Sinza kuna mtu anaitwa Wambura, naye hutishia watu bastola hadharani

Sinza kuna mtu anaitwa Wambura, naye hutishia watu bastola hadharani

Nilisikiliza mashuhuda wa tukio la huyo jamaa kuua. Marehemu aliyepigwa risasi kosa lake kubwa ni kumfuata mlevi mwenye silaha, tena ameshamrisha DJ azime muziki na kupiga risasi mbili juu eti kumpa tahadhari aache bugdha. Alichotakiwa kufanya ni kumlia timing na kumpokonya ile silaha bila kutoa onyo lolote. Alitakiwa kijipima kama anaweza kumdhibiti na afanye hivyo kwa haraka bila kumsemesha. Vinginevyo alitakiwa kuondoa haraka sana eneo la tukio. Hivi huyo afisa usalama anayesemekana alikuwepo hakuna na silaha am-shoot? Au pengine alikuwa hajabeba silaha.
Hivi wewe kwa akili zako watu wa usalama wapo baa wamuone mlevi ana silaha anaitotoa/anaichezea chezea halafu wameshamuonya wao waendelee kukaa hapo wakati wanajua kinachofuata na madhara yake. Sana sana watakuwa waliondoka fasta kwenda kutoa taarifa kunakohusika na kama ilifanyiwa kazi kwa wakati au laa mimi na wewe hatuwezi kujua. Shida ya watanzania wengi bado hawana macho ya kuona hatari mbele yao na hawachukui tahadhari mpaka yawakute. Siku zote ukishaona mtu mahali hasomeki halafu anachezea chezea silaha hata kama ni panga/kisu wewe sepa zako ikiwezekana katoe taarifa kunakohusika huko mbele ya safari lakini sio kuendelea kukaa karibu nae.
 
Huyu naye ni wa hapa hapa Sinza kwa Remi, ana bastola lakini ana akili kama za yule aliyeua, msijesema hatukuwaambia, enyi polisi, huyu hutoa silaha hadharani na kutishia.
Niya kweli au usijekuwa ni toy
 
na hizi taarifa mzitoe kwa uhakika,,,,sio ushaliwa kuku wako basi unatafuta vilipizi...toa taarifa kamili zitakazo saidia kutokutokea madhara menginbe.....sawa CHINEMBE.....???
 
Hivi wewe kwa akili zako watu wa usalama wapo baa wamuone mlevi ana silaha anaitotoa/anaichezea chezea halafu wameshamuonya wao waendelee kukaa hapo wakati wanajua kinachofuata na madhara yake. Sana sana watakuwa waliondoka fasta kwenda kutoa taarifa kunakohusika na kama ilifanyiwa kazi kwa wakati au laa mimi na wewe hatuwezi kujua. Shida ya watanzania wengi bado hawana macho ya kuona hatari mbele yao na hawachukui tahadhari mpaka yawakute. Siku zote ukishaona mtu mahali hasomeki halafu anachezea chezea silaha hata kama ni panga/kisu wewe sepa zako ikiwezekana katoe taarifa kunakohusika huko mbele ya safari lakini sio kuendelea kukaa karibu nae.
UKO SAHIHI....tunajichekesha hata kwenye hatari......ELIMU YA USALAMA WA RAIA MUHIMU MNO.....
 
Niya kweli au usijekuwa ni toy
Nyie ndio wake wanaotesti sumu kwa kuilamba. Whether ni yenyewe au toy it has nothing to do with your life mzee. Just kula kona hiyo wataprove watakaolambwa risasi.
 
Simaanishi kuwa atishie watu kwa bastola ila nimesema kuwa wana uwezo kwa kuwa kuna mtu amesema kuwa anajimwambafy aonekane ana hela. Ndio maana nikasema hela wanayo
Elewa quote brother, sijasema hana hela, nimesema anaweza asiwe na hizo pesa anazotaka watu wajue anazo. Nafikiri umenielewa!

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Viwanja vya sinza si vya kula bata..vimejaa washamba
 
Elewa quote brother, sijasema hana hela, nimesema anaweza asiwe na hizo pesa anazotaka watu wajue anazo. Nafikiri umenielewa!

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
Nimekuelewa ila wana hela hao kina Mungai hilo lazima tulitambue. Unachoongelea nimekuelewa sana. Yule dogo ndivyo alivyo kitambo ana mitabia ya ajabu ajabu toka anasoma na kipindi hiki wamerithishwa mali za mzee wao ndio vurugu mjini
 
Huyu naye ni wa hapa hapa Sinza kwa Remi, ana bastola lakini ana akili kama za yule aliyeua, msijesema hatukuwaambia, enyi polisi, huyu hutoa silaha hadharani na kutishia.
Taarifa zake huyu zilishafika maeneo husika zinafanyiwa kazi mda si mrefu kitamuumana..
 
Nimekuelewa ila wana hela hao kina Mungai hilo lazima tulitambue. Unachoongelea nimekuelewa sana. Yule dogo ndivyo alivyo kitambo ana mitabia ya ajabu ajabu toka anasoma na kipindi hiki wamerithishwa mali za mzee wao ndio vurugu mjini
Ninekupata, anakosea kuwachokoza wengine sasa, atakutana na vichwa panzi wataruka na kichwa chake.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Muliro kashamkamata leo huyo isac Robert maarufu wambura na anamchukulia hatua za kisheria ikiwepo kufutiwa umiliki
 
Wakurya bwana, Mwanza ni jiji bora Tanzania lenye kabila la wasukuma, wakarimu i think kuliko kabila lolote Tanzania. alakini baadhi ya wakurya na wachagga wanaiharibu mwanza, ukatili ukatili ukatili ukomeshwe. Heri wapunguzwe warudishwe kwao musoma na Moshi wawaachie jiji lao pendwa.
 
Muliro kashamkamata leo huyo isac Robert maarufu wambura na anamchukulia hatua za kisheria ikiwepo kufutiwa umiliki
Safi kabisa... Kuna Jamaa anaitwa Mshana wa Mwenge naye Kakamatwa alitishia Polisi na Bastola ya Kakaye. Wote wapo ndani
 
Back
Top Bottom