Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mjukuu wa shetaniho is hamuza??? hii code inafikilisha sana
saf sana mkuuSHETANI RUDISHA AKILI ZETU.
MTUNZI : SINGANOJR.
SEHEMU YA 153.
Simba wa nyika.
“……sifa zangu ni matokeo ya kuutafuta uhuru na kuendelea kuishi kwa kushinda vikwazo”
Mara baada ya mkurugenzi wa kitengo cha TIMISA kunona sehemu alioweka kidole mkuu wa majeshi. palepale alijua alikuwa akilenga nini .
“Afande unamaanisha kilichotokea Kilwa baada ya Wabrazili kufungua kanisa lao ndani ya hili eneo?”Aliuliza kwa kutokuwa na uhakika na mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa kukubaliana nae.
“Lakini mkuu mpaka sasa bado najiuliza , kulikuwa na haja ya wanajeshi wetu kuingilia hili swala na kuwazuia hawa wabrazili kutofungua kanisa lao , hapa Dar es salaam wamekuwepo kwa muda mrefu lakini hakukuw ana tatizo lolote na hata kama ni swala la kijamii viongozi wa serikali ndio walipaswa kuingilia na sio wanajeshi”
“Shida sio kutokuwa na tatizo lolote , nadhani mnajua ni kipi kinaendelea ndani ya hili kanisa , ni kanisa gani ambalo linapokea kila imani?”Aliongea Afande mwingine.
“Kwa ninachojua kuhusu hili kanisa sio swala tu la imani ila ni lengo moja ndio linalowaunganisha , ni kweli kuna watu wana imani tofauti lakini wana muda tofauti wa kuhudhuria ibada na siku moja ya kujumuika pamoja”aliongea mwingine.
“Lakini nyie hamna shauku , kama kweli lengo lao ni kutoa mahubiri ya imani yao kuna haja ya kwenda kuweka kanisa Kilwa , yapo maeneo mengi ambayo wangeweka makanisa lakini wakachagua eneo ambalo lina ukinzani mkubwa”
“Labda ni kwasababu lina ukinzani ndio maana wamemua kuanza katika eneo hilo”Alikisia mwingine.
“Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu hili swali , kama kweli mpango wao ni kuleta kile wanachoamini ni mafundisho ya kiimani ya kuzaliwa upya baada ya kufa, hata kama kama wameona ndio sehemu sahihi ya kuanzia kujipanua , lakini kwanini wapeleke kundi la watu wote wale tena wageni kutoka nje ya nchi?”
“Jenerali kuna sababu yoyote unaifikiria?”aliuliza mwingine lakini Jenerali alitingisha kichwa kuonyesha hajui.
“Naona ni vizuri tukiweka umakini sana juu ya haya makanisa ya Wabrazili, lazima kuna kitu kinaendelea”Aliongea na muda huo huo simu ya Afande Himidu ilianza kutoa mwito wa kuita.
Afande Himidu mara baada ya kuona anepiga alitoa tabasamu kidogo na kisha alipanga kuipokea palepale.
“Mshauri mkuu ni mara yangu ya kwanza kuona simu yako ikiita katikati ya kikao”Alitania mwanajeshi mmoja.
“Kuna baadhi ya simu unapaswa kupokea muda wowote”Aliongea
“Oh! Au ndio mteule ndio anaepiga simu?”
“Hii ni simu zaidi ya mteule”Aliongea na palepale alipokea simu ile.
“Bosi usiku sana , kuna tatizo?”
Mshangao wa kutotarajia uliwashika kila mmoja aliekuwepo ndani ya hilo eneo baada ya kumsikia mshauri mkuu akiita mtu Bosi. Walijiuliza ni mtu gani huyo ambae anaweza kumfanya Himidu kupokea simu mbele kabisa ya mkuu wa majeshi.
Midomo ya Mkuu wa mejeshi ilicheza kidogo , hakuongea kitu zaidi ya kuinua kikombe chake cha kahawa na kunywa kidogo huku akionekana kuwa na hali ya umakini mkubwa.
“Bosi nimekuelewa nitakupigia asubuhi , ngoja niangalie cha kufanya sasa hivi”
Afande Himidu mara baada ya kumaliza kuongea na simu hio , mwonekano wake ulikuwa na hisia mchanganyiko.Baada ya kukata simu ile aligeuka na kumwangalia Mkuu wa majeshi na tabasamu lililojaa uchokozi.
“Simba Nyika acha kujifanyisha , wengine hapa wanaweza wakawa hawajasikia , lakini masikio yako yamesikia kila kitu alichokuwa akiongea alienipigia upande wa pili”
“Kwahio vipi kama nimesikia? M,ara ya mwisho uliniambia unataka tuongee dili na huyo mtu ambalo litapelekea mafanikio kwa jeshi letu , nadhani huu ni muda sahihi wa kuongea nae au wewe unaonaje?”Aliongea na Himidu alitingisha kichwa kukubaliana nae na kisha palapale aligusa mkoa wa Dodoma na kidole chake.
“Afande Mazengo , kama kijana wako ni busara kuja kukutembelea katika siku yako ya kutimiza miaka tisini”
Mara baada ya kuongea hivyo kila mmoja aliekuwa katika meza alishangazwa na kauli yake.
*****
Saa kumi za alfajiri katika familia ya Chifu Mazengo , karibia watu wote wamekwisha kuamka kasoro wafanyakazi pekee..
Meja jenerali Daudi Chalula alikuwa amekaa na ndugu zake pamoja na marafiki na walikuwa wakinywa kahawa huku wakiongea na kujadiliana namna ya kudili na swala la kifamilia lililotokea jana.
“Kaka sidhani kama ni vizuri kufanya hivi , kwanini tusiongee na Mzee Mirambo, ni kweli tunaweza kupata hasara upande mwingine lakini hatuwezi kuacha hili swala liingilie sherehe ya baba”Aliongea Mtemi, mdogo wake Daudi.
“Unadhani wanataka tuongee nao? Kama wanataka tuongee nao wasingetusababishia matatizo kwanza . Ni kheri kutoenda kwao kusababisha matatizo zaidi”Aliongea Mdogo wake mwingine..
“Siwezi kukaa na kuendelea kusubiri , nitakuja kumfanya kitu mbaya sana Imani na familia yake”Aliongea Daudi huku akisaga meno kwa hasira
“Alfajiri yote hii mbona makelele ya vitisho mengi”Sauti ya kizee ilisikika kutoka nyuma na kuwafanya wageuke.
Watoto hao wa Mzee Mazengo walishagnaa baada ya kuona ni baba yao maana sio kawaida kuamka mapema.
“Baba kwanini umeamka mapema?”Aliongea Daudi na palepale alisimama na kwenda kumsaidia baba yake kutembea lakini Mzee Chalula alimsukuma asimsaidie.
“Mbona unanishika , unadhani siwezi kutembea! Mtu mmoja anatosha”Aliongea na kisha alisaidiwa na mzee Sauli kukaa kwenye kiti .
“Nimesikia kuna tukio limetokea jana?”Aliuliza na muda ule Mzee Daudi aliona haina haja ya kuendelea kumficha baba yake.
“Sikutaka kukusumbua baba , ila jana Danny na Stanley walikamatwa kwenda kufanyiwa mahojiano kwa kosa la kuhujumu jeshi. Lakini sio kweli kuhusu hili lazima ni huyu mkongwe fisadi wa familia ya Mirambo ndio kahusika”Aliongea kwa hasira.
“Hebu kaa kimya!”Alifoka Mzee Chalula.
“Wakati Mzee Mirambo akiwa ni mwanasiasa nguli nchini wewe ulikuwa mtoto , ukiheshimu watu na wao watakuheshimu. Unadhani maneno yako haya yakisikika nini kitatokea”Aliongea na kufanya ndugu wote kukaa kimya na hasira zao kupotea.
“Wanategemea kukamilisha uchunguzi lini na kuwaachia huru?”Aliuliza baada ya kutulia.
“Nadhani ndani ya wiki moja au mbili . Nishawasiliana na baadhi ya watu ndani ya kamati na wamesema uchunguzi bado unaendelea na ni mpaka ukamilike. Baba hofu yangu ni kama wakiongea ujinga na kujikuta wakiingia katika mtego”Aliongea Mzee Daudi kwa wasiwasi.
“Kama kuna makosa wamefanya hawawezi kulaumu wakipatikana na hatia . Familia yetu pia inafuatiliwa sana kwenye kufanya maamuzi ni kawaida watu kuwa na maoni tofauti”
“Ndio baba”Waliitikia wote lakini bado walionekana kuwa wanyonge.
“Baba kawaida una amka saa mbili za asubuhi , mbona umewahi sana leo?”Aliuliza Afande Daudi.
“Leo ni siku ya kipekee sana , kuna mgeni muhimu anatarajia kufika hapa kwa ajili ya kunipongeza kufikisha miaka tisini , ndio maana nimeamka “
“Mgeni wa muhimu ? Baba kuna wageni kutoka Ikulu wanaokuja leo?”Aliuliza Daudi na wenzake wote pia walionekana kuwa na shauku , maana kama ni nje ya Ikulu isingekuwa na haja ya kuwasiliana na Mzee Mazengo mwenyewe .
“Mgeni anaekuja ni mtu ambae ni ngumu kukutana nae kuliko viongozi wa Ikulu”Aliongea lakini ni muda huo huo mfanyakazi alikuja haraka haraka upande wao kutoa taarifa.
“Babu! Mkuu wa Majeshi na Mshauri mkuu wamefika kwa ajili ya kukutembelea na kutoa pongezi zao”
Mara baada ya maneno hayo kusikika , wanafamilia wote waliokuwa katika eneo hilo walijikuta wakishangaa ni kama hawakuwa wakiamini.
Ikumbukwe kwamba Mkuu wa Mejeshi amekuwa ni mtu wa kujitenga sana na mara nyingi aliwakilishwa katika sehemu nyingi , kuja mpaka hapo iliwafanya washangae.
Miaka kadhaa nyuma kazi zote ambazo zilikuwa ni za mkuu wa majeshi , ziliwekwa chini ya Mhauri Mkuu wa jeshi na ilikuwa ni mara chache sana Mkuu wa jeshi kuhusishwa katika kazi za kila siku labda kwa matokeo maalumu tu.
Sasa mkuu huyo kuja mpaka hapo kwa ajili ya kumtembelea Chifu Mazengo ilishangaza wengi waliosikia taarifa hio.
“Haraka , wakaribisheni ndani”Aliongea Mzee Chalula akiwa na utulivu.
Mara baada ya kutoa kauli hio , dakika chache mbele wanaume wawili waliingia katika eneo hilo mmoja akiwa amevaa kombati za kijeshi za cheo cha ukuu kabisa na mwingine akiwa amevaa kombati za kijeshi cheo cha Jenerali.
Kitendo cha Meja Jenerali Daudi kukutanisha macho na Mkuu wa Majeshi walijikuta wakianza kutetemeka kutokana na hali ya kutokuwa wa kawaida ya mkuu huyo , alikuwa akisababisha msisimko ambao ulifanya nywele zao kusimama kama vile mbele yao alikuwa amesimama Jini.
“Jenerali Mstaafu Chalula kheri ya siku yako ya kuzaliwa na pongezi kwa kutimiza miaka tisini ni hatua ndefu”Aliongea akiwa na tabasamu , lakini hata hivyo haikutosha kufanya wanajeshi waliokuwa katika eneo hilo kuwa katika hali ya utulivu.
“Mzee wangu mimi pia nakutakia kheri ya kuzaliwa na pongezi ya kutimiza miaka tisini Jenerali Mstaafu na pia tunaomba radhi kwa kuja asubuhi asubuhi”Aliongea Afande Himidu huku akipiga saluti na kumfanya Afande Mazengo kucheka.
“Karibuni sana , wala hakuna haja ya kuomba radhi na uzee wangu huu Mkuu wa majeshi na Mshauri mkuu kuja kunitembelea ni heshima, Karibuni mketi”
“Mtu aletee chai wageni wetu”Aliongea
Baada ya Mkuu wa majeshi na Mshauri mkuu kukaa waliinua sura zao na kuwaangalia wanajeshi waliokuwa wamesimama kikakamavu.
“At Easy Ma’afande , tupo hapa kwa ajili ya kumpongeza Mzee wetu”Aliongea na palepale wanajeshi wale walilegeza.
Kulingana na sheria za jeshi kwasababu hawakuwa katika kombati za kijeshi hawakupaswa kupiga saluti badala yake walibana t*ko.
Baada ya chai na kahawa kuandaliwa pamoja na maongezi kidogo ya hapa na pale , familia ya Mzee Mazengo walijikuta wakiangaliana wakifikiria namna ya kumuomba mkuu wa mejshi msaada juu ya ndugu waliokamatwa , hakuna aliekuwa na ujasiri.
Kwa cheo chake kauli yake moja tu ingetosha kuwafanya kuachiliwa huru moja kwa moja.Isitoshe hata kwa namna gani koneksheni ya kisiasa waliokuwa nayo familia ya Mirambo lakini mkuu wa majeshi ni m kuu wa majeshi.
Lakini kutokana na wengi wao hapo wamekutana na mkuu huyo mara chache sana , iliwafanya kugubikwa na hofu kubwa.
Dakika hio hio wakati wakiangaliana kwa ishara ya kutaka mmoja wapo aanze , mhudumu alifika tena na kutoa taarifa ya kurudi kwa Danny na Stanley.
Mara baada ya kusikia taarifa hio familia nzima walishikwa na mshangao isipokuwa tu kwa Mzee Mazengo.
Dakika hio hio vijana wawili waliokuwa katika mavazi ya kiejshi waliingia katika ukumbi kwa ari kubwa na walipiga saluti baada ya kufika kama ishara ya salamu kwa wakubwa zao na kisha walipewa ishara ya kulegeza.
“Babu , Baba samahani kwa kuwafanya kuwa na wasiwasi”Waliongea
“Danny mko sawa , vipi kuhusu kesi yenu?”
“Ndio baba tupo sawa , kuhusu kesi yetu hatujaambiwa chochote na tumeruhusiwa tu kurudi nyumbani na watu wa kamati wametuomba radhi wakisema kuna mkanganyiko wa kitaarifa uliotokea na hatukuwa na kosa”
Mara baada ya kusikia kauli hio wanafamilia hao walishangaa zaidi , bado hawakuelewa nini kinaendelea. Ni Mzee Chalula Mazengo pekee alieonekana kujua kinachoendelea na palepale aliinua kikombe cha chai na kuwapa ishara Mkuu wa Majeshi na Mshauri mkuu .
“Asanteni kwa zawadi ya siku yangu ya kuzaliwa Simba”
“Mstaafu , tumekuja haraka haraka na tumejikuta hakuna tulichoandaa , tumeona tutoe tu msaada kidogo ili mradi hotujali”
“Hii zawadi ni kubwa zaidi ya dhahabu na fedha”Aliongea Mzee huyo akiwa na mwonekano uliojaa usiriasi.
Mzee Daudi na nduguze walisimama palepale na kutoa shukrani kwa mkuu wa majeshi na Mshauri Mkuu, hata kama watoto hao hawakuwa na kosa lakini kitendo cha Mkuu wa majeshi kuingilia kilikuwa na maana kubwa sana kwao.
“Haina haja ya kunishukuru mimi moja kwa moja , nimekuja hapa kwa ajili ya kutoa pongezi zangu lakini vilevile kwasababu mmoja wa mwanafamilia wenu amenipa kazi ya kulimaliza hili swala mapema , Kama hili linahesabika kama zawadi basi na mwanafamilia alieniagiza anapaswa kujumuishwa”
“Kumbe bado tuna watu ndani ya familia yetu wenye uwezo wa kumuomba mkuu wa majeshi kusaidia kutatua shida kama hii?”Aliongea Mzee Mazengo kwa mshangao.
“Mstaafu inaonekana bado hujajua , namzungumzia mwanaume ambae mjukuu wako amemleta kwenu, ni bwana mdogo ambae sio mwepesi”
Mara baada ya maneno hayo palepale Afande Daudi alijua nani anazungumziwa .
“Hamza!!”
Wanafamilia wengine walishangazwa na jambo hilo , ijapokuwa walijua Hamza uwezo wake sio wakawaida lakini hakuna aliedhania anaweza kumpa kazi mkuu wa Majeshi na kuitekeleza.
“Nilisikia Hamza na Mshauri mkuu wana ukaribu mkubwa , sikutarajia hata wewe Mkuu wa Majeshi? Najikuta kuwa na shauku kubwa juu yake , unaonaje ukinielezea kidogo kuhusu huyu Hamza ni nani haswa?”Aliongea Mzee huyo na wanafamilia wote walimwangalia mkuu wa majeshi kwa shauku kubwa lakini na wasiwasi kwa wakati mmoja , hususani Mzee Daudi ambae alimfokea sana Hamza tokea kufika kwake.
“Mzee wangu sio sehemu salama kutoa taarifa kuhusu Hamza , leo Simba amefika hapa kwasababu anahitaji kuongea nae , tutaomba sehemu iliojitenga kwa ajili ya maongezi”Aliongea Afande Himidu.
Familia nzima walijikuta wakiwa katika mshangao , ilikuwa ngumu sana hata kwa wao wenyewe wanajeshi kukaa meza meja na kuongea na Mkuu wa Majeshi.
Lakini kijana mdogo sana kama Hamza ambae si tu kumuomba mkuu wa majeshi kusaidia kuwachiliwa kwa Danny na Stanley lakini vilevile amemwita Mkuu wa Majeshi kwa ajili ya kuongea nae.
“Afande Himidu mbona mna haraka sana wakati mnasafiri na ndege binafsi?”
Sauti iliweza kusikika , alikuwa ni Hamza aliekuwa akija upande wao kwa hatua ndefu kusogea alipo Afande Himidu na Mkuu wa Majeshi.
Mkuu wa Majeshi palepale aligeuka na kumwangalia Hamza na macho yaliojaa ukali na mkandamizo mkubwa wa nishati za mbingu na ardhi ulimtoka na kuwasababishia Afande Daudi na wenzake kukakamaa miili yao kwa hofu.
Hamza upande wake hakuwa na hali ya wasiwasi kabisa na alikaziana macho na Mkuu wa majeshi huku akitoa tabasamu la uchokozi , hakuonekana kuathirika na mkandamizo wa nishati za mbingu na ardhi ambao mkuu huyo alikuwa akimjaribu nazo.
Wanajeshi waliokuwa hapo walimwangalia Hamza na walishangaa kuona hakuonyesha ishara yoyote ya hofu wala kuathiriwa na mkandamizo ule na walijikuta wakianza kumhofia.
Katika macho yao Hamza alikuwa amezidi kuwa hatari . Hakuonekana tena kama kijana mdogo katika umri wa miaka ishirini na kuendelea , alikuwa ni kama jitu kwao.
Mzee Mazengo macho yake yaliishia kuchanua , aliishia kutingisha kichwa chake kwa ishara ya kumkubali Hamza .
“Hamza shukrani kwako nimefikisha miaka tisini kwa furaha kubwa”
“Huna haja ya kunishukuru Babu , wajukuu zako hawakuwa na kosa ndio maana wameachiliwa huru”
“Haha .. upo sahihi, hakuna mwanafamilia wangu anaeweza kulihujumu jeshi , ikitokea akiwepo nitaanza kumwadabisha mimi mwenyewe kabla ya sheria za nchi”Aliongea kwa ridhiko kubwa.
Upande wa Afande Daudi alikuwa katika hali ya sintofahamu . Mwanzoni alimpiga mkwala Hamza ili kupima uwezo wake lakini hakuamini Hamza angeweza kuwatoa watoto wake kwa simu moja tu na zaidi sana kuwaleta watu wazito katika familia yao.
Kutokana na hilo alijikuta akikosa namna ya kuweza kupinga tena mahusiano ya Yonesi na Hamza.
Mkuu wa Majeshi alimwangalia Hamza kwa dakika kadhaa , akionekana kama mtu ambae anawaza jambo lakini hakuongea chochote.
Hamza mara baada ya kuona macho ya mkuu huyo yalivyo kuna hali iliokuwa ikimsemesha kwa kumwambia kuna kitu hakipo sawa lakini hakuweza kujua ni kitu gani hicho. Ilikuwa ni kama mkuu huyo kuna mtu anajaribu kumfananisha nae.
“Afande Mkuu , kuna kitu kipo kwenye sura yangu , kwanini unanikodolea macho namna hio?”
Mara baada ya kusikia Hamza akiongea kwa staili hio wanajeshi wote waliokuwa hapo walijikuta wakihisi hewa imegeuka barafu, ulikuwa ni ujasiri mkubwa Hamza kuongea na mkuu wa majeshi kama mshikaji wake.
Lakini hata hivyo mkuu wa Majeshi hakuonyesha kukasirika na kauli ya Hamza na palepale alisimama na kunyoosha mkono kusalimiana na Hamza.
“Nimesikia jina lako muda mrefu sana , kinachonishangaza ni namna unavyonekana kuwa mdogo nje ya mategemeo yangu”
Mara baada ya kuongea hivyo wanafamilia walijikuta katika hali ya mshangao huku wakijiuliza inakuwaje Mkuu wa majeshi anasema amelisikia jina la Hamza muda mrefu ,anazungumzia muda mrefu upi?.
Tatizo kubwa lililoleta zaidi sintofahamu ni kwamba familia hio hakuna ambae ashawahi kusikia jina la Hamza mpaka Yonesi alivyomleta.
Kila mtu alimwangalia Hamza na usiriasi katika macho yake , muda huo Hamza akisalimiana na Mkuu wa majeshi kwa salamu ya mkono.
“Simba Nyika ni jina lako maarufu la utani ambalo nimelisikia kutoka kwa wanajeshi wengi , lakini hata mimi sijategemea kukuona ukiwa na mwonekano mdogo kama hivi”Aliongea Hamza.
“Simba Nyika uliemsikia wakati ukiwa mdogo sio mimi , nimerithi cheo cha Simba wa Nyika miaka kumi iliopita”Aliongea na Hamza alionekana kushanga kwasababu ilikuwa ndio mara yake ya kwanza kusikia jambo hilo.
Unachopaswa kuelewa ni kwamba ukiachana na cheo cha ukuu wa jeshi , kama cheo cha juu zaidi , kulikuwa na cheo kingine cha heshima ambacho ni zaidi ya ukuu wa jeshi na cheo hiki ni Simba Nyika, haijawahi kuwa wazi ni vigezo gani vinazingatiwa mpaka mtu kupata cheo hiki , lakini anaepewa mara nyingi ni yule anaestahili pekee ambae ana mafunzo ya juu ya nishati za mbingu na ardhi .Anaweza kuwa mkuu wa jeshi ama asiwe mkuu wa jeshi .Kitendo cha mkuu wa jeshi kuwa na vyeo vyote viwili kwa wakati mmoja ilikuwa ni mara ya kwanza kutokea katika historia ya Tanzania tokea cheo hiko kiingizwe katika muundo wa vyeo.
Jambo lingine ni kwamba asilimia kubwa ya walioshika cheo hiki katika nyakati zilizopita hawakuwahi kufahamika kwa sura ndio huyu mkuu wa kwanza wa jeshi sura yake kuonekana.
Sasa Hamza anaona kama kweli alichosema ni sahihi , ina maana waliostaafu wengine cheo hiko bado wapo Tanzania? Watu ambao wana mafunzo ya juu ya nishati za mbingu na ardhi.
“Kumbe! Basi nadhani ni muda sahihi wa kutafuta mahali tulivu na kuanza maongezi yetu”Aliongea Hamza akipotezea mshangao wake.
“Hicho ndio ninachotaka pia”Aliongea mkuu huyo
“Simba Nyika kwanini msielekee kule nyuma kwenye bustani katika ukumbi wa mapumziko ? Ni sehemu iliotulia”Alipendekeza Mzee Mazengo.
“Hakuna haja Chifu Mazengo , tutatafuta sehemu yoyote tutakayo ona inafaa”Aliongea na palepale kufumba na kufumbua alipotea alipokuwa amesimama na kuacha watu wakikodoa macho licha ya upepo mkali uliobakia.
Hamza palepale aliangalia uelekeo aliopotelea na alikimbia nduki kama mwanariadha na sekunde mbili tu na yeye alipotea kwa kuruka juu kama amefyatuliwa.
“Jamani mniwie radhi na mimi naondoka mapema , la sivyo sitowaona”Aliongea Afande Himidu na palepale alipotea kama mwanga.
Lakini wanajeshi hao ambao pia walikuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi waliweza kumtofautisha Hamza , Mkuu wa Majeshi na Himidu , spidi ya Himidu iliokuwa ndogo kuliko ya Hamza na Mkuu wa majeshi.
“Kaka huyu Hamza ni nani ? Imekuwaje Yonesi akakutana na mtu kama huyu na kuwa boyfriend wake?”Aliongea Stanley akimuuliza Danieli.
Mzee Daudi aliishia kuwaza kimya lakini kadri alivyokuwa akifikiria alishindwa kupata jijbu
“Haijalishi ni nani , lakini hawezi kuwa kitu kinachoelea”Aliongea kauli tata Mzee Mazengo na palepale alitoa ishara ya kutaka kusimama huku wengine akiwapa ishara ya kuendelea.
*****
Ni katika msitu wa kupanda katika eneo la jeshi la Tanzania , katikati ya msitu huo kulikuwa na uwanja maalumu , sehemu ambapo mara nyingi hutumika kwa ajili ya mafunzo ya kulenga shabaha kwa wanajeshi.
Eneo hilo kawaida huwa kuna ukimya mno na kutokana na kuwa asubuhi ukimywa wake ulikuwa mkubwa mno.
Muda huo alieanza kutua katika eneo hilo ni Afande Simba na kisha akafuatia Hamza alietua kama vile ni kimondo .
Wote wawili walionekana ni kama viumbe vya ajabu kwa namna walivyotumia spidi kufika katika eneo hilo.
Afande Simba aliishia kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa bila ya kuongea na kisha palepale alipiga hatua mbili mbele na kusimama mbali na Hamza kwa mita kama kumi na tano hivi.
“Ni jina gani rasmi nikuite , Selafi , Prince au Usifa?”Aliongea kwa sauti nzito.
“Potezea hayo majina , hakuna haja ya kuyakumbushia wewe niite tu Hamza Mzee”
“Lakini hayo ndio majina matatu yanayokutambulisha juu ya uhalisia wako na yale yote uliyoyafanya lakini ninachoona ni kama huyapendi kabisa”
“Zama ya Selafi ilikuwa ni ya upweke na mahuzuniko makuu , Zama ya Usifa ni ya majonzi na bidii , kuhusu Prince ni jina la wakati mchache uliopita linalonifanya kuchoka mwili na akili. Sioni maana yoyote juu ya majina hayo”
“Kijana mtazamo wako kuhusu maisha umekosa msingi wa matarajio . Hivi unajua ni watu wangapi wanatamani kuwa kama wewe ? Kuna watu wengi sana wanatamani kuwa juu, lakini katika kipindi cha miaka mia moja iliopita ni wewe tu ulieweza kufanya makubwa na kupata sifa ulizonazo”
“Kwangu mimi kuwa maarufu , utajiri na madaraka sio kitu kilichonileta kwenye sayari hii , sifa zangu ni matokeo ya kuutafuta uhuru na kuendelea kuishi kwa kushinda vikwazo”
“Kwahio wewe ni mwanaume usiependa umaarufu?”
“Nadhani hivyo! Halafu kwanini nahisi ni kama unaniwekea mtego wa maneno?”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu, walikuwa wameachana umbali kama vile wanaogopana na kufanya waongee kwa sauti kubwa kidogo.
“Haha.. sitaki kuingia katika ugomvi na mjukuu wa shetani , ninachotaka ni kukujua kidogo tu”
“Hakuna unachoweza kunielewa kuhusu mimi ,unaweza kunifahamu kwa hili dogo napenda uhuru na wanawake warembo , hivyo ni kheri tukienda moja kwa moja kwenye mazungumzo yetu. Umenifanyia fadhila awamu hii , vipi unataka nikulipe? Nataka pia nipate taarifa za kibailojia kutoka katika Earth Axis , unaweza kuweka masharti yako nione kama naweza yatimiza”Aliongea Hamza.
SEHEMU YA 135.
Mkuu wa majeshi mara baada ya kusikia kauli ile ya Hamza alijikuta akiaungua kicheko.
“Leo tutapotezea kuhusu fadhila ndongo niliokufanyia , isitoshe wewe ndio uliehusika kuzamisha manowari ya kijeshi ya America , jambo ambalo nasikia limeshusha morarali sana kwa wanajeshi wa kitengo cha Delta Zero kufeli kwao, kufanikiwa kwa majaribio kisiwani Chole na wafanyakazi kurudi salama salimini ni swala la kukushukuru kitaifa. Tupo tayari kukupatia tafiti zote za kibailojia zitakazotoka katika Earth Axis lakini unapaswa kulipia gharama”
“Unataka nifanye nini? Huwa sipendi sana kuzunguka zunguka”Aliongea Hamza na aliingiza mkono kwenye koti lake na kutoa sigara na kiberiti na kuiwasha, haikujulikana ameitoa wapi.
Lakini licha ya kuvuta sigara mbele yake , Mkuu huyo wa majeshi wala hakuonekana kujali kabisa.
“Baada ya kukaa chini na viongozi kadhaa wa juu katika serikali , walitoa mapendekezo mengi lakini tukakaa chini na kuyajadili na kupata mapendekezo machache na utachagua kati ya hayo”
“Oh! , inaonekana nina vitu kadhaa mmeviona kutoka kwangu na kuvitamani”Aliongea Hamza huku akitoa moshi wa sigara akimpa ishara mkuu wa majeshi kuendelea.
“Mosi tunaitaka Barham”Aliongea na kumfanya Hamza macho yake kusinyaa.
“Mmiliki wa Barham ni Asazi, haipo chini yangu”Aliongea na Mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa na kisha aliinua kidole chake juu.
“Pili tunahitaji Daffodil”
“Daffodil sio ya kwangu , ni ya Asmuntisi kama mnaihitaji ni mpaka niongee na Asmuntisi ila sina uhakika wa kuipata”aliongea na Mkuu wa Majeshi alitingisha kichwa na kisha akainua juu kidole cha tatu.
“Ombi letu la tatu ni kutupatia tafiti zote zinazohusiana na Ankh , nina taarifa kwamba kabla ya kifo cha Dokta Genesha ulikutana nae hapa nchini”Aliongea.
“Si nilishawaambia wale walionihoji kuhusu Ankh , inamaana taarifa hazijakufikiia? Kipindi kile niliongea na Himidu na kumwambia maswala yanayohusiana na Ankh yasitishwe juu yangu , lakini naona kaamua kuvunja ahadi yake”
“Umekosea kuhusu Mshauri mkuu , hata kama Mshauri mkuu asingeniambia chochote kuhusu Ankh unadhani mimi mkuu wa vitengo vyote ningeshindwa kujua ?”Aliongea huku akicheka.
Hamza alitingisha kichwa , ukweli ni kwamba hakujali sana , alijiambia hata kama alievujisha siri ni Himidu angemwelewa.
“Sio kwamba sipo tayari kutoa taarifa zote zinazohusiana na Ankh, sababu ni kwamba utafiti wake bado haujakamilika , kuna elementi muhimu zimekosekana na njia ya kuzipata ni kujua lugha ya kitabu chake kitu ambacho mpaka sasa sijaweza kutafsiri”Aliongea Hamza na kumfanya Simba Nyika kumwangalia Hamza kuona kama anadanganya au La na hatimae alitingisha kichwa kuonekana kukubali.
“Nimesikia Asazi na Asimuntisi wao ni kama Leviathan tu , wote wanakutii kwa kila unachowaambia , ili kukidhi masharti yetu , ongea nao na utupatie kati ya hivyo vitu viwili tulivyoomba, ukikamilisha tupo tayari kushirikiana na wewe juu ya tafiti zote za kibailojia zinazotokana na Earth Axis”
“Ngoja nirudie tena , ulichoomba ndio asili ya nguvu za jamaa zangu , wamezipata kwa juhudi kubwa sana , najua ni kweli nikiongea nao watanipatia lakini siwezi fanya hivyo”aliongea Hamza akiwa katika hali ya usiriasi mkubwa.
Afande Simba Nyika alifumba macho kwa sekunde kadhaa huku akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na alifungua macho na kumwangalia Hamza.
“Kama hayo maombi yameshindikana basi tupatie mtu”
“Nani mnamtaka?”
“Sally”
Sekunde ambayo alitaja hilo jina Hamza alipotea alipokuwa amesimama na ile anatokea alikuwa mbele ya Simba Nyika.
Hamza alikuwa na macho yaliojaa hasira kali mno na macho yake ni kama yalikuwa yakiungua na moto na palepale aliinua ngumi na kumpiga Simba nyika kumlenga kichwani.
Afande Simba hakuwa mzembe alishituka mapema kwani palepale alinua mikono yake juu na kukinga shambulizi lile
Bam!!
Shindo kubwa ilisikika . Hamza ngumi yake haikuweza kumfikia Afande Simba bali iligonga katika ‘Dhana’ ambayo ilifanana na ile mikanda wanayozawadiwa wacheza ndondi au mieleka.
Afande Simba alidhania ameweza kukinga shambulizi lile la Hamza lakini palepale alihisi wimbi kubwa la nishati likiongezeka kutoka nyuma yake kama vile ni sunami na kumvuta kwa nguvu, palepale alizidi kuongeza nguvu kuhimana na mvuto ule lakini alianza kusumbuka..
“Hii ni…”
Alijikuta akiwa katika mshituko mkubwa baada ya kuhisi ni kama vile anaishiwa nguvu na kutaka kudondoka chini wakati huo akisukumwa kurudi nyuma kwa kuteleza, lakini hata hivyo alikuwa vizuri, ili kuhimili mwili wake alitanguliza mguu mmoja mbele kwa namna ya kuukunja na mguu wa kushoto akaunyoosha kwenda nyuma na ukakita chini ya ardhi kama mtalimbo, staili hio ilikuwa ni ya Kung Fu maarufu kama Jin Dagger movement.
Mpaka anakuja kusimama chini alijikuta akiinua uso wake na kumwangalia Hamza na macho yake yalikuwa katika hali ya mshituko mkubwa.
Hamza alikuwa amebadilika na kuwa mtu mwingine kabisa mwili wake ulikuwa umetawaliwa na kivuli kama cha mnyama wa ajabu mwenye mabawa anaelea angani huku akiangalia kitoweo chini .
Mkuu wa majeshi alijikuta jasho likimtoka kwa wingi kwenye paji la uso wake , alijua fika kwamba kama Hamza akija kumshambulia tena anaweza shindwe kuhimili na kitu pekee ni kukimbia maana hakuna namna.
“Huyu kweli ni kiumbe hatari kama nilivyosikia”Alijikuta akiongea mwenyewe.
“Sally ni ndugu yangu wa damu , siwezi kuruhusu mtu yoyote yule kumgusa”Aliongea Hamza kwa sauti nzito sana huku mwili wake ukiwa umefunikwa na kivuli cha mnyama mkubwa kama Mwewe.
“Nilijua tu huwezi kukubali , isitoshe nilisikia sababu kubwa ya kugombana kwako na Mfalme Giza ni kwasababu ya Sally. Lakini kwasababu sharti hilo limekwama basi sina jinsi na kubadilisha , chukulia tu kama hujasikia nikitaja kuhusu hili”
“Ongea unataka nini kutoka kwangu”
“Unapaswa kufanya vitu vitatu kwa kitengo chetu cha Malibu , vitu hivyo vitatu tutakaa chini na kuamua.”
“Hapana , umeongea ki upana sana , kama nikikubali bila ya kujua ni vitu gani si sawa na kujiingiza kwenye mtego?”
“Nakuhakikishia ni masharti ambayo hayatazidi nilichoomba mwanzo”
“Hata kama ni hivyo lazima kuwe na ukomo”
“Taja ukomo wako nijue”,
“Masharti yenu hayapaswi kugusa familia yangu, Jamaa au marafiki , pia siwezi kufanya mambo ovu ya aina yoyote yanayokiuka asili ya ubinadamu”
“Kuna maswala mengine kuua ni swala ambalo halikwepeki! Vipi utaweza kufanya na hivyo?”
“Ili mradi anaekufa anastahili kufa hakuna shida”Aliongea Hamza.
“Nakuhakikishia Tanzania ni nchi inayoendeshwa katika misingi ya haki na hatuwezi kuomba kitu kinachokiuka asili ya binadamu”Aliongea Afande Simba na kumfanya Hamza kufikiri kidogo.
“Kama ni hivyo ni lini nitaweza kupata taarifa za Earth Axis?”
“Utaweza kupata taarifa zake baada ya kukamilisha kile tutakachokupangia”
“Nini! Inamaana hamjakaa na kuamua bado , nisubiri mpaka lini?”
“Usiwe na wasiwasi ndani ya miaka mitatu tutaweza kukupatia taarifa , unapaswa kujua Tanzania ni nchi ambayo inaanza kupiga hatua katika Teknolojia kuingia ulimwengu wa pili , mambo mengi yanafanyika kwa taratibu maalumu hivyo hatuwezi kuharakisha”
Hamza alifikiria kidogo na palepale aliona miaka mitatu sio mingi sana ni kama kufumba na kufumbua tu.
“Kama ni hivyo mniambie masharti yenu haraka sana niyafanyie kazi na nibakie kuwadai”Aliongea Hamza hakuhofia Mkuu huyo kumgeuka baadae , alijiambia akimdanganya basi cha moto atakipata .
“Nadhani mpaka hapo tumefikia makubaliano , nitaondoka na kuweka haya mbele ya mkuu wangu”Aliongea.
“Hakuna shida , mimi narudi nyumbani kwa Mzee Mazengo hivyo siwezi kukusindikiza tena”Aliongea Hamza akipanga mwakati maandalizi ya sherehe yakianza akazame chumbani kwa Yonesi na kujaribu bahati yake.
“Subiri kwanza”Aliongea Mkuu wa majeshi au Afande Simba Nyika.
“Kuna kitu kingine unataka kuongea Afande?”Aliuliza Hamza.
“Baba yako ndio alikuwa mzungu au ni mama yako?”Aluliza
“Sijafuatilia hivyo sijui”Aliongea Hamza akiwa amekunja sura.
“Oh! Kama ni hivyo basi chukulia kama sijauliza”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kukubali.
“Niagie kwa Himidu , mwambie sitoweza kuonana nae kwa leo , tutaongea ana kwa ana siku nyingine”Mara baada ya kuongea hivyo Hamza aliruka juu na palepale alifyatuliwa na kupotea.
Baada ya mkuu wa majeshi kutembea mita kama mianne hivi aliweza kukutana na Himidu ambae alikuwa akimsubiri kwa mbali.
Ili kuepuka kutoonekana na Hamza , Himidu hakusogea karibu.
“Umemaliza! Vipi amekubali ombi lipi?”Aliuliza Himidu akiwa na tabasamu.
“Ni kama ulivyotarajia , umekuwa sahihi pia amenipiga ngumi”Aliongea kwa wasiwasi.
“Haha.. umekula ngumi moja tu ? Siku za nyuma ilikuwa ukimtaja Sally atakupiga mpaka maji uyaite Mma”Aliongea huku akicheka sana na kumfanya Afande Simba kusikitika na tabasamu la uchungu.
“Halafu Bosi amevua mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi , vipi umemshindwa na wewe pia licha ya hivyo?”
“Una uhakika sio kama amejifunza upya ndani ya miaka yote? Nakumbuka hata wewe ulipoteza uwezo wako mwanzo?”
“Ni kweli ila bosi hajawahi kunidanganya , akisema amevua uwezo wake wa nishati basi jua ni kweli”Aliongea.
“Duh! Kweli nimeamini sio wa kawaida , nadhani ndani ya jeshi letu ni Nyakasura pekee anaeweza kupigana nae”Aliongea huku akishika kiuno.
Himidu mara baada ya kusikia jina la Nyakasura alitingisha kichwa kukubaliana nae lakini alionekana kukuna kichwa kama vile hana uhakika.
“Simba! Nimesikia Nyakasura amesema amechoka kukaa mpakani na anapanga kwenda Dar es salaam kwa siku kadhaa kupunga upepo wa baharini . Vipi unapanga kumpa kazi, maana nahisi ni kama safari yake ina mipango mingine”
“Amekuambia anataka kwenda Dar es salaam?”Aliuliza huku akionekana kusita kidogo kama mtu ambae hana taarifa hio.
“Ngoja nitamuuliza , sijampa kazi yoyote Dar”Aliongea.
*****
Hamza mara baada ya kurudi kwenye makazi ya familia ya Chifu Mazengo alitaka kwenda kujaribisha kupata kitumbua cha asubuhi na Yonesi lakini bahati mbaya mwanamke huyo alikuwa amekwisha kuondoka kwenda hospitalini.
Hamza hakushangaa sana kuwahi kwa Yonesi kwenda hospitalini , isitoshe ndio walikuwa wanawake pekee yeye na mama yake katika familia hio.
Muda ambao amerudi wafanyakazi walikuwa bize sana na wale ambao wanakuja asubuhi walikuwa washafika na kulikuwa na ubize mwingi wa kuandaa sherehe.
Hamza mara baada ya kupumzika kidogo na kujisafisha alikaribishwa kwenye ukumbi kwa ajili ya kifungua kinywa na wanafamilia wengine.
Baadhi ya wanafamilia hao walikuwa na soni kutokana na kumdharau mwanzo na kujikuta wakikosa amani , lakini Hamza hakuonekana kujali kabisa, alikula kama yupo nyumbani.
Baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa alimwomba Mzee Sauli gari na kisha akaanza safari ya kuelekea hospitalini.
Mara baada ya kufika wodini Mama yake Yonesi alikuwa amesharejewa na fahamu na ameamka usingizini na alikuwa akiongea na Yonesi.
Ijapokuwa alikuwa ameunganishwa na mavifaa yanayomsaidia , lakini alionekana kuwa sawa kabisa . alipaswa kupumzika kwa siku kadhaa mshono upone ndio arejee nyumbani.
“Mama vipi kidonda kinauma na unapumua vizuri?”Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu na mama huyo baada ya kumuona Hamza alikuwa na hisia mchanganyiko.
“Nimesikia wewe ndio daktari ulienifanyia upasuaji , Asante sana najisikia vizuri kwasasa”
“Ni kheri hali yako inaonekana kuwa nzuri kwasasa la sivyo Yonesi hatoweza kurudi Dar”Aliongea.
“Ijapokuwa umeniokoa kitu ambacho nashukuru lakini siwezi kukusamehe kwa kutaka kumfanya binti yangu mchepuko”
“Mama.. Mwili wako bado ni dhaifu haina haja ya kufikiria kuhusu hili”Aliongea Yonesi haraka.
“Mama usinielewe vibaya , kukufanyia upasuaji kuokoa afya yako haina maana kuna kitu nataka kutoka kwa Yonesi?”
“Oh, kama ni hivyo unataka nini?”
“Nimeyaokoa maisha yako kwasababu mimi ni daktari , nilivyokuona na dalili za kuumwa ni kawaida kama daktari kutaka kukutibu , hata kama mgonjwa ni adui yangu nitaanza kumtibu kwanza, ni maswala ya Medical Ethics na siwezi kuyaingiza na maswala yangu binafsi . Hivyo usije ukahisi kama nakudai “Aliongea na kumfanya mwanamama huyo kumwangalia Hamza kwa mshangao kidogo.
Yonesi pia alishangazwa na namna ambavyo Hamza alionekana kuwa siriasi na muungwana na alizidi kuona Hamza ana upande wa tofauti sana uliomfanya kuzidi kuvutiwa nae.
Hamza mara baada ya kuongea alichukua nafasi hio kuangalia vipimo vya mgonjwa kuona maendeleo yake na aligundua hakukuwa na tatizo kabisa hivyo aliondoka.
Muda mfupi baadae Dr Ivan Bridge alifika akiongozana na mtoto wake Christiani na Ivan alitumia fursa hio kuanza kumsifia Hamza na vilevile alimwambia Maria namna Hamza alivyoweza kumponyesha na Christiani.
Mama huyo mara baada ya kusikia kuhusu Christiani mpwa wake kutibiwa na Hamza alijikuta akiingia kwenye tafakari nzito.
*****
Sherehe ya kumpongeza Mzee Chalula Mazengo kwa kutimiza miaka tisini ilifana sana, watu wengi wenye ukaribu na familia hio walialikwa na kusherehekea pamoja.
Swala la mkuu wa Majeshi kufika na kuitembelea familia hio liliwafikia watu wengi na kufanya heshima ya familia hio izidi kukua
Mwanzoni familia hio haikuwa na mpango wa kumwandalia Hamza kiti cha kukaa , lakini walijikuta wakifanya hivyo na kutenga kiti cha mbele kabisa pamoja na Yonesi.
Baada ya sherehe kuisha Hamza aliaga kwa ajili ya kurudi Dar siku inayofuata.
Alikuwa na haraka ya kurudi kutokana na kwamba siku ya kesho kutwa yake Irene alimwalika kwa ajili ya kuhudhuria mashindano ya vipaji maalumu kwa mkoa wa Dar es salaam kwa shule zote na wale ambao wangeshinda wangeweza kupata ufadhili wa masomo nje ya nchi.
Juzi yake wakati Irene anamwomba Hamza hela ilikuwa ni kwa ajili ya kumchangia katika maandalizi ya siku hio.
Irene alikuwa na kipaji cha kuimba pamoja na kupiga kinanda na ndio upande ambao alipanga kwenda kushindania na kwasababu msichana huyo alisisitiza sana aliona haina haja ya kukataa, isitoshe msichana huyo kwa mara ya kwanza alionekana kuwa siriasi mno.
Upande wa Yonesi asingeweza kurudi Dar kutokana na hali ya mama yake ilivyo , hivyo Hamza siku iliofuata saa kumi za jioni alipanda treni kurudi Dar es Salaam.
Muda ambao alifika Dar ilikuwa ni usiku tayari na mara baada ya kumkumbuka Regina palepale aliona ni vyema akienda na zawadi ya kumbembeleza na kitu pekee amabcho aliona kinaweza kumlainisha mwanamke huyo ni boksi la Donati kutoka supermarket , kadi ya kuombea msamaha pamoja na ua zuri.
Licha ya kwamba ilikuwa usiku aliweza kupata kila alichopanga na kisha alianza safari ya kurdi.
Mpaka anafika nyumbani ilikuwa ni saa nne za usiku tayari na Shangazi alikuwa ashaenda kulala muda mrefu , lakini mwanga wa taa katika chumba cha Regina cha kujisomea zilikuwa zinawaka bado.
Hamza mara baada ya kuingia ndani alienda moja kwa moja mpaka katika chumba cha kujisomea cha Regina na kisha aligonga mlango lakini hakuna aliemwitikia kwa ndani.
Alirudia tena , lakini bado hakuitikiwa kwa ndani na alichofanya ni kutega sikio kusikilizia kwa ndani na aliweza kusikia sauti za mtu kuchapa kwa kutumia Keyboard ya tarakishi na alijua palepale atakuwa ni Regina amabe anaendelea kufanya kazi, hivyo alifungua mlango na kuingia.
“Wife , Vipi uko bize sana?”
Regina alikuwa amevalia sweta kama blauzi ya mikono mirefu yenye mkato wa V shingoni iliofanya vimanyonyo vyake kuchomoza kama miba, pamoja na namna alivyosiriasi alizidi kuonekana mrembo.
“Sijakuruhusu uingie”Aliongea huku akimwangalia Hamza bila hisia zozote
“Nimegonga sana mlango lakini hujafungua , labda ulikuwa bize ndio maana hujanisikia”
“Nimekusikia vizuri tu , ila sitaki kukuona, hebu toka nje”Aliongea kikauzu na kumfanya Hamza kujisikia vibaya , aliona kweli Regina alikuwa ni tafsiri halisi ya mwanamke Kauzu.
ITAENDELEA. watsapp 0687151346
Saa ngapi mkuuBadae
Tuwe na subra tuone mda sahihiSaa ngapi mkuu
Tunakusubiri mkuuAsante mkuu
Mkuuu tunakusubiria.Asante mkuu