Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SEHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 28.
Hamza ilibidi amuelezee Regina kwanini anataka aachane nae , alimwambia kwamba kama wataendeea kuwa pamoja kuna watu lazima wataendelea kufika kumtafuta na kusababisha matatizo , hivyo watu wa karibu yake watakuwa hatarini , hivyo hakutaka kumuingiza yeye katika matatizo yake.
“Usiwe na wasiwasi kabisa, nitalipa malipo ya kuvunja mkataba , pia haina haja ya kunilipa kupitia kampuni , nitaondoka bila kuchukua hela”Aliongea Hamza.
Regina macho yake yalichanua , hakujua kwanini lakini licha ya uhusiano wao kuwa wa kimkataba ila baada ya Hamza kusema anataka waachane kila mtu ajue mambo yake , alijihisi kukosewa , kutokubali na kujisikia vibaya.
“Kama ukiondoka sasa hivi , nitadili vipi na familia ya Mzee Benjamini , nitaenda kuwaambia nini wazazi wangu , unataka kuondoka halafu uniachie matatizo, huo ni ubinafsi usingekubali tokea mwanzo kama ungeondoka unapojisikia”Aliongea Regina huku akiwa amebadilika kabisa.
“Regina nilijua tu utakasirika , lakini jua ukiwa na mimi utajiingiza kwenye matatizo , hivyo ni kheri mimi kuondoka kuliko kuhatarisha usalama wako”
“Nimekasirika ndio lakini siogopi hatari yoyote itakayonijia kwanini unanisemea?”
“Lakini hizi ni hatari za kujitakia hazikuhusu kabisa , wewe ni wa nje tu , hivyo haina haja ya kujiingiza kwenye matatizo yangu”
“Wa nje? , wewe si ndio wa nje?”
“Unamaanisha nini?”
“Sikukuambia chochote kuhusu James wakati ule unasaini mkataba lakini pia wazazi wangu , sasa kwasababu yangu unachukiwa na James na familia yake na wazazi wangu hawakupendi pia, katika hili hata wewe ni wa nje tu na halikuhusu lakini mimi ndio nimekuingiza , kwanini hukuondoka wakati ule na kuamua kuondoka sasa baada ya matatizo yako?”Aliuliza Regina na kumfanya Hamza kushangaa , ni kweli hakuwahi fikiria juu ya hilo.
“Ngoja nikuambie sababu , hukuondoka kwasababu huwaogopi, wewe ni muongo, wasifu wako ni feki , kila kitu ni feki , pengine hata jina lako sio Hamza lakini kitu kimoja ambacho nina uhakika nacho , hukuwahi kuwahofia James na familia yake kama wangeamua kukushambulia , si ndio”Aliongea Regina na Hamza alishindwa kujibu chochote.
“Sasa hivi ndio umeniingiza kwenye matatizo ndio unataka tuvunje mkataba , unanichukuliaje? , unaniona dhaifu sio??, unadhani mimi sio mvumilivu?”
Hamza na Regina waliishia kuangaliana tu kama mambwa wanaobwekeana, lakini kwa upande wake baada ya kuona namna mwanamke huyo alivyokasirika na muonekano wa kukosewa Hamza alishindwa kujizuia na kutabasamu.
“Sio kwamba nakuona dhaifu , niwe tu mkweli mimi sio mtu wa kufikiria mbali kama wewe , ninachotaka ni kutokukuingiza kwenye matatizo tu”
“Kwahio unadhani ukiondoka na matatizo yangu ndio yataisha?,unadhani tokea niwe CEO nishawahi kuwa salama , hivi unadhani kwanini nimeweka bajeti kubwa kwa ajili ya kitengo cha ulinzi wa kampuni na hata kumuajili Yonesi kutoka jeshini kwa ajili ya kuwafundisha wenzake?,wewe ni mwanaume lakini matatizo yakitokea unataka kukimbia, Uoga tu ndio unakusumbua?”
Hamza hakudhania Regina angelichukulia hilo swala kwa namna hio , alichokuwa akijaribu kufanya ni kuhakiksiha anabakia kuwa salama.
“Regina nimesema muda gani nakimbia matatizo , umenielewa vibaya , kama kweli unaniona mimi muoga unadhani ningekuja kukuokoa?”
“Kama wewe sio muoga na mimi kama mwanamke siogopi kitu , kinachokugopesha nini mpaka unataka kunikimbia?”Aliuliza Regina huku akimwangalia Hamza machoni.
“Ungejua ninachojaribu kukuepushia ni kheri usingejibishana na mimi na kukubali mara moja”Aliwaza Hamza katika kichwa chake lakini hakutaka kuongea waziwazi na aliishia kutoa tabasamu kwa namna Regina alivyoonyesha ujasiri mbele yake.
“Kwasababu wewe ndio umesema hivyo basi sitofanya kama nilivyosema”Mara baada ya mrembo huyo kusikia hivyo alivuta pumzi.
“Unadhani unaweza kuja kwenye maisha yangu na kuondoka , unadhani unaweza kuwa msaidizi wangu na Boyfriend feki unavyojisikia , hata kama unataka kuvunja mkataba mimi ndio mhusika mkuu lazima nikubali maana nimekuajiri”
“Ni kweli wewe ndio mwenye kauli ya mwisho , lakini tuishie hapa , sitotaka kukuelezea zaidi kuhusu mimi , isitoshe uhusiano wetu ni wa kikazi zaidi hivyo sio wajibu wangu”Aliongea Hamza.
“Okey , nitakuacha kwa leo , lakini nitajua tu iwe ni mapema au kwa kuchelewa”
Mpaka hatua hio Regina ashaona kabisa Hamza alikuwa akificha vitu vingi sana kuhusu yeye , kitu ambacho kilimfanya yeye mwenyewe kuvutiwa kujua zaidi.
Asichokijua Regina ni kwamba baada ya hapo hatokuwa wa kawaida tena, hisia zake mbele ya Hamza ndio zilianza kubadilika mara moja kuanzia siku hio.
Hamza na yeye aliishia kumwangalia mwanamke huyo , alikuwa mzuri mnno wa kuvutia kwa macho , licha ya madhaifu machache lakini upande wake mzuri ulikuwa umeyafunika.
Ghafla tu Hamza alijiktua akiangua kicheko , jambo ambalo lilimshangaza Regina.
“Unacheka nini?”
“Nimekumbuka ulivyosema hata jina langu linaweza kuwa feki , Mimi naitwa Hamza Mzee ndio jina langu halisi”Mara baada ya kusikia hivyo alijikuta akiona aibu za kike.
“Wewe ni mjinga , nani kasema anataka kujua jina lako halisi , hata kama umedanganya tutaenda na hili hili la Hamza”
“Vizuri , kwasababu mimi ni mfanyakazi tu huna haja ya kuwa na wasiwasi na mimi sana haha…”
“Hebu harakisha uko , chakula kinapoa kwa kuongea muda wote pumba”
“Sawa sawa , nitamaliza , ni bahati tu nimebakisha miezi mitatu pekee , vinginevyo nani anaweza kukuvumilia..”
“Unasemaje?”
“Ah .. sijasema kitu”
“Wewe, tutaona , mshahara wako lazima ni ukate”
“Haiwezekani Boss , nimefanya kosa gani”
******
Swala la Regina kutekwa liliisha kimya kimya , huku likijulikana kati ya Hamza na Regina mwenyewe , upande wa Regina hakuwa mdhaifu dhaifu hivyo halikumuathiri , ilikuwa ni kama kitu cha kawaida tu kumtokea.
Kils siku kama kawaida Regina alikuwa na utaratibu wa kutumia Makeup kwa mbaali na kufanya uso wake ambao tayari ni wa kirembo kuzidi kuvutia .
Kila nguo Regina aliovaa ilikuwa ikimpendeza , iwe ni rangi nyeusi , ya kijani au nyekundu, nguo nyingi za kike ambazo zilimfiti ni kama ametengenezewa yeye tu.
Hamza alijiuliza inakuwaje mwanamke akawa mrembo hivi , siku za nyuma wanawake aliowaona kama kipozeo tu kwa mwanaume , hakuwahi kupenda hapo kabla wala kumhusudu mwanamke , alijua kila mwanamke mzuri ni mali ya wenye nazo kwa ajili ya kutuliza akili zao.
Hamza alitamani Regina awe anakaa siti ya mbele lakini alipendelea kukaa nyuma na kushindwa kuuthaminisha vizuri urembo wake , kitu ambacho kilimshangaza zaidi jana walikuwa wakiongea na kucheka wakati wakurudi , lakini asubuhi hio Regina alikuwa kauzu isivyokuwa kawaida.
Hali hio ilimfanya Hamza kuona labda kuna kosa amefanya asubuhi na kumsababishia mwanamke huyo kukasirika..
“Hakikisha kesho hukai mbali na mimi?”Aliongea Regina aliekuwa siti ya nyuma ya gari.
“Kesho si jumamosi wikiendi , unakuja kazini pia?”
“Kuna mgeni wa muhimu tutakutana nae kesho muda wowote , ni Mfaransa na wewe unakijua vizuri kifaransa , hivyo itakuwa vizuri ukiwa na mimi kama msaidizi”
“Okey Boss”
Tokea asubuhi itimie ndio mara ya kwanza Regina ananyanyua mdomo na kumuongelesha.
“Hivi Regina , kuna kitu chochote ambacho nimefanya kimekukasirisha?”Aliuliza Hamza.
“Kwanini?”
“Kwasababu umekuwa kauzu sana”
“Wasiwasi wako tu , au unataka nikuchekee chekee muda wote”
“Sio hivyo , nakosa tu amani ulivyo mkimya”Aliongea na Regina aliishia kuonyesha muonekano wa kimapozi bila kubadili muonekano.
“Otea..”Aliongea
“Naoteaje sasa?”
“Basi tafuta majibu”Mara baada ya kuongea hivyo hakuonekana kujisumbua tena na Hamza.
Hamza aliona bora hata asingeuliza maana amejitia mawazo tu , hajafannya chochote lakini anaambiwa atafute majibu.
Mara baada ya kufika kazini Hamza alifanya kazi kama kawaida , hakuwa akizembea , ijapokuwa kila akifanya kazi alitafuta muda wakupumzisha akili yake kwa kufanya vitu anavyopenda mtandoani lakini kazi alizopatiwa alizifanya vizuri tu.
Muda wa mchana kama kawaida alishuka mpaka mgahawani na kuchukua chakula chake na kisha mara baada ya kumuona Yonesi akiwa peke yake kwenye meza alienda kukaa.
Hamza hakuwa muongeaji mara baada ya kukaa katika maeza ya Yonesi aliendelea kujiweka bize na chakula hata kwa Yonesi ni kama vile alikuwa ashazoea tu na hakumfukuza Hamza , lakini alikuwa na wasiwasi kutokana na utulivu wa Hamza , alimzoea kuwa roporopo.
“Unafikiria nini?”.
“Unaniuliza mimi?”
“Kuna mtu mwingine hapa?”
“Umeanza lini kunijali?”
“Nani kasema anakujali , nimekuuliza swali tu kama hutaki kujibu acha, wasiwasi wangu muhuni kama wewe kuna kitu lazima unakipnga kichwani”
“Kapteni wewe na Regina mmefahamiana kwa muda gani?”
“Muda mrefu tu , kwanini unauliza?”
“Regina ni mtu wa kubadilika badilika kuna muda unaweza kuongea nae vizuri lakini dakika chache zijazo anakuwa mtu mwingine kabisa , nimejairbu kuwaza labda nimemkosea mahali lakini nimeshindwa kukumbuka kabisa”Yonesi baada ya kusikia kauli ya Hamza alijikuta akishangaa lakini muonekano wake ulibadilika na kuwa ule wa kejeli.
“Unafikiria sana vitu visivyo na maana , Mkurugenzi akuongeleshe wewe ni nani , hayo ni mawazo yako tu ndio yanakusumbua”
“Kama ni hivyo basi nyie wanawake hamueleweki”
Hamza licha ya kwamba amepitia maisha flani ambayo mtu wa kawaida hawezi kupitia na hata kuwa na uzoefu wa hali ya juu lakini likija swala la kumuelewa mwanamke ilikuwa ngumu mmno kwake.
Baada ya lunch, Hamza alichukua matunda kama kawaida na kwenda nayo juu, wakati anatoka kwenye lift aliweza kukutana na Eliza ambae alionekana alikuwa akitoka ofisini kwa Regina.
“Eliza umerudi!?”Aliuliza Hamza huku wakionyesha furaha ya kumuona mrembo huyo.
“Huruhusiwi kuonyesha unanijua sana tukiwa kazini”Aliongea Eliza kikauzu.
“Oh , hakuna shida , halafu vipi mbona upo hivyo , hujafurahi kuniona?”Aliuliza Hamza mara baada ya Eliza kuonekana hataki kuongea nae.
“Nina kazi kibao, tutaonana”Aliongea Eliza na kisha aliingia kwenye lift akimuacha Hamza akimwangalia mpaka mlango ulipojifunga.
Hamza alijikuta akihema kwa nguvu na kujiuliza kwanini leo ni kama vile kila mwanamke hakuwa akitaka kumuongelesha.
Aliamua kuingia zake kwa Mkurugenzi ili kukabidhi yale matunda , Regina alikuwa bize kama kawaida yake akiwa na furushi la makatarasi juu ya meza yake.
“Mkurugenzi , kula matunda kidogo usifanye kazi na njaa”
“Sawa , unaweza kuyaweka hapo”Aliongea Regina bila hata ya kuinua macho.
Kwa namna Regina alivyokuwa makini Hamza alikuwa na shauku ya kutaka kujua mwanamke huyo ni kitu gani anafanyia kazi , hivyo alisogea karibu na upande wa meza yake kuchungulia.
“Hey , usichungulie, toka ofisini kwangu”Aliongea kikauzu na kumfanya Hamza kulazimisha tabasamu na kimya kimya akatoka huku akimwemwesa midomo na kujiambia wanawake wa aina hii ni ngumu sana kuendana nao vizuri hata kama una nia nzuri kwao.
Hamza mara baada ya kuingia ofisini kwake alianza kumfikiria Eliza na muonnekano wake wa dakika kadhaa zilizopita , baada ya kufikiria alihisi pengine Eliza na Regina waliongea kuhusu yeye ndio maana alionekana kana kwamba alikuwa akimkwepa.
Hamza mara baada ya kushikwa na wazo hilo palepale , hakutaka kusubiri alinyanyuka na kuelekea katika ofisi ya Eliza ili kujua kwanini mrembo huyo ni kama hana furaha kumuona.
Dakika chche tu alikuwa ameshafika katika idara ya mauzo(Sales department) , Eliza alikuwa akiongoza idara hio kama meneja mara baada ya kupandishwa cheo kutoka kuwa msaidizi wa Regina.
Baada ya kufika katika idara hio alikaribishwa , alijulikana tayari kama msadizi wa Regina hivyo mara baada ya kutaja shida yake ni kuonana na Eliza alielekezwa katika ofisi yake.
“Come in” Sauti kutoka ndani iiliitikia baada ya Hamza kugonga mlango na kumfanya aingie.
Eliza ambae alikuwa akiangalia tarakishi alishangaa mara baada ya kuona ni Hamza.
“Kwanini upo hapa?”Aliuliza na Hamza alitembea na kwenda kuweka mikono yake yote juu ya meza huku akimwangalia mrembo huyo kwenye macho.
“Eliza je kuna kitu chochote unahisi kunishuku?”
“Kukushuku , unamaanisha nini?”Aliuliza Eliza huku akiwa na muonekano wa kushangaa na kuchanganyikiwa kwa wakati mmoja.
“Unaonekana kutokuwa furaha hata pale uliponiona , au kuna mtu alisema chochote kunihusu mimi?”
Eliza mara baada ya kujua kile kilichomleta Hamza hapo aliishia kuweka mikono yake juu ya meza na kupitisha vidole vyake na kuishia kutoa tabasamu.
“Hakuna”
“Kama ni hivyo kwanini unaonyesha kutokuwa furaha baada ya kuniona?”
“Otea”
Hamza mara baada ya kusikia kauli hio hakujua alie au acheke , maana hata Regina alimwambia hivyo hivyo.
“Eliza hebu acha kunitesa na kujitesa , naoteaje sasa kitu nisichokijua , hatujaongea zaidi ya wiki sasa , mimi nitajua ni wapi nimekukosea?”
“Kwahio unakiri kabisa hatujaongea wiki nzima , tuseme hukuwa na salio kunipigia , vipi hata meseji umeshindwa kunitumia?”Hamza sasa alijua wapi kosa lake lilipo.
“Eliza nisamahe , mimi sio mzoefu sana likija swala la mahusiano ndio maana sikupiga simu”
“Nani aamini maneno yako , sipo kichwani mwako ndio maana, usingenikiss kabisa kama unashindwa kujua namna ya kuwajibika”Eliza alitaka kusema umenikisi kitaalamu vile halafu unasema huna uzoefu ila hakutaka kuongea hivyo na kubadilisha maneno.
“Eliza kukukiss na kukupigia simu ni vitu viwili tofauti , nilikosa tu sababu ya kukupigia ndio maana , ila nilikuwa nikikuwazia”
“Kwahio unapiga ukiwa na sababu ya kunipigia , hebu toka ofisini kwangu acha kunipotezea muda nina vitu vya kufanya”Aliongea huku akionyesha kukasirika akiwa amesimama.
Hamza aliona kuendelea kuongea nae akiwa amekasirika hivyo haina maana tena , alimsogelea Eliza kwa haraka na kushika kiuno chake na kisha akamkiss na kumfanya Eliza kutoa macho maana hakutegemea kile kitendo , Eliza aliishia kushika mbavu za Hamza na kuziminya , alikuwa hataki lakini kujiondoa alishindwa.
Baada ya dakika moja Hamza alimuachia , alijua akiendelea wanaweza kuingia katika hatua isiofaa katika mazingira hayo ya kazini.
“Nakuahidi kuanzia sasa nitakuwa nakupigia bila hata ya sababu”Aliongea Hamza huku akimwangalia Eliza ambae ameshikwa na aibu lakini kwa namna moja alijisikia vizuri mno na furaha.
“Nimekusikia ,ushamaliza kazi zako , niache nimaliza na zangu”
“Jumapili utakuwa na muda , unaonaje tukitoka out hata kwenda kupunga upepo baharini na kula mihogo?”
Eliza alifikiria kwa muda na kweli aliona hana ratiba yoyote Wikiend hivyo aliishia kutingisha kichwa kukubali.
Muda huo huo mlango wa ofisi ya Eliza uligongwa na sauti ya Mirium ilisikika.
“Meneja , hali sio nzuri huku , kuna tukio kubwa limetokea”.Eliza alijiweka sawa huku akiondoa hali ya aibu usoni na kurudia ile ya kazini na kisha alisogelea mlango na kuufungua.
“Nini tatizo?”
Mirium mara baada ya kuona na Hamza yupo ndani ya ofisi aliishia kutingisha kichwa kumpa ishara ya salamu.
“Dakika chache zilizopita kupitia taarifa ya habari Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Omega ametangaza kukubali kutia saini kwa niaba ya kampuni yake kuuzwa kwenda Zena Corporation”
Eliza macho yake yalisinyaa na alitoka moja kwa moja na kwenda katika ofisi kubwa pana iliokuwa na Tarakishi nyingi za wafanyakazi wa idara ya mauzo.
Muda huo wafanyakazi wa kampiuni nzima walikuwa wakiangalia taarifa hio ya bahari.
Zena Corporation ilikuwa chini ya familia ya mzee Benjamini baba yake na James.
Kila mtu alionekana kuwalaani Zena kwa kukosa aibu na kuingilia dili lao la kuiunua kampuni ya Omega.
Eliza aliongoza wafanyakazi wenzake katika idara ya mauzo kujadili kile kilichokuwa kimetokea.
Upande wa Hamza alikuwa akijua dili hilo la kampuni ya Dosam kutaka kuinunua Omega hivo kuona taarifa hio alijua na Regina atakuwa katika hali mbaya, ukweli hakujua kama Regina atakuwa katika hali gani.
“Kama sio pingamizi kutoka kwa wakurugenzi wasaidizi , Zena wasingeweza kufanikiwa”
“Ndio , Mkurugenzi alikuwa sahihi pia , kama sio hivyo mnadhani Zena wangefikiria kuinunua Omega?”
“Mimi nashindwa kuelewa , hawa wakurugenzi ni wazee lakini bado wanashindwa kuelewa soko linakoelekea , kwanini wanapinga ustawi wa kampuni”
Wafanyakazi walikuwa wakiongea wao kwa wao huku wakimuonea huruma bosi wao kwa namna ambavyo wakurugenzi wenzake wamemsaliti mpaka kufanikisha Zena kuinunua Omega.
Mipango ya Regina katika kupanua kampuni ilikuwa wazi kwa kila mmoja , alitaka kununua kampuni ya maswala ya Tehama ya Omega kwa ajili ya kuingia katika biashara ya Akili Mnemba(Artificial intelligence), alijua ili kampuni yake iweze kupanuka zaidi alihitaji kitu ambacho kinaendana na wakati uliopo na ujao , kwa Regina aliona mfumo wa akili bandia utakuwa ndio kesho ijayo.
“Meneja ni nini tunapaswa kufanya , Omega ndio hio tushaikosa , unadhani mauzo yetu yataendelea kupanda”’Aliuliza Asha na wengine wote.
“Tupo kwenye idara ya mauzo, tunachotakiwa kufanya ni kutimiza wajibu wetu , hili swala lipo chini ya idara ya Trustees , Mikakati na masoko , tunamuamini Mkurugenzi wetu Regina, najua atapata ufumbuzi ,nimeongea vya kutosha sasa , tungieni kazini”Aliongea huku akipiga makofi akitawanya wafanyakazi wote kurudi katika nafasi zao za kazi.
Hamza mara baada ya kuona hilo alijua lazima Regina atakuwa anajisikia vibaya , ilionekana dhahiri kuna mtu ndani ya kampuni alivujisha taarifa.
Muda wote wa mchana wafanyaazi wa juu wa kampuni waliingia ndani ya ofisi ya Afisa mtendaji mkuu wa kampuni mmoja baada ya mwingine , ilikuwa ni kama kampuni yote ilikuwa katika hatari , Hamza aliweza kuona namna ambavyo Regina amechoka wakati wa kuondoka.
Mara baada ya kuingia kwenye lift aliishia kuegamia lift na hakuongea neno , Hamza na yeye hakutaka kumsumbua , ilikuwa ni mara ya kwanza kuona mwanamke huyo akionyesha hali ya kukosa utulivu na kwa namna flani Hamza alimuonea huruma.
Kwa mfanyabiashara kama Regina kwake hela inakuwa sio kipaumbele tena , bali kipaumbele ni malengo ya kampuni kutimia.
Kitendo cha kufika katika maegesho ili kuingia kwenye gari waliweza kuona gali nyeusi aina ya Caddilac ikiwa imeegeshwa.
Mabodigadi wawili wenye miili ya kibaunsa walikuwa wamesimama pande zote za gari wakiwa na miwani za jua huku mlango wa kuingilia katika gari hio ukiwa umefunguliwa na alionekana James ambae alikuwa amevalia shati la mikono mirefu na suruali ya kitambaa pamoja na saa ya dhahabu.
Ukiachana na mabodigadi hao pamoja na James kulikuwa na mtu mwingine mzee hivi , alikuwa amevalia shati refu mfano wa kaunda rangi ya bluu bahari , kitu kimoja ambacho hakikuwa cha kawaida kutoka kwa mzee huyo ni macho yake , yalikuwa yamejaa uovu sio wa kawaida.
Dakika ile le Kaptenni Yonesi pamoja na walinzi walitokea mbio mbio
“Mkurugenzi , samahani tumeshindwa kuwazuia ndani ya muda”Aliongea Yonesi.
Regina macho yake yalikuwa yamejaa ukauzu na alionyesha kila ishara ya kuwa na hasira , mara baada ya kumwangalia James kwa sekunde alitembea kulisogelea gari lake.
Lakini James alitabasamu kikejeli na alimkinga Regina kwa mbele na kisha akamwangalia na Hamza aliekuwa nyuma.
“Wewe kumbe bado upo tu , nimesikia umekuwa msaidizi , hio nafasi inakufaa sana kwenye maisha ya Regina”Aliongea.
Hamza alimwelewa alichokuwa akimaanisha , hakutaka kukubali yeye na Regina ni wapenzi
Regina upande wake hakutaka uhusiano wake kutambulika kwa walinzi hivyo alimwambia James ampishe apite.
“Regina achana na ukauzu wako , najua haupo kwenye mudi leo lakini hayo ni maswala ya kibiashara, maswala yetu binafsi hayawezi kuathirika”
“Hakuna maswala binafsi kati yangu na wewe”
“Kinachokukasirisha ni kuikosa Omega, wasiwasi wa nini , mimi na wewe tukishaoana familia yenu na yetu itaungana , nimeandaa mahali tayari ambayo familia yako itaipenda”
“James acha kwenda mbali , upo ndani ya maegesho ya kampuni yetu , Mkurugenzi anataka umpishe, sijui unanisikia?”
“Nisipompisha utanifanya nini wewe Mal**ya”
“Unanitukana wewe mwanaharamu”
Yonesi hakutaka kujizuia tena , hakupenda matusi na aliona amshikishe adabu lakini Regina alimzuia.
“Yonesi punguza hasira”
“Mkurugenzi .. amenitukana umemsikia..”Aliongea lakini aling’ata meno yake kwa hasira na kutulia.
“James unachotaka kutoka kwangu ni nini mpaka unatoa matusi hapa?”Aliuliza Regina.
“Sitaki chochote , kwanini nitake kitu kutoka kwa mwanamke ninaempenda kama wewe, nataka ukubali kutoka na mimi usiku kwa ajili ya chakula”
“Sijisikii vizuri”
“Kama hujisikii vizuri nitakupeleka hospitalini”Regina aliishia kumwangalia kwa macho ya hasira , hakupenda uking’ag’anizi wa James hata kidogo.
“Regina unatakiwa kujua tayari umeshindwa, kama ukiendelea kuhangaika kama hivi , hali itakuwa mbaya zaidi kwako na kwa watu wanaokuzunguka , kama una akili kubali kuolewa na mimi na tuishi maisha ya furaha , nakuhakikisha hototeseka”
Mara baada ya kuongea hivyo alinyoosha mkono akitaka kumshika Regina kidevu.
Yonesi mara baada ya kuona tukio hilo alimkinga Regina na mwili wake.
“Acha ukichaa wako , huruhusiwi kumsogelea Mkurugenzi”
“Fu**ck , wanaumee, hebu muondoen huyu ch*ko”’
“Yes sir”
Mabodigadi wawili waliovalia suti nyeusi walisogea mbele kwa ajili ya kumtoa Yonesi.
Walinzi waliofika na Yonesi , mara baada ya kuona kapteni wao anasogelewa na wao walisogea na kuwakinga wale mabodigadi.
Mabodigadi wa upande wa kampuni ya Dosam walikuwa wanne na walishindana na mabodigadi wawili aliofika nao James, walikuwa wengi na walikuwa maveterani wa jeshi hivyo ilikuwa faida kwao.
Yonesi mara baada ya kuona maadui zake wanazidiwa aliruka na teke na kumpiga moja ya bodigadi na akaenda mzima mzima chini na palepale wale wengine walimdhibiti yule mmoja.
Regina mara baada ya kuona walinzi wake wameweza kufanikiwa kushinda alivuta pumzi ya ahueni.
Lakini James hakuwa na wasiwasi wowote na aligeuza shingo yake na kumwangalia yule mzee.
“Master Konki huyu mwanamke sio wa kawaida , hata kama ukimshambulia haiwezi kuonekana unamnyanyasa maana ni mwanajeshi”Aliongea James.
Yule Mzee alieitwa Master Konki alimwangalia Yonesi kwa macho ya kumchunguza na aliishia kwenye kifua chake akithaminisha urembo wa mwanamke huyo.
“Mwanamke mrembo kama huyu lakini anataka kushindana nguvu na wanaume , hebu ngoja nimfundishe adabu kidogo aanze kufikiria namna ya kumhudumia mwanaume”Aliongea hukuwa akiwa na tabasamu la kifedhuli.
Yonesi mara baada ya kuona mzee huyo anamsogelea uso wake ulizidi kuwa siriasi , alijua kitendo cha James kuja hapo akiwa anajiamini akiongozana na mwanaume huyo basi lazima atakuwa na uwezo wa juu.
Hamza palepale alipitisha macho yake ya ki uchunguzi kwenye mwiali wa mzee huyo na aliweza kuona kitu kilichomfanya kukunja sura na kumuonea huruma Yonesi matatizo anayojitafutia
“Nina wasiwasi naweza nimshindwe huyu mzee”Aliwaza Yonesi kwa hofu.
“Kapteni huyu mwanaume amezeeka lakini bado anaonekana kuwa na tamaa , nipe nafasi nimfundishe adabu mimi”Aliongea moja ya mlinzi wa kampuni.
“Sogea mbali , mimi ndio kiongozi wewe ni msaidizi tu nitamshikisha adabu mimi”Aliongea Yonesi kwa kujigamba.
“Kapteni kuwa tu makini , mimi nitakushangilia ukishinda”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Huna haja ya kuongea”Alijibu.
“James nadhani ushanipa ruhusa ya kumkamata huyu mwanamke na kuondoka nae”
“Usiwe na wasiwasi Master Konki , mimi shida yangu ni mchumba wangu Regina , huyo mwanamke unaweza kumfanya chochote ukishamshikisha adabu, nakuhakikishia hivi , hakuna kitengo cha usalama cha aina yoyote ndani ya taifa hili kitakuuliza”
“Vizuri sana kijana , nimekaa mafunzoni kwa muda mrefu bila kuonja nyama tatu , kwa urembo wa huyu binti atakidhi kabisa matamanio yangu”Aliongea Konki.
“Na uzee wote huo lakini unaongea bila busara , usamehewe bure , isitoshe mpaka kuja na James hapa inaonyesha ni kwa namna gani huna akili”Aliongea Yonesi kwa hasira.
Dakika hio hio Yonesi aliamua kukaa mkao wa kijeshi , huku akimwangalia Mzee Konki na macho ya tahadhari.
“Sogea mrembo nione ni kipi una cha kunishangaza”
“Umeomba mwenyewe usije kunilaumu”Aliongea Yonesi na palepale aliinua mguu wake na kudhamiria kumpiga yule mzee lakini kabla hata hajamfikia Konki alikuwa ashainua mkono wake na kuzuia lile teke huku vidole vyake vitatu vikitengerneza umbo kama kucha za Tai na kwa ustadi wa hali ya juu alimchoma na vidole vile eneo la mguuni.
“Arghhhhh..”
Yonesi alijikuta akipiga ukulele wa maumivu na bila ya kupenda alirudi nyuma huku akisikiliza maumivu , hakuamini vidole vitatu tu vinaweza kumletea maumivu makali ya namna hio.
“Mbinu ya kimapigano ya kucha za Tai”Aliongea huku akiwa na mshituko, Yonesi hakutarajia mzee kuwa na uwezo huo , kwa kawaida Yonesi alikuwa mzoefu likija swala la mbinu za kimapigano , wakati alipokuwa jeshini alishahudhuria kozi ya kimapigano katika taifa la Thailland na China.
Unachopaswa kujua likija swala la mapigano kama vile Kung fu , unachoona mtaani au kwenye filamu mara nyingi ni kwa ajili ya maoneysho tu lakini likija yale mapigano halisi , mbinu zake ni ngumu sana kuona zikitumika mfano wake ni kama mbinu ya hio ya vidole vya Tai, ni mbinu ambayo anaejifunza anafundishwa kuua siku zote na mara nyingi unamlenga mtu katika maeneo dhaifu ya mwili.
Licha ya Mzee Konki kuonekana mzee lakini spidi yake haikuwa ndogo na nguvu ya vidole pia haikuwa haba mpaka kufanikiwa kumsabishia Yonesi maumivu makali.
Mzee Konki hakuacha kushambulia , alizidi kumsogelea Yonesi huku akiwa na macho ya uchu, kama sio uwezo wake wa kukwepa pengine vidole vingeweza kumtoboa eneo la kifuani.
Regina ambae alikuwa akiangalia mpambano huo aliishia kukunja sura , hakuamini James ameenda mbali mpaka kukodi mtu wa aina hio.
“Mzee Konki usiwe sana siriasi , nataka umshikishe tu adabu nisije onekana mtu mbaya mbele ya mchumba wangu”Aliongea James.
“Msichana nimependa sana hio miba hapo kifuani kwako , kubali tuondoke pamoja kuliko kuendelea kuwa mlinzi”Aliongea Mzee Konki.
“Kwenye ndoto zako”Aliongea Yoinesi na kuzunguka na teke akimlenga kumpiga Konki kwenye shingo lakini mguu wake ulishikwa.
“Haipendezi kwa mrembo kama wewe , ila ngoja tu nikuvunje mguu mmoja , tuone kama utaendelea kuleta ukinzani hehe..”
Aliongea Master Konki huku akicheka na palepale aliweka vidole vyake katika mkao wa kucha za Tai ili kumponda nazo Yonesi kwenye mguu.
Dakika ambayo Yonesi anawaza anakwenda kuvunjwa mguu wake na kuishia kufumba macho alikuja kugundua hakuna kilichomtokea.
“Hamza?!”
Yonesi alimkodolea macho Hamza , bila hata ya kujua Hamza alikuwa ashatokea pembeni yake na kushika mkono wa Mzee Konki.
Mzee Konki alikunja sura na kujaribu kusogeza mkono wake lakini aligundua hakuweza hata kujitoa na aliishia kuachia mguu wa Yonesi na mkono mwingine aligeuza kuwa vidole vya Tai na kujaribu kumshambulia Hamza kwenye macho.
Lakini ile mkono unamkaribia Hamza na yeye alikuwa ashatengeneza staili ileile ya vidole vya Tai na Mzee Konki mara baada ya kwenda kugusana na vya Hamza alijikuta akitamani kutoa ukulele kwa maumivu yaliozidi mpaka vidole vikashikwa na ganzi, kidogo tu vidole vyake vivunjike.
Hamza mara baada ya pale alimsukuma nyuma yule mzee na kumfanya ajikokote asidondoke.
“Wewe Mzee , Kapteni Yonesi ni kama mjukuu wako lakini huoni aibu unataka kumvunja mguu”Aliongea
Mzee Konki alibakia katika mshituko wa ajabu huku akimwangalia Hamza , hata kwa Regina na Yonesi walikuwa wamepatwa na mshituko , James muonekano wake ulikuwa ni ule wa kukakamaa.
“Unaijua sanaa ya ndole za Tai pia!!?”Aliuliza Mzee Konki huku akiwa na mshituko kwani Hamza alitumia mbinu yake.
“Kwani hii mbinu ina ugumu gani kutumia?”
“Unaongea ujinga , hii ni mbinu ya sanaa ya kucha za Tai , ngoja nikuonjeshe utamu wake”
Mzee Konki aliona ni kama udhalilishaji hivyo kwa hasira aliruka hewani kama mshale huku akitanguliza mkono wake wenye staili ya kucha za Tai kumlenga Hamza katika shingo yake.
Hamza alivyosimama kizembe ni kama vile amekosa cha kufanya na anasubiria shambulio hilo , lakini ile Mzee huyo anamkaribia na yeye alinyoosha mkono wake katika staili ya kucha za Tai na kumzuia kwa kubananisha vidole vyake na vya yule Mzee.
Baada ya kuvibananisha katika vidole vyake alizungusha kwa nguvu na kwa hasira kali.
“Arghhhhhhhhh..”
Mzee Konki alitoa ukulele wa aina yake , mifupa ya vidole vyake ilisikika ikitoa mlio wa kuvunjika kutokana na nguvu aliotumia Hamza na mara baada ya kutua chini aliangalia mkono wake akiwa katika maumivu makali huku akimwangalia Hamza katika mshangao.
“Wewe mtoto .. umejifunzia wapi hii mbinu!!?”
Mzee Konki alikuwa akiamini kwenye taifa la Tanzania hakuna mtu ambae anaweza kumshinda likija swala la mapigano bila ya siraha , hasa katika kutumia mbinu yake hio ya Kucha za Tai.
Alikuwa amefika bongo na mpango wake ni kwenda kushindana na wanajeshi wote ambao wanajita makomandoo , alikuwa akitaka kujihakikishia yupo mwenyewe mwenye mafunzo makali ya kimapigano, lakini kwa bahati mbaya anakutana na Hamza kabla hata ndoto yake haijatimia na anashikishwa adabu , kitu cha kumshangaza zaidi aliemshikisha adabu alikuwa ni kijana mdogo sana kuliko yeye ambae amejifunza kwa miaka mingi kuimaster hio mbinu.
Regina ,Yonesi na wengine pia walikuwa wanamwangalia Hamza kwa maswali , walishaona Yonesi hakuwa na uwezo wa kumzidi huyo mzee licha ya kupitia kitengo cha special forces jeshini.
James mara baada ya kuona tukio lile aliishia kupiga hatua moja kurudi nyuma , alikumbuka baba yake alichomwambia kuna uwezekano huyo Hamza asiwe mwepesi na sasa ndio anaamini.
“Mtu alienifundisha ni maarufu sana dunia nzima , anajulikana kila kona ya dunia kutumia hii mbinu, nikikuambia jina lake unaweza kupatwa na mshituko”Aliongea Hamza.





SEHEMU YA 29.
“Acha makusudi ya kujikweza , sheria namba moja katika ulimwengu wa mapigano ni kujitambulisha wewe na shirka lako , mimi ni mwanafunzi kutoka Shirka ya Tai Mweusi, jitambulishe Shirka lako na wewe kama ujasiri huo unao , udhalilishaji wa leo utalipwa mara mia zaidi”
“Nimefundishwa na Master Kato Hawk ushawahi kumsikia?”Aliuliza Hamza
“Kato Hawk , mbona sijawahi kumsikia ni raia wa wapi?”Aliuliza Mzee Konki akionyesha kutomjua.
James mara baada ya kuona Mzee Konki anaanza kuuliza maswali ya kipuuzi alitamani kwenda na kumpiga , ila uwezo huo hakuwa nao.
James alikuwa akimjua Kato Hawk, mtu yote mpenda filamu za angemfahamu Kato Hawk.
“Ushawahi kumsikia mtu anaeitwa Kato Hawk huko jeshini?.”Aliuliza Regina ki udadisi swali hilo likienda kwa Yonesi.
Yonesi na wenzake walikuwa wakimjua ndio lakini hawakutaka kumwelezea Regina na walishangaa kwanini hamjui.
“Taja jina la Shirka ulilojifunzia, sijawahi kusikia jina la mtu uliemtaja?”
“Kama hujawahi kumsikia mtu maarufu kama huyo , basi sioni haja ya kukuambia nenda kaulize”Aliongea Hamza akiwa na muonekano wa kejeli.
Mzee Konki alikuwa na hasira mno , kama sio kuumia mkono wake angejaribu kuzipiga tena na Hamza , alijua kuvunjika kwa vidole vyake hawezi kupona ndani ya siku kadhaa.
“James , turudi kwa leo ila naahidi , nisipokuja kulipiza hili labda sio mimi Konki Master”Aliongea Konki kwa hasira , hakuamini miaka yake yote ya kujifunza mapigano na kutia mguu Tanzania anakuja kukutana na udhalilishaji.
James mara baada ya kusikia hivyo alifurahi , alijua lazima mzee huyo atakuja tu kulipiza kisasi.
James ashaona kabisa Hamza sio saizi yake hivyo aliondoka kimya kimya
Regina alimwangalia Hamza kwa macho ya kiulizo na alijiambia ndio maana aliweza kumuokoa kiwepesi tu, hali hio ilimfanya kukosa hiari ya moyo wake na kujisikia hali isioelezeka.
Wakati wa kurudi nyumbani kulikuwa na foleni kubwa mno hivyo gari ilisogea taratibu taratibu.
“Kwahio Master wako ndio anafahamika kwa jina la Kato Hawk , umefahamiana nae nje ya nchi nini?”Aliuliza Regina.
Swali lile lilimfanya Roma kushituka na kidogo tu akanyage kwenye pedeli tofauti na breki kugonga magari ya mbele yake.
“Regina inamaana hujawahi kusikia hilo jina?”
“Ningekuuliza kama najua , hata Yonesi nimemuuliza ameonekana hajui”
Hamza alijifikiria na kujiambia inakuwaje hawamjui , lakini hata hivyo aliona kwa mwanamke kama Regina ni haki kutokumjua.
“Nilikuwa nikiongea ujinga tu pale , usichukulie siriasi”Aliongea Hamza.
“Kwanini unakuwa hivyo ,unaona aibu kuwa na Master eh?”
“Haha.. nimeongea kumugopesha tu yule usichukulie siriasi”
“Usiponiambia nitatafuta mtandaoni na lazima nitajua tu”Baada ya kuongea hivyo alichukua simu yake na kuingia kwenye mtandao wa google na kuandika jina la Kato Hawk.
Hamza aliishia kutingisha kichwa tu na kujiuliza kwanini huyu mwanamke ana shauku ya kujua siri zake namna hio.
Ndani ya nusu dakika tu , Regina mashavu yake yalikuwa mekundu na aliishia kung’ata lips zake na kuweka simu chini bila kuongea chochote.
Hamza mara baada ya kuona muonekano wa Regina alijua tayari ashaujua ukweli kuhusu Katona alitamani kucheka kicheko kikubwa.
“Hehe, nilikuambia mimi usitafute haya ona sasa?”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Muhuni sana wewe..”Aliongea Regina akiwa na hasira , hakuaminni alikuwa ameuliza swali hilo kwa Yonesi na wenzake , alijihisi kuona aibu
“Nilishakuambia nilikuwa nikiongea ujinga, halafu kingine Kato Hawk hawezi kuwa na vigezo vya kuwa master wangu , uwezo wangu wa mapigano kwa kutumia vidole ni wa juu mno”
“Kimya , endesha gari” Regina hakutaka kumsikiliza tena , alitamani kumsogelea na kumpiga kibao.
“Basi ngoja nikuambie ukweli , kama usiponiamini unaweza kujaribu kutafuta tena”
“Ukiongea ujinga tena nitakata mshahara wako”
“Sawa Madam , kama hutaki kusikia basi nitakaa kimya”Aliongea Hamza huku akitamani kucheka.
****
Upande mwingine wa jiji kulikuwa na kikao kilichojumuisha kundi la watu wenye mafunzo ya kimapigano lifahamikalo kwa jina la Tanzania Martial Art Association.
Kundi hili halikuwa la kihalifu lakini kwa namna moja lilitafsirika kama la kihalifu kutokana na usiri mkubwa wa ajenda zao , unaweza kusikia kuna kundi hili lakini huwezi kujua ni kitu gani wanachokifanhya wakikutana.
Kuna wanaosema kundi hilo hufadhiliwa na Binamu , hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa madai hayo., lakini taarifa ya kuaminika hata baadhi ya wanajeshi wenye vyeo vya ukomandoo jeshini walikuwa ni wanachama na hawakujiunga kwasababu walitaka bali walipambanishwa na wenzao na kukidhi vigezo na kuingia katika umoja huo na kulikuwa na faida kubwa sana ya kimaslahi kwa kila mwanachama wa kundi hilo.
Sasa katika moja ya jumba la kifahari lililopo Tegeta kulikuwa na kundi la watu ambao walikuwa wamevalia mavazi ya suti na walikuwa wamekaa eneo la sebule yenye masofa mengi ya thamani ya juu.
Kwa muonekano wao ilionyesha kabisa hawakuwa watu wadogo katika jamii , mmoja ambae alikuwa katikati ndio kiongozi alifahamika kwa jina la Fanueli Yowe au unaweza muita Kanali Yowe.
Ndio alikuwa ni Komandoo wa jeshi la taifa lakini pia mwanachama wa umoja huo wa sanaa ya mapigano.
Ukiziangalia sura zote zilizokuwa ndani ya eneo hilo usingeamini kama walikuwa na uwezo wa kupigana wa hali ya juu na baadhi yao ni makomandoo wa jeshi.
“Nadhani kila mmoja wenu amesikia , mwanachama wetu mpya Mzee Konki amekutana na mtaalamu wa hali ya juu wakati alipokodiwa na Mzee Benjamini wa kampuni ya Zena?”
“Hii maana yake ni kwamba mpaka sasa hakuna mmoja wetu hapa anaemuweza mtu huyu , maana tunajua fika Mzee Konki ndio mwanachama wetu mpya ambae ametushinda wote kimapigano, hii ni taswira mbaya kwa umoja wetu na maslahi yetu kwa ujumla katika nchi hii, kwa kusema hayo nimeitisha kikao hiki ili kuwauliza mnaonaje hili swala?”
“Kwa mtazamo wangu lazima mtu huyo atakuwa si wa hapa Tanzania na hata kama ni wa Tanzania basi amerudi hivi karibuni na pengine ameajiriwa kulinda kampuni ya Dosam”
“Mimi pia nadhani huyu ndio mtu alieripotiwa kwetu na Amosi , unajua Amosi licha ya kutokuwa na uwezo wa hali ya juu lakini ana macho ya kuona mtu ambae ana uwezo mkubwa , nasikia baada ya hapo Amosi alipokea vitisho kutoka kundi la Chatu aache kabisa kumchokoza yule mwanamke mfadhili wetu anaemtaka”
“Unamaanisha Dina ndio aliingilia , nadhani kadri siku zinavyoenda ndio anasababisha matatizo zaidi”Aliongea mwanaume mwingine aliefahamika kwa jina la Gosu au Mzee Gosu ni mstaafu kutoka polisi.
“Kwanini mnampa bichwa yule msichana ,tunajua wote hapa hatumuwezi lakini hatuwezi kumsujudia pia”
“Mimi nadhani tuachane na swala la Dina , na Mzee Konki mwenyewe atuelezee ni kwa namna gani tutarudisha heshima yetu , wenzetu kutoka nje ya nchi wakisikia kuhusu hili watadharau na hawatukubali kufanya biashara na sisi”
“Nadhani kwanza tumfahamu ki undani ni nani , alitaja Master jina la Master aliemfundisha lakini sikuweza kumfahamu , nadhani kati yetu hapa kwenye huu umoja lazima atakuwa amesikia jina hilo , amesema anaitwa Kato Hawk na ni maarufu sana”
“Eeh!!
“Watu wote walikaa kimya na kufanya hali itulie na kitendo kile kilimfanya Mzee Konki kushangaa.
“Mbona kila mtu amekaa kimya?, au inamaana mnamjua tayari?”
“Mzee Konki nadhani ni kweli umechoka mno , unaonaje ukiingia chumbani kupumzika kwanza”
“Mkuu kwanini nipumzike , hiki kikao si kinanihusu mimi na yule mpuuzi?”
“Mzee Konki acha kututania , yaani unatuambia mcheza filamu za ngono anaejitamba mtandaoni kuwa ni Bruce lee ndio mtaalamu wa mbinu ya kucha za tai.”
“Nini !!, Mcheza filamu za ngono , mnamaanisha nini?”
“Mzee Konki hatukulaumu , wewe ndio mzee hapa hivyo hutumii sana mtandao wa internet hivyo ni rahisi kutomfahamu Kato Hawk, huyo mtoto inaonekana alikudanganya makusudi , haina haja ya kuwa siriasi hivyo”Aliongea Mzee Fanueli Yowe.
Mzee Konki mara baada ya kuagalia sura ya kila mmoja alijikuta akishindwa kuzuia kicheko na muda huo huo watu wote walimuunga mkono na kuanza kucheka na ghafla tu akaacha na wote wakaacha.
“Mpuuzi sana yule mtoto , nitamchuna ngozi”Aliongea kwa hasira , hakuamini haikuwa swala la kupigwa tu lakini vilevile ametajiwa mcheza filamu za utupu kama Master.
Kato Hawk kabla ya kuwa muigizaji wa filamu za kimapigano alifahamika kama Gerald Lupe alikuwa ni mcheza filamu za ngono maarufu sana , kitendo cha kubadilika kutoka ugiizaji wa filamu hizo na kuingia katika sanaa ya mapigano huku akijifananisha na Bruce lee ndio alijibatiza jina la Kato, uhusika wa Bruce lee katika filamu ya Green Hornet(1966) ,hakuna mtu ambae alikuwa akiamini kama Gerarld Lupe au Kato alikuwa akijua mapigano , kilichomfanya kuwa maarufu sana hadi Tanzania ni wakati alipofika nchini katika uigizaji wa filamu huko Ngorongoro na kupewa mapokezi makubwa kwa kigezo cha kutangaza utalii, kilichomfanya pia kuwa maarufu dunia nzima ni namna ambavyo alikuwa akijibrand kwa kutengeneza vidio fupi fupi katika mtandao wa Tiktok na Reel Instagram akionyesha staili mbalimbali za mapigano kama Bruce Lee lakini ikaja kujulikana anafanya Editing huku kile watu walichokuwa wakiona sio uhalisia.
Skendo hio ya kufanya editing ilimfanya kuzomewa na watu wengi mtandaoni huku wakimuonya asitumie utambulisho wa kusema yeye ni Bruce lee aliezaliwa(Recarnated) katika mwili wa Gerald Lupe kwani ni kuchafua hadhi ya kumbukumbu za kishujaa za Bruce lee.
Hivyo ukiingia mtandaoni ukiandika jina la Kato Hawk ni Gerald Lupe mcheza filamu za ngono maarufu anaedai ni Bruce lee aliezaliwa katika mwili wa Gerald Lupe.
“Mzee Konki haina haja ya kuwa na hasira , tunachopaswa kuamini kwasasa ni kwamba huyu mtoto sio wa kawaida , kama ni hivyo unadhani kwanini hajatoa jina la Shirka analotokea.
“Kesho mapema narudi Thailland kwenye Shirka langu , nipo tayari kualika hata wataalamu wa hali ya juu wa kimapigano kwa ajili ya kumshikisha yule mtoto adabu”Aliongea kwa hasira.
Kauli ile iliwafnaya wote waliokuwa hapo ndani kufurahi , walijua fika Mzee Konki kama ninja wa daraja la juu lazima atakuwa anafahamiana na maninja wengine wa uwezo wa juu.
“Mzee Konki tutasubiria kurudi kwako kama ndio hivyo , ruhusa unayo kutoka kwetu”Aliongea Mzee Yowe.
******
Siku iliofuata ilikuwa ni jumamosi , Kwasababu ilikuwa wikiend haikuwa lazima kwenda kazini mapema , hivyo Hamza alitoka nje kwenye uwanja wa bustani ya nyumba na kuanza kuchukua mazoezi.
Mazoezi yake Hamza hayakuwa ya kawaida hata kidogo , hayakuwa ya kukimbia wala ya kuruka ruka.
Ilikuwa ni kama vile anakata mauno kwa jinsi alivyokuwa akifanya , lakini utofauti ulikuwa kwenye viungio vya miguu yake vilikuwa vikipinda katika mjongeo wa aina yake.
Kwa lugha nyepesi ni kama vile anajaribu kucheza cheza tu kupoteza muda , hakukuwa na kitu cha kushangaza sana kwa kile anachokifanya na mtu asiejua anachokifanya angeishia kucheka , kilichokosekana ni mziki wa saida Karoli wa Maria Salome tu.
Lakini Hamza alikuwa siriasi mno , alikuwa tena amefumba macho kabisa huku akiendelea kukata mauno.
“Wewe, wewe umekuwa chizi , kwanini unakata mauno asubuhi asubuhi yote hii ?”Ilikuwa ni sauti tamu ya Regina na ilimfanya Hamza afumbue macho yake.
Regina alikuwa amevalia tisheti ya rangi ya pink iliomfanya chuchu zake kuchomoza kama miiba , kikaptura cha rangi nyeupe na raba aina ya Converse , alionekana kama vile ni mwanafunzi wa chuo anaejiaandaa kwenda Jogging.
“Mbona unanikodolea na macho yako?”Aliuliza Regina huku akiona aibu za kike.
“Regina kumbe na wewe una ratiba za kuchukua mazoezi”
“Wiki nzima kazini , siku mbili za mazoezi , unadhani ukiwa na shida ya mwili unaweza kufanya vizuri kazini , halafu acha kubadilisha topiki , kwanini unacheza kibwebwe asubuhi asubuhi?”
“Kibwebwe ndio nini , hii sio mchezo ni mbinu yangu ya mazoezi , ina nguvu ya ajabu mno”
“Mh ,mbingu gani hio ya mazoezi ya kukata viuno , jina lake inaitwaje?”
“Jina lake .. dah hata sijawahi kulifkiria.. kwa mtu wa kawaida anaweza kuona nacheza au kufanya maigizo lakini usichokijua ni kwamba nisingeweza kuwa na uwezo niliokuwa nao leo hii kama sio hii mbinu”
“Unajaribu kumdanganya nani , mimi nadhani ni kwasababu tayari wewe ni kichaa hivyo hata sikulaumu ukikata viuno asubuhi asubuhi”Aliongea Regina na alijua kabisa Hamza anaendelea na mchezo wake wa kumdanganya.
“Unadhani nadanganya , ijapokuwa kuna maelezo mengi ambayo naweza kukuelezea mpaka uelewe ila hii ni mbinu inayokuwezesha kuwa na muunganiko wa kimapigano”
“Acha uongo wako , kama ukiona kichaa kishaamka tafuta sehemu ya mbali ucheze midundiko yako , usije kumuua Shangazi kwa presha”Aliongea Regina na hakutaka kuongea nae zaidi bali alitoka nje ya geti na kuanza kukimbia katika barabara ya ufukwe wa bahari kuchukua mazoezi.
Mara baada ya Regina kutoka Hamza hakujali kejeli za Regina kabisa aliendelea kucheza kama vile ni mchawi , alikuwa akicheza anapanda juu anaenda mpaka chini halafu anarudi tena na kutingisha kiuno , kwa namna alivyokuwa akifanya ungeishia kucheka tu na kujisemea bangi ya asubuhi asubuhi sio nzuri.
Baada ya lisa kupita hatimae Regina alirudi akiwa anakimbia na kwa kuangalia mwili wake tu alijua Regina hakuwa mzembe kabisa na ilimshangaza na kujiuliza kwanini hakuona hilo mapema, au ni kwasababu ya urembo wake ndio maana hakumchunguza, Hamza aliishia kuguna tu na kujiuliza Regina ana siri gani na kuwa na mwili wa kijeshi.
Hamza mara baada ya mazoezi aliamua kuingia ndani na kujisafisha na kisha alikaa mezani kwa ajili ya Breakfast ambayo ilikuwa imeandaliwa na shangazi.
Regina na yeye alikuwa ndio wa mwisho kukaa mezani , kama kawaida ya tabia ya wanawake kujiremba ndio maana alichukua muda mrefu na mara baada ya kukaa mezani alikula kidogo tu tena nusu kikombe cha maziwa.
Wakati Hamza akiwa bize aliweza kuona simu ya Regina inaita kupitia kio chake , ilikuwa ni ya Linda sekretari wa Regina.
“Linda Mr Frei amefika tayari?”Aliuliza Regina mara baada ya kupokea.
“Ndio Mkurugenzi , Mr Ferney ndege yake imekwisha kutua, anajiandaa kuelekea Hotelini , nasikiliza maelekezo yako?”
“Haina haja ya kumsumbua kwasasa , atakuwa amechoka sana , tukiongea nae sasa hivi anaweza asitoe ushirikiano mzuri,tuma barua pepe kwa msaidizi wake na muulize ni saa ngapi tunaweza kukutana”
“Sawa madam”
Mara baada ya kukata simu Regina alimgeukia Hamza aliekuwa bize kumalizia vitafunwa vyote.
“Nimekuandalia nguo kadhaa na zimewekwa kabatini chumbani kwako , kazivae kama zilivyo muda si mrefu tunaondoka”Aliongea Regina.
ITAENDEEA
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI:SINGANOJR

ILIPOISHIA

Wakati Hamza akiwa bize aliweza kuona simu ya Regina inaita kupitia kio chake , ilikuwa ni ya Linda sekretari wa Regina.
“Linda Mr Frei amefika tayari?”Aliuliza Regina mara baada ya kupokea.
“Ndio Mkurugenzi , Mr Ferney ndege yake imekwisha kutua, anajiandaa kuelekea Hotelini , nasikiliza maelekezo yako?”
“Haina haja ya kumsumbua kwasasa , atakuwa amechoka sana , tukiongea nae sasa hivi anaweza asitoe ushirikiano mzuri,tuma barua pepe kwa msaidizi wake na muulize ni saa ngapi tunaweza kukutana”
“Sawa madam”
Mara baada ya kukata simu Regina alimgeukia Hamza aliekuwa bize kumalizia vitafunwa vyote.
“Nimekuandalia nguo kadhaa na zimewekwa kabatini chumbani kwako , kazivae kama zilivyo muda si mrefu tunaondoka”Aliongea Regina.

SEHEMU YA 29.
“Kuna ulazima wa kubadilisha na wikiend yote hii , nguo zangu nishazifua ni safi na hazina tatizo , kuna haja gani ya kuvaa nguo mpya?”Aliongea Hamza huku akiangalia Tshirt yake ya rangi ya bluu aliovaa na pensi yake.
“Kwahio zikiwa safi ndio nini, ni brand gani na umenunua shilingi ngapi?”Aliuliza Regina akiwa na muonekano wa kukereka.
“Kuhusu hilo ,.. sijui pia”Aliongea Hamza akigoma kujibu amenunua nguo zake shilingi ngapi.
“Mgeni tunae enda kukutana nae ni Mr Felini , mkurugenzi wa kitengo cha ubunifu kutoka Zara Group , sio mtu wa kawaida ni mbunifu namba moja duniani likija swala la mavazi, sasa akikuona na hayo mavazi yako unadhani atatuchukuliaje , anaweza asikubali kuongea biashara kabisa na sisi”Aliongea Regina.
Hamza alifikiri kidogo lakini aliona hakuna haja ya kujibishana na Regina hivyo alitingisha kichwa kukubali.
“Kama ni hivyo nitaenda kubadilisha”
Lakini sasa kabla hata hajasimama kutoka kwenda juu kubadili mavazi yake simu yake ilianza kuita na jina lilitokea Frida na palepale bila ya kujiuliza mara mbilimbili alipokea.
“Hello , Dr habari za asubuhi?”Alisalimia Hamza.
“Hamza haraka sana fika nyumbani kwangu , haraka sana ni dharula”Aliongea Frida na sauti yake ilikuwa na kitetemeshi na hilo Hamza alihisi.
“Kuna nini Dokta Frida?”Aliuliza Hamza huku akikunja sura na alihisi lazima kutakuwa na shida imempata lakini hakusikia sauti tena kwani simu ilishakatwa, Hamza alijifikiria kwa dakika kadhaa na aligeuka na kumwangalia Regina.
“Regina kuna dharula kuna sehemu naenda , hivyo nitatangulia”
“Dharula gani?” Aliuliza Regina lakini Hamza alikuwa ashatoka kwenye meza na alikuwa akitokomea nje
“Wewe , unaenda wapi , tuna kazi ya kufanya leo , rudiii”Aliongea Regina akimwangalia Hamza kwa mbali na Hamza alimuonesha ishara tu ya simu akimaanisha atapiga.
“Nimekufukuza kazi kwanzia leo, usije ukarudi hapa”Aliongea Regina kwa hasira lakini hakujua kama Hamza alikuwa amemsikia.
Shangazi mara baada ya kuona tukio hili aliishia kutingisha kichwa chake tu huku akuonyesha wasiwasi wa mahusiano ya Regina na Hamza.
Hamza alitumia dakika therathini hivi kutoka anapoishi mpaka Madale , alitumia taksi hivyo njia za mikato zilikuwa nyingi ili kuepuka foleni barabarani.
Kitendo cha taksi kusimama katika geti ya nyumba hio , Frida alikuwa tayari yupo nje na mara baada ya Hamza kufungua mlango kutoka, Frida alimpa ishara ya kurudi ndani ya gari na Frida na yeye aliingia.
“Tupeleke Asante Restaurant”Aliongea Regina.
“Malipo yataongezeka boss wangu”
“Just drive”Aliongea Regina na palepale dereva aligeuza gari na kurudi alikotoka.
Hamza alimwangalia Frida , alionekana kuwa na wasiwasi mno kana kwamba ni mwizi anaefukuzwa.
“Kuna nini Frida?”
“Tutaongea”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa , alijua Frida hakutaka kuongea mbele ya dereva.
Mgahawa wa Asante haukuwa mbali sana ni mita kadhaa kutoka anapoishi Frida mkabala na kanisa la wakatoliki na walishuka hapo huku Frida akitoa elfu therattini na kumkabidhi yule dereva n baada ya kupokea hela hio alionekana kuridhika.
Tuingie mgahawani sasa?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona mwanamke huyo ana sita sita.
“Hapana tunatembea taratibu taratibu nitakuelezea kadri tunavyotembea”Aliongea na Hamza alishukuru jua sio kali sana.
“Kuna nini?”Hamza alivunja ukimya.
“Wiccan wameanza kunifuatilia , leo nachukuliwa kwenda kuhojiwa”
“Kuhojiwa , unamaanisha nini?”
“Siwezi kusema sana , ila nimevunja kanuni za ki uanachama na baada ya mahojiano pengine nitaingia kwenye adhabu ya siku arobaini”Aliongea Frida akiwa na wasiwasi mno na swala hilo lilimshangaza Hamza.
Frida alikuwa akiangalia nyuma na mbele , ni kama alikuwa akiangalia kama kuna anaemchunguza.
“Kabla ya kuja kuchukuliwa nilihitaji tuonane, maana kuna uwezekano tusiweze kuonana tena kwa muda mrefu kidogo”Aliongea na kumfanya Hamza kumwagalia mrembo huyo machoni.
“Kosa ulilofanya linahusiana na mimi?”Aliuliza Hamza na Frida alitingisha kichwa kukataa.
“Sijui nani ananiandama , lakini taarifa zimefikia umoja mimi ni shushu wa Sinagogi , napaswa kupinga vikali shutuma hizi katika mahojiano lakini sina uhakika”Aliongea Frida huku akishika mkoba wake vizuri.
“Mbinu zinazotumika kutuhoji sio za kawaida , kuna uwezekano nitaelezea kila kitu hata zile siri ambazo zipaswi kusema , sina muda mrefu wa kuongea na wewe , nataka kukuuliza swali moja tu?”
“Uliza?”Aliongea Hamza huku ndita zikijikunja kiasi.
“Baada ya kupata taarifa ya vifo vya kundi la wawindaji kutoka Samar , moja kwa moja nilijua kuna uwezekano umehusika na vifo vyao, kweli si kweli?”Aliuliza Frida na Hamza hakujua mwanamke huyo alijuaje lakini alitingisha kichwa kuashiria ndio na Regina alivuta pumzi nyingi na wote walikuwa wamesimama.
Kwa jjinsi walivyokuwa wakionekana ni kama Frida na Hamza ni wapenzi na hata baadhi ya watu waliokuwa wakiwaangalia walikuwa wakiwaonea wivu , isitoshe Frida alikuwa mwanamke mrembo na watu wengi katika mitaa hio walikuwa wakimjua kama mwanamke mgumu na wa hadhi ya juu.
“Naamini walichokifuata ni kitabu alichokuachia Dokta Genesha, huwa inanishangaza kuona watu wanawinda hiki kitabu ilihali hakuna katika dunia hii mtu anaeweza kutafsiri lugha yake”Aliongea Frida na kumfanya Hamza midomo kucheza.
“Unaonekana kujua mambo mengi mno , sishangai kwa jasusi kama wewe , ila niambie unadhani ni kweli hakuna mtu wa kuweza kutafsiri maandishi ya hiko kitabu?”
“Tofauti na wewe sidhani kama kuna mtu anaweza kukitafsiri , hata Dokta Genesha mwenyewe uwezo huo hana ndio maana alikupatia , haikuwa kwa bahati mbaya , wewe ndio mtu pekee ambae utaweza kutafsiri lugha yake, swala ambalo linaweza kuwa hatari zaidi”
“Kila mtu ananiambia ninaweza kutafsiri lakini bado nashindwa kuelewa natafsiri vipi lugha ambayo hakuna ambae anaijua?”Aliongea Hamza huku akikuna nywele zake.
“Hamza njia pekee ya kumjua Mzee ni kukitafsiri , hakuna namna nyingine , kwa maelezo ya dokta Genesha wewe pekee utaweza kukitafsiri baada ya kuujua uhalisia wako , namaanisha kumbukumbu za maisha yako ya nyumba ambazo umesahau?”
“Hey! Unaongea nini , kumbukumbu gani ambazo nimesahau , nina kumbukumbu zangu zote kasoro za wazazi wangu tu?”Aliongea Hamza na muda huo walikuwa washaanza kutembea , Frida alikuwa akiangalia saa yake.
“Kiihusu swala la kumbukumbu zako siwezi kusema sana , ila ni swala la ndoto ulioanza kuota, muda wangu umeisha , nilichokuitia ni kukukabidhi Mshumaa alioniachia Dokta Genesha”Aliongea Frida na palepale aliingiza mkono kwenye mkoba wake na kumpatia Hamza kiboksi.
“Mshumaa!!?”
“Ndio , Mshumaa huo ndio kitu ambacho Dokta Genesha ameniachia nikupatie , ni Mshumaa wa Nuru wa kuamsha ndoto , ukifika sehemu tulivu utaona vifaa vyake vyote vipo , hakikisha ikifika saa tano usiku unautumia ,ila ni hiari yako kuutumia katika huo muda , ndio njia ya wewe kutafsiri kitabu alichokuachia Dokta Genesha na ndio njia pekee ya kuujua uhalisia wako na kumfahamu Mzee, maelekezo yote namna ya kutumia yapo ndani”Aliongea na kumkabidhi Hamza ambae bado alikuwa na mshangao.
“Nilidhani ulisema mpaka tuingie kwenye chumba cha Nuru?”
“Maelezo ya Dokta Genesha wewe ndio mtu pekee unaejua chumba cha Nuru kilipo , lakini umesema hujui , njia pekee kwasasa nikutumia huo Mshumaa”Aliongea Frida.
“Umeongea sana Frida , lakini mpaka leo hii ni siku ya tatu tunaonana , sijui historia yako licha ya mambo ulionielezea , nakuamini vipi katika hili?”
“Huna haja ya kuniamini, Amini nafsi yako na kila unalopanga litafanikiwa , muda wangu ushaisha , endelea kutembea bila kuangalia nyuma”Aliongea na Hamza alikifiria kidogo na kisha aliendelea kutembea kama alivyosema na baada ya hatua kama isihirini na nane aliishia kukunja sura.
“Mateso mema Frida” Aliwaza Hamza peke yake.
Nyuma Frida hakuonekana tena , haikueleweka alipotelea wapi lakini watu walikuwa wakiendelea na shughuli zao na hawakuwa kabisa na habari na Hamza.
Kwa lugha nyepesi tukio ambalo sio la kawaida lilitokea nyuma ya Hamza lakini watu hawakuweza kuona kabisa wala kuhisi.
Hamza hakuona haja ya kupoteza muda , alijua ashamkasirisha Regina tayari kwa kuondoka bila ya kumpa maelekezo ya kutosha , hivyo aliona awahi kuelekea huko hata kama ni kwa kuchelewa.
Alipiga mahesabu kutoka Umoja Road mpaka Tegeta Kibaoni ingemchukua dakika nyingi kutembea wa mguu hivyo alihitaji usafiri , wakati akijishauri ni usafiri wa aina gani aliweza kusikia honi ya gari ambayo ilimpita na kwenda kusimama mbele yake.
Ilikuwa ni gari aina ya BMW X7 rangi nyekundu , kwa uelewa wa haraka wa Hamza aliona gari hio ni ya thamani na hakujua ni nani anapigiwa honi lakini mara baada ya kuchunguza aliona alikuwa peke yake.
Dakika ileile akijiuliza kama yeye ndio anaepigiwa honi , mlango wa gari ulifunguliwa na alitoka mwanamke mrembo katika ile gari alievalia suruali ya suti rangi ya ugoro hivi na viatu vya High Heels.
Alikuwa mrembo haswa na kumfanya hata Hamza mwili wake kumsisimka.
Mwanamke yule mrembo alionyesha ishara ya kuinua mkono akimwita Hamza na kitendo kile kilimfanya Hamza amkazie macho na palepale aliikumbuka sura hio ya kirembo , alikuwa ni Prisila Singano, Mrembo aliekutaa nae katika hoteli ya Dosam V wakati alivyofika kufanya usaili..
Hamza alitoa tabasamu , ukweli ni kwamba alikuwa akijiuliza mrembo huyo yupo wapi , kuna siku alitamani hata kumuuliza Regina lakini alihofia Regina anaweza kumfikiria vibaya.
Ila Hamza alijiuliza ilikuwaje mwanamke huyo alimuona maana walionana siku moja tu na pili yeye alikuwa amempa mgongo, inamaana hakuona sura yake kwani uelekeo aliokuwa akielekea na gari hio ndio ilipokuwa ikielekea.
Upande wa Prisila licha ya kusimamisha gari lakini alionekana kidogo kuwa na uso uliokuwa siriasi na aliingia ndani ya gari kabla hata Hamza hajamfikia.
Hamza alijiongeza na kuzuguka upande mwingine na kufungua mlango na kuingia ndani.
Gari ya mwanamke ni ya mwanamke tu , ilikuwa na harufu nzuri mno na ubaridi usiokera.
“Asante sana kwa Lift Prisila, habari za toka siku ile?”Aliongea Hamza huku akiweka muonekano wake wa kizembe.
“Unakumbuka jina langu?”Aliuliza Prisila huku akirudisha gari barabarani na muonekano wake uliimarika zaidi mara baada ya Hamza kutaja jina lake.
“Mwanaume yoyote ambae anaweza kusahau jina la mwanamke mrembo kama wewe atakuwa na matatizo”
“Kwa jinsi ulivyokuwa ukiniangalia nilijua umenisahau , ila nimeshangaa uko peke yako , yule mrembo yupo wapi?”Aliuliza Prisila huku akikaza macho barabarani.
“Mrembo gani?”
“Ulieshuka nae pale Asante Restaurant, nilikuwa ndani , nilitegemea mtaingia ila niliona mkiondoka , unadhani ningekufahamu kwa kuangalia mgongo wako tu?”Aliongea na kumfanya Hamza sasa kuelewa.
Prisila alikuwa na sauti nzuri mno na kila dakika ambayo mwanamke huyo alivyokuwa akiongea ndio mwili wake ulivyokuwa ukisisimka.
Hamza mara baada ya kusikia kauli hio sasa ndio alijua kumbe Prisila alimuona wakati akishuka na Frida pale mgahawani , ilileta maana kwani kulikuwa na watu wengi ndani ya mgahawa huo ndio maana Frida akasema watembee.
“Ni heshima kubwa kukumbukwa na mwanamke mrembo kama wewe?”
“Hakuna cha kushangaza kukumbuka , mimi ndio nilikukutanisha na Regina , si rahisi kusahau mpenzi feki wa bosi wangu , anyway hadhi yako imepanda pia , Dokta Frida sio mwanamke anaeweza kutangulizana na yoyote”
“Unamjua Dokta Frida?”Aliuliza Hamza na Prisila alitingisha kichwa.
“Baadhi ya watu wa kawaida wanaweza wasimfahamu Frida , lakini katika ulimwengu wa wanataaluma wengi tunamfahamu , ndio maana nimeshangaa kukuona ukiwa na Frida ,Dokta namba moja wa taasisi ya Haliz, una siri gani ambayo hatuijui?”
“Siri gani tena?”Aliuliza Hamza na kuna kitu alishajua kuhusu Prisila ni mwanamke ambae yupo siriasi sana , ijapokuwa alionekana kama maneno yake yapo na viashiria vya urafiki lakini alionekana ni mwanamke anaehitaji majibu ya haraka.
“Kwa mtu yoyote aliewaona atasema mna ukaribu , kama sio wa kimapenzi, ni wa kindugu na kama sio wa kindugu basi pengine ni wa kikazi , lakini kwenye uhusiano wa kikazi ni asilimia chache sana uwezekano huo kuwepo , Frida ni mwanasayansi wewe ni mwanafunzi wa chuo taaluma mbili tofauti?”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa.
“Uliosema yote hayawezekani , mimi na Frida ni mtu na mfayakazi wake, ulivyotuaona nilikuwa nikipokea maagizo pale”Aliongea Hamza huku akicheka.
Prisila aliongeza umakini barabarani baada ya kufika makutano ya barabara ya Tegeta.
“Nimekupa lift ila hujanniambia unaelekea wapi?”Aliuliza na kumfanya Hamza kukuna kichwa.
“Nilipaswa kwenda na bosi wangu kwenye kikao na mgeni wake ila nilipata dharula , sijui ni hoteli gani?”.
“Nini!, Dharula hio ni kukutana na Frida?, Regina akijua anakufukuza kazi?”
“Dharula ni dharula kwanini anifukuze kazi?”
“Sikulaumu , hujakaa muda mrefu na Regina , kama mpenzi feki kazi unayo?”Aliongea huku akicheka.
Prisila ndio mtu pekee ambae alikuwa akijua mahusiao yake na Regina ni feki , pengine ni kwasababu Prisila ndio aliweka tangazo mtandaoni na hata kumpokea Hamza katika usaili , kufikiria hilo Hamza shauku ilimjaa,haikuwa rahisi kwa Regina kumpatia kazi nyeti kama hio Prisila , ilimaanisha wawili hao lazima watakuwa na ukaribu.
Prisila kwa kutumia gari yake hio ya kisasa alipangusa katika kioo na kisha akapiga namba ya Linda na Hamza alitoa tabasamu na kuona huyu mwanamke ni jiniasi , amefanya kile ambacho alikuwa akiwazia amuombe afanye.
Hamza alikuwa ashapiga namba ya Regina kabla hata hajaingia kwenye gari ya Priisila lakini haikupokelewa tena ilikatwa baada ya kuita kidogo,alijaribu na ya Linda hivyo hivyo lakini pia ilikatwa.
“Linda mpo hoteli gani?”
“Madam Prisila kwanini unauliza?”Sauti upande wa pili ilisikika . ilikuwa ya Linda na ilionyesha heshima.
“Nataka kujua kikao kinafanyikia wapi?”
“Tupo Seaview hoteli”Aliongea.
“Okey!!”
Prisila palepale alikata simu na kumwangalia Hamza na Hamza alitabasamu.
“Uwezo wako wa kumsoma mtu ni wa juu , upo kama baba yako”
“Usifurahi sana , nimekusaidia hii inamaanisha una deni kwangu”
“Nipo tayari kulipa muda wowote Madam”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu la kizembe na Prisila alitoa kicheko hafifu.
“Nitakuacha Jogoo , nadhani itakuwa rahisi kupata usafiri wa kukufikisha Serena”
“Nitashukuru sana”
“Kama unanishukuru niambie ukweli mahusiano yako na Frida?”
“Ah..!” Hamza aliishia kushika pua yake na kujiambia inamaana bado swala la Frida linamsumbua huyu mwanamke , lakini hayo ni mambo yake binafsi kwanini anauliza sana.
“Ni kama nilivyosema”
“Okey!”Aliongea Prisila na muda huo walikuwa washafika tayari kituo cha Jogoo na Regina alisimamisha gari.
“Prisila asante sana kwa lift , nadhani tutaonana kazini?”Aliongea Hamza na Prisila alitingisha kichwa.
Hamza alitoka na kufunga kioo na Prisila aliondoa gari tataribu huku wengi wakiikodolea macho gari ile na ilipokumja kushoto waligeuza macho na kumwangalia Hamza.
Hamza kwa jinsi alivyoshushwa alijisikia vibaya kupanda daladala , lakini aliona pia daladala sio chaguo sahihi kama anataka awahi hivyo aliiita boda na kupanda , ili mbele kwa mbele achukue taksi itakayomfikisha Seaview.
Baada ya kupata pikipiki huku akihakikisha mzigo wake aliopewa na Frida upo salama aliondoka.
Nusu saa mbele wakati akiingia ndani ya hoteli ya Serena aliweza kuiona ile Lexus lx 600 ni alijua mara moja ni ya Regina maana ndio moja ya gari la kifahari ambalo lipo katika maegesho ya muda mfupi.
Hamza alijua kabisa Regina atakuwa aliendesha gari yake mwenyewe mpaka kuja hapo.
Hamza mara baada ya kufika alijipiga kichwani , hakujua Regina atakuwa katika floor ipi wala anakutana nae vipi na Hamza alisita huku akijiuliza au aende front desk kuuliza lakini kabla hata hajaamua cha kufanya aliweza kumuona Linda na hatimae Regina katika floor ya kwanza upande wa mhagawa na alijikuta akivuta pumzi ya ahueni na kisha alizipiga hatua kuwasogelea.
“Mkurugenzi , Linda , mbona mmekaa hapa , ndio manisubiri au?”Aliuliza Hamza.
Regina mara baada ya kumuona Hamza hakuweza kujizuia kukunja ndita na alimwangalia mara moja tu na kisha akashusha kichwa chake chini akijiweka bize na juisi yake huku akimpotezea, ilionekana alikuwa amekasirishwa na kitendo cha Hamza kuondoka bila kupata ruhusa yake kumuwahi mwanamke aliemsikia akiitwa Dokta Frida.
“Mkurugenzi alihitaji uwe mkalimani katika kikao chetu lakini ukaamua kuondoka kana kwamba jambo hili sio la muhimu , huhitajiki tena kwa kazi ya ukalimani hivyo unaweza kuondoka”Aliongea Linda.
“Kwanini niondoke, naamini hata bado hamjakutana na Mr Felini”Aliongea Hamza huku akiondoa wasiwasi wake na tabasamu.
“Tunaweza kuongea na Mr Felin kwa kingereza tu hata bila ya uwepo wako , na isitoshe kwa mavazi uliovaa ukikutana na mgeni wa heshima huyo ni kuleta matatizo tu”Aliongea Linda na kumfanya Hamza kuangalia mavazi yake.
“Kwanini unasema hivyo , sioni tatizo juu ya mavazi yangu”
“Mavazi gani hayo ambayo yashaanza kufubaa kwa kufuliwa mara nyingi, halafu staili yake ni ya kizamani kama vile upo karne ya ishirini”
“Hii ni Retro style, ina radha ya kifasheni ya upekee”Aliongea na Linda wakati alipokuwa akitaka kuendelea kujibishana nae aliacha mara baada ya kuona watu wakitokea upande wa lift.
“Mkurugenzi , Mr Felini na timu yake wale wanakuja”Aliongea Linda na mara baada ya Regina kusikia kauli hio aliweka glasi yake chini na kisha akasimama ili kwenda kuwapokea lakini kabla hata hajaanza kupiga hatua alimgeukia Hamza.
“Usinifuate unaweza kubakia hapa au ukiona hapakufai ondoka”
Hamza mara baada ya kusikia kauli ile alijihisi kama vile amekosewa na alijiambia inamaana mavazi yake yanaonekana sio ya thamani kiasi kwamba wanamnyanyapaa, Hamza aliangalia mavazi yake na aliona ya kawaida , isitoshe ni mavazi ambayo anahistoria nayo kubwa tu.
Lakini Hamza hakutaka kumuudhi Regina , ilionekana kabisa mwanamke huyo alikuwa akikipa kikao hicho thamani kubwa hivyo aliamua kukaa kusubiri.
Muda uleule Regina na Linda waliweza kuwafikia wazungu wale na kuwasalimia.
Felini alikuwa mrefu mwenye kifua kipana akiwa na nywele alizofunga kwa nyuma kama Halaand, alikuwa amevalia suti ya rangi ya bluu na nyekundu , shati jeupe ambalo lina kola ilionakshiwa kwa mua maua , jeans na sendo za ngozi.
Mtu wa aina hio na mavazi yake ilikuwa rahisi kumtofautisha na yule mzungu mwingine moja kwa moja hasa kwenye saa yake ya Patek Phillipe.
“Oh, you must be Miss Regina , I’ m really sorry , I took a break at the hotel and made you visit for a long time”Aliongea bwana huyu mzungu akiomba radhi kwa kumsubirisha Regina kwa muda mrefu wakati akiwa amepumzika, alionekana kuwa mkarimu.
Regina upande wake aliishia kutoa tabasamu hafifu , ijapokuwa lilioneksha hali ya ukaribisho lakini kwa ukauzu wake ni mara chache sana kumuona akitoa tabasamu la aina hio.
“Umekuwa kwenye ndege kwa masaa mengi hivyo ni haki yako kupata muda kidogo wa kupumzisha mwili , nimekuwa na matarajjio makubwa juu ya kikao hiki , sasa hivi tayari ni saa sita muda wa chakula cha mchana , mnaonaje tukipata chakula pamoja?”Aliongea Regina kwa kingereza
“Nimeshapata chakula tayari nilipokuwa kwenye ndege hivyo sitopata muda wa chakula cha mchana , napaswa kwenda Dubai baada ya hapa kutembelea matawi yetu na baada ya hapo nitaelekea Paris, ratiba yangu imebanana sana”Aliongea na jambo lile lilimshangaza Linda na Regina kwani hawakutegemea kama Fellin angekaa Tanzania kwa muda mfupi sana.
Lakini ilikuwa sawa kwa mtu mbunifu maarufu kama huyo muda ulikuwa ni kitu cha thamani sana , maana ukiachana na kubuni mavazi ya kampuni lakini vilevile alikuwa akibuni mavazi yake mwenyewe kwa ajili ya maonyesho.
Kitendo cha mfanyabishara kama yeye kumualika mtu bize kama huyo kuja mpaka Tanzania ilikuwa ni heshima kubwa.
“Kama ni hivyo kwanini tusitafute sehemu na kukaa kwenda moja kwa moja kwenye maongezi?”Aliongea Linda.
“Yes”Aliongea na muda ule aligeuka nyuma kama kwamba kuna mtu mwingine alikuwa akimsubiria na kweli alinyanyua mkono mara baada ya kumuona mwanamke.
“Hey!, Salma , I am here..”
Mara baada ya kuona Fellin kuna mtu anamwita iliwafanya Linda na Regina kugeuka pia kuangalia mtu alieitwa Salma.
Alikuwa ni mwanamke mrembo haswa alievalia gauni lenye kola nyeusi la chui chui ambalo limebana sana , alikuwa amependeza mno kwa jinsi vazi hilo lilivyomkaa huku akivalia viatu vya skuna , alitembea kwa kujiamini mno.
Kwa jinsi alivyovalia unaweza kusema anaenda kwenye date lakini muonekano wake pamoja na makeup ilimfanya kuwa na muonekano wa kimaringo na kumfanya watu wengi wamwangalie.
“Salma Mohamed Salah!!”
Wasiwasi ulionekana katia macho ya Regina huku akimwemwesa midomo kwa kutaja jina hilo.
Hata kwa yule mwanamke mrembo mwenye kuchanganya rangi ya kiarabu na kiafrika alionekana kumfahamu Edna na alionyesha tabasamu lenye viashiria vya dharau.
“Regina na wewe upo hapa kwa ajili ya ushirikiano wa kibiashara na Fellini?, Nadhani nikuambie tu kwamba umechelewa na utaishia kukata tamaa”Aliongea.
“Salma unafahamiana na Miss Regina?”
“Ndio , tumesoma shule moja High school , baada ya kumaliza kila mtu alichukua uelekeo wake , hatujawahi kuonana kuanzia hapo mpaka wote tulipokuja kuwa wafanyabiashara na kuingia kwenye ushindani”Aliongea Salma.
“Basi vizuri , kama mnafahamina nadhani ni vizuri tukianza kuongea kuhusu ushirikiano , kuna mgahawa hapa hivyo haina haja ya kutafuta eneo lingine”Aliongea na palepale mzungu yule pamoja na msaidizi wake walisogea upande wa mgahawa.
Hamza mara baada ya kuona kundi hilo la watu limesogea karibu na yeye hakutaka kumkasirisha Regia hivyo hakuwasalimia kabisa na kula buyu.
Ukweli ni kwamba Linda na Regina hawakuwa na time nae kabisa na Regina muda huo mara baada ya kuona Salma alikuwa na mawasiliano na Fellini alijua kabisa mazungumzo yashaingia doa , mshindani wake mkubwa wa kibiashara kwa ukanda Afrika mashariki na kati ni kampuni ya Salah, lakini hata hivyo hakuwa na jinsi na kukubali kupitia changamoto hio, angejua kampuni ya Salah ilikuwa ikitaka pia ushirikiano na Fellini pengine angejiandaa zaidi, kingine ambacho kilimshangaza Regina ni kwamba Salma alikuwa akisimamia kampuni ya mitindo upande wa China lakini ghafla anaonekana mbele yake, moja kwa moja alijua lazima kampuni imempa kazi ya kuhakikisha dili la ushirikano na Zara liafanikiwa kwa namna yoyote.
Wote kwa pamoja walitafuta siti zao na sasa kukawa na makundi matatu yanayowakilisha kampuni tatu tofauti , Regina akiwakilisha Dosam , Salma akiwakilisha Salah na Fellini akiwakilisha Zara.
“Mr Fellini , we have an appointment to meet privately , joining of Salah family’s representative , I’ m afraid, is not appropriate”Aliongea Regina akimaanisha kwamba walikuwa na ahadi ya kukutana lakini kuunganisha na familia ya Salah , sio sawa.
Upande wa Felini alipewa Kiko ya kuvutia sigara na kuwasha na kisha akavuta moshi huku akiwa na tabasamu lenye utulivu.
“Usiwe na wasiwasi Miss Regina , nilikutana na Salma kwenye maonyesho ya wiki ya Fasheni jijini New York na kugusia swala la kibiashara , najua familia yake ndio wamiliki wa kampuni kubwa ya mavazi ya Salah kutoka Uturuki , lakini sina mahusiano yoyote na yeye zaidi ya maswala ya kibiashara, yoyote kati yenu ambae atakuja na vipengele pamoja na ofa nzuri ya ushirikiano wa kibiashara sitokuwa na upendeleo wa kuchagua , kwa haki na uwazi nitachagua upande sahihi”
“Hehe.. Regina unaogopa nini, nakukumbusha tu familia yetu ndio wa kwanza kabisa kuwa wakala wa bidhaa za kifahari kutoka makampuni makubwa kabla yenu, Vigezo vyake ni vingi sana , sisi ni tofauti na kampuni yeu ambayo ipo kila sekta”Aliongea Salma.
“Kuwa na vigezo vingi haimaanishi chochote , nakubali nyie ndio mlianza kuleta mavazi ya kimitndo Tanzania lakini baada ya kampuni yetu kuingia katika biashara hio tuliwapita miaka mingi tu , Zara ni kampuni ambayo malengo yao ni kuendeleza utawala wao wa kimavazi katika kila soko , unadhani ni rahisi kuingia mkataba na kampuni ambayo inalega lega sokoni”Aliongea Regina.
“Una mawazo ya kimasikini , hivi unadhani kujipanua kwenu kusiko na malengo ndio uwezo wa kampuni , sisi kama kampuni sio fasheni tu tunayoheshimu bali na utamaduni pia unaoendana na mavazi, kampuni yetu inaendeshwa kwa misingi ya kisera ilioweka tokea kuanzishwa kwake, hatuwezi kufanya kila biashara ambayo tunaona tunaweza kupata faida , kwetu sisi hela sio malengo bali ni kukuza utamaduni, tunataka ushirikiano na Fellini kwasababu malengo yetu ni kuhakikisha tunateka soko la fasheni inayoendana na utamaduni wetu wa kiafrika”aliongea Salma kwa kingereza akimjibu Regina na Felini aliweza kusikia majibishano yao .
“Salma yupo sahihi , kampuni ya Zara haingii katika ushirikano wa kibiashara na kampuni ambayo ina Asset nyingi wala thamani ya hisa sokoni, tunajua fika uchumi wa kampuni ni moja ya kigezo lakini kwa vyovyote vile tunazingatia kampuni ambayo ina sera zinazoendana na mazingira ya jamii husika”Aliongea Fellini.
“Mr Fellini nakiri kwamba katika biashara ya mavazi , kampuni ya Salah ina uzoefu mkubwa na taaluma , lakini tupo na nia ya dhati pamoja na ari ya kujiamini katika kuifanya kampuni ya Zara kuuza sana katika soko la Afrika”Aliongea lakini kauli ile ilimfanya Fellini kukunja ndita.
“Miss Regina , naomba uniwie radhi kama nitatoka nje ya mpaka , ukweli ni kwamba nimejaribu kufanya uchunguzi kiasi kuhusu wewe na nikiri nakuheshimu sana kwasabau upo katika kundi adimu la watu wenye akili nyingi duniani , lakini hata hivyo nimefuatilia malengo ya kampuni yenu sera yenu kubwa ni kujipanua na kuhakikisha mnaingiza faida kwa kiasi kikubwa , hivyo mbinu zenu za kibiashara zipo kwa ajili ya kutengeneza hela..”
Regina alishangazwa na kauli za Felllini na alianza kujisikia wasiwasi katika moyo wake.
“Kama nilivyosema sera ya kampuni yetu ni kutamfuta mshirika ambae anatulewa ili kusambaza tamaduni zetu, tunachouza sokoni sio bidhaa tu bali ni wazo , huduma na ustaarabu ulioendelea katika jamii”
“Mr Fellin naelewa unachosema , sitoingilia mapendekzo ambayo mtakuwa mnatoa kama kampuni , ninachotaka kusema ni kwamba tunao uwezo wa kuwafikia wateja kwa haraka na kwa wingi zaidi kuliko kampuni yoyote ndani ya Afrika mashariki na kati”
“A nouveu riche is a nouveu riche , Regina huelewi tu , anachotafuta Mr Felleni ni mshirika wa kibiashara na sio muuzaji, maana yake ni kwamba lazima na wewe kama kampuni ushiriki katika mawazo ya ubunifu wa bidhaa, michoro , aina ya kitambaa na eneo la uzalishaji , ukishajua hatua zote hizo inamaana utaelewa na kilichokusudiwa katika bidhaa na itakuwa rahisi kumfikia mteja na kumfanya anunue .’listen up , its not the consumer its customer”
Kulikuwa na kila ishara ya furaha katika uso wa Mr Fellini mara baada ya kusikia msemo aliomalizia nao Salma.
“Yes , Miss Salma is right , As expected of a talented girl who graduated from parsons school of Design , My analysis is very thorough , that is what I mean”Aliongea akimaanisha kama alivyotegemea kwa msichana mwenye kipaji aliemaliza chuo cha ubunifu cha Parson , uchambuzi wake ni yakinifu.
Salma mara baada ya kusifiwa alifurahi mno meno yote nje na alimwangalia Regina kwa tabasamu la uchokozi.
“Regina jikatie tu tamaa , wewe endelea na biashara ya kununua ardhi , kujenga viwanda na kununua hisa , mambo ya fasheni hayakufiti kabisa”
Kwa jinsi alivyoongea ni kama vile alikuwa akishindana na Regina au alikuwa na kinyongo cha muda mrefu.
Regina aliishia kubaki kimya na alimwemwesa lips zake , huku pembeni Linda akiwa na uso uliopauka kwa hasira.





SEHEMU YA 30.
Fellini alifikiria kwa muda na kisha alimwangalia Regina kwa uso kidogo uliokuwa hauna ridhiko.
“Miss Regina , naomba nikuambie tu kwamba hatuwezi kufanya kazi pamoja zaidi kwasababu hatuna maelewano ya kisera kati ya kampuni zetu”
“Inakuwaje Mr Fellini , tulijiandaa kukutana na wewe kwa muda mrefu na tumeshaandaa mipango ya kibiashara ya muda mrefu ya ushirikiano wetu, hujaona hata vipengele vya mkataba lakini kwasababu ya kutofautiana mtazamo unatukataa , hii sio haki”Aliongea Linda.
“Wewe ni msaidizi tu , hujapewa ruhusa ya kuongea”Aliongea Salma.
“Haina haja ya kubembeleza zaidi Linda , alichoongea Mr Fellini ni sahihi kabisa , mimi sina maarifa mengi likija swala la fasheni”
“Mkurugenzi wewe sio mbunifu wa mavazi na hujasomea fasheni , haina haja ya kuwa mnyonge , ulichoongea wewe ni katika jicho la kibiashara”
Upande wa Fellini alionekana kwenye kutafakari kwa dakika kadhaa na kisha aliwaangaia wote wawili yaani Salma na Regina.
“Mnaonaje tukifanya hivi , wote wawili mmevaa na mmependeza sana , je kuna sababu yoyote ya kuchagua staili ya mavazi mliovaa leo?, watu wenye pesa hatuvai kupendeza tu , kuna mengi zaidi ya kuelezea kuhusu aina ya maisha yetu kupitia nguo , nataka kusikia kutoka kwenu”Aliongea , Fellini hakutaka kuonekana mkatili ndio maana alitaka kumpa Regina nafasi ya mwisho.
“Bila shaka nitaelezea”Aliongea Salma na kisha alisimama akiwa na tabasamu na kuonyesha vazi lake.
“Mr Fellini nadhani utakuwa umejua hili ni vazi kutoka Louis Vuitton lililovuma kwenye maonyesho ya wiki ya mitindo jijini Paris?”Aliuliza na Fellini alitingisha kichwa akikubali.
“Hili vazi linaweza kuonekana la kawaida lakini linadhihirisha ujasiri wa mbunifu, mpangilio wa eneo la kiuno unamfanya mwanamke yoyote ambae amevaa kumpa heshima yake kwa kuonyesha ni kiasi gani ni mrembo, dizaini iliotumika ni ya kibalkani na udarizi wa eneo la mkanda wa kiunoni pamoja na vazi lote juu hadi chini linaashiria tabia , sifa yangu kubwa ni ucheshi ndio maana nimechagua vazi hili leo hii”Aliongea na kisha akakaaa
“Vipi kuhusu Miss Regina , wewe unasemaje?”
“Vazi langu ni mtindo toleo la mwisho kutoka Zara”Aliongea na Fellini alitingisha kichwa.
“Najua kabisa ndio ni kutoka Zara , mimi ndio nilihusika na ubunifu wake, tulilipatia jina la Norse Goddes style , limekupendeza mno ulivyovaa ni kama tulikutengenezea wewe peke yako”
“Kweli… kwahio staili yake ndio inaitwa Norse , sikuwa hata nikijua , kwa macho yangu mimi ni gauni kama gauni tu, nimenunua kwa zaidi ya Euro elfu ishirini na tatu , lakini sokoni kuna staii hii hii bilaBrand ya Zara na wanauza kati ya milioni moja mpaka tano, kwangu mimi niliona ni vazi linalonipendeza na nikalipenda mno ndio maana nimelivaa lakini sababu nyingine niliamini kuvaa mavazi ya kampuni ya Zara itatuweka karibu zaidi kibiashara”
Mara baada ya kumaliza Fellin alishangaa hata kwa Linda alikuwa amekakamaa mwili wakati wa maelezo ya Regina.
Upande wa Hamza na sikio lake kama antenna za kisimbuzi cha Zuku aliweza kusikia kila kitu na alionekana kumkubali Regina , aliona ni kama kuna kitu ameelewa katika maelezo yake.
“Mr Fellini nadhani sasa umeona , Regina kila anachoongea ni katika msingi wa kibiashara , huyu ni mashine ya kutengenezea hela na hajali chochote zaidi ya faida , hawezi kujua thamani halisi ya vazi nje ya gharama yake”
Fellini upande wake alionesha kukatishwa tamaa kabisa na Regina na kulikuwa na ishara ya kukereka katika macho yake.
“Miss Regina nimependa ulivyomuwazi”
“Asante sana Mr Fellini , natumaini siku zijazo utajifunza pia kutoka kwangu na kuwa muwazi, maana umekuja nchini ukiwa tayari na mpango wa kufanya kazi na kampuni ya Salah na sio sisi , hivyo sidhani kulikuwa hata na haja ya kukutana”
“Hapana, umenielewa vibaya , sijafanya maamuzi kabla”Aliongea Fellini akijitetea.
“Kutoka mwanzo mpaka mwisho ulikuwa ukiongelea maswala ya utamaduni wa kampuni na sera ila hukuniuliza hata swala la soko lilivyo na mtaji kiasi gani tulipanga kuwekeza kwenye ushirikiano wetu , unajua kabisa nimesomea maswala ya uchumi , masoko na usimamizi , lakini mmeanza na kuongea nadharia zenu za fasheni na mambo mengine ambayo yapo nje ya taaluma yangu , unanilinganisha na Salma ambae amesoma chuo kikubwa dunniani cha mitindo na kazi yake ni ubunifu wa mavazi , ulichofanya ni kama kutengeneza mazingira ya kampuni ya Salah kushinda na si vinginevyo”
Mr Fellini mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta kwa namna flani akiona aibu lakini alivuta moshi wa sigara kidogo kujituliza.
“Kama ndio unavyoamini basi sidhani kuna haja ya kuendelea na haya mzungumzo , kwa bahati mbaya hatuwezi kushirikiana na kampuni yako”
“Nashukuru hujachagua kampuni yetu kwani nisingependa kuishi katika ulimwengu wa kufikirika na mshirika mnafiki”
“Unasemaje , mimi ni mnafiki?”Aliongea mzungu yule huku uso wake ukijikunja .
Alikuwa maarufu kwa zaidi ya miaka ishirini sasa na kila mtu alikuwa akimheshimu lakini leo hii anatukanwa na msichana mdogo kutoka taifa masikini kama Tanzania.
Upande wa Regina hakujali tena kuhusu hasira za Fellini alimpa ishara Linda na kisha walisimama kuondoka.
“Regina simama hapo hapo”Alifoka Salma.
“Unaonyesha tabia gani mbele ya mtu mwenye heshima zake kama Fellin , unadhani ni mtu unaeweza kumtusi hivi hivi tu , omba msamaha kabla hujaondoka
“Miss Regina nakuhakikishia utalipa kwa dharau ulizonionyeshea, usisahau mikataba ulioingia na baadhi ya kampuni za mavazi tunamiliki hisa zetu pia”
Regina alisimama na kisha aligeuka , macho yake ya kirembo yalikuwa na ukauzu usiokuwa wa kawaida.
“Kwahio mnajaribu kuniogopesha na kunitishia?”
“Kwahio vipi , ulimwengu wa mitindo sio mtu wa hadhi ya chini kama wewe unaweza kuingia unavyotaka”Aliongea Salma.
“Vyovyote vile , mwisho wa siku sio mimi nitakae anguka bali ni mtu mwingine”
Mara baada ya kumaliza kauli hio sauti ya mtu akipiga makofi ilisikika , alikuwa ni Hamza.
“Vizuri sana , hakika bosi wetu una ujasiri wa hali ya juu,Awesome”Aliongea Hamza huku akicheka akisogea karibu.
Regina na Linda waliishia kushangaa , ni kama sasa wanakumbuka Hamza alikuwa hapo , akiwa kimya tu akisikiliza.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Salma huku akikunja mdomo.
“Kwa majina yangu naitwa Hamza Mzee , Msaidizi namba mbili wa bosi Regina , kuwa sahihi zaidi unaweza niita dereva wake”
“Haha.. Dereva, Hamza!!”Salma alicheka kwa nguvu kwa kejeli.
“Regina vigezo vyako ni vya chini mno , yaani umemuajiri mshamba kutoka porini huko kuwa dereva wako?, nadhani maamuzi ya Mr Felllini ni sahihi kabisa , kufanya kazi na mtu asiezingatia hadhi ya wafanyakazi wake ni kujidhalilisha tu na kushusha thamani ya Brand ya kampuni”Aliongea na kisha alimwangalia Fellini kama anamsapoti katika dhihaka zake.
Lakini upande wa Fellini alikuwa akimwangalia Hamza kwa macho kodo kana kwamba alikuwa ameona mzimu, alikuwa ameshikwa na bumbuwazi ashindwe kusema neno.
Hata kwa Regina waliona muonekano wa Fellini , alionekana kama ni mtu mwenye wasiwasi.
“Nini tatizo Mr Fellini , huyu mshamba kakuogopesha?”Aliongea Salma.
“No ,, impossible”Aliongea Fellini akisema haiwezekani huku akimsogelea Hamza karibu.
Mara baada ya kumfikia alishindwa kujizuia na kunyoosha mkono wake na kushika kolla ya nguo alizovaa Hamza.
Cha kushangaza ni kwamba mikono yake ilikuwa ikimtetemeka kana kwamba ameshika kitu cha thamani sana.
“Mr Fellini umepatwa na shida gani?”Aliuliza Salma asijue kwanini huyo mzungu alionekana kama vile amepandwa na wazimu.
Regina upande wake pia alikuwa kwenye hali ya kushangaa na alijiuliza au Fellini alikuwa amevutiwa na uchakavu wa tisheti ya Hamza
“Wewe Mzungu vipi , acha kunigusa bwana mimi sio bwabwa”Aliongea Hamza na kumzuia Fellini kwa kumshika mkono.
“Umesema unaitwa Mr Hamza si ndio , naomba nikuulize swali , umezipata wapi hizi nguo ulizovaa?”
“Kuna mzee ambae ni rafiki yangu alinnipatia kama zawadi , ni miaka mingi kidogo imepita”Alijibu Hamza.
“Mzee rafiki yako , unaweza kunitajia jina lake?”Aliuliza na kumfanya Hamza kukunja kichwa.
“Mimi napenda kumuita Mzee Roboti , ila jina lake lote ni Alec sijui nini”
“Ni Alec Von Blumer sio”
“Ewaaa.. hilo ndio jina lake yule mzee , amenipa nguo nyingi sana kama zawadi, ni mkarimu sana haha..”
Mara baada ya kusikia hivyo Fellini alijikuta akijikokota kurudi nyuma kwa mshangao na alijitahidi kujiegamiza kwenye sofa asidondoke
“Mr Fellini what wrong?” Aliuliza msaidizi wake huku Salma na Regina wakiwa wameshangazwa pia na tukio hilo.
Fellini kwa haraka haraka alichukua glasi ya maji na kuigida yote na kuiweka chini akijitahidi kujituliza.
“Master George Alec Von Bliimer ndio mwalimu wangu , kwa maneno mengine ndio mbobezi …”Mara baada ya kuongea hivyo Regina , Linda na Salma walishikwa na mshangao wa kutokuamini.
“Mr Fellini si umehitimu kutoka chuo cha sanaa cha London , kwanini unasema una mwalimu wako?”Aliuliza lakini Felini alimdharau Salma kwa ujinga.
“The real art of clothing is not in any Academy , but in Seville street , Miss Salma haven’t you heard about it ?”Aliuliza Fellini.
“Najua ndio , Sevile ni mtaa uliopo ndani ya London Mayfair , sehemu wanapopatikana mafundi nguo maarufu , hususani mafundi wa nguo za kiume, ukisikia neno ‘Customized clothes’ asili yake ni katika mtaa huo, wafalme na viongozi wakubwa duniani walipendelea sana wazo la kushonewa nguo zinazoendana na wao katika mtaa wa Sevile , maduka mengi ndani ya Sevile yana historia ya karne kadhaa”Aliongea Salma.
Ilikuwa ni kweli kabisa, kama ilivyokwa mtu wa kawaida kupendelea kwenda kwa cherehani kushona suti inayoendana na vipimo vya mwili wake basi ipo hivyo hata kwa matajiri na viongozi wa daraja la juu ikiwemo wafalme wa mataifa makubwa.
Sasa mtaa wa Seville ndani ya London Mayfair ndio kunapatikana mafundi cherehani ambao hushona nguo hizo za watu wazito wazito.
Regina hata yeye ashawahi kusikia kuhusu Seville lakini hakujua hadhi ya mtaa huo ilivyo.
“Upo sahihi , tokea nilipokuwa mtoto ndoto yangu ilikuwa ni kuja kuwa mbunifu wa watu wazito wazito duniani , hivyo niliweka bidii na hatimae nikaja kufanikiwa kuingia mtaa wa Seville kama mwanafunzi wa ufundi cherehani na mbunifu , nilijifunza ufundi kwa mwalimu wangu George na hatimae nikawa fundi wa daraja la chini kigezo ambacho kilinifanya kushindwa kuendelea kuwa chini ya George , ni kwasababu sikuwa na kipaji kikubwa cha ushonaji , hivyo mara baada ya kutopata nafasi zaidi niliamua kuachana na maswala ya ushonaji nikaingia chuo “

“Nini, Mr Fellin mbona unakipaji kikubwa mno , unasemaje huna kipaji”Aliongea Salma.
“Salma unaweza ukwa umemaliza kwenye chuo kikubwa na ukawa mbunifu wa kimataifa lakini huwezi kufikia hadhi ya mwalimu wangu George , wateja wake ni wafalme , malkia , Watoto wa wafalme na Princess au watu matajiri duniani na wanasiasa wakubwa, hahitaji umaarufu wowote ndio maana wengi hawamfahamu , unadhani ana haja gani ya kutengenezea nguo watu wa kawaida , ki ufupi muda huo hana ndio maana hajawahi kujitangaza”
Maneno yale yalimsahgnaza Salma , Fellini alikuwa mtu mzito kwenye ubunifu lakini kulikuwa bado kuna watu wa hadhi ya juu kuliko yeye, liishangaza zaidi na zaidi.
Tatizo hapo sasa sio swala la huyo anaeitwa mwalimu kushonea nguo watu wazito , tatizo ni kwamba Hamza alikuwa amevaa nguo ambazo zimetengenezwa na mtu huyo.
Regina na Linda hawakutaka kukubali kirahisi , kwani dakika chache zilizopita walikuwa wakibeza mavazi ya Hamza.
Walijikuta wote wakiangalia mavazi ya Hamza lakini bado yalionekana ya kawaida mno , aina ya mavazi ambayo unaweza ukayakuta katika soko la mtumba .
Regina alienda mbali na kukumbuka aligombana na Hamza kwa kutotaka kutupa mavazi yake , alishindwa kuzuia hisia mbaya zilizoanza kumvaa na kujiambia kama kweli anachosema Fellini ni kweli basi mavazi hayo ya thamani si yatamfanya aonekane mjinga na mshamba.
“Mr Fellini macho yako yatakuwa yanakudanganya , haya mavazi aliovaa unaweza kuyakuta kila mkoa ndani ya Tanzania yanauzwa”Aliongea Regina kuepusha kuabika.
“Msiniambie hakuna ambae anaona uzuri wa mavazi aliovaa Mr Hamza pamoja na pensi yake?”Aliongea huku akiwaangalia mmoja mmoja kana kwamba anaomba kuungwa mkono.
Lakini wote walitingisha vichwa vyao kukataa , hakuna cha maana kwenye hayo mavazi zaidi ya uchakavu tu”
“Nyie watu hamjui kabisa , nadhani kwasababu sio mafundi, katika ulimwengu wa kifundi utaalamu wa juu zaidi ni kutengeneza vazi ambalo unao uwezo wa kulirudisha upya kwa mchakato mwepesi sana na ukauza sokoni kwa bei ileile”Aliongea mzungu huyo lakini hakuna hata mmoja ambae alielewa anachomaanisha, hata Salma aliesomea Person chuo namba moja cha mitindo kutoka Marekani hakuelewa.
MWISHO WA SEASON ONE.
Unadhani Hamza ni nani mpaka kuvaa nguo zilizotengenezwa na George Alec Von Blumer fundi nguo wa wafalme , matajiri na watu wa hadhi ya juu.
Unadhani Hamza ana siri gani tokea kuokolewa kutoka kwenye janga la Radi mpaka kuwa nchini Tanzania akiwa mtu mzima.
Vipi kuhusu kitabu kinachowindwa na watu , vipi kuhusu lugha iliokuwa katika kitabu hicho ambayo hakuna binadamu anaeijua , unadhani ni kweli Hamza anao uwezo wa kuijua lugha hio, Frida anamaanisha nini kusema Hamza kuna kumbukumbu hazikumbuki.
Unadhani Binamu ni Cousin mtoto wa Mjomba au Shagazi au ni kitu kingine tofauti, vipi Sinagogi ni watu gani.
ITAENDELEA , WASILIANA NA MIMI WATSAPP KUJIUNGA GRUPU NAMBA NI 0687151346
 
Back
Top Bottom