Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

DO NOT SHOUT

Sehemu ya..........29

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Email: saulstewarty@gmail.com

ILIPOISHIA....
Sophia anaanguka na kuzimia baada ya kushambuliwa na Caren. Anakimbizwa hospitali ya chuo upesi. Sasa Caren na Yusto wanasubiri majibu ya daktari bila kujua pia wakati huo Jasusi Brandina alikuwa akiwafuatilia kwa siri hatua kwa hatua.
Upande wa pili John anamteka mama kichaa ambae ni mama mlezi wa Yusto lakini cha ajabu mama huyo anaonekana kumfahamu John ambapo John nae pia anahisi kuwahi kumuona mama huyo lakini kumbukumbu zake haziko sawa.

Je nini kutafutaa?

SASA ENDELEEA...
Caren alibaini huenda Yusto akawa ameambiwa na Sophia tukio alilolifanya usiku wa Jana kuwapoteza kimtazamo majasusi baada ya kuigiza kama mke wa mtu na mama wa mtoto mmoja ili waache kumfuatilia.

"Ooh mungu wangu nitafanyaje Mimi" Caren aliongea huku hofu yake ya kumpoteza Yusto ikionekana dhahiri.

Wakiwa katika hali hiyo mara alifika daktari akitokea ICU chumba cha wagonjwa mahututi alipolazwa Sophia.

"Daktari daktari vipi hali ya Sophia,anaendeleaje, atapona?" Yusto aliuliza maswali mfurulizo hali akiwa na hofu.
"Ooh taratibu kijana usijali Sophia yuko salama, ajali aliyopata imemsababishia hitirafu kiasi kwenye kichwa chake amepata mtikisiko wa ubongo kitaalamu tunaita brain concussion, lakini kwa sasa yupo kwenye uangalizi maalum atapona tu japo itachukua muda kidogo, tuwe na subira tafadhali" alisema daktari Kisha akaondoka.

Yusto alibaki ameduwaa akitafakari maelezo ya daktari kwa muda Kisha akageuka na kumtazama Caren,
Caren alimtazama Yusto kwa macho ya huruma akihitaji msamaha.

Akiwa na hasira Yusto alimkamata Caren mkono akawa anamvuta huku akitembea kwa kasi hadi mbele ya mlango wa chumba alicholazwa Sophia.
Alipofika hapo akamuachia.

" Haya angalia, muangalie mwenzako, umefurahi Sasa nakuliza umefurahi" Yusto aliongea kwa ukali huku akinyooshea kidole kwa Sophia aliyekuwa amelala kitandani kimya akipumulia mtungi wa gesi.
"Yusto mpenzi nisi...."
"Kimya, nani mpenzi wako, huoni hata aibu, mwanamke tapeli wewe kwanini umekuja kwenye maisha yangu Caren kwani nini, umeniumiza mimi umeona haitoshi unataka kumuuwa hadi mtu anaeniheshimu na kujali hisia zangu mtu anaenipenda kwa dhati, Caren why why Caren mbona hata hufanani" Yusto aliongea kwa uchungu.

"Sio hivyo Yusto, sikukusudia kufanya yote hayo"

"Hukukusudia? unauhakika, una mume, una mtoto hujawahi kunieleza kwangu ulitaka nini sasa Caren, ulitaka nini nakuliza, nijibu" Yusto alifoka

Caren alibaki kimya huku akilengwa na machozi swali la Yusto lililokuwa na ugumu mno kulijibu, haikuwa rahisi kumweleza ukweli kwamba alikuwa anaigiza tu yeye sio mke wa mtu wala hana mtoto
kufanya hivyo ilikuwa ni sawa na kuharibu kazi yake, japo alimwamini Yusto lakini angeanzia wapi kumweleza.

"Kimya, maana yake huna jibu, huna cha kujitetea, ulifikiri sito jua eti Caren, haya nimejua sasa mtu anaenipenda ambae umetaka muuwa ndiyo aliyeniletea hizo taarifa na hawezi nidanganya. shukuru mungu nimedanganya kuwa ameanguka la sivyo ungekuwa polisi mda huu" Yusto alisema huku akikwepesha kuelezakuwa nae pia alikuwepo eneo la tukio na aliona na kusikia kila kitu.
Caren alitaka kusema neno lakini Yusto alinyanyua mkono wake juu ikiwa ni ishara kuwa hataki kusikia maelezo yoyote.

" Huna ulichobakiza caren, ondoka na upotee kwenye maisha yangu Jumla nisikuone tena, otherwise nitakuuwa" alisema Yusto akiwa ametoa macho akimaanisha kile alichokizungumza.

"Ondokaaa....."

Taratibu Caren alianza kupiga hatua kuondoka huku akiwa na huzuni ya hali ya juu. Alitembea hatua kadhaa akageuka kumtazama Yusto.

Yusto alikuwa akimtazama huku nae machozi yakimlenga, wawili hawa walikuwa wakipenda si kidogo.
****

Nusu saa baada ya Caren kuondoka Yusto alionekana akiwa amekaa pembeni ya kitanda alicholazwa Sophia, alikuwa akimtazama mwanamke ambae amekuwa nae kwa kipindi kirefu kama rafiki wakipita kwenye vipindi vyote vya shida na raha.

"Am real sorry Sophia"
Alisema Yusto akijiona kuwa yeye ndio mwenye hatia na chanzo cha yote.

Hapo alikumbuka simu yake, akaichukua na kuitazama,alikuwa amepigiwa simu mara kadhaa na Frank rafiki yake.

Alifungua pia upande wa WhatsApp na huku anakutana na video aliyotumiwa na John adui yake mkubwa,
video ikimuonyesha mama yake mlezi yule kichaa akikamatwa kwa nguvu na watu wasiojulikana Kisha kupelekwa kwenye gari.

"TUCHEZE KIMYA KIMYA BILA KELELE ZA POLISI UKIZINGUA HUTOMUONA MAMA YAKO KICHAA, ACHANA NA CAREN"
Maandishi haya kutoka kwa John yaliyojaa dharau na kejeli yalifuata chini ya video hiyo.

Yusto hakuamini anachokiona mkono wake ulikuwa ukimtetemeka akajikuta anashindwa kustahimili kuendelea kuishika simu yake ikadondoka chini sakafuni wala hakujali.
Ni kweli John alikuwa amemshika pabaya tena pabaya mno, Yusto alikuwa ni Moto wa kuotea mbali, alimpenda sana mama huyo pengine kuliko kitu kingine chochote.

Yusto alitoka mle ICU akiwa na ghadhabu kubwa akapiga hatua kuelekea chumbani kwake.
****

Baada ya Caren kufukuzwa na Yusto pale hospitali alijikuta anakosa nguvu za kutembea umbali mrefu akaenda na kukaa kwenye bustani moja ya maua ndani ya chuo hicho.
Machozi yalikuwa yakimtoka hakuamini kama amempoteza Yusto kirahisi namna ile moyo wake uliumia sana sana.

Ili kulinda kazi yake ilimbidi kufanya hivyo aliwaza kama ataharibu kazi basi atawapoteza mama na mdogo wake.
Caren alikuwa chini ya usimamamizi wa watu wa mama tajiri anaejulikana kama madam Jane, huyu mama ndiye aliyekuwa anammiliki Caren na wenzake na yeye ndiye aliyekuwa amewatuma kwenda kushambulia biashara za tajiri mwenzake Mark moon.
Naam hii ilikuwa ni vita ya matajiri wawili ambao wanawatumia vijana wa kazi kufanikisha malengo yao.

Caren hakuwa na budi kutii kile alichoagizwa ukizingatia watu hao walimpa msaada mkubwa kwa kuwatibu mama na mdogo wake waliokuwa karibu kufa.
kwa sababu hiyo Caren aliapa kutimiza kila jukumu atakalopewa ikiwa kama fadhila kwa Madam Jane na watu wake waliomchukua nchini Burundi akiwa binti mdogo kabisa.

"Lakini Yusto wangu nimuelewa hata nikimweleza Siri hii hawezi kuitoa kokote nina uhakika"
Mara wazo hili lilimjia Caren akawaza kuliko kumpoteza Yusto ni heri akamwambia ukweli kuwa yeye ni agent wa siri katumwa na bosi madam Jane ,pasipo kujua kuwa Yusto nae ni mlinzi wa siri wa bosi Mark moon.

Caren aliinuka pale alipokuwa ameketi akaanza kutembea haraka kurudi hospitali.
***

Alifika na kuingia moja kwa moja chumba alichokuwa amelazwa Sophia akiamini angemkuta Yusto lakini haikuwa hivyo Yusto hakuwepo badala yake aliona simu ya Yusto ikiwa chini sakafuni.

Taratibu Caren aliiokota ile simu akaitazama,
Kulikuwa na video iliyotumwa na John.
Caren akabinya 'play'
akaitazama video ile akaona kila kitu pamoja na yale maandishi ya vitisho pale chini kutoka kwa John.

"TUCHEZE KIMYA KIMYA BILA KELELE ZA POLISI UKIZINGUA HUTOMUONA MAMA YAKO KICHAA, ACHANA NA CAREN"

Caren alirudiarudia kuyasoma mandishi hayo mara mbili mbili, akawa haelewi lakini baadae akaelewa.

"Oh my God, John you you're going too far" (Oh Mungu wangu, John unafika mbali)
Alisema Caren, wakati huo pembeni yake Sophia alikuwa anafumbua macho taratibu, fahamu zikimrejea.

Je nini kitafuata?
ITAENDELEA....


BADO SAFARI YETU NI NDEFU NA SIMULIZI HII, NJOO WHATSAPP BEI PUNGUZO, TSH 1200 KUMALIZIA SIMULIZI HII HADI MWISHO ep80
 
DO NOT SHOUT

Sehemu ya..........29

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Email: saulstewarty@gmail.com

ILIPOISHIA....
Sophia anaanguka na kuzimia baada ya kushambuliwa na Caren. Anakimbizwa hospitali ya chuo upesi. Sasa Caren na Yusto wanasubiri majibu ya daktari bila kujua pia wakati huo Jasusi Brandina alikuwa akiwafuatilia kwa siri hatua kwa hatua.
Upande wa pili John anamteka mama kichaa ambae ni mama mlezi wa Yusto lakini cha ajabu mama huyo anaonekana kumfahamu John ambapo John nae pia anahisi kuwahi kumuona mama huyo lakini kumbukumbu zake haziko sawa.

Je nini kutafutaa?

SASA ENDELEEA...
Caren alibaini huenda Yusto akawa ameambiwa na Sophia tukio alilolifanya usiku wa Jana kuwapoteza kimtazamo majasusi baada ya kuigiza kama mke wa mtu na mama wa mtoto mmoja ili waache kumfuatilia.

"Ooh mungu wangu nitafanyaje Mimi" Caren aliongea huku hofu yake ya kumpoteza Yusto ikionekana dhahiri.

Wakiwa katika hali hiyo mara alifika daktari akitokea ICU chumba cha wagonjwa mahututi alipolazwa Sophia.

"Daktari daktari vipi hali ya Sophia,anaendeleaje, atapona?" Yusto aliuliza maswali mfurulizo hali akiwa na hofu.
"Ooh taratibu kijana usijali Sophia yuko salama, ajali aliyopata imemsababishia hitirafu kiasi kwenye kichwa chake amepata mtikisiko wa ubongo kitaalamu tunaita brain concussion, lakini kwa sasa yupo kwenye uangalizi maalum atapona tu japo itachukua muda kidogo, tuwe na subira tafadhali" alisema daktari Kisha akaondoka.

Yusto alibaki ameduwaa akitafakari maelezo ya daktari kwa muda Kisha akageuka na kumtazama Caren,
Caren alimtazama Yusto kwa macho ya huruma akihitaji msamaha.

Akiwa na hasira Yusto alimkamata Caren mkono akawa anamvuta huku akitembea kwa kasi hadi mbele ya mlango wa chumba alicholazwa Sophia.
Alipofika hapo akamuachia.

" Haya angalia, muangalie mwenzako, umefurahi Sasa nakuliza umefurahi" Yusto aliongea kwa ukali huku akinyooshea kidole kwa Sophia aliyekuwa amelala kitandani kimya akipumulia mtungi wa gesi.
"Yusto mpenzi nisi...."
"Kimya, nani mpenzi wako, huoni hata aibu, mwanamke tapeli wewe kwanini umekuja kwenye maisha yangu Caren kwani nini, umeniumiza mimi umeona haitoshi unataka kumuuwa hadi mtu anaeniheshimu na kujali hisia zangu mtu anaenipenda kwa dhati, Caren why why Caren mbona hata hufanani" Yusto aliongea kwa uchungu.

"Sio hivyo Yusto, sikukusudia kufanya yote hayo"

"Hukukusudia? unauhakika, una mume, una mtoto hujawahi kunieleza kwangu ulitaka nini sasa Caren, ulitaka nini nakuliza, nijibu" Yusto alifoka

Caren alibaki kimya huku akilengwa na machozi swali la Yusto lililokuwa na ugumu mno kulijibu, haikuwa rahisi kumweleza ukweli kwamba alikuwa anaigiza tu yeye sio mke wa mtu wala hana mtoto
kufanya hivyo ilikuwa ni sawa na kuharibu kazi yake, japo alimwamini Yusto lakini angeanzia wapi kumweleza.

"Kimya, maana yake huna jibu, huna cha kujitetea, ulifikiri sito jua eti Caren, haya nimejua sasa mtu anaenipenda ambae umetaka muuwa ndiyo aliyeniletea hizo taarifa na hawezi nidanganya. shukuru mungu nimedanganya kuwa ameanguka la sivyo ungekuwa polisi mda huu" Yusto alisema huku akikwepesha kuelezakuwa nae pia alikuwepo eneo la tukio na aliona na kusikia kila kitu.
Caren alitaka kusema neno lakini Yusto alinyanyua mkono wake juu ikiwa ni ishara kuwa hataki kusikia maelezo yoyote.

" Huna ulichobakiza caren, ondoka na upotee kwenye maisha yangu Jumla nisikuone tena, otherwise nitakuuwa" alisema Yusto akiwa ametoa macho akimaanisha kile alichokizungumza.

"Ondokaaa....."

Taratibu Caren alianza kupiga hatua kuondoka huku akiwa na huzuni ya hali ya juu. Alitembea hatua kadhaa akageuka kumtazama Yusto.

Yusto alikuwa akimtazama huku nae machozi yakimlenga, wawili hawa walikuwa wakipenda si kidogo.
****

Nusu saa baada ya Caren kuondoka Yusto alionekana akiwa amekaa pembeni ya kitanda alicholazwa Sophia, alikuwa akimtazama mwanamke ambae amekuwa nae kwa kipindi kirefu kama rafiki wakipita kwenye vipindi vyote vya shida na raha.

"Am real sorry Sophia"
Alisema Yusto akijiona kuwa yeye ndio mwenye hatia na chanzo cha yote.

Hapo alikumbuka simu yake, akaichukua na kuitazama,alikuwa amepigiwa simu mara kadhaa na Frank rafiki yake.

Alifungua pia upande wa WhatsApp na huku anakutana na video aliyotumiwa na John adui yake mkubwa,
video ikimuonyesha mama yake mlezi yule kichaa akikamatwa kwa nguvu na watu wasiojulikana Kisha kupelekwa kwenye gari.

"TUCHEZE KIMYA KIMYA BILA KELELE ZA POLISI UKIZINGUA HUTOMUONA MAMA YAKO KICHAA, ACHANA NA CAREN"
Maandishi haya kutoka kwa John yaliyojaa dharau na kejeli yalifuata chini ya video hiyo.

Yusto hakuamini anachokiona mkono wake ulikuwa ukimtetemeka akajikuta anashindwa kustahimili kuendelea kuishika simu yake ikadondoka chini sakafuni wala hakujali.
Ni kweli John alikuwa amemshika pabaya tena pabaya mno, Yusto alikuwa ni Moto wa kuotea mbali, alimpenda sana mama huyo pengine kuliko kitu kingine chochote.

Yusto alitoka mle ICU akiwa na ghadhabu kubwa akapiga hatua kuelekea chumbani kwake.
****

Baada ya Caren kufukuzwa na Yusto pale hospitali alijikuta anakosa nguvu za kutembea umbali mrefu akaenda na kukaa kwenye bustani moja ya maua ndani ya chuo hicho.
Machozi yalikuwa yakimtoka hakuamini kama amempoteza Yusto kirahisi namna ile moyo wake uliumia sana sana.

Ili kulinda kazi yake ilimbidi kufanya hivyo aliwaza kama ataharibu kazi basi atawapoteza mama na mdogo wake.
Caren alikuwa chini ya usimamamizi wa watu wa mama tajiri anaejulikana kama madam Jane, huyu mama ndiye aliyekuwa anammiliki Caren na wenzake na yeye ndiye aliyekuwa amewatuma kwenda kushambulia biashara za tajiri mwenzake Mark moon.
Naam hii ilikuwa ni vita ya matajiri wawili ambao wanawatumia vijana wa kazi kufanikisha malengo yao.

Caren hakuwa na budi kutii kile alichoagizwa ukizingatia watu hao walimpa msaada mkubwa kwa kuwatibu mama na mdogo wake waliokuwa karibu kufa.
kwa sababu hiyo Caren aliapa kutimiza kila jukumu atakalopewa ikiwa kama fadhila kwa Madam Jane na watu wake waliomchukua nchini Burundi akiwa binti mdogo kabisa.

"Lakini Yusto wangu nimuelewa hata nikimweleza Siri hii hawezi kuitoa kokote nina uhakika"
Mara wazo hili lilimjia Caren akawaza kuliko kumpoteza Yusto ni heri akamwambia ukweli kuwa yeye ni agent wa siri katumwa na bosi madam Jane ,pasipo kujua kuwa Yusto nae ni mlinzi wa siri wa bosi Mark moon.

Caren aliinuka pale alipokuwa ameketi akaanza kutembea haraka kurudi hospitali.
***

Alifika na kuingia moja kwa moja chumba alichokuwa amelazwa Sophia akiamini angemkuta Yusto lakini haikuwa hivyo Yusto hakuwepo badala yake aliona simu ya Yusto ikiwa chini sakafuni.

Taratibu Caren aliiokota ile simu akaitazama,
Kulikuwa na video iliyotumwa na John.
Caren akabinya 'play'
akaitazama video ile akaona kila kitu pamoja na yale maandishi ya vitisho pale chini kutoka kwa John.

"TUCHEZE KIMYA KIMYA BILA KELELE ZA POLISI UKIZINGUA HUTOMUONA MAMA YAKO KICHAA, ACHANA NA CAREN"

Caren alirudiarudia kuyasoma mandishi hayo mara mbili mbili, akawa haelewi lakini baadae akaelewa.

"Oh my God, John you you're going too far" (Oh Mungu wangu, John unafika mbali)
Alisema Caren, wakati huo pembeni yake Sophia alikuwa anafumbua macho taratibu, fahamu zikimrejea.

Je nini kitafuata?
ITAENDELEA....


BADO SAFARI YETU NI NDEFU NA SIMULIZI HII, NJOO WHATSAPP BEI PUNGUZO, TSH 1200 KUMALIZIA SIMULIZI HII HADI MWISHO ep80
Ipo poa ntakuja whatsap
 
Ngoja nije tu huko WhatsApp tmalizane huko huko
 
  • Thanks
Reactions: y-n
0756862047
761679127.jpg
 
DO NOT SHOUT
USIPIGE KELELE

Sehemu ya........ 30

ILIPOISHIA....
Yusto anaamua kukatisha safari ya mapenzi aliyokuwa ameianzisha na msichana mrembo Caren hii ni baada ya kubaini kuwa Caren ni mke wa mtu tena ni mama wa mtoto mmoja jambo ambalo ki uharisia lilikuwa si kweli.
Yusto anapata video kutoka kwa adui yake John akionyesha mama yake mlezi ambae ni mlemavu wa akili akitekwa. Yusto anachanganyikiwa na kuondoka ghafula.
Caren nae anawaza kwenda kumuweka wazi Yusto juu ya kazi anayoifanya lakini hakumkuta pale alipomuacha kwa bahati anaokota simu ya Yusto na kufanikiwa kuiona ile video ya vitisho kutoka kwa John.....


SASA ENDELEA...

"TUCHEZE KIMYA KIMYA BILA KELELE ZA POLISI UKIZINGUA HUTOMUONA MAMA YAKO KICHAA, ACHANA NA CAREN"

Caren alirudia tena kuusoma ujumbe huu kutoka kwa John.
Akili yake iliweza kufanya kazi upesi akajua kabisa lazima kuna shida kati ya Yusto na John na sababu ilikuwa ni yeye.
Tayari alishapata taarifa za John kuwa alikuwa ni kijana hatari sana anaetumia jeuri ya pesa kuwanyanyasa watu wengine. Kuna kipindi aliwahi hadi kuuwa lakini kesi yake ilipanguliwa kwa nguvu kubwa za pesa akarudi uraiani. Alikuwa ni aina ya mtu ambae hawezi kukubali kushindwa akikitaka kitu atahakikisha anakipata,
alikuwa radhi kufanya jambo lolote lile bila kujali litaleta madhara kiasi gani.
Pesa zake zilikuwa ndio kila kitu kwake.

Kwa taarifa hizo, Caren alijua kwa vyovyote vile Yusto atakuwa hatarini kama tu atajaribu kupambana na John, ilikuwa ni lazima afanye kitu kumlinda.

Alipotaka kutoka mara akasikia sauti ya Sophia akikohowa pale kitandani.
Caren ligeuka haraka kutazama hapo akamshuhudia Sophia akiwa amerejesha fahamu zake.

Akasogea na kumvua ile mask ya hewa ya oxygen.

"Sophy mama are you okay" alisema Caren huku akisogea zaidi pale kitandani akakaa pembeni ya Sophia.

"Nisamehe Sophy sikujua kama ni wewe wala sikutegemea kukuumiza hivi"alisema Caren huku akimshika shika Sophia kichwani.

Sophia alitulia kwa muda akatamani kusema jambo lakini mara ghafula alianza kutetemaka mwili mzima.
Akawa anarusha miguu na kutupa tupa mikono, macho yake akawa anayageuza geuza.

"Soph sophy.. Sophia.....doktaaaa"
Caren alipiga kelele akihitaji msaada,
sekunde chache baadae timu ya madaktari na manesi walifika haraka na kuanza kutoa huduma kwa Sophia.

"Binti hebu toka nje kwanza"
Alisema Daktari mmoja huku akimtaka Caren asogee pembeni.

"Daktari Bp inashuka, Heart rate ziko juu, oxygen 57% dokta tunafanyaje"

"Anapata shinikizo la chini la msukumo wa damu, angalia"
"Nicolas fanya CPR, Odetha ongeza oxygen nyingine, chukua mtungi mkubwa stoo, nesi Mbundo inua kitanda nyuzi 30' chini harakaaa...."

Haya yalikuwa ni maongezi ya wahudumu wa afya wakipigania maisha ya Sophia

Caren alikuwa pembeni akishuhudia madtari na manesi wakikimbizana huku na huku kuokowa maisha ya mtu,
roho yake ilimuuma sana kwa dakika kadhaa akajikuta anasahau tena kuhusu Yusto na ile video kutoka kwa John.

Jitihada ziliendelea ili kuokoa maisha ya Sophia huku daktari mkuu akiendelea na uchungiziwa kina kubaini tatizo.
Baada ya muda mfupi Sophia alitulia tena.
Mapigo yake ya moyo yakarudi kama kawaida, lakini alirudi katika hali ya kutojitambua.

"Vipi daktari" aliuliza nesi mmoja.
"Kuna damu imevujia kwenye ubongo wa medulla, anahitaji oparesheni ya dharula la sivyo tutampoteza"
Alieleza daktari
"Kwa hiyo tumuandae"
"Yes muandaeni lakini tatizo ni damu yake imeshuka iko chini Hb 5.1g/dl, hatuwezi kumfanyia oparesheni haraka, anahitaji kuongezewa damu kwanza"
"Ni kundi lipi la damu"
" Group B negative"
" Ooh my God, adimu sana hii tutachelewa kuipata, stoo ya damu hatuna, tunafanyaje labda tuingie thyeta hivyo hivyo bila kumuongezea damu"

"Hapana daktari itakuwa ni sawa na kummalizia damu 5.1 ni ndogo, na hii ni oparesheni ya kichwa lazima atapoteza damu nyingine nyingi"
Alisema Daktari mkuu, wote wakatulia huku wakitafakari namna ya kuokowa maisha ya Sophia.

"Niko hapa Dr naweza kuchangia damu tafadhali, kundi langu ni O negative, naweza kuchangia mtu yoyote" alisema Caren.

"Mungu mkubwa, asante dada, haya muandaeni upesi"
***
Taratibu zote zilifanyika haraka haraka, Caren akafanyiwa vipimo muhimu Kisha akatolewa damu.

"Tunashukuru sana Caren, utakuwa umesaidia kwa kiwango kikubwa kuokoa maisha ya Sophia mungu akubaliki, hakikisha unakula chakula kizuri Kisha upumzike sawa binti".
Alisema Daktari.

Caren alitikisha kichwa kukubaliana na maelezo ya daktari, lakini moyoni aliwaza vingine.
"Nina mtu mwingine wa kumsaidia Dr siwezi kupumzika, Yusto wangu yuko hatarini pia" Caren alijisemea mwenyewe kimoyo moyo kisha akaanza kuondoka kuelekea chumbani kwa Yusto.
***
Alifika na kusimama mlangoni kwa bahati nzuri alikuta malango uko wazi, akaingia taratibu.
Mara Caren alisimama ghafula na kurudi nyuma baada ya kuona kitu ambacho hakuwa ametarajia kukiona.
Yusto alikuwa amesimama mbele ya meza yake kubwa akipakia risasi kwenye bastola yake ndogo.
Caren alipatwa na mshangao mkubwa hakuwahi kuwaza kuwa mpenzi wake Yusto anauwezo wa kumiliki na kutumia siraha za moto.

Alishika mdomo wake kwa mshangao huku akiwa amejibana ukutani nje ya chumba cha Yusto.
Kwa bahati nzuri Yusto hakumuona Caren alipoingia, alikuwa amegeuka na kumpa mgongo.

Yusto alikuwa amepaniki sio kidogo, kitendo cha mama yake kutekwa na John kilimuumiza sana. Sasa John alikuwa amewasha moto ambao kuuzima ilikuwa ni habari nyingine.

Yusto alitoka kwenye chumba chake kwa kasi akipiga hatua ndefu ndefu kiasi cha kulifanya koti lake kubwa jeusi lipepee.
Caren akiwa amejificha mahali alimuona Yusto wakati akiondoka.

"Noo, Mimi ndiyo sababu, lazima nifanye kitu, Yusto anaweza kuwa hatarini"
Alisema Caren Kisha akageuka akijaribu kukimbia kuelekea bwenini kwao akajiandae.
Alipopiga hatua kadhaa akapatwa na kizunguzungu cha ajabu akadondoka chini.
Alikumbuka ushauri wa daktari aliopewa kuwa apumzike lakini hakutaka kukubali hilo. Akajikaza na kusimama tena huku akipepesuka.

Je nini kitafuata?
JITIHADA ZA MADAKTARI ZITAZAA MATUNDA?
NINI KITATOKEA KWA YUSTO JOHN NA CAREN?


NAKATA KUKWAMBIA KWAMBA SASA TUNAELEKEA KUINGIA KWENYE KIINI CHA STORI YENYEWE SASA HUKO KOTE TULIKOTOKA ULIKUWA NI UTANGULIZI.....
KWA NINI DO NOT SHOUT????


NJOO JIPATIE SIMULIZI HII YOTE 1-80 KWA PAMOJA BEI PUNGUZO KABISA...


0756862047,,, KARIBU
KAMA HUNAN PESA USIJALI ENDELEA KUFUATILIA TUTAENDA MDOGO MDOGO MPAKA EP YA MWISHO 80
 
DO NOT SHOUT 1-80 Tsh 1400
BAKI NA MIMI 1-80 Tsh 1400

M-pesa 0756862047-saul Halopesa 0625874816-saul

WhatsApp
0756862047
 
  • Thanks
Reactions: y-n
DO NOT SHOUT
(usipige kelele)

Sehemu ya.............31
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA....

Caren alipopiga hatua kadhaa akapatwa na kizunguzungu cha ajabu akadondoka chini.
Alikumbuka ushauri wa daktari aliopewa kuwa apumzike lakini hakutaka kukubali hilo. Akajikaza na kusimama tena huku akipepesuka.

Je nini kitafuata?

Aliendelea kutembea kwa kujikongoja akipandisha ngazi kuelekea juu hadi ghorofa ya pili kilipokuwepo chumba chake akaingia.

Haraka alifungua kabati akachukua vidonge fulani vitatu akavimeza, hivi vilikuwa ni vidonge vyake maalum kwa ajili ya kumuongezea nguvu pale anapotingwa. Angalau sasa alikuwa na nguvu kiasi.

Caren alichukua siraha yake pamoja na vifaa vingine muhimu ambavyo aliamini vingemsaidia mbeleni, akaviweka kwenye koti lake kubwa kisha akatoka chumbani kwake huku akikimbia.

Hakujali wale kufikiri kuwa tayari Yusto alishamuacha na hakutaka kuendelea kuwa na mahusiano ya kimapenzi Caren hakujali hilo kabisa.

Alitoka nje ya chuo chao, akasimamisha bajaji akaingia.

"Unaelekea wapi mrembo" aliuliza dereva
"Subiri kwanza"
"Nisubiri?"
"Ee subiri, kwani hujaelewa nini hapo"
Caren alifoka huku akichukua simu yake akapiga mahali.

"Yes Revocatus, samahani nina dharula tafadhali naomba unisaidie ku-track hii namba ya simu nitakayokurushia nataka kujua huyu mtu alipo Sasa hivi" alisema Caren akakata simu, kisha anaandika sms akamrushia namba ya Yusto.

" Mh! Dada kwani wewe ni Askari? Alafu hiyo teknolojia ya kujua mtu alipo kwa kutumia simu yake ipo hapa kwetu bongo" aliuliza yule dereva.

Lakini kabla Caren hajamjibu mara simu yake iliita haraka akapokea.
"Ndio Revo"
"Bosi mbona location ya hiyo namba tunaipata hapo hapo ulipo?"
"OOH shit"
Caren alilalamika baada ya kubaini kumbe alitoa namba ya simu kubwa ya Yusto na simu hiyo alikuanayo yeye mwenyewe baada ya kuiokota pale hospitali aliitunza.

"Okay levo nakutumia namba yake nyingine, yuko na simu ndogo"
Alisema Caren na haraka akatuma namba ya simu ndogo ya Yusto na punde alirushiwa 'Location'/ muelekeo alipokuwepo Yusto wakati huo.
"Asante Revo endelea kumfuatilia akibadilisha location/ muelekeo niambie tafadhali"
"Vipi Caren kuna shida tuje kukusaidia"
"Aah hapana, nikihitaji msaada nitawambia msijali"
Alisema Caren Kisha akakata simu.

"Twende naelekea soko la matunda HUWE pale nipeleke haraka"
"Sawa afande" alijibu yule dereva bajaji na hapo akaondoka kwa kasi akielekea kule alikoelekezwa.
****

Dakika 15 baadae tangu Yusto aondoke chuoni.
Alionekana akiwa eneo la soko la HUWE eneo maarufu kwa kuuza na kununua matunda mbali mbali.
Soko hilo lilikuwa jirani kabisa na eneo ambalo John alimteka mama mlezi wa Yusto masaa machache yaliyopita.

Yusto alikuwa akiangaza macho huku na huku ni kama vile alikuwa akimtafuta mtu.

Naam ni kweli, macho yake yalitua na kutulia kwa kijana mmoja ambae alikuwa bize akiuza matunda.
Yusto akaanza kupiga hatua ndefu ndefu kumfuata kijana huyo.
Yule kijana alipoinua macho yake akamuona Yusto anakuja,
alitoa macho kwa mshangao Kisha akakurupuka na kuanza kutimua mbio, huku akipamia vigenge vya watu na kumwaga matunda, akawa anaambulia matusi lakini hakujali.

Yusto nae alianza kumkimbiza yule kijana kwa kasi,
Watu wakawa wanawashanga wasijue kinachoendelea.

Haukupita mda Yusto alimkamata yule kijana, akamnyanyua juu juu na kumbananisha ukutani.

"Unakimbia nini, si nilikupa kazi ya kumuangalia mama yangu wewe"
Yusto alifoka.
"Bro bro..oo...oo.utaniua usinikabe sana hivyo...ooo.ooo"
"Nitakuua kweli, sema mama yuko wapi, si nakulipa, nani kuamchukua mama yangu"

"Walikuja watu hapa broo... Siwajui niliogopa niliona wanasiraha"

"Kwa hiyo, kwa nini hukunipigia simu"
"Nilikutumia meseji kaka itakuwa mtandao, nilishindwa kupiga kwa sababu nilikuwa nawafuatilia wanakoenda"
" Ni wapi, wapi wameenda"
"Kule bandalini, ile bandali ya zamani ya Uhuru pale"
"Bandari ya uhuru ile ya zamani"
"Ee ndio bosi, regeza ba...basi kidogo bro.."

Baada ya kusema hivyo Yusto alimuachia yule kijana na kumtupa pembeni, akaanguka chini huku akikohowa baada ya kubanwa vikali shingo yake.

Yusto aliondoka akamuacha yule kijana amelala pale chini akiwa hoi.

"Bro bro.. wanasiraha usisahau hilo, alafu mi..Mimi nimeacha kazi" alisema yule kijana maelezo ambayo wala Yusto hakuyajali.
****

Maeneo ya bandari ya uhuru, bandari ilivyokuwa ikitumika zamani sana lakini ilihamishiwa sehemu nyingine na pale pakawa hapatumiki tena.

Eneo hilo lilitawaliwa na ukimya wa ajabu na Palikuwa na makontena mengi chakavu yaliyotelekezwa.
Ndani ya kontena moja ndimo walipokuwa John pamoja na watu wake.

Mama mlezi wa Yusto alionekana akiwa anekalishwa kwenye kiti na kufungwa kwa kamba miguu na mikono, Kisha alifungwa na plasta kubwa mdomoni, hakuweza kutoa sauti.
Hawakujali kuwa mama huyo ni kichaa wala nini.

John alikuwa amekaa kwenye kiti kingine pembeni akiwa ameinama huku akichimba chimba chini kwa kijiti alionekana kuzama kwenye dimbwi la mawazo.

Mara mtu wake wa karibu bwana Abdullah alifika akiwa na picha mkononi.

" Bosi nimefanikisha kazi uliyonipa hii hapa picha nimeipata" alisema Abdullah.

John alikurupuka kutoka kwenye dimbwi la mawazo akainyakuwa ile picha kutoka mikononi mwa Abdullah, akawa anaitazama.

John aliona mama yake mzazi maarufu kama madam Jane akiwa kwenye picha ya pamoja na mama mlezi wa Yusto ambae yupo nae kama mateka kwa Sasa.

Picha hiyo ilionyesha ni kipindi cha zamani sana kipindi ambacho mama mlezi wa Yusto na mama yake John walikuwa bado ni vijana kama miaka 25 hivi.

John aliitazama picha hiyo huku maswali mengi yasiyo na majibu yakipita kichwani kwake. Haikuwa mara ya kwanza kuiona picha hiyo, kipindi mdogo mara kadhaa alimuona mama yake akiwa na picha kama hiyo na alipenda sana kuitazama mara kwa mara ndio maana John alipomuona mama mlezi wa Yusto alihisi aliwahi kumuona sehemu naam alimuona kwenye picha hiyo ya mama yake zamani.

" Mama anamfahamu vipi mama Yusto?"
"Waliwahi kuishi pamoja kivipi"
" Mbona kwenye picha mama anaonekana hakuwa na hela kabisa kama hivi sasa kwa nini"

Haya ndiyo maswali aliyojiuliza Yusto asipate majibu.
Hapo akaona ipo sababu ya yeye kwenda kuongea na mama yake, madam Jane mama mwenye pesa zake hivi sasa, pesa zilipompa jeuri hadi mtoto wake John.

"Abdullah" John aliita
"Naam bosi"
"Natoka mara moja, imarisha ulinzi eneo hili, yoyote atakaekuja hapa akataka kuharibu mipango yetu uwa, kwa Sasa naenda kuonana na mama, nikirudi nitakwimbia kinachofuata"
"Sawa bosi, ila vipi kama Yusto akija"
" Atapajuaje hapa? Alafu nimekwambia mtu yoyote akija uwa, Yusto yeye sio mtu?" John alifoka kisha akatoka zake nje ya lile kontena.

Aliingia kwenye gari akaiwasha na kuondoka.

Sekunde chache tu baada ya John kuondoka mara upande wa pili wa barabara ukasikika muungurumo mkubwa wa pikipiki aina ya boksa,
punde akachomoza mtu akiwa na pikipiki hiyo akija kwa kasi eneo hilo la bandari.

Sura yake haikuwa ikionekana Kutokana na helment aliyokuwa amevaa kichwani,
kasi aliyokuwa anakuja nayo ililifanya koti lake kubwa kupepea Kutokana upepo mkali ulokuwa ukimpuliza.
Naam huyu hakuwa mwingine bali Yusto.

JE, NINI KITAFUATA?
KWA NINI MAMA MLEZI WA YUSTO NA MAMA YAKE JOHN (MADAM JANE) WAKO KWENYE PICHA YA PAMOJA?

ITAENDELEA...

Sasa ni muda wa kuingia kwenye kiini cha story yetu DO NOT SHOUT njoo WhatsApp chapu kupata ofa simulizi hii...

0756862047
 
Back
Top Bottom