Siri: Kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde

hapa juzi huku nako ilikuwa kulipa pesa isiyojulikana,

sasa hili kanisa inakuwaje, tutahamia wapi
Majuzi Arusha waumini ikabidi wakomboe hotel ya Corridor Spring kutoka benki ya CRDB, mikopo ya aina hiyohiyo. Sharika zikapangiwa uwiano usiolipilika, waumini wakajikamua hadi deni likaisha. Bado tu hawakomi hawa viongozi?

KKKT kuna tatizo kubwa, ifike mahali waumini tukatae kubebeshwa mizigo ya madeni yanayoingiwa na Maaskofu hawa.

Huko Lushoto Askofu Munga naye alifanyaga yake hadi SeKOMU ikawa hayati.

Aiseee?!
 
Asilimia kubwa ya waumini wao wamebemendwa. Hawataki kukua Kiroho fahari yao ni mambo ya mwilini.

Hawajui kuwa balaam ndio mfano halisi wa manabii wa uongo Yesu aliokuwa akiwaongelea na kutahadharisha elewa tu shughuli hapo ni mzito.

Huu mgogoro ambao Askofu Mkuu anajaribu kuutatua haandiki waraka kwa kondoo wengine nchi nzima wafanye maombi na mafungo ili kupatikane suluhu. Wote mnajua alivyo shikia bango suala Mbowe.
 
hapa juzi huku nako ilikuwa kulipa pesa isiyojulikana,

sasa hili kanisa inakuwaje, tutahamia wapi
Madhara ya uasi toka katoliki ndio hayo

Dhambi ya uasi inaendelea KKKT

Kuna siku watagawana mbao

Lutheran iliasi toka katoliki, Hivyo waasi wanaendelea kuasi, Usishangae ikaanzishwa Lutheran Church of Wanyakyusa

Una wajua wanyakyusa vizuri kwa ulokole? Watagawana mbao hao hawajali kitu
 
Wanayo katiba ambayo Mkuu wa Kanisa hana mamlaka yaliyo wazi kwa maaskofu wenzake. Mkuu wa kanisa akitaka kutumia mamlaka yake kushughulikia matatizo kama huu mgororo inabidi azunguke kwelikweli na haina uhakika atafanikiwa.

Katiba inaruhusu Maaskofu wa Dayosisi kula kutokana na urefu wa kamba zao na sadaka kutoka Dayosisi au sadaka kutoka marafiki wengine ndio ziweze kuendesha Makao Makuu.

Mkuu wa Kanisa ni ceremonial zaidi kuliko hicho kinacho itwa Ukuu kwa maana ya madaraka. Kukitokea wapakwa mafuta wabadhirifu ndio hivyo migogoro ya kifedha na yaki mamlaka inalikumba kanisa. Kuwajibishana kwa wakati hakuko.

Mtumishi akivuruga sehemu moja anahamishiwa sehemu nyingine kwa waumini wasiojua hayo mapungufu yake ili akaharibu zaidi huko alikohamishiwa.
 
Hiyo ndiyo shida ya badala ya kueneza dini wanafanyabiashara
 
Nakumbuka sana chuo cha SEKOMU kilifirisika kwa sababu ya hawahawa viongozi wa KKKT na mzigo uliletwa kwa waumini yaani wao walikula hela,waumini wakalipa
Haiwezekani kabisa. Kula wale wao, kulipa tulipe sisi!
 
linaanza kuonekana ni kanisa la kihuni, watulize hali ya hewa kwa kweli. Wakristo wa huko wanaonekana ni wajuha sasa
 
Mimi hili kanisa sijawahi kukuelewa kabisa maana tangu nikiwa mdogo nimekuwa nikisikia migogoro ndani ya kanisa hili, na chanzo ni matumizi mabaya ya Fedha,na ndo maana wamejiingiza hadi kwenye siasa,yaani ni Kama kikundi Cha ujasiliamali tu ,kwa kweli wabadilike wamtumikie Mungu na sio matumbo yao
 
Mleta mada ww ni miongoni mwa zoazoa mnaoharibu JF. Kitu kama umekopi na kupest onyesha upande uliopo.
 
1.7B mpaka 4.7B ongezeko la 176%.


Kwa wastani ni riba ya 22% kwa mwaka
 
Jerry alikua noma sana nafikiri ilikuwa miaka ya late 1990 au early 2000 kama sijakosea. Jamaa nasikia alikuwa akipiga pamba na kusukuma ndinga kali balaa pamoja na chuchuz.
 
Gazeti hili limeandika tofauti na chanzo kinachojulika

Chanzo cha mgogoro ni juu ya wapi pawe makao makuu ya Dayosisi ya Konde, Mbeya mjini au yawe Tukuyu. Hata kesi aliuoipeleka mahakamani Askofu Mwaikali ni ya kuhusu wapi pawe makao makuu, hili la ufisadi ndo nalisikia.

Kama ni hivyo basi na Mwaikali ni mnafiki,hajasema kile kinacholisibu Kanisa.

Lakini hayo yamepita maana Mkutano mkuu ambao ndicho chombo chenye mamlaka ya juu kimeisha amua tayari tangu tarehe 22.03.2022 na ni kwa mujibu wa katiba ya KKKT
 

Fuatilia vizuri waumini walinunua nyumba iwe kitega uchumi hapo Mbeya mjini pengine wakilenga kupambana na machungu ya deni.

Bahati mbaya Baba Askofu Mwaikali akahamishia makao makuu Mbeya na kitega uchumi kikageuka makazi yake na familia.

Uko uongo uongo mwingi sana unasemwa kwenye huu mgogoro.
 
Hii inapotosha ukweli kabisa,kiini cha mgogoro uliopo ni kuhamisha makao makuu ya dayosisi kutoka Tukuyu na kwenda Mbeya Mjini katika usharika wa Ruanda,ofisi za Askofu ziko ofisi ya Rwanda ingawa Usharika anaosali Uko Betheli na kuna kiti chake cha Askofu ila KITI CHA UASKOFU KIPO USHARIKA WA RWANDA.

Baada ya kulazimisha kibabe makao makuu yahamie Mbeya mjini na stering Mkuu ni mkuu wa jimbo ambapo hapo Usharika wa Ruanda ndipo ilipo ofisi ya jimbo.

Mchungaji mwakihaba alijiuzuru usaidizi wa Askofu maana alikua msaidizi wa Askofu Mwaikali aliyetenguliwa baadae katibu mkuu naye akajiuzuru nafasi yake,mgogoro ulianza kushika kasi baada ya washarika kuanza kuandamana hasa wa Tukuyu ambapo yalikua makao makuu baada ya jengo la dayosisi kupangishwa bank ya CRDB kwa njia za panya.

Baadae sharikanza Mbeya mjini nazo zikaanza mgomo kwa kusitisha mapato ya kila jumapili kwenda jimboni na dayosisi hapo mgogoro ukakua Kwa sababu wachungaji walishindwa kupata mishahara toka dayosisi.

Mgogoro kiini chake ni kuhamishwa ofisinza dayosisi na sio hayo maelezo ya kihuni. Askofu Shoo aliingilia kati baada ya kuona washarika wa dayosisi ya Konde wameshagawanyika,wachungaji nao wamegawanyika na takribani wachungaji 50 walisimamishwa uchungaji akiwepo Askofu mteule Mchungaji mwakihaba,

Vimefanyika vikao zaidi ya 55 kusuluhisha mgogoro lakini ilishindikana ndipo Baba Askofu aliingilia kati kwa kusimamisha halmashauri kuu ya dayosisi na ikaundwa kamati ya kusimamia ikiwa chini Askofu Malasusa ambao walikua na jukumu kuivusha dayosisi hadi uchaguzi ufanyike,pande zote mbili wale waliohamisha dayosisi na wale wanaotaka dayosisi irudi Tukuyu lakini hawakufikia muafaka baada ya upande wa Askofu Mwaikali kukacha vikao kisa wanasema Askofu Shoo kawaingilia na hana mamlaka hayo wakati sio Kweli.

Ilipofikia sasa hivi Askofu Mwakihaba ni Askofu halali ila mamlaka ya kiti bado wanacho kina Mwaikali na mkuu wa jimbo ambaye ndiye swaiba wake mkuu na Ndio mcheza michezo michafu yote.kwa kifupi ndo iko hivyo ingawa bado juhudi za kuchukua kiti zinaendelea
 

Usilo lijua wewe hawa watu wamejianika wenyewe huku uraiani kwa vile kila kikao cha pande mbili zinazovutana kinakuwa na waandishi wa habari. Fanya utafiti wako vizuri. Kila upande unamapungufu yake.

Na Katiba ya KKKT ina vipengele baadhi vinavyo ifanya kujisimamia yenyewe iwe na ugumu flani hivi. Wako watu wahusika kuiandika walichomeka maslahi yao flani ambayo kimsingi si maslahi ya Kazi ya Mungu na Bwana Yesu Kristo.

Vikao vingi vya Dayosisi lazima viitishwe na Mkuu wa Dayosisi sawa. Mkuu wa Dayosisi akiwa ni agenda ya kikao anaitishaje kikao kitakacho mjadili na pengine kumng'oa? Hivyo hivyo kwa majimbo na makanisa yao.

Kukitokea tatizo linalo muhusu Kiongozi kulitatua inabidi waumini watumie njia ya crisis kama hivi, ndiyo hiyo migogoro inazuka.
 
Umesoma vizuri content yangu?mi nilichoelezea kiini cha mgogoro ni kuhusu kuamishwa kwa ofisi za dayosisi na sio hicho walichoandika hapo kua ni ishu ya pesa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…