Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

Kimya kingi mkuu na ngoma imefikia patamu sana.
 
DO NOT SHOUT
(Usipige kelele)
Sehemu ya..............20
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Email: saulstewarty@gmail.com.

ILIPOISHIA...

Majasusi wanafanikiwa kuidukua simu ya Caren ikiwa ni katika harakati za kumpeleleza ili kujua kama ni kweli Caren ndiye agent anaehusika na matukio kadhaa yaliyotokea chuoni.
Yusto nae akiwa na pamoja na majasusi hao anaradhimika kuifanya zaki yake lakini moyoni akiwa bado anampenda Caren.


Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA...

Jasusi Simigo na Brandina waliendelea kusubiri huku wakiwa wameelekeza macho na masikio yao kwenye compyuta kufuatilia kila kitakachoendelea kwenye simu ya Caren.
***

Caren akiwa chumbani kwake alionekana kukosa raha kabisa, matukio kadhaa yaliyotokea siku hiyo yalimuondolea mudi kabisa.
Kwanza alikutana na John kijana anaelazimisha kuwa na mahusiano nae, na mara kadhaa amekuwa akimpa vitisho kuwa atamfanyia kitu kibaya Yusto kama tu ataendelea kuwa nae.
Pili amekutana na Sophia ambae anaonyesha kumpenda sana Yusto na yuko tayari kufanya chochote ili ampate, hali inayopelekea wao kuwa kama maadui.
Tatu na kubwa zaidi ni suala lake la mahusiano na Yusto. Kwa taratibu na sheria za kazi anayoifanya Caren hakuwa akiruhusiwa kuwa na mahusiano na mwanaume yoyote, lakini tayari Caren alishavunja sheria hiyo na kujikuta anaangukia penzini na kijana Yusto. Anashindwa kujizuia kabisa kutokana na msukumo wa sihia dhidi ya kijana huyo zinazotoka ndani kabisa ya moyo wake. Pasipo kujua kuwa Yusto alikuwa ni mlinzi wa Siri wa chuo hicho na hii ilikuwa ni hatari kwake kama Yusto atagundua.
Caren anatiwa upofu na mapenzi.

Wakati akiwa bado kwenye dimbwi la mawazo mara simu yake iliita na haraka Caren akaipokea, ilikuwa ni namba ya rafiki yake ambae pia ni agent wanaefanya kazi moja ya kuangusha biashara za bosi Mark moon.
Wakati Caren akiipokea simu, Simigo na Brandina nao tayari walinasa mawasiliano haraka wakavaa headphone kubwa masikioni wakakaa wa kutulia ili kufuatilia mawasiliano hayo kati ya Caren na namba iliyompigia
"Hallo best"
"Yes Caren habari"
"Ni nzuri kiasi ndugu yangu vipi huko"
"Huku kwema, vipi kuna tatizo"
"Ndiyo rafiki angu, mwenzako nimenasa huku"
"Umenasa kivipi, au umeharibu kazi"
"Aah hapana ila nimejikuta tu nampenda mtoto wa mtu huku, nimeshindwa kabisa kujizuia rafiki yangu, nimeshindwa"
"Wee Caren wewe, huoni kama ni hatari"
"Ntafanyaje sasa rafiki angu hebu nishauri nafanyajee." Alisema Caren huku akiangalia sms iliyoingia kwenye simu yake ilikuwa sms kutoka kwa Yusto akimtaarifu kuwa amefika yupo mlangoni.

"Best naomba nikupigie baadae" alisema Caren kisha akakata simu.

Alijiweka sawa kisha akasogea mlangoni akafungua.

"Wow, karibu Yusto" alisema Caren huku wakitazama na Yusto wakatabasamu, Yusto akaingia ndani.
*****
Jasusi Simigo na Brandina walimaliza kusikiliza mawasiliano kati ya Caren na rafiki yake.

"Vipi kuna kitu chochote umekipata" aliuliza Simigo huku akimtazama Brandina ambae alitikisa kichwa kuashiria hajapata chochote katika maongezi hayo.
"Hapana kipo Brandina hebu fikiria, kwanza kauliza kama Caren kaharibu kazi kazi gani hiyo, lakini pili kwa nini huyu mwanamke kasema ni hatari kitendo cha Caren kupenda, kwanini iwe hatari" aliuliza Simigo huku akiendelea kumtazama Brandina usoni, lakini Brandina alionekana yuko mbali kimawazo huku akiwa amekodolea macho kwenye compyuta.
Simigo alishangazwa na hali hiyo akageuka kutazama ni nini alichokuwa akikiangalia Brandina.
Aliona ule ujumbe wa Yusto alioutuma kwa Caren mda mfupi uliopita.

"""Nimefika Caren niko hapa nje mlangoni kwako"""

Simigo aliusoma ujumbe huo kisha akageuka na kumtazama Brandina kwa sekunde kadhaa.
Ilionyesha wazi ujumbe huo haukuwa umemfurahisha Brandina hata kidogo. Kitendo cha Yusto kwenda chumbani kwa Caren, kilimuumiza.

"Brandina"
Kimyaa...
"BRANDINAAA....."

"Eeh..aah umesemaje" Brandina alikurupuka kwenye dimbwi la mawazo baada ya Simigo kumuita mara ya pili kwa nguvu.

",Hivi unashida gani siku hizi, unawivu, Yusto kwenda kwa Caren imekuumiza, haya umeshajua kama hawa wawili ni wapenzi potezea sasa fanya kazi uzembe uzembe sitaki" alifoka Simigo.
Brandina alimtazama Simigo kwa macho fulani ya kebehi.
"Aliyekwambia nimempenda Yusto nani"
"Hebu acha kujishau bana hata mtoto mdogo anaweza kujua kama umempenda"
"Achana na Mimi, nambie nini kinafuata, tukamkamate Caren au" aliuliza Brandina huku akijaribu kupotezea mada.
***

John maarufu kama Master Joo kijana aliyekuwa anatikisa chuo kizima akionena kuwa na pesa kuliko wengine wote anajikuta kwenye mtihani mzito baada ya kushindwa kulipata penzi la binti mrembo Caren.
Mwanzo alifikiri mambo yatakuwa ni rahisi kwani hakuna alichokitaka akakikosa kutokana na jinsi alivyokuwa akiishi na kuogopeka chuoni pale lakini anakutana na Caren mwanamke mwenye misimamo yake, anakataa wazi wazi huku kikwazo kikubwa akiwa ni Yusto.

Pamoja na kumtishia Yusto mara kadhaa akiamini labda Yusto ataachana na Caren kwa kumuogopa lakini Yusto hayuko tayari kufanya hivyo.

Mwisho Jonh akiwa na chuki nzito dhidi ya Caren anaamua kuingia rasmi katika jukumu la kutaka kumuadabisha kijana huyo ambae amekuwa mwiba mchungu kwake.
***
John alionekana akiwa anaendesha pikipiki moja ya kisasa. Alikatiza mitaa kadhaa na mwisho alifika kwenye jengo moja kubwa nje kidogo na jiji la Dar es salaam. Alifika na kusimama nje ya geti baada ya walinzi waliokuwa wamevalia suti nyeusi kumzuia asiingie.

John alivua helmet yake kichwani, hapo wale walinzi waliinamisha vichwa vyao chini ikiwa ni kumpa Jonh heshima aliyostahili.

John alishuka kwenye pikipiki yake, kwa dharau akamrushia helmet mmoja wa wale walinzi pale nje kisha akaanza kupiga hatua kuingia ndani ya jengo hilo kubwa la kisasa.

Ilionekana ni jengo lililokuwa kama kiwanda cha kutengeneza bidhaa fulani, kulikuwa watu wengi mle ndani na kila mmoja alionekana kuwa bize na kazi yake.
Kila alipopita kijana John watu waliinamisha vichwa chini kama ishara ya kumuheshimu.
Jonh alitembea mwendo wa dharau majigambo na kujiamini bila kujali alikutana na nani mzee au kijana.

Kwa ufupi John alikuwa ni mtoto wa pekee wa mama mmoja tajiri, maarufu kama Madam Jane ambae alitajwa kuwa mmoja wa wanaweke matajiri afrika.
Madam Jane, alibahatika kuwa na mtoto mmoja ambae ni Jonh na hili jengo lilikuwa ni moja ya kati ya viwanda vyake vya kibiashara.
***
Jonh alitembea na mwisho aliingia ndani ya chumba kimoja kikubwa ndani akawakuwa watu wengi kila mmoja akiwa bize na kompyuta yake.
Chumba kilikuwa na mitambo mingi na screen kibao zikizokuwa ukutani kuzunguuka chumba hicho.

Jonh alipiga hatua mwisho akasimama mbele ya mtu mmoja aliyekuwa bize na compyuta yake.

"Aah master Joo siku nyingi, naona leo umekuja kututembelea" alisema yule bwana huku akijitahidi kumchangamkia Jonh.

John aliingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake akatoa picha moja na kuiweka meza, ilikuwa ni picha ya Yusto.

"Nataka kujua kila kitu kumuhusu huyu mtu, ni nani kutoka wapi, maisha yake ya nyuma na sasa kila kitu nataka kujua" alisema John.
Hii ndio njia pekee aliyoona bora kuitumia ili kukabiliana na Yusto,

"Ukitaka kumpigia vizuri adui yako tafuta udhaifu wake" aliwaza John huku akitabasamu.

Je, nini kinafuata...
Vipi kuhusu Caren na Yusto?
Brandina na Simigo?
Sophia na Frank?

ENDELEA KUFUATILIA MKASA HUU.



Jipatie simulizi hii mwanzo hadi mwisho kwa Tsh 1500 tu. USIACHE pia kufuatilia simulizi yangu mpya THE MODERN WAR(Vita ya kisasa).

0756862047
 
Safi mkuu, usisite kuweka uhondo huu bampa tu bampa
 
Mkiamua kuleta story leteni full kama ni biashara wekeni heading sema unauza
 
DO NOT SHOUT
(usipige kelele)
Sehemu ya............. .21

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Email: saulstewarty@gmail.com.

ILIPOISHIA...

Wakati majasusi wakiendelea na harakati za kuifuatilia simu ya Caren baada ya kuduliwa, upande wa pili John anaanza kutafuta namna ya kukabiliana na Yusto ambae amemuharibia sifa chuoni baada ya kukataa kuachana na mwanamke anaemuhitaji.

SASA ENDELEA....
Nataka kujua kila kitu kumuhusu huyu mtu, ni nani kutoka wapi, maisha yake ya nyuma na sasa kila kitu nataka kujua" alisema John.
Hii ndio njia pekee aliyoona bora kuitumia ili kukabiliana na Yusto,

"Ukitaka kumpigia vizuri adui yako tafuta udahifu wake" aliwaza John kisha akatabasamu.

"Mkuu kuna shida kidogo hapa" alisema yule bwana aliyopewa kazi na John.
"Ipi"
"Tunashindwa kuzipata taarifa za nyuma kumuhu Yusto, zilizopo ni kuanzia siku alipojiunga na chuo cha Mark moon, taarifa za nyuma zote hakuna kitu, ni kama zilishafutwa" alieleza yule bwana

"Unaongea nini wewe, kwa nini usizipate yeye ni nani hadi taarifa zake zisiwepo"
"Aah..bosi kama nilivyokwambia zimefutwa"
"Kwa nini zifutweee!??" John alifoke huku akipiga ngumu mezani kwa hasira, watu wote waliokuwemo mle ndani waligeuka kuwangalia.
"Hu..huenda akawa sio mtu wa kawaida bosi, kufuta taarifa za mtu hufanywa kwa malengo maalum na sio rahisi, huenda kukawa na mtu mkubwa nyuma ya Yusto" aliongea yule bwana kauli ambayo ilikuwa na ukweli ndani yake.
Yusto na Frank baada ya kuajiliwa na tajiri mark moon walifutiwa kila kitu kuwahusu na maisha yao yakaanza upya hii ikiwa kama njia ya kujilinda dhidi ya maadui.

Ilikuwa ngumu kumuingia John akilini kwani aliamini Yusto ni mtu wa kawaida saana.

"Kwa hiyo unataka kusema Yusto ni nani"
" Bosi inawezeka...." Alisema yule bwana lakini kabla hajamalizia sentensi yake akaja mfanyakazi mwingine na kuomba kuzungumza na Yusto.

"Aah bosi usijali kama picha yake ipo, tunaweza kufuatilia maisha yake ya nyuma kwa hiyo hiyo picha japo itachukua muda kama masaa 12 hivi baada ya hapo tutakupa taarifa" alisema yule mtu kwa unyenyekevu mkubwa.

" Ahahaha.. wewe ndo unaakili haya fanya hivo, narudi chuoni utanitumia kila kitu kwenye emali yangu"
Alisema John huku alitabasamu.
****

Yusto akiwa chumbani kwa Caren walikuwa wamekaa juu kitandani wakizungumza, wakati huo bado Caren alionekana mnyonge kutokana na matukio aliyopitia siku hiyo yakamfanya kuwa hivyo.

"Caren" Yusto aliita huku akimshika Caren mikono.
"Abeeh"
" Am sorry kama nitakuwa sababu ya kuharibu siku yako leo, nimesikia umegombana na Sophia, aah ukweli Sophia ni...." Kabla hajamalizia sentensi yake Caren aliweka kidole chake mdomoni akimtaka anyamaze.

"Najua Yusto najua nini kinaendelea kati yenu wala usijali" alisema Caren akatulia kwa muda kisha akaendelea kuzungumza
"Yusto"
"Naam"
"Do you love me"
"Yes I do, nakupenda sana Caren zaidi ya vile unavyojua wewe"
"Kweli''
"Yes sina ukweli mwingine zaidi ya huo Caren, nakupenda"
"Then, unajua nini maana ya mapenzi"
"Mmmh"
"Yes, what is love"
"Okay baby nitakujibu
love is caring for each, love is sacrifice"
"Kwa hiyo unamaanisha unaweza kujitoa katika kila hali kwa ajili yangu Yusto"
"Haijarishi nini kitatokea kati yetu Caren I'll STAY WITH YOU, nitabaki na wewe kwa sababu nakupenda"
"Yusto"
"Yes Caren"
"Unaniamini kwa kiasi gani"

Swali hilo lilimfanya Yusto abaki kimya kwa sekunde kadhaa.
"Nakuuliza Yusto, unaniamini"
"Aah Caren"
"Mmm, nambie"
"Ukweli sitaki kujua wewe ni nani unafanya nini kwa nini nachojua na kukiamini kwako ni kwamba unanipenda hilo tu linanitosha,naamini katika upendo huo hutofanya jambo lolote baya likaniumiza Caren, hata bila kupepesa macho, hata ikitokea nikaamshwa usingizi ghafula nitajibu hivi hivi kuwa Caren wangu ananipenda sana"
Yusto aliongea kwa kumaanisha, kauli iliyomfanya Caren amatazame kwa macho ambayo kwa mbali yalionekana kulengwa na machozi.
Alichokisema Yusto ndicho alichotamani kukisikia.

" I love you Yusto" alisema Caren huku safari hii akishindwa kujizuia chozi likamtoka.
Yusto aliitambua hali aliyokuwa nayo Caren, alisogea na kumkumbatia kisha akambusu shingoni na baadae mdomoni.
Hapo wakaanza kupeana mabusu moto moto na haukupita muda wakajitupa kitandani wakaanza kufurahia tunda la penzi lao kwa mara ya kwanza.....
****
Sophia akiwa chumbani kwake aliendelea kuwaza ni jinsi gani ataweza kummiliki Yusto ambae siku zote amekuwa alimchukulia kama rafiki. Alijikuta akiwaza kuhusu Caren mwanamke aliyekuja ghafula na kumnyang'anya tonge mdomoni. Akajikuta anamchukia sana Caren.

"Nutakuuwa kwa mikono yangu wewe mwanamke" alisema Sophia huku akikucha ngumi yake kwa hasira.
****
Frank rafiki kipenzi wa Yusto alikuwa chumbani kwake huku akipata kinywaji taratibu, taswira ya mwanamke mrembo Brandina haikuwa imefutika kichwani kwake.
Hakina alikuwa amempenda mno jasusi Brandina.
"Nitakupata kwa gharama yoyote ile" alisema Frank huku akitabasamu.
****
Tayari John alikuwa amerejea chuoni, akiwa chumbani kwake alikuwa akipitia pitia account ya Instagram ya Caren akawa anatazama picha za mrembo huyo ambae aliumbika mashallah, zikazidi kumchanganya John akajikuta anazidisha chuki na Yusto.
Alikuwa anaisubiri report yake kwa hamu ili ajue ni wapi atamkamatia.
"Nitakupata tu Caren iwe kwa jasho iwe kwa damu lazima nikupate"
Alisema John.
****

Brandina na Simigo bado walikuwa kwenye kile chumba chao cha Siri wakisubiri ni nini kitaendelea kwenye simu ya Caren ili kujiridhisha na kile walichokuwa wakikihisi kuwa Caren ni Agent wa siri.
Lakini hali ilikuwa si hali kwa Brandina ambae alijikuta moyo wake ukizidi kuuma kila alipowaza kuwa Yusto yupo chumbani na Caren. Alijiuta anashindwa kabisa kutulia.

"Yusto, Yusto kwa nini niteseke hivi kwa ajili yako, kwanza upo na jambazi na unashindwa kugundua nitamuuwa huyo mwanamke" aliwaza Brandina huku akiuma meno yake kwa hasira.
***

Saa moja baadae Yusto na Caren walionekana wakiwa hoi kitandani,kila mmoja alikuwa amechoka, mwili ukiwa jasho kiasi.
Wakiwa watupu kama walivyozaliwa walijifunika shuka jepesi wakawa wanatazamana huku kila mmoja akitabasamu.

"Thank you baby, nime-enjoy sana" alisema Caren.
"Thank you too Caren, hata sikudhani kama utanipelekesha hivi" alisema Yusto na wote wakacheka kwa sauti.
Huo ndio ulikuwa ukweli, Yusto na Caren walionekana kupenda sana sana.

Lakini hatari kubwa iko katikati ya penzi lao, ni kweli Yusto na Caren watasimama pamoja kama walivyo ahidiana
Naam hii ni Do not shout-21....

ITAENDELEA 22....



ILI KUPATA SIMULIZI HII KATIKA UKAMILIFU WAKE(1-80)
NITAFUTE KWA NAMBA HII..
0756862047
 
Usijali tunaendelea lakini jitahidi upate yote kwa haraka bei ni rahisi sana 1500,,,, story bado ni ndefu, mwisho ep 80.

0756862047
Ukiwa mtunzi jitahidi uwe wakala wa huduma ya pesa wa mitandao ya simu.Tuwe tunatuma pesa Moja kwa Moja kwenye namba ya wakala.Haya matozo ndio yanayotufanya tusitume pesa🤔
 
Ukiwa mtunzi jitahidi uwe wakala wa huduma ya pesa wa mitandao ya simu.Tuwe tunatuma pesa Moja kwa Moja kwenye namba ya wakala.Haya matozo ndio yanayotufanya tusitume pesa[emoji848]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Huu ushauri sijui nicheke
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Huu ushauri sijui nicheke
Kwani nimeaongopa?Nilituma pesa Kwa mke wangu,Toka CRDB simbanking Kwenda mpesa,ya kununua gas mtungi mdogo elfu 22,nimekuta nimekatwa jumla elfu 8.Yaani wanakata kotekote.Nikamshauri mke wangu Bora afungue account CRDB Ili niwe natuma Hapo.Na mtunzi awe na account za bank tuwe tunaingiza huko.Huko hakuna makato ya kutuma🤔
 
Kwani nimeaongopa?Nilituma pesa Kwa mke wangu,Toka CRDB simbanking Kwenda mpesa,ya kununua gas mtungi mdogo elfu 22,nimekuta nimekatwa jumla elfu 8.Yaani wanakata kotekote.Nikamshauri mke wangu Bora afungue account CRDB Ili niwe natuma Hapo.Na mtunzi awe na account za bank tuwe tunaingiza huko.Huko hakuna makato ya kutuma[emoji848]
Saf sana
 
DO NOT SHOUT
(Usipige kelele)
Sehemu ya................22

Mtunzi: Saul David
Tel: +255756862047
Email: saulstewarty@gmail.com

ILIPOISHIA...
.

"Thank you baby, nime-enjoy sana" alisema Caren.
"Thank you too Caren, hata sikudhani kama utanipelekesha hivi" alisema Yusto na wote wakacheka kwa sauti.
Huo ndio ulikuwa ukweli, Yusto na Caren walionekana kupenda sana sana.
Lakini hatari kubwa iko katikati ya penzi lao, ni kweli Yusto na Caren watasimama pamoja kama walivyo ahidiana
Naam hii ilikuwa Do not shout-21...


SASA ENDELEA....
Hakika kila mmoja alionyesha kulidhika na penzi la mwenzake, furaha iliyokuwa mioyoni mwa wawili hao haikuwa na mfano. Hakuna aliyewaza kazi tena, hakuna aliyekumbuka jukumu alilonalo chuoni hapo mapenzi yalichukua nafasi kubwa mioyoni mwao, si Caren wala si Yusto kila mmoja alikuwa tayari kufanya chochote kwa ajili ya kupigania penzi la mwenzake .

"Nikaoge sasa mpenzi" alisema Caren.
" Nikaoge au tukaoge? mbona unajipenda hivyo, hujaona ulivyonichosha"
"Aah nenda chumbani kwako bana, unataka kuhamia humu au"
"Sawa tu muhimu niko na wewe Caren wangu"
"Aah sitaki kufukuzwa chuo mie ndo kwanza nimehamia"
"Kwa hiyo unanifukuza"
"Akuu, mimi sijakufukuza..."

Wakati wakiwa katika mazungumzo hayo yenye mahaba mazito ndani yake mara kuna meseji iliingia kwenye simu ya Caren, haraka akachukua simu yake na kusoma ujumbe aliotumiwa.

KABLA HUJAFANYA CHOCHOTE LEO USIKU NAOMBA WOTE TUKUTANE ARENA HOTEL SAA 3 USIKU, NINA MAONGEZI MUHIMU NA NINYI WOTE, KUWA MAKINI.

Ulikuwa ni ujumbe wa maandishi uliobadili tena mudi ya Caren kwa mara nyingine, tabasamu alilokuwa nalo likafifia tena ghafula.
Taratibu aliinua uso wake na kutazama saa ukutani ilikuwa ni saa moja kasoro jioni.

"Vipi Caren kuna usalama?"
"Ye..yes niko poa Yusto" Caren alijibu kwa kigugumizi kiasi.
****

Simigo na Brandina wakiwa ndani ya jiko la chuo kwenye chumba chao cha siri, walishitushwa na meseji ambayo ilikuwa imeingia sekunde chache zilizopita kwenye simu ya Caren waliyoidukuwa.

KABLA HUJAFANYA CHOCHOTE LEO USIKU NAOMBA WOTE TUKUTANE ARENA HOTEL SAA 3 USIKU, NINA MAONGEZI MUHIMU NA NINYI WOTE, KUWA MAKINI.

Waliusoma ujumbe huo mara mbili mbili huku taa nyekundu ikiwaka kwenye akili zao.

"Hatujakosea Simigo, Caren ndio muhusika wa yote haya hapa chuoni, huyu mwanamke kumbe ni hatari tofauti na muonekano wake" alisema Brandina.

"Ni kweli ni yeye lakini hii meseji haitoshi kuthibitisha hilo Brandina" alisema Simigo

"Simigo nini ambacho hujaelewa hapa mpaka sasa, hii meseji inaonyesha wazi kuwa Caren anamambo yake ya siri, tena kuna kazi alitakiwa kuifanya leo kazuiliwa mpaka wakutane na huyu aliyemtumia hii sms"

"Ni kweli Brandina uko sahihi, hiyo ndiyo hali halisi lakini maana yangu ni kwamba kwa hii meseji moja haitoshi kuthibitisha hayo yote uliyoyasema"
"Kwa hiyo tunafanyaje"
"Sikia, inavyoonekana Caren hayuko peke yake kwa ujumbe huu inaonyesha kuna timu zaidi ya watu wawili ambao wote lengo lao ni moja kuangusha biashara za mark moon, kama tukiwakamata wote tutakuwa tumemsaidia sana bosi Moon, chuo chake na biashara zake nyingine zitakuwa salama, ni wazi hii ni vita ya kiuchumi, CAREN NI AGENT WA SIRI" alisema Simigo, akili yake ikifanya kazi upesi sana kwa kunganisha matukio mpaka dakika hiyo alielewa kila kitu.

"Brandina"
"Yap"
"Wasiliana na mpili kule nje mwambie kila kitu kuhusu hili, awahi hoteli ya ARENA akaandae mazingira, wapigie simu Yusto na Frank waje hapa mara moja, mimi na wasiliana na bosi atuongeze watu wa kutusaidia leo ni lazima tuwakamate Caren na wenzake wote" alisema jasusi Simigo, akanyoosha mkono akachukua simu ya mezani akabonyeza vitufe kadhaa na kuiweka sikioni, Brandina nae hakutaka kupoteza muda akafanya kama vile alivyoelekezwa.
****

Dakika 11 baadae tayari Yusto na Frank walikuwa kwenye kile chumba cha siri cha majasusi. Wote walikuwa na shauku ya kujua ni nini kinaendelea, kwa nini wameitwa kwa dharula.

Frank alimtazama Brandina wakatazama lakini Frank akakwepesha macho, ni kweli alikuwa anampenda Brandina lakini kuongea ulikuwa ni mtihani mwingine.
Brandina alijikuta anatabasamu kisha akamuangalia Yusto kwa macho makali kuanzia juu hadi chini.

"Kaoge uko" alisema Brandina kauli iliyowafanya Yusto na Frank watazamane.
Brandina alikuwa na hasira dhidi ya Yusto alijua wazi kuwa Yusto alikuwa chumbani kwa Caren muda si mrefu.

"Aah hebu tukae kwanza" alisema Simigo na bila kuchelewa akaanza kuwasimulia kwanzia mwanzo namna walivyofanikiwa kudukuwa mawasiliano ya simu ya Caren, akawasimulia pia ujumbe uliotumwa hivi karibuni ambao ndio iliyokuwa sababu hasa ya wao kuitwa.
Sasa hatua iliyokuwa inafuata ni wao kwenda kuwakamata Caren na wenzake.

"Iko hivyo, Yusto tunaamini kuwa huenda wewe ukawa na mahusiano ya kimapenzi na Caren hilo halipingiki wala hatuna haja ya kujadili, hatuna imani kama ulikuwa unampeleleza au kweli mnapendana ila nimekwambia hivi ili ujione ni kwa kiasi gani umekuwa mzembe wa kushindwa kugundua hili mapema kuhusu Caren, sasa tunakwenda kufanya kazi naamini hautatuangusha kwa namna yoyote ile, nilitamani nikutoe kwenye hii misheni lakini nimeona nikupe nafasi nyingine ila usisahau macho yangu yote mawili yatakuwa yakikutazama" alisema Simigo.

Kimya kilitawala kwa muda kisha Yusto akaongea.
"Ni kweli nakili kuna uzembe kiasi nimefanya, lakini nataka kuuliza hii meseji pekee ndiyo inatosha kuonyesha kuwa Caren ndiye agent aliyetumwa hapa chuoni"

"Yes kwa asilimia 85 ni Caren, ukiisoma hii meseji kwa makini usijali imebeba vitu vingi sana mtu wa kawaida hawezi kuandikiwa sms kama hiyo" alisema Brandina

" tutajua kila kitu huko tayari tumeshamtuma mpili ametangulia ARENA hoteli, atatega vinasa sauti kwenye eneo watakalo kutana. Kabla ya kuwakamata tutasikiliza kwanza maongezi yao na huo ndio utakuwa ushahidi wetu wa mwisho" aliongezea Jasusi Simigo, akatulia kwa muda kisha akaendelea

"Yusto na Frank niliambiwa kuwa mlipewa siraha na kila mtu anajua namna ya kutumia, hii kazi inaweza kuwa ngumu lolote linaweza kutokea tuwe makini"

"Aah tuko vizuri usijali" alisema Frank
"Sawa basi tuanze kujiandaa kwenda ARENA wakati nasubiri vijana wengine kutoka kwa bosi"
"Sawa"..
*****

Sasa ilikuwa ni saa mbili na dakika 15, zikiwa zimesalia dakika 45 pekee ufike muda uliopangwa kukutana ARENA hotel.
Caren alikuwa chumbani kwake akimalizia kujiandaa, alivaa track suti nyeusi iliyouchora mwili wake vizuri, koti refu jeusi, miwani,kofia na gloves nyeusi pia.
Alipiga hatua akasimama mbele ya kioo akajitazama kisha akaachia tabasamu.

ITAENDELEAA...
Je, nini kinakwenda kutokea ARENA HOTEL?
Yusto ataweza vipi kukabiliana na Caren?
Vipi kuhusu John anaefuatilia taarifa za Yusto?...


USIACHE KUFUATILIA SIMULIZI YANGU MPYA INAYOITWA 'THE MODERN WAR" (vita ya kisasa)

Whatsapp=> 0756862047
 
Back
Top Bottom