Siri: Kiini cha mgogoro unaofukuta ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde

Kumbe na huku kkkt nako wanagombanaga nilidhani hayo mambo yapo kwenye makanisa madogo madogo tu

Hizi dini hakuna wa kumcheka mwenzake
 
Sasa naelewa kwanini watawa wa Roman catholic hawaoi
Huko nako matatizo ni yale yale hao watawa wanawalawiti watoto wa kiume

Haya makanisa hakuna wa kumnyooshea kidole mwenzake
Wote janja janja tu
 

Ndio sababu yule Mkuu wa jimbo mpambe wake alisema imefikia mpaka anatishiwa maisha lakini hatakubali Katiba ya Konde ikanyagwe.

Ok now I know.
 
Raia Mwema inajulikana kw habari za kughushi.

Mtoa habari angetoa hata nyaraka za kuthibitisha madai wanayoandika.
 
Pole sana mkuu, wewe pia ulilawitiwa ulivyokuwa mdogo?
Nyie waumini mnajitoaga ufahamu,ina maana wewe husikii kwenye vyombo vya habari duniani kuhusu hizo taarifa na kashfa kutoka vatican mpk mapapa wanajiuzulu?

Au wewe ndio umekuja duniani dakika hii hukuwepo.

Acha utahaira
 
Askofu Shoo na Bagonza wanakopa fedha halafu wanawapa Chadema kwa ajili ya kufanya siasa
 
Kaleta habari kutoka gazetini. Sasa yeye hajui nini?
Mleta mada hujui chochote kuhusu huo mgogoro,ila upo upande mmoja usioujua kiundani.
Kuhusu chuo kamuulize mstaafu mmoja mdegela atakuambia A to Z.
 
Nakumbuka sana chuo cha SEKOMU kilifirisika kwa sababu ya hawahawa viongozi wa KKKT na mzigo uliletwa kwa waumini yaani wao walikula hela,waumini wakalipa
BARAZA la Vijana wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT, Dayosisi ya Konde, limemtupia lawama Mkuu wa kanisa hilo nchini, Askofu Dk. Fredrick Shoo, likidai kuongoza mkutano wa kumwondoa Askofu wa dayosisi hiyo, Dk. Edward Mwaikali, badala ya kutafuta njia sahihi ya kumaliza mgogoro ....

[https://res]

unaofukuta.

Akisoma taarifa ya msimamo wa vijana wa dayosisi hiyo jana, Marko Mahenge, alidai Askofu Dk. Shoo amekuwa sehemu ya kukuza mgogoro huo badala ya kutafuta njia sahihi ya kujadili namna ya kushughulika na jambo hilo ambalo linaendelea kuyumbisha Dayosisi ya Konde.

Alisema kwa muda mrefu vijana walikuwa kimya wakifuatilia mwenendo ya mgogoro huo huku wakitarajia kufanyika kwa hekima na busara katika kushughulikia maridhiano ya kuhamisha makao makuu ya dayosisi hiyo kutoka mjini Tukuyu katika Wilaya ya Rungwe na kupelekwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

“Sisi vijana wa Jimbo hili la Mbeya na maeneo mengine ya dayosisi hii tunapinga vikali uamuzi wa Mkuu wa Kanisa kumwondoa Askofu Mwaikali kwenye kiti chake kwa sababu mkutano uliofanyika Machi 22, katika Ushirika wa Uyole ulikuwa batili, tunamtambua Dk. Mwaikali kuwa ndiye askofu wetu na hapa jimboni haondoka wala mchungaji au Mkuu wa Jimbo,” alisema Mahenge.

Aidha, Mahenge aliliomba Baraza la Maaskofu wa kanisa hilo nchini kuingilia kati mgogoro huo kwa kuiita halmashauri kuu ya dayosisi na viongozi wengine ili kukubaliana mambo ya kufanya.

Akizungumza wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa Kuu la Ruanda, yalipo makao makuu ya Dayosisi ya Konde, Mkuu wa Jimbo, Mchungaji Nyibuko Mwambola, alisema Halmashauri Kuu haitambui mkutano ulioitishwa na Askofu Dk. Fredrick Shoo kwa madai kuwa ulikuwa batili.

Alimtupia lawama Askofu Dk. Shoo kama mkuu wa kanisa kwa kushindwa kusuluhisha mgogoro huo na kuwa sehemu ya kuchochea hali ambayo alidai inazidi kuongeza chuki na mfarakano.

Kadhalika, alisema baada ya mkutano wa kumchagua askofu mwingine, Geofrey Mwakihaba, Askofu Dk. Shoo alituma waraka kwa taasisi zote za kifedha kufunga akaunti za dayosisi.

Alisema hatua hiyo imewasababishia kushindwa kufanya malipo yoyote ikiwamo mishahara ya wachungaji na watumishi wengine wa dayosisi hiyo.

Vile vile, alidai kuwa Dk. Shoo amewatumia barua wachungaji wote wa Dayosisi ya Konde kuhudhuria kikao kinachofanyika kesho jijini Dodoma, bila kumpa taarifa Askofu wa Jimbo Dk. Mwaikali, na kwamba Halmashauri Kuu imesema naye atashiriki kikao hicho.

“Mkuu wa Kanisa ameonyesha dhahiri upande alipo kwa sababu ameshindwa kutukutanisha pamoja viongozi wa dayosisi na kujadili pamoja namna bora ya kumaliza huu mgogoro badala yake ameonesha wazi kushindwa kusimamia jambo hilo na kuchangia kuchochea suala hili, sisi tunamtambua bado Askofu Mwaikali ndiyo anasimamia dayosisi yetu ya Konde,” alisisitiza.

“Haiwezekani Mkuu wa Kanisa aitishe mkutano na kufanya uchaguzi wa kumchagua askofu mwingine, tena kwa siku moja, inaonyesha dhahiri kuna chuki binafsi na sio suala la kuhamisha makao mkuu ya dayosisi.”

Machi 22 mwaka huu Mkuu wa Kanisa la KKKT nchini, Askofu Dk Fredrick Shoo, pamoja na wajumbe 201 walifanya mkutano katika Usharika wa Uyole jijini Mbeya kwa lengo la kumaliza mgogoro huo ambapo liliibuka suala la wajumbe kutokuwa na imani na Askofu Dk. Edward Mwaikali.

Katika mkutano huo ambao uliendeshwa na Askofu Dk. Shoo na kudumu kwa saa 10, ulitumika kumchagua Askofu mwingine Mchungaji Geofrey Mwakihaba, ambaye alitangazwa mbele ya wajumbe wa mkutano.

Kutokana na uamuzi huo baadhi ya vijana wa KKKT mkoani Mbeya walieleza kuwa mchakato uliotumika kuwa ulikuwa batili.

Hata hivyo, Askofu Dk. Shoo alipotafutwa na Nipashe kwa simu jana, muda wote hakupatikana kuzungumzia suala hilo.

Mgogoro wa kwanini yahamishwe makao makuu ya dayosisi kutoka mjini Tukuyu katika Wilaya ya Rungwe na kwenda Halmashauri ya Jiji la Mbeya, ulianza kufukuta tangu mwaka 2017 hadi sasa.
 
Ndiyo maana naamini hao kina Mwaikali watakula sahani moja na dola.

Mpaka kuondolewa bila heshima mtu amepoteza heshima yake yote kutokana na ukaidi.
 
Sijawahi sikia baraza la vijana KKKT KONDE kuwa namamlaka yakutoa tamko.

Chawa wote wa Mwaikali wanapoteza muda.

1.Mkuu wa jimbo unatoa tamko kwa wajumbe wa mkutano mkuu huku ukijua unawajibika kwao.
2.Mkuu wa jimbo sio msemaji wa Dayosisi na wala wewe sio mtendaji Mkuu wa Dayosisi.
3.Mkuu wa jimbo unamtolea tamko Mkuu wa kanisa.
4.Mkuu wa jimbo hujuwi mipaka yako kiutumishi na huduma.
5.Mkuu wa jimbo hujui usajili wa Dayosisi ya konde ipo kitalu gani.
6.Mkuu wa kanisa amefanya yampasayo.Kama Mwaikali alikuwa sahihi hao wajumbe wa mkutano Mkuu hawangeitikia wito wa mgeni,wangesema hatukutambui.

ENYI WAPAMBE WA MWAIKALI KUBALINI BOSI WENU ALIONYESHA DHARAU KUHAMISHA UASKOFU MAHALIA BILA TARATIBU ZILIZOMPA FIMBO YA KIASKOFU
 
Lie and love ni moja ya baadhi ya mapepo yanayo litafuna KKKT.
 

Katiba ya Dayosisi ya Konde inasema nani ataitisha mkutano Mkuu kwa kufuata utaratibu gani?

KKKT limekuwa Vuguvugu. The church with a lukewarm faith.

The church which allows its ecomomic prosperity to cause it spiritual bankruptcy.

Wanachotakiwa sasa ni kufanya Overhaul ya Katiba ya KKKT ambayo ni reflection ya hizo za Dayosisi zake.

Migogoro ni mingi sana ambayo wanaweza kuitafuta vyanzo nini na wakaweka vipengele vitakavyo kuwa ni suluhisho.
 
Endeleeni kupeleka sadaka huko wengine wameshaweka ndani 1.7b sisi waafrika sijui nani ametuloga na hizi dini za wazungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…