Siri: Kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde

Siri: Kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde

Umesoma vizuri content yangu?mi nilichoelezea kiini cha mgogoro ni kuhusu kuamishwa kwa ofisi za dayosisi na sio hicho walichoandika hapo kua ni ishu ya pesa

Moto lazima uanze kama cheche. Na cheche lazima isababishwe.
 
Gazeti hili limeandika tofauti na chanzo kinachojulika
Chanzo cha mgogoro ni juu ya wapi pawe makao makuu ya Dayosisi ya Konde, Mbeya mjini au yawe Tukuyu. Hata kesi aliuoipeleka mahakamani Askofu Mwaikali ni ya kuhusu wapi pawe makao makuu, hili la ufisadi ndo nalisikia.Kama ni hivyo basi na Mwaikali ni mnafiki,hajasema kile kinacholisibu Kanisa.
Lakini hayo yamepita maana Mkutano mkuu ambao ndicho chombo chenye mamlaka ya juu kimeisha amua tayari tangu tarehe 22.03.2022 na ni kwa mujibu wa katiba ya KKKT

Kwahiyo kuhusu hilo deni ni uongo?
 
Mleta mada ww ni miongoni mwa zoazoa mnaoharibu JF. Kitu kama umekopi na kupest onyesha upande uliopo.

Mleta mada kakopi gazeti na kaweka nakala hapo, kazi yake imeishia hapo…. wewe tupe ufafanuzi kama kuna unachokifahamu.
 
SIRI imefichuka, kwamba kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde, Mbeya, kinatajwa kuwa ni kuficha udanganyifu kwenye mkopo uliochukuliwa na Kanisa hilo, takribani miaka minane iliyopita.

Raia Mwema ilielezwa kuwa baadhi ya viongozi wa Dayosisi ya Konde, wanatuhumiwa kughushi nyaraka za Kanisa, ikiwamo mihutasari wa vikao vya Bodi kwa lengo la kuwezesha kutolewa mkopo huo (miaka 8 iliyopita).

Taarifa kutoka ndani ya Kanisa hilo zinasema, baadhi ya wakubwa ndani ya KKKT wameanzisha mgogoro katika Dayosisi ya Konde, ili kuficha udhaifu wa deni la takribani Sh bilioni 4.7 zinazodaiwa Kanisa na benki ya kibiashara ya CBA.

Benki ya CBA Commercial Bank of Africa-ilitoa kwa Kanisa Sh bilioni 1.7, kufadhili ujenzi wa ukumbi katika chuo kikuu cha Makumila, tawi la Mbeya, kilichoko Uyole (kilikufa kwa ubadhirifu), ambacho zamani kilitambulika kama Chuo cha Ualimu Uyole.

Hata hivyo, mkopo huo haukutumika kama ulivyopangwa, badala yake waliokuwa viongozi wa Kanisa, walizielekeza kwenye matumizi mengine binafsi ambayo hayakufahamika na Kanisa. Mpaka sasa, deni la Benki kwa KKKT, Dayosisi ya Konde limefikia Sh. bilioni 4.7 na tayari benki hiyo, imekwenda mahakamani na kupata amri ya kulipwa deni lake.

Mkopo huo, ulichukuliwa wakati Dayosisi ya Konde, ikiongozwa na Askofu Israel Mwakyolile (Msaidizi wake akiwa Mwakihaba aliyeteuliwa kuwa Askofu sasa), huku Mkuu wa KKKT, akiwa Askofu Dk. Alex Malasusa, ambaye alimaliza utumishi wake kwa mujibu wa Katiba ya Kanisa hilo mwaka 2015.

Nyaraka ambazo gazeti Raia Mwema imezipata, zinaonesha kuwa Kanisa lilitumia majengo ya hoteli ya Matema Beach yaliyopo Ziwa Nyasa Kyela, kama dhamana ya kujipatia mkopo benki.

"Askofu Mwakyolile akishirikana na Mchungaji Mwakihaba walichota fedhia za mkopo, lakini ghafla Mwakihaba ameteuliwa na Askofu Shoo kuwa Askofu wa Konde katika mazingira ya kutatanisha," alieleza mmoja wa wachungaji wa Kanisa hilo

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, kinachomponza Askofu Mwaikali, ni msimamo wake wa kugoma kusaini nyaraka za kuitoa hoteli ya Matema Beach kwa "wafanyabiashara wawili mashuhuri jijini Mbeya (wamiliki wa hoteli kubwa jijini Mbeya), ambao wamekubali kulipa deni la benki (nyongeza kwa ahadi ya kusimamia hoteli kwa miaka 100).

Benki ya CBA ilipeleka shauri mahakamani kulishitaki Kanisa. Wakati huo Malasusa aliishaondoka madarakani na Askofu Shoo Akakana kulijua hilo deni.

Kanisa likaunda Tume iliyoongozwa na Askofu wa Singida, Alinikisa Mkumbo, ikabaini 'madudu' yaliyomgusa Askofu Mwakyolile na kustaafu kabla ya wakati.

Askofu Shoo alishikilia msimamo, kuwa mkopo si wa Kanisa, lakini akaamua kuwaacha akina Mwakyolile kwa sababu binafsi, Hili linalotokea sasa, chanzo chake ni hicho"

Baraza la Maaskofu la KKKT, linatarajiwa kukutana Dodoma, Jumatatu ijayo ambako moja ya ajenda zinazotarajiwa kutawala, ni mgogoro ulioibuka kwenye Dayosisi ya Konde

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Kanisa hilo, maaskofu karibu wote, wamekasirishwa na kitendo cha mkuu wao wa Kanisa, Askofu Dk Fredrick Shoo kuchochea mgogoro kwenye Dayosisi hiyo na makanisa mengine ya KKKT.

"Haya mambo yakiachwa hivi, kesho hawa watu wanaweza kutengeneza magenge na kuwang'oa maaskofu wasiowataka," alieleza Askofu mmoja wa KKKT, ambaye hakupenda kutajwa gazetini.

Alisema, "tunakwenda Dodoma, tukiwa tunakumbuka madhila yaliyompata mwenzetu. Tunakwenda tukiwa wamoja na tunataka vitendo hivi vya kupinduana kinyemela vikomeshwe kwenye Kanisa letu.

Chanzo: Raia Mwema, Machi 26, 2022

NB
Kwanini Shoo kajiingiza kwenye mgogoro? Baadhi wanadai siku zote toka achaguliwe Askofu Mwaikali na baadhi ya maaskofu wasomi wamekuwa tishio kwa Askofu Shoo kuchukua nafasi yake.


View attachment 2165336
Inawezekana kukawapo na deni kweli,lakini chanzo Cha mgogoro ni kuhamisha makao kinyemela. Mgogoro umeanzia chini na siyo huko unakokusema. Sasa Kama na Mwaikali ameona naye atafute wa kufa naye sawa.

Alipofukuzwa kanisani Askofu Mwaikali huko Tukuyu,Askofu Shoo alikuwepo? Au Malasusa? Mwaikali alikosea na sisi wanakonde tunaelewa. Awali makao makuu ya Dayosisi ya Konde yalikuwa Manow na yaliyamishiwa Tukuyu na Askofu Amon Mwakisunga, kwa nini hakukutokea mgogoro? Mwakisunga alishirikisha vikao vyote na vilitoa baraka zote.

Tusihamishe magoli chanzo cha mgogoro huu, ni kuhamishwa makao makuu kinyemela na ubabe wa baadhi ya wapambe wa Askofu Mwakisunga. Aidha ni vema kuelewa Askofu wa Dayosisi yoyote ya KKKT huchaguliwa na mkutano mkuu wa Dayosisi Hakuna Askofu anayechaguliwa na KKKT makao makuu ikimuondoa Dr. Mwakabana ambaye pia hakuwahi kuwa na Dayosisi Bali alitumika kusimamia Dayosisi zinazokuwa na migogoro mpaka itakapotatuliwa na akachaguliwa Askofu mwingine na mkutano mkuu wa Dayosisi husika then anaondoka na hii iliwahi tokea pindi Dayosisi ya Masharikina na Pwani ilipokuwa na mgogoro uliomuondoa Askofu Mgwamba kabla ya kuchaguliwa kwa Askofu Dr. Alex Malasusa.

Kuwepo kwa Askofu Dr. Shoo na Malasusa kwenye mkutano mkuu huwa Ni kawaida kwani uchaguzi wowote wa Askofu ni awepo msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Askofu kutoka Dayosisi nyingine atakayealikwa na halmashauri kuu ya dayosisi yenyewe au kupitia kwa Askofu aliyepo madarakani anayemaliza kama Ni uchaguzi wa kawaida.

Wajumbe wa mkutano mkuu huundwa na wajumbe kutoka sharika zote za Dayosisi. Idadi hutegemea na ukubwa wa sharika, kwamba sharika yenye washarika wengi huwa na idadi kubwa ya uwakilishi. Na mkutano mkuu wa Dayosisi ya Konde ulikuwa na wajumbe zaidi ya 1000. Na ndio waliopiga kura ya kumchagua Askofu mpya.

Mkuu wa kanisa husimamia zoezi la kumsimamisha au kumuondoa Askofu aliyekiuka maadili kwa kupokea taarifa kutoka halmashauri kuu ya dayosisi husika. Hushirikiana na maaskofu wengine kwa kufuata katiba ya kanisa.

Kwa kuwa Askofu anawekwa wakfu na kusimikwa na maaskofu, washarika wao huishia kumkataa tuu na siyo kumtoa kwani hawakumsimika wao.

Hivyo ni sahihi kwa Askofu Shoo kuwepo na kusimamia shughuli nzima na anaweza kumualika Askofu yeyote wa kusaidiana naye.
Kama kuna eneo siko Wana KKKT wamo humu watakosoa au wataboresha.
 
Madhara ya uasi toka katoliki ndio hayo

Dhambi ya uasi inaendelea KKKT

Kuna siku watagawana mbao

Lutheran iliasi toka katoliki, Hivyo waasi wanaendelea kuasi, Usishangae ikaanzishwa Lutheran Church of Wanyakyusa

Una wajua wanyakyusa vizuri kwa ulokole? Watagawana mbao hao hawajali kitu
Ni vizuri ukaitafuta vizuiri historia ya waluteri,.na pia ukaitafuta pia historia ya wakatoriki na siyo kama unavyosimulia humu,Sina hakika kama hata makao ya ukatoliki yalitokana na hongo iliyotolewa na Benito Mussolini aliyekuwa mtawala wa Italy enzi hizo,ili linyamaze atakapoanza kuua watu.
 
Aidha ni vema kuelewa Askofu wa Dayosisi yoyote ya KKKT huchaguliwa na mkutano mkuu wa Dayosisi Hakuna Askofu anayechaguliwa na KKKT makao makuu ikimuondoa Dr. Mwakabana ambaye pia hakuwahi kuwa na Dayosisi Bali alitumika kusimamia Dayosisi zinazokuwa na migogoro mpaka itakapotatuliwa
Chaguzi kama za ccm. Hiki ndio chanzo cha kuchaguliwa maaskofu corrupt.
 
Halaf waje waseme hafai kuwa Mkuu wa Kanisa maana hashughulikii migogoro kwenye dayosisi

Yule Askofu Mwaikali mhuni tu, yupo sawa na Askofu mmoja wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani aliitwa Jerry Mngwamba, huyu alikuwa Askofu hapa halaf familia inaishi Ulaya, kila weekend anapanda zake ndege anakwenda kula bata Ulaya Kanisa likakosa Uongozi
Jerry alikuwa mafia sana mzaramo yule

Any way alitikisa sana miaka ya 90's na kashifa ya sembe
 
Inawezekana kukawapo na deni kweli,lakini chanzo Cha mgogoro ni kuhamisha makao kinyemela. Mgogoro umeanzia chini na siyo huko unakokusema. Sasa Kama na Mwaikali ameona naye atafute wa kufa naye sawa.
Alipofukuzwa kanisani Askofu Mwaikali huko Tukuyu,Askofu Shoo alikuwepo? Au Malasusa? Mwaikali alikosea na sisi wanakonde tunaelewa.
Awali makao makuu ya Dayosisi ya Konde yalikuwa Manow na yaliyamishiwa Tukuyu na Askofu Amon Mwakisunga, kwa nini hakukutokea mgogoro? Mwakisunga alishirikisha vikao vyote na vilitoa baraka zote.
Tusihamishe magoli chanzo cha mgogoro huu, ni kuhamishwa makao makuu kinyemela na ubabe wa baadhi ya wapambe wa Askofu Mwakisunga.
Aidha ni vema kuelewa Askofu wa Dayosisi yoyote ya KKKT huchaguliwa na mkutano mkuu wa Dayosisi Hakuna Askofu anayechaguliwa na KKKT makao makuu ikimuondoa Dr. Mwakabana ambaye pia hakuwahi kuwa na Dayosisi Bali alitumika kusimamia Dayosisi zinazokuwa na migogoro mpaka itakapotatuliwa na akachaguliwa Askofu mwingine na mkutano mkuu wa Dayosisi husika then anaondoka na hii iliwahi tokea pindi Dayosisi ya Masharikina na Pwani ilipokuwa na mgogoro uliomuondoa Askofu Mgwamba kabla ya kuchaguliwa kwa Askofu Dr. Alex Malasusa.
Kuwepo kwa Askofu Dr. Shoo na Malasusa kwenye mkutano mkuu huwa Ni kawaida kwani uchaguzi wowote wa Askofu ni awepo msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Askofu kutoka Dayosisi nyingine atakayealikwa na halmashauri kuu ya dayosisi yenyewe au kupitia kwa Askofu aliyepo madarakani anayemaliza kama Ni uchaguzi wa kawaida.
Wajumbe wa mkutano mkuu huundwa na wajumbe kutoka sharika zote za Dayosisi. Idadi hutegemea na ukubwa wa sharika, kwamba sharika yenye washarika wengi huwa na idadi kubwa ya uwakilishi. Na mkutano mkuu wa Dayosisi ya Konde ulikuwa na wajumbe zaidi ya 1000. Na ndio waliopiga kura ya kumchagua Askofu mpya.
Mkuu wa kanisa husimamia zoezi la kumsimamisha au kumuondoa Askofu aliyekiuka maadili kwa kupokea taarifa kutoka halmashauri kuu ya dayosisi husika. Hushirikiana na maaskofu wengine kwa kufuata katiba ya kanisa.
Kwa kuwa Askofu anawekwa wakfu na kusimikwa na maaskofu, washarika wao huishia kumkataa tuu na siyo kumtoa kwani hawakumsimika wao.
Hivyo ni sahihi kwa Askofu Shoo kuwepo na kusimamia shughuli nzima na anaweza kumualika Askofu yeyote wa kusaidiana naye.
Kama kuna eneo siko Wana KKKT wamo humu watakosoa au wataboresha.

Waambie wampelekee barua Askofu Mwaikali ya kumfahamisha kuhusu huo mkutano ulio muondoa ndicho anacho subiri.

Huku kwenye vyombo vya habari anasema wajumbe wa huo mkutano wameokotezwaokotezwa dada na kaka.
 
SIRI imefichuka, kwamba kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde, Mbeya, kinatajwa kuwa ni kuficha udanganyifu kwenye mkopo uliochukuliwa na Kanisa hilo, takribani miaka minane iliyopita.

Raia Mwema ilielezwa kuwa baadhi ya viongozi wa Dayosisi ya Konde, wanatuhumiwa kughushi nyaraka za Kanisa, ikiwamo mihutasari wa vikao vya Bodi kwa lengo la kuwezesha kutolewa mkopo huo (miaka 8 iliyopita).

Taarifa kutoka ndani ya Kanisa hilo zinasema, baadhi ya wakubwa ndani ya KKKT wameanzisha mgogoro katika Dayosisi ya Konde, ili kuficha udhaifu wa deni la takribani Sh bilioni 4.7 zinazodaiwa Kanisa na benki ya kibiashara ya CBA.

Benki ya CBA Commercial Bank of Africa-ilitoa kwa Kanisa Sh bilioni 1.7, kufadhili ujenzi wa ukumbi katika chuo kikuu cha Makumila, tawi la Mbeya, kilichoko Uyole (kilikufa kwa ubadhirifu), ambacho zamani kilitambulika kama Chuo cha Ualimu Uyole.

Hata hivyo, mkopo huo haukutumika kama ulivyopangwa, badala yake waliokuwa viongozi wa Kanisa, walizielekeza kwenye matumizi mengine binafsi ambayo hayakufahamika na Kanisa. Mpaka sasa, deni la Benki kwa KKKT, Dayosisi ya Konde limefikia Sh. bilioni 4.7 na tayari benki hiyo, imekwenda mahakamani na kupata amri ya kulipwa deni lake.

Mkopo huo, ulichukuliwa wakati Dayosisi ya Konde, ikiongozwa na Askofu Israel Mwakyolile (Msaidizi wake akiwa Mwakihaba aliyeteuliwa kuwa Askofu sasa), huku Mkuu wa KKKT, akiwa Askofu Dk. Alex Malasusa, ambaye alimaliza utumishi wake kwa mujibu wa Katiba ya Kanisa hilo mwaka 2015.

Nyaraka ambazo gazeti Raia Mwema imezipata, zinaonesha kuwa Kanisa lilitumia majengo ya hoteli ya Matema Beach yaliyopo Ziwa Nyasa Kyela, kama dhamana ya kujipatia mkopo benki.

"Askofu Mwakyolile akishirikana na Mchungaji Mwakihaba walichota fedhia za mkopo, lakini ghafla Mwakihaba ameteuliwa na Askofu Shoo kuwa Askofu wa Konde katika mazingira ya kutatanisha," alieleza mmoja wa wachungaji wa Kanisa hilo

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, kinachomponza Askofu Mwaikali, ni msimamo wake wa kugoma kusaini nyaraka za kuitoa hoteli ya Matema Beach kwa "wafanyabiashara wawili mashuhuri jijini Mbeya (wamiliki wa hoteli kubwa jijini Mbeya), ambao wamekubali kulipa deni la benki (nyongeza kwa ahadi ya kusimamia hoteli kwa miaka 100).

Benki ya CBA ilipeleka shauri mahakamani kulishitaki Kanisa. Wakati huo Malasusa aliishaondoka madarakani na Askofu Shoo Akakana kulijua hilo deni.

Kanisa likaunda Tume iliyoongozwa na Askofu wa Singida, Alinikisa Mkumbo, ikabaini 'madudu' yaliyomgusa Askofu Mwakyolile na kustaafu kabla ya wakati.

Askofu Shoo alishikilia msimamo, kuwa mkopo si wa Kanisa, lakini akaamua kuwaacha akina Mwakyolile kwa sababu binafsi, Hili linalotokea sasa, chanzo chake ni hicho"

Baraza la Maaskofu la KKKT, linatarajiwa kukutana Dodoma, Jumatatu ijayo ambako moja ya ajenda zinazotarajiwa kutawala, ni mgogoro ulioibuka kwenye Dayosisi ya Konde

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Kanisa hilo, maaskofu karibu wote, wamekasirishwa na kitendo cha mkuu wao wa Kanisa, Askofu Dk Fredrick Shoo kuchochea mgogoro kwenye Dayosisi hiyo na makanisa mengine ya KKKT.

"Haya mambo yakiachwa hivi, kesho hawa watu wanaweza kutengeneza magenge na kuwang'oa maaskofu wasiowataka," alieleza Askofu mmoja wa KKKT, ambaye hakupenda kutajwa gazetini.

Alisema, "tunakwenda Dodoma, tukiwa tunakumbuka madhila yaliyompata mwenzetu. Tunakwenda tukiwa wamoja na tunataka vitendo hivi vya kupinduana kinyemela vikomeshwe kwenye Kanisa letu.

Chanzo: Raia Mwema, Machi 26, 2022

NB
Kwanini Shoo kajiingiza kwenye mgogoro? Baadhi wanadai siku zote toka achaguliwe Askofu Mwaikali na baadhi ya maaskofu wasomi wamekuwa tishio kwa Askofu Shoo kuchukua nafasi yake.


View attachment 2165336
Mbona hukugusia chanzo cha kuhamisha ofisi kutoka tukuyu kwenda mbeya?

Makao makuu ya Diocese kkkt yalikuwa Rungwe ambako ndio chimbuko la misionari katika kanda hii ya kusini.

Viongozi wa dini acheni kumsononesha Robo Mtakatifu kwa kupenda fedha; tunataka kuwa na viongozi wanaompenda Mungu hata ktk mazingira ya kipato kidogo nyinyi ni bora kuliko ndege wa angani
 
Kwahiyo kuhusu hilo deni ni uongo?
Ni uongo deni sio sababu ya mgogoro uliopo.

Mgogoro umesababishwa na kuhamishwa makao makuu toka Tukuyu na kupelekwa Mbeya mjini na fukuza fukuza ya wachungaji wanaokataa matakwa ya Mwaikali,ilipofika sass hivi hakuna Usharika unapokea mchungaji mpya tena,Sharika haziwapi hifadhi tena
 
Ni uongo deni sio sababu ya mgogoro uliopo.Mgogoro umesababishwa na kuhamishwa makao makuu toka Tukuyu na kupelekwa Mbeya mjini na fukuza fukuza ya wachungaji wanaokataa matakwa ya Mwaikali,ilipofika sass hivi hakuna Usharika unapokea mchungaji mpya tena,Sharika haziwapi hifadhi tena
Kanisa katoliki huwezi kukuta Mambo Kama hayo ,kwa vyovyote vile chanzo Cha mgogoro huu lazima iwe pesa,hata Kama ni kuhamisha makao makuu,lakini msingi wake utakuwa kupata pesa au maisha mazuri,
 
Kisheria Mwaikali ameshashindwa kupitia katiba ya Konde.

1.Waliompigia kura awe askofu ndio haohao wamekosa imani nae.

2.Usajili wa Dayosisi upo serikalini(Rita)

Ikieleza wapi makao makuu ya Dayosisi,kitalu No ngapi.

Kabla yakupeleka kiti cha uaskofu Mbeya mjini alitakiwa apeleke mhutasari wa badiliko la makao makuu.

3.Kiti kinaweza kubarikiwa kingine na akakitumia aliyechaguliwa.Mwisho wake ni aibu kwa Mwaikali.

Wazee wa konde mumuonye Mwaikali asiwe mhuni kiasi hicho
 
Hii inapotosha ukweli kabisa,kiini cha mgogoro uliopo ni kuhamisha makao makuu ya dayosisi kutoka Tukuyu na kwenda Mbeya Mjini katika usharika wa Ruanda,ofisi za Askofu ziko ofisi ya Rwanda ingawa Usharika anaosali Uko Betheli na kuna kiti chake cha Askofu ila KITI CHA UASKOFU KIPO USHARIKA WA RWANDA.baada ya kulazimisha kibabe makao makuu yahamie Mbeya mjini na stering Mkuu ni mkuu wa jimbo ambapo hapo Usharika wa Ruanda ndipo ilipo ofisi ya jimbo.Mchungaji mwakihaba alijiuzuru usaidizi wa Askofu maana alikua msaidizi wa Askofu Mwaikali aliyetenguliwa baadae katibu mkuu naye akajiuzuru nafasi yake,mgogoro ulianza kushika kasi baada ya washarika kuanza kuandamana hasa wa Tukuyu ambapo yalikua makao makuu baada ya jengo la dayosisi kupangishwa bank ya CRDB kwa njia za panya.
Baadae sharikanza Mbeya mjini nazo zikaanza mgomo kwa kusitisha mapato ya kila jumapili kwenda jimboni na dayosisi hapo mgogoro ukakua Kwa sababu wachungaji walishindwa kupata mishahara toka dayosisi.
Mgogoro kiini chake ni kuhamishwa ofisinza dayosisi na sio hayo maelezo ya kihuni.Askofu Shoo aliingilia kati baada ya kuona washarika wa dayosisi ya Konde wameshagawanyika,wachungaji nao wamegawanyika na takribani wachungaji 50 walisimamishwa uchungaji akiwepo Askofu mteule Mchungaji mwakihaba,vimefanyika vikao zaidi ya 55 kusuluhisha mgogoro lakini ilishindikana ndipo Baba Askofu aliingilia kati kwa kusimamisha halmashauri kuu ya dayosisi na ikaundwa kamati ya kusimamia ikiwa chini Askofu Malasusa ambao walikua na jukumu kuivusha dayosisi hadi uchaguzi ufanyike,pande zote mbili wale waliohamisha dayosisi na wale wanaotaka dayosisi irudi Tukuyu lakini hawakufikia muafaka baada ya upande wa Askofu Mwaikali kukacha vikao kisa wanasema Askofu Shoo kawaingilia na hana mamlaka hayo wakati sio Kweli.
Ilipofikia sasa hivi Askofu Mwakihaba ni Askofu halali ila mamlaka ya kiti bado wanacho kina Mwaikali na mkuu wa jimbo ambaye ndiye swaiba wake mkuu na Ndio mcheza michezo michafu yote.kwa kifupi ndo iko hivyo ingawa bado juhudi za kuchukua kiti zinaendelea
na huu ndiyo ukweli.
 
Kisheria Mwaikali ameshashindwa kupitia katiba ya Konde.
1.Waliompigia kura awe askofu ndio haohao wamekosa imani nae.
2.Usajili wa Dayosisi upo serikalini(Rita)
Ikieleza wapi makao makuu ya Dayosisi,kitalu No ngapi.
Kabla yakupeleka kiti cha uaskofu Mbeya mjini alitakiwa apeleke mhutasari wa badiliko la makao makuu.
3.Kiti kinaweza kubarikiwa kingine na akakitumia aliyechaguliwa.Mwisho wake ni aibu kwa Mwaikali.Wazee wa konde mumuonye Mwaikali asiwe mhuni kiasi hicho

Askofu Mwakali na Mchungaji mmoja Mkuu wa Jimbo wanasema wajumbe wa huo mkutano Mkuu hawakupatikana kwa kufuata Katiba ya Konde inavyo ainisha.

Wanasubiri barua ya kuongoa Askofu Mwaikali wapange next move.
 
Hii inapotosha ukweli kabisa,kiini cha mgogoro uliopo ni kuhamisha makao makuu ya dayosisi kutoka Tukuyu na kwenda Mbeya Mjini katika usharika wa Ruanda,ofisi za Askofu ziko ofisi ya Rwanda ingawa Usharika anaosali Uko Betheli na kuna kiti chake cha Askofu ila KITI CHA UASKOFU KIPO USHARIKA WA RWANDA.baada ya kulazimisha kibabe makao makuu yahamie Mbeya mjini na stering Mkuu ni mkuu wa jimbo ambapo hapo Usharika wa Ruanda ndipo ilipo ofisi ya jimbo.Mchungaji mwakihaba alijiuzuru usaidizi wa Askofu maana alikua msaidizi wa Askofu Mwaikali aliyetenguliwa baadae katibu mkuu naye akajiuzuru nafasi yake,mgogoro ulianza kushika kasi baada ya washarika kuanza kuandamana hasa wa Tukuyu ambapo yalikua makao makuu baada ya jengo la dayosisi kupangishwa bank ya CRDB kwa njia za panya.
Baadae sharikanza Mbeya mjini nazo zikaanza mgomo kwa kusitisha mapato ya kila jumapili kwenda jimboni na dayosisi hapo mgogoro ukakua Kwa sababu wachungaji walishindwa kupata mishahara toka dayosisi.
Mgogoro kiini chake ni kuhamishwa ofisinza dayosisi na sio hayo maelezo ya kihuni.Askofu Shoo aliingilia kati baada ya kuona washarika wa dayosisi ya Konde wameshagawanyika,wachungaji nao wamegawanyika na takribani wachungaji 50 walisimamishwa uchungaji akiwepo Askofu mteule Mchungaji mwakihaba,vimefanyika vikao zaidi ya 55 kusuluhisha mgogoro lakini ilishindikana ndipo Baba Askofu aliingilia kati kwa kusimamisha halmashauri kuu ya dayosisi na ikaundwa kamati ya kusimamia ikiwa chini Askofu Malasusa ambao walikua na jukumu kuivusha dayosisi hadi uchaguzi ufanyike,pande zote mbili wale waliohamisha dayosisi na wale wanaotaka dayosisi irudi Tukuyu lakini hawakufikia muafaka baada ya upande wa Askofu Mwaikali kukacha vikao kisa wanasema Askofu Shoo kawaingilia na hana mamlaka hayo wakati sio Kweli.
Ilipofikia sasa hivi Askofu Mwakihaba ni Askofu halali ila vmamlaka ya kiti bado wanacho kina Mwaikali na mkuu wa jimbo ambaye ndiye swaiba wake mkuu na Ndio mcheza michezo michafu yote.kwa kifupi ndo iko hivyo ingawa bado juhudi za kuchukua kiti zinaendelea
Kiti ni nini?? Kwamba wamekipeleka kwao nyumbni au??
 
Huu mgogoro kiukweli haukutakiwa kusuluhishwa na malasusa Kwan anamaslah katika mgogoro huu.

Kwao ni huko tukuyu

Cjajua mgogoro wa wa dayosisi ya kusini umefikia wapi, maana jimbo la mufindi ni kma Crimea katika nchi ya Ukraine
 
Askofu Mwakali na Mchungaji mmoja Mkuu wa Jimbo wanasema wajumbe wa huo mkutano Mkuu hawakupatikana kwa kufuata Katiba ya Konde inavyo ainisha. Wanasubiri barua ya kuongoa Askofu Mwaikali wapange next move.
Waache wakutane na jela.

Anafahamu maana ya:
1.Mkuu wa kanisa?
2.Askofu Mkuu?

Akijua kutofautisha 1 na 2 atulie.

Kanisa la KKKT ndilo lenye usajili nchini.

Hakuna KKK KONDE bila mwavuli wa KKKT.Mahakama ilimshauri wakakae mezani,waliomwita mezani wakampa arudishe kiti hakutii.

Anadhani Mkuu wa kanisa anafanya kazi bila vyombo vya ulinzi kiini cha mgogolo.Askofu hadi unafukuzwa msibani huwezi Jitafakari
 
Back
Top Bottom