SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #41
DO NOT SHOUT
(usipige kelele)
Sehemu ya........13
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
baada ya Yusto na Caren kufanikiwa kumuokoa mtoto albino asiuwawe na majambazi,wanaludi chuoni huku kila mmoja akiwaza na kumuhisi mwenzie kuwa huenda akawa siyo mtu wa kawaida kutokana na namna walivyokabiliana na majambazi wale wakiwa wawili tu.
Asubuhi ya siku iliyofuata wakiwa chuoni wanafunzi wachuo hicho wanaandamana baada ya kuchoshwa na mfululizo wa matukio ambayo hawaelewi nini chanzo chake...
SASA ENDELEA
Hali ilionekana si shwari, wanafunzi wa chuo hicho walikuwa wamechafukwa haswaa.
Ada waliokuwa wakitoa chuoni hapo nikubwa mno ilikuwa ni aibu kwa chuo kikubwa kama icho kupitia matukio ya ajabu kiasi kile. Mara waharishe chuo kizima,mara moto uwake, mara maji yakate,mara shoti za umeme hii ilikuwa kero kubwa kwa watoto hao wa kishua
Yusto na frank wakiwa kama walinzi wa siri wa chuo hicho walijikuta kwenye sintofahamu nzito wasielewe nini cha kufanya.
⭐⭐⭐
Ndani ya chumba kimoja kikubwa cha mkutano wanaume sita wakiwa wamevalia suti nadhifu zenye rangi nyeusi walionekana wamekaa wakijadili swala nyeti mno. Naam, hao ndio walikuwa viongozi wa juu kabisa wa chuo hicho kilichokuwa kikikumbwa na mfurulizo wa matukio yaliyoibua sintofahamu.
"Kwani Frank na Yusto wanafanya kazi gani?" alihoji mmoja wa wale watu
"Mimi pia nashangaa niwazi wameshindwa kufanya hii kazi labda tufikirie njia nyingine"
"Njia gani nyingine mzee"
"Hapana tatizo siyo Yusto wala Frank tatizo ni mtu anaeshambulia biashara za bosi Mark moon anaonekana kutumia akili kubwa sana"
"Kwaiyo tufanyaje na wanafunzi wameshaandamana bosi akipata taarifa sisi sote tutaonekana niwazembe"
Majadiliano yalionekana kuwa nimazito mno kama viongozi, yaliyokuwa yakiendelea chuoni pale yaliwafanya kuchanganyikiwa
"Jamani mimi nina wazo moja " alisema mmoja wa watu hao wote wakageuka na kumtazama wakiwa na shauku ya kumsikia anataka kusema nini.
lakini kabla hajasema chochote mara mlango wa chumba icho ulitoa kishindo baada ya kufunguliwa kwa nguvu wote walishituka na kugeuka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia.
Hakuwa mwingine bali bosi Mark moon tajiri na mmiliki wa chuo cha MARK MOON PSP INTERNATIONAL UNIVERSITY aliingia akiwa ameongozana na watu watatu nyuma yake .wote walio kuwamo ndani ya chumba kile walisimama kuonyesha heshima kwa bosi Mark moon hali nyuso zao zikionyesha wasi wasi mkubwa walio kuwa nao.
Mark moon hakuwa mtu wa masihara kabisa kazi zake alizifanya kwa umakini wa hali ya juu.
Akiwa Sudan kusini, alipata taarifa ya mambo yanayoendelea chuoni kwake alighairisha safari yake ya kwenda Canada akalazimika kurudi tanzania.
Mark Moon alipitiliza na kusimama mbele ya watu wake ambao bado walionekana kuogopa, wala hakutaka kuketi akaanza kuzungumza.
"Huyu anaitwa Simigo, huyu anaitwa Mpili,na huyu anaitwa Brandina hawa wote ni majasusi nimetoka nao kenya watatusaidia katika hili tatizo linalotokea chuoni, waiteni hapa Yusto na Frank waje mara moja na ripoti kamili walipoanzia mpaka walipofikia" alisema Mark moon na punde simu ilipigwa kuwaita Yusto na Frank walio kuwa chuoni.
Wakati wakisubiri mark moon na wale majasusi watatu walianza kujadili baadhi ya vitu ikiwa ni pamoja na kupitia ramani ya chuo,
majasusi hao walionekana kuwa makini isivyo kawaida.
Punde mlango ulifunguliwa Yusto na frank waliingia huku kila mmoja akiwa na file mkononi waliinamisha vichwa vya chini kwa heshima na kuanza kusogea mbele.
Yusto alikuwa akiwatazama watu walio kuwemo kwenye chumba kile kichwani akiwa na maswali yasiyo na majibu. Wala hakuwaza tena kuhusu Caren. Kwa sasa alijali kibalua chake kuliko kingine chochote.
Macho yake yakatua kwenye uso wa Brandina. Brandina nae akamtazama, wakawa wanatazamana kwa macho yanayozungumza.
Brandina nae alikuwa si haba bali ni mrembo haswa, kwa haraka haraka ukimuona usingefikiri anafanya kazi ile ngumu na hatari ya ujasusi. Walitazamana kwa zaidi ya sekunde 30 kiasi cha kumfanya Mark moon awatazame.
ITAENDELEA.....
Vipi kuhusu John na Sophia?
Caren kaletewa majasusi, ataweza kweli kuifanya kazi yake?
Sasa tuna Sophia, Caren na Brandina!!
SIMULIZI HII INAPATIKATA YOTE,,, WASILIANA NAMI KUPITIA NAMBA HII (call/WhatsApp)
0756862047
(usipige kelele)
Sehemu ya........13
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
baada ya Yusto na Caren kufanikiwa kumuokoa mtoto albino asiuwawe na majambazi,wanaludi chuoni huku kila mmoja akiwaza na kumuhisi mwenzie kuwa huenda akawa siyo mtu wa kawaida kutokana na namna walivyokabiliana na majambazi wale wakiwa wawili tu.
Asubuhi ya siku iliyofuata wakiwa chuoni wanafunzi wachuo hicho wanaandamana baada ya kuchoshwa na mfululizo wa matukio ambayo hawaelewi nini chanzo chake...
SASA ENDELEA
Hali ilionekana si shwari, wanafunzi wa chuo hicho walikuwa wamechafukwa haswaa.
Ada waliokuwa wakitoa chuoni hapo nikubwa mno ilikuwa ni aibu kwa chuo kikubwa kama icho kupitia matukio ya ajabu kiasi kile. Mara waharishe chuo kizima,mara moto uwake, mara maji yakate,mara shoti za umeme hii ilikuwa kero kubwa kwa watoto hao wa kishua
Yusto na frank wakiwa kama walinzi wa siri wa chuo hicho walijikuta kwenye sintofahamu nzito wasielewe nini cha kufanya.
⭐⭐⭐
Ndani ya chumba kimoja kikubwa cha mkutano wanaume sita wakiwa wamevalia suti nadhifu zenye rangi nyeusi walionekana wamekaa wakijadili swala nyeti mno. Naam, hao ndio walikuwa viongozi wa juu kabisa wa chuo hicho kilichokuwa kikikumbwa na mfurulizo wa matukio yaliyoibua sintofahamu.
"Kwani Frank na Yusto wanafanya kazi gani?" alihoji mmoja wa wale watu
"Mimi pia nashangaa niwazi wameshindwa kufanya hii kazi labda tufikirie njia nyingine"
"Njia gani nyingine mzee"
"Hapana tatizo siyo Yusto wala Frank tatizo ni mtu anaeshambulia biashara za bosi Mark moon anaonekana kutumia akili kubwa sana"
"Kwaiyo tufanyaje na wanafunzi wameshaandamana bosi akipata taarifa sisi sote tutaonekana niwazembe"
Majadiliano yalionekana kuwa nimazito mno kama viongozi, yaliyokuwa yakiendelea chuoni pale yaliwafanya kuchanganyikiwa
"Jamani mimi nina wazo moja " alisema mmoja wa watu hao wote wakageuka na kumtazama wakiwa na shauku ya kumsikia anataka kusema nini.
lakini kabla hajasema chochote mara mlango wa chumba icho ulitoa kishindo baada ya kufunguliwa kwa nguvu wote walishituka na kugeuka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia.
Hakuwa mwingine bali bosi Mark moon tajiri na mmiliki wa chuo cha MARK MOON PSP INTERNATIONAL UNIVERSITY aliingia akiwa ameongozana na watu watatu nyuma yake .wote walio kuwamo ndani ya chumba kile walisimama kuonyesha heshima kwa bosi Mark moon hali nyuso zao zikionyesha wasi wasi mkubwa walio kuwa nao.
Mark moon hakuwa mtu wa masihara kabisa kazi zake alizifanya kwa umakini wa hali ya juu.
Akiwa Sudan kusini, alipata taarifa ya mambo yanayoendelea chuoni kwake alighairisha safari yake ya kwenda Canada akalazimika kurudi tanzania.
Mark Moon alipitiliza na kusimama mbele ya watu wake ambao bado walionekana kuogopa, wala hakutaka kuketi akaanza kuzungumza.
"Huyu anaitwa Simigo, huyu anaitwa Mpili,na huyu anaitwa Brandina hawa wote ni majasusi nimetoka nao kenya watatusaidia katika hili tatizo linalotokea chuoni, waiteni hapa Yusto na Frank waje mara moja na ripoti kamili walipoanzia mpaka walipofikia" alisema Mark moon na punde simu ilipigwa kuwaita Yusto na Frank walio kuwa chuoni.
Wakati wakisubiri mark moon na wale majasusi watatu walianza kujadili baadhi ya vitu ikiwa ni pamoja na kupitia ramani ya chuo,
majasusi hao walionekana kuwa makini isivyo kawaida.
Punde mlango ulifunguliwa Yusto na frank waliingia huku kila mmoja akiwa na file mkononi waliinamisha vichwa vya chini kwa heshima na kuanza kusogea mbele.
Yusto alikuwa akiwatazama watu walio kuwemo kwenye chumba kile kichwani akiwa na maswali yasiyo na majibu. Wala hakuwaza tena kuhusu Caren. Kwa sasa alijali kibalua chake kuliko kingine chochote.
Macho yake yakatua kwenye uso wa Brandina. Brandina nae akamtazama, wakawa wanatazamana kwa macho yanayozungumza.
Brandina nae alikuwa si haba bali ni mrembo haswa, kwa haraka haraka ukimuona usingefikiri anafanya kazi ile ngumu na hatari ya ujasusi. Walitazamana kwa zaidi ya sekunde 30 kiasi cha kumfanya Mark moon awatazame.
ITAENDELEA.....
Vipi kuhusu John na Sophia?
Caren kaletewa majasusi, ataweza kweli kuifanya kazi yake?
Sasa tuna Sophia, Caren na Brandina!!
SIMULIZI HII INAPATIKATA YOTE,,, WASILIANA NAMI KUPITIA NAMBA HII (call/WhatsApp)
0756862047