Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA

Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA

Vitabu vya bibilia havipo kwa ajili ya kila mtu, kila kitabu kipo kwa ajili ya jamii fulani ya watu na kizazi fulani. Waumini wa leo huosoma mambo waliyoambiwa wayahudi kuendana na tamaduni zao na lugha zao na kuzileta kwenye tamaduni zao kwa lugha tofauti na walengwa. Lugha ni utamaduni, tafsiri ni ubatili kwa baadhi ya maneno. Ivyo baadhi ya vitabu tuvisome tu kama riwaya.

Vile vyenye ujumbe kwa watu wote (vichache) ndo vituongoze hasa mafundisho ya paulo maana yeye alisafiri mabara yote akifundisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimepata pia kuiona injili ya Barnaba (the Gospel of Barnabas) ila haimo kwenye Biblia. Jee hii nayo imetolewa au haikuwemo tangia awali?
 
Nimepata pia kuiona injili ya Barnaba (the Gospel of Barnabas) ila haimo kwenye Biblia. Jee hii nayo imetolewa au haikuwemo tangia awali?
Mkuu hiki kitabu hakikuwepo wakati huo biblia inakuwa compiled maana kimepatikana karne ya 17 ilihali biblia ilishakuwa compiled zaidi ya miaka 1000 kabla hakijapatikana. Hivyo kwa kujibu swali lako ni kwamba hakikutolewa kwenye biblia maana hakikuwahi kuwepo kwenye bible kwa sababu niliyotoa hapo juu.
 
Nimefurahishwa saana kwa huu ufafanuzi.....
Tatizo watu wa GT wanazani wamesoma kila kitu wamemaliza kumbe si kweli, wengi ni vi 'hoja' wanaokoteza kwa wafuasi wa mashetani na kuja kupotosha watu.

Mleta mada ameleta mada vikorishi kwa watu wasiojua maandiko wala imani.

Biblia ni kitabu kilicho vuviwa kila moja kwa wakati wako ila kwa dhumuni moja tuu kama kuna vilivyo acjwa maana dhumuni ni tofauti na hivi vingine ambavyo Mungu alikusudia vitufikie.

Kama zama hizo manabii haikua rahisi kuwaamini mpaka kujaribiwa wengine unadhani ni waongo wangapi waliibuka wakijifanya wanatoka kwa Mungu?? Na ndio maana Mtume s.w.a anawaambia waislamu Quran imekamilishwa na taorati, zaburi, injili pamoja na Quran yenyewe kwakua msingi wa Imani kwa Mungu wa kweli ni kutoka kwa wayahudi kama taifa teule.

Biblia kwangu ni kitabu kisicho na shaka bali ni kimbilio na majibu ya maswali yangu yoote maana hata hichi kuulizwa juu ya kweli kutiliwa shaka ilashanijulisha.

Wakristo tusome biblia, waislamu tusome biblia na Quran.
Umeleilewa kweli hilo bandiko?
 
Shida na wewe mtoa mada biblia bado hujaielewa na tafisiri ndio shida kwako',mfano ukisoma mathayo 4:1-11 ni kweli alifunga siku 40 lkn Yohana 2:1haisemi siku tatu baada ya kubatizwa yesu alikuwa kwenye harusi ya Cana!!bali inasema na siku ya tatu palikuwa na harusi huko Cana(kana)na mama yake Yesu alikuwepo.)-yohana hajasema siku tatu baada ya ubatizo rejea kwenye biblia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisayansi unapata vip usiku na mchana bila ya jua..!
Mimea inastawi vip bula uwepo wa jua
Biblia kwenye sayans ya leo ime fail sana kwa sayans ya kawaida kabisa...kina sehem inasema dunia ni duara kuna sehem inasema dunia tambarare ukikubaliana na hoja zote inamaana dunia ipo kama disc.!

Sent using Jamii Forums mobile app
lengo la biblia sio kujibu sayansi na wala biblia haipo ili kueleza na kutatua matatizo ya sayansi.

biblia ipo ili kufafanua na kueleza kweli za kiimani pekee. kweli kumuhusu Mungu. waandishi wa izo kweli za kiimani wamezifafanua kulingana na mazingira, maisha, maarifa, elimu na sayansi ya watu wa nyakati zile wakati kitabu husika kinaandikwa na sio leo. pia kweli hizo ili zieleweke hazina budi kuwepo katika lugha ya kibinadamu yenye mapungufu mengi tu kama ambavyo mwanadamu mwenyewe asivyo mkamilifu mia kwa mia.

"inapoishia sayansi ndipo imani inapoanzia"
 
Shida na wewe mtoa mada biblia bado hujaielewa na tafisiri ndio shida kwako',mfano ukisoma mathayo 4:1-11 ni kweli alifunga siku 40 lkn Yohana 2:1haisemi siku tatu baada ya kubatizwa yesu alikuwa kwenye harusi ya Cana!!bali inasema na siku ya tatu palikuwa na harusi huko Cana(kana)na mama yake Yesu alikuwepo.)-yohana hajasema siku tatu baada ya ubatizo rejea kwenye biblia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimetoa mifano mingi tu hivyo haitakuwa vyema tukianza debate mstari mmoja tu mfano unaweza pia kunisaidia na hapa Je yakobo alizikwa wapi??

Mwanzo 50:13
13 kwa kuwa wanawe wakamchukuwa mpaka nchi ya Kanaani, nao wakamzika katika pango ya shamba la Makpela, iliyo mbele ya Mamre, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake pa kuzikia

Matendo 7:15-16
15 Basi Yakobo akashuka mpaka Misri; akafa yeye na baba zetu;
16 wakachukuliwa mpaka Shekemu wakazikwa katika kaburi lile, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa kima cha fedha kwa wana wa Hamori, huko Shekemu
.

Je nani ni mkweli kati ya Stephano au Musa??

Na je kama kuna mgongano mtu akihoji je kama vitabu vyote vya biblia vilivyoachwa vina uvuvio wa roho mtakatifu (sababu iliyotumika kuvifuta vingine) kivipi taarifa muhimu kama hizi zikinzane ilihali vimevuviwa na Roho mtakatifu ambaye hawezi kusahau kama sisi wanadamu??

Ntashukuru ukinisaidia na jibu ili niweze kuielewa Biblia kama wwe
 
Aende makanisani akaonane na wachungaji kama kweli ana nia ya kujifunza.

Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app
Mkuu JF imewekwa kwa ajili ya mambo kama haya kushare mawazo na mada tofauti ili kuongeza maarifa na kuelimishana na humu kuna wachungaji wengi tu na watu wenye uelewa wa biblia ndio maana nkianza mada za kidini huwa nawatag ingekuwa hivyo JF ifungwe maana jukwaa la siasa mngesema wakaulize maswali yao kwenye vyama .... Jukwaa la biashara ungesema waende kariakoo sokoni n.k ni vizuri kama kitu hukifahamu kiache wanaojua watakuja ndio maana kuna watu nimewatag so kama haupo interested unaiacha tu au kama una majibu unatoa sio unakuja humu kutoa kejeli tu na matusi unakuwa hausaidii wanaotaka kujifunza.
Soma mwazo 50:9 mpka 15 utaelewa.hakuna contradiction yoyote zaidi ya maelezo yanayofanana na yanayozungumzia kisa hicho hicho cha kifo cha baba yake yusuph ndo maana mandiko yote mawili yanajibu ahadi ibrahim aliyopewa na MUNGU.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimesoma ila inataja yakobi kazikwa Macpelah mwingine anasema kazikwa shechem ambayo miji hiyo bado ipo na ni maenwo tofauti kabisa! Hapo bado makabila yaliyouza hayo makaburi mmoja ni Mhiti ila Stephano anasema ni amorites sasa hayo ni makabila tofauti kabisa yanayotajwa kwenye mwanzo 10 kama wana wa Canaan sasa kwanini kuwepo discrepancy kama hizi kama kitabu kina uvuvio wa Roho mtakatifu??

Naomba unisaidie kunielewesha
 
Ukitumia akili zako kuisoma biblia hakika hutaielewa biblia.Jitaidi sana uombe roho mtakatifu akufundishe akuonyeshe na akupe tafsiri ya yalioandikwa kwenye biblia.Mwisho biblia ujue imeandikwa kwa kuongozwa na roho mtakatifu,kuna maono kwenye biblia hivyo ni ngumu kutumia akili zako kuielewa biblia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukitumia akili zako kuisoma biblia hakika hutaielewa biblia.Jitaidi sana uombe roho mtakatifu akufundishe akuonyeshe na akupe tafsiri ya yalioandikwa kwenye biblia.Mwisho biblia ujue imeandikwa kwa kuongozwa na roho mtakatifu,kuna maono kwenye biblia hivyo ni ngumu kutumia akili zako kuielewa biblia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na hii ndio shida sasa ulikuja spidi ukasema sielewi biblia nakupa mstari unieleweshe unadai nasoma kwa akili zangu!! Sasa mtu kaandika Nyerere kazikwa Butiama alafu mwingine kaandika nyerere kazikwa Kisarawe alafu nikiuliza naambiwa natumia akili za kawaida?? Mbona hamkusema hivyo kwa book of Enoch au Gospel of Judas??

Embu pitia hii thread taratibu mpaka mwisho alafu urudi na kejeli zako maana shida mtu akihoji anaonekana mpagani!!

Zifahamu siri 7 zilizofichika kuhusu sikukuu ya Pasaka - JamiiForums
 
Kuna watu wanafurahishwa sana na hekaya za abunuasi hata wengine kuamini ni kweli . Mf . Unaambiwa shikilia ghorofa ya juu nabomoa ya chini . Ni kichekesho lakini ni hadithi tu !! The same to Bible . Gharika kuu , uumbaji , ( ufufuko - not a historical event ) . Ni kulingana na mawazo yangu japo mtaniona mwehu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kwamba sijakuelewa bali hata nikikuelewesha bado utatumia akili zako kutafuta majibu!:Ndio maana nimekujibu kwa ufupi kwamba ili uijue biblia omba roho mtakatifu akufumdishe utaielewa vizuri!,Kwa ufupi ni roho mtakatifu afundishaye kila anayeitaji kujifunza biblia si mwanadamu maana mwanadamu naye majibu anayotoa kwa roho mtakatifu.

Naomba usifikirie kwamba nimekukejeri bali nakupa mwongozo usitafute majibu kwa mwanadamu bali tafuta majibu kwa kungozwa na roho mtakatifu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom