SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #301
ππ πππ πππππ
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
Wakati sherehe hiyo ikiendelea ndani ya chuo cha Mark Moon, nje ya geti lilipaki gari moja la kifahari, vijana watatu wakashuka na kuingia ndani ya chuo hicho bila wasiwasi wowote kama vile wanafunzi wanaosoma chuo hicho. la hasha, hawa walikuwa ni vijana kutoka kwa Madam Jane waliotuma kuja kuchukua sampuli yoyote kutoka kwa Yusto ambayo itatumika kufanya kipimo cha vinasaba yaani DNA.
Madam Jane alitaka kuthibitisha kwanza kama Yusto ni mtoto wake au laa...
SASA ENDELEA...
[emoji294][emoji294][emoji294]
Yusto na Caren walikumbatiana kwa zaidi ya dakika 3, hakika kila mmoja alionekana amemkumbuka mwenzake kwa kiwango kikubwa.
Tukio hilo liliteka hisia za wanafunzi wengi waliokuwa wamehudhulia sherehe hiyo. Kwa macho ya kawaida tu kila mtu aliona wazi kuwa Yusto na Caren walikuwa wakipendana sana, haikuwa na sababu ya kujiuliza mara mbili mbili.
"Yusto baba"
"Naam Caren wangu"
"Kwa nini umenifanyia hivi kwa nini lakini"
"Nisamehe mpenzi wangu, nitakueleza kila kitu baadae"
"Kwa hiyo wewe ndio umeandaa hii sherehe"
"Hapana hata sijui ni nani, nahisi ni Frank na marafiki zangu wengine, hata sikuwa nakumbuka siku yangu ya kuzaliwa"
"Hahaha nilijua tu, nafurahi kukuona uko salama mpenzi"
"Asante mimi pia Caren, nilikumiss mno, haya basi twende tukakae tumalizane na hili kwanza"
Yusto na Caren waliokuwa wakiongea kwa sauti ya chini, walishikana mikono na kuongozana kuelekea kwenye viti ambavyo vilikuwa vimeandaliwa kwa ajili yao.
"Ona watu walivyofurahi Yusto, yaani naona kama nafunga ndoa na wewe vile"
"Ahahaha usijali one day yes, bado tunasafiri ndefu sana mimi na wewe, si unajua"
"Najua Yusto ila nimesha kwambia no matter what I'LL STAY WITH YOU, NITABAKI NA WEWE Yusto wangu"
"Asante Caren naomba umaanishe kweli, BAKI NA MIMI kuna mengi makubwa yanakujaa huko mbele"
"Yapi tena babangu, kwanza hawa watu wamejuaje kama sisi ni wapenzi"
"hata sijui ila hii ni akili ya Frank kijana wa hovyo sana yule"
Alisema Yusto huku wote wakikaa kwenye viti vyao.
"Umemuona huyo Frank sasa" aliuliza Caren
"Hapana , yuko wapi"
"Yule pale mbele na Sophia"
"Ooh wow Sophia amepona kumbe"
"Ee yuko vizuri japo si sana, tumeshinda wote tangu jana tunakutafuta"
"Hahaha poleni"
Sophia na Frank walionekana wamekaa viti vya mbele kabisa huku nyuso zao zikionekana kujawa na furaha tere, wakawa wananong'ona maneno fulani huku wakiwatazama Yusto na Caren.
"Ulibuni kitu kizuri sana Sophia" alisema Frank huku akigeuka na kumtazama Sophia.
"Hahah nilikwambia ukabisha ona sasa wanavyopendezana kuwa pamoja" alisema Sophia kisha akatabasamu.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo wale vijana kutoka kwa madam Jane tayari walishajipenyeza na kuingia ukumbini, wakajichanganya na watu waliokuwa wamehudhulia sherehe hiyo, wakawa wanawinda winda ni vipi watapata sampuli ya kupima vinasaba kutoka kwa Yusto.
"Sasa sikia hapa tunahitaji kitu kidogo sana, damu, nywele, mate au kitu chochote kutoka kwenye mwili wa Yusto, ni hivo tu, ikitokea nafasi tuitumie haraka tusepe" alisema mmoja wa wale vijana ambae alionekana kuwa kiongozi wa wenzake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Revocatus alionekana akiongea na mtu kwenye simu mara tu baada ya kurejea kambini akitokea kwa Osman Azizi.
"Anko Azizi"
"Ndiyo Revo niambie"
"Aisee, nimefika kambini sijamkuta Zubeda"
"Mmh kweli, au Caren kaondoka nae"
"Hapana angeniambia, hata hivyo nimekuta milango iko wazi"
"Dah hiyo ni mbaya sana Revo, hebu anza kumtafuta hakikisha unamrudisha si unajua huyo mama ni kama akili yake siku hizi imeanza kusoma vizuri ataleta shida kama akiingia mtaani tena"
"Sawa anko nimekuelewa"
"Lakini usimwambie Caren, akiuliza wewe sema Zubeda yupo"
"Sawa anko"
Revocatus alikata simu huku kijasho kikimtoka, akajifuta na kuvaa koti lake kisha akaanza kazi ya kumtafuta Zubeda ambae alikuwa ameondoka kitambo sana akaingia msituni.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Asubuhi ya siku inayofuta wakati sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa Yusto ikiendelea kule chuoni Zubeda yeye alikuwa msituni akiendelea kutembea asijue anako elekea.
Alikuwa ametembea usiku kucha lakini mama huyo kichaa hakuonekana kuchoka hata kidogo.
Mwisho aliifikia barabara ya lami iliyokuwa ikikatisha katika ya msitu huo.
Zubeda alionekana kufurahia sana mara tu baada ya kuiona barabara hiyo, akakimbia na kuanza kugaragara katikati ya barabara hiyo huku akichekelea sana.
Mara alisikia muungurumo wa gari linakuja. Zubeba alisimama akaangaza macho huku na huku kisha akakimbia msituni na kujificha nyuma ya mti mmoja mkubwa hali akiwa bado anacheka.
Kwa mbali aliona msafara wa magari matatu madogo yaliyoongozana unakuja. Alitulia akasubiri hadi pale yalipofika karibu kabisa na usawa aliokuwepo.
Ghafula Zubeda alikimbia na kwenda kusimama katikati ya barabara kisha akatanua mikono yake yote miwili kama vile anataka kuizuia gari isipite.
La haura, dereva aliyekuwa kwenye gari ya mbele alishtuka kumuona mtu anatokea msituni ghafula na kusimama mbele ya gari katikati ya barabara. Lilikuwa ni kutukio ambalo hakulitegemea.
Dereva alijitahidi kufunga breki na kujaribu kumkwepa Zubeda lakini jitihada zake hazikuzaa matunda kwa asilimia mia moja.
Zubeba aligongwa na gari kisha akarushwa pembezoni mwa barabara huku yale magari yaliyofuta nyuma nayo yakagongana baada ya lile gari la mbele kufungua breki ghafula.
Ilikuwa ni ajali ambayo ilileta maafa kwa kiasi. Hakuna gari iliyoanguka lakini hali ilikuwa ngumu kwa Zubeda ambae alikuwa amelala pembeni ya barabara hoi taabani.
Zubeda alikuwa akipumua kwa shida sana, damu ikawa inamtoka puani na masikioni.
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa.
Mwisho milango ya magari yote ilifunguliwa watu kadhaa wakatoka kwenda kumuangalia yule mtu aliyewasababishia ajali kisha na yeye akajeruhiwa vibaya.
Walimzunguuka Zubeda wakawa wanamshangaa kisha mmoja wao akainama na kumgusa mshipa wa shingoni.
"Vipi?"
"Ni mzima, anapumua pia"alisema yule mtu aliyemgusa Zubeda.
Baada ya kusema hivyo, mmoja kati ya wale watu waliosimama alikimbia hadi lilipokuwa gari la katikati akagonga kioo cha mbele siti ya pembeni kwa dereva.
Kioo kikashushwa taratibu.
"Bosi, yule mama ni mzima" Alisema yule mtu.
"Basi mchukue mpelekeni kwenye hospitali yangu, msiache arama yoyote kuonyesha kulikuwa na ajali, mimi natangulia"
Sauti ya mtu aliyekuwa ndani ya lile gari ilisikika kisha akaonekana anafunga kioo taratibu.
Amani usiamini ndugu msomaji, mtu huyo hakuwa mwingine bali ni bosi Mark Moon tajiri na mmliki wa chuo cha kimataifa cha mark Moon, mume wa zamani wa madam jane yaani baba yake John (master joo).
Mark moon alifunga kioo na dereva akawasha gari, wakaondoka taratibu.
Je, nini kitafuata?
Zubeda kwenye mikono ya mark moon...!!
Wakati huo madam Jane anatafuta sampuli ya Yusto kwa ajili ya kupima vinasaba....!!
Osman Azizi anapanga nini....!!
Nini hatima ya Brandina, Yusto na Caren....!!
WhatsApp
0756862047
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
Wakati sherehe hiyo ikiendelea ndani ya chuo cha Mark Moon, nje ya geti lilipaki gari moja la kifahari, vijana watatu wakashuka na kuingia ndani ya chuo hicho bila wasiwasi wowote kama vile wanafunzi wanaosoma chuo hicho. la hasha, hawa walikuwa ni vijana kutoka kwa Madam Jane waliotuma kuja kuchukua sampuli yoyote kutoka kwa Yusto ambayo itatumika kufanya kipimo cha vinasaba yaani DNA.
Madam Jane alitaka kuthibitisha kwanza kama Yusto ni mtoto wake au laa...
SASA ENDELEA...
[emoji294][emoji294][emoji294]
Yusto na Caren walikumbatiana kwa zaidi ya dakika 3, hakika kila mmoja alionekana amemkumbuka mwenzake kwa kiwango kikubwa.
Tukio hilo liliteka hisia za wanafunzi wengi waliokuwa wamehudhulia sherehe hiyo. Kwa macho ya kawaida tu kila mtu aliona wazi kuwa Yusto na Caren walikuwa wakipendana sana, haikuwa na sababu ya kujiuliza mara mbili mbili.
"Yusto baba"
"Naam Caren wangu"
"Kwa nini umenifanyia hivi kwa nini lakini"
"Nisamehe mpenzi wangu, nitakueleza kila kitu baadae"
"Kwa hiyo wewe ndio umeandaa hii sherehe"
"Hapana hata sijui ni nani, nahisi ni Frank na marafiki zangu wengine, hata sikuwa nakumbuka siku yangu ya kuzaliwa"
"Hahaha nilijua tu, nafurahi kukuona uko salama mpenzi"
"Asante mimi pia Caren, nilikumiss mno, haya basi twende tukakae tumalizane na hili kwanza"
Yusto na Caren waliokuwa wakiongea kwa sauti ya chini, walishikana mikono na kuongozana kuelekea kwenye viti ambavyo vilikuwa vimeandaliwa kwa ajili yao.
"Ona watu walivyofurahi Yusto, yaani naona kama nafunga ndoa na wewe vile"
"Ahahaha usijali one day yes, bado tunasafiri ndefu sana mimi na wewe, si unajua"
"Najua Yusto ila nimesha kwambia no matter what I'LL STAY WITH YOU, NITABAKI NA WEWE Yusto wangu"
"Asante Caren naomba umaanishe kweli, BAKI NA MIMI kuna mengi makubwa yanakujaa huko mbele"
"Yapi tena babangu, kwanza hawa watu wamejuaje kama sisi ni wapenzi"
"hata sijui ila hii ni akili ya Frank kijana wa hovyo sana yule"
Alisema Yusto huku wote wakikaa kwenye viti vyao.
"Umemuona huyo Frank sasa" aliuliza Caren
"Hapana , yuko wapi"
"Yule pale mbele na Sophia"
"Ooh wow Sophia amepona kumbe"
"Ee yuko vizuri japo si sana, tumeshinda wote tangu jana tunakutafuta"
"Hahaha poleni"
Sophia na Frank walionekana wamekaa viti vya mbele kabisa huku nyuso zao zikionekana kujawa na furaha tere, wakawa wananong'ona maneno fulani huku wakiwatazama Yusto na Caren.
"Ulibuni kitu kizuri sana Sophia" alisema Frank huku akigeuka na kumtazama Sophia.
"Hahah nilikwambia ukabisha ona sasa wanavyopendezana kuwa pamoja" alisema Sophia kisha akatabasamu.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo wale vijana kutoka kwa madam Jane tayari walishajipenyeza na kuingia ukumbini, wakajichanganya na watu waliokuwa wamehudhulia sherehe hiyo, wakawa wanawinda winda ni vipi watapata sampuli ya kupima vinasaba kutoka kwa Yusto.
"Sasa sikia hapa tunahitaji kitu kidogo sana, damu, nywele, mate au kitu chochote kutoka kwenye mwili wa Yusto, ni hivo tu, ikitokea nafasi tuitumie haraka tusepe" alisema mmoja wa wale vijana ambae alionekana kuwa kiongozi wa wenzake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Revocatus alionekana akiongea na mtu kwenye simu mara tu baada ya kurejea kambini akitokea kwa Osman Azizi.
"Anko Azizi"
"Ndiyo Revo niambie"
"Aisee, nimefika kambini sijamkuta Zubeda"
"Mmh kweli, au Caren kaondoka nae"
"Hapana angeniambia, hata hivyo nimekuta milango iko wazi"
"Dah hiyo ni mbaya sana Revo, hebu anza kumtafuta hakikisha unamrudisha si unajua huyo mama ni kama akili yake siku hizi imeanza kusoma vizuri ataleta shida kama akiingia mtaani tena"
"Sawa anko nimekuelewa"
"Lakini usimwambie Caren, akiuliza wewe sema Zubeda yupo"
"Sawa anko"
Revocatus alikata simu huku kijasho kikimtoka, akajifuta na kuvaa koti lake kisha akaanza kazi ya kumtafuta Zubeda ambae alikuwa ameondoka kitambo sana akaingia msituni.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Asubuhi ya siku inayofuta wakati sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa Yusto ikiendelea kule chuoni Zubeda yeye alikuwa msituni akiendelea kutembea asijue anako elekea.
Alikuwa ametembea usiku kucha lakini mama huyo kichaa hakuonekana kuchoka hata kidogo.
Mwisho aliifikia barabara ya lami iliyokuwa ikikatisha katika ya msitu huo.
Zubeda alionekana kufurahia sana mara tu baada ya kuiona barabara hiyo, akakimbia na kuanza kugaragara katikati ya barabara hiyo huku akichekelea sana.
Mara alisikia muungurumo wa gari linakuja. Zubeba alisimama akaangaza macho huku na huku kisha akakimbia msituni na kujificha nyuma ya mti mmoja mkubwa hali akiwa bado anacheka.
Kwa mbali aliona msafara wa magari matatu madogo yaliyoongozana unakuja. Alitulia akasubiri hadi pale yalipofika karibu kabisa na usawa aliokuwepo.
Ghafula Zubeda alikimbia na kwenda kusimama katikati ya barabara kisha akatanua mikono yake yote miwili kama vile anataka kuizuia gari isipite.
La haura, dereva aliyekuwa kwenye gari ya mbele alishtuka kumuona mtu anatokea msituni ghafula na kusimama mbele ya gari katikati ya barabara. Lilikuwa ni kutukio ambalo hakulitegemea.
Dereva alijitahidi kufunga breki na kujaribu kumkwepa Zubeda lakini jitihada zake hazikuzaa matunda kwa asilimia mia moja.
Zubeba aligongwa na gari kisha akarushwa pembezoni mwa barabara huku yale magari yaliyofuta nyuma nayo yakagongana baada ya lile gari la mbele kufungua breki ghafula.
Ilikuwa ni ajali ambayo ilileta maafa kwa kiasi. Hakuna gari iliyoanguka lakini hali ilikuwa ngumu kwa Zubeda ambae alikuwa amelala pembeni ya barabara hoi taabani.
Zubeda alikuwa akipumua kwa shida sana, damu ikawa inamtoka puani na masikioni.
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa.
Mwisho milango ya magari yote ilifunguliwa watu kadhaa wakatoka kwenda kumuangalia yule mtu aliyewasababishia ajali kisha na yeye akajeruhiwa vibaya.
Walimzunguuka Zubeda wakawa wanamshangaa kisha mmoja wao akainama na kumgusa mshipa wa shingoni.
"Vipi?"
"Ni mzima, anapumua pia"alisema yule mtu aliyemgusa Zubeda.
Baada ya kusema hivyo, mmoja kati ya wale watu waliosimama alikimbia hadi lilipokuwa gari la katikati akagonga kioo cha mbele siti ya pembeni kwa dereva.
Kioo kikashushwa taratibu.
"Bosi, yule mama ni mzima" Alisema yule mtu.
"Basi mchukue mpelekeni kwenye hospitali yangu, msiache arama yoyote kuonyesha kulikuwa na ajali, mimi natangulia"
Sauti ya mtu aliyekuwa ndani ya lile gari ilisikika kisha akaonekana anafunga kioo taratibu.
Amani usiamini ndugu msomaji, mtu huyo hakuwa mwingine bali ni bosi Mark Moon tajiri na mmliki wa chuo cha kimataifa cha mark Moon, mume wa zamani wa madam jane yaani baba yake John (master joo).
Mark moon alifunga kioo na dereva akawasha gari, wakaondoka taratibu.
Je, nini kitafuata?
Zubeda kwenye mikono ya mark moon...!!
Wakati huo madam Jane anatafuta sampuli ya Yusto kwa ajili ya kupima vinasaba....!!
Osman Azizi anapanga nini....!!
Nini hatima ya Brandina, Yusto na Caren....!!
0756862047