Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SHETANI RUDISHA NAFSI ZETU.



MTUNZI:SINGANOJR​



SEHEMU YA 149.

Kijana mdogo hasira kubwa

Mara baada ya Yonesi kusikia kauli hiyo, mwili wake ulitetemeka kwa sekunde kadhaa. Haraka aligeuza kichwa chake pembeni na kuziba uso wake kwa mikono miwili. Moyo ulikuwa ukienda mbio mno.

“Haha, Yonesi jana uliniuliza swali kwa ujasiri mno, kwanini sasa unakuwa na aibu hivyo?”

Yonesi alijikuta akivuta pumzi mara mbili. Hakuwa tayari kushindwa tena. Aligeuka na kumtazama Hamza akiwa na ujasiri.

“Unaongea ujinga, nani anaona aibu?” Aliongea, na Hamza akaona hakuna haja ya kuendelea kumchokoza.

“Okey okey, ni kweli huna aibu, basi chukua kwanza upate chochote uchangamshe tumbo, safari ndefu hii.” Aliongea Hamza, na kumfanya Yonesi kumkodolea macho, asijue mwanaume huyo anafikiria nini.

Hata chakula alipokea kimya kimya na kuendelea kula taratibu, akiendelea kuwaza.

“Hivi vidude ni vitamu mno lakini wanauza ghali…” Aliongea Hamza huku akitafuna.

Yonesi hakuona utamu wowote. Moyo wake muda huo ulikuwa umefumbwa na hisia mchanganyiko, na kumfanya kuona kama alikuwa ndotoni.

“Yonesi, unawaza nini? Mbona umekodoa macho hivyo?”

“Ni kweli unaenda nyumbani kwetu?”

“Ndio, si nishakwambia? Kama siendi kwenu kwanini nipande treni?”

“Lakini unaenda kuwaambia nini wazazi wangu? Mkurugenzi anajua unasafiri?” Aliuliza akiwa na wasiwasi mkubwa.

“Hata sijali kuhusu hilo, ninachojua nakupenda. Ijapokuwa sijui ni kwa kiasi gani, lakini siwezi kukuona ukiolewa na Mdudu.”

“Huoni kama unafanya mambo kwa kukurupuka? Ijapokuwa familia yetu si kama nyingine kubwa, lakini haimaanishi wataweza kuingilika kirahisi. Isitoshe, kama Mkurugenzi akisikia kuhusu hili atakasirika mno.”

“Hata kama familia yenu ingekuwa ya raisi, hakuna wa kunizuia. Kama familia yenu ni ya kawaida kwanini wanizuie? Kuhusu mke wangu, hilo niachie mimi. Nitajua namna ya kumbembeleza. Nikichanganywa na mwanamke mmoja kama mwanaume nitaishi vipi?”

“Wewe, aisee unajua kukurupuka kweli,” aliongea Yonesi, akikosa neno.

“Hehe… mwenzako Eliza jana kasema kanipendea kwa sababu ya kukurupuka kwangu, wewe unaonaje?”

“Kwahiyo jana ulikuwa na Da’ Eliza?”

“Ndio, nimetokea kwake asubuhi ya leo na kuja moja kwa moja stesheni.”

Yonesi alijikuta akituliza hisia na kujiambia kweli huyu playboy ameshindikana. Hata hivyo, alikuwa katika hali ya kupaniki maana alishindwa kujua ni kitu gani Hamza anapanga kufanya wakifika nyumbani.

Saa sita kasoro ndio muda walioweza kufika stesheni kuu ya treni Dodoma, na wakati wakiwa wanatoka waliweza kumuona mwanaume mzee wa makamo akiwa amesimama pamoja na wanaume wengine wawili waliovalia mavazi ya suti.

“Yonesi, hatimaye nakuona tena,” mwanaume yule aliyevalia suti ya kijivu aliongea kwa uchangamfu.

Yonesi, mara baada ya kumuona mzee huyo, na yeye pia alitabasamu na kumsogelea kumsalimia kwa furaha.

“Mjomba Sauli, unaendeleaje?” Aliuliza Yonesi, lakini swali lake lilikuwa la kijinga sana kutokana na kwamba mzee huyo alikuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi katika levo ya mzunguko kamili, maana yake umri wake wa kuishi ni mkubwa na si rahisi kuumwa kirahisi.

Hamza, mara baada ya kuona mzee huyo ndiye aliyekuja kumpokea Yonesi, aliona kweli familia ya Yonesi ilikuwa ya kijeshi na kichifu.

Kuna muda Hamza mwenyewe alikuwa akijiuliza , katika mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi Tanzania haikuwa na muda mrefu sana tokea ipate ufahamu wa mafunzo haya , lakini kulikuwa na wazee wengi ambao walionekana kuwa na mafunzo hayo muda mrefu sana na kujiuliza wametokea wapi.

Mzee Sauli hakuwa mwanajeshi wa moja kwa moja , alikuwa ni wazee tu waliochipukia katika familia ya Chifu Mazengo na kupewa kazi ya ulinzi na kusimamia kazi zote za familia , kama ni wazungu wangempa cheo cha Buttler.

“Unaonekana kukua kiasi chake Yonesi”Aliongea huku akichunguza mwili wa Yonesi na aliweza kuhisi amekuwa tofauti , ijapokuwa hakujua ni mafunzo gani lakini aliweza kuona utofauti hasa upande wa ukomavu wake wa kiakili.

Yote hayo yalikuwa ni mafunzo ya Hamza aliomwelekeza Yonesi kutumia.

Muda uleule yule mzee aliinua uso wake na kumwangalia Hamza . Alikuwa ameishi maisha marefu sana ndani na nje ya Tanzania na kuona watu wengi wa kawaida na wasiokuwa wa kawaida , lakini kitendo cha macho yake kutua kwa Hamza aliweza kugundua sio mtu wa kawaida palepale.

“Bwana mdogo , Yonesi ni rafiki yako?”

“Haha.. wewe endio Mzee Sauli si ndio , wakati tukiwa njiani Yonesi alikuwa akinielezea habari zako na anasema wewe ndie uliekuwa ukimpenda sana , wakati akiwa mdogo wazazi wake wakimfokea alikuja kwako kukulalamikia,. Mimi kama mpenzi wa Yonesi nichukue fursa hii kukushukuru kwa kumjali kwa wakati wote mpenzi wangu”Aliongea Hamza huku akiwa amemshika mkono yule mzee na matendo yake yalimfanya Mzee Sauli kuwa katika mshangao.

Yonesi alishindwa kuona namna uso wake umeiva , hakujua Hamza atakuwa spidi spidi kwenye kujitambulisha mapema kama mpenzi wake kama hivyo.

“Wewe.. kwahio ndio mpenzi wa Yonesi?”Aliuliza kwa shauku lakini kwa wakati mmoja akiwa katika hali ya wasiwasi.

“Mjomba tuondoke kwanza , ni stori ndefu”Aliongea Yonesi akiingilia maongezi.

Mzee Yule aliishia kuvuta pumzi na kuzishusha , alikuwa kama mtu ambae ametegemea kuna jambo kubwa litatokea wakati wa sherehe ya Mzee Chalula.

Maisha aliokuwa akiishi Yonesi Dar pamoja na kazi yake utadhania hakuwa wa kishua , familia yake ni moja ya familia tajiri sana ndani ya mji wa Dodoma na yenye historia yenye mizizi mirefu.

Baada ya kutoka nje kabisa waliingai katika Mercedenz Benz nyeusi na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwao.

Wakiwa njiani kuelekea huko Yonesi alipewa taarifa kwamba , familia ya Mdudu wapo nyumbani na wamekusanyika wengi wa ukoo wao wakiamini kabisa hatimae ile siku ya kuunganisha familia hizo mbili imewadia .

Kutokana na taarifa hio , Yonesi alizidi kushikwa na wasiwasi mkubwa mno , upande wa Hamza yeye hakuwa na wasiwasi kabisa , macho yake yote yalikuwa nje akiangalia mazingira na alikuwa akiuliza maswali yaliokuwa nje kabisa ya mada.

Mzee huyo aliishia kumwangalia Hamza na kuona hakuwa na uwezo kabisa wa kujua ni kitu gani kinamfanya Hamza kujiamini na kutokana na mwonekano huo alizidi kuona sio mtu wa kawaida.

Ukweli ni kwamba kama familia ya Mzee Chalula wangetumia koneksheni yao kutaka kumjua Hamza kupitia kitengo cha Malibu , wangeweza kujua swala la kisiwani Chole , lakini kwa bahati mbaya swala la kisiwani kule lilikuwa ni siri sana na ni watu wachache sna ndani ya vitengo cya usalama walikuwa wakilifahamu.

Baada ya nusu saa gari kutembea , hatimae gari iliingia katika mtaa maarufu wa Kwa Chifu Mazengo au Mvumi Makulu, sehemu hio ilikuwa ikiitwa kwa Chalula kutokana na kwamba Mzee Chalula ndio mtu wa kwanza kabisa kujenga hapo na baadae serikali ilifanyia eneo hilo marekebisho na kuita Mji mpya lakini hata hivyo pamezoeleka zaidi kama Kwa Chifu Chalula wa Mazengo.

Nyumbani kwa Yonesi kulikuwa kumezungukwa na miti mingi na uoto wake ulikuwa ni ule wa kupandwa na sio wa asili kutokana na maeneo mengi kutofautiana na eneo hilo.

Baada ya kushuka katika megesho maalumu , kulikuwa na magari mengi yaliokuwa ndani ya eneo hilo tayari na mengi yalikuwa ni V8 na Prado.

Mandhari ya eneo hilo yalimfurahisha Hamza, na akajiambia angalau watu wa mkoani walikuwa wakiishi vizuri, ijapokuwa nyumba zilizokuwa ndani ya eneo hilo zilikuwa na muundo wa kikale, lakini mazingira yake hayakuwa mabaya.

"Yonesi, babu yako, baba yako na mama wapo kule nyuma. Nikupeleke kwanza chumbani kwako ukabadili mavazi au unaelekea moja kwa moja kuwasalimia?" aliuliza mjomba.

"Haina haja ya kubadili. Mjomba, naomba uniitie mtu kunisaidia kubeba mabegi yangu, nitaenda kusalimiana nao kwanza," aliongea Yonesi na kisha alimgeukia Hamza.

"Mpango wako ni upi?" Aliuliza Yonesi, akimwangalia Hamza.

"Na mimi naenda kuwasalimia na pia kuwaelezea swala letu kwa familia yako," alijibu Hamza akiwa na tabasamu, lakini Yonesi alionyesha ishara ya kutaka kumzuia.

"Acha wasiwasi, tunaenda pamoja. Huwezi kunizuia hivyo, ni bora ukaanza kujiamini kuanzia hapa," alisema Hamza.

"Basi usiwe mkali sana, mama yangu afya yake si nzuri sana, akishikwa na hasira anaweza kupandwa na presha," alisema Yonesi, na Hamza alitikisa kichwa kukubaliana naye.

Staili ya ujenzi wa eneo hilo ilikuwa ya kizamani sana. Japo nyumba zilikuwa nzuri, upangiliaji wake ulifanya ionekane kama kituo cha afya.

Baada ya kuingia kwenye korido ndefu iliyojitegemea, walipita bustani kadhaa zilizotengenezwa vizuri, na hatimaye wakaingia kwenye uwanja mdogo uliokuwa umepandwa mizambarau.

Njiani, baadhi ya wafanyakazi waliomwona Yonesi na Hamza waliishia kumwangalia kwa kumshangaa na kumsalimia kwa wakati mmoja.

Baada ya kuzunguka hadi nyuma, hatimaye waliweza kufika kwenye ukumbi mmoja uliokuwa umejengwa kwa makuti, na kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakiongea na kucheka kwa sauti, hali iliyofanya eneo hilo kuwa la furaha na kuchangamka.

Kadri walivyokuwa wakisogelea eneo hilo, ndivyo Yonesi alivyozidi kujawa na wasiwasi. Aliishia kujikaza kijeshi na kufanya hatua zake zionekane kama mtu anayejiamini.

Mbele kabisa, kulikuwa na mzee mtu mzima kabisa aliyevalia koti kubwa la manyoya la kitamaduini kabila la wagogo na kofia kichwani. Huyu alikuwa babu yake Yonesi. Ijapokuwa mwonekano wake ulikuwa wa kizee, macho yake yalionekana kuona vizuri kabisa.

Upande wa kulia kwake kulikuwa na mwanaume mwingine wa makamo, aliyevalia kombati za kijeshi za cheo cha Meja Jenerali. Huyu alikuwa baba yake Yonesi, Afande Daudi Chalula. Pembeni yake kulikuwa na mwanamke mwenye mwonekano wa kitajiri, maarufu kama Mama Danny. Huyu ndiye mama mzazi wa Yonesi.

Kulikuwa na wanaume wengine waliokuwa katika mavazi ya kijeshi, karibu wengi wakiwa na vyeo vya nyota tatu na ngao, na ilionekana walikuwa ni ndugu wa Yonesi.

Hata hivyo, waliokuwa wakimpa wasiwasi zaidi Yonesi ni watu waliokuwa wamekaa upande wa kushoto, upande wa wageni, wakiongozwa na Afande Mdudu na wazee wachache wa ukoo wake. Macho yao yote yalikuwa kwa Yonesi kama kwamba ndiye mtu pekee waliyekuwa wakimsubiria.

"Yonesi!" Mama Danny, mara baada ya macho yake kutua kwa Yonesi, aliinuka na kumkimbilia, akamkumbatia kwa hisia kubwa.

Yonesi alikuwa amemmisi sana mama yake. Alimwangalia na kuona alikuwa amezeeka mno, na alishindwa kujizuia kushikwa na hatia, akatoa chozi.

Unaweza ukashangaa kwa nini mzazi huyo asingesafiri kuja mpaka Dar kumuona mtoto wake kama alikuwa amemmisi sana, lakini baada ya Yonesi kutoroka nyumbani akiikimbia ndoa baada ya kufeli mafunzo nchini Chile, baba yake, Meja jenerali Daudi, alipiga marufuku familia nzima kutomtafuta Yonesi, ikiwemo mke wake.

"Hamza!" Afande Mdudu aliita mara baada ya kumuona, huku uso wake ukifubaa.

"Mdudu, unamfahamu yule kijana?" wazee wa familia yake waliuliza.

"Mjomba, yule ndiye Hamza, ndiye mtu anayefahamiana na mshauri mkuu na kuniambia nisimsumbue tena Yonesi," aliongea Mdudu, huku akionyesha kuwa bado alikuwa na hasira na Hamza.

Mdudu, tokea amkose Yonesi kwa kupewa vitisho na Hamza, aliomba kuacha jeshi na kujiingiza katika siasa. Alikuwa ni mjukuu wa kwanza Chifu Mirambo. Mjomba wake Imani alikuwa ni moja ya viongozi wa juu wa serikali akiwa amehudumu kama Waziri wa ulinzi chini ya Rais Mbilu. Ijapokuwa kwa wakati huo alikuwa mbunge tu baada ya kushinda uchaguzi, lakini alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa katika nafasi za juu za kuteuliwa uwaziri katika serikali mpya.

Baada ya Imani kusikia kwamba Hamza ndiye aliyeingilia swala la ndoa ya Mdudu na Yonesi, alijikuta hakuridhishwa na hali hiyo.

"Jenerali, kwa nini huyu mtu amekuja hapa? Kuonekana kwake katika familia yako si kama kutudharau?" aliuliza Mrambo kwa hasira, huku akipiga meza.

“Yonesi sogea hapa haraka na umwambie babu yako nini kinaendelea , huyo uliekuja nae ni nani?”

Yonesi ilibidi aachiane na mama yake na kisha alienda mpaka walipo wazee na kisha kuanza kusalimia

“Anaitwa Hamza ni ra…”

“Yonesi ni mpenzi wangu”Hamza alisogea haraka na kuongea.

Mara baada ya kusikia kauli hio watu wote katika ukumbi huo walijikuta wakishikwa na mshangao . Yonesi aliishia kukunja ngumi tu huku mikono yake ikishikwa na jasho kwa wasiwasi.

“Mzee Chalula , nini kinaendelea , Hawa watoto si ndio waliosema wenyewe wanakwenda kusahau yaliopita na kukubali kuchumbiana? Mdudu mwenyewe amekubali kuacha yaliopita na yupo hiari kumuoa mjukuu wako , Au hii inamaanisha familia yenu haijawahi kuchukulia hili suala kwa uzito wake ndio maana mnaenda mbali hivi?”Aliongea Mirambo kwa hasira huku akipiga meza.

“Mzee Mrambo punguza jazba , Familia yetu imekuwa na taswira nzuri kwa muda mrefu . Kama binti yangu amekosea , nipo tayari kuomba radhi”Aliongea Afande Daudi na kisha akamgeukia binti yake.

"Yonesi, hebu tuambie kama alichoongea huyu kijana ni kweli," aliuliza, na Yonesi aliishia kukaa kimya, akiwa ameinamisha kichwa chake chini, akishindwa kukubali. Isitoshe, Hamza hakuwahi kumtongoza vizuri na kumkubali.

Mama Danny wasiwasi ulimshika kutokana na kubadilika kwa hali ya hewa na alimshika mkono binti yake.

“Yonesi ongea , Kwanini ghafla tu umekuja na mpenzi?”

“Mama ni .. nampenda Hamza”Baada ya kusita aliishia kung’ata meno kuutafuta ujasiri na hatimae akafanikiwa kuongea.

Maneno hayo baada ya kumtoka kila mtu aliekuwa katika ukumbi huo alipiga kimya .

Hamza kwa upande wake alifurahishwa na kauli hio mno na palepale kwa kujiamini alisogea mbele na kusimama kando ya Yonesi.

“Wazee wangu kwanza naomba niwape salamu wote , nadhani wachache wananijua kwa kuniona na kunisikia , kwa wale wasionijua kwa jina naitwa Hamza Mzee na kwa mpangilio wa kinachoendelea hapa nadhani litakuwa jambo la busara kama mipango ya ndoa ikibadilika kidogo . Kutoka mwanzo mpaka mwisho , hakuna mmoja wenu aliemuuliza Yonesi kama anampenda Mdudu , kwa mantiki hii naona kabisa hatua muhimu imerukwa, Karne za kumtafutia mtoto wa kumuoa ama kuolewa nae zishapitwa na wakati, Au mnasemaje wazee wangu?”

Mdudu mara baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Hamza ni kama alikuwa akisiliza matusi na alishindwa kujizuia na kusimama.l

“Hamza acha kutumia ubabe kupata kila unachotaka ! Wewe tayari umeoa na mke wako anajulikana ni Regina mmiliki wa makampuni ya Dosam , unadhani sijakufanyia uchunguzi , inamaana unataka kumgeuza Yonesi Mchepuko?”

Maneno ya Mdudu yalikuwa ni kama bomu lingine lilowaangukia wazee hao na kusababisha kila ndugu wa Yonesi sura kukunja kama wamelishwa pilipili. Yonesi aliishia kutetemeka asijue ni kipi anaweza kufanya

“Kama unadhani hiyo ni pointi sana, basi nitaanza mchakato wa kubadilisha uraia na kuchagua taifa ambalo linaruhusu mwanaume kuoa wanawake wengi, kwanza nina jina la kiislamu unasemaje hapo” aliongea Hamza.

“Wewe…” Mdudu alijikuta akishangazwa na kauli ya Hamza maana hakuitegemea. Katika maisha yake hakuwahi kuona mtu aliyekosa aibu kama Hamza.

“Kikubwa ni kwamba nampenda Yonesi, na yeye pia ananipenda, na tuna furaha kuwa pamoja iwe nimeoa ama sijaoa, na hakuna cha kufanya juu ya hili.”

“Wewe mwanaharamu usiye na heshima mbele ya wazee. Unadhani tunaweza kuendelea kuvumilia kejeli zako kwa sababu tu unajuana na Mshauri Mkuu. Mdudu anaweza kuwa mdogo na kuhofia kitengo cha Malibu, lakini mimi, Mzee Imani Mirambo, sijawahi kuogopa mtu.” Mara baada ya kuongea kauli hiyo, aligeuza macho yake na kuwaangalia ndugu wa familia ya Chalula.

“Mzee Chalula, Jenerali, naona binti yenu ni mkanuni mno. Yaani juzi amekubali, na leo anaenda kinyume na maneno yake bila hata kutupa taarifa. Tumeishia kuja tu hapa kupoteza muda wetu. Kaka akisikia hili naamini anaweza akaghairi kumsindikiza mkuu wa nchi na kuja hapa mwenyewe. Sijategemea swala kama hili kutokea hapa leo hii, ni kwa bahati nzuri kaka hajaja mwenyewe, la sivyo asingezikubali hizi dharau. Mimi, mzee Imani Mirambo, nishaongea yangu na inatosha, lakini niwahakikishie kuanzia leo na kuendelea mmejitengenezea uadui na familia yetu na hakuna rangi mtaacha kuona.”

Mara baada ya kusikia maneno hayo, ndugu wote wa familia ya Yonesi walijikuta wakianza kupaniki. Likija swala la ushawishi, familia yao ilikuwa ndogo sana kulinganisha na familia ya Mirambo.

“Mzee Mirambo, tuliza jazba na ukae chini tuongee! Unajua binti yangu ni mwenye masihala mengi, alichoongea ni maamuzi ya kukurupuka na sio sahihi, nadhani hata wewe mwenyewe unajua?”

“Jenerali, tushaongea hili na tumemaliza. Ni juu ya kuamini ama kutokuamini, lakini nikuhakikishie uwepo wangu hapa, familia ya Mirambo haiwezi kuwafanya chochote,” aliongea Hamza.

Jenerali Daudi alikuwa na hasira mno kiasi kwamba macho yalishaanza kuwa mekundu.

“Kaa kimya na ondoa mikono yako kwenye mwili wa binti yangu,” alifoka, na Hamza aliishia kushangaa kidogo. Pale pale alitoa mikono yake akiwa na haya usoni, aliona ilikuwa sio sahihi kumshika Yonesi kiuno mbele ya wazazi wake.

“Ondoka! Hatutaki kukukaribisha katika familia yetu,” aliendelea kufoka Meja Jenerali.

“Baba, usiwe hivi. Huelewi tu, lakini Hamza amenisaidia sana…”

“Kaa kimya na wewe! Tumekupigia simu na kukueleza, ukasema umekubali, na sasa hivi unaanza kumtetea huyu mshenzi mwenzako?”

“Lakini baba, sikusema kabisa kama nimekubali kuolewa na Mdudu. Nilisema nitafikiria, lakini sio kukubali. Nimekaa na kuona siwezi kuolewa na mwanaume ambaye simpendi, ni sawa na kujifunga kwenye gereza la hisia zangu mwenyewe.”

Mdudu, mara baada ya kusikia kauli hiyo, uso wake uliiva kwa hasira, na aliishia kusimama na kumwangalia Yonesi kwa macho makali.

“Yonesi, unaongea nini wewe? Kwahiyo unadhani wewe ndio mwanamke pekee ninaweza kuoa? Nimekuchagua wewe kwa sababu nimeona unafaa kuwa mke wangu, lakini unapata ujasiri wa kusema hunipendi?”

Maneno hayo mara baada ya kuwafikia ndugu wa familia ya Yonesi, waliishia kukunja sura, lakini hakuna aliyeweza kusimama na kuongea. Ni mama yake Yonesi pekee aliyepata ujasiri wa kusimama na kuongea.

“Mdudu, kwa nini unaongea hivyo wewe mtoto? Hata kama alichoongea binti yangu kinauma, lakini ana kosa gani kuchagua mtu anayempenda na kua nae?”

Mama huyo mara baada ya kuongea hivyo, Mdudu palepale alijikuta akiona haya baada ya kuona amekosea.

“Mama , naomba usikasirike kwa kunielewa vibaya. Ni kutokana na kuchanganyikiwa. Nimempenda sana Yonesi kwa muda mrefu, ndio maana nimekuja tena kumchumbia, lakini hiki kinachotokea…” Alijikuta akitingisha kichwa.

Mzee Mirambo aliishia kumwangalia mdogo wake, na palepale alimkodolea macho Hamza.

“Wewe mwanaharamu, hivi unadhani ndoa kati ya familia ya Mirambo na Mazengo ni mchezo wa kitoto eh? Unaweza kuingilia utakavyo na kuuharibu? Tayari una mke lakini bado unapata ujasiri wa kuja hapa kujitambulisha kama mpenzi wa binti wa Mzee Daudi. Kama ningekuwa wewe, ningeshikwa na aibu na nisingepata huo ujasiri. Lakini kwa ulichokifanya, umeonyesha ni kwa jinsi gani umekosa aibu,” aliongea kwa hisia kubwa sana. Maneno yale yalimwingia vizuri Afande Daudi, na palepale aliwaangalia walinzi wake.

“Njooni mumchukue, mkamtupe nje huyu mwanaharamu hatumtaqki hapa,” aliongea, na palepale walinzi wa familia hiyo wapatao nane walikimbia kuja eneo hilo. Wote walionekana kuwa na mafunzo makali na ilionyesha walikuwa ni wanajeshi wakakamavu.



































SEHEMU YA 150.

Mara baada ya kuona wale walinzi wanataka kumshambulia ,Yonesi haraka sana aliingilia.

“Baba, usifanye hivyo”

“Kaa kimya na nenda kwenye chumba chako , huruhusiwi kutoka”Alifoka

Yonesi alikuwa na wasiwasi mno , hakuwa na wasiwasi juu ya Hamza bali alikuwa akiwaonea huruma hao walinzi waliotaka kumshika Hamza.

Wale walinzi hata hawakuelewa na palepale walimshika Hamza mkono wakitaka kumuweka chini ya ulinzi.

Lakini sasa kadri walivyokuwa wakijaribu kumvuta Hamza , hawakuweza kumsogeza hata inchi , licha ya kutumia nguvu zao karibia zote.Hamza alikuwa amesimama kama sanamu tu akiwa anawaangalia wanavyohangaika.

Sura za ndugu wote wa Yonesi zilifubaa. Walinzi hao walikuwa na mafunzo na mazoezi makali mno na baadhi yao walikuwa wakijifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi pia.Lakini kitendo cha kushindwa hata kumsogeza kidogo Hamza kiliwashangaza mno.

“Jenerali haina haja ya mimi kuondolewa hapa , nimekuja kwa ajili ya kumpongeza Babu Chalula kwa kutimiza miaka tisini , ndio maana nimeona pia kuwa muwazi juu ya uhusiano wangu na Yonesi , najua hili ni swala gumu kwako kukubali kama mzazi , lakini kulingana na historia ninavyoijua nyie kama warithi wa moja kwa moja wa Chief Mazengo familia yenu ni kubwa kuliko hata ya Mirambo , tukikaa chini na kuongea nina uhakika tunaweza kukubaliana”Aliongea Hamza.

“Kukaa chini na kuognea? Unataka kuongea na sisi nini?”

“Namaanisha unaweza kuweka masharti yako na nitaangalia namna ya kuyatimiza na kisha uniruhusu niondoke na Yonesi , nipo tayari kufanya chochote utakachoongea”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu lakini dakika hio hio mzee Mirambo aliingilia

“Haina haja ya kuendelea kuongea nae , huyu kijana anaona kujiamini kwake anaweza kudharau kila mtu aliekuwepo hapa na tukamsikiliza tu , Jenerali kama familia yako imeshindwa kumuondoa hapa familia yangu ipo tayari”

Mara baada ya kuongea hivyo aligeuka na kumwangalia mwanaume aliekuwa na sura ngumu alievalia koti la leather na miwani ya jua , alikuwa siriasi mno na alama ya kovu la upanga kwenye sura yake lilikuwa waziwazi kabisa.

“Nino hebu mfundishe huyu mpuuzi namna ya kuwa na adabu mbele ya wakubwa”

Yule bwana aliefahamika kwa jina la Nino macho yake yalionekana kuungua kwa tamaa , alionekana kama vile alitamani sana kupambana na Hamza hasa baada ya kuona wale walinzi kushindwa kumsogeza kabisa.

“Bosi wewe ndio ulietoa maagizo , mimi ni nani hata niyakatae , nayapokea kwa mikono yote miwili”Mara baada ya kusikia kauli hio ya mlinzi wa Mzee Mirambo ndugu wa Yonesi wote waliishia kukunja sura

“Mzee Mirambo hata kama unataka kumuondoa hapa huyu mtu , ila ni kheri sisi familia tukihusika katika hili na sio mtu wako maana nyie wote ni wageni”

“Unaongea nini wakati vijana wako wameshindwa hata kumsukuma , kama unahofhia uwezo wa Nino ondoa mashaka kabisa , maana ndio kinara kwenye kambi yake ya mafunzo na juzi tu hapa jeshi limemtumia barua ya kuwa mkufunzi wa Kambi ya Maji ya bluu”

Kila familia kubwa iwe zile za kichifu au za kawaida ilikuwa na kambi yao ya mafunzo ya nishati na mbingu na ardhi ambayo ilikuwa ikifadhili na kusimamia na hii ndio maana ilifanya familia baadhi kuwa na nguvu kubwa kuliko zingine , kutokana na kwamba kadri mbinu yao ya mafunzo inavyofanya kazi na kuwa na wabobezi maana yake pia wanajeshi hao wote wanakuwa chini ya familia hio kusikiliza maagizo yote.

Kambi ya familia ya Mirambo ilifahamika kwa jina la Kambi ya Maji ya Bluu , jina hilo limetokana na mbinu yao ya mafunzo ya nishati ya mbingu na ardhi.

Hamza tokea anaingia hapo alishamwona Nino muda mrefu kama mwanajeshi ambae alikuwa na uwezo mkubwa kutokea upande wa familia ya mirambo.

Upande wa familia ya Mzee Chalula au Chifu Mazengo baada ya kusikia kauli ya Mzee Mirambo , licha ya kuona sio vizuri lakini waliishia kukubali na hio yote ni kutokana na ukweli kwamba hawakuwa na mtaalamu wa kushindana na Nino upande wao.

Nino palepale alipiga hatua kusogea mbele huku akimwangalia Hamza na macho makali.

“Unatoa wapi uthubutu wa kumpokonya bosi wangu mchumba wake , nimesikia uwezo wako ni wajuu sana , nipo hapa kuona ni wa juu kiasi gani”Aliongea Nino kwa kujiamini sana na palepale alisogea ghafla tu na kumsogelea Hamza na kumrushia ngumi ya kichwa.

Hamza ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na mtaalamu wa mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi ya ufunuo wa Maji ya bluu na alitamani kuona mbinu zao za sanaa ya mapigano zipoje , hivyo aliishia kuzuia shambulizi lile na kupiga hatua kadhaa kurudi nyuma na wawili hao walisogea mpaka eneo la uwazi mbele ya ukumbi huo.

“Anga la bluu chanzo cha maji ya bluu , hatua elfu moja za ufunuo wa miguu na mikono!”Aliongea kwa nguvu huku akianza kuchezesha mwili wake kwa namna ya upekee mno kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitaka kimtokee.

Na kadri alivyokuwa akitengeneza mjongeo wa mikono palepale mikono yake na miguu ilianza kuongeza spidi ya hali ya juu kwa zaidi ya mara tatu, alikuwa ni kama vile ni mcheza karate lakini spidi yake ilikuwa ni tofauti na Karate na kutokana na mkono wake na mikuu ilivyokuwa ikicheza kwa spidi ghafla tu ni kama miguu yake imeongezeka na kuwa mingi, palepale alimsogelaa Hamza kwa spidi.

Hamza mara baada ya kuona nguvu yake sio haba alijikuta akilazimika kurudi nyuma zaidi ya mara tatu huku akjitahidi kumkwepa asimshambulie eneo la kifuani.

Nino alijaribu kuendeleza ile mbinu yake kwa spidi lakini kila alivyojaribu kumshambulia Hamza alikosa kabisa na alijikuta akishikwa na mshangao.

“Unashangaza , umewezaje kuzuia ufunuo wa hatua therathini za miguu na mikono yangu bila ya kuwa na nishati ya mbingu hata kidogo ?”Alishangaa.

Kikubwa ni kwamba Hamza hakuwa na mabadiliko makubwa sana , yaani wakati mwenzake akitumia juhudi kubwa kujitutumua na kukusanya nisahti za mbingu na rdhi kushambulia lakini yeye aliishia kujilinda tu na hakupata madhara.

“Unajua kwamba ufunuo wa hatua elfu moja za miguu na mikono zinaenda sawa na mbinu ya Kung Fu ya kichina maarufu kama Tyrant spear? Msingi wa mbinu hio ni kwenye nguvu ya miguu yako , bila kuwa na nguvu ya miguu huna cha maana unachoweza kufanya . Naona upo levo ya Ukaidi wa asili hatua ambayo kama unataka kushindana na mimi kwa kutumia miguu na mikono itakuwa ngumu sana , unaonaje ukijaribu kutumia siraha”

“Unaonekana kuwa mtaalamu kuweza kuona daraja ambalo nipo .. ila wewe huna siraha halafu unataka nitumie siraha , huoni kama nitakuonea?”

“Haha.. msingi wako umeanzia katika kutumia siraha , na mimi msingi wangu unategemea mikono , unannionea kivipi kama huwezi kunishinda?”Aliongea Hamza.

Palepale yule bwana alimwangalia mwenzake aliekuwa pembeni na kisha alimpa ishara na alirushiwa ‘Dhana’ maalumu ya rangi ya silver ambayo yenyewe ukali wake huamshwa na nishati ya mbingu na ardhi.

Kitendo cha Dhana ile kutua katika mikono ya Nino muonekano wake ulibadilika mara moja na kutengeneza msisimko kwa watu wote waliokuwa katika eneo hilo kama vile amegeuka na kuwa mchawi ghafla.

“Kuwa makini , hii Dhana jina lake ni Sifongo hivyo usiitolee sana macho’”Aliongea Nino huku akiwa anajiamini kuliko mwanzo na mara baada ya kuongea kauli yake hio palepale alifyatuka na hatua moja tu alikuwa mbele ya Hamza na kumshambulia na ile siraha.

Lakini Hamza ni kama kuna kiru kimemvuta kwani alisogea pembeni kwa ustadi wa juu sana na siraha ile ikapita juu ya kichwa chake , asingekuwa na wepesi kidogo tu ingemgonga kwenye paji la uso.

“Safi sana , umebobea vizuri kwenye matumizi ya hio siraha”

Ijapokuwa Hamza mwanzo alimdharau Nino , lakini aliona uwezo wake wa kutumia hio siraha ulikuwa unashangaza kiasi chake.

Nino mara baada ya kuona staili yake ya kwanza ya kushambulia haikumletea Hamza madhara yoyote alijikuta akishangaa lakini mwili ulimsisimka na kuona hatimae amepata mshindani sahihi.

“Mjongeo wa nyoka!”

Aliongea kwa nguvu huku akimsogelea Hamza na ile siraha huku akiichezesha na kuifanya kuonekana kama vile ni nyoka jamii ya Cobra.

Hamza alikuwa akikwepa kwa spidi kubwa mno na kilichomtatiza ni kwamba siraha ile ilikuwa ikiacha kivuli na kutengeneza udanganyifu wa macho.

Spidi yao ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba wale ambao hawakuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi hawakuona namna ambavyo Nino anashambulia , walichoona ni kama Nino katengeneza duara pekee.

“Mbona unakimbia tu bila kushambulia , kuna haja gani ya kuendelea kupigana sasa?”Aliongea Nino mara baada ya kuona muda wote yeye ndio aliekuwa akishambulia.

Ijapokuwa alichofanikiwa ni kumchania Hamza shati lake , lakini bado alishindwa kumgusa mwili wake kwa kushindwa kumkadiria eneo lake alipo.

Asichokijua mwenzake alikuwa akijifunza mbinu yake na Hamza mara baada ya kuona staili sita za mbinu hio aliona sasa ni wakati sahihi.

“Muda wa kumaliza mchezo”

Nino palepale alichukua fursa na kuanza kumshambulia Hamza kwa kumlenga kifuani, lakini tofauti na mwanzo Hamza alikuwa amesimama tu bila kufanya chochote na ile siraha yake ikiwa inakaribiana na mwili wake Hamza aliidaka kwa mbele na kumfanya kufadhaishwa na jambo lile.

Alijikuta akijitahidi kuisukuma kutaka kumchoma nayo Hamza , lakini kadri alivyokuwa akijitahidi alishindwa kuisogeza mbele hata nchi moja , mbaya Zaidi Hamza alikuwa ameshikilia eneo la mbele la siraha ile kwenye makali lakini hakuwa na ishara yoyote ya damu kumtoka, ilikuwa ni kama vile mikono yake imetengenezwa na chuma.

“Wewe .. unawezaje ..”Nino alijikuta akibabaika huku akimwangalia Hamza kwa mshangao , wakati akiwa kwenye m shangao Hamza aliipiga ile siraha teke na kufanya mikono ya Nino kuuma na kuiachia bila kupenda na ilifyatuka na kuelekea angani.

Na Dakika hio Hamza ni kama amegeuka mpira kwani palepale alienda kumgonga kwa nguvu Nino.

Bam!!

Nino alijikuta akifyatuliwa na kwenda kutua mita kadhaa nyuma na kudondoka chini.

Tukio hilo liliwafanya watu wote waliokuwa katika bustani hio kupigwa na butwaa wakiwa wanamwangalia Hamza.

Hamza aliishia kunyoosha mkono wake juu na kuidaka ile siraha na kisha kwa nguvu aliikita ardhini.

“Imeisha , imemalizika”Aliongea Hamza akitumia msemo ambao aliusikia mahali..

Tukio hilo lilifanya hali ya watu wote kuwa kimya na zilikuwa ni sauti za vishindo vya Hamza akirudi kwenye ule ukumbi na mara baada ya kuona kundi hilo la watu walikuwa wakimwangalia kama mzimu aliishia kutoa tabasamu.

“Mbona mnaniangalia kwa mwonekno huo , sijamuua mtu , Mtu wenu Nino hajafa kaumia tu pale”Aliongea

Mdudu na Mjomba wake Mirambo nyuso zao zilikuwa zishaanza kuumuka kama unga wa ngano , hawakuwahi kuwaza Hamza anaweza kuwa na nguvu mpaka Nino kutokuwa saizi yake.

Mpaka hapo waliona kweli wapo katika hatari ,walianza kujihisi wapo hatarini .

Yonesi alitamani kuruka ruka kwa furaha kwa namna ambavyo Hamza alionyesha ujasiri, alihisi kujivunia.

Msichana kama yeye ambae amekuzwa na familia ya kijeshi , angependelea kuwa na mwanaume mwenye nguvu na sio mwanaume wa kawaida legelege , hivyo alianza kupata ujasiri mbele ya familia yake.

Pah! Pah !

Chifu Mazengo au Mzee Chalula alijiktua akishindwa kujizuia na kuanza kupiga makofi . Meja Jenerali Daudi Chalula Mazengo ambae alikuwa kimya muda wote macho yake yalichanua.

“Kijana mdogo hasira kubwa, safii, ndio maana mjukuu wangu amepata ujasiri wakuongea mbele ya wazee kwa ajili yako”Aliongea Chifu Mazengo.

“Baba tunafanya nini?”Meja jenerali Daudi alikuwa na wasiwasi.Ijapokuwa alitokea kumchukia Hamza lakini kutokana na uwezo wake hata kama hampendi hakujua namna ya kunzuia.

“Nitafanya maamuzi kama ilivyo ada kwa mkuu wa familia na Chifu wa kizazi cha pili cha Mzee Mazengo, Kijana! Yonesi yupo chini yako kwanzia sasa, mke au mpenzi sijali . Nimetokea kukukubali sana”Aliongea Mzee huyo kwa sauti hafifu lakini yenye msisitizo na kumfanya Hamza kucheka.

“Babu macho yako yanaona mbali kweli , hakika wewe ndio Chifu wa Machifu mrithi wa busara , bila kuzingatia mambo mengi lazima umeshaona urithi wa vina saba vya damu yangu utaleta familia yenye nguvu kwenye ukoo wako, si ndio?”Aliongea Hamza alikuwa akiijua vyema historia ya Chief Mazengo moja ya marafiki wakubwa wa Mwalimu Nyerere , moja ya machifu ambao ndio waliofanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi.

Yonesi mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akiona aibu na kutamani kwenda kumpiga ngumi Hamza , aliona matani ya Hamza hayachagui kabisa mazingira.

Meja Daudi Chalula aliishia kukunja sura akionekana kufubaa , pembeni yake akiwepo Mzee Imani Mirambo rafiki yake ambae anakwenda kumpoteza.

“Mzee Mirambo unaonanaje ukitulia kwanza kuhusu hili swala . naahidi nitakupa maelezo wewe na familia yako”Aliongea , ukweli ni kwamba walikuwa marafiki wakubwa na siku zote Afande Daudi alitaka msaada mkubwa kutoka kwa familia hizo kubwa ili kutimiza malengo yake ya kuwa Mkuu wa majeshi.

Lakini muda huo alijikuta akishindwa kufanya chochote , Hamza alikuwa akijiamini sana na mtu asie na aibu na kumfanya ashindwe kupata udhaifu wake , ki ufupi alifikia hatua ya kushindwa kumfokea tena na kumfukuza nyumbani kwake.

“Kutupa maelezo? Unapanga kutupa maelezo gani? Binti yako ashaongea tayari anataka kuwa mchepuko na hayupo tayari kuolewa na Mdudu . Kwanzia sasa hatuna mpango wa kuendelea kukaribisha sura zetu hapa kwa ajili ya kumuwinda msichana ambae hata hajui kuja kwetu hapa ni favour tu!

“Mdudu ataenda kupata mwanamke mwingine , kuna wanawake warembo sana kutoka familia nzuri tu ndani ya Tanzania nzima , sio nyinyi tu mwenye mtoto wa kike” Mara baada ya kuongea hivyo alisimama na kisha akaamrisha watu wake kuondoka.

“Chifu Mazengo , sisi tunaondoka uniwie radhi sipo tayari kukutakia maisha marefu”Aliongea na Chifu Mazengo alitingisha tu kichwa.

Upande wa Mdudu aliishia kumwangalia Hamza kwa macho makali na kisha akamgeukia na yonesi na bila kuongea neno aliondoka.

Nino mwanajeshi wa kambi ya Maji ya Bluu alifuatia na yeye huku akionekana kuugulia maumivu.

Kitendo cha kumtoa Nino kupambana na Hamza ilikuwa ni kuwakilisha familia yake ya Kichifu , lakini baada ya kuchapika ilikuwa dharau kubwa kwa familia yake na kwa mantiki hio ni kwamba hata wanajeshi ambao wapo chini yao hawakuwa na uwezo wa kushindana na Hamza kutokana na kwamba Nino ndio aliekuwa juu zaidi na kusifika katika ukanda wao.

Baada ya familia hio ya watangulizi wa Chifu Mirambo kuondoka, Yonesi alipatwa na ujasiri wa kuongea.

“Baba , Mom , Babu najua hili linaweza lisiwe zuri kulingana na maadili , lakini nipo siriasi”

“Wewe mtoto usie na shukrani , bado tu unapata uthubutu wa kuongea , Unajua ni mume wa mtu lakini bado unataka kuwa nae ? Unadhani swala hili likitoka nje familia yetu itaonekanaje huko nje?”Aliongea Afande Chalula.

“Jenerali , si nishasema nipo tayari kufidia taswira yenu yote itakayoharibika ? Kama una ombi lolote kutoka kwangu tukae chini na tuongee”

“Kufidia ! Unaenda kufidia vipi? Sijawahi kuona mtu kichaa na mwanaharamu kama wewe”Aliongea kwa hasira.

“Vipi kama nikiifanya familia yako kuwa familia namba moja ya kichifu hapa nchini , vipi inatosha kuniachia Yonesi?”Aliongea Hamza

“…”

Afande Daudi Chalula alijikuta akishangazwa na kauli ile hata ndugu zake wengine wote walikuwa katika mshangao .

Mzee Chalula Mazengo macho yake ya kizee yalichanua huku midomo yake ikicheza na palepale alitoa tabasamu kama vile anadhihaki kile alichoongea Hamza huku akiamini kwa wakati mmoja.

“Angalia Afande sidhani kama itakuwa swala kubwa hata kama lipo nje ya maadili mimi kuendelea kuwa na Yonesi , ili mradi kile mnachopata katika makubaliano yetu ni kikubwa zaidi , ukiangalia hata mpango wenu wa kumuozesha Yoinesi kwa familia ya Mirambo si ilikuwa kwa ajili ya hadhi ya familia yenu? Tuache kuongea mambo ambayo hayana msingi nipeni masharti na nitaangalia kama naweza kuyatimiza na tumalize hili swala kiwepesi sana”Aliongea Hamza akijinadi.

Yonesi mara baada ya kuona hali ya kusita ya baba yake alijikuta moyo wake ukiuma , ukweli ashaelewa tokea mwanzo swala la kutaka kuozeshwa kwa familia ya Mdudu ni kama dili la kibiashara na kutokana na hilo aliona ni kheri kuwa mchepuko kwa mwanaume anaempenda kuliko kuuzwa kwa Mdudu.
“Mna matatizo gani nyie , mbona kila mtu ni kama anaendeshwa na nguvu za giza, Mume wangu mbona umekuwa kimya ghafla na huongei?”Aliongea mama yake Yonesi huku akiwa na sura iliopauka mno kutokana na yale yote yaliokuwa yakiendelea , mama huyo wa kichaga licha ya kwamba alitokea katika asili ya familia ya watafutaji lakini swala la mtoto wake alikuwa siriasi sana.

Afande Chalula alishindwa kuongea lolote , isitoshe bado alikuwa akifikiria kuhusu ukweli wa maneno ya Hamza , hakuwa akimjua Hamza ni nani na nyuma yake ana nguvu gani ya kuongea maneno hayo , alichojua pekee ni kwamba alikuwa na uhusiano wa karibu sana na Mshauri Mkuu.

“Yonesi mwanangu ni kweli unataka kuwa na huyu mwanaume , hata kama thamani yako inaenda kushuka unahisi upo tayari?”Aliongea

“Mama..”Yonesi aliishia kuangalia chini akishindwa kujua cha kuongea mbele ya mama yake , ukweli ni kwamba hata yeye hakujielewa alijua Hamza ameoa na yupo katika mahusiano na Eliza , lakini mara zote alipokuwa akimuona Hamza na Eliza wakiwa pamoja alijihisi kuwa na wivu mkali mno.

Mama Danny mara baada ya kuona Yonesi haongei alimsogelea na kuanza kumpiga vibao vya mgongoni.

“Wewe mtoto mjinga sana , kwanini unanipandisha presha , hivi ndio nilivyokulea?”Alijikuta akishindwa kujizuia na machozi kuanza kumtoka , hakupata picha kwa namna alivyokuwa akjitoa kwa wanawake wenzake kuhudhuria harusi zao na kutoa michango lakini binti yake ambae alimtegemea anakwenda kufidia juhudi zake ndio huyu kakubali kuwa mchepuko , ukiachana na hilo kulingana na tamaduni aliona sio sawa.

“Mama usiwe hivi .. hali yako sio nzuri bado ..” Muda ambao Yonesi anaongea hivyo palepale Mama Danny alionekana kama mtu ambae ameshikwa na pumu ghafla kwani alishindwa kuhema vizuri na alijikuta akishika kifua chake na kukaa chini taratibu.

“Mama!!”

Palepale alidondoka chini na kupoteza fahamu na kumfanya Afande Daudi na wengine kushikwa na mshituko mkubwa.

“Dokta , mwiteni daktari haraka!!”Afande Daudi aliongea kwa nguvu.

Hamza mara baada ya tukio lile haraka sana alimsogelea mama yake Yonesi na kushika mkono wake na kuanza kupima msukumo wa damu na kisha palepale aliegamiza sikio kifuani kusikiliza mapigo ya moyo.

END OF SEASON 05.. 0687151346 .
 
SHETANI RUDISHA NAFSI ZETU.



MTUNZI:SINGANOJR​



SEHEMU YA 149.

Kijana mdogo hasira kubwa

Mara baada ya Yonesi kusikia kauli hiyo, mwili wake ulitetemeka kwa sekunde kadhaa. Haraka aligeuza kichwa chake pembeni na kuziba uso wake kwa mikono miwili. Moyo ulikuwa ukienda mbio mno.

“Haha, Yonesi jana uliniuliza swali kwa ujasiri mno, kwanini sasa unakuwa na aibu hivyo?”

Yonesi alijikuta akivuta pumzi mara mbili. Hakuwa tayari kushindwa tena. Aligeuka na kumtazama Hamza akiwa na ujasiri.

“Unaongea ujinga, nani anaona aibu?” Aliongea, na Hamza akaona hakuna haja ya kuendelea kumchokoza.

“Okey okey, ni kweli huna aibu, basi chukua kwanza upate chochote uchangamshe tumbo, safari ndefu hii.” Aliongea Hamza, na kumfanya Yonesi kumkodolea macho, asijue mwanaume huyo anafikiria nini.

Hata chakula alipokea kimya kimya na kuendelea kula taratibu, akiendelea kuwaza.

“Hivi vidude ni vitamu mno lakini wanauza ghali…” Aliongea Hamza huku akitafuna.

Yonesi hakuona utamu wowote. Moyo wake muda huo ulikuwa umefumbwa na hisia mchanganyiko, na kumfanya kuona kama alikuwa ndotoni.

“Yonesi, unawaza nini? Mbona umekodoa macho hivyo?”

“Ni kweli unaenda nyumbani kwetu?”

“Ndio, si nishakwambia? Kama siendi kwenu kwanini nipande treni?”

“Lakini unaenda kuwaambia nini wazazi wangu? Mkurugenzi anajua unasafiri?” Aliuliza akiwa na wasiwasi mkubwa.

“Hata sijali kuhusu hilo, ninachojua nakupenda. Ijapokuwa sijui ni kwa kiasi gani, lakini siwezi kukuona ukiolewa na Mdudu.”

“Huoni kama unafanya mambo kwa kukurupuka? Ijapokuwa familia yetu si kama nyingine kubwa, lakini haimaanishi wataweza kuingilika kirahisi. Isitoshe, kama Mkurugenzi akisikia kuhusu hili atakasirika mno.”

“Hata kama familia yenu ingekuwa ya raisi, hakuna wa kunizuia. Kama familia yenu ni ya kawaida kwanini wanizuie? Kuhusu mke wangu, hilo niachie mimi. Nitajua namna ya kumbembeleza. Nikichanganywa na mwanamke mmoja kama mwanaume nitaishi vipi?”

“Wewe, aisee unajua kukurupuka kweli,” aliongea Yonesi, akikosa neno.

“Hehe… mwenzako Eliza jana kasema kanipendea kwa sababu ya kukurupuka kwangu, wewe unaonaje?”

“Kwahiyo jana ulikuwa na Da’ Eliza?”

“Ndio, nimetokea kwake asubuhi ya leo na kuja moja kwa moja stesheni.”

Yonesi alijikuta akituliza hisia na kujiambia kweli huyu playboy ameshindikana. Hata hivyo, alikuwa katika hali ya kupaniki maana alishindwa kujua ni kitu gani Hamza anapanga kufanya wakifika nyumbani.

Saa sita kasoro ndio muda walioweza kufika stesheni kuu ya treni Dodoma, na wakati wakiwa wanatoka waliweza kumuona mwanaume mzee wa makamo akiwa amesimama pamoja na wanaume wengine wawili waliovalia mavazi ya suti.

“Yonesi, hatimaye nakuona tena,” mwanaume yule aliyevalia suti ya kijivu aliongea kwa uchangamfu.

Yonesi, mara baada ya kumuona mzee huyo, na yeye pia alitabasamu na kumsogelea kumsalimia kwa furaha.

“Mjomba Sauli, unaendeleaje?” Aliuliza Yonesi, lakini swali lake lilikuwa la kijinga sana kutokana na kwamba mzee huyo alikuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi katika levo ya mzunguko kamili, maana yake umri wake wa kuishi ni mkubwa na si rahisi kuumwa kirahisi.

Hamza, mara baada ya kuona mzee huyo ndiye aliyekuja kumpokea Yonesi, aliona kweli familia ya Yonesi ilikuwa ya kijeshi na kichifu.

Kuna muda Hamza mwenyewe alikuwa akijiuliza , katika mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi Tanzania haikuwa na muda mrefu sana tokea ipate ufahamu wa mafunzo haya , lakini kulikuwa na wazee wengi ambao walionekana kuwa na mafunzo hayo muda mrefu sana na kujiuliza wametokea wapi.

Mzee Sauli hakuwa mwanajeshi wa moja kwa moja , alikuwa ni wazee tu waliochipukia katika familia ya Chifu Mazengo na kupewa kazi ya ulinzi na kusimamia kazi zote za familia , kama ni wazungu wangempa cheo cha Buttler.

“Unaonekana kukua kiasi chake Yonesi”Aliongea huku akichunguza mwili wa Yonesi na aliweza kuhisi amekuwa tofauti , ijapokuwa hakujua ni mafunzo gani lakini aliweza kuona utofauti hasa upande wa ukomavu wake wa kiakili.

Yote hayo yalikuwa ni mafunzo ya Hamza aliomwelekeza Yonesi kutumia.

Muda uleule yule mzee aliinua uso wake na kumwangalia Hamza . Alikuwa ameishi maisha marefu sana ndani na nje ya Tanzania na kuona watu wengi wa kawaida na wasiokuwa wa kawaida , lakini kitendo cha macho yake kutua kwa Hamza aliweza kugundua sio mtu wa kawaida palepale.

“Bwana mdogo , Yonesi ni rafiki yako?”

“Haha.. wewe endio Mzee Sauli si ndio , wakati tukiwa njiani Yonesi alikuwa akinielezea habari zako na anasema wewe ndie uliekuwa ukimpenda sana , wakati akiwa mdogo wazazi wake wakimfokea alikuja kwako kukulalamikia,. Mimi kama mpenzi wa Yonesi nichukue fursa hii kukushukuru kwa kumjali kwa wakati wote mpenzi wangu”Aliongea Hamza huku akiwa amemshika mkono yule mzee na matendo yake yalimfanya Mzee Sauli kuwa katika mshangao.

Yonesi alishindwa kuona namna uso wake umeiva , hakujua Hamza atakuwa spidi spidi kwenye kujitambulisha mapema kama mpenzi wake kama hivyo.

“Wewe.. kwahio ndio mpenzi wa Yonesi?”Aliuliza kwa shauku lakini kwa wakati mmoja akiwa katika hali ya wasiwasi.

“Mjomba tuondoke kwanza , ni stori ndefu”Aliongea Yonesi akiingilia maongezi.

Mzee Yule aliishia kuvuta pumzi na kuzishusha , alikuwa kama mtu ambae ametegemea kuna jambo kubwa litatokea wakati wa sherehe ya Mzee Chalula.

Maisha aliokuwa akiishi Yonesi Dar pamoja na kazi yake utadhania hakuwa wa kishua , familia yake ni moja ya familia tajiri sana ndani ya mji wa Dodoma na yenye historia yenye mizizi mirefu.

Baada ya kutoka nje kabisa waliingai katika Mercedenz Benz nyeusi na kuianza safari ya kuelekea nyumbani kwao.

Wakiwa njiani kuelekea huko Yonesi alipewa taarifa kwamba , familia ya Mdudu wapo nyumbani na wamekusanyika wengi wa ukoo wao wakiamini kabisa hatimae ile siku ya kuunganisha familia hizo mbili imewadia .

Kutokana na taarifa hio , Yonesi alizidi kushikwa na wasiwasi mkubwa mno , upande wa Hamza yeye hakuwa na wasiwasi kabisa , macho yake yote yalikuwa nje akiangalia mazingira na alikuwa akiuliza maswali yaliokuwa nje kabisa ya mada.

Mzee huyo aliishia kumwangalia Hamza na kuona hakuwa na uwezo kabisa wa kujua ni kitu gani kinamfanya Hamza kujiamini na kutokana na mwonekano huo alizidi kuona sio mtu wa kawaida.

Ukweli ni kwamba kama familia ya Mzee Chalula wangetumia koneksheni yao kutaka kumjua Hamza kupitia kitengo cha Malibu , wangeweza kujua swala la kisiwani Chole , lakini kwa bahati mbaya swala la kisiwani kule lilikuwa ni siri sana na ni watu wachache sna ndani ya vitengo cya usalama walikuwa wakilifahamu.

Baada ya nusu saa gari kutembea , hatimae gari iliingia katika mtaa maarufu wa Kwa Chifu Mazengo au Mvumi Makulu, sehemu hio ilikuwa ikiitwa kwa Chalula kutokana na kwamba Mzee Chalula ndio mtu wa kwanza kabisa kujenga hapo na baadae serikali ilifanyia eneo hilo marekebisho na kuita Mji mpya lakini hata hivyo pamezoeleka zaidi kama Kwa Chifu Chalula wa Mazengo.

Nyumbani kwa Yonesi kulikuwa kumezungukwa na miti mingi na uoto wake ulikuwa ni ule wa kupandwa na sio wa asili kutokana na maeneo mengi kutofautiana na eneo hilo.

Baada ya kushuka katika megesho maalumu , kulikuwa na magari mengi yaliokuwa ndani ya eneo hilo tayari na mengi yalikuwa ni V8 na Prado.

Mandhari ya eneo hilo yalimfurahisha Hamza, na akajiambia angalau watu wa mkoani walikuwa wakiishi vizuri, ijapokuwa nyumba zilizokuwa ndani ya eneo hilo zilikuwa na muundo wa kikale, lakini mazingira yake hayakuwa mabaya.

"Yonesi, babu yako, baba yako na mama wapo kule nyuma. Nikupeleke kwanza chumbani kwako ukabadili mavazi au unaelekea moja kwa moja kuwasalimia?" aliuliza mjomba.

"Haina haja ya kubadili. Mjomba, naomba uniitie mtu kunisaidia kubeba mabegi yangu, nitaenda kusalimiana nao kwanza," aliongea Yonesi na kisha alimgeukia Hamza.

"Mpango wako ni upi?" Aliuliza Yonesi, akimwangalia Hamza.

"Na mimi naenda kuwasalimia na pia kuwaelezea swala letu kwa familia yako," alijibu Hamza akiwa na tabasamu, lakini Yonesi alionyesha ishara ya kutaka kumzuia.

"Acha wasiwasi, tunaenda pamoja. Huwezi kunizuia hivyo, ni bora ukaanza kujiamini kuanzia hapa," alisema Hamza.

"Basi usiwe mkali sana, mama yangu afya yake si nzuri sana, akishikwa na hasira anaweza kupandwa na presha," alisema Yonesi, na Hamza alitikisa kichwa kukubaliana naye.

Staili ya ujenzi wa eneo hilo ilikuwa ya kizamani sana. Japo nyumba zilikuwa nzuri, upangiliaji wake ulifanya ionekane kama kituo cha afya.

Baada ya kuingia kwenye korido ndefu iliyojitegemea, walipita bustani kadhaa zilizotengenezwa vizuri, na hatimaye wakaingia kwenye uwanja mdogo uliokuwa umepandwa mizambarau.

Njiani, baadhi ya wafanyakazi waliomwona Yonesi na Hamza waliishia kumwangalia kwa kumshangaa na kumsalimia kwa wakati mmoja.

Baada ya kuzunguka hadi nyuma, hatimaye waliweza kufika kwenye ukumbi mmoja uliokuwa umejengwa kwa makuti, na kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakiongea na kucheka kwa sauti, hali iliyofanya eneo hilo kuwa la furaha na kuchangamka.

Kadri walivyokuwa wakisogelea eneo hilo, ndivyo Yonesi alivyozidi kujawa na wasiwasi. Aliishia kujikaza kijeshi na kufanya hatua zake zionekane kama mtu anayejiamini.

Mbele kabisa, kulikuwa na mzee mtu mzima kabisa aliyevalia koti kubwa la manyoya la kitamaduini kabila la wagogo na kofia kichwani. Huyu alikuwa babu yake Yonesi. Ijapokuwa mwonekano wake ulikuwa wa kizee, macho yake yalionekana kuona vizuri kabisa.

Upande wa kulia kwake kulikuwa na mwanaume mwingine wa makamo, aliyevalia kombati za kijeshi za cheo cha Meja Jenerali. Huyu alikuwa baba yake Yonesi, Afande Daudi Chalula. Pembeni yake kulikuwa na mwanamke mwenye mwonekano wa kitajiri, maarufu kama Mama Danny. Huyu ndiye mama mzazi wa Yonesi.

Kulikuwa na wanaume wengine waliokuwa katika mavazi ya kijeshi, karibu wengi wakiwa na vyeo vya nyota tatu na ngao, na ilionekana walikuwa ni ndugu wa Yonesi.

Hata hivyo, waliokuwa wakimpa wasiwasi zaidi Yonesi ni watu waliokuwa wamekaa upande wa kushoto, upande wa wageni, wakiongozwa na Afande Mdudu na wazee wachache wa ukoo wake. Macho yao yote yalikuwa kwa Yonesi kama kwamba ndiye mtu pekee waliyekuwa wakimsubiria.

"Yonesi!" Mama Danny, mara baada ya macho yake kutua kwa Yonesi, aliinuka na kumkimbilia, akamkumbatia kwa hisia kubwa.

Yonesi alikuwa amemmisi sana mama yake. Alimwangalia na kuona alikuwa amezeeka mno, na alishindwa kujizuia kushikwa na hatia, akatoa chozi.

Unaweza ukashangaa kwa nini mzazi huyo asingesafiri kuja mpaka Dar kumuona mtoto wake kama alikuwa amemmisi sana, lakini baada ya Yonesi kutoroka nyumbani akiikimbia ndoa baada ya kufeli mafunzo nchini Chile, baba yake, Meja jenerali Daudi, alipiga marufuku familia nzima kutomtafuta Yonesi, ikiwemo mke wake.

"Hamza!" Afande Mdudu aliita mara baada ya kumuona, huku uso wake ukifubaa.

"Mdudu, unamfahamu yule kijana?" wazee wa familia yake waliuliza.

"Mjomba, yule ndiye Hamza, ndiye mtu anayefahamiana na mshauri mkuu na kuniambia nisimsumbue tena Yonesi," aliongea Mdudu, huku akionyesha kuwa bado alikuwa na hasira na Hamza.

Mdudu, tokea amkose Yonesi kwa kupewa vitisho na Hamza, aliomba kuacha jeshi na kujiingiza katika siasa. Alikuwa ni mjukuu wa kwanza Chifu Mirambo. Mjomba wake Imani alikuwa ni moja ya viongozi wa juu wa serikali akiwa amehudumu kama Waziri wa ulinzi chini ya Rais Mbilu. Ijapokuwa kwa wakati huo alikuwa mbunge tu baada ya kushinda uchaguzi, lakini alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa katika nafasi za juu za kuteuliwa uwaziri katika serikali mpya.

Baada ya Imani kusikia kwamba Hamza ndiye aliyeingilia swala la ndoa ya Mdudu na Yonesi, alijikuta hakuridhishwa na hali hiyo.

"Jenerali, kwa nini huyu mtu amekuja hapa? Kuonekana kwake katika familia yako si kama kutudharau?" aliuliza Mrambo kwa hasira, huku akipiga meza.

“Yonesi sogea hapa haraka na umwambie babu yako nini kinaendelea , huyo uliekuja nae ni nani?”

Yonesi ilibidi aachiane na mama yake na kisha alienda mpaka walipo wazee na kisha kuanza kusalimia

“Anaitwa Hamza ni ra…”

“Yonesi ni mpenzi wangu”Hamza alisogea haraka na kuongea.

Mara baada ya kusikia kauli hio watu wote katika ukumbi huo walijikuta wakishikwa na mshangao . Yonesi aliishia kukunja ngumi tu huku mikono yake ikishikwa na jasho kwa wasiwasi.

“Mzee Chalula , nini kinaendelea , Hawa watoto si ndio waliosema wenyewe wanakwenda kusahau yaliopita na kukubali kuchumbiana? Mdudu mwenyewe amekubali kuacha yaliopita na yupo hiari kumuoa mjukuu wako , Au hii inamaanisha familia yenu haijawahi kuchukulia hili suala kwa uzito wake ndio maana mnaenda mbali hivi?”Aliongea Mirambo kwa hasira huku akipiga meza.

“Mzee Mrambo punguza jazba , Familia yetu imekuwa na taswira nzuri kwa muda mrefu . Kama binti yangu amekosea , nipo tayari kuomba radhi”Aliongea Afande Daudi na kisha akamgeukia binti yake.

"Yonesi, hebu tuambie kama alichoongea huyu kijana ni kweli," aliuliza, na Yonesi aliishia kukaa kimya, akiwa ameinamisha kichwa chake chini, akishindwa kukubali. Isitoshe, Hamza hakuwahi kumtongoza vizuri na kumkubali.

Mama Danny wasiwasi ulimshika kutokana na kubadilika kwa hali ya hewa na alimshika mkono binti yake.

“Yonesi ongea , Kwanini ghafla tu umekuja na mpenzi?”

“Mama ni .. nampenda Hamza”Baada ya kusita aliishia kung’ata meno kuutafuta ujasiri na hatimae akafanikiwa kuongea.

Maneno hayo baada ya kumtoka kila mtu aliekuwa katika ukumbi huo alipiga kimya .

Hamza kwa upande wake alifurahishwa na kauli hio mno na palepale kwa kujiamini alisogea mbele na kusimama kando ya Yonesi.

“Wazee wangu kwanza naomba niwape salamu wote , nadhani wachache wananijua kwa kuniona na kunisikia , kwa wale wasionijua kwa jina naitwa Hamza Mzee na kwa mpangilio wa kinachoendelea hapa nadhani litakuwa jambo la busara kama mipango ya ndoa ikibadilika kidogo . Kutoka mwanzo mpaka mwisho , hakuna mmoja wenu aliemuuliza Yonesi kama anampenda Mdudu , kwa mantiki hii naona kabisa hatua muhimu imerukwa, Karne za kumtafutia mtoto wa kumuoa ama kuolewa nae zishapitwa na wakati, Au mnasemaje wazee wangu?”

Mdudu mara baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Hamza ni kama alikuwa akisiliza matusi na alishindwa kujizuia na kusimama.l

“Hamza acha kutumia ubabe kupata kila unachotaka ! Wewe tayari umeoa na mke wako anajulikana ni Regina mmiliki wa makampuni ya Dosam , unadhani sijakufanyia uchunguzi , inamaana unataka kumgeuza Yonesi Mchepuko?”

Maneno ya Mdudu yalikuwa ni kama bomu lingine lilowaangukia wazee hao na kusababisha kila ndugu wa Yonesi sura kukunja kama wamelishwa pilipili. Yonesi aliishia kutetemeka asijue ni kipi anaweza kufanya

“Kama unadhani hiyo ni pointi sana, basi nitaanza mchakato wa kubadilisha uraia na kuchagua taifa ambalo linaruhusu mwanaume kuoa wanawake wengi, kwanza nina jina la kiislamu unasemaje hapo” aliongea Hamza.

“Wewe…” Mdudu alijikuta akishangazwa na kauli ya Hamza maana hakuitegemea. Katika maisha yake hakuwahi kuona mtu aliyekosa aibu kama Hamza.

“Kikubwa ni kwamba nampenda Yonesi, na yeye pia ananipenda, na tuna furaha kuwa pamoja iwe nimeoa ama sijaoa, na hakuna cha kufanya juu ya hili.”

“Wewe mwanaharamu usiye na heshima mbele ya wazee. Unadhani tunaweza kuendelea kuvumilia kejeli zako kwa sababu tu unajuana na Mshauri Mkuu. Mdudu anaweza kuwa mdogo na kuhofia kitengo cha Malibu, lakini mimi, Mzee Imani Mirambo, sijawahi kuogopa mtu.” Mara baada ya kuongea kauli hiyo, aligeuza macho yake na kuwaangalia ndugu wa familia ya Chalula.

“Mzee Chalula, Jenerali, naona binti yenu ni mkanuni mno. Yaani juzi amekubali, na leo anaenda kinyume na maneno yake bila hata kutupa taarifa. Tumeishia kuja tu hapa kupoteza muda wetu. Kaka akisikia hili naamini anaweza akaghairi kumsindikiza mkuu wa nchi na kuja hapa mwenyewe. Sijategemea swala kama hili kutokea hapa leo hii, ni kwa bahati nzuri kaka hajaja mwenyewe, la sivyo asingezikubali hizi dharau. Mimi, mzee Imani Mirambo, nishaongea yangu na inatosha, lakini niwahakikishie kuanzia leo na kuendelea mmejitengenezea uadui na familia yetu na hakuna rangi mtaacha kuona.”

Mara baada ya kusikia maneno hayo, ndugu wote wa familia ya Yonesi walijikuta wakianza kupaniki. Likija swala la ushawishi, familia yao ilikuwa ndogo sana kulinganisha na familia ya Mirambo.

“Mzee Mirambo, tuliza jazba na ukae chini tuongee! Unajua binti yangu ni mwenye masihala mengi, alichoongea ni maamuzi ya kukurupuka na sio sahihi, nadhani hata wewe mwenyewe unajua?”

“Jenerali, tushaongea hili na tumemaliza. Ni juu ya kuamini ama kutokuamini, lakini nikuhakikishie uwepo wangu hapa, familia ya Mirambo haiwezi kuwafanya chochote,” aliongea Hamza.

Jenerali Daudi alikuwa na hasira mno kiasi kwamba macho yalishaanza kuwa mekundu.

“Kaa kimya na ondoa mikono yako kwenye mwili wa binti yangu,” alifoka, na Hamza aliishia kushangaa kidogo. Pale pale alitoa mikono yake akiwa na haya usoni, aliona ilikuwa sio sahihi kumshika Yonesi kiuno mbele ya wazazi wake.

“Ondoka! Hatutaki kukukaribisha katika familia yetu,” aliendelea kufoka Meja Jenerali.

“Baba, usiwe hivi. Huelewi tu, lakini Hamza amenisaidia sana…”

“Kaa kimya na wewe! Tumekupigia simu na kukueleza, ukasema umekubali, na sasa hivi unaanza kumtetea huyu mshenzi mwenzako?”

“Lakini baba, sikusema kabisa kama nimekubali kuolewa na Mdudu. Nilisema nitafikiria, lakini sio kukubali. Nimekaa na kuona siwezi kuolewa na mwanaume ambaye simpendi, ni sawa na kujifunga kwenye gereza la hisia zangu mwenyewe.”

Mdudu, mara baada ya kusikia kauli hiyo, uso wake uliiva kwa hasira, na aliishia kusimama na kumwangalia Yonesi kwa macho makali.

“Yonesi, unaongea nini wewe? Kwahiyo unadhani wewe ndio mwanamke pekee ninaweza kuoa? Nimekuchagua wewe kwa sababu nimeona unafaa kuwa mke wangu, lakini unapata ujasiri wa kusema hunipendi?”

Maneno hayo mara baada ya kuwafikia ndugu wa familia ya Yonesi, waliishia kukunja sura, lakini hakuna aliyeweza kusimama na kuongea. Ni mama yake Yonesi pekee aliyepata ujasiri wa kusimama na kuongea.

“Mdudu, kwa nini unaongea hivyo wewe mtoto? Hata kama alichoongea binti yangu kinauma, lakini ana kosa gani kuchagua mtu anayempenda na kua nae?”

Mama huyo mara baada ya kuongea hivyo, Mdudu palepale alijikuta akiona haya baada ya kuona amekosea.

“Mama , naomba usikasirike kwa kunielewa vibaya. Ni kutokana na kuchanganyikiwa. Nimempenda sana Yonesi kwa muda mrefu, ndio maana nimekuja tena kumchumbia, lakini hiki kinachotokea…” Alijikuta akitingisha kichwa.

Mzee Mirambo aliishia kumwangalia mdogo wake, na palepale alimkodolea macho Hamza.

“Wewe mwanaharamu, hivi unadhani ndoa kati ya familia ya Mirambo na Mazengo ni mchezo wa kitoto eh? Unaweza kuingilia utakavyo na kuuharibu? Tayari una mke lakini bado unapata ujasiri wa kuja hapa kujitambulisha kama mpenzi wa binti wa Mzee Daudi. Kama ningekuwa wewe, ningeshikwa na aibu na nisingepata huo ujasiri. Lakini kwa ulichokifanya, umeonyesha ni kwa jinsi gani umekosa aibu,” aliongea kwa hisia kubwa sana. Maneno yale yalimwingia vizuri Afande Daudi, na palepale aliwaangalia walinzi wake.

“Njooni mumchukue, mkamtupe nje huyu mwanaharamu hatumtaqki hapa,” aliongea, na palepale walinzi wa familia hiyo wapatao nane walikimbia kuja eneo hilo. Wote walionekana kuwa na mafunzo makali na ilionyesha walikuwa ni wanajeshi wakakamavu.



































SEHEMU YA 150.

Mara baada ya kuona wale walinzi wanataka kumshambulia ,Yonesi haraka sana aliingilia.

“Baba, usifanye hivyo”

“Kaa kimya na nenda kwenye chumba chako , huruhusiwi kutoka”Alifoka

Yonesi alikuwa na wasiwasi mno , hakuwa na wasiwasi juu ya Hamza bali alikuwa akiwaonea huruma hao walinzi waliotaka kumshika Hamza.

Wale walinzi hata hawakuelewa na palepale walimshika Hamza mkono wakitaka kumuweka chini ya ulinzi.

Lakini sasa kadri walivyokuwa wakijaribu kumvuta Hamza , hawakuweza kumsogeza hata inchi , licha ya kutumia nguvu zao karibia zote.Hamza alikuwa amesimama kama sanamu tu akiwa anawaangalia wanavyohangaika.

Sura za ndugu wote wa Yonesi zilifubaa. Walinzi hao walikuwa na mafunzo na mazoezi makali mno na baadhi yao walikuwa wakijifunza kuvuna nishati za mbingu na ardhi pia.Lakini kitendo cha kushindwa hata kumsogeza kidogo Hamza kiliwashangaza mno.

“Jenerali haina haja ya mimi kuondolewa hapa , nimekuja kwa ajili ya kumpongeza Babu Chalula kwa kutimiza miaka tisini , ndio maana nimeona pia kuwa muwazi juu ya uhusiano wangu na Yonesi , najua hili ni swala gumu kwako kukubali kama mzazi , lakini kulingana na historia ninavyoijua nyie kama warithi wa moja kwa moja wa Chief Mazengo familia yenu ni kubwa kuliko hata ya Mirambo , tukikaa chini na kuongea nina uhakika tunaweza kukubaliana”Aliongea Hamza.

“Kukaa chini na kuognea? Unataka kuongea na sisi nini?”

“Namaanisha unaweza kuweka masharti yako na nitaangalia namna ya kuyatimiza na kisha uniruhusu niondoke na Yonesi , nipo tayari kufanya chochote utakachoongea”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu lakini dakika hio hio mzee Mirambo aliingilia

“Haina haja ya kuendelea kuongea nae , huyu kijana anaona kujiamini kwake anaweza kudharau kila mtu aliekuwepo hapa na tukamsikiliza tu , Jenerali kama familia yako imeshindwa kumuondoa hapa familia yangu ipo tayari”

Mara baada ya kuongea hivyo aligeuka na kumwangalia mwanaume aliekuwa na sura ngumu alievalia koti la leather na miwani ya jua , alikuwa siriasi mno na alama ya kovu la upanga kwenye sura yake lilikuwa waziwazi kabisa.

“Nino hebu mfundishe huyu mpuuzi namna ya kuwa na adabu mbele ya wakubwa”

Yule bwana aliefahamika kwa jina la Nino macho yake yalionekana kuungua kwa tamaa , alionekana kama vile alitamani sana kupambana na Hamza hasa baada ya kuona wale walinzi kushindwa kumsogeza kabisa.

“Bosi wewe ndio ulietoa maagizo , mimi ni nani hata niyakatae , nayapokea kwa mikono yote miwili”Mara baada ya kusikia kauli hio ya mlinzi wa Mzee Mirambo ndugu wa Yonesi wote waliishia kukunja sura

“Mzee Mirambo hata kama unataka kumuondoa hapa huyu mtu , ila ni kheri sisi familia tukihusika katika hili na sio mtu wako maana nyie wote ni wageni”

“Unaongea nini wakati vijana wako wameshindwa hata kumsukuma , kama unahofhia uwezo wa Nino ondoa mashaka kabisa , maana ndio kinara kwenye kambi yake ya mafunzo na juzi tu hapa jeshi limemtumia barua ya kuwa mkufunzi wa Kambi ya Maji ya bluu”

Kila familia kubwa iwe zile za kichifu au za kawaida ilikuwa na kambi yao ya mafunzo ya nishati na mbingu na ardhi ambayo ilikuwa ikifadhili na kusimamia na hii ndio maana ilifanya familia baadhi kuwa na nguvu kubwa kuliko zingine , kutokana na kwamba kadri mbinu yao ya mafunzo inavyofanya kazi na kuwa na wabobezi maana yake pia wanajeshi hao wote wanakuwa chini ya familia hio kusikiliza maagizo yote.

Kambi ya familia ya Mirambo ilifahamika kwa jina la Kambi ya Maji ya Bluu , jina hilo limetokana na mbinu yao ya mafunzo ya nishati ya mbingu na ardhi.

Hamza tokea anaingia hapo alishamwona Nino muda mrefu kama mwanajeshi ambae alikuwa na uwezo mkubwa kutokea upande wa familia ya mirambo.

Upande wa familia ya Mzee Chalula au Chifu Mazengo baada ya kusikia kauli ya Mzee Mirambo , licha ya kuona sio vizuri lakini waliishia kukubali na hio yote ni kutokana na ukweli kwamba hawakuwa na mtaalamu wa kushindana na Nino upande wao.

Nino palepale alipiga hatua kusogea mbele huku akimwangalia Hamza na macho makali.

“Unatoa wapi uthubutu wa kumpokonya bosi wangu mchumba wake , nimesikia uwezo wako ni wajuu sana , nipo hapa kuona ni wa juu kiasi gani”Aliongea Nino kwa kujiamini sana na palepale alisogea ghafla tu na kumsogelea Hamza na kumrushia ngumi ya kichwa.

Hamza ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na mtaalamu wa mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi ya ufunuo wa Maji ya bluu na alitamani kuona mbinu zao za sanaa ya mapigano zipoje , hivyo aliishia kuzuia shambulizi lile na kupiga hatua kadhaa kurudi nyuma na wawili hao walisogea mpaka eneo la uwazi mbele ya ukumbi huo.

“Anga la bluu chanzo cha maji ya bluu , hatua elfu moja za ufunuo wa miguu na mikono!”Aliongea kwa nguvu huku akianza kuchezesha mwili wake kwa namna ya upekee mno kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitaka kimtokee.

Na kadri alivyokuwa akitengeneza mjongeo wa mikono palepale mikono yake na miguu ilianza kuongeza spidi ya hali ya juu kwa zaidi ya mara tatu, alikuwa ni kama vile ni mcheza karate lakini spidi yake ilikuwa ni tofauti na Karate na kutokana na mkono wake na mikuu ilivyokuwa ikicheza kwa spidi ghafla tu ni kama miguu yake imeongezeka na kuwa mingi, palepale alimsogelaa Hamza kwa spidi.

Hamza mara baada ya kuona nguvu yake sio haba alijikuta akilazimika kurudi nyuma zaidi ya mara tatu huku akjitahidi kumkwepa asimshambulie eneo la kifuani.

Nino alijaribu kuendeleza ile mbinu yake kwa spidi lakini kila alivyojaribu kumshambulia Hamza alikosa kabisa na alijikuta akishikwa na mshangao.

“Unashangaza , umewezaje kuzuia ufunuo wa hatua therathini za miguu na mikono yangu bila ya kuwa na nishati ya mbingu hata kidogo ?”Alishangaa.

Kikubwa ni kwamba Hamza hakuwa na mabadiliko makubwa sana , yaani wakati mwenzake akitumia juhudi kubwa kujitutumua na kukusanya nisahti za mbingu na rdhi kushambulia lakini yeye aliishia kujilinda tu na hakupata madhara.

“Unajua kwamba ufunuo wa hatua elfu moja za miguu na mikono zinaenda sawa na mbinu ya Kung Fu ya kichina maarufu kama Tyrant spear? Msingi wa mbinu hio ni kwenye nguvu ya miguu yako , bila kuwa na nguvu ya miguu huna cha maana unachoweza kufanya . Naona upo levo ya Ukaidi wa asili hatua ambayo kama unataka kushindana na mimi kwa kutumia miguu na mikono itakuwa ngumu sana , unaonaje ukijaribu kutumia siraha”

“Unaonekana kuwa mtaalamu kuweza kuona daraja ambalo nipo .. ila wewe huna siraha halafu unataka nitumie siraha , huoni kama nitakuonea?”

“Haha.. msingi wako umeanzia katika kutumia siraha , na mimi msingi wangu unategemea mikono , unannionea kivipi kama huwezi kunishinda?”Aliongea Hamza.

Palepale yule bwana alimwangalia mwenzake aliekuwa pembeni na kisha alimpa ishara na alirushiwa ‘Dhana’ maalumu ya rangi ya silver ambayo yenyewe ukali wake huamshwa na nishati ya mbingu na ardhi.

Kitendo cha Dhana ile kutua katika mikono ya Nino muonekano wake ulibadilika mara moja na kutengeneza msisimko kwa watu wote waliokuwa katika eneo hilo kama vile amegeuka na kuwa mchawi ghafla.

“Kuwa makini , hii Dhana jina lake ni Sifongo hivyo usiitolee sana macho’”Aliongea Nino huku akiwa anajiamini kuliko mwanzo na mara baada ya kuongea kauli yake hio palepale alifyatuka na hatua moja tu alikuwa mbele ya Hamza na kumshambulia na ile siraha.

Lakini Hamza ni kama kuna kiru kimemvuta kwani alisogea pembeni kwa ustadi wa juu sana na siraha ile ikapita juu ya kichwa chake , asingekuwa na wepesi kidogo tu ingemgonga kwenye paji la uso.

“Safi sana , umebobea vizuri kwenye matumizi ya hio siraha”

Ijapokuwa Hamza mwanzo alimdharau Nino , lakini aliona uwezo wake wa kutumia hio siraha ulikuwa unashangaza kiasi chake.

Nino mara baada ya kuona staili yake ya kwanza ya kushambulia haikumletea Hamza madhara yoyote alijikuta akishangaa lakini mwili ulimsisimka na kuona hatimae amepata mshindani sahihi.

“Mjongeo wa nyoka!”

Aliongea kwa nguvu huku akimsogelea Hamza na ile siraha huku akiichezesha na kuifanya kuonekana kama vile ni nyoka jamii ya Cobra.

Hamza alikuwa akikwepa kwa spidi kubwa mno na kilichomtatiza ni kwamba siraha ile ilikuwa ikiacha kivuli na kutengeneza udanganyifu wa macho.

Spidi yao ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba wale ambao hawakuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi hawakuona namna ambavyo Nino anashambulia , walichoona ni kama Nino katengeneza duara pekee.

“Mbona unakimbia tu bila kushambulia , kuna haja gani ya kuendelea kupigana sasa?”Aliongea Nino mara baada ya kuona muda wote yeye ndio aliekuwa akishambulia.

Ijapokuwa alichofanikiwa ni kumchania Hamza shati lake , lakini bado alishindwa kumgusa mwili wake kwa kushindwa kumkadiria eneo lake alipo.

Asichokijua mwenzake alikuwa akijifunza mbinu yake na Hamza mara baada ya kuona staili sita za mbinu hio aliona sasa ni wakati sahihi.

“Muda wa kumaliza mchezo”

Nino palepale alichukua fursa na kuanza kumshambulia Hamza kwa kumlenga kifuani, lakini tofauti na mwanzo Hamza alikuwa amesimama tu bila kufanya chochote na ile siraha yake ikiwa inakaribiana na mwili wake Hamza aliidaka kwa mbele na kumfanya kufadhaishwa na jambo lile.

Alijikuta akijitahidi kuisukuma kutaka kumchoma nayo Hamza , lakini kadri alivyokuwa akijitahidi alishindwa kuisogeza mbele hata nchi moja , mbaya Zaidi Hamza alikuwa ameshikilia eneo la mbele la siraha ile kwenye makali lakini hakuwa na ishara yoyote ya damu kumtoka, ilikuwa ni kama vile mikono yake imetengenezwa na chuma.

“Wewe .. unawezaje ..”Nino alijikuta akibabaika huku akimwangalia Hamza kwa mshangao , wakati akiwa kwenye m shangao Hamza aliipiga ile siraha teke na kufanya mikono ya Nino kuuma na kuiachia bila kupenda na ilifyatuka na kuelekea angani.

Na Dakika hio Hamza ni kama amegeuka mpira kwani palepale alienda kumgonga kwa nguvu Nino.

Bam!!

Nino alijikuta akifyatuliwa na kwenda kutua mita kadhaa nyuma na kudondoka chini.

Tukio hilo liliwafanya watu wote waliokuwa katika bustani hio kupigwa na butwaa wakiwa wanamwangalia Hamza.

Hamza aliishia kunyoosha mkono wake juu na kuidaka ile siraha na kisha kwa nguvu aliikita ardhini.

“Imeisha , imemalizika”Aliongea Hamza akitumia msemo ambao aliusikia mahali..

Tukio hilo lilifanya hali ya watu wote kuwa kimya na zilikuwa ni sauti za vishindo vya Hamza akirudi kwenye ule ukumbi na mara baada ya kuona kundi hilo la watu walikuwa wakimwangalia kama mzimu aliishia kutoa tabasamu.

“Mbona mnaniangalia kwa mwonekno huo , sijamuua mtu , Mtu wenu Nino hajafa kaumia tu pale”Aliongea

Mdudu na Mjomba wake Mirambo nyuso zao zilikuwa zishaanza kuumuka kama unga wa ngano , hawakuwahi kuwaza Hamza anaweza kuwa na nguvu mpaka Nino kutokuwa saizi yake.

Mpaka hapo waliona kweli wapo katika hatari ,walianza kujihisi wapo hatarini .

Yonesi alitamani kuruka ruka kwa furaha kwa namna ambavyo Hamza alionyesha ujasiri, alihisi kujivunia.

Msichana kama yeye ambae amekuzwa na familia ya kijeshi , angependelea kuwa na mwanaume mwenye nguvu na sio mwanaume wa kawaida legelege , hivyo alianza kupata ujasiri mbele ya familia yake.

Pah! Pah !

Chifu Mazengo au Mzee Chalula alijiktua akishindwa kujizuia na kuanza kupiga makofi . Meja Jenerali Daudi Chalula Mazengo ambae alikuwa kimya muda wote macho yake yalichanua.

“Kijana mdogo hasira kubwa, safii, ndio maana mjukuu wangu amepata ujasiri wakuongea mbele ya wazee kwa ajili yako”Aliongea Chifu Mazengo.

“Baba tunafanya nini?”Meja jenerali Daudi alikuwa na wasiwasi.Ijapokuwa alitokea kumchukia Hamza lakini kutokana na uwezo wake hata kama hampendi hakujua namna ya kunzuia.

“Nitafanya maamuzi kama ilivyo ada kwa mkuu wa familia na Chifu wa kizazi cha pili cha Mzee Mazengo, Kijana! Yonesi yupo chini yako kwanzia sasa, mke au mpenzi sijali . Nimetokea kukukubali sana”Aliongea Mzee huyo kwa sauti hafifu lakini yenye msisitizo na kumfanya Hamza kucheka.

“Babu macho yako yanaona mbali kweli , hakika wewe ndio Chifu wa Machifu mrithi wa busara , bila kuzingatia mambo mengi lazima umeshaona urithi wa vina saba vya damu yangu utaleta familia yenye nguvu kwenye ukoo wako, si ndio?”Aliongea Hamza alikuwa akiijua vyema historia ya Chief Mazengo moja ya marafiki wakubwa wa Mwalimu Nyerere , moja ya machifu ambao ndio waliofanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi.

Yonesi mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akiona aibu na kutamani kwenda kumpiga ngumi Hamza , aliona matani ya Hamza hayachagui kabisa mazingira.

Meja Daudi Chalula aliishia kukunja sura akionekana kufubaa , pembeni yake akiwepo Mzee Imani Mirambo rafiki yake ambae anakwenda kumpoteza.

“Mzee Mirambo unaonanaje ukitulia kwanza kuhusu hili swala . naahidi nitakupa maelezo wewe na familia yako”Aliongea , ukweli ni kwamba walikuwa marafiki wakubwa na siku zote Afande Daudi alitaka msaada mkubwa kutoka kwa familia hizo kubwa ili kutimiza malengo yake ya kuwa Mkuu wa majeshi.

Lakini muda huo alijikuta akishindwa kufanya chochote , Hamza alikuwa akijiamini sana na mtu asie na aibu na kumfanya ashindwe kupata udhaifu wake , ki ufupi alifikia hatua ya kushindwa kumfokea tena na kumfukuza nyumbani kwake.

“Kutupa maelezo? Unapanga kutupa maelezo gani? Binti yako ashaongea tayari anataka kuwa mchepuko na hayupo tayari kuolewa na Mdudu . Kwanzia sasa hatuna mpango wa kuendelea kukaribisha sura zetu hapa kwa ajili ya kumuwinda msichana ambae hata hajui kuja kwetu hapa ni favour tu!

“Mdudu ataenda kupata mwanamke mwingine , kuna wanawake warembo sana kutoka familia nzuri tu ndani ya Tanzania nzima , sio nyinyi tu mwenye mtoto wa kike” Mara baada ya kuongea hivyo alisimama na kisha akaamrisha watu wake kuondoka.

“Chifu Mazengo , sisi tunaondoka uniwie radhi sipo tayari kukutakia maisha marefu”Aliongea na Chifu Mazengo alitingisha tu kichwa.

Upande wa Mdudu aliishia kumwangalia Hamza kwa macho makali na kisha akamgeukia na yonesi na bila kuongea neno aliondoka.

Nino mwanajeshi wa kambi ya Maji ya Bluu alifuatia na yeye huku akionekana kuugulia maumivu.

Kitendo cha kumtoa Nino kupambana na Hamza ilikuwa ni kuwakilisha familia yake ya Kichifu , lakini baada ya kuchapika ilikuwa dharau kubwa kwa familia yake na kwa mantiki hio ni kwamba hata wanajeshi ambao wapo chini yao hawakuwa na uwezo wa kushindana na Hamza kutokana na kwamba Nino ndio aliekuwa juu zaidi na kusifika katika ukanda wao.

Baada ya familia hio ya watangulizi wa Chifu Mirambo kuondoka, Yonesi alipatwa na ujasiri wa kuongea.

“Baba , Mom , Babu najua hili linaweza lisiwe zuri kulingana na maadili , lakini nipo siriasi”

“Wewe mtoto usie na shukrani , bado tu unapata uthubutu wa kuongea , Unajua ni mume wa mtu lakini bado unataka kuwa nae ? Unadhani swala hili likitoka nje familia yetu itaonekanaje huko nje?”Aliongea Afande Chalula.

“Jenerali , si nishasema nipo tayari kufidia taswira yenu yote itakayoharibika ? Kama una ombi lolote kutoka kwangu tukae chini na tuongee”

“Kufidia ! Unaenda kufidia vipi? Sijawahi kuona mtu kichaa na mwanaharamu kama wewe”Aliongea kwa hasira.

“Vipi kama nikiifanya familia yako kuwa familia namba moja ya kichifu hapa nchini , vipi inatosha kuniachia Yonesi?”Aliongea Hamza

“…”

Afande Daudi Chalula alijikuta akishangazwa na kauli ile hata ndugu zake wengine wote walikuwa katika mshangao .

Mzee Chalula Mazengo macho yake ya kizee yalichanua huku midomo yake ikicheza na palepale alitoa tabasamu kama vile anadhihaki kile alichoongea Hamza huku akiamini kwa wakati mmoja.

“Angalia Afande sidhani kama itakuwa swala kubwa hata kama lipo nje ya maadili mimi kuendelea kuwa na Yonesi , ili mradi kile mnachopata katika makubaliano yetu ni kikubwa zaidi , ukiangalia hata mpango wenu wa kumuozesha Yoinesi kwa familia ya Mirambo si ilikuwa kwa ajili ya hadhi ya familia yenu? Tuache kuongea mambo ambayo hayana msingi nipeni masharti na nitaangalia kama naweza kuyatimiza na tumalize hili swala kiwepesi sana”Aliongea Hamza akijinadi.

Yonesi mara baada ya kuona hali ya kusita ya baba yake alijikuta moyo wake ukiuma , ukweli ashaelewa tokea mwanzo swala la kutaka kuozeshwa kwa familia ya Mdudu ni kama dili la kibiashara na kutokana na hilo aliona ni kheri kuwa mchepuko kwa mwanaume anaempenda kuliko kuuzwa kwa Mdudu.
“Mna matatizo gani nyie , mbona kila mtu ni kama anaendeshwa na nguvu za giza, Mume wangu mbona umekuwa kimya ghafla na huongei?”Aliongea mama yake Yonesi huku akiwa na sura iliopauka mno kutokana na yale yote yaliokuwa yakiendelea , mama huyo wa kichaga licha ya kwamba alitokea katika asili ya familia ya watafutaji lakini swala la mtoto wake alikuwa siriasi sana.

Afande Chalula alishindwa kuongea lolote , isitoshe bado alikuwa akifikiria kuhusu ukweli wa maneno ya Hamza , hakuwa akimjua Hamza ni nani na nyuma yake ana nguvu gani ya kuongea maneno hayo , alichojua pekee ni kwamba alikuwa na uhusiano wa karibu sana na Mshauri Mkuu.

“Yonesi mwanangu ni kweli unataka kuwa na huyu mwanaume , hata kama thamani yako inaenda kushuka unahisi upo tayari?”Aliongea

“Mama..”Yonesi aliishia kuangalia chini akishindwa kujua cha kuongea mbele ya mama yake , ukweli ni kwamba hata yeye hakujielewa alijua Hamza ameoa na yupo katika mahusiano na Eliza , lakini mara zote alipokuwa akimuona Hamza na Eliza wakiwa pamoja alijihisi kuwa na wivu mkali mno.

Mama Danny mara baada ya kuona Yonesi haongei alimsogelea na kuanza kumpiga vibao vya mgongoni.

“Wewe mtoto mjinga sana , kwanini unanipandisha presha , hivi ndio nilivyokulea?”Alijikuta akishindwa kujizuia na machozi kuanza kumtoka , hakupata picha kwa namna alivyokuwa akjitoa kwa wanawake wenzake kuhudhuria harusi zao na kutoa michango lakini binti yake ambae alimtegemea anakwenda kufidia juhudi zake ndio huyu kakubali kuwa mchepuko , ukiachana na hilo kulingana na tamaduni aliona sio sawa.

“Mama usiwe hivi .. hali yako sio nzuri bado ..” Muda ambao Yonesi anaongea hivyo palepale Mama Danny alionekana kama mtu ambae ameshikwa na pumu ghafla kwani alishindwa kuhema vizuri na alijikuta akishika kifua chake na kukaa chini taratibu.

“Mama!!”

Palepale alidondoka chini na kupoteza fahamu na kumfanya Afande Daudi na wengine kushikwa na mshituko mkubwa.

“Dokta , mwiteni daktari haraka!!”Afande Daudi aliongea kwa nguvu.

Hamza mara baada ya tukio lile haraka sana alimsogelea mama yake Yonesi na kushika mkono wake na kuanza kupima msukumo wa damu na kisha palepale aliegamiza sikio kifuani kusikiliza mapigo ya moyo.

END OF SEASON 05.. 0687151346 .
Thanks
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU.



MTUNZI:SINGANOJR



SEHEMU YA 151.​

Mkuu wa Majeshi​

Hamza mara baada ya kuinama na kumchunguza mgonjwa hali yake , palepale aligeuka na kumwangalia baba yake Yonesi.

“Alikuwa akisumbuliwa na nini?”

“Hebu pisha njia, halikuhusu hili swala”Aliongea Afande Daudi kwa hasira.

“Sitafuti ugomvi hapa , nakuuliza kwasababu mimi ni daktari , niambie kama anashida ya mzunguko wa damu kati ya moyo na mapafu?”

Mara baada ya kusikia hivyo mzee huyo alijikuta akinywea , hata baadhi ya ndugu walishangaa maana hawakujua kama Hamza ni dokta mpaka kuweza kugundua shida ya mgonjwa haraka hivyo.

“Umejuaje , juzi mke wangu ametoka hospitalini na kuambiwa ana mvilio kwenye ateri ya kupeleka damu kwenye mapafu..”Aliongea Afande huku akiona ni ajabu Hamza kuweza kuona tatizo kwa kwa kusikiliza mapigo yake ya moyo pekee.

“Tumpelekeni hospitalini kwanza, mgonjwa alikuwa katika hali mbaya lakini mkaamua kumtoa hospitalini,”aliongea Hamza.

“Hamza mama yangu hali yake ni mbaya sana?,”aliuliza Yonesi akiamini kwa uwezo wa Hamza hawezi kudanganya kuwa daktari.

“Kwasasa siwezi kusema chochote kwasababu hakuna vipimo vya kitaalamu , ila kwa ninachoona sio Thrombosi ya kawaida”Alisema.



“Acha kutuogopesha , mke wangu yupo sawa na atapona”Aliongea kibishi na palepale muda huo gari ya kuchukulia wagonjwa ilifika na taratibu za kuwahishwa hospitalini zikaanza.

Aliebakia nyumbani alikuwa Mzee Chalula peke yake , watu wote walipanda gari nyingine binafsi kuelekea hospitali kubwa ya jeshi Dodoma na mara baada ya kufika mgonjwa alipokelewa na alipewa huduma ya kwanza haraka haraka na aliweza kurudiwa na fahamu. Lakini hata hivyo alitakiwa kufanyiwa vipimo vingine.

Dokta aliekuwa akimhudumia alikuwa ni mganga mkuu msaidizi wa hospitalini hio akifahamika kwa jina la Dokta Leornard Milanzi, ambae pia alikuwa ni mwanajeshi.

Na kama kawaida kutokana na mgonjwa kuwa mke wa Meja Jenerali madaktari bingwa waliitwa mara moja kwa ajili ya kumwangalia afya yake kwa kusaidiana.

Dokta Milanzi alikuwa ameshikilia mkanda wa picha za kifua za mgonjwa na alikuwa akiifanyia uchunguzi.

“Jenerali , angalia huu mkanda unaonyesha kuwepo kwa uvimbe aina ya mvilio ndani ya mshipa unaotoa damu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye mapafu ..”

“Dokta Milanzi hakuna ninachoelewa hapo , tueleze kwa lugha nyepesi ni kwa namna gani mke wangu anaweza kupata matibabu na kupona?”Aliongea lakini Hamza palepale alisogea na kuchukua ule mkanda wa picha na kuanza kuuchunguza lakini kitendo kile kilimfanya Dokta Milanzi kumwangalia Hamza kwa macho ya kutoridhika na tabia yake.

“Wewe ni nani?”

“Mimi ni daktari Bingwa zaidi yako”Aliongea Hamza

Dokta Milanzi alijihisi ni kama hajasikia vizuri lakini aligundua hakuwa na shida ya masikio.

“Jenerali ,huyu ndio dokta uliekuja nae?”Aliuliza .

“Hamza unafanya nini? Mke wangu hali yake ni mbaya hebu acha kujaribu kusababisha matatizo mengine hapa?”aliongea Afande Daudi kwa kukaripia lakini Hamza wala hakujali na palepale alianza kuongea kwa lugha ya kingereza.

“Embolization of the pulmonary artery from the trunk all the way to the left side of the pulmonary artery. If you do an operation, it will still be a little difficult to remove the intima of the pulmonary artery.”Aliongea akimaanisha kwamba damu imeganda na kuziba njia kutoka kwenye shina la mshipa kuelekea upande wa kushoto wa ateri ya palmonari na hata kama upasuaji ukifanyika itakuwa ngumu.

Mara baada ya kusikia maneno yake ya kingereza yaliojaa mantiki , madaktari waliokuwepo hapo waliangaliana kwa mshangao.

“Dokta Milanzi! Alichoongea ni sahihi?, mimi nimeelewa hapo aliposema upasuaji utakuwa mgumu”aliongea akiwa ni kweli hajaaelewa vizuri lakini kingereza chake cha mawasiliano kilimtosha kung’amua maneno ya Hamza na vilevile kutokana na madaktari hao walivyokuwa kimya ilimtia wasiwasi.

“Jenerali , alichoongea ni kweli , lakini kama tutatumia njia ya vidonge anaweza kupona kabisa na hakutakuwa na shida kubwa”Aliongea.

“Umekosea na unaongea ujinga”aliongea Hamza akiwa amekunja sura.

“Wewe ni nani kwanza na unatoa wapi ujeuri wa kukaidi ushauri wa kitabibu unatoka kwa wataalamu?”

“Yaani ukubwa wote huo wa mvilio mnataka kutumia vidonge, kama sio kumsababishia mgonjwa kifo cha ghafla ni nini?. Kama mnaogopa kufanya upasuaji na kuishia kutoa vidonge si sawa tu na kuhatarisha maisha ya wagonjwa?”

“Kifo cha ghafla!?” Afande Daudi alishangazwa na kauli hio na alimwangalia Dokta Milanzi kwa maswali.

“Dokta Milanzi alichoongea ni kweli?”Aliuliza akiwa siriasi na kumfanya Dokta Milanzi jasho kuanza kumtoka

“Ki nadharia inawezekana lakini asilimia za kutokea hivyo ni ndogo sana, usiwe na wasiwasi”

“Kitakachomponya ni upasuaji pekee , angalau nikiufanya mimi huo upasuaji nina uwezo wa kumponya mama yako kwa asilimia mia moja”Aliongea Hamza na kumfanya Yonesi kushikwa na wasiwasi wa kutoamini maneno ya Hamza.

“Hamza hivi unajua kweli kufanya upasuaji? Wewe ni dokta?”Aliuliza na Hamza aliishia kutoa kicheko cha chini.

“Kwanini nikudanganye sasa , huu sio muda wa kufanya masihala , kuponya na kuokoa maisha ya mgonjwa ni swala linalohitaji umakini mkubwa na usiriasi”.

“Hata kama upasuaji ufanyike tutafanya wenyewe, kwanza udaktari wako umeupatia wapi , leseni unayo?”Aliuliza Dokta Milanzi na kumfanya Hamza kushindwa kujibu maana hakuwa na hizo leseni na nyaraka za kumtambulisha kama daktari.

Mara baada ya kuona Hamza anashindwa kutoa jibu , Dokta Milanzi alizidi kujawa na kejeli zidi ya Hamza.

“Jenerali , tutaandaa utaratibu wa kumfanyia upasuaji mke wako , usiwe na wasiwasi kabisa , sisi ni madaktari wazoefu na tuna asilimia chache sana za kufeli”

“Sio suala la asilimia chache za kufeli , ninachotaka kusikia ni kama hamtoshindwa”aliongea Afande.

“Kuhusu hilo Jenerali , nadhani unajua upasuaji una hatari zake , tafadhari unapaswa kutuelewa maana mambo mengine yapo nje ya uwezo wetu”

“Hakutakuwa na hatari nikifanya mimi”aliongea Hamza aliekuwa pembeni.

“Huna hata leseni ya udaktari lakini unapata ujeuri wa kuongea hivyo? Kwenye ulimwengu huu ni Daktari gani ambae hawezi kufanya makosa ! Uhatari unaoweza kuibuka wakati wa upasuaji ni kitu ambacho hakuna daktari anaweza kutarajia. Mweupe sana kichwani wewe”Aliongea Dokta Milanzi na Hamza hakujali na alimwangalia Afande Daudi.

“Jenerali , kama unataka mke wako kupona kwa asilimia tisini na nane au mia unapaswa kufikiria kwa umakini”Aliongea Hamza.

Upande wa Afande Daudi alikuwa akipingana mwenyewe ndani kwa ndani , hakumwamini kabisa Hamza , isitoshe alimuona ni mdogo sana kuwa mtaalamu anaeweza kufanya upasuaji wa moyo.

Lakini hata hivyo aliona kwakuwa mdogo na kisha kuwa na uwezo wa kimapigano wa namna ile alioshuhudia lazima atakuwa jiniasi kweli na atakuwa hadanganyi lakini bila uthibitisho hakutaka kuamini.

“Siwezi kubetia uhai wa mke wangu kwa maneno yako pekee , upasuaji huu utaendelea kuwa chini ya Dokta Milanzi”Aliongea , hakuthubutu kumruhusu Hamza kwani alikosa leseni ya kumthibitisha kweli ni daktari.

Hamza aliona ni haki yake kuwa makini , hata yeye pengine asingekubali bila ya kuwa na ushahidi.

“Kama ni hivyo , naomba nitoe pendekezo lingine?

“Pendekezo gani?”

“Mgonjwa ashawahi kufanyiwa kipimo cha PET-CT?”aliuliza Hamza.

“Ndio nini hicho?”

“Jenerali PET_CT ni Positron Emission Tomography and Computed Tomography. Lakini kwanini unataka tufanye hiki kipimo wakati tushajua kila kitu kuhusu shida ya mgonjwa?”Aliuliza Dokta Milanzi.

“Nadhani itakuwa vizuri mkifanya hiki kipimo, kwasababu nilivyomuona mgonjwa niligundua sio tu kwamba alikuwa na shida ya kupumua lakini mwonekano wake ulikuwa ni wa kuchoka mno , ni kama alikuwa na maumivu ya mgongo”

“Ndio mke wangu ana shida ya maumivu ya mgongo , inahusiana na huu ugonjwa?”Aliuliza Afande Daudi mara baada ya kusikia maelezo ya Hamza na siku zote hakuwahi kuwaza labda shida yake ya mgongo inaweza kuwa na uhusiano na shida yake ya moyo , alifikiria labda itakuwa ni kutokana na kuzeeka.

Dokta Milanzi na wenzake walionekana wameweza kufikiria kitu na kupatwa na ufumbuzi wa jambo.

“Are you saying that Madam may have pulmonary artery sarcoma?”Aliuliza kwa kingereza kwa mshangao akimaanisha kama anadhani Madam anaweza kuwa na saratani.

“Nahisi hivyo ,ijapokuwa ni saratani adimu lakini mara inapotokea inakuwa na dalili sawa kabisa na za Pulmonary Embolisim, isitoshe pia kulingana na taarifa , wapo wagonjwa wengi walifanyiwa upasuaji huku diagnosis za ugonjwa zikikosewa, au nakosea?”Aliongea Hamza.

Ijapokuwa wanafamilia wengi wa Mzee Daudi hawakuelewa istilahi za kimatibabu lakini mara baada ya kusikia neno saratani walijua hali sio nzuri kwa mgonjwa wao.

“Dokta Milanzi fanya haraka na mfanyie hicho kipimo kuona kama ni kweli”aliongea afande bila kujali kitu kingine tena.

Ijapokuwa Dokta Milanzi aliona sio swala la kupaniki sana lakini aliishia kukubali na kuanza utaratibu wa kipimo hicho, uzuri ni kwamba Hospitali ya jeshi ya Dodoma ni moja ya hospitali kubwa sana ukiachana na Mayaya Clinic na Benjamini Mkapa, hivyo ilikuwa na kila aina ya kipimo.

Saa moja baadae vipimo vya PET-CT viliweza kukamilika na baada ya matokeo kutoka , madaktari bingwa wa hospitali hio sura zao zilibadilika na kuwa mbaya kama wametafuna nzi kwa bahati mbaya.

Dokta Milanzi ambae ndio aliekuwa ameshikilia matokeo , mikono yake ilianza kutetemeka na hakujua hata namna ya kuanza kuelezea.

“Ni uvimbe mkubwa sana , ndio maana alikuwa akipata maumivu ya mgongo”Aliongea Hamza akikodolea sehemu nyeupe katika picha na kisha akaendelea kuongea .

“Kulingana na ukubwa wake hawezi kuishi zaidi ya mwezi bila kufanyiwa upasuaji”

“Hamza kwahio unasema mama yangu ni kweli ana cancer? Kama ni hivyo tunafanya nini jamani?”aliongea Yonesi sasa akiamini zaidi Hamza kuwa daktari.

“Usiwe na wasiwasi , naweza kumfanyia upasuaji na akapona kabisa , hakuna kibaya kinaweza mkuta”aliongea Hamza akiwa amemshika mkono Yonesi kumtuliza.

“Madaktari nadhani mlifanya makosa?”Aliongea Afande Daudi akiwa na uso uliokuwa umezidi kuongezeka weusi.

“Ni kweli , Samahani sana Jenerali hatukutegemea , kawaida aina hii ya uvimbe ni adimu sana kutokea katika mshipa wa damu, hatukuweza kufikiria mbali”

“Sio kwamba hakumfikiria mbali , shida yenu moja mnatanguliza hadhi ya mgonjwa kabla ya shida yake , kwasababu ni mke wa mkuu wa jeshi kila mtu anataka kuhusika katika matibabu yake. Ukiweka uzito wako sehemu ambayo sio sahihi , matokeo yake ni kufanya makosa makubwa.Mtu wa Bucha akikosea kukata sehemu wakati wakuuza nyama anachokifanya ni kubadili sehemu tu lakini vipi kuhusu daktari?”aliongea Hamza kama vile anafokea watoto wadogo , ikumbukwe Dokta Milanzi hakuwa Mganga mkuu kibahati bahati alikuwa na uzoefu wa zaidi ya miaka ishirini na tano katika fani ya kupasua moyo na kufanya diagnosis.

“Hata kama upo sahihi , utaweza kufanya upasuaji? Unapaswa kuelewa adhesion ya huu uvimbe ni kubwa mno , bila ya upasuaji wa kutumia nguvu huwezi kuukata”Aliongea Dokta Milanzi akikataa kuwa mnyonge.

“Jisemee nafsi yako, nina jiamini kwa asilimia mia moja ninao uwezo wa kuifanya na ikafanikiwa”

“Acha majigambo , kwahio unadhani sisi wataalamu wote hapa hatuna uzoefu? Upasuaji mgumu siku zote unafanikiwa kwa kushirikiana na wataalamu wengi”walianza kubishana.

“Upusuaji unaanza saa ngapi au lini? Siwezi kuona mke wangu akiishi kwa mwezi mmoja tu”Aliongea Afande Daudi kitemi mara baada ya kuona wanaendelea kubishana bila kuwa na mwafaka.

“Jenerali tunaweza kuufanya leo hii’

“Kama ni hivyo kwanini hamfanyi maandalizi?”Aliongea , hakutaka tena kuongea kipole

Dokta Milanzi alichukuana na wataalamu wenzake na kisha walikaa chini na kuanza kujadiliana namna ya kuanza upasuaji huo . Lakini alikuwa na wasiwasi mno , ni kama mtu ambae anaweka maisha yake rehani.

“Baba si umwache tu Hamza afanye huo upasuaji , ndio alieweza kujua shida ya mama kikamilifu , mimi namwamini”aliongea Yonesi na kumfanya Afande Daudi kumkodolea macho Hamza.

“Kama unamwamini ni wewe ila sio mimi , kama nikimwacha akifanya upasuaji na kufanikiwa kumukoa mama yako si ataanza kujinadi kwetu”

“Baba hili ni swala la kujali sasa hivi? Kupona kwa mama ndio muhimu”

“Dokta Milanzi ana uzoefu wa kutosha , hawezi kufeli namwamini sana”Aliongea kibabe na kisha alimsukuma Yonesi pembeni na kutembea kutoka nje kwa hatua ndefu na buti zake za kijeshi.

“Yonesi usiwe na wasiwasi , nitaingia nao kwenye chumba cha upasuaji baadae na kujifanyisha naangalia , likitokea tatizo nitachukua hatua”Aliongea Hamza akimfariji Yonesi.

Mrembo huyo mwanajeshi aliishia kumwangalia Hamza na macho yenye wekundu na kutingisha kichwa.

Jioni hatimae upasuaji ulianza na Hamza alisema anaenda kuangalia tu na kuingia ndani , Afande Daudi alitaka kumzuia lakini alijikuta akisita kufanya hivyo.

Kundi la madaktari bingwa walisimama nje ya chumba wakiangalia upasuaji huo katika srini kubwa huku wakiwa na maiki kwa ajili ya kutoa msaada kwa Dokta Milanzi amabe anaongoza upasuaji huo , maana wasingeweza kuingia wote kwenye chumba cha upasuaji.

Dokta Milanzi mara baada ya kushika kisu mkononi alifumba macho kwa sekunde kadhaa na kisha alivuta pumzi nyingi na kuzitoa nje na kisha alitangaza kuanza kufanya upasuaji wa kuondoa uvimbe(Pulmonary Artery tumor).

Hamza alikuwa amesimama mbali kidogo akiangalia madaktari bingwa hao wakiwa bize na hakuongea chochote.

Dokta Milanzi mara baada ya kupasua na kuona uvimbe wenyewe,macho yake yalicheza kwa wasiwasi.

“Dokta nashindwa kuona uvimbe ulipoanzia”Aliongea msaidizi wake na kumfanya Dokta Milanzi kuona hali imekuwa siriasi kuliko alivyotegemea.

“Increase the size of the surgical opening and give me the scalpel …”aliongea na palepale waliongeza ukubwa wa mpasuo na mara baada ya Dokta Milanzi kuchungulia sura iligeuka ya kijivu.

“Naona uvimbe ni mkubwa mpaka umefikia kwenye tundu la chemba ya kulia ya moyo”

“Profesa tunafanyaje , tutaweza vipi kuukata?”Aliongea msaidizi akiwa na wasiwasi mkubwa na kumfanya Dokta Milanzi Kung’ata meno .

“Hakuna namna tunapaswa kuukata tu hivyo hivyo, fanya haraka na ondoa kwanza hizo pincer?”aliongea na palepale alianza kujaribu kuukata lakini mishipa ya damu ilikuwa ikimzuia kufanya chochote kwa kuogopa kuitaka

“Dokta mbona jasho linakutoka sana?”

“Dokta Milanzi sidhani kama unaweza kuendelea kwa staili hio , naona tumekosea kuchukulia ukubwa wa uvimbe”Aliongea dokta aliekuwa nje akitoa ushauri.

Afande Daudi Chalula Mazengo mara baada ya kusikia kauli hio , alijikuta akishikwa na wasiwasi mno kiasi cha uso kumfubaa.

“Milanzi mbona huendelei , si umesema unaweza kufanya upasuaji na kufanikiwa?”aliuliza kwa hasira.

Dokta Milanzi alikuwa amechanganyikiwa na alijiambia kama ni mgonjwa wa kawaida angeachana nae tu ajifie, lakini siku hio mgonjwa alikuwa ni wa mkuu wake wa jeshi na kama akifeli kaburi linamwita.

Muda huo Hamza alisogea na kisha alimsukuma Dokta Milanzi pembeni.

“Hebu sogea pembeni huko naona unatetemeka tu”Aliongea Hamza na kisha palepale aliinua uso wake na kuangalia nje kupitia Kamera.

“Jenerali ninakwenda kumfanyia upasuaji mke wako , kama unataka atoke hapa akiwa hai ni kheri kutoa maagizo hawa watu hapa wanisikilize ninachowaambia”aliongea Hamza na Afande Daudi kumwangalia mke wake aliekuwa hajitambui alijikuta akishindwa kuvumilia.

“Sawa! Kwanzia sasa Hamza ataendelea na upasuaji na toeni ushirikiano wenu”Aliongea na walitingisha vichwa.

Hamza palepale aligeuka na kuomba kuvalishwa miwani maalumu ya kukuza na nesi hakubisha na haraka haraka alimvalisha Hamza kila kitu muhimu kama dokta anaeongoza upasuaji.

Hamza aliangalia kwanza ile sehemu waliopasua kwa sekunde kadhaa na kisha bila kujali kitu kingine alianza kazi.

Tofauti na Milanzi , mbinu ya Hamza ilikuwa ya haraka na sahihi kwa asilimia kubwa , ni kama alikuwa amefanya upasuaji kama huo huo mwanzo.

“Dokta upo spidi sana , vipi unapanga kuukata uvimbe wote?” Madaktari wasaidizi wawili walishangazwa na spidi ya Hamza na kile alichokuwa akipanga kufanya, hata kwa Dokta Milanzi mwenyewe alikuwa katika mshangao.

Mara baada ya kuona hivyo Afande Daudi na Yonesi walijikuta wakishikwa na tumaini.

“Tunaanza kuukata uvimbe , wewe sijui dokta Milanzi hyebu acha kusimama na kuangalia tu nisaidie kuvuta uvimbe kwa mbele”Aliongea Hamza na Dokta Milanzi hakutaka ego kumvaa , kutokana na uwezo wa Hamza haraka sana alisogea na kuwa msaidizi wa kwanza.

Hamza umakini wake wote alikuwa ameuweka kwenye kuondoa uvimbe na spidi yake ilifanya madaktari wote waliokuwa wakiangalia upasuaji huo kushikwa na mshangao.

“Nitaanza na ujenzi wa Right ventricular outlet ..”aliongea Hamza na madaktari walitingisha kichwa kukubaliana nae.

“Dokta hii mbinu… inamaana hatukati kwanzia upande wa kushoto wa mapafu?”

“Unaongea ujinga gani?”

“Kwanini , vipi kama uvimbe ukikua na kuhamia upande wa kushoto wa mapafu?”

“Wewe huoni uvimbe tushaukata tayari , hawezi kupata shida ili mradi akishapona”aliongea Hamza kwa kingereza na wale madaktari waliishia kutingisha kichwa kumwelewa.

“Don’t waste time, start with the heart membrane… First assistant, you will also need to suture the pulmonary artery simultaneously…”

Ndani ya chumba cha upasuaji Hamza aliweza kufanya kila kitu katika mpangilio sawia kabisa na kufanya madaktari waliokuwa na wasiwasi juu ya uwezo wake kupumua kwa ahueni lakini kwa wakati mmoja wakimwangalia kama kiumbe kisichokuwa cha kawaida , ilikuwa mara yao ya kwanza kuona daktari wa kariba ya Hamza , namna yake ya kufanya upasuaji hakuwa na wasiwasi kabisa.

Upande wa wanaongalia mlango wa kuingia ulifunguliwa na mwanaume wa makamo mzungu akiwa ametangulizana na mabodigadi kadhaa na kijana mmoja ambae anaonakana kufanana nae sana.

Afande Daudi mara baada ya kumuona huyo mtu palepale hali yake ilibadilika na alionyesha ishara za kutofurahishwa na ujio wake.

“Vipi hali ya dada yangu?”aliongea yule bwana.

“Mjomba!!”Aliita Yonesi.

“Bridge kuna haja ya kuja na mabodigadi wote hao ndani ya hospitali?”aliuliza Afande Daudi.

Dokta Bridge na mama yake Yonesi walikuwa ndugu , wakati baba yake Ivan anafika Tanzania na kuanzisha makazi aliamua kumwasili Maria(Mama yake Yonesi) na kumfanya kuwa mtoto wake wa kwanza na baadae ndio akaja kuzaliwa Ivan ambaye ndio huyo sasa na tokea hapo licha ya kwamba Ivan na Maria hawakuwa na undugu wa damu lakini walikuwa wakipendana sana kama ndugu.

Ivan Bridge ndio yule aliekuwa na mtoto wake mgonjwa Morogoro , ambae Hamza alimfanyia upasuaji kama njia ya kulipa fidia ili kuachiliwa kwa baba yake Eliza.

Ni ngumu sana kuamini mama yake Yonesi alikuwa na udungu wa karibu sana na Dokta Bridge , ukweli ni kwamba kwa Bridge, Maria ndio ndugu yake wa pekee nchini.

Miaka kadhaa nyuma wakati Afande Daudi anakutana na mke wake , hakumjua kwa undani kama alikuwa na uhusiano na familia ya Dokta Bridge na ni mpaka baadae alipokuwa amekufa na kuoza kwa mwanamke huyo na kujikuta hakuwa na jinsi.

Moja ya sababu Afande Daudi kutokumpenda Dokta Bridge ni kutokana na biashara zake haramu alizokuwa akifanya , pamoja na kuwa mwanachama wa umoja wa Black Trinity, siku zote Dokta Bridge alikuwa akitumia koneksheni na familia hio ili kufanya biashara bila kuingiliwa na jambo hilo lilimuuzi sana kwa kuona linamtia doa.

Sasa Ivan kama sehemu ya ndugu upande wa Maria walifika Dodoma kwa ajili ya kusherehekea kutimiza kwa miaka tisini ya Mzee Chalula Mazengo na wakati wa kufika ndio walipokea taarifa ya kupoteza fahamu kwa dada yake ndio maana aliharakisha kufika hapo.

“Nimekuja hapa kuona kama tatizo la dada yangu wewe ndio umelisababisha , kama ni kweli mimi Ivan siwezi kuacha lipite kirahisi”aliongea mzungu huyo kwa kiswahili , licha ya kwamba lafudhi yake kidogo ilikuwa na uzungu lakini alikuwa hana utofauti na mbongo kwenye kuongea kiswahili.

“Mjomba baba hajafanya kitu , mama ana uvimbe ndio maana” aliongea Yonesi akimtetea baba yake.

“Haina haja ya kumwelezea kama ashachukua lake la kufikiria” aliongea Afande Daudi na Dokta Bridge wala hakuonyesha kujali na alikaza macho yake kwenye skrini iliokuwa ikionyesha maendeleo ya upasuaji.

“Vipi hali ya dada yangu?”

“Si unaona hapo , operesheni ishakaribia mwisho”aliongea na kumfanya bwana yule kuangalia madaktari waliokuwa bize kufanya upasuaji lakini muda uleule uso wake ulijikunja.

Alihisi kwamba ijapokuwa madokta hao walikuwa wamevalia barakoa , lakini aliekuwa akiongoza upasuaji huo ni kama alikuwa akimfahamu.

“Ni Hamza!!”Aliongea kwa kusahngaa na kumfanya Afande Daudi kumwangalia.

‘Unamjua?”

“Sio kumjua , Christiani aliweza kupona kwasababu ya kufanyiwa upasuaji na Hamza la sivyo ningempoteza mrithi wangu. Wakati Christiani akiwa hoi ilinibidi kualika daktari Bingwa kutoka Italia , lakini hakuwa na maana kabisa na bahati nzuri niliweza kukutana na Hamza”Aliongea na palepale alimgeukia kijana shombeshombe aliekuwa ameambatana nae.

“Christiani unapaswa kumpa shukrani zako Dokta Hamza ,ndie aliekufanyia upasuaji na ukapona”Alimwongelesha mtoto wake kwa lugha ya kingereza.

“Yes Father”.

Kila mmoja wa ndugu alieweza kusikia mazungumzo hayo alijikuta akishangazwa.

“Vipi Daudi wewe ndio uliemwalika Hamza kuja kumfanyia Dada yangu upasuaji ? Kwa mara ya kwanza umenifurahisha kuonyesha ni kwa jinsi gani unamjali dada yangu Maria kwa kualika Daktari Bingwa kama Hamza”Aliongea akionyesha hali ya kuridhika.

Afande Daudi alionyesha hali ya kushikwa na haya usoni akikumbuka namna ambavyo alimdharau Hamza alivyojitambulisha kama daktari na hata kuwa daktari anaefanya upasuaji huo ni kutokana na kulazimisha na sio kwamba wamemwalika kama ambavyo Ivan akitafsiri hali hio.

























SEHEMU YA 152.

Ivani alishangazwa na sura za ndugu hao na alimgeukia Yonesi na kumuuliza kinachoendelea.

Katika familia hio ya Mzee Mazengo , mtu pekee ambae Ivani alikuwa na ukaribu nae ni Yonesi na hata wakati Yonesi anatoroka kutoka kwao kwenda Dar es Salaam ni Ivan aliempa msaada wa kifedha baada ya kuwasiliana kwa siri na dada yake.

Yonesi pia hakumficha ‘Mzungu huyo wa mchongo’ , alimwelezea kila kitu mwanzo mwisho na palepale alikunja sura.

“Daudii inamaana ulimkataza Dokta Bingwa mwenye utaalamu wa hali ya juu kumfanyia dada yangu upasuaji na yeye ndio alielazimisha?”Aliuliza akiwa amekasirika lakini Afande Daudi hakuongea neno zaidi ya kubakia kimya.

Isitoshe kila kitu kilikuwa wazi sasa , Hamza ndio aliefanikisha kumuokoa mke wake.

Baada ya upasuaji kuisha , Hamza aliweza kutoka akiwa na utulivu nyuma yake akiwemo Dokta Milanzi ambae muda huo hakuwa yule mwenye ujuaji , alikuwa na hali ya heshima sana kwa Hamza.

Hamza mara baada ya kutoka nje alishangaa sana kumuona Dokta Bridge mwanaume ambae alimshikilia mateka baba yake Eliza.

“Wewe na Mtoto wako mnafanya nini hapa?”Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu.

“Christiani hebu acha kusahngaa njoo na mshukuru Hamza kwa kuyaokoa maisha yako”aliongea Bridge na Christiani haraka haraka alimsogelea Hamza na kutaka kumpigia magoti lakini Hamza almzuia.

“Kijana naona umekwisha kupona sasa , mimi ni daktari na sihitaji wagonjwa niliowatibu kunipigia magoti, fanya mpango hata wa bahasha tu napokea”Aliongea Hamza huku akicheka.

“Bila shaka Dokta , niachie namba yako ya simu au unapoishi nitafikisha mzigo”Aliongea na Hamza alijifanyisha hajasikia na kumsogelea Yonesi.

“Upasuaji umeenda vizuri kabisa , akiamka ndani ya masaa ishirini na nne bila shida yoyote basi shida yake itakuwa imeisha kabisa”Aliongea Hamza na Yonesi alishindwa kujizuia na palepale alimkumbatia Hamza akimpotezea hata baba yake aliekuwa akimwangalia kwa macho ya tahadhari.

“Hivi kumbe una undugu na Ivan Bridge?”Aliuliza Hamza .

“Mimi na Maria tunaweza tusiwe ndugu wa damu lakini ndio dada yangu wa kipekee , lazima nitimize wosia wa Baba kuhakikisha namlinda”aliongea Dokta Ivan na kauli hio ilimfanya Hamza kupata mbili tatu bila hata ya kuelezwa vizuri.

“Kama tungejua siku ile , kusingekuwa na sababu ya kulazimishana ilihali sisi ni ndugu tayari”Aliongea Hamza akicheka.

“Haha , upo sahihi , unaonaje tukipata kinywaji usiku wa leo, kwa utaalamu wako naamini Dada yangu amekwisha kupona lakini pia Yonesi asante kwa kunipatia ndugu mpya”aliongea na kumfanya Hamxa kucheka huku Yonesi akishikwa na aibu zaq kike.

Ijapokuwa Hamza alijua Mzee Ivani alikuwa akimchangamkia kwa ajili ya kujenga ukaribu lakini wala hakujali kutokana na kufahamu alikuwa mjomba wake Yonesi.

Kitendo cha Hamza kuwa bize na Mzee Ivani ilimfanya Afande Daudi kujihisi ni kama ametengwa.

Baada ya kutoka hospitalini Hamza alirudi nyumbani kwa Mzee Mazengo , hakuna mwanafamilia hata mmoja ambae alithubutu kumfukuza Hamza.

Ki ufupi ni kwamba alianza kupewa heshima yake kama mgeni muhimu kwa familia hio na Mzee Sauli ndio aliechukuwa suala zima la kumkirimia kwa kumuonyesha sehemu ya kulala pamoja na kuandaliwa chakula.

Habari za Hamza kutumia uwezo wa hali ya juu katika matibabu na kumuokoa mke wa Jenerali zilisambwazwa na watu wa Dokta Bridge kwa ndugu wote , hata Mzee Mazengo mara baada ya kusikia habari hizo alifurahi pia.

Usiku Hamza alijumuika na Yonesi pamoja na Mzee Ivani na mwanae na kuanza kunywa pombe na nyama choma ya mbuzi.

Mpaka inafika usiku wa saa tano Mzee Ivani alikuwa amelewa chakali kiasi cha kuanza kuleta usumbufu lakini Hamza licha ya kushusha chupa nyingi hakuwa amelewa na kufanya watu wamshangae pia.

Baada ya Mzee Ivani kuchukuliwa kwenda kulala, Yonesi alimchukua Hamza na kumpeleka upande wa makazi ya wageni.

Yonesi alikuwa amevalia koti la kujikinga na baridi , ijapokuwa hakukuwa na baridi sana lakini upepo ulikuwa ukivuma mno , kutokana na mwezi Hamza alijikuta akimwangalia mrembo huyo kimahaba kiasi cha kumfanya Yonesi kushikwa na haya za kike.

“Hebu acha kuniangalia hivyo, unashangaa kitu gani wakati mimi ni yuleyule?”

“Yonesi unajua umebadilika , yaani unavyoonekana nyumbani kwenu ni tofauti na nilivyokuzoea , unaonekana kama msichana wa kawaida na mrembo”

“Hebu nitokee huko , umemuoa mwanamke mrembo kama Regina , nina uzuri gani mie?”aliongea Yonesi lakini ukweli alikuwa na furaha ndani kwa ndani.

“Huna haja ya kuanza kujilinganisha nae , urembo wako wewe ni wa tofauti”

“Hebu anza kwanza kutafuta namna ya kumbembeleza hata kwa kumpigia simu , mimi naondoka”Aliongea Yonesi mara baada ya kufika mlangoni, lakini Hamza alimzuia kwa kumshika mkono.

Ulikuwa ni usiku wa baridi ambao ni hatari sana kwa mazingira kama hayo mwanaume na mwanamke kushikana , Hamza alijiambia kama asipochukua hatua ya kumuweka chini huyu mrembo ataipata hio nafasi lini.

“Wewe .. nini tena?

Yonesi mapigo ya moyo yalikuwa yakienda mbio mno , ukweli ni kwamba tokea anaanza safari ya kumsindikiza Hamza kuja chumbani kwake alikuwa na wasiwasi kitu kinaweza kutokea baina yao lakini hakudhania Hamza atakuwa na shambulizi la moja kwa moja namna hio

Hamza hakutoa jibu , vitendo pekee vilitosha , kwani palepale alimvuta Yonesi na kisha alimwegamiza kwenye ukingo wa fensi ya chuma na kuanza kumpiga denda.

Mwanzoni Yonesi alikuwa amekakamaa , lakini kadri ambavyo Hamza alikuwa akitalii kwenye mwili wake , ghafla tu alianza kulainika.

Alijihisi kupata fursa ya kuruhusu hisia zake kumwendesha , kwa hali aliokuwa nayo aliamini kama Hamza atataka kufanya nae chochote asingeweza kukataa.

“Tusifanyie hapa.. twende ndani”Aliongea Yonesi kwa sauti ya chini.

“Hapa hapa nje ni pazuri mno , kwanza hakuna anaekuja upande huu”Aliongea Hamza kwa suati ye kitetemeshi kwa namna ya kumnong’oneza.

“Ah.. hapana bwana ..nina aibu”Aliongea Yonesi huku akianza kuishiwa na pumzi.

“Haha.. babe Yonesi kumbe una aibu eh , mimi nilijua wewe ni jasiri”

“Sijawa…”Yonesi hakujua namna ya kumwambia Hamza hajawahi kufanya mapenzi kwani muda huo Hamza alikuwa ashaanza kushusha chini nguo zake.

Hamza mara baada ya kuona hali ya wasiwasi , hakutaka kuendelea hapo hapo , hivyo alimbeba juu juu na kutaka kuelekea ndani , lakini ghafla tu walianza kusikia vishindo vya miguu ya mtu kusogea upande huo na Yonesi haraka sana alishuka na kusogea mbali na kugeuza uso wake kuelekea upande wa korido.

Hamza alijikuta aking’ata meno kwa hasira na kujiambia hawa watu wanafanya nini huku usiku wote huu.

Alikuwa ni Afande Daudi aliekuwa ameongozana na kundi la watu na mara baada ya kumuona binti yake akiwa katika hali ya aibu uso wake ulizidi kuwa mweusi na alimwangalia Hamza kwa macho ya ukali.

“Kwasababu yako familia yangu imeingia katika matatizo makubwa,. Hivi hata unajua kinachoendelea?”

“Matatizo gani , kuna kilichomtokokea mgonjwa?”aliuliza Hamza kwa ishara kidogo ya wasiwasi.

Yonesi pia alijikuta akishikwa na wasiwasi ,. Isitoshe wakati wanarudi bado mama yake hakuwa amerejewa na fahamu

“Nini kimemtokea mama?”Aliuliza.

“Sio mama yako , ni kaka zako , wamekamatwa usiku huu na wapo chini ya uchunguzi wa jeshi”Aliongea

“Kwanini wamekamatwa , si tulikuwa nao mchana?”aliuliza Yonesi kwa mshangao.

Kaka zake Yonesi walikuwa washarudi mchana na waliweza kukutana , lakini hata hivyo hawakuongea sana kutokana na kwamba hakukuwa na mazoea makubwa kati ya yao .

“Ni watu wa Kamati ya nidhamu ndio waliotoa maagizo kukamatwa kwao , wakisema kwamba wanajihusisha na mfanyabiashara Zack Monyo aliekamatwa miezi miwili iliopita , sijajua mpaka sasa wametoa wapi ushahidi mpaka kuwahusisha lakini ni kweli kaka zako walikutana na mfanyabiashara Zack wakati wa chakula cha usiku , kuonekana kwao pamoja ndio maana wamekamatwa kwa ajili ya uchunguzi”Aliongea.

“Itakuwa ni familia ya Mzee Mirambo washaanza yao”Aliongea Hamza.

“Kama sio Mirambo , unadhani ni nani wengine wanaweza kutuchokoza, kesho ni siku ya sherehe ya baba lakini wajukuu zake wawili wamekamatwa , wanafanya haya yote kwa ajili ya kuvuruga hii sherehe na kuibua maneno kwa tuliowaalika”aliongea na kisha alimkazia Hamza macho.

“Haya yote yanatokea kwasababu yako , umewachokoza na sasa wanalipiza kwa kuchokonoa familia yangu”

“Baba hatupaswi kumlaumu Hamza kwa hili, hii sio mara ya kwanza kutumia koneksheni zao serikalini na kujaribu kuonea watu, kingine kama Kaka zangu hawana hatia sidhani kuna haja ya kuhofia maana hawawezi kuwafanya chochote”

“Embu kaa kimya , kwanza usiku wote huu unafanya nini hapa na mume wa mtu halafu huna aibu na kuanza kumtetea”Aliongea na kisha baada ya kuona Yonesi kanywea alimwangalia Hamza kwa macho makali.

“Ikifikia kesho mchana hujatafutia ufumbuzi wa hili swala , nakuhakikishia nitakuvunja vunja”

“Babaa!!”Aliingilia Yonesi lakini Hamza alimzuia.

“Kwahio mzee unasema nikifanikisha kulitatua hili , hutoendelea kupinga uhusiano wangu na Yonesi?”

“Tutaona kwanza , wewe si ndio umesema huogopi familia ya Chifu Mirambo , nataka kuona meneno yako katika vitendo na sio maneno ya bure tu”Aliongea.

“Kama ni hivyo basi usiwe na wasiwasi , nakuahidi mpaka saa nne asubuhi hili swala litakuwa limeisha”Aliongea Hamza kwa kujiamini na kumfanya Mzee Daudi kumwangalia kwa macho ya kutokumwamini tena.

“Unapanga kufanya nini?”

“Sijafikiria bado , lakini naamini sitokosa njia”

“Wanangu wasipoachiwa kesho asubuhi , sitaki kuendelea kukuona nyumbani kwangu , hata kama umemponya mke wangu haina maana”Mara baada ya kuongea palepale aliwapa ishara watu wake na kuondoka na ilionyesha alikuwa na mpango mwingine kichwani na alitaka kwanza Hamza awajibike.

“Hamza una njia ya kutatua hili swala?”Aliuliza Yonesi.

Hamza alijiambia moyoni alikuwa na njia nyingi mno , ijapokuwa ni kweli familia ya Mdudu ilisifika kwa kuwa na koneksheni nyingi nchini lakini akiamua kuiogopesha uwezo huo anao , ni swala la kupiga simu moja tu na vijana wake wangeingia nchini na kuanza kuchimba uchafu wao wote.

Lakini hata hivyo Hamza aliona haina haja ya kuleta vijana wake nchini kwa ajili ya familia ndogo kama ya Mdudu kwani ingeweza kuleta wasiwasi kwa watu wengi na kujaribu kumfuatilia kutaka kumjua ni nani.

“Nitampigia simu Himidu na kuona kama tunalitatua vipi”Aliongea Hamza baada ya kuwaza kwa dakika kadhaa.

“Himi.. unamaanisha Mshauri mkuu?”

“Ndio , yule hakosagi namna”

“Lakini hata kama mshauri mkuu akiingilia sidhani kama ataweza kufanya chochote la sivyo itatengeneza mgongano mkubwa. Unapaswa kuelewa licha ya Mzee Mirambo kustaafu lakini bado ana nguvu na pia anaheshimika ndani ya umoja wa machifu”aliongea Yonesi kwa wasiwasi

Hamza aliishia kutabasamu na kisha palepale alitoa simu yake na kuitafuta namba ya Himidu,.

******

Upande mwingine Mkoani Morogoro katika moja ya ofisi za kambi ya jeshi , walionekana walinzi waliokuwa na sura zilizojaa usiriasi wakiwa wamesimama nje ya jengo la kisasa la ghorofa mbili kwenda juu wakiimalisha ulinzi.

Ndani kabisa ya jengo hilo kulikuwa na ukumbi mkubwa uliokuwa na meza ndefu ambayo juu yake ilikuwa na ramani kubwa pamoja na michoro kadhaa , kulikuwa na wanaume na wanawake wote wakiwa katika mavazi ya kawaida waliokuwa wameizunguka meza wakiwa wameshikilia vikombe vya kahawa lakini kwa wakati mmoja walionekana kujadiliana huku macho yao yote yakiangalia ramani na michoro iliokuwa ikionekana mbele yao.

“Tumefanikiwa kuipata Manowari ya kikosi cha Delta Zero ilipozamia, itatuchukua zaidi ya siku kama nne kuweza kuitoa nje ya maji , lakini jeshi la America wapo makini sana kuangalia kila tunachofanya , sidhani kama inaweza kuwa rahisi”Aliongea mwanaume alievalia miwani.

“Profesa Yoze sidhani kama kuna haja ya kuitoa majini , teknolojia ya manowari yao na ambayo Yulia anaendelea kujenga hazijapishana sana”Aliongea mwanaume mwingine wa umri wa makamo.

“Haha.. Mkurugenzi unadhani nalenga kupata teknolojia ya Manowari yao , ninachotaka ni kujua siri ya teknolojia yao ya ile Suti ya kivita, wanajeshi wengi wameona namna ilivyokuwa na uwezo “Aliongea.

“Sasa kama mpango wako ni kupata teknolojia ya hio suti si utume wanajeshi wa maji wafanye Drill na kuitoa hio suti nje?” Aliongea Afande Elikana Msofena kisha alimwangalia Afande Himidu.

“Au mshauri mkuu unasemaje?”

“Iwe ni Manowari au suti yao ya kivita , hakuna haja ya kutafuta chochote, kinachotakiwa ni kutengeneza maigizo tu ili kupata Attention yao”Aliongea Afande Himidu.

“Kwanini?”Aliuliza Profesa Yoze.

“Sehemu ilipozama hapajaonekana mionzi ya nyuklia , maana yake Reactor yao ilikuwa na ulinzi wa kujilinda na mlipuko wowote wa kinyuklia , kuhusu Suti zao za kivita ni moja tu ilionekana, jambo ambalo linatuambia bado wanahangaika katika kutengeneza nyingi , hivyo sidhani kama ni swala la kuogopa. Mkumbuke tuna Earth Axis ambayo tunaendelea kuifanyia utafiti , naamini tutaweza kupata teknolojia kubwa ambayo itakuwa ni zaidi ya suti yao . Tutakachokifanya kwasasa ni kutuma wanajeshi wetu kwenda kuzunguka zunguka katika lile eneo ili kuwafanya waone kama kuna kitu tunachokitafuta au tunafuatilia teknolojia yao , hii itawafanya waamini bado hatujapiga hatua katika teknolojia na kuamini wao wako juu,m hivyo watatupunguza presha ya kutufuatiulia na sisi tutapata utulivu kuendeleza misheni zetu za kigunduzi”Aliongea na watu wote walitingisha vichwa kukubali wazo lake.

“Kweli wewe ni Mshauri mkuu”Aliongea Mkurugenzi wa kitengo cha TIMISA , Afande Elikana Msofe.

Muda ule Afande Himidu aligeuza macho yake na kumwangalia mwanaume mwenye umri mkubwa aliekuwa amekaa upande wa kulia kwake mwisho wa meza kama kiongozi.

Mwanaume huyo alikuwa na macho yaliojaa nyusi nyingi na mwonekano wake ulimfanya kuwa tofauti na kila mmoja aliekuwa hapo ndani na kumtengenezea hadhi ya juu.

Alikuwa amevalia koti refu la ngozi , rangi nyeusi na kwa kumwangalia tu utajua sio mtu wa kawaida.

“Afande upo kimya sana leo sio kawaida yako”Aliongea Mshauri mkuu kwa shauku.

Mwanaume huyo ndie aliekuwa Mkuu wa Majeshi mwenye mamlaka ya kuongoza jeshi lote pamoja na vitengo vyake vyote vya intellijensia , ikiwemo Malibu na TIMISA.

Licha ya kuonekana kama mzee , lakini ukweli ni kwamba cheo chake hakukipata kirahisi rahisi, alistahili kuwa katika cheo hicho.

Mara baada ya kuulizwa lile swali , aliinua mkono wake na kisha aliweka kidole juu ya ramani ya Tanzania na kufanya watu wote kuangalia eneo alilogusa.

“Mmesikia kuhusu tukio lililotokea hapa?”Aliuliza kwa sauti nzito.
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU.

MTUNZI : SINGANOJR.





SEHEMU YA 153.​

Simba wa nyika.​

“……sifa zangu ni matokeo ya kuutafuta uhuru na kuendelea kuishi kwa kushinda vikwazo”



Mara baada ya mkurugenzi wa kitengo cha TIMISA kunona sehemu alioweka kidole mkuu wa majeshi. palepale alijua alikuwa akilenga nini .

“Afande unamaanisha kilichotokea Kilwa baada ya Wabrazili kufungua kanisa lao ndani ya hili eneo?”Aliuliza kwa kutokuwa na uhakika na mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa kukubaliana nae.

“Lakini mkuu mpaka sasa bado najiuliza , kulikuwa na haja ya wanajeshi wetu kuingilia hili swala na kuwazuia hawa wabrazili kutofungua kanisa lao , hapa Dar es salaam wamekuwepo kwa muda mrefu lakini hakukuw ana tatizo lolote na hata kama ni swala la kijamii viongozi wa serikali ndio walipaswa kuingilia na sio wanajeshi”

“Shida sio kutokuwa na tatizo lolote , nadhani mnajua ni kipi kinaendelea ndani ya hili kanisa , ni kanisa gani ambalo linapokea kila imani?”Aliongea Afande mwingine.

“Kwa ninachojua kuhusu hili kanisa sio swala tu la imani ila ni lengo moja ndio linalowaunganisha , ni kweli kuna watu wana imani tofauti lakini wana muda tofauti wa kuhudhuria ibada na siku moja ya kujumuika pamoja”aliongea mwingine.

“Lakini nyie hamna shauku , kama kweli lengo lao ni kutoa mahubiri ya imani yao kuna haja ya kwenda kuweka kanisa Kilwa , yapo maeneo mengi ambayo wangeweka makanisa lakini wakachagua eneo ambalo lina ukinzani mkubwa”

“Labda ni kwasababu lina ukinzani ndio maana wamemua kuanza katika eneo hilo”Alikisia mwingine.

“Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu hili swali , kama kweli mpango wao ni kuleta kile wanachoamini ni mafundisho ya kiimani ya kuzaliwa upya baada ya kufa, hata kama kama wameona ndio sehemu sahihi ya kuanzia kujipanua , lakini kwanini wapeleke kundi la watu wote wale tena wageni kutoka nje ya nchi?”

“Jenerali kuna sababu yoyote unaifikiria?”aliuliza mwingine lakini Jenerali alitingisha kichwa kuonyesha hajui.

“Naona ni vizuri tukiweka umakini sana juu ya haya makanisa ya Wabrazili, lazima kuna kitu kinaendelea”Aliongea na muda huo huo simu ya Afande Himidu ilianza kutoa mwito wa kuita.

Afande Himidu mara baada ya kuona anepiga alitoa tabasamu kidogo na kisha alipanga kuipokea palepale.

“Mshauri mkuu ni mara yangu ya kwanza kuona simu yako ikiita katikati ya kikao”Alitania mwanajeshi mmoja.

“Kuna baadhi ya simu unapaswa kupokea muda wowote”Aliongea

“Oh! Au ndio mteule ndio anaepiga simu?”

“Hii ni simu zaidi ya mteule”Aliongea na palepale alipokea simu ile.

“Bosi usiku sana , kuna tatizo?”

Mshangao wa kutotarajia uliwashika kila mmoja aliekuwepo ndani ya hilo eneo baada ya kumsikia mshauri mkuu akiita mtu Bosi. Walijiuliza ni mtu gani huyo ambae anaweza kumfanya Himidu kupokea simu mbele kabisa ya mkuu wa majeshi.

Midomo ya Mkuu wa mejeshi ilicheza kidogo , hakuongea kitu zaidi ya kuinua kikombe chake cha kahawa na kunywa kidogo huku akionekana kuwa na hali ya umakini mkubwa.

“Bosi nimekuelewa nitakupigia asubuhi , ngoja niangalie cha kufanya sasa hivi”

Afande Himidu mara baada ya kumaliza kuongea na simu hio , mwonekano wake ulikuwa na hisia mchanganyiko.Baada ya kukata simu ile aligeuka na kumwangalia Mkuu wa majeshi na tabasamu lililojaa uchokozi.

“Simba Nyika acha kujifanyisha , wengine hapa wanaweza wakawa hawajasikia , lakini masikio yako yamesikia kila kitu alichokuwa akiongea alienipigia upande wa pili”

“Kwahio vipi kama nimesikia? M,ara ya mwisho uliniambia unataka tuongee dili na huyo mtu ambalo litapelekea mafanikio kwa jeshi letu , nadhani huu ni muda sahihi wa kuongea nae au wewe unaonaje?”Aliongea na Himidu alitingisha kichwa kukubaliana nae na kisha palapale aligusa mkoa wa Dodoma na kidole chake.

“Afande Mazengo , kama kijana wako ni busara kuja kukutembelea katika siku yako ya kutimiza miaka tisini”

Mara baada ya kuongea hivyo kila mmoja aliekuwa katika meza alishangazwa na kauli yake.

*****

Saa kumi za alfajiri katika familia ya Chifu Mazengo , karibia watu wote wamekwisha kuamka kasoro wafanyakazi pekee..

Meja jenerali Daudi Chalula alikuwa amekaa na ndugu zake pamoja na marafiki na walikuwa wakinywa kahawa huku wakiongea na kujadiliana namna ya kudili na swala la kifamilia lililotokea jana.

“Kaka sidhani kama ni vizuri kufanya hivi , kwanini tusiongee na Mzee Mirambo, ni kweli tunaweza kupata hasara upande mwingine lakini hatuwezi kuacha hili swala liingilie sherehe ya baba”Aliongea Mtemi, mdogo wake Daudi.

“Unadhani wanataka tuongee nao? Kama wanataka tuongee nao wasingetusababishia matatizo kwanza . Ni kheri kutoenda kwao kusababisha matatizo zaidi”Aliongea Mdogo wake mwingine..

“Siwezi kukaa na kuendelea kusubiri , nitakuja kumfanya kitu mbaya sana Imani na familia yake”Aliongea Daudi huku akisaga meno kwa hasira

“Alfajiri yote hii mbona makelele ya vitisho mengi”Sauti ya kizee ilisikika kutoka nyuma na kuwafanya wageuke.

Watoto hao wa Mzee Mazengo walishagnaa baada ya kuona ni baba yao maana sio kawaida kuamka mapema.

“Baba kwanini umeamka mapema?”Aliongea Daudi na palepale alisimama na kwenda kumsaidia baba yake kutembea lakini Mzee Chalula alimsukuma asimsaidie.

“Mbona unanishika , unadhani siwezi kutembea! Mtu mmoja anatosha”Aliongea na kisha alisaidiwa na mzee Sauli kukaa kwenye kiti .

“Nimesikia kuna tukio limetokea jana?”Aliuliza na muda ule Mzee Daudi aliona haina haja ya kuendelea kumficha baba yake.

“Sikutaka kukusumbua baba , ila jana Danny na Stanley walikamatwa kwenda kufanyiwa mahojiano kwa kosa la kuhujumu jeshi. Lakini sio kweli kuhusu hili lazima ni huyu mkongwe fisadi wa familia ya Mirambo ndio kahusika”Aliongea kwa hasira.

“Hebu kaa kimya!”Alifoka Mzee Chalula.

“Wakati Mzee Mirambo akiwa ni mwanasiasa nguli nchini wewe ulikuwa mtoto , ukiheshimu watu na wao watakuheshimu. Unadhani maneno yako haya yakisikika nini kitatokea”Aliongea na kufanya ndugu wote kukaa kimya na hasira zao kupotea.

“Wanategemea kukamilisha uchunguzi lini na kuwaachia huru?”Aliuliza baada ya kutulia.

“Nadhani ndani ya wiki moja au mbili . Nishawasiliana na baadhi ya watu ndani ya kamati na wamesema uchunguzi bado unaendelea na ni mpaka ukamilike. Baba hofu yangu ni kama wakiongea ujinga na kujikuta wakiingia katika mtego”Aliongea Mzee Daudi kwa wasiwasi.

“Kama kuna makosa wamefanya hawawezi kulaumu wakipatikana na hatia . Familia yetu pia inafuatiliwa sana kwenye kufanya maamuzi ni kawaida watu kuwa na maoni tofauti”

“Ndio baba”Waliitikia wote lakini bado walionekana kuwa wanyonge.

“Baba kawaida una amka saa mbili za asubuhi , mbona umewahi sana leo?”Aliuliza Afande Daudi.

“Leo ni siku ya kipekee sana , kuna mgeni muhimu anatarajia kufika hapa kwa ajili ya kunipongeza kufikisha miaka tisini , ndio maana nimeamka “

“Mgeni wa muhimu ? Baba kuna wageni kutoka Ikulu wanaokuja leo?”Aliuliza Daudi na wenzake wote pia walionekana kuwa na shauku , maana kama ni nje ya Ikulu isingekuwa na haja ya kuwasiliana na Mzee Mazengo mwenyewe .

“Mgeni anaekuja ni mtu ambae ni ngumu kukutana nae kuliko viongozi wa Ikulu”Aliongea lakini ni muda huo huo mfanyakazi alikuja haraka haraka upande wao kutoa taarifa.

“Babu! Mkuu wa Majeshi na Mshauri mkuu wamefika kwa ajili ya kukutembelea na kutoa pongezi zao”

Mara baada ya maneno hayo kusikika , wanafamilia wote waliokuwa katika eneo hilo walijikuta wakishangaa ni kama hawakuwa wakiamini.

Ikumbukwe kwamba Mkuu wa Mejeshi amekuwa ni mtu wa kujitenga sana na mara nyingi aliwakilishwa katika sehemu nyingi , kuja mpaka hapo iliwafanya washangae.

Miaka kadhaa nyuma kazi zote ambazo zilikuwa ni za mkuu wa majeshi , ziliwekwa chini ya Mhauri Mkuu wa jeshi na ilikuwa ni mara chache sana Mkuu wa jeshi kuhusishwa katika kazi za kila siku labda kwa matokeo maalumu tu.

Sasa mkuu huyo kuja mpaka hapo kwa ajili ya kumtembelea Chifu Mazengo ilishangaza wengi waliosikia taarifa hio.

“Haraka , wakaribisheni ndani”Aliongea Mzee Chalula akiwa na utulivu.

Mara baada ya kutoa kauli hio , dakika chache mbele wanaume wawili waliingia katika eneo hilo mmoja akiwa amevaa kombati za kijeshi za cheo cha ukuu kabisa na mwingine akiwa amevaa kombati za kijeshi cheo cha Jenerali.

Kitendo cha Meja Jenerali Daudi kukutanisha macho na Mkuu wa Majeshi walijikuta wakianza kutetemeka kutokana na hali ya kutokuwa wa kawaida ya mkuu huyo , alikuwa akisababisha msisimko ambao ulifanya nywele zao kusimama kama vile mbele yao alikuwa amesimama Jini.

“Jenerali Mstaafu Chalula kheri ya siku yako ya kuzaliwa na pongezi kwa kutimiza miaka tisini ni hatua ndefu”Aliongea akiwa na tabasamu , lakini hata hivyo haikutosha kufanya wanajeshi waliokuwa katika eneo hilo kuwa katika hali ya utulivu.

“Mzee wangu mimi pia nakutakia kheri ya kuzaliwa na pongezi ya kutimiza miaka tisini Jenerali Mstaafu na pia tunaomba radhi kwa kuja asubuhi asubuhi”Aliongea Afande Himidu huku akipiga saluti na kumfanya Afande Mazengo kucheka.

“Karibuni sana , wala hakuna haja ya kuomba radhi na uzee wangu huu Mkuu wa majeshi na Mshauri mkuu kuja kunitembelea ni heshima, Karibuni mketi”

“Mtu aletee chai wageni wetu”Aliongea

Baada ya Mkuu wa majeshi na Mshauri mkuu kukaa waliinua sura zao na kuwaangalia wanajeshi waliokuwa wamesimama kikakamavu.

“At Easy Ma’afande , tupo hapa kwa ajili ya kumpongeza Mzee wetu”Aliongea na palepale wanajeshi wale walilegeza.

Kulingana na sheria za jeshi kwasababu hawakuwa katika kombati za kijeshi hawakupaswa kupiga saluti badala yake walibana t*ko.

Baada ya chai na kahawa kuandaliwa pamoja na maongezi kidogo ya hapa na pale , familia ya Mzee Mazengo walijikuta wakiangaliana wakifikiria namna ya kumuomba mkuu wa mejshi msaada juu ya ndugu waliokamatwa , hakuna aliekuwa na ujasiri.

Kwa cheo chake kauli yake moja tu ingetosha kuwafanya kuachiliwa huru moja kwa moja.Isitoshe hata kwa namna gani koneksheni ya kisiasa waliokuwa nayo familia ya Mirambo lakini mkuu wa majeshi ni m kuu wa majeshi.

Lakini kutokana na wengi wao hapo wamekutana na mkuu huyo mara chache sana , iliwafanya kugubikwa na hofu kubwa.

Dakika hio hio wakati wakiangaliana kwa ishara ya kutaka mmoja wapo aanze , mhudumu alifika tena na kutoa taarifa ya kurudi kwa Danny na Stanley.

Mara baada ya kusikia taarifa hio familia nzima walishikwa na mshangao isipokuwa tu kwa Mzee Mazengo.

Dakika hio hio vijana wawili waliokuwa katika mavazi ya kiejshi waliingia katika ukumbi kwa ari kubwa na walipiga saluti baada ya kufika kama ishara ya salamu kwa wakubwa zao na kisha walipewa ishara ya kulegeza.

“Babu , Baba samahani kwa kuwafanya kuwa na wasiwasi”Waliongea

“Danny mko sawa , vipi kuhusu kesi yenu?”

“Ndio baba tupo sawa , kuhusu kesi yetu hatujaambiwa chochote na tumeruhusiwa tu kurudi nyumbani na watu wa kamati wametuomba radhi wakisema kuna mkanganyiko wa kitaarifa uliotokea na hatukuwa na kosa”

Mara baada ya kusikia kauli hio wanafamilia hao walishangaa zaidi , bado hawakuelewa nini kinaendelea. Ni Mzee Chalula Mazengo pekee alieonekana kujua kinachoendelea na palepale aliinua kikombe cha chai na kuwapa ishara Mkuu wa Majeshi na Mshauri mkuu .

“Asanteni kwa zawadi ya siku yangu ya kuzaliwa Simba”

“Mstaafu , tumekuja haraka haraka na tumejikuta hakuna tulichoandaa , tumeona tutoe tu msaada kidogo ili mradi hotujali”

“Hii zawadi ni kubwa zaidi ya dhahabu na fedha”Aliongea Mzee huyo akiwa na mwonekano uliojaa usiriasi.

Mzee Daudi na nduguze walisimama palepale na kutoa shukrani kwa mkuu wa majeshi na Mshauri Mkuu, hata kama watoto hao hawakuwa na kosa lakini kitendo cha Mkuu wa majeshi kuingilia kilikuwa na maana kubwa sana kwao.

“Haina haja ya kunishukuru mimi moja kwa moja , nimekuja hapa kwa ajili ya kutoa pongezi zangu lakini vilevile kwasababu mmoja wa mwanafamilia wenu amenipa kazi ya kulimaliza hili swala mapema , Kama hili linahesabika kama zawadi basi na mwanafamilia alieniagiza anapaswa kujumuishwa”

“Kumbe bado tuna watu ndani ya familia yetu wenye uwezo wa kumuomba mkuu wa majeshi kusaidia kutatua shida kama hii?”Aliongea Mzee Mazengo kwa mshangao.

“Mstaafu inaonekana bado hujajua , namzungumzia mwanaume ambae mjukuu wako amemleta kwenu, ni bwana mdogo ambae sio mwepesi”

Mara baada ya maneno hayo palepale Afande Daudi alijua nani anazungumziwa .

“Hamza!!”

Wanafamilia wengine walishangazwa na jambo hilo , ijapokuwa walijua Hamza uwezo wake sio wakawaida lakini hakuna aliedhania anaweza kumpa kazi mkuu wa Majeshi na kuitekeleza.

“Nilisikia Hamza na Mshauri mkuu wana ukaribu mkubwa , sikutarajia hata wewe Mkuu wa Majeshi? Najikuta kuwa na shauku kubwa juu yake , unaonaje ukinielezea kidogo kuhusu huyu Hamza ni nani haswa?”Aliongea Mzee huyo na wanafamilia wote walimwangalia mkuu wa majeshi kwa shauku kubwa lakini na wasiwasi kwa wakati mmoja , hususani Mzee Daudi ambae alimfokea sana Hamza tokea kufika kwake.

“Mzee wangu sio sehemu salama kutoa taarifa kuhusu Hamza , leo Simba amefika hapa kwasababu anahitaji kuongea nae , tutaomba sehemu iliojitenga kwa ajili ya maongezi”Aliongea Afande Himidu.

Familia nzima walijikuta wakiwa katika mshangao , ilikuwa ngumu sana hata kwa wao wenyewe wanajeshi kukaa meza meja na kuongea na Mkuu wa Majeshi.

Lakini kijana mdogo sana kama Hamza ambae si tu kumuomba mkuu wa majeshi kusaidia kuwachiliwa kwa Danny na Stanley lakini vilevile amemwita Mkuu wa Majeshi kwa ajili ya kuongea nae.

“Afande Himidu mbona mna haraka sana wakati mnasafiri na ndege binafsi?”

Sauti iliweza kusikika , alikuwa ni Hamza aliekuwa akija upande wao kwa hatua ndefu kusogea alipo Afande Himidu na Mkuu wa Majeshi.

Mkuu wa Majeshi palepale aligeuka na kumwangalia Hamza na macho yaliojaa ukali na mkandamizo mkubwa wa nishati za mbingu na ardhi ulimtoka na kuwasababishia Afande Daudi na wenzake kukakamaa miili yao kwa hofu.

Hamza upande wake hakuwa na hali ya wasiwasi kabisa na alikaziana macho na Mkuu wa majeshi huku akitoa tabasamu la uchokozi , hakuonekana kuathirika na mkandamizo wa nishati za mbingu na ardhi ambao mkuu huyo alikuwa akimjaribu nazo.

Wanajeshi waliokuwa hapo walimwangalia Hamza na walishangaa kuona hakuonyesha ishara yoyote ya hofu wala kuathiriwa na mkandamizo ule na walijikuta wakianza kumhofia.

Katika macho yao Hamza alikuwa amezidi kuwa hatari . Hakuonekana tena kama kijana mdogo katika umri wa miaka ishirini na kuendelea , alikuwa ni kama jitu kwao.

Mzee Mazengo macho yake yaliishia kuchanua , aliishia kutingisha kichwa chake kwa ishara ya kumkubali Hamza .

“Hamza shukrani kwako nimefikisha miaka tisini kwa furaha kubwa”

“Huna haja ya kunishukuru Babu , wajukuu zako hawakuwa na kosa ndio maana wameachiliwa huru”

“Haha .. upo sahihi, hakuna mwanafamilia wangu anaeweza kulihujumu jeshi , ikitokea akiwepo nitaanza kumwadabisha mimi mwenyewe kabla ya sheria za nchi”Aliongea kwa ridhiko kubwa.

Upande wa Afande Daudi alikuwa katika hali ya sintofahamu . Mwanzoni alimpiga mkwala Hamza ili kupima uwezo wake lakini hakuamini Hamza angeweza kuwatoa watoto wake kwa simu moja tu na zaidi sana kuwaleta watu wazito katika familia yao.

Kutokana na hilo alijikuta akikosa namna ya kuweza kupinga tena mahusiano ya Yonesi na Hamza.

Mkuu wa Majeshi alimwangalia Hamza kwa dakika kadhaa , akionekana kama mtu ambae anawaza jambo lakini hakuongea chochote.

Hamza mara baada ya kuona macho ya mkuu huyo yalivyo kuna hali iliokuwa ikimsemesha kwa kumwambia kuna kitu hakipo sawa lakini hakuweza kujua ni kitu gani hicho. Ilikuwa ni kama mkuu huyo kuna mtu anajaribu kumfananisha nae.

“Afande Mkuu , kuna kitu kipo kwenye sura yangu , kwanini unanikodolea macho namna hio?”

Mara baada ya kusikia Hamza akiongea kwa staili hio wanajeshi wote waliokuwa hapo walijikuta wakihisi hewa imegeuka barafu, ulikuwa ni ujasiri mkubwa Hamza kuongea na mkuu wa majeshi kama mshikaji wake.

Lakini hata hivyo mkuu wa Majeshi hakuonyesha kukasirika na kauli ya Hamza na palepale alisimama na kunyoosha mkono kusalimiana na Hamza.

“Nimesikia jina lako muda mrefu sana , kinachonishangaza ni namna unavyonekana kuwa mdogo nje ya mategemeo yangu”

Mara baada ya kuongea hivyo wanafamilia walijikuta katika hali ya mshangao huku wakijiuliza inakuwaje Mkuu wa majeshi anasema amelisikia jina la Hamza muda mrefu ,anazungumzia muda mrefu upi?.

Tatizo kubwa lililoleta zaidi sintofahamu ni kwamba familia hio hakuna ambae ashawahi kusikia jina la Hamza mpaka Yonesi alivyomleta.

Kila mtu alimwangalia Hamza na usiriasi katika macho yake , muda huo Hamza akisalimiana na Mkuu wa majeshi kwa salamu ya mkono.

“Simba Nyika ni jina lako maarufu la utani ambalo nimelisikia kutoka kwa wanajeshi wengi , lakini hata mimi sijategemea kukuona ukiwa na mwonekano mdogo kama hivi”Aliongea Hamza.

“Simba Nyika uliemsikia wakati ukiwa mdogo sio mimi , nimerithi cheo cha Simba wa Nyika miaka kumi iliopita”Aliongea na Hamza alionekana kushanga kwasababu ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kusikia jambo hilo.

Unachopaswa kuelewa ni kwamba ukiachana na cheo cha ukuu wa jeshi , kama cheo cha juu zaidi , kulikuwa na cheo kingine cha heshima ambacho ni zaidi ya ukuu wa jeshi na cheo hiki ni Simba Nyika, haijawahi kuwa wazi ni vigezo gani vinazingatiwa mpaka mtu kupata cheo hiki , lakini anaepewa mara nyingi ni yule anaestahili pekee ambae ana mafunzo ya juu ya nishati za mbingu na ardhi .Anaweza kuwa mkuu wa jeshi ama asiwe mkuu wa jeshi .Kitendo cha mkuu wa jeshi kuwa na vyeo vyote viwili kwa wakati mmoja ilikuwa ni mara ya kwanza kutokea katika historia ya Tanzania tokea cheo hiko kiingizwe katika muundo wa vyeo.

Jambo lingine ni kwamba asilimia kubwa ya walioshika cheo hiki katika nyakati zilizopita hawakuwahi kufahamika kwa sura ndio huyu mkuu wa kwanza wa jeshi sura yake kuonekana.

Sasa Hamza anaona kama kweli alichosema ni sahihi , ina maana waliostaafu wengine cheo hiko bado wapo Tanzania? Watu ambao wana mafunzo ya juu ya nishati za mbingu na ardhi.

“Kumbe! Basi nadhani ni muda sahihi wa kutafuta mahali tulivu na kuanza maongezi yetu”Aliongea Hamza akipotezea mshangao wake.

“Hicho ndio ninachotaka pia”Aliongea mkuu huyo

“Simba Nyika kwanini msielekee kule nyuma kwenye bustani katika ukumbi wa mapumziko ? Ni sehemu iliotulia”Alipendekeza Mzee Mazengo.

“Hakuna haja Chifu Mazengo , tutatafuta sehemu yoyote tutakayo ona inafaa”Aliongea na palepale kufumba na kufumbua alipotea alipokuwa amesimama na kuacha watu wakikodoa macho licha ya upepo mkali uliobakia.

Hamza palepale aliangalia uelekeo aliopotelea na alikimbia nduki kama mwanariadha na sekunde mbili tu na yeye alipotea kwa kuruka juu kama amefyatuliwa.

“Jamani mniwie radhi na mimi naondoka mapema , la sivyo sitowaona”Aliongea Afande Himidu na palepale alipotea kama mwanga.

Lakini wanajeshi hao ambao pia walikuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi waliweza kumtofautisha Hamza , Mkuu wa Majeshi na Himidu , spidi ya Himidu iliokuwa ndogo kuliko ya Hamza na Mkuu wa majeshi.

“Kaka huyu Hamza ni nani ? Imekuwaje Yonesi akakutana na mtu kama huyu na kuwa boyfriend wake?”Aliongea Stanley akimuuliza Danieli.

Mzee Daudi aliishia kuwaza kimya lakini kadri alivyokuwa akifikiria alishindwa kupata jijbu

“Haijalishi ni nani , lakini hawezi kuwa kitu kinachoelea”Aliongea kauli tata Mzee Mazengo na palepale alitoa ishara ya kutaka kusimama huku wengine akiwapa ishara ya kuendelea.

*****

Ni katika msitu wa kupanda katika eneo la jeshi la Tanzania , katikati ya msitu huo kulikuwa na uwanja maalumu , sehemu ambapo mara nyingi hutumika kwa ajili ya mafunzo ya kulenga shabaha kwa wanajeshi.

Eneo hilo kawaida huwa kuna ukimya mno na kutokana na kuwa asubuhi ukimywa wake ulikuwa mkubwa mno.

Muda huo alieanza kutua katika eneo hilo ni Afande Simba na kisha akafuatia Hamza alietua kama vile ni kimondo .

Wote wawili walionekana ni kama viumbe vya ajabu kwa namna walivyotumia spidi kufika katika eneo hilo.

Afande Simba aliishia kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa bila ya kuongea na kisha palepale alipiga hatua mbili mbele na kusimama mbali na Hamza kwa mita kama kumi na tano hivi.

“Ni jina gani rasmi nikuite , Selafi , Prince au Usifa?”Aliongea kwa sauti nzito.

“Potezea hayo majina , hakuna haja ya kuyakumbushia wewe niite tu Hamza Mzee”

“Lakini hayo ndio majina matatu yanayokutambulisha juu ya uhalisia wako na yale yote uliyoyafanya lakini ninachoona ni kama huyapendi kabisa”

“Zama ya Selafi ilikuwa ni ya upweke na mahuzuniko makuu , Zama ya Usifa ni ya majonzi na bidii , kuhusu Prince ni jina la wakati mchache uliopita linalonifanya kuchoka mwili na akili. Sioni maana yoyote juu ya majina hayo”

“Kijana mtazamo wako kuhusu maisha umekosa msingi wa matarajio . Hivi unajua ni watu wangapi wanatamani kuwa kama wewe ? Kuna watu wengi sana wanatamani kuwa juu, lakini katika kipindi cha miaka mia moja iliopita ni wewe tu ulieweza kufanya makubwa na kupata sifa ulizonazo”

“Kwangu mimi kuwa maarufu , utajiri na madaraka sio kitu kilichonileta kwenye sayari hii , sifa zangu ni matokeo ya kuutafuta uhuru na kuendelea kuishi kwa kushinda vikwazo”

“Kwahio wewe ni mwanaume usiependa umaarufu?”

“Nadhani hivyo! Halafu kwanini nahisi ni kama unaniwekea mtego wa maneno?”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu, walikuwa wameachana umbali kama vile wanaogopana na kufanya waongee kwa sauti kubwa kidogo.

“Haha.. sitaki kuingia katika ugomvi na mjukuu wa shetani , ninachotaka ni kukujua kidogo tu”

“Hakuna unachoweza kunielewa kuhusu mimi ,unaweza kunifahamu kwa hili dogo napenda uhuru na wanawake warembo , hivyo ni kheri tukienda moja kwa moja kwenye mazungumzo yetu. Umenifanyia fadhila awamu hii , vipi unataka nikulipe? Nataka pia nipate taarifa za kibailojia kutoka katika Earth Axis , unaweza kuweka masharti yako nione kama naweza yatimiza”Aliongea Hamza.































SEHEMU YA 135.

Mkuu wa majeshi mara baada ya kusikia kauli ile ya Hamza alijikuta akiaungua kicheko.

“Leo tutapotezea kuhusu fadhila ndongo niliokufanyia , isitoshe wewe ndio uliehusika kuzamisha manowari ya kijeshi ya America , jambo ambalo nasikia limeshusha morarali sana kwa wanajeshi wa kitengo cha Delta Zero kufeli kwao, kufanikiwa kwa majaribio kisiwani Chole na wafanyakazi kurudi salama salimini ni swala la kukushukuru kitaifa. Tupo tayari kukupatia tafiti zote za kibailojia zitakazotoka katika Earth Axis lakini unapaswa kulipia gharama”

“Unataka nifanye nini? Huwa sipendi sana kuzunguka zunguka”Aliongea Hamza na aliingiza mkono kwenye koti lake na kutoa sigara na kiberiti na kuiwasha, haikujulikana ameitoa wapi.

Lakini licha ya kuvuta sigara mbele yake , Mkuu huyo wa majeshi wala hakuonekana kujali kabisa.

“Baada ya kukaa chini na viongozi kadhaa wa juu katika serikali , walitoa mapendekezo mengi lakini tukakaa chini na kuyajadili na kupata mapendekezo machache na utachagua kati ya hayo”

“Oh! , inaonekana nina vitu kadhaa mmeviona kutoka kwangu na kuvitamani”Aliongea Hamza huku akitoa moshi wa sigara akimpa ishara mkuu wa majeshi kuendelea.

“Mosi tunaitaka Barham”Aliongea na kumfanya Hamza macho yake kusinyaa.

“Mmiliki wa Barham ni Asazi, haipo chini yangu”Aliongea na Mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa na kisha aliinua kidole chake juu.

“Pili tunahitaji Daffodil”

“Daffodil sio ya kwangu , ni ya Asmuntisi kama mnaihitaji ni mpaka niongee na Asmuntisi ila sina uhakika wa kuipata”aliongea na Mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa na kisha akainua juu kidole cha tatu.

“Ombi letu la tatu ni kutupatia tafiti zote zinazohusiana na Ankh , nina taarifa kwamba kabla ya kifo cha Dokta Genesha ulikutana nae hapa nchini”Aliongea.

“Si nilishawaambia wale walionihoji kuhusu Ankh , inamaana taarifa hazijakufikiia? Kipindi kile niliongea na Himidu na kumwambia maswala yanayohusiana na Ankh yasitishwe juu yangu , lakini naona kaamua kuvunja ahadi yake”

“Umekosea kuhusu Mshauri mkuu , hata kama Mshauri mkuu asingeniambia chochote kuhusu Ankh unadhani mimi mkuu wa vitengo vyote ningeshindwa kujua ?”Aliongea huku akicheka.

Hamza alitingisha kichwa , ukweli ni kwamba hakujali sana , alijiambia hata kama alievujisha siri ni Himidu angemwelewa.

“Sio kwamba sipo tayari kutoa taarifa zote zinazohusiana na Ankh, sababu ni kwamba utafiti wake bado haujakamilika , kuna elementi muhimu zimekosekana na njia ya kuzipata ni kujua lugha ya kitabu chake kitu ambacho mpaka sasa sijaweza kutafsiri”Aliongea Hamza na kumfanya Simba Nyika kumwangalia Hamza kuona kama anadanganya au La na hatimae alitingisha kichwa kuonekana kukubali.

“Nimesikia Asazi na Asimuntisi wao ni kama Leviathan tu , wote wanakutii kwa kila unachowaambia , ili kukidhi masharti yetu , ongea nao na utupatie kati ya hivyo vitu viwili tulivyoomba, ukikamilisha tupo tayari kushirikiana na wewe juu ya tafiti zote za kibailojia zinazotokana na Earth Axis”

“Ngoja nirudie tena , ulichoomba ndio asili ya nguvu za jamaa zangu , wamezipata kwa juhudi kubwa sana , najua ni kweli nikiongea nao watanipatia lakini siwezi fanya hivyo”aliongea Hamza akiwa katika hali ya usiriasi mkubwa.

Afande Simba Nyika alifumba macho kwa sekunde kadhaa huku akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na alifungua macho na kumwangalia Hamza.

“Kama hayo maombi yameshindikana basi tupatie mtu”

“Nani mnamtaka?”

“Sally”

Sekunde ambayo alitaja hilo jina Hamza alipotea alipokuwa amesimama na ile anatokea alikuwa mbele ya Simba Nyika.

Hamza alikuwa na macho yaliojaa hasira kali mno na macho yake ni kama yalikuwa yakiungua na moto na palepale aliinua ngumi na kumpiga Simba nyika kumlenga kichwani.

Afande Simba hakuwa mzembe alishituka mapema kwani palepale alinua mikono yake juu na kukinga shambulizi lile

Bam!!

Shindo kubwa ilisikika . Hamza ngumi yake haikuweza kumfikia Afande Simba bali iligonga katika ‘Dhana’ ambayo ilifanana na ile mikanda wanayozawadiwa wacheza ndondi au mieleka.

Afande Simba alidhania ameweza kukinga shambulizi lile la Hamza lakini palepale alihisi wimbi kubwa la nishati likiongezeka kutoka nyuma yake kama vile ni sunami na kumvuta kwa nguvu, palepale alizidi kuongeza nguvu kuhimana na mvuto ule lakini alianza kusumbuka..

“Hii ni…”

Alijikuta akiwa katika mshituko mkubwa baada ya kuhisi ni kama vile anaishiwa nguvu na kutaka kudondoka chini wakati huo akisukumwa kurudi nyuma kwa kuteleza, lakini hata hivyo alikuwa vizuri, ili kuhimili mwili wake alitanguliza mguu mmoja mbele kwa namna ya kuukunja na mguu wa kushoto akaunyoosha kwenda nyuma na ukakita chini ya ardhi kama mtalimbo, staili hio ilikuwa ni ya Kung Fu maarufu kama Jin Dagger movement.

Mpaka anakuja kusimama chini alijikuta akiinua uso wake na kumwangalia Hamza na macho yake yalikuwa katika hali ya mshituko mkubwa.

Hamza alikuwa amebadilika na kuwa mtu mwingine kabisa mwili wake ulikuwa umetawaliwa na kivuli kama cha mnyama wa ajabu mwenye mabawa anaelea angani huku akiangalia kitoweo chini .

Mkuu wa majeshi alijikuta jasho likimtoka kwa wingi kwenye paji la uso wake , alijua fika kwamba kama Hamza akija kumshambulia tena anaweza shindwe kuhimili na kitu pekee ni kukimbia maana hakuna namna.

“Huyu kweli ni kiumbe hatari kama nilivyosikia”Alijikuta akiongea mwenyewe.

“Sally ni ndugu yangu wa damu , siwezi kuruhusu mtu yoyote yule kumgusa”Aliongea Hamza kwa sauti nzito sana huku mwili wake ukiwa umefunikwa na kivuli cha mnyama mkubwa kama Mwewe.

“Nilijua tu huwezi kukubali , isitoshe nilisikia sababu kubwa ya kugombana kwako na Mfalme Giza ni kwasababu ya Sally. Lakini kwasababu sharti hilo limekwama basi sina jinsi na kubadilisha , chukulia tu kama hujasikia nikitaja kuhusu hili”

“Ongea unataka nini kutoka kwangu”

“Unapaswa kufanya vitu vitatu kwa kitengo chetu cha Malibu , vitu hivyo vitatu tutakaa chini na kuamua.”

“Hapana , umeongea ki upana sana , kama nikikubali bila ya kujua ni vitu gani si sawa na kujiingiza kwenye mtego?”

“Nakuhakikishia ni masharti ambayo hayatazidi nilichoomba mwanzo”

“Hata kama ni hivyo lazima kuwe na ukomo”

“Taja ukomo wako nijue”,

“Masharti yenu hayapaswi kugusa familia yangu, Jamaa au marafiki , pia siwezi kufanya mambo ovu ya aina yoyote yanayokiuka asili ya ubinadamu”

“Kuna maswala mengine kuua ni swala ambalo halikwepeki! Vipi utaweza kufanya na hivyo?”

“Ili mradi anaekufa anastahili kufa hakuna shida”Aliongea Hamza.

“Nakuhakikishia Tanzania ni nchi inayoendeshwa katika misingi ya haki na hatuwezi kuomba kitu kinachokiuka asili ya binadamu”Aliongea Afande Simba na kumfanya Hamza kufikiri kidogo.

“Kama ni hivyo ni lini nitaweza kupata taarifa za Earth Axis?”

“Utaweza kupata taarifa zake baada ya kukamilisha kile tutakachokupangia”

“Nini! Inamaana hamjakaa na kuamua bado , nisubiri mpaka lini?”

“Usiwe na wasiwasi ndani ya miaka mitatu tutaweza kukupatia taarifa , unapaswa kujua Tanzania ni nchi ambayo inaanza kupiga hatua katika Teknolojia kuingia ulimwengu wa pili , mambo mengi yanafanyika kwa taratibu maalumu hivyo hatuwezi kuharakisha”

Hamza alifikiria kidogo na palepale aliona miaka mitatu sio mingi sana ni kama kufumba na kufumbua tu.

“Kama ni hivyo mniambie masharti yenu haraka sana niyafanyie kazi na nibakie kuwadai”Aliongea Hamza hakuhofia Mkuu huyo kumgeuka baadae , alijiambia akimdanganya basi cha moto atakipata .

“Nadhani mpaka hapo tumefikia makubaliano , nitaondoka na kuweka haya mbele ya mkuu wangu”Aliongea.

“Hakuna shida , mimi narudi nyumbani kwa Mzee Mazengo hivyo siwezi kukusindikiza tena”Aliongea Hamza akipanga mwakati maandalizi ya sherehe yakianza akazame chumbani kwa Yonesi na kujaribu bahati yake.

“Subiri kwanza”Aliongea Mkuu wa majeshi au Afande Simba Nyika.

“Kuna kitu kingine unataka kuongea Afande?”Aliuliza Hamza.

“Baba yako ndio alikuwa mzungu au ni mama yako?”Aluliza

“Sijafuatilia hivyo sijui”Aliongea Hamza akiwa amekunja sura.

“Oh! Kama ni hivyo basi chukulia kama sijauliza”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kukubali.

“Niagie kwa Himidu , mwambie sitoweza kuonana nae kwa leo , tutaongea ana kwa ana siku nyingine”Mara baada ya kuongea hivyo Hamza aliruka juu na palepale alifyatuliwa na kupotea.

Baada ya mkuu wa majeshi kutembea mita kama mianne hivi aliweza kukutana na Himidu ambae alikuwa akimsubiri kwa mbali.

Ili kuepuka kutoonekana na Hamza , Himidu hakusogea karibu.

“Umemaliza! Vipi amekubali ombi lipi?”Aliuliza Himidu akiwa na tabasamu.

“Ni kama ulivyotarajia , umekuwa sahihi pia amenipiga ngumi”Aliongea kwa wasiwasi.

“Haha.. umekula ngumi moja tu ? Siku za nyuma ilikuwa ukimtaja Sally atakupiga mpaka maji uyaite Mma”Aliongea huku akicheka sana na kumfanya Afande Simba kusikitika na tabasamu la uchungu.

“Halafu Bosi amevua mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi , vipi umemshindwa na wewe pia licha ya hivyo?”

“Una uhakika sio kama amejifunza upya ndani ya miaka yote? Nakumbuka hata wewe ulipoteza uwezo wako mwanzo?”

“Ni kweli ila bosi hajawahi kunidanganya , akisema amevua uwezo wake wa nishati basi jua ni kweli”Aliongea.

“Duh! Kweli nimeamini sio wa kawaida , nadhani ndani ya jeshi letu ni Nyakasura pekee anaeweza kupigana nae”Aliongea huku akishika kiuno.

Himidu mara baada ya kusikia jina la Nyakasura alitingisha kichwa kukubaliana nae lakini alionekana kukuna kichwa kama vile hana uhakika.

“Simba! Nimesikia Nyakasura amesema amechoka kukaa mpakani na anapanga kwenda Dar es salaam kwa siku kadhaa kupunga upepo wa baharini . Vipi unapanga kumpa kazi, maana nahisi ni kama safari yake ina mipango mingine”

“Amekuambia anataka kwenda Dar es salaam?”Aliuliza huku akionekana kusita kidogo kama mtu ambae hana taarifa hio.

“Ngoja nitamuuliza , sijampa kazi yoyote Dar”Aliongea.

*****

Hamza mara baada ya kurudi kwenye makazi ya familia ya Chifu Mazengo alitaka kwenda kujaribisha kupata kitumbua cha asubuhi na Yonesi lakini bahati mbaya mwanamke huyo alikuwa amekwisha kuondoka kwenda hospitalini.

Hamza hakushangaa sana kuwahi kwa Yonesi kwenda hospitalini , isitoshe ndio walikuwa wanawake pekee yeye na mama yake katika familia hio.

Muda ambao amerudi wafanyakazi walikuwa bize sana na wale ambao wanakuja asubuhi walikuwa washafika na kulikuwa na ubize mwingi wa kuandaa sherehe.

Hamza mara baada ya kupumzika kidogo na kujisafisha alikaribishwa kwenye ukumbi kwa ajili ya kifungua kinywa na wanafamilia wengine.

Baadhi ya wanafamilia hao walikuwa na soni kutokana na kumdharau mwanzo na kujikuta wakikosa amani , lakini Hamza hakuonekana kujali kabisa, alikula kama yupo nyumbani.

Baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa alimwomba Mzee Sauli gari na kisha akaanza safari ya kuelekea hospitalini.

Mara baada ya kufika wodini Mama yake Yonesi alikuwa amesharejewa na fahamu na ameamka usingizini na alikuwa akiongea na Yonesi.

Ijapokuwa alikuwa ameunganishwa na mavifaa yanayomsaidia , lakini alionekana kuwa sawa kabisa . alipaswa kupumzika kwa siku kadhaa mshono upone ndio arejee nyumbani.

“Mama vipi kidonda kinauma na unapumua vizuri?”Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu na mama huyo baada ya kumuona Hamza alikuwa na hisia mchanganyiko.

“Nimesikia wewe ndio daktari ulienifanyia upasuaji , Asante sana najisikia vizuri kwasasa”

“Ni kheri hali yako inaonekana kuwa nzuri kwasasa la sivyo Yonesi hatoweza kurudi Dar”Aliongea.

“Ijapokuwa umeniokoa kitu ambacho nashukuru lakini siwezi kukusamehe kwa kutaka kumfanya binti yangu mchepuko”

“Mama.. Mwili wako bado ni dhaifu haina haja ya kufikiria kuhusu hili”Aliongea Yonesi haraka.

“Mama usinielewe vibaya , kukufanyia upasuaji kuokoa afya yako haina maana kuna kitu nataka kutoka kwa Yonesi?”

“Oh, kama ni hivyo unataka nini?”

“Nimeyaokoa maisha yako kwasababu mimi ni daktari , nilivyokuona na dalili za kuumwa ni kawaida kama daktari kutaka kukutibu , hata kama mgonjwa ni adui yangu nitaanza kumtibu kwanza, ni maswala ya Medical Ethics na siwezi kuyaingiza na maswala yangu binafsi . Hivyo usije ukahisi kama nakudai “Aliongea na kumfanya mwanamama huyo kumwangalia Hamza kwa mshangao kidogo.

Yonesi pia alishangazwa na namna ambavyo Hamza alionekana kuwa siriasi na muungwana na alizidi kuona Hamza ana upande wa tofauti sana uliomfanya kuzidi kuvutiwa nae.

Hamza mara baada ya kuongea alichukua nafasi hio kuangalia vipimo vya mgonjwa kuona maendeleo yake na aligundua hakukuwa na tatizo kabisa hivyo aliondoka.

Muda mfupi baadae Dr Ivan Bridge alifika akiongozana na mtoto wake Christiani na Ivan alitumia fursa hio kuanza kumsifia Hamza na vilevile alimwambia Maria namna Hamza alivyoweza kumponyesha na Christiani.

Mama huyo mara baada ya kusikia kuhusu Christiani mpwa wake kutibiwa na Hamza alijikuta akiingia kwenye tafakari nzito.

*****

Sherehe ya kumpongeza Mzee Chalula Mazengo kwa kutimiza miaka tisini ilifana sana, watu wengi wenye ukaribu na familia hio walialikwa na kusherehekea pamoja.

Swala la mkuu wa Majeshi kufika na kuitembelea familia hio liliwafikia watu wengi na kufanya heshima ya familia hio izidi kukua

Mwanzoni familia hio haikuwa na mpango wa kumwandalia Hamza kiti cha kukaa , lakini walijikuta wakifanya hivyo na kutenga kiti cha mbele kabisa pamoja na Yonesi.

Baada ya sherehe kuisha Hamza aliaga kwa ajili ya kurudi Dar siku inayofuata.

Alikuwa na haraka ya kurudi kutokana na kwamba siku ya kesho kutwa yake Irene alimwalika kwa ajili ya kuhudhuria mashindano ya vipaji maalumu kwa mkoa wa Dar es salaam kwa shule zote na wale ambao wangeshinda wangeweza kupata ufadhili wa masomo nje ya nchi.

Juzi yake wakati Irene anamwomba Hamza hela ilikuwa ni kwa ajili ya kumchangia katika maandalizi ya siku hio.

Irene alikuwa na kipaji cha kuimba pamoja na kupiga kinanda na ndio upande ambao alipanga kwenda kushindania na kwasababu msichana huyo alisisitiza sana aliona haina haja ya kukataa, isitoshe msichana huyo kwa mara ya kwanza alionekana kuwa siriasi mno.

Upande wa Yonesi asingeweza kurudi Dar kutokana na hali ya mama yake ilivyo , hivyo Hamza siku iliofuata saa kumi za jioni alipanda treni kurudi Dar es Salaam.

Muda ambao alifika Dar ilikuwa ni usiku tayari na mara baada ya kumkumbuka Regina palepale aliona ni vyema akienda na zawadi ya kumbembeleza na kitu pekee amabcho aliona kinaweza kumlainisha mwanamke huyo ni boksi la Donati kutoka supermarket , kadi ya kuombea msamaha pamoja na ua zuri.

Licha ya kwamba ilikuwa usiku aliweza kupata kila alichopanga na kisha alianza safari ya kurdi.

Mpaka anafika nyumbani ilikuwa ni saa nne za usiku tayari na Shangazi alikuwa ashaenda kulala muda mrefu , lakini mwanga wa taa katika chumba cha Regina cha kujisomea zilikuwa zinawaka bado.

Hamza mara baada ya kuingia ndani alienda moja kwa moja mpaka katika chumba cha kujisomea cha Regina na kisha aligonga mlango lakini hakuna aliemwitikia kwa ndani.

Alirudia tena , lakini bado hakuitikiwa kwa ndani na alichofanya ni kutega sikio kusikilizia kwa ndani na aliweza kusikia sauti za mtu kuchapa kwa kutumia Keyboard ya tarakishi na alijua palepale atakuwa ni Regina amabe anaendelea kufanya kazi, hivyo alifungua mlango na kuingia.

“Wife , Vipi uko bize sana?”

Regina alikuwa amevalia sweta kama blauzi ya mikono mirefu yenye mkato wa V shingoni iliofanya vimanyonyo vyake kuchomoza kama miba, pamoja na namna alivyosiriasi alizidi kuonekana mrembo.

“Sijakuruhusu uingie”Aliongea huku akimwangalia Hamza bila hisia zozote

“Nimegonga sana mlango lakini hujafungua , labda ulikuwa bize ndio maana hujanisikia”

“Nimekusikia vizuri tu , ila sitaki kukuona, hebu toka nje”Aliongea kikauzu na kumfanya Hamza kujisikia vibaya , aliona kweli Regina alikuwa ni tafsiri halisi ya mwanamke Kauzu.



ITAENDELEA. watsapp 0687151346
 
Back
Top Bottom