Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Mtu wangu wa karibu kaenda kijijini kwao kusalimia[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
[emoji16]
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SITINI NA MOJA
SONGA NAYO................


Mzee huyo alikuwa anaongea wakati huo akiwa anajinyoosha, alikuwa amefunguliwa tayari na kuruhusiwa aweze kuondoka. Dayana alikuwa amefanya makosa makubwa kwa sababu kosa la kwanza ni lile la kumteka lakini lile wangelimaliza ila kumtesa mtu ambaye umemteka bila ridhaa yake tena mtu tajiri kama yule ilikuwa ni kesi nyingine kama ingefika kwenye mamlaka za juu ukizingatia mtu huyo alikuwa ana watu kila pande ya nchi.
Mzee huyo alitoka ndani ya hiyo sehemu ambayo alikuja kugundua kwamba lilikuwa kontena ambalo lilitengenezwa kwa usahihi ndani ila kwa nje usingeweza kulidhania kabisa maana lilikuwa limechakaa. Dayana alibaki amekaa kwenye meza akiwa haamini mambo ambayo aliyasikia, mzee huyo alikuwa na roho ngumu mno kumuingiza mwanae kwenye ile hatari kubwa kiasi kwamba ikaenda na maisha yake.
“Umefanya jambo la hatari sana kumtesa vile, likifahamika tutakuwa kwenye hatari kubwa mno”
“Huyu mtu asingeweza kusema bila kumfanyia vile”
“Inawezekana kweli lakini njia ambayo tumeitumia sio sawa halafu tumemuacha aende mwenyewe vipi kama akipata tatizo njiani?”
“Nimemuwekea kifaa kwenye nguo yake hivyo tutajua kila anako kwenda. Hii ilikuwa ni njia pekee ya kuweza kujua haya mambo huenda bila kutumia nguvu huenda tusingeweza kuyafahamu. Nadhani mmeshajua kwamba mtu ambaye tunatakiwa kumtupia jicho kwa umakini zaidi muda huu ni mkuu wa majeshi. Ni mtu mwenye ujivuni sana bwana yule, huwa anajihisi yeye ndiye kila kitu kwenye hili taifa hali ambayo itahatarisha zaidi maisha yake”
“Unamaanisha unataka sisi tukamlinde mkuu wa majeshi?”
“Hapana”
“Ila?”
“Tunatakiwa kufuatilia kila hatua ambayo anaipiga, itakuwa ni rahisi kama Gavin anaenda kwake sisi kujua hivyo tutadili nao wote wawili. Sijali kuhusu kufa kwake lakini hatuwezi kuruhusu huyu mtu kama ni kweli afe wakati huu kwa sababu tayari taifa lipo kwenye wakati mgumu na msiba wa first lady”
“Unajua kabisa ni hatari kumfuatilia mkuu wa majeshi, tukikamatwa kwenye hili ni kifo kinatuangalia”
“Na wakati huu wa msiba ndio ambao Gavin anaweza kutekeleza mambo yake kirahisi kwa sababu anajua kutakuwa na mikusanyiko ya watu wengi”
“Upo sahihi, huu unaweza kuwa wakati ambao utakuja na mambo mengi mabaya zaidi kwa sababu atahitaji kuutumia kwa ajili ya kutekeleza mambo yake kwani itakuwa ni rahisi zaidi. Tunatakiwa kukutana na mkuu wa majeshi haraka”
“Kukutana naye tena?”
“Ndiyo. Bila hivyo itakuwa ngumu, inatakiwa awe na hizi taarifa mapema”
“Kama ni mtu wa kukutana naye ni bosi hivyo tunatakiwa kukutana na bosi saivi kwa sababu mpaka hapa tunahitaji msaada wake”
“Tangu aondoke jana sikumpata tena”
“Simu yake usiku ilionekana kwamba alikuwa Ikulu, huenda kuna mambo ya siri ambayo alikuwa anayafuatilia”
“Amemtafuta hata mmoja wetu?”
“Hapana”
“Dayana, unatakiwa kwenda kwake ukutane naye, hili jambo ni mhimu mno”
“Kila mtu akaifanye kazi yake kwa usahihi ili tunapokutana tena tuwe na jibu moja la namna ya kumtia Gavin Luca kwenye mikono yetu”
“Roger that” maongezi yao yaliishia hapo ambapo kila mtu alitawanyika na kushika njia yake kwenda kutekeleza majukumu ambayo yalikuwa mbele yake.



THE IMMORTALS
Lilikuwa ni kundi la watu ambao wao walijitanabaisha kwamba hawafi, hiyo ndiyo maana halisi ya hilo neno la kiingereza. Hawakuwahi wao wenyewe kutokea hadharani kujielezea kwamba ni kwanini walikuwa wanalitumia jina hilo kuwa utambulisho wao.
Watu hao hawakuwa wakijulikana kabisa kwamba makao yao yalikuwa wapi, haikujulikana kwamba kiongozi wao alikuwa nani na sababu ya msingi ya kuanzishwa kwake ilikuwa ni ipi, huenda ni watu wa kuhesabika tu ndio ambao walikuwa wanajua uhalali na uwepo wa hilo kundi.
Ni kundi ambalo liliaminika kuwa hatari kulingana na namna lilivyokuwa limewekeza kwa upande wa nguvu na kuwa na watu wengi ambao walikuwa nyuma yake, lilidaiwa kumiliki watu wakubwa, kumiliki viongozi wakubwa lakini pia lilikuwa lina nguvu kubwa na lisilo na mipaka. Kundi hilo lingefanya lolote na wakati wowote ule na mahali popote pale lakini lilianza kuingiwa na mashaka na wasiwasi mkubwa baada ya ujio wa mtu ambaye alionekana kuwa hatari kwao kwa wakati huo.
Ujio wa maisha mengine ya Gavin Luca ilionyesha uhatari wa wazi wa uwepo wa kundi hilo, halikuwa na amani tena wala watu wake wa ndani hawakuwa na amani ya kutosha hususani baada ya uelewa juu ya kwamba watu wao walikuwa wakifa kila wakati. Kifo cha Zara ambaye alikuwa mtoto wa mwanachama mwenzao, kufa kwa waziri wa mambo ya ndani, kufa kwa makamu wa raisi wa zamani, kufa kwa Douglas Shenzi pamoja na yale ambayo yalitokea ndani ya msitu wa Mau. Ilikuwa ishara mbaya juu ya uvamizi ndani ya huo umoja wao.

Hapakuwa pema sana, kuna mambo yaliendelea ndani ya nchi ambayo yalimshtua mpaka raisi mwenyewe, hakuwa na uwezo wa kupambana na hali ambayo ilikuwa inaendelea kwa upande wake. Usiku alipokea ugeni wa mkurugenzi kwenye ofisi yake, mazungumzo yao yaliishia pabaya ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya afunge safari kwenda kuomba msaada kwa kiongozi wa umoja huo, kiongozi mkuu wa hao watu ndiye ambaye raisi George alihitaji kwenda kupata msaada kwake, hakuona mtu mwingine ambaye alikuwa anaweza kumsaidia kwa jambo hilo zaidi ya huyo bwana.

Alisafiri mpaka ilipo bandari kuu, aliingia kwenye boti akiwa na walinzi wake wa kutosha. Baada ya kusafiri kwa muda ndani ya boti alikutana na meli ambayo kwa juu yake kulikuwa na helikopita, alitakiwa kuipanda kwa ajili ya kueleka huko ambako yeye alikuwa anakutaka. Alifungwa macho wakati anaingia ndani ya helikopter, hakuwahi hata siku moja kukutana na huyo kiongozi wake wala hakuwahi kabisa kumfahamu kwamba mtu huyo alikuwa ni nani. Mara zote kwenye mikutano walikuwa wanamsikia mtu huyo kwenye kipaza tu, huenda ilikuwa inaenda kuwa mara yake ya kwanza kabis akuweza kukutana na bwana huyo.

Safari yao ilienda kwa muda mrefu ambapo hakuelewa kama walikuwa wanaenda ni mbali sana au alikuwa anazungushwa kwenye eneo husika ili asiweze kujua kwamba walienda wapi na ni muda gani waliutumia, hesabu za hivyo zinaweza kumsaidia mtu kujua mahali ambapo alikuwepo hususani kwa watu wenye hesabu zao kali wanapokuwa wanalifanya jambo fulani.
Baada ya muda wa takribani masaa kadhaa helikopita hiyo ilisimama, alishushwa akiwa bado kwenye kitambaa usoni, eneo ambalo alkuwa anapitishwa bila shaka alikuwa anahisi kama ni kwenye pori japo hakuwa na uhakika kabisa na hayo mawazo yake ila lilionekana kuwa na upepo safi mpaka pale alipo anza kuhisi hali ya joto ni baada ya lango kusikika likifungwa. Hapo alifunguliwa sasa, hakuelewa ni wapi alikuwepo, pango sio pango, godauni sio godauni ila aligundua kwamba yupo chini ya ardhi kutokana na namna jengo hilo lilivyo dizainiwa.
Kulikuwa na walinzi wa kutosha ndani ya eneo hilo, kila hatua kadhaa ungekutana na watu wa walinzi wa kutosha. Alifika eneo ambalo lilikuwa na ukubwa, kuna watu walikuwa wanafanya ibada za ajabu wakiwa na mavazi ya kininja na baada ya kufika kwake walipotea. Kuna wengine walikuwa wanaifanyia ibada miili ya watu kadhaa ambao walionekana kuuawa wakiwa bado hai. Alianza kuogopa mheshimiwa raisi ila hayakuwa yakimhusu yale, alitakiwa kudili na yale ambayo yalimfanya yeye kuwepo hilo eneo wakati huo.
Alipelekwa mpaka ndani ya chumba kimoja kikubwa ambacho kilitengenezwa kwa ubora mkubwa mno, kilikuwa kimenakishiwa kwa dhahabu tupu. Alibakishwa hapo na kuambiwa amsubiri mtu amabaye alimjia. Hakuwa na wazo lolote kama alikuwa ni wapi eneo hilo, kwahiyo kama jambo lolote lingetokea huko ulimwengu usingekuwa na taarifa yake yoyote ile, ikawa ishara ya kuwa makini na matumizi ya lugha huku akiwa hajui ni mtu wa namna gani alikuwa anaenda kukutana naye.

61 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SITINI NA MBILI
SONGA NAYO................


Zilisikika hatua za watu zikiwa zinakuja kwa mbali, aligeuka kuangalia hatua hizo lakini hakuziona, alihisi kama anaota mpaka pale alipogeuka tena alitaka kukimbia. Aliwaona watu watatu wakiwa mbele yake, hakuelewa watu hao walifikaje kwani hakuzisikia kabisa hatua zao wakiwa wanakaribia hilo eneo, ule mshtuko ulimfanya adondokee nyuma hatua kadhaa akiwa anahema kwa nuvu na jasho likimtoka mfululizo mwilini.
Mshtuko haukuwa tu kwa sababu ya kuwaona watu mbele yake ila ni mtu ambaye alimuona, bado alihisi hakuwa hai, huenda alikuwa amefika kuzimu ila sio kweli! Alikuwa na uhakika kabisa kwamba alikuwa hai, sasa jambo hilo liliwezekana vipi? Ni mtu alikuwa anaichezea akili yake? Akakumbuka kwamba yeye ni raisi mtu hawezi kucheza na hiyo akili yake kirahisi namna hiyo hivyo kwa namna yoyote ile kile ambacho alikuwa anakiona mbele yake haikuwa ndoto bali ulikuwa ni uhalisia.

Natron Vinza ndiye mtu aliye muona mbele yake, huyu alikuwa ni raisi wa Tanzania miaka ya zamani sana, huyu ndiye ambaye alipigishwa magoti na Lucas muuzaji wa madawa ya kulevya ili aweze kukubali kulisaidia taifa, huyu ndiye yule ambaye alipewa amri ya kujiuzulu ili taifa lisaidiwe na akafanya hivyo. Huyu ndiye yule bwana ambaye alidhalilishwa mno na muuza madawa ya kulevya yule baada ya kuhitaji robo ya utajiri wa bwana yule.
Ni miaka mingi iliyopita kila mtu alijua kwamba bwana huyo alikufa lakini haikuwa kweli, bwana huyo kakufa kama ambavyo dunia na Watanzania waliamini. Mtu ambaye alikuwa na njaa ya mafanikio kama yeye asingeweza kuyaondoa maisha yake kijinga eti kwa sababu tu ya kumhofia muuza madawa ya kulevya, hakuwa amefikia hatua ya ujinga wa kipuuzi namna hiyo ila yeye ndiye ambaye aliuhadaa ulimwengu ukaamini kupitia mtego wake aliokuwa ameuweka.
Aliiaminisha dunia kwamba amekufa na kweli dunia ikaamini hivyo, aliufanya ulimwengu uamini kwamba historia yake ilikuwa imezikwa kwa miaka mingi sana ila haikuwa kweli, bwana huyo alikuwa mzima tena yu buheri wa afya kabisa kuliko hata alivyokuwa miaka ya huko nyuma. Mwili wake haukuonekana umekaa kihasara kama alivyokuwa anashinda kula bata kipindi yupo Ikulu, mwili wake ulikuwa umekomaa mno, mwili ambao ulionekana kuwa na nguvu zisizo za kawaida akiwa ndani ya kanzu safi nyeupe ambayo ilimkaa vizuri.
Sasa bwana huyo alikuwa ni nani hasa kwenye hiyo dunia mpaka raisi wa nchi ajikute anaingia kwenye mikono yake na kuuhitaji msaada wake kwa ukubwa namna hiyo? Pembeni yake alikuwa amezungukwa na maninja wawili ambao walikuwa makini kwenye kila hatua yake ambayo alikuwa anaipiga. Alikuwa analindwa mno bwana huyo.
Huyo ndiye alikuwa mwanzilishi na kiongozi mkuu wa hilo kundi la THE IMMORTALS, huyo ndiye alikuwa msingi wa hilo kundi na ndiye ambaye alikuwa na kauli ya mwisho juu ya kila kitu. Mtu huyo alikuwa anaishi nyuma ya pazia kiasi kwamba watu wake hawakuwahi kujua wanamtumikia nani lakini raisi siku hiyo aliipata hiyo bahati.

Alikuwa ana wasiwasi isivyokuwa kawaida, alikuwa mtu wa mashaka mno akiwa bado anahisi yupo ndotoni. Kiongozi wa zamani ambaye binafsi alihisi alishakufa mpaka watu walishamsahau alikuwa hai bado. Kwanini yeye? Aliogopa sana.
“Mheshimiwa?”
“Naona umeshtuka sana kuniona nipo hai George” alimeza mate akiwa anaogopa hata kujibu baada ya kuisikia ile sauti ya kukwaruza isiyokuwa na utani ndani yake.
“Mheshimiwa ulikufa na nilihudhuria mazishi yako, sasa inakuwaje upo huku na upo mzima wa afya kabisa?”
“Una uhakika mimi nilikufa?”
“Ndiyo, niliona na mwili wako”
“Wewe ni raisi George, unaamini kuna jambo haliwezekani hapa duniani?”
“Hapana kiongozi”
“Nyanyuka ukae kwenye kiti kwa sababu mimi na wewe leo tunaenda kuwa na mazungumzo marefu kidogo”
“Asante kiongozi” alinyanyuka na kwenda kukaa kwenye kiti cha dhahabu ambacho hakikuwa mbali na pale ambapo alikuwa amedondokea.
“Mimi sikufa wala sijawahi kufa George”
“Sasa aliyekufa alikuwa nani?”
“Alikuwa kijana wangu ambaye alikubali kuifanya kazi ile ili familia yake iishi maisha mazuri”
“Ambayo uliwapa?”
“Huwa siishi nje ya ahadi yangu, yeye alikufa lakini familia yake imeishi maisha mazuri mpaka leo”
“Naheshimu hilo lakini sikutegemea kama ni wewe ndiye ambaye ningekukuta hapa”
“Ulitegemea kukutana na nani?”
“Sijajua lakini haukuwa akilini kabisa”
“Unakumbuka zamani nikiwa raisi?”
“Ndiyo kiongozi”
“Ni jambo gani ambalo lilikuwa linaongelewa sana mtaani kuhusu mimi?”
“Kwamba ulipenda sana starehe”
“Kitu ambacho ni sahihi hata wewe uliamini kwamba ni kweli si ndiyo?”
“Ndiyo kiongozi”
“Lakini unajua kwanini kuna baadhi ya watu wanapenda starehe?”
“Hapana kiongozi”
“Kuna vitu vingi vinafanya baadhi ya watu wanafanya hayo mambo lakini kuna mambo makuu ambayo ndiyo hupelekea yote hayo. Jambo la kwanza ni kupata vikubwa ambavyo nafsi yako inaamini kwamba haukustahili, huwa inambadilisha mtu moja kwa moja na kumfanya kuwa wa hovyo huku yeye akiona kwamba ni fahari kufanya hayo. Jambo la pili ni kukosa mambo ya mhimu ya kufanya, mimi nilikuwa nagawa majukumu tu kwa watu wengine ila sikuwahi kuhitaji niyatimize mwenyewe, kugawa majukumu yote kwa watu wengine wa chini yangu kulinifanya muda mwingi nisiwe na la kufanya
Siku zote ukiwa hauna la kufanya hata akili haiwezi kutulia na kupambana na mambo ya maana, hapo ndipo akili huwa inaanza kuwaza mambo mazuri kama wanawake warembo, kufika sehemu nzuri za gharama na za kupendeza duniani, unajikuta haujali tena kama wewe ni raisi wa kuwaongoza raia wako. Hilo ndilo ambalo mimi nililifanya na nina uhakika hata wewe unafanya hivyo, sijawahi kukuingilia kwa sababu najua unakilinda ambacho kilikufanya uwe hapo
Lakini bwana George hayo yote huwa yanabadilika pale tu ambapo unakuwa na sababu ya msingi ya kukufanya uwe na jambo la kuwaza. Mimi niliachana na hayo mambo baada ya kufanya maamuzi magumu ya kufa kwa watu, yaani dunia ilitakiwa kuamini kwamba mimi sijawahi kuishi tena baada ya maisha yake, lakini unaijua sababu ya msingi?
Sababu ilikuwa ni watu, mimi kama raisi nilidhalilishwa mno, kama raisi nilionekana toi la kuchezea na baada ya siku ile hakuna mtu ambaye angeniheshimu tena, wote wangekuwa wananicheka kila ninapopita ndiyo maana niliamua kupotea kabisa kwenye nyuso za watu ili nije kuishi sehemu ambayo sitakuwa na mtu wa kumuogopa
Hata vijana siku hizi wanashindwa kupata mafanikio kwa sababu ya kushindwa kuielewa hii formula. Ukitaka kufanya mambo makubwa kwa amani bila presha, nenda eneo ambalo wale watu wanao yajua madhaifu yako hawawezi kukuona. Hautakuwa na mtu wa kumuogopa tena, utayafanya mambo yako kwa amani na uhakika kwa sababu huna jambo la kupoteza ila kuendelea kupambana sehemu ambayo watu wanayajua zaidi madhaifu yako?
Hiyo inakuwa ni hatari kwako kwa sababu asilimia kubwa utafeli tu na asilimia za kufaulu ni ndogo mno George
Mimi niliamua kuja kuishi huku kwa sababu ya yule mtu ambaye ndiye aliifanya heshima yangu kupotea kabisa. Niliishi na kisasi kizito kwenye moyo wangu kwa miaka mingi nikiamini kwamba ingefika siku ningekuja kulipa, nadhani unayakumbuka maisha ya zama zile George”
62 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SITINI NA TATU
SONGA NAYO................

“Ndiyo kiongozi”
“Unahisi ungekuwa wewe ungefanya nini?”
“Huenda ningeihama nchi kwa sababu nisingeweza kuivumilia ile presha”
“Hahaha hahaha George siku zote adui yako akikufanya ufanye kila ambacho anataka yeye halafu ukamkimbia unakuwa haujashinda bali unakuwa ni mpuuzi ambaye umemuogopa na kumtukuza, yule kusikia nimekufa alijinadi kwamba mimi namuogopa yeye sana, alijiona mshindi lakini kupata yale majivuno ndio ulikuwa mwanzo wake wa kuubusu mchanga”
“Kwahiyo sababu ya kuanzisha haya yote ilikuwa tu ni kulipa kisasi kwa kuiteketeza ile familia?”
“Hapana George”
“Sijakuelewa mheshimiwa”
“Huwezi kunielewa kirahisi kwa sababu haukupitia hali ambayo niliipitia mimi. Lengo langu lilikuwa ni kuiua ile familia yote kisha niupate ule utajiri kwenye mikono yangu na baada ya hapo ndipo ningeweza kujitokeza hadharani na kuutangazia ulimwengu kwamba mimi sikufa, kila mtu angejua kwamba mimi nipo hai baada ya kuwa mtu mwenye pesa zaidi ndani ya bara zima la Afrika, ningekamilisha mpango wangu wa kuwa mtu mwenye nguvu kubwa zaidi lakini kwa bahati mbaya sana mpaka muda huu bado sijafanikiwa kuzipata hizo pesa kwenye mkono wangu ndiyo maana sijajitokeza kwenye maisha yenu ya kawaida ya kuwaongoza wapuuzi wa huko nje ambayo huwa hawaelewi lolote juu na namna taifa lao linavyokwenda zaidi ya kupiga makelele kwenye mitandao tu
Hizo ndizo sababu ambazo zilinifanya nikae chini na kuanzisha kundi hili la THE IMMORTALS watu ambao niliamini kwamba hawawezi kufa ama hawafi mpaka siku nikifanikisha kile ambacho ninakita
Ukiwa na maana kwamba pesa zipo kwenye mkono wa Gavin Luca ambaye kwa miaka yote tulijidanganya kwamba amekufa?
“Haupo hapa kuhitaji kunihoji Goerge kwa sababu naweza kuyabeba maisha yako kama hautakuwa na umuhimu wa kutetea kilicho kufanya ukaja hapa. Msaada gani ambao unahitaji mimi nikusaidie?” George swali alilisikia vizuri ila maelezo ya mwanzo pia yalimtisha, alijikohoza na kuvuta pumzi ili kumshawishi bwana huyo kuweza kumsikiliza na kumpa msaada aliokuwa anautaka.


“Naomba unisaidie kumpata waziri mkuu wako wa zamani”
“Hassan Gambo?”
“Ndiyo”
“Huyo mtu ni mfu kwa sasa”
“Hapana kiongozi”
“Unataka kusemaje?”
“Inaonekana naye alipitia njia kama zako kwa sababu yupo hai”
“Mhhhhh kivipi awe hai na nisiwe na hizi taarifa?”
“Hizi taarifa ni mpya kwa kila mtu kiongozi”
“Wewe umezipatia wapi?”
“Kwa rafiki yake wa zamani ambaye ndiye mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi kwa sasa”
“Kwamba yeye alijua kuwa huyu mtu yupo hai tangu muda mrefu?”
“Hapana kiongozi, mtu huyu alimtafuta kukutana naye na ndiye ambaye amemwambia mambo mengi sana kuhusu sisi, mambo haya ni hatari sana kwetu ndiyo maana nahitaji nimpate kwa namna yoyote ile”
“Ni hatari kwako au kwetu?”
“Kama ni hatari kwangu maana yake ni hatari mpaka kwangu pia”
“Kuna kitu gani kingine?”
“Kwa sababu ndiye babu yake na Gavin”
“Umesema?”
“Huyu bwana mdogo ambaye tunamtafuta yule waziri mkuu wakati wewe ukiwa raisi ndiye babu yake kabisa”
“Bado sijakuelea unamaanisha nini!”
“Kama kumbukumbu zako zitakuwa sawa ni kwamba bwana yule alikuwa na mtoto wa kike Glady, lakini mtoto yule baadae akiwa mtu mzima alipotea ghafla kwenye macho ya watu sijajua kama alikupa wewe sababu gani kama uliwahi kumuuliza ila ukweli ni kwamba yule binti yake alikuja kuolewa na yule muuaza madawa ya kulevya ambaye alikufanyia yale yote na ndiye alizaa wale watoto”
“Hahahah hahaha haha imenishangaza mimi kutokuwa na hizi habari kwa miaka yote hii? Hassan yupo hai? Natakiwa kumpongeza kwa hili kuweza kujificha kiasi kwamba sijui lolote kuanzia wakati ule nikiwa raisi mpaka sasa. Haya yote yaliwezekana vipi mbona kama kuna nukta inapelea hapa?”
“Sijajua bado ndiyo maana nipo hapa nikihitaji msaada wako kwa sababu naona mwisho unaenda kuwa mbaya”
“Hilo umelijuaje?”
“Mkurugenzi ameniuliza kama nahusika kwenye haya mambo ili aweze kunilinda kwa sababu amedai kwamba Gavin muda wowote kuanzia sasa anaweza kunifikia na haya mambo yakienda kwa wananchi inaweza kuwa hatari kubwa kwangu”
“Nadhani ni wakati sahihi wa huyo mkurugenzi kuweza kufa au kukubali kufanya kazi kwa kukusikiliza kila ambacho unakitaka wewe. Kama kweli Hassan yupo hai basi ni muda mwafaka wa mimi kujitokeza hadharani ili nikaushangaze ulimwengu, bila shaka ni wakati ambao hawajajiandaa kunipokea kwa mara nyingine, naenda kuutangaza ufalme wangu rasmi kwenye taifa hili”
“Sawa kiongozi, lakini kuna jambo lingine”
“Ongea haraka kwa sababu muda wako unakaribia kuisha”
“Mke wangu ameuawa”
“Najua na pole kwa hilo”
“Nataka kumjua aliye husika”
“Una uhakika unataka kumjua aliye husika?”
“Ndiyo”
“Nenda kaongee na Medrick Savato, anajua kila jambo ambalo lilitokea”
“Hapana kiongozi Savato nilikuwa naye hivyo hajui lolote”
“Una uhakika na hilo?”
“Ndiyo”
“Basi sina kitu ambacho naweza kukusaidia kwa sasa. Unajua George mimi sijisikii vibaya kwa mke wako kufa kwa sababu huenda alistahili kufa ila jambo moja ambalo linanishangaza kwako ni kwamba nimekupa nguvu zote ndani ya hili taifa ila umeshindwa kuzitumia, kumbuka ni siku kadhaa tu zijazo utatakiwa kuniachia Ikulu niiongoze mwenyewe kama imekushinda. Umekuwa miongoni mwa maraisi wadhaifu kwenye historia ya hili taifa, najua huna akili hizo lakini angalau ungezungukwa na watu wenye akili nyingi wangekusaidia kufika mbali ila kwa sababu ya ujinga wako watu wenye akili karibia wote umewaua umebakia na wapuuzi tu ambao wanaunga mkono kila jambo ambalo unalifanya ili wakufurahishe. Kwenye maisha kuna wakati unawahitaji watu ambao ni imara na wapo tayari kwenda tofauti na wewe pale ambapo wanahitaji kuona unafanya jambo ambalo ni sahihi. Unaweza kwenda”
Mtaalamu huyo wa zamani ambaye ndiye alikuwa kiongozi mkuu wa kundi hilo la hatari la THE IMMORTALS, alimtaka raisi aondoke kutekeleza ambayo yalikuwa kwenye uwezo wake hayo mengine alikuwa ameyapokea na angedili nayo kwa mkono wake mwenyewe. Alizipokea habari hizo kwa hali ya ukawaida lakini kiuhalisia ndani yake hakuwa wa kawaida, jambo hilo lilimpa hofu na mashaka makubwa.

63 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SITINI NA NNE
SONGA NAYO................


Alikuwa anaweza kuzipata taarifa nyingi hususani za zamani sasa hakuelewa hiyo familia iliwezaje kumhadaa na kuudanganya ukweli huku akijua ni yeye pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kuudahaa ulimwengu. Mr Hassan alikuwa waziri mkuu wake ambaye ni yeye mwenyewe alimteua akiwa madarakani kuwa mratibu mkuu wa serikali, sasa ilitokeaje mpaka mtu huyo akaweza kudanganya mpaka mwanae kuolewa na muuza madawa ya kulevya? Kulikuwa na makubaliano yapi hasa mpaka afanye jambo la hatari kama hilo? Kichwa kilianza kuwaka moto akiwa anahisi jambo hilo analiota.

Kuna picha ilianza kumjia kwa kasi na kuanza kuamini kwamba huenda ndiyo sababu ilimfanya kuzikosa zile pesa licha ya miaka mingi kupita. Kama ndivyo hivyo maana yake pesa zilikuwepo na zilikuwa kwenye usimamizi wa watu fulani akiwepo huyo kijana wake wa zamani, angefanikiwa kumpata huyo basi huenda kila kitu kingeenda kwenye njia kama ambavyo alikuwa anataka. Huyo ndiye angemsaidia pia kumpata hata Gavin Luca ambaye alikuwa anawaletea mkanganyiko kwa sababu ni mtu ambaye alidaiwa kufa mara mbili yote lakini bado alidaiwa kuendelea kuonekana.
“Hivi unaamini kwamba kweli huyu bwana mdogo yupo hai au alikufa lakini Hassan akamtengeneza mtu mwingine kuichukua nafasi yake?” aliuliza hilo swali kwa kijana wake wa karibu ambaye alikuwa amejaza sana kwenye mwili wake, huyo alikuwa amevaa suti alikuwa ni tofauti na wale maninja wa mwanzo.
“Yule ni yeye mwenyewe bosi” Kijana huyo alijibu akionekana kutokuwa na mashaka na jibu lake.
“Kwanini una uhakika na hilo jambo?”
“Kwa sababu kuna taarifa mbaya kidogo kutoka china”
“Ambazo ni?”
“Kipindi kile tumeenda china kwa ajili yale mafunzo ya kuongezewa nguvu mwilini, bila shaka unakumbuka kwamba baada ya kukamilika ulihitaji upewe nguvu za ziada za kukufanya usigusike na mtu yeyote yule”
“Ndiyo na nakumbuka sikufanikiwa kuzipata”
“Sahihi kabisa, sasa yule mwalimu ambaye aligoma kukupatia zile nguvu ambazo ziliaminika kwamba zilihifadhiwa kwenye ule upanga amekufa”
“Kwahiyo hilo linahusikaje na sisi?”
“Ni kwamba kabla ya kufa zile nguvu na ule upanga aliziingiza kwa mtu ili azitunze”
“Bila shaka aliwapa moja ya vijana wake”
“Hapana”
“Unataka kusemaje?”
“Haijulikani alimpatia nani lakini inasemekana kwamba kuna mtu mmoja mtanzania ambaye alikabidhiwa hizo nguvu kwa siri”
“Wote tunajua kwamba hawawezi kuzitoa zile nguvu kwenye himaya yao hivyo hilo ni jambo ambalo haliwezi kuwa la kweli”
“Nasikitika kusema kwamba ni kweli, kwa sababu hizi taarifa nimezipata kwa watu wa ndani sana kutoka china”
“Na unahisi kwamba Gavin kama yupo hai ndiye alipewa hizi nguvu?”
“Ndiyo kiongozi”
“Why?”
“Mpaka sasa sina majibu kuhusu hilo, kama amepewa zile nguvu maana yake hata ule upanga wao wa urithi atakuwa nao mwenyewe”
“Tukisema anazo, kwamba alifundishwa namna ya kuzitumia?”
“Hilo ni gumu kwa sababu kwa mujibu wake ni kwamba huwa wanafundishwa kuzimudu vizuri tu ila huwa hawafundishwi namna ya kuzitumia sana kwa sababu ni za hatari na huenda kama anazo maana yake anaweza kuwa na nguvu kubwa za asili kuliko zako hapa ndipo hatari kubwa ilipo”
“Hakuna mtu anaweza kuwa na nguvu kubwa kunishinda mimi, hayupo. Imetumika miaka mingi mimi kuwa hapa”
“Maana yake inatakiwa tuupate ule upanga haraka iwezekanavyo kama ni kweli upo Tanzania kwa sababu ule upanga ndio ambao una uwezo wa kumtuliza mtu yeyote ambaye aliingiziwa hizo nguvu kwenye mwili wake”
“Ina maana inatakiwa nimpate mmoja wapo kati ya Gavin Luca mwenyewe au Hassan!”
“Ndiyo kiongozi”
“Mpigie simu Davoc Mavambo, mpe maagizo ya kulitekeleza hilo haraka”
“Sawa kiongozi”

Ilikuwa ni mara ya kwanza anajidhihirisha kwamba yeye ndiye alikuwa nyuma ya mambo yote hayo lakini pia wakati anafanya hayo yote ilionekana mambo yanamuendea vibaya upande wake. Mwanaume huyo mtu mzima hakuonekana kuwa wa kawaida kwa sababu hata yeye alidaiwa kwamba aliwahi kwenda huko kwa wachina kuweza kuzipata nguvu hizo za siri na huo upanga ambao ulidaiwa kuwa unatafutwa kwa nguvu kubwa.


***********
Double E, jina lake halisi Ethan Ezra au Ezra ethani alikuwa ni afisa wa polisi kutoka kituo cha polisi cha Osterbay. Tangu kuibuka kwa kesi kubwa ya mauaji ya waziri wa mambo ya ndani ya Tanzania, hakuridhika na uamuzi wa kesi hiyo kutoka kwenye mikono yake kwenda kwenye mikono ya watu wa usalama, moyoni hakuridhika kabisa na jambo hilo.
Watu hao hawakuishia hapo tu bali kesi zote ambazo zilifuata waliwataka wao kukaa kando kwani waliamini kuwa ni wao pekee ndio walikuwa na uwezo wa kudili na hizo kesi. Kwake aliona alikuwa na jukumu la kushughulika na kesi za namna hiyo hata kama wakubwa hawakuwa wakihitaji yeye adili nazo hivyo hakuwa tayari kuweza kuziachia njiani licha ya mwenzake kumuonya sana lakini hakuwa tayari kuweza kuzitupa.
Kijana huyo ambaye alikuwa na njaa kali kwenye utafutaji wa maisha yake, aliamini kwamba kazi yake ingeweza kumfikisha mbali ikiwa ni pamoja na kumkutanisha na watu wengi ambao huenda wangekuja kuutambua umuhimu wake. Lengo lake kubwa alikuwa anahitaji kupanda madaraja kwenye kazi yake, alitamani kuwa mtu ambaye angeheshimika kila sehemu ambayo angeonekana sio kwa sababu ya vazi lake tu bali kwa kazi kubwa ambayo alikuwa ameifanya nyuma.

Hakuwahi kuridhika na kuonekana kwamba anapotezewa ama kutengwa pembeni, alikuwa anaelewa namna siasa ilivyokuwa inafanya kazi. Ethan alijua kabisa sehemu ambayo wanahusika wanasiasa basi upuuzi na ujinga mwingi huwa unaingizwa kwa sababu wanasiasa wanajali matumbo yao tu na kupambana kutumia madaraka kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kinaenda kwenye njia zao kama ambavyo wanahitaji wao. Kwa minajiri hiyo aliamua kuzifuatilia hizo kesi yeye mwenyewe binafsi, hakuna jambo ambalo lilimshawishi yeye kukata tamaa licha ya kupewa onyo kwa muda mrefu kwamba kama angeendelea kufanya mambo hayo ingekula kwake.

Ethan baada ya kupokwa ile kesi ya waziri wa mambo ya ndani Slyvester Mboneka. Yeye ndiye alikuwa wa kwanza kabisa kufika kwenye eneo la tukio hivyo taarifa za tukio lile alikuwa nazo kwa sababu alizikusanya na kuziripoti mpaka kesi yake inabebwa. Hakupenda Ethan, njaa yake dhidi ya kupata mafanikio ilikuwa ni kubwa mno, yeye alijua kabisa kwamba hakuwa na rasilimali za kutosha za kumfanya apate majibu ya moja kwa moja kama wengine lakini bahati ilikuwa kwake alikuwa mtoto wa mtaani, Ethan alielewa namna mitaa inavyotakiwa kuwa, alijua ukiwa na uhitaji na jambo fulani mtaani unatakiwa umuone nani na nani ambao wangekusaidia kukusanya taarifa hata za zamani.

Hilo ni jambo ambalo lilimpa imani kubwa ya kufanikisha kila alilo litaka yeye hivyo akalivalia njuga kimpango wake. Ethan baada ya kutoka ndani ya lile eneo hakukaa kama zoba bali alisafiri mpaka kilipo chuo cha DIT, karibu na hilo eneo kulikuwa na rafiki yake mmoja ambaye aliwahi kusoma naye shule ya msingi alikuwa ana duka hapo la vifaa vya simu. Kijana huyo alikuwa anazuga na duka hilo lakini kazi yake kubwa alikuwa ni mdukuzi maarufu sana kwa sababu ndiyo biashara ambayo ilikuwa inampatia mamilioni ya pesa.

64 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
Back
Top Bottom