Simulizi ya Kijasusi: Noti Bandia

Simulizi ya Kijasusi: Noti Bandia

SEHEMU YA 58



Mtoto huyu wa mbabe wa dawa za kulevya, ambaye baba yake alitoka katika familia ya mwalimu na mkulima, aliambatana na msichana mrembo, Serina Wilson.

Jakna hakuruhusiwa kusikiliza mazungumzo ya Carlos na mgeni wake Emilio, hivyo aliketi katika meza nyingine karibu akisubiri. Wakati wote Carlos alikuwa hafanyi kosa, alijua kufanya kosa moja kunaweza kumgharimu. Aliwatumia hawa kupokea na kusambaza dawa, lakini mambo yake ya ndani, hakupenda kuwashirikisha kabisa.

"Karibu sana, hii ndiyo Tanzania", Carlos alimwambia Emilio, wakasimama na kushikana mikono.

"Asante sana Carlos, vipi hali ya biashara hapa?", Emilio alihoji.

"Tuko vizuri", Carlos alijibu kwa mkato.

"Si kweli Carlos, nimelazimika kuja hapa, ili tuzungumze kwa kirefu kidogo, nini tatizo, haiwezekani mzigo ukwame Adis Ababa kwa muda mrefu kiasi hicho, halafu unasema uko vizuri?", Emilio aliuliza.

"Kuhusu hilo tumelimaliza, ni kweli kulikuwa na tatizo kidogo kwa wenzetu wa uwanja wa ndege, lakini jambo hilo limekwisha, kila kitu kimekaa vizuri, mzigo unaweza kuwasili Dar es Salaam leo, kuhusu hilo, ondoa shaka, tumelimaliza".

"Nini kilikwamisha huo mzigo kuingia hapa, kama ni pesa mnazo za kutosha, mnaweza kumnunua mtu yeyote, au unasemaje Carlos?".

"Hilo halina ubishi, ilitokea tatizo ngazi za juu, huko serikalini, mtu mmoja alipewa cheo akajiona tayari amekuwa Mungu, akahamia uwanja wa ndege, baadhi ya watu wamekamatwa, lakini si wa upande wetu, hata hivyo pesa imefanya kazi yake, mtu huyo ameondolewa, mzigo unaingia leo, mamlaka zote zina taarifa kuhusu mzigo huo kuingia", Carlos alieleza.

"Nilitaka kujua hivyo, haiwezekani nchi ndogo kama Tanzania kuwe na usumbufu wakati wa kuingiza mzigo, wakati nchi kubwa kama Marekani, China, Japan na South Afrika mzigo unaingia haraka na bila shaka. Nimekuelewa Carlos, nitaondoka leo, hakikisha biashara yetu inashamili na kupata watumiaji wengi zaidi, huo ndio msimamo wetu", alieleza Emilio huku akisimama kwa ajili ya kuaga na kuelekea kwenye helikopita iliyomleta eneo hili.

"Hatutalala, amini hivyo", alidokeza Carlos huku wakipeana mikono ya kwaheri, akaaga na kuondoka, akiacha maswali mengi kwa Carlos. .

Baada ya Emilio kuondoka, Carlos alimwita Jakina.

"Tukiendelea kucheza ngoma za sindiba, tunaweza kupoteza kazi, unamfahami huyu jamaa?", Carlos alimuuliza Jakina.

"Hapana", Jakina alieleza.

"Huyu ni Mkurugenzi wa Shirika la Tuwezeshe, anatoka Marekani, alipenda kuonana na mimi kwa ajili ya mambo fulani, tukimaliza kazi hii salama, nitamuomba twende wote, yaani mimi na wewe tuishi Marekani, ukaishi huko Jakina", Carlos alidanganya.

"Hakuna kitakachoharibika bosi, tumejipanga vizuri mno, naamini mzigo utaingia usiku huu, Hawa amefanya kila jambo, hakuna wa kuzuia", Jakina alijinasibu.

Wakati huo, Mama Feka alikuwa ameketi upande wa pili kwenye kona akiwaangalia. Alipoona sasa ni wakati mwafaka, alitoka na kujipitisha mbele yao. Mama Feka alipita mbele ya meza waliyoketi Carlos na jakina, kama hajawaona vile akatafuta meza akaketi.

"Bosi, umemuona yule dada mshenzi wa Supermarket?", Jakina alimuuliza Carlos.

"Na wewe husahau, kama alikukela msamehe, nenda mwambie aje aketi na sisi hapa", Carlos aliagiza.

"Achana na huyo mshenzi, atatupotezea muda wetu, mbona wasichana wapo wengi tu bosi", Jakina alieleza msimamo wake.

"Hapana, nimesema nenda mwambie aje hapa".

"Mkorofi yule bosi".

"Jakina, elewa kuwa si ombi, nasema nenda mwambie aje aketi na sisi hapa, ni wakati wa kumuomba msamaha kwa yaliyopita", Carlos alieleza huku Jakina akisimama,



****Naam simulizi inazidi kupamba moto

*********ITAENDELEA
BURE SERIES
 
SEHEMU YA 57



Huku mapigo yake ya moyo yakimwenda kasi, Jakina alitembea hadi mahali alipoketi Mama Feka. Aliona njia pekee ni utani, hivyo alimtokea kwa nyuma na kumshika bega.

"Helo, hujambo mrembo", alisema Jakina huku Mama Feka akigeuka. Macho yao yalipokutana, Mama Feka akaonyesha mshangao wa uongo.

"Haaa, wewe ndiye yule kipofu wa Supermarket?", Mama Feka alihoji.

"Hapana, ilikuwa bahati mbaya".

"Ilikuwa bahati mbaya, mbona ulikusudia kunipiga?".

"Ibilisi tu dadangu, bosi amenituma kwako".

"Bosi amekutuma kwangu, anasemaje?".

"Anaomba uhamie kwenye meza yake, tupate chakula pamoja".

"Tupate chakula pamoja, nikikuita kipofu unachukia, hapa unaona nakula, halafu unasema tukapate chakula pamoja na bosi wako, mbona siwaelewi?".

"Tunaweza kuhama na chakula chako, tafadhali niruhusu nikubebee chakula", Jakina aliomba.

"Hapana, mwambie bosi wake sina muda huo", Mama Feka alieleza.

"Sawa, lakini unapoteza bahati yako", Jakina alimwambia.

"Acha ipotee", Mama Feka alieleza kwa kujiamini.

Jakina alirejea kwenye meza ya Carlso.

"Yule msichana ni jeuri sana, anasema hana muda wa kuonana na wewe, nimemwambia anapoteza bahati amesema acha ipotee, anajiamini sana, yawezekana ni mtoto wa kigogo", Jakina alieleza.

"Achana naye, iko siku atanasa", Carlos alieleza, baada ya kupata vinywaji na chakula, Carlos na mpambe wake Jakina waliondoka. ****************

Niliendesha gari kwa mwendo wa kasi ili tuwahi kufika. Wakati huo nilikuwa nikiendesha gari aina ya Isuzu Troupe steshen wogan yenye rangi ya kijani, Fred alikaa kimya akiniangalia, bila shaka aliuhofia mwendo wangu. Tulipofika kwenye taa za kuongoza magari zilizoko katikati ya Barabara za Mandela na Uhuru, eneo la Buguruni, nilisimama ili kusubiri ruhusa ya taa hizi.

Kila mmoja alikaa kimya akitafakari nini hatma ya jukumu lililokuwa mbele yetu, magari yalipoanza kuondoka, niliongeza mafuta nikayapita baadhi ya magari yaliyokuwa mbele, tulipofika kwenye taa za Tazara, zinazoruhusu magari yanayotumia Barabara za Nyerere na Mandela, tulisimama tena hadi zilipoturuhusu kuendelea na safari.

Dereva wa gari lililokuwa mbele yetu alinionysha ishara ya taa, nikalipita gari hili kwa mwendo wa kasi, nadhani dereva huyu alitambua haraka tuliyokuwa nayo, akaamua atupishe. Ni madereva wachache sana barabarani wenye uelewa kama huyu, nilipiga honi ya asanye, nikaongeza mwendo.
.
"Uko vizuri", nilimwambia Fred aliyekuwa kimya.

"Niko sawa", alisema huku akiniangalia.

"Lolote laweza kutokea, lazima tukubaliane na hali hiyo", nilimwambia Fred.

"Najua hivyo bosi, lolote laweza kutupata, lakini naamini kuwa tutashinda, wewe ukisimamia jambo sidhani kama linashindwa", alinipamba.

"Ni kweli, lakini kila jambo na wakati wake", nilisema wakati nikiingia kwenye maegesho ya magari ya Uwanja wa Ndege. Nilitafuta mahali pazuri nikaegesha gari.

"Fred... Hapa tumekuja kufanya kazi moja tu, kumkamata Afisa Ukaguzi, tukifanikiwa kumkamata huyu, kazi yetu itakuwa rahisi, vinginevyo itategemea kudra za Mwenyezi Mungu".
 
"Atakamatwa tu", Fred alisema kwa kujiamini.

"Sikiliza Fred, ingia ndani omba kuonana na Mr. Raymond Kenoko, ndiye Afisa Ukaguzi mwandamizi. Utakapomuona, mwambie kuna mgeni wake ndani ya gari, akifika hapa tumemaliza kazi", nilimwambia Fred. Aliniangalia kwa sekunde kadhaa halafu akavuta shati na kutoa bastola yake ndogo, akaigagua.

"Iweke hapo kwenye droo ya gari, hapa si mahali pake", niliagiza, akafungua droo ya gari akahifadhi silaha yake, akafungua mlango wa garu na kutoka taratibu kama ilivyo kawaida yake.

Kwa wasiomfahamu Fred, ni mmoja wa vijana watanashati, mtaratibu, hata vitendo vyake huvifanya taratibu, ukimuona ghafla unaweza kudhani ni mtu zoba, lakini ukihitaji undani wake, unaweza kuingia kwenye mto wenye mamba ili asikutie mikononi mwake.

Wakati nikimsubiri Fred, niliwasiliana na Kanali Emilly, kumuomba ajiweke tayari kuonana nasi wakati wowote kuanzia sasa. Niliwasiliana pia na Claud Mwita na Julius Nyawamiza kuwatahadharisha na hali ya sasa pia kuwaandaa kwa kazi.

Nikiwa ndani ya gari niliweza kuona kila mtu aliyekuwa karibu yangu, nikisaidiwa na aina ya vioo ya gari hii, kwani mtu akiwa ndani haonekani kabisa, lakini unaweza kumuona mtu wa nje kwa ufasaha zaidi. Mara Fred alifungua mlango akaingia.

"Huyu jamaa ametoka hapa dakika ishirini zilizopita, wanasema amekwenda kupata chakula pale Transt Motel, tumsubiri hapa au unasemaje bosi?", Fred alihoji.

"Hapana, hapana twende haraka", nilisema huku nikitoa shilingi elfu moja ili Fred akalipie ushuru wa maegeshi ya uwanja.

Haraka nikaliweka gari barabarani, nilipoona taa za Barabara ya Nyerere zitatuchelewesha kupita, niliamua kuliingiza gari huku madereva wa magari mengine wakitupigia honi, nikapenya na kuliegesha gari mbele ya Transt Motel, karibu kabisa na Reli ya kati.

Nilitoa picha ndogo ya Raymond Kenoko nikaiangalia kwa mara nyingine, haikuwa rahisi kumfahamu moja kwa moja hivyo ilitulazimu kutumia akili zaidi. Mara nikawaona watu wawili wakitoka ndani ya Transt Motel, walifanana urefu na maumbo yao, akili yangu ikacheza.

"Atakuwa mmoja kati ya hawa. Shuka muite kwa jina, atakayeitika ndiye", nilimwambia Fred akafungua mlango na kuita, "Habari ya kazi Mr. Ray?".

"Nzuri kaka, habari yako", Raymond alisema huku akisogea ili kumshika Fred mkono, mwenzake alitembea hatua chache akasimama kumsubiri. Bahati nzuri alivaa kitambulisho chake shingoni, kikiwa na jina la RH Kenoko.

"Samahani kwa usumbufu, naitwa Jabir Idrisa, nimefika ofisini kwako nikaelezwa kuwa umetoka kwa ajili ya chakula, nikaona nikufuate, kwa ufupi ni kwamba nina mzigo umekwama, lakini nimeelezwa kuwa nikikuona waweza kunisaidia, sasa tunafanyaje kaka?", Fred alidanganya.

"Nani kakutuma uje kwangu?" Alihoji kwa sauti nzito.

"Carlos", Fred alidanganya.

"Ahaa, sawa sawa, ni mzigo tofauti na unaoingia leo?", alihoji.
 
"Ndiyo, ni aina nyingine, labda tuingie ndani ya gari ili tuelekezane vizuri, uangalie uwezekano".

"Hakuna shaka", Raymond Kenono alisema huku akimuelekeza mwenzake atangulie ofisini. Fred alifungua mlango wa gari wakaingia.


"Mnanipeleka wapi jamani?", Raymond Kenoko alihoji, wakati naingiza gari kwenye Barabara ya Nyerere kuelekea mjini, baada ya kuiacha barabara inayoingia Uwanja wa ndege.

"Uwe mpole kaka, sehemu ambayo utaweza kujibu maswali yetu vizuri", nilimwambia kwa sauti ya ukali kidogo. Nilifungua droo ya gari nikatoa kitambulisho changu, nikamuonyesha.

"Nimekosa nini jamani?", alihoji kwa sauti ya kukata tamaa huku mikono yake ikitetemeka.

"Sikiliza kaka, sisi ni watu wema kabisa, watumishi wenzio katika serikali, huna budi kutulia na usijaribu kufanya lolote ambalo linaweza kuyahatarisha maisha yako", Fred alimwambia.

"Nimekuelewa kaka, sasa napaswa kufanya nini? kama kuna tatizo linahitaji ufafanuzi tuzungumze tu, dunia ya sasa hakuna siri, mnilinde jamani", Raymond Kenoko alieleza.

"Sikiliza Mzee Ray, tunakuhitaji kwa mazungumzo ya dakika ishirini hivi, halafu tutakuacha utarudi kazini kwako, cha msingi ni ushirikiano, wewe unajua kwa nini tumekukamata, naamini hivyo", nilimwambia.
.
"Hapana, hakika sijui lolote", alisisitiza.

"Sawa, kama hujui tutakusaidia kujua, cha msingi ni wewe kuwa na ushirikiano", Fred alisema.

Tulipofika kwenye makutano ya barabara za Nyerere na ile inayokwenda Vingunguti, tuliiacha barabara ya Nyerere, nikachepuka na kuingiza gari kwenye barabara ndogo ya dharura, inayopita kushoto, pembeni mwa barabara hii ya Nyerere, nikaliongeza gari mwendo.

"Mtanisaidiaje?", alihoji.

"Kuhusu nini?", Fred alimuuliza.

"Kuhusu kusaidiana ili tumalize jambo hili lisifike mbali, maana ukipuuzia upole, kitakuwa kidonda", alibainisha.

"Ni kweli, lakini ni jambo gani wakati wewe umesema hujui kwa nini tumekukamata?", nilimwambia.

"Kwa vyovyote vile kutakuwa na sababu, haiwezekani maofisa kama nyie mnikamate tu bila sababu, lazima ipo sababu ndiyo maana nikasema tuzungumze kirafiki, tusiharibiane kazi. Tusaidiane", alijitetea.

Mara simu yangu ya kiganjani ikaita, Kanali Benny Emilly alitaka kujua tumefikia wapi, maana kabla hatujatoka uwanja wa ndege kuelekea Transt Motel nilimjulisha wapi atusubiri, nilimweleza kila kitu akatuelekeza mahali alipo.

Tulipofika kwenye ofisi za kiwanda cha sigara cha Master Mind, kilichoko kando ya barabara hii, geti la kuingia liliachwa wazi, hivyo niliingiza gari moja kwa moja. Kama unavyojua sheria inaturuhusu kutumia ofisi yoyote ya umma na binafsi mahali popote, wakati wowote kwa ajili ya usalama wa nchi. Kanali Emilly alikuwa amefika mapema sehemu hii na kuandaa ofisi ya muda, kwa ajili ya kazi hii.

Meja Iddi Satara, mmoja wa wasaidizi wa karibu wa Kanali Emiily alinionyesha ishara nikalisogeza gari mahali alipokuwa, wakati haya yanafanyika Raymond Kenoko alibaki ameduwaa asijue la kufanya.

"Mtanisaidiaje?", alijitetea kwa mara nyingine.
 
SEHEMU YA 60

"Amini tutakusaidia, twende kwanza uongee na mkubwa, cha msingi uwe mkweli, vinginevyo utaozea jela, haki ya Mungu", nilimwambia wakati tunatoka ndani ya gari, tukaelekea kwenye ofisi ya Kanali Emilly ya muda.

Kanali Emilly aliketi mbele ya meza kubwa iliyozungukwa na viti kadhaa vya wageni, ilikuwa ofisi ya kuvutia sana, Meja Satara alimuonyesha Raymond sehemu ya kuketi, bila ajizi akaketi.

"Karibu bwana Raymond Kenoko, Afisa Mkaguzi Mwandamizi wa Uwanja wa ndege. Naitwa Kanali Benny Emilly, kwa ufupi mimi ndiye nimewatuma vijana wangu wakukamate, ili ufike mbele yangu ujibu maswali mawili matatu, halafu tunakuachia, kikubwa hapa ni ushirikiano, tusaidie tukusaidie, bila shaka umenielewa?", Kanali Emilly alimwambia.

"Ndiyo baba, niko tayari kujibu maswali yako na kutoa ushirikiano unaotakiwa", alijibu kwa hofu.

"Una muda gani sasa toka umepata ajira serikalini?", Kanali Emilly alimuuliza.

"Miaka kama ishirini na sita hivi", alijibu.

"Miaka kama ishirini na sita, unaonyesha kuwa huna hakika", Kanali Emilly alihoji.

"Ni miaka ishirini na sita, hakika ni ishirini na sita sasa", alisisitiza.

"Umeoa?".

"Ndiyo baba, nimeoa".

"Una watoto?".

"Yes, nina watoto watatu".

"Wazazi wako hai?".

"Hapana, wote ni marehemu".

"Una nyumba ndogo, namanisha mke mwingine?".

Akaonekana kubabaika, baada ya kutafakari kwa sekunde kadhaa akasema, "Yupo rafiki wa kike, lakini hayuko karibu sana, unajua hali ya maisha sasa ni ngumu".
.
Kanali Emilly aliendelea kumuuliza Raymond maswali mengi ambayo aliyajibu vizuri. Pamoja na maswali hayo ya kirafiki, akili ya Raymond ilikuwa katika dimbwi la mawazo, akijiuliza kimya kimya, hususan swali la Carlos. Fred alipomwita kwenye gari, alijitambulisha kama kijana wa Carlos, ndiyo maana akakubali kupanda gari, sasa alijiuliza kwanini watu hawa walimtaja Carlos lakini baadaye wakamkamata na kumweka chini ya ulinzi.

"Unamfahamu mwana mama mmoja anaitwa Hawa Msimbazi?", Kanali Emilly alimuuliza Raymond.

"Hapana, simjui".

"Humjui, na huyu mzungu anayeitwa Carlos?", swali hili lilimchanganya kidogo, akaweweseka.

"Simjui pia", alisema huku akitingisha kichwa chake kukataa kwa msisitizo.

"Unamjua", nilirukia.

"Siwezi kusema kitu ambacho sikijui, haki ya Mungu simjui Hawa wala Carlos", alisisitiza kwa mara nyingine.

Kanali Emilly alisimama, alitoka mahali alipokuwa ameketi akatembea hadi kwenye mgongo wa Raymond. Mzee huyu alikuwa na huruma kwa kila kiumbe kilichotengenezwa na Mungu, lakini pia alikuwa katili kwa viumbe vilivyokuwa hatari kwa maisha ya viumbe wengine. Alipenda kucheka sana, lakini pia alikuwa mwenye hasira sana.

"Unadhani sisi ni wapumbavu, unadhani hatuna kazi zingine za kufanya mpaka tukulete hapa, nilitegemea utakuwa muungwana, utajibu maswali yangu vizuri kama tulivyoanza, kumbe naongea na mpumbavu. Sikiliza, naomba ujibu swali langu. Unamfahamu Carlos Dimera", Kanali Emilly alihoji kwa sauti ya kutisha.
 
Raymond aliinamisha uso wake chini, akabaki kimya. Kanali Emilly aliendelea kusimama nyuma yake, akisubiri jibu.

"Sikiliza, wewe ni raia wa Tanzania, tena mtumishi wa umma, Carlos ni mzungu, ametoka mbali sana, mpaka anafika hapa nchini, taarifa zake zote tunazo, mpaka anawasiliana na wewe kuhusu mzigo uliokwama Adis Ababa, Ethiopia tunajua, nashangaa kwanini unaficha jambo ambalo liko wazi kabisa", nilimwambia.

"Mr Raymond, unakumbuka kabla hatujapanda gari uliniuliza swali gani, ulisema ni huu mzigo unaoingia leo au mzigo mwingine, sasa unaficha nini inaeleweka hivyo", Fred alimwambia.

"Raymond, unataka usaidiwe au uishie jela?", Kanali Emilly alimuuliza.

"Naomba nisaidiwe", alisema huku machozi mengi yakimtoka.

"Tutakusaidiaje wakati hutaki kufunguka, jaribu kusema ukweli ili tuangalie jinsi ya kukusaidia", Meja Satara alieleza.

"Kabla sijasema chochote naomba mnihakikishie usalama wangu, huyu Carlos ni mtu hatari sana, anaweza kuniangamiza", Raymond alieleza.

"Kuhusu hilo ondoa shaka, tutakulinda kwa gharama yoyote", Fred alimwambia.

"Na vipi kuhusu familia yangu?" alihoji.

"Kuhusu familia yako, wako chini ya uangalizi wa jeshi la polisi kabla hata hatujakukamata, hivi tunavyoongea hapa mkeo na watoto wako mikononi mwa polisi, lakini kwa ajili ya usalama wao tu", nilimwambia akaonekana kushangaa.

Baada ya maelezo hayo, Raymond alieleza kila kitu kuhusu Carlos, alieleza jinsi alivyotambulishwa kwake na Denis, Afisa Ukaguzi mstaafu, ambaye sasa ni marehemu, alieleza jinsi alivyofahamiana na Hawa Msimbazi na mengine mengi, pia alieleza mbinu wanazotumia kuingiza dawa za kulevya nchini, na mkakati wa kuua yeyote anayeonekana kuingilia biashara yao.

"Asante, kazi yako imekwisha, Meja Satara, hakikisha huyu jamaa anapelekwa mahabusu ya siri mpaka nitakapojulisha vinginevyo", Kanali Emilly aliagiza.

"Hakuna tatizo mkuu", Meja Satara alieleza huku akijiandaa kuondoka na Raymond.

"Mlisema mtanisaidia, imekuwaje?".

"Tulisema tutakusaidia baada ya kazi hii kwisha salama", nilimwambia. Kiasi fulani nilifurahi kumkamata mtu huyu, maelezo yake yalitufanya tupate mwanga. Niliwapigia simu Claud na Nyawaminza kuwafahamisha kilichotokea wakaeleza furaha yao.

.
**********************

Wakati huo Mama Feka alikuwa kwenye foleni ya kununua tiketi ya kuingia California Dreema. Alivaa vizuri kiasi cha kumfanya mwanaume yeyote kuingiwa na tamaa, baada ya kupata tiketi yake alipenya mlango na kujitosa ndani ya ukumbi huu.

Muziki laini ulikuwa ukipenya masikioni mwa wapenzi wa starehe, kila mmoja alionekana akicheza na mpenzi wake, huku wengine wakiwa wameketi kwenye meza za pembeni wakiupiga mtindi.

Kama ilivyo kawaida yake, Mama Feka alipita akatafuta sehemu nzuri ambayo anaweza kuonekana kwa urahisi, alifanya hivi baada ya kuwa amemuona Carlos Dimera na wapambe wake wakiwa wameizunguka meza iliyojazwa vinywaji vya kila aina.

Ili aweze kuonekana, Mama Feka alianza kulicheza rhumba, alicheza vizuri huku akigeuka kila upande,
 
kijana mmoja aliyekuwa karibu yake alivutiwa na mwana mama huyu, hivyo akajisogeza na kumuomba wacheze. Lakini hilo lingemfanya auhalibu mtego wake, alichofanya Mama Feka ni kumkwepa kijana huyo, akaendelea kucheza peke yake, kijana huyo kwa aibu akajiondoa eneo hilo.

Jakina alifanikiwa kumuona Mama Feka, hakufanya ajizi, haraka alizifikisha habari kwa Carlos, ambaye alikuwa ameketi kwenye meza ya vinywaji na akina dada kadhaa.

"Bosi, unamuona yule mbabe wa Supermarket?", Jakina alimwambia Carlos Dimera.

"Yuko wapi?" Dimera alihamaki.

"Yule anacheza peke yake pale".

"Oh, nimemuona, sasa sikiliza, tafuta mbinu ya kuwafanya hawa malaya wengine wasinisogelee, asije akaniona mhuni. Kwa vile wewe na yeye damu zenu zimetofautiana, acha niende mimi mwenyewe, nimuombe tucheze kidogo", Carlos alimwambia Jakina huku akielekea mahali alipokuwa Mama Feka.

"Helo, habari yako?" Carlos alisalimia baada ya kumshika bega. Haraka Mama Feka aligeuka na macho yao kukutana.

"He, na wewe unakuja huku?" Mama Feka alihoji.

"Mimi ni mtu wa starehe, lazima nifike sehemu kama hizi, nimekuja kukuomba tucheze kidogo", Carlos aliomba.

"Unataka ucheze na mimi wakati mlitaka kunipiga kule Supermakrt?".

"Ilikuwa bahati mbaya, waswahili mnasema wanaogombana ndiyo wanaopatana, pole kwa yaliyotokea, msamehe kijana wangu hakuwa na nia mbaya", Carlos alieleza.

"Sawa, nimekuelewa, karibu tucheze", Mama Feka alifurahi kupata nafasi hiyo, wakaanza kucheza huku wameshikana.

"Unaitwa nani?" Carlos alihoji.

"Sweety".

"Oh, jina zuri sana, unafanyakazi gani Sweety?".

"Niko nyumbani tu, nimemaliza shule, ndiyo natafuta kazi".

"Umesomea nini?"

"Mambo ya Maabara", Mama Feka alidanganya.

Oh, very god, umepata kazi, mimi namiliki kiwanda kikubwa cha madawa".

"Asante, na wewe unaitwa nani?".

"Carlos, au ukipenda unaweza kuniita Carlos Dimera".

"Wewe ni Mtaliano?".

"No, hapana, si kila mzungu Mtaliano. Mimi ni raia wa Colombia", Carlos alifafanua.

"Unafanya kazi gani?".

"Yaani mimi nifanye kazi, mimi ni mfanyabiashara, business men".

"Unafanya biashara gani?".

"Ohoo, sasa hapa umekuja kustarehe au kunihoji".

"Hapana, nilitaka tufahamiane tu".

"Utanifahamu tu, si bado tuko pamoja".

"Sawa", wakaendelea kucheza.

Mama Feka akamshukru Mungu kwa kazi aliyoifanya kwa muda mfupi, aliyakumbuka maneno ya Teacher kuwa Carlos ni mtu hatari, lazima awe makini, akaupiga moyo wake konde na kujiweka tayari kwa lolote, akimtanguliza Mungu katika jukumu hilo zito, lililoko mbele yake.
.
Boing 787, mali ya Shirika la Ndege la Uholanzi, iliwasili na kutuwa taratibu kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius K. Nyerere, Jijini Dar es Salaam, majira ya saa nne na dakika arobaini na tano usiku. Baada ya abiria wa Dar es Salaam kutoka ndani ya ndege hii. Kazi ya kutoa mizigo ilichukuwa masaa kadhaa, hatmaye kila abiria alitoka na mzigo wake, baada ya kutimiza masharti.

ITAENDELEA
 
.
Mimi na wenzangu, Claud Mwita, Julius Nyawaminza na Fred Libaba, tulikuwa tumewasili uwanjani hapa masaa mawili kabla ya ndege hii kushuka katika ardhi ya Tanzania, wakati huo tukitumia magari manne tofauti. pia tukiwa tumejiwekea usalama wa kutosha. Tulijipanga vizuri kwa lolote. Ili kufanikisha kazi iliyokuwa mbele yetu, Claud na Nyawaminza, walitumia gari ndogo aina ya Toyota IST rangi ya Blue yenye vioo vyeusi ambavyo mtu hawezi kuona ndani.

Nje kabisa ya uwanja, liliegeshwa gari lingine lililochaa aina ya Suzuki Escudo, vijana wawili waliovalia mavazi machakavu, Tumain Changasi na China Kilinda, walionekana wakihaha kurekebisha sehemu ya gari hii, Ukweli ni kwamba vijana hawa walikuwa hapo kwa kazi maalumu,

Claud aliyekuwa akiendesha gari IST, aliliingiza gari upande wa pili kwenye maegesho ya taksi. Kama ilivyo kawaida baadhi ya madereva taksi wanaoegesha magari yao eneo hili walilifuata gari hilo ili kumfahamisha dereva kuwa sehemu hiyo magari ya watu wa kawaida tofauti na taksi hayaruhusiwi.

Vijana wawili wawili ambao ni madereva taksi haraka walilifikia gari hili na kugonga kioo upande wa dereva, Taratibu Claud alishuka kioo hicho na kuacha ufa kidogo ili aweze kuwasikiliza.

"Ondoa gari, eneo hili ni kwa ajili ya taksi tu", alisema mmoja wa vijana hawa aliyeonekana kuwa na jazba, Clauud alimwangalia kwa sekunde kadhaa halafu akauliza..

"Kwenu, ondoa gari ndiyo salamu?".

"Salamu ya nini, nimesema ondoa gari lako, hii ni sehemu ya taksi tu, vinginevyo gari lako litafungwa minyororo na faini yake ni elfu hamsini, mimi nakusaidia usipigwe faini wewe unaleta jeuri, ukitaka salamu tii sheria kwanza", kijana huyo aliongeza kwa jazba.

Ok, kama unaona fahari, enedelea kupaza sauti yako", alisema huku akipandisha kioo cha mlango cha upande wake na kuwaacha vijana hao wakiendelea kusuburi. Walisimama kwa dakika kadhaa halafu wakaondoka huku wakilalama.

Kabla ya kufika eneo hili, nilikuwa nimewaelekeza wenzangu kila kitu. Fred akiwa peke yake alitumia gari ndogo aina ya Toyota Starlet, rangi nyekundu iliyochoka kidogo, aliliegesha gari hilo karibu na sehemu ya kutokea abiria, bahati nzuri Fred hakupatwa na misukosuko ya kuulizwa maswali kama wenzake.

Mimi nikitumia gari ndogo pia, Toyota Corolla, ambalo pia mtu akiwa ndani huwezi kumuona kutokana na vioo vyake kuwa vyeusi, nililiegesha gari kwenye barabara ndogo inayotoka kituo cha mafuta cha PUMA. Karibu yangu kuliwekwa bango linalokataza magari kuegeshwa mahali hapo, nikalipuuza/

Niliwakumbuka vijana wetu wa bodaboda ambao Peter Twite aliwaweka sehemu mbalimbali kwa kazi maalumu, nikajuwa huu ndiyo muda wao itakapobidi.

Tulikuwa tumejipanga vizuri. Hatukufanya kosa hata kidogo, tukiwasiliana kila baada ya dakika chache,
 
hatmaye, Fred alinidokeza kwa njia ya simu kuwa mambo yamewiva. Nikajuwa kazi imeanza, nilichukua bastola yangu iliyokuwa kwenye droo ya gari nikaiondoa usalama.

Mara nikaliona gari wanalotumia Claud na Nyawaminza linapita taratibu mbele yangu, mapigo ya moyo ya moyo wangu yakanienda kasi. Baada ya muda mfupi, Mitsubishi Pajero lenye rangi nyekundu ambalo dereva wake aliwasha taa, kuashiria hatari lilipita likikifuatwa kwa nyuma na gari kubwa Lori aina ile ile ya Mitsubishi, dereva wa gari hilo alijaribu kuyapita magari yote yaliyokuwa mbele yake, akaliingiza kwenye Barabara kuu ya Julius Nyerere kwa ajili ya kuelekea mjini huku gari lingine likiwafuata kwa nyuma.

"Kumekucha", nilimwambia Claud kwa njia ya simu ya mkononi, "Endesha kwa mwendo wa kasi kidogo, yapite magari ya adui, angalia msifanye chochote, nitalianzishea mimi", nilimwambia wakati naingiza gari langu kwenye barabara ya Nyerere.
.
Magari yoteyalipokipita kituo cha mafuta cha OILCom, karibu na stendi ya daladala ya Kipawa, mimi nilikuwa karibu yao zaidi. Haraka niliwasha taa za mbele, nikaanza kulichezesha gari langu, nikimbana dereva wa gari la mbele kumtaka aegeshe gari hilo kando ya barabara, vivyo hivyo, Fred alifanya kwa gari kubwa lililobeba mzigo, magari yote matatu yalichepuka kutoka barabara kubwa na kuegeshwa kando.

Hawa Msimbazi aliyekuwa katika mawani meusi, akionekana kama haelewi chochote, alishusha kioo upande wa pili wa dereva, "Nini unatuvamia kama sisi wahalifu?", aliuliza,macho yake yalipokutana na yangu akaanza kugwaya.

"Habari ya kwako, samahani kwa usumbufu, bila shaka unajuwa kwa nini tumewasimamisha hapa?", nilimuuliza.

"Hapana, sijui kwanini tusimamishwe, mzigo wetu ni malighafi za kiwanda kwa ajili ya kutengeneza tembe za kutibu malaria. Tunaziingiza nchini baada ya kufuata taratibu zote za serikali", Hawa Msimbazi alieleza huku akishuka kutoka ndani ya gari hilo.

"Una hakika?", nilimuuliza baada ya Fred kusongea karibu. Claud na Nyawamiza wao walibaki ndani ya gari wakiangalia usalama wetu.

"Hakika kabisa, taratibu zote za kuingiza mzigo huu zimefanyika, upekuzi umefanyika, hatujaingiza mzigo tofauti na matakwa ya serikali", alisisitiza.

"Si kweli, fungua tuhakikishe", niliagiza.

"Wewe ni mtaalam wa kugundua aina ya poda zinazoingizwa nchini na kupelekwa viwandani?, haifunguliwi mpaka ifike sehemu husika, hii ni malighafi hatari, unaweza kunusa sumu ukafa, tukaulizwa kwanini tuliruhusu".

"Nimesema fungua tuhakikishe", nilimwambia kwa sauti ya ukali kidigo, baada ya kujiuliza akarudi ndani ya gari na kujaribu kupiga simu, lakini nilikuwa mwepesi kuchukuwa simu hiyo. Nilitoa kisu changu kidogo kilichokuwa mfukoni nikazikata kamba.

Kulikuwa na shehena kubwa ya dawa za kulevya, aina tofauti tofauti, nilimwangalia mwanamama huyu kwa hasira, wakati huo alikuwa akiniangalia kwa macho ya hasira pia, akitweta nikaliona gari la akina
 
SEHEMU YA 65

Tumaini linasogea kwa ajili ya kuimalisha ulinzi,

"Unamfahamu, mtu mmoja anaitwa Raymond Kenoko?", nilimuuliza.

"Raymond Kenoko?, Mmmm, simjui", alijbu baada ya kutafakari.

"Humjui mtu aliyefanikisha mpango wenu wa kuingiza dawa za kulevya hapa nchini?. Mtu aliyewatengenezea mazingira ya kutoa huu mzigo".

"Nimesema simjui, hivyo usilazimishe kujibu swali ambalo sijui".

"Sawa, mtakutana mahakamani, huu ni ushahidi wa kutosha kabisa kuwatia hatiani, haya ni madawa ya kulevya aina ya heroin", nilimwambia.

"Kama ni madawa ya kulevya mimi siyajui, usinihusishe na mzigo huo, si wangu". Hawa Msimbazi alieleza msimamo wake.

Tuliwachukuwa watu hawa na kuwahifadhi sehemu ambayo pesa haiwezi kutumika, nilijione mwenye bahati kufanikisha nusu ya zoezi hili, Hawa Msimbazi na wenzake walikuwa kimya wakitafakari kilichotokea. Shehena kubwa ya dawa za kulevya iliyokuwa iingizwe nchini imekamatwa na kufuta ndoto zao za kupata utajiri.

Gari moja ambayo hata sisi hatukuitilia shaka, ilisimama hatua kadhaa, kutoka mahali tulipokuwa, watu wanne walitoka ndani ya gari hiyo na kutuangalia kwa hasira, Fred alipojaribu kuwafuata walirudi ndani ya gari na kuondoka kwa mwendo wa kasi, wakiacha vumbi. Hata hivyo Claud alijaribu kulifuata gari hilo, likapotelea eneo la Vingunguti.


*************************

Carlos Dimera ndiyo kwanza alikuwa amerejea kutoka kwenye starehe, habari za kukamatwa kwa Hawa Msimbazi na vijana wake wengine zilionekana kumshitua sana, Jakina Nombo na wengine walikuwa wameduwaa wasijue cha kufanya.

"Kwanza niwafahamishe, huyu ni mchumba wangu, anaitwa Sweety", Carlos alisema huku akiwaangalia vijana wake, halafu akamgeukia Sweety, "Mpenzi, hawa ni wafanyakazi wangu, jione uko huru, usihofu kuwa na sisi, kilichotokea tutakirekebisha, ni ajali katika kazi", alieleza Carlos.

"Asante, nakushukuru sana baby kwa kunitambulisha, habari zenu?", Mama Feka alisalimia.

"Habari nzuri, mbaya yote ni habari", Nombo alisema.

"Oke, sasa nataka kujuwa, ilikuwaje mkaleta taarifa za uongo, kuwa Teacher ameuawa, Nombo wewe ndiye ulileta taarifa hiyo, ilikuwaje kuleta taarifa ambazo huna hakika nazo?", Carlos alihoji kwa sauti ya kutetemesha.

"Bosi Carlos, huu si wakati wa kulaumiana, waswahili walisema maji yakimwagika hayazoleki, cha msingi ni kuangalia nini kifanyike kuwaokowa wenzatu, halafu mambo mengine yatafuata", Jakina alieleza.

"Ndiyo, lakini ni vyema kujuwa, ukisema tuangalie mbele, bila kukumbuka nyuma, hatuwezi kufanikiwa, taarifa iliyopo ni kwamba Teacher aliuawa wakati wa shambulizi, gari yake iliteketezwa vibaya kwa mjibu wa Nombo. Leo ameharibu mipango yetu, mtu mmoja Teacher ambaye siamini kabisa kama ana mbinu za kutushinda", Carlos alieleza kwa hasira.

"Hakika ninaposikia habari hii, nashindwa kuamini bosi, tulimfuatilia Teacher kuanzia mwanzo mpaka anaingia Benjamin Mkapa, gari aliyoingia nayo ni ile ile iliyopigwa kombora, mtu mmoja alikufa katika shambulizi hilo, siami", Simba alibainisha.
 
"Yule ni mpelelezi wa siku nyingi, huenda aligundua kitu akampa mtu mwingine kuendesha gari hilo, kama yuko hai basi ni mjuzi wa hali ya juu, mbinu za ziada zinahitajika", Nyati aliongeza.

Mama Feka alikaa kimya akiwasikiliza kwa makini, kiasi fulani aliogopa maneno ya watu hawa, alimuonea huruma Teacher, akajiona mwenye bahati kufanikiwa kuingia ndani ya ngome hiyo, lakini pia akijiuliza, iwapo atabainika itakuwaje.

Waliongea mambo mengi, wakipanga hili na lile, hatimaye wakaweka azimio kuwa mzigo mwingine wa dawa za kulevya ulikuwa stoo uhamishwe haraka iwezekanavyo, kupisha upekuzi wa polisi baada ya hapo utarejeshwa na kuingizwa sokoni.

"Walichofanya ni kupunguza kasi tu, lakini hii itatuongezea kasi zaidi, mtu mjinga, mtu asiyependa kuishi maisha ya kifahari, wenzake wanakula kuku na bata, yeye anakosa usingizi kwa ajili ya kuziba mianya ya wengine", Carlos alilalama.
.
"Binadamu hatulingani bosi", Nombo alisema.

"Wakati huu msilale, fanyeni kazi usiku huu mpaka alfajiri tupate taarifa za Hawa na wenzake wamewekwa kituo gani cha polisi, shilingi ngapi inahitajika kumaliza jambo hilo, mzigo uhamishwe, kazi zingine zote zisimame mpaka hapo nitakapowajulisha vinginevyo.

"Ametuchokoza, ajiandae kulia", Jakina alieleza huku akisimama.

Ni wakati wa kuwashirikisha wageni, wamesafiri kutoka huko kuja hapa nchini kwa kazi moja, kufanikisha jambo hili", aliagiza Carlos.

Watu wote walikaa kimya ndani ya chumba cha mkutano. Carlos Dimera alionyesha dhahiri hali ya woga na hasira, akivuta sigara kubwa iliyosokotwa kwa karatasi ngumu, alitembea kutoka kona moja ya chumba hiki kwenda kona nyingine huku akitafakari kwa kina kilichokuwa kimetokea. Alijitahidi kuvuta sigara hiyo mpangilio na kupuliza moshi mwingi hewani. Hali iliyowafanya wafuasi wake wapatwe na hofu.

Mama Feka au Sweety, kama alivyojitambulisha kwa Carlos, alikuwa mmoja wa watu waliokuwa ndani ya chumba hiki cha
mkutano wa siri, akishiriki kama mjumbe wa kawaida. Lengo la Carlos ilikuwa kumshirikisha mama huyu katika biashara ya dawa za kulevya.

Mzungu huyu aliutambua urembo wa Mama Feka, awali alikuwa ameteta na Jakina, kuwa unapokuwa na msichana mrembo kama
huyu kwenye biashara yako asilimia tisini mambo yatakuwa shwari. Hata aliposhiriki kikao hiki wajumbe walilitambua kusudi la Carlos, wakampokea Mama Feka kwa mikono miwili.

Mfano wa mtu aliyeshikwa na kigugumizi, Carlos alivunja ukimya uliokuwepo kwa kusema. ..."Imenishangaza mno, watu makini, watu mnaojitambua, kuyachezea maisha yenu mbele ya Simba mwenye njaa, sielewi nini kimewalevya mpaka mnazidiwa maarifa na wajinga?. Haiwezekani, Hawa na Tony wakamatwe kama kuku, halafu, shehena yote ipotee. Lakini cha ajabu na kusikitisha zaidi, wenzetu hawa wamefika mahakamani. Mmmmm, imenifedhehesha sana Nauliza kila baada ya dakika kuhusu
 
hatima ya jambo hili, wakubwa wanataka kujua nini mkakati wetu au tumejipangaje kumaliza tatizo hili, pesa si tatizo, mtu mmoja, mtu mmoja mpuuzi hawezi kufanya tuonekane wapuuzi", alitembea tena kutoka upande mmoja wa chumba hiki kwenda upande mwingine huku wajumbe wakimwangalia.

"Inachosema ni hakika bosi, lakini usitishwe na ukimya huu, ukadhani labda tumeridhishwa na jambo hili, niseme wazi kuwa adui anaishi kwa mbinu, ambazo hakika siku zake za kuishi sasa zinahesabiwa, hivi tunavyoongea, vijana wetu wako katika msako mkali kujua mjinga huyu yuko wapi. Naamini msako huu utafanikiwa haraka iwezekanavyo, kwani tunatumia vifaa vya kisasa", Nombo alieleza.

Haraka Jakina akasimama, tofautu na mwenzake aliyeongea ameketi. "Kama ulivyosikia bosi, mahakama ilikuwa itoe
hukumu ya kesi hii leo, lakini kutokana na jitihada kubwa zilizofanywa, hukumu imeahilishwa mpaka kesho ili tuweze
kujipange. Nakuhakikishia Hawa na Tony kesho wakati kama huu watakuwa huru, mwanasheria wetu pia ni mtu makini sana, cha msingi tuwe wavumilivu, tumalize tatizo hili ndipo tujiulize wapi tulijikwaa", Jakina alieleza.

"Maneno mazuri sana, lakini hayana ufumbuzi wa jambo hili, kila mmoja anaongea kwa mtazamo, kama tunaweza kuwatoa Hawa na Tony kwenye mikono ya sheria, swali langu ni je, huu mzigo utapatikana au utapotea?. Tunapojadili jambo nyeti kama hili, lazima tuangalie uwezekano huo pia", alihoji.

"Swali zuri bosi. Mara tu baada ya Hawa na Tony kukamatwa, haraka tuliwasiliana na watu wetu katika vitego mbalimbali vya usalama wanaopokea mshahara kutoka kwetu, kuwajulisha kilichotokea, hakika ushirikiano wao ni mkubwa mno. Kama unavyojua msimamo wa serikali sasa, unapofikishwa mbele ya mahakama na ushahidi, moja kwa moja unakumbwa na kifungo, lakini maofisa hao ndiyo waliofanikisha mahakama kusogeza hukumu ya kesi hii mbele ili tuweze kujipanga", alisema Nombo.

"Baby naomba uketi", Mama Feka alimwambia Carlos kwa sauti ya mahaba. Sauti ya Mama Feka, ilimfanya Carlos, atabasamu kidogo.

"Asante Sweety wangu, usijali mpenzi, mambo yanapokwenda ndivyo sivyo, lazima tuketi na kutafakari njia sahihi, usiogope Sweety mpenzi, uwe na amani nitaketi", Carlos alisema, halafu akaendelea. ..."Jamani, tupunguze maneno, tupunguze porojo, jukumu lililo mbele yetu ni zito mno, yatupasa kujipanga vyema, Hawa na Tony ni watu kutoka miongoni mwetu. Nasema kwa gharama yoyote lazima watakuwa huru kutoka katika mikono ya sheria. Nataka kuona jambo hill linafanyika haraka iwezekanavyo, hebu jiulize mfano ungekuwa wewe ingekuwaje?", Carlos alihoji baada ya kutoa agizo.

Lakini Carlos na kikosi chake walikuwa wamekosea jambo moja. Hawakujua kama, Mama Feka alikuwa hapo kwa kazi maalumu, alitumia simu yake ya kiganjani kwa usiri wa hali ya juu kurekodi mazungumzo
 
hayo na kuyatuma wakati huo huo moja kwa moja kwenye simu ya Teacher. Carlos Dimera na wafuasi wake waliendelea kujadiliana hili na lile, waliongea mambo mengi, wakipanga hili na lile, hatimaye wakafikia mwafaka.

"Nitalala usingizi mnono iwapo nitasikkia Teacher amekufa, sasa naagiza, kwa gharama yoyote ya pesa, atafutwe ikiwezekana auwawe haraka kabla ya hukumu kesho, uwepo wake unaweza kuharibu mipango yetu", Carlos alisisitiza, huku kila mmoja akipewa jukumu lake.

Hata hivyo, Carlos Dimera aliamua kutumia uzoefu wake wa siku nyingi katika kazi hizi za hatari, aliwatuma kwa siri, vijana wawili Gabriel na George, bila kuwashirikisha wenzake. Hawa walikuwa wakiishi nchini Tanzania kwa siri, wakisubiri matukio kama haya. Vijana hawa wenye uzoefu mkubwa wa mambo ya ujasusi walipewa jukumu la kumtafuta Teacher.

Carlos, aliwaamini sana vijana hawa, waliokuwa wakifanya mazoezi wakati wote, aliujuwa vizuri muziki wao, Ni vijana
ambao wakitumwa kukileta kichwa cha mtu yeyote, wanaweza, kutokana na imani yake kwao, aliwaagiza kumleta Teacher mbele yake akiwa hao ili athibitishe kuwa ndiye, halafu amuue yeye mwenyewe. Hili alilifanya kwa siri kubwa, bila hata Sweety kujuwa.
.
Mara nyingi majasusi hutumia mbinu tofauti katika kufanikisha mambo yao, Gabriel na George waliishi nchini kwa siri, hakuna mtu aliyefahamu uwepo wa majasusi hawa. Hata Jakina aliyekuwa karibu zaidi na Carlos hakuwajuwa vijana hawa.

Gabriel na George walikuwa majasusi waliohitimu mafunzo ya juu ya ujasusi katika vyuo mbalimbali duniani, walilingana kwa kimo na umri, walionekana kama mapacha, lakini ukweli ni kwamba kila mmoja alikuwa na sifa zake,

George akiwa amezaliwa katika mji wa Kano, nchini Nigeria, huku Gabriel akiwa raia wa Afrika Kusini. Vijana hawa walikutana katika chuo kimoja nchini Cuba, ambako walishabihiana kwa kila kitu, hata walipohitimu mafunzo yao ya ujausi walipangwa pamoja, baada ya kununuliwa na wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya kwa ajili ya kulinda maslahi yao.

*************************

Wakati huo huo, mkutano mwingine wa siri, ulifanyika katika Hoteli ya King Air katikati ya Jiji la Bogota, nchini Colombia, ambapo Wafanyabiashara wakubwa, matajiri wa dawa za kulevya walikutana kwa siri kama ilivyo kawaida yao.

Watu hawa walikutana kujadili mafanikio ya biashara yao pamoja na shehena yao kubwa ya dawa za kulevya kukamatwa Jijini Dar
es Salaam, Tanzania na watu wao kufikishwa mahakamani.


Emilio, mfanyabiashara kigogo, aliyefika Dar es Salaam, kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa kuingiza dawa hizo, ambazo awali zilikwamba Ethiopia, alitakiwa kuwaeleza wakubwa hawa kwa nini shehena hiyo ikamatwe baada tu ya kuingia Tanzania.

"Inawezekana hatukuwa makini wakati wa kusafirisha shehena hii? Tanzania kama Tanzania ndiyo njia yetu ya kusafirisha dawa za kulevya kwenda katika nchi nyingine za ukanda wa mashariki. Leo tujiulize,
 
nini kimetokea mpaka shehena hii hii kubwa ikamatwe?", Mfanyabiashara tajiri, ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa mtandao huu, Enock Jonson, alihoji.

"Ni wakati wa Emilio kutoa maelezo, ndiye mtu wetu pekee aliyesafiri hadi Dar es Salaam, lengo la safari ilikuwa kuweka mambo sawa, sasa kama hali ya usalama nchini humo ilikuwa hairuhusu, ilikuwaje wewe ukaruhusu shehena hiyo kuingizwa bila kuwa na uhakika wa hali ya usalama nchini Tanzania", Stephan Bad ambaye kiutendaji ndiye msimamizi mkuu wa biashara ya dawa za kulevya alihoji.

Emilio alikohoa kuweka koo lake sawa, alipaswa kueleza ukweli. Tabia ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya kumuua mwenzao haikuwa tatizo. "Naomba kueleza kuwa wakati naingia Dar es Salaam juzi, njia zote zilikuwa vizuri na wazi kabisa, tukumbuke kuwa nilikwenda Dar es Salaam, baada ya shehena hiyo kukwama, Adis Ababa, Ethiopia, Carlos alikuwa amenieleza kuwa hali haikuwa nzuri wakati huo, lakini baada ya kuweka mambo sawa, hali ikawa shwari, sasa si wakati wa kulaumiana, vijana wanajaribu kila njia kuweka mambo sawa. Tusubiri".

"Wakati mwingine tuwe makini na jambo hili, tusikurupuke kutoa maamuzi", Stephan Bad alieleza. "Hakika, lakini nimesikia kuwa nchini Tanzania sasa njia nyingi zimefungwa, serikali ya nchi hiyo imekuwa macho zaidi, lakini watu wetu Dar es Salaam wamefikishwa mahakamani leo, Carlos amenihakikishia kuwa watatoka kesho,

Hakimu wa kesi hiyo ni mtu wa upande wetu, inasemekana alishinikizwa atoe huku leo, lakini pesa imefanya kazi yake,
ametumia vifungu vya sheria kuweka mambo sawa, jambo hili litakwisha kesho", Emilio alidokeza.

"Punda afe mzigo ufike, nchini Tanzania hatuna mkataba na mtu zaidi ya Carlos Dimera, hao wengine ni vibaraka tu, lazima mtambue kuwa tuna nguvu kubwa Dar es Salaam, hao waliokamatwa tuwaache wafungwe, ili iwe rahisi kuupata huo
mzigo, nakuhakikishia wakifungwa hawa itakuwa na nafasi nzuri kwetu kuupata mzigo huo", Stephan Bad alieleza msimamo wake.

"Itakuwa ngumu zaidi, Carlos amenihakikishia uwezekano wa kuwatoa upo, hakuna sababu ya kuwatosa", Emilio alishauri.

"Hapana, wakati mwingine tumia akili yako ya ziada, fahamu kuwa watu hawa wakifungwa, serikali itatangaza kuteketeza shehena ya dawa hizo, lakini kabla hazijateketezwa zinarejeshwa kwetu, wahusika wanateketeza maboksi na makuti ya mnazi chini ya ulinzi mkali, hatimaye mzigo unaingia sokoni, ndivyo tunavyofanya", Stephen Bad alieleza.

"Ushauri mzuri, Carlos aelezwe kuhusu jambo hili, japokuwa siamini kama anaweza kukubaliana nasi", Emilio alidokeza.

"Hili ni agizo, asikubali yeye nani? Nakuhakikishia Emilio, kama tuna nia njema ya kuupata mzigo huo, hatuna budi kuwatosa Hawa na Tony, waliokamatwa, lakini ukijaribu mbinu nyingine tumeumia", Stephan Bad alisisitiza.

"Hofu yangu ni kwamba tunaweza kukosa mama na mwana", Emilio alidokeza.
 
Back
Top Bottom