SHETANI RUDISHA AKILI ZETU
MTUNZI:SINGANOJR.
SEHEMU YA 19.
Kitendo cha Linda kumwelezea namna utaratibu wa CEO unavyokuwa kila akifika kazini , hatimae lift iliweza kufnguka katika floor ya saba na ndio sehemu ambapo idara ya uwekezaji inapatikana na meneja wa idara hio alikuwa tayari ameshaandaa nyaraka nje ya lift na kumpatia Regina.
“Mkurugenzi malighafi mpya ambazo zinatengenezwa na Taita Chemical, zinaenda kubadilisha kabisa teknolojia ya utengenezaji wa raba na kuzima teknolojia ya zamani katika maeneo mengi , hii itapelekea kupunguza gharama za udhalishaji wa bidhaa zote zinazotumia raba kwa zaidi ya asilimia arobaini na tano, tulikubaliana katika kikao kuongeza hisa zetu ndani ya kampuni ya Taita kwa asilimia 4.3%”Meneja wa idara ya uwekezaji alisoma ripoti kwa haraka.
Regina alipitia nyaraka ambayo alikuwa amekabidhiwa haraka haraka na baada ya pale aliitupia kwenye lift na ukauzu ukamvaa.
“Uza hisa zote tunazomiliki ndanni ya kampuni ya Taita”Aliongea na kauli ile ilimfanya meneja kushangaa , kana kwamba amesikia vibaya.
“Mkurugenzi kwanini kuuza katika wakati muhimu kama huu?”
“Bidhaa zao zinaenda kupoteza thamani muda si mrefu na kudorora sokoni hivyo hisa zao kushuka”Aliongea na kauli ile ilimchanganya meneja.
“Umeshindwa kuona mabadiliko ya wafanyakazi ndani ya kampuni ya Taita , unadhani ni kwanini idara ya usafirishaji imeongeza wafanyakazi katika maghala yao?”
“Kwasababu uwezo wao wa kudhalisha umefika mwisho , hivyo presha ya bidhaa kuwa kubwa kuliko uwezo wao.., kwanini sikulifikiria hili”Aliongea yule Meneja huku akijiona mzembe .
Meneja yule kabla hata hajaanza kutaka kumsifia Regina kwa uwezo wake wa kuona mbali Linda alikuwa ashabonyeza kitufe tayari na lift ilijifunga.
Ilienda kufunguka tena katika floor nyingine na Regina hakutoa kwenye lift lakini mbele yake kulikuwa na mwanamama wa makamo na alimkabidhi Linda nyaraka ambazo alimpatia Regina.
“Mkurugenzi!, Farida Group hawapo tayari kuhamisha umiliki wa ardhi kwetu, wanasema wanataka ongezeko la milioni mia mbili , tuchukue hatua gani?”
Regina palepale alichukua karamu ya rangi nyekundu na aliandika maandishi makubwa kwa lugha ya kingereza
“Waambie tutawaongezea mpaka milioni mia tano’
Mwanamama yule mara baada ya kuona maandishi yale alishangaa na aliona pengine Boss wake amekosea.
“Mkurugenzi wanataka ongezeko la thamani la milioni mia mbili tu”
“Fanya kama nilivyokuambia , kisha subiri mpaka wafanye maamuzi na kuja kwangu kwa ajili ya kusaini”
Mwanamama yule aliishia kutoa mdomo tu lakini aliishia kutingisha kichwa asijue bosi wake anachopanga ni nini.
Lift ilijifunga tena na Hamza ambae alikuwa amesimama nyuma ya Regina alikuwa kwenye dumbuwazi na alishikwa na shauku ya kutaka kujua kauli ile ilimaanisha nini.
“Mkurugenzi au nimesikia vibaya , kama wanahitaji ongezeko la thamani ya milioni mia mbili kwanini uwaongezee mpaka milioni mia tano , inamaana unatoa milioni miatatu ya bure?”
Regina hakujibu swali lile kwani Lift ilikuwa ishafunguka tayari na kwa mara nyingine kulikuwa tayari na mtu aliekuwa akisubiri na alikabidhi nyaraka ambazo zilisainiwa na Regina.
Floor kwa floor mwanamke huyo alipita na kila floor alikuwa akifanya maamuzi na kuweka sahihi baadhi ya mambo kwa umakini mkubwa na mengi ya maamuzi yalikuwa kinyume na meneja wa idara husika lakini licha ya hivyo hakuna ambae alipinga maamuzi yake , ilikuwa ni kama vile walijua maamuzi yake yapo sahihi zaidi kuliko ya kwao waliokubaliana.
Kilichomshangaza zaidi Hamza ni namna walivyofika katika floor ya juu zaidi baada ya kukutana na mama mtu mzima alieonekana kuwa na uzoefu wa muda mrefu lakini alitii kauli ya Regina bila ya kuuliza kabisa.
Baada ya kumaliza floor zote za jengo hilo , hatimae walifika floor ya juu kabisa ambapo ndio ofisi ya mrembo huyo hupatikana , ilikuwa ni ofisi kubwa mno yenye vioo vikubwa ambavyo havipitishi risasi
Kupitia madirisha hayo ya vioo alikuwa na uwezo wa kuona hadi maeneo ambayo yapo nje ya jiji la Dar es salaam.
Hakukuwa na mapambo mengi ukiachana na vyungu vya maua na shelf kadhaa za mafaili , yaani ilikuwa ofisi kubwa lakini vitu vichache na rangi yake iliendana na wajihi wa Regina kabisa.
Regina alikaa katika kiti chake cha kibosi huku kulia akiwepo Hamza na kushoto akiwepo Linda ambae alimkabidhi Regina nyaraka nyingine kuzipitia.
Regina alitumia muda mrefu kidogo kupitia zile nyaraka na Hamza alionyesha kuchoka hivyo alijikalia zake kwenye sofa huku akicheza game la pooltable kwenye simu yake lakini muda uleule Regina aliinua macho yake na kumwangalia.
“Linda mpatie nyaraka za Farida Group”Aliongea Regina na Linda alifungua faili kupitia kishikwambi na kumpatia Hamza ambae alianza kusoma mara moja
“Hii inahusu nini?”
“Si uliuliza swali kwanini nimeongeza pesa zaidi licha ya ongezeko la thamani waliloomba katika kipande cha ardhi nilichotaka kununua?”Aliuliza Regina na Hamza alitingisha kichwa.
“Sasa nakupa nusu saa unitafutie sababu kwanini nimefanya maamuzi hayo kupitia hizo taarifa za kiuchunguzi za kampuni ya Farida Group , ukifanikiwa utapatiwa ofisi ya kwako peke yako”
“Ofisi ya kwangu , unamaanisha itakuwa na tarakishi kabisa?”Hamza alikuwa na mpango wake , alijua ofisi kubwa kama hizo zina mtandao wa internet wenye spidi hivyo atatumia muda huo kutengeneza pesa online.
“Ndio, kila kitendea kazi”Aliongea na Hamza aliona vizuri na kwa haraka sana alianza kusoma taarifa hio.
Regina hakumjali tena , alichokifanya ni kwa ajili ya kumzuia Hamza kuwa bize kwa muda , akijua fika hawezi kupata sababu ndani ya muda wa dakika ishirini ,hata Linda mwenyewe alijua kabisa Hamza hawezi kutoboa na kujua sababu , lakini baada ya dakika tano Hamza alipumua kwa nguvu huku akijinyoosha.
“Nini tatizo?”Aliuliza Regina.
“Acha kumsumbua Mkurugenzi na sauti zako za ajabu”Aliongea Linda kwa kuonya
“Sio kama namsumbua , nishaona sababu tayari”
“Mh , nakupa nafasi nyingine tafuta kwa umakini”Aliongea Regina , hata Linda mwenyewe alijua haiwezekani kwa muda mchache hivyo , ukweli ni kwamba alijua Hamza hata hakumaliza kabisa kusoma taarifa yote maana ilikuwa na kurasa za kutosha.
“Farida ni kampuni ambayo ineonekana imara kwa nje lakini kwa ndani wapo katika hatari ya mlolongo wao wa kimapato . kama hii ardhi hawatoiuza mapema ili kupata pesa , kuna uwezekano wakafirisika”Aliongea Hamza na kauli ile ilimfanya Regina kumkazia Hamza macho
Katika akili yake alikuwa akishangaa na kujiambia yaani ndani ya dakika tano tu alikuwa ashaona taarifa iliojificha ya namna hio katika nyaraka hio , spidi yake ya kusoma aliona ni ya kutisha mno.
Linda hata yeye alikuwa kwenye mshangao , hakuamini kama Hamza aliweza kumaliza kusoma tayari hio nyaraka ndani ya dakika chache.
“Murugenzi niseme tu mbinu yako ni kuntu sana , kama ungeongeza milioni mia mbili kama walivyohitaji wangekuuzia haraka , lakini kitendo cha kuongeza milioni mia tano zaidi watapatwa na mashaka na kujiuliza kwanini unataka kununua ardhi yote kwa gharama kubwa kiasi hicho , watajiuliza au kuna kitu ambacho hawakuzingatia kuhusu hio ardhi ambacho kinaweza kukupa faida kubwa , kwa mbinu hio watasita kwanza kuuza ili wajue sababu ya wewe kutaka kununua kwa gharama kubwa , lakini wakati huo hakuna kampuni ambayo itakuwa tayari kununua ardhi kwa bei kichaa kama hio , hivyo wasiwasi wao utawafanya kupitisha siku muhimu ya kuuza na siku watakayo ona wakuuzie kwa ongezeko la milioni mia tano , unachofanya ni kuwakataa tu kiana na hawatakuwa na jinsi tena , mwishowe watakuuzia kwa thamani ya mwanzo kabisa, hawatokuwa hata na ubavu wa kuomba kuongezewa milionni mia mbili nyingine kwasababu hawana muda wa kutafuta mnunuzi mwingine”
Baada ya Hamza kumaliza kuongea Regina macho yake yalionyesha ishara ya kuridhika na jibu lake , aliona hakuwa amekosea tokea mwanzo , ijapokuwa Hamza anaonekana kama mwanaume muhuni muhuni mwenye tamaa na mbahili lakini akili yake ilikuwa ikifanya kazi vizuri , anao uwezo wa kujifunza na kuelewa kitu kwa haraka na kwa tabia hio ana uwezo wa kufanya jambo kubwa baadae. Hayo ndio yalikuwa mawazo ya Regina kwenda kwa Hamza.
Linda ambae alikuwa pembeni ya Regina alijikuta akishagnaa pia , aliona alikuwa amemchukulia poa huyo msaidizi mpya wa bosi wake lakini aliona yeye ndio alikuwa na makosa , inakuwaje bosi wake mwenye akili kubwa kutafuta mtu ambae hana uwezo , hivyo hakumpa sifa Hamza kwa kuwa na akili bali sifa alizielekeza kwa bosi wake kwa kuwa na jicho la ziada katika kujua uwezo wa mtu.
“Murugenzi, kama hii mbinu ikifanikiwa , nakuambia watu wa kampuni ya Farida watakuchukia kufa , watapata athari kubwa za mzunguko wa pesa ndani ya kampuni yao”Aliongea Hamza.
“Ukiwa mfanyabiashara , soko unalichukulia kama uwanja wa vita , kwasababu wao wenyewe ndio wameonyesha tamaa na kwenda kinyume na bei ya mwanzo , sidhani wanahaki ya kunilaumu kwa kutokuwa na huruma, pili kama wana akili ni kheri wakanifuata na kuniuzia ikiwa mapema , wakichelewa watakuwa wanajiingiza wenyewe katika mtego wangu kwa tamaa zao”
“Bosi , una akili sana , mtu wa kawaida hawezi kufikiria kwa namna yako”Hamza alimsifia.
“Hata wewe upo vizuri , sio mbaya umeweza kujua sababu ndani ya dakika tano tu”
Hamza mara baada ya kusifiwa kwa mara ya kwanza aliachia cheko lakini ambalo lilikuwa la kistaarabu kidogo
“Hamna , unajua nini bosi , mimi ni wa kawaida sana, akili yangu ipo ndani ya wastani wa kila mtu”
“Don’t be too arrogant , our CEO is a member of Pars Society , don’t think that just because you’re a little smart, you’re that great”Aliongea Linda kwa kujiamini kwa kingereza akimaanisha kwamba aache majigambo kwani bosi wake ni mwanachama wa Pars , hivyo kwa viakili vyake vidogo asijione mkubwa na kuanza kupandisha mabega.
Upande wa Hamza alishangaa mara baada ya kusikia Regina ni mwanachama wa Pars.
“Kwahio Boss wetu ni moja ya wanachama wa jamii za watu wenye IQ kubwa?”
“Unaonekana kujua mengi kama umeelewa sentensi yangu , ndio bosi wetu ana IQ 180 hivyo huhesabika kama Genius , kama sio hivyo unadhani kwanini kila mtu ndani ya kampni anaamini maamuzi yake na kuyafauta?”
The Standard wisdom societies ni umoja ambao wanachama wake wana IQ kubwa, inasemekana ili kujiunga katika umoja huo mtu anapaswa kufikia angalau vipimo vya IQ kuanzia 175 na kuendelea , sio umoja ambao unaweza kujiunga kwa pesa na hadhi.
Kwa kadri ambavyo alikuwa akielewa watu ambao huhesabika kama Genius ambao IQ zao ni kuanzia 180 wana uwezo wa juu sana katika maswala ya kitafiti , ubunifu na biashara , lakini wakati huo huo wakiwa vibaya sana katika baadhi ya sehemu kiasi kwamba wanaonekana kama watu dhaifu.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba majiniasi wanaweza kuwa juu ki uwezo aidha iwe katika maswala ya kitafiti au biashara lakini likija sehemu nyingine wanafanya vibaya sana , na hili linaweza kukushangaza, ki ufupi ni kwamba wanaonekana sio wa kawaida na maamuzi yao yanaweza kuwa ajabu mno.
Hamza aliweza kuliona hilo , hasa ukizingatia na tabia ya Regina mbele ya familia yake, alikuwa na mahusiano mabaya sana na baba yake.
“Huruhusiwi kuongea kuhusu jamii hio tena siku nyingine”Aliongea Regina na kumfanya Linda kufubaa kwa kuona alifanya kosa, lakini aliitikia kwa adabu.
Hio ndio moja ya sifa nyingine ya Regina , wafanyakazi wa kampuni hio walikuwa wakijua taarifa hio nyeti juu ya kuwa mmoja ya mwanachama wa jamii ya watu wenye busara na hawakuwa wakizungumzia hilo hadharani.
Sasa hata wakurugenzi wa bodi walielewa kwanini Mkurugenzi wa Zamani yaani babu yake Regina aliweka ngumu kumfanya msichana mdogo aliekulia katika kituo cha kulelea Yatima kuwa kichwa cha kampuni , kwa taarifa walizokuwa nazo alionyesha kuwa na akili isiokuwa ya kawaida tokea akiwa mdogo, kitu pekee ambacho wakurugenzi wa bodi hawakuwa wakifahamu ni ukichaa wa Regina, kutokana na Regina kuwa na akili nyingi ndio moja ya sababu ambayo ilimpelekea kuwa na ugonjwa wa nafsi mbili.
“Mnaweza kuondoka sasa, Linda muonyeshe Hamza ofisi yake”Aliongea Regina.
Hamza alikuwa na hamu ya kuona ofisi yake hivyo hakuwa na pingamizi na mkufuata Linda kwa haraka.
“Linda ,vipi kama nisingeweza kujibu , ni ofisi gani ningepelekwa?”Aliuliza Hamza mara baada ya kufikishwa katika ofisi ndani ya floor hio hio ambayo ilikuwa haina vitu vingi zaidi ya tarakishi ya thamni ya kampuni ya Apple na printer
“Haijalishi ungejibu kwa kukosea au kupatia , hii ofisi ndio niliandaa tokea juzi kwa maelekezo ya boss”
Hamza aliona kabisa Regina alikuwa akimchora tu , aliona kabisa Regia anatumia akili yake vibaya kumchezea akili.
Hamza mara baada ya kuchunguza tarakishi hio alitoa tabasamu , ilikuwa na sifa zote za kuitwa tarakishi yenye uwezo wa juu na kwa kuliona hilo alijua kabisa mpango wake wa kuvuna Bitcoin ungeenda vizuri sana. Mara baada ya kujinyoosha kwa kuanza kazi yake ya kutengeneza pesa, Linda aliingia akiwa na rundo la nyaraka na kuzitua mezani.
“Boss amesema unajua kuongea kifaransa kwa ufasaha , anataka utafsiri nyaraka zote kuwa katika lugha ya kingereza , ndio kazi yako utakayofanya kwanzia leo mpaka Ijumaa, ukimaliza print na niletee ofisini kwangu mlango unaofuatia”Aliongea katika sauti ya kiheshima.
Hamza alipitia nyaraka hizo kwa haraka haraka na aligundua ni taarifa za moja ya kampuni ya kifaransa na ilionekana ni nyaraka ambazo hazikupatikana kirahisi ndio maana hawakutaka mtu wa nje ya kampuni kuzitafsiri kutokana na unyeti wake.
“Huyu mwanamke , inaonekana alikuwa amepanga kunipa kazi tokea muda mrefu na sio kwasababu ya kumdanganya Eliza”Aliwaza Hamza mara baada ya kuona kazi ya kwanza ni kutafsiri kifaransa.
“Naona sasa nina kazi ya kufanya”
“Hakikisha unafanya kazi na huleti uzembe , kampuni yetu inajali sana watu wachapakazi na sio watu wazembewazembe kazini”
“Sawa”
Alijibu Hamza lakini mara baada ya Linda kutoka Hamza alikimbilia mlango na kuufunga kwa ndani na kisha alirudi kwenye tarakishi yake na kuanza kazi ya kutengeneza mzingira ya kuvuna sarafu.
“Kama nilivyotarajia spidi ya hii internet ni kiboko”Alijiongelesha Hamza , lakini alishituliwa na simu yake ilioanza kuita , aliitoa mfukoni na mara baada ya kuangalia jina la anaepiga ni mama Iryn.
Hamza alishasahau kama alikuwa na mwanafunzi na ni kama simu hio ilimkumbusha alikuwa na miadi ya kumfundisha Iryn wiki hio.
“Habari za uzima mwanangu?”Sauti iliita , Mama Iryn alikuwa akipendelea kumuita Hamza mwanae.
“Salama kabisa mama , habari za nyumbani?”Hamza aliongea alikuwa na upole kabisa.
“Salama kabisa , wiki hii mwanafunzi wako alikungojea hujatokea , kanikumbusha nikupigie simu”Hamza mara baada ya kusikia kauli ile alishindwa kujua afanyaje , kama ingekuwa siku kadhaa nyuma asingekuwa na shida ya kujibu lakini muda huo ni mwajiriwa wa milioni kadhaa hakuona haja ya kwenda kufundisha.
“Naomba unisamehe sana mama , ila nipo field kwasasa , muda wa masomo unanibana sana , semister yetu hii ya mwisho mwisho”Hamza alijitetea , ndio namna pekee alivyoona ajibu.
“Oh! , ndio nilichomwambia Iryn lakini hanielewi , mimi naelewa upo mwaka wa mwisho na unahitaji muda mwingi kujiandaa”
“Ni kweli kabisa mama , nahitaji muda wa kujiandaa”Aliongea Hamza , ukweli ni kwamba hajawahi hata kufanya discussion na wenzake , maisha yake ya chuo yeye ni kama vile anafanya utani , lakini likija test hajawahi kufeli.
“Basi hakuna shida baba yangu , nikutakie masomo mema na kujiandaa kwema”
“Asante mama nikutakie na wewe afya njema na masomo mema kwa Iryn”
Baada ya kuongea hivyo mama Iryn aliaga na kukata simu na kumfanya Hamza avute pumzi na kujiambia ni bora kukiepuka kikombe hicho,alijua kwenda kwa Iryn kwa vyvoyte vile ni kujiingiza kwenye majaribu ya mwanafunzi huyo wa Advance.
Hamza hakutaka kuwaza sana na alirudi kwenye kazi aliokuwa akitaka kuendelea nayo.
Baada ya kupoteza lisaa lizima kwenye mtandao wa Blockchain alirudi katika kazi ya kutafsiri , Hamza aliangalia nyaraka alizokuwa amepewa na aliona haikuwa kifaransa kigumu, ni kile cha kibiashara hivyo alikaa vizuri kwenye tarakishi na kuanza kuchapa kwa spidi kubwa , alikuwa na spidi sio ya kawaida na ndani ya masaa matatu bila ya kupumzika alikuwa amemaliza kila kitu na alipoangalia saa ilikuwa ni saa saba kasoro mchana, hivyo alimalizia kuprint kabisa.
Baada ya kumaliza alisimama na kuanza kujivuta vuta lakini ni dakika hio hio sauti kutoka nje pamoja na kugongwa kwa mlango ilisikika , alikuwa ni Linda aliekuwa akimtaka kufungua.
“Kwanini umejifungia?”
“Ofisi ni yangu ni maamuzi yangu kufunga na kufungua”Aliongea na kumfanya Linda amwangalie kwa kejeli huku akimpita na kusogelea tarakishi.
“Ulichokuwa ukifanya umeficha wapi?”Aliuliza
“Nliichokuwa nikifanya, unamaanisha nini?”
“Ulikuwa ukicheza michezo yako ya Blockchain”
“Umejuaje nilikuwa nikifanya hivyo?”
“Unadhani idara ya IT inafanya kazi gani ,spidi ya Internet ilipungua kwa kiasi kikubwa na kufanya uanze kufuatiliwa unachofanya”
Hamza mara baada ya kusikia hivyo alijikuta akianza kujikuna kichwa na kuona ni ukatili kwa kampuni kufatilia kile wanachokifanya wafanyakazi ndani ya ofisi zao.
“Nimepewa maagizo nikakuripoti kwa Mkurugenzi na kulingana na sheria mshahara wako unakatwa asilimia ishirini”Mara baada ya kuongea kauli hio Linda aligeuza kutaka kuondoka.
“Hebu subiri kwanza , kazi ulionipatia nishaimaliza , kwanini mnikate mshahara , sikuwa na chakufanya ndio maana nikaingia kwenye vitu vingine”
“Unaongea nini wewe , yaani umemaliza kazi ya siku tatu ndani ya masaa machache?”
“Ndio , kama huamini angalia , sikupata muda tu wa kukukabidhi kazi”Aliongea Hamza huku akimpatia Linda katarasi ambazo ashamaliza kuziprint.
Linda alijikuta akishangaa mara baada ya kukagua karatasi hizo , zilikuwa zimeandikwa kwa usanifu mzuri sana tena kwa kingereza rasmi cha kikazi kabisa, lakini hata hivyo hakutaka kumuamini , aliingia kwenye mtandao na kujaribu kukopi na kupaste baadhi ya maneno ya kifaransa katika programu ya kutafsiria ili kuhakiki na kweli ilikuwa sahihi kabisa na aliishia kumwangalia Hamza kwa maswali mengi.
“Umewezaje kukamilisha kazi hii kwa muda mfupi tu?”Aliuliza na Hamza alitingisha mabega.
“Halafu kuna baadhi ya maneno yalikosewa kuandikwa , nimeyawekea alama na kisha nikayabadilisha wakati wa kutafsiri unaweza hakiki pia”Aliongea Hamza huku akimkabidhi Linda zile karatasi nyingine.
Linda aliishia kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa na kisha akageuka.
“Ni muda wa lunch unaweza kwenda kula , nitampatia hizi nyaraka mkurugenzi”
“Subiri kwanza ,vipi kuhusu mshahara wangu sasa?”
“Kwa leo nitaacha hili lipite , ukirudia tena kufanya mambo nje ya utaratibu wa kazi kwa tarakishi za kampuni sitolifumbia macho”Aliongea na kisha alifungua mlango kutoka nje.
“Vipi wewe huendi kula , Mkurugenzi yeye anakula wapi?”
“Nipo kwenye diet , kuhusu mkurugenzi hali chakula mchana , hivyo jali mambo yako”Aliongea na hakutaka tena kuendelea kuongea na Hamza hivyo aliondoka.
Hamza licha ya kwamba alikuwa feki mbele ya Regina lakini kusikia kwamba hakuwa akila chakula cha mchana aliona mwanamke huyo anatia huruma na pengine jambo hilo hata Shangazi hakuwa akilijua la sivyo angekuwa mkali, lakini kwasababu hakuwa na chakufanya aliamua kupotezea na kutoka ndani ya ofisi yake na kwenda chini kabisa mgahawani .
Kampuni kubwa kama hio hakukuwa na haja ya kuongelea maswala ya maisha mazuri ya wafanyakazi wakiwa kazini , mgahawa wa kampuni ulikuwa mzuri mno na kulikuwa na kila aina ya chakula kizuri
Kila mtu alikuwa bize na chakula , wafanyakazi walikuwa wengi na baadhi yao walikuwa makundi makundi , kwasababu Hamza alikuwa mgeni yeye alienda zake kuchukua chakula na kisha kutafuta pakukaa.
Kampuni hio ni kama ilikuwa na upendeleo na wanawake kwani walikuwa wengi mno kuliko wanaume , Hamza licha ya kwamba alikuwa mgeni hakutaka kujitenga hivyo aliona sehemu sahihi ni mahali ambapo kuna watu ili kujenga kidogo mazoea.
Lakini kabla hata hajapata sehemu , aliitwa na kumfanya ageuke na hapo ndio aliweza kumuona Asha pamoja na msichana mwingine aliemfahamu kwa jina la Mirium , walikuwa ni wasichana ambao aliwakuta pamoja na Eliza wakiwa mwembeni Bar.
“Hello, nakuona Asha ulivyopendeza”Aliongea Hamza.
“Kwahio umemuona Asha tu , mimi hujaniona?”Aliongea Mirium huku akijifanyisha mwanamke mwenye wivu.
“Ndio”Alijibu Hamza akiwa siriasi na kufanya warembo wale kumshangaa kidogo na kisha waliangua kicheko.
“Eliza hajarudi kutoka safarini bado , lakini alituambia umepata kazi hapa makao makuu kama msaidizi namba mbili wa bosi , Hamza usitusahau kwenye ufalme wako”Aliongea Asha kwa tabasamu.
“Ah! , msinitegemee sana , mwenyewe sijui ni kwa muda gani nitafanya kazi , pengine ninaweza kufukuzwa ndani ya miezi mitatu tu”
“Sio kirahisi hivyo , kama umemfanya bosi kukupa kazi muhimu kama hio basi ni wazi upo vizuri upstairs “
“Hebu acheni soga bwana , tutafuteni pakukaa kwanza muda unaenda”Aliingilia Mirium ambae alionekana kuchoka kusimama na kuachwa kwenye mazungumzo.
Baada ya kusogea upande wa kushoto mwa mgahawa huo Hamza aliweza kuona nafasi za wazi na kulikuwa na mwanamke mmoja tu aliekuwa akila peke yake na alimfahamu , alikuwa ni Kapteni Yonesi mkuu wa idara ya usalama wa kampuni.
“Twendeni pale”Aliongea Hamza, alitokea kumkubali Yonesi , ijapokuwa alikuwa na tofauti sana na wanawake wengi waliokuwa hapo ndani lakini ukauzu wake ulimfanya kuvutia , isitoshe alikuwa mrembo
“Unamaanisha tutakae na Kapteni Yonesi, Akha hatuendi pale sie”Aliongea Asha.
“Kwanini sasa , yule si mtu kwanini kama mnamnyapaa?”
“Ana sheria ngumu sana ukikaa nae kwenye meza , hataki muongee ongee wakati wa kula, hasa umbea umbea , yaani ukikaa nae Mjeda yule hakuna amani na chakula ni kama unakula sumu”Aliongea Mirium.
“Halafu ukimchokoza kidogo tu atakasirika , lazima akushikishe adabu , ni mkali mno mbele ya wafanyakazi , na hakuna wa kumfanya lolote maana anaaminiwa sana na Mkurugenzi”
“Hamza usije kujaribu bahati yako pale , kuna wenzako waliowahi kufika hapa na wakajifanya wana swaga na kuanza kutupia maneno pale , kilichowakuta ni udhalilishaji”Asha naMirium walikuwa wakipokezana kumjadili Yonesi na washasahau walikuwa wameshikilia vyakula mkononi.
“Kama nyie hamtaki kukaa pale , tafuteni eneo lingine mimi nitakaa”Aliongea Hamza na hakusubiri hata majibu yao na alitembea mpaka katika meza aliokaa Kapteni Yonesi.
Wafanyakazi waliokuwa ndani ya mgahawa huo waliona kitendo kile na kwasababu walishamjua Hamza ni mgeni , walitaka kuona kile kitakachotokea.
Yonesi alikuwa zake bize na chakula na mara baada ya kuhisi mtu kuongezeka katika meza yake ndio aliinua uso wake na alishangaa kumuona ni Hamza.
“Ni wewe?”
“Niambie Kapteni naona tunakutana tena”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu na kukaa mkao wa kula.
“Kakae kwenye meza nyingine”Aliongea Yonesi , kibabe.
SEHEMU YA 20.
Yonesi kama bodigadi alikuwa na taarifa zote za Regina kuajili msaidizi wake mwingine na mara baada ya kufahamu ni Hamza aliishia kushangaa na kujiuliza nini kinachoendelea , hakuwa na taarifa zote, alihisi kuna kitu kinaendelea kati yao lakini aliona ni kheri ajirushe baharini aliwe na mamba kuliko kuamini Regina anaweza kutoka kimapenzi na mwanaume kama Hamza.
Kingine ambacho kilimfanya Yonesi kumdharau Hamza ni tabia yake ya kukosa aibu na uwoga woga usio na maana , yeye alipenda wanaume ngangari lakini kitendo cha siku ile kumuachia msaala kule gongo la mboto alimuondolea nyota ya heshima kama mwanaume.
“Kapteni, unapaswa kuwa na sababu ya msingi kunifukuza kwenye hii meza, hakuna sheria inayonizuia kukaa kwenye hii meza si ndio?”
“Nenda kakae meza inayofuatia haina mtu , kwani lazima ukae hapa”
“Siendi popote”Aliongea Hamza.
“Kwanini?”Aliuliza huku akiwa amekunja ndita.
“Kwasababu nataka kuona namna mwanamke mrembo kama wewe unavyokula”
Yonesi alikuwa ni mweupe kabisa , kauli ile japo haijamshangaza sana lakini kulikuwa na viashiria vyote, sura yake ilianza kubadilika rangi na kuwa nyekundu.
Ni kweli anatongozwa sana , lakini haijawahi kutokea mwanaume kuongea kuhusu muonekano wake bila wasiwasi kama Hamza, lakini ilikuwa ni dakika ile aling’ata meno yake kwa hasira
“Wewe mpuuzi , rudia kauli yako tena uone”
“Kapteni nimesema wewe ndio mrembo kuliko wote hapa , lakini ajabu umekaa mwenyewe”
“Ukiendelea kuongea ujinga wako , nitakushushia kipigo hapa hapa bila kujali watu”
“Ah!, basi yaishe Kapteni , nimeacha usije kunipig”Aliongea Hamza akijifanyisha kuwa mzembe huku akinywa juisi yake kwenye glasi.
Yonesi alikosa hata nguvu ya kumfukuza Hamza tena na aliamua kujiweka bize na chakula chake , lakini kadri alivyokuwa akila ndio alivyokosa ule uhuru aliokuwa nao na aliinua macho yae na kumwangalia Hamza , lakini ndio anaona Hamza alikuwa akimkodolea macho eneo la kifuani.
Hamza alikuwa akifurahia chakua chake , kilichomfanya kumkodolea Yonesi macho ni aneo la kifuani tu , alikuwa akiona namna manyonyo yake yalivyokuwa yakivutia.
“Mh , juzi nadhani sijamwangalia vizuri , anaita sio poa”Aliwaza Hamza ndani kwa ndani
“Unaangalia nini?”Aliuliza Yonesi kibabe.
“Unataka kujua kweli wa ninachoangalia?”
“Jibu swali?”
“Naangalia hayo mayai kwenye sahani yako”
“Kuna mayai gani kwenye sahani yangu!!?”Yonesi aliongea kwa hasira mno huku akipiga kofi meza na kufanya watu kugeuka na kuangalia kinachoendelea, lakini Hamza alijifanyisha kuwa bize kula chakula chake.
“Kapteni ni kweli nimekuona na mayai kabisa , tena mawili ..”Hamza aliendelea kumchokoza Yonesi.
“Mbwa wewe ,nani ana mayai , sema ulichokuwa ukiangalia lasivyo nitakufanya kipofu”Aliongea huku akimnyooshea Hamza na uma.
“Kama unabisha , wewe unadhani nilikuwa nikiangalia nini?”
“Kwahio unabishana na mimi , unadhani maneno yangu ni ya bure siwezi kukufanya chochote”
Yonesi kwenye maisha yake hakutaka kuonewa kizembe na kwasababu hasira zishamvaa aliona amshikishe adabu Hamza hapo hapo , hivyo alichukua uma na kumlenga nayo uelekeo wa macho.
Watu waligeuka mara baada ya kuona tukio hilo wakitaka kujua mwisho wake
Lakini Hamza hakukwepa wala kufanya chochote , alikuwa akiendelea kutafuna huku Uma ile ikimkaribia machonni .
Yonesi asingeweza kumchoma nayo kweli machoni na baada ya kufika nchi kadhaa karibu na jicho la Hamza aliishia njiani , upande wa Hamza hakupepesa macho hata kidogo.
Kitendo kile kiliwashangaza watu , maana mtu yoyote angeogopa kwa kulengwa na ncha machoni , lakini Hamza hakuonyesha hofu.
“Kapteni unajua kila mtu anatuangalia , huoni sio vizuri kunichokoza mchana yote hii”Aliongea Hamza akitabasamu , alijiambia Yonesi hata amshikilie bunduki hawezi kuogopa.
Yonesi aliishia kushusha uma chini huku akijiuliza imekuwaje huyo mpuuzi leo kujiaminni hivyo.
“Leo nitakusamehe , ukinichungulia siku nyingine hutoamini nitakachokufanyia” Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu tu.
“Kapteni , naomba kuuliza?”
“Nini?”
“Wewe ni D au F?”
“”…”
Yonesi alishindwa hata kuongea kutokana na namna alivyokuwa amekasirika kwa mara nyingine na Swali lile.
“Mpuuzi wewe , ulikuwa kweli ukinichungul..”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake alijizuia mara baada ya kuona ameongea kwa sauti kubwa na kufanya watu kumwangalia , uso wake ulikuwa umebadilika mno kutokana na hasira , hakuwahi kudhalilishwa kiasi hicho ndani ya kampuni.
“Hamza nifuate”Aliongea kwa kuamrisha , hakutaka kuleta fujo ndani ya mgahawa , aliona ni bora amtoe hapo akampe kibano pembeni.
“Sijamaliza kula”Hamza alikataa.
“Wew..”
Kitendo kile kilifanya Yonesi agundue watu walikuwa wakicheka kwa siri na aliishia kusugua meno yake kwa hasira na alifyatua mkono wake wa kulia kijeshi kwa ajili ya kumshika Hamza tai , lakini Hamza alirudi nyuma na kufanya mkono wake kupita.
Yonesi aliona Hamza aliotea hivyo alizunguka upande wa pili kwa ajili ya kumshika , Hamza hakuwa na haraka mara baada ya kuona Yonesi anamkaribia alipiga kiti teke ambacho kilienda kumvaa afande Yonesi na kumfanya akose mhilimili na kuelekea chini akitanguliza uso.
“Ahh..”
Yonesi alijua alikuwa akidondoka vibaya , kitendo cha Hamza kupiga kiti teke hakukiotea kabisa ,sekunde hio akiona anakwenda kudondoka vibaya Hamza alikuwa ashamzuia kwa mkono mmoja na kumshikilia kifuani sehemu ileile ambayo ilimfanya kukasirika kwa kuchunguliwa.
Yonesi ni kama alikuwa amepigwa na shoti , alijikuta akitetemeka mara baada ya kuona namna mkono wa Hamza ulivyoyashikilia manyonyo yake
“Wewe muhuni umenigusa..”
“Kapteni , unamaanisha nini kugusa wakati nakuzuia usidondoke”Aliongea Hamza na muda uleule Yonesi alisimama vizuri, mara baada ya kuona macho ya wafanyakazi yamezidi kuongezeka , alimwangalia Hamza kwa macho makali.
“Subiri uone , inaweza isiwe sasa hivi ila nitakufanya ujutie kwa ulichonifanyia leo”Aliongea Yonesi kwa hasira na kisha aligeuka zake na kuondoka huku kichwa kikiwa chini , kwa mara ya kwanza mbabe wake ndani ya kampuni alipatikana.
Kila mtu alimwangalia Hamza kwa mshangao na kumkubali , hio ilikuwa mara yao ya kwanza kuona Yonesi akitawaliwa na mwanaume na ashindwe kufanya chochote, wanaume wengi walionekana dhaifu mbele ya Yonesi.
Hamza wala hakujali vile vitisho na baada ya kumaliza kula alichukua matunda ya apple kwenye friji na kisha akaweka kwenye mfuko na kuondoka nayo , alijua Regina hajala hivyo alijihisi sio vizuri kutopeleka chochote hata kama ataonekana anajipendekeza.
Mara baada ya kutoka kwenye lift moja kwa moja alienda mpaka kwenye mlango wa mkurugenzi na kugonga.
“Come in”
Hamza alisukuma mlango na kisha akaingia , aliweza kumuona Regina akiwa bize amekodolea tarakishi yake huku akionekana kuandika vitu kwa karamu kwenye notebook.
Mbele yake kulikuwa na nyaraka nyingi ambazo ilionekana alikuwa akizifanyia kazi pia , ki ufupi alikuwa bize.
“Weka ripoti hio juu ya meza na unaweza kuondoka”Aliongea Regina bila ya kuangalia aliengia , alijua ni Linda sekretari wake.
Mara baada ya Hamza kuweka matunda yale juu ya meza ndio sasa Regina aliinua macho na kumwangalia.
“Kwanini ni wewe?”
“Sekretari wako kasema hupendelei kula chakula cha mchana na nimeona sio vizuri , kula hata matunda nimekuletea”
“Nishakula na haikuhusu kama nimekula au sijala”Aliongea bila ya ishara ya furaha yoyote.
“Kwahio umekula?”Aliongea Hamza huku akizungusha macho yake na ndio alipoweza kuona mfuko uliojaa makopo , yalikua kama kumi na mbili hivi.
“Gum- syrup!!”Hamza alionekana kushangaa ,
“Hiki kinywaji ndio unachotumia kama chakula cha mchana ?”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kumwangalia.
“Kumbe unajua hata jina lake kwa kingereza ni Gum syrup?, kweli wewe ni mwanachuo una exposure ya kujua vitu vingi”Aliongea Regina lakini Hamza hakujali.
“Hata kama unataka kuzuia njaa hutakiwi kutumia aina hii ya kinywaji cha virutubisho , unatakiwa kula chakula?”
“Chakula kinaathiri mzunguko wa damu na oxygen kwenye ubongo na muda wangu wa kufanya kazi ni muhimu sana, sitaki kusinzia, kitu kingine huna kigezo hata kimoja cha kunijali”Aliongea kikauzu.
“Kula angalau hata hayo matunda , kuliko kushinda na tumbo ambalo halina kitu”
Licha ya kwamba Hamza alikuwa akionyesha kumjali , lakini kwake alimuona kama mtu asiemfahamu tu.
“Ondoka nayo , sitokula”Aliongea lakini Hamza alitoa kicheko na kisha akashika simu yake.
“Ngoja nimpigie shangazi na kumwambia unashindia vinywaji vya virutubisho mchana na huna ratiba ya chakula cha mchana”
Regina mara baada ya kuona anachotaka kufanya Hamza alijua maana yake ni nini , kama kweli Shangazi angelifahamu hilo angekuwa na wasiwasi mno maana kwake ni kama mama.
“Weka simu chini , acha kupiga”
“Nitafanya hivyo kama utakula matunda yote nilioleta la sivyo hili swala nitalifikisha kama lilivyo kwa Shangazi”
“Mbona unapenda kunisumbua na mitunda yako mibaya mibaya”Aliongea huku akionyesha hasira za wazi.
“Nakusumbua sio,ngoja tuone kama nakusumbua , mimi nampigia”
“Wewe inakuhusu ni nini kwanza kula kwangu , unanijali kama nani?”
“Nimeshiba tayari ila kuona hujala chochote nimejikuta na shikwa na huzuni”
“”..”
Regina aliishia kuegamia kiti chake huku akimwangalia Hamza , ni kama hakuwa ametegemea angetoa jibu la aina hio.
“Huzuni utoe wapi , umekaa kiuongo uongo tu”
“Acha maswali mengi , unakula au huli”
“Nitakula , acha kuendelea kunichukiza”
“Hilo ndio jibu sasa , nitakaa hapa hapa mpaka nione umemaliza ndio naondoka”Aliongea lakini Hamza alimwangalia mara baada ya kuona Regina amekunja sura huku ameshikilia mkononi apple.
“Sipendi kula na maganda yake na mimi mvivu wa kumenya”
“Ukila na maganda yake ndio vizuri , yamebeba Asidi ya kutosha inayosaidia kuondoa uchomvu”
“Ndio hivyo sipendi sasa , unalazimisha”
“Uvivu tu ndio unasumbua “
Aliongea Hamza na kwasababu hakuwa na chaguo lingine ilibidi atafute kisu na kuanza kuyamenya moja moja na kuyaweka kwenye sahanni.
Spidi yake ya kumenya ilikuwa kubwa mno na ndani ya dakika chache tu alikuwa ashamaliza yote.
Regina alianza kuyatafuna haraka haraka , alitaka kumaliza ili aendeee na kazi yake.
“Halafu una malengo gani , kwanini unalazimisha nile haya matunda?”
“Sina malengo yoyote , ninachotaka ni ujaze hilo tumbo lako , kwanini una mawazo mabaya kila ninachofanya”
“Umekaa kimashaka mashaka ndio maana”Aliongea huku akiendelea kula kama abiria anaetaka kumaliza haraka apande basi.
Baada ya Regina kumaliza kula alionekana kukumbuka kitu na kumwangalia Hamza.
“Zile nyaraka ulizotafsiri nimeziona , umetafsiri vizuri sana kuliko hata Freelancer tuliemwajiri kututafsiria mara ya mwisho, nadhani uwezo wako wa kuongea kifaransa na kingereza ni C2?”
“C2 maana yake ndio nini?”
“Hujui?, Inamaana hujawahi kufanya DEF test?, C2 maana yake ni kiwango cha juu cha kuongea lugha ambayo sio uliozaliwa nayo”
“Sijajifunza kifaransa na kingereza kwa njia rasmi, wakati nilipokuwa nje ya nchi nilikuwa nikiongea na watu mara kwa mara ndio maana nilizidi kuzoea”
“Ushawahi kuwa nje ya nchi, masomoni au?”Aliuliza Regina kwa mshangao , alihisi ni vizuri kumjua Hamza angalau kidogo.
“Ndio nilipofikisha miaka kumi nilidhamia nje ya nchi, kutokana na maisha kuwa magumu nilijikuta nikifanya kila aina ya kazi, bahati nzuri kutokana na muonekano wangu wa kuchanganya rangi nikapata familia”
“Sasa ilikuwaje ukarudi?!!”
“Kuna mambo yalitokea ,nilishindwa kuendelea kuishi katika familia yangu mpya mara baada ya kugundulika kama mtanzania”Aliongea Hamza , Regina japo alikuwa na maswali mengi aliona aishie hapo kuuliza , alitamani kujua ilikuwaje mpaka akafika chuo.
Mara baada ya kumaliza kutafuta yale matunda alihisi ukakasi kwenye midomo na alihitaji maji ya moto kwa ajili ya kusukutua.
“Nitakusaidia kumimina maji?”Aliongea Hamza mara baada ya kumuona Regina akisogelea Dispenser ya maji ya moto.
“Nishafika tayari , haina haja”Aliongea na kumfanya Hamza arudi kukaa kwenye sofa.
Lakini sasa kitendo cha Regina kuinama ili achukue Glasi ilifanya gauni lake kupanda juu kutokana na kuwa na shepu kubwa , alikuwa amechukua tahadhari ya kugeukia upande wa nyuma lakini akasahau kuna kioo ambacho kina akisi mwanga.
Hamza alikaza macho , alikuwa na shauku ya kutaka kuona mwanamke kauzu kama Regina huko ndani atakuwa anavaaje.
Regina mara baada ya kugeuza uso wake na kumuona Hamza anapoangalia alishituka na kugeuka nyuma na hapo ndipo alipojua alikuwa akionekana kwenye kioo kwa nyuma.
“Wewe…!!!”
Regina alijikuta akisimama wima huku akijiweka vizuri na kisha akageuka huku akimkazia macho Hamza , wazo la kumuua Hamza lilimvaa palepale.
Hamza alikuwa ashageuza macho yake na alijifanyisha kushangaa kwa mabadiliko ya Regina.
“Mkurugenzi nini shida , kwanini unafoka?”
“Hujawahi kuona mwanamke , umekuwa chizi?”Aliongea akiwa amekasirika.
“Boss kama unataka kunifokea ni bora ukaniambia sababu , sijafanya kosa lolote”
“Sijawahi ona mwanaume mshenzi kama wewe ambae huna aibu na kuchungulia watu”
“Nini!, unamaanisha nini kukuchungulia , mimi muda wote nilikuwa nikifurahia mandhari mazuri ya jiji letu, Mkurugenzi utakuwa unanifikiria vibaya”
“Bado unabisha tu”Aliongea na wakati huo alimimina maji ya moto kwenye kikombe na kumsogelea Hamza.
“Boss unataka kufanya nini?”
“Kwanini?, unadhani nataka kukumwagia maji kama huna kosa?”
“Mkurugenzi , ni kweli umenifikiria vibaya . ila kama dhamira yako ni kunimwagia maji ya moto basi ni kheri nikimbie tu”Aliongea Hamza lakini muda ule mikono ya Regina ilicheza na kufanya maji ya moto kutoka katika kile kikombe na kuelekea katika miguu yake .
Lakini Hamza alikuwa na spidi kwani aliyakinga yale maji kwa kupitia viganja vyake ili yasimfikie na kitendo kile kilimshitua Regina na mara baada ya akili yake kufanya kazi aliwahi kuweka kile kikombe chini
“Hujaungua?”
“Mikono yangu inasugu na ngozi yake ni ngumu , maji kidogo hivi hayawezi niunguza”Aliongea na Regina mara baada ya kuangalia mikono ya Hamza haijaungua kidogo alijisikia amani.
“Sorry , sijamwaga makusudi”Aliongea Regina bila ya kumwangalia Hamza machoni, hakutegemea kama Hamza angechukua hatua ya kukinga maji na mikono yake yasimuunguze.
“Hakuna shida, ili mradi tu Mkurugenzi hutoendelea kunifikiria vibaya, nitaacha hili lipite”
Mara baada ya kuona namna Hamza alivyoongea kipole aliona pengine ni kweli alimfikiria vibaya na hakuwa akimchungulia.
“Ni kweli hujanichungulia?”Aliuliza kwa kusitasita.
“Kama huniamini basi siwezi kuendelea kujielezea , narudi ofisini kwangu”Mara baada ya kuongea hivyo Hamza alisimama na kupiga hatua kuondoka ndani ya ofisi hio akimuacha Regina kwenye mawazo.
“Mkurugenzi , kabla sijaondoka naomba nikuulize swali?”Aliongea Hamza mara baada ya kufika mlangoni.
“Uliza?”
“Huwa unapendelea rangi ya pink plain au pink yenye maua maua?”Aliuliza na kabla hata hajajibiwa alishatoka na kufnga mlango.
Upande wa ndani Regina alinyanyua kikombe kile cha glasi na kurusha mlangoni , lakini ashachelewa na kilichosikika ni sauti ya kuvunjika tu.
“Hamzaaa..!!!”
Regina alitoa ukulele wa hasira huku sura yake yote ikiwa nyekundu.
Aliona mpango wake wa mwanzo wa kumfundisha kazi kulingana na kozi yake anayosomea ulikua ni wa kijinga , dakika hio hio alishaona alikuwa amemsingizia kumbe yote hayo alikuwa akichezewa akili.
Upande mwingine mara baada ya Hamza kuingia tu katika ofisi yake simu yake ilianza kuita na alipoangalia jina la anaepiga alikuwa ni Amiri rafiki yake.
Alishangaa kidogo kwani tokea siku ambayo alimsaidia kutega kamera hawajaonana.
“Hello!!”
“Bro vipi?”Sauti ya Amiri ilisikika na ilikosa utulivu jambo ambalo Hamza alilijua haraka sana.
“Poa kabisa , mambo vipi?”
“Mambo sio shwari kaka?”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Hata sijui nikuelezee vipi , ila nimechanganyikiwa tokea jana”Aliongea na Hamza aliamini lazima ni swala linalohusiana na Mellisa.
“Ni swala la Mellisa nini?”
“Ndio kaka, sijui ni mauza uza gani yanaendelea kwa huyu mwanamke , ila naomba tuonane leo hii , ikiwezekana hata sasa hivi , pengine unaweza kuwa na majibu ya nilichokiona”
“Kwasasa kuna mishe imenishika hapa , unaonaje baadae saa kumi na moja”
“Sina jinsi kaka nitasubiri , wewe ndio mtu wangu wa karibu ninaeweza kukushirikisha hili , pengine unaweza kuwa na majibu , mimi nimekwama”
“Sawa nitakushitua”
Hamza baada ya simu ile alikaa kwenye kiti , alikuwa na shauku pia ya kujua ni kitu gani ambacho kimetokea , maana kwa alichokuwa akiongea Amiri alijua kuna jambo kubwa ameona kupitia zile Kamera za siri.
******
Upande mwingine Amosi alionekana akiegesha gari yake katika kituo cha kujazia mafuta cha Puma kandokando ya barabara ya Haile Selasie na mara baada ya kutoka katika gari hio nyeusi aina ya Mercedenz alipiga hatua na kuingia uelekeo wa hoteli ya Peninsula.
Alikuwa makini mno katika tembea yake , ni kama vile mtu ambae anaogopa kufatiliwa, wakati huo simu ilikuwa sikioni na mara baada ya kuignia ndani kabisa ya hoteli hio eneo la mapokezi aliongea maneno machache tu na kisha alisonga mbele na kuzisogelea ngazi.
Jengo la hoteli hio halikuwa refu sana na mara baada ya kufika floor ya tatu alisimama katika mlango wa chumba na akagonga mlango na hazikuchukua hata dakika chache mlango wa chumba ulifunguliwa na ksiha akaingia ndani.
Chumba hakikuwa cha ghali sana , kilikuwa cha kawaida tu kitanda kikubwa cha sita kwa sita pamoja na Tv.
Mtu aliemfungulia mlango alikuwa ni mwanaume wa makamo hivi mrefu mweusi ambae ana nywele ndefu na masharubu.
“Mzigo vipi?”Aliongea Amosi mara baada ya kusalimiana kwa kugongesheana tano.
“Huu hapa boss”Aliongea yule kijana na kuchukua bahasha iliokuwa juu ya kitanda na kumpatia.
Amosi alifungua bahasha ile kwa kuihakiki na kisha alitingisha kichwa kuonyesha kuridhika.
“Kuna maagizo mengine?”
“Hamna , nimepatiwa hizo tu”Aliongea yule bwana na kumfanya Amosi kukagua chumba hicho kwa dakika kadhaa na kisha alitingisha kichwa na kugeuka kuondoka.
“Simama hapo hapo?”Sauti kutoka nyuma ilisikika ikimwamrisha na kumfanya ageuke huku akiinua mikono yake juu mara baada ya kuona amenyooshewa Bastora, huku yule mtu akiwa hana utani hata kidogo kwenye macho yake.
Ni dakika ileile mlango wa bafuni ulifunguliwa na akatoka mwanamke ambae ni kama alikuwa akitoka kuoga kutokana na kwamba hakuwa na nguo zaidi ya Bathrobe ya rangi nyeupe, alikuwa mrembo haswa.
“Tresha!!”Aliongea Amosi kwa mshangao.
“Amosi!!”
ITAENDELEA
SEHEMU YA 21
Mwanamke ambae alikuwa amepambwa na tabasamu mbele ya Amosi alikuwa ni Tresha , pengine Hamza angekuwepo ndani ya hilo eneo angemfahamu mara moja , ndio mrembo ambae alimpagawisha katika Apartment za Dosam Homes , mwanamke ambae kwa maelezo ya Amiri uzuri wake ni wa kutengeneza na inasemekana ni mfanyakazi wa Binamu Island.
Amosi alimwangalia Tresha kwa dakika kadhaa na kisha akayainua macho yake na kumwangalia mwanaume aliemnyooshea Bastora.
Upande wa Tresha hakuonyesha ishara yoyote ya furaha , ilionekana alikuwa akifahamiana na Amosi lakini muda huo alikuwa siriasi.
“Tresha nini hiki, kwanini upo hapa na nini kinaendelea?”Aliuliza Amosi.
“Nikuulize wewe Amosi unafanya nini hapa?”Aliongea Tresha na alimsogelea Amosi na kisha alichukua ile bahasha.
Amosi alikuwa na wasiwasi mno na kwa haraka haraka alijua kabisa yupo ndani ya mtego.
“Tresha najua unachomaanisha , lakini swala hili linahusiana vipi na wewe?”.
“Swali hilo ulitakiwa kumuuliza aliekupa kazi , nilishakuonya siku nyingi ikitokea umeingilia njia zangu tutakuwa maadui wakubwa na leo tupo hapa”Aliongea na hapo sasa hisia mbaya zilianza kumvaa Amosi na kitu kilichomjia akilini kwake mara moja ni kujiokoa.
Alimjua mwanamke huyo fika , licha ya kuonekana mwanamke mrembo lakini ni kibaraka wa watu wa Binamu Island ambae hana huruma hata kidogo.
“Usije kufikiria kufanya chochote cha kijinga , sekunde ambayo utasogea hata nchi moja ndio utakuwa mwisho wa uhai wako Amosi”
“Unataka nini kutoka kwangu Tresha , kama Binamu wameagiza kifo changu haikuwa na haja ya kuniwekea mtego kama huu”
“Haha.. hubadiliki hata kidogo , siku zote akili yako inafanya kazi kwa haraka ukiwa katika hatari , ungekuwa sawasawa kiakili ungejiuliza maswali mengi kabla ya kuwa mtumwa wa pesa, niambie Amosi umeahidiwa kiasi gani cha malipo kwa ajili ya kufanya kazi ya hatari namna hii , unaniuliza nini nataka kutoka kwako? , hakuna chochote ninachotaka kutoka kwako , Curiosity killed the cat “
Mara baada ya kumalizia msemo ule wa shauku ilimuua paka alimpa ishara yule bwana kumpiga Amosi risasi.
“Wait!!”Amosi alizuia kifo chake na kumfanya Tresha kumpa ishara yule bwana asiruhusu risasi.
“Unataka kusema nini Amosi , kitakachokufanya uendelee kuishi”
“Naomba niulize swali?”
“Kwasababu ya historia yako unaweza kuuliza kabla ya kupoteza uhai”
“Kanali Dastani ndio aliekupatia taarifa juu ya ninachofuatilia?”Aliuliza Amosi akiwa na macho yaliojaa uchungu.
“Ukishajua ni Dastani utafanya nini , unadhani kuna uwezekano wa kulipiza kisasi hata baada ya kufa”
“Kwasababu jibu lako linaweza kunifanya nikupatie kitu cha thamani zaidi kuliko kifo changu”
“Amosi nipo hapa kwa maamgizo ya Binamu , unadhani ni kipi unaweza kuniambia nikaenda kinyume, una kitu gani cha thamani zaidi ya kifo chako?”Aliongea Tresha huku muonekano wake ukiwa siriasi lakini swali lile lilimfanya Amosi aone bado hawezi kufa kizembe.
“Nawajua nje ndani Night Shadows na namna ya kuwasiliana nao!!!”Aliongea Amosi na kauli ile ilimfanya yule bwana ambae alikuwa ameshikilia bastora kupepesa macho kwa kumwangalia Tresha na hio ndio nafasi adhimu ambayo Amosi alikuwa akiitafuta.
“Clang!!!”
Ilikuwa ni wepesi wa hali ya juu mno , kitendo cha yule mtu alieshikilia siraha kupepesa macho pembeni baada ya kutaja Night Shadows Amosi alikuwa ashahama aliposimama na kumtupia Bedlamp iliopasuka kwenye mikono yake na bastora kwenda pembeni.
Tresha ambae alikuwa mita kadhaa kutoka alipo Amosi hakuweza kufanya chochote kwani hakuwa na siraha.
Amosi hakuzubaa , mpango wake ilikuwa ni kukimbia na sio kushindana na Tresha , alijua mwanamke huyo likija swala la map[igano hamuwezi maana ni Ninja aliepitia mafunzo na mafunzo yakamzoea.
“Bang!!!”
Bahati mbaya spidi yake haikutosha na bastora iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti ilikohoa , kama sio kupinda kidogo tu pengine ingekuwa mwisho wake palepale.
Amosi licha ya kupigwa risasi hakutaka kusikilizia maumivu , bahati nzuri alikuwa hajauloki mlango , hivyo spidi yake ya kutoka ndani ya chumba hicho ilimfanya kukoswa koswa na risasi nyingine.
“Fuckk!!!”
Tresha alitoa tusi huku yule bwana alieshikilia bastora kutaka kukimbilia nje lakini alizuia.
“Carlos Stop!!!”Aliongea Tresha kwa nguvu na mwanaume mweusi ambae sasa tunafahamu jina lake ni Carlos aliishia mlangoni.
“Tresha tunapaswa kumuua kama oda yetu ilivyo”Aliongea Carlos.
“Umefeli kumuua akiwa mbele yako unadhani unaweza kumuua akiwa kwenye korido , unataka kuibua taharuki , unataka kuonekana katika Kamera”Aliongea Tresha huku akionyesha hali ya kukasirika.
“Wewe ndio umesababisha misheni imefeli , nilikuambia tokea mwanzo hili nitalimaliza mwenyewe , kulikuwa na haja gani ya kutaka kushiriki?”Aliongea Carlos na kauli ile ilimfanya Tresha kutoa tabasamu.
“Ndio tulipaswa kumuua , lakini ni mpaka atupe taarifa tuliohitaji , likija swala la kuua Carlos unatoka nje ya malengo ya misheni”Aliongea na kumfanya Carlos kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Ninachojua mimi ni kuua, nimefundishwa hivyo?”
“Ndio maana ya uwepo wangu hapa Carlos, tunapaswa kupata taarifa tunayotaka kutoka kwake , ndio tumuue sio vinginevyo?”
“Ameshakimbia , unadhani itakuwa rahisi?”
“Hilo niachie mimi , namjua Amosi nje ndani , nimefanya nae kazi kwa muda mrefu”Aliongea na kisha mwanamke huyo aliangalia mazingira ya chumba na kisha alichukua bahasha ambayo Amosi alionekana kuifuata na kutoa makaratasi na kuyakagua kwa muda.
“Unapaswa kuondoka”Aliongea Tresha ambae alipanda juu ya kitanda na kujiachia na kumfanya Carlos kumwangalia mrembo huyo kwa macho ya kimatamanio lakini Tresha hakujali macho yake na palepale aliweka bastora yake kwenye kiuno na kutoka nje huku akidhibiti hasira zake.
Upande mwingine Amosi alikuwa amesambaza matone ya damu kila mahali ndani ya hoteli hio lakini hakujali , hata watu aliopishana nao wakati akiwa ameshikilia ubavu wake wa kushoto hakutaka kuwapa hata nafasi ya kuona sura yake , ki ufupi akili yake ilikuwa katika tahadhari ya kujiokoa na alikimbia kweli.
Hoteli hio ilisifika kwa ulinzi mkali na usalama lakini kilichotokea kiliwashangaza watu.
Dakika chache alikuwa ashatokezea barabarani na kuanza kujikongoja kusogelea gari lake.
“Amosi!!”
Sauti ilimwita, ilitokea katika gari nyeupe RAV4 iliosimama kando ya barabara , Amosi aliangalia gari hio na kuonekana kuitambua na bila ya kujiuliza mara mbilimbili aliisogelea, mlango wa gari hio ulifunguliwa na aliingia ndani na hapo hapo ikaondoshwa.
*****
Hamza mara baada ya kumaliza kuongea na simu iliotoka kwa Amiri alikaa kwenye tarakishi na kisha alianza kufanya utundu wake , alishajua tarakishi za wafanyakazi zinafuatiliwa hivyo alitaka kuifunga tarakishi yake ki ujanja aendelee na mambo yake bila kushitukiwa.
Dakika ambayo ndio anamaliza kuseti mitambo , Linda aliingia akiwa na rundo la makaratasi mkononi , zilikuwa nyingi kiasi kwamba hata kubeba alionekana kupata shida.
“Hizi nyaraka unatakiwa kuzitafsiri kutoka kingereza kwenda lugha ya kiswahili , ziishe zote leo hii”Aliongea kikauzu na kauli ile ilimshangaza Hamza.
“Linda haiwezekanni ni nyingi mno kumalizika kwa siku moja “
“Bosi ndio kasema , eti kwasababu uwezo huo unao hataki kuona ukipotea bure”Linda aliweka nyaraka zile mezani na kisha kwa maringo alitoka.
Alikuwa akijua kabisa Hamza amemchokoza bosi , kwani alisikia akipiga makelele kutoka ndani ya ofisi yake ndio maana akapewa adhabu hio.
Ki ufupi kwa Regina ilikuwa ni kisasi mwanzo mwisho ili kumkomesha.
Hamza aliishia kujisikia uchungu lakini hata hivyo alikuwa akiupenda mshara wake hivyo aliishia kukubali kufanya kazi.
“Bora ningejifanyisha tu sijaona kitu , angalia sasa msala niliojitengenezea”Aliwaza Hamza.
Mpaka inafika jioni Hamza aliweza kutafsiri nusu tu ya kazi yote aliopewa na aliona hakuna uwezekano wa kumaliza yote na aliona atafute namna yoyote ya kuongezewa siku.
Lakini kabla hata hajajua cha kufanya mlango wa ofisi yake ulifunguliwa na Linda.
“Ni muda wa kuondoka kazini sasa , nenda maegeshoni na washa gari , washa AC na kisha msubiri bosi”Aliongea na Hamza alivuta pumzi ya ahueni , alikuwa amechoshwa kweli kuendelea kukaa hio sehemu.
Aliingia zake kwenye lift ambayo ilimpeleka moja kwa moja mpaka maegesho ya chini kabisa ya jengo hilo na kutoka , lakini wakati akitaka kusogelea gari ya Regina aliweza kumuona Kapteni Yonesi akiwa amesimama pembeni huku akimwangalia kwa macho yaliojaa sumu.
Ilionyesha ni dhahiri alikuwa amejitega hapo ili kumpata Hamza amshikishe adabu.
“Wewe mhuni hatimae umejitokeza”Aliongea kikauzu.
“Kapteni ndio unajiandaa kutoka kazini na wewe , hehe kwaheri tutaonana kesho”Aliongea Hamza akijifanyisha mjinga.
“Nani kakuambia naondoka?, unadhani naweza kusahau kirahisi kilichotokea mchana”
“Mchana kumetokea kitu gani?, mbona hata sina kumbukumbu”
“Wewe mpuuzi usie na aibu , kwahio unakataa kosa lako sio , umenidhalilisha mbele ya watu na sijakufanya chochote , huu ndio muda , nisipokushikisha adabu siwezi kuendelea kuitwa Kapteni”Aliongea na sekunde ileile alifyatuka kama mshale akitanguliza mguu akilenga maeneo nyeti ya Hamza.
Hamza aliishia kukwepa pigo lile na kumfanya Yonesi kupita.
“Kapteni ukiendelea hivi utanikasirisha ujue , mimi ni mwanaume na sio vizuri kupigana na mwanamke”
“Unajiita mwanaume , kwangu wewe ni mwanaume ulievaa suruali tu, kama unajiamini pigana na mimi tuone”Baada ya kuongea hivyo alijiandaa kumshambulia tena Hamza lakini aliishia njiani mara baada ya mlango wa lift kufunguka na Regina kutoka.
Regina mara baada ya kuona tukio lile alijikuta akishangaa huku akikunja sura.
“Yonesi , nini kimetokea?”
“Boss nina mashaka na tabia ya huyu mtu …”Aliongea Yonesi na kuanza kuelezea kilichotokea mchana juu ya Hamza kumchungulia manyonyo yake na kisha kumdhalilisha mbele ya wafanyakazi.
“Boss tusipomshikisha adabu mapema , hii tabia itafanya wafanyakazi kunidharau”Aiongea Yonesi akipigilia msumari.
“Mkurugenzi , usimsikilize Yonesi na porojo zake , mimi hio tabia ya kuchungulia watu sina kabisa , mimi nilikuwa nimekaa zangu kwenye meza tukiwa tunaangalia na nilimsifia kidogo tu kama ni mrembo na ndio akakasirika”Hamza alijitetea , lakini kwa bahati nzuri au mbaya Regina na Yonesi wote ni wahanga wa tabia ya Hamza na kwa muda huo alikuwa akimchukia mno Hamza kiasi kwamba mpaka meno yake yalikuwa yakimuwasha., Alidhani swala lile lilimtokea yeye tu kumbe alikuwa amemfanyia uhuni na Mlinzi wa kampuni .
Dakika hio hio Regina aliona aungane na Yonesi kumshikisha Hamza adabu l akini hakutaka kuonyesha kama alikuwa na yeye ni mhanga wa kupigwa chabo.
“Kama ni hivyo basi unaruhusa yangu ya kumshikisha adabu , angalia tu usije kumuua au akalazwa, anapaswa kuja kazini”Aliongea Regina na kumfanya Hamza amwangalie na kuona namna ambavyo Regina alikuwa amejaa sumu juu yake.
“Usijali mkurugenzi , najua ninachokifanya”Aliongea Yonesi na palepale muonekano wa kishujaa ulimjaa, alikuwa kama komandoo anaejiandaa kwa misheni ‘shikisha adabu’.
Subiri kwanza , twendeni mpaka floor ya pili katika chumba cha mazoezi”Aliongea Regina , alijua ikitokea mfanyakazi wa kampuni kushuhudia tukio la Yonesi kumpigwa Hamza inaweza kuleta shida
“Kuna haja ya hili , mkurugenzi au unakinyongo na mimi?”Aliuliza Hamza.
“Eliza alisema wewe ndio uliemsaidia kumuokoa katika udhalilishaji , naamini unao uwezo wa kushindana na Yonesi japo kidogo, chukulia kama mazoezi ya kukuweka fiti kidogo uonekane mwanaume”Aliongea Regina.
Hamza hakuwa na jinsi zaidi ya kutii maagizo ya Mkurugenzi na kwenda katika floor ya pili kwa ajili ya kushikishwa adabu.
Dosam ilikuwa ni kampuni yenye wafanyakazi wengi na biashara zao zilihusisha bidhaa za thamani , hivyo walikuwa na kitengo cha ulinzi ambacho ikitokea mzigo unasafirishwa basi ndio huhusika kuimarisha ulinzi , hivyo kwa ajili ya idara ya ulinzi ilitengwa floor nzima ya pili kwa ajili ya mazoezi , kulikuwa na kila aina ya vifaa ikiwemo Gym na hata eneo la kupimana nguvu.
Ilikuwa ni muda wa kuondoka kazini , hivyo hakukuwa na watu ndani ya eneo hilo.
Yonesi alimchukua Hamza na kumpeleka katika Arena , alifanya hivyo ili isitokee Hamza akakimbia wakati wa kumpiga.
“Ni kweli unataka kupigana na mimi?”Aliuliza Hamza.
“Usiwe na wasiwasi , ngoja nikunyooshe nyooshe viungo , lakini sitokuua”
“Basi hakuna shida , ila kumbuka miguu na mikono haina macho hivyo kuwa makini”
“Acha woga , jali usalama wako kwanza”
Mara baada ya kumaliza sentesi hio Yonesi alimsogelea Hamza kwa spidi huku akinuia kumchapa ngumi ya bega.
Lakini alichokifanya Hamza ni kuwa na spidi kidogo tu kwani mara baada ya ngumi ile kumfikia aliinama ikapita lakini muda huo huo bila ya Regina kuona Hamza alishainua mkono na kugusa msambwanda.
“Ahhhhhh…”
Yonesi alijikuta akipiga makelele mara baada ya kuhisi mkono ukimgusa upande wa kushoto.
“Mshenzi wewe” Ishara ya mauaji ilimvaa Yonesi.
“Kapteni vipi tena , mbona unafoka wakati tunapigana?”Aliongea Hamza ambae alikuwa amejificha kwenye kona ya steji.
“Umenigusa tena”,
“Unamaanisha nini nimekugusa , kwahio wewe unaweza kunipiga lakini mimi siruhusiwi kukugusa, kama ni hivyo unaweza kuniua hapa hapa”.
“Mhenzi wewe , hujui kupigana kazi yako ni kugusa tu”
“Nimegusa wapi?”Hamza alikuwa akijua fika ni wapi amegusa lakini alijifanyisha hajui , alijisikai vizuri, alitaka kumshikisha adabu mjeda huyu bila hata ya kumpiga.
Regina alikuwa akiangalia pambano na hakuwa akielewa kinachotokea , kutokana na spidi ya Hamza.
Yonesi hakujua namna ya kuongea tena hivyo alijiamulia kupambana tu , awamu hio alikuwa amedhamiiria kumpiga Hamza kwa kutumia mguu na sio ngumi tena
Hamza aliishia kuvuta pumzi na dakika ambayo shambulizi linamfikia alishafanikiwa kusogea kushoto.
Yonesi alijikuta akipandwa na hasira mara mbili mara baada ya kuona amepiga hewa , lakini hakutaka kujiuliza Hamza kaweza vipi kukwepa shambulizi lake hivyo aligeuka na kumsogelea tena na kuanza kurusha ngumi mfululizo.
Hamza alikuwa akijifanyisha kuwa muoga wa ngumi zile na kurudi nyuma kila mara Yonesi alipokuwa akishambulia , alionekana kama amezidiwa lakini ukweli ni kwamba yeye ndio aliekuwa na maamuzi ya kumaliza pambano hilo au kulirefusha
Yonesi aliishia kumkimbiza Hamza kila mahali alipohama lakini mwisho wa siku yeye ndio aliekuwa wa kwanza kuchoka.
“Kwanini unakuwa muoga na kukimbia kimbia kama panya , kama kweli wewe ni mwanaume usikimbie na tupigane ana kwa ana”
“Kapteni unachofanya ni kulazimisha nifanye kitu ambacho sitaki na kwasababu sitaki nitaendelea kukimbhia”
“Kuwa mwanaume basi”Aliongea kwa kufoka.
Hata Regina ambae alikuwa akiangalia alishindwa kuvumilia mara baada ya kuona Hamza anachofanya ni kukwepa tu na hashambulii.
“Hamza jikaze basi hata kidogo?”Aliongea.
“Nijikaze niumie , naogopa nisije kupoteza taifa la kesho hapa hapa”
“Huna lolote , pigana na mimi acha kukimbia”Aliongea Yonesi na palepale alimsogelea Hamza kwa mara nyingine , uwezo wa Yonesi kuanzisha mashambulizi haukuwa wa kawaida , alikuwa akijua kujipima wakati wa kushambulia mno alichokosa ni spidi tu basi na ndio maana kila shambulizi alilorusha Hamza alikuwa na uwezo wa kulikwepa bila shida yoyote
Mwishowe Yonesi aliona kabisa Hamza pengine kuna kitu anaficha , inawezekana vipi mtu wa kawaida kuweza kuwa na stamina ya aina hio , maana yeye alikuwa amechoka lakini Hamza ni kama bado ndio anaanza na anahema kawaida tu.
Kilichomkasirisha zaidi ni kwamba mpuuzi huyo alikuwa akimwigizia na hakuwa akionyesha uwezo wake kabisa , kitendo hicho kilimfanya Yonesi aone ni udhalilishaji.
Mara baada ya kufeli zaidi ya mara tano , hatimae alipata wazo ambalo lilimfanya adondoke chini kwa kupiga magoti na kufunika uso wake na viganja na kuanza kulia kwa kwikwi.
Kwa namna ambavyo Yonesi alikuwa akilia ilikuwa ni kama mke aliefiwa na mume wake , mtu yoyote angemuona mjeda huyo mrembo angemuonea huruma.
Hamza alijikuta akiingiwa na aibu baada ya kuona Yonesi analia hata kwa Regina hivyo hivyo alishangaa kuona Yonesi analia, maana ilikuwa mara yake ya kwanza kumuona afande akilia baada ya kupigwa.
Ukweli ni kwamba Regina hakuona Hamza akimpiga Yonesi na upande mwingine alimjua Yonesi kama mwanamke jasiri na mkali.
“Hamza muombe msamaha Yonesi , kama mwanaume unatakiwa kujua wakati wa kuacha”Aliongea Regina lakini Hamza alijihisi ni kama anaonewa , maana hakumpiga hata kidogo Yonesi.
Hamza hakutaka kuona Yonesi akiendelea kulia na alimsogelea kwa ajili ya kumbembeleza
“Kapteni usiendelee kulia , nimekosa mimi nisamehe sa…”
Kabla hata Hamza hajamaliza kuongea Yonesi aliibuka na kibao na kumchapa nacho Hamza upande wa kushoto, baada ya kibao aliunganisha na ngumi kwenye tumbo na kumfanya Hamza kutoa mguno.
“Naomba unisamehe Kapteni , vinauma , vinauma”Hamza alibembeleza asemehewe huku akifanya kuugulia maumivu chini sakafuni.
“Wewe mpuuzi nitahakikisha kila siku utakayoniona unanikimbia”Aliongea Yonesi huku akisimama na kupumua kwa ahueni.
Regina aliekuwa chini ya steji alishia kushangaa mara baada ya kugundua kumbe Yonesi alikuwa akijifanyisha mdhaifu kutafuta nafasi ya kumshitukiza Hamza.
Mashambulizi yale yalionekana kumuumiza Hamza na Regina alijiuliza atakuwa katika hali gani.
Mara baada ya kilichotokea Regina aliishia kumlaani Hamza ndani kwa ndani kwa kujifanyisha kijeba na kuchungulia chungulia wanawake na kujiambia anastahili kweli kipigo.
Mara baada ya kumshinda Hamza , Kapteni Yonesi hakuhisi hata kidogo furaha wala mafanikio , alikuwa akijua kabisa yeye ndio ambae ameshindwa.
Aliishia kujiwazia huyu Hamza kila dakika anazidi kuonekana sio wa kawaida na pengine hata kufanywa kuwa msaidizi ni kutokana na Regina kufahamu hilo.
“Mkurugenzi , nitaondoka sasa , kwaheri”Aliongea Yonesi.
“Ni kweli unapaswa kwenda kupumzika , siku imekuwa kubwa kwako”Aliongea.
Hamza alikuwa bado amelala kwenye steji licha ya Yonesi kuondoka na Regina alimwangalia kikauzu.
“Uko sawa wewe? , kama bado hujafa amka tuondoke”
“Regi nimeumia kwa ndani”Aliongea Hamza.
“Acha maigizo , kama huamki naondoka zangu”
“Nataka busu ili niamke”Aliong ea na kauli ile ilimshangaza Regina na kumfanya kuona aibu za kike , lakini tofauti na kuwa na hasira alimuuliza.
“Wapi unataka upigwe busu?”
Hamza mara baada ya kusikia swali lile alijikuta akifurahi na kujiambia kumbe kupigwa nako kuna faida na kwa haraka haraka alitumia kidole chake kuonyesha eneo la mdomoni.
Regina alivuta pumzi nyingi huku ukauzu ukizidi kumvaa , aliangalia pembeni na kuona kifaa cha kuchukulia mazoezi ya mkono na mara baada ya kukiokota alimlenga nacho Hamza mdomoni.
“Kiss your ass!!”
Hamza aliweza kukwepa haraka kifaa kile kabla hakijampata na kusimama na kumwangalia mwanamke huyo alivyokuwa amefura kwa hasira.
“Hey! Nilikuwa nakutaia tu usikasirike hivyo”
“Ukiendelea kuongea ujjinga nitahakikisha unapata mshahara nusu”
“Ah , boss basi yaishe, nimekosa mimi naomba usinikate mshahara , nitaenda kuwasha gari tuondoke sasa”
Hamza hakutaka kukosa pesa kwa tukio dogo kama hilo , isitoshe kutafsiri makatarasi yote yale haikuwa kazi ndogo ambayo anaweza kukubali kukatwa mshahara kizembe.
Lisaa limoja baadae wote waliweza kufika nyumbani na Shangazi alikuwa bize kuandaa chakula cha usiku.
“Hamza vipi siku yako ya kwanza kazini?”Aliuliza na Hamza alitaka kusema amenyanyaswa siku nzima lakini Regina alimpiga jicho asije kuongea ujinga na akaacha na kuanza kucheka.
“Haha.. Shangazi siku yangu ilikuwa nzuri sana , sitaki tu kuongelea ilivyokuwa lakini ,itoshe kusema nimepata Vitamini ya macho”
Kauli yake ilikuwa na zaidi ya maana na kumfanya Regina aliekuwa pembeni yake kupandwa na hasira na kutaka kumpiga na rimoti palepale.
Hamza alikuwa na miadi yake hivyo hakutaka kukaa sana nyumbani , ijapokuwa chakula ndani ya nyumba hio kinawahishwa hakutaka kula kwanza mpaka amalizane na Amiri., hivyo alipandisha juu kujiandaa kuondoka lakini wakati anashuka aliweza kumsikia Regina akiongea na simu na moja kwa moja aliweza kujua ni baba yake aliekuwa akiongea nae lakini aliishia kukaa kimya , ilionekana kuna jambo ambalo liliwafanya kujibishana tena.
“Shangazi natoka kidogo , kuna rafiki yangu nataka kuonana nae”Aliongea Hamza.
“Lakini chakula cha usiku kinakaribia kuiva utawahi kurudi?”
“Sijajua Shangazi , kama nitachelewa naomba uniwekee tu nitakula nikirudi , anaonekana kuwa na matatizo”Aliongea Hamza na Shangazi alionekana kumuelewa , ukweli alifurahi kuona Hamza alikuwa angalau na rafiki.
“Sawa, wahi ukamuone rafiki yako”
Hamza mara baada ya kuaga alitaka amuage Regina lakini mwanamke huyo alionekana bado alikuwa akiongea na simu , huku muonekano wake ukiwa umebadilika hivyo alijua maongezi hayo ni siriasi.
Alitoka nje na kuchukua ile Lexus ya Regina na kuondoka , akiwa njiani alimpigia Amiri lakini hakupokea , lakini hata hivyo hakutaka kughairi , aliendelea kuendesha na wakati anakaribia daraja la kigamboni simu iliita.
“Uko wapi bro , nilikuwa nimetingwa kidogo”
“Okey , ndio nimetoka niambie tuonane wapi?”
“Samaki Samaki bro , ukikaribia nishitue”
“Poa”
Licha ya kwamba anakoenda ni mbali , lakini kutokana na kuwa na gari kali hakuona shida , pili hakuwa ametoka usiku muda mrefu.
Ilikuwa ni saa moja kwenda na nusu na foleni hazikuwa kubwa sana upande wa magari yanayorudi mjini , hivyo hakupata shida kubwa, dakika arobaini tu aliweza kufika Samaki Samaki na alimpigia simu Amiri.
“Bro umewahi mno , nikajua kwa foleni utachukua muda kidogo kufika”
“Nipo na usafiri binafsi , tuonanae wapi”
“Ah kumbe , nisubiri hapo mgahawani nakuja muda si mrefu”
Hamza aliangalia mazingira ya eneo hilo na palionekana kuchangamka, kulikuwa na magari mengi.
Kutokana na gari yake kuwa ya bei ghali hakupata shida ya kuegesha , watu waliomuona akitoka kwenye gari hio ya Lexus walimwangalia kwa macho ya maswali mengi.
“Bro!!!”
Hamza kabla hata hajapiga hatua kuingia ndani ya mgahawa aliweza kuitwa kwa nyuma na aligundua aliekuwa akimwita ni Amiri.
“Nilijua utachukua muda”Aliongea.
“Nilikuwa maeneo haya haya , njoo tuongee kwenye gari”Aliongea Amiri huku akizungusha macho.
Amiri alikuwa ameegesha Aud yake katika maegesho ya muda mfupi na waliingia ndani wote , jamaa huyo alionekana kuwa na haraka mno na hilo Hamza aliliona.
“Unaonekana akili haijatulia lakini kwa muonekano wako nadhani hali sio mbaya kama nilivyofikiria”Aliongea Hamza.
“Nimechanganyikiwa kutokana na kuwa na maswali mengi , lakini bado nina hofu , pengine unaweza kunipa jibu ambalo linaweza kuifanya hali yangu kuwa mbaya zaidi”Aliongea.
“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , wewe ndio ambae ulichukua hatua , inabidi kuyakabili matokeo”
“Nadhani tuongelee hapa hapa kwenye gari , nina miadi na Melisa , nimepata ahueni tumeonana kabla ya kukutana nae”
“Unakutana nae sasa hivi?”
“Ndio , nilimuahidi nitamtoa Out leo , japo nina wasiwasi na kinachoendelea lakini angalau nataka kuondoa huu mkanganyiko kabla hatujaonana”Aliongea na palepale alitoa simu pamoja na Earpod na kumpa Hamza.
“Sikiliza hio na unipe majibu”
“Nisikilize tena , nikajua ni Vidio”
“Bro , tuliweka kamera za vidio ndio lakini sikuweza kuona cha maana, mpaka siku moja nilipoona tukio ambalo sio la kawaida , ndio ambalo lilinipelekea kuweka kinasa sauti”
“Tukio gani?”Hamza aliuliza kwa shauku.
“Sikiliza kwanza hio sauti niliosikia kutoka ndani kwake”Aiongea na Hamza alitingisha kichwa kukubali.
SEHEMU YA 21.
Hamza kadri alivyokuwa akisikiliza ndio uso wake ulionyesha mabadiliko , hayakuwa mabadiliko ya mshangao bali ya kuchanyikiwa pia.
“Mbona nasikia lugha ambayo sijawahi kuisikia popote ni lugha gani hii?”Aliongea Hamza na kumfanya Amiri na yeye kuonyesha ishara ya kutokujua.
“Hapo ndio pamenichanganya sana , hio sauti ni ya Mellisa wangu , siwezi kosea Bro , lakini anaongea lugha ambayo siijui”Aliongea Amiri na Hamza aliongeza umakini katika kusikiliza ili ajaribu kutafsiri nini kinaongelewa , alikuwa akisikia sauti ndio lakini lugha hajawahi kuisikia.
“Hii lugha sijawahi kuisikia popote , au ni lugha sizizo rasmi za kimakabila, wanaongea nini”Hamza alionekana kujiuliza.
“Baada ya hapo watabadili lugha , sikiliza kwa umakini bro”Aliongea Amiri na Hamza alitingisha kichwa na kusikiliza.
“Silvia kadri tunavyochelewa ndio uwezekano wa kurudi kuwa mdogo , tunatakiwa kumpata Princess Natasha mapema kabla ya Profesa”
“Rosaron hatujui mpaka sasa roho ya Natasha inaishi katika mwili wa nani , sio rahisi kumpata”
“Atatutafuta yeye mwenyewe baada ya teknolojia ya Somnus kufanikiwa , tunatakiwa kusubiri lakini kuwa tayari vilevile, kosa kidogo tu litamuamsha na Profesa , wakiungana itakuwa ngumu kwetu”
“Rosaron unadhani tupo sahihi , namaanisha Pincess Natasha kuwepo hapa Tanzania!!?”
“Tumefika hatua hii kutokana na imani tulioaminishwa , njia pekee ya sisi kuonekana ni kurudi, Silvia wewe ndio uliekuwa mpenzi wake , mapenzi yana nguvu akiamka atakutafuta wewe, ndio maana upo hapa”
Hio ndio namna ambavyo sauti zilisikika , lakini katika maongezi hayo Hamza na Amiri wote hakuna ambae alisikia neno Mellisa , kwa maana kwamba maongezi hayo hayakumhusu Mellisa.
“Sijasikia jina la Mellisa”Aliongea Hamza
“Sijasikia jina lake pia , lakini sauti ni yake”
“Una uhakika hio ni sauti ya Mellisa?”
“Ndio , siwezi kusahau sauti ya Mellisa hata niwe nimelewa pombe”Aliongea na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.
“Vipi sauti ya pili unaitambua , namaanisha hio ya mwanaume?”
“Sijawahi kuisikia , lakini kwa rafudhi yake anaonekana sio mbongo”Aliongea na Hamza pia alikubaliana na Amiri sauti ya pili ilikuwa sio mtu mwenye rafudhi ya kiswahili.
“Hebu subiri”Aliongea Hamza na kisha alichukua Earpord zote mbili na kuzitumbukiza kwenye masikio na kupelekea mbele ile rekodi ya sauti, Amiri alibakia kimya asijue nini ambayo Hamza anajaribu kufanya.
Hamza alikuwa akisikiliza ka kurudisha nyuma sauti na kwenda mbele na ndani ya dakika tano alitoa Eapord zile masikioni.
“Umegundua nini?”
“Najiuliza kwanini hawakuendelea kuongea kwa ile lugha na kubadilisha katika lugha ya kiswahili , pia sauti ya mwanaume tuliokuwa tukisikia ni ya Mzungu rafudhi yake , tena mzungu wa Ulaya kila kitu kinaonyesha alikuwa akiongea na Mellisa kutumia kifaa maalumu au simu”
“Unamaanisha hakuwa ndani kwa Mellisa?” Aliuliza Amiri na Hamza alitingisha kichwa.
“Kama hakuwepo unazungumzia nini kuhusu jina la Silvia , kwanini huyo mzungu kamtambua kama Silvia mpenzi wangu?”
“Hapa siwezi kukupa jibu la moja kwa moja , kuna mawili ambayo yote yanawezekana , kuna uwezekano ni kweli Mellisa ni Silvia au huenda ana multiple Personality, kuhusu kuwa Silvia hilo halina maelezo mengi lakini kama kweli ana ugonjwa wa nafsi mbili ni ngumu kufanya mawasiliano na mtu au mtu kupigia akitarajia Mellisa kuwa Silvia au Silvia kuwa Mellisa”
“Kaka sijakuelewa kabisa , umenichanganya?”Aliongea Amiri na kumfanya Hamza amwangalie machoni , ni kweli bwana huyu alionekana kuchanganyikiwa.
“Ushawahi kuagalia filamu ya Split?”
“Bro mimi sio mpenzi wa Filamu kabisa”Aliongea Amiri na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.
“Okey , ipo hivi ninachomaanisha mpenzi wako Mellisa kuna uwezekano akawa mgonjwa wa akili wa kuwa na nafsi mbili , yaanni nafsi ya Mellisa na muda mwingine anakuwa Silvia kama ulivyosikia, ila kwa hapa nashindwa kuamini moja kwa moja , kwasababu kama kweli ni Silvia kwanini akaongea lugha ambayo haieleweki na baadae akahamia katika lugha ya kiswahili kama kawaida, vipi kuhusu alichokuwa akiongea ni kitu cha uhalisia?”
“Kwahio unamaanisha anaweza asiwe mgonjwa wa akili au vipi , mpaka kuweka hayo maswali?”
“Ndio anaweza asiwe na shida hio?”
“Kama sio hivyo atakuwa na shida gani?”
“Kuna kitu nakiwaza lakini sina uhakika nacho , hata kama nikikuambia nitazidi kukuchanganya , kitu kimoja ambacho nina uhakika nacho Mellisa hakusaliti kama ulivyomdhannia, sauti ya mwanaume ukisikiliza kwa umakini sio katika ile nyumba”
“Bro unaonekana kujua vitu vingi na ndio sababu ya mimi kukushughulish, awali nilitaka kuona kama kweli Mellisa ananisaliti lakini hisia zako na zangu sasa hivi zimefanana , lakini hilo sina shida nalo , Mellisa ana tatizo na mimi kama mpenzi wake napaswa kumsaidia , Bro yule mwanamke nampenda na napanga kumuoa kabisa , hili swala lazima nilipatie ufumbuzi”Aiongea Amiri akiwa siriasi.
“Hili swala nitakusaidia lakini utahitaji kuwa mvumilivu , kitu ninachotaka kujua kutoka kwako je kuna chochote kitu ambacho sio cha kawaida ushawahi kuona pale anapoishi na kwanini ulidhania anakusaliti?”
“Alianza kubadilika , nilikuwa na tabia ya kwenda kwake usiku , lakini siku moja nakumbuka ilikuwa Jumaane miezi minne iliopita , nilikuwa nimelewa siku ile nilipofika kwa Mellisa alikataa kabisa nikiingia ndani na alipogundua ni mimi hakufungua kabisa, kutokana na pombe sikujua kilichotokea , lakini asubuhi nilikuwa ndani kwake , mwanzoni nilidhani baada ya kulewa nilikuja kwake akanifungulia kawaida nikaingia , lakini mara baada ya tukio la pili ndio kumbukumbu za siku hio zikajirudia na kukumbuka alikataa kunifungulia”
“Tukio la pili likoje”
“Hii siku hakunikatalia kuingia ndani , ila alinisubirisha kwenye mlango , jambo hili halikuwa la kawaida , baada ya dakika kama tano niliingia ndani lakini kuna harufu kama marashi hivi ambayo Mellisa hatumii , nilitafuta haya marashi wakati akiwa amelala lakini sikuyaona , haikuwa hivyo tu usiku alikataa kunipa kabisa, haikuwa mara ya kwanza au mbili tu Bro , imekuwa kama ratiba , kila nikienda kwa Mellisa siku ya Jumanne lazima anifanyie janja janja nisile mzigo”Aliongea na kumfanya Hamza kumwangalia Amiri.
“Umesema kila Jumanne , inamaana hata siku ulioenda kwake amelewa na mara ya pili kunusa harufu ambayo sio ya kawaida , ilikuwa Jumanne?”
“Ndio nakumbuka siku niliolewa ilikuwa jumanne , ki ufupi Mellisa kila ikifika Jumanne hataki tuonane kabisa , hii ndio sababu ya kumuwekea kinasa sauti , zile kamera zilikuwa zikileta picha tu ila sauti hakuna , nikaenda kuweka kinasa sauti na jana ndio nimesikia hiki ulichosikia”
Muda uleule simu ya Amiri ilianza kuita na mara baada ya kuangalia jina alimpa ishara Hamza kwamba ni Mellisa ndio anapiga.
“Muda mzee , nilioahidiana nae”Aliongea Amiri na Hamza alimpa ishara apokee simu kwanza.
“Babe uko wapi , mbona hutokei?”
“Nakuja dakika chache , nipo maeneo haya haya”
“Sawa , wahi njaa inaniuma”
“Sawa love , nakuja”
“Kwahio unasemaje Mzee?”Aliuliza Amiri mara baada ya kumaliza kuongea na simu.
“Kuwa nae karibu kwanza , angalia kama kuna kitu kisicho kawaida , au matumizi ya dawa yoyote, kwasasa nina shauku na hii lugha waliokuwa wakiongea mwanzo, naweza kuchukua sauti zao nikaitafutie ufumbuzi?”
“Nakuachia kila kitu mtaalamu , mwenyewe nina shauku ya kutaka kujua Mellisa anaongea lugha gani , mwanzoni nilijua labda ni roho mtakatifu , yule ni mkristo na wakristo kuna muda wanaongea lugha zisizoeleweka”
“Kunena kwa lugha wanaita , inawezekana mpenzi wako alikuwa akinena kwa Lugha wakati akiongea na Rosaroni”Aliongea Hamza na kumfanya Amiri kutabasamu.
“Unazingua kaka”
“Sijazingua , naamaanisha ni kitu ambacho hakiwezekani kunena kwa ligha huku unaongea na mtu , tena mzungu”
Amiri alichomoa flash na kuunganisha na OTG kisha akakopi faili lile la sauti na kumpa Hamza.
“Ukipata chochote nishitue nakuaminia sana mtaalamu”
“Nikifanikiwa nitakuambia , ila kuhusu hii lugha…anyway nitakushitua”Aliongea Hamza na kisha alishuka kwenye gari.
“Sema mzee hatujaonana kama wiki na nusu hivi ila muonekano wako umebadilika sana, umekuwa bomba”Aliongea Amiri akiwa ameshusha kioo , ni kama sasa anamuona Hamza akia na mavazi ya bei ghali.
“Nimeangukiwa na bahati , pengine ninaweza kubadilika zaidi ya hivi”Aliongea Hamza huku akitabasamu.
“Haha.. hapo kidogo mrembo Anitha anaweza kukusikiliza , halafu umekuja na usafiri gani , ulipokuwa ukiongea ni kama ulikuwa ukiendesha?”
“Nilikuwa nikiendesha ndio , kuna mtu niliomba niendeshe gari yake”Aliongea Hamza hakutaka kumuonyesha Amiri kama alikuja na ile Lexus , maswali yangekuwa mengi .
Hamza mara baada ya kuachana na Amiri alifikiria kidogo , aliwaza kurudi nyumbani lakini wazo hilo ni kama halikuwa kipaumbele kwenye halmashauri yake ya kichwa, lakini mara baada ya kukumbuka alimwahidi Shangazi angekula akirudi aliona arudi nyumbani tu moja kwa moja.
****
Upande wa Regina hakupata hata hamu ya kula mara baada ya kuongea na simu, baba yake alimpigia akimlaumu kwanini anataka kuunua kampuni ya Omega inayojihusha na uhandisi wa Programu endeshi za tarakishi.
Baba yake alimwambia sio vizuri lakini pia ingemgharimu hela nyingi kununua kampuni hio kwani hisa zake zimepanda.
“Regina kwanini unafanya maamuzi bila ya kushirikisha wajomba zako na wakurugenzi wa bodi?”
“Huu ni mpango ambao ulishapitishwa tayari katika kikao kilichofanyika mwezi uliopita”Aliongea Regina.
“Unadhani walichopitisha ndio wanachotaka , wamefanya yote kukusikiliza kwasababu wanakuamini sana lakini vilevile hawana uelewa na maswala ya komputa , Tanzania kwa mara ya kwanza tunaingia katika biashara ya uhandishi wa Programu endeshi , kwanini unataka kujiingiza katika vitu ambavyo huna uzoefu navyo , isitoshe ni mpaka wakurugenzi wote wa bodi wakubali”Aliongea Mzee Wilsoni.
“Kwanini hawakujitokeza kwenye kikao na kunipinga waziwazi?”
“Wewe mtoto , hawakujitokeza mbele yako kwasababu wanaheshimu mawazo ya babu yako , ndio watu waliokuwa wakifanya kazi na babu yako kwa miaka na miaka , wanachokifanya ni kutotaka kuona unafanya maamuzi ambayo yapo nje ya sera ya kampuni”
“Baba , ijapokuwa wewe ni moja ya mmiliki mkubwa wa hisa lakini huna nafasi yoyote ya uongozi , hivyo siwezi kuzungumza hili swala na wewe , kama wao ndio wanataka kuongea basi waache waongee na mimi mwenyewe , sio wewe kuwa msemaji wao”
“Hakuna shida , bodi ya wakurugenzi kesho itakaa kikao na unapaswa kutushawishi kwa fact , ukishindwa kutushawishi usije kutulaumu tukipiga kura ya kutokuwa na imani na wewe kuendelea kuwa katika nafasi ya ukurugenzi wa kampuni, na ikitokea hivyo utapoteza kila kitu”
Wajomba ambao walikuwa wakizungumziwa hapo mmoja wapo alikuwa ni Mzee Willium , huyu alikuwa makamu raisi wa kampuni na mwingine alikuwa ni Mzee Sebastian ambae pia alikuwa Mkurugenzi msaidizi., wote hao walishikiria nafasi hizo kutokana na hisa walizokuwa wakimiliki ndani ya kampuni ya Dosam.
Regina hakutaka kuendelea kujibishana na baba yake na alimwambia kesho ahudhurie kikao cha bodi kama kweli anataka kupinga mpango wa kununua kampuni mpya ambayo imeanza kustawi inayojihusiaha na uhandisi wa programu endeshi, pamoja na akili mnemba.
Ijapokuwa Regina alikuwa ashaweka mizizi yake kama kiongozi wa kampuni lakini bado kuna waliokuwa na nguvu ya ushawishi na haikuwa rahisi ya kuwaondoa.
Wafanyakazi kama Eliza , Prisila na wengineo ambao wananafasi za juu na wanamuamini Regina katika maamuzi ukweli ni kwamba ushaiwhi wao unahesabika kama mdogo mno , kwao walikuwa kama wafanyakazi tu.
Hivyo hata kama viongozi hao wakae kikao na kutaka kufanya maamuzi makubwa yasingepita moja kwa moja , lazima yangepita katika bodi ya wakurugenzi na kisha wao ndio wanapiga kura ya kupitisha maamuzi hayo , huo ndio utaratibu kwasababu kampuni ya Dosam haikuwa ya Regina peke yake.
Kilichokuwa kikimuuzi Regina zaidi ni pale ambapo baba yake alikuwa akitumiwa na watu wa nje kujaribu kumbadilisha mawazo , haikuwahi kutokea Mzee Wilsoni kukubaliana na mawazo ya binti yake , siku zote ni mwenye kumpinga.sio kwamba hakuwa akikubaliana nae bali ni kwasababu alikuwa akijaribu kumlinda kwa staili yake , alijua akimfanya Regina kupunguza kujiamini ndio anamlinda.
Sasa wakati Hamza akiwa SamakiSamaki kama angeingia katika mgahawa huo angeweza kumuona James na baba yake wakiwa pamoja na wazee wawili ambao wana miaka makadirio kama ya miaka hamsini hivi wakiwa wamezungukwa na wahudumu ambao walikuwa wamevalia kimitego.
“Mzee Willium kwahio ni kweli Regina anataka kuinunnua Omega?”Aliuliza baba yake James.
Mzee Willium alikuwa na nywele rangi nyeupe tupu, wakati huo walikuwa ameshikilia mrembo mmoja mkono huku akijaribu kuthaminisha maumbile yake.
“Ni kweli kikao cha wahisani kilishapita mbona”Aliongea huku akicheka.
“Mzee Willium nina marafiki zangu kadhaa na tumefanikiwa kumshawishi Wilsoni , tunapanga kupinga kila ambacho Regina ataongea kesho”Aliongea Mzee Sebastiani na kauli ile ilimshangaza kidogo baba James.
“Mzee Wilsoni amekubali?”Aliuliza.
“Wilsoni bado ni mtoto na hajui mambo mengi , tulichofanya ni kusema maneno machache ya hapa na pale na akatuamini , nadhani mpaka sasa amempigia simu binti yake na kumlalamikia lakini ninavyojua mimi Regina hawezi kumchukulia siriasi”
“Kesho katika kikao lazima Regina atakuja na mbinu za kutaka kuwashawishi ili kuinunua Omega , muda huo nitahitaji mnitumie taarifa hio”Aliongea Baba James.
“Usiwe na wasiwasi huna hata haja ya kuomba , tumekuwa tukifanya kazi pamoja kwa muda mrefu , hatuwezi kumruhusu Regina kufanikiwa kuinunua”Aliongea Mzee Willium.
“Ni kweli kabisa alichoongea Willium , tunachosubiri hapa ni James kufunga ndoa na Regina , pumbavu kabisa tunaruhusu vipi undugu wa kitajiri tuliojenga kwa miaka kuishia katika mikono ya msichana mdogo kama Regina”
James mara baada ya kusikia kauli ile alitoa cheko na kisha aliinua chupa ya wine akiwa amesimama.
“Asanteni sana wazee wangu , ili kuonyesha ni namna gani ninashukuru nitawamiminia kinywaji, Baadae kama nikifanikiwa katika mpango wangu Dosam tutainganisha na kampuni yetu , nawahakikishia sitowaangusha , mtapata hisa za kutosha katika kampuni yetu”Aliongea James na mabwana wale matabasamu yalikuwa njenje.
“Usiongee sana unamaliza mate , tunajua ukubwa wa familia yenu , hatuewezi kuishi kwa kujibana bana chini ya utawala wa yule msichana mkatili”Waliongea huku wakicheka na kwa pamoja waliinua glasi zao na kugongesheana.
Baba yake na James alimwangalia mrembo aliekuwa nyuma yake na kisha alimpa ishara, mwanamke yule alielewa somo na kimapozi kabisa alizungusha mkono katika shingo ya mzee Willium huku akilegeza jicho.
“Pedeshee Willium muda umeenda na naogopa , unaonaje ukinipa lift kwenda nyumbani”Aliongea huku akiwa amerembua , alikuwa mweupe na mapaja yake makubwa yalivutia mwanaume yoyote rijali.
“Hakuna tatizo mrembo , wewe niambie unaishi wapi , halafu kama ni mbali kwanini hukuongea mapema , pengine tungeanza safari mapema”Aliongea huku akimkonyeza.
“Aiyaa, Mzee Willium unajua … mimi sitaki bwana….”Aliongea yule mwanamke lakini wakati huo akihakikisha manyonyo yake kumsugua vilivyo Mzee Willium.
Upande wa Mzee Sebastian hakutaka kulembesha na alikuwa akichimba mgodi hapohapo mezani kwa mrembo mwenye umbo matata rangi ya kunde, wote walionekana vilevi vimewakolea.
James na baba yake waliangaliana na wote kwa pamoja walitoa tabasamu lenye uovu ndani yake.
****
Siku iliofuata Hamza alienda kazini kama kawaida na alihakiksiha tarakishi yake haifuatiliwi ili afanye mambo yake.
Hamza alijua alikuwa na kazi kubwa hivyo alihakikisha kwanza kiporo cha jana anakimaliza ili awe na muda wa kutosha wa kufanya ambo yake bila wasiwasi.
Mpaka inafika mchana alikuwa ashamaliza kazi yote na alijifisia kwa kuwa na uwezo mkubwa wa akili wa kufanya vitu haraka haraka.
Baada ya kuona njaa inauma moja kwa moja alitoka na kuelekea mpaka chini kwenye mgahawa.
Kitendo cha kuingia katika mgahawa huo wa kamuni macho yalikuwa yakimwangalia , ukweli ni kwamba tukio la jana ni kama limempa umaarufu na kufanya watu wengi wamfatilia na walifahaua laikuwa msaidizi wa bosi.
Ukiachana na alichokifanya jana siku hio wafanyakazi wa kike ikiwemo Asha na Mirium hamu yao ilikuwa ni kuona namna Yonesi na Hamza wataendeleza pale walipoishia jana, hawakuwa na uelewa kilichotokea jana kwa Yonesi kupigana na Hamza.
Wafanyakazi wengi walikuwa wakiamini lazima Yonesi na Hamza wataishia kuwa wapenzi na hicho ndio ambacho walikuwa wakitamani kuona.
Hamza marra baada ya kuchukua chakula chake hakuhaingika kutafuta sehemu ya kukaa kama jana , aliangalia tu kushoto na alimuona Yonesi akiwa peke yake na alipiga hatua na kwenda kukaa pembeni yake.
“Habari za mchana Kapteni?”Aliongea Hamza
ITAENDEEA-NITAFUTE WATSAPP 0687151346