FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #241
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
SONGA NAYO................
*********
Mr George, raisi wa Tanzania alikuwa na siku ndefu mno, ni siku ambayo alimpoteza mkewe kipenzi, siku ambayo alienda kukutana na yule mwanamama Aurelia lakini huko akaishia kukutana na mambo ya ajabu. Ni wakati ambao hakuwa anampata hata mkurugenzi wa usalama wa taifa jambo ambalo halikuonyesha usalama wala hali ya kueleweka kwa upande wake.
Lakini pia muda ulikuwa umeenda mno akiwa kwenye ofisi yake kusubiri majibu ambayo hakuwa na uhakika tena kama atayapata. Aliwatuma vijana wake waende kumchukua mwanamama huyo huko Yombo lakini mpaka wakati huo hakukuwa na majibu yoyote ambayo yalipatikana. Alikuwa anampigia simu mlinzi wake bila mafanikio yoyote yale mpaka akahisi kuchanganyikiwa, mwili ulikuwa una joto jingi, hakuna kitu kilikuwa kinaenda kama alivyo hitaji yeye.
Simu pekee ambazo alikuwa anazipata wakati huo zilikuwa za viongozi wakubwa wa mataifa mengine ambao walikuwa wanampa pole kwa kumpoteza mkewe huku wengine wakiwa wanaahidi kuweza kufika msibani na wengine walidai wangetuma wawakilishi kwa ajili ya kuja kumfariji. Hayo yote hakuyajali kabisa kwa sababu kwa wakati huo hayakuonekana kuwa ya mhimu hali ambayo ilimfanya kuzima kabisa simu zote hizo za ofisi. Aliifungua pombe na kuimimina kwenye bilauri akiwa mwingi wa jazba tena mwenyewe, alikuwa anatamani kumpata mtu wa kuweza kumaliza hizo hasira zake lakini hakumpata.
Akiwa kwenye hizo hasira nyingi mheshimiwa ndipo alipata simu ambayo iliingia kwenye namba yake binafsi ambayo ndiyo pekee hakuwa anaizima hata siku moja, mtu ambaye alimpigia muda huo alikuwa na hasira naye kali mno ambazo asingeweza hata kuzielezea kwa lugha ya kawaida. Othman Micho, mkurugenzi wa shirika lake la TIGI ndiye ambaye alikuwa anampigia simu wakati huo. Alisonya kwa sauti kubwa na kuipokea simu hiyo, bwana huyo alimwambia kwamba ndani ya dakika kumi na tano angekuwa anaingia hapo Ikulu kwa sababu alikuwa na mambo ya mhimu ya kuzungumza na bosi wake.
Kwake ilikuwa ni habari njema kwa sababu alikuwa ana usongo mkubwa na huyo bwana, alihisi huyo alikuwa moja ya watu ambao waliisababisha hali ya hatari kuweza kutokea kwa mke we hivyo alihitaji kumalizia hasira kwake na kama ingewezekana angeweza kumuondoa kwenye hiyo nafasi.
“Othman kipindi nakupa hii nafasi uliapa kulilinda taifa hili kwa gharama yoyote na kuhakikisha amani muda wote, kwenye kulilinda taifa, moja kati ya majukumu yako makubwa ni kuweza kumlinda raisi wako pamoja na familia yake kwa ujumla. Lakini leo hii mke wangu amepigwa risasi alasiri, kwenye simu hupatikani mpaka unakuja wakati kama huu ambao mimi nipo kwenye majonzi makubwa. Unaweza ukaniambia labda ulikuwa wapi na kuna sababu zipi za msingi ambazo zitanishawishi mimi kuendelea kukuweka wewe kwenye hiyo nafasi mpaka muda huu?”
“Kwanza nikupe pole kwa kuweza kumpoteza first lady, huu msiba sio wako tu bali ni msiba wa taifa zima lakini hata hivi sipo hapa kukuomba msamaha mheshimiwa juu ya kile ambacho kimetokea alasiri ya leo”
“Umesema?”
“Mimi na shirika langu kwa ujumla hatuhusiki kwa lolote lile kwa sababu wewe una kitengo binafsi ambacho kinakulinda hivyo hao ndio ambao walitakiwa kuwajibika kwa namna moja ama nyingine sijajua kwa sababu gani unataka kuona kama mimi ndiye mhusika mkuu kwenye hili jambo”
“Naona umeanza kunikosea heshima siku hizi Othman, unakumbuka mahali nilipo kutoa?”
“Naheshimu hilo la wewe kunipa nafasi hii kubwa kuweza kulitumikia taifa langu ila sidhani kama ni sababu tosha ya kufanya mimi kuwa mhusika wa kila jambo hususani sehemu ambayo sitakiwi kupewa lawama”
“Unajua Othman wahenga walikuwa na maana kubwa kusema kwamba kuku akiwa mgeni unatakiwa kumfunga kamba mguuni kwa sababu kama akipotea kuna nafasi ndogo ya yeye kupatikana tena lakini ikitokea siku kuku huyo akayazoea mazingira basi mara nyingi unamuamini kwa sababu unajua hata kama ataenda wapi bado ni lazima tu atarudi nyumbani. Umeshakuwa kuku mwenyeji hivyo sikuwa na mashaka na wewe ndiyo maana sikutaka kukufunga kamba mguuni lakini naanza kuona sehemu ambayo nilifeli mimi kama raisi wa hili taifa”
“Mheshimiwa samahani, unamaanisha kwamba ulikuwa unataka kuanza kunichunguza mimi”
“Mpaka sasa unatakiwa kuchunguzwa kwa sababu sina imani kama naweza kukuamini tena Othman” mkurugenzi alijisikia hasira kali mno, ni siku hiyo ambayo alitoka kuhakikishiwa kwamba hata huyo raisi alikuwa ni miongoni mwa wale washenzi ambao walikuwa wanalihujumu taifa ambalo yeye alikuwa analipambania halafu muda huo alikuwa anaambiwa ujinga na raisi huyo huyo.
“Mimi niliapa kukulinda wewe kupitia hatari za nje, niliapa kulilinda taifa hili na kulipigania pindi liingiapo kwenye hatari kubwa lakini hakuna sehemu hata moja ambayo niliapa kuyalinda maslahi ya mtu binafsi mheshimiwa, hili ni jambo ambalo hautakiwi kulisahau hata siku moja unapo ingia ndani ya ofisi yako”
“Whaaaaat! Unamaanisha kumlinda mke wangu ni kuyalinda maslahi binafsi? Unatamani kufa Othman?” raisi alifoka kwa hasira macho yakiwa mekundu vibaya mno.
“Huenda upo sahihi kuniambia kwamba mimi nilikuwa kuku mgeni ila kwa sasa nimekuwa mwenyeji, najitawala, nastahili kufungwa kamba tena jambo ambalo mimi na wewe wote tunajua kabisa kwamba haliwezi kutokea mheshimiwa labda kama utaamua kuyatumia madaraka yako vibaya kulazimisha hilo sawa kwa sababu wewe ni raisi unaweza kufanya hilo. Lakini jambo la msingi ambalo limenileta hapa sio kifo cha mke wako bali sababu iliyo nyuma ya kifo chake inaweza kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na maisha yako binafsi”
“Unataka kusemaje Othman?”
“Kuna mambo mengi ya hovyo ambayo huwa unayafanya ila huwa siwezi hata kukwambia kwa sababu wewe ndiye bosi wa taifa hili, najua unaweza kufanya lolote utakalo kwa sababu taifa ni lako lakini mambo yote hayo mimi huwa nakulinda na mara kadhaa nimetengeneza mpaka taarifa za uongo kwenye vyombo vya habari ili uwe salama na jina lako lisiwe baya kwa wananchi ila kilicho nileta leo hapa kwako ni kutaka kujua kama kuna mambo yako binafsi ambayo unahisi kwamba siyajui na napaswa kuyafahamu kabla mambo hayajaharibika zaidi ya hapa kwa sababu bila kujua kumbuka sitakuwa na uwezo wa kukulinda lolote likitokea na lawama zitakuja kwangu kama ambavyo wewe unanilaumu hapa”
“Kuna kitu gani ambacho unakifahamu Othman kuhusu mimi?”
“Ndiyo maana nipo hapa ili niweze kukifahamu kutoka kwako mwenyewe”
“Umekutana na nani ambaye amekulisha hii sumu?”
“Kama ningelishwa sumu basi nisingekuwa hapa muda huu mheshimiwa, nimekuja kukwambia na kutaka kujua ukweli kwa sababu inaweza kuwa njia pekee ya sisi kumaliza jambo hili. Najua viongozi wengine wanaogopa kukwambia ukweli kwa sababu unaweza ukazibeba nafasi zao ama kuwaua, mimi nipo tayari kwa hilo ila sipo tayari taifa liangamie kwenye mikono yangu nikiwa natazama, watu wanakufa kila siku, mauaji imekuwa kama kawaida siku hizi, viongozi kila siku wanapotea kwa sababu ya makosa ambayo yalifanywa huko nyuma ndiyo maana nataka kujua kama kuna jambo ambalo silijui kuhusu wewe napaswa kulijua ili nianze upya hesabu zangu kuhakikisha nalirudisha taifa kwenye hali yake ya mwanzo”
“Unataka kuniambia unahisi raisi wa nchi nahusika kulihujumu taifa langu mwenyewe?”
“Hakuna sehemu ambayo nimetamka hivyo mheshimiwa”
“Ila una maana gani kuja kunidhalilisha na kunianza kunisanifu wakati mke wangu ndo kwanza hata hajapumzishwa?”
“Kwa sababu ndiyo njia pakee ya kulirudisha taifa kwenye njia yake ya mwanzo na hii inaweza kuwa namna bora ya kumfanya mkeo akapumzika kwa amani” Raisi alicheka kwa sauti kubwa, mezani kwake kulikuwa na bastola, aliibeba na kumnyooshea kiongozi huyo wa usalama ndani ya taifa lake.
54 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
SONGA NAYO................
*********
Mr George, raisi wa Tanzania alikuwa na siku ndefu mno, ni siku ambayo alimpoteza mkewe kipenzi, siku ambayo alienda kukutana na yule mwanamama Aurelia lakini huko akaishia kukutana na mambo ya ajabu. Ni wakati ambao hakuwa anampata hata mkurugenzi wa usalama wa taifa jambo ambalo halikuonyesha usalama wala hali ya kueleweka kwa upande wake.
Lakini pia muda ulikuwa umeenda mno akiwa kwenye ofisi yake kusubiri majibu ambayo hakuwa na uhakika tena kama atayapata. Aliwatuma vijana wake waende kumchukua mwanamama huyo huko Yombo lakini mpaka wakati huo hakukuwa na majibu yoyote ambayo yalipatikana. Alikuwa anampigia simu mlinzi wake bila mafanikio yoyote yale mpaka akahisi kuchanganyikiwa, mwili ulikuwa una joto jingi, hakuna kitu kilikuwa kinaenda kama alivyo hitaji yeye.
Simu pekee ambazo alikuwa anazipata wakati huo zilikuwa za viongozi wakubwa wa mataifa mengine ambao walikuwa wanampa pole kwa kumpoteza mkewe huku wengine wakiwa wanaahidi kuweza kufika msibani na wengine walidai wangetuma wawakilishi kwa ajili ya kuja kumfariji. Hayo yote hakuyajali kabisa kwa sababu kwa wakati huo hayakuonekana kuwa ya mhimu hali ambayo ilimfanya kuzima kabisa simu zote hizo za ofisi. Aliifungua pombe na kuimimina kwenye bilauri akiwa mwingi wa jazba tena mwenyewe, alikuwa anatamani kumpata mtu wa kuweza kumaliza hizo hasira zake lakini hakumpata.
Akiwa kwenye hizo hasira nyingi mheshimiwa ndipo alipata simu ambayo iliingia kwenye namba yake binafsi ambayo ndiyo pekee hakuwa anaizima hata siku moja, mtu ambaye alimpigia muda huo alikuwa na hasira naye kali mno ambazo asingeweza hata kuzielezea kwa lugha ya kawaida. Othman Micho, mkurugenzi wa shirika lake la TIGI ndiye ambaye alikuwa anampigia simu wakati huo. Alisonya kwa sauti kubwa na kuipokea simu hiyo, bwana huyo alimwambia kwamba ndani ya dakika kumi na tano angekuwa anaingia hapo Ikulu kwa sababu alikuwa na mambo ya mhimu ya kuzungumza na bosi wake.
Kwake ilikuwa ni habari njema kwa sababu alikuwa ana usongo mkubwa na huyo bwana, alihisi huyo alikuwa moja ya watu ambao waliisababisha hali ya hatari kuweza kutokea kwa mke we hivyo alihitaji kumalizia hasira kwake na kama ingewezekana angeweza kumuondoa kwenye hiyo nafasi.
“Othman kipindi nakupa hii nafasi uliapa kulilinda taifa hili kwa gharama yoyote na kuhakikisha amani muda wote, kwenye kulilinda taifa, moja kati ya majukumu yako makubwa ni kuweza kumlinda raisi wako pamoja na familia yake kwa ujumla. Lakini leo hii mke wangu amepigwa risasi alasiri, kwenye simu hupatikani mpaka unakuja wakati kama huu ambao mimi nipo kwenye majonzi makubwa. Unaweza ukaniambia labda ulikuwa wapi na kuna sababu zipi za msingi ambazo zitanishawishi mimi kuendelea kukuweka wewe kwenye hiyo nafasi mpaka muda huu?”
“Kwanza nikupe pole kwa kuweza kumpoteza first lady, huu msiba sio wako tu bali ni msiba wa taifa zima lakini hata hivi sipo hapa kukuomba msamaha mheshimiwa juu ya kile ambacho kimetokea alasiri ya leo”
“Umesema?”
“Mimi na shirika langu kwa ujumla hatuhusiki kwa lolote lile kwa sababu wewe una kitengo binafsi ambacho kinakulinda hivyo hao ndio ambao walitakiwa kuwajibika kwa namna moja ama nyingine sijajua kwa sababu gani unataka kuona kama mimi ndiye mhusika mkuu kwenye hili jambo”
“Naona umeanza kunikosea heshima siku hizi Othman, unakumbuka mahali nilipo kutoa?”
“Naheshimu hilo la wewe kunipa nafasi hii kubwa kuweza kulitumikia taifa langu ila sidhani kama ni sababu tosha ya kufanya mimi kuwa mhusika wa kila jambo hususani sehemu ambayo sitakiwi kupewa lawama”
“Unajua Othman wahenga walikuwa na maana kubwa kusema kwamba kuku akiwa mgeni unatakiwa kumfunga kamba mguuni kwa sababu kama akipotea kuna nafasi ndogo ya yeye kupatikana tena lakini ikitokea siku kuku huyo akayazoea mazingira basi mara nyingi unamuamini kwa sababu unajua hata kama ataenda wapi bado ni lazima tu atarudi nyumbani. Umeshakuwa kuku mwenyeji hivyo sikuwa na mashaka na wewe ndiyo maana sikutaka kukufunga kamba mguuni lakini naanza kuona sehemu ambayo nilifeli mimi kama raisi wa hili taifa”
“Mheshimiwa samahani, unamaanisha kwamba ulikuwa unataka kuanza kunichunguza mimi”
“Mpaka sasa unatakiwa kuchunguzwa kwa sababu sina imani kama naweza kukuamini tena Othman” mkurugenzi alijisikia hasira kali mno, ni siku hiyo ambayo alitoka kuhakikishiwa kwamba hata huyo raisi alikuwa ni miongoni mwa wale washenzi ambao walikuwa wanalihujumu taifa ambalo yeye alikuwa analipambania halafu muda huo alikuwa anaambiwa ujinga na raisi huyo huyo.
“Mimi niliapa kukulinda wewe kupitia hatari za nje, niliapa kulilinda taifa hili na kulipigania pindi liingiapo kwenye hatari kubwa lakini hakuna sehemu hata moja ambayo niliapa kuyalinda maslahi ya mtu binafsi mheshimiwa, hili ni jambo ambalo hautakiwi kulisahau hata siku moja unapo ingia ndani ya ofisi yako”
“Whaaaaat! Unamaanisha kumlinda mke wangu ni kuyalinda maslahi binafsi? Unatamani kufa Othman?” raisi alifoka kwa hasira macho yakiwa mekundu vibaya mno.
“Huenda upo sahihi kuniambia kwamba mimi nilikuwa kuku mgeni ila kwa sasa nimekuwa mwenyeji, najitawala, nastahili kufungwa kamba tena jambo ambalo mimi na wewe wote tunajua kabisa kwamba haliwezi kutokea mheshimiwa labda kama utaamua kuyatumia madaraka yako vibaya kulazimisha hilo sawa kwa sababu wewe ni raisi unaweza kufanya hilo. Lakini jambo la msingi ambalo limenileta hapa sio kifo cha mke wako bali sababu iliyo nyuma ya kifo chake inaweza kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na maisha yako binafsi”
“Unataka kusemaje Othman?”
“Kuna mambo mengi ya hovyo ambayo huwa unayafanya ila huwa siwezi hata kukwambia kwa sababu wewe ndiye bosi wa taifa hili, najua unaweza kufanya lolote utakalo kwa sababu taifa ni lako lakini mambo yote hayo mimi huwa nakulinda na mara kadhaa nimetengeneza mpaka taarifa za uongo kwenye vyombo vya habari ili uwe salama na jina lako lisiwe baya kwa wananchi ila kilicho nileta leo hapa kwako ni kutaka kujua kama kuna mambo yako binafsi ambayo unahisi kwamba siyajui na napaswa kuyafahamu kabla mambo hayajaharibika zaidi ya hapa kwa sababu bila kujua kumbuka sitakuwa na uwezo wa kukulinda lolote likitokea na lawama zitakuja kwangu kama ambavyo wewe unanilaumu hapa”
“Kuna kitu gani ambacho unakifahamu Othman kuhusu mimi?”
“Ndiyo maana nipo hapa ili niweze kukifahamu kutoka kwako mwenyewe”
“Umekutana na nani ambaye amekulisha hii sumu?”
“Kama ningelishwa sumu basi nisingekuwa hapa muda huu mheshimiwa, nimekuja kukwambia na kutaka kujua ukweli kwa sababu inaweza kuwa njia pekee ya sisi kumaliza jambo hili. Najua viongozi wengine wanaogopa kukwambia ukweli kwa sababu unaweza ukazibeba nafasi zao ama kuwaua, mimi nipo tayari kwa hilo ila sipo tayari taifa liangamie kwenye mikono yangu nikiwa natazama, watu wanakufa kila siku, mauaji imekuwa kama kawaida siku hizi, viongozi kila siku wanapotea kwa sababu ya makosa ambayo yalifanywa huko nyuma ndiyo maana nataka kujua kama kuna jambo ambalo silijui kuhusu wewe napaswa kulijua ili nianze upya hesabu zangu kuhakikisha nalirudisha taifa kwenye hali yake ya mwanzo”
“Unataka kuniambia unahisi raisi wa nchi nahusika kulihujumu taifa langu mwenyewe?”
“Hakuna sehemu ambayo nimetamka hivyo mheshimiwa”
“Ila una maana gani kuja kunidhalilisha na kunianza kunisanifu wakati mke wangu ndo kwanza hata hajapumzishwa?”
“Kwa sababu ndiyo njia pakee ya kulirudisha taifa kwenye njia yake ya mwanzo na hii inaweza kuwa namna bora ya kumfanya mkeo akapumzika kwa amani” Raisi alicheka kwa sauti kubwa, mezani kwake kulikuwa na bastola, aliibeba na kumnyooshea kiongozi huyo wa usalama ndani ya taifa lake.
54 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.