Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

HOROMBO.

5b9b773c85ba173c3a61848751efa146.jpg


Katika vituo vyote sehem niliyoipenda zaidi kukaa ni horombo. Ilituchukua masaa karibu 9/10 kufika HOROMBO. Ni sehem iliyo changamka.. kama kijiji fulani hivi..katika safari yetu Kuna vituo vya kupumzika.. Na pia kuna sehem huko huko barabarani ni stop kwa ajili ya Lunch... Kuna upepo na baridi sana yaani kuliko kukaa nje mtu unaenda chooni upepo usikupige. Vyoo ni Safi na vimejengwa vizuri.

nakumbuka nikiwa nakaribia kibao cha Horombo I was excited kwamba nimefika after a long walk, nikaanza kutembea haraka huku nashangilia na kupiga mayowe, haikuchukua hata sekunde kadhaa hali yangu ikabadilika I couldn’t walk, mapigo ya moyo hayakua sawa kutembea nikashindwa, kihere here chote kikaishia hapo.. ikabidi nipumzike chini na waanze kuniangalia hali yangu. baada ya dakika kadhaa hali yangu ilivyokua sawa ndio nikafika hapo. Yaani usicheze na mambo ya altitude..

Complication..

Ilipofika usiku nikaanza kujisikia vibaya... Yaani sijielewi elewi hali yangu sio nzuri, nikaenda kupima oxygen na vitu vingine wakanambia niko safi tu laba uoga na mawazo. Na kweli I was scared. Nikaingia kulala mapema nikashtuka kama saa 7 USIKU, MAPIGO YANGU ya moyo yanapiga kwa kasi ya ajabu, siwezi kuhema vizuri, nikiangalia pembeni naona kama kila mtu kalala, nikalaani kitendo cha kushtuka mida hiyo nikihesabu muda naona hadi kukuche its like forever. Na nikawa naogopa pia kulala usingizi what if hivi ninavyoshindwa ku breathe ndio nipitilize moja kwa moja.

Sim hazitoki... hakuna mtandao..The only thing nilifanya ni kusikiza music tu mpaka kunakucha. Nimesikiza album za Maher Zain hapoo wee.. Asubuhi tunavyohadithiana kumbe kila mtu anasema I couldn’t sleep last night..





Sent from my iPhone using JamiiForums
Hyo reception ya hapo mandara nimejenga mm hyo kench kuisimamisha ilitusimbua maana kulikuwa na baridi sanaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiii reception ya mandara nakumbuka ilivonitesa kujenga na kukaguliwa kila sikuuu daaaah
Safari ya Mandara.

f75e778e28a5a00dfe275f01fe7babc5.jpg


Hii ndio ilikua point yangu ya kwanza baada ya kutoka getini. Nilikua na personal porter anaitwa FREDY. Mwenyewe alinipokea bag na kijitambulisha vizuri kwangu. Ukiwa na personal guide ina maana yeye atakua na wewe bega kwa bega.. atakubebea back pack.. achana na wale guide wa group.

Tulianza kwa story akanielezea safari zake milimani.. yeye keshapanda mara 6 hadi Uhuru peak.. I was excited..mwanzo story zilikolea baadae zikakata ule uchovu.
Tunavyopanda tulikua tunakutana na makundi ya watu wanarudi na wengi walikua wanatuambia “pole pole” nadhani huu ndio msemo maarufu ukifuatiwa na “Jambo”.
Nilianza kuchoka jinsi masaa yanavyokwenda.. Nikawa kama siwezi kupumua vizuri muda mwingi Fred alikua ananisitiza kunywa maji...

Kuna muda wenzangu walikua mbele.. baada ya kupumzika nikasema hebu nikae hili kundi sitaki kubaki nyuma... Enhee bana kumbe kasi yao haiendani na mimi.. ila kutembea hata dakika 5 nyingi.. nikaona kama roho inataka kutoka mapigo ya moyo yanaenda mbio hatari roho kama yataka kuchomoka.. joto likanipanda.. Fred as usual akaniambia pumzika. Nikakaa chini vua sweta nikanywa maji.. baada ya muda ndio nikarudi hali ya kawaida.. Nilishaanza kupanick kuwa nakufa sasa. maana hapo si tulishaambiwa watu wanakufa huko sana na kila mtu unamwbia unaenda Kupanda Mlima unakuwa na doubt.. Mimi nikajua mama yangu hapa na mimi ndio bye bye

Akanishauri kuwa kila mtu ana speed yake so i should keep same speed maana tunazidi kupanda juu.. hali ya hewa ni ya mgandamizo.. Tunaingia Mandara saa 2/3 usiku. i was excited kwamba after a long walk kuna sehem tumefika tupumzike. Kitu cha kwanza ni ku register majina.. kulikua na baridi hatari mikono ilikua na ganzi hata kuandika nilishindwa waliiandikia jina nikaweka sign tu.


Tukaonyeswha dormitories nikatafuta kitanda changu cha chini..

c282b3eeccab55a3f072cfe19f3a018c.jpg


yaani kuna bariiidi hatari nikajifunika sleeping bag nikajilaza.. nina hasira kishenzi.. ukiuliza hasira za nini sijui..
Usingizi ukanipitia baada ya muda kidogo mtu akaja kuniamsha kwa ajili ya dinner yaani nilichukia nikaona sijawahi kukutana na mtu mbaya na katili duniani kama huyo alieniamsha kula.. Na hapo tunasisitizwa kwamba ni lazima ule kama unataka kufika juu.. Kufika kileleni nataka ila kama hali ndio hii NO WAY

Nikaanza kulia ndani ya sleeping bag... lia kishenzi.. Makamasi na machozi yanatiririka tu ila nalia kimya kimya watu wasinisikie. mtu unaweza kushangaa kama ni the same person niliyekuwa nashangilia muda mchache uliopita.. Nikawa najiuliza hivi nimekuja kufanya nini huku?? Baridi lote hili tena nikale huko nje.... nikaja kuamshwa tena hapo wenzangu hawawezi kula hadi watu wote watimie.. Nimefika dinning sijataka kuongea na mtu.. wakinichekesha najilazimisha kucheka. Huo muda Akili inawaza mambo kibao.

Chakula chenyewe nakutana na vegetable soup.. macaroni.. ndio siyapendi kudadadeki.. mikate.. chai... Chakula ni kizuri ila hamu ya kula sikua nayo hata kidogo.. Duh nakula then straight in bed sisemeshani na mtu. Na mtandao ni hakuna so no whatsup. Instagram wala JF.

Hii ni asubuhi.. tunajiandaa kwenda Horombo

57e4798f9e4bd7a8400770fcc660ae35.jpg


Huko ni njiani tu...


View attachment 981761


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA

Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.


Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..

c449ae42b836bcda5f243c52a04c237b.jpg


MAANDALIZI YA SAFARI.

Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.

Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.

Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..


KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.

Tent tulizotumia kulala
181393d9af06585dd377fcf76f9b607e.jpg



Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi

e388057a293813c80ee7f191631c286c.jpg


The View
16bc00a84e515adb383cf530a5c579ce.jpg


3f673959c9f79e081a5f7c6109e53c62.jpg



Nitaendelea Next post.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Wewe ni mtu wa DAR or sisi wa kanda hii ndio kama kwenda Beach tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sema tu unaenda kujirusha kwenye sherehe za kuupokea mwaka mpya wa 2019. Hongera sana kwa ujasiri wako pamoja na kujua fika kwamba ungeweza kupoteza uhai wako kwa uamuzi wako wa kufika kileleni. Vilele vingine ni hatari sana 😉😉😉

Kesho best.... Nimechoka zangu.

ASANTE


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Naenda kuleeee kileleni [emoji4]


1e4b57f88fbaa7f5071f6234d5e45cb9.jpg


Huyu mtoto ana miaka 10 alitokea SA.. wakiwa na Trek4Mandela.. Sijui alifika summit

1659e050ed47d9aae8fcd9741fa10165.jpg


Hii ndio sehem ya mwisho maji kupatikana

fb4082a14402e62a0786908a5e18d88e.jpg


Angalia hao porters

c347751072ae8b7ac44d5b216c81dae0.jpg


e7a1be1ead060058f678e2ab411d2978.jpg


Huyu baba kapanda Mlima mara 18 na siku zote alifika kileleni
cf04cf91cf6d364bffcf48953a4f356a.jpg


Hiko kitanda cha pembeni juu kabisa ndio nililala hapo.. Chini kulikua na mdada mzungu anatapika kishenzi..

4fe4ba885b7b3b2101e99f1c0d788559.jpg


Mandhari ya Horombo

f812dcd0ea12517e859d013166f0921d.jpg


Sehem ya kupumzika

438448f24dab6db9fc860a0d5c9a7ad8.jpg


Kulikua na baridi nje.. Hiko choo nilienda kuingia ndani.. Ushawahi kuona unakaa chooni na unaona ndio sehem nzuri kabisaa kuliko nje

f706f46ae3d08f281b5a3431cf16fe1b.jpg





Sent from my iPhone using JamiiForums
Hongera Heaven, hii njia kweli nzuri hadi kuna vitanda[emoji2297][emoji2297][emoji2297].......nilipanda mlima siku sita, kitanda nilikuja kukiona siku ya saba tulivyoshuka sijui ni mweka pale sijui mwika...nimesahau jina, ajabu tulipanda siku 6 lkn kushuka ni siku moja tu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu na lile baridi kweli unaweza usiwe na habari nae, nadhani utakuwa umeamua tu kutufurahisha humu

Sent using Jamii Forums mobile app
Huwezi ndugu coz kulala tu kwenye huwezi kujinyoosha, unajikunja ili upate joto, halafu nguo za kulalia zinabana fulani hivi mfano zetu zilikuwa zinaitwa thermos, ukivaa hizo nguo then shuka ni kama mfuko hivi, unaingia zako kwenye hilo shuka....unajikunja kuutafuta usingizi

Salute to those porters.....niliwashangaa wale watu lkn pia nilimshangaa Mungu..... kwenye jiwe la kubusu sisi tunawaza tutapitaje manake ukiteleza kidogo tu wanakusahau lakini wao wanapita utadhani wanapita kwenye barabara tena na mizigo kichwani au mgongoni na mkifika kituoni mnakuta wameshafunga matent, kila mtu bag lake limeshawekwa kwenye tent lake, wameshaivisha chakula, meza zimeshaandaliwa and they are so kind and humble. Nilisikitikaga sana kusikia zile kampuni zinawalipa ujira mdogo sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo jiwe la kubusu ndo lipoje im trying to Imagine hata sielewi
Jiwe la kubusu ni hivi, ili kutoka pale barango kwenda karanga lazima mpite mlimani, na mkiwa pale barango mlima unauona uleeeee, mkifika pale mlimani njia ni nyembamba sana, sasa kuna sehemu kuna jiwe kubwa ili kupita hapo lazima ulikumbatie hilo jiwe na unapita upande upande lakini mbaya zaidi chini kuna korongo so ukikosea step kidogo tu unaweza kujikuta uko korongoni, so mnapita mmoja mmoja na kwa uangalifu mkubwa. Nakumbuka kundi letu tulikuwa zaidi ya watu 30 tulitumia almost 2hrs kuvuka hapo....na slogan ya mlimani ni Pole Pole....no hurry

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiwe la kubusu ni hivi, ili kutoka pale barango kwenda karanga lazima mpite mlimani, na mkiwa pale barango mlima unauona uleeeee, mkifika pale mlimani njia ni nyembamba sana, sasa kuna sehemu kuna jiwe kubwa ili kupita hapo lazima ulikumbatie hilo jiwe na unapita upande upande lakini mbaya zaidi chini kuna korongo so ukikosea step kidogo tu unaweza kujikuta uko korongoni, so mnapita mmoja mmoja na kwa uangalifu mkubwa. Nakumbuka kundi letu tulikuwa zaidi ya watu 30 tulitumia almost 2hrs kuvuka hapo....na slogan ya mlimani ni Pole Pole....no hurry

Sent using Jamii Forums mobile app
Ruwaa[emoji134]kumbe ndo hivyo basi hiyo njia sio poa
Ahsante kwa ufafanuzi
 
Kwa mimi nafikiria kuja kupanda tena miaka ya mbeleni uko ila bado sijapanga nitaenda lini ila kwa ushauri mdogo tu kwa wanaotaka kupanda mlima kilimanjaro hauhitaji mazoezi sana ili ufike kileleni labda uwe mtu wa kushinda kwenye gari kutembea huna kumbukumbu ulitembea lini hata nusu saa kwa siku hapo fanya mazoezi mepesi tu kinacho washinda watu wengi kufika kileleni ni kwa sababu mlima kilimanjaro unajitengenezea hali yake una zaidi ya hali3 utakazo kutana nazo equatorial,Savannah, mediteranian nk so unakuta mtu mwili wake unashindwa kuhimili hali hii nyingine anaweza ukiwa kwenye Savannah unaweza hata huumwi kichwa ila ukienda sehemu nyingine hali inabadirika unaanza kuumwa na kunakua na mgandamizo wa hewa so kunakushinda
Cha kufanya pima afya yako vaa na beba mavazi na vifaa rafki tokana na ushahuri wa watu wanaokuongoza naamini unaweza toboa maana kule wanaenda wanajeshi ila kunawashinda sababu ya hali ya hewa ila ma porters na tour guiders muda mwingine unakuta wamevaa t-shirts na suruali tu na they're fine ila wewe unavaa mikoti na mikoti ila bdo hali inakusumbua tu
Mimi pia nilipita njia nzuri ya marangu na baridi lipo kuanzia mandara me siku ya kwnza tu betri ya simu ilikata moto wakt sikuitumia hata
All the best kwa mwendaji yeyote mwaka huu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom