Sio kila mwanaume anaenda chooni kujisaidia, wengine kuangalia Salio. Mabinti kuweni makini sana na hizo ofa mtalia

Sio kila mwanaume anaenda chooni kujisaidia, wengine kuangalia Salio. Mabinti kuweni makini sana na hizo ofa mtalia

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Hili ni angalizo kuelekea wikendi.

Mabinti, msiwaamini sana wanaume! Kama mna hela, hakikisheni mnakabeba. Sio kila mwanaume anayeenda chooni anaenda kujisaidia, wengine huenda kuangalia salio lililobaki. Wengine wakiona bili ni kubwa, wanatafuta njia ya kutokea karibu na choo.

Nawaambia, mtaaibika! Hali si nzuri, wanaume siku hizi hawana mshipa wa aibu. Jana nimeona dada mmoja yamemkuta, walimng’ang’ania hadi tukachangishana kumsadia. Kibaya zaidi, tulilipa hadi vinywaji alivyokunywa maana alitelekezwa!

Hili lilinikumbusha kilichonipata mwaka 2018 kwenye baa moja Mikocheni. Nilipotoka kazini, shemeji yangu wa zamani aliniita nikaungane naye. Nilipofika, nilimkuta anakunywa na jamaa mmoja, akasema ni mfanyakazi mwenzake. Wakaniletea bia tatu na chakula, nikakula.

Ghafla jamaa akaondoka, nikamuita mhudumu niletewe bili yangu, shemeji akasema jamaa anarudi na atalipa zote. Ilipotimu saa tatu usiku, jamaa bado hapatikani. Nikamwambia shemeji yangu nalipa vya kwangu, akaniomba nisaidie zake, nikamwambia siwezi!

Mhudumu alileta bili yangu, nikailipa. Lakini yao ilikuwa shilingi 49,000! Akaja meneja, akasema tusiondoke mpaka polisi waje. Nikamwambia naondoka, na kama kuna tatizo, asome namba ya gari langu.

Nililipa nilichokula na kunywa, kisha nikazima simu. Baadae nikamhadithia kaka yangu, akacheka sana na kuniambia "ukome mteremko!"

Huyu sasa ni shemeji X kabisa! Sijui hata waliishiaje au kama aliniset na jamaa yake aliyekuwa naye.

Muwe makini na hizi ofa! Kama huna kitu mfukoni, jihadhari. Kukimbiana kwenye baa na klabu imekuwa michezo ya mjini kwa sasa. Mungu awalinde, wikendi njema!
 
Ukitokaa na pic km hii utembee na pesa ya kutosha mkuu ,c pesa ya kwenda kuchungulia chooni 😅😅😅

Wanaume tuna kazii sanaaa
JamiiForums194157065.jpeg
 
Nakumbuka when I was in my late 20s nilimuita demu akaja na rafiki Yake mmoja na mdogo wake mmoja halafu akawa anawaita wenzake wawili analazimisha waje utadhani yeye ndo analipa hela. You know what bili ikaja kama elfu Tisini na mbili nikamwambia mhudumu akaongeze bia moja moja ile mhudumu kaondoka nikawaambia jamani eeh Mimi nilimuita huyu hapa peke Yake ila mmekuja wengi mmeagiza hovyo hovyo. Mimi sina Hela hiyo kwa hiyo naomba tukimbieni wote tuanze mmoja mmoja, naanza mimi kuondoka na nyie nifuateni
 
kwa sasa wanawake wana shida nyingi sana, na hii yote inatokana na kutaka kuishi extravaganda lifetyle ambayo hawana uwezo wa kuimudu. Unakuta kapanga, yupo kwenye michezo mitatu ya elfu 2 kila siku, anadaiwa mikopo ya kausha damu, hapo bado hajala, hajapendeza, hajanunua bando la kuingia insta kila siku kupost picha akiwa kwenye lift, hotelini, swimming pool n.k kutaka kuonekana anaishi luxuryblife style, na unakuta hana kazi wala biashara ya maana

Linapokuja suala la kutengeneza circle na wanawake tuwe tunazingatia ilo eneo la finance. Tutengeneze circle na decent women vile vile kwenye masuala ya mitoko ni vyema kukubaliana kabisa ulipaji wa bill kabla ya kufika eneo la tukio.

Mimi binafsi sijawahi kupitia mambo kama haya kwa sababu nikiingia viwanja akija demu kuomba nimnunulie bia huwa namwambia wazi sina hela, na hapo simaanishi sina kitu mfukoni maana yangu ni kwamba kwenye bajeti yangu hakuna hela niliyotenga kwa ajiri yake.

Kama demu akiniomba tutoke out namdadisi kabisa kujua mfuko wake upoje nikigundua hayupo poa namwambia mapema kabisa aje peke ake.

Tusione noma ku-negotiate masuala ya bill
 
Kitu nimejifunza wanawake ni matapeli sana kuliko hata wanaume.
Mi Binafsi hata mtaani sitaki mazoea na Wanawake aka watu wa Vizinga na matepeli wa kimya kimya.
 
kwa sasa wanawake wana shida nyingi sana, na hii yote inatokana na kutaka kuishi extravaganda lifetyle ambayo hawana uwezo wa kuimudu. Unakuta kapanga, yupo kwenye michezo mitatu ya elfu 2 kila siku, anadaiwa mikopo ya kausha damu, hapo bado hajala, hajapendeza, hajanunua bando la kuingia insta kila siku kupost picha akiwa kwenye lift, hotelini, swimming pool n.k kutaka kuonekana anaishi luxuryblife style, na unakuta hana kazi wala biashara ya maana

Linapokuja suala la kutengeneza circle na wanawake tuwe tunazingatia ilo eneo la finance. Tutengeneze circle na decent women vile vile kwenye masuala ya mitoko ni vyema kukubaliana kabisa ulipaji wa bill kabla ya kufika eneo la tukio.

Mimi binafsi sijawahi kupitia mambo kama haya kwa sababu nikiingia viwanja akija demu kuomba nimnunulie bia huwa namwambia wazi sina hela, na hapo simaanishi sina kitu mfukoni maana yangu ni kwamba kwenye bajeti yangu hakuna hela niliyotenga kwa ajiri yake.

Kama demu akiniomba tutoke out namdadisi kabisa kujua mfuko wake upoje nikigundua hayupo poa namwambia mapema kabisa aje peke ake.

Tusione noma ku-negotiate masuala ya bill
Hili la mwisho neno muhimu SANA mkuu mkubaliane mapema bana una ngapi m na hiki

Kingine ulizen bei mapema m hiio issue ya bar mikocheni nilikunywa boa tatu kumbe Moja 3500. Nkajua 2000. BAHATI nilikuwa na Salio nkalipa

Moshi chips kuku ingawa n nyingi nkakutana na 17000. So kuuliza sio ujinga kabla amjajiandaa kuutumia
 
Back
Top Bottom