya mambo yale kwasababu ya kutaka wewe na Edna kuishi kwa furaha”
Wakati wa kuongea alikuwa akimwangalia Edna kwa sura ya kumwambia amsadie kumuomba mume wake lakini Edna alionekana kumpotezea.
“Usingekuwa hai mpaka sasa kama sio kwa uhusiano uliopo kati yako na Edna , hiyyo acha kuzunguka zunguka na sema kilichokuleta”
“Sawa nitaenda moja kwa moja , mkuu wa miliki ya Panas anataka kuongea na wewe , kama utakataa kwenda katika miliki au kwenda Rwanda yupo tayari kuongea na wewe kwa njjia ya vidio Call , ukikataa kusikiliza utakuja kujutia baadae”
Ijapokuwa ulimwengu wa kijini ulikuwa ukijitegemea lakini majini waliokuwa wakiishi huko walikuwa na uwezo wa kufanya mawasiliano na ulimwengu wa nje bila shida yoyote kutokana na teknolojia ya ajabu ambayo iliasisiwa na mababu wa miliki hizo.
Kuhusu Roma hakushangazwa na maneno yake kwani alikuwa ashajua kiasi kuhusu miliki hizo za kijini hiyo aliamini ilikuwa ikiwezekana.
“Kama ni hiyo niunganishe nitaongea nae"
Raisi Jeremy alijisikia furaha na kujivunia huku akijiambia pengine Roma alikuwa akiogopa miliki ya Panas.
“Nifuate nje tutafute sehemu nzuri kama ni hiyo , kuna watu wengi hapa”
“Hakuna haja , hawa wote ni marafiki zangu na familia yangu hiyyo sio lazima kuficha kitu kwao, labda kama mheshimiwa Jeremy anaogopa kugundulika ana uhusiano na majini?”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la uchokozi.
Baada ya kusikia maneno hayo hakutaka kusita tena na alitoa kishikwambi cha aina yake na alianza kukipangusa na ilionekana Panas walikuwa washajiandaa muda mrefu kupokea simu hio.
Sura ya jini Gefu iliweza kuonekana katika kioo cha kishikwambi hicho na alikuwa ndani ya ofisi yake.
“Sir, Mr Roma Ramoni yupo hapa tayari kwa kuongea na wewe”Aliongea Jeremy kwa sauti ya unyenyekevu huku akiwa amepamba uso wake na tabasamu.
“Sikutegemea kukutana kwetu kwa mara ya kwanza kutakuwa kwa namna hii , Roma hakika ni ngumu sana kukupata”Aliongea Gefu akiwa na tabasamu.
“Oh! Kumbe mkuu wa miliki ya Panas ndio upo hiyyo ..”Aliongea Roma lakini upande wa pili Gefu hakuelewa Roma anachomaanisha.
“Nilikuwa na haja ya kuonana na wewe kwa haraka kwasababu nina jambo muhimu napaswa kukuambia linahusiana na usalama wako na wanaokuzunguka”
“Unajaribu kumaanisha kuna kundi la majini ambao wanataka kuniua muda si mrefu?”
“Ndio , kwasasa ni kama unatembea juu ya barafu nyembamba, lakini sio tu kwmaba najua maadui zako wote lakini pia nipo tayari kukusaidia”
“Haina haja , sijakubaliana kuongea na wewe ili kusikia unaongea upumbavu”
“Nini!!. Roma unamaanisha nini kuongea hivyo au huamini maneno yangu?”
“Sio maswala ya kuaminiana, mimi nilitaka tu kujua mkuu wa miliki ya Panas anaonekana ipi ili nikiivamia miliki yenu nisipate shida ya kukutafuta na kukuua”
Ishara ya hasira iliweza kuonekana katika uso wa Gefu mkuu wa miliki ya Panas lakini fasta sana alirudi katika hali yake.
“Kijana mdogo chunga kauli zako naamini haipaswi kuwa na ugomvi kati yetu”
“Nyie ndio mliovujisha taarifa ya Rufi kuishi Tanzania kwenda kwa miliki ya Xia , hio ni sababu tosha ya mimi kutaka kuivamia miliki yenu na kulipa kisasi kwa umbea wenu”Aliongea Roma bila ya ishara ya utani.
Maneno yake ya kibabe yalimshitua Master Namba nne huku akijiuliza Roma alijuaje yeye ndio alivujisha taarifa.
“Kwa muonekano wenu inaonyesha nilikuwa sahihi , kama ifahamikavyo ukuu wa miliki ya Panas katika kujua kinachoendelea kwenye ulimwengu wa kawaida”
Upande wa Gefu alijua Roma hakuwa na ushihidi hivyo hakutaka kukamatika kizembe na alijua pengine Roma anamjaribu.
“Unathubutu ipi kunijaribu wewe bindamu?”
“Kwahio unatakaje?”
“Unafikiri tunakuogopa , tunakupatia nafasi ya mwisho ya kuungana na Panas, kwasasa umekuwa adui wa miliki ya Xia ,Kekexil na Braki , unadhani kujificha huko nje ya nchi kunaweza kukufanya ukawa salama na miungu wenzako dhaifu kukusaidia?”Aliongea kwa kufoka.
“Braki!!!”
Roma sura ilijikunja mara baada ya kusikia anahusishwa na Braki na kujiuliza Braki ndio kitu gani lakini Gefu alionekana kujua kinachoendelea kupitia sura ya Roma.
“Unajisikiaje kutokujua baadhi ya maadui zako?”
Roma hakujibu swali na badala yake palepale alipiga chini kile kishikwambi na kupasuka pasuka vipande vipande.
“Siogopi kiumbe chochote mimi , kama kuna adui anajiona mbabe anitafute tumalizane”Aliongea Roma na palepale macho yake yalisinyaa wakati wa kmwangalia Jeremy.
“I am not in a good mood , so get lost now when I still give a damn about your relationship with my wife”Aliongea akimaanisha aondoke wakati anajali uhusiano uliopo kati yake na mke wake.
“You .. you are Vexing … kwa ajili ya Edna!?, Roma nataka nikupatie ushauri … sisi binadamu tunao wajibu wa kufuata sheria za hii dunia , kila mtu yupo chini ya sheria na kila mtu atakushambulia kama utazivunja kutokana na ukiburi wako na wakati hayo yanatokea hakuna ambaye atakusaidia”
Baada ya kuongea kauli hio palepale licha ya kuwa na hasira zake aliondoka ndani ya eneo hilo , kwani alijihisi kutamani kumuua Roma ni hivyo tu uwezo huo hakuwa nao.
Mara baada ya kuondoka Roma alisimama na kusogelea dirisha na kuangalia upande wa uwanjani ambako mechi ilikuwa mapumziko , huku hali ya hewa ikiwa sio ya kawaida ndani ya eneo hilo kwani watu wake wa karibu wote walionekana kuwa na wasiwasi.
Bila kujua Roma alikuwa amejiongezea adui mwingine ambaye hamfahamu anaefahamika kwa jina la Braki.
Ukweli ni kwamba alikuwa na maadui wengi ambao hakuwa akiwajua na baadhi yao walitokana na wanawake wake na wengine walikuwa wakimchukulia kama adui kutokana na kuwa na uwezo mkubwa.
“Rufi unajua chochote kuhusu miliki ya Braki?”Aliuliza Roma mara baada ya kujituliza.
“Sijawahi kuisikia , Nanny ushawahi kuisikia?” Rufi alionekana kutokukujua na alimtupia swali Sui lakini hata yeye alionyesha kutokujua chochote.
Ijapokuwa ilikuwa ikihusiana na ulimwengu wa majini lakini kutokana na ukawaida wao hawakuwa wakiijua.
“Mimi nadhani Braki inahusiana na familia ya Mzee Sharif , si ulisema walishawahi kuleta majini wengi kupambana na wewe , nadhani tufikirie hivyo kwa sasa?”Aliongea Rose na Roma alitingisha kichwa baada ya kuona alikuwa na pointi .
“Hubby unataka kweli kwenda kuivamia miliki ya Panas?”Aliuliza Edna ambaye alikuwa amekunja sura.
“Hautaki niende?”
“Nili…”
“Edna siwezi kukusikiliza awamu hii , kila kitu kingekuwa sawa lakini katika vitu ambavyo vinahusisha uhai wa wengine sitokuruhusu ubadilishe mawazo yangu”
Edna mara baada ya kuona usiriasi uliopo katika macho yake alishia kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Sijasema nataka kukuzuia , nikwamba naona itakuwa hatari sana”
“Tatizo hata kama niseme nisiende kuwavamia na kuwasambaratisha najua hawawezi kutulia na watatafuta tu namna ya kutaka kuniua … Hili ni daraja ambalo napaswa kuvuka na nikishapita kila kitu kitakuwa kimekwisha”Aliongea.
“Roma sidhani kama itakuwa ni rahisi, tayari tuna uadui na miliki tatu za kijini kubwa na tuna maadui maelfu na maelfu , unadhani ni sawa kuua na kuendelea kutengeneza maadui? , mimi naona labda hakuna haja ya kuua na tunaweza kutatua haya matatizo kwa njia nyingine , wao wanasheria zao pia na pale wanapojihakikishia kwamba huwezi zivunja hawawezi kukufanyia chochote”Aliongea Sophia.
“Sophia unaongea ujinga , hivi unajua tafsiri ya sheria mbele ya watu wenye nguvu ni tofauti na inavyotafsirika mbele ya watu dhaifu?”
Aliongea Roma na kisha alinyoosha kidole kuelekea uwanjani wakati wachezaji wakitoka katika vyumba ya mapumziko kwa ajili ya kuanza kwa kipindi cha pili.
“Hivi unajua ni kwasababu gani mpira wa miguu ni maarufu sana duniani na kwanini watu wengi kama hivi wanaupenda?”
Wanawake hao wote waliishia kushangaa tu wasiweze kuelewa swali lake,walijiambia wanaongea topiki ya hatari hiyo kuna haja gani ya kuhusisha mpira wa miguu lakini Roma alionekana kutojali mawazo yao.
“Ni kwasababu katika mechi ya mpira haijalishi timu ni bora kiasi gani au ni dhaifu kiasi gani lakini siku zote matokeo yanaanza sifuri kwa sifuri na mpira unachezwa kwa sheria, hii inamaanisha kwamba haijalishi timu ni dhiafu lakini kama watakuwa tayari kupambana katika kukaba kukimbia na kufunga hata wao pia wanaweza kuwa mabingwa , kwa maneno mengine hapo ndio wakati watu ambao sio wachezaji ndio wanajipatia riziki , sehemu ambayo uvumiliu wao huonekana , katika uwanja mshindi ndio bingwa hata kama ni dhaifu au alipendelewa kwa namna yoyote ile ili mradi tu ameifunga timu bora na yenye nguvu hata kama ni mara moja katika historia yake , hii inamaanisha kwamba wao pia wanayo nafasi ya kuwa nyota na hii ndio maana mpira wa miguu ni wa kuvutia sana”Aliongea na kisha akavuta pumzi na kuendelea.
“Lakini unadhani hio ni sawa kati ya wachezaji na wamiliki wa timu au wasimamizi wa mashindano? , ingawa mechi inaanzia sifuri kwa sifuri lakini kwa matajiri na wasimamizi wa UEFA mambo ni tofauti , kwao haijalishi nani anashinda bado watapiga pesa na kupata faida na ipo hivyo siku zote , kwa mfano mchezaji katika timu kama akishindwa kutoa ushirikiano wa maelekezo viongozi wanaweza kuto kumjumuisha katika mechi na kutoa sababu kama vile ni majeruhi au haendani na mfumo na mengineyo .. ,kwa lugha nyepesi ni kwamba wanaoendesha michezo na timu ndio wenye maamuzi ni taarifa gani iwafikie mashabiki na kuamua mchezo uwe vipi , unaweza kuona mechi kabisa hii mshindi ni wa kupangwa lakini wewe kama shabiki utafanya nini tofauti na kuongea ongea na kugoma, hakuna cha ziada ambacho unaweza kufanya kwasababu kwa nje wewe unaburudika na wachezaji wakicheza mpira lakini kwa ndani kuna mfumo ambao umetengenezwa kwa ajili ya kurahisisha maswala mengi aidha yawe ni ya kifedha au Ajenda zao za kijamii labda tu kama watu waache kuangalia mpira .. na huu ni mfumo endelevu na utaendelea hivi labda siku tu watu dunia nzima waseme hawaangalii mpira tena , sasa hili halipo kwenye mpira tu kila michezo maarufu yote wewe kama shabiki utaona ni burudani lakini nyuma ya pazia kuna mfumo..”
“Ndio inaweza kuonekana yanayofanyika ni uchafu lakini maisha ya kibinadamu tokea mwanzo yalianzia katika uchafu , sasa tuseme mimi ni kama mchezaji , Kocha au tuseme timu nyenye nguvu ambayo imepata umaarufu hivi karibuni, viongozi waandamizi na matajiri wote macho yao yatakuwa kwangu kwasababu mbili tu; mosi nifanye kazi kwao na niwasaidie kupata pesa au kutimiza ajenda zao , pili hawataki niwasaidie wengine kupata pesa, kwa maneno mengine ili nipate faida lazima na wao wapate faida na sasa hapa hizi ndio sheria ambazo wameweka ambazo hawataki mchezaji kuzivunja kwasababu zinaathiri utajiri wao pamoja na ushawishi wao”
“Kama nitafanya kazi nzuri kama mchezaji wataniacha niendelee kuishi kama mchezaji na kunifanya niendelee kuwa maarufu na watanipatia Ballon d‘or au Kiatu cha Dhahabu au watafanya hata timu yangu ya taifa kuwa bingwa wa dunia au club yangu kuwa bingwa wa UEFA na kama sitofanya vizuri au nikikataa matakwa yao watahakikisha wananizimisha aidha kwa kuniundia mchezaji uwanjanni ambaye atanijeruhi au kuanza kunitengenezea Zengwe nyingi tu ili kunitoa mchezoni hizi ndio sheria ambazo wameweka .. wakati nikiwa chini hawakuwa na habari na mimi na hawakuwahi kunichukulia siriasi lakini sasa nimekuwa tishio kwao hawataki kuzembea, hii haipo kwenye mpira tu kwa kila nyanja kuna huu mfumo na ambao wanasuka mipango hii ya kimfumo hawatojionyesha kamwe mpaka sekunde ya mwisho , isitoshe lazima wahakikishe mchezo ulikuwa ni wa haki”
Kila mmoja alijikuta akiwa kimya na kuangalia uwanjwani ambako mechi ilikuwa ikiendelea.
Maneno ya Roma yanaweza kuonekana kama yamebase upande mmoja lakini yalikuwa yamejaa ukweli mgumu(Harsh truth).
“Ijapokuwa hatuwezi kushiriki katika vita yako lakini kama mtu ambaye unapambania maisha ninaelewa hisia zako”Aliongea mmoja wapo na kumfanya Roma kuonyesha shukrani na palepale alimbeba Lanlan na kumpakata.
“Sina chaguo nyingine , kwasababu mpaka sasa hawaniangalii kama mtu Dhaifu , kama ninataka kuendelea kuishi ni aidha nishirikiane nao au kama sitaki kushirikiana nao niwaweke chini yangu kwa kuwapiga na kisha kuweka sheria zangu mimi”Aliongea na kisha aligeuza macho yake na kuangalia warembo wake waliokuwa wakimwangalia kwa macho ya matamanio na kisha akageuzia macho kwa Lanlan.
“Sio mimi tu lakini ni kwenu pia na kwa mtoto wangu”Aliongea Roma kwa sauti hafifu akionekana kama vile ni mtu ambaye anakumbukia maisha yake yaliopita na kitendo kile kilimfanya Blandina kukosa ujasiri wa kuendeea kusikiliza na machozi yalimtoka na kwenda kumkumbatia Roma na Lanlan na kuanza kulia.
Kila mmoja alijua hisia za Blandina zinatokea wapi , ilionekana alikuwa na hatia kama mzazi na kumfanya mwanae kupitia magumu mengi lakini kwa wakati huo machozi yake hayakuwakilisha huzuni tu lakini bali kujivunia kwa mafanikio ya mtoto wake.
Ukumbuke hapa ni ndani ya Chumba cha VIP ndani ya uwanja wa Wembley hivyo ni kama wamejitenga na mashabiki wengine.
Unadhani Roma yupo sahihi , ni kweli kuna mifumo ambayo imewekwa kwa ajili ya kushikiria mafanikio ya watu??






SEHEMU YA 736.
Ni upande wa Tanzania jijini Iringa muda wa mchana katika makazi ya Afande Kweka kulikuwa na kikao cha siri kilichokuwa kikiendelea.
Kikao hichi kilikuwa kikijumuisha watu kama saba hivi ambao ni Paster Cohen, Mellisa , Phill Knight , Nadia Alphonso , Suzzane , Linda na mwanamama mrembo kutoka Hungury afahamikae kwa jina la Zoe Kovacic.
Nadia ndio ambaye alikuwa akionekana kusoma ripoti licha ya kwamba kila mmoja ambaye alikuwa hapo ndani alikuwa ameshikilia kishikwambi, ilionekana ni kama vile walikuwa wakirudia kile ambacho Nadia alikuwa akisoma.
“Mzee kama mwanachama mkongwe wa jamii yetu, viongozi wameniagiza nikuelezee kuhusu ubini wa kiongozi wetu”Aliongea Mellisa kwa lugha ya kingereza.
“Kiongozi amekwisha kupatikana?”
“Ndio Komredi katika kikao cha mwisho kilichofanyika Saudi Arabia tumeweza kupata mawasiliano na Kiongozi kwa mara ya pili”Aliongea Pastor Cohen na kumfanya Nadia kuangaliana na Suzzane.
“Kulingana na Kalenda ya jamii yetu kiongozi alipaswa kufanya mawasiliano na viongozi wa juu ndani ya tarehe husika , ijapokuwa ilikuwa ni hatua ya pili ya kumthibitisha kama kiongozi, umoja umefurahi kwamba mpango A wa kalenda ulitimia na kwanzia tarehe hio Edna Adebayo anatambulika kama kiongozi wa Umoja wa Ant-Illuminat”Aliongea Mellisa na kumfanya Linda kuonyesha mshangao huku Afande Kweka yeye macho yake ya kizee yakichanua.
“Komredi ni kama tulivyotarajia”Aliongea Pastor Cohen.
“Kuna maswali mengi juu ya hili Komredi nilijua kiongozi ni Seenteen kulingana na maelezo yako Komred”
“Wote tulidhania kiongozi anakwenda kuwa Seenteen, kuna maswali mengi juu ya hili lakini kulingana na maelekezo ya mwasisi wa umoja wetu anasema Kalenda inakwenda kujibu maswali yote lakini ni Aidha kama Binadamu tutafanikiwa kuishinda vita na Miungu”.
“Viongozi wengi pia hawakuamini kama siku ya kikalenda Edna angefanya mawasiliano na sisi lakini ajabu alifanya hiyo na kila mmoja alishangaa lakini imeondolea umoja harakati za kuona mchoro wa Unabii?”
“Huu mchoro wa Unabii unaonyesha kitu gani , kwanini imekuwa kitu muhimu kwa pande zote mbili Mellisa?”
“Hatuwezi kujua kwa uhakika mchoro huu unamaanisha nini na nani anaonekana katika picha lakini makisio yetu ni kwamba mchoro huu unahusiana na kiongozi wa umoja wetu”
“Kwa taarifa za Shekh Assad ni kwamba mchoro huu pia una umuhimu kwa Illuminat na ndio kiongozi ambaye wanamsubiria, kama usemayo ni sahihi Edna ana uhusiano na huu mchoro wa unabii lakini si inamaanisha kwamba pia ndio kiongozi wao ambaye wanamtarajia kulingana na unabii?”
“Upo sahihi Zoe lakini kwasasa hata Illuminat wenyewe bado hawajaweza kuona mchoro huu wa Unabii kwani upo chini ya Vatican”Alijibu Mellisa.
“Madam kuna uwezekano wa Edna kuwa Seventeen?”Aliuliza Nadia.
“Kulingana na mpango ulivyokuwa , Seventeen ni zao la mpango LADO kama alivyo Roma Ramoni lakini majukumu yao tokea mwanzo yalikuwa ni tofauti , ijapokuwa mpaka sasa hivi hatujui Seventeen yupo hai chini ya Zeros lakini tokea mwanzo Seventeen ndio alikuwa ni msingi wa kufanikiwa kwa Ant-Illuminat”
“Kama ni hivyo kwanini Edna ndio awe kiongozi , sijawahi kuona ishara yoyote ya Edna kujua chochote kuhusu Ant- Illuminat?”Aliongea Suzzane.
“Ukweli ni kwamba tunaamini Seventeen amekwisha kufariki mpaka sasa chini ya maagizo ya Athena na kwa maelezo ya Chriss ili mchoro wa unabii kukidhi vigezo vya ki’unabii hakupaswi kuwa na uwepo wa watu wawili wenye sura zinazofanana”Aliongea Mellisa.
“Melllisa hili linajibu kilichopo kwenye mchoro huo wa Unabii , kama kweli maneno ya Chriss ni sahihi basi kuna uwezekano Mchoro wa Unabii unaonyesha sura ya Edna au Seventeen lakini kwasababu ni unabii wa mtu mmoja basi moja kwa moja mmoja wapo lazima atoweke”
“Naunga hoja ya Komredi lakini kwangu bado swali linaibuka Athena ni nani na kwanini mchoro wa Unabii kuwa na sura ya Edna , wote kati yetu tunajua mpango wa Athena ni nini zidi ya binadamu na hatari ya mipango yake kufanikiwa?”
“Afande mpaka sasa hatuwezi kujibu maswali lakini pia hatuwezi kufanya makisio kwani ipo kalenda ambayo inatuongoza ambayo haijawahi kufeli na hata pale ilipofeli kulikuwa na mpango B, nadhani wote tuamini katika Kalenda”
“Naunga hoja ya Mellisa akini je wakuu wanasemaje kuhusu hali inayoendelea kwa sasa?”Aliuliza Phill.
“Unazungumzia kushuka kwa joto la dunia?”Aliuliza Zoe na kufanya kila mmoja kumwangalia mwenzake kwa shauku kubwa ya kusikia jibu.
“Kulingana na Kalenda tukio muhimu ambalo ndio ishara kubwa ya hatua muhimu ya Athena kuchukua lakini vilevile hatua ambayo Umoja wetu unapaswa kuchukua ni kuona majira ya theluji katika bara la Afrika, nadhani hali hii ya hewa tunaelekea kuona ishara hii hivi karibuni hivyo tunaweza kusema mpaka sasa tunaingia katika hatua muhimu sana katika umoja wetu na kwa dunia kwa ujumla , hiki ndio ambacho viongozi waeniusia nikiseme katika kikao hichi na sio hapa tu dunia nzima vikao vya ajenda hii kwa wenzetu vinaendelea”Aliongea Mellisa.
“Mellisa yupo sahihi kushuka kwa joto la Dunia sio nchi moja bali ni dunia nzima lakini ni Afrika pekee ambayo inaonyesha joto kupungua taratibu sana , hii inamaanisha mpaka nyakati za theluji zikitufikia kuna uwezekano baadhi ya maeneo ya Dunia joto kushuka sana kiasi cha kuathiri maisha ya binadamu”
“Nadhani ndio maana Wanachama wengi wa Freemason na Illuminat wamenunua maneo mengi ndani ya Afrika kwa kipindi cha hivi karibuni huku wakifosi sheria nyingi za kimataifa kupitishwa , hii inaonyesha walikuwa wakiandaa mazingira rafiki kwa ajili ya kuishi wakiwa huru”Aliongea Zoe.
“Hii ni kweli na ni swala ambalo tulikuwa tukipambana nalo kama umoja,kuna baadhi ya mataifa ambayo tumeyachagua kama nguzo muhimu ya Umoja kwa ajili ya kulinda tamaduni zake ikiwemo Tanzania lakini kuna maeneo ambayo pia ndani ya Afrika yapo chini ya Illuminat na ushawishi wao ni wa juu na hili hatuwezi kulifanyia kazi kwani litaibua migororo”
“Nadhani naona unachojaribu kumaanisha Miss Mellisa , ni miezi kadhaa iliopita mataifa zaidi ya kumi ya Kiafrika yamepitisha sheria ya Ushoga kuwa huru hili ni swala ambalo linahusiana na ulichosema”
“Upo sahihi Linda , Tanzania ilikuwa ni nchi ambayo ingekuwa ya kumi na moja kutangaza hii sheria kama sio sisi kuingilia , shukrani kwa Suzzane na Nadia wameweza kutiisha misheni yao vizuri na sasa Tanzania imekuwa Neutral kwa sisi pamoja na wao”
“Urusi wanazungumziaje hili?”Aliuliza Afande Kweka.
“Wapo ndani ya mfumo , wanaweza kupinga wazi lakini ni taifa ambalo limegawanyika katika pande mbili”.
*******
Pumbavu zako Roma Ramoni , nitakuua tu siku moja”Aliongea Gefu kwa sauti kubwa na kwa hasira zake alipelekea kuharibu kila kitu kilichokuwa ndani ya ofisi yake lakini bado haikuwa ikitosha kutuliza hasira zake.
Mbele yake alikuwa ni Master Namba nne na mwingine mmoja ambao wote walikuwa katika hali ya wasiwasi kutokana na hasira za kiongozi wao mara baada ya kumaliza maongezi yake na Roma Ramoni.
Ilikuwa ni mara chache sana kwa Gefu kuwa katika hasira kama hizo , kitendo cha Roma kumdharau waziwazi mara nyingi mfululizo kilimfanya chuki yake kuongezeka maradufu.
“Kaka punguza jazba, ni sawa tu kama amekataa kuungana na sisi na kwasababu maadui zake ni pamoja na Braki lazima atakufa na sisi ndio tutachukua fursa hio ya kummalizia akiwa chini kabisa”
“Hawa majini kutoka Braki hawajawahi kuwepo katika uso wa dunia kwa zaidi ya milenia moja , nimesikia kutoka kwa wazee wanasema hawajui kabisa uwepo wa binadamu mwenye uwezo mkubwa kama Roma , Roma huyu mjinga amejitengenezea uadui na hawa mashetani ambao walikuwa wameshasahaulika”
“Namba nne fanya mawasiliano na Jeremy kusitisha mipango yetu yote ya kimsaada na Tanzania hususani familia ya Raisi Senga na kisha atasubiria maelekezo yangu ya mpango wa pili unaofuatia , pia tuma barua kwenda katika miliki zote zenye uadui na Roma hususani katika miliki ya Xia na Kekexil na waambie kupitia mashushusu wetu waliopo katika kila pande ya dunia ya kawaida watasaidia kujua nchi ambayo Roma anaishi na familia yake na kama wanahitaji msaada watuambie”
“Sawa kaka”Aliongea Master namba nne.
“Gegu chukua baadhi ya wazee kuelekea mlima Yoshe na mrudishe yule mtu kurudi Panas”
“Kaka namba moja sio kwamba ni mapema sana kumrudisha?”
“Fanya kama nilivyosema , vipi kama Roma akitushambulia unadhani nitaweza kuilinda miliki mwenyewe?”
“Umeeleweka bro”
Lakini sasa muda huo huo sura zao zilibadiika mara baada ya kuhisi kitu ambacho sio cha kawaida na Gefu ndio aliekuwa wa kwanza kupotea ndani ya ofisi hio na kuja kuibukia nje na kufuatiwa na wengine.
Wingu jeusi lilikuwa limejikusanya katika upande wa Kusini mwa eneo la miliki ya Panas , ngurumo na mwanga wa Radi vilikuwa vikisikika na kuonekana.
Sauti za ngurumo za radi zilikuwa kubwa kama vile anga linataka kuondoka chini.
Majini wengi wa miliki hio walikuwa nje wakiangalia hali hio ya kustaajabisha ambayo ni adimu sana kuonekana katika miliki za majini.
“Hii nii…”Jini mmoja ambaye alikuwa katike levo ya maji ya barafu aliongea.
“Hahaha…. tayari amekwisha kuipita levo ya maji ya kiroho , hii ni radi ya mapigo tisa ya adhabu ya anga”Aliongea mkuu wa miliki ya Panas kwa furaha.
“Hakika inashangaza ni juzi tu hapa Anjiu wa Xia ameweza kupita levo hii na leo ni zamu ya Rozu”
“Huu ni wakati wa kuwa na majini wa levo za juu katika ulimwengu wetu,ni heshima kwetu kuangalia kitu kama hichi kikubwa”Aliongea na kufanya wazee pamoja na majini wa miliki hio kuonyesha furaha zao.
“Kimya!!, huu ni mwanzo tu lakini hatuna uhakika kama ataweza kuvumilia mapigo hata matatu ya radi ya rangi ya Zambarau”
Baada ya kusikia kauli hio kila mmoja alipiga kimya kwani ni kweli radi hio haikuwa imeshuka bado na walikuwa na wasiwasi kwamba wanaweza kumpoteza mtu wao.
Majini wanaweza kupitia radi lakini sio wote ambao wanaweza kuihimili kwani ilikuwa na nguvu kubwa kwani dhumuni la kushuka kwake sio kwa ajili ya kunufaisha jini bali ni kwa ajili ya kutoa Adhabu kwa kukiuka sheria za anga.
Dakika chache mbele radi hio ilianza kuonyesha ghadhabu yake na boriti ya radi iliokuwa katika rangi ya Zambarau na bluu ilionekana ikishuka kama vile ni nyoka na kwenda kupiga katika sehemu ambayo yupo jini aliefahamika kwa jina la Rozu.
Ilikuwa ni sauti ya kuumiza masikio ya mwangwi ndio iliweza kusikika na kuwafanya majini kuogopa na kuwafanya wengine kukimbia
“Hii inatisha , sidhani kama Rozu ana Dhana ambayo inaweza kumkinga,atakuwa na uwezo wa kupita hii Adhabu bila kifo kweli?”
“Ni ngumu kusema na hatuwezi hata kusogelea eneo alipo kwasasa bila ya kupoteza nafsi zetu , hata mimi sijui kama ataweza kweli kuhimili?”.
Kila mmoja alikuwa akijiuliza swali linalofanana na kuna ambao walikuwa wakijutia kwa Rozu kukasirisha anga mpaka kupatwa na radi hio.
Dakika chache mbele radi ya pili ilipiga na ilikuwa kubwa kuliko ya mwanzo kiasi cha kutengeneza shimo na ndani ya dakika chache mara baada ya kufifia kitu kinachofanana na Dhahabu kilionekana katka lile eneo.
Kuna ambao waliweza kuona kitu hicho lakini hawakuweza kujua ni kitu gani lakini wakuu wa miliki hio walikuwa na uwezo wa kuhisia Rozu alikuwa hai bado kutokana na msisimko aliokuwa akidhalisha.
Hali hio iliwafanya wazee kujiuliza amewezaje kutoathirika katika mapigo hayo ya radi.
Radi ya tatu iliweza kupiga kwa awau nyingine na ilikuwa na nguvu kubwa zaidi lakini hata hivyo kile kitu ambacho kilikuwa katika muonekano wa Dhahabu bado kilikuwa kikionekana katika eneo lile.
Radi ile ilionekana haikuwa na mpango wa kuendeleza mapigo kwani mara baada ya mapigo matatu wingu lilianza kutawanyika na palepale shimo kubwa lilionekana kwa macho.
“Rozuu..!!!”
Mkuu wa miliki ndio aliekuwa wa kwanza kuita jina hilo lakini kufumba na kufumbua palepale alionekana mwanamke jini ambaye ameshikilia upinde wa Dhahabu akisogelea mbele ya kila mmoja akitokea eneo lile
Nywele zake ndefu zilikuwa hazijafungwa na zilisambaa kulingana na upepo ulivyokuwa ukivuma lakini licha ya hivyo hazikuweza kuficha uzuri wake wa ajabu na macho yake angavu , alikuwa mrembo haswa kwanzia ngozi , umbo la uso na kila kitu.
Alikuwa na muonekano wa ajabu kidogo mzungu sio mzungu , alikuwa ni kama vile ni mfilipino.
Ijapokuwa hakuwa na mavazi ya kirembo kama wanawake wa kidunia lakini upole wake pamoja na uwezo wake ulimfanya kuzidi kupendeza na kuwa ni mwenye kutamanika.
Huyu mwanamke alikuwa akifanana kwa kila kitu na mrembo ambae Hermes mjumbe wa miungu alikuwa akiongea nae katika kilele cha mlima kilimanjaro muda kadhaa mara baada ya Roma kumuokoa Edna katika mikono ya Vampire waliokuwa wakitafuta mshipi feki.
Ki ufupi ni kwamba ni huyu mwanamke bila shaka na haikueleweka ilikuwaje akawa katika jamii ya majini wa miliki ya Panas lakini ndio hivyo alionekana kupitia levo ya mapigo matatu ya radi ya mbingu na jina lake alikuwa akifahamika kwa jina la Rozu.
Ijapokwa Rozu hakuwa ameonyesha uwezo wake wote lakini kwa majini hao walijua alikuwa ni wa levo za juu sana , pengine alikuwa akilingaina ki uwezo na Jini Anjiu wa miliki ya Panas au kumpita.
“Hongera sana , kwasasa upo na uwezo mkubwa wa nguvu za kijini na hakuna ambaye anaweza kukushinda katika ulimwengu wa majini watu”Aliongea Master namba nne huku ile hofu yake ya kumhofia Roma na Anjiu ikiwa imetoweka kabisa , alijua kwa uwezo aliokuwa nao Rozu anapaswa kuwa na amani.
“Hongera sana , nilikuwa na wasiwasi muda si mrefu lakini kwa bahati nzuri umeweza kufanikiwa kupitia mapigo ya radi”Aliongea Mkuu wa miliki hio huku akijiuliza kimoyo moyo.
“Imekuwaje akapitia mapigo hayo ya dhiki ya radi kirahisi hivyo , anaonekana hajapatwa na majeraha ya aina yoyote yale”Aliwaza.
Ukweli ni kwamba kuna namna majini hao walikuwa wakimjua Rozu kama Rozu jini mwenzao lakini hawakumjua Rozu kama sehemu ya miungu , kitendo cha Rozu kuongea na Hermes juu ya mlima kilimanjaro ilimaanisha kwamba ni sehemu ya miungu lakini jina lake halifahamiki ni lipi katika miungu yote iliobaki ambayo hatujawaona wahusika wake.
“Kama hizi ni pongezi za dhati basi sina budi ya kuzipokea”Aliongea mwanadada mrembo Rozu huku akimwangalia Gefu kwa macho makali kidogo kiasi cha kumfanya Mkuu wa miliki hio kuwa na wasiwasi lakini alijitahidi kuonyesha tabasamu.
“Unapenda sana utani , sina haja ya kumuonea wivu mdogo wangu wa kike mafanikio yake , leo ni siku ya kusherehekea, uwepo wako unatufanya tusimhofie tena jini Anjiu”Aliongea.
Ukweli ni kwamba Rozu na Anjiu kidogo walikuwa na tofauti , wakati wa Anjiu anapokea mapigo ya radi chungu cha Roma ndio ambacho kilimkinga lakini kwa jini Rozu yeye ilikuwa tofauti kwa maana kwamba mapigo yote ya radi yalimfikia.
Majini wote walikuwa kwenye shangwe wakimzunguka Rozu na kumpa pongezi za dhati kabisa kwa kupigi hatua hio Adhimu.
Kuipita Dhiki ya radi ni hatua kubwa sana katika ulimwengu wa majini ndio maana.
Rozu mara baada ya kuweka upinde wake wa Dhahabu katika hifadhi ya pete alivuta pumzi nyingi na kisha kutoa tabasamu.
“Anjiu huna uwezo tena wa kunizidi, Hades namsapoti Athena na mipango yake na nataka nione ikifanikiwa”Aliwaza.
Haya sasa kuna kiumbe kingine katika miliki ya Panas , unadhani huyu jina lake halisi ni lipi kati ya miungu kumi na mbili ya mlima Olympus kutoka sayari ya Mars.
Hades A.k. a Roma Ramoni atamuweza kweli?.




SEHEMU YA 737.
Upande wa Roma mara baada ya mechi kumalizika hakuna ambaye alitamani kuangalia ugawaji wa makombe na medali hivyo walirudi moja kwa moja kwenye boti yao ya kifahari.
Upande wa Raisi Jeremy hakuwasumbua tena kwani alikuwa ndani ya Uingereza kwa ajili ya kikao cha Umoja wa mataifa kinachohusu mabadiliko ya hali ya hewa na hata Raisi Senga alikuwa ni moja ya viongozi ambao walihudhuria kikao hicho muhimu.
Kilikuwa ni kikao muhimu kutokana na mabadiliko ya ghafla ya hali ya hewa ya joto la dunia kuporomoka na kusababisha baridi kali licha ya kwamba katika maeneo mbalimbali ya dunia ilipaswa kuwa majira ya joto.
Ukiachana na wakuu wa mataifa lakini pia wanasayansi wengi na watu wa maswala ya kimazingira walikuwa wakihudhuria kikao hicho ili kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo mara baada ya kujua chanzo.
Clark ni moja ya wanasayansi muhimu kabisa ambao walialikwa katika kikao hicho muhimu lakini licha ya hivyo hakukuwa na maelezo ya moja kwa moja ambayo angeongea kwani ni swala ambalo bado hakuwa amelifanyia utafiti.
Roma mara baada ya kuingia katika boti ndio maandalizi ya kurudi katika visiwa vya wafu yalianza rasmi lakini ndio muda ambao aliweza kupokea simu kutoka kwa Afande Kweka.
“Wewe mtukutu hivi utaacha lini kuwa na huo ukiburi?”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kuishia kushangaa.
“Ongea vizuri mzee basi”
“Kwanini umekataa kuongea na wajumbe wa Hongmeng ?, angalau hebu ongea nao maana kwasababu yako kila saa wapo ndani ya makazi yetu, unafikiri nadili nao vipi viumbe wa ajabu kama hawa?”
“Unamaanisha huyo Xuan Jizi yupo ndani ya makazi yako?”Aliuliza Roma huku hasira zikianza kumvaa maana aliona ni kama usumbufu.
“Anaonekana kuwa na hasira sana na amesema kama hutorudi mapema anaenda kutoa taarifa Hongmeng , hebu rudi udili na hii hali nishazeeka sitaki kuingizwa kwenye matatizo ya namna hii mimi”Aliongea na palepale alikata simu ikionyesha dhahiri alikuwa amekasirika.
Roma aliweka simu yake mfukoni na kisha aliwasogelea wanawake wake na kuwaambia juu ya hali inayoendelea nchini Tanzania hivyo anapanga kuondoka.
Kwasababu walikuwa ni waelewa hawakumzuia Roma na dakika hio hio alianza safari kurejea nchini Tanzania.
Ulaya na Tanzania masaa yalipishana kidogo sana hivyo Roma alifika wakati wa usiku pia ndani ya jiji la Iringa na wakati wa kutua tu aliweza kuona kuna wageni wamekaa katika sebule ya wageni ndani ya nyumba hio , walikuwa wawili na wote ni Wachina.
Moja kati yao alikuwa akimjua na mwingine hakuwa akimjua lakini alionekana kuwa handsome mno , ilikuwa ni kama vile sio mchina na alikuwa katike levo ya maji ya kawaida.
“Naona Mjumbe umeimarika kuliko mara ya mwisho tulivyoonana”Aliongea Roma akimlenga mjumbe wa Hongmeng mpenda rushwa.
“Haha… sipo hapa kwa ajili ya kukumbushia namna tulivyoonana mara ya mwisho nimemleta balozi”Aliongea na kisha alimpa ishara balozi Xuan Jizi.
“Wewe ndio Roma Ramoni ulietibua hali ya hewa katika miliki ya Kekexil na Xia?”Aliuliza yule bwana bila hata ya salamu , alionekana kuwa na hali ya ujeuri hivi.
“Ndio umekuja kote huku kwa ajili ya kuuliza ujinga?”
“Acha maneno yako makali , hivi unajua upo kwenye matatizo?”
“Nielimishe”
“Nikuelimishe nini? , unadhani kuna hata haja ya kufanya hivyo , unajua mwenyewe namna ambavyo umekasirisha majini kutoka miliki ya Xia na Kekexil , ukaenda mbali na kuchokoza miliki ya Braki , nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif , unaonekana kabisa unaogopa ndio maana ukaikimbiza familia yako nje ya nchi”
“Umongea sana lakini sijui kilichokuleta ni nini?”
“Nipo hapa kwa ajili ya kupitisha maagizo niliopewa na wakuu wa miliki ya Hongmeng, wasimamizi wakuu wa sheria ya the gods treaty , ili kuongezea nguvu utulivu wa dunia na kukuzuia kupigana na miliki za kijini na kusumbua raia , Hongmeng kwasasa itakuwa ndio kimbilio lako licha ya kwamba kutakuwa na mashariti, ukikukubali hakuna miliki yoyote ambayo itakugusa”
“Roma usishangilie bado kuna masharti”Aliongea yule mjumbe na Xuan jizi aliendeea.
“Umekiuka sheria nyingi sana na kutumia uwezo wako vibaya na kuua wajumbe ambao waliagizwa kuja duniani kutimiza majukumu yao , lakini licha ya hivyo Hongmeng hawataki kulipiza kisasi na wameaua kukusamehe ili mradi tu kwa hiari yako utoe mbinu yako ya mafunzo , vidonge na Dhana ya Chaos cauldron na baada ya hapo sisi tutakupatia ulinzi”Aliongea akiwa siriasi na kumfanya Roma kuangua kicheko.
“Unacheka nini?”
“Wewe Mzee Jizi, lazima kwenye kwenye kichwa chako kuna nati zimechomoka au hao Hongmeng hawajui nini kinaendeea , nadhani napaswa kuwafafanulia kwa sentensi rahisi”
“Acha kunitukana … tunazo taarifa umeiba hazina yote ya Kekexil na Xia na unazo Dhana na vidonge kedekede , hivi unadhani vitu vya thamani kama hivyo utaweza kuvilinda peke yako, hivyo acha ukiburi na sikiliza tunachokuambia”
“Vipi kama nikikataa mtanifanya nin?”
“Roma acha kujifanyisha kijogoo , sekunde ambayo nitakuripoti katika miliki ya Hongmeng basi ndio utakuwa mwisho wako kwani utakuwa ni adui namba moja wa Hongmeng”
Roma aliwaza na kujiambia tokea siku anajua uwepo wa Hongmeng ndio uadui wao ulipoanzia hivyo hana mpango wa kuwasikiliza kwa chochote , kwanza kabisa alikuwa na deni kwa Zenzhei kumsaidia kulipa kisasi na tokea siku waagane ni kama Zenzhei katika ulimwengu huo wa kijini alikuwa akimsubiria.
Roma bila ya kujiuliza mara mbili mbili aliita nguvu ya Cauldon bila ya kukitoa nje na kuingiza katika mwili wa Xuan Jizi na kuanza kunyonya nguvu zake za kijini na nguvu ya Cauldron ilikuwa kubwa mno na ndani ya dakika chache tu alikuwa ashapoteza uwezo wake wote na kubakia binadamu wa kawaida.
Xuan Jizi hakuwa jini kama jini wa Hongmeng , alikuwa ni binadamu tu ambaye alikuwa na mafunzo ya kijini hivyo ilikuwa rahisi kwa Roma kudili nae kwani alikuwa ndio kwanza yupo katika levo ya maji ya kawaida.
Hakuna ambaye alitegemea Roma kuchukua maamuzi kama yale , lakini kwa Roma alitaka kuonekana kuwa siriasi na kutangaza vita vyake rasmi na Hongmeng kabisa na ili kuonekana yupo siriasi alitaka kwanza kumuadabisha balozi wao.
Mjumbe wa Hongmeng aliebakia ndio alipewa jukumu la kurudi Hongmeng na kutoa taarifa ya kile kilichotokea,
“Rudi ujinini na toa taarifa hizi , kama hao majini wanataka Dhana zangu , vidonge vyangu na mbinu yangu ya mafunzo basi waje huku nilipo wavichukue kwa nguvu kama nilivyofanya katika miliki ya Kekexil,likija swala la watu wenye nguvu kama haina haja ya kutii sheria za ulimwengu bali sheria ya msituni ndio itumike , atakae weza kuishi mpaka mwisho huyo ndio mtawala”
Baada ya kusema hivyo Roma alimbeba mzobemzobe yule Xuan Jizi na kisha kumtupia mbele ya walinzi akiwaagiza kwenda kumtupia mtaani huko kwani ashakua ni wa kawaida.
Alijua asingeweza tena kurudi Hongmeng kwani miliki hio haichukui majini wadhaifu kama yeye.
“Vipi kila kitu kimemalizika?”Aliuliza Afande Kweka mara baada ya Roma kuingia katika sebule ya kawaida na Roma aliishia kutingisha kichwa tu akiitikia amemaliza.
“Unajisababisha matatizo zaidi na zaidi juka uchao kulikuwa na haja gani ya kumuondolea nguvu zake za kijini?”Aliongea Afande Kweka bila ya kubadilisha muonekano wake , yaani hakuwa na furaha wala hakuwa na huzuni na hata usingizi hakuwa nao licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda.
“Babu hicho ndio kitu pekee ambacho unaweza kuongea”
“Unadhani ni kipi ambacho naweza kuongea , mwenyewe nipo najiuliza mambo ambayo yanaendelea katika hii dunia, nina hasira nyanya zangu zote zimekauka kutokana na baridi kali , hii baridi sijawahi kuiona na uzee wangu huu”Aliongea na kumfanya Roma amuone huyu mzee anaonekana kuficha mambo mengi na kila anachoongea ni kama anamwigizia lakini hakutaka kumhoji sana.
Huo ndio ulikuwa ukweli ugomvi wa Roma na majini ulikuwa ni wa kutisha lakini ulikuwa haukwepeki lakini kubwa zaidi ni kwamba Mzee huyo alitamani sana Roma kwenda kuwashambulia Hongmeng ili kulipa fadhila za Zenzhei kwa kumlinda kwa miaka mingi, ukiachana na hilo lakini pia Afande Kweka ni mwanachama wa umoja wa Ant- illuminat na ni juzi tu hapo alikuwa na kikao cha siri na baadhi ya wanachama na alikuwa akijua Edna ndio mkuu wake.
Yani kwa lugha nyepesi ni kwamba Edna ni mkuu mbele ya Afande Kweka lakinin mzee huyo licha ya kujua hayo yote hakuwa tayari kumwambia Roma kwani alijua itafikia siku yeye mwenyewe atakuja kujua ukweli na hata hivyo sheria za umoja huo hazikumpa ruhusa ya kuongea chochote kwani ingeharibu kabisa mipango inayoendelea.
“Babu nadhanni baada ya Hongmeng kupokea ujumbe wangu sitoweza kuendelea kuishi hapa Tanzania kwa muda , unaonaje na wewe ukielekea visiwani kwa muda , unaweza kuondoka na baadhi ya watu wako wa karibu pia”
“Unataka nitoke hapa Tanzania kwenda wapi na kwanini?”
“Si kila kitu kipo wazi mzee , sitaki waje wakukamate na kutaka kunitishia uhai wako kama chambo cha kunikamata”
“Mimi nipo nje ya maswala yote ambayo yanahusiana na maadui zako na sio kwangu tu hata kwa baba yako , kinachoendelea ni vita kati yako na majini na hayahusiani na ukoo wetu hivyo pambana kivyako”
“Unaongea tu lakini wanaweza wakapania sana na kutumia njia yoyote ile”
“Hata iweje nasema hapa siondoki “Aliongea kibishi.
“Kwannini sasa , huu sio muda wa kuonekana shujaa mzee”
“Mimi ni mzee wa taifa hili lakini pia mkuu wa familia ya Kweka , siwezi kuondoka na kwenda mahali pengine nje ya Tanzania, unaweza kutafuta chumba ulale , muda umeenda naenda kupumzika”Aliongea na kisha aligeuza na kuingia chumbani kwake.
Roma alikuwa na usingizi na wakati akiwaza kwenda katika chumba cha wageni kwa ajili ya kulala simu yake ilianza kuita mlio wa kuingia meseji na alipoangalia ilikuwa imetokea kwa Tannya.
“Master kuna kundi la majini wamefika na wanakuulizia hapa Bagamoyo”Ujumbe wa meseji ulisomeka hivyo.
“Naona hatimae wamejitokeza licha ya kwamba ni kwa kuchelewa kama nilivyotegemea lakini ni bora wamekuja kabla sijarejea katika ulimwengu wa majini watu”Aliwaza Roma
Sasa mara baada ya Roma kuona kwamba nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya mzee Sharif imejitokeza hakutaka kupoteza muda kabisa na shauku ya kutaka kujua Braki ni majini wa namna gani ilimvaa.
Roma mara baada ya kuondoka ndani ya eneo la Iringa dakika chache tu aliweza kufika mkoa wa Pwani katika makazi ya Sharif na aliweza kumuona Tannya akiwa amesima katikati ya ukumbi wa mikutano , ilikuwa ni eneo ambao hutumika kupokelea wageni mara nyingi.
Mbele yake kulikuwa na wanachama wa familia ya Sharif na mara baada ya kuwachunguza kwa umakini Roma aligundua hawakuwa wa kawaida wote walionekana kama waarabu hivi na hajawahi kuwaoana na walikuwa na nguvu za kijini.
Tannya tokea muda tu alikuwa amebadilisha wafanyakazi wote wa Sharif na kuweka wa kwake , ijapokuwa alikuwa mjapani lakini alikuwa mjuzi sana katika kuigiza na tokea siku ambayo amefika na kujifanyisha ni Maimuna hakuwahi kuonyesha dosari yoyote na hata ibada alikuwa akiongoza.
Roma kwa kutumia jani lake la upofu aliishia kujificha juu ya jengo hilo huku akihakikisha anasikia kinachoendelea kwa kutumia uwezo wake na majini hao hakuna hata mmoja ambaye aliweza kugundua uwepo wake.
Kulikuwa na majini jumla saba, wote walikuwa wamevalia kanzu kwa upande wa wanaume na wanawake wenyewe walikuwa wamevalia Abaya nyeusi , karibia wote walikuwa na muonekano wa ki utu uzima.
Kati yao mmoja tu ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa mafunzo ya kijini kwani alikuwa mwanzoni mwa maji ya kiroho. Na wengine wote walikuwa katika levo za maji ya barafu kushuka mpaka moto wa njano.
“Wewe ndio kiongozi wa familia ya Sharif katika ulimwengu huu unaefahamika kwa jina la Maimuna si ndio?”Mwanaume ambaye alikuwa na muonekano wa kizee alimuuliza Tannya , alikuwa na nywele nyeupe na ndevu nyeupe kama vile ni Nandra Modi waziri mkuu wa India na ndio ambaye alikuwa na uwezo wa juu wa kijini.
“Ndio , kwasasa mimi ndio nililazimika kuwa kiongozi , hivyo sina uhakika namna ya kuwaita kwani siwafahamu”Aliongea Tannya aliekuwa katika sura ya Maimuna.
“Hakuna shida kwani hata babu yako Sharif hana uwezo wa kututambua,kwa majina nafahamika kama Zando , nikiwa mwanachama kutoka makao makuu ya miliki , hapa kuna mzee Nuli na Yejini pamoja na majini wanne unao waona , tumekuja hapa kujua ni kipi kinachoendelea kwasababu hatukuweza kusikia habari zozote kuhusu mwizi alieiba hazina yetu , taarifa za kubadilika kwa kiongozi wa familia na imani ni zaidi ya matarajio yetu”












SEHEMU YA 739.
Katika moyo wake Tannya ukweli hakuwa akijua namna ya kujibu, ijapokuwa alikuwa akijua muda kama huo ungewadia lakini ndio mara yake ya kwanza kukutana na majini wa namna hio na angalau ni kwamba alikuwa tayari ashamtumia Roma ujumbe wa meseji.
Tannya simu yake ilitoa mnguruo mara baada ya kutaka kujibu na mara baada ya kuangalia aliona Roma alikuwa ametuma ujumbe kwa lugha ya kijapani.
“Tafuta njia yoyote upate taarifa zinazohusiana na wanakotokea na historia yao kwa ujumla”Aliongea Roma katika ujumbe huo.
Roma alitumia kijapani kwa kuamini ingekuwa ngumu kwao kuelewa kile alichokuwa ameandika.
Tannya mara baada ya kujua Roma ashafika hali ya kujiamini iliongezeka kidogo na palepale aliomba radhi
“Naombeni mniwie radhi wakubwa zangu, nilitamani pia kutoa taarifa kuja makao makuu lakini kwa bahati mbaya babu , walinzi na wengine walikufa vifo vya haraka sana na sikujua namna ya kuwasiliana na nyie hivyo…”
“Haina haja ya kujilaumu , hata sisi pia tunaelewa namna ilivyo ngumu kuwasiliana na sisi , umefanikisha kuongoza familia ndani ya muda mfupi na kuendeleza ibada taarifa hizi zikimfikia mkuu wetu atafurahi”Aliongea.
“Tafadhari naomba mniwie radhi kama nitavuka mpaka , lakini je mnaweza kunielezea historia yote ya familia pamoja na imani yake , ili mimi Maimuna niweze kuwa na uelewa mzuri na kufanya vizuri kwa ajili ya manufaa ya miliki kwa ujumla”
“Kwasababu umekuwa kiongozi pekee uliebakia basi ki asili umekidhi vigezo vya kujua historia yote ya Kibraki , Babu yako Sharif ana uelewa mdogo sana kuhusu jamii ya majini wa Braki pengine amewahi kusikia hili jina mara moja au mara mbili tu , lakini kutokana na mabadiliko ya hali na matukio ya kutotarajia hapa duniani makao makuu wameona ni sahihi familia za binadamu zinazotuwakilisha hapa duniani kujua uhalisia wa historia yetu na imani yote kwa ujumla, hivyo nitakuelezea kila kitu”
Roma ambaye alikuwa akipiga chabo alijikuta akifurahi mara baada ya kusikia kauli hio kwani hakutegemea jini aliefahamika kwa jina la Zando angeweka wazi kuhusu nguvu iliokuwa nyuma ya familia ya Sharif.
*****
Miaka elfu hamsini iliopita dunia iliingia katika hatua nyingine kubwa katika ustaarabu.
Wakati huu pia upande wa majini walikuwepo pia na wengi wao walikuwa katika levo za juu sana pengine levo ambayo haijawahi kufikiwa katika nyakati za sasa.
Kipindi hiki ni kabla ya miungu kufika katika sayari ya Dunia na ndio kipindi ambacho majini wengi walianza kupotea katika uso wa dunia na kuwaacha binadamu na baadhi ya majini watu.
Majini ni vumbe ambavyo vipo vya aina nyingi sana na tabia tofauti , ni kama ilivyo kwa makabila ya kibinadamu basi ndio ilivyo kwa majini hivyo hivyo.
Sasa kati ya majini wa enzi hizo ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uso wa dunia ni majini pepo na hawa majini pepo wenyewe walikuwa wamegawanyika katika aina nyingi sana.
Inasemekana katika kipindi hichi majini walikuwa wengi kuliko hata idadi ya binadamu kutokana na spidi yao ya kuzaliana.
Kati ya majini pepo ambao waliweza kufahamika enzi hizo ni kama vile Mbweha na Majoka ambao ndio walikuwa na uwezo mkubwa sana .
Majinii jamii ya Mbweha walikuwa ndio wenye busara kubwa na mbinu nyingi za kimaajabu tofauti hata na majini Joka ambao walikuwa wamezaliwa na nguvu za kimwili sana sana.
Ukiachana na majini hao lakini pia majini watu hawakuwa nyuma pia kwani wengi wao walikuwa katika levo za juu kwa kuweza hata kudhibiti radi na ilikuwa ni kawaida kwa majini watu kuweza kumiliki Dhana za hali ya juu kabisa na shida ilikuwa tu kwamba licha ya uwezo wao hawakuweza kupata mbinu ambayo inaweza kuwainua zaidi na zaidi.
Hawa majini watu ndio ambao walipenda kuwa wa wazi kabisa na waliweza kuishi katikati ya binadamu wa kawaida tofauti na majini pepo ambao walikuwa ni hatari kabisa kwa binadamu.
Majini pepo waliishi katika maumbo yao ya kawaida pasipo ya kubadilika na ukweli ni kwamba walikuwa wakitisha sana na hali hio ki ufupi ni kwamba hawakuipenda na hii iliongeza chuki yao zidi ya binadamu na majini watu.
Lakini mwishowe walijitahidi kutafuta namna ya kuboresha muonekano wao ndipo walipokuja kugundua mbinu mbadala ambayo ilikuwa ni kuamsha pepo wao wa ndani tofauti na kuwazimisha au kuwakata kama ilivyokuwa kwa majiini watu ,hapo sasa ndio ikazaliwa majini halisi ambao walikuwa na nguvu za kijini, majini ambao walikuwa na uwezo wa kupaa.
Sasa kutokana na kuwa na maumbo yenye nguvu kubwa pamoja na kumiliki nguvu za kijini pamoja na kuwa wengi walikuja kuwa tishio kubwa kwa jamii nyingine za kijini na binadamu wa kawaida kiasi cha kupelekea kuibuka kwa vita ambayo majini watu waliungana na binadau kuwashambulia Majoka.
Sasa kati ya majini pepo wakaja kuibuka jamii nyingine kati ambao walijiita mashetani pepo wa anga , hawa ndio walikuwa wabaya zaidi kwani walikuwa na uwezo wa kumuingia binadamu na kumfanya afanye kila anachotaka huku wale majini pepo wengine wakichinja binadamu na kunywa damu yao.
Binadamu alionekana kuingia katika hatari na kuanza vita na viumbe hawa majini ,vita ambayo ilidumu kwa muda mrefu sana takribani miaka mia moja na siku moja tu ilitokea majini pepo wengi katika ulimwengu wa kawaida kuanza kupotea ikiwemo Mbweha na Majoka.
Kupotea kwao baadae ilikuja kujulikana walikuwa wakivutwa katika ulimwengu mwingine kwa kutumia aina ya mitego ambayo ilikuwa imewekwa mfano wa mnara ambao Roma aliingia.
Ni asilimia chache tu ya majini pepo ambao walibakia na kati yao hawakuwa hata na uwezo mkubwa na hapo ndipo majini watu wa enzi hizo walipoona hakuna haja ya kuwaua bali kwenda kuwafungia katika ulimwengu Tenganifu wa jangwa.
Kitendo cha mashetani pepo wa anga, Majoka na Mbweha kufungiwa katika ulimwengu wa Jangwa Tenganifu kwa muda mrefu iliwafanya kuchukulia hapo kama makazi yao rasmi.
Mara baada ya kuwasili kwa miungu katika uso wa dunia ndipo ilipoibuka vita kati ya majini watu yaani Hongmeng na jamii nyingine za kijini , vita ambayo ilidumu muda mrefu sana mpaka Zeus na Athena kushindwa vita na kuzaliwa kwa the Gods treaty.
Mpaka vita hio inakuja kufikia mwisho majini pepo ambao walikuwa katika ulimwengu wa jangwa tenganifu walikuja kugundua miliki za majini watu walikuwa wamepungukiwa nguvu sana kutokana na kupigana vita na miungu na wengi wao kuuliwa na hapo ndipo walipoona ni fursa adhimu ya kujiendeleza wao wenyewe kutokana na kipindi hicho majini watu kutokuwa nao makinu.
Mbinu pekee ambayo iliwafanikisha kujiendeleza ni kufanya ushirikiano wa kiimani na binadamu wa ulimwengu wa kawaida taratibu taratibu kwa namna ambayo waliweza wao na mwisho wa siku wakajikuta wanakuwa na nguvu kubwa kwani walijipatia mali asili nyingi kutoka Duniani na kuziingiza katika ulimwengu wao huku wakibadilishana na binadamu madini mengi ya thamani.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba majini pepo wengi ikiwemo majoka na Mbweha ambao walikuwa na uwezo mkubwa walimezwa katika ulimwengu wa majini pepo kwa njia ambazo mpaka siku hio hawakuelewa imetokeaje , huku upande wa majini watu , yaani majini wa kawaida ambao mbinu zao sio kuamsha mapepo wao walijitenga na binadamu wa kawaida mara baada ya kugundua Dimension nyingine na kuanzia hapo kila majini wakajitegemea na kukawa na ulimwengu wa majini watu , ulimwengu wa majini pepo na ulimwengu wa Jangwa Tenganifu sehemu ambayo hupatikana miliki moja tu ya kijini ambayo hufahamika kwa jina la Braki.
Kwa historia hio ilimaanisha kwamba hapo zama za kale majini na binadamu waliishi katika ulimwengu mmoja kabla ya vita kutokea, vita ambayo mpaka wakati huo majini wote wanajiuliza ilimalizwa na nani kwani sio wao ambao waliwafanya majini pepo wenye nguvu kuvutwa kwenye ulimwengu mwingine.
Sasa kati ya majini pepo hao ambao walivutwa ni kama vile Aoiline Mbweha wa mikia tisa , Majoka na mashetani pepo wa anga.
Roma mara baada ya kusikia habari hio aliishia kushangaa , katika ulimwengu wa majini pepo Zimo alisema ulimwengu wao ulikuwa ni wa miaka mingi kuliko hata Hongmeng na hio ilimaanisha kwamba kabla ya kumezwa ulimwengu huo ulikuwepo.
Sasa Roma mara baada ya historia hio anajua nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif ni majini pepo na ni sawa na kusema ni ndugu wa Aoiline.
Kulinganana msaada ambao Aoiline alimfanyia na wengine Roma aliona ni dhambi kama ataingamiza miliki hio ya Braki ambayo inapatikana katika Ulimwengu wa Jangwa na anachopaswa ni kujaribu kufanya urafiki nao lakini kabla ya yote lazima ajue hazina yao ilikuwa ikimaanisha nini.
“Asante sana kwa kunielezea haya”
“Hivyo licha ya familia ya Sharf kuumiza watu wengi katika ulimwengu huu wa kawaida lakini kwa upande wetu sio jambo kubwa sana na sio maagizo yetu , Sisi sio kama majini kutoka Hongmeng na miliki nyingine ambao wanachotaka ni umaarufu tu , sisi leo tumetoka kuja katika ulimwengu wa kawaida kwasababu ya muovu Roma Ramoni ambae ameiba hazina yetu”
“Je naweza kuuliza, Hazina hio ina matumizi gani , je kutakuwa na athari zozote kama isipokuwa kwenye mikono yetu?”Aliuliza Maiuna feki na hapo ndipo Roma alipokuwa akitaka kujua ile kokoto ina maana gani.
ITAENDELEA ,WATSAPP 0687151346
Eid el fitri. Tunaipokeaa na hades
 
Back
Top Bottom