Hio ni negative mindset tuliyonayo wafrika, tukiona ngozi nyeusi ambayo sio kabila letu linafanikiwa huwa tunalenga zaidi kuwasagia kunguni badala ya kujifunza kutoka kwao.
sipati picha kabila kama wasukuma wanaoongza kwa idadi kubwa ambao wapo takribani milioni 5 wangeyumia hii system.
Yani wangejikusanya wawe hata elf 10 tu basi wasingegusika
wasukuma elf 10 x 50,000 = milioni 500 pesa cash taslim kila mwezi
hio ni pesa nyingi mno, ni bilioni 6 kwa mwaka hio, hapo inatengwa bilioni 3 kwajili ya mitaji,nyingine inayobaki wanapeleka wale vipanga haswaa waende kusomea vyuo 10 bora duniani warudi na elimu za kisasa za kusaidia nchi ma jamii yao sio hizi elimu zetu za kikoloni, pesa nyingine ijenge madarasa huko vijijini, pesa nyinginr kusaidia wanafunzi wenye uwezo mkubwa kuendelea na vyuo vya hapa bongo waje kuwa wanasheria, madaktari, n.k.
ila ndio hivyo tena, mchawi anatafutwa ila huwa ni sisi wenyewe watu weusi, utakuta hata huo muungano ukiwa na watu 10 tu kila mtu anataka pesa iliyochangushwa imsaidie mdogo wake au kaka yake hata kama hawezi biashara.