Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

K
Mkuu yale hayakuwa mauaji dhidi ya watutsi tu bali ilikuwa ni VITA yaani wakati wahutu wanachinja watutsi na hao Watutsi wanachinja wahutu kutumia vikundi vyao vya waasi mfano INTEREHAMWE/FDLR,APERHUTU kwa Wahutu na be it UPRONA/RPF kwa watutsi na ndio maana kule Uganda kwenye mitaala ya shule haiitwi Rwanda genocide kule tulisoma inaitwa Rwanda civil war yaani VITA sio Mauaji!!

Ila yaonekana kagame alikua kajipanga zaidi hivyo baada ya kushinda vita naye akalipiza kisasi akawachinja hao wahutu wakakimbilia DRC ambapo aliwafuata na kuwateketeza na tokea hapo nguvu ikahama kutoka kwa Wahutu ikaja kwa watutsi na imekua hivyo mpaka leo.

Wahutu sio kwamba wali-fight for nothing" ila walishashinda vita tokea 1959 na wakajikomboa kutoka mikono ya watutsi so walienjoy uhuru wao mpaka 1990 ambapo uvamizi wa Watutsi ulianza. Hivyo ile vita ilikua ni ya kujilinda zaidi dhidi ya uvamizi wa watutsi na sio kuvamia watutsi kama unavyodhani. Yaani kama watutsi wasingetishia kuvamia Rwanda kulikua hakuna haja ya wao kuwaua maana madaraka yalikua kwa wahutu.

Hope umepata picha mkuu
Kwa mantiki hiyo mkuu, naamini kwa namna moja au nyingine wahutu watakua wanajipanga kulipiza ili washike hatamu wawachomoe Watusi.

Swali in je wanatumia mbinu gani kujipanga? Tuliona Kagame alitumia RPF akitokea msituni.
 
Mkuu je hizo silaha walikuwa wanapewa na Nani?serikali iliyopo madarakani au Kuna ufadhili walikua wanaupata?

Sent using Jamii Forums mobile app
Silaha za interahamwe zilikuwa..jembe.marungu .haya marungu yaligongwa misumari ya nchi sita kila sehemu mfano wa tunda la stafeli.nyengo.mapanga.mashoka.n.k.

Hizi silaha zilinunuliwa nchini china zililetwa rwanda makontena na makontena kwa ufadhili wa mfanya biashara ambaye alikuwa kiongozi wa interahamwe wakati huo george rutaganda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haha lool thanks

Haya mambo bwana tangu zama za ukoloni wa wabelgiji hukoo ndo walianza kuwaambia watutsi wao ni special na wakawa favored kushirikiana na mkoloni kuliko wahutu ila ubaya hutu ndo wengi sana kuliko tutsi
Ni ubaguzi wa tangu 1800 huko...mkoloni akitumia system ya 'divide and rule'
Kama vile Tanzania makabila flani yalivyojaribu kujimwambafai mana wakoloni walianza peleka elimu na umishenari kwao ila Nyerere na marais wote wa watanzania hasa Magu saivi ni wajanja sana kwenye kufyekelea mbali ishu za makabila flani yenye nia ovu ya kuligawa taifa

Lakini pia nchi yetu kubwa mnoo na makabila ni mengi sana ...wale walojaribu kujigawa hakyanani nakuambia wangeishia huku..viongozi huwa wanaona mbali
Mana Rwanda ni kama mkoa mmoja tu wenye makabila mawili

watu hawajui tu haya mambo ya kujiona kabila flani ni keki/grade one wkt watu ni nchi moja yakikomaa kwa muda mrefu haya ndo matokeo yake

Nashukuru TZ washasema makabila flani hawezi mtu kuwa raisi kutoka hapo na Nyerere aliamua kusambaza watoto shule kujimix mikoa ya mbali ili waone wao ni kama wengine tu
Na kuoleana tushaoleana sanaaa na watu kabila zote washasoma sanaa inasaidia baadhi ya makabila kuona kumbe wao ni kama wengine tu

Bt mtu ukiwa kabila lililokuwa 'priviledged' na mkoloni usijimwambafai haya ndo madhara ya watutsi kuwa 'priviledged' na wabelgiji na hata sasa wao ndo wameshika hatamu bado unafikiri wahutu wanajiskiaje?!!kitanuka siku PL Slim akitoka hapo
Nilisoma wikipedia
@LadyRed bwana, hili Jambo naona huwa unalizungumzia sana. Linakuumiza kwani? Ni kweli kuwa zipo jamii zilikuwa na privilege nyakati za mkoloni, ilà trust me nao walijiongeza sana tu, na wanazidi kujiongeza to-date. Zipo jamii hapa bongo hadi leo hii pamoja na fursa kuwa kwa kila mtu lakini bado they lag behind, hatuwezi kufanana na kuna watu naturally wapo gifted katika utafutaji na kusaidiana. Kuna sehemu leo hii ukienda vijijini japo ni afrika lakini hutaamini kuona palivyo, na kuna mahali ukienda unaweza kuishia kutoa machozi, ndani ya hii bongo.

So pamoja na privilege kuwepo kwa wote, kuna gifted hands, kuna watu wanabebana sanaaa, na wapo ambao hata dada mtu anaona wivu kwa mdogo mtu kuwin maisha.

Ya huko Rwanda siyajui sana, unaweza kuwa sahihi kwa analysis uliyofanya, ila kwa bongo mmmh.
 
Mkuu hapa ame eleza vizuri
Unanichanganya mkuu.inamana gani kusema hakuna kabila ya tusi na hutu? Sasa waliokuwa wanaopigana ni kabila gani vs kabila gani.maana tumesikia ni Vita ya wahutu na watusi.
Mkuu yale hayakuwa mauaji dhidi ya watutsi tu bali ilikuwa ni VITA yaani wakati wahutu wanachinja watutsi na hao Watutsi wanachinja wahutu kutumia vikundi vyao vya waasi mfano INTEREHAMWE/FDLR,APERHUTU kwa Wahutu na be it UPRONA/RPF kwa watutsi na ndio maana kule Uganda kwenye mitaala ya shule haiitwi Rwanda genocide kule tulisoma inaitwa Rwanda civil war yaani VITA sio Mauaji!!

Ila yaonekana kagame alikua kajipanga zaidi hivyo baada ya kushinda vita naye akalipiza kisasi akawachinja hao wahutu wakakimbilia DRC ambapo aliwafuata na kuwateketeza na tokea hapo nguvu ikahama kutoka kwa Wahutu ikaja kwa watutsi na imekua hivyo mpaka leo.

Wahutu sio kwamba wali-fight for nothing" ila walishashinda vita tokea 1959 na wakajikomboa kutoka mikono ya watutsi so walienjoy uhuru wao mpaka 1990 ambapo uvamizi wa Watutsi ulianza. Hivyo ile vita ilikua ni ya kujilinda zaidi dhidi ya uvamizi wa watutsi na sio kuvamia watutsi kama unavyodhani. Yaani kama watutsi wasingetishia kuvamia Rwanda kulikua hakuna haja ya wao kuwaua maana madaraka yalikua kwa wahutu.

Hope umepata picha mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani wakuu naomba mnijuze hapa
Katika mauaji ya Rwanda inaonekana waliolengwa na kuuliwa zaidi ni watutsi yaani ni kama watutsi walikua wapokea kipigo tu mwanzo mwisho

Sasa ikawaje tena baada ya hapo Rais wa rwanda akawa Mtutsi

Inamaana wahutu pamoja na kujipigania na kuua wahutsi bado hawakuweza kusimamisha kiongozi wa kihutu

Naona KG ndo mbabe sasa, Kwahiyo hutu walistruggle for nothing

Sent using Jamii Forums mobile app
Kitabu cha bodigad wa slim shade kinasema RPF walikua wanavaa kama interamwe na kwenda kuua watus wenzao ili wapate huruma ya dunia
 
Acha tu bro, bossless kanikumbusha moja ya tukio baya sana nililiona kwa macho yangu nikiwa na miaka 10 jamaa walikuwa wawili ilikuwa saa tisa na dk 17, alasiri tarehe 26/4/1994. Utanzania uliniokoa dogo huyo aliyekuwa rafiki yangu alipewa thiodan ile dawa tunayopulizia nyanya shambani dogo akawaambia anasikia kiu wakamwongeza nyingine alikufa namwona hv siku nilipoenda musozi kwa mara ya kwanza niliona picha ya dogo pale ndio maana naamini dogo amelala pale afu babu yake wakaondoka nae sijamwona hadi leo

Yaan ningekuwa na uwezo wale jamaa nikiwakuta jehanamu au mbiguni niwauwe tena[emoji24][emoji24][emoji24] basi tu

Rip Jean, babu huko uliko neema za Mungu ziwe nawe

Sorry bossless kuingilia uzi wako

Sent using Jamii Forums mobile app
Matukio kama hayo mi naona sawa mkiweka kwasabu mtoa mada hajaona yote kwahiyo fresh tu.
 
Silaha za interahamwe zilikuwa..jembe.marungu .haya marungu yaligongwa misumari ya nchi sita kila sehemu mfano wa tunda la stafeli.nyengo.mapanga.mashoka.n.k.

Hizi silaha zilinunuliwa nchini china zililetwa rwanda makontena na makontena kwa ufadhili wa mfanya biashara ambaye alikuwa kiongozi wa interahamwe wakati huo george rutaganda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nasikia majamaa yalikuwa kama mazombi ,,,,utapiga risasi hola linakufuata kibabe Mpaka likucharange ..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli siasa haina nguvu hapa kwa watanzania ni ya kimasilahi hawana (philosophy) itikadi, lakini pia makabila pia hayana nguvu kuna watanzania wengi hata wanaogopa kuongea lugha za kikabila yao kwa sababu ya 'inferioty complex' wengi wanajificha kwenye kiswahili hata wakiwa nyumbani

kwahiyo nivingumu watanzania kupigana kwa hayo mambo mawili tu......jambo linalo weza kuleta hisia za watu kwa kiwango cha kuuwana ni Dini, Waislama hawana mzaha na Dini yao na pia it's second to none, wako tayari kuyilinda dini yao hata kama ni kupoteza utaifa au asiri yao hili lilidhihirika pale Rwanda wakati wa Rc walikimbilia misikitini kuliko makanisani hamna Muislamu wanaweza kuua muislam mwenzie kwa sabb ya kua mtusi au muhtu Waislamu wana umoja katika hilo wanasemaga 'Muislamu ndugu ye Muislamu' ....... kuanzia 1992 Dini ya Kiislamu ina heshimika sana Rwanda nawanyarwanda wameslimu wengi wameona Uislamu ni 'pragamatic religion'.

Kitu kama hicho kutokea hapa nchini labda kipitie kwenye Imani za Dini serikali iwe makini ifanye 'fair play' sio kupendelea dhehebu moja nakuache mengine inaweza ikashutua mihemuko na hisia za watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na kuna kitu kinaendelea kwa sasa, tunagawanywa kutokana na maeneo tunayotoka, japo sioni yakifika huko kwenye chuki ila sioni kama ina afya nzuri kwa taifa. Ukanda unaweza kutugawa kwa kiasi kikubwa tu, Kanda ya ziwa, Kanda ya kaskazini, Kanda ya kati na Kanda ya kusini. Na inasemekana Meku ndio aemeleta haya.
 
K

Kwa mantiki hiyo mkuu, naamini kwa namna moja au nyingine wahutu watakua wanajipanga kulipiza ili washike hatamu wawachomoe Watusi.

Swali in je wanatumia mbinu gani kujipanga? Tuliona Kagame alitumia RPF akitokea msituni.
Ukifika Rwanda utaona kama nchi yenye utulivu wa kutosha. Hata uhalifu mkubwa kama ujambazi na uporaji wa kutumia silaha umedhibitiwa kwa kiasi kikubwa,iliyobakia ni udokozi mdogomdogo tu.

Lakini ukiangalia kwa undani utagundua kua Rwanda kuna tension ya hali ya juu sana miongoni mwa raia wake. Ule utulivu na amani ni kama vimeshikiliwa na kamba nyembamba. Unahisi kwenye nyoyo za watu kuna kutokuridhika flani hivi na kilichokuwepo ni kuogopa mkono fulani wa chuma

Kwa maoni yangu Rwanda ya baada ya Kagame lazima iwe handled very careful vinginevyo kitanuka tena! Nilisafiri kutoka Kigali kwenda Goma DRC kupitia Gisenyi na pote upitapo na kuonana na watu na kuongea nao unahisi ni watu wenye wasiwasi sana na hasira! Tuiombee Rwanda yasijirudie yaliyopita
 
Samahani wakuu naomba mnijuze hapa
Katika mauaji ya Rwanda inaonekana waliolengwa na kuuliwa zaidi ni watutsi yaani ni kama watutsi walikua wapokea kipigo tu mwanzo mwisho

Sasa ikawaje tena baada ya hapo Rais wa rwanda akawa Mtutsi

Inamaana wahutu pamoja na kujipigania na kuua wahutsi bado hawakuweza kusimamisha kiongozi wa kihutu

Naona KG ndo mbabe sasa, Kwahiyo hutu walistruggle for nothing

Sent using Jamii Forums mobile app
Hutu walikuwa wanapigana vita mbili.jeshi lilijikita kupigana na waasi kina kagame..walibaki wanajeshi wachache wakiungana na interahamwe kupigana vita ya ndani ya kuua raia wote wa kitutsi na kihutu ambao hawaungi mkono juhudi .
Sasa ikatokea vita ya kijeshi .waasi walikuwa vizuri wakawashinda jeshi la rwanda wakafanikiwa kuingia ndani.ikapigwa ya ndani wakashinda tena.interahamwe wakakosa sapoti ya jeshi na hawakuwa na silaha za kisasa.pia waliopunguzwa sana .wakasilimu amri wakakimbilia congo.tanzania.na wengine walijichanganya na raia wema kwenye makambi ya wakimbizi.maofisa wa jeshi la rwanda nao walikimbia nchi.ndio chanzo cha kagame kuwa na nguvu.kwasababu alishinda vita.kwahiyo kuna wahutu wengi interahamwe nje ya rwanda ambao wanatamani sana kurudi rwanda lakini wanamuogopa kagame.ndio maana tunahisi siku kagame akipoteza power.hawa wahutu wakirudi wanakiwasha tena.safari hii watawachoma mishikaki kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaendelea ..............

Sasa nimelazimika kuandika hii mapema Sanaa asubuhi ili kumpa mwenyewe simu yake andelee na mambo yake .(simu ya wife)

Sasa tuendelee tukafika province ya GITARAMA tukashudia Jambo la ajabu Sanaa yani kumepowaa watu wachache Sanaa wanatembea mtaani Ila maduka yako wazi biashara inaendelea tu Kama hakuna kitu kinachoendelea Rwanda nikashangaa Sanaa huwezi amini ilibidi tusimame hapo kwanza kwa muda magari yote yakasimima tukawa tunashuka tumepumzika wengine wanaenda dukani lakini hakuna anaerudi na kitu ikawa ni Yale Yale nipe kitu nikupe kitu ,yani una hela nyingi za manyarwansa unaenda dukani mwenye duka anakwambia Kama unataka labda soda nipe Hilo jacket lako aise ikawa pale watu wanauza majaketi na masweta njaaa............ni hatariii.

Unajua ule mji wa GITARAMA Kuna baridi hatari naifananisha na baridi ya njombe na tunduma mwezi wa sita .yani unavaa jacket ili baridi isiingie kwenye mifupa lakini bado inakuchapa tu Kama kawaida ,watu wakawa wanabadilishana na saa za mikononi kwa biskuti daa njaaa....

Gari zikawashwa tukaanza Sasa safari ya kuelekea province nyingine(nimeisahau jina) tukawa tunaendelea tu na safari Kama kilomita 150 tunamaliza Sasa ndo live tunayakuta majeshi ya hayajulikani Ila baadae niliambiwa ni ni batalio ya PK yanii wapo full vijana wembamba warefu wa kitusi ,Ila nchi ya Rwanda niyakipumbavu Sanaa,Sasa katika kuchunguza kwangu nikagundua Kuna baadhi yao wanahaiba ya kihutu kabisa Sasa nikawa najiuliza hii Vita gani? Mbona sielewi ni yakikabila au ya kimaslahi nikawa nikaaachana na Hilo wazo wakatusimamisha lakini kiistarabu Kama traffic hawa wa kwetu wanavyosimamisha magari ya tukasimama .

Sasa ikawa wanaongea na balozi wetu Ila baadae ilikuja julikana kuwa walikuwa wanadai kipande kilichobaki Cha kuingia mpakani Kati ya Burundi na rwanda Kuna mtanange unaendelea( Wanaume wanachapana risasi ikumbukwe mpaka mda huo Kuna miji ambayo tayari ikishakuwa chini udhibiti wa majeshi ya kagame akitafuta mbinu za kuingia Kigali ) tukashauriwa tusubiri kwanza hali itakapokuwa imetulia Hali tutaendelea na safari

Tukatulia hapo inaelekea saa kumi na mbili ya jioni muda ukawadia tukaruhusiwa Sasa Cha ajabu wale wanajeshi wote walikuwepo wakapanda kwenye yale maroli tukawa tunaelekea njia moja kila roli na wanajeshi Kama nane hivi au kumi nyuma ya bodi safarii ikaanza wazee wapo tayari tayari kwa Hali ile nikasema Sasa hapa tunaingia vitani rasmi safarii ikawa inasonga ,Kuna kitu nilijifunza vitani Mara nyingi vitani wanajeshi wanaongea kwa ishara na Kama wakiamua kuongea Basi huongea kwa sauti ya chini Sanaa.

Sasa tukawa Kama tumeshatembea Kama kilomita 30 hivi Sasa tukaanza kusikia risasi zinarushwa hovyo hovyo kutokea maeneo ya polini wale wanajeshi wakastukia kiongozi wao nikasikia anatoa sauti flani hivi ya kutaka Kama kujibu mashamulizi hivi wale wanajeshi nao wakawa wanarusha risasi hivyo hivyo msituni yani AK 47 zinanguruma kwenye masikio yetu live huku magari yanaendelea tu kutembea Ila kwa mwendo mkali Sanaa jamaa wakawa wanajibu Kuna askali alikuwa amesimama upande wangu alikuwa ana RPG na bunduki akawa anaweka vizuri rocket Ili alivurumishe kwenye vile vichaka akinipa Ak47 halafu ananionyesha niendelee kufyatua risasi kwa mbali kupitia tundu la bodi ya gari (yani nilivyoishika ile chuma Kama dakika mbili tu nikajikuta yani nimepata ujasiri mkubwa bila kutarajia hapo ndo nilisema mwanzo nami nikawa nimepigana angalau Vita kidogo yule mwanajeshi akavurumisha lile li rocket Polini mle ndo risasi zikawa zimepoa safari ikawa inaendelea kwa kasi .

Tukaenda tukafika mbele kidogo Kuna Kijiji kimoja wakashuka wakabaki wanajeshi wachache tu tukaendelea na safari hapo wakatwambia kazi imeisha Sasa tunaweza kwenda Hadi boda tukawa nao wale wachache Hadi boda tukafika Kama saa mbili usiku hivi.

Sasa angalia chakushangaza tukalikuta lile defenda jeupe na wanajeshi wale njemba Saba walioshuka ubalozini siku ile yani wamechafuka vibaya sanaa yani vumbi Hadi kwenye kope wamevaa combati hizi hizi za jeshi letu lakini hazina majina yao wala begi ya bendera ya Tanzania wakasalimiana na wale tuliowa wachukua njiani hapo Sasa nikajiongeza nikajua Hawa wazee ,tofauti na pale ubalozi hawakutaka kuongea na mtu pale wakawa wanasaidia watu kushuka halafu wanatupa na pole kabisa huku wanatabasamu ,majitu yameshiba

Sasa Kuna Jambo pembezo ya mpaka likawa linawashangaza watu ,kwenye ukingo wa Barbara wa daraja watu wakawa wanakimbilia pale kwa wingi kuangalia majini usiku wa mbalamwezi huo( kwa taarifa tu Mpaka wa Burundi na rwanda unatenganishwa na mto au niseme maporomoko Kama Yale ya rusumo sijui jina lake) namimi nikawa nimesogea pale lahaulaaa maiti zinatoka upande wa Burundi wa mto zinaingia upande wa Rwanda wakiwa wamechomwa na miti tumboni nasehemu za sili nikasema hii ni Sasa na burundi kimechafuka au ? Sasa nikawa najiuliza tunaenda wapi tunaluka majivu tunakanyaga Moto .
.
Ukisikia kukataa tamaa ya kuishi ndo ikawa Sasa nimekata tamaa nilijua tukifika Burundi ndo ntakuwa sasa nimepona Sasa nao wamaenza kuchinjana Tena ....watu wa boda usiku huo wakaruhusu magari tu kuvuka upande wa pili wakasema watu Hadi kesho tukalala chini pale boda.....maishaaa

Itaendelea..............


(Narudisha simu kwa wife nikipata muda Tena ntamuomba niendelee sijaenda kwa fundi Leo mvua inanyesha, halafu watu wengi wanajua naishi Dar, japo nimezaliwa Ilala nimekulia Magomeni mapipa mtaa wa kizingo nyumba namba Siri yangu Ila kwa Sasa Mimi naishi Morogoro -wilaya mpya ya Mlimba .tarafa,kata,Kijiji Siri yangu najishughurisha na kilimo Cha mpunga na biashara ya mchele) jumapili njema .

Sent using Jamii Forums mobile app

Barikiwa sana Mkuu,shukran kwa Wife kukuachia simu yake japo kwa muda ili utupe hii simulizi ya kusisimua! Jumapili njema na kwako pia!
 
Ukifika Rwanda utaona kama nchi yenye utulivu wa kutosha. Hata uhalifu mkubwa kama ujambazi na uporaji wa kutumia silaha umedhibitiwa kwa kiasi kikubwa,iliyobakia ni udokozi mdogomdogo tu.

Lakini ukiangalia kwa undani utagundua kua Rwanda kuna tension ya hali ya juu sana miongoni mwa raia wake. Ule utulivu na amani ni kama vimeshikiliwa na kamba nyembamba. Unahisi kwenye nyoyo za watu kuna kutokuridhika flani hivi na kilichokuwepo ni kuogopa mkono fulani wa chuma

Kwa maoni yangu Rwanda ya baada ya Kagame lazima iwe handled very careful vinginevyo kitanuka tena! Nilisafiri kutoka Kigali kwenda Goma DRC kupitia Gisenyi na pote upitapo na kuonana na watu na kuongea nao unahisi ni watu wenye wasiwasi sana na hasira! Tuiombee Rwanda yasijirudie yaliyopita
Kwamba itakua wahutu ndio wanaleta hali ya wasiwasi ? I'm so curious to know the cause of that tension to citizens whilst there is Peace.
 
Sijui ni umaskini? Kutokujali na kupuuzia kwa serikali?? au tu kutokujua hatari waliyokuwemo raia wa Tanzania pale ubalozini, yaani mimi nafikiri ilitakiwa zishuke helicopter za JWTZ pale ziwachukue raia na kurudi. Safari ya uokoaji kwa usafiri wa malori ilikuwa ni ya hatari kubwa sana, maana kuyasoma tu waliyokuwa wanayapitia siku za mwisho za kuokolewa pale najisikia vibaya sana sijielewielewi nafikiria wahanga wale walikuwa na hali gani, ni jehanum ya duniani.
Haaaa nchi ilikuwa inaongozwa na serikali goigoi by nyerere @@@ raisi alikuwa mzenji legelege siyo kama huyo balozi mama wa kipemba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
na CCM ndo watakao iangamiza nchi kwa kuleta machafuko, angalia kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa walichokifanya, kama siyo uungwana wa kijinga wa watanzania wa kukubali kudhulumiwa haki zao hiyo tu ilikuwa ni tiketi ya kuipeleka nchi kwenye machafuko.

Msimuliaji wa kisa hiki kuna jambo moja la maana sana kalielezea kuwa ukiona vyama vya siasa vimeanzisha vikundi vyao vya ulinzi ujue kuwa imani kwa jeshi la polisi imekwisha na kinachofuata hapo ni nchi kuingia kwenye machafuko.

Nterahamwe kikosi kikuu cha mauaji kilikuwa ni kikundi cha ulinzi kilichoanzishwa na chama tawala na ndicho kilichoendesha mauaji ya hatari sana nchini Rwanda ambayo kwa kiasi fulani na mimi niliyashuhudia kwa kuwa nilikuwa karibu na maeneo hayo ndo maana sina swali lolote kwa msimuliaji wa kisa kwa kuwa na mimi niliguswa.

Ukiachilia mauaji ya kuuawa kamanda Mawazo, kwa macho yangu nimeshuhudia wagombea 2 wa upinzani wanapigwa mapanga mbele yangu na vijana wa kikundi cha ulinzi cha CCM katika uchaguzi wa serekali za mitaa wa mwaka 2014 kwa kuwa tu CCM walitaka wapite bila kupingwa.

Hata hivi vikundi vya ulinzi ndani ya vyama waanzilishi walikuwa ni CCM.
Hivi vikundi vilipaswa kupigwa marufuku, green guard na red brigade vyote havifai kwa faida ya Taifa letu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom