Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 58
Mtoto huyu wa mbabe wa dawa za kulevya, ambaye baba yake alitoka katika familia ya mwalimu na mkulima, aliambatana na msichana mrembo, Serina Wilson.
Jakna hakuruhusiwa kusikiliza mazungumzo ya Carlos na mgeni wake Emilio, hivyo aliketi katika meza nyingine karibu akisubiri. Wakati wote Carlos alikuwa hafanyi kosa, alijua kufanya kosa moja kunaweza kumgharimu. Aliwatumia hawa kupokea na kusambaza dawa, lakini mambo yake ya ndani, hakupenda kuwashirikisha kabisa.
"Karibu sana, hii ndiyo Tanzania", Carlos alimwambia Emilio, wakasimama na kushikana mikono.
"Asante sana Carlos, vipi hali ya biashara hapa?", Emilio alihoji.
"Tuko vizuri", Carlos alijibu kwa mkato.
"Si kweli Carlos, nimelazimika kuja hapa, ili tuzungumze kwa kirefu kidogo, nini tatizo, haiwezekani mzigo ukwame Adis Ababa kwa muda mrefu kiasi hicho, halafu unasema uko vizuri?", Emilio aliuliza.
"Kuhusu hilo tumelimaliza, ni kweli kulikuwa na tatizo kidogo kwa wenzetu wa uwanja wa ndege, lakini jambo hilo limekwisha, kila kitu kimekaa vizuri, mzigo unaweza kuwasili Dar es Salaam leo, kuhusu hilo, ondoa shaka, tumelimaliza".
"Nini kilikwamisha huo mzigo kuingia hapa, kama ni pesa mnazo za kutosha, mnaweza kumnunua mtu yeyote, au unasemaje Carlos?".
"Hilo halina ubishi, ilitokea tatizo ngazi za juu, huko serikalini, mtu mmoja alipewa cheo akajiona tayari amekuwa Mungu, akahamia uwanja wa ndege, baadhi ya watu wamekamatwa, lakini si wa upande wetu, hata hivyo pesa imefanya kazi yake, mtu huyo ameondolewa, mzigo unaingia leo, mamlaka zote zina taarifa kuhusu mzigo huo kuingia", Carlos alieleza.
"Nilitaka kujua hivyo, haiwezekani nchi ndogo kama Tanzania kuwe na usumbufu wakati wa kuingiza mzigo, wakati nchi kubwa kama Marekani, China, Japan na South Afrika mzigo unaingia haraka na bila shaka. Nimekuelewa Carlos, nitaondoka leo, hakikisha biashara yetu inashamili na kupata watumiaji wengi zaidi, huo ndio msimamo wetu", alieleza Emilio huku akisimama kwa ajili ya kuaga na kuelekea kwenye helikopita iliyomleta eneo hili.
"Hatutalala, amini hivyo", alidokeza Carlos huku wakipeana mikono ya kwaheri, akaaga na kuondoka, akiacha maswali mengi kwa Carlos. .
Baada ya Emilio kuondoka, Carlos alimwita Jakina.
"Tukiendelea kucheza ngoma za sindiba, tunaweza kupoteza kazi, unamfahami huyu jamaa?", Carlos alimuuliza Jakina.
"Hapana", Jakina alieleza.
"Huyu ni Mkurugenzi wa Shirika la Tuwezeshe, anatoka Marekani, alipenda kuonana na mimi kwa ajili ya mambo fulani, tukimaliza kazi hii salama, nitamuomba twende wote, yaani mimi na wewe tuishi Marekani, ukaishi huko Jakina", Carlos alidanganya.
"Hakuna kitakachoharibika bosi, tumejipanga vizuri mno, naamini mzigo utaingia usiku huu, Hawa amefanya kila jambo, hakuna wa kuzuia", Jakina alijinasibu.
Wakati huo, Mama Feka alikuwa ameketi upande wa pili kwenye kona akiwaangalia. Alipoona sasa ni wakati mwafaka, alitoka na kujipitisha mbele yao. Mama Feka alipita mbele ya meza waliyoketi Carlos na jakina, kama hajawaona vile akatafuta meza akaketi.
"Bosi, umemuona yule dada mshenzi wa Supermarket?", Jakina alimuuliza Carlos.
"Na wewe husahau, kama alikukela msamehe, nenda mwambie aje aketi na sisi hapa", Carlos aliagiza.
"Achana na huyo mshenzi, atatupotezea muda wetu, mbona wasichana wapo wengi tu bosi", Jakina alieleza msimamo wake.
"Hapana, nimesema nenda mwambie aje hapa".
"Mkorofi yule bosi".
"Jakina, elewa kuwa si ombi, nasema nenda mwambie aje aketi na sisi hapa, ni wakati wa kumuomba msamaha kwa yaliyopita", Carlos alieleza huku Jakina akisimama,
****Naam simulizi inazidi kupamba moto
*********ITAENDELEA
BURE SERIES
Mtoto huyu wa mbabe wa dawa za kulevya, ambaye baba yake alitoka katika familia ya mwalimu na mkulima, aliambatana na msichana mrembo, Serina Wilson.
Jakna hakuruhusiwa kusikiliza mazungumzo ya Carlos na mgeni wake Emilio, hivyo aliketi katika meza nyingine karibu akisubiri. Wakati wote Carlos alikuwa hafanyi kosa, alijua kufanya kosa moja kunaweza kumgharimu. Aliwatumia hawa kupokea na kusambaza dawa, lakini mambo yake ya ndani, hakupenda kuwashirikisha kabisa.
"Karibu sana, hii ndiyo Tanzania", Carlos alimwambia Emilio, wakasimama na kushikana mikono.
"Asante sana Carlos, vipi hali ya biashara hapa?", Emilio alihoji.
"Tuko vizuri", Carlos alijibu kwa mkato.
"Si kweli Carlos, nimelazimika kuja hapa, ili tuzungumze kwa kirefu kidogo, nini tatizo, haiwezekani mzigo ukwame Adis Ababa kwa muda mrefu kiasi hicho, halafu unasema uko vizuri?", Emilio aliuliza.
"Kuhusu hilo tumelimaliza, ni kweli kulikuwa na tatizo kidogo kwa wenzetu wa uwanja wa ndege, lakini jambo hilo limekwisha, kila kitu kimekaa vizuri, mzigo unaweza kuwasili Dar es Salaam leo, kuhusu hilo, ondoa shaka, tumelimaliza".
"Nini kilikwamisha huo mzigo kuingia hapa, kama ni pesa mnazo za kutosha, mnaweza kumnunua mtu yeyote, au unasemaje Carlos?".
"Hilo halina ubishi, ilitokea tatizo ngazi za juu, huko serikalini, mtu mmoja alipewa cheo akajiona tayari amekuwa Mungu, akahamia uwanja wa ndege, baadhi ya watu wamekamatwa, lakini si wa upande wetu, hata hivyo pesa imefanya kazi yake, mtu huyo ameondolewa, mzigo unaingia leo, mamlaka zote zina taarifa kuhusu mzigo huo kuingia", Carlos alieleza.
"Nilitaka kujua hivyo, haiwezekani nchi ndogo kama Tanzania kuwe na usumbufu wakati wa kuingiza mzigo, wakati nchi kubwa kama Marekani, China, Japan na South Afrika mzigo unaingia haraka na bila shaka. Nimekuelewa Carlos, nitaondoka leo, hakikisha biashara yetu inashamili na kupata watumiaji wengi zaidi, huo ndio msimamo wetu", alieleza Emilio huku akisimama kwa ajili ya kuaga na kuelekea kwenye helikopita iliyomleta eneo hili.
"Hatutalala, amini hivyo", alidokeza Carlos huku wakipeana mikono ya kwaheri, akaaga na kuondoka, akiacha maswali mengi kwa Carlos. .
Baada ya Emilio kuondoka, Carlos alimwita Jakina.
"Tukiendelea kucheza ngoma za sindiba, tunaweza kupoteza kazi, unamfahami huyu jamaa?", Carlos alimuuliza Jakina.
"Hapana", Jakina alieleza.
"Huyu ni Mkurugenzi wa Shirika la Tuwezeshe, anatoka Marekani, alipenda kuonana na mimi kwa ajili ya mambo fulani, tukimaliza kazi hii salama, nitamuomba twende wote, yaani mimi na wewe tuishi Marekani, ukaishi huko Jakina", Carlos alidanganya.
"Hakuna kitakachoharibika bosi, tumejipanga vizuri mno, naamini mzigo utaingia usiku huu, Hawa amefanya kila jambo, hakuna wa kuzuia", Jakina alijinasibu.
Wakati huo, Mama Feka alikuwa ameketi upande wa pili kwenye kona akiwaangalia. Alipoona sasa ni wakati mwafaka, alitoka na kujipitisha mbele yao. Mama Feka alipita mbele ya meza waliyoketi Carlos na jakina, kama hajawaona vile akatafuta meza akaketi.
"Bosi, umemuona yule dada mshenzi wa Supermarket?", Jakina alimuuliza Carlos.
"Na wewe husahau, kama alikukela msamehe, nenda mwambie aje aketi na sisi hapa", Carlos aliagiza.
"Achana na huyo mshenzi, atatupotezea muda wetu, mbona wasichana wapo wengi tu bosi", Jakina alieleza msimamo wake.
"Hapana, nimesema nenda mwambie aje hapa".
"Mkorofi yule bosi".
"Jakina, elewa kuwa si ombi, nasema nenda mwambie aje aketi na sisi hapa, ni wakati wa kumuomba msamaha kwa yaliyopita", Carlos alieleza huku Jakina akisimama,
****Naam simulizi inazidi kupamba moto
*********ITAENDELEA
BURE SERIES