Pre GE2025 Singida: Tundu Lissu adai kufuatiliwa na Watu wasiojulikana

Pre GE2025 Singida: Tundu Lissu adai kufuatiliwa na Watu wasiojulikana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu ambaye yuko Mkoani Singida kwa ajili ya Mikutano ya Kijiji kwa Kijiji, ametangaza hadharani kwamba, kuna watu wanaomfuatilia kila anapofanya mikutano yake ya hadhara na kwamba watu hao Hawajulikani kuwa miongoni mwa wanavijiji hivyo na kwamba, watu hao wakifika eneo la Mkutano hujificha ili wasionekane kirahisi.

Lissu amesema kwamba ni vema watu hao wakajitambulisha kama ni Polisi na waseme wametumwa na nani, kufanya nini ili iweje, Vinginevyo atawalipua kwa wananchi ambao wataamua cha kuwafanya.

Zaidi soma hapa
---
"Toka nimeanza ziara yangu kuna gari inatufatilia halafu wakifika kwenye mkutano wanajificha, nyinyi mnajua mimi nimeshambuliwa sasa nikiona hali kama hiyo ninaogopa, nataka niseme kama ni Askari mje mniambie ili niwe na amani msiposema kesho kwenye mkutano wangu nitawanyooshea kidole maana vijana wangu wameshawatambua" Tundu Lissu, akiwa kwenye mkutano katika kata ya Matumbo Jimbo la Singida Kaskazini. Leo Juni 5, 2024.

Screenshot_2024-06-05-18-47-51-1.png


======

Pia soma:
- Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali
 
Watu wanaofanya uhalifu hapo Tanzania kwa wale wote wanaoonekana ni threats kwenye utawala wa kifisadi na usiokuwa na tija, huwa wanakuwa eliminated au kuwekewa shida kubwa kuficha madudu yao.

Lissu was almost dead, but he did not. Lissu anamaanisha mengi kwa watanzania kushinda kiongozi yoyote wa CCM combined ambao over 60 years nchi ipo vile vile kama TUpo
Kizimu.

Lissu anatoa TAHADHARI, na sisi tunatoa tahadhari, upumbavu uliofanyika 2017 ukirudiwa tena , we will deal with them , watu wanaofanya upumbavu kama huo wanaishi mitaani kama watanzania wengine, they have nothing special and we will get busy with them as well .
CCM mnapotaka Tanzania ifike, itafika….. it is just a matter of time.

Lissu asisumbuliwe, he is the only hope kwa tanzania kwa sasa who can speak the truth and he has our blessings
 

Attachments

  • IMG_2141.jpeg
    IMG_2141.jpeg
    207.4 KB · Views: 6
Vita yao ndani ya chama imefika pabaya, ila vyombo vya dola Jeshi la Polisi, serikali ya Rais Samia kwa ujumla watamuongezea ulinzi wa dhahiri na kificho.

Kama tuvyeo twa chadema ambato hatuna posho, wanataka kumalizana, hawa ndio wa kuwakabidhi nchi? Watauana au kupinduana kila siku na nchi itajaa ghasia na mauaji
 
Hayo majukwaa Kwa level ya Makamo Mwenyekiti wa CHADEMA tena ambaye ana mguu mbovu Si sawa,

Pesa ya Uchaguzi IPO ya kutosha, ila majukwaa sasa ya Lissu 🤔
 
Back
Top Bottom