Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 26
Nikamkuta Carlos akiwa amesimama huku akitabasamu.
Nikashtuka sana kwani sikumtegemea Carlos kwa wakati ule kabisa.
Ikabidi nimuulize kwanza kabla ya kumkaribisha ndani.
"Khee Carlos mbona gafla! Halafu umekuja moja kwa moja nyumbani"
"Kwani ni vibaya kukutembelea Sabrina?"
"Si vibaya ila ungekuja kwa taarifa kamili kuliko kunishtukiza kama hivi"
"Usijali Sabrina, nilikuwa napita hapa nje kwenu nikaona itakuwa vyema kama nikija kuwasalimia kwanza"
"Kwahiyo leo humwogopi wifi?"
"Sina kawaida ya kumwogopa mtu na nimekuja kwa lengo la kumwonyesha wifi yako kuwa mimi ni binadamu wa kawaida tu kama wengine."
Ikabidi nimkaribishe Carlos ndani kabisa kwani alijitoa kututembelea.
Kuingia ndani, tulimkuta wifi akiwa amekaa tena na mawazo sana.
Ile kumuona tu Carlos akiingia ndani kabisa, wifi akainuka na kuanza kuongea kwa hasira.
"Sabrina, kwanini umemkaribisha huyu mtu ndani?"
"Amekuja kututembelea wifi"
Wifi akamwangalia Carlos na kuanza kusema.
"Wewe shetani toka kwenye nyumba yangu"
Carlos akaanza kucheka tena kwa furaha kabisa.
"Unaniita shetani sababu nazijua siri zako! Au niziseme zingine hapa mbele ya Sabrina?"
Wifi akanywea kwanza na kusema.
"Najua unataka kunipunguzia imani kwavile umeona kuwa mimi ni mcha Mungu"
Carlos akacheka tena na kusema.
"Tatizo lako kubwa ni kuniita mimi shetani ndio useme sasa ushetani wangu uko wapi?"
Nikamuona wifi akiwa kimya kabisa na kukosa cha kujibu kwakweli. Wifi alikuwa akimuangalia Carlos kwa uoga tu.
"Unapokuwa mtu mwema jaribu kusema yote unayoyafanya siri ili uaminike. Wewe mwanamke, umeweka siri ngapi hadi leo? Niziseme kwa Sabrina?"
Wifi alitulia kimya kabisa na kushindwa kusema chochote, nilimuona akikaa kitini kwa uoga.
Carlos akamsogelea wifi na kumnong'oneza kitu sikioni kisha akanifata na kuniaga huku akitaka nimsindikize, kwakweli nilikuwa nimetulia kimya muda wote nikiangalia mabishano ya Carlos na wifi yangu.
Nikaongozana na Carlos hadi nje, akapanda kwenye gari yake na kuniambia.
"Nitakuja badae kukutembelea"
"Badae ya muda gani? Maana muda umeisha!"
"Ooh samahani, namaanisha kesho"
Kisha Carlos akaondoka.
Nikiwa bado pale nje nikaona gari ya kaka ikiwasili, naye akaingiza gari na kushuka kisha nikaongozana nae kuingia sebleni.
Tukamkuta wifi ametoa mimacho kama mtu anayeugua, kaka akamshtua wifi nae wifi aliposhtuka moja kwa moja akataja "James" kaka akadakia.
"Kafanyaje mtoto wetu James?"
Nadhani ni hapo wifi akarudiwa na ufahamu wa kawaida.
"Hajafanya kitu mume wangu"
"Mbona ulikuwa umetoa mimacho hapa?"
"Ni uchovu tu mume wangu"
Basi kaka akaongea pale mawili matatu na kupumzika kwa uchovu pale sebleni.
Muda wa kula ulipofika, tulienda kula.
Baada ya kupumzika nikainuka ili niende kulala, wifi akaninong'oneza
"Kuwa makini usiku wa leo Sabrina"
Nikamuitikia wifi na kwenda kulala huku nikiyatafakari maneno yake ila usingizi nao ukanipitia.
Wakati nimelala nikamuona yule kijana wa ndotoni akiwa mahali na mimi kwa mazungumzo.
"Unapenda kuumia Sabrina?"
Nikatingisha kichwa nikiashiria kuwa sipendi.
"Je, unapenda kuutesa moyo wako kwa maumivu?"
Nikakataa pia.
"Basi kama hupendi rudi nyumbani kwenu"
Hapo nikashangaa na kushtuka, ile sauti ikawa inapiga kama mwangwi mule chumbani.
"Rudi kwenu Sabrina, rudi nyumbani"
Nikaanza kuogopa na kutetemeka kwani mambo ya ajabu yalinianya tena, nikabahatika kuinuka pale kitandani na kukimbilia sebleni.
Nikamkuta wifi akimbembeleza mtoto wake aliyekuwa analia sana usiku ule, ila nae aliponiona akaniambia.
"Rudi nyumbani Sabrina"
Nikaogopa na kumuuliza vizuri.
"Unasemaje wifi?"
Wifi nae akajibu kwa mshangao.
"Kwani nimesemaje?"
"Inamaana hujui ulichokisema?"
"Sijasema chochote Sabrina, si unaona mwenyewe nahangaika na mtoto hapa hataki hata kulala"
"Mmh wifi! Umeniambia nirudi nyumbani"
Ni hapo ambapo wifi alishtuka na kuniuliza kwa makini nami nikarudia nilichosema.
"Kuna kitu Sabrina, kuna kitu kipo ndani humu. Siwezi kukwambia hivyo hata mara moja. Ona mtoto anavyolia hataki hata kutulia. Nipe mikono yako Sabrina"
Wifi akanishika mikono na kuanza kuomba, haikupita muda sana hali ikawa shwari kabisa ila sikujisikia tena kulala.
Niliongea na wifi pale hadi mtoto akalala, halafu mimi na wifi tukalala pale pale.
Kulipokucha tuliendelea na kazi kama kawaida kisha wifi akaniuliza kuhusu usiku uliopita.
"Hivi ni kweli ulinisikia mimi usiku nikiongea ulivyosema?"
"Ndio wifi, wewe ndio ulisema"
"Mimi siwezi kukwambia hayo maneno Sabrina, huyo ni shetani na lazima tumuaibishe"
"Kivipi wifi?"
"Lazima shetani aaibike, wewe huendi popote utabaki hapa hapa na kesho nitakupeleka kwa mchungaji akakufanyie maombi kamili"
"Sawa wifi yangu, nitafurahi ikiwa hivyo ili na mimi niweze kuwa huru"
"Najua hilo Sabrina, amekufanya kuwa mtumwa wake na lazima ashindwe"
Mara nikapigiwa simu muda huo huo na Carlos.
Nikapokea ili kumsikia anachotaka kuniambia.
"Naomba tuonane Sabrina"
"Tuonane wapi?"
"Palepale pa siku zote"
Sikuwa na pingamizi kwavile nimekuwa nikikutana nae mara nyingi tu.
Nikamuaga wifi kuwa naenda dukani, nae hakunizuia kwavile hakujua niendako.
Nilimkuta Carlos mahali pale akiwa na hasira sana hadi nikashangaa kwani sijawahi kumuona Carlos akiwa na hasira kiasi kile.
"Mbona umechukia hivyo Carlos?"
"Kuna watu wanataka niwaonyeshe kuwa nina uwezo wa kiasi gani na mimi ni mtu wa aina gani"
"Kwanini?"
Akaniangalia sana na kuniuliza.
"Unaniamini Sabrina?"
"Ndio nakuamini kwani vipi?"
"Vizuri sana kama unaniamini, nakuahidi kuwa nitakufanyia mambo mengi sana"
"Kama yapi?"
"Tulia utauona uwezo wangu niliopewa na Mungu"
Nikamuangalia tu bila ya kuelewa chochote, kisha akasema.
"Unajua kwanini wifi yako alishindwa kutoa ile mimba?"
"Mi sijui ila nadhani ni kwavile imani yake haimruhusu"
"Imani yake haimruhusu! Unajua ni mimba ngapi alitoa hapo kabla?"
Nikazidi kumshangaa Carlos, kisha akaniambia kuwa nikamuulize kuwa ni mimba ngapi alitoa kabla na kusema atakuja badae kunitembelea tena. Nikaondoka na kurudi nyumbani bila kuelewa nia na dhumuni la Carlos ni nini kwenye maisha ya wifi yangu.
Nilipofika nyumbani wifi alikuwa ametulia kama kawaida yake na aliponiona akafurahi kurudi kwangu.
"Bora umerudi wifi yangu"
"Kuna kitu nataka nikuulize wifi"
"Uliza tu"
"Ushawahi kutoa mimba?"
"Swali gani hilo Sabrina? Unajua wazi kutoa mimba ni dhambi, haina tofauti na kuua. Kwani umepata mimba mdogo wangu?"
"Hapana, sina mimba wifi"
"Mbona umeniuliza kuhusu kutoa mimba? Unataka nikwambie maumivu yake? Kama una mimba Sabrina usithubutu kuitoa, ni dhambi sana mbele za Mungu wetu"
"Sawa wifi nimekuelewa"
Ila hakujibu swali langu kama amewahi kutoa mimba au la.
Nikiwa nazungumza na wifi, nikapigiwa simu na Sam.
Ile kupokea tu akaanza kuongea moja kwa moja.
"Hata kama tumegombana Sabrina, si vizuri kunitumia ujumbe wa kunitusi kiasi hiki"
"Ujumbe wa kukutusi? Nimekutumia saa ngapi? Umechanganyikiwa wewe"
"Sabrina, asante sana hata kama unasema kuwa nimechanganyikiwa asante sana ila kunitusi si vizuri. Kukupenda sio kosa Sabrina"
Halafu akakata simu, nikabaki nashangaa tu. Mara kidogo ukaingia ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwa Sam.
"Poa tu Sabrina kwa kunikatia simu"
Hapo nikahisi ni wazi Sam hajielewi kwa sasa na kudhani labda amechanganywa na Lucy, sasa hasira zake ndio anamalizia kwangu.
Na ubaya simu yangu haikuwa na salio hivyo nikashindwa kumpigia wala kujibu ujumbe wake kwahiyo nikawa kimya kabisa huku nikitafakari na kushangaa tu kuwa kwanini Sam amekuwa vile alivyokuwa.
Ila haukupita muda sana nikapigiwa simu na Carlos kisha akaomba kuzungumza na wifi yangu, nikamuwekea wifi ile simu sikioni ila baada ya dakika chache niliona wifi akishusha ile simu taratibu tena bila ya kusema chochote, nikamuuliza.
"Amekwambiaje kwani?"
Wifi alinitazama tu bila ya kunijibu, ikabidi nikaendelee na kazi zangu za jioni hadi pale kaka aliporudi toka kwenye kazi yake.
Nikamsalimia na kuendelea na mambo mengine, nikaandaa chakula mezani lakini hawakuja kula ikabidi nile na kwenda chumbani kwangu kupumzika kwani wifi hakunijibu chochote tangu muda alioongea na Carlos.
Usiku wa leo ulikuwa wa ajabu sana, nilikosa raha kabisa nikiwa mule chumbani ukizingatia hata chakula nilichopika hakikuliwa na wifi pamoja na kaka kwahiyo nikawa najiuliza nini tatizo mpaka inakuwa hivi.
Sikupata jibu lolote kwakweli, nikaamua tena kwenda sebleni kuona kama wifi na kaka wameenda kulala, ila niliwakuta pale pale tena kaka akiwa amelala kwa kujinyoosha kwenye kitu kitendo ambacho kilinichanganya.
Wifi alikuwa amekaa na mtoto mikononi, nikaamua kumsogelea na kumuuliza kuhusu kaka ili amwamshe akalale, na muda huu wifi alinijibu kila nilichomuuliza pale.
"Wifi mbona hivyo, mwamshe kaka akalale ndani"
"Mwangalie kaka yako alivyo Sabrina"
Moyo wangu ukalia paaa kwa uoga, na kuuliza kwa taharuki.
"Kwani ana nini?"
"Wee msogelee tu umwangalie"
Nikamsogelea kaka kwa uoga na kumwangalia kwa makini huku na uoga ukiniandama ila nilimuona kuwa yupo sawa.
"Mbona yupo sawa wifi!"
"Mwangalie vizuri Sabrina"
Huku wifi machozi yakimlengalenga nami hofu ikanizidi na kujaribu kumuamsha kaka ila hakushtuka wala kutingishika alikuwa kama vile mtu aliyekufa, uoga ukanijaa zaidi.
Itaendelea…!!
Nikamkuta Carlos akiwa amesimama huku akitabasamu.
Nikashtuka sana kwani sikumtegemea Carlos kwa wakati ule kabisa.
Ikabidi nimuulize kwanza kabla ya kumkaribisha ndani.
"Khee Carlos mbona gafla! Halafu umekuja moja kwa moja nyumbani"
"Kwani ni vibaya kukutembelea Sabrina?"
"Si vibaya ila ungekuja kwa taarifa kamili kuliko kunishtukiza kama hivi"
"Usijali Sabrina, nilikuwa napita hapa nje kwenu nikaona itakuwa vyema kama nikija kuwasalimia kwanza"
"Kwahiyo leo humwogopi wifi?"
"Sina kawaida ya kumwogopa mtu na nimekuja kwa lengo la kumwonyesha wifi yako kuwa mimi ni binadamu wa kawaida tu kama wengine."
Ikabidi nimkaribishe Carlos ndani kabisa kwani alijitoa kututembelea.
Kuingia ndani, tulimkuta wifi akiwa amekaa tena na mawazo sana.
Ile kumuona tu Carlos akiingia ndani kabisa, wifi akainuka na kuanza kuongea kwa hasira.
"Sabrina, kwanini umemkaribisha huyu mtu ndani?"
"Amekuja kututembelea wifi"
Wifi akamwangalia Carlos na kuanza kusema.
"Wewe shetani toka kwenye nyumba yangu"
Carlos akaanza kucheka tena kwa furaha kabisa.
"Unaniita shetani sababu nazijua siri zako! Au niziseme zingine hapa mbele ya Sabrina?"
Wifi akanywea kwanza na kusema.
"Najua unataka kunipunguzia imani kwavile umeona kuwa mimi ni mcha Mungu"
Carlos akacheka tena na kusema.
"Tatizo lako kubwa ni kuniita mimi shetani ndio useme sasa ushetani wangu uko wapi?"
Nikamuona wifi akiwa kimya kabisa na kukosa cha kujibu kwakweli. Wifi alikuwa akimuangalia Carlos kwa uoga tu.
"Unapokuwa mtu mwema jaribu kusema yote unayoyafanya siri ili uaminike. Wewe mwanamke, umeweka siri ngapi hadi leo? Niziseme kwa Sabrina?"
Wifi alitulia kimya kabisa na kushindwa kusema chochote, nilimuona akikaa kitini kwa uoga.
Carlos akamsogelea wifi na kumnong'oneza kitu sikioni kisha akanifata na kuniaga huku akitaka nimsindikize, kwakweli nilikuwa nimetulia kimya muda wote nikiangalia mabishano ya Carlos na wifi yangu.
Nikaongozana na Carlos hadi nje, akapanda kwenye gari yake na kuniambia.
"Nitakuja badae kukutembelea"
"Badae ya muda gani? Maana muda umeisha!"
"Ooh samahani, namaanisha kesho"
Kisha Carlos akaondoka.
Nikiwa bado pale nje nikaona gari ya kaka ikiwasili, naye akaingiza gari na kushuka kisha nikaongozana nae kuingia sebleni.
Tukamkuta wifi ametoa mimacho kama mtu anayeugua, kaka akamshtua wifi nae wifi aliposhtuka moja kwa moja akataja "James" kaka akadakia.
"Kafanyaje mtoto wetu James?"
Nadhani ni hapo wifi akarudiwa na ufahamu wa kawaida.
"Hajafanya kitu mume wangu"
"Mbona ulikuwa umetoa mimacho hapa?"
"Ni uchovu tu mume wangu"
Basi kaka akaongea pale mawili matatu na kupumzika kwa uchovu pale sebleni.
Muda wa kula ulipofika, tulienda kula.
Baada ya kupumzika nikainuka ili niende kulala, wifi akaninong'oneza
"Kuwa makini usiku wa leo Sabrina"
Nikamuitikia wifi na kwenda kulala huku nikiyatafakari maneno yake ila usingizi nao ukanipitia.
Wakati nimelala nikamuona yule kijana wa ndotoni akiwa mahali na mimi kwa mazungumzo.
"Unapenda kuumia Sabrina?"
Nikatingisha kichwa nikiashiria kuwa sipendi.
"Je, unapenda kuutesa moyo wako kwa maumivu?"
Nikakataa pia.
"Basi kama hupendi rudi nyumbani kwenu"
Hapo nikashangaa na kushtuka, ile sauti ikawa inapiga kama mwangwi mule chumbani.
"Rudi kwenu Sabrina, rudi nyumbani"
Nikaanza kuogopa na kutetemeka kwani mambo ya ajabu yalinianya tena, nikabahatika kuinuka pale kitandani na kukimbilia sebleni.
Nikamkuta wifi akimbembeleza mtoto wake aliyekuwa analia sana usiku ule, ila nae aliponiona akaniambia.
"Rudi nyumbani Sabrina"
Nikaogopa na kumuuliza vizuri.
"Unasemaje wifi?"
Wifi nae akajibu kwa mshangao.
"Kwani nimesemaje?"
"Inamaana hujui ulichokisema?"
"Sijasema chochote Sabrina, si unaona mwenyewe nahangaika na mtoto hapa hataki hata kulala"
"Mmh wifi! Umeniambia nirudi nyumbani"
Ni hapo ambapo wifi alishtuka na kuniuliza kwa makini nami nikarudia nilichosema.
"Kuna kitu Sabrina, kuna kitu kipo ndani humu. Siwezi kukwambia hivyo hata mara moja. Ona mtoto anavyolia hataki hata kutulia. Nipe mikono yako Sabrina"
Wifi akanishika mikono na kuanza kuomba, haikupita muda sana hali ikawa shwari kabisa ila sikujisikia tena kulala.
Niliongea na wifi pale hadi mtoto akalala, halafu mimi na wifi tukalala pale pale.
Kulipokucha tuliendelea na kazi kama kawaida kisha wifi akaniuliza kuhusu usiku uliopita.
"Hivi ni kweli ulinisikia mimi usiku nikiongea ulivyosema?"
"Ndio wifi, wewe ndio ulisema"
"Mimi siwezi kukwambia hayo maneno Sabrina, huyo ni shetani na lazima tumuaibishe"
"Kivipi wifi?"
"Lazima shetani aaibike, wewe huendi popote utabaki hapa hapa na kesho nitakupeleka kwa mchungaji akakufanyie maombi kamili"
"Sawa wifi yangu, nitafurahi ikiwa hivyo ili na mimi niweze kuwa huru"
"Najua hilo Sabrina, amekufanya kuwa mtumwa wake na lazima ashindwe"
Mara nikapigiwa simu muda huo huo na Carlos.
Nikapokea ili kumsikia anachotaka kuniambia.
"Naomba tuonane Sabrina"
"Tuonane wapi?"
"Palepale pa siku zote"
Sikuwa na pingamizi kwavile nimekuwa nikikutana nae mara nyingi tu.
Nikamuaga wifi kuwa naenda dukani, nae hakunizuia kwavile hakujua niendako.
Nilimkuta Carlos mahali pale akiwa na hasira sana hadi nikashangaa kwani sijawahi kumuona Carlos akiwa na hasira kiasi kile.
"Mbona umechukia hivyo Carlos?"
"Kuna watu wanataka niwaonyeshe kuwa nina uwezo wa kiasi gani na mimi ni mtu wa aina gani"
"Kwanini?"
Akaniangalia sana na kuniuliza.
"Unaniamini Sabrina?"
"Ndio nakuamini kwani vipi?"
"Vizuri sana kama unaniamini, nakuahidi kuwa nitakufanyia mambo mengi sana"
"Kama yapi?"
"Tulia utauona uwezo wangu niliopewa na Mungu"
Nikamuangalia tu bila ya kuelewa chochote, kisha akasema.
"Unajua kwanini wifi yako alishindwa kutoa ile mimba?"
"Mi sijui ila nadhani ni kwavile imani yake haimruhusu"
"Imani yake haimruhusu! Unajua ni mimba ngapi alitoa hapo kabla?"
Nikazidi kumshangaa Carlos, kisha akaniambia kuwa nikamuulize kuwa ni mimba ngapi alitoa kabla na kusema atakuja badae kunitembelea tena. Nikaondoka na kurudi nyumbani bila kuelewa nia na dhumuni la Carlos ni nini kwenye maisha ya wifi yangu.
Nilipofika nyumbani wifi alikuwa ametulia kama kawaida yake na aliponiona akafurahi kurudi kwangu.
"Bora umerudi wifi yangu"
"Kuna kitu nataka nikuulize wifi"
"Uliza tu"
"Ushawahi kutoa mimba?"
"Swali gani hilo Sabrina? Unajua wazi kutoa mimba ni dhambi, haina tofauti na kuua. Kwani umepata mimba mdogo wangu?"
"Hapana, sina mimba wifi"
"Mbona umeniuliza kuhusu kutoa mimba? Unataka nikwambie maumivu yake? Kama una mimba Sabrina usithubutu kuitoa, ni dhambi sana mbele za Mungu wetu"
"Sawa wifi nimekuelewa"
Ila hakujibu swali langu kama amewahi kutoa mimba au la.
Nikiwa nazungumza na wifi, nikapigiwa simu na Sam.
Ile kupokea tu akaanza kuongea moja kwa moja.
"Hata kama tumegombana Sabrina, si vizuri kunitumia ujumbe wa kunitusi kiasi hiki"
"Ujumbe wa kukutusi? Nimekutumia saa ngapi? Umechanganyikiwa wewe"
"Sabrina, asante sana hata kama unasema kuwa nimechanganyikiwa asante sana ila kunitusi si vizuri. Kukupenda sio kosa Sabrina"
Halafu akakata simu, nikabaki nashangaa tu. Mara kidogo ukaingia ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwa Sam.
"Poa tu Sabrina kwa kunikatia simu"
Hapo nikahisi ni wazi Sam hajielewi kwa sasa na kudhani labda amechanganywa na Lucy, sasa hasira zake ndio anamalizia kwangu.
Na ubaya simu yangu haikuwa na salio hivyo nikashindwa kumpigia wala kujibu ujumbe wake kwahiyo nikawa kimya kabisa huku nikitafakari na kushangaa tu kuwa kwanini Sam amekuwa vile alivyokuwa.
Ila haukupita muda sana nikapigiwa simu na Carlos kisha akaomba kuzungumza na wifi yangu, nikamuwekea wifi ile simu sikioni ila baada ya dakika chache niliona wifi akishusha ile simu taratibu tena bila ya kusema chochote, nikamuuliza.
"Amekwambiaje kwani?"
Wifi alinitazama tu bila ya kunijibu, ikabidi nikaendelee na kazi zangu za jioni hadi pale kaka aliporudi toka kwenye kazi yake.
Nikamsalimia na kuendelea na mambo mengine, nikaandaa chakula mezani lakini hawakuja kula ikabidi nile na kwenda chumbani kwangu kupumzika kwani wifi hakunijibu chochote tangu muda alioongea na Carlos.
Usiku wa leo ulikuwa wa ajabu sana, nilikosa raha kabisa nikiwa mule chumbani ukizingatia hata chakula nilichopika hakikuliwa na wifi pamoja na kaka kwahiyo nikawa najiuliza nini tatizo mpaka inakuwa hivi.
Sikupata jibu lolote kwakweli, nikaamua tena kwenda sebleni kuona kama wifi na kaka wameenda kulala, ila niliwakuta pale pale tena kaka akiwa amelala kwa kujinyoosha kwenye kitu kitendo ambacho kilinichanganya.
Wifi alikuwa amekaa na mtoto mikononi, nikaamua kumsogelea na kumuuliza kuhusu kaka ili amwamshe akalale, na muda huu wifi alinijibu kila nilichomuuliza pale.
"Wifi mbona hivyo, mwamshe kaka akalale ndani"
"Mwangalie kaka yako alivyo Sabrina"
Moyo wangu ukalia paaa kwa uoga, na kuuliza kwa taharuki.
"Kwani ana nini?"
"Wee msogelee tu umwangalie"
Nikamsogelea kaka kwa uoga na kumwangalia kwa makini huku na uoga ukiniandama ila nilimuona kuwa yupo sawa.
"Mbona yupo sawa wifi!"
"Mwangalie vizuri Sabrina"
Huku wifi machozi yakimlengalenga nami hofu ikanizidi na kujaribu kumuamsha kaka ila hakushtuka wala kutingishika alikuwa kama vile mtu aliyekufa, uoga ukanijaa zaidi.
Itaendelea…!!