Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

JE Dunia ina umbo gani?


  • Total voters
    710
Huu mjadala nimeufatilia miaka mingi sana naona pande zote kuna vitu wana miss.

Hili swali la usiku na mchana limeulizwa sana na sijaona majibu yake,ila kuna mdau alijibu kwa concept ya kwamba..

Jua ni dogo kuliko dunia sahani,yaani chukulia sahani ya kula watu 10 ndio dunia na jua ni kama kitenesi cha watoto.

Hivyo inakuwa ni vigumu sana jua kumulika pande zote za dunia kwa sababu jua ni dogo na dunia ni kubwa.

Hivyo kwa kuwa jua ni dogo basi mwanga wake utakuwa haufiki baadhi ya sehemu,na hizo sehemu ndizo zitakuwa ni usiku.
Samahani.
Hiyo concept ya "Jua ni dogo kuliko dunia" inaweza kuthibitishwa vipi?
Sio kwamba ni nadharia tu?
 
Samahani.
Hiyo concept ya "Jua ni dogo kuliko dunia" inaweza kuthibitishwa vipi?
Sio kwamba ni nadharia tu?
usiku na mchana ni uthibitisho tosha kwamba dunia ni kubwa na jua dogo kwa kufuata fikra ya dunia tambarare sahani.

KWa maana jua ni dogo haliwezi kumulika dunia nzima kwa concept ya dunia sahani tambarare.

Je hiyo inamake sense kwako mkuu,kama haimake why ?
 
Je, nini kitatufanya tuhitimishe kuwa hoja yako ndio ukweli na sio vinginevyo kama nilivyoelezea??
Mkuu kama ulivyokiri kwamba hoja yangu juu ya jua inaweza kumake sense.

Na mimi nakiri pia hoja yako juu ya jua inaweza kumake sense pia kwa mujibu wa maelezo yako.

So hapo utaona kwamba kila mmoja maelezo yake yanamake sense kwa mujibu wa kile anachokishikilia.

Hivyo inanipa tabu kusema ni kitu gani kitathibitisha usahihi wa maelezo yangu,kama ambavyo na wewe unaweza kupata tabu kuweka kitu ambacho kitathubitisha usahihi wa maelezo yako.

Nadhani hili suala tuendelee kulijadili bila kuegemea upande wowote,binafsi nimezisoma hoja tata z watu wa pande zote na nakiri kusema kwamba kila upande una hoja ambazo ni znuri na zinafikirisha sana.
 
Mkuu kama ulivyokiri kwamba hoja yangu juu ya jua inaweza kumake sense.

Na mimi nakiri pia hoja yako juu ya jua inaweza kumake sense pia kwa mujibu wa maelezo yako.

So hapo utaona kwamba kila mmoja maelezo yake yanamake sense kwa mujibu wa kile anachokishikilia.

Hivyo inanipa tabu kusema ni kitu gani kitathibitisha usahihi wa maelezo yangu,kama ambavyo na wewe unaweza kupata tabu kuweka kitu ambacho kitathubitisha usahihi wa maelezo yako.

Nadhani hili suala tuendelee kulijadili bila kuegemea upande wowote,binafsi nimezisoma hoja tata z watu wa pande zote na nakiri kusema kwamba kila upande una hoja ambazo ni znuri na zinafikirisha sana.
Kama hutojali, ningependa nijue nini kimekufanya binafsi uamini zaidi kuwa jua huzunguka dunia tambarare na kuleta usiku na mchana na sio kwamba dunia mfano wa tufe huzunguka jua.

Binafsi nafahamu kimsingi kuwa dunia ni tufe kwa sababu mbalimbali kama vile;

1. Uwepo wa picha za setelite zinazo oneshe dunia ikiwa na umbo hilo(mfano wa tufe)

2. Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa nchi zinazopatikana kwenye poles za dunia(mfano. Greenland na Canada)

Gravitational force inashikilia vitu vilivyopo duniani huku dunia ikizunguka kwa kasi.

Je, sababu kama hizi haziipi nguvu hoja ya kuwa dunia ni mfano wa tufe na si tambarare?
Tunawezaje kuelezea Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa baadhi ya nchi(mfano. Greenland na Canada) katika dunia iliyo tambarare?
 
Samahani.
Hiyo concept ya "Jua ni dogo kuliko dunia" inaweza kuthibitishwa vipi?
Sio kwamba ni nadharia tu?
Mfano mdogo
Flat%20Earth.gif
 
Kama hutojali, ningependa nijue nini kimekufanya binafsi uamini zaidi kuwa jua huzunguka dunia tambarare na kuleta usiku na mchana na sio kwamba dunia mfano wa tufe huzunguka jua.

Binafsi nafahamu kimsingi kuwa dunia ni tufe kwa sababu mbalimbali kama vile;

1. Uwepo wa picha za setelite zinazo oneshe dunia ikiwa na umbo hilo(mfano wa tufe)

2. Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa nchi zinazopatikana kwenye poles za dunia(mfano. Greenland na Canada)

Gravitational force inashikilia vitu vilivyopo duniani huku dunia ikizunguka kwa kasi.

Je, sababu kama hizi haziipi nguvu hoja ya kuwa dunia ni mfano wa tufe na si tambarare?
Tunawezaje kuelezea Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa baadhi ya nchi(mfano. Greenland na Canada) katika dunia iliyo tambarare?
Hapo vipi
tapatalk_1586876384610.jpg
Flat%20Earth.gif
 
Kama hutojali,
Usijali mkuu tupo pamoja maana na mimi napenda sana kujifunza kistaarabu kama wewe.
ningependa nijue nini kimekufanya binafsi uamini zaidi kuwa jua huzunguka dunia tambarare na kuleta usiku na mchana
Sijaamini ila bado nipo kwenye utafiti na kuona kwamba ina make sense kwa kiasi fulani.

So badala ya kusema kilichonifanya niamini mimi naomba kubadilisha na kusema KILICHONIFANYA NIONE INA MAKE SENSE hoja ya jua kuzunguka dunia ni hivi..

1.naona kwa macho yangu kwamba jua ndio huzunguka na dunia haizunguki iko imetulia na tunafahamu kwamba macho ni katika milango ya fahamu hivyo kinachoonwa na macho kinaweza kuwa na ukweli.


Uwepo wa picha za setelite zinazo oneshe dunia ikiwa na umbo hilo(mfano wa tufe)
Katika hii point nina maelezo ya namna mbili mkuu.

1.picha zina utata sana na haziwezi kuamua hoja tata kama hii nadhani unafahamu utata wa watu kwenda mwezini licha ya kwamba zipo picha lakini bado suala ni tata,hivyo picha sio hitimisho.

2.hii nadhania ya kwamba dunia ni kama sahani duara pia inaweza kuleta picha ya tufe kama mtu akiwa juu ya dunia sahani.

Kwa sababu hakuna picha itakayoonesha umbo la tufe lote bali picha yoyote ile itaoneshq sehemu ya mbele ya tufe ambayo itaonekana kama sahani duara.

Hivyo hata kwa dunia tambarare ambayo ipo kama sahani nao wakienda juu kupiga picha na satelite basi dunia itaonekana na umbo la tufe pia kutokana na ule utambarare wakw kuwa kama sahani duara.

Hivyo inshu ya kwamba picha za satelite zinaonesha tufe hiyo hata kwa flat earthers inaweza kuonesha tufe pia mkuu.
Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa nchi zinazopatikana kwenye poles za dunia(mfano. Greenland na Canada)
Tukirejea pia katika nadharia ya dunia tambarare sahani na jua ni dogo utaona kabisa kwamba kama jua linatembea katika njia yake maana yake kuna maeneo mwanga hautafikiwa kwa urahisi na hiyo inafanya kuwe na kipindi kidogo cha jua.

Hivyo uwepo wa kipindi kifupi cha jua pia inaweza kuwasapoti watu wa dunia tambarare sahani.
Gravitational force inashikilia vitu vilivyopo duniani huku dunia ikizunguka kwa kasi.
MKUU ambavyo vipo duniani vinashikiliwa na ARDHI na wala sio gravitational force.

Kila kitu ambacho utakirusha juu basi kinarudi ardhini kwa maana ardhi ndio inashikilia vitu na wala sio gravitational force.

Majengo yote yapo ardhini,milima majumba watu,hivi vyote vinashikiliwa na ardhi.

Assume upo outer space alafu hakuna gravitational force wala hakuna ardhi je unadhani vitu vitaangukia wapi mkuu ? Si vitabaki vinaelea milele bila kupata sehemu ya kudondokea au maana kwa tunavyofundisha huko outer space huwezi kusema upande huu ndio juu na upande mwingine ni chini kwa hiyo vitu vinavyoelewa haviwezi kudondokea upande wowote kwa sababu hapa duniani vitu vinadondoka kufuata ardhi ?

Je kama vile vinaelea tu havipati sehemu ya kudondokea unaweza ukasema kwamba gravitational force ndio imevishikilia vitu hivyo ?

So unaona namna ambavyo gravitational force ingekuea outer space bila ardhi basi isingeweza kushikilia vitu vikatulia kama sisi na majumba tulivyotulia hapa duniani Kwenye ardhi tukufu ya Muumba ?

Tunawezaje kuelezea Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa baadhi ya nchi(mfano
Hii nimeielezea hapo juu mkuu natumai umeona.

Mwisho niseme tu kwamba na mimi najadili idea na kujifunza mkuu so usichoke kuniuliza na kama sijui nitasema sijui maana mimi nienjoy kujifunza na pia Na mimi sitochoka kukuuliza pia ili nijifunze zaidi.
 
Asante.
Lakini ningependa zaidi kujua kati ya dhana ya dunia ni tambarare na dinia ni duara ipi ni ya ukweli. Maana haziwezi kuwepo zote kwa pamoja.
Ni either ni ya duara au ya tambarare.

Nikirejea ulichotuma hapo, tunaona jua na mwezi vyote vinatoa mwanga.
Utakubaliana na mimi pia, kulingana na ulichotuma hapo; wakati ambapo jua halimuliki eneo fulani la dunia (wakati wa usiku), mwezi ndio humulika eneo hilo.
Yaani pasipo kua na jua basi kutakua na mwezi (ndani ya siku hiyo)

Tunaona pia mwezi unazunguka dunia kwa kasi iliyo sawa na kasi ambayo jua linazunguka jua.
Na hakuna uwezekano kabisa mwezi kuonekana wakati wa mchana.

Hicho ndicho kinachoonekana kwenye video uliyoituma.

Nafikiri wote tutakua na uzoefu kuwa, si kila nyakati za usiku mwezi huonekana. Yaani mwezi huonekana kwa baadhi ya siku tu za mwezi (mf. Mwezi huu wa August, kuna siku ambazo tutaona mwezi na siku nyingine ambazo hautoonekana)

Kuna kipindi pia tunaona mwezi ukiwa nusu na wakati mwingine robo.
Zaidi, kuna wakati tunaona mwezi wakati wa mchana.

Maswali yangu kwako mkuu;

1. Kama jua na mwezi vyote vinatoa mwanga, ni kwanini hakuna nyakati ambapo tunaona jua likiwa robo au nusu(wakati wa mchana) kama tunavyoona kwa mwezi (wakati mwingine wa usiku).
Kwanini wakati mwingine ni sehemu tu ya mwezi ndiyo huonekana na si mwezi mzima?

2. Je, utawezaje kuelezea hali ya kutoonekana kwa mwezi katika baadhi ya siku za mwezi kwenye dunia iliyo tambarare?

3. Je, utawezaje kuelezea hali ya kuonekana kwa mwezi wakati wa mchana katika dunia tambarare?

Tukichukulia dunia iliyo mfano wa tufe, ikirotate on its axis na pia ikilizunguka jua,
Mwezi ukiwa unaizunguka dunia pasipo kutoa mwanga, hayo yote yanaelezeka.

Mwezi unaoneka baada ya kuakisi mwanga wa jua(mwezi hautoi mwanga).
Kwa kuwa mwezi na jua vyote vinazunguka dunia, kunakuwa na phase mbalimbali (kulingana na position ya mwezi, jua, na dunia) ambazo hupelekea mwezi kuoneka wote, robo, nusu au usionekane kabisa.

Mwezi hutumia takribani siku 27 kuzunguka dunia.
Hii upelekea kuonekana kwa mwezi(full moon) ndani ya siku hizo(27) za mwezi.

Dunia hutumia masaa 24 kurotate on its axis na kuleta usiku na mchana.
Hii ni tofauti na mwendo utumiao mwezi kuzunguka dunia.

Ningefurahi kama ungejibu maswali yangu.


images (19).jpeg
 
Mkuu ulijisomesha au ulipewa Grant / Mkopo kwa jasho la peasants huko vijijini (Kodi) ?

Kama ndivyo nadhani haujawatendea Haki
 
Sijaamini ila bado nipo kwenye utafiti na kuona kwamba ina make sense kwa kiasi fulani.
Kama ndio hongera sana inabidi uwe mtu wa kujoji na sio kumeza kila unacholetewa
So badala ya kusema kilichonifanya niamini mimi naomba kubadilisha na kusema KILICHONIFANYA NIONE INA MAKE SENSE hoja ya jua kuzunguka dunia ni hivi..

1.naona kwa macho yangu kwamba jua ndio huzunguka na dunia haizunguki iko imetulia na tunafahamu kwamba macho ni katika milango ya fahamu hivyo kinachoonwa na macho kinaweza kuwa na ukweli.
Ulishawahi kupanda basi au treni na treni jirani yako ikaanza kuondoka ukadhani ni wewe (treni uliyopanda ndio inatembea) kumbe wewe bado umesimama ?

Nadhani proof ya jua kuwa stationary mbona zipo nyingi tu yaani ukiweka evidence za for and against wala hautabaki na shaka lolote kuhusu hili; Nadhani endelea kusoma available information; utaona kwamba muda unaotumia kufanya huu utafiti ungeutumia more constructively
 
Usijali mkuu tupo pamoja maana na mimi napenda sana kujifunza kistaarabu kama wewe.

Sijaamini ila bado nipo kwenye utafiti na kuona kwamba ina make sense kwa kiasi fulani.

So badala ya kusema kilichonifanya niamini mimi naomba kubadilisha na kusema KILICHONIFANYA NIONE INA MAKE SENSE hoja ya jua kuzunguka dunia ni hivi..

1.naona kwa macho yangu kwamba jua ndio huzunguka na dunia haizunguki iko imetulia na tunafahamu kwamba macho ni katika milango ya fahamu hivyo kinachoonwa na macho kinaweza kuwa na ukweli.



Katika hii point nina maelezo ya namna mbili mkuu.

1.picha zina utata sana na haziwezi kuamua hoja tata kama hii nadhani unafahamu utata wa watu kwenda mwezini licha ya kwamba zipo picha lakini bado suala ni tata,hivyo picha sio hitimisho.

2.hii nadhania ya kwamba dunia ni kama sahani duara pia inaweza kuleta picha ya tufe kama mtu akiwa juu ya dunia sahani.

Kwa sababu hakuna picha itakayoonesha umbo la tufe lote bali picha yoyote ile itaoneshq sehemu ya mbele ya tufe ambayo itaonekana kama sahani duara.

Hivyo hata kwa dunia tambarare ambayo ipo kama sahani nao wakienda juu kupiga picha na satelite basi dunia itaonekana na umbo la tufe pia kutokana na ule utambarare wakw kuwa kama sahani duara.

Hivyo inshu ya kwamba picha za satelite zinaonesha tufe hiyo hata kwa flat earthers inaweza kuonesha tufe pia mkuu.

Tukirejea pia katika nadharia ya dunia tambarare sahani na jua ni dogo utaona kabisa kwamba kama jua linatembea katika njia yake maana yake kuna maeneo mwanga hautafikiwa kwa urahisi na hiyo inafanya kuwe na kipindi kidogo cha jua.

Hivyo uwepo wa kipindi kifupi cha jua pia inaweza kuwasapoti watu wa dunia tambarare sahani.

MKUU ambavyo vipo duniani vinashikiliwa na ARDHI na wala sio gravitational force.

Kila kitu ambacho utakirusha juu basi kinarudi ardhini kwa maana ardhi ndio inashikilia vitu na wala sio gravitational force.

Majengo yote yapo ardhini,milima majumba watu,hivi vyote vinashikiliwa na ardhi.

Assume upo outer space alafu hakuna gravitational force wala hakuna ardhi je unadhani vitu vitaangukia wapi mkuu ? Si vitabaki vinaelea milele bila kupata sehemu ya kudondokea au maana kwa tunavyofundisha huko outer space huwezi kusema upande huu ndio juu na upande mwingine ni chini kwa hiyo vitu vinavyoelewa haviwezi kudondokea upande wowote kwa sababu hapa duniani vitu vinadondoka kufuata ardhi ?

Je kama vile vinaelea tu havipati sehemu ya kudondokea unaweza ukasema kwamba gravitational force ndio imevishikilia vitu hivyo ?

So unaona namna ambavyo gravitational force ingekuea outer space bila ardhi basi isingeweza kushikilia vitu vikatulia kama sisi na majumba tulivyotulia hapa duniani Kwenye ardhi tukufu ya Muumba ?


Hii nimeielezea hapo juu mkuu natumai umeona.

Mwisho niseme tu kwamba na mimi najadili idea na kujifunza mkuu so usichoke kuniuliza na kama sijui nitasema sijui maana mimi nienjoy kujifunza na pia Na mimi sitochoka kukuuliza pia ili nijifunze zaidi.
Asante mkuu.

Kwanza, nakubaliana na wewe kwamba macho ni moja ya milango ya fahamu na ni muhimu kuyatumia kugundua na kudadisi mambo.

Lakini utakubaliana na mimi kuwa wakati mwingine tunaweza kudhani tumeona vitu kwa macho yetu lakini visiwepo kiuhlisia.
Wakati mwingine milango yetu ya fahamu inaweza ikatupo majibu kinyume na uhalisia.

Mfano.
1. Wakati wa jua kali jangwani au hata kwenye barabara ya rami tunaweza kuona "mirage" na milango yetu ya fahamu(macho) ikatuambia ni maji.

2. Vinywaji mbalimbali vinatengezwa kwa "flavour" za matunda mbalimbali na hivyo mtu huweza kudhani kinyaji kimengezwa kwa tunda halisi(kwa kutumia ulimi) kumbe sivyo.

Hivyo basi, tunahitaji utafiti na uchunguzi zaidi ili kuhitimisha kitu ni sahihi zaidi ya kutumia milango yetu ya fahamu.


Pili, ili tuendelee ningependa kujua kama unatambua uwepo wa satelites katika maeneo mbalimbali ya anga la dunia.

Kama jibu ni ndio, basi ningependa kukujuza kua satelite ikipiga picha haioneshi ardhi yote ya dunia bali sehemu tu.
Yaani picha moja inayopigwa na satelite imekua ikionesha dunia ni duara lakini si eneo lote la dunia linaloonekana.
(Nimeambatanisha na picha mwishoni)

Lakini baada ya kuchukua picha katika "angle" tofauti, maeneo mengine ya dunia(ambayo hayakuonekana awali) huonekana.

Hivyo, maeneo yote yaliyo kwenye uso wa dunia yameweza kuonekana baada ya kuchukua picha zaidi ya moja kutokea angle mbalimbali.

Hivo basi, katika dunia tambarare (sahani duara), pengine picha moja ya satelite ingeweza kuonesha eneo lote la uso wa dunia.
Zaidi, pasingekuwepo hata na "angle" ambayo setelite ingetembea ili kuona maeneo mengine.

Unakubaliana na mimi mkuu?


Tatu, napata ugumu kidogo kuelewa nama jua linazunguka dunia tambarare na kupelekea uwepo wa kipindi kifupi cha jua katika baadhi ya maeneo.

Unless kama inafanani na kilichopostiwa #948.

Kama ni hivyo, ningeomba unasidie kujibu maswali yaliyopo post #951


Mwisho, sijakuelewa unaposema vitu vinashikiliwa na ardhi na si gravitational force.

Ningependa kujua kama unakubali uwepo wa force ulimwenguni.(tukiachana na gravitational force)

Kama jibu ni ndio, basi tambua kuwa Kani (kwa Kiingereza force) ni athira ya nje inayoweza kubadilisha hali ya utulivu au mwendo kwenye gimba.
Yaani ni hali inayofanya kitu kisicho na mwendo kipate mwendo au kilicho na mwendo kiongeze/kupunguza mwendo au hata kusimama kabisa.

Force HAIITAJIKI kufanya kitu kisicho na mwendo kuendelea kukosa mwendo au kilicho kwenye mwendo kubaki kwenye mwendo huo huo.

Yaani kitu kilicho kwenye mwendo kitabaki kwenye mwendo, na kisicho na mwendo kitaendelea kukosa mwendo mpaka force iact kwenye kitu hicho.

Zaidi, ile hali ya kuvuta au kusukuma kitu ndio force yenyewe.

Unaposema vitu vikiruka vinarudi kwa sababu vinashikiwa na ardhi, Je, ardhi imekua ikivishikilia vikiwa angani pale vinaporuka?

Bila shaka vimevutwa.
Hiyo hali ya kuvuta ndio force sasa.
Ni aina gani ya force?
Gravitational force.

Umenielewa mkuu?

Tukienda na sheria nilizo elezea awali, basi unaporuka juu tunategemea huendelee kwenda juu tu(endapo hakuna force inayokuvuta).

Lakini kutakana na uwepo wa force inayo kuvuta chini, basi utashuka chini.

Vitu vilivyopo kwenye ardhi si kwamba "vimeshikiliwa" tu bali kuna force inavuta hivo vitu chini.
Ndio maana ulipo simama pakitoboka, Utashuka chini, kwa sababu kuna force itakuvuta chini.

Umenielewa mkuu?

Sasa gravitational force ni aina moja wapo ya force tu.
Ni attractive force inayo act kwenye vitu vyote vyenye uzito.

Yaani vitu viwili au zaidi vyenye uzito huvutana kwa gravitational force.

Lakini ni muhimu kujua uzito wa kitu ndio unao bainisha kiasi cha gravitational force kiliyo nayo au itakayo act kwacho.
Kitu kizito huwa na gravitation force kubwa kuliko chepesi.

Hii upelekea vitu vizito, kama dunia kuweza kuattract watu na vitu vingine vilivyopo(toward the center of gravity)

Pia, ni muhimu kujua force of gravity inakikomo chake. Yaani kuna umbali ukifika, force hiyo haita act kwako.


Unapokua kwenye outer space, unakua mbali na dunia pamoja na sayari nyingine.
Hivyo basi HAKUNA force yeyote, ikiwemo gravity, inayo act kwako, katika upande wowote ule.

Hivyo ukirejea sheria za force nilizo orodhesha awali, kama haupo kwenye mwendo utaendelea kutokua kwenye mwendo tu.

Umenielewa mkuu?

Nimejitahidi kukuelezea kwa kiasi flani lakini kama unahitaji ujuzi zaidi nimeweka link ya baadhi ya article juu ya gravitational force.

Gravity | Definition, Physics, & Facts

Newton's Law of Universal Gravitation





images (22).jpeg



images (21).jpeg
 

Attachments

  • images (21).jpeg
    images (21).jpeg
    46.8 KB · Views: 4
Huu mjadala nimeufatilia miaka mingi sana naona pande zote kuna vitu wana miss.

Hili swali la usiku na mchana limeulizwa sana na sijaona majibu yake,ila kuna mdau alijibu kwa concept ya kwamba..

Jua ni dogo kuliko dunia sahani,yaani chukulia sahani ya kula watu 10 ndio dunia na jua ni kama kitenesi cha watoto.

Hivyo inakuwa ni vigumu sana jua kumulika pande zote za dunia kwa sababu jua ni dogo na dunia ni kubwa.

Hivyo kwa kuwa jua ni dogo basi mwanga wake utakuwa haufiki baadhi ya sehemu,na hizo sehemu ndizo zitakuwa ni usiku.
Universe inaundwa na galaxies ambayo galaxies inaundwa na nyota, sayari na sayari zenyewe si hizo walizotufunza mashuleni, pili hakuna kitu kinachoitwa mfumo wa jua(solar system) bali kuna mfumo wa dunia unaoongozwa na jua na mwezi.

Nb. Jua sio nyota, jua haliko umbali wanaotuaminishw kuwa lipo kilometa nyingi kutoka dunian, bali jua ni dogo kiumbo kuliko dunia

Pili dunia haizunguki bali jua na mwezi ndio huizunguka dunia na kusababisha usiku na mchana na mabadiriko ya majira.

Tatu, hakuna kitu kinachoitwa gravitational force wala Space, huko wanakorusha satellite zao ni anga la hapa hapa dunian hakuna pimbi aliyewai na atakaewai kutoka nje ya anga la dunia, satellite zote zipo hapa hapa ndani ya anga la dunia.

Nne, dunia si duara ndiomaana mpaka leo hakuna aliyewai kuonesha picha halisi ya dunia ikionesha huo mduara bali wanatumia picha feki kutoka kwa NASA zilizotengenezwa ktk Computer na kuonesha umbo la uongo, ramani za uongo.

Dunia ni tambarare iyo ktk umbo la chapati, yaani mzunguko wenye tambarare, proof hii utaipata kwa kufuatilia kutoka ktk picha za angani kwenye ndege na sio hizo wanazoita satellite, pili kutoka ktk vilele vya milima mirefu,

Ushahidi wa dunia tambarare unaupata kwa njia nyingi sana
1)njia ya radio waves, kupima vizingiti vya kuzuia mawimbi ya radio kutoka kituo A kwenda kituo B ktk uso wa bahari , ambako kituo A kinawekwa Radio transmitter za kusafirisha mawimbi mpaka kituo B ambacho kinawekwa Radio waves receiver ambacho kituo hiki B kinakuwa umbali mrefu kutoka A, na umbali wa A - B unapitiliza ile distance ambayo ktk picha na ramani fake za dunia huonesha ule mduara(CURVE)
unachotakiwa kujua ktk umbo la duara mawimbi ya radio kutoka kituo A mpka kituo B hayawez kupokelewa sababu za kizuizi cha muinuko wa ardhi inayounda mduara, lkn kwakua A- B kiuhalisia inapopimwa ili kuprove kama kuna mduara majibu yake mawimbi ya radio yanapokelewa kituo B, kuprove kuwa hakuna kizuizi chochote
Nb.upimaji huu ufanyika ktk uso wa bahari ambako hakuna milima ya kusumbua transferring ya mawimbi.

2)ushahidi wa matumizi ya RADAR, hiki kifaa matumizi yake ni kudetect flying objects ambapo function ya kifaa hiki kamwe haiwez kufanya kaz ktk umbo la mduara(wanasayansi wanajua) hii ni shahidi nyingine ya umbo halisi la duara.

3)ushahidi wa safari za ndege, unaposafiri ktk ndege kama dunia ingekuwa duara basi ndege ingelazimika kuongeza Flying height kwenda juu ili kuukwepa mduara wa dunia badala yake ndege inapopaa kutoka sehem fulan, height from the ground to the air inaposafiri inakuwa constant mpaka mahala inapofika kwanini? Kwanini isiongeze height kwenda juu ili kuikwepa ile CURVE wanayoisema wanaoamin dunia duara?

4)picha kutoka ktk ndege+balloon ni ushahidi mwingine wa dunia si mduara bali flat.

5)ushahidi wa picha za Telescope zinazopigwa kutoka kituo A mpaka kituo B ambako kama dunia ingekuwa mduara basi picha za kituo B zisingeokana lkn kupitia umbo tambarare kuna muonekano dhahiri.

6. Huu ni ushahidi kwa wale wanaoamini ktk dini, ukifuatilia ktk stories za Yoshua alisimamisha Jua ili siku zigande kusiwepo na usiku bali mchana tu ili wapate kupambana na maadui zao, jiulize kwanini huyo jamaa hakuisimamisha dunia isilizunguke jua badala yake akalisimamisha jua ili lisimame lisisababishe mabadiriko ya usiku na mchana?[emoji23].

Shahidi ni nyingii ila kwa uchache tu elimu ya umbo feki la dunia imeanzishwa juzi tu na wahuni waliotaka tuwaamini wao, ambao ndio hao hao waliofake ramani ya dunia inayoonesha Uongo wa mpangilio wa mabala na nchi, kiramani ambacho kinaionesha Asia ni kubwa kuliko Africa, wakat huo kwa vipimo Africa ni kubwa kuliko mabala yote hapa dunian, je kwanini walifake hii kitu? Majibu utayapata walifake ili kututawala kifikra tujione tunaishi sehemu ndogo na wao kwao kukubwa ili kututisha tu na tujione wanyonge kirasilimali.

Niishie hapa, Tizama video hiyo utaelewa
 
Samahani.
Hiyo concept ya "Jua ni dogo kuliko dunia" inaweza kuthibitishwa vipi?
Sio kwamba ni nadharia tu?
Kwa kutazama utagundua, macho hayajawai kudanganya, hivi wew kwa akili zako unadhani dunia inazunguka? Wakati huo wew mwenyewe unaliona jua likifanya movements kila siku kutoka mashariki kwenda magharibi na kusababisha usiku na mchana.

Kwa kulitazama tu utagundua ukubwa wake, huitaji kudanganywa na vitabu vya washenzi waliotupotosha na nadharia zao za uongo
 
Kama hutojali, ningependa nijue nini kimekufanya binafsi uamini zaidi kuwa jua huzunguka dunia tambarare na kuleta usiku na mchana na sio kwamba dunia mfano wa tufe huzunguka jua.

Binafsi nafahamu kimsingi kuwa dunia ni tufe kwa sababu mbalimbali kama vile;

1. Uwepo wa picha za setelite zinazo oneshe dunia ikiwa na umbo hilo(mfano wa tufe)

2. Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa nchi zinazopatikana kwenye poles za dunia(mfano. Greenland na Canada)

Gravitational force inashikilia vitu vilivyopo duniani huku dunia ikizunguka kwa kasi.

Je, sababu kama hizi haziipi nguvu hoja ya kuwa dunia ni mfano wa tufe na si tambarare?
Tunawezaje kuelezea Uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa baadhi ya nchi(mfano. Greenland na Canada) katika dunia iliyo tambarare?
Picha za satellite sio za kweli na mpaka sasa hakuna chombo chochote kinachojishughulisha na safar za anga kimewai kuweka picha halisi za dunia kutoka angani, bali hutumia picha feki za dunia wanazounda ktk computer na kuzirusha na kupublish ktk makala na nakala za kutudanganya, hao NASA wakiongoza hii operarion,

Swali dogo, jiulize hao USA, Russi na china ni maadui lkn kwanini linapokuja suala la Anga na safari za angani hushirikiana mpaka kuunda chombo chao wanachokiita ISS(international space station) ambacho wametuaminisha kipo nje ya dunia yaan ktk space? Kwnn ktk masuala muhimu ya uchumi wanabondana lkn mambo ya kipuuzi ya anga wako pamoja? Sababu kuu ni wao hushirikiana kuficha ukweli kuhusu Umbo halisi la dunia.

Ukitaka uone dunia iko vipi chukua balloon ifunge camera na uirushe umbali mrefu kutoka usawa wa bahari na uanze kurecord movement zote za hiyo balloon na itembee distance kutoka ulipo mpaka mahali unapoonesha ktk ramani kuwa panamkunjo/mduara unapoanzia mpka unapoishia then leta majibu, na kwa bahat mbaya/nzuri majibu siku zote ni DUNIA TAMBARARE,

Pili ukitaka kuona umbo halisi la dunia tumia akili yako mwenyewe panda ktk kilima/mlima mrefu anza kutafiti muonekano wa dunia(mabonde+milima haviundi umbo la dunia bali ni vitu vilivyopo ktk umbo flat la dunia)

Tatu, tumia picha zinazopigwa na telescope kifaa kinachonasa picha za mbali ktk dunia, sasa wew weka point A ambako utaanzia kupiga picha za point B unayoamini iko upande wa pili wa mduara kwaiyo kwa kupiga picha sehemu hii haitoonekana maana itazuiwa na muinuko wa mduara wa dunia kwa mtizamo wako, lkn kwa bahat mbaya sehemu hiyo itaonekana vizuri tu kwanini? Kwa sababu dunia ni flat.

NB. Upigwaji picha huu hufanyika point A ya nchi kavu kwenda point B ambayo inatenganisha hizi sehemu kwa bahar, kama ujuavyo baharin hakuna vizingiti vya picha kama milima, majengo na miti

Njia ni nyingi sana
 
Picha za satellite sio za kweli na mpaka sasa hakuna chombo chochote kinachojishughulisha na safar za anga kimewai kuweka picha halisi za dunia kutoka angani, bali hutumia picha feki za dunia wanazounda ktk computer na kuzirusha na kupublish ktk makala na nakala za kutudanganya, hao NASA wakiongoza hii operarion,

Swali dogo, jiulize hao USA, Russi na china ni maadui lkn kwanini linapokuja suala la Anga na safari za angani hushirikiana mpaka kuunda chombo chao wanachokiita ISS(international space station) ambacho wametuaminisha kipo nje ya dunia yaan ktk space? Kwnn ktk masuala muhimu ya uchumi wanabondana lkn mambo ya kipuuzi ya anga wako pamoja? Sababu kuu ni wao hushirikiana kuficha ukweli kuhusu Umbo halisi la dunia.

Ukitaka uone dunia iko vipi chukua balloon ifunge camera na uirushe umbali mrefu kutoka usawa wa bahari na uanze kurecord movement zote za hiyo balloon na itembee distance kutoka ulipo mpaka mahali unapoonesha ktk ramani kuwa panamkunjo/mduara unapoanzia mpka unapoishia then leta majibu, na kwa bahat mbaya/nzuri majibu siku zote ni DUNIA TAMBARARE,

Pili ukitaka kuona umbo halisi la dunia tumia akili yako mwenyewe panda ktk kilima/mlima mrefu anza kutafiti muonekano wa dunia(mabonde+milima haviundi umbo la dunia bali ni vitu vilivyopo ktk umbo flat la dunia)

Tatu, tumia picha zinazopigwa na telescope kifaa kinachonasa picha za mbali ktk dunia, sasa wew weka point A ambako utaanzia kupiga picha za point B unayoamini iko upande wa pili wa mduara kwaiyo kwa kupiga picha sehemu hii haitoonekana maana itazuiwa na muinuko wa mduara wa dunia kwa mtizamo wako, lkn kwa bahat mbaya sehemu hiyo itaonekana vizuri tu kwanini? Kwa sababu dunia ni flat.

NB. Upigwaji picha huu hufanyika point A ya nchi kavu kwenda point B ambayo inatenganisha hizi sehemu kwa bahar, kama ujuavyo baharin hakuna vizingiti vya picha kama milima, majengo na miti

Njia ni nyingi sana
Unaprove gani satelite ni uongo?

Una evidance gani picha zinazosemwa kuwa zimepigwa setelite zimetengenezwa kwa computer tu?

Unapicha yoyote ya flat earth?
Kama ipo, vipi na mimi nikisema imetengenezwa kwa computer tu?

Hizo nchi ulizotaja, kwanini unadhani zinataka kutuficha juu ya umbo la dunia?
Wanapata faida gani ikijulikana dunia ni sphere?
Wanapata hasara gani ikujulikana dunia ni flat?

Ukipanda juu ya mlima utaona horizon ambayo inathibitisha dunia ni sphere.
Unajua horizon ni nini?

Picha za baloon zinaonesha either horizon au curvature kutegemeana na umbali baloon lilipo.
Vyote hivi vinathibitisha dunia ni sphere.

Nioneshe picha ya baloon inayo onesha dunia ni flat.

Experiment ya telescope uliyoiongelea ina walakini.

Ungetoa hata evidence kwa picha ungekua umefanya la maana.
Mf. Picha iliyopigwa na telescope iliyopo Russia, na nyingine iliyopigwa na telescope iliyopo Africa.
Picha hizo zioneshe feature zilizo kwenye uso wa dunia zinazofanana.

Hujaelezea kabisa sababu uwepo wa kipindi kifupi cha jua kwa nchi zinazopatikana kwenye poles za dunia(mfano. Greenland na Canada) katika dunia tambarare.

Umeishia kukataa vitu bila sababu za msingi.
Unatoa shutuma kwa hisia zako bila hata evidance.

Sidhani kama mjadala na wewe utakua na afya tukiendelea kwa mtindo huu.
 
Kwa kutazama utagundua, macho hayajawai kudanganya, hivi wew kwa akili zako unadhani dunia inazunguka? Wakati huo wew mwenyewe unaliona jua likifanya movements kila siku kutoka mashariki kwenda magharibi na kusababisha usiku na mchana.

Kwa kulitazama tu utagundua ukubwa wake, huitaji kudanganywa na vitabu vya washenzi waliotupotosha na nadharia zao za uongo
Kwanza, Wakati mwingine tunaweza kudhani tumeona vitu kwa macho yetu lakini visiwepo kiuhalisia.

Mfano.
Wakati wa jua kali jangwani au hata kwenye barabara ya rami tunaweza kuona kwa mbali "mirage" na macho yakatuambia ni maji.
Umewahi shuhudia ili?

Hivyo basi, si kweli kwamba macho hayajawahi danganya.
Uchunguzi na utafiti uhitajika ili kupata majibu sahihi.


Pili, ningependa kujua:
Ni vitabu gani hivyo vya washenzi?
Nini kinakufanya uviite "vitabu vya washenzi"?

Hujaonesha upotoshaji.
Hujaeleza faida wanazopata hao washenzi wanapo potosha.
Hujaeleza hasara wanazopata wasipo tupotosha.
 
Wakati mwingine milango yetu ya fahamu inaweza ikatupo majibu kinyume na uhalisia.
Sahihi mkuu lakini hii haitufanye tusizingatie yale meeengi ya uhalisia ambayo yanathibitishwa na milango yetu ya fahamu.

Maadamu milango ya fahamu inathibitisha uhalisia wa mambo mengi basi haina budi tuyazingatie mambo hayo mpaka pale kutakapokuwa na uthibitisho unaopingana na uhalisia tunaouexperience kwa milango yetu ya fahamu,tena uthibitisho ambao hauleti utata kama vile mirage sote tunafahamu kwamba yale sio maji yaani haina utata hiyo hakuna atakayebisha hiyo.
Kama jibu ni ndio, basi ningependa kukujuza kua satelite ikipiga picha haioneshi ardhi yote ya dunia bali sehemu tu.
Yaani picha moja inayopigwa na satelite imekua ikionesha dunia ni duara lakini si eneo lote la dunia linaloonekana.
(Nimeambatanisha na picha mwishoni
Mkuu kuhusu picha zinazotolewa na satelite tulishazungumza kwamba zina utata,hazina uhalisia mfano hiyo picha ya chini ni ya kutengeneza sio halisi.

Kumbuka kwamba kwa technolojia ilivyo hatuwezi kuamini mambo kwa picha tu maana utaalamu ni mwingi so picha za satelite BADO hazitoshi kuonesha umbo la dunia kwa sababu kuna utata katika hilo na picha za kutengeneza.

Hivo basi, katika dunia tambarare (sahani duara), pengine picha moja ya satelite ingeweza kuonesha eneo lote la uso wa dunia.
Kama umewaza hivi mkuu kwa kudhani kwamba dunia tambarare itakuwa ni ndogo tu basi sivyo,dunia tambarare nao husema kwamba dunia ni kuuuubwaaa saaana licha ya utambarare wake.

Hivyo dunia tambarare nayo ni kuuuubwaaa pia kiasi kwamba haiwezekani satelite moja ikamulika sehemu yooote ya dunia.
Tatu, napata ugumu kidogo kuelewa nama jua linazunguka dunia tambarare na kupelekea uwepo wa kipindi kifupi cha jua katika baadhi ya maeneo.
hii hoja mkuu nitaijadili peke yake katika comment moja alafu tuone kama maelezo yangu yatamake sense kwako ama laa.

Kwa sababu tunajadili idea na uwezekano na wala hatujadili mambo ambayo tayari yana uhakika.

So nakuahidi mkuu suala hili la kipindi kifupi cha jua nitalielezea katika comment ya peke yake.
Ningependa kujua kama unakubali uwepo wa force ulimwenguni.
Naamini ksbisa Mkuu wangu uwepo wa force.
Force HAIITAJIKI kufanya kitu kisicho na mwendo kuendelea kukosa mwendo au kilicho kwenye mwendo kubaki kwenye mwendo huo huo.
Mkuu nasema kwamba "FORCE ZAIDI INAHITAJIKA ILI KITU KILICHO KWENYE MWENDO KIENDELEE KUWA KWENYE MWENDO"

Tunaporusha jiwe angani maana yake lile jiwe linasukumwa na force ya mkono force tuliyotumia kurisha jiwe.

Hivyo basi kadri muda unavyozidi kwenda ile force inapungua ns jiwe litarudi chini(sio kwa sababu ya gravit.force) bali kwa sababu force imepungua.

HIvyo basi tungekuwa constant force kwenye lile jiwe ambalo tumerusha basi jiwe lisingerudi chini tena lingeenda juu tu,lakini kwa kuwa force inapungua na jiwe litarudi chini.


Hovyo basi kama tunahitaji jiwe liendelee kutembea kwenda juu maana yake tunahitaji force zaidi ili jiwe liendelee kutembea,lakini kama hakuna force zaidi jiwe litarudi chini.

Assume umerusha jiwe limeenda mita 10 juu,then kabla halijaanza kushuka mtu mwingine akalirusha likaenda 10m juu trna ,then akalidaka mwingine akarusha 10m juu na kuendelea, UNADHANI NINI KIMESSABABISHA JIWE LISIRUDI CHINI ?

bila shaka ni kwa sababu ya force mpya ambayo tumeiapply katika jiwe baada ya kila 10m ambazo jiwe lilitaka kurudi.

Maelezo haya ni yakuitetea hoja yangu ya kwamba "FORCE ZAIDI INAHITAJIKA ILI KITU KILICHO KWENYE MWENDO KIENDELEE KUWA KWENYE MWENDO" na hii nimetoa dhidi ya hoja yako isemayo "FORCE HAIHITAJIKI ILI KITU KILICHO KWENYE MWENDO KIBAKI KWENYE MWENDO HUO HUO".

Sasa tuingie radmi kwenye inshu ya gravitational force hapa nami nitatoa maelezo marefu kwa kuquote comment yakomkuu,I hope utasoma maelezo hayo.
Unaposema vitu vikiruka vinarudi kwa sababu vinashikiwa na ardhi, Je, ardhi imekua ikivishikilia vikiwa angani pale vinaporuka?
NA mimi hapa naweza kuuliza "UNAPOSEMA VITU VIKIRUKA VINARUDI KWA SABABU YA GRAVITY FORCE,JE HIYO GRAVITY FORCE KWA NINI ISIVISHIKILIE VITU HIVYO PALE VINAPORUKA TU ANGANI ??

Nimerudisha swali kwa sababu swali lako linaweza kuwa dhidi yako juu ya gravitational force.

Kwa sababu nikirusha jiwe juu mbona gravitational force haifanyi kazi pale pale badala yake inasubiri jiwe lieendee mbali kisha likiishiwa nguvu ndio gravity anakuja kuJITAPA KWAMBA yeye ndio kafanya jiww lirudi.

Yaani ni kama kubeba meli ukiwa majini ukasema wewe ubaibeba kumbe ile meli inaelea kwenye maji.

Hivyo tulitarajia pia kuona gravitationa force inaact soon tu baada ya kurusha jiwe,lakini hatuoni hilo,sasa ni sawa na kusema gravitationa force anatuibia,yaani anajificha then jiwe linapopoteza ile force yake then gravitation force anatokea anatuzuga kwamba yeye ndio anarudishs vitu chini ?

Kama kweli yeye gravitation force anafanya kazi hiyo kwa haki na uzalendo basi tuliratajia kuona kwamba hakuna kitu kiende juu hata point moja kwa sababu gravitational force always yupo.

Sijui umeyaoata maelezo yangu mkuu ?
Ndio maana ulipo simama pakitoboka, Utashuka chini,
Hapa mkuu nikupe mfano.

Mimi nasema kazi ya mlango ni kufanya mtu asiingie,kwa hiyo kama lango haupo maana yake watu wataingia.

Hovyo hatuwezi kusema kwamba mlango haujafanya kazi yake wakati haupo pale,lazima uwepo mlango kisha ndio mlango huo utafanya kwzi yake.

Nirudi kwenye point.

ARDHI NDIO HUSHIKILIA VITU kwa maana ardhi inakazi ya kushikilia vitu viwe juu yake.

Hivyo ardhi ikitoboka maana yake hapo palipotoboka hapana ardhi tena,na kama ardhi haipo basi tusitegemee ile kazi ya kushikilia kitu hicho ipatikane wakati huyo mfsnyaji(ardhi) hayupo (katoboka).

Hivyo ardhi ikitoboka maana yake haipo na kama haipo na kazi yake pia haitokuwepo yaani ileeèeee kazi ya kushikilia ardhi,hivyo hapo hatuwezi kuilaumu ardhi kwamba haijafanya kazi yake wakati ardhi yenyewe haikuwepo.

lakini kama tunakubali kwamba grav.force ndio inavuta vitu chini basi tukubali kwamba haya majumba yote na binadamu wote wapo hapa sio kwa ajili ya gravitational force bali kwa ajili ya ardhi,kwa sababu ardhi ikitoboka tu sote tunaenda chini,so why now hatuendi ? Kwa sababu mwamba ardhi yupo anatushikilia na gravitationa force(kama ipo) kawekwa pembeni kwanza.
 
Sahihi mkuu lakini hii haitufanye tusizingatie yale meeengi ya uhalisia ambayo yanathibitishwa na milango yetu ya fahamu.

Maadamu milango ya fahamu inathibitisha uhalisia wa mambo mengi basi haina budi tuyazingatie mambo hayo mpaka pale kutakapokuwa na uthibitisho unaopingana na uhalisia tunaouexperience kwa milango yetu ya fahamu,tena uthibitisho ambao hauleti utata kama vile mirage sote tunafahamu kwamba yale sio maji yaani haina utata hiyo hakuna atakayebisha hiyo.
Ni kweli tunapaswa kutumia milango yetu ya fahamu mpaka tutakapo kuwa na uthibitisho vinginevyo.

Mfano wangu wa mirage ulikua na lengo la kuonesha kuwa kuna mambo yanaweza kuonekana kwa macho tukadhani ni kitu fulani, kumbe ni tofauti kabisa na tunachokiona.
Yaani, tunachokiona kwa mbali ni KAMA maji lakini kiuhalisia ni effect ya refraction of lights tu.

Mtu asiyejua mambo ya refraction akiona mirage na ukamwambia yale sio maji atabisha.
Hii ni kwa sababu amategemea milango yake ya fahamu pekee kujua ukweli wa mambo.

Mfano wa kunywa kinywaji chenye flavour ya tunda ulikua na kusudi hilo hilo.

Mkuu kuhusu picha zinazotolewa na satelite tulishazungumza kwamba zina utata,hazina uhalisia mfano hiyo picha ya chini ni ya kutengeneza sio halisi.

Kumbuka kwamba kwa technolojia ilivyo hatuwezi kuamini mambo kwa picha tu maana utaalamu ni mwingi so picha za satelite BADO hazitoshi kuonesha umbo la dunia kwa sababu kuna utata katika hilo na picha za kutengeneza.
Mkuu,
Nilikuuliza awali kama unatambua uwepo wa setelite katika maeneo mbalimbali ya anga la dunia.

Kama unatambua uwepo wake, ningeomba nijue japo kazi moja ya hizo satelite.

Ni kweli kwamba hatuwezi kuamini mambo kwa picha tu.
Lakini picha iliyo halisi inaweza kuwa kithibitisho tosha cha ukweli wa jambo.

Ningependa pia kujua kwanini unasema kuna utata au kukosa uhalisia kwa hizo picha.
Je, umeangalia features gani ukatambua kuwa hizo picha si za uhalisia bali ni za kutengeneza tu?


Je, unadhani waliozitengeneza wanapata faida gani kwa kufanya hiyo kazi ya kutengeneza picha za uongo kuhusu dunia?

Je, kunapicha zozote(zisizo za kutengenezwa) zimewahi pigwa na satelite?
Tutajuaje kama si za kutengenezwa tu?

Kama umewaza hivi mkuu kwa kudhani kwamba dunia tambarare itakuwa ni ndogo tu basi sivyo,dunia tambarare nao husema kwamba dunia ni kuuuubwaaa saaana licha ya utambarare wake.

Hivyo dunia tambarare nayo ni kuuuubwaaa pia kiasi kwamba haiwezekani satelite moja ikamulika sehemu yooote ya dunia.
Umeongelea satelite.

Unatambua uwepo wa picha za setelite katika maeneo mbalimbali ya anga la dunia?
Nisaidie kazi mojawapo ya hizo satelite.

hii hoja mkuu nitaijadili peke yake katika comment moja alafu tuone kama maelezo yangu yatamake sense kwako ama laa.

Kwa sababu tunajadili idea na uwezekano na wala hatujadili mambo ambayo tayari yana uhakika.

So nakuahidi mkuu suala hili la kipindi kifupi cha jua nitalielezea katika comment ya peke yake.
Sawa mkuu.
Nasubiri.

Mkuu nasema kwamba "FORCE ZAIDI INAHITAJIKA ILI KITU KILICHO KWENYE MWENDO KIENDELEE KUWA KWENYE MWENDO"

Tunaporusha jiwe angani maana yake lile jiwe linasukumwa na force ya mkono force tuliyotumia kurisha jiwe.

Hivyo basi kadri muda unavyozidi kwenda ile force inapungua ns jiwe litarudi chini(sio kwa sababu ya gravit.force) bali kwa sababu force imepungua.

HIvyo basi tungekuwa constant force kwenye lile jiwe ambalo tumerusha basi jiwe lisingerudi chini tena lingeenda juu tu,lakini kwa kuwa force inapungua na jiwe litarudi chini.
Ni kweli tunaporusha jiwe angani maana yake lile jiwe linasukumwa na force ya mkono yaani force tuliyotumia kurusha jiwe.

Nilichoshindwa kuelewa ni namna hiyo force itakavyo potea kadri muda unavyozidi kwenda.

Itapotea kwenda wapi mkuu?
Hewani?
Nini kinafanya isiendelee kudumu tu bali ipotee?
Hapa kweli nimetoka kapa.
Fafanua nipate kuelewa.

Kwa ninivyojua, jiwe litarudi chini kwa sababu ya grivitational force inayolivuta kuja chini.

Jiwe linapo rushwa mwanzoni, huwa na kasi kubwa kutakana force iliyotumika kulirusha.
Lakini gravitational force uact kwenye hilo jiwe kwenye kwa mwelekeo(kwenda chini) ulio kinyume na mwelekeo jiwe lilipo rushwa(kama limerushwa juu).

Ni kama unapojaribu kukimbia then mtu anakuvuta shati kukurudisha nyuma.

Hivyo basi, baada ya muda jiwe lile hupunguza kasi yake ya kuelekea juu, then husimama, na kisha kubadilisha mwelekeo wake na kuanza kuja chini(towards gravity).


Kumbe, ile force iliyotumiwaa kurusha imebaki "constant" kabisa, ila tu kuna force nyingine, iliyo kinyume na ya awali imetenda kazi(gravitational force)


Hovyo basi kama tunahitaji jiwe liendelee kutembea kwenda juu maana yake tunahitaji force zaidi ili jiwe liendelee kutembea,lakini kama hakuna force zaidi jiwe litarudi chini.

Assume umerusha jiwe limeenda mita 10 juu,then kabla halijaanza kushuka mtu mwingine akalirusha likaenda 10m juu trna ,then akalidaka mwingine akarusha 10m juu na kuendelea, UNADHANI NINI KIMESSABABISHA JIWE LISIRUDI CHINI ?

bila shaka ni kwa sababu ya force mpya ambayo tumeiapply katika jiwe baada ya kila 10m ambazo jiwe lilitaka kurudi.
Kama nilivyoeleza;
force iliyotumiwa kurusha imebaki "constant" kabisa, ila tu kuna force nyingine, iliyo kinyume na ya awali imetenda kazi(gravitational force).

Tukitaka jiwe lisirudi chini, hatuna budi kulirusha kutumia force itakayo lifanya jiwe hilo lipate kasi isiyopungua escape velocity, 11.2km/s.
Hii force ita overcome gravitatinal force na jiwe halitarudi.

Mfano uliutoa hapo sijweza kuuelewa vizuri. Pengine ungeurudia kwa maneno mengine ili twende sawa.

NA mimi hapa naweza kuuliza "UNAPOSEMA VITU VIKIRUKA VINARUDI KWA SABABU YA GRAVITY FORCE,JE HIYO GRAVITY FORCE KWA NINI ISIVISHIKILIE VITU HIVYO PALE VINAPORUKA TU ANGANI ??

Nimerudisha swali kwa sababu swali lako linaweza kuwa dhidi yako juu ya gravitational force.
Ni vizuri ukitumia neno "kuvuta" na si "kushikilia".
Maana unaweza kuvuta kitu pasipo kukishikilia.
Mf. Sumaku huweza kuvuta vitu vilivyo mbali kidogo pasipo hata kuvishikilia.

Gravitational force inavuta, haishikilii.

Kwa sababu nikirusha jiwe juu mbona gravitational force haifanyi kazi pale pale badala yake inasubiri jiwe lieendee mbali kisha likiishiwa nguvu ndio gravity anakuja kuJITAPA KWAMBA yeye ndio kafanya jiww lirudi.
Mkuu,
Ukirusha jiwe juu, gravitatinal force ina act palepale.

Lakini kwa kipindi kifupi baada ya kulitupa, jiwe linakua na initial momentum.

Momentum ni ile hali ya kitu kuendeleza hali yake ya kasi au utulivi.
Hapa momentum huathiriwa na ukubwa wa jiwe hilo, pamoja na kasi ambayo jiwe lilitupwa awali kabisa.
Hivyo,kutokana na momentum, kwa kipindi fulani jiwe litaenda juu kwa kasi japo force of gravity ipo, na inaendelea kuvuta.

Gravity hii ndio hupelelekea kupungua kwa kasi ya kwenda juu(kadri muda unavyoenda, tangu liliporusha awali).
Hii ni kutakana na kwamba force hupelekea change in momentum(i.e kupungua kwa momentum).

Kupunguakwa momentum huku hupelekea kupungua kwa kasi(momentum=uzito×kasi)

Baadae jiwe hufikia kwenye hiyo hali unayoitambua kama "kuishiwa nguvu" (kasi ya kwenda juu imepungua kabisa) na huanza kuja chini, towards gravity.



Hivyo tulitarajia pia kuona gravitationa force inaact soon tu baada ya kurusha jiwe,lakini hatuoni hilo,sasa ni sawa na kusema gravitationa force anatuibia,yaani anajificha then jiwe linapopoteza ile force yake then gravitation force anatokea anatuzuga kwamba yeye ndio anarudishs vitu chini ?

Kama kweli yeye gravitation force anafanya kazi hiyo kwa haki na uzalendo basi tuliratajia kuona kwamba hakuna kitu kiende juu hata point moja kwa sababu gravitational force always yupo.

Sijui umeyaoata maelezo yangu mkuu ?
Nimekuelewa na nimetoa maelekezo juu hapo.
Hapa mkuu nikupe mfano.

Mimi nasema kazi ya mlango ni kufanya mtu asiingie,kwa hiyo kama lango haupo maana yake watu wataingia.

Hovyo hatuwezi kusema kwamba mlango haujafanya kazi yake wakati haupo pale,lazima uwepo mlango kisha ndio mlango huo utafanya kwzi yake.

Nirudi kwenye point.

ARDHI NDIO HUSHIKILIA VITU kwa maana ardhi inakazi ya kushikilia vitu viwe juu yake.

Hivyo ardhi ikitoboka maana yake hapo palipotoboka hapana ardhi tena,na kama ardhi haipo basi tusitegemee ile kazi ya kushikilia kitu hicho ipatikane wakati huyo mfsnyaji(ardhi) hayupo (katoboka).

Hivyo ardhi ikitoboka maana yake haipo na kama haipo na kazi yake pia haitokuwepo yaani ileeèeee kazi ya kushikilia ardhi,hivyo hapo hatuwezi kuilaumu ardhi kwamba haijafanya kazi yake wakati ardhi yenyewe haikuwepo.
Nakubaliana na wewe kwamba ardhi inashika vitu vilivyo juu yake. Na ukiiondoa utadondoka.

Nilicho ongezea tu ni kwamba;
gravitational force yenyewe inavuta vitu kuelekea chini(haivishiki).
Na kwamba pasipo kuvishikilia na ardhi iliyopo juu(mf. Chini pakitoboka) basi hivyo vitu vitashuka chini kwa sababu ya gravity.

Zaidi, gravitational force ipo tu, vitu vikiwa either vimeshikiliwa au havijashikiliwa.
Lakini matokeo yake yameonekana baada ya vitu hivyo kuacha kushikiliwa(na ardhi).

Ni kama unaposhikilia kitu chepesi kwenye upepo mkali.
Ukikiachia kitapeperuka.
Hakitapeperuaka ukiwa umekishika vizuri.

Haimaanishi nguvu ya upepo ilikua haipo kilipo kua kimeshikwa.

lakini kama tunakubali kwamba grav.force ndio inavuta vitu chini basi tukubali kwamba haya majumba yote na binadamu wote wapo hapa sio kwa ajili ya gravitational force bali kwa ajili ya ardhi,kwa sababu ardhi ikitoboka tu sote tunaenda chini,so why now hatuendi ? Kwa sababu mwamba ardhi yupo anatushikilia na gravitationa force(kama ipo) kawekwa pembeni kwanza.
Nimejaribu kulezea hapo juu mkuu.

Utanisamea sana kwani ninapata ugumu kukueleza vitu vingine in details as ni masomo marefu na yanahitaji muda mwingi.

Mfano. Mambo ya momentum, laws of motion n.k ni msingi mkubwa wa maswali unayoweza kupata.

Nilichojaribu kueleza ni kidogo sana kati ya mengi.
Hivyo sitashangaa kama bado utakua na maswali zaidi na zaidi.

Pengine itahitajika somo zima la msingi wa maswala ya motion na gravity ili tuelewane kikamilifu.
Kama uko interested na kujua hayo mambo ili uweze kuhitimisha kama ni ya kweli au uongo, unaweza pitia link nilizo ziweka hapo awali.


Uneweza ongeza na hii.

Kama utahitaji info zaidi niko tayari kushare na wewe source mbalimbali ili tujifunze.

Ukiwa na maswali, niko hapa kujibu.
 
Back
Top Bottom