Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Naomba kuelekezwa jinsi ya kutoa hichi kidude cha blue kwenye secreen kila nikiingia jf
 
Mfateni kwenye group lake la wasap, mbona huwa anatangazaga hapa
ni swala la mda2...siku mfkon zikiwemo lazima nimfate kulekule..maana jamaa ana madini ambayo yananifanya nipende kufuatilia kila simulizi yake...
 
ni swala la mda2...siku mfkon zikiwemo lazima nimfate kulekule..maana jamaa ana madini ambayo yananifanya nipende kufuatilia kila simulizi yake...
Hahahaa ila kumbuka ni stories tu hizo hakuna binadamu anayeishi kama jamaa anavowachoraga
 
Hahahaa ila kumbuka ni stories tu hizo hakuna binadamu anayeishi kama jamaa anavowachoraga
najua sana....ila kupitia hzo story kuna vitu tunajifunza...hata hvyo tunaburudika pia...but kusoma simulizi n hobby yangu..kwhy mwamba alete mwendelezo watu tuburudike plus refreshing our mind..
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR

SEASON 2.
Regina alienda mbali na kukumbuka aligombana na Hamza kwa kutotaka kutupa mavazi yake , alishindwa kuzuia hisia mbaya zilizoanza kumvaa na kujiambia kama kweli anachosema Fellini ni kweli basi mavazi hayo ya thamani si yatamfanya aonekane mjinga na mshamba.
“Mr Fellini macho yako yatakuwa yanakudanganya , haya mavazi aliovaa unaweza kuyakuta kila mkoa ndani ya Tanzania yanauzwa”Aliongea Regina kuepusha kuabika.
“Msiniambie hakuna ambae anaona uzuri wa mavazi aliovaa Mr Hamza pamoja na pensi yake?”Aliongea huku akiwaangalia mmoja mmoja kana kwamba anaomba kuungwa mkono.
Lakini wote walitingisha vichwa vyao kukataa , hakuna cha maana kwenye hayo mavazi zaidi ya uchakavu tu”
“Nyie watu hamjui kabisa , nadhani kwasababu sio mafundi, katika ulimwengu wa kifundi utaalamu wa juu zaidi ni kutengeneza vazi ambalo unao uwezo wa kulirudisha upya kwa mchakato mwepesi sana na ukauza sokoni kwa bei ileile”Aliongea mzungu huyo lakini hakuna hata mmoja ambae alielewa anachomaanisha, hata Salma aliesomea Person chuo namba moja cha mitindo kutoka Marekani hakuelewa.





SEHEMU YA 31.
Regina mara baada ya kuona haelewi alichomaanisha Fellini aliomba aeleze kwa lugha nyepesi, bado hakuwa amekubali nguo alizovaa Hamza ni za bei ya juu.
“Mr Fellini unaonaje ukituelezea kwa urahisi tupate kuelewa?”Aliongea na Fellini alimwangalia Hamza.
“Mr Hamza naomba ruhusa yako kushika nguo zako”
“Hakuna shida , ungeniambia vizuri ningekuelewa tokea mwanzo”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Salma nadhani utakuwa unajua ni malighafi za nguo za namna gani zimetumika”Aliongea akimpa ishara Salma kusogea karibu na yeye pia alishika lakini dakika ileile muonekano wake ulibadiika.
“Noble family material!!?”Aliongea Salma huku akishangaa.
“Correct, hii ni aina ya kitambaa cha SCUBA ambacho kiliongezewa ubora kwa mara ya kwanza nchini Ubelgiji na baadae kikawa kitambaa namba mmoja kinachotumiwa ndani ya Savile , ni aina ya kitambaa ambacho mchakato wa kukitengeza kuwa mgumu na ndio maana sio swala la hela tu kununua kitambaa hiki, sasa unadhani nguo yoyote ambayo imetengenezwa na aina hii ya kitambaa inaweza kuwa ya kawaida?”
Regina mara baada ya kusikia kauli hio alishindwa kujizuia na kusogea na yeye ili kugusa kitambaa hicho kwa umakini , ijapokuwa alishawahi kugusa nguo za Hamza mwanzo lakini ile kejeli juu ya nguo hizo hakuweza kuona kitu special.
Lakini muda huo alivyogusa nguo hio ki uchunguzi ndio sasa anagundua ni kweli kitambaa chake hakikuwa cha kawaida kabisa.
“Mnajua nini kimeongezewa upande wa hio michirizi ya pensi kushoto na kulia?, angalia kwa pembeni utaona ni kama inabadilika rangi kutokana na mwanga?”Aliuliza Fellini na wanawake wote waliangalia kwa kutumia angle ya macho na kuona ni kweli rangi ya nguo inabadilika, lakini hakuna ambae alikuwa na majibu.
“Ngoja niwaambie , ni nyuzi nyuzi za madini ya Platinum kutoka Afrika ya kusini, hii inafanya kitambaa chake kuwa cha thamani ya juu mno na adimu dunia nzima, gharama ya uzalishaji wa kutengeneza suruali ni Euro laki moja”Aliongea
Euro laki moja inamaana Hamza amevaa nguo ya thamani ya milioni mia tatu za kitanzania , Regina , Linda na Salma mara baada ya kusikia kauli hio walishindwa hata kupumua vizuri.
“Hey usiongee kwa nguvu , unataka watu wasikie na kuniwinda wanivue nguo nitembee uchi”Aliongea Hamza akimwambia Fellini.
Fellini alijikuta akigundua alikuwa na mzuka kiasi kwamba alikuwa akiongea kwa sauti na aliinamisha kichwa kuonyesha ishara ya kuomba radhi.
“Hilo ni la kwanza , kinachofuata na kutofautisha hizi nguo ni aina yake ya ushonaji”Aliongea na kisha alishika kola ya tisheti ya Hamza na kuinyanyua kwa juu.
“Nadhani mshawahi kusikia teknolojia ya Hermes ya ushonaji wa nguo za leather wanatuia SDD- stilt method , hii njia ya ushonaji mara nyingi inatumia sindano mbili kwa wakati mmoja na kufanya bidhaa yoyote ya kampuni ya Hermes ya Leather kuwa imara sana na kupendeza kwa wakati mmoja
Ukweli ni kwamba kati ya washonaji wengi , kuna mbinu ya kale ambayyo ipo karibu kupotea , inaitwa Concealment Saddle needle techinique, hii ndio mbinu ambayo Master George anatumia , lakini mpaka leo hii hata yeye mwenyewe hajabobea kuitumia kwa asilimia mia moja , mbinu hii inakupa nafasi ya kutumia nyuzi tatu katika uzi mmoja, hivyo kufanya nguo kuwa imara na kudumu kwa muda mrefu”Aliongea na Regina na Salma walisogea karibu kuangalia namna ya ushonaji ulivyokaa na kwa kuangalia tu waligundua mashine ya cherehani ni ngumu sana kufanikisha ushonaji huo.
“Hakuna ushonaji wa aina yoyote duniani unaoifikia hii mbinu , cha kufurahisha zaidi ukitaka kuifumua nguo yote kwa urahisi unagusa sehemu moja na unatoa nyuzi zote na nguo inarudi katika kitambaa na baada ya hapo inaweza kufanyiwa maboresho na kisha kurudishwa katika muonekano wake mpya”
Regina aliishia kukosa hiari na kuamini kabisa maamuzi yake ya wakati ule hayakuwa sahihi , lakini aliona pia Hamza alikuwa ni mshenzi sana , yaani mtu anavaa nguo ya thamani kubwa namna hio lakini anajifanyisha ni masikini tena mbaya zaidi anajifanyisha mtu anaependa sana hela.
“Hamza kwahio ni kweli unafahamiana na huyo Master Alec , kwanini hukusema?”Aliuliza Regina.
“Umesahau nilikuambia nguo hizi nilipewa na rafiki yangu , halafu sio kama uliniuliza ni rafiki gani?”Aliongea na kumfanya Regina kumwemwesa midomo , ilikuwa ni kweli hakuuliza ni rafiki gani.
“Wewe ni dereva tu , kwanini nguo zako zitengenezwe na mafundi wanaoshonea nguo wafalme , au umeziiba ndio maana umeshindwa kujua thamani yake?”Aliongea Salma.
Fellini mara baada ya kusikia kauli hio ni kama hata yeye wazo hilo lilimwingia , kwani ni ngumu mtanzania kama Hamza kuwa na nguo ambayo imetengenezwa na Alec , hata kama Hamza alionekana kuchanganya damu ya kizungu lakini bado ilikuwa ni ngumu kuamini, isitoshe swala la kuchanganya damu halikuwa la kushangaza sana , Waafrika wengi walikuwa wanaanza kupoteza rangi yao halisi kutokana na kuzaa na watu weupe, hivyo kumuona mtu mwenye muonekano wa Hamza sio swaa la kushangaza.
Leo hii unaweza kukuta watoto wa mtaani wenye muonekano wa kizungu na kiafrika au waarabu na waafrika.
“Sidhani ni sahihi kusema hivyo , maana ninazo nguo nyingine nyingi tu ambazo ametengeneza Alec?”
“Nani anajua , pengine uliiba furushi la nguo , kama una urafiki na mtu mkubwa kama huyo inakuwaje leo hii upo hapa Tanzanina , tena Dereva , si ulitakiwa uwe Ulaya huko?”Aliuliza Salma , hakutaka kukubali kabisa.
“Kwahio vipi msaidizi wangu kuwa dereva , kwahio siku hizi tunabaguana kwasababu ya mavazi?”Aliongea Regina , hakutaka kuona Salma anapandisha mdomo mbele ya Hamza.
“Regina haijalishi unachoongea , tena nimezidi kuwa na mashaka , kuna namna mmepanga bada ya kuhisi hamuwezi kushidana na kampuni yetu , hivyo mnacheza kamchezo ka kumfanya Fellini kukubaliana na nyie”
“Unaumiza kichwa chako bure kwa kufikiria sana , kama nilivyosema , sina mpango wa kushirikiana tena na Zara, tuondokeni”Aliongea Regina lakini muda ambao Regina alianza kupiga hatua kuondoka hapo alizuiwa na Hamza.
“Hamza , unafanya nini?”
“Msaidizi wako nimeitwa mwizi , unadhani tunaweza kuondoka hivi hivi?”Aliongea.
“Kwahio wewe sio mwizi?”Aliuliza Salma.
“Mr Hamza , je una ushahidi wowote wa kutuonyesha hizi nguo ni za kwako au unafahamiana na Master Goerge?”Aliuliza Fellini.
“Sasa hivi ni saa saba kasoro hivyo itakuwa ni Asubuhi London , nadhani Mzee Roboti muda huu atakuwa macho , ninaweza kumpigia simu”Aliongea
“Nini , unasema una namba ya Master?, wakati hata mimi sina”Aliongea Fellini kwa mshituko.
“Unaongea ujinga , kama hakutengenezei nguo , kwanini uwe na namba yake”Aliongea na kumfanya Fellini kukakamaa mwili , alikuwa akijisikia vibaya kana kwamba ameona mende.
Regina na Linda wote walikuwa na hali ya shauku na matarajio kwa wakati mmoja , upande wa Salma alikuwa na wasiwasi mno.
Hamza alitaka kutumia simu yake kupiga lakini alisahau kwamba ni kimeo hivyo alimwangalia Regina.
“Mkurugenzi niazime simu yako , siwezi kupiga kimataifa kupitia simu yangu”Aliongea na Regina alitoa Iphone yake na kumkabidhi Hamza na palepale aliingiza namba alizokariri na kupiga na ndani ya dakika chache tu simu ilipokelewa baada ya kuita.
“Who is it …”Sauti ya kingereza ya kizee upande wa pili ilisikika , ilikuwa nzito mno na lafudhi ya London na Hamza alitoa tabasamu mara baada ya kutambua sauti hio ambayo hajaisikia muda mrefu.
“Elmo , its me..”Aliongea Hamza upande wa pili kulikuwa na kimya kama cha sekude arobaini hivi.
“Do you finally rembember this lowly person!?”Sauti upande wa pili ilijibu na ndio dakika ileile Hamza aliweka simu aweze kusikia yeye tu ili wasije kusikia jina ambalo Alec anaweza kumuita.
Hamza asingejua namna ya kujieleza kama wangesikia Alec anamwita kwa cheo chake cha heshima.
“Mzee Roboti sio kama nimekusahau , mpaka sasa kila nilipokuwa ikivaa mavazi ulionipa kama zawadi nakukumbuka , ni miaka mingi lakini nguo zako bado nazivaa”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.
“Niheshima kwangu kufanya kazi na wewe na nilikuwa nikitegemea tuendelee kufanya kazi pamoja ila umepotea , nakumbuka wakati nakutengenezea hizo nguo ilikuwa ni miaka mitatu iliopita”Aliongea mzee huyo akionekana kama vile analalamika.
“Okey , Okey mzee nilikupa likizo kwanza ili ujali afya yako , lakini kwasababu unaonekana kuwa tayari kunitengenezea tena nguo basi nakupa ruhusa , nitakutumia anuani ya ninapoishi kwasasa , nadhani unajua ninachopendelea”
“Kweli !, nipo tayari kufahamu sehemu unayoishi kwasasa , najua umeondoka bila kuaga hivyo itakuwa siri yetu kama tunawasiliana”
“Mzee japo umezeeka lakini akili yako inafanya kazi vizuri , ninakuamini ndio maana nimeamua kukupigia”Aliongea Hamza huku akicheka, alikuwa akiongea kingereza na lafudhi yake ni kama vile amekulia jijini London.
“Mimi kama kijakazi wako lazima niwe na akili japo kidogo , vinginevyo nitaweza vipi kutimiza wajibu wangu wa kukuhudumia?”Aliongea.
“Sawa sawa , tuachane na hayo kwanza , nimekupigia leo kwasababu kuna baadhi ya mambo nataka unisaidie kuyaweka sawa”Aliongea Hamza.
“Usisite kabisa kuniambia , nipo tayari kufanya chochote , hata kama nikuhatarisha maisha yangu”
“Sio swala kubwa sana , usiwe na wasiwasi , je kuna mwanaume anaefahaika kwa jina la Fellini kati ya wanafunzi wako ?"Aliuliza Hamza na wakati huo alikuwa akimwangalia Fellini.
Muda huo Fellini uso wake wa kizungu ulikuwa umepauka na kulikuwa na viashiria vya jasho katika paji la uso wake , alikuwa akijiuliza kama kweli Hamza aliekuwa akiongea nae ni Master Alec , Hamza mwenyewe atakuwa ni nani
Salma na yeye alikuwa aking’ata lipsi zake huku akiwa amekunja ngumi , alionekana kuwa na wasiwasi mno.
“Mkurugenzi ni kweli anafahamiana na huyo mtu mzito , mbona naona kama anatufanyia magizo?”Aliuliza Linda.
Upande wa Regina yeye alikuwa katika kuwaza na aliishia kutingisha kichwa ,huku akishindwa kuongea neno, alijiambia atajua baada ya matokeo.
Lakini muda huo mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda kasi mno , alijiambia kama ni kweli basi koneksheni ya Hamza ni kubwa mno kama vile yupo ndotoni.
“Felini!?, Oh nimemkumbuka sasa , Fellini ni mwanafunzi aliekuja akiwa mdogo katika duka langu kwa ajili ya kujifunza kushona, lakini hakuweza kudumu sana maana moyo wake ulikuwa haujatulia sehemu moja , ijapokuwa alikuwa na kipaji lakini hakuwa na Ari ya kuja kuwa mshonaji mkubwa hivyo aliondoka , kwanini unamuulizia , Mshonaji kama Fellini ni wa daraja la pili na hana hadhi ya kuandaa nguo zako”Aliongea.
“Hamna mzee, sijakutana nae kwa ajili ya kunitegneenea nguo , nimekutana nae kwa bahati mbaya na ameweza kugundua maazi yangu wewe ndio umeyatengeneza, ila haamini amesema mimi mwizi”
“Nini!!, anakitafuta kifo , tafadhari bwana wangu naomba usiwe na hasira juu ya tabia ya Fellini , nitamwambia Eric amfukuze , mtu kama yeye hawezi kutuingiza kwenye mgogoro na wewe , kama bado hutoridhika unaweza kumfanya chochote nitaandaa maelezo”Aliongea na kumfanya Hamza kutamani kucheka kutokana na namna Alec alivyopaniki.
“Ndio maana nakuita Mzee Roboti unaishi kikanuni sana , haina haja ya kupaniki , sina mpango wa kumfanya chochote , nitampatia simu uongee nae , ninachotaka ni wewe kumthibitishia tunafahamiana , usiongee zaidi kuhusu mimi , nadhani umenielewa”Upande wa pili kimya kilitawala.
“Sawa sawa , najua nini chakufanya”Alijibu na Hamza alimpatia Fellini simu.
Upande wa Fellini mikono ilikuwa ikimtetemeka , ilimchukua sekunde kadhaa mpaka kupokea simu hio kutoka kwenye mikono ya Hamza.
Hakuwahi kuongea na mwalimu wake huyo kwa zaidi ya muongo mmoja,sasa wazo la kuona kwamba anakwenda kuongea na mwalimu wake huyo mtu mzito sana ndio maana alikuwa na hofu.
“Nice to talk to you , Master Alec”Aliongea Fellini kwa kitetemeshi lakini upande wa pili hakukuwa na jibu.
“I heard from Eric that you’re now quite famous outside ?”Sauti upande wa pili iliongea na palepale Fellini ni kama vigoti vinamlainika
“Hapana Master ,Mimi ni kivuli cha Sir Eric tu , nimekosea Master naomba radhi”Aliongea na upande wa pili ilionyesha ni kiasi gani Alec alikuwa amekasirika.
Muonekano aliokuwa nao Fellini ulimfanya Salma ambae alikuwa pembeni kushangaa mo , Mbobezi maarufu wa ulimwengu wa fasheni amebadilika na kuwa kama piritoni hivyo kwa kuongea na mtu kwenye simu
Regina na Linda na wao walikuwa sasa washaamini mtu ambae anaongea na Fellini ni kweli ni huyo Alec mweye hadhi ya juu.
“Sikiliza wewe mtoto , mtu uliekutaa nae huwezi kumwita mwizi , ukimfaya akasirike basi hutonilaumu tukikutoa kwenye circle yetu na umaarufu wako kupotea , nadhani unajua ninachomaanisha”
Fellini alikuwa na hofu mno , alikuwa akijua maneno ya Alec sio ya kumuogopesha tu , ukweli ni kwamba kauli yake moja tu hawezi kuwa na umaarufu aliokuwa nao , alijua nguvu iliokuwa nyuma katika fasheni ya mavazi ilitawaliwa na watu kama Alec.
“Master usiwe na wasiwasi , najua nini napaswa kufanya”Aliongea.
“Mrudishie simu”
Fellini alimwangalia Hamza kama vile ni kiongozi wa heshima na jambo hilo liliwashangaza zaidi Regina , Linda na msaidizi wa Alec, upande wa Salma muonekano wake ulikuwa mbaya mno , maana kile kinachoendelea ni kama matusi kwake .
Hamza aliongea na Alec kwa dakika kama mbili hivi na kisha alikata simu na kumrudishia Regina.
“Sasa nadhani kila mtu amethibitisha nguo hizi ni zangu , Mkurugenzi , tunaweza kuondoka sasa”Aliongea Hamza.
Regina alijihisi ni kama yupo ndotoni na aliishia kutingisha kichwa huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi.
Upande wa Fellini aliona haiwezi kuwa nzuri kama atamuacha Hamza aondoke akiwa na kinyongo.
“Mr Hamza nakiri ilikuwa ni ujinga wangu , hivyo naomba msamaha wako , kama ningejua na wewe ni mmoja ya watu wa kampuni ya Dosam nisingesita kufanya nao ushirikiano, naomba unipe nafasi ya kurekebisha makosa , nipo tayari kampuni ya Zara kushirikiana na Dosam Group”
“Mr Fellini huwezi kufanya hivi , tushakubaliana kampiuni zetu zinaenda kushirikiana”Aliongea Salma kwa hasira.
“Miss Salma, hakuna mkataba wowote tuliosaini kati yetu , hivyo siwezi kusema kuna makubaliano ya kufanya kazi pamoja , baada ya kufikiria kwa kina nimeona kampuni ya Dosam inaweza kukuza hadhi yetu”
“Kwanini unaenda kinyume na maneno yako?” Aliongea Salma huku akiona swala hilo ni kama udhalilishaji, lakini Fellini alimpotezea kabisa.
“Kama nilivyokwisha kujitambulisha, mimi ni msaidizi tu , unapaswa kuongea na Mkurugenzi akikubali sina neno”Aliongea Hamza.
“Miss Regina naomba mazungumzo yetu yaanze upya , naomba kuona mipango yenu”Aliongea mara baada ya kupata ruhusa.
Upande wa Regina alikuwa asharudi katika hali ya kawaida akiuzima mshangao wake na alimwangalia Salma kwa macho ya uchokozi na palepale alichukua mkataba ambao ulikuwa umeshikiliwa na Linda na kuuchana mbele yake.
“Cooperation is fine , but we need to redesign the cooperation proposal”Aliongea akimaanisha ushirikiano hakuna shida lakini wataenda kuandaa upya vipengele.
Fellini aliishia kuangalia chini , kwa wakati huo Regina alikuwa na Upperhand , hivyo ni kama yeye ndio anaomba ushirikiano na kampuni ya Dosam na sio Regina kumuomba yeye ushirikiano., Regina alishaliona hilo hivyo alitaka kubadilisha vipengele ili kuinufaisha kampuni yake.
“Hakuna shida, nipo tayari kusubiri kwa siku kadhaa”Aliongea Fellini , hakuwa yule mwenye ratiba iliobanana tena.
Hamza alimwangalia Regina kwa macho ya kuridhika , alimuona Regina kama mwanamke ambae akili yake inafanya kazi kuendana na hali kwa haraka , hali ya mazungumzo ya kibiashara imebadilika hivyo hakutaka kwenda na mkataba uleule.alitaka kubadilisha mbinu ili kujinufaisha.kitaalamu alimuona Regina kama mwanamke ambae sio mzembe kabisa likija swala la fursa.
Kwa vyovyote vile Kampuni ya Zara lazima ishirikiane na Dosam kama Fellini anataka kulinda hadhi yake katika ulimwengu wa fasheni.
Fellinni aliwasindikiza kabisa Hamza na Regina mpaka kwenye gari yao na kuwafungulia mlango huku akiwa na heshima kubwa .
Upande wa Salma alimwangalia Hamza kwa macho yenye ukali mno na kisha aliondoka bila hata ya kuaga.
“Mr Fellini huna haja ya kuwa hivi , ijapokuwa leo sijafurahishwa na namna tulivyoanza lakini nimeridhika na matokeo”Aliongea Regina.
“Ili Mradi Mkurugenzi umeridhika , hakuna tatizo kabisa , natarajia kufanya kazi na Dosam kwa miaka mingi”
“Kama hakuna lingine tunaondoka”Aliongea Hamza.
“Mr Hamza tafadhari subiri kidogo , najua nimekukosea leo , naomba uniwie radhi , kama kuna mahali ambapo hujaridhika tafadhari naomba uniambie nitarekebisha”
“Usiwe na wasiwasi , ili mradi kila kitu kitaenda sawa mimi sina shida , nitakusaidia pia kukupigia chepuo kwa Alec “
“Thank you so much, you are so magnanimous”Aliongea na muda huo Hamza alikumbuka aliachaga nguo kwenye hilo gari.
“Mkurugenzi , hivi zile nguo zangu bado zipo humu?”
Regina muonekano wake ulikuwa na hali ya kukosa utulivu na alinyoosha mkono nyuma na kutoa ule mfuko , mwanzoni alitumia nguo hizo kumdharau Hamza lakini dakika chache zilizopita zimegeuka kuwa hazina.
Hamza alichomoa shati kutoka kwenye mfuko huo na alivyolinusa lilinuka jasho kali mpaka akakunja sura, lakini katika macho ya Fellini alionekana kuwa katika mchangao.
“Unaweza kuchukua hizi nguo , chukulia kama zawadi kutoka kwangu kwa kuingia makubaliano ya kibiashara”Aliongea Hamza na kumkabidhi mfuko wote Fellini aliepokea kwa mikono miwili.
Hamza hakuwa na wasiwasi na nguo tena , alishaahidiana na Alec angeletewa nguo nyingine mpya
Mtu yoyote angeona shati ambalo Hamza amemkabidhi Mzungu Fellini wangesema huyo mzungu ni kichaa.
“Mr Hamza asante sana kwa ukarimu wako, nitaweka nguo hizi sehemu salama kabisa nikirudi” Aliongea Fellini, alipanga kuzifanya nguo hizo kama sehemu ya maonyesho ofisini kwake , ili kutukuza uwezo wa Master Alec katika swala zima la ushonaji.
Isitoshe Master Alec alikuwa ametengeneza kwenye maisha yake nguo nyingi sana lakini sio watu wengi ambao washawahi kuona nguo yenye muonekano wa kawaida kama hio lakini ya thamani , Rare things are priceless.Aliwaza Alec.
Kwa furaha mazungumzo yao yaliisha hivyo na Hamza aliendesha gari kurudi nyumbani.
Linda ambae alifika na gari yake aliweza kuangalia gari ya Regina ikitokomea huku akiwa na muonekano usioelezeka , katika macho yake kulikuwa na hali flani hivi ya kukata tamaa.
******
Upande mwingine ndani ya jiji la London ilikuwa ni asubuhi karibia maeneo yote , Uingereza haikuwa kama nchi ya Marekani ambayo ina Time Zone zaidi ya nne, pengine ni kutokana na udogo wa kijiografia wa nchi hii yenye maendeleo makubwa sana katika nyanja zote.
Katika mtaa wa Savile Row mwanaume mzungu mzee hivi mwenye nywele nyeupe pamoja na miwani alionekana akishuka katika ngazi katika moja ya jengo kwa kukimbia, alikuwa amevalia shati jeupe na Vest nyeusi.
“Erice, John”Mwanaume yule aliita kwa nguvu.
Dakika hio hio mwanaume bonge mzungu alijitokeza akiwa ameambatana na mwanaume mwingine kimbau mbau ,wote walionekana katika umri wa iaka hamsini hivi na walikuwa wameshikilia vitambaa.
“Mwalimu , una maagizo yoyote”Yule bonge ndio aliitwa Erice na ndio alieuliza.
“Wote nyie acheni kazi zenu zote kwa sasa na mnifuate , nahitaji kutengeneza nguo nyingi suti na suruali”
“Mwalimu , bado hatujamaliza kutengeneza nguo za Mfalme wa Hispania na Prince wa Wales, sidhani kama tunaweza kukusaidia”Aliongea John.
“King or Prince let them all wait, For the past week, we have served one lord” Aliongea akimaanisha Mfalme au mwana mfalme wote wasubiri. kwani kwa wiki za nyuma walikuwa wakihudumia bwana mmoja tu.
“Mwalimu unamzungumzia bwana gani?”Erice aliuliza.
“Seraph”Aliongea Alec huku akigusa gusa kifua chake.
Erice na John mara baada ya kusikia jina hilo moja kwa moja walielewa ni mtu gani anaelengwa na wote kwa pamoja walikakamaa huku wakitamka kwa juu “Divine Wrath”








SEHEMU YA 32.
Kwa zaidi ya dakika ishirini au therathini hivi hakuna aliemuongelesha mwenzake , Regina alidhania Hamza angempa sababu japo kidogo tu ya kutuliza shauku yake , alitamani kusikia hata kisingizio tu pengine angeelewa lakini licha ya hivyo Hamza alikuwa akiendesha huku akipiga ukimya.
“Huna kitu chochote cha kuniambia?”Aliuliza Regina baada ya kukosa uvumilivu na kumfanya Hamza kuangalia kioo cha nyuma.
“Ni kweli asubuhi nilikuwa na dharula muhimu , ningechelewa kidogo kungekuwa na tatizo , alikuwa ni mteja wangu alienipigia , sikutaka kumpotezea”Aliongea Hamza lakini Regina hakuwa hata na haja ya kusikiliza hizo porojo.
“Sitaki kusikia kuhusu hilo , kwanini hukuniambia unafahamiana na huyo Master Alec?”
“Ah.. Unamzungumzia mzee Roboti , kwanini nimzungumzie sasa bila sababu?”
“Wakati ule nilikuambia ukatupe mavazi yako lakini ukang’anania kubaki nayo , kwahio ulikuwa ukinikejeli kisirisiri kwa kuwa mshamba sio , unaonekana kabisa umeisubiria kwa hamu hii siku kwa ajili ya kuniumbua mbele za watu, sasa hiivi nadhani unajichekea mwenyewe moyoni kwa raha zako”Aliongea huku akionyesha kinyongo.
“Regina unaongea nini , sikufikiria sana wakati ule ni kwamba tu nimezoea haya mavazi ndio maana, ni zawadi kutoka kwa mzee , isingekuwa vizuri kuyatupa ilihali aliweka moyo wake wote kwenye kuyatengeneza”
“Basi niambie wewe na huyo Master Alec mnafahamina vipi?”
“Nilikutana nae Shardland Bar huko Uingereza kipindi flani hivi cha mwaka mpya na ndio tulianza kuongea kwa kubishana na urafiki wetu ukaanzia hapo”
“Unaniona mjinga , unadhani naweza kuamini huo uongo , mbona unapenda kuniona kama kichekesho?”
“Ananiona mjinga huyu sijui yukoje , yaani mtu amemtisha Fellini vile lakini sasa hivi anasema amekutana nae bar “Aliwaza Regina huku akiwa na hasira kali.
Muda uleule wakati washafika Kigamboni Hamza alisimamisha gari pembeni na kumshitua Regina aliekuwa kwenye mawazo.
“Wewe .. unafanya nini?”Aliuliza lakini Hamza hakujibu zaidi ya kufungua mlango na kutoka nje na kutembea upande wa madukani, Regina na yeye hakutaka kukaa ndani ya gari , alishuka na kumfuata huko huko na kufanya watu kumkodolea macho kutokana na urembo wake.
Baada ya kumfikia Hamza alimuona akiwa amesimama mbele ya Freezer akichagua Ice Cream za Bakhresa na alichukua yenye Strawberry na kumpa Regina ambae aliipokea bila kupenda.
“Unafanya nini sasa?”
“Mrembo maswali mengi ya nini , huoni hio ni Ice Cream”Aliongea na muda huo Hamza alichukua na ya kwake ya ukwaju na kisha akaenda kulipa na sasa hapo ndio Regina alijua kumbe huyu mwehu kaja kununua Ice Cream.
“Acha kusimama hapo twende , tumeegesha gari sehemu mbaya , hata kama una hela huwezi vunja sheria za barabarani”Aliongea Hamza na kumshitua Regina ambae alikuwa kwenye mshangao.
“Nani kakuambia nina shida ya Ice Cream , jali mambo yako”
“Kama hutaki ilete basi ninao uwezo wa kula zote mbili kwa pamoja”Aliongea Hamza akijaribu kumpokonya lakini Regina alipindisha mkono mbali.
“Unasema huitaki , nataka kuichukua unaktaa , nyie wanawake ni viumbe wa ajabu sana”
“Unasemaje wewe…”Aliuliza Regina lakini Hamza alijifanyisha mjinga na kumuacha Regina akiwa amesimama
Wateja baadhi na watu wauza maduka waliishia kutabasamu , kwani walionekana kama wapenzi.
Hamza mara baada ya kuingia garini aliliwasha na kupiga honi na kumfanya Regina kwa hasira kukimbilia na kuingia.
Baada ya wote kuingia kwenye gari na Hamza kulirudisha kwenye barabara aliendesha kwa mkono mmoja huku mwingine ukishikilia Ice Cream , Regina hakuuliza tena swali , aliona hata akiuliza kusingekuwa na majibu hivyo alijikaliza zake kimya , huku akila Ice Cream kwa kutumia kijiko
Kama alivyosema Hamza wanawake hawaeleweki , Kwa Regina ilikuwa hivyo hivyo kulikuwa na wanaume kibao ambao washawahi kumtongoza kwa kumpatia zawadi kama vile magari , vito vya thamani na ahadi kibao , lakini kitendo cha Kununuliwa Ice Cream ndio zawadi ya thamani ya juu iligusa moyo wake.
Wakati wanafika nyumbani Shangazi alikuwa sebuleni akiangalia TV, na hata walivyoingia hakuweza kuwaona.
“Shangazi unaangalia nini , mpaka kuwa siriasi hivyo?”Aliuliza Regina.
“Taarifa ya habari , wanasema kumekuwa na mauaji mfululizo ya wanawake ndani ya jiji la Dar es saalam na muuaji hafahamiki hivyo wanaasa raia kuwa makini, Regina uwe makini , ukitoka kazini hakikisha uwe na Hamza pembeni yako , wakati wa mchana usitoke peke yako pia”
Hamza aliangalia taarifa hio ya habari na alishangaa na kuona namna muuaji alichokuwa akifanya , tofauti na kuua tu alikuwa pia akikata maeneo nyeti ya wanawake kama vile manyonyo na ngozi, yalikuwa mauaji ya kikatili mno.
“Muuaji wa namna hii muda si mrefu atakamatwa , shangazi huna haja ya kuwa na wasiwasi sana”
“Natamani wakimuona wampige risasi wamuue kabisa , jamani mtu anaua watu wasio na hatia kikatili namna hio , tena wasichana wadogo”Aliongea Shangazi na muda huo huo kengele iligonga ikionyesha kuna mgeni.
Shangazi alienda kufungua mlango wa geti na alishangaa baada ya kuona ni Polisi.
“Ndugu polisi kwanini…”
Walikuwa ni Polisi wanne wote wakiwa katika sare zao za kipolisi , aliekuwa mbele alikuwa na uso ulichongoka na mweusi Tii.
“Mama hapa ni nyumbani kwa Regina Wilson?”
“Ndio , upo sahihi , mnamtafuta?”
“Naitwa Afande Mlonga kutoka kituo cha polisi mjini kati idara ya uchunguzi , kuna kesi inayomhusu Regina Wilsoni na tupo hapa kwa uchunguzi”
Muda uleule Regina alikuwa ashatoka nje baada ya kuona Shangazi harudi na mara baada ya kuona ni polisi alimwambia shangazi awaruhusu.
Polisi wale walikaribishwa mpaka ndani sebuleni huku wakiangaza angaza kulia na kushoto kwa namna ya kuchunguza uzuri wa jumba hilo kabla ya kukaa kwenye sofa.
Shangazi kwa haraka hraka alikimbilia friji na kuwaletea maji kama walivyoomba , lakini alikuwa na wasiwasi mno kiasi cha mikono yake kutetemeka.
Afande Mlonga macho yake yalikuwa kwa Hamza tu , ni kama alikuwa akimchhunguza , upande wa Hamza alikuwa zake bize akitafuna ma’apple’.
“Miss Regina naomba kuuliza huyu Mr hapo ni nani kwako?”Aliongea Mlonga na swali lile lilimfanya Regina kusita lakini kutokana na uwepo wa Shangazi aliamua kuongea.
“Ni mpenzi wangu”
Baada ya kujibu hivyo Afande Mlonga na wenzake ni kama hawajatarajia jambo hilo.
“Tulisikia habari nyingi unaenda kuolewa na mtoto wa Mzee Benjamini , hatukutarajia kuona tayari una Boyfriend”
“Naona taarifa zangu zinazagaa sana lakini hili linanihusu mimi na yeye , sikuona haja ya kuliweka wazi, sidhani kama ni kosa?”
“Hakuna mgongano wowote baada ya hili na familia ya Mzee Benjamini?”Aliuliza Mlonga huku wakionyesha kunakiri majibu.
“Nyie wote ni polisi , sidhani ni vizuri kuuliza maisha yangu binafsi”
“Usituelewe vibaya Madam , ni kwasababu kilichotuleta hapa kina uhusiano na maisha yako binafsi”Aliongea na muda uleule Afande Mlonga aliweka picha chini , zilikuwa ni za gari ya Regina.
“Hili gari limesajiliwa kwa majina ya Regina Wilsoni ambapo tunaamini wewe ndio mmiliki halali , juzi limeonekana katika kijini cha Wavuvi Zinga bagamoyo na Dereva aliekuwa akiendesha gari hio ni moja ya mhangwa wa mauaji.. wakati wa kurudi gari ilikuwa ikiendeshwa na huyu mwanaume ambae umesema ni Boyfriend wako”Aliongea huku akiweka picha ya Hamza akiendesha gari hio hio na gari ikiendeshwa na mwanamke, alikuwa ni Corresa.
Regina mikono yake ilicheza na bila hata kujijua alihikilia sketi yake , akiwa na wasiwasi, mwanamke aliekuwa kwenye picha alimfahamu ni moja ya watekaji.
“Kwahio amekufa?”
“Kwanini unauliza , inamaana hujui kama amekufa, tunaamini watu wote waliokufa walikuwa ndani ya gari lako”
Regina aliishia kugeuza kichwa chake na kumwangalia Hamza lakini upande wa Hamza hakuonyesha wasiwasi kabisa , lakini kwake aliona hio kesi sio nyepesi, baada ya kufikiria kwa muda Regina aliona aeleze moja kwa moja kilichotokea.
“Nilitekwa siku hio , lakini sikujua watu wale walikuwa ni wakina nani maana walikuwa ni raia wa kigeni , nilikuwa sina fahamu na pale niliposhituka nilikuwa nishaokolewa tayari na Hamza , kuhusu watu hao kufa sikuwa nikijua chochote”
“Kwahio unamaanisha huyu Mr Hamza ndio aliekuokoa na baada ya hapo akawaua hawa wahalifu?”
“Ma afande mnakosea , sijaua mtu , mimi nilienda nikawapa kichapo tu , sidhani kama mnaweza kunilaumu kwa hilo”Aliongea Hamza lakini Regina aliona hali inazidi kuwa mbaya na alitaka kutumia nguvu yake hivyo alisimama.
“Afisa mna ushahidi wowote wa kuonyesha Hamza ndio aliewaua?”
“Usipaniki Madam , hata kama Mr Hamza ndio aliehusika sio kosa , kwasababu hawa wahalifu ni kama Mr Hamza tu , lakini tunahitaji kuchunguza hili swala, tunataka kujua imekuwaje Mr Hamza akawa na uwezo wa kuua hawa wahalifu wa daraja la juu , wanaosakwa dunia nzima”
“Mimi ni mwanafunzi wa chuo na fundi , nina nguvu nyingi hivyo mapigano yalikuwa makali sana , lakini sijua mtu”Aliongea Hamza.
“Mr Hamza tunakuahidi hatutokutia hatiani kwa kuuwa hawa watu , tunachotaka kujua ni kilichotokea katika mazingira ya kirafiki tu”AliongeaMlonga huku akiwa na tabasamu bandia.
“Kama mnao ushahidi wa kutthibitisha niliwaua basi nitawaelezea kilichotokea , lakini ushahidi hamna na mpo hapa mnanijaribu siwezi kuwaambia chochote”
Polisi hao walijikuta wakiwa kimya , alichoongea Hamza kilikuwa na ukweli ,hata hivyo kesi haikuwa chini yao , baada ya kesi hio kutolewa ktuoka kitengo cha MALIBU na kuhamishiwa idara ya polisi Afande Mlonga ndio alipewa kazi ya kuongoza uchunguzi , lakini licha ya kupata picha hakukuwa na alama za vidole zinazomlenga moja kwa moja Hamza ndio alifanya mauaji.
“Afande Mlonga kama hakuna ushahidi siwezi kukubali mpenzi wangu kusingiziwa , kama kuna ambacho nitaweza kufanya kwasasa ni kumshirikisha mwanasheria wangu ili muongee nae yeye , hivyo naomba muondoke nyumbani kwangu na mkatafute Warantt kwanza”
“Madam , mpaka sasa nadhani umeona taarifa ya habari inayohusisha muuaji anaeua wasichana wadogo kwa kuwakata viungo vya siri , unadhani ni salama kwako kukaa na mtu ambae humjui vizuri”
“Chunga maneno yako afande , chochote utakachoongea bila ushahidi nitakushtaki nacho”Polisi wengine walitaka kuongea lakini Afande Mlonga aliwazuia.
“Kama ni hivyo basi hatuna haja ya kukaa zaidi na tutaondoka , ila kama kuna ushahidi tutarudi”Aliongea na kisha wote kwa pamoja walitoka nje.
“Regina nini hiki kinaendelea , ulitekwa?”Shangazi ndio aliekuwa akiuliza huku akionekana kuwa na maumivu ya moyo.
“Shangazi sikufanya makusuti kutokukuambia , sikutaka kukufanya kuwa na wasiwasi , lakini lishaisha”Aliongea na Shangazi aliishia kuvuta pumzi huku akijikalia kwenye sofa.
“Asante Mungu angalau amekukutanisha na Hamza angalau anaweza kukulinda, ningefanya nini mimi kama ningekuwa peke yangu”Aliongea Shangazi akijituliza lakini wakati huo Regina alimwangalia Hamza kwa macho ya kuchukia.
“Sijui kama umeua au hujaua , lakini hili swala linapaswa kuisha ukiwa hujaua”Aliongea.
“Haha.. Regina asante sana kwa kunijali”
“Eti kukujali , sitaki kuhusika katika hili ndio maana , nina kazi nyingi za kufanya”Mara baada ya kuongea hivyo kwa hasira alipandisha juu huku akifunga mlango kwa nguvu.
Upande wa Shangazi alimwangalia Hamza kwa macho yenye umakini mkali , ni kama kuna kitu anakitafuta.
“Hamza hukupata tatizo?”Aliuliza.
“Shangazi usiwe na wasiwasi ni swala dogo na lishaisha”Aliongea na Shangazi alitingisha kichwa kuelewa.
“Naona unatafuna sana matunda , kama hamjala mchana niwaandalie chochote”
“Hakuna shida shangazi”
*****
Upande mwignine mara baada ya mafande wale kutoka walisogelea gari ya Land Cruiser na kuingia ndani , kulikuwa na watu wawili ndani ya gari hio tayari , mmoja akiwa dereva na mwingine akiwa ni mwanaume mnene hivi mwenye kitambi aliekaaa nyuma.
“Kanali , tumemaliza mahojiano nae , lakini mambo yamekuwa magumu kuliko tulivyotarajia”Aliongea Mlonga akimwambia yule mzee aliekuwa kwenye gari.
“Nini kimetokea?”
“Amekataa yeye kutohusika kabisa , cha kushangaza sio dereva wala mlinzi tu ni Mpenzi wa bosi Regina”
“Nini , mpenzi!!, Sio James tena”
“Hata sisi tumeshangaa , inaonekana kuna kinachoendelea , lakini sidhani kama kinahusiana na hii kesi”Aliongea Mlonga na kumfanya mwanaume alieitwa Kanali kufikiria kidogo.
“Mlonga nakuamini uwezo wako wa kumjua mtu kwa kumwangalia tu , wewe unamuonaje , unadhani ndio aliehusika kuua watu hatari kama wale?”
“Dastani sijui hata namna ya kumuelezea , ukiachana na ushombeshombe wake nimemuona kama mtu wa kawaida sana… lakini kuna kitu sio cha kawaida nimekiona”Aliongea.
“Kitu gani mmekiona?”
“Hakupaniki kabisa , ni kama vile alitarajia ujio wetu na wala hakuonyesha kukasirika hata tulivyomwambia ameuwa watu wale , ki ufupi hakuonyesha kuwa na wasiwasi wakati tunamuuliza maswali, lakini ukiachana na hilo sioni kama ni mtaalamu , anaonekana kama vile ni mfanyakazi wa kawaida tu wa kwenda kazini na kurudi nyumbanni kuangalia TV”Aliongea na Kanali Dastani alionekana kuwaza.
“Kanali hii kazi haiwezi kuwa rahisi kama ikiendelea kuwa chini ya Idara ya polisi , Kitengo cha MALIBU kina kila rasilimali ya kufanikisha hili”Aliongea Mlonga.
“Unadhani hatujui kuhusu hilo , unadhani kwanini sikutaka kuambatana na nyie moja kwa moja kwenda kufanya mahojiano nae , hizi ni taratibu za kitengo pia katika hatua za ki uchunguzi”
“Mkuu unamaanisha na nyie mnaendelea na uchunguzi kimya kimya?”
“Mlonga licha ya kwamba upo vizuri kwenye mahojiano lakini kuna baadhi ya sehemu haupo vizuri , Ni lini ushawahi kuona MALIBU wakimhoji raia moja kwa moja , tunatumia idara ya polisi kufanya kazi hii , hivyo mlichofanya ni kutimiza wajibu wenu na sisi tutatimiza wajibu wetu”Aliongea na Mlonga alitingisha kichwa kukubali
“Ila Kanali kama kweli ndio amehusika na mauaji ya maninja kutoka Ufilipino basi ni mtaaamu wa hali ya juu na atakuwa ameficha ushahidi wa sisi kumfikia , hivyo uchunguzi chini ya idara yetu utakuwa mgumu kweli”
“Kama unahisi hivyo , basi atakuwa haogopi hata tukiwa na ushahidi kuna kinachoniambia sio wa kawaida”Aliongea moja ya polisi akitoa mchango wake.
“Kama ulivyosema ni sahihi , unadhani kwanini hakukuwa na alama yoyote hata ya vidole tu kuonyesha yeye ndio muuaji , alionekana kuwa makini , hata kama ameonekana kwenye gari ashajiandaa namna ya kujitetea”
“Kanali kwanini tusimkamate moja kwa moja , kuna uwezekano akawa na uhusiano na mauaji ya wanawake yanayoendelea”
“Hatuwezi kwenda moja kwa moja kwenye hitimisho , iwe yeye ndio muuaji au sie kama polisi mnapaswa kuendeleza uchunguzi wetu na kuwe na ushahidi , muuaji lazima akamatwe na haya ni maagizo kutoka juu , mkitimiza wajibu wenu na sisi wa kwetu kazi itakuwa rahisi , Mlonga hili lipo juu yako na timu yako, Ondoa gari napaswa kwenda kuripoti makao makuu”Aliongea Kanali na gari iliendeshwa muda uleule.
Nusu saa tu Kanali Dastani alikuwa akiingia katika kitengo cha MALIBU makao makuu , na alipiga hatua zake kana kwamba hataki kufanya watu wajue amefika.
Hakuelekea moja kwa moja katika ofisi ya mkuu wake bali alienda moja kwa moja katika ofisi yake , alitaka kukusanya ripoti kamili kabla ya kuiwasilisha.
Siku kadhaa nyuma alipewa kazi ya kuhakikisha anajua ni nani aliehusika katika kuuwa wale raia wa kigeni na kazi hio alikuwa ameifanya kwa uadilifu mkubwa mpaka kumpatia majibu aliokuwa akitaka.
Mara baada ya kufika katika ofisi yake aliingiza nywira katika tarakishi yake na palepale ilionekana Vidio ambayo ilionekana ilikuwa ikicheza lakini ikasitishwa kwa muda.
Kanali mara baada ya kukaa kwenye kiti aligusa batani na palepale Vidio ile ilianza kuonyesha Kapteni Yonesi akipigana na Master Konki na kudhibitiwa na ghafla tu Hamza anaingilia na kumuadhibu Master Konk.
Aliichezesha kwa kuirudisha mbele na nyuma kwa zaidi ya mara tano na alionekana kufikiria kitu.
Baada ya kukaa kwa muda katika ofisi yake , ujumbe wa meseji uliingia kupitia watsapp na alipoona jina lililomtumia ujumbe huo alifungua haraharaka na alikuta kuna kiambatanisho cha nyaraka iliokuwa katika mfumo wa PDF.
Kwa haraka haraka aliihamishia kwenye tarakishi yake na kisha akaigeuza nyaraka ile kwa kuiprint, kadri alivyokuwa akiisoma ndio jinsi uso wake ulivyojikunja.
“Hamza ndio muhusika , nina uhakika asilimia mia moja , kabla ya ripoti ngoja nikutane na Yonesi kwa siri kwanza”Aliongea na kisha palepale alizima tarakishi yake na kuchukua karatasi alioprinti na kujiandaa kutoka lakini muda uleule simu yake iliiita na alipoangalia jina lilisomeka Dokta Bensoni.
“Bensoni’Aliongea mara baada ya kupokea.
“Amosi amerudiwa na fahamu nusu saa iliopita” sauti ilisikika na kufanya moyo wa Kanali Dastani kudunda.
“Nakuja sasa hivi Dokta , mdunge kwanza sindano ya usingizi?”
“Kuna tatizo Dastani”
“Tatizo gani?”
“Nimefanya kupigiwa simu baada ya kurudiwa na fahamu , lakini nafika hospitalini Amosi hayupo”Aliongea na Kanali Dastani palepale uso wake ulikunjamana.
“Unamaanisha nini Bensoni”
“Ametolewa hospitalini na haieleweki amepelekwa wapi , ki ufupi Amosi ametoweka”
“Fu**ck , unanitania Bensoni , Amosi anatoweka vipi ndani ya hospitali ya jeshi”
Kanali Dastani hakuwa hata na muda wa kumfikiria tena Yonesi , aliona analo swala muhimu zaidi la kushughulika , hofu ilimvaa , kama Amosi ametoweka bila ya kupata maelekezo yake kuna hatihati familia yake inaweza ikawa mashakani , lazima Amosi atakuwa anafikiria kulipa kisasi kwa kumsaliti.
****
Hamza hakuwa hata na wasiwasi juu ya polisi waliofika hapo , mawazo yake yalikuwa siku ya kesho wapi anamtoa out mpenzi wake Eliza, ki ufupi hata swala la Frida hakulitilia maanani kabisa.
Sio kama hakuwa na uzoefu , ukweli ni kwamba pengine Eliza anaenda kuwa mwanamke wake wa kwanza kuwa nae katika mahusiano yenye usiriasi.
Hamza aliona kabisa amekuwa mzembe , kitendo cha mrembo Anitha wa chuo kumkataa ilithibitisha kabisa alikuwa mzembe na mvuto wake umeshuka , hivyo alitaka kujua namna ya kumpagawisha Eliza.
Baada ya kuwaza kwa muda alienda mpaka chumba cha kujisomea cha Regina na aligonga mlango na kuambiwa aingie na mara baada ya kuingia Hamza alianza kuangalia vitabu vilivyokuwa kwenye Shelf bila ya kuongea.
“Wewe unafanya nini?”Aliuliza Regina , wakati huo aliwaza Hamza alifika kwa ajili ya kuelezea kwanini wale watekaji walikuwa wamekufa lakini anaanza kuchunguza vitabu vyake.
“Naangalia kama nitaona kitabu cha kunifaa hapa”
“Naona umekumbuka kuwa ni mwanachuo , kitabu gani unataka?”
“Hehe.. kinachohusiana na mapenzi”Aliongea na kauli ile ilimshangaza Regina.
“Yaani hakuna kitabu cha maana unachotafuta zaidi ya vitabu vya kipuuzi namna hio?”Aliongea kwa hasira.
“Nataka kujifunza namna mapenzi yanavyoendeshwa , jinsi vitu vya kumfanyia mpenzi wako akolee bila ya kumhonga , kuna haja gani ya kukasirika hivyo bosi?”
Mapenzi!, Regina hakujizuia na kuwaza au Hamza anataka wawe wapenzi kweli , baada ya wazo hilo aliona aibu za kike na kugeuka.
“Sina hivyo vitabu , unaweza kuondoka”Aliongea akiwa siriasi.
“Kama huna ngoja nikatafute mtandaoni, nilijua pengine na wewe una shauku ya mapenzi yalivyo”Aliongea Hamza na kisha alitoka nje.
Regina mara baada ya Hamza kutoka alijikuta akivuta pumzi nyingi , mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi mno kana kwamba amekutana na Simba mkali , alijikuta akishika uso wake na kuona umepatwa na joto.
“Mjinga huyu , kuna haja hata ya kusoma kwenye kitabu..”Aliwaza.
Baada ya kukaa akifikiria kwa muda alishika tarakishi yake na alisita kwa muda lakini alijikuta akiingia mtandao wa Google na kuandika , How to fall in love.
*****
Asubuhi kama kawaida Hamza aliamka mapema na kucheza mdundiko nje katika mpangilio maalumu , na baada ya kunywa chai alibadili katika mavazi mapya kabisa alionunuliwa na Regina.
Wakati akishuka kutoka chini Regina alikuwa sebuleni akiangalia taarifa ya habari kupitia CNN.
“Regina nadhani leo hakuna kazi yoyote , si ndio?”
“Ndio huna kazi ya kufanya leo , vipi unatoka?”Aliuliza na kumwangalia Hamza namna alivyopendeza.
“Ndio , nitatoka leo siku nzima , msinihesabu chakula cha mchana wala usiku”
“Unaenda wapi , kwenye kazi zako za ufundi kama kawaida , kama ni kazi ninazo nyingi tu unaweza kunisaidia”Aliongea Regina huku maneno yake akiwa hana uhakika nayo , alijua Hamza alikuwa na koneksheni kubwa hivyo hata hela lazima alikuwa nazo sasa alijiuliza kwanini anasoma chuo , kwanini aliishi maisha ya kimasikini kama vile hana hela.
“Wewe usinipe kazi ,nimepndeza vyote hivi niende kufanya kazi tena za nini, nina mtoko na mtoto mzuri leo , hivyo bosi leo ni siku yangu usinipigie simu”
Regina mara baada ya kusikia kauli hio , alijikuta akinywea lakini alibadilika dakika hio hio.
“Haina haja ya kuripoti una mtoko na mtoto mzuri”
“Haja ipo , tunaishi ndani ya nyumba moja na mimi ni mfanyakazi wako , sitaki itokee dharula nikiwa nakula bata uniambie nirudi nitamkera mpenzi wangu , lakini hata hivyo usiwaze sana , mpango wangu ndani ya miezi mitatu ikiisha sitotaka kuchelewa kuondoka hapa hata kwa sekunde, ila kwasasa nitahakikisha jambo letu linaendelea kuwa siri “
“Sina haja ya kujua kama una mpenzi hayo ni maisha yako ungeondoka zako tu bila kuniaga , kuna haja gani ya kuniambia”Aliongea Regina kihasira na kutupa Rimoti kwenye sofa na kupandisha zake juu.
Hamza aliishia kukuna kichwa chake na kujiambia kwani kosa lake ni lipi hapo , yeye kaomba ruhusa kwa bosi ni kufuata itifaki, hakutaka itokee anakula maisha na mrembo Eliza mara Regina anapiga wakutane.
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU .

MTUNZI: SINGANOJR

SEHEMU YA 33.
Hamza aliona hakuwa na uhusiano wowote na Regina zaidi ya mkataba tu hivyo hana kosa , mara baada ya kuwaza hilo moyo wake ulijaa amani tele , na alizipiga hatua kutoka ndani ya nyumba hio kwenda nje.
Japo Regina ana magari mengi lakini hakutaka kutumia gari , isitoshe anapoishi Eliza ni wilaya hio hio na Eliza ana gari.
Baada ya kutoka mji huo wa kisasa wa Egret alichukua boda ambayo ilienda kumuacha nje ya jengo la Apartment za Lotus na aliruhusiwa kuingia moja kwa moja.
Alipishana na warembo kadhaa lakini hakuwa na habari nao na moja kwa moja alienda kusimama nje ya mlango wa Apartment ya Eliza na kisha alibonyeza Kengere.
Ilichukua dakika kama moja na nusu hivi mpaka kufunguliwa na Hamza alishangaa kumkuta mrembo huyo akiwa katika nguo za kulalia tena na Mask usoni, alishangaa maana sio kitu alichotarajia , alijua muda huo pengine Eliza atakuwa ashajipodoa na kupendeza tayari.
Eliza baada ya kuona aliekuwa mlangoni ni Hamza na alikuwa ametoka kulala alitimua nduki kurudi ndani na kuingia moja kwa moja bafuni.
“Eliza mbona unakimbia?”
“Mbona umekuja mapema hata kuniambia kwa simu ,, bado sijajiandaa”Sauti ya Eliza ilisikika kutoka bafuni.
Hamza alisogelea mlango wa bafuni na kisha alianza kuinama kutafuta upenyo wa kupiga chabo.
“Haina shida , ni mzuri hata wakati wa kuamka”
“Naonekana kama zombie , hebu kakae sebuleni usinichungulie”Aliongea huku akifunga mlango wa bafuni vizuri na Hamza alirudi zake sebuleni kukaa.
Baada ya kufika hapo ndio aliweza kuona nyaraka kibao zimesambaa kwenye meza na wazo la Eliza kufanya kazi usiku kucha licha ya kuwa wikiendi lilimvaa, pengine ndio maana amechelewa kuamka, Hamza hakuona ni jambo baya , pengine Eliza alifanya hivyo kwa ajili ya kumaliza viporo vyote ili kupata amani wakati wa kutoka out pamoja, alijikuta akitoa tabasamu.
Baada ya nusu saa Eliza alitoka bafuni , ule mpauko wa uso ulimfanya avutie mno.
“Endelea kunisubiri nivae nguo haraka haraka”Aliongea huku akikimbilia chumbani na kufanya Hamza kuishia kumeza mate na uvumilivu ulimshinda na kumfuata huko huko , alitaka kuona urembo wa Eliza wakati akibadili mavazi.
Lakini sasa ile anafika mlangoni ni kama Eliza alishitukia Hamza angemchungulia na alirudi mlangoni kwa ajili ya kuuloki na hapo ndio alipoiona sura ya Hamza ikiwa imekodoa macho.
“Wewe muhuni , ukiendelea hivi tutaachana ujue”Aliongea huku akimkodolea macho na Hamza alisimama vizuri na kuweka nguo sawa.
“Umenielewa vibaya nilikuwa nataka kwenda chooni ,nimekosea mlango ..”Hamza alijibaraguza lakini Eliza hakuwa hata na muda wa kumsikiliza kilichosikika ni mlango kubamizwa kwa nguvu huku ufunguo ukizungushwa kwa ndani na kumfanya Hamza kwa masikitiko kurudi kwenye sofa.
Baada ya kukaa kwenye sofa kwa zaidi ya dakika ishirini uvumilivu ulimshinda tena na kujiambia au hizo nguo zinamshinda kuvaa maana muda unaenda mno , lakini dakika ambayo anataka kugonga mlango hatimae ulifunguliwa.
Eliza nywele zake zilikuwa zimechanwa vizuri huku eneo la mbele zikipindishwa kidogo na ule weusi wake wa chocolate ulimfanya kuvutia mno , Hamza alikosa hiari na kuwaza ndio maana mtu kama Zefa alitaka kumbaka, Eliza alikuwa mrembo na urembo wake unahitaji ukaribu zaidi.
Alikuwa amevalia kitopu cha rangi ya kijani isiokolea cha maua maua, huku kikiwa na mistari flani hivi upande wa mabega , chini sketi ya rangi ya Dark Bluu iliovuka magoti lakini yenye kuacha wazi miguu ya bia.
Utofauti wa Eliza na wanawake wa kileo ni muonekano wake wa kiutu uzima licha ya sura yake kumpunguzia hio sifa , licha ya kwamba alikuwa akivaa kama wale waimba kwaya lakini alivutia mno.
Eliza alijikuta akiwa na furaha kwa namna ambavyo Hamza alikuwa akimwangalia kwa mshangao , hakuwahi kuweka juhudi kwenye kujivalisha kama hivyo kwa muda mrefu , alivyokuwa single hakujali sana.
“Hamza tuondoke sasa nishamaliza”Aliongea mara baada ya kukohoa kidogo kusafisha koo.
Hamza alijikuta akicheka kidogo na kisha kumsogelea Eliza na kumshika mkono.
“Tutaanza na chakula cha mchana kwanza , nimepata eneo tulivu kwa ajili yetu”Aliongea Hamza.
“Mh , chakula cha mchana mapema yote hii?”Aliuliza na kumfanya Hamza kukuna kichwa.
“Sasa Babe ni wapi unataka twende kwanza ?”
“Nataka kwenda kumsalimia mama kwanza , Daktari anaesimamia wodi ya Sanatorium alinipigia jana , amesema kuna kitu anataka tuzungumze , pili nataka mtu wa kwanza kuniona nikitoka out na mpenzi wangu ni Mama , nataka aone nimeshatoka kivulini na sasa nipo tayari kuyakaribisha maisha mapya”Aliongea na Hamza upande wake aliona sio wazo baya , ijapokuwa mama yake alikuwa katika hali ya kutoweza hata kuongea lakini alikuwa ni mama yake na lazima angefurahi kuona binti yake hapotezi maisha yake kumhudumia yeye tu na ana mpenzi sasa.
“Hakuna shida , tukishamaliza kumsalimia mama yetu tutaenda kula chakula cha mchana”
“Mama yetu?!”Aliongea Eliza huku akiona aibu za kike.
“Ndio ni mama mkwe , kuna tatizo?”
“Unajiaminisha sana , unadhani nimekukubalia moja kwa moja wakati ndio tunaanza kuwa wapenzi”
“Sawa bibie , vyovyote vile nitahakikisha anakuwa mama yetu”Aliongea Hamza kwa kujivunia na wakati huo walishatoka tayari na E.liza kufunga mlango na kuingia kwenye lift.
Baada ya kufika maegeshoni ya magari, Eliza alikuwa na gari nzuri sana , ilikuwa ni mali ya kampuni lakini kwa wakati huo ni ya kwake kwani sio kwamba angeacha kufanya kazi ndani ya Dosam leo au kesho, isitoshe cheo chake kinapanda siku hadi siku na ni mchapakazi mzuri , ilikuwa ni Sedan, Toyota Crown Camry Silver Mettallic.
Hamza ndio aliekuwa dereva , isitoshe Eliza alikuwa amevalia High heels hivyo ingekuwa ngumu kuendesha, uzuri ilikuwa ni upande huo huo wa Kigamboni na kadri walivyokuwa wakienda mbele ndio walivyoingia kwenye eneo lenye miti mingi ikiwemo Miarobaini(Neem tree).
Jua lilikuwa la saa tano lakini ni kama la saa saba na kufanya eneo kuwa na harufu ya kuungua kwa majani ya miti.
Baada ya Eliza kumuonyesha sehemu ya kuegesha gari , hatimae wote walitoka.
“Mazingira ya hapa naona sio mabaya na hili eneo naona ni jipya kabisa,si utakuwa unalipa kiasi kikubwa cha pesa kumuweka mama yako hapa?”
“Hii ndio sehemu nzuri zaidi Dar nzima kwa huduma ya watu wasiojiweza, nalipia jumla ya milioni sitini kwa mwaka”
“Milioni sitini , hizo zote ni hela zako tu?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.
“Baba ni mstaafu na yupo kijijini kwa sasa akiendeleza maisha na kiinua mgongo chake cha ualimu , sikuona haja ya kumpa mzigo kumuuguza mama , usiwe na wasiwasi nimemhamishia mama hapa mara baada ya kupanda cheo na kuwa meneja wa idara ya mauzo, mshahara wangu sio mdogo , ukijumlisha na posho ninazopata”
Aliongea na Hamza aliona huyo mrembo alikuwa na majukumu makubwa mno ya kifedha, kwa haraka haraka aliamini lazima mshahara wake wote anatumia kumuuguza mama yake , jambo ambalo sio baya lakini yeye kama mwanaume alimuonea huruma.
Wote waliingia kwenye jengo hilo la ghorofa , kulikuwa na lift pana mno ya kutosha kitanda cha mgonjwa , baada ya kufika floor ya nne walitoka na kwenda moja kwa moja kwenye chumba alichokuwepo mama yake Eliza.
Baada ya kuingia ndani ya chumba hicho kulikuwa na vitanda viwili , vyote vilikuwa na wagonjwa ambao walikuwa katika hali ya Vegetative, walimkuta nesi pia ambae mara baada ya kumuona Eliza alitoa tabasamu na aliandika vitu flani kwenye Cardboard yake na kisha akaondoka kuwaacha.
Hamza aliweza kumuona mama ambae sio mtu mzima sana , aliekonda upande wa kushoto na alijua bila ya kuambiwa ni mama yake Eliza maana walionekana kufanana rangi.
“Mama, mwanao nimekuja kukuona”Aliongea Eliza akiwa amekaa kwenye kitanda akishika kwa namna ya kupangusa paji la uso wa mama yake.
“Naomba unisamehe mama yangu , nimekuwa bize wiki hii kazini ndio maana sikupata muda wa kuja kukuona , usikasirike mama…”Aliongea huku macho yake yakianza kugeuka mekundu , mama huyo hakuwa amefumba macho alikuwa akiona lakini hakuwa na uwezo wa kuongea.
Hamza aliamua kukaa kwenye sofa la mtu mmoja huku akimwangalia Eliza na mama yake , hakutaka kwenda moja kwa moja alitaka Eliza yeye ndio amtambulishe.
Eliza alitumia muda mwingi kumwambia mama yake kila stori iliomjia akilini na mambo yanayoendelea nyumbani na baadae alimgeukia Roma.
“Mama nimekuja leo na mpenzi wangu , nimepata mpenzi mama anaitwa Hamza , ni mhuni kidogo lakini anajua kunilinda , kwanzia sasa mama usiwe na wasiwasi , nina mwanajeshi pembeni yangu…”
Baada ya kumtambulisha Hamza hatimae alirudi katika hali yake ya kawaida akizima majonzi yake.
“Naenda kuonana na daktari , vipi nisindikize?”Aliuliza na Hamza alitingisha kichwa bila hiyana , hata yeye alikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini dokta anamtafuta Eliza , alitaka kujua kama kuna tatizo ili aweze kusaidia.
Walitoka kabisa nje ya jengo hilo na kwasababu ilikuwa jumapili , wafanyakazi wengi hawakuwepo na kufanya eneo kuwa kimya mno.
Jengo la madaktari lilikuwa upande wa pili na walitembea katikati ya barabara hio yenye maua mpaka katika jengo hilo na kusimama katika mlango uliokuwa na bango CHIEF PHYSICIAN OFFICE na Eliza aligonga.
“Dokta Maonga..”Aliongea Eliza kiheshima akimsalimia mwanaume aliekuwa na umri wa makadirio ya miaka theratini na tano kwenda arobaini hivi , alikuwa amevaa miwani ya macho na alikuwa na uwalalaza , ila alipendeza kwa namna alivyozichana nywele zake , alionyesha kujipenda.
“Eliza umefika, karibu”Aliongea na muda huo mara baada ya kuiona sura ya Hamza uso wake ulijikunja.
“Huyu ni…”
“Ni rafiki yangu , nimekuja nae”Aliongea Eliza , alitaka kusema ni mpenzi wake lakini aliamua kuwa makini.
Upande wa Dokta Maonga aliweza kuona kuna kitu hakipo sawa , lakini alijitahidi kuweka muonekano wake wa kitaaluma.
“Kumbe ni rafiki yako , lakini maongezi ya leo ni ya siri , hivyo itakuwa vizuri huyu bwana akitembea tembea kuona mazingira ya hospitali yetu”Aliongea na mara baada ya kusikia hivyo Eliza alijisiikia vibaya kidogo.
“Hamza nisame..”
“Usijali Eliza , ngoja ninyooshe nyooshe miguu , nipigie simu ukishamaliza”Aliongea na Eliza aliishia kutingisha kichwa tu.
Mara baada ya Hamza kuondoka Maonga alimkaribisha Eliza na baada ya hapo alifunga mlango kwa ndani.
“Dokta nini kimekufanya kuwa makini sana kuhusu afya ya mama?”Aliuliza Eliza lakini Dokta Maonga alisogelea kwanza Dispenser na kumimina maji kwenye glasi.
“Usiwe na wasiwasi Eliza , nitakuelezea taratibu taratibu , kunywa kwanza maji”
“Asante Dokta”Eliza alikuwa na kiu , kutokana na haraka alishindwa hata kukumbuka kunywa maji.
“Kiua tatizo juu ya afya ya mama yangu?”Aliuliza mara bada ya kumaliza kunywa maji yote.
“Mgonjwa Ratifa Mlowe amekuwa katika hali ya kutojitambua kwa zaidi ya miaka miwili sasa , uwezekano wa yeye kupona ni chini ya asilimia tano , nafikiri..”
“Dokta hata kama ni asilimia moja , siwezi kumkatia tamaaa mama , kama unataka hela zaidi nipo tayari kulipa lakini naomba usiache kumtibu”Aliongea Eliza kwa kubembeleza.
“Bila shaka tupo tayari kutumia fursa hii lakini kama ujuavyo kuna hospitali chache sana ndani ya taifa hili ambazo zimejikita katika kuhudumia wagonjwa wasiojiweza , kikawaida kutokana na asilimia chache za Ratifa kuamka ilitakiwa ndani ya mwaka mmoja awe amesharudishwa na kuugulia nyumbani na kusubiria wakati wa Mungu kumchukua”
“Lakini Dokta wakati namleta mama hapa ulinihakikisha kutakuwa na matibabu ya hali ya juu ambayo yatamuwezesha mama kuamka , inamaana hukumaanisha”
“Usinielewe vibaya , uwezekano huo upo lakini mpaka sasa tunapokea wagonjwa wengi sana na wengi wameomba nafasi katika wodi zetu , tukisema tukuruhusu mama yako aendelee kutibiwa hapa , itahitajika malipo makubwa zaidi ya mwanzo”
“Hayo malipo yatakuwa ni kiasi gani?”Aliuliza Eliza, hakuwa tayari kuona mama yake anarudishwa nyumbani kwenda kusubiria kifo chake , hata kama kulikuwa na asilimia moja ya matumaini alitaka kuishikiria hio hio.
Dokta Maonga aliishia kunyanya kidole hewani na kuchora namba na Eliza macho yalimtoka.
“Milioni saba kwa mwezi!!?”
Eliza alijikuta akipagawa , kiasi hicho kilikuwa sawa na mshahara wake wote ukiondoa posho , ijapokuwa alikuwa katika nafasi ya juu ya kampuni lakini hakuwa kama Regina ambae ni Mkurugenzi maana yeye hakuwa na hisa kama wafanyakazi wenzake , wakati wenzake wakinunua hisa za kampuni kama njia ya uwekezaji yeye alikuwa akimuuguza mama.
“Hapo tu haitoshi kwani lazima nikaombe kwa wakubwa kumuacha mama yako aendelee na matibabu , wanataka wagojywa wanaobaki wawe angalau na asilimia ishirini na tano za kuamka”
Eliza hakujua kwanini lakini mara baada ya kusikia hio namba saba , kichwa chake kilikuwa kikimzunguka, lakini baada ya kufikiria kidogo alipata wazo.
“Hata kama ni hio hela nitalipa tu ili kumuacha Mama aendelee na matibabu”Aliongea lakini kwa Dokta Maonga alionyesha ishara ya ajabu.
“Ukweli ni kwamba kuna namna ya kuokoa kiasi hicho cha pesa na utaendelea kulipia milioni nne kwa mwezi kama kawaida”Aliongea na Eliza aliona sio wazo baya.
“Ni njia gani hio?”Aliuliza na Maonga palepale alinyanyua mdomo wake na kutoa tabasamu la ajabu , alisimama kutoka kwenye kiti chake na kumsogelea Eliza
“Eliza unajua tokea mara ya kwanza na kutia machoni nilikuona mwanamke mrembo sana , tena unaendana na mimi vizuri”Aliongea huku akinyoosha mkono wake kutaka kumshika Eliza lakini mwanamke huyo aliwahi kushituka na kusimama.
“Dokta naomba usifanye hivi … nipo tayari kulipia kiasi ulichonitajia lakini sio hili”
“Eliza kama unataka mama yako kuendelea kutibiwa hapa ni kheri utulie na kukubali ombi langu”
“Wewe… kwahio unamtumia mama kuni…”Eliza alijihisi kichwa chake kikianza kuwa kizito mno huku kizunguzungu kikimvaa na macho yalianza kujfiumba yenyewe bila ridhaa yake.
“Haha.. vipi tena , naona unataka kusinzia?”Muda uleule ndio sasa Eliza aliangalia kikombe alichotumia kunywa maji na kuhisi tatizo.
“Umeniwekea dawa kwenye maji?”
“Hehe.. ndio ili usishituke niliweka dawa nyingi maji yote , lakini dozi yake inatosha kukufanya usinzie , usiwe na wasiwasi kabisa , mpaka muda utakaoshituka kila kitu kitakuwa kimemalizika”
Eliza moyo wake ulianza kujawa na majonzi huku akijihisi kuwa dhaifu kutokana na ukali wa dawa aliowekewa ,hakuamini dokta kama huyo anaweza kufanya kitendo cha namna hio, lakini hata hivyo aliona sio wa kumlaumu Dokta Bensoni pia alionekana kama mtu wa heshima kwake lakini mwisho wa siku alimuomba rushwa ya ngono.
Eliza alijiona kama mwanamke mwenye mikosi na hapo hapo machozi yalianza kumbubujika , katika maisha yake alipona chupuchupu kubakwa mara nying , pengine jaribio la siku hio linakwenda kuwa mara ya tano katika maisha yake.
Alijikuta akilegea na kwenda kukalia sofa bila ya kupenda , muda huo Dokta Maonga alikuwa na tabasamu la ushindi na aliingiza mkono kwenye koti lake la kidaktari kutoa simu.
“Ni muda wa mzee Gabusha kutimiza ahadi ya upande wake”Aliongea huku akiwa haamini anakwenda kupokea hela nyingi.
Lakini sasa kabla hajafanya chochote mlango wa chumba hiko ulipigwa teke na kufunguka kwa nguvu, japo ulikuwa umefungwa kwa ndani lakini loki zake zilipinda na ukafunguka.
Kitendo kile kilimshitua Dokta Maonga kiasi cha kudondosha simu chini na mara baada ya kuona ni Hamza alijikuta akipandwa na hasira.
“Wewe.. unathubutu..”
“Dakika ambayo umeniona nikifika hapa ulionekana kutoridhika na ujio wangu kana kwamba nimeingilia mpango wako , kila ulichokuwa unakiwaza kilikuwa kimejiandika kwenye uso wako , unadhani ingekuwa ngumu kwangu kutokukushitukia”Aliongea Hamza.
“Hamza… naomba unisaidie…”Eliza alikuwa ndio anasinzia , alimuona Hamza lakini alidhani ni kama anaota.
“Lala tu usiwe na wasiwasi , nitakulinda”Aliongea Hamza huku akiwa na uchungu moyoni, ukweli hakuwa hata na haja ya kumruhusu alale maana ilikuwa ndio sauti yake ya mwisho kabla ya kupotelea usingizini.
Dokta Maonga baada ya kuona kitumbua kimeingia mchanga aliangalia mlango na kitendo cha Hamza kuangalia pembeni aliusogelea kwa spidi , lakini Hamza anamwachaje akimbie kwa mfano.
Ile anapiga tu hatua alikuwa ashainua mguu na kumpiga eneo la kigoti cha mguu na kilichosikika ni’ kacha’.
“Arghhh…!!”
Maonga alijikuta akipiga ukulele huku akikaa chini na kidogo tu apoteze fahamu maana maumivu hayakuwa ya kawaida.
“Nisamehe , Bwana mdogo naomba usiniue nina familia”Maonga alijikuta akibembeleza ili kujiokoa katika hali hio , lakini Hamza hakutaka kumuacha alimpiga teke lingine na kumvunja mguu mwingine na alipotaka kuzimia Hamza alimshika shingo kwa nguvu.
“Umeweka nini katika maji uliompatia mpenzi wangu?”
“Hapana … ni vidonge vya usingizi .. uwiii miguu yangu , naomba usinipige tena”Aliongea huku mwanaume akitokwa na machozi mfufulizo.
Hamza alijikuta akivuta pumzi ya ahueni , aliona angalau huyu mhuni hajatumia dawa ambayo haieleweki la sivyo mambo yangekuwa magumu.
Hamza alichukua simu ya Maonga iliodondoka chini na kisha aliitoa nywira na kwenda moja kwa moja upande wa Vidio rekodi.
“Nataka ujirekodi kila kitu ulichofanya kupitia hii simu , vipi unajiona upo tayari au niongeze kidogo maumivu?”
Hamza hakutaka kumuua , wala pia hakutaka itokee Maonga kuja kumshitaki hivyo aliona atengeneze ushahidi kabla ya kuondoka hapo.
“Una chaguzi mbili tu , ya kwanza ni kuongea kila kitu ulichofanya na pili nipigie simu polisi na nikufungulie kesi ya ubakaji, hivyo fikiria kipi ni nafuu kwako”
Maonga alijua chochote atakachochagua hakuna namna anaweza kulipiza kisasi , lakini vilevile alitamani kumtaja Mzee Gabusha kama ndio alimpa kazi hio lakini hakuwa tayari kwa hilo , alijua nguvu ya Gabusha anaweza akawa hai ndio lakini ni rahisi kupotezwa na Gabusha muda wowote, hivyo aliona bora achague chaguo la kwanza pengine akipona anaweza kuendelea kuwa daktari huku akipata fidia kutoka kwa Gabusha.
Alikuwa na akili mno , alikuwa na familia hivyo akili yake ilikuwa ikicheza, hakuwa na jinsi na alielezea mwanzo mwisho mpango wake wa kutaka kumbaka Eliza kupitia matatizo ya mama yake.
Hamza mara baada ya kuridhika alituma ushahidi huo katika Email yake na akamchukua Eliza kimyakimya na kumuingiza katika gari.
Bila ya watu kushitukia kinachoendelea aliweza kutoka ndani ya gari na kuingia ndani ya jengo la hospitali , akiwa na mpango wa kutafuta dawa ya kumumsha Eliza haraka iwezekanavyo ili waendelee na mtoko wao.
Bahati ilikuwa kwake baada ya kufika katika chumba cha dawa mlango ulikuwa umerudishiwa tu na aliingia haraka haraka na kutafuta baadhi ya dawa na pamoja na sindano na kutoka nazo.
Alirudi kwenye gari na kisha alifyonza maji katika kijichupa na kuchanganya na unga unga kisha alivuta na kumwingizia Eliza kwenye mshipa wa damu kutumia sindano.
Kwa jinsi alivyokuwa akifanya Hamza utadhani ni daktari mzoefu wa miaka mingi , alionekana kujua kile alichokuwa akifanya.
Eliza alikuwa amelala mpaka anatoa sauti lakini alionyesha dalili ya jasho hivyo Hamza alimwegamiza vizuri kwenye siti na kumtoa kibanio cha nywele na baada ya hapo alirekebisha ubaridi wa gari, nusu saa kupita hatimae Eliza alifumbua macho kivivu.
Bado dawa ya usingizi ilikuwa kali hivyo alikuwa akiona ukungu tu , kwa dakika tano hatimae akili yake ilirudi katika hali ya kawaida na kukumbuka kilichomtokea na alikaa kitako kwa mshituko na kuangalia pembeni.
“Hamza imekuwaje nikafika kwenye gari , kidogo tu ni…”
“Usiwe na wasiwasi tena , yule mpuuzi nimempa kibano lakini sijamuua”Aliongea Hamza na mara baada ya Eliza kusikia hivyo alijikuta akihema kwa nguvu akionyesha ahueni.
Lakini mara baada ya kuwaza kilichotaka kumtokea hali ya woga iliamza kumvaa na kadri alivyokuwa akifikiria ndio macho yake yalivyoanza kuwa mekundu na ghafla tu alianza kulia kwa kwikwi.
“Eliza usilie sasa , hili limeisha”Aliongea Hamza akijaribu kumfariji.
“Asante , asante sana kwa kuniokoa mara nyingine , lakini vipi kuhusu mama yangu mimi , nini kitampata mama kwa staili hii”
Wazo la kuona mama yake akikosa matibabu sahihi moyo ulizidi kumuuma.
Hamza hata yeye hakufikiria hilo lakini alijikuta akiwaza kwa mdua namna ya kufanya.
“Eliza usiwe na wasiwasi , kuna daktari namfahamu na uwezo wake sio mbaya sana , unaonaje tukimchukua mama na kumrudisha nyumbani kwanza na kumtafutia mtu wa kumhudimia na nitawasiliana na huyo dokta , akifika atamwangalia au ikishindikana tutamsafirisha moja kwa moja nje ya nchi”
“Una rafiki ktuoka nje ya nchi ambae ni dokta, na yeye anahusika na ugonjwa kama wa mama?”
“Sijui ila anaonekana kama Dokta wa magonjwa yote , ni MD hata kama hajui jinsi ya kutibu lazima atakuwa anafahamu madokta wenye uwezo”Eliza alitaka kuongea neno lakini alisita mara baada ya kuona sindano na mabomba ndani ya gari.
“Hizi sindano ndio ulinichoma nazo , sio kama umenitingisha nikaamka?”
“Ndio nimekuchoma , wewe unadhani ungemka mapema hivi?”
“Kwahio unajua kumchoma mtu sindano?”
“Mimi ni dokta ndio tena wa moyo , mambo ya kushika kisu na kumchana mgonjwa kwangu rahisi sana , nikishamaliza kumpima kama hivi kazi inaanza taratibu , shwa , shwaa!!”Hamza alikuwa akifanya utani huku akijifanyisha anampima Eliza mapigo ya moyo kumbe anashika nyonyo, ila kitendo kile kilimfanya Eliza kuficha kifua chake.
“Unamdanganya nani hapa , eti daktari, mateja tu wanajua kujichoma sindano , unadhani nadanganyika kirahisi”
“Sawa bwana kama huniamini”
“Kwahio umenichoma dawa gani na umezitoa wapi?”Aliongea huku akinyanyua vijichupa vya dawa vilivyokuwa kwenye siti.
“Nizitoe wapi tena wakati mimi sio Dokta , niliziiba wakati wakiwa bize na simu zao , hii hapa sijui wanaiita Benzo nini huko ila kazi yake ni kupoza nguvu ya vidonge vya usingizi “
“Vipi kuhusu hii nyingine?”Aliuliza
“Hio ni Mannitol “
“Kazi yake?”Aliuliza na kumfanya Hamza kusugua pua yake.
“Eliza unaonaje tukienda kula kwanza , unaonekana una njaa”
“Acha kubadilisha topiki , niambie kwanza hii dawa kazi yake?”
“Ni nzuri kwa afya yako , kwanini unauliza sana?”
“Kama ni nzuri kwangu niambie kazi yake nini?”
“Kuhusu hio.. basi ngoja nikuambie , vipi kwanza hujisikii mkojo kukubana”
“Labda wewe ndio mkojo umekubana , niambie kazi ya hii dawa acha kuzunguka zunguka”
“Hio ni dawa ya kukufanya ukojoe ili kupunguza sumu mwilini”
“Kwanini umenipa dawa ya kunitoa mkojo wakati tupo date”Aliongea Eliza huku akimpiga piga Hamza na kumfanya acheke.
“Usinipige bwana , nilikuwa na wasiwasi , kama usingemka mapema kuna uwezekano ungejikojolea , bahati nzuri umewahi kuamka”Eliza alitaka kumpiga lakini alihisi mafuriko yakijikusanya na aliishia kusugua meno kwa hasira.
“Nitakushikisha adabu nikirudi, ngoja uone”Aliongea na kisha alifungua mlango na kutimua nduki kwenda chooni kama mwanariadha.
Wakati wa kurudi alishindwa kuzuia aibu aliokuwa nayo.
“Babe naona sasa umekaa sawa , haha ..tuendelee zetu na mtoko sasa , tunaanza kula kwanza”
“Nitakusamehe leo kwasababu umeniokoa , ila siku nyigine ukinichoma sindano zisizoeleweka , sikuongeleshi tena”Aliongea na Hamza hakutaka kurefusha hilo jambo hivyo alikubali kwa kutingisha kichwa.
Kabla hajawasha gari wazo lilimjia palepale na aliinama kuelekea upande wa Eliza na kisha alichomoa mkanda wa siti.
Eliza alijua kuna kitu Hamza anataka kumfanyia , lakini mara baada ya kuona ni mkanda wa gari alijikuta akipumua kwa ahueni.
“Nitafunga mwenyewe”
“Tulia hivi hivi , jana nimekula shule ya mapenzi mtandaoni na wamesema ukimsaidia mpenzi wako kufunga mkanda unajinyakulia pointi za mapema sana , ni namna ya kuonyesha unajali”
Kauli ile ilimfanya Eliza kujikuta akicheka mpaka basi.
“Vipi kama mpenzi wako hataki kufungwa mkanda?”
“Hapo ndio pagumu sasa maana walinihakikishia kabisa nitajinyakulia pointi , vipi wewe hupendi kufungwa mkanda?”
“Haha..hebu endesha huko , siku nyingine nitafunga mwenyewe .. unalishwa matangopori unayabeba kama yalivyo”
Hamza alijikuta akijifanyisha kuona aibu na mara baada ya kumwangalia Eliza walijikuta wakicheka wote.
****
Muda wa saa sita Mchana Mzee Gabusha aliingia nyumbani kwake na wala hakumjali hata Chriss aliekuwa bize na simu bali alivua koti la suti pamoja na tai na kisha alikimbilia friji na kuibuka na Vodka pamoja na glasi.
Kwa haraka haraka alimimina kinywaji kile katika ile glasi na kupiga pafu kwa nguvu kana kwamba anakunywa maji.
Kitendo kile cha baba yake kurudi akiwa katika hali hio alijua lazima kuna swala ambalo limetokea na hio ilimpa shauku Chriss.
“Mzee nini tatizo?”Aliuliza Chriss.
“Hakuna tatizo”Aliongea huku kifua kikipanda na kushuka.
“Dad tunaishi wote na nakujua ukiwa katika mudi tofauti tofauti , ukiwa na kitu kinachokusumbua lazima utumie Vodka”
Kabla hata hajajibu swali la Chriss simu yake ilinguruma na aliitoa haraka haraka na kuangalia jina la anaepiga na alipokea palepale.
“Boss ashaanza matibabu, amevunjika miguu yote miwili”
“Vipi kuhusu Eliza hajaongea chochote , hakunitaja wala kutoa ushahidi wowote?”
“Imekuwa ngumu kumhoji kwasasa maana ndio amerejewa na fahamu , bosi nitachukua maelezo kutoka kwake”
“Sawa nitaarifu ukifanikiwa”Aliongea na kisha akakata simu na Chriss shauku ilizidi kumjaa.
“Mzee nini kinaendelea”
“Yule boya kamvunja Maonga miguu yote”Aliongea na kauli ile ilimfanya Chriss kuwa na hali ya kuchanganyikiwa.
“Baba unamaanisha boya yupi?”
“Alievuruga mpango wangu na Eliza na kumfanya Amosi kujitoa kabisa baada ya Chatu kumtishia maisha yake”Aliongea huku akichukua kinywaji kingine na ukigida na kufanya jicho kuwa jekundu.
“Imekuwaje Maonga akaingia katika hili sakata Mzee ..usiniambie?”Aliongea Chriss na wazo lilimjia palepale na kujikuta akikaa kwenye sofa huku akimwangalia mzee wake kwa mshangao.
Mzee Gabusha hakujali muonekano wa chirss na alichukua koti lake pamoja na tai na kisha aligeuza akitoka nje , haikueleweka alikuwa akienda wapi maana ndio amefika nyumbani.
Chriss aliishia kutingisha kichwa tu, huku akijiambia mzee ni mkatili sana na hakutarajia kama angekamilisha mpango wake muovu.
Dakika chache kupita mlango wa kuingilia ulifunguliwa na Alex ambae alikuwa na yeye mbiombio na kumfanya Chriss ajiulize leo hawa ndugu zake wana matatizo gani.
“Hey! Chriss , mjomba amekuwaje mbona mbiombio hata namsalimia haitikii?”
“Mpango wake na Eliza unaonekana kubuma , ndio maana yupo hivyo?”Aliongea Chriss kivivu na Alex mara baada ya kusikia kauli ile alienda kukaa haraka haraka kwenye sofa na kumkazia Chriss macho.
“Kulikuwa na mpango ambao siujui?”
“Unajuaje wakati siku sita zote huonekani na hata taarifa hujatoa , unazingua?”Aliongea na kumfanya Alex kunywea kidogo.
“Niliitwa na Madame , yule mwanamke akisema njoo hata upo chooni unaacha unaenda , sikupata muda wa kukutaarifu. Niambie ni mpango ngani uliofeli?”
“Unajua Mzee na mambo yake , juzi ananiambia ana mpango wa kumtia Eliza mimba , hivyo ameanza kufatilia mzunguko wake wa hedhi?”
“Nini , Mjomba anajua mzunguko wa hedhi wa Eliza , kivipi?”
“Mzee juhudi anazowekwa kwa huyu mwanamke ingekuwa ni kwenye biashara zetu tungeipita hata Dosam muda mrefu , lakini ndio hivyo juhudi anazoweka hazimpi majibu, Inaonekana huyu Eliza anapata maumivu wakati wa hedhi na kutumia vidonge flani hivi vya kuyapunguza, duka analopenda kununulia Vidonge hivyo ni lile la Mzee Benjamini kule Kigamboni , nadhani ndio alijua hapo kwa kupiga mahesabu ya siku ambayo anaingia kwenye mzunguko”Aliongea Chriss na kumfanya Alex kutoa macho.
“Aisee Mjomba kafanya yote haya kwa ajili ya huyo mwanamke , mbona shauku inanijaa , nataka kumuona huyo mrembo”
“Hata mimi nimejikuta nikipatwa na shauku ya kutaka kumuona , nilitaka kutumia kisingizio cha kwenda kumuona Prisila kazini kwake ili anikutanishe na huyo Eliza ila kwasasa yupo likizo”
“Sasa imekuwaje mpango ukafeli?”
“Wewe mpaka hapo ulitakiwa uwe ushaelewa nini mzee angefanya , mpango wake ulikuwa ni kumbaka Eliza akiwa katika siku za hatari ili amtie mimba , juzi wakati ananiuliza maswala ya mzunguko wa hedhi yanavyokuwa nilimdadisi lakini hakufunguka sana , ila leo baada ya kurudi akiwa amefura nishausoma mchezo mzima, Dokta Maonga ni Mkuu wa Vizda Sanatorium na huyo Eliza mzazi wake ni mgonjwa ambae hajitambui hivyo ni lazima atakuwa yupo huko Vizda na Mzee Kamtumia Maonga kufanikisha mpango matokeo yake Maonga kavunjwa miguu”Aliongea huku akicheka.
“Maonga kavunjwa miguu?”
“Ndio na Mzee kwa ninavyoona wasiwasi wake ni kama Maonga amemtaja katika tukio hilo, nadhani ndio kinachomsumbua zaidi akili kwa sasa”
“Huyo jamaa aliefanikisha kitendo cha kumvunja miguu Dokta Maonga ni nani huyo, au ndio yule yule aliemfanya Jasusi kukimbbia”
“Ndio huyo , kasema tu yule boya kaharibu mpango wangu”Alex alijikuta akifikiria.
“Siwezi kumcheka Mjomba wakati na mambo yangu hayajakaa sawa kabisa , Frida katoweka na sijui kaelekea wapi?”
“Katoweka au kasafiri?”Aliuliza
“Kusafiri unajua mtu kaenda wapi , ila huyo katoweka , sijui hata kama amesafiri”
“Amesafiri huyo na atarudi ,unadhani mfanyakazi wa taasisi kubwa kama Haliz anaweza kupotea tu hivi hivi , tumia akili bro”
“Nimefikira hivyo pia , lakini hata akirudi sidhani kama pale nitang’oa , itafikia hatua naweza kutumia hata njia ya mjomba”
“Wewe na Mjomba mnafanana sana tabia , nimehangaika na Prisila mwaka wa ngapi huu lakini sijaambulia chochote zaiti ya mate tu , lakini sijawahi kufiikiria kumfanyia hila , nitaenda nae taratibu mpaka ajae kwenye himaya yangu”Aliongea.
“Wewe Chriss unachofanya ni uboya , endelea na ubaba paroko ,utakuja kushitukia demu sio wako tena , unaweza ambulia mate kuna mwenzako anapewa zaidi ya hivyo”
“Acha uboya Alex , namjua Prisila vizuri, unadhani mpaka muhuni kama mimi ku fall in love ni rahisi hivyo”Aliongea .
“Simu yako inaita”Aliongea Alex akinyooshea simu iliokuwa juu ya meza ya kioo,
Chriss aliichukua haraka haraka na mara baada ya kuangalia jina la mpigaji mapigo yake yalienda mbio.
“Huyu Jasusi baada ya wiki kupita ndio ananipigia sasa hivi simu, nimemtafuta sana”Aliongea kwa hasira mara baada ya kuona jina la Mzee Amosi kwenye kioo cha simu yake.
******
Hali ya Eliza iliimarika mara moja na hio ilimpa amani ya kuendelea na siku yao kama walivyopanga.
Walitoka hospitalini na moja kwa moja walienda kwenye mgahawa ambao Hamza aliuchagua , wakiwa njiani Hamza alimwelezea Eliza namna alivyodili na Dokta Maonga.
Eliza hata yeye baada ya kusikia kibano alichokutana nacho aliona haina haja ya kwenda kushitaki , kwani ingempotezea muda tu , isitoshe vitendo vya namna hio vilikuwa vikikemewa kila siku lakini havikuwahi kukoma.
Kwa mara ya kwanza mrembo huyo alijisikia vizuri sana ana mwanaume ambae anaweza kumlinda wakati wote , siku zote alikuwa peke yake akihangaika huku na huko na hata kuombwa rushwa ya ngono , lakini malaika Hamza kujitokeza ni kitu kilichomfanya ampende zaidi.
Siku nzima hakuacha kumwangalia Hamza huku akiwa na tabasamu
Upande wa Hamza na yeye alifurahi kuwa karibu na mrembo huyo na ni mwanamke wake wa kwanza kuingia nae katika mahusiano kwa kipindi kirefu.
Aliweza kumjua kiundani zaidi Eliza na alijua ashawahi kuwa katika mahusiano huko nyuma , hakushangaa , kwa uzuri wa Eliza lazima wanaume wengi walijaribu bahati zao na ni ngumu kuwakatalia wanaume wote, ki ufupi hakuona tatizo Eliza kuwa na Ex.
Saa tatu kamili za usiku ndio Hamza alimaliza mtoko wake na mtoto mzuri Eliza , ijapokuwa ilikuwa mapema lakini kwasababu siku iliofuatia ni Jumatatu hivyo Eliza alitaka kuwahi kupumzika.
Hamza wakati anafika nyumbani aliweza kumkuta Shangazi akiwa bado macho , akiwa bize na kuandaa vifungua kinywa kwa ajili ya siku inayofuara asubuhi.
“Hamza bora umewahi kurudi , hebu chukua hizi doghnut na hio chai ya maziwa umpelekee Regina , hajakula chochote tokea mchana”
“Regina hajala chochote tokea mchana?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.
“Ndio , nadhani ni maswala ya kampuni ndio yanamuumiza kichwa , nashindwa hata kumuelewa ila anaonekana kutokuwa na raha kabisa , nimeenda hapo supemarket na kununua hizi Doghnut”
Hamza alishangaa kuona Shangazi na giza lote ameenda kutafuta Doghnut kwa ajili ya Regina , kwenye mfuko zilikuwa nane na zilikuwa zikinukia harufu flani hivi nzuri ya Strawberry, Hamza aliishia kujiuliza Regina atamaliza zote hizo.
Ukweli ni kwamba mwenyewe alikuwa aksihangaa yaani mtu aache kula chakula cha usiku na ale doghnut saa nne kasoto ya usiku.
“Usiwe na wasiwasi kabisa , Regina huwa anazipenda sana hizo , huwa akiwa hana hamu ya kula ndio naendaga kuzinunua na kumpa , hizo nane ni chache sana mbona”Aliongea Shangazi lakini Hamza hakuamini, aliishia kuchukua maziwa yaliochanganywa na majani na kisha kupandisha juu.
“Regina upo ndani?”Aligonga lakini hakuna suati iliosikika kutoka ndani.






SEHEMU YA 34.
Hamza aligonga mlango kwa muda mrefu kidogo , lakini hakusikia majibu hivyo aliamua kushika kitasa na kuufungua kisha akaingia ndani.
Mara baada ya kuingia katika chumba hicho cha kujisomea aliweza kugundua Regina alikuwa amelalia meza akiwa usingizini , huku mbele yake kukiwa na furushi la nyaraka ambazo ilionekana alikuwa akizifanyia kazi, Hamza aliishia kujiuliza inamaana huyu mwanamke tokea mchana alikuwa akifanya kazi licha ya kwamba ni jumapili.
Hamza licha ya kwamba alikuwa mpenzi feki , lakini kumuona namna alivyokuwa akijitesa kwa kufanya sana kazi alijisikia vibaya.
Alijikuta akisogea upande mwingine na kumwangalia Regina , na kwa jinsi alivyokuwa amelala alikuwa ni kama mdoli kwa jinsi alivyokuwa mzuri , ule ukauzu wote ulikuwa umepotea akiwa usingizini na kumfanya kuzidi kuvutia.
“Sura yako ingekuwa muda wote kama hivi , ingekuwa vizuri lakini tabia yako ya ukauzu inaficha mengi ya kuvutia”Alijiongelesha Hamza.
Chumba kilikuwa na ubaridi wa AC mkali mno lakini bado alikuwa amelala na kutoa sauti kabisa , Hamza hakutaka kumuamsha hivyo aliweka alivyoshika mkononi na aliona shuka kwenye sofa na kumfunika lakini kitendo cha kumaliza tu Regina alishituka.
Aliishia kuegamia kiti chake huku akitoa miayo na mara baada ya kufikicha macho yake ndio sasa anagundua kuna mtu pembeni yake
Hamza upande wake alikuwa amekodoa macho tu , alikuwa akiushangaa uzuri wa mrembo Regina hata wakati wa kuamka.
“Unafanya nini hapa , nani kakuruhusu kuingia?”Aliongea kibabe.
“Sijafanya makusudi kuingia bila ya ruhusa , ulikuwa umelala , Shangazi kanipatia hizi doghnut na chai nikupe , anasema hujala chakula cha usiku”
“Mh Doghnut! “Regina alijikuta akigeuza macho yake na aliweza kuona Doghnut nane kwenye sahani na alishindwa kujizuia zaidi ya kumeza mate.
Kitendo hicho kilimfanya Hamza kuona itakuwa kweli Regina anapenda sana hizo Doghnut.
Regina muda ule alijihisi kuna kitu kilikuwa kimemfunika mabega yake hivyo alipeleka mkono nyuma kukitoa na aligundua ni shuka.
“Wewe ndio ulinifunika?”
‘Ndio , chumba umekifanya kimekuwa na ubaridi mkali ndio maana nimekufunuka , haina haja ya kunishukuru kwa upendo wangu”
“Nani kasema nitakushukuru , ulitakiwa kuniamsha baada ya kunniona nimelala sio unanifunika”
“Nilikuwa nikijali kuhusu afya yako , ningejuaje kama ulitaka kuendelea na kazi”
“Huna haja ya kunijali, hatuna uhusiano wowote , nadhani itakuwa vizuri ukiweka akili yako kwenye kumjali mpenzi wako , unaweza kuondoka sasa”Aliongea kikauzu.
Hamza aliishia kupumua kwa masikitiko , alikuwa akionyesha vitendo vya kumjali kama bosi wake , lakini anakasirika , alijiuliza kwanini kuna utofauti mkubwa kati ya Eliza na huyu mrembo.
Ijapokuwa Regina alikuwa amemzidi kila kitu Eliza kwanzia muonekano , akili , mali mengineyo lakini Eliza alikuwa rahisi sana kuishi nae.
“Kheri nikale zangu tembele kila siku na Eliza kuliko kula vinono na Regina, mtu gani ana tabia kama za Mzimu uliolazimishwa ndoa bila mahari”Aliwaza Hamza.
“Una mwemweseka nini?”
“Hamna , naenda na mimi kula hivyo vitairi”
“Utajua mwenyewe , toka nje”
“Nani kakuambia nataka kuendelea kukaa hapa?”Hamza alitamani kuongea kwa sauti lakini aliishia kumezea ndani kwa ndani na kutoka kwa hasira.
Hamza wakati anataka kuelekea kwenye chumba chake Shangazi alimwita tena.
“Hamza njoo tena”
“Shangazi kuna nini tena?”
“Nimesahau kuweka sukari kwenye ile chai , hebu nisaidie ukamuwekee”Aliongea Shangazi na kumpatia Hamza mkononi.
Hamza alitamani kutoa chozi , alijiuliza kwanini huyu shangazi alikuwa akimuonea hivyo , lakini baada ya kukumbuka ni mpenzi akiwa hapo nyumbani aliishia kukubali kinyonge.
Awamu hio alikuwa na hasira hivyo baada ya kufikia mlango hakujisumbua hata kugonga na alisukuma mlango na kuingia.
Lakini picha alioiona pengine asingeisahau kwenye maisha yake kuonyeshwa na mwanamke kama Regina.
Regina alikuwa ameshikilia Doghnut mbili mikono yote huku zikiwa zimeng’atwa zote , mdomo ulikuwa umetuna kiasi kwamba alikuwa akitafuna kwa shida, kilichomshangaza zaidi alikuwa akitingisha kichwa kwa furaha zote kiasi kwamba kiti kilikuwa kikinesa nesa.
Hamza alijiambia huyu Regina aliemfurusha ndani kwake ni wa tofauti sana , kama mbingu na ardhi , hakuwa na ule kauzu tena bali muda huo ni kama mtoto anaeshindana na chakula.
Hama alijiuliza au Regina ana tatizo la akili la kuwa na nafsi mbili kwa wakati mmoja .
Ughh!!
Regina alijikuta akitoa macho mara baada ya kugundua kuna mtu ameingia na aligeuza uso wake na kugundua ni Hamza , aliishia kupepesa macho kama ana kifafa huku akianza kuwa mwekundu.
Tukio lile lilimfanya Hamza kujiambia atakuwa ameona kitu ambacho hakustahili kuona
Alijifanyisha Mzembe na kisha alipeleka sukari mpaka kwenye meza.
“Samahani bosi kwa kukusumbua wakati unakula , shangazi kaniambia nikuletee hii sukari kwa ajili ya kuweka kwenye maziwa”
Baada ya kumaliza aliondoka haraka hraka ndani ya chumba hicho akiwa katika hali ya utulivu na kufunga chumba.
Baada ya Hamza kutoka Regina kivivu alijikuta akiweka kila alichoshikilia kwenye mikono yake na kulalia mikono yake kuzika kichwa , uso ulipata moto na alitamani kuingia chini ya meza kwa aibu alizokuwa akisikia.
Upande wa Hamza picha ya Regina kutuna mashavu huku akisindilia vile vitairi ilikuwa ikijiurudia rudia na alijikuta akikaa kwenye ngazi na kutoa kicheko cha ajabu kama kichaa.
Kutokana na tukio hilo hasira yake zidi ya Regina iliisha mara moja , aliona tukio hilo linachekesha zaidi kuliko la kule kazini.
Hamza mara baada ya kurudi chumbani kwake na kumaliza kuoga , aliweza kuona lile boksi alilopewa na Frida jana yake na shauku ilimvaa hapo hapo na kutaka kujua ni mshumaa gani ambao alikuwa akizungumzia.
Hamza alichukua kile kiboksi na kurudi nacho kwenye kitanda haraka sana na kufungua ndani na mara baada ya kuona kilichokuwa ndani yake aliishia kuguna tu , haukuwa mshumaa kama mshumaa , bali kifaa cha kieletroniksi kilichokuwa na muonekano kama wa mshumaa , pengine ndio maana kiliitwa mshumaa, kwa chini kulikuwa na kitako kama cha Bunsen Burner za gesi , kilikuwa cha rangi ya zambarau huku eneo la katikati kukiwa na kifaa kama kioo , juu kabisa kulikuwa na kioo pia kama vile ni hadubini.
Hamza aliangalia kwenye boksi na aliweza kuona pia waya wenye adapter, ilionekana ni kama chaji ya kifaa hiko, hakukuwa na kingine cha ajabu zaidi kutoka katika huo mshumaa wa nuru zaidi ya Manual, kikaratasi flani hivi cha maelekezo.
Hamza aliweka pembeni na kuanza kusoma kile kikaratasi taratibu na aliweza kuelewa maana kiliandikwa kwa lugha ya kingereza.
Hakuwa na cha ajabu sana zaidi ya maelekeo ya kufunga mlango na madirisha wakati wa kulala na kuchomeka kifaa hicho kati ya saa tano na saa sita za usiku kwenye umeme.
Hamza hakuwa akimwamini Frida bado hivyo hakutaka kukurupuka na kufauta maelekezo aliompatia.
Hivyo alirudisha kama vilivyo na kujitupa kitandani na hakuchuua muda alishapotelea usingizini.
*****
Ilikuwa ni siku ya jumatatu na mara baada ya Hamza kushituka aliona kwanza siku hio aende kazini na siku inayoafuata aelekee chuo kwa ajili ya kwenda kuchukua barua na kujua utaratibu wa kimasomo utaendelea vipi.
Baada ya kujiweka sawa kimwili walivaa mavazi yake kama kawaida na kisha alishuka chini.
Regina alikuwa tayari ashajiandaa na alikuwa mezani akipata kifungua kinywa na muonekano wake ulikuwa uleule wa siku zote, ilikuwa ni kama jana hakuna kilichotokea.
Upande wa Hamza aliona Regina alikuwa akiigiza kuwa kauzu tu mbele yake hivyo aliona inafurahisha sana.
Baada ya wote kumaliza kifungua kinywa Hamza alishika usukani na safari ya kuelekea kazini ilianza, wakati huo Hamza alikumbuka swala la kampuni ya Zena ilio chini ya James kununua kampuni ya Omega na shauku ilimvaa.
“Regina hivi..”
“Kaa kimya, sitaki kuongea chochote na wewe”Aliongea na kumfanya Hamza kushangaa na aliwaza au alidhani anauliza swala la jana.
“Sio kama nataka..”
“Nimekwambia kaa kimya , kama huwezi funga mdomo wako shuka kwenye gari”Aliongea akiwa siriasi na Hamza aliishia kuufyata.
Hamza palepale alipata wazo na alitumia mkono mmoja kuendesha gari na mkono mwingine alitoa simu yake na kuandika maneno kadhaa kwenye simu na kumuonyesha Regina kuona.
“Nilitaka kuuliza kama kuna tatizo kubwa na kampuni ya Zena juu ununuzi wa Omega?”
Regina mara baada ya kuona aliona alikuwa amemdhania vibaya juu ya kile alichotaka kuongea , ukweli hakutaka utani wowote kutoka kwa Hamza juu ya tukio la jana ndio maana alizidisha ukauzu.
“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , nina mpango wangu”Alijibu
“Nauliza , hata hivyo haina maana mimi kuwaza , ninachotaka kusema usijipe presha sana , jaribu kutafuta kitu kitakachokufanya angalau utulie, kama vile jana ulivyokuwa ukisindilia…”
“Nyamaza”Alifoka Regina , kwa jinsi alivyobadirika ni dhahiri angekuwa na nyundo ingetua katika kisogo cha Hamza.
“Hey , usipaniki hivyo nimeacha”
*****
Baada ya kufika kwenye kampuni Hamza kama kawaida aliingia katika ofisi yake na kuanza kuvuna Bitcoin mpaka inatimia mchana muda wa chakula ndio alitoka.
Baada ya kwenda mgahawani na kuonekana mbele ya wafanyakazi watu walionekana kumwangalia.
Warembo wengi walionekana kumwangalia kwa macho ya kumkubali kitu kilichomfanya kujiuliza kwanini wanamwangalia sana.
“Hamza kumbe haikuwa utani unajua mapigano hata kumzidi Yonesi , hatimae tumejua siri kwanini umefanywa kuwa msaidizi wa bosi kumbe upande mwingine ni bodigadi”Aliongea Asha wa idara ya mauzo na sasa Hamza alijua kwanini walikuwa wakimwangalia.
Wiki iliopita kitendo cha kumdhibiti Master Konki mara baada ya Yonesi kupigika , swala hilo lilionekana kusambaa katika kampuni kwa wafanyakazi wote.
“Hamza hebu tuambie , tulisikia sijui ulitumia mbinu ya kucha za tai , hivyo vidole unaweka vipi tuonyeshe”Aliongea Mirium rafiki yake Asha.


Hamza aliwaza na kujiambia mbinu hio ya Kucha za tai ina historia kubwa sana tokea enzi za kale , sasa anawezaje kuwaelezea kirahisi, lakini mara baada ya kuona wamejawa sana na shauku , aliamua kuwaelezea ki uwongo uwongo kama mtoto anaejifanysiha kujua mapigano, kitendo kile kiliwafanya Mirium na Asha kuvuta midomo na kumuacha.
Lakini hata hivyo Hamza kutokana na kuangaliwa na wafanyakazi wengi kwa macho yaliojaa sifa , kichwa kilimvimba na mara baada ya kuchukua chakula chake alibadili mwendo kabisa na kuanza kudunda huku akisogelea meza aliokaa Yonesi akiwa peke yake.
“Habari Kapteni , naona leo sioni Suasage kwenye sahani yako?”
“Hebu jali mambo yako , muone kichwa kilivyokuvimba , kumfukuza yule mzee ndio unaona umefanikisha kitu kikuubwa?, mpaka mwendo unabadilika”Aliongea Yonesi
“Hehe .. najua hata wewe mwenyewe unanikubali lakini unaona aibu kusema waziwazi , hata usiongee mimi naelewa unachojjisikia moyoni”
“Nani anakukubali , unadhani mimi ni chizi?, Wewe nisubiri nishaanza kufanya mazoezi makali , nakuhakikishia lazima nikupige mpaka uombe msamaha , ni kazi tu ziliniweka bize na nikaacha kuchukua mazoezi ndio maana”Hamza hakuongezea neno na aliishia kukaa kimya.
“Unadhani natania , nilibweteka kwa muda tu ndio maana”
“Najua kapteni wewe ni mtaalamu wa hali ya juu”Aliongea Hamza lakini Yonesi hakuridhika.
“Najua unanidanganya tu kunifariji , kwenye moyo wako unaniona mnyonge”
“Kapteni , unadhani ni kipi napaswa kukuambia ili nipate amani ya kula chakula changu”
“Kama unataka kula chakula chako , nenda meza nyingine, kwani lazima ukae kwenye meza yangu”
“Hapana lazima nikae meza moja na wewe”Aliongea Hamza na Yonesi hata yeye aliona kabisa Hamza alikuwa kila siku na mpango wa kukaa meza moja na yeye , ukweli ni kwamba kulikuwa na wanawake wengi ambao walikuwa wazuri kuliko yeye , hivyo aliuliza kwanini analazimisha wakae meza moja.
“Kwanini?”
“Huchoki kula peke yako kila siku , mimi nipo hapa kukupa kampani , anagalu sasa hivi sio mpweke sana maana una rafiki”
Yonesi mara baada ya kusikia hivyo alishangaa na kuguswa na jambo hilo na mwili wake ulikakamaa.
Yonesi hakuwa mzaliwa wa jijini Dar , ki ufupi ni wa mkoani na kutokana na baadhi ya mambo alijikuta akitofautiana na wazazi wake na ndio maana alikuja kuhamia Dar akiwa nje ya kazi , katika kipindi hicho cha upweke ndipo alipokuja kukutana na Regina na akafanywa mkuu wa kitendo cha ulinzi wa kampuni ya Dosam baada ya Regina kutumia ushawishi wake serikalini na Yonesi kupewa ruhusa.
Lakini sasa kutokana na mazingira aliokulia na namna alivyosoma elimu yake kuanzia akiwa mdogo mpaka ukubwani , ilimfanya kuwa ngumu sana kutengeneza marafiki , hata kwa walinzi wenzake wakike hakuweza kuendana nao zaidi ya maswala ya kikazi tu.
Alikuwa akiishi peke yake , kazi alikuwa akifanya peke yake , kula peke yake, kila kitu peke yake , kila siku ilikuwa hivyo kwa miaka mitatu yote.
Kula kwake ndani ya mgahawa wa kampuni ukiachana na wanaume ambao walikuwa na ajenda zao mpaka kutaka kula nae hakuna mtu alishawahi kuja katika meza yake kwa ajili ya kuwa rafiki tu , wala kujali kama alikuwa mpweke.
Katika macho ya wafanyakazi wenzake , Yonesi alionekana kama sio mtu wa kawaida wa kufanya nae urafiki.
Yonesi alikuwa imara kwasababu alikuwa ni mwanajeshi hivyo anao uwezo hawa wa kuishi jangwani , lakini haikumaanisha kwamba yeye sio mwanamke ambae upweke haumuathiri.
Hivyo mara baada ya Hamza kusema ni mpweke alijihisi huzuni moyoni mwake , aliishia kugeuza macho yake pembeni ili asionekane machozi yalikuwa yakitaka kumtoka.
“Napenda kula peke yangu , sijawahi kusema mimi ni mpweke , na pili sihitaji muhuni kama wewe kuwa rafiki yangu , kaa mbali na mimi”
Upande wa Hamza hakumjali kabisa na aliishia kucheka tu huku akiendelea kuwa bize na chakula chake.
Yonesi aliishia kutulia na kuendelea kula chakula chake taratibu huku mara kwa mara akimwangalia Hamza kwa jicho la pembeni.
Hamza mara baada ya kula kama kawaida alichukua matunda na kupandisha nayo juu.
Baada ya kufika katika ofisi ya Regina aliweza kukuta baadhi ya sura anazozifahamu na nyingine asizozifahamu , walikuwa ni wafanyakazi wa juu wa kampuni na ilionekana kuna kikao kilichokuwa kikiendelea na kitendo cha kuingia bila ya hodi ni kama iliwafanya wote wamkodolee macho.
ITAENDELEA.- watsapp me 0687151346
 
Kusema ukweli singanojr siku hizi umekuwa muongo jamani, tifauti na ulivyoanza story ya Roma ulikuwa mwaminifu, ukiahidi unatenda, siku hizi sasa lol[emoji119][emoji119]
Changamoto Madam si unajua tena
 
  • Thanks
Reactions: ram
Kusema ukweli singanojr siku hizi umekuwa muongo jamani, tifauti na ulivyoanza story ya Roma ulikuwa mwaminifu, ukiahidi unatenda, siku hizi sasa lol[emoji119][emoji119]
Huyu siku hizi ana dharau mnooo umarufu kidogo humu umemlevya hata wasap unaweza mtext akajibu baada ya week keshalewa sifa
 
Back
Top Bottom