Simulizi ya mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu

Simulizi ya mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu

Duh mbona kazi sana,, ila shukran kwa muendelezo japo kiduchu
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 09

“Mbona unaogopa?” Aliuliza huku akinikazia macho.

“Ahaa….sijawahi kuona mbwa wakubwa kama hawa, Isitoshe hata mbwa ninawaogopa sana kila nikiwaona" . Nilizungumza kwa woga

“Ohoo pole sana, karibu nchini Kenya. Tanzania na kenya ni majirani na Marafiki wakubwa sana” . Dada huyu alizungumza huku akinirudishia hati yangu ya kusafiria.

“Asante” Nikaichukua kwa haraka, nikasoma maelekezo ya wapi pa kutoteka, nikafanikiwa kupaona. Taratibu nikaanza kutembea kueleka katika eneo hili huku nikigeuka nyuma mara kadhaa nikitazama wanajeshi walio kuwa wanakuja eneo nililo kuwa nimesimama ila sikuwaona. Nikaitoa Waleti yangu mfukoni na kutazama picha cha Chalamala ili kukumbuka rangi ya Nguo atakazokuwa amezivaa.

"Atavaa hivi". Nilizungumza huku nikiitazama picha yake. Nikafanikiwa kufika eneo la watu wanapo wasubiria abiria wanao toka kwenye uwanja huu, nikaanganza angaza huku na kule, nikafanikiwa kuona bango lililo andikwa Gilbert Mwaitika nikamuona Chalamala akiwa amelishika bango hilo. Nikaanza kumfwata kwa kasi sana hadi sehemu alipo simama.

“Ah kumbe ni wewe Gilbert umekuja!!! Karibu Kenya bwana rafiki yangu"... Aliniambia huku akinikumbatia

” “Asante sana broo. Tutoke tu kwanza hapa maana sina hata hamu ya kuongea". Nilimjibu huku nikijitoa mwilini mwake. Chalamala akanipokea begi langu na tukaanza kutembea kueleka sehemu ya maegesho ya magari. Furaha kubwa sana ikanijaa moyoni mwangu, kwa mara ya kwanza nimeweza kufanya kazi ya kusafirisha mzigo wa madawa ya kulevya wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 4.6 za Kitanzania, na bosi Clara ameniahidi kunipatia Milioni mia Tano endapo nitafanikisha mzigo kufika salama.

Maskini mimi. Sikujua, sikujua kinakwenda kutokea nini.

“Hei simama”
Tulisikia sauti ya ukali nyuma yetu na kujikuta sote tukigeuka nyuma na kutazama ni nani anayetusimamisha, Walikuwa ni askari wakija huku wakiwa na mbwa mikononi mwao. Kwa haraka Chalamala akachomo bastola kiunoni mwake, kwa haraka akaanza kufyatua risasi kuelekea kwa askari hawa. Milio ya risasi za Chalamala zikawafanya watu wengi waliopo nje ya uwanja huu kuanza kutawanyika kila mmoja akijaribu kuyaokoa maisha yake. Chalamala akanishika mkono na tukaanza kukimbia huku nikimfwata anapo nipelekea. Tukaingia ndani ya gari aina ya Land Cruse, Akawasha gari kwa haraka, akaanza kulirudisha nyuma, akaliweka sawa na tukuondoka eneo hili kwa kasi sana.

Furaha yote ya kuupata utajiri mbele yangu ikanipotea kabisa, mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi, kwani kwa kupitia kioo cha pembeni mwangu, nikaona gari nyingi za polisi zikitufukuzia.

"Ina maana Chalamala ni gaidi huku au? Iweje ashambulie Askari wakati hatujagundulika?" niliwaza huku nikitazama kioo cha pembeni kuwatazama polisi wanafanya nini,

“Funga mkanda”

Chalamala alizungumza huku akifunga na yeye mkanda wake. Nikatii amri huku nikimtazama akiendesha gari hili la Bei mbaya ambalo lina sifa kubwa ya kwenda kasi sana, nadhani alijua nini kitatokea ndio maana akaja na gari hii. Kusema kweli anaendesha gari kwa kasi na kwa umakini sana, japo kuna magari mengi sana barabarani ila anayapita kwa kasi huku akitakwepa kwa ustadi mkubwa sana.

“Wajinga kweli hawa, pumbavu! ” Chalamala alizungumza huku akizidi kuendesha gari lake, huku akitazama mwanga wa Helicopter unaotumulika kutokea juu. Chalamala akakanyaga breki za gafla, kisha akakunja kona ya kulia kwangu kwa kasi sana na tukazidi kusonge mbele.

“Gilbert jiamini usiogope sana, hawa mbwa koko tunawatoka”... Alinitia Moyo. Yaani mbele ya polisi unitie Moyo? Kwakweli akili yangu haikuwa hapo, niliwaza maisha yangu baada ya hapa endapo nikikamatwa, niliwakumbuka wazazi wangu, Mara ya mwisho kuwasiliana nao ni pindi nikiwa Kilimanjaro, baada ya hapo ndio majanga yakanitokea pindi nasafirisha madawa kuelekea Dar,.

“Wamenigundua mimi au ni wanakutaka wewe….?” Niliuliza huku nikitetemeka kwa woga, nikiamini kwamba askari wamenishtukia na Chalamala anajitahidi kunitorisha mimi na mzigo wangu wa madawa.

“Hapana, mimi ndio muhusika mkubwa hapa, kuna mara nyingi sana huwa wananitafuta. Sasa leo wameniona ndio maana wananifukuzia hivi” Chalamala alizungumza huku akiendelea kuendesha kwa kasi gari hili. Kioo cha pembeni yangu kinacho nisaidia kutazama nyuma, nikastukia kukiona kikipasuliwa kwa risasi. Woga ukazidi kuongezeka mara dufu hadi haja ndogo ikanibana kisawa sawa.

“Inama chini”
Chalamala alizungumza kwa ukali sana, nikainama chini huku mikono yangu nikiziba kichwa changu, upepo mwigi ukaanza kuingia ndani ya gari hili, nikageuza shingo yangu kidogo na kuona kiooo cha upande wangu kikiwa kimefunguliwa, huku Chalamala mkono wake wa kulia ulio shika bastola ukiwa juu mgongo wangu. Milio ya risasi inayosikika juu ya mgongo wangu ukanifanya haja ndogo kunitoka taratibu. Nikayaziba masikio yangu kwani Chalamala hajali kwamba milio hiyo ina sauti kubwa sana na inaogopesha.

“Ooh Shiiit” Chalamala alizungumza kwa hasira

“Risasi zimekwisha” alizungumza huku akinitazama usoni mwangu kwa macho yaliyo jaa uwekundu wa hasira. Nikakosa hata cha kumjibu kwani akili yangu haipo sawa kabisa.

“Unaweza kuendesha gari?” Nikamjibu kwa kutingisha kichwa kwamba sijui vizuri.

“Ahaaa Claraa ameniletea watu gani hawaaa” Chalamala alizungumza kwa hasira huku akiupiga piga mskani wa gari hili kwa kitako cha bastola aliyokuwa ameishika.

Nikatazama nyuma, nikaona gari nyingi za askari zikizidi kuja kwa kasi sana, mianga mikali ya helicopter ikazidi kuongezeka ikiashiria kwamba helicopter za polisi zimezidi kuongezeka hawani.

“Dogo hapa kuna kufa na kupona, sasa wewe sali sala zako za mwisho sawa” Nikatamani kuzungumza kitu ila koo likanisaliti, Chalamala akatoa mskoto wa bangi kwenye koti lake hili, akaubana mdomoni mwake, akatoa kiberiti cha gesi kwenye mfuko wa nje wa koti lake. Cha kushangaza akaachia mskani wa gari na kuanza kuwasha msokoto huu wa bangi, nikaona jinsi spidi za gari hili zikizidi kuongezeka huku mbele yetu kukiwa na barabara iliyo nyooka na kuna magari mengi sana.

Moshi mkali wa bangi ambao kwenye maisha yangu niliapa kutokuuvuta, ukaanza kunipalia na kujikuta nikianza kukohoa sana. Chalamala akavuta mafundo kadhaa, kisha akashika mskani wa gari hili, akalikwepa lori kubwa la mafuta ambalo kusema kweli tulibakisha mita chache kabla ya kuligonga kwa nyuma.

“Shika Dogo Piga fumba moja” Chalamala alizungumza huku akinikabidhi msokoto huu wa bangi.

“Situmii” Nilizungumza kwa upole huku nikiendela kutetemeka.

“Dogo sasa unasafirisha mzigo wote huu alafu utumii vitu kama hivi?” “Ahaa…aa…”
akanitazama kwa macho makali sana, kisha akaendela kuvuta msokoto huu wenye moshi mwingi uliotawala ndani ya hili gari ambalo ni dogo na lina ingia watu wawili tu ndani. Chalamala kwa utaalamu mkubwa akakunja kona kali ya hii barabara na tukazidi kusonga mbele, hata kabla hatujafika mbali. Tukaona gari nyingi za polisi zikiwa zimesimama mbele yetu huku wakiwa wameifunga barabara, nyuma yetu napo kuna gari nyingi za polisi, juu kuna helicopter nyingi za polisi. Cha kushangaza Chalamala akazidi kuendesha gari kama hajawaona polisi hawa. Ama kweli nilikiri Chalamala ni Jasusi, si yule rafiki yangu wa kipindi kile tukiwa Mbeya Tanzania, anajiamini hadi mbele ya Askari wengi kiasi hiki....

Ghafla nikashtukia kuona kifua chake kikimwaga damu nyingi sana huku kioo cha mbele kwa upande wake kikijaa matundu mengi sana ya risasi, macho ya mshangao yakanitoka sana mara baada ya kuona gari letu likililenga gari moja la polisi lililo ziba barabara kwa ajili ya kulizuia gari letu lisipite katika eneo hili, mbaya zaidi Chalamala tayari amepigwa risasi nyingi za kifuani na kufa hapohapo ndani ya gari na mimi sina uwezo wowote wa kulifanya gari letu kusimama ili kuzuia ajali mbaya inayo kwenda kutokea ambayo kusema kweli sijui kama nitatoka hai ndani ya gari hili mara baada ya kuligonga gari la polisi liliopo mbele yetu. Nilianza kujuta makosa yangu yote mbele Ya Mungu nikimweleza anihurumie maana ni kutokana na Moyo wangu kuwa mgumu na kumkimbia yeye, nilitubu dhambi hata zile ambazo sidhani kama niliwahi kuzifanya, ama kweli nilichanganyikiwa

Picha ndo kwanza limeanza. Je Gilbert atafanikiwa kutoka salama mbele ya polisi hawa?.

Offer yetu inaendelea kwa 1000 utavipata vipande vyote 30. Lipa kwenda Halopesa namba 0621249611 kisha nitext whatsapp kwa namba 0621249611
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 10
Kwa haraka akili yangu ikapata wazo ambalo sikuhitaji hata kulifikiria mara mbili, nikaushika mskani wa gari hili na kujitahidi kukunja upande wangu, cha kumshukuru Mungu gari likakubali kukunja kona na kutoka barabarani na kuanza kuporomoka kwenye mporomoko mfupi na kuingia kwenye mtaro wa maji ulipo pembezoni mwa hii barabara. Nikajikuta nikihema sana mara baada ya gari hili kutulia tuli ndani ya mtaro huu.

Hazikupita hata dakika mbili nikastukia mlango ukifunguliwa na askari walio shika bunduki zao wakijihami kwa chochote ambacho kitatokea kwa muda huu. Wakaanza kunifungua mkanda wa siti niliyokalia kisha wakanichomoa mimi na kunilaza chali huku wakinizunguka. Wakayatoa mabegi yangu ambayo yana viatu, wakamtazama Chalamala kisha na yeye wakamchomoa ndani ya gari hili. Gari maalumu la wagonjwa likafika katika eneo hili, madaktari waliovalia makoti meupe kwa haraka wakashuka katika eneo nililolazwa na askari hawa, wakaniweka juu ya machela yao.

Madaktari hawa wakaninyanyua na kunipeleka barabarani na kuniiingiza kwenye gari lao la wagojwa. Askari watatu nao wakaingia kwenye gari hili wakiwa na pingu mikononi mwao.

"Jela inanihusu mimi, ee Mola nisaidie"

Nilizungumza kimoyo moyo huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, furaha ambayo niliipata kwa muda mchache mara baada ya kuonana na Chalamala, yote imetoweka kwani kwa akili za haraka haraka tayari nimeshagundua kwamba hali imekuwa tete kwa upande wangu. Hata madaktari wanacho niuliza kwa ishara ya vitendo sikuweza kuvielewa kutokana na kujawa na hofu kubwa sana ya kukamatwa na polisi hawa.

‘Eheee mama huko ulipo nisaidie Gilbert mwanao, ninakwenda Jela mimi’

Niliendelea kuzungumza kimoyo moyo huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu, dripu la maji niliyo tundukiwa mkononi mwangu wala sielewi hata utendaji wake wa kazi unakwenda vipi.

Nikastukia mlango wa nyuma wa hili gari ukifunguliwa, askari hawa wenye bunduki wakaanza kuruka kwenye hili gari, kisha madaktari hawa wakasaidia kunitoa katika gari hili, nikapakizwa kwenye kitanda cha wagongwa kilicho zungukwa na manesi. Nikaanza kupelekwa nisipo pajua, askari hawa hawakuhitaji kuniacha hata hatua moja kwani muda wote wapo pembeni yangu. Tukaingia ndani ya lifti, hapa nikapata nafasi ya kuhesabu namba zilizopo katika lifti hii na inaonyesha tunaelekea gorofa ya Tano. Hatukumaliza hata dakika ndani ya lift hii, ikafunguliwa na manesi wakaendelea kusukuma kitanda changu hadi tukafika katika moja ya mlango, ukafunguliwa na tukaingia. Wakanilaza kwenye kitanda kimoja tulicho kikuta humu ndani, askari mmoja akatoa pingu mfukoni mwake akauchukua mkono wangu wa kushoto na kuufunga kisha akaiiunganisha na kitanda hichi cha chuma.

Machozi yakazidi kunimwagika usoni mwangu nikiamini kwamba tayari maisha yangu yamesha haribika. Nikajikuta nikianza kulaani ni kwa nini nimeingia kwenye biashara ngumu ya kuhatarisha maisha yangu. Nikazidi kulaani ni kwa nini wazazi wangu hawakuwa na maisha mazuri yenye pesa!!!
Nesi mmoja akachukua sindano ndogo, akanichoma kwenye mkono wangu ulio fungwa pingu, taratibu nikijikuta usingizi ukianza kutawala mboni zangu za macho na mwishowe nikalala fofofo.

***

Nilikuja kufumbua macho yangu nikiwa sikumbuki yamepita masaa mangapi ama siku ngapi, Pembeni yangu nikamuona askari mwengine wa kike ambaye sijamuona tangu kuja kwangu hapa.

Askari huyu alipo gundua kwamba nimeyafumbua macho yangu, kwa kupitia simu yake ya upepo aliyo ichomeka kwenye bega lake la kushoto, akaanza kuzungumza zungumza maneno kwa Lugha ya Kingereza, hakuna hata moja ambalo ninalielewa maana kingereza sikifahamu kabisa. Mlango huu ukafunguliwa wakaingia madaktari wawili, wakazungumza kudogo na huyu askari kisha askari huyu akanisogelea hapa kwenye kitanda na kunifungua pingu yangu. Taratibu madaktari hawa wakanisaidia kunikalisha kitako, askari huyu akanishika mikono yangu vizuri na kuniomba kwa ishara niinyooshe mbele nikatii, akanifunga pingu aliyo nifungua.

Daktari mmoja akamkabidhi askari huyu kitabu ambacho sijui hata kimandikwa kitu gani, askari huyu akaandika andika kisha akamrudishia daktari huyu. Askari huyu akanishika mkono wangu na kunishusha hapa kitandani. Tukatoka ndani humu, nje nikakuta askari wengine wanne wakiwa na silaha mikononi mwao. Wakanifunga mnyororo wa miguu ambao unaniwezesha vizuri kutembea, kisha wakaniweka katikati na tukaanza kutembea kueleka kwenye lifti. Ninatamani kulia ila machozi hayatoki kabisa usoni mwangu, ninatamani sana kuiona Tanzania yangu ila sina tena nafasi ya kuweza kuiona kwa maana hapa ninakwenda kunyongwa jela na sijui kama nitatoka, Nilimlaani sana Bosi Clara maana safari ya kuja Huku Nililazimishwa nikitishiwa kuuwawa ama Kulawitiwa.

"Mungu wangu ninaomba ufanye muujiza, tazama mimi ni kijana bado mdogo sana. Ndio kwanza nina miaka 21."

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishuhudia jinsi lifti hii inavyozidi kwenda chini, tukatoka katika lifti hii na nikaingizwa kwenye gari kubwa la polisi.

"Clara bosi wangu ninafia huku kenya, Bora ningechagua kuuwawa siku ile uliponipa machaguo mawili" ... Niliwaza
Hapakuwa na askari hata mmoja ambaye alijaribu kutabasamu mbele yangu wala kunisemesha chochote. Jinsi sura zoa zilivyo jaa ‘ukauzu’ unaweza kusema ni wanaume fulani waliotoka vitani. Baada ya dakika kama arobaini na tano hivi, tukafika katika Kambi moja, nikashushwa huku ulinzi ukiwa ni mkali sana. Moja kwa moja nikapelekwa hadi kwenye chumba kimoja kikubwa, kina meza moja na viti viwili vinayo angaliana na hapa katikati vimetenganishwa na meza hiyo. Askari akanikalisha kwenye moja ya kiti akatoka chumbani humu na kuniacha mimi peke yangu. Nikaanza kutazama kila kona ya chumba hichi, nikaona kamera za ulinzi jinsi zilivyojaa kila kona ya chumba hichi. Mara baada ya muda wakaingia wanaume wawili wakiwa wamevalia suti nzuri, mmoja ni mweusi na mrefu kwenda juu, mwengine ni mfupi kiasi ila ana asili ya Kipemba. Mkononi mwa Kaka huyu wa kipemba ameshika mabegi yangu, mapigo ya moyo yakanienda kasi sana, jasho likaanza kunimwagika japo ndani ya chumba hichi kuna hewa ya ubaridi(A/C).

“Gilbert habari yako”

Kaka huyu mweusi alizungumza huku akikaa kwenye kiti cha mbele yangu. Nikatabasamu kidogo mara baada ya kuona kwamba nimekutana na mtu anaye fahamu Kiswahili vizuri.

“Salama shikamoo”

“Marahaba, unaheshima sana Gilbert, sijategemea kama ungenisalimia shkamoo"

Nikazidisha tabasamu huku nikiwa na tumaini kubwa sana baada ya kumuona ana ukarimu ambao tangu nikamatwe na hawa Wakenya sikuweza kuupata kabisa.

“Ninaitwa Daniel, mimi ni askari mpelelezi”

Hapo nikakumbuka hata Tanzania kuna Mpelelezi mahiri anayeitwa Daniel mwaseba

Alizungumza huku akinonyesha kitambulisho chake, nikakisoma kwa sekunde kadhaa kisha akakitoa mbele yangu na kukirudisha mfukoni mwake.

“Huyu mwenzangu anaitwa Martin, naye ni askari mpelezi. Hili begi unalifahamu? ”. Aliniuliza

Ofa yetu inaendelea bado. Lipia Tshs 1000 kwenda namba
Halotel 0621249611 jina GILBERT EVARIST
Kisha nitext au njoo whatsapp kwa namba 0621249611 ujipatie vipande vyote 30.
FB_IMG_1642427614746.jpg
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 10
Kwa haraka akili yangu ikapata wazo ambalo sikuhitaji hata kulifikiria mara mbili, nikaushika mskani wa gari hili na kujitahidi kukunja upande wangu, cha kumshukuru Mungu gari likakubali kukunja kona na kutoka barabarani na kuanza kuporomoka kwenye mporomoko mfupi na kuingia kwenye mtaro wa maji ulipo pembezoni mwa hii barabara. Nikajikuta nikihema sana mara baada ya gari hili kutulia tuli ndani ya mtaro huu.

Hazikupita hata dakika mbili nikastukia mlango ukifunguliwa na askari walio shika bunduki zao wakijihami kwa chochote ambacho kitatokea kwa muda huu. Wakaanza kunifungua mkanda wa siti niliyokalia kisha wakanichomoa mimi na kunilaza chali huku wakinizunguka. Wakayatoa mabegi yangu ambayo yana viatu, wakamtazama Chalamala kisha na yeye wakamchomoa ndani ya gari hili. Gari maalumu la wagonjwa likafika katika eneo hili, madaktari waliovalia makoti meupe kwa haraka wakashuka katika eneo nililolazwa na askari hawa, wakaniweka juu ya machela yao.

Madaktari hawa wakaninyanyua na kunipeleka barabarani na kuniiingiza kwenye gari lao la wagojwa. Askari watatu nao wakaingia kwenye gari hili wakiwa na pingu mikononi mwao.

"Jela inanihusu mimi, ee Mola nisaidie"

Nilizungumza kimoyo moyo huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, furaha ambayo niliipata kwa muda mchache mara baada ya kuonana na Chalamala, yote imetoweka kwani kwa akili za haraka haraka tayari nimeshagundua kwamba hali imekuwa tete kwa upande wangu. Hata madaktari wanacho niuliza kwa ishara ya vitendo sikuweza kuvielewa kutokana na kujawa na hofu kubwa sana ya kukamatwa na polisi hawa.

‘Eheee mama huko ulipo nisaidie Gilbert mwanao, ninakwenda Jela mimi’

Niliendelea kuzungumza kimoyo moyo huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu, dripu la maji niliyo tundukiwa mkononi mwangu wala sielewi hata utendaji wake wa kazi unakwenda vipi.

Nikastukia mlango wa nyuma wa hili gari ukifunguliwa, askari hawa wenye bunduki wakaanza kuruka kwenye hili gari, kisha madaktari hawa wakasaidia kunitoa katika gari hili, nikapakizwa kwenye kitanda cha wagongwa kilicho zungukwa na manesi. Nikaanza kupelekwa nisipo pajua, askari hawa hawakuhitaji kuniacha hata hatua moja kwani muda wote wapo pembeni yangu. Tukaingia ndani ya lifti, hapa nikapata nafasi ya kuhesabu namba zilizopo katika lifti hii na inaonyesha tunaelekea gorofa ya Tano. Hatukumaliza hata dakika ndani ya lift hii, ikafunguliwa na manesi wakaendelea kusukuma kitanda changu hadi tukafika katika moja ya mlango, ukafunguliwa na tukaingia. Wakanilaza kwenye kitanda kimoja tulicho kikuta humu ndani, askari mmoja akatoa pingu mfukoni mwake akauchukua mkono wangu wa kushoto na kuufunga kisha akaiiunganisha na kitanda hichi cha chuma.

Machozi yakazidi kunimwagika usoni mwangu nikiamini kwamba tayari maisha yangu yamesha haribika. Nikajikuta nikianza kulaani ni kwa nini nimeingia kwenye biashara ngumu ya kuhatarisha maisha yangu. Nikazidi kulaani ni kwa nini wazazi wangu hawakuwa na maisha mazuri yenye pesa!!!
Nesi mmoja akachukua sindano ndogo, akanichoma kwenye mkono wangu ulio fungwa pingu, taratibu nikijikuta usingizi ukianza kutawala mboni zangu za macho na mwishowe nikalala fofofo.

***

Nilikuja kufumbua macho yangu nikiwa sikumbuki yamepita masaa mangapi ama siku ngapi, Pembeni yangu nikamuona askari mwengine wa kike ambaye sijamuona tangu kuja kwangu hapa.

Askari huyu alipo gundua kwamba nimeyafumbua macho yangu, kwa kupitia simu yake ya upepo aliyo ichomeka kwenye bega lake la kushoto, akaanza kuzungumza zungumza maneno kwa Lugha ya Kingereza, hakuna hata moja ambalo ninalielewa maana kingereza sikifahamu kabisa. Mlango huu ukafunguliwa wakaingia madaktari wawili, wakazungumza kudogo na huyu askari kisha askari huyu akanisogelea hapa kwenye kitanda na kunifungua pingu yangu. Taratibu madaktari hawa wakanisaidia kunikalisha kitako, askari huyu akanishika mikono yangu vizuri na kuniomba kwa ishara niinyooshe mbele nikatii, akanifunga pingu aliyo nifungua.

Daktari mmoja akamkabidhi askari huyu kitabu ambacho sijui hata kimandikwa kitu gani, askari huyu akaandika andika kisha akamrudishia daktari huyu. Askari huyu akanishika mkono wangu na kunishusha hapa kitandani. Tukatoka ndani humu, nje nikakuta askari wengine wanne wakiwa na silaha mikononi mwao. Wakanifunga mnyororo wa miguu ambao unaniwezesha vizuri kutembea, kisha wakaniweka katikati na tukaanza kutembea kueleka kwenye lifti. Ninatamani kulia ila machozi hayatoki kabisa usoni mwangu, ninatamani sana kuiona Tanzania yangu ila sina tena nafasi ya kuweza kuiona kwa maana hapa ninakwenda kunyongwa jela na sijui kama nitatoka, Nilimlaani sana Bosi Clara maana safari ya kuja Huku Nililazimishwa nikitishiwa kuuwawa ama Kulawitiwa.

"Mungu wangu ninaomba ufanye muujiza, tazama mimi ni kijana bado mdogo sana. Ndio kwanza nina miaka 21."

Nilizungumza kimoyo moyo huku nikishuhudia jinsi lifti hii inavyozidi kwenda chini, tukatoka katika lifti hii na nikaingizwa kwenye gari kubwa la polisi.

"Clara bosi wangu ninafia huku kenya, Bora ningechagua kuuwawa siku ile uliponipa machaguo mawili" ... Niliwaza
Hapakuwa na askari hata mmoja ambaye alijaribu kutabasamu mbele yangu wala kunisemesha chochote. Jinsi sura zoa zilivyo jaa ‘ukauzu’ unaweza kusema ni wanaume fulani waliotoka vitani. Baada ya dakika kama arobaini na tano hivi, tukafika katika Kambi moja, nikashushwa huku ulinzi ukiwa ni mkali sana. Moja kwa moja nikapelekwa hadi kwenye chumba kimoja kikubwa, kina meza moja na viti viwili vinayo angaliana na hapa katikati vimetenganishwa na meza hiyo. Askari akanikalisha kwenye moja ya kiti akatoka chumbani humu na kuniacha mimi peke yangu. Nikaanza kutazama kila kona ya chumba hichi, nikaona kamera za ulinzi jinsi zilivyojaa kila kona ya chumba hichi. Mara baada ya muda wakaingia wanaume wawili wakiwa wamevalia suti nzuri, mmoja ni mweusi na mrefu kwenda juu, mwengine ni mfupi kiasi ila ana asili ya Kipemba. Mkononi mwa Kaka huyu wa kipemba ameshika mabegi yangu, mapigo ya moyo yakanienda kasi sana, jasho likaanza kunimwagika japo ndani ya chumba hichi kuna hewa ya ubaridi(A/C).

“Gilbert habari yako”

Kaka huyu mweusi alizungumza huku akikaa kwenye kiti cha mbele yangu. Nikatabasamu kidogo mara baada ya kuona kwamba nimekutana na mtu anaye fahamu Kiswahili vizuri.

“Salama shikamoo”

“Marahaba, unaheshima sana Gilbert, sijategemea kama ungenisalimia shkamoo"

Nikazidisha tabasamu huku nikiwa na tumaini kubwa sana baada ya kumuona ana ukarimu ambao tangu nikamatwe na hawa Wakenya sikuweza kuupata kabisa.

“Ninaitwa Daniel, mimi ni askari mpelelezi”

Hapo nikakumbuka hata Tanzania kuna Mpelelezi mahiri anayeitwa Daniel mwaseba

Alizungumza huku akinonyesha kitambulisho chake, nikakisoma kwa sekunde kadhaa kisha akakitoa mbele yangu na kukirudisha mfukoni mwake.

“Huyu mwenzangu anaitwa Martin, naye ni askari mpelezi. Hili begi unalifahamu? ”. Aliniuliza

Ofa yetu inaendelea bado. Lipia Tshs 1000 kwenda namba
Halotel 0621249611 jina GILBERT EVARIST
Kisha nitext au njoo whatsapp kwa namba 0621249611 ujipatie vipande vyote 30.View attachment 2085053
patamu hapo
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 11

Daniel alizungumza huku Martin akiliweka begi langu juu ya meza hii. Nikalitazama kwa woga huku nikishauri kichwani mwangu, nilikatae au kulikubali.

“Ninakuuliza unalifahamu begi hili?”

Daniel alizungumza kwa ukali sana hadi nikastuka.

“Ndio, ndio, ninalifahamu”

“Ohooo vizuri sana. Unaweza kunitajia vitu livyomo humu ndani?”

“Ndio”

“Kuna nini?”

“Kuna.... Kun....kuna Pedi za Kike...". Nilijibu kwa kujiumauma

Askari huyu mwenye asili ya Kipemba akafungua zipu ya begi hili na kuanza kutoa Pedi moja moja baada ya nyingine, akatoa Kisu kidogo cha kukunja kwenye mfukono wa koti lake la suti na kukiweka pembeni ya hizi Pedi,

“Kwa hiyo una uhakika ni Pedi hizo tu ulizozitaja?”

“Eheee”

“Unaweza kuniambia kwamba ndani ya Pedi hizi kuna nini?”

“Eheee……?”

“Mara nyingi sipendi uswahili hapa ni Kenya na sio Tanzania, ukiulizwa swali jibu swali”

Daniel akanibadilikia kabisa, hata ule ukarimu alio nionyesha alivyokuwa ameingia ndani ya chumba chihi umetoweka na amekuwa kama Mbogo aliye jeruhiwa kwa risasi. Nikameza fumba zito la mate huku mwili mzima ukiendelea kunitetemeka, nikamtazama,

“Unahitaji kwenda jela eheeee?”

“Ahaa….haaa….ahaapana”

“Sema unajua ndani ya hizo Pedi kuna vitu gani?”

“Hakuna kitu”

“Haki ya Mungu Gilbert unakwenda kunyongwa jela, sema kwenye hayo mapedi ndani kuna nini?”

Daniel alizidi kuzungumza kwa ukali, nikajikuta natetemeka huku machozi yakinibubujika kwani amezidi kuwa mkali sana kwangu.

“Dogo dogo, hapa sihitaji upuuzi wa kulia, sihitaji upuuzi wa kipumbavu sema humu ndani kuna nini?”

“Kuna dawa”

Maneno haya yalinitoka pasipo kutarajia kabisa, nikamuona Daniel akitabasamu, kisha akampa ishara askari huyu mwingine akachukua pedi moja, akaichana katikati, tukakuta pakti moja ya madawa ya kulevya iliyo fichwa kitaalamu kabisa. Wakaingia askari wengine wawili huku wakiwa wamevalia gloves mikononi mwao, wakaanza kusaidiana na askari mwenzao kuzichana hizi pedi na kukuta kila moja kuna pakti ya madawa ya kulevya. Walipo maliza zoezi hili wakatoka humu ndani na kuniacha na askari Daniel.

“Kwenye maisha kama kijana unapaswa kutafuta pesa lakini si kwa njia Haramu kama hizi"

Daniel alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti chake, akashika moja ya pakti na kuitazama vizuri kisha akairudisha juu ya meza.

“Dogo ulijua kwamba unakuja Buza eheee?”

Daniel alizungumza huku akinikazia macho usoni mwangu nikazidi kutetemaka kwa woga mwingi sana.

“Sasa ukweli wako ndio unaweza kukuweka huru, sema hizi dawa umezitoa wapi?”

Sawali lake likanirudisha kumbukumbu za makubaliano mengine ambayo nilizungumza na bosi Clara,

"Endapo ikatokea umekatwa, hakikisha kwamba hutaji ni nani amekukabidhi huu mzigo endapo utafanya hivyo basi tambua Wazazi wako waliopo mbeya nitawaua kwa mikono yangu, "

“Nimekuuliza Dogo huu mzigo umetoka wapi?”

Daniel alizidi kunifokea huku akisogela karibu, akanishika bega langu la upande wa kulia na akaanza kuliminya minya.

“Zungumza haraka”

“Ni wa kwangu”

Nikapata ujasiri wa kukubali mzigo huu kwamba ni wangu ili kuyaokoa maisha ya wazazi wangu.

“Hahaaa.. Hahahahaaaaa, Gilbert wewe bado ni kijana mdogo sana na hali yako inaonekana, unadhani unaweza kunidanganya kwamba huu ni mzigo wako”

“Ndio ni wangu kwani unahisi kwamba mimi siwezi kufanya hicho unachokiona”

Nikajikuta ujasiri ukizidi kuongezeka, woga ukanipotea kabisa tayari moyoni mwangu nimesha amua liwalo na liwe na hata kunyongwa ni bora ninyongwe kuliko kuona maisha ya wazazi wangu yanaingia kwenye hali ngumu ambayo niliwaahidi wazazi wangu kwamba nitahakikisha kwamba ninatafuta pesa kwa namna yoyote ile.

“Heee okay mimi sio mzungumzaji sana ila utawaambia hao ni wapi mzigo huu umeutoa na nini muhusika mkuu katika mzigo huu”

Wakaingia wanaume wawili wenye miili mikubwa na iliyo jijenga kwa misuli, mmoja wao akaninyanyua juu juu huku akiniweka begani mwake, kila ninavyo jaribu kukurupuka anishushe chini ninashindwa kabisa kwani amenishikilia kikamilifu.
ITAENDELEA

Ofa inaendelea. Lipia Tshs 1000 tu utumiwe whatsapp hadi mwisho vipande vyote 30. Namba ya malipo ni HALOPESA NAMBA 0621249611 au Mpesa namba 0765824715 jina Gilbert
Namba ya whatsapp ni 0621249611
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 11

Daniel alizungumza huku Martin akiliweka begi langu juu ya meza hii. Nikalitazama kwa woga huku nikishauri kichwani mwangu, nilikatae au kulikubali.

“Ninakuuliza unalifahamu begi hili?”

Daniel alizungumza kwa ukali sana hadi nikastuka.

“Ndio, ndio, ninalifahamu”

“Ohooo vizuri sana. Unaweza kunitajia vitu livyomo humu ndani?”

“Ndio”

“Kuna nini?”

“Kuna.... Kun....kuna Pedi za Kike...". Nilijibu kwa kujiumauma

Askari huyu mwenye asili ya Kipemba akafungua zipu ya begi hili na kuanza kutoa Pedi moja moja baada ya nyingine, akatoa Kisu kidogo cha kukunja kwenye mfukono wa koti lake la suti na kukiweka pembeni ya hizi Pedi,

“Kwa hiyo una uhakika ni Pedi hizo tu ulizozitaja?”

“Eheee”

“Unaweza kuniambia kwamba ndani ya Pedi hizi kuna nini?”

“Eheee……?”

“Mara nyingi sipendi uswahili hapa ni Kenya na sio Tanzania, ukiulizwa swali jibu swali”

Daniel akanibadilikia kabisa, hata ule ukarimu alio nionyesha alivyokuwa ameingia ndani ya chumba chihi umetoweka na amekuwa kama Mbogo aliye jeruhiwa kwa risasi. Nikameza fumba zito la mate huku mwili mzima ukiendelea kunitetemeka, nikamtazama,

“Unahitaji kwenda jela eheeee?”

“Ahaa….haaa….ahaapana”

“Sema unajua ndani ya hizo Pedi kuna vitu gani?”

“Hakuna kitu”

“Haki ya Mungu Gilbert unakwenda kunyongwa jela, sema kwenye hayo mapedi ndani kuna nini?”

Daniel alizidi kuzungumza kwa ukali, nikajikuta natetemeka huku machozi yakinibubujika kwani amezidi kuwa mkali sana kwangu.

“Dogo dogo, hapa sihitaji upuuzi wa kulia, sihitaji upuuzi wa kipumbavu sema humu ndani kuna nini?”

“Kuna dawa”

Maneno haya yalinitoka pasipo kutarajia kabisa, nikamuona Daniel akitabasamu, kisha akampa ishara askari huyu mwingine akachukua pedi moja, akaichana katikati, tukakuta pakti moja ya madawa ya kulevya iliyo fichwa kitaalamu kabisa. Wakaingia askari wengine wawili huku wakiwa wamevalia gloves mikononi mwao, wakaanza kusaidiana na askari mwenzao kuzichana hizi pedi na kukuta kila moja kuna pakti ya madawa ya kulevya. Walipo maliza zoezi hili wakatoka humu ndani na kuniacha na askari Daniel.

“Kwenye maisha kama kijana unapaswa kutafuta pesa lakini si kwa njia Haramu kama hizi"

Daniel alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti chake, akashika moja ya pakti na kuitazama vizuri kisha akairudisha juu ya meza.

“Dogo ulijua kwamba unakuja Buza eheee?”

Daniel alizungumza huku akinikazia macho usoni mwangu nikazidi kutetemaka kwa woga mwingi sana.

“Sasa ukweli wako ndio unaweza kukuweka huru, sema hizi dawa umezitoa wapi?”

Sawali lake likanirudisha kumbukumbu za makubaliano mengine ambayo nilizungumza na bosi Clara,

"Endapo ikatokea umekatwa, hakikisha kwamba hutaji ni nani amekukabidhi huu mzigo endapo utafanya hivyo basi tambua Wazazi wako waliopo mbeya nitawaua kwa mikono yangu, "

“Nimekuuliza Dogo huu mzigo umetoka wapi?”

Daniel alizidi kunifokea huku akisogela karibu, akanishika bega langu la upande wa kulia na akaanza kuliminya minya.

“Zungumza haraka”

“Ni wa kwangu”

Nikapata ujasiri wa kukubali mzigo huu kwamba ni wangu ili kuyaokoa maisha ya wazazi wangu.

“Hahaaa.. Hahahahaaaaa, Gilbert wewe bado ni kijana mdogo sana na hali yako inaonekana, unadhani unaweza kunidanganya kwamba huu ni mzigo wako”

“Ndio ni wangu kwani unahisi kwamba mimi siwezi kufanya hicho unachokiona”

Nikajikuta ujasiri ukizidi kuongezeka, woga ukanipotea kabisa tayari moyoni mwangu nimesha amua liwalo na liwe na hata kunyongwa ni bora ninyongwe kuliko kuona maisha ya wazazi wangu yanaingia kwenye hali ngumu ambayo niliwaahidi wazazi wangu kwamba nitahakikisha kwamba ninatafuta pesa kwa namna yoyote ile.

“Heee okay mimi sio mzungumzaji sana ila utawaambia hao ni wapi mzigo huu umeutoa na nini muhusika mkuu katika mzigo huu”

Wakaingia wanaume wawili wenye miili mikubwa na iliyo jijenga kwa misuli, mmoja wao akaninyanyua juu juu huku akiniweka begani mwake, kila ninavyo jaribu kukurupuka anishushe chini ninashindwa kabisa kwani amenishikilia kikamilifu.
ITAENDELEA

Ofa inaendelea. Lipia Tshs 1000 tu utumiwe whatsapp hadi mwisho vipande vyote 30. Namba ya malipo ni HALOPESA NAMBA 0621249611 au Mpesa namba 0765824715 jina Gilbert
Namba ya whatsapp ni 0621249611
Daaaah aseeeeeeeeee
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 12
Wakaniingiza katika chumba chenye maji kwenye sakafu, wakanivua nguo zangu zote na nikabaki kama nilivyozaliwa. Mmoja akachukua mpira mrefu wa maji uliounganishwa kwenye koki iliyopo humu ndani, akafungua maji hayo na yakaanza kutoka kwa wingi.

Mwanaume huyu bila ya huruma akaanza kunimwagia maji haya yenye nguvu kubwa, ninayafananisha na maji ya kikosi cha zima moto cha nchi yetu ya Tanzania. Kusema kweli sina nguvu ya kuhimili nguvu ya maji haya, nikajikuta nikianguka chini. Mwanaume huyu akaendelea kunimwagia maji naya yalio zidi kuniumiza kila sehemu ya mwili wangu yanapo nigusa. Nikajikunja mwili wangu huku nikipiga kelele ya maumivu, sipo tayari kusema kweli kuzungumza ukweli wa nani ni muhisika wa huu mzigo.
Alipoona sizungumzi chochote na wametumia zaidi ya dakika kumi na tano kuniumiza na maji haya, wakabadilisha adhabu.

Wakasimama nje ya mlango wa chumba hichi sehemu ambayo haina maji kabisa na ipo juu kidogo, wakaingiaza nyaya mbili, mwili mzima ukaanza kutetemeshwa kitendo kilicho nifanya zidizi kulia kwa uchungu sana

“Sema mzigo ni wa nani?”

Daniel alizungumza huku akiwa amesimama mlangoni pamoja na wanaume hawa, sikumjibu chochote zaidi ya kumtazama kwa macho makali yaliyojaa hasira kali sana.

“Gilbert utakufa, huu ni umeme wewe, zungumza acha ubishi wa kijinga. Huna hamu ya kurudi Tanzania eheee?”

Wakazichomoa nyaya hizi na kujikuta nikishusha pumzi kwani umeme huwa ni rahisi sana kupita kwenye maji.

“Zungumza huo mzigo ni wa nani?”

“U…na….ataka nikuda…..nganye, nimekuambia kwamba mzigo ni wakwangu. Kama kuna cha kufanya chochote nyinyi fanyeni ila ukweli huo mzigo ni wa kwangu”... Nilizungumza kwa ujasiri sana huku nikiendelea kujikunyata mwili mzima.

“Gilbert, mdogo wangu haya ni maisha. Natambua kwamba vijana wengi wa Tanzania mnafanya hivi kwa ajili ya kutoka kimaisha, ila itakuwa ni vizuri ukanitajia ni nani muhusika wa huu mzigo kwa manaa mtoto kama wewe huwezi kuwa na mzigo kama huu, mzigo ambao kusema kweli hapa hakuna mtu anaye weza kuamini kama unaweza kuwa nao. Hembu niambie basi mdogo wangu”
Daniel alianza kunibembeleza kwa maneno malaini hali iliyonipelekea kupandisha hasira zangu. Kuniadhibu anihadhibu halafu sahivi iniite kinafiki?

"We fanya unalotaka Daniel, nishakwambia mzigo ni wangu brother, tena usiniite mimi mdogo wako kinafiki wakati unataka kuniua kwa mateso."
Maneno yangu yaliamsha hasira zake zote na akazitumbukiza zile nyanya za umeme kwenye maji yaliyomo ndani ya hichi chumba na nikaanza kupigwa na shoti mwili mzima. Nikayakaza meno yangu kwa hasira kali sana huku nikimtazama Daniel kwa Jazba. Laiti ningetoka pale hakika ningemuua,
“Gilbert utakufa mdogo wangu, Sema haya madawa ni ya nani?”

"Unataka nikudanganye sio?. Ni ya kwako basi!!"
Nilimjibu kama mbogo huku nikiendela kumtazama , akazichomoa nyaya hizi za umeme na kunifanya niheme kwa nguvu kwani mtetemesho umetoweka mwilini mwangu. Nikamuona akazungumza na Mabaunsa hawa, akaingia mmoja wao, akaninyanyua na kunitoa ndani ya chumba huku nikiwa uchi, akanisimamisha mbele ya Daniel.

"Unaonekana una sura nzuri sana Gilbert. Huku ni mombasa ujue, Sasa unakwenda gerezani, wewe si jeuri utapelekwa gereza la Wanaume watukutu walioshindikana, huko watakulawiti na sura yako hiyo kama ya kike nakwambia utajuta, Huko Tanzania si ulikuwa unasikiaga tu habari za Mombasa? Nakuhakikishia moto utakaokutana nao ni zaidi ya Kwa Mparange huko buza kwenu Tanzania."
Maneno yake yalinishtua kiasi flani maana niliwahi kusikia Mombasa kuna Wanaume mashoga wengi sana, Lakini nilijipa matumaini nitapambana kama napelekwa gereza la wababe.................

“Poa haina shida nyie nipelekeni tu" nilimjibu kwa kujiamini

“Na kesi yako nitahakikisha ninaisimia unanyongwa hadi unakufa Mbwa wewe” Daniel aliniambia kwa jazba kama simba aliyekosa chakula.

“Sijali, Amekufa rafiki yangu, dada yangu sembuse mimi”. Nilijibu

“Hahahahahaha una kiburi etiii eheee?” Daniel alizungumza kwa dharau huku akinisogezea sura yake pembeni, nikayakusanya mate mdomoni mwangu kisha nikamtemea usoni mwake na kumfanya ayafumbe macho yake kwa muda kisha nikastukia kibao kikali kikitua kwenye shavu langu la kulia na kuniyumbisha kwa muda kisha nikaanguka chini.

“Ninakuambia nilazima ufe” Shoga wewe, Mpelekeni Kwa mashoga wenzake haraka sanaaaaaaa!!"... Alipiga kelele kama mbogo



. Mabaunsa hawa wa kiume wakanikamata kwa nguvu. Wakanitoa katika chumba hichi na nikaingizwa kwenye chumba kingine ambacho nikamkuta Martin yule mwenye asili ya kipemba akiwa na Askari wengin watatu, wakanifungua pingu pamoja na nyororo za miguuni, kisha wakanikabidhi nguo aina ya overall lenye rangi ya chungwa. Sasa niliamini naenda jela maana ndio kwanza jezi nimekabidhiwa,.
Taratibu nikaanza kulivaa huku nikiwatazama kwa ujasiri. Kusema kweli sifahamu ni kitu gani kimenipata hadi nakuwa jasiri kiasi cha kujibizana na Askari kwa Dharau.
Wakanikabidhi raba nikazivaa, kisha nikafungwa pingu tena pamoja na nyororo miguuni mwangu. Wakanitoa ndani ya chumba hichi huku wakiniweka chini ya ulinzi mkali,

Tukaingia kwenye lifti, taratibu ikaanza kushuka chini, tukafika chini kabisa, nikakuta basi refu la magereza, ndani kuna wanaume wengi walio valia sare kama zangu. Nikaingizwa ndani ya basi hili, Wafungwa hawa wenye rika tofauti tofauti waliomo ndani ya hili basi wakanitazama nami nikawatazama ili nifahamu sura zao na vimo vyao, kusema kweli hakuna mwenye mwili kama wangu na wote hawa wana miili mikubwa sana na vimo kuliko mimi. Wamejazia misuli huku wakiwa na sura za kikatili, ni siti mbili tu ambazo hazina mtu na zote pembeni wamekaa Wafungwa wanene na wenye sura za kutisha kiasi huku miili yao wakiwa wamejichora chora tattoo huku mmoja kichwani mwake akiwa amenyoa upara. Taratibu nikaa pembeni ya baba mmoja, japo uso wake una jeraha la kuchanwa na kitu chenye ncha kali ila nikajikaza na kukaa naye kwani hatoweza kunifanya kitu chochote kutokana na askari wapo eneo hili. Askari akanifunga mnyororo wangu na siti kisha akaondoka zake. Uzuri wa wafungwa tuliomo ndani ya hili basi tumetoka mataifa tofauti tofuati hii ni kutokana na muonekano wa sura zoa pamoja na rangi za miili yao. Wengine waarabu, wazungu, wasomali na hata wapemba pia,
ITAENDELEA
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 12
Wakaniingiza katika chumba chenye maji kwenye sakafu, wakanivua nguo zangu zote na nikabaki kama nilivyozaliwa. Mmoja akachukua mpira mrefu wa maji uliounganishwa kwenye koki iliyopo humu ndani, akafungua maji hayo na yakaanza kutoka kwa wingi.

Mwanaume huyu bila ya huruma akaanza kunimwagia maji haya yenye nguvu kubwa, ninayafananisha na maji ya kikosi cha zima moto cha nchi yetu ya Tanzania. Kusema kweli sina nguvu ya kuhimili nguvu ya maji haya, nikajikuta nikianguka chini. Mwanaume huyu akaendelea kunimwagia maji naya yalio zidi kuniumiza kila sehemu ya mwili wangu yanapo nigusa. Nikajikunja mwili wangu huku nikipiga kelele ya maumivu, sipo tayari kusema kweli kuzungumza ukweli wa nani ni muhisika wa huu mzigo.
Alipoona sizungumzi chochote na wametumia zaidi ya dakika kumi na tano kuniumiza na maji haya, wakabadilisha adhabu.

Wakasimama nje ya mlango wa chumba hichi sehemu ambayo haina maji kabisa na ipo juu kidogo, wakaingiaza nyaya mbili, mwili mzima ukaanza kutetemeshwa kitendo kilicho nifanya zidizi kulia kwa uchungu sana

“Sema mzigo ni wa nani?”

Daniel alizungumza huku akiwa amesimama mlangoni pamoja na wanaume hawa, sikumjibu chochote zaidi ya kumtazama kwa macho makali yaliyojaa hasira kali sana.

“Gilbert utakufa, huu ni umeme wewe, zungumza acha ubishi wa kijinga. Huna hamu ya kurudi Tanzania eheee?”

Wakazichomoa nyaya hizi na kujikuta nikishusha pumzi kwani umeme huwa ni rahisi sana kupita kwenye maji.

“Zungumza huo mzigo ni wa nani?”

“U…na….ataka nikuda…..nganye, nimekuambia kwamba mzigo ni wakwangu. Kama kuna cha kufanya chochote nyinyi fanyeni ila ukweli huo mzigo ni wa kwangu”... Nilizungumza kwa ujasiri sana huku nikiendelea kujikunyata mwili mzima.

“Gilbert, mdogo wangu haya ni maisha. Natambua kwamba vijana wengi wa Tanzania mnafanya hivi kwa ajili ya kutoka kimaisha, ila itakuwa ni vizuri ukanitajia ni nani muhusika wa huu mzigo kwa manaa mtoto kama wewe huwezi kuwa na mzigo kama huu, mzigo ambao kusema kweli hapa hakuna mtu anaye weza kuamini kama unaweza kuwa nao. Hembu niambie basi mdogo wangu”
Daniel alianza kunibembeleza kwa maneno malaini hali iliyonipelekea kupandisha hasira zangu. Kuniadhibu anihadhibu halafu sahivi iniite kinafiki?

"We fanya unalotaka Daniel, nishakwambia mzigo ni wangu brother, tena usiniite mimi mdogo wako kinafiki wakati unataka kuniua kwa mateso."
Maneno yangu yaliamsha hasira zake zote na akazitumbukiza zile nyanya za umeme kwenye maji yaliyomo ndani ya hichi chumba na nikaanza kupigwa na shoti mwili mzima. Nikayakaza meno yangu kwa hasira kali sana huku nikimtazama Daniel kwa Jazba. Laiti ningetoka pale hakika ningemuua,
“Gilbert utakufa mdogo wangu, Sema haya madawa ni ya nani?”

"Unataka nikudanganye sio?. Ni ya kwako basi!!"
Nilimjibu kama mbogo huku nikiendela kumtazama , akazichomoa nyaya hizi za umeme na kunifanya niheme kwa nguvu kwani mtetemesho umetoweka mwilini mwangu. Nikamuona akazungumza na Mabaunsa hawa, akaingia mmoja wao, akaninyanyua na kunitoa ndani ya chumba huku nikiwa uchi, akanisimamisha mbele ya Daniel.

"Unaonekana una sura nzuri sana Gilbert. Huku ni mombasa ujue, Sasa unakwenda gerezani, wewe si jeuri utapelekwa gereza la Wanaume watukutu walioshindikana, huko watakulawiti na sura yako hiyo kama ya kike nakwambia utajuta, Huko Tanzania si ulikuwa unasikiaga tu habari za Mombasa? Nakuhakikishia moto utakaokutana nao ni zaidi ya Kwa Mparange huko buza kwenu Tanzania."
Maneno yake yalinishtua kiasi flani maana niliwahi kusikia Mombasa kuna Wanaume mashoga wengi sana, Lakini nilijipa matumaini nitapambana kama napelekwa gereza la wababe.................

“Poa haina shida nyie nipelekeni tu" nilimjibu kwa kujiamini

“Na kesi yako nitahakikisha ninaisimia unanyongwa hadi unakufa Mbwa wewe” Daniel aliniambia kwa jazba kama simba aliyekosa chakula.

“Sijali, Amekufa rafiki yangu, dada yangu sembuse mimi”. Nilijibu

“Hahahahahaha una kiburi etiii eheee?” Daniel alizungumza kwa dharau huku akinisogezea sura yake pembeni, nikayakusanya mate mdomoni mwangu kisha nikamtemea usoni mwake na kumfanya ayafumbe macho yake kwa muda kisha nikastukia kibao kikali kikitua kwenye shavu langu la kulia na kuniyumbisha kwa muda kisha nikaanguka chini.

“Ninakuambia nilazima ufe” Shoga wewe, Mpelekeni Kwa mashoga wenzake haraka sanaaaaaaa!!"... Alipiga kelele kama mbogo



. Mabaunsa hawa wa kiume wakanikamata kwa nguvu. Wakanitoa katika chumba hichi na nikaingizwa kwenye chumba kingine ambacho nikamkuta Martin yule mwenye asili ya kipemba akiwa na Askari wengin watatu, wakanifungua pingu pamoja na nyororo za miguuni, kisha wakanikabidhi nguo aina ya overall lenye rangi ya chungwa. Sasa niliamini naenda jela maana ndio kwanza jezi nimekabidhiwa,.
Taratibu nikaanza kulivaa huku nikiwatazama kwa ujasiri. Kusema kweli sifahamu ni kitu gani kimenipata hadi nakuwa jasiri kiasi cha kujibizana na Askari kwa Dharau.
Wakanikabidhi raba nikazivaa, kisha nikafungwa pingu tena pamoja na nyororo miguuni mwangu. Wakanitoa ndani ya chumba hichi huku wakiniweka chini ya ulinzi mkali,

Tukaingia kwenye lifti, taratibu ikaanza kushuka chini, tukafika chini kabisa, nikakuta basi refu la magereza, ndani kuna wanaume wengi walio valia sare kama zangu. Nikaingizwa ndani ya basi hili, Wafungwa hawa wenye rika tofauti tofauti waliomo ndani ya hili basi wakanitazama nami nikawatazama ili nifahamu sura zao na vimo vyao, kusema kweli hakuna mwenye mwili kama wangu na wote hawa wana miili mikubwa sana na vimo kuliko mimi. Wamejazia misuli huku wakiwa na sura za kikatili, ni siti mbili tu ambazo hazina mtu na zote pembeni wamekaa Wafungwa wanene na wenye sura za kutisha kiasi huku miili yao wakiwa wamejichora chora tattoo huku mmoja kichwani mwake akiwa amenyoa upara. Taratibu nikaa pembeni ya baba mmoja, japo uso wake una jeraha la kuchanwa na kitu chenye ncha kali ila nikajikaza na kukaa naye kwani hatoweza kunifanya kitu chochote kutokana na askari wapo eneo hili. Askari akanifunga mnyororo wangu na siti kisha akaondoka zake. Uzuri wa wafungwa tuliomo ndani ya hili basi tumetoka mataifa tofauti tofuati hii ni kutokana na muonekano wa sura zoa pamoja na rangi za miili yao. Wengine waarabu, wazungu, wasomali na hata wapemba pia,
ITAENDELEA
nashushia na chapat ya nguvu hapa
 
Bora kuisubiri iishe kuepuka uraibu...
 
SIMULIZI YA MAISHA ; Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 13

Baada ya kama nusu saa safari ikaanza huku ulinzi wa gari za polisi ukiwa ni mkali , Tukafika sehemu yenye geti kubwa pamoja na ukuta mrefu kwenda juu huku kukiwa na bango lililo andikwa Jommo Kenyatta Prisional nikajikuta nikimeza fumba zito la mate ambalo hata kupita kooni mwangu kidogo limechukua sekunde kadhaa. Ulinzi mkali wa askari umeimarishwa kila eneo, taa kubwa sana zinazo mulika kila eneo la hili geraza zinazunguka zunguka huku zikiwa juu sana. Basi letu likaanza gongwa kwa kuwashtua baadhi ya wafungwa wezangu ambao wamepitiwa na usingizi. Askari wanne wa kiume wakaingia huku wakiwa wameshika bunduki mikononi mwao, tukaanza kufunguliwa makufuli tuliyo fungwa kwenye siti kupitia minyororo yetu.

Taratibu nikaanza kushuka huku mikono yangu nikiwa nimeitanguliza mbele kutokana na pingu tulizo fungwa mikononi. Kwa amri ya askari mmoja mrefu aliye jazia mwili wake, akatuamrisha kupanga mstari mmoja, mimi na wezangu wote tukapanga mstari, ila baunsa lililonyoa upara likabaki likimtazama askari huyu ambaye kusema kweli anatisha sana kutokana na jinsi mwili wake ulivyojazia kwa misuli mikubwa sana.

Baunsa hilo lenye upara likajaribu kumsukuma askari huyu akarudi nyuma kidogo kisha akaanza kumtandika kwa kirungu chake sehemu tofauti za mwili wake. . Woga ukaanza kunijaa kwa maana sikuwahi kuona mtu akipigwa kipigo kama hichi ambacho kwa haraka haraka unaweza kukifananaisha na kipigo cha wezi ambao niliwahi kuwashuhudia kipindi nipo Tanzania. Tukaanza kuhesabiwa namba huku kila mmoja akifunguliwa pingu zake. Bunduki karibia za askari wote wanaoimarisha ulinzi gerezani hapa wamezielekezea kwetu. Baada ya zoezi hili tukaongozana na askari baadhi na kila mmoja akaanza kuelekezwa sehemu ya kuingia, nikaingia kwenye chumba kimoja na kumkuta mwanaume mmoja mwenye asili ya kipemba akiwa amelala kwenye godoro lililolazwa chini na amejifunika blangeti zito. Taa ya chumba hichi ikazimwa na kujikuta nikikaa kwenye kitanda kisicho na mtu.

‘Ohoo Mungu wangu, leo hii ndio kwanza nimeingia gerezani’

Nilitafakari huku nikikumbuka sana maisha ya nyumbani kwetu Tanzania. Hakuna njia yoyote ya mimi kuweza kutoka humu gerezani na wala sielewi kama nitaachwa hai kwani kitendi cha kumjibu Daniel dharau na kumtemea mäte sijui kama ataniacha salama maana yeye ndiye atakayesimamia kesi yangu.

“Hey do you speak Swahili” Kijana niliyemkuta humu ndani ya hili gereza aliniuliza kwa sauti ya chini sana. Kwakweli sikuelewa ameongea nini ila nilikariri tu neno Swahili, Nikajikuta namwambia ndio nini maana yake, kisha kwa bahati akanijibu kwa kiswahili kwa kuniuliza

"Wewe ni Mbongoe!"

“Ndio...... wewe ni Mtanzania?” nami nilijibu na kuuliza

“Yap mimi ni Mzanzibar, , ila zungumza kwa sauti ya chini usije ukapigwa” alinijibuvkwa sauti ya chini

“Sawa” Nilizungumza kwa kunong’oneza huku nikijilaza kwenye kigodoro kilicholazwa chini. Kilikuwa hakina tofauti na mkeka, kimechakaa na isitoshe kina matundu.

“Hili gorodo au nini?” Nilizungumza kwa sauti ya chini sana.

“Mh ulijua upo kwenu? Hapa si Ukonga wala segerea jomba, ndio uzoee”

"Duh! Haya bwana, unaitwa nani?" Niliuliza jina lake

" Mimi ninaitwa Kinje wewe unaitwa nani?”

“Gilbert “ nilijibu kwa mkato.

Ohoo kumbe, Una umri gani?” aliniuliza, nilitafakari kwanza kabla ya kumjibu nikaona hana makuu wala ubabe hivyo anaweza kuwa rafiki yangu huku jela.

“Nina 21”

“Duu kumbe wewe bado serengeti boy, umefanya kosa gani?” Nikakaa kimya huku nikilitafakari swali la Kinje, Pia kitendo cha kuniita Serengeti boy kiliniachia swali.

“Nimekamatwa leo na madawa ya kulevya" nilimjibu

“Yaani kuna mwenzangu aliyekuwa akilala kitanda hicho ulicho lalia amenyongwa leo asubuhi, kosa lake lilikuwa eti ni kukutwa na madawa ya kulevya, yaani nashangaa huku ukikutwa na madawa ni miaka 40 jela ila yeye alikuwa na kisa na Inspekta aliyekuwa anasimamia kesi yake"
Maneno ya Kinje yakanifanya nitetemeke, woga ukazidi kunitawala mwili wangu wote, nikajikuta nikikaa kimya pasipo kuzungumza chochote, Nilikumbuka maneno ya Daniel kwamba nitanyongwa hadi nife.

"Gilbert mbona upo kimya, unawaza nini?”
Kinje aliniita kwa sauti ya chini, hata kabla sijamjibu nikastukia mlango huu wa nondo kubwa ukigongwa gongwa kwa nguvu kwa kirungu. Tukakaa kimya huku nimtazama askri anaye mulika mulika tochi ndani ya chumba chetu. Taratibu nikachukua blangeti lililokunjwa vizuri na kujifunika. Askari huyu akaondoka zake mara baada ya kuniona nimemaliza kujifunika blangeti, Kinje hakuzungumza chochote, ukimya ukatawala ndani humu. Wingi wa mawazo ulionijaa kichwani mwangu ukanifanya nipitiwe usingizi nilale fofofo.
Siku inayofuata mlio mkali wa kengele ukanikurupusha kitandani, nikajifunua blangeti langu na kukaa kitako godoroni, nikamuona Kinje akinyanyuka kitandani mwake huku akipiga miyayo. Hapa ndipo tukapata nafasi kuonana vizuri sura zetu maana jana nilipoingia tu taa zilizimwa na isitoshe ilikuwa ni usiku tayari,

“Umeamkaje?” Kinje aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.

“Salama Kinje” nilimjibu. Alinitazama kwa muda usoni mwangu kisha akaniambia
“Jaribu kuyazoe maisha ya jela, muda wa kuamka ni saa kumi na moja alfajiri”
alizungumza huku akisimama, hapo nikapata fursa ya kumuona vizuri urefu wake pamoja na umbo lake, Kweli kuna wanaume Wazuri kama wakike duniani sijapata kuona, Kinje alikuwa na weupe uliochanganywa na weusi kidogo, sura yake kama ya kitoto hivi, macho kama ya kike kabisa, nilikiri kweli wanaume wa kipemba ni wazuri. Japo mimi ni Mwanaume ila nilimsifu kimoyomoyo Mungu amemjalia Uhandsome boy.

“Mbona unanishangaa”... Aliniuliza

“Nashangaa jinsi ulivyo yaani, duh wapemba kumbe mpo hivi"... Nilimjibu

Hahahaa dogo, hapa nilikuja nikiwa bonge la HB kiasi kwamba hadi polisi wa kike walianza kunitamani, lakini sio sasa Gilbert, tena ulivyo na mashavu nakuapia hilo shavu lako lazima liishe maana chakula cha hapa sio ugali kama wa huko Tanzania, ni Ugali wa Pumba za kuku yaani, Tukibahatisha sana tunakula makande tena yasiyokuwa hata na ladha”

“Mmmmmm kumbe," nilijibu kwa mkato

“Hebu Simama”
Kinje alizungumza mara baada ya kusikia mlango wa chuma cha pembeni ukigongwa gongwa kwa kirungu na askari huyu aliye fika katika eneo hili. Nikasimama kwa haraka huku sote tukiwa tunatazama mlangoni, askari huyu mnene kiasi mwenye sura nyeusi akanitazama kwa muda, akaachia msonyo kisha akapita na kuhamia chumba kingine.
ITAENDELEA
 
SIMULIZI YA MAISHA ; Mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 14

“Hili jamaa lina roho mbaya kishenzi na wiki hii ndio zamu yake”
Kinje alizungumza huku akinitazama, nikataka kukaa ila kwa ishara ya kichwa akanikataza huku akipiga miyayo ya uchovu, na mimi nikajikuta nikipiga miyayo.

“ vitanda vyetu kuja kuvikalia ni hadi jioni muda wa kurudi kulala, inabidi ujikaze kiume Gilbert”. Kinje aliniambia huku nikishikwa na butwaa.

“Duh! Mara mia kule Segerea Tanzania, Ina maana hata kukaa siruhusiwi?” niliuliza

“Ndio, yaani Gilbert hapa unatakiwa kuwa mpole, ukijafanya kukiuka sheria za hawa askari utakufa mapema sana kwa maana kwa wao swala la kumuua mfungwa ni sawa na wewe unavyomuua sisiminzi anayekupandia mwilini mwako” ..... Alijibu Kinje

“Hivi Kinje una umri gani?”, nilibadili mada

“Nina miaka 33, nina takribani miaka 6 Humu gerezani". Alijibu

"Kumbe napaswa kukuita kaka, maana tumepishana miaka kumi na mbili hivi,". Nilimjibu kimasihara,

Mlango wetu taratibu ukafunguka.

“Nifwate mimi, sawa”

“Sawa” ........ nilimjibu.

Kinje akatangulia kutoka katika chumba hichi, nikamfwata kwa nyuma. Sikuamini macho yangu kuona wafungwa wengi sana kwenye hii kordo. Sote tukapanga foleni kwenye hii kordo kila mfungwa pembezoni mwa mlango wao.

“Dogo!. tunahesabiwa namba, kisha tunapewa majukumu ya kila mfungwa kwenda kufanya” . aliongea Kinje

“kumbe! sawa” . nilimjibu

Askari walio shika mbwa wakubwa wakaanza kukatiza katikati ya mistari hii miwili tuliyo panga, baada ya kuhesabiwa namba, wakaanza kugawa majukumu kwa lugha ya Kingereza, bahati mbaya kwangu kingereza sikijui.

“Amezungumza nini maana sielewi kingereza”. Nilimuuliza Kinje

“Tumepangiwa kufanya usafi kwenye bwalo la chakula”

“Kumbe!, sasa kwa nini wasituwekee mkalimani maana wengine hatukijui kingereza” . nilijaribu kumuuliza Kinje.

“Hahahahaha usinichekeshe dogo!. Kwani tupo uraiani au kwenye shirika ambalo huyo mkalimani tutamlipa?”
Kinje alinijibu huku akiendelea kutembea . Kila ninapo katiza wafungwa wezangu wananitazama kwa macho makali yanayonipa hofu, baadhi ya wanaume niliowatazama walininyooshe kidole cha kati ikiwa ni ishara ya kunitukana. Ama kweli hii ni mombasa, nilikiri binafsi.

“Gilbert, humu ndani ya gereza kuna makundi mbali mbali ambayo yana viongozi wao, sasa kama una ubabe ule wa mitaani huku haupo, huku kuna wasenge wanapiga kama wanaua yaani, kuwa makini kama unapenda kuishi" . Kinje alinitisha kidogo na alichoniambia, nililinganisha maneno yake na hali waliyonionyesha wale mabaunsa yalinipa hofu kidogo,.

“Sawa nimekuelewa, Hivi Kinje huku eti Wanaume wanalawitiana? Maana yule Askari anayesimamia kesi yangu aliniambia nijiandae kuwa shoga eti". Nilimuuliza lakini palepale alinipa ishara ya kukaa kimya baada ya kuona Polisi wakipita,
Tukaingia katika chumba kikubwa kilichojaa vifaa vya kufanyia usafi, Kinje akachukua gloves kubwa, akanikabidhi kisha na yeye akachukua za kwake. Tukachukua mafagio pamoja na ndoo zenye mafagio maalumu ya kudekia.

"Siamini kama mwanaume mzima naenda kudeki, huu ni Umama kabisa yaani dah!".
Nililalamika peke yangu huku Kinje akibaki kugunaTukaondoka eneo hili na kufika katika ukumbi ambao tunatakiwa kufanya usafi, cha kushangaza katika ukumbi huu mkubwa sana tupo watu wanne tu.

Likaingia kundi la mabaunsa kama nane hivi, wakatutazama huku wote wakionekana kunikazia macho mimi. Kinje hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kunitazama kwa macho ya kiuba iba, Mabaunsa hawa walio weusi kama waghana vile wakatuzingira na kutuweka kati. Mmoja wao anaye onekana ndio kiongozi wao, akanitazama kwa umakini taratibu akanishika Sehemu ya makalio yangu, nikajikuta nikirudi nyuma kidogo huku nikiutoa mkono wake kwenye makalio yangu. Baunsa huyu aliyejichora picha ya nyoka aina ya Cobra kwenye mkono wake wa kulia, akanitandika ngumi ya Mbavu na kujikuta nikipepesuka na kuanguka chini huku nikiyasikilizia maumivu ya ngumi hii ambayo nilihisi imevunja mbavu za upande wa kulia. Hivi haya ndo maisha ya Jela ama?, Nilimlaani Daniel, nikamlaani Bosi Clara lakini haikuleta tumaini lolote kw
Baunsa huyu aliyenipiga ngumi ya mbavu akachuchumaa huku akinitazama usoni mwangu akinikonyeza. Akaanza kunionyesha kidole chake cha katikati cha mkono wa kulia juu ya uso wangu huku usoni mwake akitabasamu, akayachezea mashavu yangu huku akijilamba ulimi wake, nilibaki tu mtazamaji nione atafanya nini.

"Hawa Wasenge wana adabu kweli, yaani wameniletea mtoto mwingine Mzuri hivi!! Vizuri sana, Kinje mpe taratibu huyu na umweleze sheria zangu ni zipi nisije nikamuua mimi...."! Alizungumza huku akiwapa ishara wenzake waondoke.

“Pole” Kinje alizungumza huku akininyanyua.

“Hili ni kundi la wababe wa humu jela, wana nguvu ya kumfanya mfungwa yoyote chochote kile wanachojisikia, huwa wanawafanyia unyama wanaume wenzao kwa kuwageuza kinyume na maumbile” Alizungumza maneno yaliyonikumbusha kauli ya Daniel kwamba atahahikisha nakuwa shoga kabla sijanyongwa.

“Sasa kazi ya hawa askari wa jela ni nini?”

“Kazi ya askari wao ni kuwalinda na kuwatetea wakenya wenzao, ila sisi ambao si wakenya huwa tunapata manyanyaso makubwa. Inafiia kipindi hadi tunachomwa visu, yaani ili mradi shida tu”
Kinje alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu. Tukaendelea kufanya usafi wa ukumbi huu, tukafanikiwa kumaliza kufanya usafi jengo lote la bwalo hili la kulia chakula.

"Hili eneo huwa wanadeki wale waliongia na kukupiga”

“Kwa hiyo unataka kuniambia kwamba tunawafanyia watu kazi”

“Ndio maana yake”. Alisema kinje, kweli bila nguvu niliona jela pagumu, nilimkumbuka rafiki yangu Chalamala aliyeuwawa na Polisi wakati tukijaribu kutoroka, alinifundisha ngumi lakini sikuiva vizuri, laiti ningejua kupigana kama yeye hakika nami ningeogopeka huku jela.
Baada ya muda mrefu kengele ikagongwa na wafungwa wote tukaingia kwenye bwalo tulilokuwa tunafanya usafi mimi na Kinje. Taratibu tukapanga foleni, hapa ndipo nikaanza kupata nafasi ya kuwaona wafungwa karibia wote ndani ya hili gereza. Wapo wababa wenye muomba makubwa sana yaliyo jengeneka kwa misuli kwa haraka haraka unaweza kuhisi ni wacheza mieleka, wazee vikongwe pia wapo pamoja na vijana wenye rika kama langu,
Nikiwa karibu kabisa na sehemu ya kuchukulia chakula, mbele yangu kwenye huu mstari akaingia Mwanaume mmoja mrefu sana amepanda hewani na mikono imetuna misuli, baada ya yeye wakaanza kuingia vijana kama Kumi hivi, cha kushangaza Askari walimo humu ndani wala hawakushuhulika na uonevu wanaoufanya Wafungwa hawa. Wafungwa wengine waliopo nyuma yangu wakaanza kulalamika huku wakininyooshea vidole vya kati kuashiria wananitukana. Nikiwa katika kushangaa shangaa, akanifwata mfungwa mmoja na kunivuta nje ya mstari hadi nikapepesuka, ila nikajitahidi kujiwekea balansi nisianguke, Nikatazama mstari huu mkubwa, wafungwa wengine wakaanza kunicheka. Kila niliyemuomba kuingia kwenye mstari ananikatalia, nikamtazama Kinje akatingisha kichwa na kwa ishara akaniomba nikapange mstari nyuma kabisa. Nikawatazama wafungwa walio sababisha mimi kutolewa kwenye mstari, kwa haraka nikaanza kutembea hadi alipo mtu wao wa wisho kuingia kwenye mstari, nikajaribu kujipenyeza ila wanisukuma. Japo mimi ni mgeni ila sikuhitaji kuwa mnyonge kiasi hiki,. nikamtandika kofi la uso msichana mmoja ambaye anaonekana kihehere na nimuongeaji katika kundi hili. Sikujua nachokoza nyuki, najuta kwanini nilimtandika, Ghafla.........

Vipande vyote 30 unaweza kuvipata kwa Tshs 1000 tu ya Kitanzania. Lipia kwenda Halopesa namba 0621249611 kisha mtext mwandishi whatsapp kwa namba 0621249611 akutumie
 
Back
Top Bottom