STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA HAMSINI NA NANE
SONGA NAYO................
“Wewe ni nani bibie na kwanini nipo hapa kinguvu?”
“Usiwe na haraka ya kuhitaji kunijua mimi, kwanza nataka nikukumbushe historia yako. Miaka kumi na mitano iliyopita wewe uliingia kwenye orodha ya majina ya wahalifu ambao walikuwa wanatafutwa sana kwenye taifa hili, unakumbuka ni kwanini uliingia huko?” Dayana swali lake lilikuwa la mtego lakini tajiri huyo lilimchanganya, hakuelewa binti huyo alikuwa na maana ipi kuuliza hilo swali.
“Kwanza natakiwa kujua nipo wapi, bila shaka kwa swali lako wewe ni mtu wa usalama na unajua kabisa ni kosa kisheria mimi kuwa hapa bila taarifa hivyo kama kuna ulazima wa mimi kuongea na wewe hakikisha unampigia simu mwanasheria wangu”
“Uhalifu wako ulikuwa ukihusiana na wewe kuhusika kwenye biashara haramu ya kusafirisha viungo vya binadamu na kutakatisha fedha. Kesi hii iliibuliwa na afisa mmoja wa polisi Zanzibar ambaye alikujulikana kwa jina la Ashrafu, hii kesi baadae ikaja kufutwa kwa amri ya jaji mkuu Emilia Clark ambaye ameuawa kwa sasa. Lakini haukuishia hapo bali pia ulimuua yule afisa wa polisi na familia yake yote kwa kukuingiza kwenye skendo chafu, kwa sababu bado jaji mkuu alikuwa upande wenu basi ile kesi hakuna mahali ilipelekwa, mzalendo yule akakosa haki yake ya msingi na kuishia kufa halafu mpuuzi mmoja kama wewe upo mpaka leo unadunda. Unaelewa maana ya haya yote?” Dayana alilipuuzia swali la tajiri huyo na kumpa machache kuhusu yeye ambayo alikuwa akiyafahamu
“Hahaha hahahaha hahaha bibie nina imani utakuwa haupo timamu kuanza kutengeneza kesi zote hizo ambazo hazina uhalisia wowote na hazijawahi kunitokea kwenye maisha yangu yote. Kama ningekuwa nafanya haya mambo basi mpaka leo nisingekuwa uraiani muda huu”
“Sipo hapa kutaka ukubali kuhusu hilo, jambo ambalo nalihitaji ni muunganiko wa haya mambo kwa sababu kwa hesabu zangu ni kwamba hata wewe umebakisha siku kadhaa tu jina lako liweze kubadilika kuwa marehemu”
“Unanitisha mimi?”
“Wala sikutishi, nipo hapa kutaka kujua ukweli ambao unaweza kuwa msaada wa kukulinda hata wewe pia”
“Hahahaha hahahaa hahah wewe hapo ndo unadai unataka kunilinda mimi?”
“Naonekaan kama nakuchekesha mzee?”
“Huna lolote binti, wewe muda huu ulitakiwa uwe unamkatia kiuno bwana yako kitandani” hiyo kauli ilimuuma sana Dayana, alinyanyuka na kwenda kuufunga mlango, wakati anafunga wenzake walishtuka na kuhitaji kuuwahi lakini walichelewa. Alisogea kwenye kamera na kuiangalia kwa umakini akijua wazi kwamba wenzake walikuwa wakimtazama kwa nje, alivuta kisanduku kimoja na kwenda kukitua pale mezani hali ambayo ilianza kumpa mashaka Ismail.
“Ni kweli mzee wangu, huenda mimi natakiwa kuwepo kitandani kumkatia bwana angu viuno muda huu lakini kwa bahati mbaya mimi ni miongoni mwa watu wachache ambao hawalali kuhakikisha tu taifa linakuwa salama kutoka kwa watu wazandiki kama wewe. Unajua kwanini nimefunga ule mlango?” aliongea akiwa anamzunguka zunguka mzee yule ambaye hakuwa na jibu la kuweza kumpa.
“Kwa sababu mimi huwa sijui mambo ya fair Play, habari za viungo kwenye mpira mimi sina hizo mambo. Kuna watu wanatutazama nje hapo, wale wanajua kabisa njia ambazo huwa nazitumia kupata kile nakitaka kwa mtu na njia zangu hazijawahi kuwa na mwisho mwema hivyo kama mlango ungebaki kuwa wazi maana yake ni kwamba wangekuja hapa kunizuia nisikuumize ila kwa sasa hawawezi kuingia tena humu ndani mpaka nimalize kazi yangu na kama watatumia njia ya ziada basi ni dakika thelathini ambazo bila shaka mimi na wewe tutakuwa tumemaliza mazungumzo yetu kwa sababu natarajia yatakuwa mafupi na sahihi”
“Bibie una familia au mtoto labda?”
“Ndiyo njia ambayo huwa mnaitumia kutishia watu ambao wanaingia kwenye maslahi yenu sio?”
“Kwa sababu nitakifuta kizazi chako chote, haujui aina ya watu ambao unaingia nao kwenye hii ligi bibie, bosi wa bosi wako analijua hili ndiyo maana wenzako wamekaa pembeni muda wote sio kwamba hawajui ila wanaheshimu mipaka ambayo wamewekewa. Jiangalie kwa sababu kuna wanaume wana hamu ya kuwaingilia wanawake wa aina yako. Hahaha hahahah hahahaa” bwana huyo licha ya kuonekana kuwa mtu wa dini lakini bila shaka ndani yake kulikuwa na ushenzi ulio tukuka na wakati huo alianza kuudhihirisha waziwazi.
“Utatamani ungenisikiliza mapema” Dayana aliongea akiwa analivua koti lake na kuliweka ukutani na kuikunja shati yake. Mzee huyo hakuwa anamjua mwanamke huyo, huenda angeelewa sababu ya yeye kuwa ndiye kiongozi wa kundi lililo jaa wanaume basi angekuwa anaongea naye kwa heshima kubwa. Dunia ilikuwa inaenda kumpa somo la maisha.
Dayana alichomoa praizi na mkasi, alimwangalia mzee huyo usoni akiwa anatabasamu, mzee huyo naye alikuwa anamwangalia kwa dharau lakini sura yake ilibadilika ghafla baada ya kushtukizwa bila kutarajia. Mkasi ulizama kwenye kidole kwa nguvu kama mtu anausimika kwenye udongo, praizi ilizamishwa kwenye kucha na kuanza kuing’oa kwa lazima huku akiwa anazungusha zungusha ili kumpatia maumivu. Mzee Ismail alipiga makelele kama mtoto mdogo mpaka inang’ooka alikuwa ameshusha machozi na kamasi zilikuwa zinachuruzika.
Dayana aliviweka vyote mezani na kusogea nyuma akainamia kwenye siko la mzee huyo.
“Bila shaka kwa sasa tunaweza kusikilizana vizuri na kuongea kiutu uzima sasa maana tulikuwa hatujuani mwanzo na sikulaumu kwa hilo” aliongea akiwa anairushia mezani picha kubwa, sura ilikuwa ni ya Gavin Luca, mzee huyo alipatwa na wasiwasi mwingi baada ya kuiona hiyo picha mbele yake.
“Ninajua kwamba wewe ni miongoni mwa wahusika ambao wanatafutwa sana na huyo bwana, kuna mambo ambayo mliyafanya miaka ya nyuma huko ambayo mliudanganya ulimwengu na watu wakawaamini. Leo hii kupitia mambo hayo mmejichumia utajiri wa kutosha lakini mwenye vyake amekuja kukusanya kila deni ambalo mlilikopa wakati huo sasa nina mambo machache ambayo nahitaji kuyajua kwako” Dayana alikuwa amebadilika mpaka sura, alitulia na kumsoma mzee huyo usoni ambaye alikuwa ana presha, ilionekana kwa jinsi alivyokuwa akizivuta pumzi zake.
“Nataka kujua kwamba ni nani anayefuata baada ya hapa, nataka kujua aliye muua Emilia, nataka kuijua sababu ya msingi ya wewe kuwa hai mpaka sasa wakati huna ulinzi wowote wa maana na nataka kujua sababu ya kwanini mtu huyo alimuua binti yako na sio wewe” maswali yalikuwa yanaeleweka vizuri na hata mzee huyo aliyasikia kwa usahihi kabisa.
“Nasikitika kwamba hakuna swali hata moja ambalo naweza kukujibu hapa binti yangu”
“Mimi sio binti yako, unahisi nipo hapa kukubembeleza?”
“Hayo maswali yapo nje ya uwezo wangu”
“Inaonekana haupendi amani kabisa” Dayana aliongea akiwa anatoa mashine ndogo ya kutindulia, ilikuwa inaweza kutindua hata miamba, ilitakiwa kuzama kwenye mwili wa mzee huyo. Alibaki akihaha na kuhema kwa nguvu kwa sababu alijua hatua zilizokuwa zinafuta.
“Kama nikisema lolote basi lazima nife na familia yangu itauawa”
“Hakuna mtu atajua kuhusu hili, haya ni makubaliano ambayo wewe unaingia na shirika la kijasusi la taifa hili”
“Hauelewi binti, hawa watu wapo kila sehemu, wapo na watu kila kona ya sehemu nyeti kwenye taifa hili hata humu ndani huenda lazima kuna mmoja wao yupo nao sasa unaniaminisha vipi kwamba hili litabaki baina yangu mimi na wewe? Sioni kama hili lina maana yoyote kwa sasa”
“Kama ni hivyo basi hakuna haja ya makubaliano na mimi, utatakiwa kusema tu kwa sababu hauna chaguo, kumbuka kwamba hakuna mtu hata mmoja ambaye anajua kwamba wewe upo hapa hivyo tunaweza kukufanya lolote lile”
“Una uhakika kwamba hakuna mtu anajua kwamba nipo hapa?” ile kauli ilimshtua Dayana, ni kama hakumuelewa mzee yule.
“Una kifaa kwenye mwili wako?”
“Ndiyo, yakipita masaa saba bila kujulikana kwamba niko wapi basi lazima nitaanza kutafutwa na hapo watajua sehemu nilipo” Dayana alitabasamu, wau hao walikuwa wamejipanga kwa kila kitu.
“Safi kabisa kwa sababu bado kuna masaa matatu mpaka watu hao waweze kukushtukia kwamba haupo, kwa maana hiyo mimi na wewe tuna muda mrefu wa kuwa pamoja humu ndani” mzee huyo alimeza mate kwa shida kubwa akiwa hana ujanja zaidi ya kutoa ushirikiano kwa watu hao.
58 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.