Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

𝗧𝗛𝗘 𝗠𝗢𝗗𝗘𝗥𝗡 𝗪𝗔𝗥
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........09
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

09-(TINO vs ARON)

𝗜𝗟𝗜𝗣𝗢𝗜𝗦𝗛𝗜𝗔...
"Anna yuko wapi" Inspekta Aron aliuliza bila hata kusalimia, askari wake wakatazamana
"Yuko ndani mkuu" mmoja akajibu
Inspekta Aron alisukuma mlango na kuingia ndani kwa kasi macho yake akayatupa kitandani moja kwa moja.

𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔...

Annah alikuwepo kitandani tena alikuwa tayari amerejesha fahamu zake
"Annah upo sawa" Inspekta Aron aliuliza huku akisogea taratibu pale kitandani
"Mkuu daktari alituambia tusiruhusu mtu kuingia bila kuvaa PPE ni hatari kwa mgonjwa" mmoja wa askari aliongea akiwa amesimama mlangoni

"Najua usijali" Alisema Inspekta Aron huku akiinama na kushikiria magoti akaanza kuvuta na kutoa pumzi kwa nguvu, hakika alikuwa amechoka sana baada ya kukimbia kwa muda mrefu. Wakati ameinama akili yake ilikuwa ikifanya kazi, aliwaza kuhusu kaka yake Tino ambaye anao uhakika yupo ndani ya hospitali hiyo.

"Yuko wapi huyu? au amekuja kumuona mama, mbona sio kawaida yake" aliwaza Inspekta Aron akihisi labda Tino amekuja kumuona mama yao ambaye amelazwa hospitalini hapo tangu mda mrefu.

"Naitwa Aron mimi ni polisi mpelelezi, nipo hapa kwa ajili yako Annah pole kwa yaliyokukuta lakini usijali uko salama nikirudi tutaongea vizuri kwa sasa pumzika kwanza" Inspekta Aron alijieza kwa kifupi kisha akaanza kutoka

"Po..polisi" Annah aliita kwa taabu kidogo huku akiinuka na kukaa pale kitandani, Inspekta Aron aliyekuwa amefika mlangoni alisimama na kugeuka.
"Nakuomba mara moja" alisema Annah kwa sauti ya chini akimtaka Inspekta Aron asogee, akafanya hivyo.

Inspekta Aron akasogea na kukaa kitandani pembeni ya Annah na hapo ndipo alipopata wasaa wa kumtazama binti huyo kwa ukaribu zaidi, alikuwa ni mzuri sana licha ya uso wake kuonekana wenye majonzi baada ya kulia kwa muda mrefu lakini haikuwa sababu ya kuuficha uzuri wake, Annah alijaliwa mashallah.

"Eti ni kweli baba na mama yangu wamekufa yaani hawapo tena Duniani?" Annah aliuliza swali huku akishindwa kuyazuia machozi yaliyoanza kumtiririka kama maji kwa mara nyingine.
Inspekta Aron alijikuta anaingia kwenye jukumu lingine la kumbembeleza anyamaze, ni kweli Annah alikuwa katika simanzi nzito sana. Kumbukumbu ya wazazi wake wakiuwawa kikatili mbele ya macho yake ilimganda kichwani, kila alipofumba na kufumbua macho yake taswira ile ilimrudia. Annah alilia, alilia sana akiwalilia wazazi wake wakati huo akiwa amejilaza kwenye kifua cha Inspekta Aron aliyekuwa akimpiga piga mgongoni kumfariji.

"Annah ilikuwa na wewe ufe, walidhamiria kukua pia lakini mungu amekunusuru kwa makusudi kabisa ili tu uwawajibishe wote waliohusika kufanya unyama huu. Annah usiogope, upo na mimi nitakulinda hadi siku utakapopata haki yako" Inspekta Aron alijaribu kutoa maneno ya faraja kwa Anna.

"Lakini kwa nini, kwa nini yule Waziri wa afya ni katili kiasi hiki sisi tulimkosea nini, ee Mungu wangu kwa nini umenipa adhabu hii baba nitawezaje kuishi yatima mimi aaa.." Annah alilia
"Okay kwa hiyo unataka kusema miongoni mwa watu waliotekeleza mauji haya waziri wa afya alikuwepo?" Aliuliza Inspekta Aron
Annah akatikisa kichwa kukubali.
"Unahakika, ulimuona?"
Annah akatikisa kichwa chake tena kukubali.
Hizi zilikuwa ni habari njema sana kwa Inspekta Aron, sasa alianza kujiona shujaa ambaye atakwenda kuuangamiza mtandao mzima wa Dokta Gondwe.
Mwanzo alitegemea Annah na familia yake watasimama kama mashahidi kwenye kesi ya mauaji aliyofanya Osward ambaye ni miongoni pia mwa watu waliopo kwenye mtandao wa Dokta Gondwe. Lakini sasa Annah amekuwa pia shahidi atakayethibitisha kuwa dokta Gondwe anahusika na mauaji ya wazazi wake.
Kabla ya yote ilikuwa ni lazima Inspekta Aron ahakikisha anamlinda Annah kwa gharama yoyote ile. Alimjua mbaya wake wa kumdhibiti mapema ni kaka yake Tino, huyu ndiye aliyekuwa kibaraka mkubwa wa Dokta Gondwe.
Baadae Annah alitulia, Aron akaona hiyo ndio nafasi ya kutoka
"Pumzika kwanza Annah, natoka mara moja nitarudi baada ya muda mfupi" alisema Aron huku akimlaza Annah taratibu kisha akatoka, nje akawakuta askari wake watatu ambao tayari walionyesha kuanza kuchoka baada ya kukaa hapo kwa muda mrefu. Aron akawasogelea na kuwatazama mmoja baada ya mwingine
"Sikilizeni, mda wote mnatakiwa muwe makini kunamazingira ambayo si salama sana hapa hospitali narudia tena ongezeni umakini sawa"
"Sawa mkuu"
"Enh! Inspekta Jada bado hajarudi?"
"Hajarudi ali..aah huyo hapo kafika mkuu"
Inspekta Aron alipiga hatua kumfuata Inspekta Jada mwanamke aliyefanya kazi kwa ukaribu sana na yeye, ndiyo kwanza alikuwa anaingia. Wote wawili wakasogoea pembeni na kuanza kuteta jambo

"Enhe! Mambo yamekwendaje Jada"
"Nimefanikiwa kuongea na ndugu wa Annah watafanya mazishi ya baba na mama Annah kesho"
"Sawa kuhusu Annah umewambiaje?"
"Nimewambia yupo hospitalini mahututi, kwa sababu za kiusalama sijawambia ni wapi"
"Safi"
"Vipi hapa kwema?"
"Si kwema sana, Tino yuko hapa hospitali nadhani wameshajua Annah yupo hai wanamtafuta"
"Mmh! sasa tunafanyaje? Na vipi hali ya Annah?"
"Kaamka"
"Wow! vipi kaongea"
"Ndiyo, kasema dokta Gondwe alikuwepo miongoni mwa wale watu waliowaua wazazi wake"
"Nini? Inspekta Aron tunasubiri nini, tukachue arrest warrant tukamkamate"
"Hapana, yule ni Waziri wa afya mtu mkubwa huwezi kumkamata kizembe hivi...."
"Inspekta Aron lakini ni...."
"Sikiliza Jada, lengo letu si dokta Gondwe pekee ila mtandao wake mzima akiwemo kaka yangu Tino"
"Mmh! sawa nimekuelewa"
"Sawa nenda kakae na Annah jaribu kumuweka sawa kisaikolojia mimi nakwenda kumuangalia Tino kule chini alipolazwa mama"
"Sawa" alijibu Jada kisha kila mmoja akaelekea upande wake

[emoji294][emoji294][emoji294]
Ghorofa ya kwanza upande wa kushoto mwishoni ndani ya hospitali ya Mountenia ndipo vilipokuwepo vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU).
Katika eneo hilo Tino kaka yake Aron alionekana amesimama nje ya chumba kimoja chenye mlango wa kioo. Ndani ya chumba hicho mama mmoja alikuwa amelala juu kitandani, pua na mdomo wake vilifunikwa na maski iliyounganishwa moja kwa moja na mtungi wa hewa ya oksijeni. Huyu hakuwa mwingine bali mama yake Tino na Aron mke wa mwanajeshi mstaafu ambaye kwa sasa ni marehemu Jenerali Phillipo Kasebele. Mama huyu maarufu kama madam Sultana kwa sasa alikuwa amemaliza miezi sita tangu alale kitandani hapo akiwa hajitambui, alikuwa akiumwa ugonjwa ambao hata madaktari wenyewe walishindwa kuutolea maelezo ya kueleweka.
Tino alikuwa amesimama wima mlangoni nje ya chumba hicho huku macho yake akiwa ameyakaza kumtazama mama yake pale kitandani. Mara simu yake ikatoa mlio ukiashiria kuna ujumbe wa maandishi, Tino akaufungua haraka na kuusoma.

,,,,,Mpango wako umefanya kazi mkuu, tayari tumeshajua ni wapi walipomficha Annah,,,,,

Tino alimaliza kuusoma ujumbe huo kisha akatabasamu, ni kweli walikuwa wamemchezea Inspekta Aron mchezo wa akili kiasi cha kumfanya yeye mwenyewe awapeleke hadi chumba alicholazwa Annah, kivipi? Ilikuwa hivi...
Tino alipaki gari lake katika eneo la wazi kwa makusudi kabisa aliamini kama mdogo wake Aron angefika na kuliona basi lazima angehisi moja kwa moja kuwa amekuja kumuua Annah hivyo angewahi kwenda kwenye chumba cha Annah kumuangalia na hivi ndivyo ilivyokuwa.
Mara tu baada ya Inspekta Aron kuanza kukimbia kuelekea ndani ya hospitali ya Mountenia tayari Tino alishawapanga vijana wake wawili ambao walianza kumfuatilia kwa nyuma hadi pale Aron alipofika na kuingia chumba alicholazwa Annah bila kujua anafuatiliwa.
Tino alijua pia kama Aron hata muona basi atakuja moja kwa moja ICU kuhakikisha kama kweli Tino yupo hospitali hapo kwa ajili ya kumuona mama yao madam Sultana.
Ni kama vile Tino alikuwa kwenye akili ya Inspekta Aron, kila alichokiwaza ndicho kilichotokea. Mara tu baada ya kimaliza kuusoma ule ujumbe alisikia mlango wa lifti ukifunguka na kufungua kisha vishindo vya mtu anaekuja nyuma yake taratibu vikasikika
Huyu hakuwa mwingine bali Inspekta Aron ambaye alitembea taratibu na kwenda kusimama pembeni ya kaka yake Tino. Wote wakawa wameelekeza macho yao mbele kumtazama mama yao hakuna aliyegeuka kumtazama mwenzake usoni. Walidumu katika hali hiyo kwa zaidi ya dakika tatu mfurulizo, hakuna aliyefungua kinywa kuongea na mwenzake kila mmoja alionekana akiwaza lake.
Tino aliwaza kumuua Annah lakini pia aliwaza kuhusu vimelea vya V-COBOS ambavyo ndiyo ilikuwa lengo lake kubwa na hii ndiyo sababu ya yeye kujiweka karibu na Waziri wa afya Dokta Gondwe. Tino hakuwa mtu wa kawaida kama alivyoonekana, alikuwa ni mtu mwenye siri na mipango mikubwa sana aliyofanya kimya kimya tena kwa akili sana, haijulikani ni wapi au ni vipi aliijua siri hii ya vimelea vya V-COBOS.
Inspekta Aron pembeni yake yeye aliwaza tu namna atakavyoendeleza jukumu lake la kuhakikisha anauangusha mtandao mzima wa Tino na Dkt Gondwe. Tayari anashahidi anaemtegemea na kumilinda kwa nguvu zote, Annah.

"Usijali mama atapona" hatimae aron alifungua kinywa kuzungumza. Tino alikaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha nae akajibu
"Ndiyo lazima apone, mama yetu hawezi kufa"
"Ni kweli hawezi kufa, baba alitukabidhi kwake"
"Atapona"
"Atapona"
Inspekta Aron na Tino waliongea kwa namna ya kufarijiana lakini kila mmoja akili yake ilikuwa mbali, wala haikuwa hapo.

𝗜𝗧𝗔𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔...
 
𝗧𝗛𝗘 𝗠𝗢𝗗𝗘𝗥𝗡 𝗪𝗔𝗥
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya...........10
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

10-(GODWIN MDUNGUAJI)
ILIPOISHIA...09
"Usijali mama atapona" hatimae aron alifungua kinywa kuzungumza. Tino alikaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha nae akajibu
"Ndiyo lazima apone, mama yetu hawezi kufa"
"Ni kweli hawezi kufa, baba alitukabidhi kwake"
"Atapona"
"Atapona"
Inspekta Aron na Tino waliongea kwa kufarijiana lakini kila mmoja akili yake ilikuwa mbali, wala haikuwa hapo....

SASA ENDELEA...
"Lakini sio kawaida yako kuja kumuona mama, leo nini kimekupata kaka" Aron alijaribu kumchimba kaka yake
"Sio kawaida yangu ndiyo, lakini huwa nakuja kwa hiyo hakuna cha ajabu hapo" Tino alijibu huku akitabasamu kiasi
"Nakumbuka mlikuwa mnagombana sana na mama, mara nyingi alikuwa anachukizwa sana na mienendo yako ukawa unakwepa hata kuonana naye, siku akiamka akasikia kama ulikuwa unakuja kumtembelea kama hivi atafurahi sana"
"Ni mama yangu, hata kama sikuwa naelewana naye lakini bado atabaki kuwa mama na ndio sababu nafanya juu chini kulipia matibabu yake kuhakikisha anapona"
"Kuua watu ndio kufanya juu chini" Inspekta Aron aliendelea kumuuliza kaka yake maswali ya kichokozi. Kabla Tino hajajibu chochote simu ya Aron iliita akaichukua kutoka mfukoni na kutazama mpigaji, ilikuwa ni namba ngeni, akapokea .

"Ndiyo, Inspekta Aron naongea...." Alisema Aron baada ya kupokea.
Mara Inspekta Aron akageuka taratibu na kumtazama Tino usoni, ilikuwa ni ishara tosha kuwa jambo alilolisikia upande wa pili wa simu ile halikuwa la kheri na lilihusiana moja kwa moja na kaka yake Tino.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati ule Inspekta Aron ametoka ndani ya gari kwa kasi, alimuacha Najma ambaye hakuweza kufanya chochote kutokana na maumivu makali ya mguu aliyokuwanayo baada ya kuumia kule gerezani. Najma alishindwa kuelewa ni kipi kimemfanya Inspekta Aron atoke kwa kasi vile, akawaza pengine yupo kwenye majukumu ya kikazi. Na ndivyo ilivyokuwa, Inspekta Aron alikuwa akiwahi kwenda kumuangalia Annah akiamini kaka yake Tino ameingia hospitali ya Mountenia kumuua.

Wakati Inspekta Aron akiingia hospitali humo huku Najma aliwaona wale vijana wa Tino ambao walijitokeza nyuma ya gari walilokuwa wamejificha wakaanza kumfuatilia Inspekta Aron nyuma yake kwa siri.

Akili ya Najma iliweza kung'amua kuwa kuna jambo ambalo si la kawaida lilikuwa likiendelea katika hospitali hiyo. Alitamani kumjulisha Inspekta Aron kuwa nyuma yake kuna watu wanamfuatilia lakini angewezaje, hakuwa na mazoea na kaka huyo hata namba yake yasimu hakuwa nayo.

"Mungu wangu nitafanyaje" Najma aliwaza huku nafsi yake ikitamani sana kumsaidia Inspekta Aron kama yeye alivyomsaidia kule gerezani na kumleta hospitali licha ya kwamba hakuwa amehudumiwa hadi dakika hii.
Mara ghafula kuna wazo likamjia, haraka akachukua simu yake na kumpigia baba yake Dokta Gondwe. Simu iliita kwa muda mwisho ikapokelewa.

"Hallo baba"
"Ndiyo Najma mwanangu" Dkt Gondwe aliitikia upande wa pili akiwa katika jengo la ubarozi ndani ya chumba kimoja ambacho alikutana na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa kwa ajili ya mazungumzo.

"Baba nina shida"
"Shida gani mwanangu"
"Noamba namba ya yule kaka askari aliyemfungulia Osward mashataka"
"Nani, Inspekta Aron?"
"Yes! huyo huyo"
"Za nini wewe?"
"Baba ninashida naye naziomba sasa hivi"
"Sawa, nakuliza unashida gani na inspekta Aron?"
"Hivi utaendelea kuniuliza maswali yako au unanipa hizo namba?" Najma aliuliza swali huku akijua fika udhaifu wa baba yake, asingeweza kuendelea kumbishia

"Sawa nakutumia sasa hivi" alijibu Dkt Gondwe kisha akakata simu. Badala ya kutuma namba Dokta Gondwe aliendeleza mazungumzo na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa. walikuwa wakijadili suala nyeti kuhusu usalama wa vimelea vya V-COBOS. Hadi dakika hiyo walikuwa hawajui ni nani haswa anahitaji vimelea hivyo akimtisha Dokta Gondwe kwamba endapo atashindwa kumpatia vimelea vya V-COBOS basi atazisambaza video zake chafu mtandaoni.

Dokta Gondwe na profesa Kulolwa walijikuta kwenye mtihani mzito wakihohofia pia usalama wa maisha yao kwani watu waliokuwa nyuma ya mpango huo madhubuti wa vimelea vya V-COBOS hawakuwa na mchezo hata kidogo, hili lilikuwa ni suala nyeti sana. Waliogopa kufanya makosa ambayo yanaweza hata kuwaghalimu maisha yao.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Najma akiwa ndani ya gari la Inspekta Aron aliendelea kusubiri atumiwe zile namba na baba yake.
Kwa mbali Big' alionekana akiwa upande wa pili wa barabara usawa wa geti kubwa la kuingilia hospitali ya Mountenia. Alikuwa akichukungulia na kufuatilia kwa ukaribu gari la Inspekta Aron ambalo alikuwa ametega bomu chini yake. Uwepo wa Najma ndani ya gari hiyo ndio uliomzuia Big asifanye kazi yake. Aliendelea kusubiri akiamini utafika muda Aron atabaki mwenyewe ndani ya gari na hapo ndipo atamsambaratisha kwa kuruhusu bomu lile lilipuke, jambo jema kwake ni kwamba rimoti yake ilikuwa na uwezo wa kufanya kazi hata kama bomu likiwa umbali wa kimomita moja kutoka alipo.
Zilikuwa zimepita dakika tano mpaka sasa bado mheshimiwa Dkt Gondwe alikuwa hajamtumia binti yake namba ya Inspekta Aron.

Najma akiwa amekasirika aliwaza ampigie tena baba yake lakini mara kuna ujumbe ukaingia kwenye simu yake, tayari Dkt Gondwe alikuwa umemtumia namba.
Bila kuchelewa Najma alipiga ile namba, ikaita sekunde chache na kupokelewa.
"Aron" Najma aliita
"Ndiyo, Inspekta Aron naongea" sauti ya kiume iliyojaa kitetemeshi ilisikika upande wa pili, alikuwa ni Inspekta Aron mwenyewe wakati huo alikuwa amesimama na kaka yake Tino nje ya chumba alicholazwa mama yao.

"Aron, mimi ni Najma uko wapi? Uko salama? Wakati unaingia hospitali kuna watu wawili niliwaona wanakufuata nyuma, vipi kuna tatizo hawajakudhuru?" Najma aliuliza maswali mfurulizo akitamani kujua kama Inspekta Aron yupo salama, ulijikuta anajali sana usalama wa mwanaume huyo kiasi cha kufanya hadi yeye mwenyewe ajishangae na kujishtukia, haikuwa kawaida yake kabisa.
Maelezo ya Najma yaliifanya akili ya Inspekta Aron kuunganisha matukio kwa kasi akajua moja kwa moja ule ulikuwa ni mtego, kama alikuwa akifuatiliwa basi ilikuwa ni njama ya kutaka kujua ni wapi alipo Annah. Inspekta Aron alijikuta anajilaumu kwa nini hakushtuka mapema.
Hakuwa na sababu ya kujiuliza mara mbili mbili akajua moja kwa moja huo ulikuwa ni mpango wa mtu ambaye yuko pembeni yake wakati huu yaani Tino kaka yake.

Inspekta Aron ageuka taratibu na kumtazama Tino usoni huku simu ikiwa bado sikioni mwake.
"Hallo...hallo... Aron unanisikia" Najma alikuwa akiongea upande wa pili baada ya kuona Inspekta Aron yupo kimya hasemi chochote.

"Okay okay nimekupata" Inspekta Aron alijibu kwa kifupi sana kisha akakata simu hakutaka kumfanya kaka yake ajue kama ameshamshtukia mchezo alioufanya.

"Naondoka, tutaonana baadae" Aron aliaga na kuondoka, akaingia kwenye lifti kisha akapanda juu kuangalia usalama wa Annah kwa mara nyingine, tayari alishajua yupo hatarini.
Mara tu baada ya Inspekta Aron kuondoka, Tino naye hakutaka kupoteza muda aliteremka kwenye ngazi upesi akapiga hatua ndefu ndefu na mwisho alifika chini kabisa ya hospitali hiyo akatoka nje.
Akiwa mlangoni Tino alikutana na wale vijana wawili.

"Mpango umekwenda vizuri"alisema Tino huku wakiongoza kurudi kwenye gari lake
"Ndiyo tumeshajua chumba cha Annah"
"Sawa, sasa sniper G' najua unaelewa nini cha kufanya tafuta usawa mzuri kwenye ghorofa ya upande wa pili kule hakikisha unamchapa risasi ya kichwa huyu binti, nakupa masaa sita tu uwe umemaliza kazi" Tino alitoa maelezo kwa kijana wake ambaye alikuwa ni mtaalamu wa kutumia bunduki zile za masafa marefu yaani mdunguaji (Sniper)
Sniper G' kama jina maarufu lakini aliitwa Godwin alifungua buti la gari akatoa begi moja kubwa na refu akalivaa mgongoni kisha akaanza kuondoka kuelekea ghorofa iliyokuwa jirani na hospitali ya Mountenia, huku ndiko aliamini atapata usawa mzuri wa kumlenga Annah shabaha ya kichwa, akawaacha Tino na wenzake ambao waliingia kwenye gari na kuondoka.

Wakati heka heka hizi zikiendelea Najma alikuwa akishuhudia yote akiwa ndani ya gari ya Inspekta Aron, si yeye peke yake hata Big' naye akiwa nje ya hospitali upande wa pili wa barabara alikuwa akishuhudia pia
[emoji294][emoji294][emoji294]

Je, nini kitafuata?
VIMELEA VYA V-COBOS NI KITU GANI?
ARON ATAWEZA KUMLINDA ANNAH DHIDI YA MDUNGUAJI(SNIPER G')?
VIPI KUHUSU BOMU CHINI YA GARI LAKE?
ITAENDELEA.....

Jipatie vipande vyote hadi 30 kwa Tsh 1500 tu
0756862047
 
𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐍 𝐖𝐀𝐑
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.........11
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

11-(AISHIIIII-NAUMIA)
ILIPOISHIA..10
Mpango aliousuka Tino unaleta mafanikio chanya na hatimae anafanikiwa kukitambua chumba alicholazwa Annah, haraka anamtuma mdunguaji wake mashuhuri sniper G' kuhakikisha anamuua Annah. Wakati huo huo Inspekta Aron anashtukia mchezo alioufanya kaka yake Tino.
Upande wa pili majadiliano kati ya Waziri wa afya Dokta Gondwe na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa yalikuwa yakiendela wakijadili kuhusu vimelea vya V-COBOS.

JE, NINI KITAFUATA?

SASA ENDELEA...
Ndani ya jengo la ubarozi mazungumzo nyeti kati ya Rais mstaafu mheshimiwa Profesa Cosmas Kulolwa na Waziri wa afya Dokta Isaack Gondwe yalikuwa yakiendela.

"Kwa hiyo unasema mtu aliyekutumia hizo picha zako za X ndiyo huyo anahitaji vimelea vya V-COBOS?" profesa Kulolwa aliuliza
"Ndiyo profesa yaani hapa nimechanganyikiwa sielewi nifanye nini, nimejaribu kumbembelaza akubali kuchukua pesa yoyote atakayo lakini wapi kakataa katakata, alafu kinachonishangaza huyu mtu kajuaje kuhusu vimelea vya V-COBOS"
"Dkt Gondwe sikiliza, aliyefanya hivi lazima awe ni miongoni mwa watu wanaoujua huu mpango wa vimelea vya V-COBOS anataka kutuzunguuka tu, anaweza akawa ni wa hapa hapa nchini kwetu au ni hawa wakubwa zetu kutoka Mexico wanageukana wenyewe kwa wenyewe"
"Ni kweli hilo hata mimi niliwaza, lakini kama ni wao mbona wanajua kabisa vimelea vipo ndani ya Maabala kuu ya serikali kwa nini asimtumie mkemia mkuu ambaye naye ni mmoja wetu anajua siri hii ya uwepo wa vimelea vya V-COBOS hapa nchini, kwa nini waje kunishambulia mimi"

"Acha kujiuliza kwa nini mimi, tufikiri tunafanyaje"
"Labda tuwape taarifa wakubwa kuwa kuna mtu anavitaka vimelea" Dkt Gondwe alitoa wazo
"Hapana hapo tutawasha moto mwingine kama ule wa mwaka juzi, kumbuka hili ni suala ambalo hawa ndugu zetu wazungu wamelipanga kwa zaidi ya miaka 10, siku wakivisambaza hivi vimela vya V-COBOS wanategemea kuvuna mabilioni ya pesa kutoka nchi zote Dunia, kumbuka walitaka kuviachia mwaka juzi lakini vikaibuka virusi vya korona wakasema tusubiri. Sisi tumeaminiwa Dkt Gondwe hatutakiwi kuwaangusha hata kidogo wakisikia kuna mtu anaviwinda vimelea kutoka kwetu nakuhakikishia watatuua" profesa Kulolwa alitoa maelezo ya kina.

"Sasa nitafanya profesa, huyu mtu ana video zangu za utupu, na mbaya zaidi siku hiyo nilikuwa na mke wa mtu tena mke wa kijana wangu ambaye namwamini sana"
"Sikiliza Dokta Gondwe, tumia akili fanya hivi mhakikishie kuwa utampa hivyo vimelea anavyovitaka kisha wewe muwekee mtego alafu mdhibiti. Mbona unavijana wazuri tu wa kazi wanaweza kufanya bila shida yoyote, kama huyu unamwita Tino yule jamaa ni professional sana mtumie"
"Mmh! Tino siwezi kumtumia kwa sababu yeye ndio haswa nilitembea na mke wake siku hiyo, yaani hizo picha na video nipo na mke wake vipi kama akitaka kujua undani wa hiyo kazi"
"Wewe mpe kazi usimwambie kwa nini anafanya"

Dokta Gondwe alitulia kwa muda akijaribu kuutafakari ushauri aliopewa na na Profesa Kulolwa, akaona kwa kiasi furani unafaa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
***********
{TANGAZO:- Epuka matapeli simulizi hii imetungwa na SAUL DAVID simu 0756862047, Tafadhali usinunue kwa mtu mwingine tofauti }
******-*-

Zilikuwa zimepita dakika 20 mpaka sasa tangu Aron alipokata simu ya Najma. Bado alikuwa ndani ya gari ya Inspekta Aron pale nje ya hospitali ya Mountenia, wasiwasi ulimjaa binti huyu wa kishua mtoto wa Waziri, ilifika mahali yeye mwenyewe akaanza kujishangaa imekuwaje anamjali sana Aron.
Akiwa katika hali hiyo mara kwa mbali alimuona Inspekta Aron anakuja akitokea ndani ya hospitali ya Mountenia. Mkono wa kulia alikuwa ameshikilia begi dogo jekundu lenye msalaba mweupe, lililokuwa ni begi la huduma ya kwanza 'first aid'.
Najma alijikuta akiingiwa na kaubaridi ka furaha akawa anamtazama Aron tangu alipokuwa mlango wa hospitali hadi alipofika kwenye gari.
Aron alifungua mlango wa kulia wa siti za nyuma alipokuwa Najma akaingia na kukaa pembeni yake.

"Uhuuu!" Aron alivuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu kisha akageuka kumtazama Najma usoni, wakatazamana.

"Vipi?" Aliuliza Aron
"Poa" Najma alijibu kwa sauti iliyotokea puani
"Sorry nilikuacha mwenyewe ghafula"
"Kulikuwa na nini mbona mikiki mikiki ilikuwa mingi hapa"
"Aah! ni mambo ya kawaida tu ndio maisha yetu sisi tushazoea"
"Ooh! kutumia bastola kila wakati, yaani sekunde yoyote unaweza kufa mmh! mnatabu sio siri"
"Kawaida, hata ungekuwa wewe ungeweza tu"
"Ahahaha wallah siwezi kabisaa" Najma aliongea na kucheka hali iliyofanya Aron auone mwanya wa binti huyo mrembo ambao ulizidisha uzuri wake maradufu, Inspekta Aron akajikuta ameduwaa akimtazama.
"Nini?" Aliuliza Najma
"Nini nini?" Aron akauliza pia
"Mbona unaniangalia hivyo?"
"Aah! kwani ajabu, mbona hata wewe hapo unaniangalia" alijibu Aron na wote wakacheka kwa pamoja, taratibu wawili hawa wakajikuta wamezoeana kwa muda mfupi sana. Wakati huo wakiwa kwenye kilele cha furaha hakuna aliyejua kuwa chini ya gari waliyopanda kuna bomu limetegeshwa.

"Alafu unajua nini Najma" alisema Aron
"Ee nambie mkaka, alaa! samahani nambie afande"
"Mmh! muone niite Aron hivyo hivyo, afande ni yule anashinda na magwanda kila siku"
"Sasa kwa nini wewe huvaagi hayo magwanda"
"Mimi ni afisa mpelelezi alafu acha kwanza niongee nilichotaka kusema usiniingilie"
"Hahahah! haya sema afande..ooh sema Aron"
"Muone, nataka nikushukuru ile simu yako ilikuwa ya muhimu sana kwangu"
"Simu gani?"
"Kwani sio wewe umenipigia simu ukasema kuna watu wananifuatilia"
"Ooh! sawa ni mimi enh kwani kuliwa nini"
"Ah! Mambo ni mengi Najma ila asante, lakini kwani namba yangu ulitoa wapi? " Aliuliza Aron wakati akifungua kile kijibegi cha huduma ya kwanza
"Kwa baba"
"Baba? Baba gani?"
"Baba yangu"
"Unamaanisha dokta Gondwe"
"Yeah"
Aron alitulia kidogo akitafakari jambo, jina la dokta Gondwe lilibadilisha kabisa hali ya hewa mle ndani, huyu ndiye alikuwa mbaya wake, mtu anaeamini kamshika masikio kaka yake Tino, na ndio huyu huyu aliyewaua wazizi wa Annah.
Ni kama Najma alielewa ni kiasi gani habari za baba yake zimemtoa Aron kwenye mudi, naye akabaki kimya.
"Haya sogeza mguu wako nikutibu ulipoumia" alisema Aron
"Mmh!" Najma aliguna huku akitoa macho kumtazama Aron, wakatazamana tena.
"Nini?"
"Kwani unajua ni wapi nimeumia?"
"Ee si mguuni"
"Sawa mguuni lakini sehemu gani"
"Aah sijui" alijibu Aron huku akimtazama Najma usoni. Najma akaelekeza kidole chake mahali alipoumia, ilikuwa ni kwenye paja lake la kushoto.
Inspekta Aron akajikuta anamtazama pembeni kwa aibu, Najma akatabasamu.

"Basi twende ndani hospitali, sikujua mimi" alisema Aron
"Sawa twende lakini..."
"Lakini nini"
"Au basi, twende"
"Kutembea vipi, huwezi kujitahidi hata kidogo" aliuliza Aron huku akifungua mlango wa gari tayari kutoka
"Hapana siwezi inabidi unibebe tena.... lakini Aron"
"Ee nambie"
"Hebu funga kwanza huo mlango"
Inspekta Aron akafungua, akageuka na kumtazama Najma kwa macho ya kuuliza.
"Ulishawahi kwenda beach?" Aliuliza Najma
"Eeh niliwahi mara nyingi tu, wauzaji wa madawa ya kulevya mara nyingi huwa nawakamata maeneo kama hayo"
"Ooh! Basi nitibu tu mwenyewe sio lazima tuingie hospitali"
"Una maana gani?"
"Kwani unashindwa nini na beach huwa unaenda uliyoyaona beach ndio utayaona hapa wewe nitibu tu usijali dakika 0" alisema najima kisha akasimama na kufungua kifungo cha suruali yake ya jeans kisha akaanza kuivua taratibu

Inspekta Aron aliduwaa akataka kusema jambo lakini tayari alishachelewa Najma alikuwa ameshavua suruali yake akaishusha hadi usawa wa chini ya magoti, akabaki na nguo ya ndani pekee
"Mungu wangu, nini hiki" Inspekta Aron aliwaza huku mapigo yake ya moyo yakienda mbio akapoteza kabisa kujiamini.

Wakati haya yote yakiendela yule jamaa aliyetegesha bomu chini ya gari la Inspekta Aron (Big') alikuwa kwa mbali akishuhudia, kwa kuwa vioo vya gari hilo vilikuwa vikionyesha kwa mbali Big' aliweza kumuona Najma amesimama na kuvua suruali yake.

"Alaah! Haka ka afande kumbe sio poa, kwa hiyo anataka kupiga vyombo kwenye gari, hahaha haki ya mungu Najma ni demu wa hovyo mbona namuona kama yuko serious sana mambo gani ya aibu anafanya sasa huyu mtoto wa waziri, haya sasa hizi habari nikimwambia Osward si atapagawa. Lakini sio mbaya sio mda afande anakwenda kufa, burudika kwa mara ya mwisho" alisema Big' huku akila ndizi alizonunua kwa wapita njia muda mfupi uliopita.

"Endelea na kazi Aron miguu yangu inahisi baridi" alisema Najma kwa sauti laini iliyozidi kumuweka Aron kwenye wakati mgumu. Halikuwa jambo jepesi kustahimili kuyaangalia mapaja laini ya mwanamke mrembo kama Najma.

"Acha ujinga Aron " hii ilikuwa ni sauti iliyopita kwenye mawazo ya Aron na hapo akagutuka na kujikuta anavaa ujasiri kama mwanaume.
Alichukua vifaa muhimu kwenye lile begi, kisha akaiinua miguu yote miwili ya Najma na kuinyoosha juu ya siti za nyuma, akavaa mipira mkononi kisha akachukua dawa na kuinyunyiza juu ya paja la kushoto la Najma kisha akaanza kuisugua taratibu kumchua.

"Aaaa...oooooh...mamaa
.. ishiiiiiii...naumia Aron taratibu" Najma alilalamika
"Vumilia kidogo namalizia" alisema Aron huku akipunguza kasi ya kumsugua
Angalau maumivu yalipungua Najma akajikuta anaanza kumkagua Aron kwa ukaribu wakati akiendelea kumtibu. Alimkagua kwanzia juu mpaka chini mwisho akatabasamu mwenyewe.

"Aron" Najma aliita

ITAENDELEA...

(Full story -1500)
0756862047-Saul David
 
𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐍 𝐖𝐀𝐑
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.............12
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

12-(INSPEKTA ARON NYUMBANI KWA WAZIRI)
ILIPOISHIA...
"Vumilia kidogo namalizia" alisema Aron huku akipunguza kasi ya kumsugua.
Angalau maumivu yalipungua Najma akajikuta anaanza kumkagua Aron kwa ukaribu wakati akiendelea kumtibu. Alimkagua kuanzia juu mpaka chini mwisho akatabasamu mwenyewe.

"Aron" Najma aliita

SASA ENDELEA....
"Yes nambie Najma" Aron aliitika huku akiendelea kumchua Najma taratibu
"Hivi kwa nini unamchukia sana baba yangu?" Aliuliza Najma, Aron akasita kuendelea kumchua akatulia kwa muda kisha akaendelea tena.
"Kwa nini umeuliza?"
"Nataka tu kujua"
"Hapana simchukii baba yako ila nachukizwa na matendo yake"
"Matendo yapi hayo Aron?"
"Unajua mimi ni askari najua ninachokifanya siwezi kukurupuka tu na kuanza kumshutumu baba yako kwa vitu vya uongo, nimefanya utafiti wa kutosha kilichobaki ni kupata tu ushahidi wa kuthibitisha matendo yake maovu"
"Sawa lakini ni mda mrefu sana umeanza kumuandama baba yangu mpaka leo hakuna chochote umethibitisha huoni kama shutuma zako ni za uongo"
"Sijashindwa Najma, sitakiwi kuongea sana juu ya hili ila kwa kuwa nakuamini basi nitakwambia kitu, Baba yako dokta Gondwe ni mtu mkubwa ukiacha yeye kuwa Waziri wa afya lakini amekuwa akifanya kazi na vigogo wakubwa wakubwa hapa nchini, ndio maana hata kesi ya Osward mtoto wa yule tajiri Mzee Matula kamkabidhi baba yako ndio asimamie kuhakikisha Osward hafungwi, baba yako anamtandao mpana wa uharifu amewaua mashahidi wote ili Osward ashinde kesi mahakamani, moja kati ya vijana anaowatumia baba yako kufanya uharifu ni kaka yangu anaitwa Tino" Aron alitoa maelekezo ya kina, wakati huo tayari alikuwa amemaliza huduma kwa Najma.
Najma alitulia huku akiivaa suruali yake taratibu akawa anayatafakari maelezo ya Inspekta Aron
"Kwa hiyo ndio maana ukawa unaniomba mimi nikatoe ushahidi kwa kesi ya Osward, mbona mimi sikuwa naye wakati wa tukio nilikutana naye wakati tayari mauaji yameshafanyika kwa hiyo sijui chochote Aron" alieleza Najma huku akipokea kopo la vidonge kutoka kwa Aron

"Sawa Usijali, hivi ni vidonge vya maumivu unameza viwili kutwa mara mbili vitakusaidia"
"Asante Aron kwa msaada wako Mungu akubariki sana"
"Asante pia, kaa vizuri basi nikupeleke nyumbani"
"Aah! Nitapanda taxi Aron hata usijali"
"Hapana huwezi kupanda taxi na mimi nipo, kuwa huru tu ngoja nikupeleke chapu" Alisema Inspekta Aron akafungua mlango akashuka na kuhamia upande wa dereva.
Kabla hajawasha gari Aron aliandika ujumbe wa maandishi kwa Inspekta Jada

,,, Natoka tena mara moja, usimuache Annah hata sekunde moja, nitarudi baada ya dakika kumi hivi,,,,

Baada ya kutuma ujumbe huo Inspekta Aron akawasha gari nakuanza safari kumpeleka Najma nyumbani kwa dokta Gondwe.
Big' naye alikuwa hachezi mbali mara tu baada ya kuliona gari la Inspekta Aron linatoka naye alianza kulifuata nyuma taratibu, lengo lake likiwa ni kuruhusu bomu lilipuke kwa kubinya rimoti yake mara tu Aron atakapo baki mwenyewe ndani ya gari.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Godwin maarufu kama Sniper G mdunguajia mashuhuri kutoka katika kikosi cha Tino tayari alikuwa ndani ya ghorofa moja refu sana lililokuwa jirani kabisa na hospitali ya kimataifa ya Mountenia. Ghorofa hilo lilikuwa ni hoteli ya kimataifa yenye nyota tano. Godwin alikodi chumba kilichokuwa usawa na kile chumba alicholazwa Annah upande wa pili.
Alisogeza meza na kiti karibu na dirisha, akafungua lile begi lake refu ambalo ndani yake kulikuwa na vifaa mbalimbali vilivyopangwa kwa ustadi mkubwa. Godwin alianza kiviunganisha vifaa vile kwa haraka kimoja baada ya kingine na baadae akafanikiwa kuiunda bunduki ya masafa marefu, sniper'
Aliiweka mezani bunduki ile yenye stendi, akafungua madirisha mawili ya vioo kisha akarudi na kukaa kwenye kiti nyuma ya bunduki ile.
Godwin alimalizia kwa kufunga lenzi maalum juu ya ile bunduki kisha akaishikilia saawia na kupima shabaha upande wa pili ilipo hospitali ya Mountenia katika chumba alicholazwa Annah.

Kupitia ile lenzi Godwin aliweza kuona kwa ukaribu kabisa kila kilichokuwa kikiendelea kwenye chumba cha Annah, habati nzuri kwake na mbaya kwao hawakuwa wamefunga mapazia ya chumba kile.
Alimuona Inspekta Jada akiwa amekaa kitandani pembeni ya Annah aliyekuwa amepumzika tena baada ya kulia sana mara tu alipopewa taarifa za mazishi ya wazazi wake.
Kwa sababu Annah alikuwa amelala hali hii ilimfanya Godwin kushindwa kuipata shabaha ya uhakika. Hakutaka kufanya makosa Godwin aliamua kusubiri mpaka pale Annah atakapo amka na kuinua kichwa chake angalau akae kama alivyokaa Inspekta Jada hivi sasa, hapo itakuwa rahisi kumtwanga risasi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Tino alionekana akiwa ndani ya ile ofisi yake ya siri ambayo inamuingizia pesa nyingi kwa njia ya kurekodi video za ngono kutoka vyumba mbalimbali vya wageni alivyotegesha kamera zake za siri.
Vijana wafanyakazi wa Tino walikuwa bize wakati huo kila mmoja na kompyuta yake. Meza aliyokuwepo Tino ilikuwa imejitenga pembeni kidogo kutoka walipokuwa vijana hao. Kupitia kompyuta iliyokuwa juu ya meza Tino alikuwa akiitazama ile video ya ngono ya mkewe akiwa na bosi wake dokta Gondwe. Video hii iligeuka na kuwa kama madawa ya kulevya kwake, kila wakati alikuwa akiiangalia na kupandisha morali ya kufanya kile alichokusudia kufanya.

"Umefanya makosa makubwa sana Dokta Gondwe, kutembea na mke wangu ni kosa kubwa ambalo litakughalimu katika kipindi chote cha maisha yako" Tino alijisemea mwenyewe kwa sauti ya chini huku akiicheza tena video ile ambayo ilikuwa imefika mwisho, ikaanza upya.
"Kupitia video hii nitahakikisha napata vimelea vya V-COBOS wala hutojua kama ni mimi. Mimi ndio nitakae kuwa muhusika wa kusambaa kwa ugonjwa huu wa Virus vya COBOS, Ulimwengu mzima utasimama kulitaja jina langu, V-COBOS itaitetemesha Dunia yote kuliko hata COVID19" Tino alizidi kujisemea mwenyewe.

Wakati akisema hayo simu yake ilikuwa mezani akisubiri taarifa mbili muhimu kwanza alikuwa akisubiri matokeo ya kijana wake mdunguaji mashuhuri sniper G' kama amefanikiwa kumuua Annah na pili alikuwa akisubiri wakati ufike awasiliane na Dokta Gondwe kujua kama atakubali kumpa vimelea vya V-COBOS au laa!
[emoji294][emoji294][emoji294]

Safari ya Inspekta Aron akiwa na Najma ndani ya gari yake ilikuwa ikiendelea. Wawili hawa ambao walikuwa wamezoeana kwa muda mfupi kila mmoja alijikuta akifurahia uwepo wa mwenzake. Najma alijikuta anatamani kuendelea kuwa karibu na Aron hivyo hivyo kwa Aron, hakutaka wafike nyumbani mapema. Najma hakuwaza tena kuhusu Osward mtoto wa mzee matula mume wake mtarajiwa ambaye yuko gerezani akisubiri hukumu yake kusomwa.

Akiwa siti ya nyuma Najma alikuwa akimuangalia sana Inspekta Aron aliyekuwa ameshikilia usukani. Taratibu alijikuta anaanza kumpenda kaka huyo mwenye chembechembe za ucheshi, anaejielewa na kujiamini sana.
Najma alizidi kumtazama huku aking'ata lips za chini za mdomo wake.
Inspekta Aron aliacha barabara kuu na kuingia kwenye barabara za mtaa akielekea ilipokuwa nyumba ya Waziri wa afya Dokta Gondwe. Alimtazama Najma kupitia kioo cha mbele cha gari yake hapo ndipo alipogundua kuwa Najma alikuwa anamuangalia sana. Aron akageuka na kumtazama akatamani kusema jambo lakini kabla hajafanya hivyo mara ghafula kukatokea mtikisiko mkubwa baada ya gari kuingia kwenye dibwi dogo la maji, Aron hakuwa ameliona wakati amegeuka kumtazama Najma.

"Mamaa! Aron vipi unataka kuleta ajali" Najma aliongea kwa hofu
"Hii njia yenu inamabonde sana alafu inaelekea kwa Waziri wa afya si aibu hii" alisema Aron huku akihangaika kuichomoa gari yake kwenye lile dimbwi la maji mwisho akafanikiwa

"Kwani hukuona maji hapo mbele wenzio huwa wanapita pembeni mbona njia iko wazi" alisema Najma
"Sikuyaona nilikuwa nakuangalia wewe"
"Unaniangalia Mimi nimefanyaje?"
"Kwa sababu unaniangalia"
"Akuu! Wala hata"
"Kweli eeh!"
"Kabisa mimi niko bize na simu yangu"
"Unachat na mumeo Osward si ndio?" Aron aliuliza swali la mtego
"Mume gani? Alafu yupo gerezani nachat nae vipi"
"Aah! kwani kuna kitu mzee Matula anashindwa kufanya kwa mwanae, anaweza hata kumpelekea swimming pool kule gerezani" alisema Aron huku akisimamisha gari yake, tayari alikuwa amefika nje ya jengo kubwa lililojengwa kisasa, hio ndio ilikuwa nyumba ya Dokta Gondwe.

Aron alipiga honi mara kadhaa mlinzi akafungua mlango mdogo akachungulia, Najma alitoa kichwa chake nje akampungia mkono na hapo bila kusita Mlinzi akafungua geti, Aron akaingiza gari taratibu.
Wakati huo Big' na pikipiki yake alibaki amesimama umbali wa mita kadhaa kutoka ilipokuwa nyumba ya Dokta Gondwe akawa anamsubiri Inspekta Aron atoke mwenyewe ndipo atekeleze azma yake ya kumsambaratisha akiwa ndani ya gari lake kwa kulilipua lile bomu.

Akiwa hapo mara aliiona gari ya mheshimiwa Dkt Gondwe naye akiingia nyumbani kwake. Alikuwa ametoka ubarozini mahali walipofanya mazungumzo nyeti pamoja na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa.

Inspekta Aron alishuka, akazunguuka nyuma ya gari na kufungua mlango, Najma akasogea akitaka kushuka

"Ee taratibu mama, usijali nitakubeba" alisema Aron baada ya kuona Najma anahangaika
"Mmmh"Najma aliguna huku akimtazama Aron kwa macho malegevu
"Mmh nini haya sogea" Najma alisogea na kupitisha mkono wake nyuma ya shingo ya Aron ambaye alimnyenyua taratibu kumtoa nje ya gari.
Najma akiwa mikononi mwa Inspekta Aron ile wanageuka tu uso kwa uso wakagonganisha macho na mheshimiwa Dkt Gondwe ambaye ndio kwanza alikuwa ameshuka kutoka kwenye gari yake.
Si Najma si Aron wote walishtuka kwani hawakuwa wametegemea kukutana na Mzee huyo katika mazingira hayo, wakabaki wanatazamana kwa zaidi ya sekunde 30 wasijue la kufanya, Najma akiwa mikononi mwa Inspekta Aron.

JE, NINI KITAFUATA?
VIPI KUHUSU BOMU?
VIPI KUHUSU TINO NA VIMELEA VYA V-COBOS?
DOKTA GONDWE ATAFANYA NINI?
VIPI KUHUSU PENZI AMBALO LINAWEZA KUCHIPUA KATI YA ARON NA NAJMA MTOTO WA ADUI YAKE?
ITAENDELEA...

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐍 𝐖𝐀𝐑
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya...........13
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

13-(SHARTI LA MTEGO)
ILIPOISHIA....
Si Najma si Aron wote walishtuka kwani hawakuwa wametegemea kukutana na Mzee huyo katika mazingira hayo, wakabaki wanatazamana kwa zaidi ya sekunde 30 wasijue la kufanya, Najma akiwa mikononi mwa Inspekta Aron.

SASA ENDELEA....
"We nishushe" Najma alinong'ona akimtaka Inspekta Aron amshushe chini
"Kuna nini? Najma nini shida?" Dokta Gondwe aliuliza huku akisogea taratibu kuwafuata pale walipo
"Aa.ni...niliumia kidogo wakati nikiwa kwa Osward kule gerezani baba" Najma alijieleza haraka haraka wakati huo Inspekta Aron alimshusha na kumuacha asimame mwenyewe, lakini Najma bado alionekana kuwa na maumivu Kiasi cha kujilazimisha kusimama kwa mguu mmoja, hakuwa na uwezo hata wa kusogea hatua moja.

"Mnashangaa nini mbebeni mpelekeni ndani" Dokta Gondwe alifoka, haraka walinzi aliokuwa wameambatana naye kutoka ubarozini walimfuata Najma wakamsaidia kumkokota na kuingia ndani.
"Asante Aron" Najma alitoa shukrani akiwa mlangoni, Inspekta Aron akatikisa kichwa kuipokea shukrani hiyo kisha akageuka kumtazama Dokta Gondwe ambaye alikuwa akipiga hatua kumsogelea.

"Inspekta Aron umepata wapi ujasiri wa kuingia nyumbani kwangu?" Aliuliza dokta Gondwe huku akisimama mbele ya Inspekta Aron, wakawa wanatazamana uso kwa uso.
"Kwani kuna ubaya gani Dokta, nimefanya msaada tu kwa binti yako, hata hivyo mimi na wewe sio maadui"
"Acha unafiki Aron, umekuwa ukiniandama zaidi ya miaka miwili mpaka sasa sijui unataka nini kwangu, hata hujui una deal na mtu wa aina gani"
"Samahani sidhani kama maneno yako ni sahihi sana kwa wakati kama huu, nenda kamuangalie binti yako kwanza. Dokta mimi na wewe wote tunawatumikia wananchi wetu wewe ni Waziri wa afya na mimi ni afisa mpelelezi hivyo yote ninayoyafanya natimiza wajibu wangu tu"
"Sasa katika kutimiza huo wajibu jaribu kuwa na mipaka, kuna sehemu sio za kugusa Aron, haya ondoka nyumbani kwangu" Dokta Gondwe aliongea kwa ukali
"Mimi sijavuka mipaka daktari ila napambana na waharifu wote kuhakikisha wanapata wanachostahili bila kujali cheo wala ukubwa wa mtu, ni hivyo tu mzee wangu" Inspekta Aron aliongea kwa kujiamini sana, wakati huo Dokta Gondwe alimkata jicho kali.
Inspekta Aron hakutaka kubishana zaidi, aliingia kwenye gari yake na taratibu akatoka nje ya jumba la dokta Gondwe, safari ya kurudi hospitali ya Mountenia ikaanza. Yalikuwa ni majira ya saa moja na nusu jioni, jua lilikuwa limezama na giza lilianza kuchukua nafasi yake.

"Dokta Gondwe anajiona nani kwani, sijawahi ona Waziri wa ajabu kama huyu, sijui hata serikali yangu iliwaza nini kumpa cheo kama hiki. Ona nyumba yake ina walinzi chungu nzima utadhani ni kasri la waturuki. Anafanya maovu mengi ndio sababu hata hajiamini" Inspekta Aron alikuwa akiwaza wakati huo anaendesha gari yake kwa mwendo wa wastani.

Big' alikuwa nyuma ya gari ya Inspekta Aron umbali kama hatua arobaini hivi akawa anamfuata taratibu na pikipiki yake, tayari alishajihakikisha kuwa Aron yuko peke yake ndani ya gari, sasa ulikuwa ni muda muafaka wa yeye kubonyeza kitufe cha remoti iliyokuwa mkononi mwake kuruhusu bomu alilolitega chini ya gari la Inspekta Aron lilipuke.

Alikuwa akisubiri sehemu nzuri ambayo atailipua gari ya Aron pasipo kuleta maafa kwa watu au nyumba jirani. Mwisho gari ya Inspekta Aron ilifika usawa ambao Big' aliona unafaa, akaishika rimoti yake vizuri.

"Hii itakuwa mfano kwa askari wote vimberembere kama wewe Inspekta Aron, ulazwe mahali pema" Alisema Big' kisha akabonyeza kitufe cha kuruhusu bomu kulipuka.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Bosi..bosi! umelala" sauti ya Bosco ilimkurupua Tino aliyekuwa amejiinamia mezani akiwa kwenye dimbwi la mawazo

"Nambie vipi, sijalala?" Alijibu Tino
"Saa mbili imefika ni mda wa kumpigia Dokta Gondwe sasa"
"Aah sawa twende"
Tino na kijana wake Bosco waliongozana hadi kwenye meza nyingine iliyokuwa na mitambo ya pekee tofauti na meza nyingine katika ofisi hiyo. Hilo lilikuwa ni eneo maalum la kuwasiliana na watu ambao wao waliwaita wateja yaani wale waliowarekodi video za faragha. Mitambo hiyo ilitengenezwa maalum kwa ajili ya mawasiliano kwanza ilikuwa na uwezo wa kubadili sauti kwa mtu anayezungumza na mteja sauti ambayo hubadilika na kuwa sauti nzito yenye muungurumo mkali lakini pili mitambo hiyo pia iliifanya namba wanayotumia kutoka hewani na kuwa namba ambayo haipo kabisa hadi pale watakapo iruhusu wenyewe.

"Piga, nipe mimi hiyo maiki niongee naye" Alisema Tino akikaa kwenye kiti, Bosco akamsogezea kinasa sauti.
Simu iliita upande wa pili, Dokta Gondwe na Najma binti yake walikuwa sebureni wakipata chakula cha usiku. Wakati huo Dokta Gondwe alikuwa akimuhoji maswali binti yake ni vipi aliweza kukutana na inspekta Aron wakasindikizana hadi nyumbani kwake.
Maongezi haya yalisitishwa na mlio wa simu ya Dokta Gondwe iliyokuwa juu ya meza ikiita.
Almanusura Dokta Gondwe apaliwe mara tu ya kupiga jicho na kuiona namba ya mpigaji, ilikuwa ni simu aliyokuwa akiisubiri kwa hamu.
Haraka alichukua simu akainuka na kupiga hatua ndefu ndefu kuelekea chumbani kwake. Najma alibaki na maswali mengi kichwani yasiyo na majibu, hivi karibuni ameona mabadiliko makubwa sana kwa baba yake amekuwa na tabia ambazo hajazoea kuziona. Najma hakutaka kulaza damu, hali akichechemea alijisogeza hadi kwenye mlango wa chumba cha baba yake akatega sikio kusikiliza mazungumzo ya simu yaliyokuwa yakiendela kati ya baba yake na mtu ambaye hakumtambua.

"Ndio Dokta nilikupa muda ujifikirie nataka kusikia maamuzi yako je, unanipa vimelea au niziachie hizi picha mtandaoni" sauti nzito kutoka upande wa pili wa simu ya dkt Gondwe ilisikika, haikuwa rahisi hata kidogo kibaini kuwa ile ilikuwa ni sauti ya kijana wake Tino.
"Ndiyo nimeshafikiri vya kutosha nilikuwa nasubiri simu yako tu" alijibu Dokta Gondwe
"Sawa, nakusikiliza"
"Nitakupatia vimelea vya V-COBOS, lakini kwa masharti"
"Masharti? Masharti yapi?"aliuliza Tino
"Kwanza nataka unihakikishie unafuta picha na video zote ulizonirekodi siku hiyo, pili kabla sijakupa hivi vimelea vya V-COBOS nahitaji mazungumzo ya ana kwa ana na wewe, unajua hawa vimelea ni suala la Dunia nzima siwezi kutoa kirahisi pasipo kufanya mazungumzo, nina hakika hata wewe unaelewa umuhimu wake"
Upande wa pili Tino alitulia kwa muda akijaribu kumuelewa Dokta Gondwe
"Okay subiri nakupigia simu baada ya dakika tano" alisema Tino kisha akakata simu

"Anajaribu kutaka kufanya nini huyu mzee?" Tino alijiuliza huku akifikiri kwa kina kuhusu masharti haya ya Dokta Gondwe
"Bosi tunafanyaje?" Aliuliza Bosco
"Sijui! nahitaji kufikiri kwanza, kuna kitu anakitaka huyu mzee sitakiwi kufanya makosa la sivyo nitawakosa hawa vimelea" alisema Tino huku akijaribu kuituliza akili yake.
Dokta Gondwe naye alitulia kusubiri dakika tano ziishe kuona kama ndege atanasa kwenye mtego wake. Hivi ndivyo walivyokuwa wameshauriana kufanya na Profesa Cosmas Kulolwa Rais mstaafu
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili - barabarani
"Hii itakuwa mfano kwa askari wote vimberembere kama wewe Inspekta Aron, ulazwe mahali pema" Alisema Big' kisha akabonyeza kitufe cha kuruhusu bomu kuripuka.
Tofauti na alivyotegemea gari ya Inspekta Aron haikuripuka, akabinya tena mara ya pili hali ikawa ni ile ile, akabinya mara ya tatu ya nne ya tano bado bomu halikuripuka

"Upuuzi gani huu" alisema Big' kisha akaongeza kasi ya pikipiki yake akasogea karibu kabisa na gari ya Inspekta Aron akiamini labda umbali ndio ulikuwa sababu ya bomu kutokuripuka, akabinya tena lakini bado hali ikawa ni ile ile.
Big' alijikuta anajawa na hasira, hakuelewa nini hasa sababu inayopelekea bomu lile lisiripuke. Kwa uzoefu wake hii ndio ilikuwa mara ya kwanza kitu kama kile kutokea. Alijiamini katika kazi yake hata siku moja hakuwahi kufanya makosa.
Baada ya kuona hali imekuwa ngumu aliendelea kumfuata Inspekta Aron nyuma taratibu huku bado akiendelea kujaribu bahati yake kwa kubinya rimoti kila baada ya sekunde kadhaa, hakujali tena kuhusu mazingira.
Mwisho Inspekta Aron alifika hadi hospitali ya kimataifa ya Mountenia akiwa salama salmini, akapaki gari yake akashuka na kuingia ndani ya hospitali hiyo akiwahi kwenda kumuangalia Annah.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda mfupi baada ya Inspekta Aron kuingia ndani ya hospitali, Big' alionekana akizuga zuga kuizunguuka gari ya Inspekta Aron. Alipoona usalama upo hakuna mlinzi wala mtu yeyote anaemuangalia, kwa kasi aliinama chini ya gari ya Inspekta Aron akalichomoa lile bomu alilokuwa amelitega awali kisha akasogea nalo pembeni.

"Fu***ck" Big' alijikuta anatukana kizungu baada ya kubaini kitu kilichosababisha bomu lisiripuke. Bomu la Big' lilikuwa limeloa na kunywa maji ya kutosha.
Kama utakumbuka wakati ule Aron akiwa na Najma ndani ya gari walinusurika kupata ajali huku gari ikizama kwenye dimbwi la maji. Hapo ndipo bomu la bwana Big' lilipoingia maji likapoteza uwezo wake wa kufanya kazi ipasavyo

"Bado hujashinda Inspekta Aron, hauwezi kutoboa hadi asubuhi" alisema Big' huku akichomoa bastola yake kutoka kiunoni, akafungua magazini na kubaini ilikuwa na risasi za kutosha, akatabasamu.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili katika Hotel iliyokuwa jirani na hospitali ya Mountenia, Mdunguaji Godwin maarufu kama Sniper G bado alikuwa makini akisubiri Annah akae usawa mzuri aweze kumtwanga risasi ya kichwa, kwa maelezo aliyopewa na kiongozi wake Tino alimpa masaa sita tu ahakikishe anamuua Annah.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande mwingine tayari Tino alikuwa ametuliza akili yake na alijua nini cha kumjibu Dokta Gondwe juu ya yale masharti aliyompa ili ampatie vimelea vya V-COBOS, akapiga simu kwa mara nyingine haraka Dokta Gondwe akapokea.

JE, NINI KITAFUATA?
SAKATA LA TINO NA BOSI WAKE DOKTA GONDWE LITAFIKIA WAPI?
NI NINI KIINI CHA VIMELEA HAWA HATARI?
VIPI KUHUSU ANNAH,NAJMA, OSWARD NA ARON?

ITAENDELEA....
0756862047
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu.............14
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

14-(MAWINDO NDANI YA HOSPTALI YA MOUNTENIA)
ILIPOISHIA...13
Tino alikuwa ametuliza akili yake na alijua nini cha kumjibu Dokta Gondwe juu ya yale masharti aliyompa ili ampatie vimelea vya V-COBOS, akapiga simu kwa mara nyingine haraka Dokta Gondwe akapokea.

SASA ENDELEA...
"Nimekubaliana na masharti yako" alisema Tino, Dokta Gondwe akatabasamu akiamini ushauri aliopewa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa unakwenda kufanya kazi.
"Sawa naomba tukutane....." Alisema Dkt Gondwe lakini Tino akamkatisha
"Hapana hutakiwi kupanga sehemu ya kukutana, mimi ndio nitakaepanga" alisema Tino
"Kivipi tena?"
"Mheshimiwa Waziri kama ulivyoomba kukutana na mimi nikakubali basi na wewe kubaliana na matakwa yangu kubali nipange sehemu ya kukutana na wewe"
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa kisha Dokta Gondwe akaongea

"Sawa nakusikiliza"
"Tutakutana baharini"
"Baharini?"
"Ndiyo habari ya hindi kesho saa tano kamili asubuhi"
"Kivipi?"
"Utakuja na boti yako na mimi nitakuwa na boti yangu, njoo usawa wa Kilagosi ukiwa hapo nitakutumia location nilipo utanifuata na boti yako, unatakiwa kuja wewe peke yako ukiwa na vimelea vya V-COBOS, mazungumzo na mambo yote tutamaliza ndani ya hiyo boti kila mtu atapata anachokitaka" Tino alitoa maelezo
Dokta Gondwe alitulia tena kwa muda kisha akakubaliana na matakwa ya Tino baada ya hapo akakata simu.
Baada ya kukata simu Najma ambaye alisikia karibu asilimia 90 ya mazungumzo yale alijivuta tena na kurudi mezani akaendelea kula chakula huku akiyatafakari mambo muhimu mawili ambayo aliyasikia kwenye mazungumzo yale, la kwanza ni vimelea vya V-COBOS na jambo la pili lilikuwa ni picha chafu, Najma akatamani kuelewa zaidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Boss inamaana utaenda kuonana na Waziri kivipi sasa?" Aliuliza Bosco
"Utaenda wewe badala yangu Bosco" alijibu Tino
"Mimi? Kivipi? anaweza hata kuniua"
"Sikiliza Bosco mimi nitakuwepo kukulinda, Dokta Gondwe akitaka kukuaa basi lazima atanitumia mimi na sio mtu mwingine, hata isipokuwa hivyo naweza kukulinda pia" alieleza Tino na mara dakika hiyo simu yake ikaita mpigaji alikuwa ni Dokta Gondwe

"Ona si nimekwambia bila shaka anataka kuzungumza juu ya hili hili jambo" alisema Tino kisha akapokea simu ya bosi wake
"Hallo bosi" Tino aliongea kwa unyenyekevu mkubwa, akawa Tino tofauti kabisa na yule aliyekuwa akimpa vitisho Dokta Gondwe dakika chache zilizopita

"Vipi umeshammaliza huyo Annah"
"Hapana bosi bado lakini..."
"Lakini nini Tino nimeshakueleza kuwa kipindi hiki unatakiwa uwe ngangali nikikuagiza kazi unafanya chapu tunaendelea na mambo mengine, vita ni kubwa kijana wangu"
"Bosi lakini nilikuahidi Annah hatoliona jua la asubuhi, leo lazima tumalize kazi niamini mimi"
"Sawa malizeni hiyo kazi haraka kesho kuna kazi nyingine muhimu nataka tufanye"
"Sawa bosi haina shida"
"Sawa, asubuhi na mapema nitafutie boti nzuri ambayo inaweza kubeba watu watatu kwa siri kamilisha hili kabla ya saa tatu asubuhi kisha tuonane"
"Nitafanya hivyo bosi"
Simu ikakatwa.

"Umeona sasa Bosco" alisema Tino baada ya kuhakikisha simu imekatwa
"Ndiyo bosi"
"Ndio maana nikakwambia wewe uende badala yangu, kwa tafsiri fupi kuna ujanja Dokta Gondwe anataka kuufanya ndio sababu anataka boti itakayobeba watu wake kwa siri"
"Hata mimi nimewaza hivyo bosi"
"Hapa kuna mawili huenda akaja na hao vimelea au asije nao, huenda akapanga kukuua au kukuteka sasa itabidi tucheze na akili yake"
Alisema Tino huku akionekana kuitafakari siku ya kesho kwa kina. Kama kawaida yake Tino alikuwa ni mtu anaetumia akili zaidi kuliko nguvu, hii ndio iliyokuwa siri kubwa ya mafanikio yake.

"Bosco" Tino aliita
"Naam bosi"
"Nataka ujue kuwa kuanzia leo wewe ndio mtu wangu wa karibu ninae kuamini sana, tayari umeshajua siri zangu nyingi sana, kama ulivyonilindia heshima kwa kutowaonyesha wenzako video ya ngono ya mke wangu naamini utafanya hivyo hata kwa mambo mengine. Utakuwa mkono wangu wa kuume kwa kila hatua nitakayopiga, tayari nimeshakueleza kwa kifupi kuhusu hivi vimelea vya V-COBOS ninavyovipigania kwa nguvu zote. Ni mimi na wewe ndio tutakwenda kuigeuza hii Dunia juu chini chini juu" Tino aliongea kwa hisia kali akiwa amemshika bega kijana wake Bosco
[emoji294][emoji294][emoji294]

Godwin maarufu kama Sniper G bado aliendelea kusubiri, hakuwa amepata usawa mzuri wa kumlenga Annah shabaha. Tangu alipolala hakuwa ameinuka hata mara moja ilifika wakati Godwin akachoka kufumba jicho moja na kufumbua jingine akiwa ameishika ile bunduki ya masafa marefu, lakini ilimlazimu kuendelea kwani kwa kufanya hivyo ilimfanya aweze kuona kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya chumba alicholazwa Annah.

Akiwa bado anakitazama chumba kile mara aliona mlango ukifunguliwa, kunamtu aliingia ndani. Godwin alichungulia vizuri akamtambua mtu huyo alikuwa ni Inspekta Aron.

"Yaani sikapendi haka ka jamaa, Tino asingekuwa kaka yako ningekaua mwenyewe bila kuagizwa na mtu yeyote" alisema Godwin huku akiiachia bunduki yake akasogea mbele akafunga yale madirisha ya chumba chake. Alimjua vizuri Inspekta Aron kuwa ni mtu makini sana kama angeendelea kukaa na bunduki yake pale dirishani pengine angemshtukia licha ya kwamba kulikuwa na umbali mrefu kutoka hospitali ya Mountenia hadi ilipo Hoteli hiyo.

Ni kweli mara tu baada ya Inspekta Aron kusalimiana na inspekta Jada alienda moja kwa moja hadi kwenye dirisha la chumba hicho alicholazwa Annah.
Inspekta Aron alikagua mazingira juu ya ghorofani chini pembeni kushoto kulia na mwisho mbele yake kulipokuwa na ile Hotel kubwa ya kifahari.

"Hukutakiwa kuacha pazia wazi" alisema Aron huku akirudisha mapazia na kufunga madirisha vizuri
"Ee jamani Aron unawasiwasi hadi sio poa"
"Alaah! ni kwa sababu tu hujawahi kukabiliana na watu wa Dokta Gondwe, hawa jamaa ni professional killer wana kila aina ya siraha ni watu waliojipanga sio kidogo"
"Haya sawa kwa hiyo inakuwaje ishu ya kumuamisha Annah chumba tofauti na hiki nakumbuka ulisema tayari Tino ameshajua"
"Shiiiii! mbona unaongea kwa sauti Annah hatakiwi kusikia utampa wasiwasi"
"Usijali hasikii chochote kalala tangu ulipoondoka"
"Kweli?"
"Yap wee humuoni" Alisema Jada na wote kwa pamoja wakageuka na kumtazama Annah aliyekua amelala pale kitandani

"Mmh maskini alafu haka kabinti ni kazuri, Inspekta Aron unafeli wapi owa basi mtoto mbichi kabisa huyu atakufaa" alisema Jada huku akitabasamu
"Hebu acha utani wako basi, aliyekwambia nahitaji mke ni nani"
"Kwa hiyo utaoa lini sasa?"
"Nikistaafu"
"Khee! Msikie huyu"
"Kweli, kwa kazi ninayoifanya sitakiwi kupenda kabisa"
"Kwa nini?"
"Maadui zangu watautumia kama udhaifu wangu, mwanamke wangu anaweza kujikuta anateseka bila hatia sitaki kumuweka hatarini mtoto wa mtu" alieleza Aron huku akipiga simu na kuiweka sikioni ikawa inaita
"Hahahah hayo ndo madhara ya kuangalia muvi za wazungu"
"Wala sio muvi Jada huu ni ukweli nakwambia"
"Kwa hiyo utakaa hivyo hadi lini, hivi hujawahi kutana na mwanamke alafu roho yako ikashtuka ukajikuta unaanza kumpenda penda hivi maana wewe ni mgumu sijawahi ona" aliuliza Jada swali ambalo liliugusa moyo wa Inspekta Aron kwa kiasi fulani akajikuta anakumbuka hali hiyo ilimtokea leo akiwa na mtoto wa Waziri wa afya yaani Najma

"Hapana sijawahi" Aron alidanganya
"Eeh basi ukapime"
"Subiri niongee na Dokta Zyunga... Hallo Dokta wapi.....ndio tupo kwa Annah humu tunakusubiri... yeah kuhusu kumuhamisha chumba....sawa...sawa Dokta" Aron alimaliza mawasiliano kisha akakata simu

"Kasemaje"
"Yupo ghorofa ya chini anakuja"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Big' alikuwa amekaa kwenye viti vilivyokuwa eneo la mapokezi sakafu ya chini kabisa ya hospitali ya Mountenia, ndio kwanza alikuwa anaingia akawa anajaribu kusoma mazingira ajue ataanzia wapi kumsaka Inspekta Aron.
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi wake Big' alipiga hatua akasogea hadi eneo la mapokezi alipokuwepo dada mmoja aliyemkaribisha kwa sura ya upendo.
"Karibu kaka"
"Asante, namuulizia Dokta Zyunga"
"mmm una-appointment naye?"
"ndiyo"
"Sawa basi kaa pale msubiri kidogo alitoka mara moja"

Big' alifuata maelezo yale akarudi na kukaa kwenye vile viti alivyokuwa awali. Alichokifanya Big' ilikuwa ni kumtafuta Dokta Zyunga ambaye anajua huwa yupo karibu sana na inspekta Aron. Dokta Zyunga ndiye aliyeufanyia vipimo mwili wa mtu aliyeuwawa na Osward. Hivyo Big' aliamini kupitia Dokta Zyunga angeweza kumpata kirahisi Inspekta Aron ndani ya hospitali hiyo.

Dakika chache baadae Big' alimuona Dokta Zyunga anaingia haraka akasimama alipopita naye akaanza kumfuata nyuma huku akimpungia mkono yule dada wa mapokezi ikiwa ni ishara kuwa amempata mtu wake.
Dokta Zyunga alipoingia kwenye lifti Big' naye akaingia, ni wakati huo ambao Inspekta Aron alipiga simu wakawa wanazungumza kuhusu kumuhamisha Annah.
Lifti ilisimama Dokta Zyunga akashuka Big' naye akashuka, hapo Dokta Zyunga akageuka na kumtazama.
"Habari ndugu unaelekea wapi?"
"Nani mimi?"
"Ndiyo"
"Aah! Ee.. naelekea idara ya magonjwa ya wanawake"
"Mmh! sasa wewe na hayo magonjwa wapi na wapi"
"Aah.. ni mke wangu yupo kule ametangulia"
"Sawa panda ghorofa inayofuata mkono wako wa kushoto utaona korido moja ina mshare wa manjano fuata huo uelekeo utaona chumba kilichoandikwa 'Obstetric' ingia humo"
"Sawa nashukuru Dokta" Big alijibu kisha akaanza kupandisha ngazi akifuta maelezo ya Dokta Zyunga.
Baada ya kuona Dokta Zyunga hamzingatii tena Big' aliendelea kumfuatilia nyuma nyuma kwa siri huku safari hii akiwa makini zaidi asionekane
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dokta Zyunga alifika hadi kilipo chumba alicholazwa Annah bila kujua nyuma yake alikuwa akifuatiliwa kwa siri na Big'. Aliwakuta Inspekta Aron na Inspekta Jada wamesimama mlangoni

"Vipi nimechelewa?"
"Hapana umefika wakati muafaka" alijibu Jada
"Anaendeleaje mgonjwa wetu"
"Anaahueni kwa sasa amepumzika"
Dokta Zyunga aliingia moja kwa moja kumuangalia Annah, kisha akawa anamchukua vipimo muhimu kufuatilia maendeleo yake

"Haya Jada kapumzike mimi nitakaa na Annah hadi asubuhi utakuja kunipokea" alisema Aron
"sawa lakini Aron kama Annah ameshathibitisha kuwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwepo wakati wa tukio kwa nini tusimkamate moja kwa moja"
"Jada sio kwamba sikuelewi, nakuelewa sana lakini hujui Dokta Gondwe ni kiumbe wa aina gani, maneno ya Annah pekee hayatotosha kumuweka hatiani"
"Mmh! sawa ngoja basi tumuhamishe alafu nitaondoka" alijibu Jada wakati huo Inspekta Aron alionekana kukaza macho yake kwenye kona moja ya ukuta hatua kadhaa mbele yao

"Vipi kuna nini"aliuliza Jada akimtazama Aron usoni
Badala ya kujibu Inspekta Aron alianza kupiga hatua taratibu akinyata kuelekea kwenye ile kona, wakati huo mkono wake aliuzunguusha taratibu nyuma ya kiuno chake akachomoa bastola. Inspekta Jada alibaki amesimama pale pale lakini naye akachomea bastola yake kwa tahadhari.

Akiwa amefika usawa wa ile kona Inspekta Aron aligeuka upande pili kwa kasi huku siraha yake ikiwa mbele, cha ajabu hakuona chochote akaangalia juu chini kushoto kulia hakuna kitu. Baada ya kuhakikisha kuna usalama alirudisha siraha yake mahali pake kisha akarudi alipotoka

"Kwani vipi Aron?" Aliuliza
"Ni kama nilimuona mtu anachungulia"
"Mmh! kweli?"
"Yeah lakini kupo shwari itakuwa niliona vibaya" alisema Aron, wakati huo Dokta Zyunga alitoka. Bila kupoteza muda wakaanza kufanya taratibu wa kumuhamisha Annah
[emoji294][emoji294][emoji294]
Macho ya inspekta Aron yaliona kitu sahihi kabisa kwenye ile kona alikuwepo Big' akiwachungulia, mara baada ya kuona Inspekta Aron ameshtukia uwepo wake Big' aliondoka kwa kasi akashuka ghorofa ya chini kwa bahati nzuri Aron hakuweza kumuona.

"Nitarudi kwa ajili yako Aron muhimu nimejua ni wapi ulipo" alisema Big' wakati akiondoka.
[emoji294][emoji294][emoji294]
USIKU...
Ilikuwa ni majira ya saa sita na nusu usiku, Godwin maarufu kama Sniper G alionekana akitoka kwa kasi nje ya Hoteli aliyokuwepo. Alikuwa kitembea na kugeuka nyuma mara kadhaa mkononi akiwa na lile begi lake kubwa ambalo ndani yake kulikuwa na bunduki yake ya masafa marefu.
Alitembea haraka haraka mwisho alitoka nje kabisa ya Hoteli hiyo. Mbele yake pembeni ya barabara kulikuwa na gari inamsubiri, alifika na kufungua mlango akaingia.

"Vipi?" Aliuliza mtu aliyekuwa amekaa kiti cha dereva mara tu baada ya Godwin kuingia, mtu huyu hakuwa mwingine bali Tino.
"Kila kitu kimekamilika mkuu" alijibu sniper G'
"Umemuua Annah si ndio"
"Ndiyo, risasi ya kichwa hawezi kupona" sniper G' aliongea kwa kujiamini
Tino aliwasha gari na kuondoka kwa kasi wakati huo simu yake ilikuwa ikiita, mmoja wa vijana wake alikuwa akimpigia, akapokea.
"Ee nambie dogo umeshapata aina ya boti ninayoihitaji?....sawa..kazi nzuri...haya mkapumzike sasa tuonane asubuhi kambini...ndiyo Godwin naye ameshakamilisha kazi yake hivi ndio nimetoka kumchukua....sawa" Tino alimaliza maongezi kisha akakata simu na kuongeza mwendo wa gari yake.
Upande wa pili ndani ya chumba alichokuwa Annah, damu ilionekana ikiwa imetapakaa kila kona.

JE, NINI KITAFUATA?
NI KWELI SNIPER G' KAMUUA ANNAH?
VIPI KUHUSU INSPEKTA ARON NA BIG'?
JE, SAKATA LA VIMELEA VYA V-COBOS LITAISHIA WAPI?

ITAENDELEA....
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu.............14
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

14-(MAWINDO NDANI YA HOSPTALI YA MOUNTENIA)
ILIPOISHIA...13
Tino alikuwa ametuliza akili yake na alijua nini cha kumjibu Dokta Gondwe juu ya yale masharti aliyompa ili ampatie vimelea vya V-COBOS, akapiga simu kwa mara nyingine haraka Dokta Gondwe akapokea.

SASA ENDELEA...
"Nimekubaliana na masharti yako" alisema Tino, Dokta Gondwe akatabasamu akiamini ushauri aliopewa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa unakwenda kufanya kazi.
"Sawa naomba tukutane....." Alisema Dkt Gondwe lakini Tino akamkatisha
"Hapana hutakiwi kupanga sehemu ya kukutana, mimi ndio nitakaepanga" alisema Tino
"Kivipi tena?"
"Mheshimiwa Waziri kama ulivyoomba kukutana na mimi nikakubali basi na wewe kubaliana na matakwa yangu kubali nipange sehemu ya kukutana na wewe"
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa kisha Dokta Gondwe akaongea

"Sawa nakusikiliza"
"Tutakutana baharini"
"Baharini?"
"Ndiyo habari ya hindi kesho saa tano kamili asubuhi"
"Kivipi?"
"Utakuja na boti yako na mimi nitakuwa na boti yangu, njoo usawa wa Kilagosi ukiwa hapo nitakutumia location nilipo utanifuata na boti yako, unatakiwa kuja wewe peke yako ukiwa na vimelea vya V-COBOS, mazungumzo na mambo yote tutamaliza ndani ya hiyo boti kila mtu atapata anachokitaka" Tino alitoa maelezo
Dokta Gondwe alitulia tena kwa muda kisha akakubaliana na matakwa ya Tino baada ya hapo akakata simu.
Baada ya kukata simu Najma ambaye alisikia karibu asilimia 90 ya mazungumzo yale alijivuta tena na kurudi mezani akaendelea kula chakula huku akiyatafakari mambo muhimu mawili ambayo aliyasikia kwenye mazungumzo yale, la kwanza ni vimelea vya V-COBOS na jambo la pili lilikuwa ni picha chafu, Najma akatamani kuelewa zaidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Boss inamaana utaenda kuonana na Waziri kivipi sasa?" Aliuliza Bosco
"Utaenda wewe badala yangu Bosco" alijibu Tino
"Mimi? Kivipi? anaweza hata kuniua"
"Sikiliza Bosco mimi nitakuwepo kukulinda, Dokta Gondwe akitaka kukuaa basi lazima atanitumia mimi na sio mtu mwingine, hata isipokuwa hivyo naweza kukulinda pia" alieleza Tino na mara dakika hiyo simu yake ikaita mpigaji alikuwa ni Dokta Gondwe

"Ona si nimekwambia bila shaka anataka kuzungumza juu ya hili hili jambo" alisema Tino kisha akapokea simu ya bosi wake
"Hallo bosi" Tino aliongea kwa unyenyekevu mkubwa, akawa Tino tofauti kabisa na yule aliyekuwa akimpa vitisho Dokta Gondwe dakika chache zilizopita

"Vipi umeshammaliza huyo Annah"
"Hapana bosi bado lakini..."
"Lakini nini Tino nimeshakueleza kuwa kipindi hiki unatakiwa uwe ngangali nikikuagiza kazi unafanya chapu tunaendelea na mambo mengine, vita ni kubwa kijana wangu"
"Bosi lakini nilikuahidi Annah hatoliona jua la asubuhi, leo lazima tumalize kazi niamini mimi"
"Sawa malizeni hiyo kazi haraka kesho kuna kazi nyingine muhimu nataka tufanye"
"Sawa bosi haina shida"
"Sawa, asubuhi na mapema nitafutie boti nzuri ambayo inaweza kubeba watu watatu kwa siri kamilisha hili kabla ya saa tatu asubuhi kisha tuonane"
"Nitafanya hivyo bosi"
Simu ikakatwa.

"Umeona sasa Bosco" alisema Tino baada ya kuhakikisha simu imekatwa
"Ndiyo bosi"
"Ndio maana nikakwambia wewe uende badala yangu, kwa tafsiri fupi kuna ujanja Dokta Gondwe anataka kuufanya ndio sababu anataka boti itakayobeba watu wake kwa siri"
"Hata mimi nimewaza hivyo bosi"
"Hapa kuna mawili huenda akaja na hao vimelea au asije nao, huenda akapanga kukuua au kukuteka sasa itabidi tucheze na akili yake"
Alisema Tino huku akionekana kuitafakari siku ya kesho kwa kina. Kama kawaida yake Tino alikuwa ni mtu anaetumia akili zaidi kuliko nguvu, hii ndio iliyokuwa siri kubwa ya mafanikio yake.

"Bosco" Tino aliita
"Naam bosi"
"Nataka ujue kuwa kuanzia leo wewe ndio mtu wangu wa karibu ninae kuamini sana, tayari umeshajua siri zangu nyingi sana, kama ulivyonilindia heshima kwa kutowaonyesha wenzako video ya ngono ya mke wangu naamini utafanya hivyo hata kwa mambo mengine. Utakuwa mkono wangu wa kuume kwa kila hatua nitakayopiga, tayari nimeshakueleza kwa kifupi kuhusu hivi vimelea vya V-COBOS ninavyovipigania kwa nguvu zote. Ni mimi na wewe ndio tutakwenda kuigeuza hii Dunia juu chini chini juu" Tino aliongea kwa hisia kali akiwa amemshika bega kijana wake Bosco
[emoji294][emoji294][emoji294]

Godwin maarufu kama Sniper G bado aliendelea kusubiri, hakuwa amepata usawa mzuri wa kumlenga Annah shabaha. Tangu alipolala hakuwa ameinuka hata mara moja ilifika wakati Godwin akachoka kufumba jicho moja na kufumbua jingine akiwa ameishika ile bunduki ya masafa marefu, lakini ilimlazimu kuendelea kwani kwa kufanya hivyo ilimfanya aweze kuona kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya chumba alicholazwa Annah.

Akiwa bado anakitazama chumba kile mara aliona mlango ukifunguliwa, kunamtu aliingia ndani. Godwin alichungulia vizuri akamtambua mtu huyo alikuwa ni Inspekta Aron.

"Yaani sikapendi haka ka jamaa, Tino asingekuwa kaka yako ningekaua mwenyewe bila kuagizwa na mtu yeyote" alisema Godwin huku akiiachia bunduki yake akasogea mbele akafunga yale madirisha ya chumba chake. Alimjua vizuri Inspekta Aron kuwa ni mtu makini sana kama angeendelea kukaa na bunduki yake pale dirishani pengine angemshtukia licha ya kwamba kulikuwa na umbali mrefu kutoka hospitali ya Mountenia hadi ilipo Hoteli hiyo.

Ni kweli mara tu baada ya Inspekta Aron kusalimiana na inspekta Jada alienda moja kwa moja hadi kwenye dirisha la chumba hicho alicholazwa Annah.
Inspekta Aron alikagua mazingira juu ya ghorofani chini pembeni kushoto kulia na mwisho mbele yake kulipokuwa na ile Hotel kubwa ya kifahari.

"Hukutakiwa kuacha pazia wazi" alisema Aron huku akirudisha mapazia na kufunga madirisha vizuri
"Ee jamani Aron unawasiwasi hadi sio poa"
"Alaah! ni kwa sababu tu hujawahi kukabiliana na watu wa Dokta Gondwe, hawa jamaa ni professional killer wana kila aina ya siraha ni watu waliojipanga sio kidogo"
"Haya sawa kwa hiyo inakuwaje ishu ya kumuamisha Annah chumba tofauti na hiki nakumbuka ulisema tayari Tino ameshajua"
"Shiiiii! mbona unaongea kwa sauti Annah hatakiwi kusikia utampa wasiwasi"
"Usijali hasikii chochote kalala tangu ulipoondoka"
"Kweli?"
"Yap wee humuoni" Alisema Jada na wote kwa pamoja wakageuka na kumtazama Annah aliyekua amelala pale kitandani

"Mmh maskini alafu haka kabinti ni kazuri, Inspekta Aron unafeli wapi owa basi mtoto mbichi kabisa huyu atakufaa" alisema Jada huku akitabasamu
"Hebu acha utani wako basi, aliyekwambia nahitaji mke ni nani"
"Kwa hiyo utaoa lini sasa?"
"Nikistaafu"
"Khee! Msikie huyu"
"Kweli, kwa kazi ninayoifanya sitakiwi kupenda kabisa"
"Kwa nini?"
"Maadui zangu watautumia kama udhaifu wangu, mwanamke wangu anaweza kujikuta anateseka bila hatia sitaki kumuweka hatarini mtoto wa mtu" alieleza Aron huku akipiga simu na kuiweka sikioni ikawa inaita
"Hahahah hayo ndo madhara ya kuangalia muvi za wazungu"
"Wala sio muvi Jada huu ni ukweli nakwambia"
"Kwa hiyo utakaa hivyo hadi lini, hivi hujawahi kutana na mwanamke alafu roho yako ikashtuka ukajikuta unaanza kumpenda penda hivi maana wewe ni mgumu sijawahi ona" aliuliza Jada swali ambalo liliugusa moyo wa Inspekta Aron kwa kiasi fulani akajikuta anakumbuka hali hiyo ilimtokea leo akiwa na mtoto wa Waziri wa afya yaani Najma

"Hapana sijawahi" Aron alidanganya
"Eeh basi ukapime"
"Subiri niongee na Dokta Zyunga... Hallo Dokta wapi.....ndio tupo kwa Annah humu tunakusubiri... yeah kuhusu kumuhamisha chumba....sawa...sawa Dokta" Aron alimaliza mawasiliano kisha akakata simu

"Kasemaje"
"Yupo ghorofa ya chini anakuja"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Big' alikuwa amekaa kwenye viti vilivyokuwa eneo la mapokezi sakafu ya chini kabisa ya hospitali ya Mountenia, ndio kwanza alikuwa anaingia akawa anajaribu kusoma mazingira ajue ataanzia wapi kumsaka Inspekta Aron.
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi wake Big' alipiga hatua akasogea hadi eneo la mapokezi alipokuwepo dada mmoja aliyemkaribisha kwa sura ya upendo.
"Karibu kaka"
"Asante, namuulizia Dokta Zyunga"
"mmm una-appointment naye?"
"ndiyo"
"Sawa basi kaa pale msubiri kidogo alitoka mara moja"

Big' alifuata maelezo yale akarudi na kukaa kwenye vile viti alivyokuwa awali. Alichokifanya Big' ilikuwa ni kumtafuta Dokta Zyunga ambaye anajua huwa yupo karibu sana na inspekta Aron. Dokta Zyunga ndiye aliyeufanyia vipimo mwili wa mtu aliyeuwawa na Osward. Hivyo Big' aliamini kupitia Dokta Zyunga angeweza kumpata kirahisi Inspekta Aron ndani ya hospitali hiyo.

Dakika chache baadae Big' alimuona Dokta Zyunga anaingia haraka akasimama alipopita naye akaanza kumfuata nyuma huku akimpungia mkono yule dada wa mapokezi ikiwa ni ishara kuwa amempata mtu wake.
Dokta Zyunga alipoingia kwenye lifti Big' naye akaingia, ni wakati huo ambao Inspekta Aron alipiga simu wakawa wanazungumza kuhusu kumuhamisha Annah.
Lifti ilisimama Dokta Zyunga akashuka Big' naye akashuka, hapo Dokta Zyunga akageuka na kumtazama.
"Habari ndugu unaelekea wapi?"
"Nani mimi?"
"Ndiyo"
"Aah! Ee.. naelekea idara ya magonjwa ya wanawake"
"Mmh! sasa wewe na hayo magonjwa wapi na wapi"
"Aah.. ni mke wangu yupo kule ametangulia"
"Sawa panda ghorofa inayofuata mkono wako wa kushoto utaona korido moja ina mshare wa manjano fuata huo uelekeo utaona chumba kilichoandikwa 'Obstetric' ingia humo"
"Sawa nashukuru Dokta" Big alijibu kisha akaanza kupandisha ngazi akifuta maelezo ya Dokta Zyunga.
Baada ya kuona Dokta Zyunga hamzingatii tena Big' aliendelea kumfuatilia nyuma nyuma kwa siri huku safari hii akiwa makini zaidi asionekane
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dokta Zyunga alifika hadi kilipo chumba alicholazwa Annah bila kujua nyuma yake alikuwa akifuatiliwa kwa siri na Big'. Aliwakuta Inspekta Aron na Inspekta Jada wamesimama mlangoni

"Vipi nimechelewa?"
"Hapana umefika wakati muafaka" alijibu Jada
"Anaendeleaje mgonjwa wetu"
"Anaahueni kwa sasa amepumzika"
Dokta Zyunga aliingia moja kwa moja kumuangalia Annah, kisha akawa anamchukua vipimo muhimu kufuatilia maendeleo yake

"Haya Jada kapumzike mimi nitakaa na Annah hadi asubuhi utakuja kunipokea" alisema Aron
"sawa lakini Aron kama Annah ameshathibitisha kuwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwepo wakati wa tukio kwa nini tusimkamate moja kwa moja"
"Jada sio kwamba sikuelewi, nakuelewa sana lakini hujui Dokta Gondwe ni kiumbe wa aina gani, maneno ya Annah pekee hayatotosha kumuweka hatiani"
"Mmh! sawa ngoja basi tumuhamishe alafu nitaondoka" alijibu Jada wakati huo Inspekta Aron alionekana kukaza macho yake kwenye kona moja ya ukuta hatua kadhaa mbele yao

"Vipi kuna nini"aliuliza Jada akimtazama Aron usoni
Badala ya kujibu Inspekta Aron alianza kupiga hatua taratibu akinyata kuelekea kwenye ile kona, wakati huo mkono wake aliuzunguusha taratibu nyuma ya kiuno chake akachomoa bastola. Inspekta Jada alibaki amesimama pale pale lakini naye akachomea bastola yake kwa tahadhari.

Akiwa amefika usawa wa ile kona Inspekta Aron aligeuka upande pili kwa kasi huku siraha yake ikiwa mbele, cha ajabu hakuona chochote akaangalia juu chini kushoto kulia hakuna kitu. Baada ya kuhakikisha kuna usalama alirudisha siraha yake mahali pake kisha akarudi alipotoka

"Kwani vipi Aron?" Aliuliza
"Ni kama nilimuona mtu anachungulia"
"Mmh! kweli?"
"Yeah lakini kupo shwari itakuwa niliona vibaya" alisema Aron, wakati huo Dokta Zyunga alitoka. Bila kupoteza muda wakaanza kufanya taratibu wa kumuhamisha Annah
[emoji294][emoji294][emoji294]
Macho ya inspekta Aron yaliona kitu sahihi kabisa kwenye ile kona alikuwepo Big' akiwachungulia, mara baada ya kuona Inspekta Aron ameshtukia uwepo wake Big' aliondoka kwa kasi akashuka ghorofa ya chini kwa bahati nzuri Aron hakuweza kumuona.

"Nitarudi kwa ajili yako Aron muhimu nimejua ni wapi ulipo" alisema Big' wakati akiondoka.
[emoji294][emoji294][emoji294]
USIKU...
Ilikuwa ni majira ya saa sita na nusu usiku, Godwin maarufu kama Sniper G alionekana akitoka kwa kasi nje ya Hoteli aliyokuwepo. Alikuwa kitembea na kugeuka nyuma mara kadhaa mkononi akiwa na lile begi lake kubwa ambalo ndani yake kulikuwa na bunduki yake ya masafa marefu.
Alitembea haraka haraka mwisho alitoka nje kabisa ya Hoteli hiyo. Mbele yake pembeni ya barabara kulikuwa na gari inamsubiri, alifika na kufungua mlango akaingia.

"Vipi?" Aliuliza mtu aliyekuwa amekaa kiti cha dereva mara tu baada ya Godwin kuingia, mtu huyu hakuwa mwingine bali Tino.
"Kila kitu kimekamilika mkuu" alijibu sniper G'
"Umemuua Annah si ndio"
"Ndiyo, risasi ya kichwa hawezi kupona" sniper G' aliongea kwa kujiamini
Tino aliwasha gari na kuondoka kwa kasi wakati huo simu yake ilikuwa ikiita, mmoja wa vijana wake alikuwa akimpigia, akapokea.
"Ee nambie dogo umeshapata aina ya boti ninayoihitaji?....sawa..kazi nzuri...haya mkapumzike sasa tuonane asubuhi kambini...ndiyo Godwin naye ameshakamilisha kazi yake hivi ndio nimetoka kumchukua....sawa" Tino alimaliza maongezi kisha akakata simu na kuongeza mwendo wa gari yake.
Upande wa pili ndani ya chumba alichokuwa Annah, damu ilionekana ikiwa imetapakaa kila kona.

JE, NINI KITAFUATA?
NI KWELI SNIPER G' KAMUUA ANNAH?
VIPI KUHUSU INSPEKTA ARON NA BIG'?
JE, SAKATA LA VIMELEA VYA V-COBOS LITAISHIA WAPI?

ITAENDELEA....
 

Mkuu umeirudia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…