Sio Lazima Mzazi wangu awe Kada, Mimi kuwa mwana CCM kindakindaki

Sio Lazima Mzazi wangu awe Kada, Mimi kuwa mwana CCM kindakindaki

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Kama kijana nimekuwa nikipata maswali mengi sana toka kwa vijana wenzangu pale ninapojaribu kuonesha husia zangu au pale ninapotoa hoja zangu zinazoonesha kuiunga mkono iwe hapa ama mahali kwingine kokote.

Maswali hayo yamekuwa wakati mwingine yakiuliza chanzo changu cha hamasa ya Chama.

Unaweza kutana na maswali kama " wewe Mzazi wako nani CCM"

Swali hili limekua likinipa mawazo mengi , maswali ambayo moja wapo ni kama uanachama wa mtu katika chama cha siasa unazingatia kigezo cha mzazi kuwa sehemu ya chama husika.

Naishia kujuiliza nia hasa halisi ya swali hilo.

Historia ya vyama vingi hapa nchini inaonesha kwamba vyama vilivyopo sasa vimeanza 1992, na kabla ya hapo hakuwahi kuwepo vyama vya upinzani tunavyoviona sasa ukiachana na vile vilivyokiwepo nyakati za ukoloni.

sasa tukianza kusema kwamba ili uwe mwanachama wa chama flani cha siasa basi mizizi iaznie kwa mzazi, wanachama wengi wa vyama vya upinzani na hata waanzilishi watakosa sifa hiyo.

Tukija katika CCM pia iliyoanza 1977 baada ya muunganikonwa ASP na TANU tunaweza kuona kwamba wanachama wa CCM waanzilishi wangekosa sifa ya kuwa wanachama.

Hivyo basi hoja ya kwamba uanachama wa mtu na umuhimu wake unatokana na mizizi yake katika chama inakua ni hoja mfu isiyo na mantiki yeyote na ninaweza iona kama hali flani tu ya kujikweza na kushindilia ubinafsi uliopitiliza pale haswa lilapokuja swala la mgawanyo wa madaraka.

Binafsi ningependa kuona kauli hii ya kibinafsi inayotaka kujijenga katika vyama vyetu vya siasa ikipingwa na kila mzalendo anayelitakia mema Taifa lake kwa nguvu zote.

Niwatakia sikukuu njema ya Mapinduzi.

Wasalaam

Stroke.

Dar es Salaam.
 
Kwa nini hasa unaulizwa ni kutokana na wewe mwenyewe unavyokinadi chama ama kukipigania chama hali yako, familia yako mna njaa ya kufa mtu wakati Nape, Rizimoko na makamba wanakula teuzi wewe mfia chama kila siku umevaa shati la kijani na kofia ni hayo tu kwa leo na mko wengi usikate tamaa.
 
CCM ina wenyewe na wenyewe ndio wanalamba teuzi.
Ama kweli.

Basi ipo haja ya kukirejesha chama katika misingi yake

Ambayo ilikua ni kusimamia maslahi ya wote na sio wachache

Hasa hasa wakulima na wafanyakazi.

Ila hapo kati kati kimetekwa na wafanyabiashara na wapiga dili.
 
Kiufupi sema tu wewe ni msukule wa kijani,kama huna mzazi au ndugu aliyekipigania chama from the beginning au Wewe mwenyewe huna historical background ya kua mwanachama mkongwe mwenye ushawishi,Pesa au deals na wanakijani waliojichimbia mizizi pale chamani Kwa maslahi Yao binafsi
Sahau kabisa kuthaminiwa la si Hivyo utaungana na wale Misukule wengine wanaopewa kofia,Fulana na vitenge vya kijani Ili watumike kama chambo kipindi Cha maslahi makubwa ya chama mfano kampeni etc
NB
Mtu mwenye akili timamu huwezi kuwa CCM kama huna maslahi mapana pale na upo Kwa faida
Nje ya hapo wewe ni
MSUKULE wa kijani!
Bitter truth hutaki kufaaaa!
Chama kina wenyewe arif
😁😁😁😁😁
 
Ama kweli.

Basi ipo haja ya kukirejesha chama katika misingi yake

Ambayo ilikua ni kusimamia maslahi ya wote na sio wachache

Hasa hasa wakulima na wafanyakazi.

Ila hapo kati kati kimetekwa na wafanyabiashara na wapiga dili.
Hilo ndio unalijua Leo?
Kalagha bhaho!
 
Umelazimishwa au kushikiwa bunduki ?

Kama unaona huko hapafai na unataka kuwa Chamani either tengeneza kinachoenda na itikadi zako / jiunge kinachoendana na itikadi zako au kibadilishe hicho kiendane na itikadi zako (ila ukiona kwamba ni vigumu kubadilisha hivyo ni kwamba wengi wanakubaliana na kinachoendelea sasa which means Mkusanyiko huo haukufai)
 
Wenye ccm hawashindi huku wakipiga kelele, wao wanasubiri teuzi majina yako kwa saa100
 
Sema unahamasika Kwa nguvu ya ule mchango wa pale kijani, ama mukono kwenda Kwa kinywa, ama zile kofia na t-shirt.
 
Unajitambua....

Unajielewa vyema....

kongole kamarade👊

Tuko wengi "aila" yako!

CCM ni Zaidi ya chama nchini hapa.....

Bila ya CCM hakika Tanzania ITAYUMBA.......

#Siempre CCM🙏
 
Unajitambua....

Unajielewa vyema....

kongole kamarade👊

Tuko wengi "aila" yako!

CCM ni Zaidi ya chama nchini hapa.....

Bila ya CCM hakika Tanzania ITAYUMBA.......

#Siempre CCM🙏
Waimba mapambio wa enzi mpya, wenzenu wa awamu ile wamebwaga manyanga hata hawana hamu na uiimbaji mapambio Tena na bahati iliyoje wengine tayari Wana maumivu ya nafsi kwa waliyoyatenda⛹️.
 
Waimba mapambio wa enzi mpya, wenzenu wa awamu ile wamebwaga manyanga hata hawana hamu na uiimbaji mapambio Tena na bahati iliyoje wengine tayari Wana maumivu ya nafsi kwa waliyoyatenda⛹️.
🤣🤣Sawa....

Ninajulikana kwa kuimba uyaitayo "mapambio" toka niko chuo kikuu awamu ya 4 ,nikaendeleza awamu ya 5 ,na leo mwendo ni HUOHUO....SIBOI ,SIPOI....

Kwangu chama kwanza.....
Kwangu Mwenyekiti wetu wa taifa kwanza.....hata ukiwa ni wewe Mwenyekiti taifa ,nitakuimbia hayo "mapambio" 🤣🤣

#Siempre JMT🙏
 
🤣🤣Sawa....

Ninajulikana kwa kuimba uyaitayo "mapambio" toka niko chuo kikuu awamu ya 4 ,nikaendeleza awamu ya 5 ,na leo mwendo ni HUOHUO....SIBOI ,SIPOI....

Kwangu chama kwanza.....
Kwangu Mwenyekiti wetu wa taifa kwanza.....hata ukiwa ni wewe Mwenyekiti taifa ,nitakuimbia hayo "mapambio" 🤣🤣

#Siempre JMT🙏
Muda SII mrefu utaanza kuniimbia Mimi, ila ni kupitia katiba mpya ya mwananchi na kile chama msicho kipenda na kukiogopa zaidi. Kukusaidia TU, Kwa kuwa umekuwa mwazi sana sii kingine ila chadema🤸.
 
Muda SII mrefu utaanza kuniimbia Mimi, ila ni kupitia katiba mpya ya mwananchi na kile chama msicho kipenda na kukiogopa zaidi. Kukusaidia TU, Kwa kuwa umekuwajuani mwazi sana sii kingine ila chadema🤸.
Nini ?!!

😳😳CHADEMA ?!!!

Endelea kuota ukiwa juani 🤣🤣

#Siempre JMT🙏
#CCM na misingi kuntu ya Taifa letu🙏
 
Nini ?!!

😳😳CHADEMA ?!!!

Endelea kuota ukiwa juani 🤣🤣

#Siempre JMT🙏
#CCM na misingi kuntu ya Taifa letu🙏
Habari ndio hiyo, kama mlima umeweza kuhamishwa kutoka ndani ya ule mjengo na kusambaratishwa dakika 0.Nini kisicho wezekana chini ya jua, au hujui Dunia ni ya Mola 🤔.
 
Yaani mtu kudhihirisha mapenzi yake kwa chama bora ni uchawa?!!!😳😳

Basi hata ninyi ni machawa kwa mkionacho bora CHADEMA 🤣
Kwani nani kakuambia mie ni mwanachama wa chadema? Wenye kadi zetu tumetulia wala hatuna wasiwasi
 
Yaani mtu kudhihirisha mapenzi yake kwa chama bora ni uchawa?!!!😳😳

Basi hata ninyi ni machawa kwa mkionacho bora CHADEMA 🤣
Hiki ni chama timamu, hivyo no uchawa ila mapenzi ya kizalendo ⛹️.
 
Habari ndio hiyo, kama mlima umeweza kuhamishwa kutoka ndani ya ule mjengo na kusambaratishwa dakika 0.Nini kisicho wezekana chini ya jua, au hujui Dunia ni ya Mola 🤔.
Ni kweli dunia ni ya mola....tunalijua hilo.....je umepata habari ya "kitakatifu" kuwa CCM inaondolewa karibuni/katiba mpya kupitishwa?!!!🤣
 
Back
Top Bottom