Sioni umuhimu wa daraja la Aga Khan - Coco beach kwa sasa

Sioni umuhimu wa daraja la Aga Khan - Coco beach kwa sasa

Wewe hujui barabara za huku Mikocheni,Mbezi beach,Msasani,Masaki. Kwa taarifa yako jinsi foleni inavyokuwa kali watu wa mikocheni au mbezi walikuwa wanaingilia maandazi road(siku hizi kuna barabara ingine ya DMDP unaingilia Tanesco Mikocheni unatokea Msasani) wanapita CCBRT wanatokea O'bay kuja kukatisha Kenyatta Drive ili kukwepa foleni ya Ali Hassan Mwinyi road. Kwa maana hii watatumia njia hio hio ila hawatarudi Kenyatta tena wataunganisha darajani. Hili daraja sio kwa watu wa Masaki tu acheni negativity.

Maneno haya haya yalisemwa wakati daraja la Kigamboni linajengwa na hadi leo watu wasiolitumia bado wanaongea ujinga kuwa daraja halina msaada wowote. Waulize wakazi wa Kigamboni wanaotumia hilo daraja wawaambie umuhimu wake.
Tofautisha umuhimu wa daraja la Kigamboni na hili, population ya Kigamboni ni kubwa activities zake ni nyingi na huko Kigamboni inakwenda kuwa manispaa.

Unataka kusema mtu wa mbezi beach akishashuka cocobeach foleni ndiyo inakwisha sidhani, ndiyo maana nimesema ni daraja la wakazi wa Masaki tena lingeitwa Masaki bridge.
 
Ndio matatizo ya kuongoza na kufanya mamiradi bila vision.... Tunapoteza pesa nyingi kwa miradi isiyo na faida wala tija.

Je kuna malori ya mizigo yanapita daraja hilo? Hakuna. Zaidi ya waenda majumbani na maofisini ambao wala hawana tatizo la foleni kiivyo
Mkuu wewe ni bonge ya Kilaza ayseeee "Waenda Maofisini wanaokaaa foleni muda mwingi hawana tija Kiuchumi"??
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni watu wachache sana, (under utilised bridge).

Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.

Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.
Kwanza nikuhakikishie serikali haikurupuki hata kidogo miladi mingi huifanyia tafiti kwanza na makosa kama yapo huanzia hapa watafiti wengi ni makanjanja hivyo hutoa matokeo yasiyo halisi na kwa kuwa ndizo tafiti pekee tulizo nazo serikali lazima izifanyie kazi.

Kingine hii miradi haizuii mingine kwamba mradi wa salanda utazuia wa jangwani hapana, wewe kama kilio chako ni jangwani sema tu tunahitaji dalaji jangwani pia? kwani kazi ya serikali ni ipi?
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni watu wachache sana, (under utilised bridge).

Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.
Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.

Serikali ya Tanzania inachangia asilimia kumi na Tisa19% na pesa yote inatolewa na serkali ya Korea sasa sie tukatae wakati ni faida kwetu?
 
Tofautisha umuhimu wa daraja la Kigamboni na hili, population ya Kigamboni ni kubwa activities zake ni nyingi na huko mbweni Kigamboni inakwenda kuwa manispaa.

Unataka kusema mtu wa mbezi beach akishashuka cocobeach foleni ndiyo inakwisha, ndiyo maana nimesema ni daraja la wakati wa Masaki tena lingeitwa Masaki bridge.
MTU wa mbezi beach akifika mwai kibaki anakutana na foleni
 
Kwahio hawa wengine wa Masaki,O'bay,Msasani,Mikocheni sio waTz?
Oysterbay ,Masaki wanakaa wazungu na viongozi wa serikalini ,ambao wengi wana magari binafsi,hawana tabu za madaladala,lakini huko uswekeni wakijenga daraja hil la mkwajuni-muhimbili hapa kati tunapiga lege tu TZ 11 ambapo ni shortcut kwahiyo nauli nauli za kwenda KKo/Posta zinapungua.
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni watu wachache sana, (under utilised bridge).

Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.

Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.
Ndio maana huoni umuhimu wa kukarabati ofisi yetu ya makao makuu pale ufipa. Sasa naanza kuelewa.
 
Watalii wanatakiwa wasiathirike kabisa na 'traffic jam'. Kwa hiyo kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Nyerere, kupitia kwenye flyover ya TAZARA, kupitia hilo daraja la Masaki, mpaka mahoteli ya ufukweni inatakiwa mtalii atembee kama yuko ma'ulaya hivi!
 
Kwanza nikuhakikishie serikali haikurupuki hata kidogo miladi mingi huifanyia tafiti kwanza na makosa kama yapo huanzia hapa watafiti wengi ni makanjanja hivyo hutoa matokeo yasiyo halisi na kwa kuwa ndizo tafiti pekee tulizo nazo serikali lazima izifanyie kazi.

Kingine hii miradi haizuii mingine kwamba mradi wa salanda utazuia wa jangwani hapana, wewe kama kilio chako ni jangwani sema tu tunahitaji dalaji jangwani pia? kwani kazi ya serikali ni ipi?
Sawa hoja yangu pia imejikita kwenye kipaumbele, kipi bora kianze daraja la salenda au la jangwani, tayari tunajua madhara ya jangwani wakati wa mvua mabasi ya mwendo kasi yalisimama kwa wiki nzima ni hasara kiasi gani ilitokea.
 
Ivi mbona nyie kaz yenu kupinga tu kila jambo? mtu unakaa kwa mtogole utaujua saa ngapi umuhimu wa barabara hii...mimi naishi kunduch na ili kukwepa foleni huwa nikifika moroko naingia msasani then oysterbay then narudi salenda...sasa kwa daraja hili ina maana nitainyoosha moja kwa moja via daraja jipya...ebu tuacheni jamani...mbona kigamboni wana kivuko wana njia ya kongowe na still walipewa daraja??
 
Aghakhani to O'bay tuwe wakweli hilo daraja la ni wadosi - foleni yetu kwenye taa za salender itabakia palepale.
 
Ndio matatizo ya kuongoza na kufanya mamiradi bila vision.... Tunapoteza pesa nyingi kwa miradi isiyo na faida wala tija.

Je kuna malori ya mizigo yanapita daraja hilo? Hakuna. Zaidi ya waenda majumbani na maofisini ambao wala hawana tatizo la foleni kiivyo
ndugu,foleni dar inapoteza mabilioni ya shilingi kwa siku,kuna kipindi hiyo barabara mitaa ya kino pale,kasi ya gari ilikua 16km/h..
 
Hilo ni tatizo lako binafsi linalotokana na mtazamo wako hasi kwa Serikali iliyopo madarakani
 
Hilo ni tatizo lako binafsi linalotokana na mtazamo wako hasi kwa Serikali iliyopo madarakani
Endelea na upofu wako tunajua kwasasa huwezi kuhoji chochote acha tulio huru kifikira tuhoji.
 
Huu ujinga wa kutengenezeana flyover za urefu wa kama pale Tazara halafu kutangaza zinasaidia kupunguza foleni ni kusababisha Tanzania nzima kuonekana machizi
fly over ya TAZARA ni kwa ajili ya wanaokwenda AirPort. Gongolamboto wameponea hapo. WaMandela rd wataendelea kulia na pini ya Buguruni mataa. Uliangalia kwa jicho la 3 hii Miradi ina UKAKASI
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni watu wachache sana, (under utilised bridge).

Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.

Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.

ingependeza zaidi kuondoa kero ya mafuriko Jangwani
 
Back
Top Bottom