Jiwe analeta ukanda na anaweza ligawa taifa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Haya mambo bwana tangu zama za ukoloni wa wabelgiji hukoo ndo walianza kuwaambia watutsi wao ni special na wakawa favored kushirikiana na mkoloni kuliko wahutu ila ubaya hutu ndo wengi sana kuliko tutsi
Ni ubaguzi wa tangu 1800 huko
Kama vile Tanzania makabila flani yalivyojaribu kujimwambafai mana wakoloni walianza peleka elimu na umishenari kwao ila Nyerere na marais wote wa watanzania hasa Magu saivi ni wajanja sana kwenye kufyekelea mbali ishu za makabila flani yenye nia ovu ya kuligawa taifa
Lakini pia nchi yetu kubwa mnoo na makabila ni mengi sana ...wale walojaribu kujigawa hakyanani nakuambia wangeishia huku..viongozi huwa wanaona mbali
Mana Rwanda ni kama mkoa mmoja tu wenye makabila mawili
watu hawajui tu haya mambo ya kujiona kabila flani ni keki/grade one wkt watu ni nchi moja yakikomaa kwa muda mrefu haya ndo matokeo yake
Nashukuru TZ washasema makabila flani hawezi mtu kuwa raisi kutoka hapo na Nyerere aliamua kusambaza watoto shule kujimix mikoa ya mbali ili waone wao ni kama wengine tu
Na kuoleana tushaoleana sanaaa na watu kabila zote washasoma sanaa inasaidia baadhi ya makabila kuona kumbe wao ni kama wengine tu
Bt mtu ukiwa kabila lililokuwa 'priviledged' na mkoloni usijimwambafai haya ndo madhara ya watutsi kuwa 'priviledged' na wabelgiji na hata sasa wao ndo wameshika hatamu bado unafikiri wahutu wanajiskiaje?!!kitanuka siku PL Slim akitoka hapo
Nilisoma wikipedia
Sent using Jamii Forums mobile app