Sipendi ugali kabisa na ninaishi

Sipendi ugali kabisa na ninaishi

Wali nikiula siku mbili mfulululizo huwa nakinai .

Vyakula vya ngano nikivila huwa vinanikereketa na kusababisha kutibuka kwa tumbo.

Ugali sijawahi kuukinai kiasi kwamba hata kipindi cha ramadhan namwambia wife anipikie ugali kama futari au daku.
Lengo lako Ni bajet na unataka mabonge ya unga yashike tumboni ..nimeshakuona mfuko wako Ni mfupi
 
Katika vyakula ambavyo huwa sivishobokei ni Ugali mimi siupendi kabisa yaani sina stim nao kabisa.

Sazingine huwa nakula tu ndo wife au beki3 kaandaa lakini kiukweli ugali sio chakula nachokipa thamani japo familia yangu mke na watoto wanaupenda balaa.

Ni mara kibao nikirudi nyumbani nikikuta wamepika ugali nitapitiliza tu chumbani kulala au nitaomba wanitafutie mbadala.

Na mara nyingi wakiwa wanaandaa huwa wanajua kabisa kwahiyo mbadala lazima iwepo.

Sazingine huwa nakula tu ili siku ipite lakini ni chakula cha hovyo kabisa, mimi naweza kukaa hata mwaka nisile ugali na nikaona fresh kabisa.

Ni kawaida kwangu siku hizi kukaa wiki au wiki mbili bila kuutia ugali mdomoni.

Kuna kitu huwa kinanishangaza sana, kuna watu wanakula ugali mchana na usiku tena siku 7 za wiki duuuh tena ugali na yale madagaa ya ziwa victoria!! Sio kwa nia mbaya au nina ego hapana mimi ugali hapana bora nile ndizi mwezi nzima lakini sio ugali.

Mwanaume unajisifia kupenda zege utakuja kupopolewa.
 
Asbh,
soseji mbili na mayai mawili ya kuchemsha na tende mbili na karanga kiganja kimoja...
Nashushia maziwa au natural juice au artificial I.e Ceres au Azam mango...

Mchana,
Wali au ugali Ina depend na mood ya siku iyo...
Maji lita Moja

Usiku,
Ugali au wali na nyama au kuku au samaki au dagaa au chair fire au maini

Hii ndio Recycling sio Siri inachosha hii Recycling

Ingependeza tupate mawazo tofaut tofaut ya kupangilia mlo 😊😊😊😊
Sasa unatakiw u explore other food lines
Kuna
1. Kande
2 Ndizi labla za maharage au ndizi nyama au ndizi za kupikia maziwa mtindi.....kuna mapishi mengi ya ndizi
3. Wali nao una mapishi mengi mfano biriani, pilau, mseto, njegere
4. Kuna tambi na vyakula vya ngano
5. ugali na mboga zake aonuna ufundi mwingi mno

huwa napenda kupika vyakula vipya na wife jikoni Inatuweka karibu sana.
 
Katika vyakula ambavyo huwa sivishobokei ni Ugali mimi siupendi kabisa yaani sina stim nao kabisa.

Sazingine huwa nakula tu ndo wife au beki3 kaandaa lakini kiukweli ugali sio chakula nachokipa thamani japo familia yangu mke na watoto wanaupenda balaa.

Ni mara kibao nikirudi nyumbani nikikuta wamepika ugali nitapitiliza tu chumbani kulala au nitaomba wanitafutie mbadala.

Na mara nyingi wakiwa wanaandaa huwa wanajua kabisa kwahiyo mbadala lazima iwepo.

Sazingine huwa nakula tu ili siku ipite lakini ni chakula cha hovyo kabisa, mimi naweza kukaa hata mwaka nisile ugali na nikaona fresh kabisa.

Ni kawaida kwangu siku hizi kukaa wiki au wiki mbili bila kuutia ugali mdomoni.

Kuna kitu huwa kinanishangaza sana, kuna watu wanakula ugali mchana na usiku tena siku 7 za wiki duuuh tena ugali na yale madagaa ya ziwa victoria!! Sio kwa nia mbaya au nina ego hapana mimi ugali hapana bora nile ndizi mwezi nzima lakini sio ugali.
Ugali wa unga wa mahindi yaliyokobolewa ni wanga (starch) tu, hauna virutubisho.

Ni chakula cha kukupa nishati tu, hakina virutubisho.

Bora hata ugali wa mahindi yasiyokobolewa, dona, una protini.

Kukoboa mahindi kunaondoa protini kwenye ugali.
 
Sasa unatakiw u explore other food lines
Kuna
1. Kande
2 Ndizi labla za maharage au ndizi nyama au ndizi za kupikia maziwa mtindi.....kuna mapishi mengi ya ndizi
3. Wali nao una mapishi mengi mfano biriani, pilau, mseto, njegere
4. Kuna tambi na vyakula vya ngano
5. ugali na mboga zake aonuna ufundi mwingi mno

huwa napenda kupika vyakula vipya na wife jikoni Inatuweka karibu sana.
Nimejifunza hapa.....

Madini sana😊😊
 
Ugali wa unga wa mahindi yaliyokobolewa ni wanga (starch) tu, hauna virutubisho.

Ni chakula cha kukupa nishati tu, hakina virutubisho.

Bora hata ugali wa mahindi yasiyokobolewa, dona, una protini.

Kukoboa mahindi kunaondoa protini kwenye ugali.
Kwaio ugali unadumaza akili 😊😊😊😊😊😊😊

Najua una exposure kubwa unaweza uka share mataifa mengi ya ulaya na Asia hata Amerika Huwa hawapendi kutumia hii nafaka katika Milo Yao....
 
Mwanaume unajisifia kupenda zege utakuja kupopolewa.
Mkuu ukitaka kujua ugali hauna hadhi NDIO maana kwenye masherehe.................

Siku ukihudhulia sherehe mf. Harusi alafu ukajiandaa kisaikolojia utakula biriyani au pilau au hata wali wa maji alafu ukakuta ugali harusini.....🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂😂
 
Mkuu ukitaka kujua ugali hauna hadhi NDIO maana kwenye masherehe.................

Siku ukihudhulia sherehe mf. Harusi alafu ukajiandaa kisaikolojia utakula biriyani au pilau au hata wali wa maji alafu ukakuta ugali harusini.....🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂😂
Hiyo inategemea sehemu na sehemu..nenda kwa wakurya au wasukuma huko utakuta ugali upo kwenye menu siku ya sherehe. Hadhi ya chakula hutegemea na watu wa sehemu husika wanapendelea nini zaidi.
 
Hiyo inategemea sehemu na sehemu..nenda kwa wakurya au wasukuma huko utakuta ugali upo kwenye menu siku ya sherehe. Hadhi ya chakula hutegemea na watu wa sehemu husika wanapendelea nini zaidi.
Ndomana kanda ya ziwa wengi vilaza
 
Ugali hapana ni siupendi toka nipo kwetu, siwezi poteza hela yangu kula ugali.Hata watoto wangu hulalamika kula ugali hivyo substitution yake ni macaroni na spaghetti
Macaroni na sphagetti ndo vyakula gani mkuu, kapicha please nivijue!
 
Ahaaaa embu kwana nicheke maana nina ka shoga kangu ka marekani kalikuja juma mosi kwangu kameondoka jana ila nimekoma yaani hawa watu vyakula vyao nadhani viko hotel kubwa.

Juma mosi usiku saa 5 kananipigia kanataka kuja kulala kwangu kako bored kwakwe hakajui kiswahili hakana wa kuongea nae kana jua "mambo" tu so kakaj kwangu.

Usiku huo mimi nilipika ndizi ahaaaaa kwani kalikula? Kakanywa chai tukalala.

Asubuhi nawaza nikapikie nini? Nikawaza mayai, kweli kalikula mayai na chai chai yenyewe hata kikombe hakawezi maliza.

Mchana nikakapikia chips, kakadono🤣

Mimi nikajipikia ugali tukala na shoga yangu mwingine, ahaaaa ndo kanauliza " Luckyline what kind of food is this? 😅 kanashangaa kweli kananisimulia marekani wengi hawaopiki wanachukua vyakula ambavyo viko tiyari na wanakula junk foods mara nyingi.

Hapo nilimuita shoga yangu aje nina mgeni basi kila kitu janashangaa na kuuliza kakasema kenyewe kanakula hotelin almost every day.

All in all nimefurahi kuwa nae tumeenjoy ila kumbe ni kazi kiasi hiki kuongea kiingereza siku mbili mfululizo? Yesuuuuuu nyie.🤣

Shoga yangu alivyokuja kukasalimia nikaona ananiangalia mashavu nikamuuliza vip? Ati hujavimba? Unawezaje kuongea na huyu kiunbe ambae hajui kiswahili.

Kuna wakati niliwaacha nikaenda dukani kufata soda mara shoga akanitumia sms " shoga wahi ubaki na mzungu wako mimi hii lugha nakaaga nayo mbali" nyie🤣

Kwa bongo hii tumejizoea kuongea kiswahili na viluga vyetu huko kijiji tukipiga simu lisaa tunaongea kiluga leo mtu anakuongelesha kimarikia siku mbili sio mchezo.

Mkiona mtu siku nzima huko ofisin anaongea kiingereza msimchukulie poa mpeni heshima zake. sio rahis kama mnavyo dhani.

Kuna rafiki yangu ni mbongo yeye halagi ugali anasema ugali ni chakula cha nguruwe. Anakula wali jan-dec
Uwiii mtoto wangu kila nikiongea ananiambia speak English, nikajisemea kimoyomoyo manina kweli weee pesa yangu mwenyewe unaniendesha nayo mxiiiuu.
 
Back
Top Bottom