Sioni tatizo lolote mtu kujiandaa kuwa Rais wa Tanzania mwaka 2030

Sioni tatizo lolote mtu kujiandaa kuwa Rais wa Tanzania mwaka 2030

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Mimi ni mwanachama wa CCM. Kwa sasa CCM ipo chini ya Samia ambaye pia ndio Rais wa JMT.

Kwa utaratibu waliojiwekea CCM ingawa haupo kwenye katiba ya chama au kanuni nyingine, mtu akiwa kwenye nafasi ya Urais kipindi cha kwanza, ni vizuri anaachiwa pia kipindi chake cha pili ili aweze kukamilisha sera zake na maono yake katika ujenzi wa Taifa. Ikitokea hataki yeye mwenyewe ndo chama kinakubali na kuweka mchakato wa kupata mwingine kama ilivyotokea kwa Idris Abdul Wakil kule Zanzibar miaka ile.

Hivyo kwa sasa ni wazi atakayependekezwa na chama CCM kugombea na kushika usukani 2025-2030 ni Rais wa awamu wa 6 Samia Suluhu Hassan. Endapo kuna mtu anataka kupambana nae kwa sasa ili ashike usukani 2025-2030 huyo bila shaka anaweza akawa anakiuka taratibu za chama ambazo ingawa hazijaandikwa popote ila chama kinaziamini haswa.

Kuhusu Mawaziri kujiandaa kuwa Marais 2030. Kwa hili sioni kosa lolote. Kwanza hili jambo ni zuri kwa sababu linawapa muda mzuri wananchi kumpima huyo mtu kwenye kila eneo kabla ya kumwamini na kumpa nafasi ya kuwa kiongozi Mkuu wa nchi.

Ningependa kuwashauri CCM kuunga mkono jambo hili na kutolichukulia kama uhaini kwa sababu hata kwao litakuja kuwapa faida hasa kwa kupata mtu sahihi kwa mazingira sahihi.

Kwa nchi nyingi Duniani viongozi hawaibuki kama uyoga tu ila wanapimwa kwa kipindi cha kutosha na pale wanapokuwa viongozi wanafahamika vizuri na wananchi wao.

Kwa Dunia ya sasa kiongozi mzuri lazima apimwe na wananchi wake hasa kwenye uwezo wake wa kifedha, Je, anaweza kutafuta fedha? Kuhusu maendeleo yake binafsi? Je, ana maendeleo ya kuridhisha binafsi? sio mtu anatuomba uongozi mkuu wakati hata yeye hakuwa na uwezo wa kujiletea maendeleo binafsi sasa atawezaje kuleta maendeleo kwa wengine?

Lazima tumjue kwa muda mrefu ili tumpime pia kifamilia kama Familia yake ikoje? anawaongozaje mke wake na watoto? Au mume na watoto maana kipimo kikuu cha uongozi kipo ktk ngazi ya familia. Lazima tujue pia uwezo.wake kiushawishi ktk kuifanya dunia ije Tanzania, ifanye biashara na Tanzania, iwekeze na kuleta mitaji Tanzania na kwa hilo hatuwezi kukiachia chama cha mapinduzi tu ndo kifanyw hilo.

Watanzania tunahitaji kuwajua wataka Urais kwa muda mrefu ili tupate muda mzuri kuwa assess hawa watu katika maeneo haya.

Hili pia litasaidia kupata kiongozi ambaye ni Mtanzania kweli na sio pandikizi. litasaidia pia kupata mtu mwenye afya njema ya akili maana kwa muda mrefu watu wattapata kujua historia yake vizuri.

Naomba kuwasilisha
 
Kwani kiongozi huwa anaandaliwa au anazaliwa?

Kuna watu walijiandaa mpaka maandalizi yanaisha na walikosa

Na kuna watu hawajawahi kujiandaa ila waliitwa tu, fulani njoo uje ukae kwenye kiti cha Urais au cheo fulani waliitwa tu kuja kukalia Kiti husika

Sasa ili usipoteze gharama na muda wako tafadhari usijiandae kama ipo ipo tu
 
Kwani kiongozi huwa anaandaliwa au anazaliwa?

Kuna watu walijiandaa mpaka maandalizi yanaisha na walikosa...
Acha kuleta nadharia zako. Tupe uthibitisho kuwa kiongozi anazaliwa?
 
Hayo maandalizi yao ya kuutaka Urais huoni kama yataharibu utendaji wao serikalini?

Mbaya zaidi, huoni kama hao mawaziri wakiachwa wanaweza kutumia vibaya nafasi zao walizopewa serikalini ili wajitengenezee mazingira ya kuupata Urais, ikiwemo vitendo vya rushwa na ufisadi visivyoisha?

Lakini pia, kama unasema taratibu zenu huko CCM ni kuachiana Rais aliyepo kipindi cha kwanza aachwe kumalizia kipindi cha pili, sasa kwanini unataka kuvunja hizo taratibu zenu mlizojiwekea?

Ukikubali kuwa mwanachama wa chama cha siasa, unatakiwa kufuata kanuni, taratibu, na miongozo mlizojiwekea, kama una doubt anything, peleka ushauri wako sehemu husika, kinyume na hapo, wewe ni msumbufu unaeweza kuwa influenced na kundi mojawapo linaloutaka huo Urais.
 
Kwa nini CCM iliweka huo utaratibu wa mtu akiwa Rais kipindi cha kwanza anapewa na kipindi cha pili ?? Kwa nini huo utaratibu haukuewkwa kwenye ubunge na udiwani??
 
Hii nchi CCM hamna Hati miliki, yaani mazoea tayari mmshejipanga mtatawala milele, uzuzu wa watanzania ndio turufu yenu, mmeua elimu kwa makusudi wakati watoto wenu wana soma nje ya nchi ili waje watawale vihiyo waliosoma kayumba schools, aliyeanzisha UPE, sekondari za kata, hata vitukuu vyao havisomi huko, wake up !
 
hii nchi ccm hamna Hati miliki, yaani mazoea tayari mmshejipanga mtatawala milele, uzuzu wa watanzania ndio turufu yenu, mmeua elimu kwa makusudi wakati watoto wenu wana soma nje ya nchi ili waje watawale vihiyo waliosoma kayumba schools, aliyeanzisha UPE, sekondari za kata , hata vitukuu vyao havisomi huko, wake up !
One-day tutawafanyia Surprise hawataamini. Mbwa hawa
 
Hayo maandalizi yao ya kuutaka Urais huoni kama yataharibu utendaji wao serikalini?

Mbaya zaidi, huoni kama hao mawaziri wakiachwa wanaweza kutumia vibaya nafasi zao walizopewa serikalini ili wajitengenezee...
Tupe uthibitisho yanaharibuje utendaji serikalini?

Mtu kujiandaa kuwa Rais kunaongezaje vitendo vya Rushwa? Rushwa zinazotokea siku zote zinatokana na Watu kujiandaa kuwa Marais?
 
Kwa nini CCM iliweka huo utaratibu wa mtu akiwa Rais kipindi cha kwanza anapewa na kipindi cha pili ?? Kwa nini huo utaratibu haukuewkwa kwenye ubunge na udiwani??
Utaratibu huu haujawai andikwa popote so hata wakitaka kuuondoa kesho wanaweza kuuondoa
 
Lord Denning said:
Kwa utaratibu waliojiwekea CCM ingawa haupo kwenye katiba ya chama au kanuni nyingine, mtu akiwa kwenye nafasi ya Urais kipindi cha kwanza, ni vizuri anaachiwa pia kipindi chake cha pili ili aweze kukamilisha sera zake na maono yake katika ujenzi wa Taifa.
Kama CCM ilivyozoea kuiba kura, ni mazoea tu, hawaoni tena ubaya wa kufanya hivyo. Mazoea yana tabu. Kama mwizi anaweza kuachiwa aibe tu kwani ni kawaida yake...hivi wana CCM, akili huwa mnazifungia wapi? Eti kwa sabau ni mazoea, yaendelee kuwa hivyo hivyo, ushetani mtupu!
 
Fanya kazi wapimaji na wapiga kura watakupima muda ukifika kupitia hizo kazi ulizokuwa ukifanya. Kufanya kampeni kabla ya muda si sawa kwa sababu:

Kunaweza kumtoa mhusika katika malengo ya msingi anayoelekezwa na serikali, akajikita kwenye malengo ya uraisi ambao hajui kama ataufikia.

Kunaweza kutengeneza makundi ya utendaji kila kundi likiwa tiifu kwa anayeaminika ana nafasi kubwa ya kuwa raisi.

Kunaweza tengeneza mtia nia mwenye nguvu nje ya nguvu ya mamlaka halisi ya raisi aliyepo madarakani. Kiongozi asiye rasmi ndani ya serikali.
 
Hayo maandalizi yao ya kuutaka Urais huoni kama yataharibu utendaji wao serikalini?

Mbaya zaidi, huoni kama hao mawaziri wakiachwa wanaweza kutumia vibaya nafasi zao walizopewa serikalini ili wajitengenezee mazingira ya kuupata Urais, ikiwemo vitendo vya rushwa na ufisadi visivyoisha...
Nani kasema utaratibu uvunjwe 2025? Umesoma kweli mada na kichwa cha mada? Au umekurupuka tu kujibu kama kawaida yako?
 
Fanya kazi wapimaji na wapiga kura watakupima muda ukifika kupitia hizo kazi ulizokuwa ukifanya. Kufanya kampeni kabla ya muda si sawa kwa sababu...
Nani kakwambia uongozi wa juu wa nchi unapimwa kwa kazi tu?

Hata vichaa wanachapa kazi. Kuna video vingi sana vya kumpima mtu na hiwezi kuvitimiza vyote ndani ya muda mfupi
 
tuko 2022 ila michumia tumbo inawaza urais 2025 badala ya kuwaza iyo 2025 kama nchi inatakiwa tuwe tumepiga hatua gani kimaendeleo...

Maana yake hata baada ya hiyo 2025 akili yote itahamia 2030 kuuwaza urais sasa unaona kuna nchi hapo?
 
Kwa nini huu utaratibu ambao haujawahi kuandikiwa popote uliwekwa kwa kuanzia?
Sababu ni zipi?
Utaratibu huu haujawai andikwa popote so hata wakitaka kuuondoa kesho wanaweza kuuondoa
 
Nani kakwambia uongozi wa juu wa nchi unapimwa kwa kazi tu?

Hata vichaa wanachapa kazi. Kuna video vingi sana vya kumpima mtu na hiwezi kuvitimiza vyote ndani ya muda mfupi
Kazi unaitafsiri vipi? Vitu vingi sana ambavyo sio kazi ni vitu gani?

Katiba yetu inataka candidates wasiwe vichaa hivyo hakuna umuhimu wa kuwazungumzia vichaa.
 
Kwa nini mbunge na diwani haawachiwi kipindi chake cha pili ili aweze kukamilisha sera zake na maono yake katika ujenzi wa jimbo lake??
Utaratibu huu haujawai andikwa popote so hata wakitaka kuuondoa kesho wanaweza kuuondoa
 
Back
Top Bottom