Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI
SONGA NAYO................

Aliona kuna kitu kinakuja kwake kwa kasi na nguvu kubwa, hakuelewa kilirushwa muda gani ila jambo ambalo alilielewa ni kwamba alitakiwa kuwa makini kuweza kuendana na spidi kubwa ya kifaa hicho. Ilikuwa ni ile spana ambayo ilitua pembeni ya alipokuwa baada ya kufanikiwa kuikwepa, kama ingempata ingempatia kovu kubwa huenda la maisha.

Alifanikiwa kuikwepa lakini hakuwa salama kwa sababu alihisi kivuli kinakuja kwa kasi kubwa pale ambapo yeye alikuwepo, alihitaji kukikwepa ila yeye alionekana kuwa mzito ndani ya lile eneo, alipokea maumivu kwenye ubavu wake wa kushoto mahali ambapo buti zito la Othman lilitua. Alihema kwa maumivu makali lakini hakuwa na muda wa kutosha kwa ajili ya kuweza kujishauri mara mbili, mwanaume alikutanishwa na mkono uliokomaa vyema ngumi ilitua kwenye kifua chake kiasi kwamba alihisi kuna nondo ilizama eneo hilo.
Alijihisi kutema mate lakini wakati anayatema hayakuwa mate ya kawaida bali alitema damu, hali yake ilionekana kabisa kuanza kuwa mbaya. Aliyumba na kuupanga mkono wake kwa sababu bado Othman alionekana kumjia wakati huo, alinesa kidogo Ezra na kuruka sarakasi ya mbele lakini haikuwa afadhali kwake, alitwishwa teke zito ambalo lilimbeba mpaka kwenye sakafu ya ile lami, alihisi kuna kitu kinakuja hivyo akalazimika kujigeuza kuelekea mtaroni ila alinasa kwenye kuta za mtaro.

Ule mguu ambao ulikuwa unashuka pale alipokuwepo uliishia kutua kwenye lami mpaka ulichimbua hilo eneo, watu walikuwa wanapita kwenye magari hakakuwa na muda nao kabisa, jiji lina njaa kali kila mtu alikuwa akijali biashara zake nani anafuatilia hayo mambo? Hakuna, japo ilionekana kuwa burudani kwa watazamaji na kuna watu kadhaa ambao walikuwa kwa miguu ndio ambao walionekana kuvutiwa na tukio hilo kiasi kwamba wakawa wanachukia video na kushangilia.
Ezra alijirusha mpaka barabarani, hakuelewa Othman alimfikia wakati gani, alikutana na kisigino cha uso, aliburuzwa na kuchubuka, alipigwa na mguu kwenye tumbo lake mithili ya mtu aliyekuwa anakutana na ule mpira aina ya Volley kwa ajili ya kuipatia timu yake goli ya ushindi, bwana huyo alitapika damu akiwa anaunguruma pale alipokuwepo. Othman alimsogelea kijana yule aliyekuwa na njaa ya mafanikio makubwa na kusikitika
“Una sababu ya msingi ya kunifanya nisikuue?”
“Othman nahitaji kumzuia Gavin anacho kifanya ni hatari kwa taifa letu, nakuomba unisaidie kwa hili. Anaweza kubeba kila kitu akaondoka nchini, hiki mnacho kifanya kinaenda kuwa hatari kwa watu wengi kwa sababu kinaua kabisa amani na kufanya tuingie kwenye hatua mbaya kama taifa”
“Kama ungekuwa na nafasi mbili za kuishi basi hilo jina hautakiwi kuja kulitaja tena” Othman wakati anaongea alikuwa ametoa kifaa kidogo ambacho kilikuwa kama kisu, alitaka kukizamisha kwenye shingo ya kijana huyo lakini aliona kitu kwenye hicho kisu, alikuwa ni mtu ambaye alishika bastola umbali kadhaa kutoka hapo akiwa anakuja kule ambako alikuwepo, mwanga wa jua ndio ambao ulimsaidia kuweza kuliona hilo hivyo alinyanyuka kwa sarakasi za hatari na za haraka mno wakati huo risasi zilianza kurindima na kuwafanya wale ambao walikuwa umbali kadhaa kwenye barabara kuanza kupiga mayowe kila mtu akishika njia yake.

Ezra alikuwa kwenye hali mbaya lakini aliona namna Othman alivyo ondoka eneo lile, aliogopa mno, mwanadamu kuwa vile ni jambo la hatari na hakufanikiwa kuingiza ngumi hata moja kwenye mwili wake halafu ndo yeye alikuwa anataka kukutana na Gavin? Hata yeye hakujiona kama yupo siriasi na jambo hilo. Lakini jambo ambalo lilikaa kwenye kichwa ni juu ya nani ambaye alifika na kumfanya mwanaume huyo kughaili zoezi la kuweza kumuua? Hakuwa na jibu la haraka kwa sababu bado alikuwa amegeuka kumuangalia Othman na alipokuwa ameishia. Kuna gari binafsi ya mtu ilipita ikiwa kwenye mwendo mkali, mwanaume huyo aliipigia hesabu na kudunda kwenye lami kisha akaja kunasa mpaka juu ya ile gari kama hakuna ambacho kilitokea ndani ya eneo lile akapotea nalo.

Ezra aligeuka tena kujua mtu ambaye allimpatia msaada wakati huo ndipo akapigwa na butwaa, alikuwa ni yule The Future, bwana huyo alikuwa na bastola kwenye mkono wake akiwa anakimbilia alipokuwepo Ezra. Hali yake ilikuwa mbaya akiwa hawezi kufanya jambo lolote hata kunyanyuka.
“Umejuaje kama nipo eneo hili?”
“Brian ameidukua simu yako kwa sababu alijua utafanya jambo la kipuuzi akaomba nikufuatilie. Wasiwasi wake umekulipa kwa sababu bila yeye mpaka wakati huu ungekuwa upo akhera huko kuweza kulipa dhambi zako ambazo umezifanya ukiwa hai maana kwa unavyo onekana hakuna nafasi kabisa ya wewe kuweza kuiona pepo”
“Shukrani sana ndugu yangu kwa kuweza kunisaidai kwa sababu nilikuwa najiona kabisa sina nafasi ya kuweza kuishi tena”
“Unaingiaje kwenye mikono ya watu hatari namna ile? Nimeshuhudia jinsi anavyo kupiga mpaka nikabaki nashangaa na kusikitika baada ya kuona Tanzania tuna watu hatari namna ile. Yule ni muuaji Ezra, ni nani yule?”
“Sio muda wa kuongelea haya mambo kwa sababu anaweza kurudi tena akatuua wote, kwa namna nilivyo muona watu kama mimi tunatakiwa tuwe angalau kumi ndipo tunaweza kuwa sawa naye” Ezra alikuwa kama amekata tamaa kabisa ya alichokuwa anakifanya, The Future alimbeba na kumpeleka kwenye gari yake ili kuweza kumuwahisha kupata matibabu, hali yake haikuwa ikiridhisha kabisa.



******
Nick alikuwa kwenye hali mbaya, alipigika vibaya na kitu chenye ncha kali kilizama mwilini mwake na kuutoboa toboa, afya yake kwa ujumla haikuwa ya uhakika. Licha ya kuwa kwenye hali kama hiyo lakini alijikongoja na kuhakikisha anafika kwa kiongozi wake, kiongozi wake alikuwa ni Bashir, kijana wa kutegemewa kabisa na mkuu wa majeshi.
Alifika akiwa amepoteza damu nyingi, mdomo wake ulikuwa unatema damu muda wote badala ya mate kiasi kwamba alimshtua mpaka mtaalamu huyo. Hakuelewa kijana huyo alikutwa na kitu gani huko ambako alikuwa ila bila shaka hapakuwa pema kabisa ndiyo maana alikuwa hivyo.
“Walijua kama tutakuwa pale, walijua” aliongea kwa shida akiwa anakalishwa kwenye kochi ili aweze kutoa maelezo kamili juu ya kila kilichokuwa kimetokea kule.
“Akina nani?”
“Siwajui”
“Tulia kisha uniambie ulicho kutana nacho huko ambako ulikuwa”
“Sijajua ni nani alikuwa pale ila inaonekana ni mtu ambaye alikuwa anakuja ile sehemu kwa ajili ya kumuokoa Sarah na familia yake, nikiwa nataka kumuua ndipo aliingia na kuua wenzangu wote, ni mimi pekee ambaye nimefanikiwa kutoka nikiwa mzima ndani ya ile sehemu”
“Unamaanisha kwamba Sarah hujamuua?”
“Ndiyo”
“https://jamii.app/JFUserGuide Nick, unajua kosa ambalo umelifanya hapa kuendelea kumuacha hai?”
“Sikuwa na namna, mtu ambaye amekuja lile eneo ana uwezo mkubwa kuliko sisi, hakuna hata mmoja wetu ambaye angeweza kupambana naye. Sarah alikuwa kwenye hali mbaya tayari, ilibakia mimi kumalizia kazi tu ila ikashindikana kwa sababu hiyo”
“Ni nani huyo mtu” mwanaume huyo aliuliza akiwa mwingi wa jazba na hasira ambayo ilijionyesha wazi wazi.
“Simjui”
“Humjui mtu ambaye amekuvamia na unadai kaua wenzako?”
“Ndiyo, kwa sababu alijifunika kitambaa usoni”
“Unajua maana ya kuwakimbia wenzako ukiwa vitani?”
“Naelewa lakini mimi nimekuja ili kutoa hii taarifa, na sina imani na usalama wa mheshimiwa hivyo mkuu wa majeshi anatakiwa kulindwa sana kwa sasa”
“Whaaaaat?”

70 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
SONGA NAYO................

“Kama alifika lile eneo kwa wakati mwafaka maana yake huenda anajua kuhusu sisi ama ana taarifa za mhimu kuhusu sisi hivyo hatupo salama. Kuanzia wakati huu tunatakiwa kujiandaa kwa jambo lolote ambalo linakuja mbele yetu”
“Tunajiandaa?”
“Ndiyo”
“Nashukuru kwa taarifa yako lakini hauwezi kuishi, umeshindwa kufanya kazi uliyopewa ni ishara ya wazi kwamba hauna faida tena ndani ya jamii hii hivyo unatakiwa kufa”
“No, no no usinifanyie hivi, nimejitoa kwa kila kitu kwa ajili ya mheshimiwa, nimemsaliti mpaka Sarah ambaye alikuwa ameanza kuniamini sana kwa ajili ya hili halafu leo unataka kuniua tena? Tafadhali Bashir mimi nitalisahihisha hili nakuahidi”
“Too late Nickson” mshahara wa dhambi ni mauti, mwanaume huyo alimsaliti mwanamke ambaye alikuwa amemuamini kwa nafasi kubwa, aliamini yeye na bwana huyo wangeyaanza maisha ya pamoja lakini bwana huyo aloionekana kuwa na mipango tofauti kabisa kwenye kichwa chake ila mwisho wake haukuwa wa kuvutia. Bashir alimzamishia kisu kwenye koromeo lake, alikitoa na kukisimika moyoni tena kwa mara nyingine hakuwa na kauli, alibaki anababaika akiwa kama mtu ambaye alihitaji kufanya jambo fulani lakini hakuwa na huo uwezo, muda wake wa kuishi ulikuwa umeisha.

Bashir aliinua mkonga wa simu na kuuweka kwenye sikio lake, simu hiyo iliita kwa muda kidogo kisha ikapokelewa;
“Bosi kuna tatizo kubwa limetokea”
“Nakusikiliza Bashir”
“Sarah ametoroka”
“Bashir, are you serious?”
“Nimefuata maagizo yako kumtuma mhusika lakini amerudi hapa akiwa kwenye hali mbaya akidai kwamba kuna mtu ambaye alienda kumuokoa pale”
“Ni nani huyo mtu?”
“Anadai kwamba hamjui kwa sababu alijifunika kitambaa”
“Kwahiyo kuna taarifa zozote kuhusu huyo mtu?”
“Hapana bosi”
“Na huyo bwana mdogo yuko wapi?”
“Nimemuua”
“Huo mwili wake unatakiwa kutupwa karibu kabisa na barabara kisha usiku wa leo hii watafute waandishi wa habari nguli ambao wanaaminika, vujisha taarifa kuhusu Sarah, apewe kesi hadharani ya mauaji ya mke wa raisi lakini pia kwa kuua wanajeshi ambao walienda kumkamata akiwepo huyo mwanajeshi mwenzake wa karibu”
“Itahitajika ushahidi kwenye hilo bosi”
“Tuna silaha ambayo aliitumia kwenye kufanyia tukio lile, maana yake mpaka hapo ni kwamba tuna finger prints zake, maana yake hatakuwa na namna ya kuweza kukataa”
“Sawa mkuu” simu ilikatwa ambayo kiukweli haikuwa njema sana kwa Medrick Savato.


***
Upande wa pili alikuwepo mkuu wa majeshi akiongea na simu hiyo, simu ilimkutia kwenye jengo kubwa la kanisa, alikuwa ameketi katikati kabisa ya jengo hilo. Nje ya kanisa hilo ambalo lilikuwa katikati kabisa ya mji kulikuwa na ulinzi mkali mno wa makomando, hakuwa na imani sana na maisha yake, alisimuliwa na mzee Hasheem aina ya mtu ambaye alikuwa anadili naye, alimtaka bwana huyo kuwa makini kwa kile sekunde ambayo ilikuwa inazidi kwenda kwa sababu kadri saa ilivyokuwa inazidi kwenda ndivyo nafasi yake ilivyokuwa inazidi kuwa ndogo ya kuendelea kuwa hai.

Eneo hilo alikuwa na miadi ya kukutana na mtu usiku huo, simu ambayo aliipokea ilimharibia siku yake kwani ratiba haikupangwa kuwa hivyo lakini alishukuru kwa sababu alikuwa na karata ya ushindi mezani kwenye hilo. Aliamini kwamba mpaka kunakucha asubuhi, habari zingezagaa kila kona, jina la Sarah lingeonekana baya kila sehemu, mwanamke huyo alikuwa anaenda kupata umaarufu kwa kuwa na kesi nzito mbele yake ya kuhusika na mauaji ya mke wa raisi wa nchi, ilikuwa ni habari mbaya na jambo la hatari mno kwake.
Akiwa amezama kwenye mawazo hayo, alisikia mjongeo wa hatua za mtu ukiwa unakuja ile sehemu ambayo alikuwepo. Hali hiyo ndiyo ambayo ilimtoa kwenye yale mawazo ambayo alizama kuyatafakari na kupima ukubwa wa mzani ambao alikuwa anatakiwa kuutumia kupimia kilo zake, mzani haukuwa ukibalansi vizuri upande wake. Mwanamke huyo Sarah alikuwa akimuumiza mno kichwa chake, kwanini? Yeye ndiye ambaye alikuwa nyuma ya mpango wa mauaji ya mke wa raisi kwa kumtumia binti huyo lakini mpaka wakati huo binti alikuwa hai na mzima wa afya, hilo kwake lilikuwa tishio kubwa na kwa bahati mbaya alidaiwa kukimbilia kusiko julikana na familia.
Usiku huo alipanga kwenda kumchafua binti huyo ila hilo halikumpa amani, aliamini kwamba hakunaga siri ya watu wengi, siri inakuwa siri inapobaki kuwa ya mtu mmoja, sasa inabaki vipi kuwa ya mmoja wakati ni wengi wanaijua na mhusika ndiye huyo alikuwa katoweka? Aliamini kuwa hai kwa Sarah kuna siku ingekuja kumtokea puani, mwanamke huyo alitakiwa kupatikana kwa gharama yoyote ile. Mheshimiwa aliona kabisa kwamba wakati wa yeye kucheza fair play uliisha, alitakiwa kuwa na roho ngumu ya kijerumani, ubaya ubaya hakutakiwa kucheka na mtu yeyote yule.

Alikuwa na jeshi nyuma yake, sasa alitakiwa kumhofia nani? Alijishangaa, mtu pekee ambaye kwake alikuwa tishio ni raisi. Vipi kama raisi akija kujua kwamba yeye ndiye mhusika halisi wa kumuua mkewe ambaye alimpenda mno? Angemuacha? Jibu lilikuwa hapana, basi mpaka hapo karata ya ushindi ilitakiwa kuwa kwake hata kwa bao la mkono. Aliguna kumpa taarifa mgeni wake kwamba alikuwa tayari kumsikiliza kwa sababu mtu huyo alikuwa amekaa mstari mmoja na mkuu wa majeshi, wote walikuwa wakiangalia mbele kana kwamba kila mtu hakuw ana muda na mwenzake. Yalikuwa maongezi ya kitaalamu ambayo yalikuwa yanafanywa na wataalamu wa kazi, hawakuwa na mapepe, kila mtu alijua kile alikuwa anakifanya na ambacho alitakiwa kukifanya.

“Najua haupendi kuonana na mimi ila nimekuja hapa kwa sababu ya msingi mno kama utakuwa tayari kuweza kunisikiliza na kuufanyia kazi ushauri ambao nimekuja kukupatia hapa bwana Savato”
“Kama nina kumbukumbu sahihi hakuna jambo lolote lile la maana ambalo umewahi kujali kuhusu mimi”
“Kwanza nasikitika kukwambia kwamba mimi najua kila kitu kuhusu wewe”
“Mhhhh ndugu yangu ni kauli nzito sana hiyo, unamwambiaje mwanaume mwenzako kwamba unajua kila kitu kuhusu yeye?”
“Sipo hapa kwa ajili ya kukuletea misemo ya kihuni ya mtaani bali nipo hapa ili uweze kuujua ukweli, unatakiwa kujua mbivu na mbichi ili ufanye maamuzi yaliyo sahihi kwani kila unavyozidi kukosea ndivyo unaikaribisha hatari zaidi kwa upande wako” sauti hiyo haikuwa ya mtu mwingine bali mkurugenzi wa usalama wa taifa, Othman Micho ndiye ambaye alifika ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kufanya maongezi na huyo kigogo mwenzake.
“Nakusikiliza”
“Taarifa ambazo ninazo kutoka kwa vijana wako ni kwamba huenda wewe ndiye mtu ambaye unafuata kwa sasa kufa. sina uhakika kama itakuwa ni kufa moja kwa moja ama mtu huyo anahitaji kukuteka ili akakuhoji, inaonekana mna historia ndefu kidogo nyie wawili”
“Hahaha hahaha hahaha, Othman unazeeka mapema sana ndugu yangu, kweli unaamini hayo maneno yako kwamba kuna binadamu ana hiyo jeuri ya kuweza kumteka mkuu wa majeshi? Kabla sijajibu hata hoja yako wewe unaona kwamba hilo jambo linakuja kwenye mzunguko wa afya ya akili yako?”
“Ni jambo linalowezekana kwa asilimia zaidi ya sabini, mimi na wewe wote tunaelewa kwamba jambo likifikisha kuanzia asilimia hamsini na kuendelea basi kufanikiwa kwake ni uhakika zaidi kwahiyo naweza kukuhakikishia kwamba linawezekana vizuri tu. Taifa lenye nguvu zaidi duniani limewapoteza maraisi wake wa nne kwa kuuawa, hilo ndilo taifa ambalo raisi wake ana ulinzi mkali kiasi kwamba hata sisimizi kumfikia pale alipo ni ngumu kuliko unavyodhani lakini waliuawa. Nalizungumzia taifa la Marekani.

71 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI NA MBILI
SONGA NAYO................


Kitu unachopaswa kukijua ni kwamba kadri sisi tunavyokuwa tunagundua namna kubwa ya kuweza kuyashughulikia haya mambo basi hata wauaji na wahalifu wanaendelea kubuni njia mpya na rahisi zaidi za kuweza kutekeleza kile ambacho wanakitaka kutoka kwetu. Wewe kuwa mkuu wa majeshi, kuzungukwa na makomando hakuzuii kuuawa, sina uhakika kama wewe unalindwa kuliko mke wa raisi lakini ameuliwa tena hadharani kabisa alasiri jua likiwa kali, wewe unaogopwa kwa sababu unaitwa kiongozi mkuu wa jeshi lakini haiondoi maana ya kwamba unafikika” mkurugenzi alimnyooshea bwana huyo ambaye alionekana kuwa mbishi na mjivuni kwa sababu tu alikuwa na watu wa kutisha ambao aliamini wangemlinda mpaka dakika za mwisho.

“Ni nani huyo ambaye unamzungumzia hapa kiasi kwamba ana hiyo jeuri ya kumjia mkuu wa majeshi na kutishia maisha yake kirahisi namna hiyo?”
“Usijifanye hujui namzungumzia nani, najua unaelewa kwamba wewe ni miongoni mwa watu ambao wapo kwenye orodha yake, nadhani umejua ni mtu wa namna gani ambaye anakutafuta, kuishi kwako ilikuwa ni jina lako kuchelewa kufika kwenye mkono wake. Ni asilimia miamoja kwa sasa kwamba lipo kwenye mkono wake”
“Gavin Luca”
“Nilijua tu unalitambua jina lake, sasa kilicho nileta hapa kwako ni kwamba kuanzia sasa unatakiwa kuwa na ulinzi mkali sana muda wote lakini kama inawezekana na vijana wangu wakuongezee ulinzi”
“Hahaha hahaha Micho, Micho unataka kuniongezea ulinzi au unataka kuwaweka karibu ili wapate taarifa ambazo unahisi kwamba zitanipotezea jumla mimi maisha yangu?”
“Kwa sababu nina uhakika unajua ambayo umeyafanya huko nyuma ndiyo maana una wasiwasi na maisha yako. Savato unatakiwa kujiandaa kuanzia sasa kwa sababu muda sio rafiki kwako, haya mambo ambayo uliyafanya na wenzako sio muda yanaenda kuishia sehemu mbaya, sioni kama ukiwa na maisha marefu uraiani hata kama ikitokea ukapona kutoka kwa Gavin japo najua hauwezi kupona”

“Una maana ipi kuniambia hivyo? Ni kama unanipa vitisho kwa jambo ambalo hauna uhakika nalo”
“Nina uhakika unajua kabisa kwamba unaongea na nani hapa hivyo unajua kabisa kwamba siwezi kukuletea taarifa ambazo binafsi sina uhakika nazo, mpaka nazifikisha taarifa zangu kwako maana yake najua kile nakileta na nina uhakika nacho, nadhani nimezunguka ndiyo maana unaigiza kama vile hauwezi kunielewa” mkurugenzi aliona kuzunguka anapoteza muda wake bure, aliamua kupita na njia ambayo ni rahisi kwake.
“Miaka kadhaa iliyopita huko nyuma wewe na wenzako mlihusika kwenye kuiteketeza familia ya Gavin ndiyo maana anawatafuta, yule bwana haui kila mtu kwa sababu tu anapenda kuua bali kuna watu wake ambao anawatafuta na wewe ukiwepo. Uwepo wenu juu ya kundi la siri la THE IMMORTALS sio habari ngeni tena, ni habari ambazo zipo tayari ila kwa sasa kitu pekee kinasubiriwa ni ushahidi juu ya hili na kama ushahidi ukikamilika, niamini mimi ni wachache ambao watapona na kuishi. Uzuri ni kwamba haupo pekeyako bwana Savato, najua hata raisi yupo ndani ya hili kundi lenu na ndiye ambaye alikuteua wewe kwenye hiyo nafasi kwa makusudi mazima kabisa ili kutimiza agano la kundi hilo.”

“Hizi taarifa umezipatia wapi Othman?”
“Niliwahi kuupata msemo wa bwana mmoja ambao ulikuwa unasema kwamba “Kuna muda huwa nafikiria kwamba naijua sababu ya kwanini Mungu alimuumba mwanamke. Lakini kujua kwamba ni kwanini Mungu alimuumba mwanaume imebaki kuwa kitendawili kigumu kuweza kukielewa” huu msemo ukituliza akili zaidi unagundua kwamba ni kweli, najua huenda haujaelewa maana ya huu msemo na sababu ambazo zinaufanya uonekane kuwa wa kweli.

Kwenye haya maisha mwanamke anatabirika, mwanamke anatabirika kwa sababu mambo yake na maamuzi yake anayafanya kutokana na hisia, akiwa na hasira unaweza ukaisoma hatua yake ambayo inafuata ila jambo hili limekuwa ni tofauti kabisa kwa mwanaume, ni ngumu kuweza kumsoma mwanaume kwa sababu ni mtu ambaye anafanya kila kitu kwa kuzingatia zaidi ubongo wake. Hata akiwa na hasira vipi ni ngumu kumsoma kwamba baadae anaenda kuichukua hatua gani ndiyo maana huwa unashauriwa kwamba ukiona mwanaume unafanya maamuzi yako kwa kutumia hisia, unatakiwa kuacha mara moja kwa sababu unakuwa umefikia hatua mbaya na hatua ya mwisho kabisa kwenye maisha, hilo ni jambo la hatari mno.

Sasa kwanini huo msemo Savato? Ni kwa sababu sisi wanaume tumebeba vingi kwenye vifua vyetu, sisi wanaume ni watu ambao huwa tunakubali kufa na maduku duku, hatutabiriki, huwezi ukajua huyu bwana anaenda kufanya kitu gani muda ujao, hilo ndilo jambo ambalo linafanya mwanaume kuwa mnyama hatari zaidi kuwahi kuishi duniani. Ni miaka mingi umekuwa mmoja wa watu ambao wanajifanya kulipigania taifa hili, umekuwa mtu ambaye unajifanya kuwa na uhasama mkubwa na wale ambao wanaitishia amani ya taifa hili huku ukijua kabisa kwamba wewe ndiye mmoja wa watu ambao wameisambaratisha amani ya taifa hili, mpaka hapo unaona mwanaume anatabirika bwana Savato? Kumwamini binadamu ni kujichimbia kaburi ambalo unajua kabisa mwanadamu huyo huyo atalitumia kuweza kukuzikia”
Maelezo na maneno ya mkurugenzi yalikuwa yanazungumza mengi mno, maelezo yake ilikuwa ni ishara tosha kwamba alikuwa anajua mengi, mpaka hapo alijionyesha wazi kwamba yeye alikuwa hatari kwa watu hao, kujua kwake kupita kiasi haikuwa ishara nzuri, watu hao walitakiwa kuwa makini isivyo kawaida.

“Haujaniambia bado hizi habari umezitoa wapi” sauti ya mkuu wa majeshi ilikuwa imebadilika, bwana huyo pembeni yake moja kwa moja mpaka wakati huo alikuwa ni adui kwake, hakutakiwa kumchekea.
“Hizi taarifa nimezipata kwa babu yake na Gavin” mkuu wa majeshi aligeuka kama mtoto ambaye alikuwa anadai kunyonya lakini muda haukuwa rafiki kwake.
“Bado sijakuelewa”
“Nina uhakika unajua kabisa kwamba waziri wa zamani yupo hai na ndiye babu yake na Gavin” bwana Savato alihema.
“Unaonekana unajua mengi tofauti na nilivyokuwa nakufikiria, ila hii sio njema sana kwa afya yako rafiki yangu. Nataka nikukumbushe umuhimu wa maisha, maisha haya tunayaaishi mara moja tu pekee na ukiyakosea basi hautaipata hiyo nafasi ya kuweza kuishi kwa mara nyingine tena. Binafsi naweza kukushauri kwamba unipatie taarifa zote ambazo unazo mpaka sasa, uuharibu ushahidi wowote ambao huenda unao mpaka sasa ili wote mimi na wewe tuweze kuishi kwa amani na maishe mengine yaendelee. Sioni umuhimu wa mimi na wewe kuwa na mwisho mbaya Othman, hatujawahi kuwa marafiki lakini kazi imetukutanisha hivyo tunaweza kulindana kikubwa ndugu yangu”
“Hii ndiyo sababu imekufanya umuue mke wa raisi?”
“What?”
“Hebu fikiria raisi akijua hili kwamba kijana wake unamzunguka, una uhakika atakuwa tayari kukuacha hai?”
“Othman!”
“Najua unatamani kunitisha ama kunivamia ila usije ukafanya hilo kosa kwa sababu nitakumaliza mwenyewe, kwa sasa nina taarifa zako nyingi sana hivyo kila hatua ambayo unaikosea, unazidi kujitengenezea nafasi mbaya zaidi kwenye hili jambo”
“Yupo wapi Mr Hassan”
“Hata mimi sijui”
“Nahitaji kuonana naye, kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu nahitaji msaada kwako”
“Kwa bahati mbaya mazingira ambayo nimekutana naye hayakuwa rafiki kunifanya mimi nifahamu alipo kwa sababu kama ningekuwa na huo uwezo basi mpaka sasa ningekuwa nimesha mkamata ili kumzuia Gavin kufanya haya ambayo anayafanya. Najua huenda ana hasira na nyie lakini sitaki kuruhusu mauaji ya halaiki kwenye taifa langu, nataka kuhakikisha inatumika sheria kuwaadhibu walio mkosea vinginevyo atakuwa anaingia vitani na mimi mweyewe binafsi”

72 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI NA TATU
SONGA NAYO................


“Ni watu wangapi wanajua kuhusu haya?”
“Kama kuna watu wengi wangekuwa wanajua unahisi ningekubali kukutana na wewe eneo kama hili kukwambia hizi habari?”
“Unaenda kuzifanyia nini?”
“Sijajua bado, kuhusu raisi hata usijali huyo mtamalizana wenyewe kwa wenyewe wala sijali sana kuhusu yeye kwa sababu naye ndo wale wale, kwa sasa jambo ambalo nalijali zaidi ni usalama wa taifa langu ila kwa sasa hakikisha una ulinzi kila sehemu unayokuwepo, usifanye kosa hata moja kwa sababu linaweza kukuletea majuto ya dunia bwana Savato kwa sababu kuna mwigizaji mmoja bwana Tyrion Lannister alisema “Death is so boring especially with so much ecitement in this world” tutaonana wakati mwingine ndugu yangu”

Wataalamu hao wawili walimaliza mazungumzo yao, yalikuwa na mwisho mbaya, kila mtu alibaki na jambo lake moyoni. Mkuu wa majeshi ndiye alivurugwa, habari hizo kuendelea kusambaa kwa watu wengi ilikuwa ni hatari kwa upande wake. Alipaswa kuwa makini kuliko hata ambavyo alikuwa anafikiria kwa sababu kama alivyokuwa ameonywa, kosa moja tu lilikuwa linapita na maisha yake mazima.

Alipata wazo, wazo jipya juu ya nini alipaswa kukitenda kwa wakati huo, akili yake ilitakiwa iwe inafanya kazi kuliko mwanzo lakini wakati huo huo alitakiwa kuanza kuchukua hatua stahiki kwani elielewa kabisa kwamba alizungukwa na watu hatari mno nyuma yake, watu ambao kwao alikuwa kibaraka tu na hata wangeamua kuyabeba maisha yake kwao lilikuwa jambo la dakika zisizo zidi hata kumi hivyo alitakiwa kuwa mbwa mtiifu kwa wafugaji wake. Aliitoa simu yake mfukoni baada ya kuhakikisha amepiga hesabu zake vizuri, mtu ambaye alimpigia wakati huo alikuwa ni raisi, alitaka kumpa habari;
“Mheshimiwa, naomba unisamehe kwa kukusumbua usiku ila ni jambo mhimu sana kwa sababu nimefanikiwa kumjua muuaji wa first lady” yalikuwa ni maelezo mafupi ambayo aliyawasilisha kwa kujiamini, alihitaji kuisuka kesi katikati yake ili yeye aweze kubaki hai.
“Sawa mkuu” alijibu akiwa anaikata simu hiyo, alitabasamu na kuiweka suti yake vizuri kisha akaanza kutoka ndani ya hilo jengo kubwa la kanisa. Hakuwa fala wa kusema alikuwa anaenda kufa kipuuzi tu bila kuwa na mpango dhabiti juu ya kile alitakiwa kuweza kukifanya kwa wakati huo. Mwanaume huyo aliamua kutumia zaidi akili kwa wakati huo kuliko nguvu, nguvu hazikuwa na umuhimu kwake, kwa wakati huo alifunga safari kuelekea Ikulu kuweza kukutana na raisi wake.


******
Bwana George raisi wa Tanzania, alikuwa amesimama karibu na lilipokuwepo bwawa la kuogelea akila upepo, alikuwa na mambo mengi anayawaza. Kubwa lilikuwa ni kumpoteza mkewe kipenzi na siku ya kesho yake ndiyo ilikuwa siku ya kuweza kufanya mazishi ya mwanamke huyo ambaye alikuwa ndiye First Lady.
Kwa mara ya kwanza alikuwa ametoka kuonana na kiongozi mkuu wa kundi la THE IMMORTALS na kumfahamu, alikuwa ni raisi wa zamani wa Tanzania. Lengo la kwenda huko ni kwa sababu alikuwa anahitaji msaada, mambo ambayo yalikuwa yanaendelea aliona kama yanakizidi kichwa chake.
Kuambiwa kwamba mkuu wa majeshi alikuwa anajua mtu ambaye alihusika kwenye mauaji ya mkewe ilikuwa ni habari mbaya kwake ila hakutaka kwenda na mihemko bali aliamua kutuliza kichwa ili kujua hatua ambayo alitakiwa kuichukua mbele ya bwana huyo. Akiwa mwenye tafakuri kubwa usiku huo ambao majira yalikuwa yamekwenda ndipo alishangaa anapokea simu ya bwana huyo ambaye alidai kwamba alihitaji kumuona wakati huo kwa sababu alikuwa ana taarifa juu ya kifo cha mkewe.
Haikumuingia sana akilini ila aliamua kulipa muda jambo hilo ili aweze kulisikiliza kisha ndipo angeweza kulifanyia maamuzi sahihi. Alikaa kwa muda mrefu eneo hilo mpaka alipokuja moja ya walinzi wake na kumpatia taarifa kwamba mkuu wa majeshi alikuwa amefika ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kumuona, aliruhusu mtu huyo aletwe kule ambako yeye alikuwepo.

“Heshima yako kiongozi”
“Kama nina kumbukumbu zangu zilizo sawa, Savato kabla ya kuwa kwenye hiyo nafasi ulikuwa ni moja kati ya vijana watiifu sana ambao walielewa namna sahihi ya kuweza kumheshimu na kumtukuza aliye muweka hapo kwenye hiyo nafasi, ila ndizo zile zile za maskini akipata basi hukalia mbwata. Unaweza ukaniambia kuna jambo gani linaendelea kwako na mimi silijui?”
“Naweza kukuhakikishia kwamba hakuna tatizo lolote kwa upande wangu kiongozi zaidi ya kutimiza majukumu ambayo yameniweka hapa”
“We are serving the same master nadhani unalitambua hilo”
“Ndiyo kiongozi”
“Ila haimaanishi kwamba mimi na wewe tupo sawa”
“Hilo nalijua mheshimiwa ndiyo maana sijawahi hata siku moja kuvuka mpaka kwenye hilo”
“Una uhakika?”
“Ndiyo mkuu”
“Kwanini natakiwa kukuamini juu ya hilo?”
“Kwa sababu nimekuwa mwaminifu kwako siku zote”
“Kwa maneno tu na kirahisi namna hiyo?”
“Hapana kiongozi”
“Ni kipi kimekuleta hapa wakati huu?”
“Mheshimiwa najua hali ambayo unaipiti kwa….”
“Acha propaganda, nieleze sababu ya uwepo wako hapa”
“Kwanza nataka nikupe taarifa kwamba nipo na kijana wako”
“Yupi?”
“Nadhani unaelewa kabisa kwamba ulimtuma Hussen Damaga kwa mama yake Gavin”
“Enhe!”
“Mimi ndiye ambaye nilimuokota kule akiwa kwenye hali mbaya”
“Kwahiyo”
“Nilitaka ujue kwamba kijana yupo kwenye mikono yangu salama”
“Kwanini unaniambia hizi habari sasa?”
“Kwa sababu unastahili kujua mheshimiwa”
“Haujajibu hoja ya swali ulilo ulizwa”
“Yule ni mlinzi wa raisi kama asipo onekana na wewe hadharani kwa muda mrefu maswali yatakuwa mengi”
“Unahisi sijui?”
“Nina imani unajua mheshimiwa”
“Basi nijibu swali langu”
“Sikutaka kukupa taarifa mapema kutokana na hali ambayo nilimkuta nayo kule”
“Kwamba sikustahili kupewa taarifa ya mlinzi wangu mwenyewe?”
“Sina maana hiyo mheshimiwa”
“Ila una maana ipi?”
“Nilihitaji angalau apate nafuu ndipo uweze kupata hizi taarifa”
“Una uhakika hilo ndilo lilikuwa lengo lako?”
“Ndiyo kiongozi”
“Ooooooh nimekusikia” Savato alijua kabisa kufanya jambo hilo ulikuwa ni msala ambao ungemuingiza kwenye matatizo makubwa.

73 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI NA TATU
SONGA NAYO................


“Ni watu wangapi wanajua kuhusu haya?”
“Kama kuna watu wengi wangekuwa wanajua unahisi ningekubali kukutana na wewe eneo kama hili kukwambia hizi habari?”
“Unaenda kuzifanyia nini?”
“Sijajua bado, kuhusu raisi hata usijali huyo mtamalizana wenyewe kwa wenyewe wala sijali sana kuhusu yeye kwa sababu naye ndo wale wale, kwa sasa jambo ambalo nalijali zaidi ni usalama wa taifa langu ila kwa sasa hakikisha una ulinzi kila sehemu unayokuwepo, usifanye kosa hata moja kwa sababu linaweza kukuletea majuto ya dunia bwana Savato kwa sababu kuna mwigizaji mmoja bwana Tyrion Lannister alisema “Death is so boring especially with so much ecitement in this world” tutaonana wakati mwingine ndugu yangu”

Wataalamu hao wawili walimaliza mazungumzo yao, yalikuwa na mwisho mbaya, kila mtu alibaki na jambo lake moyoni. Mkuu wa majeshi ndiye alivurugwa, habari hizo kuendelea kusambaa kwa watu wengi ilikuwa ni hatari kwa upande wake. Alipaswa kuwa makini kuliko hata ambavyo alikuwa anafikiria kwa sababu kama alivyokuwa ameonywa, kosa moja tu lilikuwa linapita na maisha yake mazima.

Alipata wazo, wazo jipya juu ya nini alipaswa kukitenda kwa wakati huo, akili yake ilitakiwa iwe inafanya kazi kuliko mwanzo lakini wakati huo huo alitakiwa kuanza kuchukua hatua stahiki kwani elielewa kabisa kwamba alizungukwa na watu hatari mno nyuma yake, watu ambao kwao alikuwa kibaraka tu na hata wangeamua kuyabeba maisha yake kwao lilikuwa jambo la dakika zisizo zidi hata kumi hivyo alitakiwa kuwa mbwa mtiifu kwa wafugaji wake. Aliitoa simu yake mfukoni baada ya kuhakikisha amepiga hesabu zake vizuri, mtu ambaye alimpigia wakati huo alikuwa ni raisi, alitaka kumpa habari;
“Mheshimiwa, naomba unisamehe kwa kukusumbua usiku ila ni jambo mhimu sana kwa sababu nimefanikiwa kumjua muuaji wa first lady” yalikuwa ni maelezo mafupi ambayo aliyawasilisha kwa kujiamini, alihitaji kuisuka kesi katikati yake ili yeye aweze kubaki hai.
“Sawa mkuu” alijibu akiwa anaikata simu hiyo, alitabasamu na kuiweka suti yake vizuri kisha akaanza kutoka ndani ya hilo jengo kubwa la kanisa. Hakuwa fala wa kusema alikuwa anaenda kufa kipuuzi tu bila kuwa na mpango dhabiti juu ya kile alitakiwa kuweza kukifanya kwa wakati huo. Mwanaume huyo aliamua kutumia zaidi akili kwa wakati huo kuliko nguvu, nguvu hazikuwa na umuhimu kwake, kwa wakati huo alifunga safari kuelekea Ikulu kuweza kukutana na raisi wake.


******
Bwana George raisi wa Tanzania, alikuwa amesimama karibu na lilipokuwepo bwawa la kuogelea akila upepo, alikuwa na mambo mengi anayawaza. Kubwa lilikuwa ni kumpoteza mkewe kipenzi na siku ya kesho yake ndiyo ilikuwa siku ya kuweza kufanya mazishi ya mwanamke huyo ambaye alikuwa ndiye First Lady.
Kwa mara ya kwanza alikuwa ametoka kuonana na kiongozi mkuu wa kundi la THE IMMORTALS na kumfahamu, alikuwa ni raisi wa zamani wa Tanzania. Lengo la kwenda huko ni kwa sababu alikuwa anahitaji msaada, mambo ambayo yalikuwa yanaendelea aliona kama yanakizidi kichwa chake.
Kuambiwa kwamba mkuu wa majeshi alikuwa anajua mtu ambaye alihusika kwenye mauaji ya mkewe ilikuwa ni habari mbaya kwake ila hakutaka kwenda na mihemko bali aliamua kutuliza kichwa ili kujua hatua ambayo alitakiwa kuichukua mbele ya bwana huyo. Akiwa mwenye tafakuri kubwa usiku huo ambao majira yalikuwa yamekwenda ndipo alishangaa anapokea simu ya bwana huyo ambaye alidai kwamba alihitaji kumuona wakati huo kwa sababu alikuwa ana taarifa juu ya kifo cha mkewe.
Haikumuingia sana akilini ila aliamua kulipa muda jambo hilo ili aweze kulisikiliza kisha ndipo angeweza kulifanyia maamuzi sahihi. Alikaa kwa muda mrefu eneo hilo mpaka alipokuja moja ya walinzi wake na kumpatia taarifa kwamba mkuu wa majeshi alikuwa amefika ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kumuona, aliruhusu mtu huyo aletwe kule ambako yeye alikuwepo.

“Heshima yako kiongozi”
“Kama nina kumbukumbu zangu zilizo sawa, Savato kabla ya kuwa kwenye hiyo nafasi ulikuwa ni moja kati ya vijana watiifu sana ambao walielewa namna sahihi ya kuweza kumheshimu na kumtukuza aliye muweka hapo kwenye hiyo nafasi, ila ndizo zile zile za maskini akipata basi hukalia mbwata. Unaweza ukaniambia kuna jambo gani linaendelea kwako na mimi silijui?”
“Naweza kukuhakikishia kwamba hakuna tatizo lolote kwa upande wangu kiongozi zaidi ya kutimiza majukumu ambayo yameniweka hapa”
“We are serving the same master nadhani unalitambua hilo”
“Ndiyo kiongozi”
“Ila haimaanishi kwamba mimi na wewe tupo sawa”
“Hilo nalijua mheshimiwa ndiyo maana sijawahi hata siku moja kuvuka mpaka kwenye hilo”
“Una uhakika?”
“Ndiyo mkuu”
“Kwanini natakiwa kukuamini juu ya hilo?”
“Kwa sababu nimekuwa mwaminifu kwako siku zote”
“Kwa maneno tu na kirahisi namna hiyo?”
“Hapana kiongozi”
“Ni kipi kimekuleta hapa wakati huu?”
“Mheshimiwa najua hali ambayo unaipiti kwa….”
“Acha propaganda, nieleze sababu ya uwepo wako hapa”
“Kwanza nataka nikupe taarifa kwamba nipo na kijana wako”
“Yupi?”
“Nadhani unaelewa kabisa kwamba ulimtuma Hussen Damaga kwa mama yake Gavin”
“Enhe!”
“Mimi ndiye ambaye nilimuokota kule akiwa kwenye hali mbaya”
“Kwahiyo”
“Nilitaka ujue kwamba kijana yupo kwenye mikono yangu salama”
“Kwanini unaniambia hizi habari sasa?”
“Kwa sababu unastahili kujua mheshimiwa”
“Haujajibu hoja ya swali ulilo ulizwa”
“Yule ni mlinzi wa raisi kama asipo onekana na wewe hadharani kwa muda mrefu maswali yatakuwa mengi”
“Unahisi sijui?”
“Nina imani unajua mheshimiwa”
“Basi nijibu swali langu”
“Sikutaka kukupa taarifa mapema kutokana na hali ambayo nilimkuta nayo kule”
“Kwamba sikustahili kupewa taarifa ya mlinzi wangu mwenyewe?”
“Sina maana hiyo mheshimiwa”
“Ila una maana ipi?”
“Nilihitaji angalau apate nafuu ndipo uweze kupata hizi taarifa”
“Una uhakika hilo ndilo lilikuwa lengo lako?”
“Ndiyo kiongozi”
“Ooooooh nimekusikia” Savato alijua kabisa kufanya jambo hilo ulikuwa ni msala ambao ungemuingiza kwenye matatizo makubwa.

73 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
Daaaah very nice story [emoji120][emoji120][emoji1363]
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KWANZA
ANZA NAYO................

NDOTO YANGU NDANI YA MSITU WA KUTISHA

MSITU WA MAU, KENYA.

Ndani ya msitu mmoja uliokuwa na miti mirefu iliyoshonana, katikati kabisa ya msitu huo palikuwa na nyumba ndogo ambayo ilijengwa kwa mbao iliyo onekana kabisa kwamba ilikuwa imetelekezwa kwa muda mrefu kama sio mhusika kuijenga kwa ajili ya kazi yake maalumu. Msitu ulikuwa kimya, ni sauti za ndege tu ambazo zilikuwa zikipenya ndani ya eneo hilo tulivu, hakukuwa na upepo uliokuwa unasikika kwa sababu ya maeneo mengi kushonana kiasi kwamba ilikuwa ni ngumu upepo kupenya mpaka chini.

Kwenye nyumba ambayo ilitelekezwa hilo eneo kulikuwa na watu kadhaa ambao walikuwa wamevaa nguo za jeshi. Ndani kabisa ya hiyo nyumba kulikuwa na mateka mmoja ambaye alikuwa amefungwa vyema kwa minyororo kwenye mwili wake. Mwili wake ulikuwa umechoka, alikuwa anavuja damu kwenye maeneo mengi ya mwili huku watu kadhaa ambao walikuwa kwenye yale mavazi ya jeshi wakiwa wamelazwa kwenye vitanda nje kidogo ya chumba hicho wakiendelea kuvuja damu.

Ni wachache ambao walikuwa ni wazima wa afya kabisa na wengine ndio ambao walikuwa naye ndani ya hicho chumba bwana huyo aliyekuwa amechakaa kwa kipigo ambacho alikipata. Pembezoni mwa hicho chumba alikuwepo mwanamke mmoja ambaye alikuwa mrembo kwa mwonekano wake japo haukuwa ukiridhisha kutokana na mazingira ambayo alikuwepo na kukosa mahitaji ya mhimu kuuweka mwili wake kwenye hali ya usafi zaidi. Mwanamke yule hakuonekana kupendezeshwa na kilichokuwa kinaendelea ndani ya lile eneo ila hakuwa na namna angeweza kufanya hivyo alitoka kwa hasira na ghadhabu kwenye nje kupunga upepo huku akiwaacha watu wale wafanye kile ambacho walikuwa wamedhamiria kukifanya humo ndani.

Ndani ya hicho chumba walibakia wanaume watatu, wawili walikuwa wamesimama pembezoni wakiwa wameegamia ukuta na mmoja ndiye ambaye alikuwa amesimama mbele ya bwana huyo aliyekuwa amefungwa kwenye kiti. Mwanaume ambaye alikuwa amesimama mbele yake, alivaa mavazi ya jeshi kasoro upande wa juu, kifuani kwake alikuwa amevaa vesti ya rangi nyeusi na kwenye mkono wake alikuwa ameishika sigara ambayo alikuwa anaivuta kwa mbwembwe iliyo changanyikana na gadhabu huku moshi akiwa anampulizia huyo mtu wake usoni.

Alitoa ishara kwa mwanajeshi mmoja, hakusita zaidi ya kulibeba dumu kubwa ambalo lilikuwa pembeni yake, dumu lilijaa mafuta ya petroli ambayo aliyamiminia kwenye mwili wa mwanaume ambaye alikuwa amefungwa kwenye kile kiti kwa umakini bila kumwaga mwaga hovyo chini. Alipo ona inatosha alisogea pembeni na kulipeleka lile dumu mbali ili isije kuwa hatari hata kwa upande wao pia, mwanaume yule ambaye alikuwa anaendelea kuivuta sigara yake aliinama kidogo mpaka alipokuwa ameketi bwana yule kwenye kiti.

"Wakati napewa kazi ya kukutafuta kwa namna na gharama yoyote, binafsi nilijua kwamba ingenichukua zaidi ya mwaka mzima au zaidi kukupata ukizingatia umetafutwa kwa miaka zaidi ya mitano na hukuwahi kujulikana kwamba ni wapi uliwahi kuwepo. Maajabu nimekupata ndani ya muda mfupi tu kiasi kwamba kazi imekuwa rahisi lakini kwa upande wako mambo hayawezi kuwa rahisi kwa sababu unatakiwa kufa leo kwa maumivu" mwanajeshi yule alivuta tena sigara na kuutoa moshi kwa mara nyingine kwa kejeli na majivuno.

"Hii usiichukulie personal ndugu yangu, hii ni kazi na walio nituma ndio wanahitaji iwe hivi kwahiyo kama nisipo kuua mimi ndiye nitakufa. It's over" aliongeza sentensi fupi kisha akasimama, alivuta sigara yake kwa mara nyingine na kuiachia kwenda kwenye mwili wa yule mwanaume ambaye alianza kupiga kelele baada ya moto kuwaka na kuanza kuuunguza mwili wake. Mwanajeshi yule aliitoa simu yake akapiga picha za kutosha na kuchukua video fupi kabla uso wa mwanaume yule haujaharibika kisha aliichomoa bastola kwenye kiuno chake, aliikoki kwa kuigongesha kwenye buti lake na kumimina risasi zote kwenye kichwa cha mwanaume ambaye alikuwa anawaka moto baada ya kuzidisha makelele.
Utulivu ulichukua nafasi, mwanajeshi mmoja alisogea na kuanza kuuzima ule moto ili usije ukaleta madhara kwenye hiyo nyumba kwa ujumla lakini kipindi anaendelea na zoezi hilo, walisikia mlio wa risasi eneo la mbali na hiyo nyumba. Hiyo hali haikuwa ya kawaida kwenye eneo kama lile, ni eneo ambalo hakuna mtu mwingine angeweza kufika kwa wakati huo, ni eneo ambalo hakuna binadamu alikuwa na ujasiri wa kwenda kufanya hata utalii kwa sababu lilikuwa linatisha na liliaminika kwamba lilikuwa na viumbe hatari ndani yake, sasa wakati huo hiyo risasi ilipigwa na nani? Kiongozi wao ambaye ndiye alitoka kumuua yule mateka wao alitoka humo ndani kwenda nje kujua ni kipi kilikuwa kinaendelea.

Kutokana na baridi kali ambalo lilikuwa huko, watu wengine ambao walikuwa pale nje ambao nao walikuwa kwenye mavazi ya jeshi walikuwa wakiota moto huku yule mwanamke ambaye alionekana wazi kwamba hakupendezwa na kile ambacho kilikuwa kinafanyika pale akiwa amejitenga mwenyewe na kuegamia kwenye mti mmoja ambao ulikuwa karibu na pale ambapo wenzake walikuwa wakiota moto na kuchoma nyama. Wote ambao walikuwa nje waliusikia ule mlio wa risasi hivyo kila mtu alitahayari kutaka kujua kwamba ni kipi kilikuwa kinaendelea.
Hawakukaa tena bali kila mtu alisimama wakiwa wanaangaza huku na huko lakini hawakuona kitu ndipo mmoja wao alishtuka baada ya kuona kuna mwenzao amekosekana hilo eneo.
"Jordan yuko wapi?" yule aliyeshtuka aliuliza kwa wasiwasi akiwa anamwangalia kila mmoja wao usoni ili kuhakiki kuhusu huyo ambaye alikuwa anamuulizia.

"Alisema anataka kupunga upepo nje kidogo ya hapa hivyo aliingia huko msituni" sauti ya mmoja wao ndiyo ambayo iliamsha hisia ambazo hazikuwa sawa, kiongozi wao huyo aliinyanyua simu yake kupiga kwa kutumia radio call ambayo kila mmoja wao alikuwa anatembea nayo. Simu hiyo iliita mara tatu mfululizo bila kupokelewa, jambo hilo lilitoa ishara mbaya, hapakuwa pema hivyo alimtaka mwanamke yule ambaye hakuwa kwenye mood nzuri kuangalia kwa kutumia kumpyuta yake kujua huyo mwenzao yuko wapi kwa wakati huo.
Alikimbilia ndani na kuhaki mfumo wa mawasiliano kupitia kifaa cha mwenzao, alionekana kuwa mita miambili kutoka walipokuwa wao na kifaa hicho kilionekana kusimama sehemu moja bila kujongea, hawakuwa na muda wa kusubiri, kiongozi wao aliwataka wajiandae kwenye kuangalia hali ya mwenzao kwa sababu ukimya kama huo haukuwa utaratibu kwenye kazi yao, maana yake hakukuwa na usalama kwa mwenzao na walitakiwa kumsaidia kwa haraka kama kuna shida yoyote ingekuwa imempata.

Walitembea kwa umakini kwa dakika mbili ndipo walifika ile sehemu ambayo ilionyesha kwamba kulikuwa na kifaa cha mawasiliano cha mwenzao, kifaa kilikutwa kikiwa kwenye nyasi pembeni yake kukiwa na damu ambayo ilionyesha kuendelea kuelekea mbele ikabidi waifuate. Hatua kumi kutoka hapo ndiyo sehemu ambayo waliukuta mwili wa Jordan shingo yake ikiwa na alama za kutoboka na kichwa kikiwa kimepasuka kwa nyuma. Jordan alikuwa amekufa na kichwa chake kilionekana kujibamiza kwenye mti sehemu ambayo ilikuwa na damu na nywele kiasi. Bastola yake ilikuwa pembeni ya mwili wake, aliyekufa alikuwa ni miongoni mwa watu wa kuaminika vilivyo, kifo chake tena cha ghafla namna hiyo ni ishara kwamba walikuwa wameupokea ugeni ambao hawakuutarajia kwa sababu mtu ambaye aliwaleta ndani ya hilo eneo walitoka kumuua muda sio mrefu. Sasa huyo mtu mwingine ambaye aliingilia hiyo shughuli alikuwa ni nani? Ilizaliwa hofu na maswali ambayo hata wao hawakuelewa namna ya kuweza kuyapatia majibu yake.


"Kuna mtu mwingine ndani ya huu msitu na huenda mpaka muda huu anatuona kwa kila tunacho kifanya hapa" aliongea kiongozi wao huku akiwa anainama kuufanyia uchunguzi mwili wa mwenzake. Mwili ulikuwa bado wa moto, ni ishara kwamba ni muda mfupi; ulipita tangu mtu huyo aweze kuuawa, alitoa ishara ya vijana wake kuweza kutawanyika kwa ajili ya kumsaka mgeni ambaye alikuwa ameingia ndani ya msitu bila wao kuwa na taarifa na kuanza kuwapunguza.
Yalikuwa ni majira ya jioni jua likiwa linazama hivyo chini ya msitu kulikuwa na mwanga kwa mbali ambao kadri dakika zilivyokuwa zinasonga ulikuwa unafifia taratibu. Mwanajeshi mmoja akiwa anatembea, alishangaa kuna shilingi ya zamani ambayo ilikuwa inang'aa ikitua mbele ya macho yake.

Hakuelewa ilirushwa na nani na ilitokea wapi hivyo alisogea ili kuweza kuyashuhudia hayo maajabu, akiwa ameikaribia na kuinama ili aipate mwili wake ulihisi uzito ambao haukuwa wake, akajua kabisa kwamba kulikuwa na ongezeko la mtu mwingine karibu yake. Aligeuka haraka akiwa ameinyoosha bastola yake ila hakuona kitu ikamlazimu kuyarudisha macho yake haraka kwenye ile shilingi ambayo ilikuwa nyuma yake.
Wakati anageuka alikutana na kitu cha ajabu, alifanikiwa kuyafungua macho yake mara moja tu pekee, kwa sababu ile shilingi hakuiona tena na alipo jaribu kuweza kuangalia alihisi kama kuna kivuli ndipo akayafumbua macho yake baada ya kuhisi kulikuwa na kivuli kutokea juu kwenye mti. Ni kweli kuna mwanaume alikuwa amenasa kwenye mti kwa kutumia miguu yake huku mikono ikiwa imeleelekezwa chini. Wakati anapata mshtuko, alihitaji kuielekezea bastola yake kuelekea kwa yule mtu, kwa bahati mbaya kidole kilizama kwenye koromeo lake na kulivunja, alirudi nyuma akiwa ameishika shingo yale ila hakumaliza hata sekunde tano, alikufa baada ya ile shilingi kuzamishwa kwenye paji yake la uso na kifua kilivunjwa kwa ngumi ambayo ilimgandamiza kwenye ule mti kiasi kwamba hata mifupa ya uti wake wa mgongo ikavunjika vibaya.

Ukimya wake uliokithiri ndio ambao ulimsogeza yule mwanamke ambaye alikuwa mtaalamu wa kompyuta karibu na eneo hilo, aliitoa sauti ya mshtuko huku moyo wake ukianza kwenda na kupiga kwa nguvu. Hakutarajia kukutana na kitu kama hicho kwa mara nyingine tena, ni muda mfupi walitoka kushuhudia mwili wa Jordan lakini haikuchukua muda mwingine tena mwenzao alikuwa ameuliwa kikatili kama mwanzo lakini huyo wa pili kwenye paji lake la uso iliachwa shilingi ambayo ilibaki imeshikilia hapo ikiwa inang'aa isivyokuwa kawaida.

Ile hofu yake ilimfanya aanze kurudi nyuma huku akiwa anaitoa simu yake mfukoni baada ya kugundua kwamba hata kile kifaa cha mawasiliano kwenye sikio lake hakikuwepo huenda ni kwa sababu alikisahau kule kwenye kumpyuta. Alisimama na kujibanza kwenye mti baada ya kuhisi kama kuna kitu kilikuwa kimempita kwa kasi nyuma ya alipokuwepo yeye, jambo hilo alihisi ni ndoto ila aliamini kwamba ni kweli baada ya kuiona ile simu yake ambayo alikuwa ameishika mkononi ikiwa imepasuka baada ya kubamizwa kwenye mti. Lilikuwa ni jambo la haraka kufanyika kiasi kwamba yeye mwenyewe alibaki anashangaa asijue tukio hilo lilitokeaje na kwanini aliyelifanya hakumdhuru yeye? Hakuwa na muda wa kusubiri zaidi ya kuanza kukimbia kuelekea upande ambao walikuwepo wenzao wakiwa wanaendelea kumsaka mtu ambaye bila shaka naye alikuwa anawasaka ndani ya msitu huo mzito.

Ndiyo kwanza tunaifungua sehemu ya kwanza kabisa ya simulizi hii, ungana nami mpaka mwisho ili tuweze kwenda sawa pamoja.

FEBIANI BABUYA.View attachment 3168470
"Akayatemna meno mawili kwa ghadhabu.. " Hapo tu broo pamenifanya niipende story nzima.... Kazi nzuri mtunzi
 
Back
Top Bottom