SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #21
Weka comment yako tuendelee....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
tuko pamoja mr nakusoma vyema kutoka taimeWeka comment yako tuendelee...
MwambaWeka comment yako tuendelee....
pamoja sanaWeka comment yako tuendelee....
Kesho njoo kwa thread [emoji16]Mkuu tuendelee.
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu.............14
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
14-(MAWINDO NDANI YA HOSPTALI YA MOUNTENIA)
ILIPOISHIA...13
Tino alikuwa ametuliza akili yake na alijua nini cha kumjibu Dokta Gondwe juu ya yale masharti aliyompa ili ampatie vimelea vya V-COBOS, akapiga simu kwa mara nyingine haraka Dokta Gondwe akapokea.
SASA ENDELEA...
"Nimekubaliana na masharti yako" alisema Tino, Dokta Gondwe akatabasamu akiamini ushauri aliopewa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa unakwenda kufanya kazi.
"Sawa naomba tukutane....." Alisema Dkt Gondwe lakini Tino akamkatisha
"Hapana hutakiwi kupanga sehemu ya kukutana, mimi ndio nitakaepanga" alisema Tino
"Kivipi tena?"
"Mheshimiwa Waziri kama ulivyoomba kukutana na mimi nikakubali basi na wewe kubaliana na matakwa yangu kubali nipange sehemu ya kukutana na wewe"
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa kisha Dokta Gondwe akaongea
"Sawa nakusikiliza"
"Tutakutana baharini"
"Baharini?"
"Ndiyo habari ya hindi kesho saa tano kamili asubuhi"
"Kivipi?"
"Utakuja na boti yako na mimi nitakuwa na boti yangu, njoo usawa wa Kilagosi ukiwa hapo nitakutumia location nilipo utanifuata na boti yako, unatakiwa kuja wewe peke yako ukiwa na vimelea vya V-COBOS, mazungumzo na mambo yote tutamaliza ndani ya hiyo boti kila mtu atapata anachokitaka" Tino alitoa maelezo
Dokta Gondwe alitulia tena kwa muda kisha akakubaliana na matakwa ya Tino baada ya hapo akakata simu.
Baada ya kukata simu Najma ambaye alisikia karibu asilimia 90 ya mazungumzo yale alijivuta tena na kurudi mezani akaendelea kula chakula huku akiyatafakari mambo muhimu mawili ambayo aliyasikia kwenye mazungumzo yale, la kwanza ni vimelea vya V-COBOS na jambo la pili lilikuwa ni picha chafu, Najma akatamani kuelewa zaidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
"Boss inamaana utaenda kuonana na Waziri kivipi sasa?" Aliuliza Bosco
"Utaenda wewe badala yangu Bosco" alijibu Tino
"Mimi? Kivipi? anaweza hata kuniua"
"Sikiliza Bosco mimi nitakuwepo kukulinda, Dokta Gondwe akitaka kukuaa basi lazima atanitumia mimi na sio mtu mwingine, hata isipokuwa hivyo naweza kukulinda pia" alieleza Tino na mara dakika hiyo simu yake ikaita mpigaji alikuwa ni Dokta Gondwe
"Ona si nimekwambia bila shaka anataka kuzungumza juu ya hili hili jambo" alisema Tino kisha akapokea simu ya bosi wake
"Hallo bosi" Tino aliongea kwa unyenyekevu mkubwa, akawa Tino tofauti kabisa na yule aliyekuwa akimpa vitisho Dokta Gondwe dakika chache zilizopita
"Vipi umeshammaliza huyo Annah"
"Hapana bosi bado lakini..."
"Lakini nini Tino nimeshakueleza kuwa kipindi hiki unatakiwa uwe ngangali nikikuagiza kazi unafanya chapu tunaendelea na mambo mengine, vita ni kubwa kijana wangu"
"Bosi lakini nilikuahidi Annah hatoliona jua la asubuhi, leo lazima tumalize kazi niamini mimi"
"Sawa malizeni hiyo kazi haraka kesho kuna kazi nyingine muhimu nataka tufanye"
"Sawa bosi haina shida"
"Sawa, asubuhi na mapema nitafutie boti nzuri ambayo inaweza kubeba watu watatu kwa siri kamilisha hili kabla ya saa tatu asubuhi kisha tuonane"
"Nitafanya hivyo bosi"
Simu ikakatwa.
"Umeona sasa Bosco" alisema Tino baada ya kuhakikisha simu imekatwa
"Ndiyo bosi"
"Ndio maana nikakwambia wewe uende badala yangu, kwa tafsiri fupi kuna ujanja Dokta Gondwe anataka kuufanya ndio sababu anataka boti itakayobeba watu wake kwa siri"
"Hata mimi nimewaza hivyo bosi"
"Hapa kuna mawili huenda akaja na hao vimelea au asije nao, huenda akapanga kukuua au kukuteka sasa itabidi tucheze na akili yake"
Alisema Tino huku akionekana kuitafakari siku ya kesho kwa kina. Kama kawaida yake Tino alikuwa ni mtu anaetumia akili zaidi kuliko nguvu, hii ndio iliyokuwa siri kubwa ya mafanikio yake.
"Bosco" Tino aliita
"Naam bosi"
"Nataka ujue kuwa kuanzia leo wewe ndio mtu wangu wa karibu ninae kuamini sana, tayari umeshajua siri zangu nyingi sana, kama ulivyonilindia heshima kwa kutowaonyesha wenzako video ya ngono ya mke wangu naamini utafanya hivyo hata kwa mambo mengine. Utakuwa mkono wangu wa kuume kwa kila hatua nitakayopiga, tayari nimeshakueleza kwa kifupi kuhusu hivi vimelea vya V-COBOS ninavyovipigania kwa nguvu zote. Ni mimi na wewe ndio tutakwenda kuigeuza hii Dunia juu chini chini juu" Tino aliongea kwa hisia kali akiwa amemshika bega kijana wake Bosco
[emoji294][emoji294][emoji294]
Godwin maarufu kama Sniper G bado aliendelea kusubiri, hakuwa amepata usawa mzuri wa kumlenga Annah shabaha. Tangu alipolala hakuwa ameinuka hata mara moja ilifika wakati Godwin akachoka kufumba jicho moja na kufumbua jingine akiwa ameishika ile bunduki ya masafa marefu, lakini ilimlazimu kuendelea kwani kwa kufanya hivyo ilimfanya aweze kuona kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya chumba alicholazwa Annah.
Akiwa bado anakitazama chumba kile mara aliona mlango ukifunguliwa, kunamtu aliingia ndani. Godwin alichungulia vizuri akamtambua mtu huyo alikuwa ni Inspekta Aron.
"Yaani sikapendi haka ka jamaa, Tino asingekuwa kaka yako ningekaua mwenyewe bila kuagizwa na mtu yeyote" alisema Godwin huku akiiachia bunduki yake akasogea mbele akafunga yale madirisha ya chumba chake. Alimjua vizuri Inspekta Aron kuwa ni mtu makini sana kama angeendelea kukaa na bunduki yake pale dirishani pengine angemshtukia licha ya kwamba kulikuwa na umbali mrefu kutoka hospitali ya Mountenia hadi ilipo Hoteli hiyo.
Ni kweli mara tu baada ya Inspekta Aron kusalimiana na inspekta Jada alienda moja kwa moja hadi kwenye dirisha la chumba hicho alicholazwa Annah.
Inspekta Aron alikagua mazingira juu ya ghorofani chini pembeni kushoto kulia na mwisho mbele yake kulipokuwa na ile Hotel kubwa ya kifahari.
"Hukutakiwa kuacha pazia wazi" alisema Aron huku akirudisha mapazia na kufunga madirisha vizuri
"Ee jamani Aron unawasiwasi hadi sio poa"
"Alaah! ni kwa sababu tu hujawahi kukabiliana na watu wa Dokta Gondwe, hawa jamaa ni professional killer wana kila aina ya siraha ni watu waliojipanga sio kidogo"
"Haya sawa kwa hiyo inakuwaje ishu ya kumuamisha Annah chumba tofauti na hiki nakumbuka ulisema tayari Tino ameshajua"
"Shiiiii! mbona unaongea kwa sauti Annah hatakiwi kusikia utampa wasiwasi"
"Usijali hasikii chochote kalala tangu ulipoondoka"
"Kweli?"
"Yap wee humuoni" Alisema Jada na wote kwa pamoja wakageuka na kumtazama Annah aliyekua amelala pale kitandani
"Mmh maskini alafu haka kabinti ni kazuri, Inspekta Aron unafeli wapi owa basi mtoto mbichi kabisa huyu atakufaa" alisema Jada huku akitabasamu
"Hebu acha utani wako basi, aliyekwambia nahitaji mke ni nani"
"Kwa hiyo utaoa lini sasa?"
"Nikistaafu"
"Khee! Msikie huyu"
"Kweli, kwa kazi ninayoifanya sitakiwi kupenda kabisa"
"Kwa nini?"
"Maadui zangu watautumia kama udhaifu wangu, mwanamke wangu anaweza kujikuta anateseka bila hatia sitaki kumuweka hatarini mtoto wa mtu" alieleza Aron huku akipiga simu na kuiweka sikioni ikawa inaita
"Hahahah hayo ndo madhara ya kuangalia muvi za wazungu"
"Wala sio muvi Jada huu ni ukweli nakwambia"
"Kwa hiyo utakaa hivyo hadi lini, hivi hujawahi kutana na mwanamke alafu roho yako ikashtuka ukajikuta unaanza kumpenda penda hivi maana wewe ni mgumu sijawahi ona" aliuliza Jada swali ambalo liliugusa moyo wa Inspekta Aron kwa kiasi fulani akajikuta anakumbuka hali hiyo ilimtokea leo akiwa na mtoto wa Waziri wa afya yaani Najma
"Hapana sijawahi" Aron alidanganya
"Eeh basi ukapime"
"Subiri niongee na Dokta Zyunga... Hallo Dokta wapi.....ndio tupo kwa Annah humu tunakusubiri... yeah kuhusu kumuhamisha chumba....sawa...sawa Dokta" Aron alimaliza mawasiliano kisha akakata simu
"Kasemaje"
"Yupo ghorofa ya chini anakuja"
[emoji294][emoji294][emoji294]
Big' alikuwa amekaa kwenye viti vilivyokuwa eneo la mapokezi sakafu ya chini kabisa ya hospitali ya Mountenia, ndio kwanza alikuwa anaingia akawa anajaribu kusoma mazingira ajue ataanzia wapi kumsaka Inspekta Aron.
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi wake Big' alipiga hatua akasogea hadi eneo la mapokezi alipokuwepo dada mmoja aliyemkaribisha kwa sura ya upendo.
"Karibu kaka"
"Asante, namuulizia Dokta Zyunga"
"mmm una-appointment naye?"
"ndiyo"
"Sawa basi kaa pale msubiri kidogo alitoka mara moja"
Big' alifuata maelezo yale akarudi na kukaa kwenye vile viti alivyokuwa awali. Alichokifanya Big' ilikuwa ni kumtafuta Dokta Zyunga ambaye anajua huwa yupo karibu sana na inspekta Aron. Dokta Zyunga ndiye aliyeufanyia vipimo mwili wa mtu aliyeuwawa na Osward. Hivyo Big' aliamini kupitia Dokta Zyunga angeweza kumpata kirahisi Inspekta Aron ndani ya hospitali hiyo.
Dakika chache baadae Big' alimuona Dokta Zyunga anaingia haraka akasimama alipopita naye akaanza kumfuata nyuma huku akimpungia mkono yule dada wa mapokezi ikiwa ni ishara kuwa amempata mtu wake.
Dokta Zyunga alipoingia kwenye lifti Big' naye akaingia, ni wakati huo ambao Inspekta Aron alipiga simu wakawa wanazungumza kuhusu kumuhamisha Annah.
Lifti ilisimama Dokta Zyunga akashuka Big' naye akashuka, hapo Dokta Zyunga akageuka na kumtazama.
"Habari ndugu unaelekea wapi?"
"Nani mimi?"
"Ndiyo"
"Aah! Ee.. naelekea idara ya magonjwa ya wanawake"
"Mmh! sasa wewe na hayo magonjwa wapi na wapi"
"Aah.. ni mke wangu yupo kule ametangulia"
"Sawa panda ghorofa inayofuata mkono wako wa kushoto utaona korido moja ina mshare wa manjano fuata huo uelekeo utaona chumba kilichoandikwa 'Obstetric' ingia humo"
"Sawa nashukuru Dokta" Big alijibu kisha akaanza kupandisha ngazi akifuta maelezo ya Dokta Zyunga.
Baada ya kuona Dokta Zyunga hamzingatii tena Big' aliendelea kumfuatilia nyuma nyuma kwa siri huku safari hii akiwa makini zaidi asionekane
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dokta Zyunga alifika hadi kilipo chumba alicholazwa Annah bila kujua nyuma yake alikuwa akifuatiliwa kwa siri na Big'. Aliwakuta Inspekta Aron na Inspekta Jada wamesimama mlangoni
"Vipi nimechelewa?"
"Hapana umefika wakati muafaka" alijibu Jada
"Anaendeleaje mgonjwa wetu"
"Anaahueni kwa sasa amepumzika"
Dokta Zyunga aliingia moja kwa moja kumuangalia Annah, kisha akawa anamchukua vipimo muhimu kufuatilia maendeleo yake
"Haya Jada kapumzike mimi nitakaa na Annah hadi asubuhi utakuja kunipokea" alisema Aron
"sawa lakini Aron kama Annah ameshathibitisha kuwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwepo wakati wa tukio kwa nini tusimkamate moja kwa moja"
"Jada sio kwamba sikuelewi, nakuelewa sana lakini hujui Dokta Gondwe ni kiumbe wa aina gani, maneno ya Annah pekee hayatotosha kumuweka hatiani"
"Mmh! sawa ngoja basi tumuhamishe alafu nitaondoka" alijibu Jada wakati huo Inspekta Aron alionekana kukaza macho yake kwenye kona moja ya ukuta hatua kadhaa mbele yao
"Vipi kuna nini"aliuliza Jada akimtazama Aron usoni
Badala ya kujibu Inspekta Aron alianza kupiga hatua taratibu akinyata kuelekea kwenye ile kona, wakati huo mkono wake aliuzunguusha taratibu nyuma ya kiuno chake akachomoa bastola. Inspekta Jada alibaki amesimama pale pale lakini naye akachomea bastola yake kwa tahadhari.
Akiwa amefika usawa wa ile kona Inspekta Aron aligeuka upande pili kwa kasi huku siraha yake ikiwa mbele, cha ajabu hakuona chochote akaangalia juu chini kushoto kulia hakuna kitu. Baada ya kuhakikisha kuna usalama alirudisha siraha yake mahali pake kisha akarudi alipotoka
"Kwani vipi Aron?" Aliuliza
"Ni kama nilimuona mtu anachungulia"
"Mmh! kweli?"
"Yeah lakini kupo shwari itakuwa niliona vibaya" alisema Aron, wakati huo Dokta Zyunga alitoka. Bila kupoteza muda wakaanza kufanya taratibu wa kumuhamisha Annah
[emoji294][emoji294][emoji294]
Macho ya inspekta Aron yaliona kitu sahihi kabisa kwenye ile kona alikuwepo Big' akiwachungulia, mara baada ya kuona Inspekta Aron ameshtukia uwepo wake Big' aliondoka kwa kasi akashuka ghorofa ya chini kwa bahati nzuri Aron hakuweza kumuona.
"Nitarudi kwa ajili yako Aron muhimu nimejua ni wapi ulipo" alisema Big' wakati akiondoka.
[emoji294][emoji294][emoji294]
USIKU...
Ilikuwa ni majira ya saa sita na nusu usiku, Godwin maarufu kama Sniper G alionekana akitoka kwa kasi nje ya Hoteli aliyokuwepo. Alikuwa kitembea na kugeuka nyuma mara kadhaa mkononi akiwa na lile begi lake kubwa ambalo ndani yake kulikuwa na bunduki yake ya masafa marefu.
Alitembea haraka haraka mwisho alitoka nje kabisa ya Hoteli hiyo. Mbele yake pembeni ya barabara kulikuwa na gari inamsubiri, alifika na kufungua mlango akaingia.
"Vipi?" Aliuliza mtu aliyekuwa amekaa kiti cha dereva mara tu baada ya Godwin kuingia, mtu huyu hakuwa mwingine bali Tino.
"Kila kitu kimekamilika mkuu" alijibu sniper G'
"Umemuua Annah si ndio"
"Ndiyo, risasi ya kichwa hawezi kupona" sniper G' aliongea kwa kujiamini
Tino aliwasha gari na kuondoka kwa kasi wakati huo simu yake ilikuwa ikiita, mmoja wa vijana wake alikuwa akimpigia, akapokea.
"Ee nambie dogo umeshapata aina ya boti ninayoihitaji?....sawa..kazi nzuri...haya mkapumzike sasa tuonane asubuhi kambini...ndiyo Godwin naye ameshakamilisha kazi yake hivi ndio nimetoka kumchukua....sawa" Tino alimaliza maongezi kisha akakata simu na kuongeza mwendo wa gari yake.
Upande wa pili ndani ya chumba alichokuwa Annah, damu ilionekana ikiwa imetapakaa kila kona.
JE, NINI KITAFUATA?
NI KWELI SNIPER G' KAMUUA ANNAH?
VIPI KUHUSU INSPEKTA ARON NA BIG'?
JE, SAKATA LA VIMELEA VYA V-COBOS LITAISHIA WAPI?
ITAENDELEA....