Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Hao watusi wa bongo naamini huko mbeleni watawaibua wahutu wao wenyewe.

Hii arrogance ya kujifaragua kuwa wao ndo 1st class citizens ikipata watu wa kutia kiberiti hisia za upande wa pili,kwisha habari.
Huko mbeleni ni ngumu kwani saivi kila mtanzania yuko priviledged kielimu kifedha wadhifa serikalini na nje ya serikali biashara nk
Yani hamna kabila linaloachwa nyuma..inakata wale waliojidhania wao ni superior wkt in real sense they are not ni raia tu ka watu wengine
 
Ubaguzi uko kwa kiwango cha juu sana unasikia tu fika pale ujionee

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanabaguana kuhusu nini?Kama fursa za kiuchumi na biashara zipo wazi na kwa usawa kwa kila mtu sioni shida Mimi rais hata angekuwa mmasai achilia mbali mtusi. Watajichelewesha kwa ujinga wao wenyewe.
 
na CCM ndo watakao iangamiza nchi kwa kuleta machafuko, angalia kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa walichokifanya, kama siyo uungwana wa kijinga wa watanzania wa kukubali kudhulumiwa haki zao hiyo tu ilikuwa ni tiketi ya kuipeleka nchi kwenye machafuko.

Msimuliaji wa kisa hiki kuna jambo moja la maana sana kalielezea kuwa ukiona vyama vya siasa vimeanzisha vikundi vyao vya ulinzi ujue kuwa imani kwa jeshi la polisi imekwisha na kinachofuata hapo ni nchi kuingia kwenye machafuko.

Nterahamwe kikosi kikuu cha mauaji kilikuwa ni kikundi cha ulinzi kilichoanzishwa na chama tawala na ndicho kilichoendesha mauaji ya hatari sana nchini Rwanda ambayo kwa kiasi fulani na mimi niliyashuhudia kwa kuwa nilikuwa karibu na maeneo hayo ndo maana sina swali lolote kwa msimuliaji wa kisa kwa kuwa na mimi niliguswa.

Ukiachilia mauaji ya kuuawa kamanda Mawazo, kwa macho yangu nimeshuhudia wagombea 2 wa upinzani wanapigwa mapanga mbele yangu na vijana wa kikundi cha ulinzi cha CCM katika uchaguzi wa serekali za mitaa wa mwaka 2014 kwa kuwa tu CCM walitaka wapite bila kupingwa.

Hata hivi vikundi vya ulinzi ndani ya vyama waanzilishi walikuwa ni CCM.

Hili suala linahitaji mjadala mpana wa kitaifa tunakoelekea si kuzuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu inaonyesha hali ilikuwa tete, kama helcopta zingetumika zingeweza kushambuliwa na sura ya vita ingebadilika kutoka ya kikabila na iwe ya Rwanda na Tanzania.
Ikiwa ndege ya rais ilipigwa chini lolote lingeweza kutokea kwa ndege zetu pia.
Sijui ni umaskini? Kutokujali na kupuuzia kwa serikali?? au tu kutokujua hatari waliyokuwemo raia wa Tanzania pale ubalozini, yaani mimi nafikiri ilitakiwa zishuke helicopter za JWTZ pale ziwachukue raia na kurudi. Safari ya uokoaji kwa usafiri wa malori ilikuwa ni ya hatari kubwa sana, maana kuyasoma tu waliyokuwa wanayapitia siku za mwisho za kuokolewa pale najisikia vibaya sana sijielewielewi nafikiria wahanga wale walikuwa na hali gani, ni jehanum ya duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna jinsi ya kuweka hizi stori copyritghts asee?? Ili wakomeshwe na huo mpango wao
Kuna raia humu wana roho mbaya, wanamshawishi baba yetu Bossless ahamishe stori kwenye kitabu

wanatamani stori ingekuwa yao wangetuhamisha watsap kwa kiingilio cha elfu 2
Mungu akaliona hilo ndo maana stori kampa mzee wetu

Ajabu watakopi na kuhamishia FB, ista na watsap, watajifanya wao ndio mzee Bossless na watawachangisha wenzao pesa ya kiingilio ili kupata stori


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabaguana kuhusu nini?Kama fursa za kiuchumi na biashara zipo wazi na kwa usawa kwa kila mtu sioni shida Mimi rais hata angekuwa mmasai achilia mbali mtusi. Watajichelewesha kwa ujinga wao wenyewe.
Jmn mbona huelewi
Ushaambiwa hamna usawa

Ni kama vile hapa bongo baadhi ya watu walipeana kazi kwa vimemo akishakujua jina tu anajua kabila gani hivyo anaamua akupe au asikupe
Kulikua na usawa hapo?.
Ama viongozi wengi wakitokea sehemu fulani unafikiri nini kinafuata iwapo hawana hekima?.si ni kupeleka maendeleo kwao na kusahau umoja wa nchi!!!
Wale waliosahaulika unafikiri wanajiskiaje na kodi zao ndo zinaimarisha upande mwingine?.!!

Sasa hivi ndo mifumo imeimarika fursa zinaenda kwa wengi zaidi nchi nzima..haikua hivi
 
Mkuu yale hayakuwa mauaji dhidi ya watutsi tu bali ilikuwa ni VITA yaani wakati wahutu wanachinja watutsi na hao Watutsi wanachinja wahutu kutumia vikundi vyao vya waasi mfano INTEREHAMWE/FDLR,APERHUTU kwa Wahutu na be it UPRONA/RPF kwa watutsi na ndio maana kule Uganda kwenye mitaala ya shule haiitwi Rwanda genocide kule tulisoma inaitwa Rwanda civil war yaani VITA sio Mauaji!!
Mkuu mbona kama unajichanganya kumbuka Rwanda civil war na Rwanda genocide ni vitu viwili tofauti.

Rwanda civil war ndiyo hiyo kuanzia 1990 na ndio maana kulikuwa na mazungumzo ya kutafuta amani ila Rwanda genocide ilikuja baadae baada ya Rais Habyarimana kuuawa.
 
Hv mnasema wanyarwanda wapo kwenye nyaxifa nyeti za kiserikali hapa bongoland huwa mnanipa wakati mgumu kuwajua ebu nipen hzo mnitoe kwenye dimbwi la kutumia kichwa.

Wanaosemaga number 1 yupo mie soon hoja ukiangalia height, history Wala haviendani japo ametokea mpakan
 
Mkuu "Mbari" ni neno la kiswahili lenye maana ya Koo "clan" "ethnicity" kitu ambacho wengi awakijuhi ni kwamba yae mauaji ya Rwanda yalikuwa baina ya koo mbili za watusi na wahutu (sio kabila) kwan uko watsi na wahutu wote wanaongea kinywarwanda na tamaduni ni sawa awa tofauti zao ni morphology yaan mwonekano....sifa ya ziada awa watusi inasadikika wana asili ya Ethiopia ndo maana ni wazuri kulinganisha na wahutu, mauaji yale kuna wakt mtu ilibidi uokolewe na nan anakujua au "kipande" id na wala sioo mwonekano wako kwan walishaingiliana so kupoteza identity...

I stnd to be corrected

Sent using Jamii Forums mobile app
Point of correction. Kiingereza Cha kimbari ni "genocide or massacre''. Yaani mauji ya watu wengi ambayo NI endelevu au kwa muda mfupi.
 
Watanzania wakitaka kitu wanakua wapole sana...ona kwenye huu uzi,kuna watu wanajua kubembeleza aisee,wanajua kujinyenyekeza..yaani tumekua wapole...ninachofurahi ni kuona bado kuna watanzania wana spirit ya kupenda kusoma ..
Watz wanapenda kusoma story....
ww lete maandiko ya kilimo cha maharage ama choroko kama utaona mtu!
 
Back
Top Bottom