Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Jiwe analeta ukanda na anaweza ligawa taifa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Helicopter ni rahisi kutunguliwa na waasi/wapiganaji kwenye vita, unless mmekuwa cleared kupita kwenye hilo anga na kutua.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa salama kwa Tanzania sio kwamba inshu za ukabila au udini hazikufanya au hazipo Ila n distance Kati ya hzo pande ndio ilkua inafanya Hilo Jambo lisiwezekane sie tuna eneo kubwa Sana alafu population yetu n ndogo katika eneo tulilonalo Mana Kuna distance Zaid ya 300km kuuacha utamadun mmoja Hadi mwingine.

Hvyo sehemu Kama Burundi, kenya, Rwanda na Uganda walifanikiwa Sana sababu yakuwa na eneo dogo na population kubwa kwenye eneo Moja pia DRC na Sudan.

Hata hapa Tanzania wanatamani Sana tuingie kwenye machafuko ya sisi kwa sisi ili waje kusema wanalinda Aman wajichukulie vyakao

Hawa wanasiasa Tena Hawa maarafu ndio agents wa kutupeleka huko kaa chin uwafuatilie utaona Kuna kitu huyu JPM anajitahidi kufikisha kijiti salama Sana japo JK ilkua imebaki kidogo tuu tuingie humo kumbuka ya green guard, red gurd, cuf sijui iliitwaje Mara panyaroad Mara vikund vya kijingajinga tuu.
 
Samahani wakuu naomba mnijuze hapa
Katika mauaji ya Rwanda inaonekana waliolengwa na kuuliwa zaidi ni watutsi yaani ni kama watutsi walikua wapokea kipigo tu mwanzo mwisho

Sasa ikawaje tena baada ya hapo Rais wa rwanda akawa Mtutsi

Inamaana wahutu pamoja na kujipigania na kuua wahutsi bado hawakuweza kusimamisha kiongozi wa kihutu

Naona KG ndo mbabe sasa, Kwahiyo hutu walistruggle for nothing

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huyo Bossless unaemwambia aache ufala ana 55yrs wew kwa hii comment yako tu inaonyesha hauzidi 30yrs....heshima ni kitu cha bure kabisa.

Sijui kama kuna kitu umenote! Wala haikuwa katika kumshambulia, comment yangu imekaa kimasihara zaidi!!

Mnapokuwa sehemu moja, iwe shule, chuo,kijiweni hata ofisini kuna masihara huwa yanaendelea hata kama rika tofaut.

Kuna sehem nimemquote nikionesha kabisa heye ni baba kwangu! Na sijaona mahala kaandika kwa kuchukua nadhani aliielewa comment yangu! Mie sio mtu wa kihivyo, sio mkosefu wa adabu kwa watu, mfano mdogo humu jf sikumbuki kama nishawahi mkosea mtu adabu mzee!

Ila asante kwa ukumbusho.
 
Inaendelea ..............

Sasa nimelazimika kuandika hii mapema Sanaa asubuhi ili kumpa mwenyewe simu yake andelee na mambo yake .(simu ya wife)

Sasa tuendelee tukafika province ya GITARAMA tukashudia Jambo la ajabu Sanaa yani kumepowaa watu wachache Sanaa wanatembea mtaani Ila maduka yako wazi biashara inaendelea tu Kama hakuna kitu kinachoendelea Rwanda nikashangaa Sanaa huwezi amini ilibidi tusimame hapo kwanza kwa muda magari yote yakasimima tukawa tunashuka tumepumzika wengine wanaenda dukani lakini hakuna anaerudi na kitu ikawa ni Yale Yale nipe kitu nikupe kitu ,yani una hela nyingi za manyarwansa unaenda dukani mwenye duka anakwambia Kama unataka labda soda nipe Hilo jacket lako aise ikawa pale watu wanauza majaketi na masweta njaaa............ni hatariii.

Unajua ule mji wa GITARAMA Kuna baridi hatari naifananisha na baridi ya njombe na tunduma mwezi wa sita .yani unavaa jacket ili baridi isiingie kwenye mifupa lakini bado inakuchapa tu Kama kawaida ,watu wakawa wanabadilishana na saa za mikononi kwa biskuti daa njaaa....

Gari zikawashwa tukaanza Sasa safari ya kuelekea province nyingine(nimeisahau jina) tukawa tunaendelea tu na safari Kama kilomita 150 tunamaliza Sasa ndo live tunayakuta majeshi ya hayajulikani Ila baadae niliambiwa ni ni batalio ya PK yanii wapo full vijana wembamba warefu wa kitusi ,Ila nchi ya Rwanda niyakipumbavu Sanaa,Sasa katika kuchunguza kwangu nikagundua Kuna baadhi yao wanahaiba ya kihutu kabisa Sasa nikawa najiuliza hii Vita gani? Mbona sielewi ni yakikabila au ya kimaslahi nikawa nikaaachana na Hilo wazo wakatusimamisha lakini kiistarabu Kama traffic hawa wa kwetu wanavyosimamisha magari ya tukasimama .

Sasa ikawa wanaongea na balozi wetu Ila baadae ilikuja julikana kuwa walikuwa wanadai kipande kilichobaki Cha kuingia mpakani Kati ya Burundi na rwanda Kuna mtanange unaendelea( Wanaume wanachapana risasi ikumbukwe mpaka mda huo Kuna miji ambayo tayari ikishakuwa chini udhibiti wa majeshi ya kagame akitafuta mbinu za kuingia Kigali ) tukashauriwa tusubiri kwanza hali itakapokuwa imetulia Hali tutaendelea na safari

Tukatulia hapo inaelekea saa kumi na mbili ya jioni muda ukawadia tukaruhusiwa Sasa Cha ajabu wale wanajeshi wote walikuwepo wakapanda kwenye yale maroli tukawa tunaelekea njia moja kila roli na wanajeshi Kama nane hivi au kumi nyuma ya bodi safarii ikaanza wazee wapo tayari tayari kwa Hali ile nikasema Sasa hapa tunaingia vitani rasmi safarii ikawa inasonga ,Kuna kitu nilijifunza vitani Mara nyingi vitani wanajeshi wanaongea kwa ishara na Kama wakiamua kuongea Basi huongea kwa sauti ya chini Sanaa.

Sasa tukawa Kama tumeshatembea Kama kilomita 30 hivi Sasa tukaanza kusikia risasi zinarushwa hovyo hovyo kutokea maeneo ya polini wale wanajeshi wakastukia kiongozi wao nikasikia anatoa sauti flani hivi ya kutaka Kama kujibu mashamulizi hivi wale wanajeshi nao wakawa wanarusha risasi hivyo hivyo msituni yani AK 47 zinanguruma kwenye masikio yetu live huku magari yanaendelea tu kutembea Ila kwa mwendo mkali Sanaa jamaa wakawa wanajibu Kuna askali alikuwa amesimama upande wangu alikuwa ana RPG na bunduki akawa anaweka vizuri rocket Ili alivurumishe kwenye vile vichaka akinipa Ak47 halafu ananionyesha niendelee kufyatua risasi kwa mbali kupitia tundu la bodi ya gari (yani nilivyoishika ile chuma Kama dakika mbili tu nikajikuta yani nimepata ujasiri mkubwa bila kutarajia hapo ndo nilisema mwanzo nami nikawa nimepigana angalau Vita kidogo yule mwanajeshi akavurumisha lile li rocket Polini mle ndo risasi zikawa zimepoa safari ikawa inaendelea kwa kasi .

Tukaenda tukafika mbele kidogo Kuna Kijiji kimoja wakashuka wakabaki wanajeshi wachache tu tukaendelea na safari hapo wakatwambia kazi imeisha Sasa tunaweza kwenda Hadi boda tukawa nao wale wachache Hadi boda tukafika Kama saa mbili usiku hivi.

Sasa angalia chakushangaza tukalikuta lile defenda jeupe na wanajeshi wale njemba Saba walioshuka ubalozini siku ile yani wamechafuka vibaya sanaa yani vumbi Hadi kwenye kope wamevaa combati hizi hizi za jeshi letu lakini hazina majina yao wala begi ya bendera ya Tanzania wakasalimiana na wale tuliowa wachukua njiani hapo Sasa nikajiongeza nikajua Hawa wazee ,tofauti na pale ubalozi hawakutaka kuongea na mtu pale wakawa wanasaidia watu kushuka halafu wanatupa na pole kabisa huku wanatabasamu ,majitu yameshiba

Sasa Kuna Jambo pembezo ya mpaka likawa linawashangaza watu ,kwenye ukingo wa Barbara wa daraja watu wakawa wanakimbilia pale kwa wingi kuangalia majini usiku wa mbalamwezi huo( kwa taarifa tu Mpaka wa Burundi na rwanda unatenganishwa na mto au niseme maporomoko Kama Yale ya rusumo sijui jina lake) namimi nikawa nimesogea pale lahaulaaa maiti zinatoka upande wa Burundi wa mto zinaingia upande wa Rwanda wakiwa wamechomwa na miti tumboni nasehemu za sili nikasema hii ni Sasa na burundi kimechafuka au ? Sasa nikawa najiuliza tunaenda wapi tunaluka majivu tunakanyaga Moto .
.
Ukisikia kukataa tamaa ya kuishi ndo ikawa Sasa nimekata tamaa nilijua tukifika Burundi ndo ntakuwa sasa nimepona Sasa nao wamaenza kuchinjana Tena ....watu wa boda usiku huo wakaruhusu magari tu kuvuka upande wa pili wakasema watu Hadi kesho tukalala chini pale boda.....maishaaa

Itaendelea..............


(Narudisha simu kwa wife nikipata muda Tena ntamuomba niendelee sijaenda kwa fundi Leo mvua inanyesha, halafu watu wengi wanajua naishi Dar, japo nimezaliwa Ilala nimekulia Magomeni mapipa mtaa wa kizingo nyumba namba Siri yangu Ila kwa Sasa Mimi naishi Morogoro -wilaya mpya ya Mlimba .tarafa,kata,Kijiji Siri yangu najishughurisha na kilimo Cha mpunga na biashara ya mchele) jumapili njema .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naam Kaka Ilikuwa hivyo hivyo ,Sasa tembea Kigali nzima ukikutana na wahutu Basi niwakuhesabu wametengwa nje ya miji chini ya udhibiti wa jeshi wanateseka vibaya hata polisi wamewekwa humo na jeshini lakini ni dhaifu tu hawajiamini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hhhhahaaa wahutu Rwanda nzima ni asilimia 80 lakini kila.uchaguzi rais mtu kagame anashinda jiongeze.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawe pia Mkuu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee hii story ikiisha naamini kuna kitu kizito utakuwa umekishusha moyoni.Ila inasikitisha ni kama movie kumbe ni habari za kweli, kupitia story hii umenifanya nianze kupekua makabrasha na kutafuta documentary mbalimbali kuhusu Rwanda genocide kuzidi kujua zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kwenye utawala uliopita kuna chembechembe nilizihisi
Makundi ya jogging yenye itikadi fulani fulani yakuwa mengi sana
Niliogopa sana wakati ule

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…